Search This Blog

JENEZA LA AJABU - 2

 

    Simulizi : Jeneza La Ajabu

    Sehemu Ya Pili (2)





    Nyumbani kwa kina

    Njoshi;

    Jua likiwa tayali

    linazama, huku sauti za ndege zikipungua na kuufanya mji wa Mwamutapa kuwa

    kimya.Ukimya huo unatokea pia katika nyumba ya kina Njoshi, ukimya unatawala

    tofauti na siku zote, kwani familia ilibakiwa na mtu mmoja tu,ambaye ni mama

    yake Njoshi  huku mwanae akiwa hajarudi

    kutoka kwa mfalme. Akiwa ameketi barazani, nje ya kibanda chao cha udongo,

    kilichoezekwa kwa nyasi, aliendelea kupunga upepo huku akiwa na huzuni sana,

    “Siamini,hatimaye

    leo hii nimebaki peke yangu, sina cha kufanya ndio tayali imeshatokea ……,eeeh

    mizimu ya babu zangu mlindeni mwanangu ” ,mama Njoshi aliongea peke yake

    kwa huzuni huku akinyanyuka sehemu aliyokuwa ameketi, na kisha kuelekea ndani

    kulala, hakuwa na njinsi kwani aliona kuketi pale nje kulizidi kumuongezea

    machungu.

    Ikulu kwa mfalme;

    Giza likiwa tayali limeshaingia huku,

    ukimya ukiwa umetawala katika ngome ya mfalme. Kijana Njoshi anamfuta machozi

    Grace, huku akiwa amemkumbatia,

    “Usijali Grace,

    naamini nitarudi salama ndani ya siku tatu “,Njoshi alimtoa hofu binti

    mfalme, msichana aliyempenda sana, na aliamini atamuoa atakaporudi kutoka

    katika msitu hatari wa majini, msitu ambao aliambiwa na mama yake hana budi

    kwenda huko, kwani huko ndiko angeupata ufalme na ukombozi wa Mwamutapa.

    “Sawa Njoshi,

    nakuamini wewe ni shujaa, nakuombea kwa mizimu yetu, urudi ukiwa mzima

    “,Grace aliongea kwa huzuni huku akitoka mikononi mwa Njoshi aliyekuwa

    amemkumbatia, na kumruhusu kuianza safari yake haraka sana, kwani alitakiwa

    kuondoka usiku huo. Na bila kupoteza muda, kijana shupavu na hodari, kijana

    pekee aliyeogopwa na askari pamoja na mfalme Mutapa kutokana na uhodari wake wa

    kupambana, anatoka katika ngome ya mfalme iliyojengwa kwa ukuta mrefu, huku

    wafanyakazi pamoja na familia nzima ya mfalme wakimtazama na kumtakia kila

    laheri katika safari hiyo, bila kutambua kuwa Njoshi alikuwa na malengo

    yaliyompeleka msituni huku swala la kuchukua jeneza la ajabu, likiwa la ziada

    tu.
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mwamutapa

    Kijana ambaye alikuwa ni rafiki yake

    Njoshi, urafiki ambao ulitokana na kijana huyo kuokolewa katika kipigo kizito

    kutoka kwa askari wa mfalme, mara tu alipofanya kazi asubuhi mpaka jioni katika

    shamba la mfalme, na pale alipojaribu kudai haki yake, askari wale walimnyima

    pesa, jambo ambalo kijana yule alishindwa kulivumilia, alijikuta akilusha

    ngumi, na kuambulia kipigo kikali kwani asingeweza kuwashinda askari zaidi ya

    kumi, huku yeye akiwa mmoja tu, lakini bila kutegemea ghafla alishangaa, askari

    wale wakipigwa mateke ya haraka haraka na kutimua mbio.

    “mimi naitwa

    Njoshi, na pole sana ndugu yangu, hawa ndio askari wetu, inatakiwa tuungane

    kuitafuta haki “,kijana yule aliikumbuka sauti ya mtu aliyemsaidia kutoka

    mikononi mwa askari wa mfalme, ikijitambulisha na kisha kumuomba waungane

    katika harakati za ukombozi wa Mwamutapa. Na huo ndio ukawa mwanzo wa urafiki

    wao, urafiki ambao umedumu kwa muda mrefu na wamekuwa kama ndugu sasa.

    “Inabidi kesho

    niende kwao nikamuone rafiki yangu, tangu jana sijaonana naye “,rafiki

    yake Njoshi, aliyejulikana kwa jina la Ngesha, alizungumza peke yake huku

    akijifunika shuka lake na kisha kuuchapa usingizi, bila kutambua kuwa muda huo

    ambao yeye analala, rafiki yake yuko safarini bila kujali giza wala hatari

    yoyote usiku huo, akielekea katika msitu wa majini, msitu ambao ulipatikana

    umbali wa kilomita arobaini kutoka katika makazi ya watu wa Mwamutapa.

    Msitu wa majini;

    Tangu asubuhi tetemeko lilipotokea, na

    malikia kutangaza hali ya hatari katika msitu, mitego ya kila aina iliweza

    kutegwa katika kila njia ya kuingilia msituni, huku jeshi la msituni likiwa

    tayali limeshika dhana mbalimbali za kivita ikiwemo mishale, na kuuzunguka

    msitu wote.

    “Aiweeeh jini

    mweupe, kiongozi wa askari wangu wa msituni, adui wetu yuko njiani anakuja,

    nakuomba jiandae kwa mapambano, uko huru kutumia nguvu za kichawi na kijini

    ulizonazo “,malikia alimpatia taarifa mkuu wa jeshi lake la ulinzi

    msituni, na haraka bila kupoteza muda alitoweka mbele ya uso wa malikia, kwenda

    kutekeleza amli aliyopewa ya kudumisha ulinzi kila kona ya msitu, na kujiandaa

    kwa ajili ya kulipiza kisasi.



    Giza likiwa linazidi

    kuwa la kutisha,ikiwa imefika mida kama ya saa nne usiku, kijana Njoshi akiwa

    amevalia bukta yake nyeusi, huku chini akiwa miguu peku, kwani watu wa

    Mwanamutapa kutokuvaa viatu ilikuwa kama tamaduni yao, kijana Njoshi aliendelea

    kutembea huku akinyosha balabala kubwa ya vumbi, balabala iliyokuwa

    ikiunganisha nchi ya Mwamutapa na nchi zingine za jirani, ikiwemo nchi ya

    Mwamuyeshi. Sauti za miguu yake ndizo zilizosikika balabala nzima, kwani watu

    hawakupita balabala hiyo mida ya usiku, kutokana na kuogopa kutekwa na

    kunyanganywa mali zao, na pengine hata kuuawa.

    Ilikuwa tofauti kwa

    Njoshi, hakuogopa jambo lolote lile, akiwa kifua mbele kwani hakuvaa shati

    lolote lile huku akiwa amebeba begi jeusi alilopewa na mama yake, aliendelea

    kusonga mbele huku akitembea kwa mwendo wa haraka, na muda mwingine alikimbia,

    ili aweze kufika katika ardhi ya msitu wa majini kabla hapajakucha siku ya

    jumanne.

    “Mpaka sasahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nimeshakimbia umbali mrefu sana, sina budi kuongeza bidii “,Njoshi

    aliongea peke yake moyoni mwake, huku akiwa tayali ameshayaacha majumba ya

    Mwanamutapa mbali sana. Kila alipokumbuka mateso yote ya Wanamutapa, nguvu za

    ajabu ziliongezeka mwilini mwake na kumfanya azidi kuongeza mwendo ili apate

    kuikomboa nchi yake haraka sana, huku mbalamwezi ikiangaza vema njia

    aliyotakiwa kupita. “Hahaha eti jeneza, siamini kama kuna watu hawataki

    kufa, yani uishi milele, na kututesa milele, hili ni jambo ambalo haliwezekani

    “,Njoshi aliongea maneno ya kejeli kwa mfalme, huku akitabasamu na kumuona

    mfalme kama mtu wa ajabu sana, mtu aliyemkabidhi fisi bucha na kula nyama zote

    za buchani.

    “Hapa mimi

    ninachofuata ni fimbo ya ufalme, fimbo ambayo inapatikana katika ngome ya

    malikia wa msituni, malikia wa majini, jeneza nitalishughulikia nikishapata

    fimbo yangu ya kuiongoza Mwanamutapa “,Njoshi alizidi kuongea peke yake,

    huku akisisitiza jambo lililompeleka msituni, kwani ili uwe mfalme nilazima

    umiliki fimbo ya kifalme kutoka katika msitu huo, na mfalme Mutapa aliipata

    fimbo hiyo ya uongozi kutokana na kurithi kwa wazazi wake,huku chanzo cha fimbo

    hiyo kikisemekana ni katika msitu wa majin. Fimbo hiyo ilimpatia mamlaka mfalme

    kutodhurika na majini wa msituni, kwani msitu wa majini ulipatikana katika nchi

    ya Mwamutapa. Wengi walifunga safari kwenda msituni kuchukua fimbo nyingine ya

    ufalme, inayofanana na fimbo ya mfalme lakini walishindwa kurudi wakiwa hai.

    Pia wasingeweza

    kupambana na mfalme kwani fimbo aliyonayo ilimpatia kiburi sana, hata

    ukilishinda jeshi lake na kumuua, usingeweza kuongoza nchi, kwani fimbo

    iliandikwa jina  la mfalme Mutapa,. Hivyo

    njia ambayo ni rahisi, ilikuwa ni kuitafuta fimbo ya ufalme msituni ,na

    kuiandika jina lako binafsi ili majini wakutambue na wasikusumbue katika

    uongozi wako,hapo ndipo ufanye mapinduzi na kumuua mfalme ili uongoze nchi ya

    Mwanamutapa.

    “Ngoja nipumzike

    kidogo hapa chini ya mti ,ninywe maji, nichukue siraha zangu kwani muda wowote

    nitaufikia msitu “,Njoshi aliongea huku akiketi katika majani mafupi chini

    ya mti wa ubuyu, na kisha kufungua begi alilopewa na mama yake. Huzuni ya kutokumuona

    tena mama yake ilimuandama, kwani aliyakumbuka maneno ya mama yake kuwa

    hatomuona tena na kufanya machozi kumtoka , mithili ya mtu aliyefiwa na mtu

    anayemtegemea. Alifungua begi na kutoa kitambaa cheusi, kitambaa ambacho

    alitakiwa akifunge kiunoni kama mkanda, huku akishikilia panga kali, panga

    ambalo linauwezo wa kuua majini. Ikiwa tayali imeshafika mida ya saa saba

    usiku, Njoshi ananyanyuka sehemu aliyokuwa amepumzika kwa takribani dakika

    tano, na kisha kusonga mbele kuusogelea msitu wa majini.

    Msitu wa majini

    Malikia wa majini anaingiliwa na hofu

    kubwa sana kwani mtu aliyekuwa anakuja kuuvamia msitu alionekana kuwa hatari

    sana, kwani kila alipojaribu kumtambua sura yake alishindwa, na ghafla

    mawasiliano yalipotea, hakuweza kumuona tena katika kiganja chake, kiganja

    kilichokuwa kikimuonesha mtu aliyekuwa njiani akielekea msituni. “Huyu

    anayekuja huku natambua kuwa ni mtoto wa mtu aliyewahi kuja huku na kutuibia

    mali zetu, lakini sura yake ningependa niifahamu lakini nimeshindwa, na kwanini

    kapotea ghafla, nashindwa kumuona tena katika viganja vyangu “,Malikia wa

    msituni alizungumza kwa hasira na mshangao mkubwa, bila kutambua kuwa Njoshi

    aliweza kuvaa kitambaa cheusi kiunoni, na kumfanya kutoonekana kama akiwa

    anafuatiliwa na majini.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapa nikizubaa,

    watu wangu watakufa “,malikia  wa

    majini, msichana aliyekuwa mrembo sana, na mwenye umri sawa na Grace,

    alizungumza huku akitafuta kichupa kidogo cha maji, na kisha kumpatia askari

    wake mmoja, kunyunyizia maji hayo kuzunguka ngome yake yote ili kujilinda. Maji

    hayo yalikuwa na uwezo wa kumgandisha mahali pale, mtu yeyote mwenye asili ya

    ubinadamu, atakapokanyaga eneo lile.

    “Hapa tayali

    nimemaliza kazi, hata kama akifanikiwa kuwapita askari wangu msituni, mimi

    lazima nitamkamata “,malikia aliongea kwa kujigamba, na kuachia tabasamu

    zuri lililoonesha vema uzuri wake.

    Nje ya msitu;

            Kwa mbali kijana shupavu na hodari

    Njoshi Nyangoma, anakamatilia panga lake kisawasawa, kwani alianza kuuona msitu

    hatari wa majini, ukiwa kama hatua mia moja mbele yake, baada ya kutembea na

    kukimbia kwa usiku mzima, na ilikua imeshafika mida ya saa kumi usiku, kuamkia

    siku ya jumanne.

    “Aiweeeh mizimu wa

    mababu zangu, mizimu wa ardhi ya Mwamutapa, asanteni kwa kunifikisha salama,

    naomba mnilinde tena na kunirudisha nyumbani salama “,Njoshi aliongea kwa

    hofu na woga, kwani alikuwa na kazi nzito, tena ya hatari ikiwa mbele yake.

    “Hapa ni mwendo wa

    kuua tu kiumbe chochote, kitakachokatiza mbe…le…y…a…ngu “,Njoshi

    alishindwa kumalizia sentesi yake baada ya kukanyaga mtego wa kamba, na kisha

    mtego huo kumning’iniza juu ya mti huku miguu ikiwa juu na kichwa kikiwa chini,

    mala tu alipokanyaga mguu wake msituni.

    Njoshi bila kupoteza

    muda, aliikata kamba ile mguuni kwake, kwa kutumia panga lake na kisha kudondoka

    chini kama mzigo huku akiwa haamini kilichokuwa kimetokea ghafla namna ile, na

    kumuongezea hofu na woga huku akitakiwa kuwa makini sana ndani ya msitu.



    Msitu wa majini;

    Viumbe hatari wa msituni ghafla

    wanasikia kishindo katika moja ya mitego waliyokuwa wametega, hali hii

    inawafanya wagundue kuwa tayali adui yao alikuwa ameshaingia msituni, kwani

    hawakuweza kumuona katika ramani zao, na hata walipotumia uwezo wao wa kijini,

    walishindwa kumuona adui yao, mala baada ya Njoshi kujifunga kiunoni kitambaa

    cheusi alichopewa na mama yake. “Jamani tayali adui alishaingia msituni,

    fanyeni kila njia mumkamate akiwa hai au amekufa “,jini mweupe, kiongozi

    wa askari wa msituni, alitoa amli ya kuanza kumtafuta adui, baada ya kufika

    katika eneo ambalo kishindo kikubwa kilisikika, na sehemu ambayo walitega mtego

    wao, na kukuta kamba ya mtego ikiwa inaning’inia baada ya kukatwa huku adui

    akiwa ameshatoweka.

    “Nazani mnaisikia

    harufu ya binadamu, hayuko mbali, mtafuteni haraka sana ” ,jini mweupe

    alizidi kuongea na kuliamlisha jeshi lake la msituni, kumtafuta adui baada ya

    kuhisi harufu yake katika eneo lile la mtego, eneo ambalo lilizungukwa na vichaka

    pamoja na miti mirefu.

    ********http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya Njoshi kuponea

    chupuchupu kutoka katika mtego, haraka sana anaingia ndani ya kichaka chenye

    majani marefu, kwani alitambua kuwa majini wa msituni lazima wafike katika eneo

    lile muda sio mrefu baada ya kusikia kishindo kile kikubwa, hivyo asingeweza

    kukimbia na kufika umbali mrefu bila kukamatwa.

    Lakini ukistaajabu ya

    Musa, utayaona ya firauni, Njoshi alishangaa sana baada ya kuliona kundi kubwa

    la majini, likifika eneo lile haraka sana huku akiwa hata hajajificha vizuri

    kwenye majani. Kwani viumbe wale walikuwa na uwezo wa kupotea na kufika eneo

    lolote walilolitaka wao, ndani ya sekunde tu, kwani hawakuwa binadamu bali

    majini, tena majini hatari wa msituni, msitu ambao ulikuwa maarufu katika nchi

    ya Mwamutapa, pamoja na ulimwengu mzima, kutokana na utajiri wake.

    “Mungu wangu,

    mbona hawanioni “,Njoshi alistaajabu sana kwani kiongozi wa askari wale,

    jini mweupe alisimama karibu sana na kichaka kile, na ilikuwa imebakia kidogo

    amkanyage Njoshi kwani alikuwa hata hajajificha vizuri katika kichaka, eneo

    ambalo mtego ulikuwepo.

    Njoshi ujasiri ukiwa

    umetoweka, alianza kutetemeka kwa woga kwani majini wale walitisha sana kwa

    kuwatazama, wengine walikuwa na mguu mmoja huku wakiwa na vichwa vingi sana,

    pamoja na mikono zaidi ya miwili. Njoshi akiwa anatetemeka aliamua kufumba

    kinywa chake asiweze kupiga kelele, kwani jini mweupe, aliyekuwa na kichwa cha

    nyoka aina ya koboko, huku akiwa na mwili mweupe tena wa binadamu, alitoa amli

    ya kumsaka Njoshi katika kichaka kile, kwani waliweza kuhisi harufu yake.

    “Asante mizimu ya

    mababu, sionekani, leo nilikuwa nimekwisha “,Njoshi akiwa amejifumba mdomo

    wake kwa kutumia viganja vya mikono, aliishukuru mizimu, kwani majini waliokuwa

    wanatisha sana walipita karibu yake bila kumwona, jambo ambalo lilimshangaza

    sana kwani sehemu kubwa ya mwili wake ilikuwa wazi na hakufunikwa vizuri na

    majani, bila kutambua kuwa mkanda ule wa kitambaa cheusi aliouvaa kiunoni,

    ndiyo uliyosababisha majini wasiweze kumuona.

    “Msitu huu niliuskia

    tu, leo nimejionea mwenyewe “,Njoshi aliongea moyoni huku akiwa

    anamshangaa askari mmoja wa msituni,mwili wake ukiwa umebakia mifupa tu,huku

    akiwa ameshika mshale, na kusonga mbele, lakini Njoshi alishindwa kutumia hata

    panga lake kuwaangamiza majini wale kwani hakutambua matumizi yake, huku yeye

    akiwa anashangaa muonekano wa majini wale na kuzidi kumuongezea woga.

    Mwamutapa

    Asubuhi mida kama ya saa moja, kijana

    Ngesha aliamka kutoka usingizini, na kunawa uso ili aelekee nyumbani kwa rafiki

    yake, ili asikute wameshaondoka kwenda shambani.

    “Mwanangu mbona

    haraka sana asubuhi hii, unaenda wapi ” ,ilikuwa ni sauti ya mama yake

    Ngesha, mama ambaye alibaki mjane baada ya mume wake kuitwa na mfalme,na

    alipokwenda huko hakuweza kurudi.Kwani alipofika ikulu kwa mfalme,alikuta kundi

    kubwa la wanaume wakiwa huko wanasaga unga wa mahindi kwa kutwanga kwenye

    vinu,lakini baada ya kumaliza kazi hiyo na kudai malipo yao ,kundi lote

    lilitupwa kwenye bwawa la mamba bila huruma ,amli iliyotoka kwa mtoto mkubwa wa

    kiume wa mfalme.

    Lakini mama Ngesha kilahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alipojaribu kuulizia kwa mfalme kuhusu mumewe ,hakuweza kupatiwa jibu sahii

    zaidi ya vitisho.Kitendo kilichomfanya mama Ngesha pamoja na mwanae kuweka

    msiba nyumbani kwani tayali waliamini mzee wao aliyejulikana kwa jina la

    Mugina,alikuwa ameuawa,jambo ambalo lilikuwa kweli.

    “Naenda kumsalimia

    rafiki yangu Njoshi,mara moja,” Ngesha alimjibu mama yake na kisha

    kutokomea huku akikimbia ili kumuwahi Njoshi,kwani  ilikuwa ndio mida  ya Njoshi na mama yake kwenda shambani.

    Ikulu kwa mfalme;

           Asubuhi na mapema siku ya jumanne,siku

    ambayo usiku uliopita kijana Njoshi alitoweka ikulu kuelekea katika msitu wa

    majini,kwenda kuchukua jeneza la ajabu kwa ajili ya kumzikia mfalme atakapokufa

    ,na kisha  kufufuka ndani ya wiki moja.

    Vilio vinatawala katika

    ngome yote ya mfalme,huku familia nzima ya mfalme pamoja na wafanyakazi wote

    wakilia kwa kwikwi,ama kweli mkuki kwa ngurue kwa binadamu mchungu,leo hii

    maneno haya yalijidhirisha waziwazi.Walizoea kuona wengine wakilia,lakini leo

    ilikuwa ni zamu ya familia ya mfalme kulia.

    “Baba rudi,baba

    rudi baba yangu nakupenda”,msichana Grace alilia kwa huzuni,huku akitamka

    maneno ambayo yaliongeza uchungu katika familia nzima ya mfalme.Walitamani sana

    Njoshi afanikiwe kurudi na jeneza salama,ili mfalme afufuke ndani ya wiki moja

    na kuishi milele,lakini hawakuamini kama kweli Njoshi atafanikiwa kurudi

    salama,kwani huko msituni alikoenda ni hatari sana.

    Nyumbani kwa kina

    Njoshi;

            Mama yake Njoshi,akiwa ameshika jembe

    kama kawaida yake tayali kuelekea shambani,huku kichwani akiwa na mawazo mengi

    juu ya hatma ya mwanae.

    Akiwa anatoka nje ya

    uzio wake wa nyumba,uzio ambao ulitengenezwa kwa nyasi,Kwa mbali alishangaa

    kumuona kijana akija uelekeo wa nyumba yake huku akikimbia.Kitendo hicho

    kilimfanya aweze kuweka jembe lake chini,pamoja na kikapu kilichokuwa na maji

    ya kunywa pamoja na chakula kwa matumizi ya shambani siku nzima.

    “Aiweee…mama

    ,Njoshi ni memkuta…aiweeh”,Ngesha alimsalimia mama yake Njoshi na kumuulza

    kuhusu rafiki yake,huku mama akipumua baada ya kumtambua kijana aliyekuja

    nyumbani kwake,na pia hakuweza kuleta taarifa mbaya.

    “Aiweeeh

    mwanangu,rafiki yako aliitwa na mfalme tangu jana asubuhi,mpaka sasa sina

    taarifa yoyote,aiweeeh”,mama Njoshi alimjibu rafiki yake mwanae,na kumtia

    hofu sana,kitendo ambacho kilimfanya Ngesha kutoweka bila hata kuaga kuelekea

    ikulu,kwani alitambua kuwa rafiki yake lazima atakua hatarini kama kweli

    alienda ikulu tangu siku iliyopita na hajarudi mpaka wakati ule.

    Kifo chahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mfalme,haitakiwi wananchi wa Mwamutapa wafahamu,zaidi ya familia ya mfalme na

    mtu aliyelifuata jeneza msituni,lakini Ngesha kaelekea ikulu kwenda kujua nini

    kinaendelea kwa rafiki yake Njoshi.…







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog