Search This Blog

MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI - 2

 






Simulizi : Mama Usinifundishe Uchawi

Sehemu Ya Pili (2)





“Mke wa Mzee Kaoneka alipotoka sokoni akamkuta mumewe ukumbini kalala kwenye mkeka. Akashangaa sana ulalaji wa mumewe maana hakumzoea akilala vile alilala chali huku mdomo ukiwa wazi na kutokwa mapovu. Ile hali ikamchanganya kichwa akajaribu kumwamsha lakini akagonga mwamba. Akajaribu kumshika kifuani kusikiliza mapigo ya moyo lakini nako hola. Mke wa Mzee Kaoneka ndipo akajua fika mumewe kashafariki kilio cha kuwashtusha majirani kilitawala kwenye nyumba punde majirani wakajaa kumfariji mwenzao.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Mbona kaaga dunia kwa kifo cha kutatanisha, nakumbuka mara ya mwisho nilimuona jana akipita nyumbani kwangu akiwa na afya,” Mama mmoja jirani alisema akimwambia jirani mwenzake aliyekaa karibu yake.



“Kwani wewe ukijui, kijiji chetu kilivyo na ushirikina?,” Mwenzake yule mama akamuuliza yule mama kwa kunong'ona asisikiwe na baadhi ya majirani wengine.



“Nilikuwa sijui, kumbe kijiji hiki hakifai.”



“Akivumi lakini kimo, tuwe makini yasije kutukuta,” Wamama wale wakaendelea kupiga soga chini chini wasisikiwe na mtu yeyote pale msibani.



Mzee Kaoneka kwakuwa alifariki jioni mazishi yake yakapangwa yafanyike kesho jioni, kesho ilipofika wakafanya mazishi kisha majirani wote wakatawanyika kurudi majumbani kwao.



**********

Sharifu na mama yake walikuwa na furaha wakasherekea sherehe babu kubwa. Binti Mngane siku hiyo akampongeza mwanae kwa ujasiri uliotukuka.



“Sasa unaelekea kuwa galacha...tukio hili nakupongeza,” Binti Mngane alisema huku akimtingisha kichwa mwanae.



“Siku zinavyosonga, naamini uwezo wangu utakuwa mkubwa zaidi,” Sharifu aliongea huku akijikuna kichwa mara baada ya Binti Mngane kumuacha kumtingisha.



“Kweli kabisa...sasa kilichobaki ni kunywa na kula, kwa kujipongeza,” Binti Mngane alisema huku akinyanyuka kwenye mkeka na kuanza kucheza kwa furaha.



Ghafla baada ya muda akaacha kucheza, akatazama juu ya paa akanyoosha mkono wa kushoto kikatokea kikombe chekundu chenye damu ya binadamu. Mama Sharifu akaendelea kuunyoosha tena mkono wake wa kuume juu nako kukatokea nyama mbichi ya Paka. Wakaangua kicheko kwa muda kisha Binti Mngane akamgawia mwanae damu na nyama kidogo wapate kusheherekea siku hiyo. Wakatumia vyema kwa kusheherekea, siku iliyofuata saa moja usiku Binti Mngane akamtuma mwanae kwenye duka lililokuwa jirani na kijiji.



“Pesa zimetuishia cha msingi kabla hatujakumbwa na janga la njaa, nenda na hili pembe ikachote pesa dukani kwa Msambaa,” Binti Mngane alimwambia mwanae kisha kumwelewesha kwa makini asije kuumbuka mbele ya umati wa watu.



“Nitatekeleza, mama,” Sharifu alisema huku akipokea pembe mara baada ya kusikiliza maelekezo kwa mama yake.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Alipopokea lile pembe pale pale pembe likageuka kuwa pesa akaenda nalo moja kwa moja dukani. Akalikabidhi kwa muuza duka kisha akataka huduma kwa haraka, kwa kuwa pembe si la kawaida ni la kishirikina hivyo msambaa hakubahatika kugundua chochote akaona kama amepewa pesa na si kitu kingine. Hii tabia hata kwenye mazingira yetu tunayoishi tunakutana nayo inatambulika sana kwa jina la chuma ulete. Hali hii hutokea sana kwenye biashara unaona mtu anakupa pesa umhudumie ukishakuja kuchanganya pesa yake na pesa zako unakuta pesa zako zipo pungufu. Maskini Msambaa hakugundua chochote hadi muda ule akaendelea kumhudumia Sharifu kama wateja wengine hatimaye kumrudishia na chenji juu. Alivyompa Sharifu chenji ndiyo amejiroga kabisa alimpatia pesa zote alizouza kwa siku hile bila mwenyewe kujua. Sharifu alipopewa chenji akapokea upesi akarudi nyumbani. Alipofika nyumbani akamkuta mama yake kajilaza kwenye mkeka akimsubiri ukumbini.



“Mwanangu umefanikiwa kupata ulichofuata?” aliuliza Binti Mngane kwa shauku ya kutaka kujua huko atokapo amekutana na nini kilichomkuta mwanae hadi achelewe kurudi.



“Nimefanikiwa ila....”



“Ila nini...umekamatwa?.”



“Hapana...kumbe?.”



“Nilikuwa na hofu.”



“Hofu ya nini?.”



“Ya kukamatwa,” Sharifu alijibu huku akihema kwa kasi kama mtu aliyetoka kukimbizwa.



“Pole sana...usingekuwa na hofu mwanangu” alisema Binti Mngane kwa kumwondoa hofu mwanae.



“Kwa nini?” aliuliza Sharifu kwa kutahamaki.



“Kwasababu wafanyabiashara wengi wa kijiji hiki hawana kinga” aliongea Binti Mngane kwa kujiamini.



Baada ya mazungumzo ya Sharifu na mama yake Sharifu akaenda kufunga mlango wa ukumbini kisha akarudi kukaa chini ya mkeka. Akazitoa pesa ambazo zilizofungwa kwenye mfuko mweusi wa malibolo akamkabidhi mama yake, Binti Mngane alipozihesabu zile pesa akakuta zipo laki tano tasrimu.



“Hizi pesa mwanangu, zinaweza kutusogeza kiasi fulani” alisema Binti Mngane kwa kuonyesha tabasamu.



“Tusipotumia kwa kufuja, zinaweza kutusogeza,” Sharifu aliongea kwa kuchangia huku akinyanyuka kwenye mkeka na kuelekea chumbani kwake.



Akaingia chumbani kwake na kutoka huku akimuaga mama yake kuwa anakwenda kujumuika na wenzake kwa ajili ya kubadilishana mawazo mawili matatu. Binti Mngane hakumzuia akamruhusu mwanae kisha yeye akaingia chumbani kwake kuzihifadhi pesa. Mara baada ya kuziweka mahali pasala akatoka chumbani akarudi ukumbini kuendelea kujilaza tena. Sharifu alipofika mtaani akaungana na vijana wenzake kwa kucheza bao. Akacheza hadi saa mbili, ndipo polepole aliporejea nyumbani na kumkuta mama yake kashaamka sasa anachakalika kupika chakula cha usiku.





“Leo naona umeenda dukani mwenyewe” aliongea Sharifu kwa utani mara baada ya kurudi nyumbani.



“Nimeenda mwenyewe, maana uliniahidi unarudi mapema hujarudi sasa ningefanyaje,” Binti Mngane alisema huku akigeuza chakula.



Sharifu akafurahi moyoni jinsi anavyomwona mama yake akinung'unika, baada ya muda kidogo akatulia na kuanza kumtia moyo mama yake kwa kumchangamsha na stori za hapa na pale huku wakisubiri chakula kiive. Wakaendelea kupiga soga mpaka nyakati za saa nne ya usiku ndipo chakula kikawa kimeiva kikapakuliwa kikawekwa mboga na kikaliwa. Binti Mngane alimfurahisha mwanae kwa kumpikia chakula akipendacho ambacho pia baadhi ya watu ukipenda si chakula kingine bali ni wali na maharagwe. Walipomaliza kula Sharifu akatoa vyombo kisha akamuaga mama yake kuwa anakwenda kulala. Binti Mngane hakupinga anajua fika kama mwanae alikuwa amechoka hivyo akamruhusu akalale. Hata yeye pia hakukaa sana nyuma naye akashindwa kuendelea kukaa peke yake akanyanyuka akaenda kufunga milango yote kisha akaenda kulala. Usiku mnene usio na makadirio Binti Mngane akaamka toka kitandani kisha akaenda chumbani kwa mwanae.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Wewe mtoto, mbona unalala sana hujui kama muda ushafika” alisema Binti Mngane mara baada ya kumwamsha mwanae.



“Najua, lakini leo najisikia uchovu,” Sharifu aliongea huku akijinyoosha viungo vya mwili mara baada ya kuamka na kukaa kitako kitandani.



“Ebu nyanyuka, tushachelewa” alinena Binti Mngane kwa kutotaka kuelewa anachosema mwanae. Akamvuta mwanae mkono kwa kumlazimisha waondoke.



Sharifu hakuwa na ujanja tena akanyanyuka kwa kujivuta hivyo hivyo na uchovu. Akajibadilisha muonekano kimiujiza kisha wakatoka nje ya nyumba yao. Walipotoka nje Binti Mngane akanyoosha kidole cha husda chini ya ardhi papo hapo kikatokea kiungo kidogo na usinga. Akakiongeza kile kiungo kimiujiza kisha wakapanda na mwanae wakakipaisha juu hatimaye wakakielekezea upande wa magharibi karibu na kijiji cha jirani kwenye nyumba ya kijana mmoja mwenye utajiri mkubwa pale kijijini. Kiungo kilipofika kwenye nyumba ya huyo kijana wakakitua kile kibeko juu ya paa la nyumba ya huyo kijana bila huyo kijana kujua kitu chochote kinachoendelea kwenye mandhari yake. Mara baada ya kutua wakadumbukia na hatimaye kutokea chumbani mwa huyo kijana na kumkuta amelala fofofo. Binti Mngane na mwanae wakamnyanyua huyo kijana kisha wakatoka naye nje kwenye mti wa ukwaju mrefu. Walipofika nje Binti Mngane akanyoosha usinga wake kila upande kisha akampiga nao huyo kijana kichwani. Huyo kijana baada ya kupigwa akaanza kuzunguka mti wa ukwaju kwa kutambaa huku akihema kwa kasi kama jibwa koko aliyetoka kukimbizwa. Hii hali inatokea sana katika maisha yetu unakuta unaamka umechoka mpaka unajiuliza hivi jana kazi gani nimefanya ya kunichokesha namna hii?. Hukumbuki kama unapolala muda mwingine wachawi wanakusulubisha kwa kukufanyisha kazi zao bila malipo. Wala huwezi kujijua ndiyo maana ukiamka unajikuta umechoka unashindwa hata kufanya kazi zako binafsi. Lakini kumbuka wachawi wanafanya hayo yote bila faida bali tu kwasababu ya wivu tu. Anasurubishwa pasipo sababu kijana wa watu asiye na hatia. Wakaendelea kumtesa mpaka kufikia hatua ya kuchoka yote hayo kisa utajiri wake ndiyo umemponza.



“Tumuache mtoto wa watu, akapumzike,” Sauti ya Sharifu ya huruma ikasikika kinywani mwake.



“Mbona unataka kuwa mpumbavu au umeridhika kuonyeshwa majivuno” aliongea Binti Mngane kwa kupayuka kwa hasira.



Binti Mngane akakasirika sana na hakutaka kumsikiliza mwanae hata kidogo. Akaendelea kumtesa kijana wa watu kwa kumkomoa, lakini baada ya muda roho ya huruma ikamtanda akaja kukumbuka maneno ya mwanae haraka. Akashirikiana na mwanae kumrudisha huyo kijana chumbani akaendelee na usingizi na wao wakachukua uamuzi wakutoweka pande zile kimiujiza wakatokea ndani ya nyumba yao. Asubuhi ya siku iliyofuata wote wakachelewa kuamka kutokana na uchovu wa jana usiku. Binti Mngane asubuhi ile akaanza kuamka kwa kujivuta kutoka kitandani akatoka nje kufanya shughuli zake za kila siku. Baada ya muda kidogo kupita Sharifu naye akatoka nje na kukuta mama yake anafagia uwanja.



“Shikamoo” alitoa salamu Sharifu kwa mama yake huku akipiga miyayo ya uchovu.



“Marahaba mwanangu,” Binti Mngane aliitika salamu ya mwanae huku akiweka ufagio sehemu husika mara baada ya kumaliza kufagia uwanja.



“Inaonekana, umechelewa kuamka maana kazi zako mpaka saa hizi inakuaga ushamaliza kufanya,” Sharifu alisema huku akilivaa shati aliloshika mkononi.



“Nimechelewa mno kwa kuwa jana nilichoka sana,” Binti Mngane aliongea huku akiingia ndani kwenda kupika uji.



Binti Mngane alipoingia ndani Sharifu akachukua mswaki ambao anatundikaga nje ya kuta yao ya nyumba huku akielekea uani. Alipomaliza akarudi ndani akakuta uji tayari ushaiva na ushatengwa kwenye vibakuli, wakaketi kwenye kirago na mama yake tayari kwa kuanza kunywa.



“Najihisi sipo sawa” aliongea Sharifu mara baada ya kunywa uji kijiko kimoja.



“Unajisikiaje?,” Binti Mngane aliuliza huku akiendelea kunywa uji.



“Mwili unauma, na hata akili yangu kwasasa haijatulia,” Sharifu akaeleza.



“Usiwe na hofu, hiyo hali haina shida lazima itokee kwa maana unapoenda kuwanga mara nyingi unatumia mwili na akili” aliongea Binti Mngane kwa kujaribu kumtoa uoga mwanae.



Binti Mngane akamueleza mwanae kisha akaachilia kunywa uji akaingia chumbani kwenda kuchukua dawa iliyo ya unga mweupe uliyofungwa kwenye karatasi ya kaki. Akachota ile dawa kiasi kupitia vidole vyake viwili dole gumba na husda. Baada ya kuchota akamkabidhi mwanae ili anyunyuzie kwenye uji. Sharifu akapokea dawa kinyenyekevu kisha akanyunyuzia kwenye uji wake na kuanza kunywa. Alipomaliza akaweka kikombe jikoni kwenye vyombo vichafu na hatimaye akaingia chumbani kwake kujilaza. Mchana alipoamka usingizini ndipo akatokea kuamini kuwa kweli ile dawa imefanya kazi yake. Hakusikia tena uchovu wala mwili kuuma, akatoka chumbani akaelekea ukumbini cha kushangaza hakumkuta mama yake ndani. Akajitahidi kumtafuta huku na kule ndipo akaja kumkuta nje nyuma ya nyumba yao tayari amejitandikia mkeka na kujipumzisha.



“Mama,” Sharifu alimwamsha mama yake kwa kumtingisha mwili.



“Eeeh!!!” aliitika Binti Mngane kwa mshtuko na mapigo ya moyo wake yakidunda kwa kasi. Akatulia kidogo akimtazama mwanae kwa jicho kali kisha akasema kwa kigugumizi na huku akihema bila mpangilio.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“Kumbe ni wewe, utaniua na presha mwenzio unaona kabisa umri wangu wenyewe ulivyokwenda ukinitoa roho yangu je” alisema Binti Mngane kwa jazba kidogo mara baada ya kujua aliyemshtua ni mwanae.



“Samahani sikuwa na lengo hilo, lengo langu nilitaka kukuhabarisha kuwa kwasasa sisikii uchovu wala maumivu ya aina yoyote tokea unipe ile dawa,” Sharifu alieleza huku akionyesha nyuso ya tabasamu.



“Ile dawa ni nzuri, ndiyo tunayotumia karibia wachawi wote wa chama chetu pindi tusikiapo hali hiyo,” Binti Mngane aliongea huku akijinyoosha miguu.



“Kwanini mama, ile dawa nami sijapewa?.”



“Mzee Damanda anatoa hii dawa kwa kila mwanachama ambaye ni kiongozi wa familia ili ije kutumiwa na mrithi wake,” Binti Mngane akanyamaza kidogo akamsikilizia mwanae atasema nini katika hilo alilolisema, alipoona kimya mwanae ajaongea chochote akaendelea yeye kuzungumza.



“Kwa hiyo wewe kwa kuwa ni mrithi wangu, dawa hii tutatumia wote aina haja kupewa nyingine ukaharibu utaratibu wa kiongozi.”



“Sawa mama...lakini mama leo nakuacha naenda kwa shangazi mara moja kumsalimu,” Sharifu alimuaga mama yake bila kujua mama yake na shangazi yake hawapatani.



**********

Shangazi yake Sharifu anaitwa Leah, alizaliwa baba mmoja na mama mmoja na baba yake Sharifu. Pia walizaliwa wawili tu katika familia yao baada ya kufariki kaka yake katika mazingira ya kutatanisha akabaki peke yake katika ulimwengu wa baradhuri.



“Mkumbuke bwana shangazi yako, siunajua wakati huu yupo mpweke” alisema Binti Mngane kinafki. Kisha akamuuliza swali mwanae kwa kebehi mara baada ya kuagwa na mwanae.



“Kwahiyo, nikuwekee chakula?.”



“Usiniwekee nitakula kwa shangazi, huenda nikakuta chakula huko” alijibu Sharifu kisha akaondoka.



Nyumba ya shangazi yake Sharifu haikuwa mbali na kijiji cha Maharaka, ilikuwa ni kijiji cha pili tu na wala ulikuwa hutembei kilometa nyingi hadi ufike katika nyumba ya shangazi yake Sharifu. Sharifu hakuchukua masaa mengi kufika kwa shangazi yake. Akafika na kumkuta shangazi yake nje ya nyumba yake akisuka mkeka.



“Mwanangu, leo umenikumbuka?” aliuliza Leah mara baada ya kumuona mtoto wa kaka yake.



“Nimekukumbuka shangazi ...................nimeamua nije kukutembelea japo wewe mgumu kuja kwetu,” Sharifu alijibu huku akikaa kwenye mkeka mara baada ya kukaribishwa na shangazi yake.



“Sio hivyo mwanangu, shangazi yako nina majukumu mengi yanayonikabili,” Leah alisema huku akipakaza mate kwa kulamba kidole cha husda kisha akaendelea kusuka mkeka wake. Akasuka kidogo kisha akaachia na kuanza kuongea kwa majonzi.



“Halafu si unajua kuwa nipo peke yangu toka mume wangu afariki, hivyo sina budi kujitafutia pesa ya kukidhi mahitaji yangu ya hapa nyumbani kwa kujiuzia mikeka miwili mitatu.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Nimekuelewa shangazi, basi acha kuwa na majonzi” aliongea Sharifu kwa kufariji.



“Sawa lakini mwanangu umekuja wakati umekuta shangazi yako nishakula...vipi ulipotoka umekula?.”



“Nisifiche shangazi yangu, sijaweka kitu chochote tumboni mwangu,” Sharifu alijibu huku akipiga miayo akiashilia njaa.





“Pole mwanangu ngoja nikakupikie chakula maana kuna Vinguruka viwili niliviacha vitakutosha kwa mboga,” Leah alizungumza huku akiinuka na kuelekea jikoni kupika chakula.



Dakika kadhaa ugali ukaiva ukawekwa kwenye sahani kisha ukafunikwa usipoe. Wakachukuliwa Nguruka wakachomwa jikoni. Walipokuwa tayari kuliwa wakawekwa kwenye sahani pembezoni mwa ugali kisha Leah akatoka nje na chakula kwaajili ya kumtengea mtoto wa kaka yake ale. Sharifu baada ya kutengewa hakuchukua muda kumaliza kula, dakika chache tu akawa amemaliza na kutoa vyombo vichafu kisha akavipeleka jikoni. Akarudi kupiga soga na shangazi yake. Akakaa kwa shangazi yake hadi muda wa jioni alipoona muda umekwenda akamuaga shangazi yake na kurudi nyumbani, alipofika nyumbani akamkuta Binti Mngane yupo ukumbini akichambua tembele la mboga ya usiku.



“Mama nimerudi, nahisi ulipooza” aliongea Sharifu kwa utani mara baada ya kuwasili nyumbani.



“Nilipooza sana mwanangu tangu muda ule ulivyoondoka labda ulivyorudi utanichangamsha,” Binti Mngane aliongea huku akionyesha sura ya uchangamfu na kutabasamu kwa mbali.



“Lakini mama unajua kama shangazi analalamika,” Sharifu alianzisha mada iliyomchukiza na kumkera sana mama yake.



“Kuhusu nini?,” Binti Mngane alionyesha kuuliza kwa sauti ya juu sana.



“Kuhusu kumtembelea.”



“Kuhusu kumtembelea!!!, yeye kwani anatutembelea?” aliuliza Binti Mngane kwa ghadhabu kubwa.



“Lakini mama tusimlaumu bure, yeye unajua fika tokea afiwe na mumewe majukumu yote yanamwelemea,” Sharifu alimtetea shangazi yake.



“Naona siku hizi mwenzangu, ushakuwa mwanasheria wa kutetea watu,” Binti Mngane alisema huku akinyanyuka kwenye mkeka na kwenda jikoni kupika mara baada ya kumaliza kuchambua matembele.



Sharifu kwa kuona wakuongea naye kaenda kwenye shughuli yake akaingia chumbani kwake naye kujipumzisha mwili. Baada ya masaa kadhaa chakula kikawa tayari Binti Mngane akakitenga ukumbini kwenye mkeka kisha akaenda kumuita mwanae waje kula.



“Sharifu baba,” Binti Mngane alimuita mwanae kwa upendo.



Ukweli kabisa Binti Mngane anampenda mwanae kwa kuwa wakati wa kumleta duniani alimpatia shida sana. Nusu afe wakati anajifungua na pia mwanae huyo ndiye aliyesababisha kizazi chake kuondolewa na kushindwa kupata watoto tena, hivyo ndiyo maana anampenda mwanae kupitiliza kama yai vile.



“Naam,” Sharifu aliitika kwa sauti ya juu pindi alivyoitwa na mama yake kisha akanyanyuka kitandani akaenda kufungua mlango atoke chumbani akajumuike na mama yake.



“Chakula tayari njoo tule, nikalale mapema,” Binti Mngane alisema huku akiongoza ukumbini.



Mama na mwana wote kwa pamoja wakajumuika kwenye chakula cha usiku. Walikula na walipomaliza Binti Mngane akaaga kuwa anakwenda kulala. Akaenda kulala huku nyuma akimuacha mwanae akitoa vyombo walivyolia na kupeleka jikoni. Mara baada ya kutoa vyombo Sharifu naye akaingia chumbani kujilaza kitandani, mwanga hafifu wa koroboi ukamfanya Sharifu kudondila kama kuku wa mdondo baada ya kujilaza. Usingizi palepale ukampitia alikuja kushtuka muda mwengine kabisa wa usiku ambao uliokuwa umejaa giza totoro na huku sauti za ndege wa ajabu zikilindima huku na kule. Sharifu katika kushtuka haraka haraka akajifunga usongo kwenye paji la uso kisha akavaa kaniki nyeusi kiunoni na uso wake papo hapo ukabadilika ukawa na unga mweupe. Alipohakikisha kamaliza kujiandaa akatoweka kimiujiza na kwenda moja kwa moja hadi kwenye nyumba ya jirani yao. Dhumuni ya kwenda huko ni kumdhuru kijana mmoja ambaye huwa analima na kusoma kwa bidii na pindi msimu wa mavuno unapofika huwa anapata mavuno mengi pale kijijini kushinda vijana wenzake wote. Kutokana na bidii yake shuleni na shambani Sharifu akatokea kuweka wivu kwa huyo kijana hivyo http://deusdeditmahunda.blogspot.com/hakutaka kumuacha salama. Akatokea chumbani kwa yule kijana na kumkuta kitandani kalala usingizi wa pono polepole akatoa kichupa kidogo cha rangi ya Gold kilichojaa maji ya betri. Akammiminia kijana wa watu machoni punde tu akatoweka akatokea chumbani kwake pembezoni mwa ukuta wake wa chumbani. Chapuchapu akajibadili kimiujiza muonekano wake kisha akaendelea kurudi kulala. Asubuhi na mapema majogoo ya alfajiri yakamwamsha kwa kuwika bila kikomo taratibu akajikongoja kutoka kitandani moja kwa moja akaenda kupiga mswaki. Alimaliza na kuelekea bustanini kwake huku akiwa na jembe lake mkononi kwenda kuchuma mbaazi kwa ajili ya mboga. Hakuchuma mbaazi peke yake pia akachimba na mihogo kwaajili ya kunywea chai ile asubuhi. Aliporudi ndani akaimenya mihogo kisha akabandika jikoni, nyakati ya masaa mawili mbele naye Binti Mngane akaamka na kumkuta mwanae kashaivisha chakula na kuitenga kwenye mkeka.



“Hujambo,” Binti Mngane alimsalimu mwanae huku akifunga kiremba chake cha mtelezo. Sharifu akaitika ile salamu kisha kumpa heshima mama yake.



“Marahaba...hongera.”



“Ya nini?.”



“Kwa kuwahi kuamka leo mapema.”



“Ooh kumbe...asantee” alitoa shukrani Sharifu kisha akaendelea na kula mara baada ya kutenga mihogo na kujumuika kwa pamoja.



**********

Kijana aliyemwagiwa maji ya betri alipoamka akashtuka sana kuona macho yake yana kasoro yalikuwa hayaoni chochote zaidi ya giza. Alipoona ile hali akapayuka kumuita mama yake kwa sauti ya juu ili aweze kusikia. Mama huyo aliposikia kupayuka kwa mwanae hakuchelewa kufika chumbani kwa mwanae akaone kilichotokea.



“Nini kilichokupata?,” Mama yule aliuliza kwa hofu.



“Mama, sioni,” Kijana yule alimwambia mama yake huku machozi yakimtiririka.



“Kwanini unasema hivyo...na unamaanisha nini?,” Mama yule aliuliza huku akijitahidi kumfuta machozi mwanae.



“Mimi ni kipofu, siwezi kuona tena,” Kijana yule alieleza kwa nyuso ya huzuni.



“Kipofu!!!...huo ukipofu umeanza lini?,” Mama yule aliuliza huku akiwa aamini anachoelezwa na mwanae.



“Imenianza asubuhi hii,” Kijana yule alisema huku akijaribu kunyanyuka kitandani atembee.



Alipojaribu kutembea akaenda kupalamia kisturi kilichokuwa mbele yake. Hapo ndipo mama wa yule kijana akaamini kama kweli mwanae aoni. Hakutaka tena kuchelewesha muda kwa kumhoji mwanae akamkokota taratibu mwanae na kumwaisha hospitali akafanyiwe vipimo na kupata matibabu pale tatizo litakapoonekana. Alipofika hospitali akaingia na mwanae moja kwa moja kwenye ofisi ya daktari mwanae akapimwe. Yule kijana alipopimwa macho ikagundulika kuwa macho yake hayana matatizo yoyote. Jambo lile likamstajabisha yule mama pamoja na mwanae moja kwa moja yule mama akajua mwanae karogwa si bure. Ikabidi akubaliane na vipimo vya daktari hivyo bila kizuizi akamchukua mwanae kisha wakaondoka kinyonge pale hospitalini.



**********

“Na leo, yaani umenifurahisha sana” alizidi kuongea Binti Mngane kwa kumpa pongezi mwanae.



“Kivipi?,” Sharifu aliuliza huku akitoa tabasamu mwanana kinywani mwake.



“Kwa kunisaidia kupika, kifungua kinywa.”



“Oooh, siku moja moja niwajibu wangu kukusaidia,” Sharifu alizidi kuongea huku akichukua kipande cha mhogo na kula.



“Kweli kabisa, siku moja moja yakupasa unisaidie nami mama yako nipumue,” Binti Mngane alisema huku naye akiendelea kushindilia mihogo kinywani.



“Sawa...lakini mama, mbona leo ulilala kama mfu?,” Sharifu akauliza.



“Kwanini?,” Binti Mngane naye akauliza badala ya kujibu swali la mwanae.



“Nilikuamsha ili twende ukanipe ushirikiano, lakini hukuamka.”



“Nilichoka sana...kwani ulitaka ushirikiano upi?.”



“Wa kwenda, kumshikisha adabu mtoto wa jirani yetu,” Sharifu alijibu huku akichota maji ya kunywa kwenye mtungi.



“Mtoto wa jirani yetu!!!, yupi?,” Binti Mngane alimuuliza mwanae kwa kutaka kujua.



“Yule Issa, mtoto wa Mama Zakia.”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“Aaah, nishamjua kumbe yule kijana?.”



“Eeeh.”



“Kisa nini, cha kumshikisha adabu mtoto wa watu?.”



“Ana majivuno...nami watu wenye majivuno siwapendi hata kidogo,” Sharifu akaongopa.



“Mh...ikawaje?.”



“Nilimmwagia maji ya betri machoni,” Sharifu alieleza huku akionyesha tabasamu pana kwa kuona kitendo alichofanya ni sahihi.



“Mh, mbona umemfanyia ubaya mkubwa mtoto wa watu?,” Binti Mngane aliuliza na kuonyesha kitendo alichokifanya mwanae ajapendezwa nacho.



“Kama nilivyosema mwanzo kuwa majivuno yake, ndiyo yaliyonifanya nimshikishe adabu.”



“Aisee, siku hizi umejivika roho ya ujasiri au unataka Mzee Damanda akupe vyeo?,” Binti Mngane aliuliza huku akimkazia macho mwanae.



“Cheo lazima nitapata na nitakuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa wanachama wenzangu,” Sharifu alisema kwa utani huku akitoa vyombo mara baada ya kumaliza kula.







“Binti Mngane shibe ilimlevya akaona uvivu kuendelea kufanya kazi. Akajipumzisha kwenye mkeka kidogo pale pale ukumbini. Sharifu alipomaliza kuviosha vyombo akavirudisha jikoni kisha akaingia chumbani kwake kujipumzisha, muda wa jioni ya saa kumi alikuwa kashaamka akajikongoja kwa kutoka hadi ukumbini, akamkuta mama yake bado yupo akiendelea kuchalaza usingizi. “Mama



*****************

************************



Binti Mngane alipomaliza kutoa risala kwa mwanae akatoka nje kuchuma maboga na akachukua fursa ya kumpisha mwanae aendelee na usafi. Dakika kadhaa zikapita Sharifu alimaliza kufagia ndani akachukua mswaki kisha akatoka nje kusafisha kinywa. Binti Mngane alipomaliza kuchuma maboga akarudi ndani na hatimaye kuelekea jikoni kupika maboga yale. Binti Mngane akayaandaa maboga kwenye sahani kisha akayatenga kwenye mkeka ukumbini na kumuita mwanae mara baada ya maboga kuiva.



“Sharifu.”



“Naam.”



“Bado, ujamaliza tu?.”



“Namalizia.”



“Hebu fanya haraka uje tule chakula kitapoa.”



Sharifu akapiga mswaki haraka kisha akarudi ndani kuungana na mama yake kula. Hawakuchukua muda mwingi kwenye kula dakika kama tano wakawa washamaliza kula.



“Ukimaliza kutoa vyombo nakuomba nikutume ukanichukulie pesa zangu” aliongea Binti Mngane mara baada ya kumaliza kula.



“Kwa, nani?,” Sharifu akauliza alipofika jikoni.



“Kwa, Mama Stumai.”



“Haina shida...lakini nitachelewa kurudi.”



“Kwanini?.”



“Nitapitia kwa Kondo, kuchukua mpini wangu wa jembe.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Usijali, pesa hiyo sina shida nayo kwa sasa...wewe pitia tu,” Binti Mngane aliongea huku akijaza maji kwenye ndoo ya uhani akaoge.



Sharifu akaingia chumbani kwake kubadilisha nguo mara baada ya kupeleka vyombo na kutoka nje tayari kwa kuanza safari ya kwenda kwa Mama Stumai. Akiwa njiani kabla hajafika alikotumwa akakutana na Mama Abuu jirani yao aliye na ujauzito wa miezi nane tumboni.





ITAENDELEA

MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI - 1







IMEANDIKWA NA : SADARI KISESA



*********************************************************************************



Simulizi : Mama Usinifundishe Uchawi

Sehemu Ya Kwanza (1)



UTANGULIZI...

“Uchawi upo japo serikali haiamini kama upo. Uchawi huleta utata kwa raia na serikali. Raia wanaamini uchawi sababu unawakuta, serikali haiamini uchawi sababu ya katiba yao. Raia wanaona uchawi ni mateso, sababu ya kufanyishwa kazi pasipo kujijua wenyewe pia wanaona mateso sababu ya kurudishwa nyuma maendeleo. Kwa kiasi kikubwa uchawi hauna nafasi serikalini tena hausikilizwi unaonekana kama ukakasi.

Uchawi ni tishio kwa binadamu uonekanapo. Humkosesha amani na humjengea hofu. Uchawi hauna faida yoyote zaidi ya mateso. Ijapokuwa wachawi wanaona kuna faida. Ukweli wanashangaza mtu anatumikia uchawi toka utoto mpaka uzee, lakini mafanikio hana! badala yake anaambulia fedheha. Hayo yote ya nini ebu...tumpe Mungu nafasi ya kubariki maisha yetu.”



SONGA NAYO....

Mkoani Morogoro, wilaya ya Mvomero, kata ya Kibaoni, na kijiji cha Maharaka. Anga yote ilikuwa imetanda kuashilia mvua saa yoyote inanyesha. Hali ya hewa si shwari baridi lilikuwa kali kupita maelezo. Ardhi baada ya muda ukali wa jua ulipoa ikaacha shamrashamra za wanakijiji zikilindima. Ndege nao walifurahia ujio wa mvua. Shorwe kwa makundi wakawa wanarukaruka na kukimbizana huku wakionyesha furaha kwa ajili ya ujio wa mvua. Yange yange hawakuachwa nyuma walikuwa kipaumbele kupendezesha anga kwa rangi zao nyeupe na kuruka kwa madaha, “Kwaa kwaaa kwaaaa”.

Alaah! Kunguru nae anafurahia ujio wa mvua kwa kurukaruka huku akitoa sauti angavu angani. Anga kikweli siku ya leo ilipendeza ama kweli Mungu hakukosea kuumba viumbe vyake. Ameumba na sasa wanamtumikia. Yaani ni kazi kwelikweli, nakuambia ujio wa mvua ulileta hekaheka hadi kwa wanakijiji. Wanakijiji walitimua mbio na kurudi majumbani wakijua mvua itanyesha kumbe lahasha!!!. Lakini katika pilikapilika za wanakijiji kujihami na mvua, alionekana kijana wa kiume chini ya mwembe akiwa kajiinamia huku mkono wake wa kuume ukiwa umeshika tama. Kijana hakuonyesha dalili ya kuhofia ujio wa mvua. Alijikatia tamaa kabisa na ndipo alipoamua kutulia chini ya mwembe. Kichwa chake kilionekana kimejaa msongo mkubwa wa mawazo huku asijue kinachoendelea angani. Alikuja kushtuliwa na mama yake mara baada ya kuitwa kwa muda mrefu na mama yake kwa kutingishwa mabega.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Naam!!!,” Kijana yule aliitika kwa mshangao na kukurupuka toka kwenye lindi la mawazo mara baada ya kusikia mama yake akimuita.



“Mbona unaonekana una mawazo sana...nini kinachokutatiza?” aliuliza mama yule huku akiangalia juu ya anga na kuhofia ujio wa mvua.



“Unajua fika mwanao ninavyoteseka kwa kulima, lakini hata mwaka mmoja sijafanikiwa kupata mafanikio” alieleza kijana yule mambo yanayomsumbua.



“Hayo mambo ndiyo yanakufanya ujikatie tamaa mapema?.”



“Sio mapema unavyodhani...ebu wewe fikiria miaka mingapi imepita lakini mimi nipo vile vile.”



“Miaka mitano si mingi, nakusihi zidi kupambana tu ipo siku utafanikiwa.”



“Lini sasa?...kama kupambana nimepambana sana hadi nimechoka.”



“Eeh...nyanyuka tukazungumzie nyumbani hapa tusije nyeshewa na mvua. Unaona hali ya hewa ilivyobadilika mvua itanyesha sasa hivi” aliongea mama yule huku akimvuta mwanae mkono wa kuume upesi anyanyuke waondoke.



Kabla kuondoka wakaficha majembe kisha wakaongoza njia kuelekea nyumbani na kufika jioni. Kijana yule akaenda chumbani kwake akamwacha mama yake akiandaa chakula cha usiku jikoni.



**********

Kijana huyu alibahatika kuishi na mama yake pekee kutokana na baba yake kufariki akiwa mdogo katika mazingira ya kutatanisha. Hakubahatika kusoma alikuwa ni mtoto wa kulima bustani na kufanya kazi za nyumbani.

Zao kubwa alilopendelea kulima hasahasa ni nyanya. Alilima Nyanya kwa uchungu huku akijipa matumaini ya kuwa ipo siku atafanikiwa. Kijana huyo na mama yake waliishi katika nyumba ya urithi iliyoachwa na marehemu baba yake aliyejulikana kwa majina ya Iddy Ramadhan Mbawala. Walisongesha maisha katika nyumba iliyojengwa kwa matofali ya kuchoma. Njaa upande wao waliizoea huku kejeli za majirani zikishamiri juu yao kwa kuwatupia vijembe vya chinichini wakisema. Wanajifanya maskini tajiri, wacha wafe na njaa.

Lakini kijana yule na mama yake waliziba masikio hawakutaka kabisa kusikiliza maneno yanayosemwa na majirani. Kipindi cha mavuno kijiji cha Maharaka huwa kinakuwa na ahueni kwa wanakijiji kwa sababu ya mavuno kupatikana kwa wingi msimu huo. Mama yake kijana yule anayefahamika kwa jina la Binti Mngane mama wa mtoto mmoja anayetambulika kwa jina la Sharifu. Kijana aliyejikatia tamaa mapema, msimu wa mavuno upande wao wanafurahia kuwa unakuwa ahueni. Binti Mngane ameishi na mwanae muda mrefu lakini hakuweza kumweleza siri iliyo ndani ya moyo aliyoficha kwa kila mtu asitambue, atakaetambua kifo kina mhusu. Usiku huo Binti Mngane aliivisha chakula hatimaye akamuita mwanae waje kula achana na kula tu bali kulikuwa na jambo analohitaji amwambie mwanae.



“Sharifuuu” aliita Binti Mngane kwa kupaza sauti.



“Naam” aliitika Sharifu kutoka kwenye chumba chake chenye mwanga hafifu wa Koroboi.



“Unafanya, nini?” aliuliza Binti Mngane huku akitenga chakula ukumbini.



“Nakunja nguo, siunajua ndani humu kulivyo na panya” alijibu Sharifu huku akitokwa na jasho usoni na pia machozi yakimtoka machoni kutokana na moshi wa Koroboi.



“Achia...ugali tayari.”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“Sawa, nakuja anzaga kula.”



Sharifu kukunja nguo ilimchukua dakika akamaliza akatoka chumbani akasogea hadi kilipo chakula. Alishangaa kumkuta mama yake akimsubiri wakati alimwambia aanze kula





“Si nilikuambia uanze kula, mbona unanisubiri tena ?,” Sharifu aliuliza huku akishangaa kumuona mama yake mikono jinsi ilivyokauka kutokana na kunawa muda mrefu.



“Mwanangu, sijazoea kula peke yangu,” Binti Mngane alijibu huku akiachilia tabasamu.



“Sawa ... lakini mboga ya leo, sijapenda,” Sharifu alisema mara tu baada ya kuona na kuila mboga ile.



“Nitafanyaje? ... muda ulikwenda nikaona mboga nyepesi ni hii.”



“Mboga nyepesi ni mrenda peke yake ... kuna mchicha, matembele kwa nini hujapika hizo ?.”



“Hizo zina utaratibu wake nazo kama vile kuchambua na kuosha lazima zingenichelewesha ... tule, tena huu leo ??nimeupika vizuri,” Binti Mngane alijibu huku akionyesha tabasamu kufurahia mrenda aliokaangiza.



Sharifu hakupendezwa nao mrenda, akala kwa kujilazimisha kwa kuwa palikuwa hakuna mboga nyingine, hivyo hakuna budi kula. Akala kwaajili ya kutuliza njaa tu, walipomaliza kula akatoa vyombo na kuvipeleka mahali koridoni.



“Ukishaweka vyombo njoo, kuna mazungumzo kidogo” alisema Binti Mngane kwa kumhabarisha mwanae.



“Kiukweli, umetahabika sana” alizungumza Binti Mngane mara baada ya mwanae kurudi ukumbini mara baada ya kuweka vyombo.



“Sanaaa ... mpaka sasa nishachoshwa na hayo matahabiko.”



“Kama ulishachoshwa mimi leo kuna kitu nahitaji nikuambie ... upo tayari ?.”



“Kitu gani hicho mama ?.”



“Si unahitaji mafanikio, sasa presha yako ya nini ?.”



“Lazima niwe na presha, kwa kuwa kitu chenyewe sikijui unachotaka kuniambia.”



“Ondoa shaka ... nitakuambia.”



“Sawa nakusikiliza, niambie nipate kujua hicho kitu.”



“Lakini si unania kweli ya kufanikiwa ?.”



“Ndiyo ... nahitaji kufanikiwa leo hata kesho.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Kwasasa ushakua mkubwa na hali ya kijijini ushaiona ... vijana wengi hapa kijijini wamepata mafanikio kwa haraka wewe hushangai hilo.”



“Naliona hilo na nashangaa ... ila bado sijakuelewa unamaanisha nini?” aliuliza Sharifu ili apate kuelewa mama yake anataka kuzungumza nini.



“Ninachomaanisha, nitakuambia,” Binti Mngane alimeza mate kidogo kisha akauliza.



“Ila una moyo ?.”



“Moyo ninao ... niambie.”



“Kama una moyo vizuri, sasa nisikilize kwa makini.”



“Eeeeh !.”



“Vijana wenzako hapa kijijini, wanafanikiwa kwa kitu hiki kimoja tu ambacho ni ...,” Binti Mngane kabla ya kuendelea kuongea akapaliwa akakohoa mfululizo hatimaye akaendelea kuongea.



“Ambacho ni uchawi, sasa wewe upo tayari kujiunga na uchawi ?.”



Sharifu alichoambiwa na mama yake kilimshangaza sana, hakuamini akafikiri kuwa labda ni mzaha hivyo akabaki akicheka sana.



“Unacheka nini ?,” Binti Mngane aliuliza huku akikunja ndita kwa hasira.



“Nimefurahi tu.”



“Kilichokufurahisha ni nini eti ?.”



“Ujue sijakuelewa ... hivi unatania au unaniambia kweli ?.”



“Kuna muda wa matani na usio wa matani, haya ninayokuambia hapa ni kweli hakuna utani wowote.”



“Kabisa!?.”



“Eeenh !.”



“Ujue mama unanichanganya kiukweli.”



“Kivipi ?.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Mimi na uchawi wapi na wapi ?.”



“Kwa hiyo unataka kusema unataka kuendelea kuteseka ... si ndiyo ?.”



“Sihitaji.”



“Kumbe ?.”



“Sio mzoefu pia naogopa mno kuwa mchawi, kwa sababu ni aibu kubwa katika jamii kujihusisha na masuala kama hayo.”



“Sijaona hapo kinachokuogopesha ... unajitakia kuteseka kumbe mwenyewe.”



“Lakini mama mbona naona kama unaning'ang'aniza unaona huko kuzuri. MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI ...... sitaki kabisa kama mafanikio yenyewe yanapatikana hivyo, bora nife nikiwa maskini tu. ”



“Nani alikuambia huko ni kubaya ?, kuwa mjinga ... utabaki kuwasindikiza vijana wenzako hadi mwisho wa dunia,” Binti Mngane alisema kwa hasira huku akinyanyuka kwenye mkeka kama ugomvi na mashavu kutunisha kama Panya buku akaingia chumbani.



Sharifu naye akaingia chumbani kwake kwa kuona mama yake kaondoka kakasirika na kumwacha peke yake ukumbini. Alipofika kitandani usingizi haukuja kabisa alikuwa bado anafikiria maneno aliyoambiwa na mama yake. Akawaza na kuwazua mara mbili mbili ndipo akagundua anayosema mama yake yana ukweli mtupu baada ya kukumbuka baadhi ya vijana wenzake waliofanikiwa pale kijijini. Sharifu kadri anavyozidi kukumbuka wivu unamshika anatamani leo kesho aweze kufanikiwa.



“Bora, nikubali tu,” Sharifu alijiwazia moyoni huku akipinduka pinduka kitandani kwa kukosa hata lepe la usingizi.



“Lakini hata nikikubali ... uchawi huo nitaupata wapi?” alijiuliza Sharifu kwa kutokujua mama yake kama yupo kwenye chama cha uchawi.



“Lakini potelea pote ............ Mama nahisi atakuwa anapajua. Ngoja nitamuuliza, ikiwezekana nijiunge. ”



Unaambiwa hakuna mkate mgumu mbele ya chai na hakuna Bausa yeyote mbele ya usingizi. Sharifu usingizi ukamnyong'onyesha akawa mpole hatimaye akapitiwa na usingizi. Kesho yake akaamka mapema akatoka nje alipofika nje akakutana na mama yake ukumbini akamsalimu lakini cha ajabu mama yake hakujibu ile salamu.



“Ina maana mama, yaani kitu kidogo tu umeninunia hivyo ?,” Sharifu akauliza.



“Umenishangaza sana yaani nafanya kwa faida yako, lakini wewe unaniona kama hayawani .... Sasa endelea kutahabika maana ndiyo hali uliyoichagua” aliongea Binti Mngane kwa sauti iliyojaa ukali.





“Mimi na wewe hatuna ugomvi ... vitu hivi ni vya kueleweshana tu.”



“Nikueleweshe mara ngapi ... wewe kama umeamua kukataa mpango wako.”



“Jana mimi sikufikiri vizuri ... ila kwasasa nishafikiria na nishaona umuhimu wa kujiunga.”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Sijakuelewa bado ... unataka kusema nini?” aliuliza Binti Mngane kwa kujifanya aelewi anachotaka kusema mwanae.



“Nimekubali, kuingia katika uchawi.”



“Vizuri sana ... sasa ushakua mkubwa yakupasa uwe mjasiri sio unakuwa mbabaishaji.”



“Lakini mama, huo uchawi nitaupata wapi ?,” Sharifu akauliza.



“Kwa kuupata usijali, niachie mimi nitashughulikia kila kitu.”



“Bado sijakuelewa hapo, unasema nikuachie wewe ... je wewe utaupataje ?.”



“Ondoa shaka ... leo usiku jiandae nitakuja kukuchukua.”



“Tunaenda, wapi ?.”



“Unapopatikana, uchawi.”



“Wewe, unapajua ulipo ?.”



“Nimekuambia ondoa shaka ... wewe si nia yako kupata uchawi sasa tatizo lako ni nini ?.”



“Sawa,” Sharifu alikubali kwa kuona jinsi na yeye lengo lake la kupata mafanikio ataweza kulifikia.



Sharifu baada ya mazungumzo na mama yake akatoka nje kufagia banda la kuku. Akafagia na hatimaye akarudi ndani kuandaa chai kisha wakanywa kwa pamoja na mama yake. Walipomaliza kunywa chai Sharifu akaaga anakwenda shamba akashika njia ya kuelekea shamba. Alipofika shamba akachukua jembe akaanza kulima akalipiga jembe mpaka kijua cha saa kumi kilipoanza kuzama ndipo naye akarejea nyumbani. Aliporudi nyumbani akamkuta mama yake anaunga mbaazi akatoa salamu kisha akaingia chumbani kujibadili akaoge, akatoka amevaa taulo na mkononi kashika ndoo ya uani. Sharifu akateka maji na kwenda kuoga wakati alipomaliza kuoga akaingia chumbani kujibadili mavazi, alijibadili kisha akaenda kuketi ukumbini kwenye mkeka akisubiri chakula cha usiku ili ale apumzike. Masaa matatu yalipita chakula kikaivishwa na tayari kwa kuliwa. Walipomaliza kula Sharifu akatoa vyombo akaingia ndani kujipumzisha. Binti Mngane akaosha vyombo na kuingia chumbani naye kulala, yapata saa nane ya usiku Binti Mngane kama alivyoahidi akanyanyuka kitandani papo hapo akabadilika sura ikawa na unga mweupe. Kwa upande wa mavazi akabadilika akawa amejifunga kiremba cheusi kichwani, kifuani na kiunoni kwaajili ya kumstili maeneo nyeti. Alipohakikisha yupo tayari akatoka chumbani akaelekea kwenye chumba cha mwanae. Alipofika akamkuta mwanae bado kalala, akachukua roho ya mwanae na mwili akabakisha pale pale kitandani. Baadaye akatokea kimiujiza kwenye mbuyu mkubwa uliokuwa na aina mbalimbali ya vitisho. Binti Mngane akashika roho ya mwanae kwa ngangari mara baada ya kuliangalia lile eneo kwa undani. Hazikupita dakika nyingi akaona baadhi ya wachawi wenzake wakiwa kwenye nyuso za kutisha, akafumbua macho ya mwanae apate kuona wanachama wenzake. Sharifu akafumbua macho aliogopa sana akapepesa macho yake kwa hofu kubwa kwa kuangalia na kuvuta picha ya kila mahali kama ataweza kupafahamu pale. Kumbukumbu zikapotea, akazidi kupitisha macho kwa kila mchawi labda ataweza kumjua yoyote lakini wapi. Hakuweza kuwatambua wale wachawi zaidi ya mama yake tu, wakati akiwa anashangaa shangaa hovyo kwa hofu ikasikika sauti ya mama yake ikisema;



“Usiogope, hapa ndipo pahala sahihi kwako.”



“Naona Binti Mngane, leo umetuletea mwanao ... sijakuelewa umemleta mwanao ili iweje atolewe kafara au laah ?,” Mzee Damanda ambaye ni mkuu wa wachawi kama inavyojulikana kwa shirika la kichawi akaingilia mazungumzo ya Binti Mnguli nawan



“Hapana, sijaja kumtoa kafara ila nimekuja ili ajiunge nasi,” Binti Mngane akajibu.



“Una uhakika mwanao ataweza kuungana nasi ?,” Mzee Damanda aliuliza kwa kutoamini kama Sharifu ataweza uchawi.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Kuweza naamini anaweza, naomba tumsaidie ili aweze kuwa mwanachama imara,” Binti Mngane aliomba kwa unyenyekevu ili mtoto wake aweze kupata kibali cha kukubaliwa.



“Mimi kama Mzee Damanda nimekuelewa .... Wanachama wenzangu nanyi mnasemaje ?,” Mzee Damanda alisema akageuka kwa wanachama wenzake na akawauliza.



“Sisi kama wanachama wenzake tunapenda kusikia hivyo, maana vijana ndiyo wanahitajika haswaa kwenye chama chetu,” Mama Kitenya ambaye ni miongoni wa mmoja wa wachawi akasema.



Mzee Damanda alipoona wachawi wamekubaliana kujiunga kwa Sharifu katika chama chao. Akamkabidhi mavazi na zana za kichawi Sharifu ukiwemo usongo mweusi, kaniki nyeusi, pembe la ng'ombe na usinga kisha akachanjwa chale maeneo husika kama kwenye paji la uso kifuani na mgongoni.



“Ushakuwa mwenzetu ni vyema ukazijua sheria zetu ... sheria zetu ni hizi yakupasa uzishike hutakiwi kusaliti chama, kutoa siri za chama na kumjaribu mwanachama mwenzako pia yakupasa uhudhurie kila siku ya kilinge,” Mzee Awaka kacha lake.



Mzee Damanda baada ya kumwapisha Sharifu kuwa mwanachama rasmi akahitimisha kikao. Sharifu tokea siku hiyo akawa mchawi aliyekubuu, siku inayofuata usiku wa saa sita Sharifu akaelekea shambani kufukia kichwa cha paka kwaajili ya kukinga shamba kama alivyoagizwa. Msomaji tatizo hili watu linawakuta katika maisha unakuta unafanya kazi kwa bidii lakini unaona mambo hayaendi. Mara nyingi huwa kuna watu wasiopenda maendeleo ya wengine hao hufanya juu chini ili waweke vipingamizi watu wasifanikiwe. Upande wa Sharifu kinga ikamsaidia kiasi zilipita siku kadhaa akatokea mzee mmoja akaenda kwenye shamba la Sharifu kutenda uchawi hakujua kama Sharifu ameweka kinga.



“Huyu mtoto, kumbe ni mshenzi ... mbona sioni shamba lake,” Mzee yule alijiongelea moyoni huku akitafuta njia ya kuondoka mara baada ya kushindwa kufanya jambo lililomleta.



Alipobahatika kuona njia akapotea kimiujiza mashambani. Asubuhi Sharifu akaagizwa na mama yake sukari akapita njia iliyokaribu na nyumba ya mzee yule aliyeshindwa kutenda uchawi shamba lake. Mzee yule alimkuta nje ya nyumba yake akipunga upepo Sharifu hakusita kutoa salamu.



“Shikamoo” alitoa salamu Sharifu kisha akasimama njiani kusubiri ajibiwe salamu.



“Ingekuwa mali, ungeenda kumpa baba yako,” Mzee yule aliongea akanyamaza kidogo kuongea akafikicha macho yaliyokuwa yakifukuta kwa kuwasha kisha akaendelea kuzungumza.



“Yaani nusu uniue, ebu ... nitokee mbele yangu” alifoka Mzee yule kwa hasira.



Sharifu hakuelewa alichozungumza mzee yule akaamua kuondoka huku akitabasamu. Alipofika dukani akanunua sukari akarudi nyumbani na kumkuta mama yake yupo jikoni akingojea sukari. Binti Mngane akakabidhiwa kifuko cha sukari na mwanae. Alipokea akaweka kiasi kwenye uji na nyingine akamtuma mwanae aweke kwenye bobo. Sharifu akaweka sukari ndani ya bobo kisha akaketi kwenye mlango wa jikoni akisubiri kifungua kinywa ndipo hapo uvumilivu ukamshinda japo hakutaka kusema ikabidi tu amweleze mama yake.



“Mzee Kaoneka ananishangaza.”



“Anakushangaza na nini ?,” Binti Mngane akauliza.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Wakati naenda dukani nilimkuta yupo nje ya nyumba yake amekaa akipunga upepo.”



“Kakufanyaje?” aliuliza Binti Mngane kwa kutaka kujua kwa kina.



“Si nilitoa salamu, alichonijibu sikutegemea kabisa.”



“Kajibuje ?,” Binti Mngane akauliza.



“Kaniambia salamu yangu ingekuwa mali, ningeenda kumpa baba yangu.”



“Kwanini, kasema hivyo ?.”



“Mimi mwenyewe, sijamwelewa kwa nini kanijibu vile.”



“Kuna kitu kibaya umemfanyia au uliwahi kumfanyia ?,” Binti Mngane alizidi kuuliza.



“Hapana ... sijawahi hata siku moja kumjibu vibaya,” Sharifu alijibu akanyamaza kidogo kwa kuona mama yake yupo bize na kukoroga uji.



“Mbona umenyamaza? ... endelea nakusikiliza,” Binti Mngane akauliza na kusema.



“Mzee yule hakuishia hapo, aliniambia kuwa jana nusu nimuue na akanifurumusha nitoke,” Sharifu aliendelea kuongea mara baada ya kupewa ruhusa na mama yake.



“Mzee Kaoneka, itakuwa ni adui yako namba moja haiwezekani akuambie maneno kama hayo angali hujamfanya chochote” alisema Binti Mngane kwa msisitizo.



Sharifu akaumia sana moyoni kusikia vile na akajiwekea nadhiri ya kumuonyesha Mzee Kaoneka kuwa naye anazo nguvu za giza. Nyakati za mchana akatimiza dhamira yake akaenda kimiujiza kwa Mzee Kaoneka akamkuta Mzee Kaoneka ukumbini akisoma gazeti lake la MWANANCHI.



“Mzee ulijua siku hizi mimi wakujaribiwa?” aliuliza Sharifu kwa hasira.



“Hapana mjukuu wangu ... kwani kuna nini ?,” Mzee Kaoneka kwa kujifanya kama hajui chochote akauliza.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Sharifu hakumsikiliza wala hakumjibu Mzee Kaoneka akaona kama anacheleweshwa muda. Akajiwekea asilimia mia kuwa Mzee Kaoneka ndiye adui yake namba moja hivyo hakumuonea huruma hata kidogo. Roho mbaya ikamwingia akamsotea kichwani Mzee Kaoneka kwa makalio akainua mikono yake juu kikatokea kisu na kuku mweusi mikononi mwake. Akamchinja Kuku yule na Kuku papo hapo alivyomalizwa kuchinjwa Mzee Kaoneka akakata roho na kuaga dunia. Sharifu mara baada ya kumaliza tukio la mauaji akapotea ghafla kimiujiza. ”







ITAENDELEA

KARIBU KUZIMU - 5

  





    Simulizi : Karibu Kuzimu

    Sehemu Ya Tano (5)





    Jini Suleiman akiwa amelala chumbani, huku nami nikiwa sebuleni nikiangalia runinga bila uwoga. Ghafla nikasikia mlango wa sebuleni ukigongwa, nikanyanyuka katika sofa kwa hofu nikaenda kufungua mlango. Ile kufungua nikakuta mgongaji hayupo, nikajipa moyo labda wenge langu sikusikia vizuri. Nikafunga mlango nikarudi tena kutazama runinga, kama nusu saa nikiwa makini na kutazama runinga mara nikasikia tena mlango ukigongwa. Sikusita kwenda kufungua, nikaelekea kufungua mlango lakini nilipofungua ikawa vile http://deusdeditmahunda.blogspot.com/vile kama awali. Sikumkuta mgongaji basi nikajisemea labda atakuwa ni jini Suleiman anafanya mauza uza pengine kwa kuniondoa upweke, hivyo nikafunga mlango huku kwa mbali nikilionyesha tabasamu langu. Nikaelekea chumbani nikamfuata Suleiman ili nimueleze huo mchezo alioanzisha sijapenda. Lakini kabla sijafika chumbani ile napiga hatua mbili tatu za kuelekea chumbani, nyuma yangu nikasikia kama mtu akitembea akinifuata. Haraka nikageuka nikashtuka, mapigo ya moyo yakaenda kasi. Maana nilichokiona niliogopa, sikuona mtu bali nikaona nyayo za binadamu zilizo na damu ambazo zimeanzia niliposimama mpaka sebuleni. Pima macho yakanitoka, nguvu zikaniishia nikanyong'onyea hata tabasamu likapotea. Mchaka mchaka nikajongea sebuleni, nawasili sebuleni sijaona chochote zaidi ya kuona zile nyayo zilizo na damu. Nikafikiria kuwa ni nani aliyeingia ndani huku ameumia, wakati milango yote nimefunga hata sikuambulia kudadavua kitu. Nikapiga moyo konde nikajirubuni kuwa labda jini Suleiman bado anaendeleza mauza uza ili niondokane na upweke, basi nikahamua kukimbilia chumbani nikaongee na Suleiman kuwa aache kunifanyia mauza uza, hata hivyo kabla sijafika tena chumbani. Nyuma nikasikia kicheko kikitokea sebuleni, kicheko kile kikanifanya niingiwe na uwoga. Punde mwili wangu ukafa ganzi, pole pole nikajongea sebuleni kwa ajili ya kuangalia ni nani anayecheka kicheko kile cha kujirudia mfano wa mwangwi. Kufika sikuona mtu wala sikusikia kile kicheko, nikashangazwa nikabaki nimeganda tu nikiduwaa na uwoga. Nikiwa nimeduwaa huku nimesimama tu mara nikashtuka niliposikia mkwenzi umepigwa, nikatumbua macho kule niliposikia mkwenzi. Ila sijaona mtu, upesi nikageuka ili nimfuate Suleiman. Lakini nikaonana ana kwa ana na jini Sulesh baada ya kugeuka.





    “Umefuata nini?,” Nikauliza japo kwa uwoga.



    “Unaniuliza nimefuata nini. Nimekufuata wewe,” Jini Sulesh alijibu huku akipalaza nywele zake taratibu kana kwamba hana uwoga.



    “Sitaki.”



    “Hutaki?. Utataka tu, ukumbuki kiasi nilichotoa. Halafu leo hii kirahisi ukatae, nani kasema,” Jini Sulesh aliongea huku akisogea niliposimama.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ah! nikakosa ujasiri. Uwoga ukatawala nikapiga ukunga, ule ukunga ukamuamsha Suleiman haraka akaamka akapotea chumbani akatokea tulipo. Akamkumta mdogo wake akisogea anibusu kilazima, Suleiman akapotea punde akatokea jirani zaidi. Akamsukuma Sulesh, Sulesh akadondokea sofani chali huku akicheka. Kicheko kile Suleiman akaigiza hajasiki, akageuka nilipo mwisho akaamuru niingie chumbani. Nikaingia.



    “Ha ha ha, te te te. Ndugu yaani ka umeomba lifti unataka kupiga na honi, ushasahau kama mke wa mtu ni sumu?,” Jini Sulesh akaongea. Maongezi yale japo nilikuwa chumbani lakini niliyasikia vema kabisa. Nikamsikia Sulesh akiongea kwa ukali na kaka yake.



    “Sulesh, mwanamke inaonyesha hakupendi. Kama hakupendi huna budi kumuachia kaka yako,” Jini Suleiman nae akaongea. Nilimsikia Suleiman akimjibu mdogo wake kwa upole sana.



    Ukimya! ukatawala. Kukawa zi zi ziiii, sikusikia maongezi tena. Dakika kadhaa ndipo nikaja kusikia ukunga wa maumivu uliopigwa na Suleiman. Hofu ikajaa, macho yakatoka pima. Nisijue kilichotokea huko sebuleni, nikiwa kwenye hali ile mara nikasikia vishindo vya miguu vikitembea kuja katika chumba changu. Akili ikaruka, upesi nikasogelea mlango nikafunga na funguo. Ndipo mtu yule aliposikia nafunga mlango, nikamsikia akiangua kicheko. Kicheko kile nilipokisikiliza nikatambua ni cha nani, ni kilikuwa cha Sulesh. Kicheko cha Sulesh kikazidi kunijaza hofu mara nikajikuta natetema tu, nilijaa na wasi wasi mpaka nikajihisi uso umeenea jasho. Kweli chumba nikakiona cha moto japo kulikuwa na ubaridi wa feni “Pangaboi”, ghafla kicheko sikukisikia tena nikajua Sulesh kashaondoka. Nikatoka chumbani taratibu huku nikijaribu kung'aza macho kila pahala labda nitaona chochote, lakini sikubahatika kuona chochote wakati ule. Nikaelekea sebuleni, ila nilipofika huko nikastaajabu na punde nikasikia mapigo ya moyo yakidunda. Sikuamini nilichokiona, nikaona Suleiman kalala sakafuni huku pale alipolala kukiwa kumetapakaa damu. Nikasogea jirani nichunguze, nilipochunguza nikagundua Suleiman tayari alikuwa kashafariki. Utumbo wote wa Suleiman nikaukuta upo nje mfano wa mzoga uliwapo na Kunguru, machozi yakanilenga. Mtoto wa kike kilio kikanitoka sio kama nalia sababu, Suleiman kafariki kifo butu. La hasha!, ninalia sababu nimejuana na nimependana nae Suleiman kwa muda mfupi sana. Naumia zaidi, nikikumbuka misaada aliyonisaidia lukuki.



    “Sasa ujanja upo wapi binti. Msaada ndio huo chini, ushakufa. Uamshe ukusaidia katika mazonge,” Jini Sulesh akasikika akiongea kwa kebehi. Aliongea huku akitomasa maungo yangu, kwa hasira nikamputa mkono asiendelee kunishika. Lakini Sulesh alionekana jeuri akaendelea kunishika, safari hii aliponishika kwa jazba nikamng'ata mkono. Cha ajabu badala ya kusikia maumivu akawa anacheka huku akifuata mwili wa nduguye, akaushika mwili hatimaye papo hapo akapotea na nduguye eneo lile.



    **********

    Usiku ule Sulesh akawasili majini na nduguye katika kumbi ya kifalme, akamlaza marehemu huku akiigiza kulia kana kwamba hausiki na kifo cha Suleiman. Akawaamsha majini wote, dakika tu wakakusanyika katika kumbi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Nini kimekukuta.... Nini kilichokuondoa duniani?,” Jini Sulesh aliigiza kulia zaidi, ili ajistili makucha katika sirika mara baada ya kuona majini wote wamewasili.



    “Sulesh. Suleiman umemkuta wapi?, na kapatwa na nini?,” Mzee Kadhir aliuliza mara baada ya kuona aelewi.



    “Alikuwa ufukweni, nikamkuta kakandamizwa na gogo la mbuyu,” Jini Sulesh alieleza huku bado akiwa anaigiza kulia.



    “Gogo la mbuyu!!, ndiyo limechukua uhai wake?,” Binti Surya aliuliza nae huku akihamaki mara baada ya kugundua mwanae mkubwa kaaga dunia.



    “Naam, nimeumia sana maana katika uzawa wetu. Tumezaliwa wawili tu ka dawa” alisema Sulesh huku akifuta machozi ya kuigiza.



    Baada ya majini wote kujua Suleiman kafariki mara sura zao zikabadilika zikawa na majonzi. Hakuna budi kufanya maziko, wakamzika Suleiman kwa hekima na heshima hatimaye majini wote wakatawanyika wakarudi majini kuendelea na majukumu uchwala.



    **********

    Usiku wa saa saba nikiwa chumbani nimelala kitandani, mara ghafla nje nikasikia upepo mkali ukipuliza. Na kupenya kwenye madirisha yangu ya chumbani, ukaleta baridi kali na kufanya nishindwe kujizuia. Nikajifunika gubi gubi ili baridi lisinipulize, lakini nikashangaa kuona upepo ule ukiwa bado unapenya kwenye maungo yangu. Ni wa ajabu, ulikuwa una nguvu balaa mpaka ukaweza kunifunua shuka kwa ghasia. Usingizi ukakata nikakaa kitako kitandani nikitafakari upepo ule wa namna gani, maana hata upepo wa kisuli suli sio vile. Nikashindwa kujua, nikabaki nikijikunyata ka kitoto cha Paka. Duh, upepo ulikuwa ni tishio nikakosa lepe la usingizi. Nikabaki nikikodoa macho tu pale kitandani, lisaa moja kupita upepo ghafla ukakata. Kukawa shwari ka awali, nikajaribu kujiegesha kitandani pengine nitapata usingizi tena. Kabla sijapata usingizi kupitia dirishani nikaona dalili ya mvua ikitaka kunyesha, niliona mweku mweku. Nikasikia mngurumo wa radi na punde nikaona mvua sasa ya rasha rasha ikinyesha, moyoni nafsi ikafurahi kwa maana mvua ilikuja wakati muafaka. Ilinibembeleza taratibu nikalala pono, muda mwingiiine kabisa nikiwa kwenye usingizi nikasikia nikiitwa kwa sauti ya juu. Mpaka kero ikanilazimu nijivute niamke, nikaamka kumuangalia aliyeniita lakini sikumuona bali niliona maajabu yakiendelea. Nikaona mlango upo wazi angali nilifunga, pia nikaona taa zote zikiwaka na kuzima ka kwenye kumbi ya starehe “Club”. Papo hapo hofu ikanitanda mwilini upesi nikajikuta nikibwata.





    “Wewe ni nani?, unayefanya hivi ni nani?...au ni Sulesh?,” Nilibwata huku nikiweweseka kwa uwoga.



    Hata maswali hayakupatiwa ufumbuzi bali yakachochea kicheko cha mwangwi kilipotoka sikujua wakati ule, hofu ikaongezeka maradufu. Ujasiri sikuwa nao hata thumni, ni uwoga tu ulionitawala. Nikatulia nikitetemeka mfano kitoto cha Paka kisikiapo baridi, mtetemo wa mwili ukachukua nafasi. Nilitetema mpaka nijajihisi kuishiwa nguvu, nikanyongea lakini ghafla kicheko kile kikafika ukomo kukawa tuli mfano umeme ukatikapo. Ujasiri ukarudi nikainuka kitandani, nikasimama ili nijaribu kupepesa macho chumbani nione ka kicheko kile kilitoka wapi. Hamadi! katikati ya mlango wa chumbani akatokea Sulesh baada ya kung'aza macho kwa muda, Uwoga ukarudi tena nilipoonana na Sulesh kwa mshtukizo. Nikabaki mpole na mara papo hapo nikazilai, fahamu nikaja kurudisha usiku wa saa kumi nikajikuta nipo kitandani nikaangaza macho kila kona ya chumba. Mtumee!! kuangalia kando nikamkuta. Jini Sulesh akiwa kando yangu.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Unataka nini?,” Nikapayuka.



    “Mapenzi. Nakupenda Prisca,” Jini Sulesh alijibu huku akikaza macho kwangu. Akionyesha kunitisha ili nije kusema neno lenye herufi nne kwa usahili.



    “Sasa sikupendi, pia sikuhitaji.... Naomba ondoka,” Nikaongea kwa sauti ya ukali, kisha nikateremka kitandani nikaelekea sebuleni kwa ajili ya kumkwepa Sulesh.



    Lakini kabla sijafika katika mlango wa chumbani, ile nanyanyua mguu tu nipige hatua ya kutoka chumbani nikaganda. Sikuweza kwenda mbele wala kurudi nyuma, kila nikijilazimisha nitembee wapi. Fadhaa ikanishika muda ule ikashikika, nikageuka nyuma kwa jazba nimuone Sulesh ka yupo kitandani au lah. Cha ajabu hakuwepo, nikageuka tena mbele nijaribu kwenda. Haraka nikashtuka baada tu ya kumuona Sulesh mbele yangu huku akitabasamu, mwili wote punde ukafa ganzi nikatamani nikimbie lakini sikuweza sababu ya kugandishwa bila kutaraji. Sikupanga yatokee ila yote ni njama za Sulesh. Niliendelea kusimama mfano sanamu, ndani ya nusu saa Sulesh nikaona akinibusu mdomoni na ghafla kumbukumbu zikapotea. Punde akanikumbatia tukapotea chumbani, tukaja kutokea chini ya bahari huku nikitembezwa kuelekea nisipopajua. Tuliendelea na matembezi mara ghafla tukapotea tena tukaja kutokea kwenye kumbi kubwa “Hall” naona ni la kifalme maana lilipendezeshwa na vito ghali, nilipofika kwenye kumbi ile nikajihisi nipo katika sayari nyingine kwa maana niliona. Viumbe ajabu ambavyo sijawahi kuviona maishani mwangu, niliona majini mbalimbali. Niliona majini Laadu, Shufaa na wengine wengi. Sababu kumbukumbu sikuwa nazo hivyo sikushangaa na wala sikuogopa sana, nikajiona jasiri tosha.



    “Baba, huyu ndiye atakayekuwa mke mtarajiwa. Anaitwa Prisca,” Jini Sulesh akatambulisha. Nami nikasikia akinitambulisha kwa mzee wa makamo, ambaye ndiye naona ni baba yake.



    “Vizuri. Mwanangu nimefurahi sana, leo kuonana na mkamwana,” Mzee Kadhir aliongea huku kweli akionyesha kufurahia ujio wangu.



    “Sasa leo nimekuja nae, ili nipate baraka,” Jini Sulesh akaongea.



    “Ni vema...lakini siunajua tumetoka kwenye pigo. Bora tuhailishe, hizo baraka tukupatie siku nyengine,” Mzee Kadhir akashauri.



    “Lakini. Baba Sulesh, kwanini tusimpatie mtoto baraka. Kama pigo tayari tushalipata hakuna kitakachobadilika, naona tumpe tu mtoto baraka, tena siunajua sisi muda wowote tutaonja umauti. Bila kumtengeneza mrithi mapema, tutakosea,” Binti Surya akaeleza.



    Mzee Kadhir akatafakari kwa muda, akaona ni ya kweli asemayo mkewe. Basi wakampatia mtoto wao baraka, Sulesh alipopatiwa baraka na wazazi akaaga kuwa anaondoka majini kwa kipindi kifupi. Ili aende nami ulimwenguni akanifunze hulka, hakukatazwa akaruhusiwa mara akapotea nami pale majini. Tukatokea sebuleni kwenye mjengo ule ule wa Mabibo hostel. Tukafikia kukaa sofani tuli huku tukitazamana, halikupita lisaa hatimaye nikamuona Sulesh kanyanyuka kwenye sofa akanifuata nilipoketi. Kisha akanibusu mdomoni na ghafla nikarudisha kumbukumbu upesi nikamkwepa nikataka kwenda chumbani, lakini akanizuia akanikalisha tena sofani kilazima. Nikachukia sana matendo mabovu ya Sulesh, yaani sikumpenda kabisa sema nitafanyaje. Wakati maji yashanifika shingoni, inabidi nikubali hali kishingo upande. Nikatulia tu nimsikilize.



    “Prisca, samahani sana. Najua kila nifanyalo na kuuzi, ila nami nitafanyaje napigania penzi langu. Nisamehe mama...nakupenda,” Jini Sulesh akajirudi.



    “Sitaki. Sikupendi, mbona unisikii...siwezi kuwa nawe. Kama imekuchoma niue tu kuliko kunitesa,” Nikapayuka.



    “Prisca....,” Jini Sulesh kabla hajamaliza kuongea. Nikamkatisha.



    “Ni nini?...au nirudie kwa herufi kubwa kuwaSIKUPENDI,” Nikagoma.



    “Ho ho ho. Shiiiiit, upuuzi huu,” Jini Sulesh aliongea kwa hasira. Hakupendezwa kabisa na matamshi niliyonena.



    Ghafla nikaona kabadilika akavimba uso mpaka uso ukawa mwekundu, dakika tu akanivaa kwa jazba na mara tukapotea sebuleni tukatokea chumbani. Ghafla akanisukuma kitandani akafunga mlango akanisogelea huku kafura.



    “Siutaki nikupende. Sasa kuanzia leo makazi yako yatakuwa humu, chochote kitakacho kutokea ni juu yako,” Jini Sulesh akaongea. Na mara akapotea akaniacha chumbani nikiwa gizani.





    Nikaishi kwenye chumba kwa tabu sana, mwanzo chumba kile kilikuwa wala hakitishi lakini hawamu hii. Chumba kilikuwa cha kutisha sana, kulikuwa na kila aina ya vitisho vya ajabu. Ikawa mara niamke nisikie sauti za kutisha, mara niamke nikute chumba kimetapakaa damu, mara niamke nikute kinyesi kitandani, mara niamke nikutane na Paka kitandani, mara siku nyengine nisikie watu wakiongea lakini nisiwaone. Basi kila siku nilikuwa nakutana na mambo ya ajabu katika chumba kile, japo nilikutana na magumu katika chumba kile lakini sikuwahi kubadili msimamo wangu. Nilisimama imara huku nikipiga moyo konde ili nishinde vikwazo, kweli nikavumilia. Nakumbuka ilikuwa ni Jumatano ya tarehe 18/03/2015 usiku, siku hii. Hali ya hewa ilikuwa nzuri wastani. Wingu zito likatanda, baridi kiasi likapuliza. Ujumla anga ilipendeza wastani, nikiwa bado katika chumba hatarishi. Sauti za chini nikazisikia sebuleni, watu wakiongea na kucheka. Mmojawapo wa watu hao akiwemo Sulesh. Nimetabiri Sulesh sababu sauti yake niliijua, na maongezi niliyoyasikia ni haya:-



    “Nduguze, nimewaita. Ili nipate ushauri wa jambo moja tu,” Nilisikia Sulesh akiongea, bila shaka alikuwa anaongea na majini wenzie.



    “Lipi?,” Nilisikia mwanamke akiuliza swali.



    “Prisca, hanipendi. Wazazi wanajua ananipenda, sasa wakijua ukweli si hatari. Hebu...nipeni ushauri, nifanye nini?,” Nilisikia Jini Sulesh akieleza kisha akauliza.



    “Mh, sasa sijui tukupe ushauri gani. Hebu...ngoja kwanza,” Safari hii nilisikia sauti ya mwanaume ikijibu, punde kimya kikatawala. Nahisi mwanaume yule alikuwa anafikiria kidogo, baada ya dakika nikasikia akiendelea kuongea huku akisindikiza kicheko.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haa haa haa, nishapata ushauri. Hivi wazazi wamekariri sura ya Prisca?,” Nilisikia mwanaume yule akiuliza mara baada ya kufikiri.



    “Ha hapana,” Jini Sulesh nilisikia akijibu huku akionyesha kusita.



    “Kama hawajaikariri sura ya Prisca. Ushauri wangu naona umuue Prisca.” Nilisikia mwanaume yule akitoa ushauri. Nikashtuka kisha nikatulia mara baada ya kusikia ushauri ule.



    “Eti nini?,” Jini Sulesh nilisikia akiuliza kwa kuhamaki.



    “Ehe, muue Prisca ili uchukue mwili wake. Uwekee roho nyengine ambayo itakayokupenda, kabla wazazi hawajajua,” Nilisikia mwanaume yule akieleza bila shaka yoyote.



    “Hiyo itakuwa poa. Kweli?,” Jini Sulesh nilisikia akiuliza kwa hofu kana kwamba hajawahi kuua.



    “Ndiyo. Itapendeza saana,” Nilisikia mwanaume yule akiunga mkono kwa furaha sana, lakini tangu mwanaume yule atoe ushauri ule sikusikia sauti ya mwanamke iunge mkono. Dhahiri inaonyesha mwanamke yule hakupendezwa na ule ushauri.



    “Sulesh, Prisca mwenyewe unaishi nae?,” Sasa nilisikia mwanamke yule akivunja ukimya kwa kuuliza swali.



    “Ninaishi nae, hapa ninavyoongea nimemfungia katika chumba kile,” Jini Sulesh nilisikia akieleza, nahisi alieleza huku akinyoosha kidole katika chumba nilipo. Ili wenzake wapate kuona chumba hicho kwa urahisi.



    “Kwa nini, sasa umemfungia?,” Nilisikia mwanamke yule akidadisi, kwa ajili ya shauku ya kutaka kujua.



    “Sababu hanipendi, na kama hanipendi. Bora akae huko...halafu muda ushakwenda ngoja niwatoe kidogo. Kuhusu ule ushauri nitaufanyia kazi kesho kutwa, baada ya kumaliza sherehe ya kuzaliwa kwa mfalme,” Jini Sulesh nilisikia akiongea. Mara kimya kikatawala, nahisi alikwenda kuwasindikiza majini wenzie kama ilivyo ada.



    Lisaa moja kupita nikamsikia Sulesh akifunga mlango huku akipuliza mruzi alikuwa katoka kuwasindikiza majini. Hakwenda kukaa, moja kwa moja akaongoza kwenye kabati dogo lenye vitabu. Akachukua kitabu kimojawapo kinachoitwa God Devil cha mwandishi wa Marekani anayeitwa Mos Cherl, akaelekea kuketi sofani tuli akisoma haya moja baada ya nyengine kwa makini. Alisoma kwa masaa mawili akaacha akajiegesha sofani akalala, usingizi bubu. Asubuhi ya alfajiri akaamka akahifadhi kitabu kabatini, hatimaye akaenda bafuni kuosha uso. Kabla hajamaliza kuosha uso akasikia nje mvumo mkali wa upepo. Haraka akajiosha uso akatoka bafuni, na wenge. Ile anatokeza sebuleni anaonana na Zusia akiwa ameketi sofani, Zusia ambaye ni jini mwenye jinsia ya kike. Ndiye jini mlimbwende ambaye makuzi ni sawa na marehemu Suleiman.



    “Ujio wako, nimesikia. Kulikoni?,” Jini Sulesh aliuliza huku pole pole akiambatana na Zusia sofani.



    “Nimerudi leo, sababu mazungumzo ya jana mie sikuyapenda. Kwa nini umuue Prisca, kisa mapenzi. Kama ni wanawake mbona wengi, tafuta mwanamke mwengine tu. Kumuua Prisca.... Si suluhu,” Jini Zusia akaeleza.



    “Lakini mie nampenda Prisca. Sitaki kumkosa kabisa,” Jini Sulesh akaongea.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wewe unampenda. Yeye hakupendi, hebu...acha ubishi, tafuta mwanamke mwengine.”



    “Hapana.”



    “Ila si lazima, lakini bora ujue kuwa jambo mlilopanga sijapenda,” Jini Zusia akaongea hatimaye akapotea, huku alimuacha Sulesh kabaki na msimamo.





    Kesho yake usiku wa saa sita. Jini Sulesh akafunga milango ya nyumba yote, kisha akapotea akatokea katika kumbi ya kifalme. Akajumuika na majini mbalimbali kwenye sherehe ya kuzaliwa baba yake, majini wote wakiwa kwenye shamra shamra za sherehe. Jini Zusia akang'aza jicho la wizi kwa Sulesh ghafla akapotea akatokea katika mjengo wa Mabibo hostel, akatalii kidogo ndani akiangalia usalama uliopo. Alipoona kupo shwari akapotea akaja kutokea katika chumba nilicho, akapuliza juu ya paa na mara taa ikawaka tukapata kuonana ana kwa ana nikashtuka.



    “Wewe ni nani?,” Nikauliza kwa kufoka.



    “Ni Zusia. Jini kutoka tawala anayotoka Sulesh,” Jini Zusia akajitambulisha.



    “Mbona mnaniandama. Na wewe umefuata nini kwangu?.”



    “Kwanza kaa ujue kuwa. Mimi si jini mbaya, bali ni jini mzuri niliyekuja kukusaidia...na Sulesh si jini mzuri kwako, yaani bila mimi kukusaidia. Utapotea.”



    “Sasa unanisaidiaje?.”



    “Sasa sikia, mie nitakutoa katika chumba hiki. Ila nikikutoa wewe inakupasa uondoke, usionekane eneo lolote la Dar es salaam. Umesikia?,” Jini Zusia akauliza kwa kukaza macho kwangu.



    “Ndiyo,” Nikakubali huku kwa mbali nikijilazimisha kuonyesha tabasamu mara baada ya kuona. Jini Zusia ndiye mkombozi wangu.



    Baada ya kukubali msaada, Zusia hakuchelewesha muda, mara akapiga jicho kali kwenye mlango ule wa kile chumba. ghafla mlango ukafunguka tukatoka mwishowe akafunga kupitia njia ile ile ya awali, kufika sebuleni akanishika mkono tukapotea pamoja. Tukaja kutokea nje ya mjengo kabisa, tulipofika hapo Zusia akaniangazia njia ya kuongoza. Nikaongoza, yeye akapotea akarudi kwenye tafrija baada ya kuona mie tayari nimetokomea. Niliongoza njia ile ya kuelekea kituo cha daladala cha Mabibo hostel, huku kwenye nguo na mwili nikiwa nimechafuka mno. Nilipofika kituo cha daladala cha Mabibo hostel, hapo ndipo nikakutana nawe nikakuomba msaada ukanisaidia.



    **********

    Prisca alimaliza kumhadithia Emmanuel simulizi ya maisha yake, ambayo iliyomfanya hii leo aonekane ka chizi kwa jinsi alivyokuwa rafu. Akajifuta machozi kisha akajiangalia mwili na mavazi, kwa huzuni. Mpaka Emmanuel alimuonea huruma sana, baada ya kugundua kuwa alipitia wakati mgumu. Emmanuel alisogea jirani ya Prisca akamfariji kwa kumkumbatia hatimaye wakaongozana kwenda kuonyeshana chumba atakacho pumzika baada ya Prisca kuonyesha uchangamfu.



    “Asante sana,” Prisca alishukuru mara baada ya kuonyeshwa chumba cha wageni, cha kupumzika.



    Kabla Emmanuel ajaongea chochote kwa wakati ule, mara simu yake ikawa inaita haraka akapokea kisha akatoka chumbani akaelekea sebuleni. Kwa ajili ya kuzungumza na simu vizuri, kwa kuwa simu ilitoka ofisini na alikuwa anahitajika haraka ofisini. Basi, Emmanuel simu ilipokata tu. Upesi akarudi chumbani kumuaga Prisca, aliaga mwisho akaondoka ofisini huko bandarini.



    **********

    Majini tafrija iliisha usiku wa saa kumi. Jini Sulesh aliaga akapotea akatokea sebuleni katika mjengo wa Mabibo hostel, alifikia kulala sababu alichoka sana. Hakukumbuka hata kukagua nyumba, wala kwenda kumtazama Prisca. Alfajiri akiwa amelala kwenye sofa akashtuka usingizini baada ya kusikia radi kali imepiga nje, akakaa kitako kwenye sofa kama nusu saa. Akanyanyuka akachungulia nje kupitia kwenye dirisha la sebuleni, akaona shwari. Akarudi tena kukaa sofani, alipokaa tu macho yake yakagongana na picha ya Suleiman iliyoko ukutani. Ghafla akamkumbuka Prisca haraka akapotea pale sebuleni akatokea chumbani, kufika huko chumbani. Macho yakamtoka pima baada ya kutomkuta Prisca kwenye kile chumba, upesi akajifikiria katika Medula Obulangata kuwa. Prisca ametokaje kwenye kile chumba. Lakini alikosa jibu stahiki, akajipa jawabu tu kuwa. Pengine Prisca ametoka labda sababu mlango hakukaza, hivyo akajaribu kung'aza macho kila dira pengine ataona alipo Prisca. Akang'aza Magharibi hakumuona, Kaskazini hakumuona, Kusini hakumuona. Lakini kuangalia Mashariki aliona Prisca jinsi alivyosaidiwa, alipofikia na mpaka alipo msamaria mwema wake. Hasira zikamshika, jazba ikampanda ghafla akajibadili kisha akapotea pale akaja kutokea bandarini eneo la mapokezi. Akiwa kwenye jinsia ya kike ya mwanamke wa kichina, ambaye anayeongea lafudhi ya kiswahili cha kubahatisha.



    “Daada, bosii wako nimeemkutaa?,” Mwanamke yule wa kichina aliuliza huku akionekana kukagua eneo lile la mapokezi kwa kupitisha macho kila kona mara baada ya kukutana na sekretari.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Umemkuta. Ila wewe ni nani?, ni mfanyabiara au ni mteja?,” Sekretari nae aliuliza mara baada ya kujibu swali la yule mwanamke wa kichina.



    “Ni mteeja.”



    “Ehee, una shida ipi?.”



    “Nataaka kuoonana nae. Anieelekeze mziigo wangu umefiikia wapi...maana hii ni siiku ya taatu sijaapata mziigo wangu.”



    “Ooh, lakini. Kwa sasa bosi ana mgeni....”



    “Usiijali nitaamsubiri,” Mwanamke yule wa kichina aliongea huku akitabasamu kwa mbali, mara baada ya kukaa katika sofa za mapokezi.



    Masaa mawili kupita, Emmanuel alitoka ofisini kwake akiwa na mgeni wake. Ambaye ni mzee wa makamo aliyepigilia suti nyekundu ya gharama, alimsindikiza mgeni yule mpaka sehemu ya kuegeshea magari “Parking”. Hapo ndipo akarudi ofisini baada ya kuhakikisha mzee yule kashapanda gari yake aina ya LANDCRUISER V8 na kuondoka, aliporudi mapokezi anataka kupita aelekee ofisini mara anasikia sekretari wake akimuita, hakuwaza akatii wito akajongea kumsikiliza sekretari.





    “Bosi, mwanamke yule wa kichina anahitaji kuonana na wewe. Bosi,” Sekretari aliongea huku akionyesha kidole kwa yule mwanamke, ili bosi apate kumuona. Ni kweli Emmanuel akageuka akamtazama yule mwanamke mara moja kisha aliongea huku akitafuna bazoka.



    “Mwambie, aje ofisini,” Emmanuel aliongea haraka na upesi akaongoza ofisini.



    Sekretari baada ya kupokea ruhusa. Akamruhusu yule mwanamke aingie ofisini kwa bosi akazungumze, nae yule mwanamke bila kuchelewa akaongoza katika ofisi. Cha ajabu kufika mlangoni kwenye kumbi ya kuingilia ofisini, yule mwanamke akajibadili akarudi kuwa. Jini Sulesh, akaingia ofisini. Ile anaingia tu wakagongana macho kwa macho na Emmanuel, mara Emmanuel akasisimka na akashtuka maana hakutegemea kukutana na Sulesh. Badala yake alitegemea kukutana na yule mwanamke wa kichina.



    “Ehe, mheshimiwa. Natumaini sina mihadi na wewe, hebu...nipishe kidogo niongee na mgeni wangu,” Emmanuel aliongea huku akikunja ndita asijue kuwa kama mwanamke yule anayehitaji kuongea nae ndiye aliye mbele kwasasa.



    “teh teh teh. Unasema huna mihadi na mie, kwani wewe una mihadi na nani?,” Jini Sulesh alianza kucheka kisha akauliza.



    “Nina mihadi na mwanamke fulani, mtu mweupe.”



    “Sasa, si ndiye mie.”



    “Hapana. Unasema ndiye wewe, kivipi?,” Emmanuel alipinga akijua yule si mhusika aliyeomba mihadi nae.



    “Ndiye mie. Ona,” Jini Sulesh alisema kisha akajibadili kuwa yule mwanamke wa kichina, na mara akarudi kwenye muonekano uliozoeleka.



    Emmanuel kuona vile akachanganyikiwa, aliona ofisi yote ndogo. Imejaa joto la ajabu japo ilikuwepo “AC” ya kutosha, ofisi yote akaiona chungu. Alitoka pale ofisini nduki akapita mapokezi upesi mpaka sekretari wake akashangaa akabaki kinywa wazi, alikwenda kwenye maegesho ya magari akapanda gari lake akatokomea nyumbani.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **********

    “Dada, kulikoni. Bosi mbona kapita mapokezi akiwa resi?,” Sekretari aliuliza mara baada ya kufika katika ofisi ya bosi wake na kumkuta Sulesh kashajibadili tena kuwa muonekano wa mwanamke wa kichina.



    “Aah, boosi wako katooka viile sabaabu kapaata simu ya msiiba,” Mwanamke yule wa kichina aliongopa kwa kuongea lafudhi ile ile ya kiswahili cha kubahatisha, ili kuficha makucha kwa sekretari.



    Hatimaye. Jini Sulesh akaaga akaondoka bandarini bila ya kumaliza maongezi na sekretari, hata hivyo. Jini Sulesh kwa kuwa akutimiza dhima kuu, alichokifanya ni kupotea akaja kutokea kwenye gari ya Emmanuel. Katika viti vya nyuma huku Emmanuel mwenyewe akitingwa na msongo wa mawazo, na foleni ya barabara ya Ally Hassan Mwinyi hasitambue chochote. Zile gari za upande wa barabara ya Ally Hassan Mwinyi ziliporuhusiwa na kuanza kutembea nae Emmanuel akakanyaga mafuta, ghafla Emmanuel akiwa kwenye mwendokasi akashtuka kusikia mtu nyuma ya kiti cha gari lake akijitambulisha bila hofu.



    “Kwa majina, naitwa Sulesh bin Kadhir. Ni jini ambaye aliyetokea kumpenda msichana mmoja tu, nae ni Prisca,” Jini Sulesh alijitambulisha huku akimpiga jicho kali Emmanuel, kupitia kwenye kioo cha mbele cha gari. Ili aone Emmanuel alivyo na hofu usoni.



    “Lakini mimi, sio Prisca. Sasa kwangu unataka nini?,” Emmanuel aliuliza huku akitetema kwa kugubikwa na uwoga kila pahala ya mwili.



    “Najua wewe sio Prisca. Ila najua unaishi nae kwa sasa, hivyo. Naomba nikabidhi Prisca kabla mambo hayajabadilika.”



    “Ila...,” Emmanuel kabla ajamaliza kuongea zaidi kwa wasaa ule, mara moshi mzito mweusi ukatanda ndani ya gari lake hadi yeye na. Jini Sulesh wakaogopa maana moshi ule ulikuwa si wa kawaida, ulikuwa ni wa ajabu sana.



    Na ghafla moshi ule ukaisha, kabla ya dakika tano kupita kwenye kiti cha nyuma ya gari alipokaa. Jini Sulesh, alitokea mzee mmoja aliyechakaa kichwani kwake na mvi. Halafu mwenye macho makali ka Paka, hakika ulikuwa ni mzimu. Mzimu wa babu yake Emmanuel, basi mzimu ule macho yake yalipogongana na macho ya. Jini Sulesh, ghafla ndani ya gari kukatokea shoti mfano wa radi. Kisha punde Sulesh akanyong'onyea haraka akapotea kwenye gari.



    “Emmanuel, Usiogope. Mjukuu wangu, nimekuja kufanya hitimisho. Unakumbuka kipindi cha nyuma kabla ya kifo changu, wewe ulipenda sana uje kujua. Umuhimu wa lile Ua la Uwaridi nililokukabidhi wakati upo na wazazi, sasa basi. Naona leo ni wakati sahihi wakujua umuhimu wa lile Ua,” Mzimu ule ulisema mara baada ya kuhakikisha. Jini Sulesh kweli amemkimbia na mjukuu wake hofu imemtoka anamsikiliza.



    “Babu, kweli nina shauku sana. Kwani Ua lile lina umuhimu gani?,” Emmanuel alidakia, akauliza kweli kwa shauku apate kujua umuhimu wa lile Ua. Ambalo babu yake amepewa na mizimu ya ukoo huko kipindi cha nyuma kwenye milima ya ajabu ya Uluguru.



    “Umuhimu wa lile Ua, ni kujilinda wewe na watu uwapendao msidhurike na kitu chochote cha hatarishi,” Mzimu ule ukaeleza.



    “Sasa, tangu unipatie lile Ua sijawahi kutumia na sijui kulitumia. Sasa Ua lile litanilindaje?,” Emmanuel akahoji. Kuhoji kwake kule ukamfanya mzimu ucheke, haukucheka kwa kuonyesha kebehi bali ulicheka kwa ajili ya swali lile lililoulizwa na mjukuu wake kwa kimue mue.



    “Sasa sikia, naona mapambano ya viumbe hatarishi yashaanza zidi yako. Kama yameanza ni kazi ndogo tu kwako, cha kufanya. Chukua lile Ua halafu kamkabidhi mtu yule unayempenda kutoka ndani ya moyo, yaani kivyovyote ile. Uwe unampenda kimapenzi au kirafiki, ukitenda hivyo. Utakuwa umemaliza mchezo wote, hamtofuatwa tena na kiumbe chochote hatarishi. Ng'o,” Mzimu ule ulielekeza mwishowe ukatokomea huko kuzimu, huku ukamuacha Emmanuel akiendelea na safari yake ya kurudi nyumbani kwake Masaki.



    **********

    Zamu hii. Jini Sulesh alikuwa anatapatapa tu, zote ni juhudi za kumrudisha Prisca kwenye himaya yake. Safari hii alikuja kutokea sebuleni kwenye nyumba ya Emmanuel, alitokea nyuma ya sofa ambalo alilokaa Prisca huku. Prisca hasitambue chochote, yeye alikuwa makini tu na kusoma gazeti la MTANZANIA DAIMA. Jini Sulesh akachukua fursa ya kupotea pale nyuma ya sofa, akaja kutokea amekaa sofani jirani na Prisca huku. Prisca hasijue ka Sulesh kashawasili, wakatulia sofani ka lisaa bila Sulesh kumbuguzi Prisca. Lilipopita lisaa lile na kuwasili lisaa lengine, mara. Jini Sulesh ikaonyesha uvumilivu umemshinda, hakashindwa kujizuia akataka kumbusu Prisca ili apotee nae. Ghafla Emmanuel akaingia huku akiwa anahema kuonyesha kuwa ametoka kukimbia kwa ajili ya kuwahi kumsaidia Prisca, hali ile kidogo Prisca alishangaa akajua kwa wakati ule Emmanuel anahitaji faraja. Basi akataka kuweka gazeti kando ili akamfariji Emmanuel kwa kumlaki, la haula!.... Alimuona. Jini Sulesh jirani yake, hapo bila kutaka ajizi akakimbilia chumbani kwa ajili ya kumkwepa Sulesh. Hazikupita dakika Emmanuel nae upesi akaingia chumbani kwake akachukua lile Ua la Uwaridi alilohifadhi kwenye sanduku la nguo, haraka akaelekea chumbani kwa Prisca. Aligonga mlango akajitambulisha akafunguliwa, na mara akaingia chumbani na kufunga mlango. Na sababu Prisca ndiye mwanamke ampendaye Emmanuel tangu awali alipompatia msaada eneo la Mabibo hostel, hivyo hata lile Ua hakusita kumkabidhi yeye. Alimshawishi Prisca haweze kukubali kupokea lile Ua ili wawe salama, Prisca sababu ni muelewa na kwa kuwa alichoka kusumbuliwa na. Jini Sulesh basi bila ajizi akakubali kupokea lile Ua, pia bila shuruti akakubali kuwa mke wa Emmanuel baada ya Emmanuel mwenyewe kumuomba awe mkewe. Ua likiwa tayari lishapokelewa na Prisca, mara ghafla kule kule akatokea Sulesh tena kwa kishindo hadi likatokea tetemeko kwenye chumba kile. Takribani nusu saa imepita, ghafla Sulesh anaonyesha kunyong'onyea mara anadondoka sakafuni baada ya macho yake makali kuangalia lile Ua la Uwaridi alilolishika Prisca. Hakukaa sana ghafla akapotea akatokomea mazima eneo lile, huku akipiga ukunga wa maumivu. Na tangu siku hiyo Sulesh aliona ulimwenguni ka kituo cha polisi, hakuthubutu tena kuja ulimwenguni. Yote sababu ya lile Ua la Uwaridi lenye nguvu ya mizimu.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **********

    Ya nini?. Ulazimishe penzi, kwa ajili ya kujikonga nyoyo na kufurahisha moyo huku wengine wakiumia. Huo ni udhariri, iweje?. Unakubali kupoteza nguvu kwa ajili ya mtu mmoja ambaye asiyekupenda, kweli?. Hii inaingia akilini, hapana. Ni hapana sababu wapo wanaopenda, sasa kama wapo. Kwanini tusiwapende hao. Itakuwa nzuri sana, maana hao watatupenda, watatuthamini na watatuheshimu sana. Hebu...sasa hii leo sambaza upendo kwa watu kama hao, wala usijivunge. Wewe onyesha upendo kwa mtu kama huyo, naamini upendo wako hautopotea bali utakuletea makuu katika maisha.”



    MWISHO.



Blog