Search This Blog

NYUMBA YA MAAJABU - 1

 https://pseudepigraphas.blogspot.com/2019/12/nyumba-ya-maajabu.html

    IMEANDIKWA NA : ATUGANILE MWAKALILE



    *********************************************************************************





    Simulizi : Nyumba Ya Maajabu

    Sehemu Ya  Kwanza (1)



    Ilikuwa ni siku ya furaha sana walipohamia kwenye hii nyumba nzuri na ya kupendeza, tena iliyovutia katika macho ya watu wengi sana.

    Mke alisikika akimuuliza mume wake,

    “Ibra, uliwezaje kuwekeza pesa nyingi za kununua nyumba nzuri kama hii?”

    “Mke wangu Sophia, kwakweli mambo ya Mungu ni mengi sana, hata mimi sikutegemea kupata nyumba kama hii kwa ile pesa ambayo nilikuwa nayo. Kwakweli tushukuru tu kwa kupata mwanga wa maisha”

    “Nadhani sasa mipango yetu itatimia mpenzi”

    “Ndio mke wangu kwa hapa lazima mipango itimie”

    “Hivi tulipanga kuzaa watoto wangapi vile?”

    “Watatu tu wanatosha mke wangu”

    “Baby kwa jinsi nyumba ilivyokubwa kwanini tusifanye wanne!”

    “Wewe ndio mzaaji mke wangu kwahiyo vyovyote tu inawezekana”

    Sophia akakumbatiana na mume wake kwa furaha kwani hii ilikuwa ni moja ya ndoto zake kwenye maisha.



    Baada ya wiki moja, Sophia aliamua kwenda kuwatembelea majirani zake wa sehemu aliyokuwa akiishi mwanzoni. Alifika na kuwakuta wakiendelea na shughuli za hapa na pale kama kawaida, moja kwa moja aliamua kwenda kwa rafiki yake wa pekee Siwema ambapo alikaribishwa vizuri sana na rafiki yake huyo.

    “Yani Sophia kama usingekuja kunisalimia kwakweli ningekuona ni mtu wa ajabu sana.”

    “Hivi Siwema naachaje kuja kukusalimia wewe! Nitakuwa nimerogwa basi, tena nitakuwa ni binadamu asiye na wema wala shukrani”

    “Eeh hebu kwanza niambie shoga yangu mmehamia wapi maana si kwa mbwembwe zile za kuondoka hadi vigoda vyako umeacha”

    “Shoga mwenzangu, yani wewe ni shoga yangu wa damu kwakweli na kukuficha siwezi. Kwakweli mwenzio nadhani kuna vitu Ibra alikuwa ananificha”

    “Kivipi? Na vitu gani hivyo alivyokuwa anakuficha?”

    “Hivi unaweza kuamini kwamba Ibra amenunua nyumba na gari!”

    “Mmh kwa hela gani? Katoa wapi hiyo pesa ya kununua nyumba na gari?”

    “Tena ninavyokwambia nyumba ni nyumba haswa shoga yangu wala sio nyumba uchwara, nitakupeleka na wewe ukajishangalie maajabu ya mume wangu Ibra”

    “Mmmh kwahiyo shoga biashara ya mamantilie hufanyi tena?”

    “Naanzaje kufanya biashara ya mama ntilie kwenye nyumba ile! Shoga hujaiona na wala sijisifii tu, kwakweli Ibra ana pesa, mpango wangu kwasasa ni kuzaa tu nicheze na wanangu pale maana nikichelewa nitakuta mwana si wangu”

    “Shoga tusiandikie mate wakati wino upo, ujue umenitamanisha sana, naomba twende sasa hivi na mimi nikajishuhudie huo mjengo. Ngoja nijiandae fasta twende.”

    Sophia akakubaliana na Siwema pale kwahiyo akamsubiri ajiandae ili aweze kwenda nae.



    Siwema na Sophia walifika kwenye nyumba husika ambapo nje tu ya nyumba hiyo Siwema alibaki kushangaa na kuduwaa kwani hakutegemea kama ile nyumba ipo vile kama alivyoikuta.

    “Khee jamani Sophia mbona umeokota dodo kwenye muharobaini shoga yangu, hebu jibebeshe mimba mapemaa maana hapa utashangaa ushaibiwa shoga yangu”

    “Yani hapa ninachotaka ni kuzaa tu, yani toka nimeuona huu mjengo na dawa za uzazi wa mpango nikaziacha pale pale saivi nawaza watoto wa kucheza nae kwenye nyumba hii”

    “Hongera sana shoga yangu ila kuwa makini na Ibra maana asije akakuletea mke mwenza bure”

    “Thubutuu huyo mke mwenza atapitia mlango gani!! Labda sio Sophia niliyepo humu ndani”

    “Nakuaminia Sophia, kama uliweza kumchunga Ibra kule uswahilini ndio ushindwe kumchunga kwenye huu mjengo”

    “Hapo sasa, yani hapa Ibra hazungushi amefika hapa Kigoma mwisho wa reli”

    Sophia alikuwa akifurahi tu na shoga yake huyu, na leo walipika pamoja na kula pamoja hadi joini ambapo mume wa Sophia aliwasili kutoka kwenye mihangaiko yake ambapo alimkuta Siwema pale kasha Siwema akawapa hongera zao na kuwaaga.

    “Hongera sana shemeji yangu Ibra, ila mimi ndio naomdoka shemeji”

    “Mmh shemeji jamani ndio haraka haraka hivyo!”

    “Shemeji nilikuwepo hapa tangu muda ila nitakuja tena maana ndio nishapapenda tayari ila saizi wacha niende”

    Basi Ibra hakuwa na jinsi yoyote zaidi ya kumuaga tu huyu Siwema.

    Kisha Sophia akatoka na kwenda kumsindikiza rafiki yake huyu,

    “Kwakweli Sophia usizembee, pale ndio umshikirie vizuri Ibra yani umgande kama ruba maana ule mjengo si mchezo shoga yangu. Yani wambea wa mtaa watanikoma nitakavyokuwa najidai kuhusu wewe Sophy.”

    Sophia akacheka tu kwani alikuwa akifurahia kile alichokuwa akiambiwa na Siwema.

    “Usicheke tu Sophy ila yafanyie kazi maneno yangu”

    “Ondoa shaka dada, mambo yataiva tu maana hata mimi nimetamani kuwa na watoto kwasasa”

    Wakabadilishana mawazo pale kasha Siwema akapanda daladala na kuagana vyema huku Sophia akisisitiza kuwa awasalimie majirani zao wengine.



    Sophy alirudi nyumbani kwake, kwavile giza nalo lilianza kuingia ikabidi aandae chakula cha usiku, na kilipokuwa tayari alikaa na mumewe na kuanza kula huku wakitabasamu.

    “Mmmh Sophy muda wote unatabasamu tu mke wangu”

    “Hivi naachaje kutabasamu Ibra!! Bahati tuliyoipata ni kubwa sana mume wangu kwakweli sikutegemea kama ipo siku tutaishi kwenye nyumba nzuri na kubwa kama hii, si unajua tulizoea chumba kimoja tu yani jiko hapo hapo, viti, vyombo, kitanda hapo hapo yani shaghalabhagala lakini sasa hivi eti tunaishi maisha ya kitajiri namna hii lazima nitabasamu mume wangu.”

    Wakamaliza kula kasha Sophy akatoa vile vyombo na kuvipeleka jikoni huku akitaka kuviosha kwanza ndimbo aende kulala na mumewe, ila Ibra alimfata kule jikoni na kumwambia,

    “Sophy mke wangu, vyombo utaviosha kesho bhana hebu twende tukalale”

    Sophy akatabasamu kisha akaacha vile vyombo na kuongozana na mumewe hadi chumbani ambako muda mwingi walionekana wakitabasamu.

    Kisha wakaenda kuoga pamoja na kurudi kitandani, Ibra alimkumbatia Sophy na kumuuliza tena,

    “Hivi ulisema tuzae watoto wangapi vile?”

    “Wanne mume wangu au wewe hupendi”

    “Mmmh hakuna kitu ambacho unakipenda wewe halafu mimi nisikipende, si unajua jinsi nikupendavyo Sophy! Yani mimi na wewe letu ni moja mke wangu”

    “Tena napenda wawili wawe wa kike halafu wawili wa kiume”

    “Wow ni mpango mzuri sana hakuna tatizo, tutazaa kadri Mungu atakavyo tujaalia Sophy wangu.”

    Wakatabasamu kisha wakalala kama kawaida.



    Kulipokucha, kama ilivyoada Ibra aliamka mapema sana kisha akajiandaa kwaajili ya kwenda kwenye kazi zake, Sophy alitaka kujaribu kuinuka ili kumuandalia mambo mbalimbali mumewe ila ibra alimzuia na kumtaka mkewe aendelee kupumzika tu ambapo naye alifanya hivyo kwani alielewa ni jinsi gani Ibra alimpenda.

    Kwenye mida ya saa mbili asubuhi, Sophy nae aliamka na kwenda kuoga ili kujiandaa kwa mambo ya hapa na pale.

    Akaenda jikoni kwa lengo la kutaka kuosha vyombo vya jana na kujiandalia chakula cha asubuhi, ila alishangaa kuona vyombo vilishaoshwa na vilipangwa vizuri kabatini.

    Hali hii ikamfanya Sophia ajiulize kuwa huenda Ibra alimzuia kuamka muda ule ili afanye kile kitu cha kumsahangaza. Kwakweli Sophia alitabasamu kwa jambo hili kwani aliweza kuona ni jinsi gani Ibra anampenda sana.

    “Najua Ibra ananipenda sana ila safari hii kazidisha mapenzi jamani mmh yani amefikia hatua hata ya kunitaka mimi nilale halafu yeye akaosha vyombo, haya ni mahaba tena motomoto kwakweli nina kila sababu ya kumzalia watoto Ibra wangu. Kipindi kile nilikuwa najibana kuzaa sababu ya maisha duni ila kwasasa nina kila sababu ya kuzaa kwakweli.”

    Kisha akajiandalia chakula pale na kuanza kukila halafu naye akatoka kwa lengo la kwenda kwenye mihangaiko yake mbalimbali.

    Wakati yupo nje ya nyumba hiyo kuna mmama alipita na kumsalimia Sophia kisha Yule mama akamuuliza Sophia kama ndiye anayeishi mule ndani,

    “Unaishi humo ndani dada?”

    “Ndio mama”

    Sophia akahisi kuwa huyu mama labda anamuona kuwa haendani na hiyo nyumba, ikabidi amuulize

    “Kwani vipi mama yangu! Kuna tatizo?”

    “Hapana ila sisi ni majirani kwahiyo ni vyema tukafahamiana, mimi naitwa mama Jane na wewe je?”

    “Mimi naitwa Sophia, na hapa naishi na mume wangu yeye anaitwa Ibra”

    “Basi ni vizuri, karibu kwangu nyumba ya jirani tu hapo”

    “Asante nitakaribia”

    “Karibu sana, usiogope kitu sisi ni majirani tu na ni vyema kufahamiana ingawa kufahamu watu waishio humo huwa ni ngumu sana”

    “Usijali utatufahamu tu”

    Kisha Sophia akaagana na huyu mama halafu yeye kuendelea na safari zake.



    Jioni ya siku hiyo Sophia akiwa ndani na mumewe akamsimulia kuhusu huyo mama aliyekutana nae wakati anatoka na vile alivyozungumza nae,

    “Kwakweli ni vizuri kufahamiana na majirani ukizingatia tangia tumefika hapa hakuna jirani tuliyemsogelea kumsalimia”

    “Basi tutafanya hivyo mume wangu. Ila kitu kingine sasa mmmhh”

    Sophy akatabasamu kwanza kabla ya kuongea na kumfanya Ibra amuulize,

    “Kitu gani hiki mpaka umeguna Sophy?”

    “Mmh naona mapenzi yamenoga mume wangu hadi leo umeosha vyombo!”

    Ibra akacheka kisha akasema,

    “Mmh acha kunichekesha Sophy yani na uvivu huu mimi nikaoshe vyombo kweli!!”

    “Sasa nani kaviosha vile vyombo asubuhi?”

    “Nikuulize wewe uliyebaki nyumbani”

    Sophia akakaa kimya kwa muda kwanza kwani hakuelewa hapo.





    Sophia akakaa kimya kwa muda kwanza kwani hakuelewa hapo, akamuangalia mumewe kanakwamba amwambie kuwa alichokuwa anakisema kilikuwa ni utani tu kisha akamwambia tena,

    “Acha masikhara Ibra”

    “Wewe ndio uache masikhara, unajua fika kuwa mimi ni mvivu wa kimataifa haya sasa huko kuosha vyombo ningeanzia wapi? Hebu kaandae chakula tule kwanza”

    “Lakini Ibra….”

    “Lakini nini Sophy? Wewe kaandae chakula tule bhana, mada zingine achana nazo usifikirie ni rahisi hivyo mimi kuosha vyombo”

    Sophia akaenda jikoni huku akiwa na mawazo sana ila kuna wakati alihisi kuwa Ibra anatania tu kwani kule ndani walikuwa wao wawili tu kwahiyo akahisi kuwa ni lazima Ibra ndio aliosha hivyo vyombo ila anajigelesha tu, alijiaminisha hivyo huku upande mwingine akiwa na mashaka kiasi.

    “Kesho nitampigia simu Da’ Siwema nimsimulie, Yule ni mtu mzima anaelewa vizuri sana”

    Kisha akaendelea na uandaaji wake wa chakula cha usiku.

    Akapeleka mezani na kuanza kula na mumewe Ibra,

    “Yani leo nimechoka Sophy maana nimejikuta nikiwa na kazi nyingi sana”

    “Pole mume wangu ila ndio ukubwa huo”

    “Kweli kabisa ukubwa jalala maana sio kwa kuchoka huku”

    Walipomaliza kula, leo Sophia hakutaka kuacha vyombo vichafu kwahiyo alienda kuviosha na kuvipanga kisha kwenda chumbani kulala na mume wake ambapo alimkuta ameshalala tayari.

    “Mmmh kweli leo Ibra kachoka jamani maana yupo hoi kabisa”

    Kisha na yeye akatafuta usingizi pale na kulala, alipopitiwa na usingizi tu akajiwa na ndoto.

    Kwenye ndoto hii alijiona yeye akiwa mjamzito ila mumewe alionekana kutokuifurahia kabisa ile mimba na alionekana kuongea maneno machafu sana ya kumkaripia,

    “Aliyekwambia ubebe mimba nani? Na utaenda kuzalia kwake huyo mtu, sitaki ujinga mimi”

    Sophia akashtuka sana kutoka kwenye ule usingizi huku akiilaani ile ndoto na kuona kuwa ni kitu cha ajabu sana kwake kwani haikuwa rahisi kwa Ibra kuikana mimba yake kiasi hicho ila ndoto hiyo ilimfanya asipatwe na usingizi tena hadi panakucha.



    Ibra alipoamka tu, Sophy nae alikuwa macho na swali la kwanza ambalo Sophy alimuuliza Ibra ilikuwa ni kuhusu mimba.

    “Hivi kwa mfano mimi nikiwa na mimba yako je utafurahi mume wangu?”

    “Sophy, ninavyokupenda hivi naachaje kufurahi? Pia nahitaji mtoto Sophy wangu, na mimi napenda niitwe baba. Nakupenda sana mke wangu, najua watoto ndio watakamilisha furaha yetu mpenzi.”

    “Asante Ibra”

    Kisha Ibra akaanza kujiandaa pale halafu akamuaga Sophy kwa kumbusu kwernye paji la uso.

    Ibra alipoondoka tu, Sophy nae akaamka na kwenda kukaa sebleni ili kujipotezea mawazo mbalimbali huku akiona wazi kuwa ile ndoto ni uchizi tu na ni kitu cha kusadikika.

    “Ndoto zingine kama zimetumwa loh! Ndoto gani sasa ile? Yani Ibra kabisa akane mimba thubutuu, yani ile ndoto ishindwe na ilegee ujinga ujinga sitaki.”

    Muda ulipoenda kidogo akampigia simu Siwema na kuanza kuzungumza naye kuhusu kilichotokea jana na vile ambavyo Ibra alimjibu kuwa hakuosha hivyo vyombo.

    “Hayo ndio mahaba mdogo wangu, mwenzako Ibra anakupima tu lakini vyombo kaosha mwenyewe, we unadhani ataosha nani wakati ndani mpo wawili tu?”

    “Ndio hapo dada nimeshindwa kuelewa kwakweli maana mimi nimekuta vimeoshwa halafu ni yeye aliyesema nisivioshe halafu anakataa kuwa hajaviosha loh!”

    “Anakuchanganya akili tu huyo mdogo wangu, kwani wanaume hujawajua tu, wanapenda kutupima Sophy mdogo wangu. Hata usiwe na shaka mwaya mwenzio saivi anakuonyesha mahaba kimya kimya”

    “Kweli dada haya ni mahaba maana ila hapendi kuosha vyombo, hata niumwe ataviacha hadi nipone ila kuona ameosha safari hii tena nikiwa mzima kabisa kweli ni mahaba”

    “Ndio mapenzi hayo mdogo wangu hata usistaajabu sana, hapo ndio kupendwa yani wewe jiongeze tu.”

    Sophia akafurahia sana ushauri aliopewa na Siwema kwani aliona ushauri huo ukimfaa sana, kisha akaagana nae kwenye simu na kuendelea na mambo mengine.

    Wakati akifanya shughuli zake za hapa na pale mule ndani, akasikia hodi na kwenda kufungua mlango ambapo alimkuta Yule mama ambaye walikutana siku ya nyuma huku akiwa ameambatana na binti aliyeonekana kufanana nae sana, Sophia akawakaribisha vizuri sana watu hao ndani kwako huku akitabasamu,

    “Karibuni sana jamani”

    “Asante tumekaribia Sophy”

    Wakaingia ndani huku Yule mama akianza utambulisho kwa binti aliyeongozana nae,

    “Huyu ni binti yangu anaitwa Jane”

    “Wow ndiomana umefanana nae sana mama, hongera kwa kuwa na binti mzuri”

    Huyu mama akatabasamu kidogo kisha akaendelea,

    “Nimeona ni vyema akufahamu jirani yetu ili hata siku akiwa mbweke nyumbani basi aje akutembelee, unajua huyu mtoto ametoka kumaliza kidato cha nne kwahiyo tunangoja matokeo tu kwasasa. Mara nyingi anashinda nyumbani kwahiyo akija kuongea ongea hapa si vibaya.”

    “Umefanya jambo jema mama maana hata mimi huwa na upweke sana maana huwa nashinda mwenyewe mahali hapa, pia hongera sana Jane kwa kuhitimu kidato cha nne.”

    “Unampa hongera ya bure tu huyu, akili yake yenyewe sijui kama atafaulu huo mtihani, na akifeli ndio atakaa nyumbani atafute mume aolewe tu”

    “Jamani mama usiseme hivyo inakuwa kama unamuombea mabaya mtoto”

    “Mabaya kajiombea mwenyewe hata sio mimi, mtu gani alikuwa anajijua kabisa kuwa ana mitihani ila ndio tamthilia sijui michezo kila kitu anakijua yeye na hatma yake inakuja kwakweli naona kabisa zero ikimuangalia.”

    Jane alionekana kuwa kimya kabisa kwani ilionyesha wazi hakupendezewa na maneno ya mama yake, ili kuondoa ule mzozo ilibidi Sophia abadilishe mada kisha akaenda jikoni na kuwaletea wageni juisi huku wakizungumza mawili matatu.

    Muda kidogo Ibra alirudi hata kumshangaza Sophia kwani alionekana kuwahi sana siku hiyo na alionekana kuwa na uchovu.

    Sophia akamkaribisha mumewe na kumtambulisha kwa wale wageni ambao walifahamiana na kusalimiana, ingawa Ibra alikuwa amechoka ila alivunga kidogo kwenda chumbani ili wale wageni wasijihisi vibaya, ila huyu mama nae aliaga muda ule ule kwahiyo Sophia akatoa zile glass na kupeleka jikoni kisha akamuaga mumewe na kwenda kuwasindikiza wale wageni, ambapo Sophia alienda nao hadi nyumbani kwao ili kuweza kupafahamu wanapoishi watu hao.

    Sophia aliweza kuona mazingira ya uswahili anayoishi huyu mama ila hakushangaa sana kwavile ndio mazingira ambayo hata yeye amekulia na ameyaishi kwa kipindi kirefu sana.

    “Sophia, ukiwa na tatizo usisiste kuja, hapa ni kama nyumabani kwenu tu kwahiyo usiogope chochote”

    “Usijali mama tupo pamoja”

    Sophia hakukawia sana kwani aliaga na kuondoka.





    Aliporudi nyumbani kwake hakumkuta Ibra pale sebleni na moja kwa moja akahisi kuwa Ibra atakuwa ameenda chumbani kupumzika tu, kisha nae akaenda chumbani alipo Ibra kwani alipenda kujua ni kwanini mumewe amechoka kiasi kile.

    Alimkuta Ibra amejilaza kitandani, akamfata na kumsogelea karibu mumewe kisha akakaa pembeni yake na kumuuliza kuwa tatizo ni nini,

    “Vipi tena Ibra mume wangu, nini kimekukumba baba?”

    “Kwakweli hata sielewi ila nimechoka mwili na viungo vyote”

    “Pole sana mume wangu, ngoja nikuandalie chakula ule kwanza ndipo ulale”

    “Usijali kuhusu hilo, nilishaenda jikoni nimepakua chakula na nimekula tayari”

    “Dah nisamehe mume wangu jamani”

    “Usijali kitu mke wangu, wale ni wageni wetu sote kwahiyo hata usijali na ndiomana hata mimi sikuona tataizo kwenda jikoni na kujipakulia chakula”

    “Pole sana mume wangu, basi ngoja nikakuandalie maji uoge”

    “Kwakweli sijisikii kuoga kwasasa subiri nipumzike kwanza ndio nitaoga”

    Sophia alitulia kwa muda akiitafakari hali ya mume wake kwani haikuwa kawaida kabisa kwa Ibra kuwa vile alivyokuwa.

    Alienda sebleni huku akihisi kuwa huenda Ibra akawa na malaria ila ndio hivyo anajikaza kwavile ni mwanaume, kisha akaelekea jikoni na kufunua sofuria alilopikia chakula na kukuta kweli kilipakuliwa kwamaana hiyo ni kweli Ibra amekula kile chakula kisha akaangalia Ibra alipoweka sahani aliyotoka kula nayo ila hakuona sahani wala nini hapo ndipo aliposhangaa na kwenda tena sebleni kuwa huenda ameiacha huko ila hakuona sahani yoyote chafu, wazo likamjia kuwa aangalie na zile glasi ambazo wageni wamenywea juisi ila hakuziona pale zaidi aliziona zimeshawekwa kabatini tena zikiwa safi kabisa,

    “Mmh huyu Ibra si anaumwa huyu sasa iweje ameosha vyombo vyake alivyolia na zile sahani jamani wakati mtu ni mgonjwa? Haya ni maajabu mapya kwangu, sasa nitamuulizaje na anaumwa? Ila lazima nimuulize?”

    Sophia akatoka jikoni na kuelekea chumbani tena alipo Ibra kwa lengo la kumuuliza kulikoni maana hakuelewa kabisa.

    Alimkuta Ibra akiwa bado anagalagala tu kitandani kwani hata usingizi haukumjia, kisha akamuuliza,

    “Mume wangu leo umechoka sana ila kwanini umeosha vyombo ulivyolia chakula?”

    “Sophy, toka lini hunijui mimi jamani! Mimi naoshaje vyombo mke wangu, kwanza naumwa halafu wewe unaniletea habari zingine kwanini unakuwa hivyo Sophy?”

    “Samahani mume wangu ila ningependa twende hospitali”
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sijisikii kwenda hospitali kwakweli, tafadhali niache nipumzike”

    Sophia hakumuelewa Ibra kabisa na akahisi huenda Ibra ana malaria ambayo imempanda kichwani na ndiomana amekuwa vile alivyokuwa.

    Sophia aliamua kuinuka tena ili atoke mule chumbani ila kabla hajafika malngoni alijihisi kichefuchefu na kumfanya aanze kukimbilia chooni ili atapike ila kabla hajafika chooni alijikuta kashatapika tayari kwahiyo chooni alienda kama kumalizia tu na alitoka akiwa amechoka sana ila hakuweza kuvumilia kuangalia yale matapishi yake yaliyotapakaa chumbani kwao karibia na mlanngo wa chooni, hivyobasi Sophia akaenda jikoni kuchukua tambala na maji kwa lengo la kufuta matapishi yale.

    Ila aliporudi chumbani ili afute alikuta yale matapishi yalishafutwa na pale palishakaushwa kabisa, kwakweli Sophia alichoka gafla, akamuangalia Ibra pale kitandani ila Ibra alionyesha kutokuwa na habari yoyote kwani alikuwa amejilaza vile vile.





    Ila aliporudi chumbani ili afute alikuta yale matapishi yalishafutwa na pale palishakaushwa kabisa, kwakweli Sophia alichoka gafla, akamuangalia Ibra pale kitandani ila Ibra alionyesha kutokuwa na habari yoyote kwani alikuwa amejilaza vile vile.



    Sophia hakuelewa kwakweli yani hakuelewa kabisa, akaenda tena pale kitandani alipokuwa amejilaza Ibra na kumshtua, ambapo Ibra aliongea kwa kulalamika,



    “Sophia jamani mbona hivyo mke wangu? Kwanini unanifanyia hivi lakini si nimekwambia kuwa najisikia vibaya! Sasa kwanini hutaki mwenzio nipumzike jamani unanifanyia mambo ya ajabu, kwanini kunishtua shtua kila muda?”



    “Samahani Ibra lakini nani kazoa matapishi yangu?”



    “Matapishi?”



    “Ndio, kwani hukunisikia wakati natapika?”



    “Sijakusikia bhana, unanisumbua tu Sophy hebu acha nipumzike”



    Ibra akageuka tena na kulala, kwakweli Sophia hakuelewa chochote alijikuta akijishika tama tu kwa mawazo kwani aliona kama vile Ibra anamchanganyia mada huku nayeye akizidi kujiuliza kuwa kama sio Ibra anayefanya hayo je yatakuwa yanafanywa na nani? Hapo ndio ilikuwa ngumu kabisa kwa yeye kuelewa.



    Akajikuta akikaa pale kitandani huku akitafakari kwa muda mrefu sana bila ya kupata majibu hadi akapata wazo la kumpigia simu tena Siwema ili amuulize ila aliona kamavile ni kumsumbua tu huyo Siwema, kwahiyo akatulia kimya kwa muda mrefu kidogo kisha akainuka pale na kuelekea jikoni kwa lengo la kuandaa vizuri mlo wa usiku.



    Akiwa jikoni alijiuliza sana kitu kilichopelekea yeye kutapika ni nini,



    “Hivi ni kwanini nimetapika ikiwa siumwi wala nini? Ni kitu gani kimepelekea mimi kutapika?”



    Alijiuliza bila ya kupata jibu la aina yoyote ile kwahiyo akaamua kuandaa chakula tu.



    Alipomaliza kuandaa chakula alitoka jikoni na kuelekea sebleni ambapo alimkuta mumewe amekaa na kwakweli alionekana kuwa sawa kabisa kwasasa tofauti na mwanzo,



    “Khee Ibra kumbe umeamka tayari!”



    “Ndio nimeshaamka”



    “Eeh unajisikiaje na hali!”



    “Nipo salama kabisa mke wangu”



    “Basi ngoja nikakuandalie maji ya kuoga”



    “Hata usijali mke wangu nimeshaoga labda ulete chakula tule”



    Basi Sophia hakutaka kuhoji zaidi kwahiyo akaenda kuleta chakula kisha yeye na mumewe wakaanza kula chakula hicho huku wakizungumza mambo mawili matatu,



    “Kwahiyo Ibra saivi unajiona umepona kabisa!”



    “Ndio nimepona kwani nilikuwa naumwa sana eehh!”



    “Yani hadi mimi ulinitia mashaka mume wangu mpaka hofu ilinitawala kabisa”



    “Hata usiwe na mashaka mke wangu maana mimi ni mzima kabisa kabisa”



    “Basi vizuri mume wangu kama ndio hivyo”



    “Ila nakushukuru sana Sophy kwa mapenzi yako unayonionyesha na jinsi unavyonijali”



    Sophia akatabasamu huku wakiendelea kula kile chakula, walipomaliza kama kawaida Sophia alitoa vyombo na kutaka kwenda kuviosha ila Ibra alimuita na kumfanya Sophia asioshe vyombo vile.



    “Sophy mke wangu napenda nikae na wewe tupumzike pamoja”



    “Naelewa mume wangu ila huwa sipendi kulala na vyombo vichafu ndani ndiomana huwa napenda kuviosha pindi tunapomaliza kula”



    “Ngoja nikuulize swali, kwani kesho unaenda wapi?”



    “Nipo tu siendi popote”



    “Sasa tatizo liko wapi hapo? Utaosha hata kesho, mi napenda tukae tuzungumze na tupumzike pamoja”



    Ikabidi Sophia atumie nafasi hii kumuuliza Ibra kuhusu matapishi yake,



    “Hivi Ibra hukunisikia wakati natapika?”



    “Kwani unaumwa?”



    “Hapana ila nilitapika”



    “Mmmh sijakusikia kwakweli”



    “Mmmh kwahiyo nani alizoa matapishi yangu?”



    “Mmmmmh Sophy acha habari hizo bhana tumetoka kula, hebu tubadilishe mada”



    Sophia hakuwa na jinsi zaidi tu ya kufata matakwa ya Ibra na kisha wakaamua kwenda kulala, Ibra alipopitiwa na usingizi Sophia akakumbuka vile vyombo akaona ni vyema akavioshe ili asipate tena maswali ya kujiuliza kuwa vyombo vimeoshwa na nani, kwahiyo akatoka mule chumbani na kwenda jikoni kwa lengo la kuosha vyombo.



    Alivikuta vyombo vipo pale pale jikoni na kisha akaanza kuviosha, muda kidogo alikuja Ibra kutoka chumbani huku akitikisa kichwa baada ya kumkuta Sophia akiosha vyombo,



    “Ona sasa mke wangu halafu unakazana kuuliza nani kaosha vyombo wakati unaamkaga mwenyewe usiku wa manane kuviosha jamani unakuwa kama mwanga, majukumu gani hayo ya usiku wa manane?”



    “Unajua nini Ibra sikupenda nipate tena shida ya kudadisi juu ya mtu aliyeosha vyombo ndiomana nimeamua kuviosha mwenyewe”



    “Kwakweli umenishangaza Sophy yani nashtuka kitandani sikuoni kumbe upo jikoni unaosha vyombo, jamani mke wangu kwanini unakuwa hivyo jamani? Nadhani mtu yeyote atakayesikia hili lazima ashangae, kwani kuna umuhimu gani wa kuosha vyombo usiku kamavile hapatakucha?”



    Ibra alionekana kutokupendezwa kabisa nah ii tabia aliyoiona leo kwa Sophy kwani yeye alipenda anapogeuka kitandani basi amkute mkewe akiwa pembeni,



    “Basi nisamehe mume wangu, nakuahidi hii hali haitajirudia tena kama nikishindwa kuosha muda ambao tumemaliza kula basi nitakuwa nasubiria hadi kesho yake. Nisamehe tafadhari”



    Basi akavimalizia na kuviacha pale juu huku akipanga kuviweka kabatini kesho yake kwani hakutaka kumkwaza mume wake zaidi.



    Wakaongozana pamoja kuelekea chumbani ambapo Ibra alionekana kutokuwa na usingizi sana kwani yote ilitokana na vile alivyolala jioni ya siku hiyo, kwahiyo walivyofika tu kitandani Ibra akaanzisha maongezi tena.



    “Hivi ulisema kuwa leo umetapika eeh”



    “Ndio nimetapika”

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Basi kama hiyo hali itaendelea itabidi twende hospitali”



    “Kama ikijirudia tutaenda mume wangu, asante kwa kunijali”



    “Unajua Sophy mi nakupenda sana na kwakweli sipendi kuona ukisumbuka wala kuhangaika mke wangu ndiomana unaniona mara nyingine nafoka”



    Kisha akamsogelea karibu na kumkumbatia ili waweze kulala, na kweli usingizi ukawapitia hadi palipokucha ambapo kama kawaida Ibra aliamka na kujiandaa kisha kumuaga mkewe na kwenda zake kazini.



    Sophia nae kama kawaida yake alipoamka alienda moja kwa moja jikoni ambapo alikuta vile vyombo alivyoviosha usiku vikiwa tayari vimepangwa kabatini,



    “Yani huyu Ibra ananikatazaga mimi ili afanye yeye ila ni sawa tu maana yupo kwenye harakati za kunionyesha upendo”



    Alipofikilia hayo akaenda kuandaa chai na kunywa halafu akaenda kuloweka nguo ili afue, baada ya kuziloweka alirudi sebleni ili akae angalau kidogo halafu ndio akafue ila alivyokaa pale sebleni akapatwa na usingizi wa gafla uliomfanya alale hadi kujisahau kuwa alipanga kwenda kufua nguo zake.



    Ibra alirudi nyumbani na kugonga sana ila kwa bahati nzuri tu alikumbuka kuwa anafunguo za ziada kwenye gari lake kisha akaenda kuchukua funguo zile na kufungua milango ambapo alimkuta Sophia akiwa amelala tena hajitambui kabisa, ikabidi Ibra ndio amshtue Sophia kutoka kwenye ule usingizi aliokuwa amelala ambapo Sophia alionekana kushtuka sana.



    “Kheee Sophia ndio kulala gani huko hadi umejisahau yani nimegonga na kugonga ila wapi”



    Ila Sophia alionekana kuchoka sana hata akajikuta anashindwa kumjibu mumewe kwa wakati, hadi alipotulia kidogo kama kurudisha akili yake vile ndio akaweza kumjibu mume wake,



    “Yani hata sijielewi ila nimechoka balaa”



    “Mmh hata kupika umepika kweli wewe?”



    “Kwakweli sijapika wala sijafanya chochote kile yani hata sijielewi”



    “Pole sana mke wangu basi twende tukajimwagie upate nguvu kisha twende tukale hotelini maana hamna namna tena”



    Sophia akakubali na kuzidi kuuona upendo wa Ibra juu yake kuwa Ibra anampenda na kumuhurumia sana kwani ile iliweza kuonyesha ni kwa kiasi gani alipendwa na Ibra.



    Walipomaliza kujiandaa wakatoka na kuelekea hotelini kama ambavyo Ibra alisema ili kuweza kula, waliagiza chakula na kuanza kula ila gafla Sophia akapatwa na kichefuchefu na kujikuta akikimbilia nje kutapika, Ibra alivyoona vile akamuomba muhudumu awafungie kile chakula kisha akaenda kumuangalia mke wake,



    “Kwani unajisikiaje Sophy”



    “Najisikia vizuri tu”



    “Vizuri wakati umetapika jamani! Itabidi kesho twende hospitali tukaangalie afya yako”



    Sophia akakubali kisha akaja Yule muhudumu na kuwapa chakula chao ambapo Ibra alilipia na kuondoka na mke wake.



    Walipofika nyumbani waliweka kile chakula na kuanza kula tena ila Sophia alionekana kula kwa kujivuta vuta sana,



    “Lazima unaumwa Sophy ingawa wewe mwenyewe unajiona kuwa mzima”



    “Ni kweli kabisa najiona kuwa mzima mimi”



    “Hata kama unajiona ni mzima lazima kesho twende hospitali maana hii hali ni mbaya mke wangu”



    “Sawa nimekuelewa kwa hilo”



    Walipomaliza kula, Ibra alibeba vile vyombo na kuvipeleka jikoni kisha akamtaka mke wake kuwa waende kulala,



    “Ila sina usingizi Ibra”



    “Hata kama, ila mi nakuomba twende tu chumbani”



    Kisha wakaelekea chumbani na moja kwa moja wakaenda kitandani ambapo ibra alikuwa akimuangalia sana mke wake kwani aliona wazi kuwa lazima atakuwa anaumwa tu ila anajikaza.



    Kulipokucha, asubuhi na mapema Ibra akamuamsha mke wake ili aweze kujiandaa na waweze kwenda hospitali ambapo Sophia alifanya hivyo ila alipomaliza kujiandaa akamwambia mume wake,



    “Lakini unajua Ibra mi siumwi kabisa na wala hata sijisikii vibaya”



    “Unaweza ukajiona kuwa huumwi kumbe ugonjwa upo ndani kwa ndani, usifikiri ni kitu rahisi kutapika vile Sophia usiwe mbishi kwani mi nakuona kabisa kuwa unaumwa”



    “Na hospitali tutaenda kujielezaje sasa?”



    “Tutajieleza kama hali halisi ilivyo”



    “Ila bado mimi sidhani kama naumwa kwani nahisi ni uchovu wa jana tu”



    “Uchovu wa jana umefanya kazi gani?”



    Sophia akafikiria kidogo na kukumbuka kuwa aliloweka nguo,



    “Mmmh jana nililoweka nguo ila sikuzifua mmh si zitanuka jamani maana nilisahau kabisa”



    “Basi usijali tutafua pamoja tukirudi”



    Sophia akatabasamu kisha akatoka na mume wake kwa lengo la kwenda huko hospitali, ila alipofika malangoni akakumbuka kitu kwenye zile nguo alizokuwa ameloweka jana yake ikabidi amwambie mumewe amsubiri akachukue.



    Alipofika uwani ambako aliloweka zile nguo alikuta zote zikiwa kwenye kamba tena zilionekana kukauka kabisa, kwakweli Sophia akashangaa sana na kumita Ibra kwa nguvu ili kumuonyesha kile anachokiona.



    Ibra nae alifika kwa haraka sana kama alivyoitwa na Sophia, kisha Sophia akamuonyesha nguo kwenye kamba ambapo Ibra aliuliza kwa mshangao



    “Kwani vipi Sophy?”



    “Nguo kafua nani?”



    “Nguo kafua nani kivipi?”



    “Kwani wewe huoni nguo kwenye kamba?”



    “Naziona ndio kwani tatizo nini?”



    “Nani kazifua sasa wakati mimi niliziloweka tu!”



    Ibra alikuwa akimshangaa tu mkewe ambapo kabla hata hajasema chochote, Sophia alianguka chini na kuzimia.



    Ibra alikuwa akimshangaa tu mkewe ambapo kabla hata hajasema chochote, Sophia alianguka chini na kuzimia.

    Ikabidi Ibra ambebe mke wake na kwenda kumpakia kwenye gari kisha kumpeleka moja kwa moja hospitali huku akihisi kuwa pengine mkewe ana maralia imempanda kichwani ndiomana anaongea mambo yasiyoeleweka.

    Walifika hospitali na moja kwa moja kupokelewa na wahudumu wa hospitali ile ambapo muda kidogo tu Sophia alionekana kuzinduka na kuwa sawa kiasi ambapo Ibra aliingia na mkewe kwa daktari na kuelezea kwa kifupi matatizo ya mke wake ambapo daktari aliwatajia vipimo vya kupima.

    Walimaliza kufanya vipimo na wakaa mapokezi wakisubiri majibu na kuitwa na daktari. Muda wote Ibra alikuwa akimtazama mkewe kwani alimuona kama mtu mwenye matatizo sana kwa kipindi hicho, Sophia alimuuliza mumewe,

    “Mbona unaniangalia sana bila ya kusema chochote?”

    “Kwakweli sina usemi mke wangu ingawa kuna mambo mengi sana najiuliza kuhusu wewe”

    “Kama mambo gani?”

    “Nadhani tutaongea zaidi tukirudi nyumbani, ngoja kwanza daktari atupe majibu ya vipimo ulivyofanyiwa”

    Muda kidogo daktari aliwaita na walipoingia ofisini tu daktari alianza kwa kumpongeza Ibra,

    “Hongera sana bwana Ibra, mkeo ni mjamzito”

    Ibra akatabasamu kiasi kisha akamuuliza daktari,

    “Kwahiyo tatizo lake ni mimba tu au kuna lingine?”

    “Hakuna lingine lolote, ni mimba tu. Tena itakuwa vyema kama mkiwahi kuja kuanza na kliniki ili kujua maendeleo ya mtoto aliyeko tumboni”

    “Sawa daktari, kwahiyo hakuna tiba yoyote anayoweza kupatiwa?”

    “Mr. Ibra, mimba si ugonjwa wa kutibiwa huwa ni hali tu inatokea kwa mwanamke kutokana na kile kitu tofauti kinachojitengeneza kwenye mwili wake. Cha muhimu kujua kuwa mkeo ana mimba na unatakiwa kuwa nae karibu sana ili uweze kumsaidia baadhi ya mambo. Mkianza kliniki mtajifunza mengi zaidi kwahiyo mzingatie hilo.”

    “Sawa basi tumekuelewa daktari, tutafanyia kazi ushauri wako”

    Kisha daktari akampatia Sophia dawa za vitamin ambazo zingemsaidia kiasi kwa hali aliyokuwa nayo kwa kipindi hicho halafu wakaanza safari ya kurudi nyumbani kwao.



    Walipokuwa njiani kurudi wanapoishi, wakamuona mtoto mdogo barabarani kwa makadirio anaweza akawa kwenye miaka mitatu, alionekana kusimamisha gari yao kanakwamba anaomba msaada ila Ibra alipita bila kusimama ambapo mbele Sophia alimshika mkono na kuonyesha kutokufurahishwa na kitendo cha Ibra cha kumpita mtoto Yule aliyeonekana kutaka msaada.

    “Hivi Ibra inamaana Yule mtoto hukumuona?”

    “Aaah Sophy, mtoto mdogo kama yule anawezaje kusimama barabarani na kusimamisha gari jamani!! Mambo mengine tutumie akili ya ziada tu mke wangu”

    “Sijapenda Ibra yani sijapenda kabisa kabisa”

    “Kwahiyo unatakaje?”

    “Turudi ili tujue ana tatizo gani”

    “Hivi unajua kama hata majambazi wanawatumiaga watoto wadogo mke wangu! Tusije tukajitafutia matatizo bure jamani”

    “Hata kama turudi tu kwakweli, hivi wewe huna hata huruma jamani! Mtoto mdogo vile unaanza kumuwekea imani za majambazi mmh! Turudi tafadhari.”

    Ibra hakutaka kumkwaza mke wake tena ukizingatia kwa ile hali yake ya ujauzito aliyoambiwa na daktari, hivyobasi akarudisha gari nyuma kwa lengo la kumfata Yule mtoto.

    Walifika pale ambapo Yule mtoto aliwasimamaisha na walimkuta pale pale ambapo Ibra alisimamisha gari kisha Sophia akashuka na kumchukua Yule mtoto kisha akapanda nae kwenye gari na kujaribu kumuuliza anapoelekea ambapo Yule mtoto aliwaonyesha kwa kidole tu anapoelekea kisha Ibra akaondoa gari na kuanza kwenda alipoonyesha Yule mtoto.

    Walifika mahali kisha Yule mtoto akasema,

    “Simama hapa hapa”

    Ibra alisimamisha gari ila kwa hofu kiasi kwani hakutegemea kama Yule mtoto anaweza kuonngea ukizingatia mwanzo aliwaonyesha kwa mkono tu.

    Kisha Sophia akafungua mlango kwa vile alikuwa amempakata mtoto huyo na kumshusha akizani labda kuna maelekezo mengine Yule mtoto atayatoa, ila Yule mtoto alivyoshuka tu aliwatazama na kuwaambia,

    “Asanteni kwa kunikaribisha rasmi kwenye maisha yenu”

    Akapunga mkono kisha akaondoka kwa kukimbia ambapo kwa sekunde chache tu alipotea kwenye macho yao.

    Ibra na Sophia wakatazamana kisha Ibra akamuuliza mkewe,

    “Hivi umemuelewa huyu mtoto?”

    “Mmmh hata sijamuelewa”

    Ibra nae akaguna kisha akaondoa gari mahali pale na kuendelea na safari yao ya kurudi nyumbani.



    Walipofika nyumbani ilionyesha wazi kuwa Ibra alichoshwa kabisa na Yule mtoto ambaye walikutana nae njiani kwani ilikuwa ngumu sana kwake kuelewa msaada ambao Yule mtoto aliuhitaji kutoka kwao, kisha akamuuliza tena mke wake

    “Hivi Yule mtoto ulimuelewa?”

    “Hapana hata sikumuelewa”

    “Safari ijayo usiwe na roho ya huruma kiasi kile itatuponza, huruma muda mwingine sio nzuri”

    “Lakini tumepungukiwa na nini mume wangu kumsaidia Yule mtoto jamani? Hata Mungu atatuongezea thawabu”

    “Thawabu zipo ila si kwa staili ile ya Yule mtoto, natumaini hakuwa na nia mbaya juu yetu”

    “Mtoto Yule bhana hawezi kuwa na nia mbaya kwakweli”

    “Sawa”

    Kisha Ibra akabadilisha mada na kumpongeza mke wake kwa mimba aliyobeba,

    “Hongera sana mke wangu, sasa furaha yetu itaenda kukamilika”

    Sophia akatabasamu kisha akamsogelewa mumewe na kumkumbatia kwani aliona mawazo yake yakianza kutimia juu ya wao kuwa na watoto wa kutosha mule ndani.

    “Hongera na wewe pia mume wangu maana hii ni furaha yetu wote”

    “Yani sipati picha kumshika mwanangu akizaliwa maana nitafurahi sana kumuona kwakweli, itakuwa furaha kubwa sana ya maisha yangu”

    “Mimi je! Nitafurahi sana sana maana sasa nitakuwa nimepata mtu wa karibu, siku ya kwanza kumshika na kumnyonyesha nitafurahi sana”

    Walionekana kutabasamu na kufurahia ambapo muda huu ibra alionekana kumuuliza mkewe kuwa atapendelea kula chakula gani maana alitaka kujitolea siku hiyo kupika kwaajili ya mke wake, Sophia akatabasamu na kumjibu mumewe kuwa atakula chakula chochote tu.

    “Leo nitakupikia mwenyewe Sophy, tafadhali wewe pumzika tu hapo nipike fasta fasta tule”

    Sophia akatabasamu na kukaa kwenye kochi huku akihisi kuwa mumewe anafanya mbwembwe tu kwani alijua muda wowote atamshtua kuwa akapike mwenyewe, Ibra alienda jikoni na kumuacha Sophia pale sebleni ambapo kwa muda mfupi kabisa Sophia alipitiwa na usingizi pale pale kwenye kochi.



    Wakati Sophia amelala pale kwenye kochi akajiwa na ndoto ambapo kwenye ndoto hiyo akamuona Yule mtoto waliyemkuta kule njiani, alionekana akitabasamu huku akimuangalia Sophia na kumwambia,

    “Nitakuwa nakusaidia kazi zote ngumu na hata zile nyepesi zikiwa nyingi nitafanya mimi, napenda ukarimu wako ila huyo mtoto ajaye atakuwa ni ndugu yangu mimi sababu yeye nitampenda zaidi”

    Sophia alijikuta akimuuliza huyu mtoto,

    “Kivipi?”

    Huyu mtoto alionekana akicheka tu bila kuongeza neon la ziada na kumfanya Sophia ashtuke sana kwenye ile ndoto na kujikuta kama akipiga kelele hivi ambapo Ibra alimfata mbio na kumuuliza kuwa kuna tatizo gani.

    “Vipi Sophy mke wangu ni nini tatizo?”

    “Mmh nimeota ndoto hata siielewi”

    “Ndoto gani hiyo?”

    “Nimemuota Yule mtoto tuliyemkuta njiani”

    “Sophy mke wangu nakuomba uachane na habari za Yule mtoto kwani naona wazi zitakuchanganya tu, yani fanya hivi kwenye akili yako kuwa hatujawahi kukutana na Yule mtoto maana bila ya hivyo sidhani kama itakuwa rahisi kumsahau. Bora ujiwekee kuwa hatujawahi kukutana nae kabisa, Yule mtoto hafai kumuweka akilini kwani hakuwa mtoto wa kawaida kabisa”

    “Kwanini unasema hakuwa mtoto wa kawaida?”

    “Wewe fikiria hata alipoingia tu kwenye gari alionyesha kuziendesha akili zetu na kujikuta tukifanya anavyotaka yeye kamavile kumpeleka pale alipopataka tena kwa maelekezo ya kidole tu, kwakweli Yule mtoto si wa kawaida hatutakiwi kumuweka akilini mke wangu.”

    “Sawa nimekuelewa mume wangu”

    “Twende basi tukale”

    “Mmh hata nina hamu ya kula basi!!”

    “Njoo tule hivyo hivyo mdogo mdogo”

    Ikabidi Sophia asogee na mumewe mezani na kuanza kula, kwakweli alimpa hongera mumewe kwa chakula kile maana kilikuwa kitamu sana,

    “Asante ingawa nimekipika kawaida tu yani hata mimi mwenyewe nashangaa kuwa kitamu hivi”

    Sophia akatabasamu kwani mumewe alimshangaza sana kusema kuwa hata yeye anashangaa utamu wa chakula wakati kakipika mwenyewe.

    Walipomaliza kula, Sophia alitoa vile vyombo na kuvipeleka jikoni kisha akaviosha ambapo muda huo Ibra alikuwa sebleni.



    Sophia alipomaliza kuosha vile vyombo, iakamjia kumbukumbu ya zile nguo chafu ambazo aliziloweka pia ikamjia kumbukumbu ya vile alivyozikuta kwenye kamba kuwa zilishafuliwa na kuanikwa, ni hapo hapo akakumbuka kuwa hiyo ndio sababu iliyomfanya azimie hapo kabla.

    Kwahiyo alipotoka jikoni tu, moja kwa moja akaelekea uwani ambako huwa anafua nguo zake, alipofika uwani safari hii hakuona nguo yoyote cahafu wala za kwenye kamba hakuziona. Akapata wazo la kwenda chumbani kuangalia, ambapo alifika chumbani na kufungua kabati alikuta zile nguo zote zilishakunjwa na kupangwa kabatini, kwakweli Sophia akaguna na kujiuliza kidogo.

    “Inamaana Ibra ndio kafanya haya mambo? Ndio lazima tu atakuwa yeye tu maana hakuna mwingine wa kufanya haya.”

    Kisha Sophia akatoka chumbani na kurudi sebleni na kwenda kukaa karibu na Ibra kisha akamwambia,

    “Asante mume wangu kwa kunisaidia udobi”

    “Udobi? Udobi gani tena?”

    “Si zile nguo chafu umezifua zote na kuzianua kisha umezipanga kabatini”

    “Mmh mbona kama sikuelewi!”

    “Hunielewi kivipi wakati zile nguo umeshaanuwa na kupanga kabatini”

    Ilionyesha Ibra alikuwa haelewi kitu kwakweli, ikabidi Sophia amshike mkono na kumpeleka mpaka uwani pa kufulia ambapo hapakuwa na nguo yeyote kwenye kamba, kisha akampeleka chumbani na kufungua kabati ambapo ilionyesha nguo zikiwa zimepangwa vizuri kabatini, Ibra akamtazama Sophia na kumuuliza

    “Nani kafanya yote haya?”

    “Unaniuliza mimi tena! Si wewe hapo”

    “Sijafanya hiki kitu mimi”

    Wakajikuta wakitazamana kwa muda kidogo, huku wakiwa na hofu kwa mbali.



    Ilionyesha Ibra alikuwa haelewi kitu kwakweli, ikabidi Sophia amshike mkono na kumpeleka mpaka uwani pa kufulia ambapo hapakuwa na nguo yeyote kwenye kamba, kisha akampeleka chumbani na kufungua kabati ambapo ilionyesha nguo zikiwa zimepangwa vizuri kabatini, Ibra akamtazama Sophia na kumuuliza



    “Nani kafanya yote haya?”



    “Unaniuliza mimi tena! Si wewe hapo”



    “Sijafanya hiki kitu mimi”



    Wakajikuta wakitazamana kwa muda kidogo, huku wakiwa na hofu kwa mbali. Kila mmoja alihisi kuwa mwenzake kuna kitu anamficha hivyo wakajikuta wakiwa kimya kwa muda.



    Ibra akaona ni vyema kupotezea hayo mambo ili asije akalumbana na mke wake bure, kwahiyo alichokifanya ni kumshika mkono na kurudi nae sebleni kisha kuanza kuongea nae mambo mbalimbali kuhusiana na mipango yake.



    “Sophy mke wangu, inatakiwa katika akili zetu sasa tuanze kupanga mipango kuhusu mtoto wetu ajaye, kwanza kabisa nakushukuru sana mke wangu kwa hiyo zawadi uliyoibeba tumboni mwako kwaajili yangu”



    Sophia akatabasamu kwani maneno ya mume wake yalimpa faraja sana, kisha nae akamwambia mumewe,



    “Hata mimi nina furaha sana kwani ile ndoto yetu ya kuwa na watoto wane naiona ikitimia kabisa.”



    “Kwahiyo umepanga mdogo wake huyu aje baada ya muda gani?”



    “Yani huyu akifikisha miaka miwili tu namletea mdogo wake”



    “Lakini nasikia kwenye uzazi wa mpango huwa wanasema angalau watoto wapishane miaka mitano mitano ili kila mmoja apate yale malezi ya kutosha ya kitoto”



    Sophia akacheka kidogo na kumwambia mumewe,



    “Achana na hayo mambo ya wataalamu na hao wa uzazi wa mpango mume wangu, katika maisha kila mtu huwa anajipangia mambo yake mwenyewe, kwetu tumezaliwa tisa tena mama alituachanisha kidogo sana, mwingine kampita mwenzie miaka miwili, mwingine mmoja, mmoja na nusu lakini wote tumekuwa vizuri tu hatuna kasoro wala dosari yoyote kama unavyotuona.”



    “Kasoro ipo Sophy”



    “Kasoro gani?”



    “Kwanza kabisa kwenu mmezaliwa wengi kushinda uwezo wa wazazi wenu, pili mlipishana karibu sana. Angalia mlivyo ni nani aliyebahatika kusoma kwenu hata aweze kuitwa msomi labda”



    Sophia akanuna kiasi kisha akamuuliza Ibra,



    “Kwahiyo kusoma ndio kasoro? Mbona nyie mpo wachache kwenu na hata hamjasoma kivile!”



    “Ni kweli kwetu tupo wachache na hatujasoma hivyo ni kutokana na uwezo wa wazazi wetu ila uchache tuliokuwa nao umefanya tuweze kupambana na ugumu wa maisha. Kwakweli kwa upande wangu kaka zangu wote wamejikwamua kimaisha, kumbuka tupo watano nyumbani kwetu. Kaka zangu watatu walishajikwamua kimaisha, dada nae alijitahidi kujikwamua na sasa kaolewa huku akiendeleza gurudumu la maisha yani nilibaki mimi tu nyuma ambapo nami nimekomboka kwa sasa tena nimewapita wote kimaisha. Haya kwa upande wa kwenu yani mwenye afadhari ni wewe tu, angalia akili za dada zako zilivyo na Yule mdogo wako wa mwisho ni nini anafanya. Kaka zako je, bangi bangi na wao hapo kuna maendeleo gani ya kuwa wengi ambao hamueleweki? Kwa walivyo wazazi wenu wangewazaa wachache na uhakika wasingeshindwa kuwasomesha”



    Sophia akanuna zaidi na kumuuliza tena Ibra tena kwa kupaniki,



    “Tungekuwa wachache mimi ningekuwepo? Nakuuliza wewe ningekuwepo? Maana mimi kuzaliwa kwetu ni mtoto wa nane ndio akazaliwa Yule mdogo wangu, mara nyingine ujifikiriage kabla ya kuongea mambo ya kijinga jinga.”



    Kisha akainuka kwa hasira na kuelekea chumbani.



    Ikabidi Ibra ainuke na kumfata mkewe chumbani ili aweze kumbembeleza ambapo akamkuta akilia,



    “Jamani mke wangu usichukulie hasira yale yalikuwa ni maongezi tu wala sikuwa na nia mbaya”



    “Hukuwa na nia mbaya wapi wakati unaisema familia yangu!”



    “Nisamehe mke wangu tafadhali, nakupenda sana Sophy”



    “Yani mi kusema watoto wapishane miaka miwili miwili umeona ndio ishu, kuna watu wanahangaika na wake zao huko sababu hawataki kuzaa zaa watazeeka ila mimi niliyejitolea kwako unaniona mjinga poa bwana.”



    “Tafadhali mke wangu nisamehe, nakuomba nisamehe sana”



    Ibra akapiga na magoti kumuonyesha mkewe kuwa anajutia kitu alichoongea, kitendo cha Ibra kupiga magoti kikampa Sophia faraja na kujikuta akitabasamu na kufanya afurahi na mume wake.



    Kwavile ilikuwa ni jioni, Ibra akamuomba mkewe watoke kidogo wazunguke zunguke maeneo ya karibu kama kufanya zoezi la kutembea tu ambapo Sophy alikubali kisha akabadili nguo na kuwafanya watoke sasa.



    Walipokuwa nje ya nyumba yao, Ibra aliona kuna upande ambao hajawahi kutembelea toka walipohamia kwenye nyumba ile na kumuomba mkewe waelekee upande ule kidogo, kisha wakatoka pale na kuanza kuelekea ule upande.



    “Ila tusiende mbali sana nitachoka mwenzio”



    “Usijali Sophy, tunatembea kwa stepu hakuna haja ya kwenda mbali sana.”



    Wakiwa njiani wakaonana na Jane ambapo Sophia alisimama kwa tabasamu na kusalimiana na huyo Jane,



    “Shikamooni”



    “Marahaba, mbona hukuja tena nyumbani wakati uliniahidi kuwa utakuwa unakuja”



    Jane akatabasamu kidogo kisha akasema,



    “Kesho nitakuja dada hata usijali”



    Waliongea kidogo pale na kuagana nae.



    Alipoondoka, Sophia akamuuliza mumewe kama anamkumbuka Yule Jane,



    “Mmh hata simkumbuki”



    “Ndio Yule binti wa Yule mama jirani yetu ambaye mwanzoni kabisa nilikutana nae pale getini kwetu, na siku amekuja na binti yake hata wewe uliporudi uliwakuta”



    “Aaah nishawakumbuka, si unajua tena kichwa hiki kina mambo mengi”



    “Loh naona kweli mambo mengi maana hata hili ulikuwa hukumbuki kweli mambo yanakutinga”



    Kisha wakaendelea na matembezi yao ya hapa na pale, kuna mahali palikuwa na kimlima kidogo ambapo Ibra akashauri warudi tu kwani alihisi kupanda kile kimlima kutamfanya mkewe achoke sana,



    “Turudi nyumbani Sophy”



    “Aah jamani, tusogee sogee kidogo yani mi ndio ushanitamanisha na kutembea, twende tukaishie pale kwenye kimlima”



    “Ila si unaona giza nalo limeanza kuingia”



    “Ndio naona ila tuishie hapo kwenye kimlima”



    Ibra hakumpinga kwavile aliyekuwa akimuonea huruma ni yeye mwenyewe, kwahiyo wakaendelea mbele kidogo na kuanza kupandisha kale kamlima.



    Walipofika juu kidogo kulikuwa tena na kamteremko kakushuka chini ila kuna kitu kilimshtua Sophy kwa kule chini na kumfanya amkumbatie mumewe kwa nguvu,



    “Nini tena Sophy?”



    “Ona kule chini”



    Ibra alipoangalia akamuona tena Yule mtoto wa mchana akiwatazama kamavile anaomba msaada, Ibra akamshika mkewe mkono na kurudi nae nyuma kisha kugeuza na kuanza kurudi nyumbani huku akiongea,



    “Yani mimi nikikataa kitu ujue lazima kuna tatizo ona sasa bora hata tungerudi pale pale nilipokataa”



    Sophia hakujibu chochote zaidi ya kukokotana na kurudi nyumbani.



    Walifika nyumbani, ila Sophia alidai kuchoka sana na kuelekea chumbani kulala ambapo ibra nae alielekea chumabani na kulala pembeni ya Sophia kwa kumkumbatia ili aweze kuwa na amani.



    Wakati usingizi umemkolea kabisa Sophia akajiwa na ndoto, akamuona tena Yule mtoto akiwa pale pale chini kidogo ya kile kilima ambapo kwenye ndoto hii Sophia alijiona akimfata Yule mtoto alipo na kumuuliza kuwa tatizo ni nini, kisha Yule mtoto akamwambia,



    “Sina ubaya na wewe Sophia, una moyo wa kujali halafu una upendo sana ila tatizo ni huyu mume wako hana huruma kabisa. Je ungependa nimfanye nini?”



    Sophia akawa kama anamshangaa huyu mtoto na kumuuliza,



    “Umfanye nini kivipi na kwanini?”



    “Mumeo ana roho mbaya sana Sophia, sipendi watu wasio na huruma wakati mimi huwa nakusaidia mambo mengi sana. Niambie basi nimfanye nini?”



    “Hapana usimfanye chochote mume wangu”



    “Usiwe na huruma hivyo Sophia kwa mtu asiye na huruma, yani mimi hata ukiniambia nimuue sasa hivi huyu mumeo namuua”



    Sophia akashtuka kutoka kwenye ile ndoto na kupiga kelele huku jasho jingi likimtoka na kufanya Ibra nae ashtuke na kumuuliza mkewe kuwa tatizo ni nini,



    “Vipi Sophy?”



    Sophia alikuwa akihema juu juu na kumjibu mumewe,



    “Nimeota ndoto mbaya sana”



    “Mmmh pole mke wangu, hiyo ndoto inahusu nini?”



    “Nimemuota tena Yule mtoto eti alitaka kukuua wewe”



    Ibra akatabasamu kwavile hakuwa mtu wa hofu kwa mambo kama hayo haswa ya kuhusu ndoto, kisha akamwambia Sophia,



    “Mke wangu, usiwe na wasiwasi juu yangu halafu ndoto za namna hiyo zisikutishe sana. Mimi ni mwanaume jasiri siwezi kuteketea kirahisi hivyo. Pia naomba Yule mtoto umtoe mawzzoni mwako mke wangu tafadhali”



    Kisha Ibra akainuka na mkewe na kwenda kuoga ili angalau kupata nguvu mpya na kuondoa uchovu uliopita hata iwasaidie kuanza upya usingizi.



    Walimaliza kuoga na kurudi tena kulala.



    Kulipokucha, Ibra aliamka na kujiandaa kwenda kwenye mahangaiko yake kisha akamuaga mke wake na kumwambia kuwa endapo kutatokea tatizo lolote basi asisite kumpigia simu.



    “Usijali nitakujulisha mume wangu”



    Kisha Ibra akmbusu mkewe kwenye paji la uso na kumuaga.



    Sophia hakuweza kuendelea kulala kwani muda ule ule aliamka na kwenda sebleni akiwa amejikalia tu kisha muda kidogo akafanya kazi zake za hapa na pale kisha kupumzika tena.



    Akiwa pale sebleni alisikia hodi na kwenda kufungua ambapo aliyeingia alikuwa ni Jane hivyo kumfanya Sophia afurahi sana kwa kupata kampani ya muda ule.



    “Bora Jane umekuja maana nilikuwa mpweke sana”



    “Ndiomana nikaamua kutimiza ahadi yangu”



    Sophia alimkaribisha vizuri sana Jane na kukaa pamoja sebleni huku wakizungumza mambo mbalimbali, ambapo Sophia alimuuliza Jane,



    “Hivi huwa unafanya nini ukiwa nyumbani mwenyewe, ukiachana na kazi za nyumbani”



    “Kwakweli dada mi napenda sana kusoma stori haswa stori za kutisha”



    “Kheee wa ajabu wewe sasa stori za kutisha unazipendea nini?”



    “Yani mi huwa napenda tu halafu huwa naona kama kweli vile”



    “Basi mimi katika vitu ambavyo sipendi ni kusoma stori haswaa za kutisha sababu huwa naona ni uongo mtupu. Waandishi wanaandika vitu vya kidhahania yani havina ukweli wowote.”



    “Mmh ila vingine vina ukweli dada, mfano mamabo ya misukule”



    Sophia akacheka sana,



    “Yani Jane na usomi wako wote bado unaamini kuhusu misukule! Hakuna kitu kama hicho duniani, tatizo lako hizo stori zimekukaa kichwani, ushawahi kuona msukule wewe? Zaidi ya kuona kwenye sinema na kusoma kwenye stori, hakuna kitu kama hicho”



    “Lakini dada mara nyingi wanaoandika stori huwa ni mambo ambayo yapo kwenye jamii ndiomana yameandikwa”



    “Aaah ni propaganda tu hizo ili wapate wasomaji wengi hakuna ukweli wowote”



    “Ila kuna mambo ni mazuri na yanatufundisha kwakweli, mimi toka nianze kusoma hizi stori nimejifunza mambo mengi sana. Kwanza siwezi kulala bila kumuomba Mungu maana usiku wetu umezingirwa na mambo mengi, na pia nikiamka lazima nimshukuru Mungu na kuomba aniongoze siku hiyo ingawa mara nyingine nasahau kuomba nikiamka kwakweli”



    Hapo hapo akajicheka tena na kusema,



    “Aah hata leo yenyewe nimeshau kusali, kwakweli Mungu anisamehe tu”



    Sophia nae akacheka na kumwambia,



    “Hebu acha masikhara yako Jane, yani mi mtu haniambii kitu kuhusu mastori ya uongo yani siwezi kupoteza muda wangu nifatilie.”



    Kisha wakabadili mada na kuanza kuongelea mambo mengine.



    Mchana ulipofika Sophia alijisikia uchovu sana na kumuomba Jane akamsaidie kupika,



    “Mdogo wangu Jane naomba msaada tafadhali”



    “Sema chochote dada nitafanya”



    “Jikoni kuna ndizi nilizimenya na nyama ipo kwenye friji, unaweza kwenda kupika ili tule”



    “Aah usijali dada, jikoni ndio wapi?”



    Sophia akamuonyesha Jane mlango wa jikoni ambapo Jane aliinuka na kuelekea jikoni.



    Alipoingia alienda moja kwa moja na kufungua friji ambapo hakuona nyama yoyote ila alipoangalia kwenye jiko aliona sufuria imefunikwa vizuri kabisa akaamua kusogea na kufunua, kwanza akasikia harufu nzuri sana ya chakula na alipoangalia aliona ni ndizi zikiwa zimepikwa vizuri kabisa tena zikiwa na nyama na bado zilikuwa za moto. Kwakweli Jane alishangaa kiasi na kujiuliza,



    “Hivi kaniambia nije nipike au nimsaidie kupakua jamani! Mbona chakula alishapika tayari! Nadhani kaniambia nije nipakue.”



    Kisha akachukua bakuri kubwa na kupakua halafu akapeleka mezani na kuweka sahani halafu akamfata Sophia na kumwambia tayari.



    Sophia akamuangalia kwa makini na kumuuliza,



    “Tayari nini?”



    “Tayari chakula kipo mezani”



    “Mmh usinitanie Jane, haiwezekani zile ndizi ziwe zimeiva! Hebua acha utani”



    Akaelekea na Jane mezani ila bado Sophia hakuamini na kumuangalia vizuri Jane kisha akamuuliza,



    “Je wewe ni binadamu wa kawaida?”



    Jane akamshangaa Sophia kwa swali lile.





    Sophia akamuangalia kwa makini na kumuuliza,

    “Tayari nini?”

    “Tayari chakula kipo mezani”

    “Mmh usinitanie Jane, haiwezekani zile ndizi ziwe zimeiva! Hebu acha utani”

    Akaelekea na Jane mezani ila bado Sophia hakuamini na kumuangalia vizuri Jane kisha akamuuliza,

    “Je wewe ni binadamu wa kawaida?”

    Jane akamshangaa Sophia kwa swali lile.

    Kwakweli Jane hakuweza kumjibu Sophia kwani lile swali pia halikuwa la kawaida na hata hivyo Sophia hakuonekana kawaida kabisa kwani alionekana ni mtu mwenye mashaka na Yule Jane.

    Wakiwa bado wanatazamana, wakashtushwa na hodi na kufanya Sophia aende kufungua ambapo aliyeingia alikuwa ni mumewe Ibra ila muda huo huo Jane nae hakuweza kukaa kwani aliaga juu juu na kuondoka zake hata Ibra aliweza kuelewa kuwa lazima kuna tatizo kwavile hakuuelewa ule uagaji wa Jane na kuondoka.

    Ibra akamuangalia mkewe na kumuuliza kuwa ni nini tatizo, Sophia akaamua kumueleza mumewe jinsi ilivyokuwa hadi kupelekea hali ile, Ibra akasikitika na kumuangalia mkewe kisha akamwambia,

    “Unajua mke wangu kila siku napenda kukwambia kuwa uwe unafikiria kwanza kabla ya kuongea jambo lolote maana maneno yako huwa katika hali ya ukali sana. Nilivyokuzoea mimi ni tofauti na mwingine alivyokuzoea.”

    “Hivi unafikiri ningemuulizaje jamani? Tatizo Ibra hukuwepo, yani mtu nimemwambia muda huo huo kuwa akapike halafu muda huo huo anaenda jikoni na kuniambia chakula tayari! Inakuingia akilini kweli? Nakwenda mezani nakuta kweli ameshaandaa chakula mmh! Kwakweli kwa upande wangu imekuwa ngumu sana kujizuia kwa hiyo hali jamani maana haiwezekani tena haiwezekani kabisa.”

    Ibra akaongozana na mkewe mpaka mezani na kuangalia zile ndizi pale mezani kisha akachukua kijiko na kuzionja, halafu akakaa kimya kwa muda na kusema

    “Mmmh ndizi tamu sana hizi sijapata kuona yani na njaa yangu hii hebu kaa hapo tuanze kula”

    “Ila upikaji wake ni wa kustaajabisha mume wangu”

    “Achana na mambo ya upikaji, mi nakujua Sophy mke wangu usikute ulimuagiza binti wa watu akapike halafu ukapitiwa na usingizi, mtu anakwambia chakula kimeiva unashtuka na kuona ni muda huo huo kwavile ulipitiwa na usingizi, hebu kaa tule”

    Ibra akaweka chakula kwenye sahani na kuanza kula vizuri kabisa huku akimsisitiza Sophia nae aweze kula ambapo Sophia aliamua kula kutokana na vile ambavyo mumewe alimsisitiza.

    Kwakweli chakula kilikuwa kitamu sana na kufanya waifurahie ladha ya kile chakula lakini bado Sophia alikuwa na mashaka sana juu ya upikaji wa kile chakula hata imani yake juu ya Jane ikapungua kabisa.

    Walipomaliza kula, Ibra akamshauri mkewe kuwa waende wakamuombe msamaha Jane,

    “Mmmh sijui atanifikiriaje sasa!”

    “Usijali twende kisha mi nitazungumza nae maana mi ndio nakufahamu vizuri wewe”

    Basi wakakubaliana na kuinuka wakielekea kwakina Jane.



    Walipofika walimkuta mama Jane akiwa nje akichambua mboga, ikabidi Sophia ajichekeleshe kidogo na kuulizia kama Jane yupo,

    “Jane karudi ila kapitiliza moja kwa moja chumbani, ngoja nimuite”

    Mama Jane akamuita Jane kisha Sophia akakaa karibu na huyu mama akimsaidia kuchambua ile mboga, Jane alipotoka moja kwa moja Ibra akamuomba pembeni ili azungumze nae ambapo alisogea na Ibra kwaajili ya mazungumzo,

    “Jane samahani kilichotokea kati yako na mke wangu naomba umzoee tu”

    “Mimi sina tatizo nae ila sikumuelewa tu alivyokuwa akifoka na kuonyesha kunishangaa”

    “Pole sana mdogo wangu, unajua nini huyu Sophy huwa ana matatizo ya kusahau anaweza fanya jambo kisha akasahau halafu muda mwingine anasahau muda sababu ya kusinzia naomba umsamehe sana”

    “Mmh mi sikujua hilo, ila kama ana tatizo la kusahau basi sasa naweza kuelewa kwanini alikuwa akifoka vile. Nimemsamehe na wala sina mashaka nae”

    “Kama umemsamehe ni vizuri, na usisite kuja kuendelea kututembelea tafadhali maana pale nyumbani huwa anabaki mwenyewe na upweke.”

    “Ilimradi nimeshagundua tatizo lake basi haitanisumbua tena”

    Kisha Ibra akamuita mkewe na kuwapatanisha ambapo Sophia na Ibra wakaaga baada ya lile tukio na kuondoka, huku Sophia akimsisitiza Jane aende kumtembelea tena kesho yake.

    Walipoondoka tu, mama Jane akamuita binti yake ili kujua kilichoendelea kwani haikuwa kawaida kwa Jane kufatwa vile nyumbani kwao.

    Jane hakumficha mama yake, akamueleza kila kitu ambacho kimetokea siku hiyo.

    “Mmh kwahiyo chakula alishapika akasahau na kukwambia wewe ukapike?”

    “Ndio hivyo mama, maana alinipa maelekezo sijui nyama ipo kwenye friji niitoe kisha niipike na ndizi, kuingia jikoni hakuna nyama kwenye friji ila nilipofunua sufuria nakuta ndizi zilishapikwa tayari tena zimenona balaa dah kafanya nimeondoka bila hata ya kula hata kidogo.”

    “Kama ndio hivyo basi kusahau kwake ni babkubwa maana mmh! Mtu unasahau kabisa kama ulishapika, ila ni bora mumewe anajua tatizo la mke wake.”

    “Ndio, kaniambia nimchukulie kama alivyo sababu ni tatizo lake la kusahau”

    “Mmh haya mwanangu ila siku nyingine uwe makini na maneno yake”

    Jane akakubaliana pale na mama yake kisha akarudi zake ndani huku akiamini kuwa Sophia alipika zile ndizi ila amesahau kutokana na tatizo lake la kusahau.



    Ibra na Sophia walipofika nyumbani moja kwa moja Ibra akakumbuka kitu,

    “Aaah! Hata nimesahau kumshukuru Yule binti kwa chakula kitamu, kwakweli anajua sana kupika”

    Sophia akamuangalia mumewe na kumuuliza,

    “Inamaana anajua kupika kushinda mimi?”

    “Mmh mke wangu jamani huo sasa ni wivu, mimi nimemsifia tu wala sijasema kama amekupita wewe. Hata hivyo hakuna anayekufikia wewe mke wangu kwa chochote wala lolote”

    Sophia akatabasamu kwani hizi sifa alizopewa na mumewe zilimfanya ajisikie vizuri sana, kisha Sophia akainuka na kuelekea meza ya chakula halafu akamuuliza mumewe,

    “Wakati tunaondoka hivi tulitoa vyombo mezani kweli?”

    “Mmh mi sikumbuki ila mezani nilikuacha wewe halafu niakenda kukaa kwenye kochi kwani vipi?”

    “Kwa kumbukumbu zangu sikumbuki kama nilitoa vyombo kwakweli ila naona vimeshatolewa je nani kavitoa?”

    “Aah Sophia jamani unakoelekea mke wangu siko kabisa yani mmh wewe kila kitu kwako kipo nyuma mbele. Kuna mtu aliniambia kuwa wanawake wajawazito huwa na tabia ya kusahau kwakweli leo naamini maneno yake. Hebu njoo kwanza mke wangu tujadili mambo ya msingi. Leo nimerudi mapema hata huniulizi kwanini mapema ila kila muda unazuka na jipya sijui ndio maisha gani haya mke wangu.”

    Sophia akaamua kusogea pale sebleni na kukaa na mumewe ingawa katika kichwa chake kilikuwa na maswali mengi sana ila aliamua kuyapuuzia kwa muda, kisha akamuuliza mumewe kuhusu kuwahi kurudi kwake,

    “Eeh mbona leo umewahi kurudi sana?”

    “Kwanza kabisa leo nilipokuwa kazini mawazo yangu yote yalikuwa juu yako kwani nilikuwa nikiwaza juu ya upweke ambao utakuwa nao. Ndiomana nimewahi kurudi ili nikuliwaze mke wangu.”

    Sophia akatabasamu kwavile aliyapenda sana maneno ya mumewe ya kumbembeleza, kisha Ibra akaendelea kuongea,

    “Halafu nimepata wazo mke wangu, kwanini tusiwe na msichana wa kazi humu akusaidie saidie”

    “Msichana wa kazi! Wa nini mimi? Kwakweli huwa sina imani na hao wasichana wa kazi mume wangu jamani nisije nikaibiwa bure bora ufikirie jambo lingine”

    “Uibiwe nini mke wangu?”

    “Nitaibiwa wewe”

    “Mmh yani huo wivu wako majanga loh! Basi itabidi ukamshawishi mdogo wako Tausi aje hapa au unaonaje?”

    “Hapo sawa, basi tutapanga ili nikaongee na mama nije nae hapa huyo Tausi anisaidie saidie ukizingatia hasomi wala nini”

    Wakakubaliana pale kisha Ibra akaamua kwenda kuoga kwanza kuondoa uchovu wa siku hiyo ambapo alipomaliza kuoga akamwambia na mke wake nae akaoge, Sophia akainika na kwenda kuoga ila alikuwa na mawazo mengi sana mule bafuni haswa kwa mambo ambayo yanamtokea halafu hayaelewi elewi, alikuwa akijiuliza vitu vingi sana bila ya kupata majibu.

    Alipotoka bafuni alimkuta Ibra akiwa kitandani amejilaza ambapo Ibra alimuita mke wake huyu ili aende pale kitandani na wajumuike nae.

    Sophia alisogea karibu na alipo mumewe ila alimuangalia tu na kufanya Ibra amuulize,

    “Sophy mke wangu mbona wanitazama tu kama hujui nilichokuitia? Unajua nimekumiss sana mke wangu”

    Kisha Ibra akamsogelea kwa karibu Sophia na kumkumbatia huku akimpapasa, iala Sophy alionekana kutofurahishwa kabisa na kumfanya Ibra amuulize kwa kumshangaa,

    “Vipi Sophy mke wangu nini tatizo?”

    “Sijisikii”

    “Hujisikii kivipi?”

    “Kwani mtu akisema hajisikii huelewi au?”

    Halafu Sophia akainuka pale kitandani na kuelekea sebleni, kitendo hicho kilimfanya Ibra amshangae sana mke wake na moja kwa moja akafikiria kuwa ni mimba iliyomfanya awe katika hali ya namna ile kwani katika maisha yao ya kawaida haijawahi kutokea hata mara moja Sophia kuongea maneno ya vile wala kumbishia mume wake katika tendo lile.

    Ibra alitulia tu pale chumbani akitafakari na kujiuliza kuwa imekuwaje kuwaje maana ilikuwa ngumu kwake kuelewa.



    Sophia alienda sebleni na kukaa kwenye kochi ila alijikuta akijifikiria sana kwa alichomjibu mumewe na moja kwa moja kujiona kuwa ana makosa, kwanza alijishangaa pia kuweza kumjibu mumewe vile wakati hajawahi hata siku moja kumkatalia hata kama akiwa hajisikii kweli.

    “Mmh hivi Ibra atakuwa ananifikiriaje jamani loh! Kwanini nimefikia hatua ya kumjibu vile wakati ni mume wangu? Nina kila sababu za kwenda kumuomba msamaha maana jambo nililofanya si la kawaida kwakweli.”

    Hivyobasi akainuka na kurudi tena chumbani ila alipoingia chumbani na kumuangalia Ibra pale kitandani hakumuona na kufanya ajiulize kuwa Ibra ameelekea wapi maana kama angetoka basi lazima angepita pale sebleni na yeye angemuona ila hakumuona kutoka, akajaribu kuita ila hakuitikiwa na Ibra. Moja kwa moja akahisi kuwa huenda Ibra yupo chooni hivyo akaamua kwenda chooni kumuangalia, ila alipofungua mlango wa choo hapakuwa na mtu yoyote na kumfanya Sophia apatwe na hofu moyoni.

    Akaamua kwenda kukaa tena kitandani, alifika na kukaa huku akiwa na mawazo mengi sana alijiinamia kwa muda kisha akaamua kujitupa kitandani huku akiwaza alipokwenda Ibra. Ila alipojitupa tu alishtuka sana kwani alihisi kuwa kuna mtu amemlalia, kitendo hicho kilimfanya Sophia ageuke kuangalia ni nini akamuona ibra akiwa amelala tena hana habari kabisa.

    Kwakweli Sophia alishtuka zaidi kwani mwanzoni hakumuona huyu Ibra hapo kitandani, akashangaa imekuwaje kuwaje.

    Akaamua kwenda kukaa tena kitandani, alifika na kukaa huku akiwa na mawazo mengi sana alijiinamia kwa muda kisha akaamua kujitupa kitandani huku akiwaza alipokwenda Ibra. Ila alipojitupa tu alishtuka sana kwani alihisi kuwa kuna mtu amemlalia, kitendo hicho kilimfanya Sophia ageuke kuangalia ni nini akamuona ibra akiwa amelala tena hana habari kabisa.

    Kwakweli Sophia alishtuka zaidi kwani mwanzoni hakumuona huyu Ibra hapo kitandani, akashangaa imekuwaje kuwaje.

    Aliamua kumtingisha Ibra na kumuamsha ambapo Ibra aliamka huku akimshangaa Sophia kwa kumuamsha kwa nguvu vile,

    “Yani kwa muda mfupi tu Ibra ndio umelala usingizi wa kiasi hicho? Kwanza niambie ulienda wapi?”

    “Kwenda wapi kivipi?”

    Ibra alikuwa akimshangaa mkewe, kisha Sophia akamueleza vile ambavyo yeye alikwenda sebleni na alivyorudi chumbani bila ya kumkuta pale kitandani na alipojaribu kumuita na kumuangalia sehemu mbalimbali bila ya kumuona na vile alivyofika pale kitandani na kushtukia kuwa amelala.

    Kwakweli Ibra alijikuta akicheka tu huku akimuangalia mkewe mpaka Sophia akapata hasira na kumuuliza Ibra kwa ukali,

    “Sasa kinachokuchekesha?”

    “Jamani Sophia mke wangu kwakweli naona sasa hiyo mimba imeanza kukuendea kombo maana si kwa mambo unayoyafanya mmh!! Hivi inakuingia akilini kweli eti mimi usinikute hapa kitandani halafu urudi tena unikute, jamani aah! Mi nilikuwa nimelala hapa maana siwezi kubishana na wewe ukizingatia ushakataa ninachokitaka, ila uzuri ni kuwa natambua hali yako na ndiomana nikaamua kulala tu ila hilo swala lako la kutokuniona na kuniona ndio linanichekesha kwakweli”

    Ingawa Ibra aliongea hayo ila ilikuwa ngumu sana kumuingia akilini Sophia ukizingatia ni jambo ambalo anajua wazi limetokea hata kama ikiwa ni kupoteza kumbukumbu basi si kwa staili ile.

    “Sogea tulale mke wangu”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ibra akamkumbatia Sophia na kumsogeza karibu yake ili wapate kulala kwani aliweza kuona kuwa mawazo ya Sophia hayakuwa sawa kwa muda huo.



    Kulipokucha kama kawaida Ibra aliamka na kujiandaa kwaajili ya kwenda kwenye shughuli zake, kma kawaida yake akamuaga Sophia kuwa anatoka ila kabla hajatoka Sophia akamzuia kutoka na kufanya Ibra amshangae na kumuuliza,

    “Mbona unanizuia Sophy?”

    “Usiende kazini leo sitaki kubaki peke yangu”

    “Jamani Sophy mke wangu kwa staili hii tutaendelea kweli? Tutapata wapi pesa kwa ajili yetu na mwanetu mke wangu? Kwanini uwe hivyo jamani!”

    “Nisamehe Ibra ila sijisikii kubaki mwenyewe”

    “Basi inuka twende kwakina Jane tumuombe urudi nae hapa na ushinde nae, tafadhali tufanye hivyo mke wangu maana kazi nayo ni muhimu pia kwenye maisha yetu haya”

    Sophia akakubali juu ya hilo, kisha akainuka pale kitandani na kutoka pamoja na mumewe wakielekea kwakina Jane.

    Walifika na kuwagongea hata mama Jane alishangaa kuwaona asubuhi yote ile pale nyumbani kwake, ikabidi watumia Kiswahili cha kumvutia ili aweze kum,ruhusu Jane kwenda muda huo na Sophia nyumbani kwake. Mama Jane alielewa na kwenda kumuamsha Jane kisha kumwambia kuhusu ujio wa wakina Sophia.

    “Mmh mama asubuhi yote hii jmani?”

    “Naelewa kama ni asubuhi mwanangu ila hawa ni majirani zetu inapaswa kuwa nao karibu.”

    Jane akaamka na kutoka nje kisha kuwasalimia Sophia na Ibra halafu akawaambia akaoge kwanza ajiandae ndio aende, ila Sophia aksamuomba Jane,

    “Beba tu nguo, twende ukaoge nyumbani Jane”

    Jane akafikiria kidogo na kukubali, kisha akaenda kuchukua nguo na kutoka halafu wakaingia kwenye gari ya Ibra ambapo aliwaacha pale nyumbani kwake kisha yeye kuelekea kwenye shughuli zake.



    Sophia na Jane waliingia ndani ambapo kabla ya yote Jane aliomba kuonyeshwa uwani ili aweze kuoga na kujisafisha, Sophia alifanya hivyo kisha nay eye akaenda kuoga maana hata yeye alikuwa bado hajaoga kisha walipomaliza wakaandaa chai na kunywa halafu wakaanza stori za hapa na pale ambapo kwanza kabisa Sophia alimuomba msamaha Jane kwa kile ambacho kilitokea.

    “Usijali dada nimeshakusamehe”

    Sophia akatabasamu ingawa kiukweli bado alikuwa na maswali mengi sana moyoni mwake kuhusu hali halisi ya maisha yaliyopo pasle.

    Muda kidogo Jane alianza na stori zake,

    “Basi bhana jana usiku nimesoma stori hiyo inatisha hadi nikaogopa kulala, yani usingizi ukachelewa kuja balaa ndiomana mpaka saizi nina usingizi”

    “Yani wewe kwa stori zinazotisha hujambo, hivi unazipendea nini jamani? Mwenzenu stori ambazo hazina uhalisia wala huwa sizifagilii”

    “Uhalisia upo dada, unajua mara nyingine mtu unaweza ukalala halafu ukaota ndoto mbaya sana na usipokuwa makini ile ndoto inakutokea kwenye maisha halisi”

    “Sasa kuhusu ndoto mbaya unakuwaje makini hapo?”

    “Unajua inatakiwa ukiota ndoto mbaya ukishtuka tu Sali ili Mungu akuepushe nay ale mabaya uliyoyaota”

    “Mmmh ila Jane wewe unanifurahishaga sana, hayo mastori yako ya kutisha ndio yamekufundisha hivyo? Kitu kama kipo kipo tu hata mtu ufanye nini”

    “Ila na wewe dada kwa kupinga sikuwezi mmh. Ila kwakweli nina usingizi sana, nataka nilale tu hapa hapa kwenye kochi.”

    “Hakuna shida wewe lala tu”

    Sophia alitulia akiangalia runinga huku Jane akiwa amejilaza kwenye kochi.

    Wakati jane akiwa amelala hoi kabisa, Sophia akasikia kama vyombo vikilia jikoni na kumfanya ashtuke sana huku akisikilizia kwa makini, kadri alivyozidi kusikiliza ndivyo mlio wa vyombo ulivyozidi kwakweli uoga ukamshika na kumfanya amshtue Jane kutoka usingizini ambapo Jane alishtuka sana huku akimuangalia Sophia kwa mshangao.

    Sophia akamuuliza Jane kwa uoga flani hivi,

    “Umesikia hiko?”

    Ila muda huo ile sauti ya vyombo haikusikika tena na kumfanya Jane azidi kumshangaa Sophia kwavile yeye hakusikia kitu chochote kile.

    “Sisikii chochote”

    Sophia akakaa kimya kwa muda na kupumua kwa nguvu kanakwamba kitu ambacho kilikuwa kimetokea kilikuwa kikubwa sana, kisha Jane akamuuliza

    “Kwani kulikuwa na kitu gani kikilia?”

    Sophia alijikuta akishindwa kumjibu Jane kwani mdomo wake ulijawa na uzoito gafla.

    Walikaa pale wakitazamana ambapo Jane aliamua tena kujilaza kwenye kochi ila Sophia aliogopa hata kwenda chooni kwa muda huo.



    Mida ya mchana Jane alishtuka na kudai kuwa kwasasa usingizi umeisha na anaweza akafanya vitu vingine, kwavile Sophia aliogopa kwenda jikoni kutokana na mlio wa vyombo akaamua kumuomba Jane akapike chakula ili waweze kula.

    “Mmh dada usije ukanifanyia kama mambo ya jana!”

    “Hapana siwezi kufanya hivyo”

    “Haya ngoja niende huko jikoni, ila unataka nipike nini?”

    “Kuna maini kwenye friji, uyachukue halafu upike na wali”

    “Hakuna tatizo”

    Jane akainuka na kuelekea jikoni ili aweze kuandaa hiko chakula, ila alipofika jikoni kama alivyoona jana ndivyo alivyoona leo kuwa sufurua zimefunikiwa jikoni, akasogea na kufunua akaona maini yakiwa yameungwa vizuri sana tena yakiwa bado yamoto, kisha akafunua sufuria lingine ambapo napo akaona wali ukiwa umepikwa vizuri sana.

    Jane akatabasamu na kujiuliza zaidi kuhusu tatizo la Sophia,

    “Yani anapika mwenyewe halafu anasahau, basi hapo nikienda kumwambia mbona umeshapika atashtuka sana bora leo nisimwambie. Ngoja nirudi nimwambie vinachemkia nione kama anaweza kukumbuka kuwa ni yeye mwenyewe ndio alipika”

    Kisha Jane akatoka jikoni na kwenda sebleni ambapo alimwambia Sophia kuwa ameacha vinachemkia, akamuona Sophia akipumua kidogo kwavile aliona kuwa siku hiyo hakuna maajabu yaliyotokea halafu wakaendelea kupiga stori mbili tatu ambapo Jane alimuuliza Sophia kuhusu swala lake la kupoteza kumbukumbu,

    “Hivi tatizo lako la kupoteza kumbukumbu lilianza lini dada?”

    “Tatizo la kupoteza kumbukumbu! Mi sina tatizo la kupoteza kumbukumbu”

    Jane akacheka kisha akasema,

    “Ama kweli mgonjwa huwa hajijui, yani dada hujui kabisa kama una tatizo la kupoteza kumbukumbu?”

    “Sina hilo tatizo Jane, niamini jamani hilo tatizo sina kabisa”

    “Haya basi ngoja nikusimulie kitu, kuna stori moja nilisoma kuhusu misukule yani unaweza ukaishi na misukule ndani bile kugundua”

    Sophia akashtuka kidogo na kumuuliza Jane,

    “Kuishi nayo kivipi”

    “Unaweza ukashangaa unakaa kwenye nyumba labda umepanga kumbe mwenye nyumba ana misukule yake basi ukikaa unashangaa kama mtu kapita halafu humuoni huyo mtu kumbe ndio hiyo misukule”

    “Uwiii mbona yanatisha hayo mambo!”

    “Pole dada nilisahau kama hizi stori huzipendi”

    “Kweli sizipendi ila ngoja kwanza, mtu unawezaje kugundua kama misukule ipo ndani na unawezaje kuiepuka?”

    “Ila dada wewe si ulisema kuwa haya mambo ni ya kufikirika halafu hupendi stori za kufikirika, naomba niishie hapo, au umesahau kama ulisema kuwa hakuna misukule duniani ni stori tu wanazitunga”

    Kisha Jane akainuka na kuelekea tena jikoni huku akiwa amemuacha Sophia akiwa na maswali mengi sana. Cha kwanza aliwaza uwepo wa misukule na matukio ambayo huwa anayaona kwenye ile nyumba kwani kwa kifupi yalikuwa yakimstaajabisha.

    Jane akarudi tena na kumwambia kuwa ameshaandaa chakula mezani ila Sophia alijikuta akitaka kufahamu mengi sana kuhusu hiyo misukule na kujikuta akimuuliza maswali Jane ambapo jane akamuomba wakaulizane maswali hayo wakati wanakula.

    Sophia alielekea mezani na kujiwekea chakula huku Jane nae akiwa amejiwekea cha kwake kisha Sophia akamuuliza tena Jane ila Jane bado alimpa masharti.

    “Si vyema kuongea wakati wa kula dada, inatakiwa tumalize kwanza kula halafu ndio tutaendelea na maongezi”

    Walikuwa wakila pale ila kichwa cha Sophia kilijawa na maswali mengi sana.



    Walipomaliza kula jane alipeleka vile vyombo vyote jikoni kisha wakarudi kukaa sebleni ambapo Sophia akaanzisha tena maswali yake,

    “Tafadhali Jane naomba unijibu maswali yangu”

    “Haya niulize sasa nikujibu”

    “Je misukule inaweza kufua nguo?”

    “Kufua nguo! Mmmh! Sijui labda mwenye ile misukule akiiongoza”

    “Sasa misukule inaweza kufanya vitu gani?”

    “Mi ninachojua misukule inaweza ikala chakula chako ndani, huwa inapelekwa kulima nadhani hata mwenye misukule akiamua kuwa iwe inafua inaweza kufanya kazi hizo maana wale ni binadamu wa kawaida ila tu huwa wanaondolewa ufahamu”

    “Basi niambie mtu unawezaje kujua kuwa unaishi na misukule na vipi unaweza kuiepuka?”

    “Kuhusu kuishi nayo unaweza kugundua kama kukuta vitu vimefanyika ndani ndivyo sivyo ila kuiepuka sijui maana mi mwenyewe ile stori sijaimalizia”

    “Mmh je misukule inaweza ikamdhuru mtu?”

    “Misukule haina ufahamu dada, sidhani kama inaweza ikamdhuru mtu”

    Sophia akawa kimya kwa muda ambapo Jane akaendelea kuongea,

    “Kweli leo nimeamini kuwa kumbukumbu zako huwa zinapotea maana nakumbuka ulivyonikanusha kuhusu hizi stori halafu leo wewe ndio umekuwa wa kwanza kutaka kujua undani wake mmh kweli dada unasahau sana”

    “Unajua nini Jane, kiukweli hizo stori mimi huwa siziamini ila kuna mambo flani hivi yananichanganya ndiomana nikakuuliza ila siku moja utayajua tu”

    Wakiwa wanazungumza pale, Ibra nae akawa amerudi kutoka kwenye mihangaiko yake ambapo Sophia alimkaribisha mumewe na moja kwa moja akaenda kumpakulia chakula kwanza huku Ibra akimshukuru sana jane kwa kuweza kushinda na mkewe kwa muda wote toka ameondoka,

    “Usijali kaka, mi nipo pamoja nanyi”

    Sophia akamkaribisha mumewe mezani ambapo Ibra alikula chakula kile huku akikisifia sana kuwa ni kitamu, kisha akauliza

    “Nani kapika?”

    “Jane huyo”

    “Khee huyu mtoto anajua kupika sana”

    Sophia akatabasamua tu, baada ya Ibra kumaliza kula Sophia akatoa vile vyombo na kwenda kuviweka na vingine vichafu pale jikoni kisha akarudi sebleni ambapo Jane nae hakutaka kukaa zaidi kwani aliaga na kufanya Sophia na mume wake kuinuka na kumsindikiza ila hawakumfikisha hadi kwao, kisha Ibra akamuomba Jane uwepo wake kesho yake tena.

    “Tafadhali Jane naomba kesho tuje tukufate tena ushinde na mke wangu”

    “Hakuna tatizo kaka”

    Kisha wakarudi na kumuacha Jane nae akielekea kwao.



    Walirudi ndani huku Sophia akifurahia uwepo wa mume wake,

    “Kwakweli nafurahi siku hizi unawahi sana kurudi”

    “Lazima niwahi kurudi mke wangu maana siwezi kukuacha na hali yako hiyo”

    Sophia akamuacha mumewe akaoge kisha yeye akaelekea jikoni ili aoshe vyombo na aweze kukaa na mumewe kuzungumza mawili matatu.

    Alipoingoia jikoni alishangaa sana kuona vyombo vyote vimeoshwa na vimeshapangwa kabatini kwakweli alijikuta akipiga kelele na kumfanya Ibra amfate kwa haraka sana,

    “Vipi Sophia nini tena mke wangu?”

    “Misukule”

    “Misukule! Misukule imefanyaje?”

    Ibra alikuwa akimshangaa mkewe na kuangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kuna chochote.



    Alipoingoia jikoni alishangaa sana kuona vyombo vyote vimeoshwa na vimeshapangwa kabatini kwakweli alijikuta akipiga kelele na kumfanya Ibra amfate kwa haraka sana,

    “Vipi Sophia nini tena mke wangu?”

    “Misukule”

    “Misukule! Misukule imefanyaje?”

    Ibra alikuwa akimshangaa mkewe na kuangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kuna chochote.

    Ila Ibra hakuona chochote mule jikoni na kumuuliza tena mke wake,

    “Sophy, misukule kivipi?”

    “Misukule imeosha vyombo na kuvipanga”

    “Misukule imeosha vyombo na kuvipanga? Wee Sophy akili yako iko sawa kweli? Unajua misukule wewe?”

    Ibra alikuwa akimshangaa mke wake na kumuona kama ni mtu aliyekuwa akichanganyikiwa maana mambo aliyokuwa akiongea hayakuwa na mantiki yoyote ile.

    Aliamua kumuinua mkewe pale chini na kuelekea nae chumbani kwani alikuwa kama kapigwa na bumbuwazi.

    Walipokuwa chumbani sasa, Ibra aliamua kumuacha kwa muda kitandani kisha yeye kwenda kuelekea kuoga kama alivyokuwa amepanga.

    Kwakweli Sophia hakujielewa kabisa na kuhisi hadithi za Jane za kuhusu misukule zikianza kumuingia akilini vilivyo na kuona ni kweli ile nyumba yao ina misukule maana kila akiangalia yale matukio kengele ya hatari ndivyo ilivyozidi kulia katika ubongo wake.

    Wakati akiwaza hayo akasikia kama mlango wa sebleni ukifunguliwa na kufungwa kanakwamba kuna mtu kaingia au katoka ila akajiuliza kuwa itawezekanaje ikiwa alishafunga mlango huo wakati wanaingia ndani, kwakweli uoga ulimshika mpaka pale Ibra alipotoka bafuni kuoga na kumkuta mkewe akiwa amejikunyata.

    Ibra alimfata mkewe na kukaa naye karibu kisha akamkumbatia na kumuuliza kwa ukaribu zaidi,

    “Kwani nini tatizo mke wangu? Unajua Napata shida sana kukuelewa!”

    “Ibra hata mimi sielewi kwakweli yani sielewi kabisa kabisa”

    “Unajua kwangu inakuwa ngumu sana kwasababu sijawahi kuishi na mwanamke mjamzito maana inawezekana haya ni mambo ya kawaida kwa wajawazito ila mimi sielewei kwakweli. Inabidi unifafanulie mke wangu kuwa ni mambo gani yanakusibu au ni vitu gani unaviona ili nijue tunaanzia wapi kupata ufumbuzi”

    “Tatizo Ibra nikisema huniamini, hebu sikia tulitoka hapa tumeenda kumsindikiza Jane ila kulikuwa na vyombo vichafu jikoni, tumerudi ili nikavioshe nakuta vyote vimeoshwa wakati humu ndani tupo mimi na wewe tu. Nimekaa hapa nasikia mlango wa sebleni ukilia sasa hayo mambo yanamaana gani mume wangu?”

    “Mmh kama hayo mambo ni ya kweli basi kuna makubwa”

    “Mi nahisi kuna misukule humu ndani”

    “Hebu Sophia tusiongelee hizo habari maana usiku huo unakuja tutashindwa kulala”

    Kisha Ibra akamuomba mkewe ajiandae ili angalau watoke waende mahali wapate kubadilisha hali ya hewa.



    Sophia alipomaliza kujiandaa, yeye na mumewe wakatoka mule ndani na kufunga milango vizuri kabisa kisha wakapanda kwenye gari yao na moja kwa moja Ibra akaelekea na mkewe hotelini ili kutimiza lengo lake la kubadilisha hali ya hewa ila kichwani alikuwa na maswali mengi sana ambayo hayakuwa na majibu kwa wakati ule.

    Kikubwa alichowaza ilikuwa ni kama Sophia anaongea ukweli kuhusu yale matukio basi lazima kuna kitu kinaendelea kwenye ile nyumba yao, pia akawaza kuwa kama ni kweli basi huenda majirani zao ni wachawi.

    Ibra alikuwa kimya tu huku akinywa juisi taratibu ambapo Sophia akamuomba kuwa kesho yake ampitishe kwa Siwema ili akamsalimie,

    “Basi kesho asubuhi unavyoondoka naomba mi ukaniache kwa Da’ Siwema nikamsalimie maana nimemkumbuka sana.”

    “Mmh kwa nikujuavyo wewe utataka kumwambia mambo yanayotokea nyumbani, tafadhari usimwambie kabla hatujayafanyia ufumbuzi”

    “Wala hata sina nia hiyo ya kumwambia, mi nataka nikamsalimie tu”

    Ibra alikubaliana na mke wake ingawa alielewa wazi lengo la mkewe ni nini ukizingatia huwa hawezi kukaa na kitu moyoni, wakazungumza zungumza pale kisha wakarudi nyumbani.

    Wakati wanarudi kama kawaida wakamuona Yule mtoto akisimamisha gari yao kama ile siku ya kwanza ila kwakweli leo Ibra hakutaka huu ujinga kabisa na akapita kamavile hajaona chochote na kufika mbele akasema kuwa hawtoenda tena kula kwenye ile hoteli kwani aliona kamavile inamahusiano ya moja kwa moja na Yule mtoto ambaye wanamkutaga njiani.

    Walifika nyumbani na moja kwa moja wakaenda kulala kwani Ibra hakutaka kupoteza muda wa kujiwekea mawazo ya tofauti.

    Kulipokucha kama walivyopanga, Ibra alijiandaa huku Sophia nae akijiandaa kisha wakatoka kwa pamoja na kufunga milango kama kawaida.



    Ibra alimpeleka Sophia mpaka kwa Siwema na kumuacha hapo, ambapo Sophia alimgongea Siwema ila alikaa kwa muda bila ya kufunguliwa na kumfanya aamue kukaa nje ya nyumba hiyo akimsubiri huyo Siwema.

    Baada ya masaa kama mawili, Siwema alitoka ndani tena alionekana akiwa amechoka choka hivi na alipomuona Sophia alimshangaa sana na kumuuliza

    “Khee Sophia mbona asubuhi subuhi! Umefika hapa saa ngapi?”

    “Nimefika muda tu dada, nimegonga weee ila hujanifungulia ndio nikaamua kukaa hapa nje.”

    “Pole sana kwakweli hata sikusikia kugonga kwako jamani, karibu Sophy. Kwanza najishangaa leo kuchelewa kuamka kiasi hiki jamani”

    Siwema akamkaribisha Sophia ndani kisha wakakaa pamoja huku Siwema akitamani kujua kilichompeleka Sophia mahali pale kwani haikuwa kitu cha kawaida kwa Sophia kwenda pale tangu alipohama.

    “Vipi kwema lakini?”

    “Kwema tu dada”

    “Kwahiyo naweza kwenda kuoga kisha tukaendelea na maongezi ya hapa na pele?”

    “Ndio dada wala hata usijali kitu”

    Siwema aliinuka na kwenda kuoga ili kuondoa uchovu wake kisha akaandaa chai na kuanza kunywa, ila Sophia alipokunywa kidogo tu alikimbia nje na kutambika hivyobasi kumfanya Siwema awe na mashaka juu ya afya ya Sophia.

    “Vipi mdogo wangu au twende hospitali?”

    “Hapana dada, nadhani nimetapika kutokana na mimba niliyonayo”

    “Wow, una mimba Sophy!”

    “Ndio dada”

    “Kwakweli hiyo ni khabari njema, hongera sana mdogo wangu. Cha msingi kwasasa ni kuzingatia chakula bora ili kuufanya mwili wako upate afya na nguvu. Kula matanda kwa wingi na mboga za majani”

    “Asante dada”

    “Vipi umeshaanza kliniki?”

    “Bado sijaanza ila nitaenda kuanza”

    “Ni vyema ukaanza kliniki mapema mdogo wangu kwani inasaidia kujua ukuaji wa mtoto na pia kuangalia mwenendo mzima wa afya yako”

    “Hakuna tatizo dada huko kliniki nitaenda tu ila yaliyonileta hapa leo sio hayo ni mengine kabisa”

    “Mmh yapi hayo tena Sophy?”

    Sophia akaanza kumueleza Siwema kuhusu mambo ambayo ameyaona hivi karibuni katika nyumba yake, pia akamuelezea kuhusu Jane jinsi walivyozoeana na jinsi ambavyo Jane amekuwa akimsimulia kuhusu habari za misukule. Pia akamsimulia kuhusu kile chakula ambacho Sophia alihisi kuwa kimepikwa na Jane kwa dakika mbili, na kumueleza alivyofahamiana na mama Jane hadi yeye kuwa karibu na huyo Jane.

    Siwema akapumua kidogo na kumuangalia Sophia kisha akamuuliza,

    “Hivi mpaka hapo hujaelewa mchezo mzima unaondelea mdogo wangu?”

    “Kivipi dada?”

    “Hebu kwanza niambie huyo Jane anajishughulisha na nini?”

    “Jane kamaliza kidato cha nne kwahiyo huwa yupo nyumbani tu akisubiri matokeo”

    “Mmmh mdogo wangu hapo akili kichwani mwako, huyo binti kwanza hashindwi kukupiku kwa mumeo ukizingatia kila mumeo anapokula chakula chake anakisifia kuwa kitamu sana, kwanza umenieleza hapa kuwa huyo binti wala hawana matumaini nae kuwa atafaulu au la kwahiyo mama yake hashindwi kumlengesha kwa Ibra ili angalau hata awe mke wa pili ampunguzie majukumu”

    “Jamani dada mbona hayo mapya sasa, inamaana na haya maajabu ya ndani kwangu yanasababishwa na yeye?”

    “Ndio, hisia zangu zinanituma kuwa huyo binti atakuwa mchawi yani ingawa simjui ila naona kabisa kuwa ni mchawi, na yote anayafanya ili kukutisha na nyumba yako. Anataka uiogope nyumba yako na ikiwezekana uondoke ili ajilengeshe kwa Ibra. Yani usipokuwa makini utashangaa anaolewa nay eye, si vizuri kuokoteza majirani mdogo wangu mwisho wa siku unapata ya kuyapata kama hivi”

    “Mmh au ndiomana ananitishia na stori zake za misukule?”

    “Ndio, anataka uoanishe matukio na stori zake ili upatwe na uoga halafu mwisho wa siku uone nyumba mbaya na uikimbie nyumba yako aingie yeye. Hivi unafikiri ni nani asiyetamani kuishi kwenye jumba la kifahari kama lilre? Nani asiyependa maisha ya raha unayopewa wewe na mumeo?Hakuna Sophy, kila mwanamke anatamani kuishi vizuri kwa furaha na amani unatakiwa uwe makini sana”

    “Nashukuru dada ila nitafanyaje kumuepuka?”

    “Kwanza kabisa mzuie kuja nyumbani kwako, halafu pili kuna mtaalamu nitakupeka atatupa dawa ili tumzuie kabisa kabisa kukanyaga na mauchawi yake.”

    “Kwahuyo mtaalamu tutaenda lini sasa?”

    “Nadhani itakuwa vyema tukienda kesho, wataalamu hawaibukiwi hovyo hovyo. Inatakiwa kudamka asubuhi na mapema na kuelekea huko.”

    Wakaendelea na stori mbali mbali huku Siwema akimfundisha Sophia namna ya kutunza mimba aliyokuwa nayo na jinsi ya kumtunza Ibra hata katika hiko kipindi cha ujauzito wake.



    Jane kama ambavyo aliongea na wakina Sophia jana yake na jinsi ambavyo walimuomba kuwa na siku hiyo aende nyumbani kwao ili akampe kampani Sophia, alipoamka tu alienda kujiandaa kisha kumuaga mama yake kuwa anaenda nyumbani kwa Sophia,

    “Mmmh kushakunogea tayari!”

    Jane akatabasamu kisha akamuaga mama yake na kuelekea huko kwa Sophia.

    Alipofika, alikuta geti liko wazi kabisa na kushangaa kuwa imekuwaje wamesahau hata kurudishia geti lile akajiuliza na kuingia kisha akalirudishia huku akiongea

    “Usikute dada Sophy bado hajatoka nje maana si kawaida hili geti kuwa bwamu kiasi hiki”

    Alipofika mlango wa ndani aligonga ila hakufunguliwa na kujaribisha kufungua ambapo nao ulifunguka na kumfanya Jane aingie ndani na kukaa pale sebleni huku akiita.

    “Dada, dada, dada Sophy”

    Ila hakujibiwa, moja kwa moja akahisi kuwa huenda Sophia ameenda Sokoni ila kwanini hakufunga milango? Akajipa jibu kuwa huenda aligundua kuwa atafika ndiomana hakufunga milango.

    Alikaa kaa pale na kuamua kuwasha video huku akimsubiri Sophia arudi ila wakati akiangalia alijikuta akipitiwa na usingizi na kulala pale pale kwenye kochi.



    Ibra alipomaliza shughuli zake aliamua kumfata Sophia kule nyumbani kwa Siwema ili aweze kurudi nae nyumbani, alimkuta mkewe akiendelea na maongezi mbalimbali na Siwema ambapo naye alijumuika kidogo kisha kuaga.

    “Ila kabla ya yote shemeji napenda kukupongeza kwa ujauzito alionao mdogo wangu”

    Ibra alitabasamu kidogo na kushukuru huku akitoka nje na Sophia, ila Sophia akamuuliza tena Siwema,

    “Vipi hiyo kesho nije au wewe utakuja nyumbani?”

    “Itakuwa vyema kama ukija Sophy”

    Kisha Sophia na Ibra wakapanda kwenye gari na safari ya kurudi kwao ikaanza.

    Wakiwa kwenye gari Ibra alimuuliza mkewe,

    “Kwahiyo siku hizi habari itakuwa ni hii ya kuletana kwa Siwema au?”

    “Mmmh jamani Ibra si leo na kesho tu, au kama utashindwa basi nitakuja mwenyewe”

    “Haya basi usinune maana na wewe siku hizi kitu kidogo tu unanuna, ila tabia yako sijaipenda”

    “Ipi tena?”

    “Yani mimba change hivyo umeshaanza kuitangaza mmh!”

    “Jamani Ibra kwani kuna ubaya gani kumwambia Da’ siwema jamani wakati ni kama ndugu yangu!”

    “Sawa umefanya vyema ila kiukweli mimba haitangazwi, acha itajitangaza yenyewe”

    Sophia akanyamaza kwani aliona kamavile ni marumbano kidogo na mume wake.

    Wakiwa wanaendelea na safari yao, ibra akapita karibia na njia ya ile hoteli ambapo mbele kidogo walikaona kale katoto ial leo kalionekana kamelala chini na kumfanya Sophia ashtuke sana kisha Ibra akamwambia,

    “Achana na habari za hako katoto, hakana jema na maisha yetu wala usishtuke. Safari ijayo sitapita tena njia hii”

    Wakaendelea na safari yao hadi walipofika kwenye nyumba yao.



    Sophia alishuka na kufungua geti kisha Ibra akaingiza gari ndani halafu wakafunga geti na kufungua mlango wa kuingia ndani, kwakweli Sophia alishtuka sana kumuona Jane akiwa amelala kwenye kochi na kuita Ibra kwa nguvu aliyekuwa akipaki gari lake vizuri.

    Ibra aliingia ndani huku nae akishangaa kwani halikuwa jambo la kawaida, Sophia alishikwa na hasira sana na kumsogelea Jane pale kwenye kochi na kumkurupua kwa kumpiga ambapo jane nae alishtuka kama chizi na kuanza kupiga kelele za mwizi tena kwa nguvu kabisa.



    Ibra aliingia ndani huku nae akishangaa kwani halikuwa jambo la kawaida, Sophia alishikwa na hasira sana na kumsogelea Jane pale kwenye kochi na kumkurupua kwa kumpiga ambapo jane nae alishtuka kama chizi na kuanza kupiga kelele za mwizi tena kwa nguvu kabisa.

    Zile kelele zilifanya watu waanze kukusanyika nje ya nyumba ya Ibra, kitu ambacho Ibra hakuona kuwa ni sahihi na kuanza kumtuliza Jane aliyekuwa na mawenge ya usingizi, kisha kutoka nae nje na kuwaomba watu msamaha kuwa hakuna jambo lolote baya ila Sophia alitamani wale watu wampige Jane kwani alikuwa sawasawa na mwizi kuingia kwenye nyumba ya watu wakati wao wamefunga milango, watu walipoanza kutawanyika kwakweli bado ilikuwa ngumu sana kwa Sophia kukubaliana na uwepo wa Jane mahali pale,

    “Tafadhali Ibra, huyo binti sitaki kumuona yani sitaki kumuona kabisa huyo binti ni mchawi, nimesema sitaki kumuona yani naweza kumfanya kitu kibaya”

    Ilibidi Ibra amuombe Jane aende kwao, kwakweli Jane aliondoka huku analia kwani hakuipenda ile kauli ya Sophia ya kumuita kuwa yeye ni mchawi.

    Ingawa Jane alikuwa akiondoka huku analia ila bado Sophia aliokota kitu chini na kumpiga nacho Jane kwa nyuma na kufanya Jane aanguke, kwakweli Ibra alishangaa sana kwani ilikuwa ni kitendo cha ghafla ambacho hakukitarajia kabisa kufanywa na mke wake Sophia.

    “Khee Sophia umefanya nini sasa? Mbona unataka kuleta mabalaa tena jamani?”

    Ibra akamkimbilia Jane pale chini na kujaribu kumuinua ila Jane alikuwa akitokwa na damu puani, kitu ambacho kilimuogopesha Ibra na kuona wazi mkewe amemdhuru Jane. Ibra aliamua kumbeba Jane na kukimbilia kumpakiza kwenye gari yake ili kumkimbiza hospitali ambapo Sophia nae alipanda kwenye hilo gari kisha Ibra akatoa gari lile na hata wakasahau kufunga milango kwani ilikuwa kama kuchanganyikiwa.



    Walipofika hospitali walipokelewa na wahudumu kama kawaida kisha Jane kukimbizwa wodini na daktari kuitwa ambapo ilibidi Ibra amuombe daktari amtibie Yule mgonjwa huku akimpa pesa ili asiambiwe maswala ya PF3,

    “Ila hii kitu tunafanya kinyume na utaratibu maana hairuhusiwi kisheria”

    “Tafadhali nakuomba daktari nisaidie naomba”

    Daktari akaanza kumchunguza Jane ni kitu gani kimempata mpaka kupelekea atoe damu puani kwani ilikuwa ikitoka nyingi huku Jane akiwa amepoteza fahamu.

    Kwakweli Ibra alikuwa kama kachanganyikiwa huku akingoja hatma ya Jane kwa wakati huo, ila Sophia yeye alikuwa kwenye gari tu wala hakushika kufatilia kam Jane atatibiwa au la kwani moyoni mwake alijikuta akiwa amemchukia Jane kupita maelezo ya kawaida na ukizingatia yale maelezo aliyopewa kuhusu uchawi wa jane na vile walivyomkuta ndani ndio kabisa vikamfanya Sophia aamini kuwa Jane ni mchawi tena ni mchawi aliyekubuhu ndiomana kila siku anamletea stori za ajabu ajabu ili kumtisha na mambo yake ya kishirikina.

    Ibra alirudi kwenye gari na kumuangalia mke wake kisha akamuuliza,

    “Hivi Sophia una mapepo au kitu gani? Akili yako ni nzima kweli?”

    “Usiniulize hayo maswali kwasababu ya Yule firauni Jane, laity ungejua kwamba Yule binti hafai kiasi gani wala hata usingenilaumu yani tena ungenisifia mna kunisapoti kuwa tummalize kabisa”

    “Jamani Sophia ni roho ya wapi hiyo uliyonayo? Kwakweli sio mke ambaye nilikuzoea mimi jamani sio kabisa kabisa, kwakweli Sophia unanishangaza tena unanishangaza sana”

    Kisha Ibra akashuka tena kwenye lile gari ili kwenda kusikilizia hali ya Jane inaendeleaje.

    Alimkuta daktari ndio ametoka kwenye kile chumba walichompeleka Jane kisha akamfata daktari huyo na kumuuliza kuwa imekuwaje kuhusu Jane.

    “Anaendelea vizuri ingawa aliumia sehemu za nyuma ila kuna dawa tutawapa ili awe anakunywa kwaajili ya kumrudisha katika hali ya kawaida.”

    “Kwahiyo tutaweza kurudi nae nyumbani?”

    “Yeah itawezekana ingawa muda utakuwa umeenda sana kwani sasa tumemuweka mapumziko kwa muda”

    Ibra alkakubaliana na maneno ya daktari kisha akatoka nje na kwenda kukaa kwenye gari huku akisubiria muda uende ila alimkuta Sophia akiwa amejilaza mule kwenye gari, hakutaka kumsumbua na kumuacha alale tu.

    Ibra nae alikuwa kimya mule kwenye gari huku akitafakari mambo mbali mbali kwani akili ya mke wake hakuielewa kwakweli ingawa hakuelewa zaidi kuhusu Jane kuwa amewezaje kuingia ndani ilihali walifunga milango yote asubuhi wakati wa kuondoka? Akabaki na maswali mengi sana kichwani bila ya kupata majibu ya aina yoyote ile.



    Kwenye mida ya saa nne usiku ndipo waliporuhusiwa kuondoka na Jane ambaye alikuwa amezinduka muda huo hata fahamu nazo zilikuwa zimemrejea, wakapatiwa na dawa ambazo zitazidi kumsaidia Jane.

    Ibra alifungua mlango wa nyuma ambapo Jane alipanda kwani pale mbele alikaa Sophia na hata hivyo hakuweza kuwaweka Sophia na Jane mahala pamoja kwa muda huo kwani alijua wazi kuiwa bado Sophia ana kinyongo na Jane.

    Ibra aliondoa gari, na alipofika mahali alisimamisha na kuagiza chips ili waweze kula wakifika nyumbani kwani alijua wazi kuwa ni ngumu kupika kwa muda huo. Muuzaji aliwafungia vizuri zile chips na kuwapatia kisha safari yao ya kurudi ikaendelea, ila Jane aliwaomba wampeleke kwao moja kwa moja ambapo Ibra alimuuliza,

    “Kwanini tusiende nyumbani kwanza ule halafu ndio tukupeleke kwenu!”

    “Hapana nitaenda kula nyumbani na hata hivyo sijisikii kula chips”

    “Ila unajua muda umeenda sana Jane, sidhani kama utakuta chakula kwenu”

    “Kwetu hawanaga tabia ya kumaliza chakula chote, nitakikuta tu”

    “Basi sema chakula unachotaka tukanunue hata hotelini uende nacho kwenu ukale”

    Sophia akaingilia kati yale mazungumzo,

    “Jamani si ameshasema anataka kwenda kwao, hebu tumpeleke maana mada zinakuwa nyingi sasa”

    Ibra hakuongeza neno lolote kwani hakutaka Sophia aongee zaidi maneno mabaya na kumkwaza Jane. Moja kwa moja walimpeleka Jane nyumbani kwao ambapo Ibra alishuka na kuongozana nae huku akimuomba Jane kuwa asiseme chochote juu ya kilichotokea kwa mama yake,

    “Tafadhali Jane, usimwambie chochote mama yako”

    “Akiuliza nilipokuwa je!”

    “Mdanganye hata tulikupeleka kutembea ila usiseme chochote kuhusu kilichotokea, nakuomba Jane”

    “Sawa”

    Kisha wakafika mlangoni na kugonga ambapo mama Jane ndiye aliyetoka kuwafungulia na alipowaona tu kuwa ni wao alianza kuongea,

    “Yani leo mmenikwaza jamani yani toka asubuhi mpaka muda huu kweli! Jane umeondoka hapa asubuhi hadi saa hizi jamani, mtatuuwa kwa presha maana wengine hatupo sawa jamani”

    Ikabidi Ibra ajaribu kumuomba msamaha pale,

    “Tafadhali mama tusamehe sisi maana hatukutoa taarifa yoyote juu ya kuondoka na Jnae, kuna mahali tulienda nae kutembea ila kwa bahati mbaya ndio tumechelewa kurudi tafadhali mama tusamehe sana”

    “Sawa ila mmenikwaza kwakweli”

    Kisha Ibra akaagana nao pale halafu akarudi kwenye gari na kuelekea nyumbani kwao akiwa na Sophia.



    Walifika na kukuta geti limefungwa vizuri ambapo Ibra alishuka na kufungua kisha akarudi kwenye gari na kuingiza gari ndani halafu akalipaki ambapo akashuka pamoja na Sophia na ule mfuko wa chips kisha akarudi kurudishia geti, alimuacha Sophia akiwa amesimama tu na alipotoka kufunga geti alimkuta kasimama vile vile na kufanya amuulize kwa mshangao,

    “Khee mbona hufungui mlango wa ndani?”

    “Fungua mwenyewe, mi sitaki miujiza”

    Ibra alikuwa akimshangaa tu mkewe kisha akachukua funguoambazo Sophia ndiye aliyemkabidhi funguo hizo na kufungua halafu wakaingia ndani ambapo kila mmoja alikuwa na mawazo yake ya kutosha tu na kuwafanya wakae pale sebleni kwanza, Kisha Sophia akamuuliza Ibra

    “Hivi kwa kumbukumbu zako wakati tunampeleka Jane hospitali tulifunga milango?”

    “Mmmh kwakweli sikumbuki”

    “Mi basi nakumbuka vizuri maana funguo nilikuwa nazo mimi, milango hatukufunga wala nini. Sasa jiulize ni nani kafunga?”

    “Kwahiyo unataka kusema Jane kafunga?”

    “Jane sio mtu mzuri mume wangu ingawaje unamtetea, yani Yule binti sio mtu mzuri kabisa. Asubuhi tumeondoka hapa na milango yote tumefunga cha kushangaza tumerudi na kumkuta ndani je alipitia wapi? Yule binti ni mchawi mume wangu wala usijitahidi kumtetea”

    Ibra alikaa kimya kwanza maana hilo swala kidogo lilimchanganya na kuhusi huenda kuna ukweli ndani yake. Kisha akainuka na kwenda kuleta sahani ili waweke zile chips na kuweza kula, alipofika na sahani akachukua ile mifuki ya chips ili aweke ila wakapatwa na mshangao kwani kwenye ile mifuko hawakukuta chips wala nini.

    Walijikuta wakishangaa na kutazamana kwa zamu zamu, Ibra alimuuliza mkewe

    “Ni nini hiki Sophy?”

    “Sasa unaniuliza mimi naelewa?”

    “Makubwa haya, sijawahi kutapeliwa hivi. Inamaana wale wauzaji hawakutupimia chips au?”

    “Hata usiwalaumu wauzaji, kwa macho yabgu niliwashuhudia wakipima na kuweka kwenye mifuko, tatizo ni kuwa tumenunua hizi chips tukiwa na Jane. Yule mtoto si mtu mzuri itakuwa amezichukua kiuchawi”

    “Mmh naanaza kuamini sasa, au ndiomana alikataa kuja huku na kujifanya hataki kula chips!”

    “Ndion hivyo Ibra, binti gani asiyependa chips? Jiulize tu utapata jibu, kwanza walivyo na dhiki pale kwao eti huwa hawana tabia ya kumaliza chakula chote loh wakati huwa wanakula hadi wanagombaniana mmh! Leo tumeingia choo kibaya mume wangu”

    “Sasa tutakula nini?”

    “Yani kale katoto kabaya kanataka tulalae na njaa loh!”

    Ibra akafikiria na kuona kuwa ni vyema hata wakakoroga uji ili angalau wale kitu na kwenda kulala,

    “Ngoja nikakoroge uji mke wangu, kwakweli leo tumepatikana dah!”

    Ibra alienda jikoni na kuanzakukoroga uji ambao baada ya muda ulikuwa tayari kisha akaanza kunywa na mkewe,

    “Kheee kwani huu uji umeweka nini?”

    “Sijaweka chochote zaidi ya sukari tu”

    “Mmh mbona mtamu hivi?”

    “Hata mimi mwenyewe nashangaa, halafu hata haujachelewa kuiva yani”

    Wakanywa na kumaliza, kisha Sophia akapeleka vyombo jikoni halafu yeye na mumewe wakaelekea chumbani kwa lengo la kulala, ila Sophia alidai amechoka sana kiasi kwamba hata kuoga anaona uvivu.

    “Kwakweli nimechoka, mi siogi bhana leo”

    “Shauri yako ila uchafu unafanyaga watu waote ndoto mbaya”

    “Mmh ushaanza maneno yako”

    “Sio hivyo, ukumbuke wewe una mimba utamfanya mtoto nae awe mchafu kwasababu yako”

    “Aah yani mi sijisikii kabisa kuoga yani”

    “Kama hujisikii sikulazimishi maana kuoga ni hiyari ya mtu”

    Kisha Ibra akaenda kuoga ila aliporudi alimkuta mkewe akiwa ameshalala muda mfupi uliopita ambapo naye akaungana nae na kulala nae.

    Ibra alimsogelea mkewe na kumkumbatia ambapo alipofanya hivyo, Sophia alishtuka kamavile kapatwa na jambo baya kwani alisema kwa nguvu

    “Niache”

    Kwakweli Ibra alimshangaa ila Sophia alikuwa akihema sana huku jasho likimtoka,

    “Khee Sophia umepatwa na nini si umelala sasa hivi tu jamani”

    “Hata sielewi”

    Huku akihema sana, Ibra alijaribu kuwa nae karibu ili kumfanya arudi kwenye hali ya kawaida kwani alihisi kuwa huenda ameota ndoto mbaya ya gafla.

    Baada ya muda kidogo wakaamua tena kulala na kulala pamoja.



    Kulipokucha leo Sophia ndio alikuwa wa kwanza kuamka na kumuamsha mumewe ambapo Ibra nae akaamka kisha kwa pamoja wakaenda kuoga, wakati wanajiandaa Ibra akamuuliza mkewe

    “Kwahiyo na leo tena kwa Siwema?”

    “Sio lazima unipeleke maana naona unataka kuniwekea vikwazo”

    “Ila Sophy mke wangu kwani umekuwaje siku hizi jamani? Unajua hukuwa hizi zamani yani tunaongea kamavile ni watu wenye maugomvi mke wangu dah!”

    “Sio maugomvi, mimi nataka kuokoa nyumba yetu wewe unaona ni ujinga ndiomana naongea hivi”

    “Haya unataka kuiokoaje hii nyumba?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hii nyumba imeingiliwa na adui Jane kwahiyo lazima niiokoe”

    “Sawa ila je kuiokoaje?”

    “Wee subiri tu nitakupa majibu badae”

    “Haya twende nikupeleke huko kwa Siwema”

    Wakamaliza kujiandaa na kutoka kisha safari ikawa ni kuelekea nyumbani kwa Siwema kwanza kisha ndio Ibra aende kwenye safari zake zingine.



    Walifika nyumbani kwa Siwema ambapo Sophia alishuka kisha Ibra akaondoka zake, moja kwa moja Sophia alienda kugonga mlango wa Siwema ambaye hakukawia kutoka na kusalimiana na Sophia kisha akamwambia amsubiri ajiandae haraka haraka waende.

    “Karibu ndani basi unisubirie”

    “Aaah acha tu nikusubirie hapa hapa nje bhana”

    “Kama unaona ni sawa basi sawa, ngoja nijiandae haraka haraka”

    Siwema akaingia ndani kujiandaa kwani alikuwa tayari ameshaoga, Sophia nae akainuka na kuusogelea mti wa mpera pale karibu na kwa Siwema ili kuangalia kama una mapera ili achume japo moja atafune ingawaje anajua wazi kuwa ule mti hauna historia ya kuwa na mapera.

    Alipokuwa chini ya ule mti, alishtuliwa na bibi mmoja ambaye alikuwa anapita mahali hapo na kumfanya Sophia ashtuke sana huku akimuangalia bibi huyo, Yule bibi akamwambia Sophia

    “Pole kwa kukushtua”

    Sophia alimuangalia kwa muda kidogo kisha akamjibu,

    “Asante”

    “Huu mti wa mpera si mzuri”

    “Kwanini?”

    “Huwezi kupata pera hata moja hapo kwavile huu mti umechezewa sana”

    “Khee unaujua huu mti wewe?”

    Huyu bibi akacheka kidogo na kusema,

    “Naujua sana huu mti, hata nyumba yako naijua”

    Sophia alimshangaa na kumuuliza,

    “Nyumba yangu unaijua kivipi?”

    “Nyumba yako ni ya maajabu”

    Sophia akashtuka na kuzidi kumshangaa huyu bibi.





    “Huu mti wa mpera si mzuri”

    “Kwanini?”

    “Huwezi kupata pera hata moja hapo kwavile huu mti umechezewa sana”

    “Khee unaujua huu mti wewe?”

    Huyu bibi akacheka kidogo na kusema,

    “Naujua sana huu mti, hata nyumba yako naijua”

    Sophia alimshangaa na kumuuliza,

    “Nyumba yangu unaijua kivipi?”

    “Nyumba yako ni ya maajabu”

    Sophia akashtuka na kuzidi kumshangaa huyu bibi, kisha akamuuliza kwa mshangao

    “Nyumba yangu ya maajabu kivipi”

    Mara Siwema akamuita Sophia ambapo Sophia alimtazama Yule bibi na kwenda alipoitwa na Siwema, kisha Siwema akamwambia Sophia

    “Yani unapoteza muda wako kabisa unaongea na Yule bibi!”

    “Kwani ana tatizo gani dada?”

    “Yule bibi ni mwanga yani kashindikana nakwambia, ni mchawi hakuna mfano. Unavyomuona hakuna hata mtu mmoja anayezungumza nae mtaani kwake yani Yule bibi hafai tena hafai kabisa kabisa”

    “Alikuwa ananiambia eti nyumba yangu ni ya maajabu”

    “Mmh usimsikilize kabisa, alikuwa anajaribu kukuteka tu kwakweli Yule bibi hafai mdogo wangu”

    “Halafu kasema eti ule mpera wako umechezewa sana na kamwe hauwezi kuzaa mapera”

    “Sophy, achana na Yule bibi yani kuhusu huo mpera ndio kauandama balaa achana nae kabisa. Tena bahati yako hajagundua kuwa una mimba maana hakawiii kuvuruga mimba za watu Yule.”

    “Mmh dada tuondoke asije akaniletea makubwa bure, nampenda mwanangu”

    Kisha wakatoka pale na kuanza safari yao ya kuelekea kwa mtaalamu.



    Walifika kwa mtaalamu na kukuta watu wengi sana wakisubiri kuingia humo, ikabidi wapange foleni na wao ili zamu yao ikifika waweze kuingia. Kwa upande wa Sophia hii ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kwenda kwa mganga wa kienyeji kwahiyo ile hali aliishangaa sana,

    “Kheee kumbe ndio kunakuwaga na watu wengi hivi!”

    “Na hapa bado, ndiomana jana nikakataa na kukwambia kuwa muda umekwenda sana maana nilijua lazima tungekuta foleni kubwa zaidi”

    “Mmh! Kwahiyo waganga wote ninaowasikiaga ndio huwa wanajaza watu hivi?”

    “Hapana si wote, mara nyingi watu hujaa kwa wataalamu wa ukweli maana mtu unakuwa umeona mafanikio na kuwaambia wengine, ila kwa upande wa wale matapeli hata hawanaga watu wengi kivile wanadanganya sana na watu wamewashtukia hawaendi”

    “Mmh yani sijawahi kwenda kwa waganga mie kwakweli Yule Jane kaninyoosha”

    “Mama yenu nae hajawahi kweli? Maana mi mama yangu ndio kanifundisha haya mambo, yeye sasa ni kitu kidogo tu anaenda kwa mganga. Kwani Jane umeonana nae tena?”

    “Tena ngoja nikusimulie kisanga cha jana”

    Sophia akaanza kumueleza Siwema yale yaliyotokea jana waliporudi nyumbani kwao na kumkuta Jane ndani ilihali walifunga milango wakati wa kutoka hadi kuhusu kuyeyuka kwa zile chips.

    “Kheee huyo mtoto mbona mchawi kiasi hicho! Hadi namchukia kabla sijamuona jamani loh, yani milango ulifunga sasa ndani kaingiaje? Na hizo chips uwiiii huyo mtoto ni wa kumuogopa kama ukoma. Tena ikiwezekana tumuombe mtaalamu atupe dawa ya kummaliza kabisa huyo binti maana si kwa uchawi huo jamani.”

    “Ndio hivyo yani toka nimfahamu mambo ya ajabu nayo yanaongezeka jamani, nilikuwa siamini mambo ya uchawi ila Yule mtoto kaninyoosha. Alikuja na gia ya kunisimulia stori zake za kutisha hadi nikaanza kuiogopa nyumba yangu kumbe ana malengo yake.”

    “Huyo mtoto ni wa kumuepuka kabisa yani tukipata dawa ya kummaliza nitashukuru sana”

    Muda wao ukafika na kuwafanya waingie kwa mtaalamu ambaye aliwapokea kwa kicheko na kuwafanya wawe kimya kimshangao, ambapo muda kidogo mtaalamu akaanza kuwaambia,

    “Tatizo lenu nalijua, mmekuja kwasababu ya binti mmoja anayewasumbua akili zenu anaitwa Jane”

    Kwakweli Sophia alishangaa sana jinsi huyu mganga alivyoweza kugundua tatizo lao kwa urahisi kiasi kile, kisha Siwema akamwambia mganga

    “Yani huyo binti anatutesa sana babu tafadhali utusaidie”

    “Mnataka tumfanye nini?”

    “Naomba tummalize kabisa maana hata hatutaki kumuona machoni petu babu, tafadhali tusaidie”

    “Basi mimi nitawapatia dawa ya kuweza kummaliza na hatoonekana tena mbele yenu”

    “Asante babu”

    Basi Yule mganga akachukua unga unga na kuufunga kwenye karatasi vizuri kabisa kisha akawapa huku akiwaambia masharti ya ile dawa,

    “Dawa hii mnatakiwa kumkaribisha Jane nyumbani kwenu, ukiona anakaribia kuja unainyunyuzia mlangoni. Kisha akija ataingia ndani, halafu nenda kamchukulie kinywaji chochote juisi, soda au maji muwekee hiyo dawa mpelekee anywe yani akinywa tu kwisha habari yake hamtasikia cha Jane wala ujinga gani”

    Sophia akaguna kidogo,

    “Mmh nitawezaje kumshawishi Jane aje nyumbani wakati jana nilimtimua?”

    Yule mganga akatoa jani dogo kisha akampa Sophia na kumwambia,

    “Chukua jani hili, ukiwa unaenda huko alipo Jane litafune halafu ukifika zungumza nae aje nyumbani hawezi kukataa hata kidogo maana jani hili huwa linawavuta wachawi, halafu akija unafanya hiyo dawa kisha mchezo unaisha”

    Sophia akachukua lile jani na kuona sasa kazi itakuwa rahisi sana katika kumshawishi Jane ili akampatie dawa ya kummaliza kabisa.

    Kisha wakaweka pesa na kuondoka kwenye kile kijumba cha mganga, kwakweli Sophia alifurahi sana na kujikuta akipanga mipango ya kummaliza Jane wakati mumewe hayupo.

    “Yani dada nitahakikisha kesho naikamilisha hii kazi ila sitaki Ibra agundue maana anavyojifanya anahuruma na Yule binti balaa tupu”

    “Ibra nae ndiomana mwisho wa siku yanamtokea puani jamani maana anatetea hadi maradhi mmh!”

    “Ila dada inamaana atafia nyumbani kwangu?”

    “Mi nadhani akishakunywa tu mtimue arudi kwao maana nahisi atakaa kaa hata dakika tano ndio afe kwahiyo wewe mtimue arudi kwao.”

    “Basi nitafanya hivyo dada yani simpendi Yule binti balaa, amenifika hapaa kwakweli simpendi jamani dah”

    “Unahaki ya kutokumpenda kwakweli maana hakuna mtu nayewapenda wachawi kwa maisha yao ukizingatia wanatutesa sana”

    Safari yao sasa ilikuwa ni kurudi nyumbani kwa Siwema ambapo Sophia aliona ni vyema akamsubirie mumewe huko.



    Leo Ibra aliwahi kutoka kwenye shughuli zake ila alipoenda kwa Siwema ili akamchukue mkewe hakuwakuta wote wawili na kufanya aondoke tena ili akazunguke zunguke kidogo huku akipanga kurudi tena badae.

    Ila akapata wazo la kwenda kumuangalia Jane nae anaendeleaje maana hakujua hali yake tangu ile jana walipomuacha pale kwao, moja kwa moja Ibra akaelekea nyumbani kwakina Jane na ikawa vyema kwani alimkuta Jane akiwa nje amepumzika tu.

    Ibra alienda pale alipo Jane na kumsalimia kisha kumpa pole kwa kilichotokea na kuanza kumuuliza kuwa anaendeleaje.

    “Vipi hali yako lakini Jane”

    “Niko safi tu, naendelea vizuri”

    “Vipi lakini dawa unatumia?”

    “Ndio natumia dawa vizuri tu”

    “Pole sana yani kwakweli jana dah hata mimi sielewi elewi vizuri kwakweli, kwani ulipofika nyumbani jana ilikuwaje hadi ukaingia ndani?”

    “Mimi nilivyofika jana nilikuta geti likowazi nikaingia na kulirudishia kidogo kwani nilijua dada amesahau kufunga kama kawaida yake ya kusahau. Nilipofika mlangoni nikagonga ila sikufunguliwa, nikajaribu kufungua mlango nikakuta uko wazi na kufanya niingie ndani ila nilimuita dada bila ya kuitikiwa ila kwa haraka haraka nikahisi labda dada ameenda sokoni na kusahau kufunga milango kwahiyo nikakaa kumsubiri. Ila sielewi ilikuwaje maana nilipatwa na usingizi mzito sana hadi nyie ndio mmenishtua halafu nilikuwa na maruwe ruwe ya usingizi na kuhisi labda pamevamiwa ndiomana nikaanza kupiga kelele za mwizi”

    Maelezo haya ya Jane yalimfanya Ibra awe na mawazo kiasi kwani hakuelewa kuwa ilikuwaje Jane akute mlango wao uko wazi wakati walifunga.

    “Kwanza kabisa Jane usitufikirie vibaya maana asubuhi tulivyoondoka milango ilifungwa kabisa na mke wangu ndiomana tuliporudi jioni alipatwa na mshangao sana kuwa wewe umeingiaje ndani”

    “Sasa kama milango ,mlifunga unafikiri mimi ningeingiaje ndani? Inawezekana mkeo alisahau kama kawaida yake na kufikiri kuwa alifunga”

    Ikabidi Ibra ajivunge hapo hapo kwani alijua wazi aking’ang’ania kauli yake ya kusema milango walifunga wakati huyu Jane kasema alikuta wazi atakuwa fika anamkandamiza huyu Jane kwa kumuhisi vibaya.

    “Kweli bhana Jane, inawezekana kabisa ni mke wangu aliyesahau kufunga na kudai kuwa alifunga maana mke wangu ni msahaulifu sana ila tafadhali naomba unisamehe mimi Jane”

    “Nimekusamehe ila kwa stahili hii nahisi siku moja nitatolewa roho na mke wako kwa matatizo yake ya kusahau. Mi nadhani ni vyema kama nisije kwenu tena”

    “Hapana Jane, wewe ndio faraja ya mke wangu ila hujui tu. Tafadhali usitufanyie hivyo.”

    Ibra akajaribu kumbembeleza Jane ili asijione vibaya kuwa anchukiwa na mkewe kwani bila kufanya hivyo alijua ni rahisi sana kwa Jane kugundua kuwa Sophia ana chuki za wazi sana juu yake. Kisha Ibra akaaga na kuondoka zake kuelekea kwa Siwema sasa.



    Alipofika kwa Siwema aliwakuta nao ndio wamerudi muda huo huo ila hakutaka kupoteza sana muda na kumuomba mkewe kuwa warejee nyumbani ambapo walienda kupanda gari yao kisha safari ya kurudi kwao ikaanza, njiani Sophia alimuuliza mumewe

    “Vipi leo hatununui chips?”

    “Kwahiyo una hamu na chips?”

    “Ndio au unahisi zitayeyuka kama jana?”

    “Aaah achana na habari za jana Sophy, ngoja tununue”

    Ibra akasimamisha gari na kununua hizo chips kisha safari yao kuendelea.

    Walipofika nyumbani tu, kitu cha kwanza Sophia alichukua sahani na kuweka zile chips na kumuomba mumewe kuwa wale huku akimwambia,

    “Si unaona leo hazijayeyuka”

    “Unamaanisha nini Sophy?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Jana tulinunua tukiwa tumeambatana na mtu mbaya mume wangu”

    “Aah Sophy jamani wale ni majirani zetu tena yatupasa tuwaombe msamaha”

    “Labda nitamuomba msamaha huyo Jane siku akiwa kaburini”

    “Sophy usiongee maneno hayo mke wangu”

    Waliendelea kula na walipomaliza tu, Ibra alimuuliza mkewe kuhusu alipoenda na Siwema,

    “Tulienda kutembea tu, kupunga upepo na kubadilisha mazingira”

    “Mmh ila Sophy usipende sana kumuamini Siwema maana Yule ni mswahili sana”

    Sophia akatabasamu tu kwani aliona mumewe kamavile anampigia mbuzi gitaa tu, wakaenda kukaa sebleni huku wakitazama luninga ila mara kidogo tu ile Tv ikazimika na kufanya washtuke kwani ilikuwa kama mtu kaizima hivi, Sophia akamuuliza mumewe kwa mshangao

    “Ni nini hiki?”

    Ibra nae akashangaa tu, ila ile Tv ikawaka tena na kuwafanya washtuke zaidi. Kwakweli kitendo hiki kilimfanya Ibra anyanyuke na kuizima ile Tv huku akimuomba mkewe waende chumbani tu.

    Sophia akamuuliza mumewe,

    “Kwani unaelewa hapo ni nini tatizo?”

    “Sijui ila nahisi inataka kuharibika, nitamleta fundi aiangalie kuwa tatizo ni nini ila twende chumbani tu tukajiandae kulala”

    Walienda chumbani na kuoga kisha kulala.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog