Search This Blog

JENEZA LA AJABU - 1

 

    IMEANDIKWA NA : HAKIKA JONATHAN



    *********************************************************************************





    Simulizi : Jeneza La Ajabu

    Sehemu Ya Kwanza (1)







    Ikulu kwa mfalme ;

    “Siwezi kufa

    kirahisi namna hii, dunia tamu bwanaaa weeeh, mali zangu hizi nitamuachia

    nani?? “,yalikuwa ni maneno ya kejeli kutoka kwa mfalme wa nchi ya

    Mwamutapa, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa mganga wake wa kienyeji kuwa

    kashindwa kumtibu maradhi yaliyokuwa yakimsumbua, hivyo asubili kufa tu. Hali

    iliyopelekea mganga yule kujuta kauli yake kwani, mfalme aliamuru auawe kwa

    kukatwa kichwa chake, na kisha kiwiliwili chake kitupwe ndani ya bwawa la mamba

    waliofugwa na mfalme kwa ajili ya kula watu waliomchukiza na kumpinga katika

    uongozi wake. “Yani mimi nife, siwezi kufa mimi, labda utangulie mpuuzi

    wewe “,mfalme Mutapa, alijitamba kwa mala nyingine tena, huku akishuhudia

    kichwa cha mganga wake kikitenganishwa na kiwiliwili,kutokana na kushindwa

    kumtibu mfalme na kumwambia asubili kifo tu, jambo ambalo mfalme alilichukulia

    kama katukanwa na kudharauliwa.

    Mitaani katika nchi ya

    Mwamutapa;
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

           Hali ngumu ya maisha inazikumba familia

    nyingi katika ardhi ya Mwamutapa, huku lawama nyingi zikitupwa kwa mfalme,

    kwani wanaume wengi wenye nguvu na vichwa vya familia, walitumikishwa kwa nguvu

    katika mashamba ya mfalme na kisha kulipwa ujira mdogo,jambo ambalo

    lilimchukiza kila raia wa Mwamutapa. Kelele zao za mateso hasikusaidia

    chochote, kwani kila mtu aliyejifanya kupinga kunyanyaswa, alijikuta akiuawa

    kikatili, hali iliyowaogopesha wengine na kujikuta wakikubaliana na manyanyaso

    kutoka kwa mfalme, kwani waliogopa kifo.

    “Naamini ipo siku

    yatakwisha, usilie mama yangu “,ilikua ni sauti kutoka kwa kijana mkakamavu

    Njoshi, akimunyamanzisha mama yake, baada ya kupokea taarifa za kifo cha mume

    wake kwani alishindwa kumtibu mfalme. “Mwanangu baba yako kaondoka,

    tumebaki wawili tu, nakuomba uachane na Grace, mfalme atakuua  na wewe, tegemeo na faraja langu lililobakia

    “,mama Njoshi alizidi kulia kwa uchungu, huku akimusisitiza mwanae

    kuachana na Grace,msichana mrembo sana na mtoto pekee wa kike wa mfalme. Jambo

    ambalo kwake aliliona ni gumu sana na halitowezekana, kwani alimpenda sana

    Grace licha ya kupokea vitisho  mala

    kadhaa kutoka kwa mfalme ili aachane na Grace. Na kila mala mfalme alipojaribu

    kumuua Njoshi alishindwa, kwani alifanikiwa kutegua mitego yote aliyotegewa ili

    aweze kufa, kwani alikua ni hodari sana na aliweza kulishinda jeshi la mfalme

    mala nyingi, moja ya sababu ambazo Grace zilimfanya ampende sana Njoshi, kwani

    alihitaji mwanaume atakaye muoa awe ni shujaa na si mwanaume suruali tu,

    asiyeweza kumlinda na hatari yoyote.

    “Usjali mama, mimi

    nipo siku zote, nitakulinda, lakini naamini ipo siku Mwamutapa itakua huru, na

    mimi nitakuwa kiongozi wake “,kijana Njoshi aliongea kwa ujasiri na

    kujiamini kwani ziku zote alifanya mazoezi ya kila aina, ili tu siku moja

    afanye mapinduzi na kuokoa wananchi dhaifu kutoka kwenye utumwa na uongozi wa

    mabavu wa mfalme Mutapa, jambo ambalo mama yake aliliona kama ndoto ya mchana,

    ambayo Njoshi alikuwa akiota.

    “Mwanangu banaa

    unanifurahisha, hebu toa upuuzi wako huko “,mama Njoshi aliongea huku

    akitabasamu kwa mbali kutokana na maneno aliyoambiwa na mwanae, na kumfanya

    asahau machungu ya kumpoteza mume, japokuwa alikuwa ameshazoea na kuona kama

    vifo ni jambo la kawaida katika familia yake, huku akikumbuka jinsi wanae

    watatu walivyopoteza maisha kutokana na njaa kali iliyotokea miaka kadhaa

    iliyopita, na kumuachia Njoshi pekee. “Nakuombea mwanangu, ndoto zako ziwe

    kweli “,mama alizungumza huku akimkumbatia mwanae, bila kutambua kuwa

    Njoshi alijawa na hasira, huzuni na machungu kwa kumpoteza baba yake na kuapa

    kulipiza kisasi, kwani hakutaka mama yake agundue huzuni hiyo na kuzidi kumpa

    machungu mama yake aliyempenda sana.

    Ikulu kwa Mfalme :

    Mganga maarufu wa kienyeji aliyesifika

    katika nchi ya Mwamuyeshi, nchi iliyopakana na Mwamutapa, na kuongozwa na

    mfalme Muyeshi ,anafika ikulu kumtibu mfalme maradhi yake, baada ya Muyeshi

    kupata taarifa za rafiki yake mpendwa kuugua kwa muda mrefu, hali iliyopelekea

    kumtafuta muganga katika ardhi yake ili amsaidie rafiki yake asiweze kupoteza

    maisha. “Karibu sana katika ardhi ya Mwamutapa,,, naamini rafiki yangu

    ndiyo kakutuma hapa “,mfalme Mutapa aliongea bila shida yoyote huku

    akitabasamu,huku akiwa amelala katika kitanda chake kwa takribani mwezi mmoja

    sasa bila kuamka kutoka kitandani, japo aliweza kuzungumza vizuri kama vile hakuwa

    mgonjwa.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

         “Ndiye mimi mtukufu mfalme, mganga

    kutoka katika ardhi ya rafiki yako Muyeshi, nimekuja kukusaidia “,mganga

    yule aliongea huku akijiamini, na kumfanya mfalme atabasamu kwani hakupenda

    kufa, na alitamani aishi milele jambo ambalo mganga yule alikua ameshalitambua.

    “Usjali mtukufu

    mfalme, mpaka sasa nimeshachelewa siwezi kukutibu, muda wowote kuanzia sasa

    utaweza kufa, lakini inatakiwa ukifa uzikwe ndani ya jeneza lililotengenezwa

    kutoka katika miti iliyo katikati ya msitu hatari wa Majini, msitu ambao uko

    katika ardhi yako ya Mwamutapa, ukizikwa ndani ya jeneza hilo, utaweza kufufuka

    baada ya wiki moja na kuishi milele “,mganga yule alizungumza maelezo

    marefu sana, huku jina la kijana Njoshi likijirudia rudia ndani ya kichwa cha

    mfalme, kwani ndiye kijana pekee aliyemuona anafaa kufanikisha swala hilo, na

    kutoka akiwa salama katika msitu hatari wa Majini, msitu ambao hakuna aliyewahi

    kuingia humo akitaka mali, watoto au ufalme kutoka kwa mizimu ya msitu huo na

    kutoka salama bila kupoteza maisha. “Na pia inatakiwa iwe siri, raia wako

    wasifahamu labda tu atakayekwenda huko msituni “,mganga alizidi kuzungumza

    huku mfalme mawazo yakiwa mbali sana, kwani mwanae Grace alishamuonya kuwa

    Njoshi siku akipata matatizo yaliyosababishwa na yeye, ataweza kujiua, jambo

    ambalo mfalme hakuwa tayali kumkosa mwanae wa kike pekee aliyenaye, kati ya

    watoto arobaini kutoka kwa wake watano alionao ,mtoto ambaye alizaliwa na mke

    wa tano baada ya wake zake wanne waliotangulia kushindwa kumzalia mtoto wa

    kike.

           “Sawa …sawa sa…wa ni…me…kusikia

    “,mfalme alijibu bila kujitambua huku mawazo na maswali lukuki

    yakikisumbua kichwa chake .



    Ikulu kwa mfalme;

    Ngome ya mfalme

    inakumbwa na majonzi mazito ,kutokana na hali ya mfalme kuwa mbaya sana. Wapo

    waliofurahi kumuona katika hali ile, hasa wananchi wake ambao hawakupendezwa na

    uongozi wake huku wakitamani afe haraka, waweze kuwa huru kutoka katika taabu

    na mateso yaliyosababishwa na uongozi wake wa kikatili wa mfalme Mutapa. Lakini

    wachache walihuzunika sana, hasa watoto wake pamoja na wake zake mfalme, huku

    wakimuomba Mungu amuepushe na umauti.

    “Mfalme mimi

    ninaondoka kurudi nyumbani, lakini zingatia yale yote niliyokuambia, kwani kama

    unavyoiona hali yako inazidi kuwa mbaya, usipokuwa makini mali zako na ufalme

    wako utakwenda na maji “,asubuhi na mapema, mganga kutoka katika ardhi ya

    Mwamuyeshi, akiwa ameshika kila kitu kwa ajili ya safari yake ya kurudi

    nyumbani, anamuaga mfalme huku akimsisitiza kuzingatia maelekezo aliyompatia na

    kisha kupanda farasi na kuondoka, huku akiongozana na askari wawili aliokuja

    nao kwa ajili ya kumlinda njiani, askari waliotoka katika ngome ya mfalme

    Muyeshi.

    Mfalme Mutapa akitikisa

    kichwa chake kuashiria kukubaliana na maelekezo ya mganga, na kumshuhudia

    akitokomea mbele ya uso wake, anaamua kutoa amli kwa kutumia maandishi Njoshi

    kufika ikulu haraka sana, kwani mfalme alishindwa hata kuzungumza hali

    iliyowatia hofu watoto wa mfalme pamoja na wakeze.

    “Baba nakuombahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    usimdhuru Njoshi kwa chochote kile, lolote baya likimtokea sitajali hali yako

    mbaya uliyonayo, nitakuua “,Grace aliongea huku akionesha kumaanisha kwa

    maneno aliyoyazungumza, bila kujali ni kiasi gani alimpenda baba yake aliapa

    kumtoa roho kwa mikono yake, kama tu kipenzi chake Njoshi akidhurika na jambo

    lolote   na kuacha familia nzima ya

    mfalme ikiwa midomo wazi, kwani hawakuamini maneno yale kama yalitoka kinywani

    kwa Grace, msichana aliyependwa sana na mfalme.

    “Hahaa, sasa mpaka

    wewe unamuua baba, sisi tutakua wapi, labda uanze kutuua sisi “,Kijana

    mkubwa wa mfalme, kijana ambaye Mutapa alimuamini sana na kumuahidi kumrithisha

    ufalme na mali zake, kutokana na uhodari wake alizungumza kwa kejeli, na

    kupelekea familia nzima kucheka na kusahau hali mbaya ya mfalme aliyokuwa nayo.

    Ghafla mfalme alitoa

    amli ya familia nzima kukaa kimya kwa kutumia ishara, huku akitaka agizo la

    Njoshi kufika ikulu, litekelezwe mala moja bila kujali onyo kali alilopokea

    kutoka kwa binti yake Grace, mtoto pekee wa kike aliyempenda sana.

    Nyumbani kwa kina

    Njoshi;

    Ilikua siku ya jumatatu

    asubuhi, kama kawaida Njoshi hufanya mazoezi makali katika siku hii kwani wiki

    nzuri huonekana siku hii, hivyo aliamini akifanya vizuri mazoezi siku ya

    jumatatu, atakuwa fiti wiki nzima. Aliamka saa kumi na moja asubuhi, na kuanza

    mazoezi ya kukimbia, siku zote alipenda kukimbia huku akiimba, kwani alikatiza

    mitaa karibu yote ya nchi ndogo ya Mwamutapa, bila kujitambua kwani nyimbo

    alizoimba zilimtia moyo na kumuondolea uchovu. “Ngoja nikimbie, nikimaliza

    nije kunyenyua vyuma, ukombozi sio lelemama lazima wachache tuumie

    “,Njoshi aliongea kwa ujasiri huku akitamani siku moja aweze kuishika nchi

    na yeye kuwa mfalme, huku Grace akiwa malikia, kwani msichana mrembo Grace

    alipendwa sana na wananchi na aliwaokoa mala nyingi walipokuwa wakionewa na

    baba yake pamoja na kaka zake, kwani aliwaombea msamaha na kusikilizwa.

    Walimuona kama ndio kondoo pekee aliyeishi ndani ya kundi la simba. Njoshi

    alizidi kukimbia lakini bila kutegemea alijikuta akiishiwa na pumzi haraka sana

    tofauti na siku zingine, bila kupoteza muda aliamua kurudi nyumbani kufanya

    mazoezi mengine. “Mwanangu kweli wewe ni shujaa, natamani ndoto zako

    zitimie nikiwa hai nishuhudie ukiwakomboa Wanamutapa wote “,ilikua tayali

    imeshafika saa moja asubuhi, mama yake Njoshi aliweza kuamka na kumkuta mwanae

    akiendelea na mazoezi, na kuzungumza maneno makali yaliyomshitua sana Njoshi,

    haikuwa kawaida kwa mama yake kumwambia maneno mazito kiasi kile.

    Njoshi alisitisha

    mazoezi na kisha kutaka kumuulza mama yake, kwanini alizungumza vile, kwanini

    mama yake asishuhudie ukombozi ambao mwanae alikuwa akiupanga, mama yake kaona

    nini mbeleni katabili nini. Njoshi alizidi kujiuliza maswali kichwani mwake,

    huku akimsogelea mama yake, mke wa marehemu Nyangoma, mganga na mtabili

    aliyekuwa akitegemewa sana na mfalme Mutapa. Kutokana na kutabili kuwa ipo siku

    mfalme atamuua kikatili bila kujali mema yote aliyomfanyia, aliamua kumfundisha

    uganga na utabili mke wake, ili siku akifa mke wake aweze kurithi mikoba.

    “Mwanangu Njoshi

    Nyangoma, naona hatari kubwa iko mbele yako, utasafiri safari ndefu yenye visa

    na mikasa ya ajabu ,mkanda huu mweusi na panga hili ndio siraha yako kuu,

    iliyomuwezesha baba yako kutoka salama katika msitu wa majini, usikatae kwenda

    huko, huko ndipo utaupata ufalme wa nchi hii, lakini ukirudi nyumbani utakuta

    kabuli langu, mimi nikiwa tayali nimeshakuwa mifupa “,mama Njoshi

    alizungumza kwa uchungu sana huku machozi yakimtoka, na kumkabidhi mwanae begi

    dogo jeusi,kwani ndio ulikuwa mwisho wa kuonana yeye na mwanae mpendwa Njoshi.

    “Sikuelewi mamahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    unaongea nini, mimi msituni huko niende kufanya nini sasa, kwanza huwezi kufa

    mimi nitakulinda mpaka dakika ya mwisho “,Njoshi aliongea huku akimfuta

    mama yake machozi, huku mama yake akiukumbuka ule msemo wa wahenga, msemo ambao

    ulikua maarufu sana enzi zile afrika ikitawaliwa na wazungu, msemo uliosema

    jambo usilo lijua ni kama usiku wa giza.

    Njoshi akiwa

    amemkumbatia mama yake, akizidi kumbembeleza aweze kunyamanza, alishangaa kuona

    kundi kubwa la vijana shupavu, likiwa limevalia bukta fupi nyeusi, pamoja na

    ngozi ya chui, huku mikononi wakiwa wameshika mikuki na kila aina ya siraha za

    kivita, bila shaka aliweza kuwatambua, lilikuwa ni jeshi la mfalme Mutapa.

    “Aiweeeeeeh

    ………Njoshi, aiweeeeh ………”,askari wale waliweza kumsalimu Njoshi, na

    kumfanya mama yake kuacha kumkumbatia mwanae na kushuhudia watu wale

    waliomsalimia mwanae. “Aiweeeeeh ………askari waaminifu wa mfalme wangu wa

    ardhi ya Mwamutapa, niwasaidie nini? “,Njoshi aliitikia salamu kwa upole

    na hekima, huku akiificha hasira yake na kisasi kizito kilicho rohoni mwake,

    kutokana na baba yake kuuawa kikatili na mfalme.

    Kwa upande wa mama yake

    hakushangaa chochote, kwani alikwishaona kila kitu kitakachotokea mbele, na pia

    siri ya mfalme ambayo wananchi hawakutakiwa kuifahamu, kuhusu kuzikwa mala

    atakapokufa na kisha kufufuka bila wananchi kutambua chochote, ili aweze kuishi

    na kutawala milele.

    “Tumekuletea

    ujumbe huu wa maandishi kutoka kwa mfalme, mkwe wako tafadhali pokea ……iweeeeh

    “askari wale waliongea huku, mmoja aliyeonekana kuwa na cheo kikubwa kuwazidi

    wenzake kutokana na kuvaa ngozi ya simba, ngozi iliyokuwa ikivaliwa na kila

    kiongozi wa nchi ya Mwamutapa, akimkabidhi Njoshi karatasi yenye maandishi na

    kisha kuisoma.

    “Iweeeeeh …mkwe

    wangu, nakuomba katika ikulu yangu, ninashida na wewe, nataka tuwekeane mkataba

    ili uweze kumuoa binti yangu Grace “,Njoshi alisoma maneno yale na kisha

    kutabasamu, tabasamu ambalo liliwafanya askari wale wa mfalme kuangaliana na

    kisha kukonyezana, hali iliyoonesha kutambua siri fulani iliyokuwa imefichika.

    “Mama peleka begi

    hili ndani, mimi ngoja nikaonane na mfalme “,Njoshi aliongea huku

    akionekana kufurahia sana, kwani hakuamini kama ipo siku mfalme atamtamkia kuwa

    yeye ni mkwe wake,kwani siku zote aliambulia matusi na kutishiwa kifo,

    alipoingia anga za mfalme Mutapa.

    “Hapana mwanangu,

    kama unanipenda, naomba hilo begi lisitoke mgongoni mwako “,mama yake

    Njoshi aliongea huku akiwa na huzuni moyoni, huku akijaribu kutabasamu kuficha

    huzuni yake, kwani huo ndio ulikuwa ni mwisho wa kuonana na mwanae katika ulimwengu

    huu.





    Msitu wa Majini;

            Ilikua mida ya jioni siku ya jumatatu ,

    tetemeko la kutisha linatokea katika msitu wa majini,Malikia wa msituni,

    kiongozi aliyemiliki msitu na kuongoza viumbe vyote vilivyopatikana ndani ya

    msitu anaamua kuitisha kikao, kwani tetemeko lile liliashiria jambo fulani,

    kama ilivyozoeleka katika msitu huo, tetemeko likitokea basi muda wowote msitu

    ulikua hatarini kuvamiwa.

    “Ndugu zanguhttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    majini, mapepo na mizimu ya mababu zetu, msitu wetu uko hatarini kuvamiwa ,na

    niwajibu wetu kuulinda msitu huu, pia inatakiwa tulipize kisasi kwani mtu

    anayekuja kuvamia msitu huu, baba yake aliwahi kuja hapa msituni na kuua ndugu

    zetu na kisha kutokomea na baadhi ya mali zetu ili awe mganga na mtabili

    hodari, japo ameshapoteza maisha “,malikia alizungumza kwa hasira, katika

    kikao cha ghafla alichokiitisha muda mfupi baada ya tetemeko kutokea, huku

    umati wa viumbe hatari sana wa msitu wa majini, msitu uliokua na utajiri

    mwingi, zikiwemo dhahabu na almasi, wakiwa makini kumsikiliza malikia wao na

    kujiandaa na mapambano.

    “Aiweeee mtukufu

    malikia wa msitu huu,tuko tayali kutekeleza maagizo yako, na kuua chochote

    kitakachokanyaga ardhi hii “,ilikua ni sauti ya majini waliohudhuria

    kikao, huku wakijawa na uchu wa kulipiza kisasi hasa wakikumbuka jinsi mzee

    Nyangoma, baba yake Njoshi jinsi alivyofanikiwa kuiba mkanda pamoja na panga

    lenye nguvu za ajabu, na kutoroka navyo huku akiua baadhi ya majini, kitendo

    kilichowakasilisha viumbe wote wa msituni.

    Ikulu kwa mfalme;

    Kijana Njoshi anafika ikulu kwa mfalme

    na kushangazwa na jambo aliloliona mbele ya macho yake, hali ya mfalme ilikua

    mbaya sana kiasi kwamba hakuweza hata kuinuka kitandani wala kufungua kinywa

    chake na kutamka neno lolote lile, kwa upande mwingine alitamani mfalme apoteze

    maisha kwani aliona ndio utakuwa mwanzo wa ardhi ya Mwamutapa kuwa huru kutoka

    katika uongozi wake wa kidikteta ,na pia yatakua ndio malipo ya dhambi zote za

    mauaji aliyoyafanya, huku baba yake akiwa miongoni mwa watu waliouawa kikatili

    na mfalme.

    Njoshi akiwa bado

    amepigwa na butwaa, alianza kupata picha kuwa inawezekana aliweza kudanganywa

    kuwa aliitwa na mfalme ili aozeshwe Grace,kwani kwa wakati ule, machozi ya

    huzuni hayakukatika machoni kwa Grace,na kumfanya aamini mawazo yake, kuwa

    palikuwa na tatizo nyumbani kwa mfalme.

    “Aiweeeeeh mtukufu

    mfalme, mtumwa wako Njoshi Nyangoma nimeitika wito wako, aiweeeeh ……mfalme

    Mutapa udumu milele”,Njoshi aliongea huku akiwa amesimama mbele ya kitanda

    cha mfalme, huku familia nzima ikiwa imekaa kimya, wakimuomba Mungu Njoshi

    akubaliane na ombi la mfalme, kwani waliamini mfalme hata akipoteza maisha

    ataweza kufufuka ndani ya wiki moja, jambo ambalo lingewezekana kama angezikwa

    ndani ya jeneza la ajabu, jeneza ambalo Njoshi inatakiwa akalitengeneze kwa

    kutumia miti inayopatikana katikati ya msitu wa majini na kisha kuja nalo ikulu

    kwa mfalme.

    “Kijana wangu

    Njoshi, utafanikiwa kumuoa binti yangu Grace, na kumiliki nusu ya ufalme wangu,

    kama tu ukikubali kwenda katika msitu wa majini, na kutengeneza jeneza kisha

    kuja nalo hapa “,yalikuwa ni maneno yaliyoandikwa kwa maandishi na mfalme,

    maneno ambayo Njoshi aliyasoma na kisha hofu ya kifo kumuandama, kwani hakuna

    mtu aliyewahi kupona kutoka katika msitu wa majini, isipokuwa baba yake

    pekee.Njoshi alikumbuka maneno ya mama yake alimwambia kuhusu hatari hii, na

    kisha kumsihi asikatae kwenda kwani huko msituni ndiyo sehemu pekee ya kuupata

    ufalme, pia Njoshi alikumbuka siraha alizopewa na mama yake na kuziweka ndani

    ya begi kisha kumsihi asiweze kulitupa begi hilo.

    “Ndiyo mfalmehttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wangu mtukufu, nimekubali, aiweeeh mfalme udumu milele, “Njoshi alikubali

    ombi la mfalme, na kufanya nyuso za familia nzima ya mfalme kutabasamu kwa

    furaha, isipokuwa Grace, kwani hakutaka mpenzi wake kwenda msituni ndio maana

    alikuwa akilia toka mwanzoni, na wala hakulizwa na hali mbaya ya baba yake

    aliyonayo, bali jambo ambalo Njoshi aliweza kuitiwa ikulu, lilikuwa la hatari

    sana na aliamini atampoteza mpenzi wake kama atakubali ombi la baba yake.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog