Search This Blog

MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI - 5





    Simulizi : Mama Usinifundishe Uchawi

    Sehemu Ya Tano (5)







    Tarehe 25, mwezi 3, mwaka 2017. Kilimo cha nyanya kikaanza katika kijiji cha Maharaka. Shamrashara za kilimo zikaanza katika kipindi hicho kwa shangwe kubwa. Vijana wengi wakalima na kipindi cha mavuno wengi wakapata mazao mengi. Katika hatua hizo zote Sharifu akapitia na akavuna nyanya kwa wingi shambani kwake. Akauza nyanya zake kwa pesa ndefu kushinda miaka yote iliyopita. Safari hii akafanikiwa kweli kweli kipesa hadi akafanikiwa kujenga jumba la wadhifa. Akafungua maduka mawili ya nafaka pale kijijini hatimaye akaonekana mtu katika watu. Japo alipata utajiri kilingeni alikuwa anaudhuria na kama kawaida.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sharifu, sasa ushapata utajiri ila zingatia kitu kimoja” alieleza Mzee Damanda siku hiyo katika kilinge. Kabla ajaendelea Mzee Damanda kuongea Sharifu akauliza.



    “Kitu gani, hicho?.”



    “Nisikilize kwa makini...utajiri wako haupaswi kuwa na mke. Ukiwa na mke tu unasababisha kilinge chetu chote kuteketea hivyo basi tulinde nasi tukulinde.”



    “Kiongozi, sasa mali zote nilizopata nani atakuwa mrithi wangu!!!?,” Sharifu aliuliza kwa kustaajabu.



    “Mrithi hatokuwepo, wewe tumia ukifika mwisho wako na mali zako zote zitateketea nadhani tumeelewana.”



    “Haya,” Sharifu aliitika kinyonge kama sitaki nataka. Mzee Damanda baada ya mazungumzo na Sharifu akanyamaza kidogo kisha akaangalia juu kwa muda huku akinena maneno ya kichawi.



    “Sundu cha ukoo, kalula manyakara,” Mzee Damanda aliomba kichawi kwenye mizimu wamletee kitu anachohitaji.



    Sekunde haikupita kikatokea chungu ndani yake kukiwa na Paka watatu. Akamtoa paka mmoja mweusi akamnyofoa shingoni kwa meno kisha akaanza kumnyonya damu Paka yule. Alipomaliza kumnyonya damu akatulia kidogo kisha akawatazama wanachama wake na kusema kwa kuanza na salamu yao.



    “Chanoga.”



    “Chanoga twala, kibakile twahipazi,” Wachawi wote kwa pamoja waliitikia salamu hile.



    “Leo ni siku muhimu sana kwa kijana wetu Sharifu.......... Tutamfanyia tafrija fupi ya kumpongeza kwa kupata mafanikio makubwa kama wanachama wengine humu,” Mzee Damanda alisema mara akanyamaza kidogo kisha akaendelea kusema.



    “Hivyo basi kwa kuwa leo ni siku ya furaha kwetu, tunyweni kwa pamoja,” Mzee Damanda aliongea huku akiwatoa Paka wawili waliobaki na kuwapa wanachama wake wanywe kwa kupokezana kama glasi ya mvinyo iliyotolewa na Yesu Kristo kwa wanafunzi wake.



    Baada ya tafrija kuisha wachawi wote wakatawanyika kwa kunyanyuka na kurudi majumbani. Sharifu na mama yake siku hiyo walichoka sana kuliko siku zote. Hivyo walivyofika kwenye mjengo wao kila mmoja akaingia chumbani kwake kupunguza usingizi. Saa moja ya asubuhi Sharifu akawahi kuamka akamwamsha na mama yake wakajiandaa kila mmoja akaenda kufungua duka lake. Maduka yao yana umbali kidogo Sharifu duka lake lipo kijijini Maharaka na mama yake duka lake lipo kijiji cha pili kutoka Maharaka. Kila mmoja alipofika kwenye duka lake akachakarika kwa kuuza anavyojua yeye. Jioni katika duka la Binti Mngane wateja wakapungua kwa muda ndipo alikuja dada mmoja aliyevaa kinadhifu akiwa anahitaji soda. Baada ya kupewa soda na kumaliza kuinywa huyo alitaka aondoke asahau kulipa lakini Binti Mngane akakumbuka kama binti yule hakulipa pesa. Hivyo akamzuia binti yule kuondoka hadi alipe pesa.



    “Binti hujanilipa pesa,” Binti Mngane alisema huku akimkodolea macho binti yule.



    “Aaaah, samahani sana nilijisahau,” Binti yule alisema huku akitoa pesa kwenye mfuko wa suruali yake na kumpatia Binti Mngane.



    “Msheeenzi wewe unadhani mimi wa kujaribiwa.... Ndiyo nini unanipa kijiti badala ya pesa,” Binti Mngane alitusi mara baada ya kugundua kama kapewa kijiti na si pesa na binti yule.



    “Fyoooo,” Binti yule aliachia sonyo takatifu kwa Binti Mngane mara baada ya kujua kagundulika.



    Binti Mngane siku zote atakagi dharau haswa kwa mtoto mdogo kama yule hivyo akaona bora amwonyeshe kuwa kuna watu si wa mchezo mchezo. Akakusanya nguvu za giza mwilini mwake kisha akamtupia kombora la haja binti yule. Looooh! Binti yule kumbe ni jini akaliona kombora la Binti Mngane akaligandisha angani kimiujiza kisha akachezesha macho ghafla. Kombora likamrudia Binti Mngane. Likampata Binti Mngane akadondoka chini puuuuuuuu! akaanza kuonekana kutokwa na damu pamoja na mapovu mdomoni hatimaye akazima ghafla. Hilo jini lilipomaliza kufanya mauaji kwa Binti Mngane akapotea eneo lile akaondoka sehemu isiyotambulika.



    **********

    Sharifu akiwa dukani machale yakamcheza, mapigo ya moyo yakaenda kasi hata raha akuwa nayo akiwa kwenye hali hile mara ghafla alikuja mtoto wa kijiji cha jirani akiwa kwenye mbio ya hatari. Alipofika dukani kwa Sharifu akapiga breki isiyo ya mfano akahema kwa kasi huku akisema kwa haraka.



    “Kaka Sharifu, mama yako kadondoka dukani kwake.”



    “Kadondoka!!!,” Sharifu aliongea kwa mshangao na haraka akafunga duka akaongozana na mtoto yule hadi kwenye duka lake la pili.



    Kufika dukani akashangaa kuona umati wa watu umejaa, akajikongoja hadi ndani ya duka hakuweza kuamini nguvu zote zikamwisha mara baada ya kumwona mama yake chini akiwa anatoka damu na mapovu mdomoni. Sharifu akachutama chini akajaribu kumfumbua macho mama yake lakini macho yakakataa kufumbua. Akachunguza mwili wa mama yake na akiwa kwenye uchunguzi katika shingo ya mama yake akaona nembo ya Mbwa Mwitu iliyoachwa na jini. Sharifu akagundua kuwa mama yake ameuwawa na kiumbe hatari kilicho na nguvu kuliko wao. Akainamia mwili wa mama yake na kulia. Akalia sana bila ya kunyamazishwa na mtu, ndipo kwa kuwa katika umati ule alikuwepo Mzee Damanda na ndiye aliyemtuma mtoto yule amuite Sharifu. Basi akasogea alipo Sharifu na kumtia maneno ya kufariji na ujasiri, kweli. Sharifu akapata ujasiri akamtoa mama yake nje na kufunga duka kisha akaita TOYO ili ichukue mwili wa mama yake na kuupeleka nyumbani. Mzee Damanda akasaidiana na Sharifu kupakiza mwili wa Binti Mngane kwenye TOYO kisha nao wakapanda na kumwamuru mwenye TOYO awapeleke nyumbani. Mwenye TOYO akawafikisha nyumbani ili waweze kuendelea na ratiba za mazishi. Sharifu akaandaa ratiba ya mazishi akishirikiana na Mzee Damanda kama inavyotambulika zaidi mazishi kufanyika jioni hivyo naye akapanga siku hiyo jioni. Mazishi bila mabadiliko yoyote yakafanyika na kila mmoja wao akatawanyika kurudi majumbani mwao. Sharifu akiwa njiani na Mzee Damanda wakielekea nyumbani huku akiwa na majonzi ndani ya moyo nyuma yao walikuwepo wamama wawili wakizungumza kwa sauti ya chini chini huku wakijua hakuna mtu anayesikia. Wakaachia vicheko vya kumsengenya Sharifu.





    “Mwenzangu, yaani ilikuwa hatari mama mchawi, mtoto mchawi ndani kulikuwa ni vurugu mechi. Mama ana wanga na mtoto ana wanga wakirudi wamechoka mmmm!, yaani hatari tupu,” Mama mmoja wapo aliongea kwa kumweleza mwenzake asiyefahamu siri za kina Sharifu.



    “Mh! Mwenzangu mbona unaniogopesha nishindwe kukaa kwa amani katika kijiji hiki,” Mama mwingine alisema kwa hofu kuhofia mambo ya kichawi yasimkute.



    “Sio kama nakutisha, ni ukweli mtupu...usimuone vile kijana yule ni mchawi puuuu!,” Mama yule alizidi kutoa siri za Sharifu kwa mwenzake na mwisho akatema mate chini kumkebehi na kumdharau Sharifu.



    Sharifu mazungumzo yale akayasikia tokea muda akayapotezea. Hili la mwisho likamchoma akageuka akamkazia macho yule mama kisha akapeleka kidole kwenye mdomo kwa ishara kumwonya yule mama asiendelee kuongea. Yule mama kwa kuwa ni kiroporopo hakusikiliza onyo akaendelea kubwabwaja siri zote za Sharifu kwa yule mwenzie. Mdomo ukaponza kichwa, yule mama akaendelea kubwabwaja. Sharifu safari hii akanyanyua mkono wake wa kushoto kisha akapeleka shingoni na kufanya ishara ya kuchinja. Papo hapo yule mama hakuomba hata maji akaenda chini na kuaga dunia. Kisha Sharifu wakati akikamilisha tukio hilo akaonyesha kuendelea na safari yake kurejea nyumbani na Mzee Damanda huku nyuma wakimwacha yule mama mwengine akisumbuka kujaribu kumwamsha mwenzake aliyenyongwa kwa nguvu za giza. Walipofika njia panda Sharifu na Mzee Damanda wakaagana na kila mmoja akaelekea kwake. Mzee Damanda akayeyuka akatokea kwake na Sharifu akayeyuka akatokea kwake sebuleni.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **********

    Miezi ikayoyoma mwaka ukakatika Sharifu alikuwa mpweke siku zote, toka udogo wake alizoea kuwa na mama. Kwa sasa mama amemtoka amekuwa kama mtoto aliyetelekezwa mtaani. Hana mbele wala nyuma, hana wa kumfariji wala wa kumshauri. Chama nacho kinampa pingamizi tata kinachomletea utata katika maisha pindi afikiriapo maneno ya Mzee Damanda.



    “Nisikilize kwa makini...utajiri wako haupaswi kuwa na mke, ukiwa na mke tu unasababisha kilinge chetu chote kuteketea hivyo basi tulinde nasi tukulinde,” Sharifu akaona ni upuuzi inawezekana vipi aishi kwenye mjumba wa wadhifa pekee yake kama msukule bila ya kuwa na mke wala watoto wa kumchangamsha na kumfariji. Ndipo hapo akaamua kukaidi maneno ya Mzee Damanda na kusema;



    “Kama liwalo na liwe tu, mimi siwezi kaa jumba lote hili kama zindiko kisa chama kinataka.”



    Adhima yake kweli akaitekeleza. Akaenda kijiji cha mbali kuchumbia na kuoa huko huko ili wachawi wenzie wasigundue kama ameoa. Akarudi kijijini kwao akiwa na jiko akaishi na mkewe kisiri sana katika kijiji cha Maharaka, takribani miezi mitatu bila ya wachawi wenzake kujua na wala mkewe kujua kwamba yeye ni mchawi. Ndani ya mwezi wa tatu siku moja ndipo siri ikagundulika. Ikajulikana na kuanza kuchunguzwa wakati mama mmoja aliye miongoni mwa wachawi wa Marahaka, akipita karibu na nyumba ya Sharifu na kusikia sauti ya mwanamke na ya Sharifu zikiongea. Akasogea jirani zaidi na dirisha ili asikilize kinachoendelea ndani humo.



    “Sharifu, nimechoka kukaa humu ndani. Wewe fikiria mwenyewe nitakaa humu ndani hadi lini........ Kila siku unaniambia kesho kesho imekuwa nyimbo ya taifa,” Mama yule alimsikia mke wa Sharifu nadhani akinung'unika kwa nini hatoki nje.



    “Vumilia kidogo Sauda, kuna mambo nataka niweke sawa mke wangu...hivyo yakiisha nitashughulikia ombi lako,” Mama yule safari hii alisikia sauti ya Sharifu ikiongea kwa upole ikimbembeleza mkewe.



    Mama yule mshakunaku akatimua mbio kupeleka umbea kwa Mzee Damanda kuwa Sharifu kakaidi sharti alilompa. Akafika kwa Mzee Damanda na kumkuta Mzee Damanda ndani akijisomea kitabu cha KUBALI TUYAMALIZE kilichoandikwa na kutungwa na mwandishi AMRI BAWJI. Akamkurupua ndani kwa kumuita nje. Mzee Damanda akasikiliza wito wa mwanachama wake akafunika kitabu na kutoka nje kumsikiliza. Mama yule alipoona Mzee Damanda ametoka akavuta pumzi ndefu kisha akauliza swali.



    “Mzee Damanda, una habari kama mwanachama wetu kaoa?.”



    “Nani tena?.”



    “Si Sharifu...inamaana huna habari?.”



    “Sina habari...lakini kaoa lini mbona sijasikia tetesi hizo?.”



    “Naona kaoa muda kidogo, maana leo nimesikia kwa masikio yangu mwanamke wake akisema...nimechoka kukaa humu ndani. Wewe fikiria mwenyewe nitakaa ndani humu hadi lini...kila siku unaniambia kesho kesho imekuwa nyimbo ya taifa.”



    “Kwa hiyo hapo tuseme Sharifu ameoa kisiri siri amemficha mkewe tusijue...si ndiyo?.”



    “Haswaaa, bila shaka.”



    “Sasa mtoto huyu, anapoelekea sipo.”



    “Kabisaaa...anapoelekea huko ndiyo mwanzo wa kuleta matatizo.”



    “Basi asante kwa kuniletea taarifa...ngoja mimi nithibitishe. Nikigundua ni kweli nitakuwa sina chaguo.”



    “Sawa kiongozi, ngoja nami niende.”



    “Sawa...tutaonana baadae kilingeni.”



    Mama yule baada ya kutoa taarifa akaondoka huku nyuma akamwacha Mzee Damanda naye akiingia ndani kwaajili ya kuendelea kusoma kitabu. Akasoma kwa muda mrefu na hatimaye pale pale akapitiwa na usingizi sebuleni na kusababisha kitabu kidondoke na udenda kuanza kumtoka. Akiwa usingizini habari za Sharifu kuoa zikamjia ndotoni na pia utekelezaji wa mauaji ya wanachama wenzake watano walioeneza habari za kwamba Sharifu kaoa zikamtawala. Ghafla akiwa katika ndoto akashtushwa na Panya aliyemng'weng'wesa miguuni na kukimbia. Mzee Damanda akasonya kwa hasira huku akitukana.



    “Sheeenzi wewe!. Unatumwa mapema unakubali tu, nitakuangamiza ukaungane na wafu,” Mzee Damanda alijisemea kisha akanyanyuka akaingia chumbani kwenda kumalizia usingizi kitandani.



    Akapiga usingizi hadi mishale ya saa mbili kamili akaamka na kuketi kitandani kwa muda kisha akayayuka na kutokea ndani mwa Sharifu kwenye mlango wa kuingilia ndani. Akanyoosha mkono mbele kikatokea kikopo cha mafuta yenye rangi ya kijani akajipaka ili asipate kuonekana na mtu yeyote. Alipojipaka akayayuka akatokea sebuleni akamkuta Sharifu anapiga mahesabu ya mauzo ya dukani. Akaachana naye na kuendelea kufanya uchunguzi kama ni kweli maneno aliyoambiwa na mwanachama wake kama yanaukweli. Akayayuka na kutokea chumbani kwa Sharifu huko ndipo akajithibitishia kama maneno aliyoambiwa ni ya kweli. Akamkuta binti mweupe na mrefu wa wastani amelala kwenye kitanda cha Sharifu. Hakuwa na haja ya kuuliza akajua bila shaka yule ndiye mke wa Sharifu. Mzee Damanda hakuchukua uamuzi wowote kwa binti yule akayayuka chumbani akarudi tena sebuleni alipo Sharifu akanena maneno ya kichawi.



    “Guto charumba, zenga chelo mangamba” ghafla ukatokea unga mweupe mkononi mwa Mzee Damanda mara baada ya kumaliza kuzungumza maneno yale.



    Akapuliza unga ule kwa Sharifu ili alale muda mrefu ashindwe kwenda kilingeni. Sharifu muda huo huo akashikwa na usingizi wa ajabu na kushindwa kuendelea na mahesabu. Akalala pale pale sebuleni. Mzee Damanda baada ya kufanya jambo kwa Sharifu akatoweka na kuelekea kilingeni. Alipofika akawakuta wachawi wenzake wote washafika wanamngoja yeye. Akatoa salamu kisha akanzisha mdahalo na wanachama wake.



    “Mtoto huyu, mbona simwelewi?,” Mzee Damanda alisema huku akiwaangalia wanachama wake.



    “Mtoto gani huyo?,” Mama Kitenya kama atambulikavyo aliuliza swali mara baada ya kutomjua mtoto azungumziwaye na kiongozi wao.



    “Sharifu,” Mzee Damanda akajibu.



    “Kafanyaje tena?,” Mama Dungo naye kama atambulikavyo aliuliza mara baada ya kutofahamu kitu alichofanya Sharifu.



    “Si kaoa!,” Mzee Damanda akajibu.



    “Mtumeee!!!, si tulimwambia asioe sasa kaoa anataka atuangamize,” Fatuma alisema kwa mshangao mara baada ya kusikia hayo.



    “Sasa huyu mtoto tukimchekea tu anatuangamiza wote,” Mama Shura kama atambulikavyo aliongea kwa sauti ya juu kidogo na kuonekana kuchukizwa mno kwa kitendo alichokifanya Sharifu.



    “Kweli kabisa unavyosema Mama Shura...mtoto huyu tumdhibiti kabla mizimu haijachukia” aliongezea kusema Mzee Damanda.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwa lini sasa anatakiwa kudhibitiwa?,” Fatuma aliuliza huku akiwaangalia wenzie kwa kutaka jibu.



    “Kwa leo haitowezekana kesho kabla atujaingia kilingeni yatupasa tukalidhibiti hili kwa kumuua mkewe maana yeye ndiye tatizo kwetu” alisema Mzee Damanda kwa kumaanisha kisha akamaliza kwa kusema.



    “Manjo, kuye,” Mzee Damanda aliwatakia usiku mwema wanachama wake kwa maneno ya kichawi kisha akapotea pale kwa kuyayuka huku nyuma wanachama wake nao wakayayuka mara baada ya kuthibitisha kuwa mdahalo umeisha.



    **********

    Sauda akaamka mapema lakini akashangaa kujikuta peke yake kitandani. Akanyanyuka akatoka chumbani akaelekea sebuleni. Alipofika sebuleni akafurahi sana, alipomuona mumewe kwenye sofa amelala huku akijikuna kutokana na mbu wa jana usiku waliomng'ata. Akamsogelea mumewe karibu kisha akamwamsha kwa sauti ya unyenyekevu yenye kubeba jumbe la upendo. Sharifu akashtuka nusura anguke mara baada ya mkewe kumwamsha akakaa wima sofani kisha akamtazama kwa kuduwaa. Mahabuba wake na laazizi wake wa ubani kwa muda akiwa ameduwaa sauti ya mkewe ikamzindua kwa kuuliza pindi ilipopenya kwenye ngoma ya masikio.



    “Sharifu, inamaana leo umelala hapa?.”



    “Eeenh...yaani jana nilikuwa kama mfu hata nilivyolala nilikuwa sijitambui.”



    “Wachawi, walikunyemelea nini?,” Sauda aliuliza kiutani.



    “Acha zako wewe, umeona mwili huu wakutembelewa na wachawi hovyo,” Sharifu alijibu naye kimasihala.





    “Haya bwana...jiandae basi unywe chai uende kazini siunajua ufunguo wa duka lile lengine unao wewe. Mtoto wa watu atakusubiri hadi atachoka sasa bora yaani uwahi ukampe ufunguo afungue duka anze kuuza.”



    “Kweli kabisa, ngoja nijiandae maana wateja ni asubuhi tukiwakosa wa asubuhi ujue ishakula kwetu hiyo,” Sharifu alisema kisha akainuliwa na mkewe akapelekwa chumbani kujiandaa mara baada ya kusafisha mwili na meno.



    Baada ya kujiandaa, akatoka chumbani akaelekea kufungua kinywa kwa chai ya maziwa na mkate. Alipomaliza kunywa na kula akamuaga mkewe kisha akaelekea kwenye duka alilokuwa akiuza mama yake ambalo kwasasa kamwajiri mtoto mmoja mchangamfu anayeishi kijiji hicho hicho cha Maharaka. Alipofika hapo dukani akamkabidhi mtoto yule funguo wa duka kisha yeye akaondoka kuelekea kwake kufungua duka. Nyakati za asubuhi hadi usiku akauza barabara, muda wa kufunga duka uliporuhusu akafunga duka na kujikongoja mdogo mdogo kurudi nyumbani. Kabla hajafika nyumbani njiani kwenye eneo la makaburini akasikia vifaranga vikilia kwa sauti ya juu. Alijipa ujasiri akaendelea na safari yake. Akapiga hatua tatu hakusikia tena vifaranga vikilia, hatua ya nne akataka kumkanyaga Chatu mbele yake akasita haraka akarudi nyuma kisha akaanza kutoa pumzi isiyo ya idadi.



    “Aaaaah!,” Sharifu hajatulia sawia akashtuka kumuona Chatu yule akiangua kicheko.



    “Wewe ni nani?,” Sharifu aliuliza kwa ujasiri. Swali halikujibiwa bali Chatu yule akajibadili akawa si Chatu tena bali akajibadili kuwa Mzee Damanda.



    “Leo nakuhitaji ufike kilingeni mapema,” Mzee Damanda alisema bila kung'ata maneno mara baada ya kutoka kwenye umbile la uchatu.



    Mzee Damanda alipomuhabarisha Sharifu akayeyuka. Akaenda kupita kila nyumba ya wanachama wake ili wasuke mpango wao. Wakausuka ukasukika kisha Mzee Damanda akarudi nyumbani kwaajili ya kusubiri muda wa kilingeni utimie. Muda ukatimia yapata saa nane kasoro tano ya usiku Mzee Damanda akajiandaa na kwenda kilingeni. Akamkuta Sharifu ameshafika muda kidogo kama alivyomwambia akiambatana na wanachama wenzake. Mzee Damanda akamtazama Sharifu kisha akaonyesha ishara ya kutikisa kichwa kumpongeza Sharifu katika kutii agizo. Hatimaye akawaangalia wanachama wengine kisha akatoa ishara ya kuinua kichwa juu. Ghafla wanachama wale wakapotea na kuwaacha kilingeni Sharifu na Mzee Damanda tu.



    “Kiongozi mbona wanachama wote wameondoka?” aliuliza Sharifu mara baada ya kuona wameachwa wenyewe.



    “Watarudi nimewatuma sehemu” alijibu Mzee Damanda kwa kumuondoa hofu Sharifu.



    **********

    Wachawi ambao ni Fatuma, Mama Shura, Mama Dungo na Mama Kitenya wakawasili nyumbani kwa Sharifu. Watatu wakabaki nje wakamtuma ndani Mama Kitenya akafanye mauaji kwa mke wa Sharifu. Mama Kitenya akayeyuka akatokea ndani akapita kila kona na kila chumba akimtafuta Sauda. Haweze kukamilisha mpango wake. Alikuja kumuona Sauda jikoni akiosha vyombo huku mkononi kashika kisu. Mama Kitenya akiwa nyuma ya Sauda akazungusha macho yake na Sauda akapinduka kumwangalia. Mama Kitenya akafumba macho yake kwa mara moja na kufumbua pale pale. Sauda akajichoma na kisu alichokishika papo hapo akaaga dunia. Baada ya mauaji Mama Kitenya na wenzake wakarudi kilingeni yapata saa kumi kamili wakamkuta Mzee Damanda na Sharifu wakiwasubiri. Sharifu alipoona wenzake wamerudi akawakaribisha na swali lenye kubeba jumbe tata kichwani kwa Mzee Damanda na wanachama.



    “Mmetoka wapi?,” Wachawi wote hawakulijibu lile swali la Sharifu wakabaki wakitazamana na kuonyesha sura ya kumficha Sharifu.



    “Mmetoka wapi?...maana ninavyojua kila pahala huwa tunatakiwa kwenda wote ila leo mmeenda wenyewe, kuna kitu mnanificha,” Sharifu aliuliza tena kisha akasema kwa manung'uniko mara baada ya kuona wenzake wote hawajamjibu mwanzoni.



    “Hakuna tunachokuficha, hawa niliwatuma kijiji cha jirani kuchunguza wachawi wa kule wanautaratibu upi,” Mzee Damanda alijaribu kudanganya ili Sharifu asijue kilichofanyika.



    “Huko ulikowatuma naona kulikuwa na vita sana...eeenh?,” Sharifu aliuliza mara baada ya kumuona Mama Kitenya akiwa na damu shingoni.



    “Kwanini umeuliza hivyo?,” Mzee Damanda akauliza.



    “Namuona Mama Kitenya ana damu shingoni,” Sharifu akajibu.



    “Oooh, hii damu ni ya Bundi.......... Tulivyokuwa njiani tulikutana na Bundi na ukiangalia nilikuwa nina kiu ya damu hivyo sikuwa na budi kumkamata na kunyonya damu yake,” Mama Kitenya alidakia mazungumzo na kujitetea kwa kudanganya.



    “Mmmh,” Sharifu alikubaliana na maelezo yaliyotolewa na Mama Kitenya japo kwa kuguna.



    Mzee Damanda baada ya mazungumzo akaanzisha mkutano, ndani ya saa moja alikuwa kashamaliza. Wakatawanyika wachawi wote kurudi majumbani. Sharifu akarudi nyumbani lakini hali aliyokutana nayo ikamshtusha na kumshangaza. Akakuta hali ya nyumbani imepoa kuanzia nje mpaka ndani. Yaani ilikuwa sio kama siku zote akashangaa zaidi kukuta jikoni kulivyokuwa rafu. Kutupa macho kwenye kona ya jikoni akamuona mkewe akiwa kalala chini na kisu kikiwa juu ya tumbo amechomwa. Akamsogelea karibu na kujaribu kumwamsha kwa kumuita jina lakini wapi mtu tayari alikuwa wajuzi. Nguvu zikamuisha na kuanza kunyong'onyea kama mtoto wa utapiamlo. Machozi yakamtiririka kwa wingi kama mama mjane aliyefiwa. Akakaa chini tuli huku akitafakari nini chanzo cha kifo cha mkewe na nani kafanya mauaji haya. Akafikiria kwa muda mrefu bila kupata majibu ya papo kwa papo. Ndipo baadaye akatuliza akili sawasawa akapata kukumbuka maneno yaliyoongelewa kilingeni.



    “Mmetoka wapi?,” Wachawi wote hawakulijibu lile swali alilouliza Sharifu wakabaki wakitazamana na kuonyesha sura ya kumficha.



    “Mmetoka wapi?...maana ninavyojua kila pahala ni kawaida kwenda wote ila leo mmeenda wenyewe. Kuna kitu mnanificha?,” Sharifu aliuliza tena kisha akasema kwa manung'uniko mara baada ya kuona wenzake wote hawajamjibu mwanzoni.



    “Hakuna tunachokuficha, hawa niliwatuma kijiji cha jirani kuchunguza wachawi wa kule wana utaratibu upi,” Mzee Damanda alijaribu kudanganya ili Sharifu asijue kilichofanyika.



    “Huko ulipowatuma naona kulikuwa na vita sana...eeenh?,” Sharifu aliuliza mara baada ya kumuona Mama Kitenya akiwa na damu shingoni.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwanini umeuliza hivyo?,” Mzee Damanda akauliza.



    “Namuona Mama Kitenya ana damu shingoni,” Sharifu akajibu.



    “Oooh, hii damu ni ya Bundi...tulivyokuwa njiani tulikutana na Bundi na ukiangalia nilikuwa nina kiu ya damu. Hivyo sikuwa na budi kumkamata na kunyonya damu yake,” Mama Kitenya alidakia mazungumzo na kujitetea kwa kudanganya.



    “Mmmh, Sharifu alikubaliana na maelezo yaliyotolewa na Mama Kitenya japo kwa kuguna.



    “Inamaana hawa ndiyo waliyomuua mke wangu!. Ndiyo maana walijaribu kunificha nisijue” alisema Sharifu mara baada ya kukumbuka na kugundua kuwa waliomuua mkewe ni wanachama wenzake.



    Sharifu akapatwa na hasira pamoja na ghadhabu usiku ule ule. Akatoka akaenda kulipiza kisasi. Akayeyuka na kutokea chumbani kwa Fatuma. Akamkuta Fatuma yupo kitandani kalala. Akapuliza kitu mdomoni kikatoka mfano wa mawingu kikaenda kuvaa pua ya Fatuma. Baada ya kumaliza kufanya tukio akayeyuka na kurudi nyumbani. Kesho yake Sharifu akaendelea na utaratibu wa mazishi, mazishi ya mkewe akayafanya jioni na majirani kila mmoja kurejea nyumbani kwake.



    **********

    Mama Kitenya asubuhi na mapema akaamka ili aelekee shambani kama kawaida yake. Mara nyingi akiwa anakwenda shambani au mtoni lazima ampitie shosti yake Fatuma. Hivyo siku hiyo akampitia shoga yake waende wote shambani kama siku zote. Lakini alichokutana nacho akastaajabu ya Musa. Akamkuta chumbani shoga yake mara baada ya kuita kwa muda mrefu bila majibu akiwa amelala kitandani huku akitokwa damu puani. Akajaribu kupeleka mkono puani asikie kama anahema hamna chochote. Alikuwa ahemi wala mapigo ya moyo yalikuwa hayatembei. Hapo ndipo machale yakamcheza kwa kugundua kuwa alikuwa ameshaaga dunia kitambo shoga yake. Ukunga wa hali ya juu ukapigwa na Mama Kitenya kuwaita majirani wengine waje kwa wingi kwa ajili ya kufanya utaratibu wa mazishi, ni kweli majirani wakaja akiwemo na Mzee Damanda. Mzee Damanda alipofika akabeba majukumu yote ya mazishi akapanga mazishi yafanyike kesho yake. Watu wakatimka wakarudi majumbani wakisubiri hiyo kesho iwasili wakamzike Fatuma. Siku iliyofuata wote wakaenda kumzika Fatuma kasoro Sharifu tu ndo akagoma kuhudhuria mazishi ya mwana kilinge mwenzake kutokana na kinyongo alichokuwa nacho baada kuhisi hao wenzake kumuulia mke wake. Mara baada ya mazishi watu wote wakatawanyika na hatimaye kurudi majumbani mwao.





    Siku tano zikafika kwa Sharifu hakumsahau mkewe na pia wale waliosababisha kifo cha mkewe. Akajitahidi kwa udi na uvumba aweze kutimiza dhamira yake. Akaanza kumwandama mwanachama mmoja baada ya mwengine. Siku hiyo akampania sana Mama Dungo. Sharifu kwa kutimiza dhamira yake siku hiyo alikwenda nyumbani kwa Mama Dungo yapata saa nane ya mchana. Akamkuta Mama Dungo yupo nje ya nyumba yake akifua nguo. Wakasalimiana na mara baada ya salamu Sharifu akapiga jicho huku na kule ili kuangalia kama kuna mtu anapita hakuona mtu yeyote. Akafurahi mno na kujua muda wowote atatimiza dhamira kuu kama aonavyo. Kama wasemavyo siku ya kufa nyani miti yote huteleza na mchagua pema pabaya panamuita. Hapo ndipo pabaya palimuita Mama Dungo. Akiwa yupo bize na kufua asijue dhumuni na dhamira ya Sharifu ghafla akamshtukia. Sharifu akawahi na kumkaba koo Mama Dungo. Akakukuruka na kutaka kupiga kelele lakini akashindwa kutokana na Sharifu kumdhibiti madhubuti kooni. Akiwa amelishikilia koromeo la Mama Dungo kwa mkono wa kuume huku mkono wake wa kushoto akakunja ngumi kisha akafanya kupeleka mbele na kurudisha nyuma kama dereva wa trekta anapochezesha gia. Pale pale Mama Dungo koromeo lake likatoka nje na kuning'inia kama bembea. Hapo ndipo ulikuwa mwisho wake wa kuishi duniani Mama Dungo. Mama Dungo baada ya kufariki Sharifu akapotea eneo lile kwa kuyeyuka na kutokea chumbani kwa Mama Shura. Akamkosa chumbani akayeyuka tena na kutokea sebuleni. Hapo ndipo alipomkuta Mama Shura akiwa amejilaza kitini kwaajili ya kupunguza usingizi. Akapitisha macho kila kona ya nyumba ya Mama Shura kama ataona kitu chochote kinachoweza kumwangamiza. Katika kuangalia angalia akaona nyundo pembezoni mwa mlango wa Mama Shura. Akanyanyua kichawi ile nyundo na kuleta mikononi mwake kisha akashika vizuri kwa mkono wa kuume na kumpiga nayo Mama Shura kwa nguvu kichwani kama mara tatu hivi. Ghafla Mama Shura akaonekana kuvuja damu kichwani na hapo hapo hakulemba tena kuendelea kukaa pale. Upesi upesi akaweka nyundo pembezoni ya kiti kichawi kisha yeye akayeyuka na kurudi nyumbani kwake. Baada ya masaa kadhaa kupita mara baada ya mauaji kutendeka mjumbe wa nyumba kumi Mzee Bemele alikuwa anapita kila nyumba kutoa vipeperushi vya kuwahamasisha wanakijiji wake wapende kuhudhuria vikao vinavyopangwa na uongozi wa kijiji. Katika pita pita zake akiendelea kufikisha vipeperushi kwa wanakijiji wake mara ghafla akamuona kijana mmoja akimfuata mbio ikabidi asimame amsubiri kijana yule ajue ana shida gani. Kufika karibu na Mzee Bemele akaongea kwa haraka huku akihema kwa kasi ya ajabu.



    “Mjumbe, kuna mauaji yametendeka.”



    “Mauaji!!!?” aliuliza Mzee Bemele kwa mshangao.



    “Eeenh.”



    “Mauaji hayo ya nani?.”



    “Mama Shura na Mama Dungo.”



    “Wewe ulijuaje kama ni mauaji?.”



    “Vifo vyao ni vya utata na vya kutisha.”



    “Ebu...twende tukaone” alisema Mzee Bemele na haraka wakaongozana na yule kijana hadi sehemu ya matukio.



    Mzee Bemele akashangaa na kusikitika mara baada ya kupitia nyumba zote zilizofanyiwa mauaji. Haraka akaingiza mkono kwenye mfuko wake wa suruali akatoa simu akatafuta namba kisha akapiga.



    “Haloooh! Halooooh! mimi ni mjumbe kutoka kijiji cha Maharaka...natumaini hapo ni kituo kidogo cha polisi cha Doma. Ninayeongea naye ni mkuu wa kituo?,” Mzee Bemele alijitambulisha na kuuliza mara baada ya simu kupokelewa.



    “Hujakosea ndiyo mwenyewe,” Mkuu wa kituo alikubali kama ndiye.



    “Asante...sasa kijiji chetu kuna mauaji yanatendeka na hivi tunavyoongea kuna watu kama wawili wameuawa kwa mauaji ya kutisha.”



    “What!!!?.”



    “Ndiyo...naomba mje mfanye uchunguzi maana suala hili litawaogopesha sana wanakijiji.”



    “Sawa sawa, nitatuma vijana wangu waje kufanya hiyo kazi...ila naomba chonde chonde mtu yeyote asiguse hizo maiti mpaka tuje kufanya uchunguzi” alieleza mkuu wa kituo kisha Mzee Bemele akakata simu mara baada ya kupokea tahadhari kutoka kwa mkuu wa kituo.



    **********

    Ndani ya kituo kidogo cha polisi cha Doma mkuu wa kituo akaitisha kikao cha polisi wenye vyeo vidogo. Akawachagua na kuwatuma vijana wake wawili waaminifu na wenye uweledi na kazi yao. Afande Chacha na Afande Regan ndiyo wanaoaminika na ndiyo waliochaguliwa kwenda kwenye kijiji cha Maharaka kufanya upelelezi wa mauaji hayo ili kuweza kumtia mikononi mhalifu. Polisi hao wakaingia Maharaka jioni wakafika maeneo ya matukio na kuzichunguza maiti na kisha kuruhusu kesho wanakijiji waweze fanya maandalizi ya mazishi. Wakagundua kama si mauaji ya kawaida bali kikatili. Siku hiyo ikabidi wakodishe chumba cha bei nafuu ili waendelee na uchunguzi wao. Wakaingia kona baada ya kona ili kuona kama wanaweza pata fununu zozote lakini wapi. Siku ile walitoka kapa wakajirudia chumbani kwao wakiwa wamechoka hoi.



    “Afande Chacha, wewe unaonaje hizi kesi za jinai?” aliuliza Afande Regan mara baada ya ukimya wa muda mrefu.



    “Naona hizi kesi ni ngumu mno japo hatujaanza kuzifanyia utafiti wa kina,” Afande Chacha alijibu huku akipiga miyayo ya kuchoka.



    “Kweli...ila nakusihi tusikate tamaa maana nakujua wewe ukiona kesi uielewi unapotezea.”

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kesi nyingi napotezea, lakini kwa hizi siwezi nitapambana mpaka mwisho niweze kufanikisha kilichotuleta.”



    “Sawa kabisa...basi tulale kesho tutajua tuanzie wapi upepelezi wetu.”



    Kwa kuwa usiku ulishaingia Afande Chacha na Afande Regan wakalala. Asubuhi na mapema wakaamka wakajiandaa kisha wakavaa kiraia wakatoka kwenda kufungua kinywa mgahawani. Wakafika mgahawani wakaagiza chai na chapati wakanywa. Wakiwa wanakunywa chai wakamsikia mama yule muuza mgahawa na mteja mmoja wakizungumza habari ya Sharifu.



    “Bi Zuena, ujue yule mtoto mchawi sana,” Mteja yule alimwambia mama yule wa mgahawani.



    “Nani...Sharifu?,” Mama yule wa mgahawani aliuliza huku akipepesa macho kila njia asije kusikiwa na Sharifu mwenyewe.



    “Eeenh, huyo huyo.”



    “Wewe ndiyo unajua leo, wakati si tumejua kitambo...hata na mama yake alikuwa mchawi.”



    “Kumbee!!!.”



    “Eeenh...tena licha ya uchawi yaani wanaua watu balaa kitu kidogo tu wanakuua” alisema Mama yule wa mgahawani kisha akajifanya kukohoa huku akitupia macho kila kona kumwangalia Sharifu anakuja mwisho umbea ukajamponza. Alipoona dalili ya Sharifu kuja haipo akaendelea kuongea.



    “Lakini iwe siri yako usije ukaropoka huko mtaani ukaniponza mimi.” Kabla ajaongea Mteja yule Afande Chacha akadakia yale mazungumzo kwa kuuliza.



    “Hivi huyo Sharifu mnayemzungumzia anaishi kijiji hiki?.”



    “Eeenh na nyumba yake si mbali na hapa umeona ile inayotuangalia,” Mama yule alisema huku akimuonyesha Afande Chacha kwa kidole nyumba ya Sharifu.



    “Oooh! nyumba yake nzuri inaonekana ana utajiri mkubwa?,” Afande Chacha akazidi kupeleleza.



    “Ni nzuri, ila nasikia amepata kwa njia ya ushirikina” aliropoka Mama yule wa mgahawa asijue anayeongea naye ni polisi.



    “Mmmh, kumbeee!!!,” Afande Chacha aliongea huku akitingisha kichwa kwa kukipeleka juu na chini. Kisha akaendelea kuongea kwa kuuliza.



    “Nimesikia hapa mkisema anaua watu balaa ni kweli?.”



    Mama yule wa mgahawa alipoulizwa swali lile akachungulia kila pahala na akaangalia nyumba ya Sharifu iliyo mbele yake hakumuona Sharifu ndipo akalijibu lile swali.



    “Eeenh, anauwa balaa...nahisi hata mama waliokufa jana amehusika yeye.”



    “Kwa sasa huyo Sharifu yupo?,” Afande Chacha akauliza.



    “Kwa sasa nahisi yupo dukani kwake.”



    “Kumbe ana duka!!!?.”



    “Tena sio moja anayo maduka mawili.”



    “Oooh maduka yake yapo wapi?.”



    “Moja lipo hapa kijijini Maharaka na lingine lipo kijiji cha pili kinachoitwa Kipunguri.”



    “Oooh! Sasa yeye anauza duka lipi hapo?.”



    “Anauza duka lililopo hapa Maharaka.”



    “Oooh, huyu bwana tajiri sana,” Afande Chacha aliongea kwa kumsifia Sharifu na huku akificha makucha yake asitambulike kama ni polisi na mama yule wa mgahawani pamoja na yule mteja.



    Baada ya muda kadhaa Afande Chacha na Afande Regan wakamaliza kula wakalipa pesa kisha wakaondoka. Wakiwa wamepata mwongozo wa kuanza utafiti wao wakaanza kumpeleleza Sharifu hatua moja hadi nyengine. Siku iliyofuata kama kawaida wakavaa kiraia wakaingia mtaani kuulizia duka la Sharifu. Wakiwa katika harakati za kufuatilia njiani wakakutana na kijana mmoja mtanashati aitwaye Kondo wakamsimamisha na kumuuliza.



    “Hallo kijana habari yako,” Afande Regan alimchangamkia yule kijana.



    “Salama,” Kondo aliitikia ile salamu huku akijaribu naye kuwatathimini kwa kuwakazia macho kila idara.



    “Wewe ni mwenyeji wa hapa?,” Afande Regan alizidi kumchangamkia Kondo.



    “Ndiyo...niwasaidie nini?” alijibu na kuuliza Kondo.



    “Eti unajua duka la Sharifu lilipo?.”



    “Hapana sijui........ Kwani nani kawaambia kuna mtu kijijini kwetu anaitwa Sharifu?,” Kondo akauliza.



    “Kuna mama mmoja wa makamo ndiye aliyetuambia...na labda nikutoe hofu sisi tunamtafuta kwa nia njema kabisa.”



    “Sharifu ni nani yenu?.”



    “Ni wajomba zake,” Afande Regan akadanganya.



    “Kwake mnapajua?.”



    “Kwake tunapajua ila tumemkosa.”



    “Aaah nami napajua kwake tu huko dukani sipajui” alizidi kudanganya Kondo.



    “Basi sawa...Samahani kwa usumbufu,” Afande Chacha alimalizia hivyo kisha wakaagana na Afande Regan wakaondoka.



    Kondo mara baada ya kumaliza mazungumzo na wale polisi akatimua mbio moja kwa moja dukani kwa Sharifu kupeleka umbea. Akampasha umbea Sharifu kisha akaendelea na safari yake. Sharifu sasa akakaa kwa makini kila pahala aendapo akijua kuna watu wanaomtafuta na si kwa lengo zuri ni kwa lengo baya.



    **********

    Siku zikayoyoma kwa Sharifu na kisasi chake kipo pale pale. Hakuogopa hao wamekusanyika tafuta hata kama watu walimpasha habari juu ya ujio wa hao polisi. Siku moja usiku mnene akiwa nyumbani akapanga aende kuendeleza kisasi kwa Mama Kitenya. Akajiandaa na kuyayuka akatokea nyumbani kwa Mama Kitenya chumbani. Akamkuta Mama Kitenya kalala usingizi wa Kobe. Usingizi ambao ulikuwa ni ule wa kuibia ibia, ile anaingia chumbani tu Mama Kitenya akakurupuka usingizini na kuvaana na Sharifu. Wakaburutana wakiwa kwenye umbile la kibinadamu. Walipochoka wakaachiana kwa muda wakawa wanatazamana kwa usongo na kila mmoja kumpania mwenzie. Baada ya mapumziko ya muda Mama Kitenya akaona akiwa katika umbo la kibinadamu hamwezi Sharifu. Hivyo akabadilika kuwa Mbwa mwitu kisha akamrukia Sharifu shingoni akamrarua kwa makucha Sharifu katika purukushani zile akaona anaelemewa. Akayeyuka na kumwacha pale chumbani Mama Kitenya mwenyewe. Sekunde kadhaa zikapita akarudi tena akiwa kwenye umbile la Jaguar na kumuweza Mama Kitenya. Mama Kitenya alipokea mikong'oto babu kubwa akaomba msamaha lakini kwa kosa walilolifanya kwa Sharifu hakutaka maridhiano wala msamaha wa aina yoyote kutoka kwa Mama Kitenya. Akaendelea kumpa mkong'oto hadi umauti ulipomchukua. Baada ya mauaji kufanyika Sharifu akarudi katika umbile lake kisha akapotea na kwenda nyumbani kujipumzisha.



    **********

    Yapata saa kumi na moja alfajiri simu ya Afande Chacha inaita kwa sauti ya juu. Afande Chacha akasikia simu yake inaita akaamka na kuipokea.



    “Afande, kuna mauaji mengine yamefanyika huku” ilisikika sauti ya mjumbe upande wa pili ikiongea mara baada ya kupokelewa simu.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sehemu gani yamefanyika?,” Afande Chacha akahoji.



    “Ni jirani na nyumbani kwangu,” Mjumbe akajibu.



    “Okay nakuja sasa hivi” alitoa ahadi Afande Chacha kwa mjumbe. Kisha akakata simu na kumwamsha mwenzie waondoke.



    Wakafika sehemu ya tukio wakiwa wamevaa kiraia wakachunguza ile maiti na kugundua kuwa maiti zote zile za mwanzo na sasa muuaji ni mmoja. Hawakuwa na uthibitisho dhahiri kuwa anayeuwa ni Sharifu au laah. Baada ya uchunguzi wakatoa ruhusa ya mazishi iendelee na wao waendelee na uchunguzi stahiki. Kutokana na ugumu wa kesi hii wakalazimika usiku wasilale. Walikuwa mitaani tu wakiendelea na uchunguzi wao kisiri japo Sharifu alijua ujio wao. Siku inayofuata wakiwa wapo katika uchunguzi tena nyumbani kwa Sharifu wakasikia upepo mkali uliokuwa unapenya hadi kwenye viungo vya mwili. Wakaamua kujibanza kwenye kichaka kimoja kilichopo maeneo yale yale ya nyumbani kwa Sharifu wakijikinga na ule upepo. Wakiwa kwenye kile kichaka wakajishuhudia kwa macho yao kumuona Sharifu akijibadilisha katika umbile lake la kibinadamu na kugeuka umbile la Tembo. Wakataharuki na kuacha vinywa wazi kwa kuduwaa wasiamini wakionacho mbele yao. Tembo lile likakamata barabara ya vumbi na kuelekea hadi kwa Mzee Damanda. Afande Chacha na Afande Regan kwa kuwa walikuwa kazini hawakupaswa kujenga uwoga miyoni mwao. Wakajijengea ukakamavu na ujasiri ndani ya roho kisha wakamfuatilia Tembo yule hadi mwisho alipoishia. Wakaamua kujificha ili waweze shuhudia Sharifu atafanya nini akiwa kwenye umbile lile.Tembo yule akaishia nyumbani kwa Mzee Damanda akazunguka nyumba ile kama mara kumi kisha akaanza kubomoa nyumba ya Mzee Damanda kwa kutumia meno yake mawili yaliyochongoka kama sururu. Mzee Damanda akiwa yupo ndani amelala akasikia vishindo vya miguu ya Tembo na kishindo cha nyumba kuanguka haraka. Akakurupuka ndani kabla mjengo haujaanguka kumletea maafa. Akatoka nje na kumuona Tembo akiendelea kufanya uharibifu katika nyumba yake. Nyumba Ikabomolewa yote kisha huyo Tembo akamrudia mwenyewe Mzee Damanda ili kutaka kutimiza dhamira yake. Kabla hajafikiwa Mzee Damanda akanyoosha mkono wake wa kuume kwa yule Tembo kukatokea mwanga mkali kwenye uso wake. Katikati ya mwanga ule ikaonekana sura ya Sharifu. Mzee Damanda akaangua kicheko kwa dharau kisha naye haraka akajigeuza Nyati kabla Sharifu hajamdhuru. Mzee Damanda alipojibadili tu Afande Chacha na mwenzie wakaonesha kuwa na uwoga tena. Wakaogopa mno nusura wapige yowe lakini wakajipa tena roho ya ujasiri na kuzidi kushuhudia mchezo wote unaoendelea bila ya chenga huku wakiongea kwa kunong'ona wasisikiwe na wachawi wale.



    “Kijiji hiki kina wachawi sijapata ona,” Afande Chacha akanong'ona.



    “Aisee, yaani katika kazi niliyopeleleza na kunipa hofu hii namba moja,” Afande Regan alitoa ushirikiano wa kuongezea kuongea kwa kunong'ona.



    Wakazidi kunong'ona huku wakiendelea kuangalia mpambano kisiri sana. Dakika zilikwenda na masaa yakaenda lakini ngoma ikawa droo droo hakupatikana mshindi. Ngoma ikaungurumishwa hadi mishale ya saa tisa na nusu usiku Tembo na Nyati wakawa hoi bin taaban. Mishale ya saa kumi kasoro usiku Nyati akachoka mno ndipo Mzee Damanda akarudi kwenye umbile la kibinadamu akiwa yupo chini na kachafuka siyo mfano. Sharifu naye akaona asimchezee rafu kiongozi wake akapata fair play ya bure ikabidi naye arudi kwenye hali yake ya ubinadamu. Katika hali hiyo ya ubinadamu akamsogelea kiongozi wake ili ammalize. Akafika karibu na Mzee Damanda akamnyanyua kiongozi wake kisha akamtupilia huko kichakani jirani na mapolisi. Afande Regan uwoga ukazidi alipoona Mzee Damanda katupwa jirani walipo wao. Akatimua mbio kujaribu kunusuru maisha yake lakini ilikuwa kazi bure hakufika mbali. Sharifu akamtokea kwa mbele kabla ajaenda kumtangazia mbovu huku amemkunjia ngumi. Akafanya kama anampiga kisha akarudisha lile konde nyuma papo hapo Afande Regan akatapatapa na roho hatimaye akaaga dunia. Afande Chacha akashuhudia mwenzake akiuawa. Roho ikamuuma na majonzi yakamtawala lakini atafanyaje wakati mtuhumiwa wake anatumia nguvu za giza ukienda kichwa kichwa unaumia. Ikabidi awe mpole na kutumia akili nyingi kwaajili ya kumdhibiti mtuhumiwa. Sharifu akaendelea kumtafuta Mzee Damanda aliyemkimbia wakati akifanya mauaji ya Afande Regan. Akamkosa lakini hakuweza kukata tamaa. Akazidi kumtafuta kwa hali na mali lakini ikashindikana ndipo wazo likamjia kichwani mwake akanena baadhi ya maneno.



    “Dukila chamkwanda buchula,” Sharifu baada ya kunena maneno yale likatokea vumbi zito na likaenea maeneo yote ya pale.



    Baada ya vumbi kusambaa Mzee Damanda akasikika kwenye kichaka kimoja wapo akikohoa kwa tabu. Kukohoa kwa Mzee Damanda kukamfanya Sharifu aweze kusikia. Akajaribu kutega sikio vyema ili aweze kusikia sauti inatokea wapi. Ndipo alipogundua kuwa sauti ya Mzee Damanda inatokea kwenye kichaka kimoja wapo kilicho jirani na nyumba yake. Akapotea ghafla na kutokea kwenye kichaka alichokuwepo Mzee Damanda. Akamkuta kiongozi wake akitetemeka kwa hofu kisha akamnyanyua kwa nguvu pale alipochuchumaa na akapepesa macho pande zote juu, chini na pembeni. Alipotazama juu akaliona tawi nene la mti wa mpingo likining'inia kichwani kwa Mzee Damanda. Sharifu akaangalia anga kwa muda punde machoni mwake kukatoka miale ya bluu. Miale ile ikaambatana na mawingu. Hayo mawingu yakaleta bonge la radi hadi ikapelekea tawi lile la mpingo kumdondokea Mzee Damanda kichwani. Mzee Damanda akafariki pale pale huku Afande Chacha akishuhudia mauaji yale. Baada ya mauaji yale kuyafanya Sharifu akaondoka na kutokomea eneo lile.



    **********

    Simu inapigwa kituo kidogo cha polisi cha Doma na anayepiga si mwingine bali ni Afande Chacha. Simu aliyoipigia ikaita kwa muda mrefu na mwisho kukata. Hata hivyo hakukata tamaa akajaribu tena kupiga kwa mara ya pili. Kwa mara nyingine simu ikaita kwa sekunde kadhaa kisha ikapokelewa.



    “Halooh!” ilisikika sauti ya mkuu wa kituo upande wa pili ikiongea kwa ustadi.



    “Eeenh mkuu,” Afande Chacha akaongea.



    “Mmefikia wapi hadi sasa?,” Mkuu wa kituo aliuliza huku akionyesha dalili ya kutojua kitu kilichotokea.





    “Japo tumefikia hatua nzuri...nasikitika kuwaambia kuwa Afande Regan hatunaye.”



    “Nini?.”



    “Afande Regan amefariki.”



    “Amefariki lini? na aliyemuua ni nani?,” Mkuu wa kituo akadodosa.



    “Amefariki leo muda huu na aliyefanya mauaji ni mtuhumiwa yule yule aliyefanya mauaji ya mwanzo.”



    “Mtuhumiwa mwenyewe ushalipata jina lake?.”



    “Ndiyo.”



    “Anaitwa nani?.”



    “Anaitwa, Sharifu.”



    “Sawa, fanya juu chini umkamate huyo mtuhumiwa...mimi kukipambazuka nitachukua polisi wawili nitakuja kufuata mwili wa Afande Regan” alielekeza mkuu wa kituo kisha akakata simu.



    Baada ya kumaliza kuongea na simu Afande Chacha akasogelea maiti ya Mzee Damanda kisha akapiga simu kwa mjumbe kumpa taarifa za mauaji yaliyotoka kutendeka muda si mrefu. Mjumbe baada ya kupata taarifa hakuchelewa kuja. Alikuja akathibitisha kisha kulipopambazuka akaita ndugu na majirani waweze kufanya utaratibu wa mazishi jioni.



    **********http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mkuu wa kituo akawasili katika kijiji cha Maharaka asubuhi na mapema kuchukua mwili wa mwenzao. Wakachukua na wakaondoka kwenda kuendelea na mazishi huku nyuma wakamwacha Afande Chacha akiendelea kufuatilia kesi yake. Baada ya mwili wa Afande Regan kuchukuliwa Afande Chacha akazidi kuendelea na kesi yake ya uchunguzi kisiri siri ili mtuhumiwa asishtukie kama kuna mtu mwengine anampeleleza. Akapita kila eneo ambalo Sharifu hupita ili kuzidi kumtafutia njia mbadala ya kumweka nguvuni. Akaweka kila mbinu lakini ikawa ngumu kumnasa Sharifu. Siku moja baada ya kutumia kila njia na kila mbinu kumkamata Sharifu na ikashindikana ndipo hapo akakaa chini akatafakari ni jinsi gani ya kumdhibiti mtuhumiwa akiwa ndani. Katika kutatafakari hayo ghafla usingizi moja kwa moja ukamchukua kisha ndoto ikampeleka mbali na ikampatia majibu. Hayo yote yalikuwa ni majibu ya kukabiliana na nguvu za giza. Afande Chacha akaota yupo juu ya maji ya mto huku akiwa amezungukwa na wachawi wa rika mbalimbali. Ghafla akiwa amezungukwa, akamuona juu angani Bundi akipita. Baadaye akanya kinyesi chake kikamdondokea mchawi mmoja. Mchawi yule alivyodondokewa na kinyesi cha Bundi wote wakamong'onyoka na kupukutika kama udongo. Na hapo ndoto ikakata na Afande Chacha akaamka akakaa kitako kitandani akatafakari ndoto.



    “Hii ndoto, ina maana gani kwangu?.”



    “Inamaana nimeonyeshwa dawa ya kumdhibiti Sharifu.”



    “Lakini kama kweli ni dawa...... sitofanikiwa kumkamata Sharifu akiwa hai na kumsweka rumande.”



    “Kwa maana inampukutisha na kuwa mavumbi...sasa nitafanyaje?.”



    “Ndiyo...sitojali kama litakalo kuwa na liwe,” Afande Chacha alichekecha kichwa kwaajili ya kuwaza na kuwazua alipopapata suluhu akakamata simu yake kisha akapiga simu kituoni kwa mkuu wa kituo.



    “Mkuu, mtuhumiwa huyu ngumu kumkamata,” Afande Chacha alisema mara baada ya mkuu wa kituo kupokea simu.



    “Kwa nini!!!?,” Mkuu wa kituo aliuliza kwa mshangao kwa kutotegemea kijana wake kushindwa kesi ile.



    “Anatumia nguvu za giza.”



    “Eti...nini?.”



    “Anatumia uchawi.”



    “Sasa wewe, kama wewe umechukua uamuzi gani?.”



    “Uamuzi wangu ni kuua tu, kuliko kumkamata nikafa mimi.”



    “Basi fanya unavyojua, kwa kuwa kesi umeishikilia wewe ya huyo mtuhumiwa.”



    Basi baada ya kupewa oda Afande Chacha akakata simu na kujua nini cha kufanya juu ya kiumbe hatari Sharifu. Akaendelea kukong'ota usingizi hadi mishale ya saa nne na robo ya asubuhi ndipo akashuka kitandani. Akajiandaa kuelekea kwa mwenyeji wake Mzee Bemele ambaye ni mjumbe wa kijiji cha Maharaka.



    “Mzee kinyesi cha Bundi hivi naweza kukipata wapi?,” Afande Chacha alimuuliza mwenyeji wake mara baada ya kufika nyumbani kwa mjumbe.



    “Cha nini kijana?...maana kupata ni adimu,” Mzee Bemele alimchangamkia mgeni wake kwa swali na kuongea kwa ucheshi.



    “Nina kazi nacho muhimu sana.”



    “Oooh, sasa kile kinyesi kinapatikana kwenye milima ile ya Mlazamrungu na kinapatikana usiku... Ukienda asubuhi, jioni au mchana hukipati hadi usiku muda wakurejea Bundi kwenye viota vyao,” Mzee Bemele alimweleza Afande Chacha kwa uwelevu zaidi huku akimuonyesha milima yenyewe kwa kidole.



    “Mmmh!!!, usiku unaweza kunipeleka?,” Afande Chacha aliuliza huku akijaribu kuangalia ile milima.



    “Ondoa shaka, nitakupeleka ila unipitie.”



    “Sawa mzee,” Afande Chacha walikubaliana na Mzee Bemele kisha akaondoka kwenda kupata chakula mgahawani.



    Huku nyuma akamuacha Mzee Bemele akikaza kitanda chake kamba. Afande Chacha alikunywa chai na maandazi mara baada ya kufika mgahawani. Alikunywa kisha akalipa pesa na kuondoka kurudi kwenye chumba alichopanga. Alipofika chumbani akalala huku akisubiri muda wa kwenda milima ya Mlazamrungu kuchukukua kinyesi. Muda wa kwenda milimani ulipowasili Afande Chacha akaamka kisha akatoka ndani akafunga mlango kwenda kwa Mzee Bemele kumpitia amsindikize. Akamkuta Mzee Bemele yupo nje akimsubiri. Wakachukuana na kuongozana milimani. Wakafika na kuchukua wanachokihitaji kisha wakarudi kijijini. Wakaachana na Mzee Bemele njiani huku Mzee Bemele akienda nyumbani kwake. Afande Chacha alikwenda kwenye chumba chake kupumzika kwaajili ya kesho kujiandaa na mashambulizi kabambe mara baada ya kupata dawa aliyoonyeshwa kwenye maono. Kulipokucha tu Afande Chacha hakuwa na muda wa kupoteza tena akavaa ujasiri kuchukua pistol JF 2 na kuichomeka kiunoni. Akachukua pia kinyesi cha Bundi na kutia kwenye maliboro nyeusi kisha akaanza safari ya kwenda kwa mtuhumiwa wake kuanzisha pambano baada ya kukamilika kila idara.



    “Upo chini ya ulinzi!. Usikukuruke wala usiyumbe yumbe,” Afande Chacha alimweka chini ya ulinzi Sharifu mara baada ya kutia timu kwenye ngome yake.



    Sharifu aliposikia na kuona silaha akatii amri. Akapiga magoti na kunyoosha mikono juu kana kwamba amesalenda. Afande Chacha alipoona mtuhumiwa kasalenda mwenyewe akataka asogee ampige pingu aende naye kituoni. Lakini haaaah wapi!. Sharifu si mjinga hivyo kama unavyodhani. Kabla hajasogea Afande Chacha, Sharifu akainua macho juu na hapo akampiga kombora la haja Afande Chacha. Afande Chacha silaha ikadondoka kule akawa yupo chini akiugulia maumivu. Hajakaa sawia akataka aongezwe kombora lingine. Wee!. Afande Chacha hakukubali. Alipoona kombora linakuja akatoa kinyesi cha Bundi akarusha kwa Sharifu ikawa ngoma droo. Katika kukuru kakara wakati Afande Chacha anajipanga ghafla kombora likampata likamuumiza na akaaga dunia papo hapo. Sharifu naye kinyesi cha Bundi kilimpata kwa wingi pale pale nae akaungua na kuanza kupukutika kama udongo wa kichanga akatoweka duniani. Mwili wa Afande Chacha ulikuja kuchukuliwa na wenzie ukazikwe baada ya taarifa ya kufariki kwa Afande Chacha kufika katika kituo kidogo cha polisi cha Doma. Taarifa za polisi kuwawa zikamfikia mkuu wa wilaya ya Mvomero Mh. Gidion Julius Mongi, akawasili kituo cha polisi cha Doma akatoa rambi rambi kwa polisi waliofariki kisha akaelekea kijiji cha Maharaka. Akakutana na uongozi wa serikali ya kijiji akaitisha mkutano wa wanakijiji wote, wanakijiji wote wakakusanyika akatoa rambi rambi napo kwa vifo vilivyotokea katika kijiji cha Maharaka. Serikali ya kijiji ikapokea rambi rambi na wanakijiji wote wakatulia tuli wamsikilize mkuu wa wilaya wao.



    “Wanakijiji...safiii,” Mkuu wa wilaya alipaza sauti mara baada ya kuona wanakijiji wamekusanyika kwa wingi.



    “Safiii,” Wanakijiji wote wakaitika kwa huzuni kidogo.



    “Poleni sana, kwa misiba iliyotokea.”



    “Tushapoaaa,” Wanakijiji wote wakaitika tena kwa kupaza sauti.



    “Wengi wenu, naamini ujio huu amkutegemea...ujio huu umewasili kwenu kwa lengo moja tu kutokomeza uchawi,” Mkuu wa wilaya aliendelea kusema.



    “Wengi tunaamini kijiji chetu kipo shwari......uchawi hamna tena baada ya kufa wachawi katika kijiji chetu. Basi ningependa kijiji chetu kiendelee hivi hivi kwasababu uchawi hauna maana, kisasi akina maana. Sasa ya nini tuendelee kung'ang'ania vitu visivyo na faida yatupasa tubadilike sasa tuwe kitu kimoja tushirikiane pamoja pia tupendane. Tukitekeleza hayo naamini kijiji chetu kitakuwa tulivu na amani.....tumeelewana?.”



    “Ndiyo, Mheshimiwaaa” walipaza sauti wanakijiji wote kwa kumuitika Mkuu wa wilaya wao.



    Baada ya kuhitimisha kikao na kuondoka Mkuu wa wilaya. Wanakijiji wote wa Maharaka tokea siku hiyo wakaishi kwa upendo na amani hakukuwa tena na uchawi wala visasi, wakapendana na kushirikiana kwa kila jambo.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **********

    Majanga tunamwachia Mwenyezi Mungu naamini atatupigania hapa duniani. Kumbuka kipindi chote mchawi hana rafiki. Mchawi ni nani?, mchawi ni mnafiki, mchawi ni mgombanishi, mchawi ni yule mkosaji. Mchawi si mtu mzuri katika jamii. Sababu mchawi ataroga mchana kweupe pee hata haya aoni. Yaani hana huruma hata kidogo kwa jamii, huyo ni mtu gani asiye na huruma. Inamaana ajui kama kuna Mungu? na kama ajui mbona akiwanga anamtanguliza Mungu?. Naona ni unafiki umemjaa. Yaani unaroga halafu unampenda Mungu uoni kama ni kosa, lakini sikatai fanya yote ila kaa ukijua ipo siku zamu yako yaja, si unajua kutesa kwa zamu. Adhabu ya kaburi aijuae maiti na mkataa pema pabaya panamuita. Wachawi wote sasa pabaya patawaita, kwa kuwa sisi wanyonge kwenu basi tunasema Insha Allah! sisi tunamwachia Mungu awadhibiti nyie wachawi.



    _____MWISHO_____

0 comments:

Post a Comment

Blog