Search This Blog

MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI - 3

 






Simulizi : Mama Usinifundishe Uchawi

Sehemu Ya Tatu (3)





“Sharifu, ina maana unioni au?,” Mama Abuu aliuliza mara baada ya kuona amepitwa bila kupewa salamu na Sharifu.



“Unataka nifanyeje?,” Sharifu naye akauliza huku akibetua mdomo kwa dharau kumdharau Mama Abuu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“Mama yako huwa unampita bila kumsalimia kama hamjaonana?.”



“Mama ni mama na wewe utabaki kuwa wewe tu...kwani ni lazima, kukupa salamu?.”



“Hama kweli mtoto umleavyo, ndivyo akuavyo yaani matendo yako ayafanani nawe kabisa,” Mama Abuu alisema kwa kutoamini majibu anayojibiwa na Sharifu.



“Unataka kunilea wewe au?, halafu mimi naona kama unachelewa nyumbani kufanya shughuli zako,” Sharifu alizidi kuonyesha dharau kwa mama Abuu wazi wazi.



“Sasa hivi, ushaanza kuvuta bangi na kama sio bangi unaugua uchizi.”



“Wewe mama sasa unanivunjia heshima, katika siku niliyokosewa leo umenikosea.”



“Acha nikukosee tu maana hujiheshimu.”



“Unijui?.”



“Kwa hiyo!,” Mama Abuu naye aliongea kwa dharau mara baada ya kugundua Sharifu anamdharau.



“Utaona,” Sharifu aliongea kwa kumaanisha japo Mama Abuu alichukulia kama mzaha.



“Aisee!!!, yaani wewe kisisimizi unanitishia maisha Tembo.”



“Unachukulia ninayoongea ni mzaha, utakuja juta baadae,” Sharifu alisema na kutoa sonyo lililojaa vitisho ndani kisha akaondoka na kumwacha Mama Abuu ameduwaa.



Sharifu akafika kwa Mama Stumai na kumkuta yupo nje kakaa kwenye kisturi anasuka mkeka. Sharifu akakaa pembeni ya mlango wa kuingilia ndani mwa Mama Stumai mara baada ya kukaribishwa.



“Eeenh, za nyumbani?,” Mama Stumai aliuliza mara baada ya kumuacha Sharifu kwa muda apumzike.



“Salama.”



“Kilichokuleta ni nini?, maana sio kawaida kuja nyumbani kwangu,” Mama Stumai alizungumza huku macho yake yakiwa bize na kusuka mkeka.



“Nimetumwa na mama nije kufuata pesa zake.”



“Mama yako siku hizi chizi eeenh!.”



“Kwa nini?.”



“Nishamueleza kuwa pesa zake simpatii hadi anilipe posho yangu ya kijumbe,” Mama Stumai aliongea kwa kukataa kukabidhi pesa. Akapumzika kuongea hatimaye akaendelea kuongea.



“Siwezi kutoa pesa mpaka nilipwe kwanza, nenda kamwambie akae akijua hivyo,” Mama Stumai alikataa katakata kutoa pesa za Binti Mngane.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Sharifu hakutaka kujibizana tena na Mama Stumai alichokifanya ni kuaga na kuondoka kuelekea kwa kina Kondo kuchukua mpini. Alipofika nyumbani kwa kina Kondo akamkuta Kondo yupo nje ya nyumba yao akitengeneza huo mpini.



“Karibu,” Kondo alikaribisha mara baada ya kuona Sharifu kawasili nyumbani kwao.



“Asante...lakini sikai nimefuata mpini wangu,” Sharifu aliongea na Kondo huku amesimama wima.



“Sawa...mpini wako ndiyo huu namalizia kwa hiyo subiri kidogo.”



“Sawa” alikubali Sharifu na hakupinga hata kidogo akasubiri, ndani ya dakika tano Kondo alikuwa kashamaliza kutengeneza mpini na akamkabidhi mwenyewe.



“Utanipa, bei gani?,” Kondo aliuliza mara baada ya kumkabidhi mpini hule Sharifu.



“Nitakupoza, na elfu tano,” Sharifu aliongea kisha akatoa pesa mfukoni na kumkabidhi Kondo.



Kondo baada ya kulipwa, Sharifu akaaga na kurudi nyumbani. Alifika ikiwa ni jioni akamkuta mama yake anamenya kunde kwaajili ya mboga.



“Mbona, umechelewa?” lilikuwa swali la kwanza la Binti Mngane akimuuliza mwanae.



“Mama Stumai, ndiye aliyenichelewesha” alijibu Sharifu kisha akakaa sakafuni.



“Kwanini?.”



“Kagoma, kunipa pesa!.”



“Kwanini?.”



“Kasema, hadi umlipe pesa za kijumbe!.”



“Mama huyu mpumbavu...naona ajanijua vizuri hivi punde atanijua tu,” Binti Mngane aliongea kwa kupayuka na kuonekana mwenye hasira mara baada ya kupewa taarifa zile na mwanae.



Sharifu alipompatia taarifa mama yake akaingia chumbani akawasha redio sauti ya juu. Masaa mawili mbele Binti Mngane akaivisha chakula na kukitenga ukumbini kwenye mkeka baada ya hapo akaenda kumuita mwanae kipenzi.



“Genda Heka,” Binti Mngane kutokana na kuwa na hasira bado ya kutopewa pesa yake ikampelekea hadi kumuita mwanae jina la ajabu.



Sharifu kwa kuwa alifungulia redio kwa sauti ya juu hata mama yake alivyomuita hakusikia. Binti Mngane kwa kuona mwanae haitiki ikabidi aende hadi mlangoni kumgongea huku akiendelea kuita jina lile la ajabu lisilostahili hata kwa jamii.



“Genda Heka.”



“Eeeh” aliitika Sharifu kwa kukurupuka kitandani mara baada ya kupunguza sauti ya redio.



“Muda wote nakuita hadi sauti inataka kukauka, kumbe ulifungulia redio lako?,” Binti Mngane aliuliza mara baada ya kugundua mwanae alifungua redio.



“Nisamehe,” Sharifu aliomba msamaha kwa unyenyekevu.



“Endelea lakini ukija kuwa kiziwi, hamna mtu atakaekupeleka hospitali,” Binti Mngane alimuonya mwanae.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“Lakini mama, redio inakufariji,” Sharifu aliongea kwa utani.



“Nitokee huko...lakini sishangai sana kwa kuwa wewe si mluguru ubishi ni jadi yako.”



“Sikatai, mimi ni mzalendo na kabila langu hivyo acha nidumishe ubishi.”



“Ebu, tufute mazungumzo maana nikiendelea kubishana nawe utasababisha tule ugali jiwe,” Binti Mngane aliongea huku akichota tonge la ugali mara baada ya kufika ukumbini na kuanza kula.



Wakafuta mazungumzo kwa muda wakala chakula. Sharifu akala matonge kadhaa akaanza kutapika mfululizo pembezoni mwa mkeka.



“Unafanya, upuuzi gani?,” Binti Mngane alibwata mara baada ya kuona mwanae anafululiza kutapika.



“Ni hasira, tu,” Sharifu alijibu kisha akatoka kutupa matapishi.



“Hasira, gani hizo?,” Binti Mngane aliuliza kwa kufura mara baada ya mwanae kurudi kwenye kutupa matapishi.



“Nina hasira, na Mama Abuu na Mama Stumai.”



“Mama Abuu, kakufanyaje tena?.”



“Mama Abuu wakuniita mimi chizi, hama zangu hama zake leo ataona.”



“Wewe umempania Mama Abuu, ila mimi nimempania sana Mama Stumai...kwa hiyo katika pilikapilika za leo hutokuwa peke yako tutakwenda wote,” Binti Mngane alisema huku akijaribu kuleta furaha moyoni.





Walipomaliza kula Sharifu akatoa vyombo akaenda chumbani na kumwacha mama yake kwenye mkeka pale ukumbini akishona khanga. Safari hii Sharifu hakutaka kusikiliza redio, alipofika kitandani akajitupa chali na kujibembeleza kwa kujitingisha miguu punde tu akapitiwa na usingizi. Alikuja kushtuka mishale mingine kuchungulia dirishani akaona giza limetanda pande zote kuashilia usiku umeingia huku likisindikizwa na wingu zito la mvua na mweku mweku zikimurika na kuzima kuwa giza. Hali ile kwa mtu muoga asingethubutu kunyanyua miguu yake na kutoka nje.



“Giza hili, naona linaniruhusu kwenda kilingeni ngoja nikamwamshe mama,” Sharifu alijisemea nafsini kisha akajibadilisha muonekano akayayuka chumbani kwake na kutoka nje kuelekea kwenye mlango wa chumbani wa mama yake na hatimaye kuongea kwa hisia na mama yake.



“Amka mama.”



“Naona leo umewahi sio kawaida yako, ama kweli umepania,” Binti Mngane aliongea naye huku akijibadilisha muonekano mara baada ya kuamka.



“Ninashauku sana na wamama wale, si wanajifanya wanajua sasa leo watakiona cha mtema makuni,” Sharifu alizungumza huku akizungusha macho yake kimiujiza.



“Kweli dhahiri, umewapania.”



“Wewe, acha tu mama,” Sharifu alimsubiri kwa muda mama yake, ghafla akamuona mama yake ametokea kimiujiza alipo yeye. Akiwa tayari kashajiandaa wakayayuka pamoja tayari kuanza safari na kabla ya kufika kwenye tukio wakashauriana.



“Unavyoona wewe, tuanze wapi?,” Binti Mngane akauliza.



“Naona kama vile kwa Mama Abuu ni karibu tuanze kwake, baadae tukishatoka kwa Mama Abuu ndiyo twende kwa Mama Stumai,” Sharifu alimjibu mama yake huku akitupa usinga huku na kule kwaajili ya kusafisha njia.



Waliposhauriana na mama yake wakaelekea moja kwa moja kutua kwenye uwanja wa nyumbani wa Mama Abuu. Walipotua wakashangazwa sana na hali waliokumbana nayo, wakakuta zizizi kumetulia huku kukichochewa na giza. Hali ile tulivu ikawafurahisha sana.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Inaonekana Mama Abuu yupo kwenye usingizi mzito, lengo letu tulifanye haraka tuondoke,” Binti Mngane alimweleza mwanae huku akiusogelea mlango wa kuingilia ndani.



“Basi niache niingie ndani, kinachojiri nitakujuza,” Sharifu alimwambia mama yake huku akiegemea mlango wa Mama Abuu na kuyayuka kutokea chumbani.



Sharifu akamkuta Mama Abuu yupo kitandani amelala na mumewe usingizi wa pono. Akamchukua kimazingara mtuhumiwa wake na kutoka naye nje. Binti Mngane alipomuona mwanae amerudi na Mama Abuu kwa kumkokota kama mkokoteni akafurahi sana.



“Naam!!!, huo ndiyo uwanaume,” Binti Mngane alimsifia mwanae mara baada ya Sharifu kufika alipo.



“Mtu wetu, huyu hapa,” Sharifu aliongea huku akimkabidhi Mama Abuu kwa Pilato.



Alipokabidhiwa kwa Binti Mngane akamwagiwa unga mweupe wa chengachenga unaofanana na mchanga unaosaidia mtu asiweze kuamka mapema. Akiwa hajitambui wala kuonyesha dalili ya kufumbua macho akawapa moyo na kuwafurahisha Binti Mngane pamoja na mwanae.



“Huyu mtu inaonyesha dawa tuliyompatia, itatufanya tufanye kazi yetu bila kipingamizi,” Binti Mngane alimwambia mwanae huku akipanda tumboni mwa Mama Abuu aliye na ujauzito wa miezi nane.



“Umejuaje?,” Sharifu aliuliza huku akimkodolea macho mama yake.



“Nimeona kuwa Mama Abuu, hana kinga.”



“Kwa hiyo tutafanikiwa, kufanya kazi yetu kwa uzuri,” Sharifu aliongea kisha kwa pamoja wakafurahi na mama yake huku wakicheza kwa kukata viuno kwa maringo.



Baada ya muda kadhaa Binti Mngane akafungua kitambaa cheusi kisha akatoa kimzizi chenye miiba mikali. Akakitemea mate kimzizi kile hatimaye akamlisha kinywani Mama Abuu. Walipohakikisha wamemaliza kumlisha kimzizi wakamrudisha Mama Abuu chumbani aendelee na usingizi.



“Mama Abuu dawa yake ipo jikoni inachemka, baada ya muda mfupi atainywa,” Binti Mngane alimweleza mwanae mara baada ya kumrudisha Mama Abuu.



“Nikiwa nawe nafarijika na kujifunza, mambo mengi sana mama yangu.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Yakupasa ujifunze mengi tunayofanya, ili baadae uweze kuwa mwanachama madhubuti,” Binti Mngane alimweleza mwanae huku akinusisha pua kila upande ajue kama kupo shwari.



“Nitajifunza kila kitu kutoka kwako...lakini mama muda ushakwenda twende kwa Mama Stumai sasa tukamalize kazi yetu,” Sharifu alimwambia mama yake mara baada ya kuona wanachelewa kwenda kwa Mama Stumai.



“Kweli tuondoke, tusije kuchelewa tukaumbuka kukipambazuka,” Binti Mngane safari hii alinusa juu ya anga kisha akamshika mikono mwanae na kuyayuka eneo lile.



Binti Mngane na mwanae wakaelekea nyumbani kwa Mama Stumai. Hali ya hewa kwa wakati ule ilionyesha anga ikiwa na mwanga hafifu huku nyota zikiendelea kumelemeta kwa mbali ikiashilia kuwa kunakaribia kupambazuka.



“Tushafika sehemu husika, nisubiri nje safari hii mimi niende nikamalize mchezo.” Binti Mngane alinong'ona mara baada ya kutua kwenye uwanja wa Mama Stumai.



“Ila kuwa makini, si unajua madhara ya hii nyumba?,” Sharifu aliuliza kwa kumhabarisha mama yake.



“Madhara gani tena? mbona unanitisha,” Binti Mngane aliuliza kwa kutaka kujua madhara ya nyumba ile.



“Wewe ushasahau, kama Mama Stumai ni mrokole?.”



“Mmh!!! nilikuwa nimeshasahau, nitakuwa mwangalifu usijali kuhusu hilo mwanangu,” Binti Mngane alisema huku akienda ndani kinyume nyume mara baada ya kufungua mlango.



“Sawa, nitakusubiri,” Sharifu aliongea huku akizunguka nyumba ya Mama Stumai kwa kusota makalio kuhakikisha usalama.



Binti Mngane alipokaribia mlango wa kuingia chumbani mwa Mama Stumai akasotea mlango kwa makalio hatimaye mlango ukafunguka kisha akaingia chumbani. Alipofika chumbani akamkuta Mama Stumai akiwa amelala nafasi ile Binti Mngane hakutaka kuichezea.



“Wewe si mjanja!. Sasa leo nakuonyesha kama kuna wajanja zaidi yako,” Binti Mngane alijisemea moyoni kwa kumtupia vijembe mzazi mwenzake.



Baada ya kutupa vijembe hakuchelewesha akanyoosha mkono wa kushoto mbele kisha likatokea pembe la ng'ombe. Akampiga Mama Stumai miguuni na lile pembe, alipoona kamaliza mchezo bila kipingamizi chochote akajipongeza kwa kicheko hatimaye akayayuka pale chumbani na kutokea nje alipomwacha mwanae.



“Sasa kazi imekwenda vizuri bila kuchelewa tutoweke eneo hili kabla akujapambazuka,” Binti Mngane alimwambia mwanae kisha wakaondoka na kuja kutua kwenye uwanja wao wa nyumbani na kila mmoja akaingia chumbani kwake kujipumzisha kwaajili ya kuondoa uchovu.



**********

Asubuhi ya alfajiri mume wa Mama Abuu akawahi kuamka kwaajili ya kuwahi shamba kama desturi yake ya siku zote, lakini alivyoamka akashangazwa na jambo aliloliona kwa mkewe.



“Wewe Siawezi,” Baba Abuu alimwamsha mkewe kwa kumpiga vibao.



“Kuna nini, Chang'ari?,” Mama Abuu aliuliza akiwa bado usingizini.



“Tumbo umelifanyaje?,” Baba Abuu alifoka na uso kaukunja kama Nyati.



“Kwani lina nini?,” Mama Abuu aliuliza na hakuelewa mumewe ana maanisha nini kutokana kuwa alikuwa bado anaendekeza usingizi.



“Mtoto wangu wa tumboni umempeleka wapi?...ushaenda kumtoa kafara nini?,” Baba Abuu aliuliza kwa sauti ya juu huku akionyesha kuwa na hasira.



“Mungu, wangu!!!,” Mama Abuu alishtuka toka usingizini mara baada ya kuona ujauzito wake kupotea. Kisha akameza mate kwa muda na kumtazama mumewe aliyefura kama mzoga wa Bata na kulijibu swali aliloulizwa.



“Mimi sielewi kitu,” Mama Abuu alijibu huku akijiangalia tumbo lake mara mbili mbili asiweze kuamini kilichotokea.



“Wewe mwanamke usinifanye sina akili, nina akili zangu timamu niambie mtoto yupo wapi?.”



“Sijui Chang'ari.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Nakuambia hivi kuanzia sasa sihitaji kukuona katika nyumba yangu mpaka pale utakapomrejesha mtoto wangu. Mwanamke gani unaendekeza ushirikina,” Baba Abuu alimfukuza mkewe kwa kumvuta atoke nje huku akimpiga ngumi za tumboni mara baada ya kuona mkewe mbishi kutoka ndani. Hakumsikiliza kabisa mkewe, akamfukuza mkewe kama Mbwa aliyemlia mboga ya ngama.



**********

Mama Stumai akaamka asubuhi akiwa na furaha tele, lakini furaha yake ikaja kuzizima bila kutarajia mara baada tu ya kunyanyua mguu wake wa kuume na kuona umepooza.



“Looh!!!, nini tena hiki?,” Mama Stumai akajiuliza.



“Siamini, mbona haya maajabu nilale mzima niamke nimepooza,” Mama Stumai alijisemea huku akijikokota kushuka kitandani na kukaa sakafuni kwaajili ya kujinyoosha miguu athibitishe.



“Nimeamini uchawi upo japo sikuamini mwanzoni, kweli usilolijua ni kama usiku wa giza,” Mama Stumai alizidi kusema na kujuta pale sakafuni. Furaha yake yote ikapotea kwa siku ile na punde tu akajikuta mwenye msongo wa mawazo. Akashindwa hata kujizuia kutoa chozi na asimuone wa kumfariji kwa nyakati ile ya matatizo kwake.



**********

Binti Mngane asubuhi na mapema akawahi kuamka na kuzifanya shughuli zake za nyumbani. Muda ulikwenda sana akaona mwanae hana hata dalili ya kuamka ndipo ikamlazimu aende kumwamsha.



“Sharifu, Sharifuu” aliita Binti Mngane kwa kupaza sauti.



“Naam!!!,” Sharifu aliitika kwa kukurupuka toka usingizini mara baada ya kuamka na kufikicha macho.



“Kulala gani hadi saa hizi?.”



“Nimechoka mama, niache nipumzike,” Sharifu alijibu kiuchovu kisha akajilaza tena kitandani.



“Mwenye usingizi peke yako, mbona nami nina usingizi ila nimeamka kufanya kazi...ebu nawe amka,” Binti Mngane alimwambia mwanae kwa kumlazimisha aamke.



“Naomba mama niache nilale kidogo. Nikiamka nitafanya hizo kazi,” Sharifu aliomba mama yake amwache alale kisha akavuta shuka akaendelea kulala.



“Lala ila jua, ukiamka kuna kazi zinakusubiri,” Binti Mngane alimuhabarisha mwanae kisha akaenda jikoni kupika. Baada ya masaa kupita Binti Mngane akawa kashaivisha uji na viazi vitamu. Akatenga chakula ukumbini kisha akaenda kumwamsha tena mwanae.



“Wewe, mtoto.”



“Naam.”



“Uji! tayari.”



“Nakuja.”



“Fanya haraka.”



Sharifu akatoka chumbani kwake mara baada ya kuitwa na mama yake huku akipepesuka kama mlevi wa gongo kutokana na usingizi. Akajifikicha macho ili aweze kuona mbele vizuri. Akajikongoja taratibu hadi ulipo mswaki kisha akauchukua na kuelekea uwani ili kusafisha meno na uso nyuma akimwacha mama yake akimngoja ukumbini.



“Sharifu,” Binti Mngane alimuita mwanae mara baada ya kuona anachelewa kurudi.



“Na naam,” Sharifu aliitika kwa shida kutokana na mswaki kuwa kinywani.



“Huko kunawa, mwaka!.”



“Nakuja, ndiyo nafunga mlango wa uwani.”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“Harakisha bwana, tuje tule,” Sharifu punde tu alirudi ndani na kuketi kwenye mkeka ukumbini mara baada ya kuchomeka mswaki ukutani.



Walipomaliza kunywa uji Binti Mngane akatoa vyombo nje avioshe. Sharifu akapumzika kidogo kisha akanyanyuka kwenye mkeka na kwenda kufagia banda la kuku. Akafagia huku akijiburudisha wimbo ambao aliwahi kufundishwa na baba yake kipindi cha nyuma kabla ya uhai wake.





“Mdooogo mwanangu mdogo...aowa owa,

Jisomeee mwanangu jisomee...aowa owa,

Uniokoooe mwanangu uniokoe...aowa owa,

Nakuombeeea baba yako nakuombea...aowa owa,

Kwa mwenyeeezi nakuombea kwa mwenyezi...aowa owa,” Sharifu aliimba nyimbo hiyo kama mara mbili na kucheza kwa kutingisha kichwa na kunyanyua miguu.



Binti Mngane alipomaliza kuosha vyombo akaenda kwenye banda la kuku kumwangalia mwanae kama anafagia au lah. Kufika akashangaa kuona mwanae akiimba nyimbo aliyoipenda kuiimba mumewe kipindi cha nyuma.



“Leo unafuraha, eenh?,” Binti Mngane aliuliza mara baada ya kufika bandani.



“Sina furaha, yoyote,” Sharifu akajibu.



“Mbona nakuona, unaimba na kucheza kwa furaha?.”



“Najiimbia tu mama yangu, nisichoshwe na kazi,” Sharifu alijibu huku akizoa kinyesi cha kuku na kukiweka kwenye ndoo ya taka.



“Umenikumbusha mbali.”



“Kivipi?.”



“Nyimbo hiyo unayoimba inanikumbusha miaka ya tisini na nne hivi, kipindi alichonioa baba yako alikuwa anapenda kweli kuimba nyimbo hiyo.”



“Kweli?.”



“Eehe!.”



“Nyimbo hii unajua, kanifundisha nani.”



“Sijajua.”



“Kanifundisha baba huyo huyo.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Nilijiuliza huyu mtoto nyimbo hii kaitoa wapi, kumbe umefundishwa na baba yako.”



“Eenh...natoka siku hiyo nimetokea kuipenda kweli hiyo nyimbo.”



“Ulikuwa kumbe na baba mzuri sana?.”



“Sana tena sana kwa jinsi alivyokuwa ananipenda baba hadi leo hii angekuwepo nisingetaabika,” Sharifu alijibu kisha akabeba ndoo na kwenda kumwaga kinyesi cha kuku.





ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog