Search This Blog

BAHARI YA HINDI - 5

 







    Simulizi : Bahari Ya Hindi

    Sehemu Ya Tano (5)



    Roda akabaki mdomo wazi,, akainamisha uso wake akalitazama tumbo lake,, akajisemea moyoni,, "Mungu wangu inamaana Tobi ni jini? pia alikuwa akiniingilia kimwili miaka yote hiyo?  sasa nimepata jibu la swali nililokuwa najiuliza kila siku, kwa nini kila nikiamka usingizini nakuta sehemu zakungu za siri zimelowana,kumbe ni Tobi,

    nini hatma yangu? CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda alijisewmea maneno hayo huku mapigo yake ya moyo yakipiga kwa kasi ya ajabu...,kumbe tarehe za kujifungua zilikuwa zimetimia,,, punde si punde akaanza kuhisi maumivu makali chini ya kiuno, pamoja na mgongoni!!  maumivu hayo yalikuwa makali kupita kiasi,, yakahamia tumboni Roda akajikuta anashindwa hata kusimama,



    wakati huohuo,,upande mwingine, lilionekana gari likiendeshwa kwa mwendo wa taratibu,, ndani ya gari hilo walikuwemo watu wawili,, mke na mume! watu hao walikuwa wamepotea njia,, kwa sababu ni wageni maeneo hayo,, walikuwa wanamtafuta ndugu yao aliyekuwa anaumwa kwa kipindi kirefu,, punde si punde Tobi akajitokeza kimiujiza ndani ya gari hilo!  akabadilisha mawazo ya dereva huyo pasipo yeye mwenyewe kujionyesha,

    Tobi aliamua kufanya hivyo ili dereva huyo akamsaidie Roda,, kumpeleka hospitali,,kisha akatoweka kimiujiza,,, punde si punde dereva wa gari hilo akaamua kukatisha kona na kuifuata barabara ya vumbi!!

    kwa mbali akaona nyumba,,,akaamua kuifuata nyumba hiyo,, alipofika akashuka na kugonga hodi,,

    wakati huo Roda alikuwa anatambaa utadhani mtoto mdogo,, huku akihisi maumivu makali kupita kiasi, (uchungu wa mimba) Roda akasikia mlango unagongwa, akaingiwa na matumaini ya kupata msaada wa kupelekwa hospitali.. akajaribu kulaza sauti huku akisema,, "FUNGUA MLANGO UPO WAZI, yule dereva akastushwa na sauti hiyo!

    akajisemea moyoni bila shaka mtu huyu ni mgonjwa,,

    dereva huyo hakujali,, akafungua mlango alipoingia upande wa ndani ya nyumba akashtuka kumuona Roda akiwa anatambaa huku machozi yakimtoka,,

    Roda akasema naomba msaada nipeleke hospitali tafadhali nahisi uchungu wa mimba!

    Dereva huyo akamnyanyua Roda na kutoka nae nje ya nyumba,, akamuingiza ndani ya gari,, mke wa dereva huyo akaingiwa na roho ya huruma akasema,,"najua unapata maumivu kupita kiasi kwa sababu hata miminpia nina watoto.. uchungubwa mimba unatesa kupita kiasi.. jikaze.. wakati anaongea maneno hayo,, dereva alikuwa tayari ameshaliondosha gari,,

    wakiwa njiani Tobi akajitokeza ndani ya gari,, Roda akamuona Tobi kaketi kando yake,, lakini dereva pamoja na mkewe hawakuweza kumuona Tobi, Roda akasema,, "haya yote umeyasababisha wewe,,, tazama ninavyoteseka!  kwa nini umenitenda hivi?

    yule dereva pamoja na mkewe wakastaajabu,, kila mmoja akabaki anajiuliza anaongea na nani?

    wakati huo Tobi alikuwa anatabasamu,, huku kashika viganja vya mikono ya Roda,

    Tobi akasema,, "usiogope,, mimi ndiye mwanaume ninayekupenda na wewe ndiye mama wa mtoto wangu,, Roda akajibu,, lakini wewe ni jini,

    mke wa dereva akamwambia mume wake,, huyu anaongea peke yake,,ni mimba ndiyo imemchanganya,, huwa inatokea kwa mama mjamzito,

    safari iliendelea,, hakuna aliyetambua Roda anaongea na nani,, walihisi ni uchungu wa mimba tu inamchanganya! CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Baada ya dakika kumi kupita wakafika hospitali.. Roda akapokelewa haraka akaingizwa kenye wodi maalumu ya wazazi,,,

    Roda akaandaliwa kwa ajili ya kusukuma mtoto atoke tumboni...

    alisukuma kwa muda mrefu lakini ikashindikana,,



    punde si punde Tobi akajitokeza ndani ya wodi hiyo,,Roda akashtuka kumuona Tobi.. alipojaribu kuongea na Tobi,, sauiti haikutoka Roda akawa kama bubu!

    Tobi akafumba macho yake,, ishara ya kuwasiliana na mama yake,(Malkia wa bahari)

    ili apewe maelekezo jinsi ya kumchukua mtoto,,, malkia wa bahari akasema,, usichelewe ndani ya sekunde tatu.. mtoto atakapotoka tumboni... endapo utachelewa basi mtoto huyo atakuwa binadamu wa kawaida,, hatoweza tena kuwa jini! hivyo tutakuwa tumepoteza aseti,, na mtoto huyo ni muhimu kwetu..

    Tobi akafumbua macho baada ya kupata maelekezo kutoka kwa Malkia wa Bahari.

    wakati huo huo zikasikika sauti za manesi wakimuhimiza Roda asukume bila kubana miguu ili mtoto atoke akiwa hai.

    punde si punde akaingia nesi mwingine.. nesi huyo alikuwa na uwezo wa kuona majini pasipo kudhurika na chochote,, pia majini walikuwa wanamuogopa sana mtu wa aina hiyo!  nesi huyo alikuwa na pete maalumu aliyoachiwa na marehemu bibi yake,, pete hiyo ni adui mkubwa wa majini.. Tobi akashtuka kumuona nesi huyo!







    Punde si punde,, ikasikika sauti ya mtu,, akimuita nesi,, aliyekuwa anaingia ndani ya wodi hiyo ya wamama wajawazito. nesi huyo akaamua kufunga mlango na kurudi upande wa nje!  kumba daktari ndiye alimuita nesi huyo,, ampe maagizo juu ya jambo fulani.



    kule ndani ya wodi,, Tobi akaanza kuwa na wasiwasi kupita kiasi!  akajisemea moyoni,, "huyu nesi anakitu ambacho ni adui wa majini,, na kama akirudi humu basi mpango wangu utavurugika,, na sijui kama mama(Malikia wa majini )atanielewa!

    wakati huo Roda alikuwa anafanya jitihada za kusukuma mtoto huku manesi wakimuhiziza,, asukume bila kukata tamaa,, endapo ataacha kusukuma atambana mtoto hivyo mtoto huyo atakufa!  Roda alijitahidi kusukuma,,

    Manesi waliokuwemo ndani ya wodi hiyo,, hawakuwa na uwezo wa kumuona Tobi,, pia sasahivi Tobi hakutaka kujionyesha machoni mwa Roda,, Tobi akajisemea moyoni,, "wacha nifanye jambo fulani,, ili mpango wangu ukamilike.,,,,baada ya kuwaza hivyo akatoweka kimiujiza! akajitokeza kwenye korido inayokwenda kwenye wodi!! akuona yule daktari aliyempa maagizo yule nesi mwenye uwezo wa kuona majini! 

    Tobi akamfuata daktari huyo,, alipomuongelesha tu,, akili ya daktari hiyo ikabadilika,, akazipiga harakaharaka kutoka kwenye kordo hiyo na kuezlekea nje kabisa,,, kwa mbali akamuona yule nesi anarudi,, ni baada ya kumuagiza akalete taarifa ya maendeleo ya mgonjwa aliyekuwa amelazwa wodi nyingine,, tofauti na wodi ya wamama wajawazito.... daktari huyo akaendelea kuzipiga hatua mpaka akamkaribia nesi huyo,, kisha akamuagiza kuwa aende kwenye maabara akalete test tube.

    nesi huyo akaondoka zake kuelekea maabara.



    wakati huo huo kule kwenye wodi ya wamama wajawazito,, alionekana Roda akiendelea kufanya jitihada za kusukuma ili mtoto atoke tumboni, wale manesi waliokuwa ndani ya wodi hiyo walostaajabu sana,, kwa sababu limepita lisaa limoja Roda anasukuma lakini hakuna dalili zozote za mtoto kutoka tumboni! nesi mmoja akatoka nje ya wodi hiyo kwenda kumuita daktari haraka,, ili wajue wanamsaidia vipi Roda! kabla nesi huyo hajatoka ndani ya wodi hiyo,, akasikia sauti ya manesi wenzake wakisema,, "jitaidi sukuma kwanguvu, mtoto ameanza kutokeza kichwa,, endelea kusukuma,, Roda akasukuma hatimae mabega ya mtoto yakaanza kuchomoza kikabaki kiuno na miguu vikiwa upande wa ndani ya tumbo la Roda,

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kule nje ya wodi alionekana Tobi akimtazama yule nesi akiishilizia kuelekea maabara..

    alipohakikisha nesi huyo kafika mbali,, Tobi akaanza kupata amani,, akatabasamu kisha akatoweka kimiujiza akajitokeza ndani ya wodi ya wamama wajawazito.. akashtuka!!! macho yakamtoka,,ni baada ya kukuta tayari Mtoto amekwishazaliwa,, hivyo amechelewa kulikamilisha jambo la kumchukua mtoto huyo ndani ya sekunde kumi ili mtoto huyo asiwe binadamu wa kawaida,awe jini!

    Tobi akajisemea moyoni,,"nimechelewa! mama (Malikia wa bahari) hawezi kunielewa!

    na sijui itakuaje? bila kuchelewa Tobi akatoweka kimiujiza! kuelekea kule ujinini.



    kutokana na kutumia nguvu nyingi, kusukuma mtoto lisaa limoja mfululizo, Roda aliishiwa nguvu baada ya mtoto kutoka tumboni alipoteza fahamu... manesi wakampa huduma ya kwanza,,ili kunusuru maisha yake!



                    ***************************************



    Upande mwingine,kule katikati chini ya bahari ya hindi,,(ujinini), alionekana Tobi akijitokeza mbele ya mama yake(Malkia wa bahari)  akaeleza yote yaliyotokea..

    Malkia wa bahari akakasirika sana,, kutokana na hasira alizokuwa nazo akabadilika na kuonekana kutisha kupita kiasi.. macho yake yalibadilika na kuwa mekundu pasipokuonekana mboni kiini cha jicho.. masikio yake yakawa marefu kama mbwa mwitu!  bahari ikachafuka,,  upepo mkali ukavuma kwa kasi... upepo huo ulitengeneza mawimbi makubwa kupita kiasi.... hata manahodha waliokuwa wakiendesha meli zilizokuwa zikipita juu ya bahari,  wakaingiwa na hofu kupita kiasi!



    kule chini ya bahari, alionekana Tobi akiwa katika hali ya uwoga wa hali ya juu,, alitambua vyema kuwa mama yake kakasirika kupita kiasi!!! na akifikia hatua hiyo ya kubadilika na kuonekana hivyo,, huwa anaingiwa na roho ya kikatiri!!mama Tobi(Malkia wa bahari)  akazipiga hatua kumsogelea Tobi,, punde si punde kucha zake za mikononi, zikawa ndefu mara kumi ya kucha zake za kawaida Tobi akazipiga hatua kurudi nyuma!!!!!





    Malikia wa bahari akanyanyua mkono wake iliamuadhibu Tobi,,

    kwa kiwango cha hasira alizokuwanazo Malkia wa bahari, ambaye ni mama mzazi wa Tobi,, hapo Tobi yupo kwenye hatari kubwa ya kuuwawa!

    Tobi akaongea maneno ya lugha ya kijini,, maneno ya lugha hiyo yanashahbiana na maneno ya lugha ya kiarabu! akimaanisha kuomba msamaha wa dhati kwa kutubu kosa lake mbele ya Malkia wa bahari!  punde si punde Malkia wa bahari akabadilika na kurudi kagika umbile lake la kawaida,, akaonekana vile vile alivyokuwa bibi kizee.

    akamtazama Tobi kwa macho ya mshangao! kisha akasema,, "pole sana mwanangu wa pekee,, haikuwa dhamira yangu kukuangamiza, ni hasira tu,,, na nimejizuia kwa kiwango cha juu... lakini bado unayo nafasi,,,ingawa ni mlolongo mrefu ambao unaweza kugharimu maisha yako,, na siwezi kukubali mtoto huyo kuishi huko duniani..

    ni lazima aletwe nyumbani kwa ujinini akiwa tayari ameshakuwa jini... mtoto huyo ni aseti ya Miungu wa bahari,, akwa sababu damu yake inamchanganyiko wa nusu binadamu na nusu jini,, hivyo anauwezo mkubwa kuliko majini wa kawaida... na asipoletwa huku ujinini basi atakuwa adui mkubwa na majini kwa sababu atakuwa anawaona na atatuangamiza bila huruma,, hivyo kutakuwa na hatari ya kizazi hiki kutoweka kabisa!

    wakati huo Tobi alikuwa makini kumsikiliza mama yake(Malikia wa bahari)  ili asije akarudia tena kufanya kosa kwa mara nyingine.kisha akauliza nifanye jambo gani ili niweze kuikamilisha kazi hii?

    Malikia wa bahari akajibu,, "itabidi uende bahari ya saba(07)ukatafute gamba la konokono mwekundu aliyekufa,, gamba hilo ni maalumu kitalazwa kichwa cha mtoto huyo juu ya gamba hilo.. ni kinga kwa mtoto huyo,,ni muhimu sana.



    bila kuchelewa Tobi akatoweka kimiujiza, kuelekea kwenye bahari ya saba(7)



      

                             ****************************************



    Upande mwingine, kule hospitali alionekana Roda akizinduka, na kupata fahamu,,akashangaa kuona tumbo lake likiwa dogo,, akajiuliza,, "inamaana nimeshajifungua?  je? mtoto yuko wapi?

    wakati Roda anasukuma mtoto,,alipotoka tumboni aliishiwa nguvu,, kwa sababu alitumia nguvu nyingi sana kusukuma mtoto,, hivyo hakujua kilichoendelea baada ya hapo kwa sababu alikuwa tayari kapoteza fahamu!

    punde si punde nesi akaingia kwenye wodi hiyo huku kambeba mtoto,, akamkabidhi Roda mwanae,, kisha akasema mnyonyeshe sasahivi,,

    Roda akampokea mtot huyo huku akimtazama kwa macho ya umakininwa hali ya juu,, akajisemea moyoni,, "asije kuwa ni jini!

    alijisemea hivyo huku akiukagua mwili wa kichanga huyo.

    akagundua kuwa ni mtoto wa kawaida na sio jini! akaanza kumnyonyesha.



    Kesho yake Roda akaruhusiwa kurudi nyumbani,, wakati anatoka akakutana na yule dereva pamoja na mkewe waliompa msaada wa kumleta hapo hospitali.. Roda hakuweza kuwakumbuka kwa sababu wakati wanamleta hospitali,, ilikuwa ni nyakati za usiku,, pia Roda alikuwa amechanganywa na maumivu makali ya uchungu wa mimba,, hivyo hakuweza kuwatazama nyuso zao!



    wakamsalimia Roda kisha yule mwanamke akasema,, "hongera wana,, unatukumbuka? Roda akamtazama mwanamke huyo kwa mshangao!  kisha akauliza,, "nyinyi ni nani?

    yule mwanamke akajibu,, "sisis ndio tulikuleta hapa hospitali jana usiku,, hivyo tulikuwa tumekuja kukujulia hali.

    Roda akaingiwa na kumbukumbu,, akakumbuka kuwa aliletwa hospitali lakini hawafahamu watu hao... akasema,, "nimekumbuka asanteni sana kwa msaada wenu.. mimi nimeruhusiwa kurudi nyumbani! CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yule dereva akasema,, "wacha tukupeleke nyumbani,  .

    Roda akakubali,, wakaongozana mpaka nje kabisa ya jengo la hospitali hiyo.. wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea nyumbani kwa Roda ikaanza.

    walipofika waka, Roda akashuka kutoka ndani ya gari akaingia ndani kwake... akashtuka kukuta madhari ya ndani ya nyumba imebadilika,, kila kitu kimebadilishwa na kuwekwa vitu vipya na nyumba ilikuwa safi kupita kiasi!

    Roda akastaajabu akajisemea moyoni,, "bila shaka huyu ni tobi ndio kafanya haya yote,, Eee Mungu nisaidie niomdolee hili balaa la huyu jini Tobi..Roda akazipiga hatua akaingia ndani ya chumba chake,, akastaajabu kukuta kumewekwa kitanda cha kifahari na xhumba kimependeza kwa mapambo ya kila aina pamoja na nguo za mtoto,, zikiwa juu ya kitanda,, Roda akaingiwa na hofu akidhani huenda Tobi yumo mdani ya nyumba! akaita Tobi,, lakini Tobi hakuitika!

    Roda akakisogelea kitanda akamlaza mtoto huku macho yake yakitazama huku na kule!

    baada ya nusu saa kupita akaanza kuingiwa na amani,, hakuona dalili yoyote ya Tobi kujitokeza,



    kumbe Tobi kabla hajaenda kule kwenye bahari ya saba,, alirudi duniani akaingia kwenye maduka kimiujiza na kuchukua vitu vyote hivyo ndani ya dakika moja.. kisha akaviweka ndani ya nyumba ya Roda,, akatoweka kimiujiza kuelekea kule kwenye bahari ya saba(7) Tobi alifanikiw kupata gamba la konokono mwekundu aliyekufa..



    Siku zilizidi kusonga,, hatiimae mtoto akatimiza miezi miwili na nusu.

    Roda alimpenda sana mwanae,, lakini akawa anaishi kwa wasiwasi kwa kuhofia huenda Tobi akamchukua mtoto wake!



    upande mwingine kule ujinini,, alionekana Malkia wa bahari, akiandaa mpango kabambe,, jinsi ya kwenda kumchukua mtoto huyo siku ya leo,, kabla jua halijazama!

    Akamuongezea Tobi nguvu za kimiujiza ili aende akamlete mtoto huyo kwa wakati unaotakiwa... Malkia bahari akasema,, "nenda huko duniani mimi nipo nyuma yako,, chochote utakachokifanya mimi nitakusaidia.

    bila kupoteza muda Tobi akatoweka kimiujiza kuelekea Duniani.. pia Malkia wabahari akatoweka kimiujiza kwa ajili ya kumlinda Tobi,, ili waikamilishe kazi ya kumchukua mtoto na kumpeleka ujinini.







    Nyumbani kwa kwa Roda, alionekana akimnyonyesha mwanae,, huku akimtazama usoni,, akatabasamu kisha akajisemea moyoni,, "hakika nimeza mtoto mzuri sana kafanana na Tobi,, lakini ninawasiwasi,, huenda Tobi akamchukua mtoto huyu,, yanipasa niende kwa mchungaji,, nimueleze jambo hili,, naamini atanisaidia.. huwa naona mahubiri yake kwenye kioindi cha Runinga akiwaomnea watu kwa imani na matatizo yao yanakwisha!!! mimi sitaki kumuona Tobi,, na siwezi kuishi na jini,,lakini naamini huu ni mpango wa Mungu kutenda haya yote,, mimi sijui sababu ni nini,, ajuaye ni yeye pekee!

    Real da aliongea maneno hayo kwa dhati ya moyo! wakati huo alikuwa akimnyonyesha mtoto,, alipomtazama akagundua kuwa mtoto amesinzia akamlaza kitandani,,,

    akaingia bafuni akaoga,,kisha akarudi chumbani akajilaza kando ya mtoto wake.. ghafla wazo likamjia akajisemea moyoni,, "kwa nini nisiende sasahivi.. kanisani kwake napajua.



                                     ****************************************



    Upande mwingine alionekana Tobi pamoja na mama yake(Malkia wa bahari)  wakijitokeza kimiujiza kando ya bahari! jirani na Cocobeach

    wakazipiga hatua kuifuata barabara iliyokuwa jirani na bahari... Tobi akasema,, "kuna watu wawili mume na mke,, niliwaongoza waifuate nyumba ya Roda pasipo wenyewe kujijua... wakampa msaada wa kumpeleka hospitali,,unaonaje tukiwatumia watu hao ili iwe rahisi kumchukua mtoto?

    Malkia wa bahari akasema ni jambo jema,, kwa sababu huwezi kumchukua hivi hivi,, ukiwa katika umbile lako halisi,, na ukiwa katika umbile la kijini pia huwezi kumchukua! kwa sababu damu yake ya yako zinamvutano,, ni damu moja.... hivyo ni lazima uingie katika kiwiliwili cha binadamu wa kawaida,, hapo ndipo utaweza kumchukua pasipo tatizo lolote!

    Tobi akaangaza angaza macho yake huku na kule.. kwa kutumia uwezo wake wa kijini.. akaweza kujua ni wapi wanapoishi wale wanandoa waliompa msaada Roda kumpeleka hospitali.. kisha akasema,, "nimeshapajua ni wapi wanapoishi.. wakatoweka kimiujiza kuelekea kwenye nyumba hiyo! CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Wakati huo huo alionekana Roda akiwa amemaliza kujiandaa kwenda kanisani kwa mchungaji,,, akatazama saa ya ukutani ilikuwa ni saa kumi na dakika kadhaa. akamchukua mtoto wake,, akambeba kwa kumkumbata kisha akatoka nje ya nyumba yake... akaelekea kwenye kituo cha daladala... kabla hajafika huko,, akaonekana mwanamke akimsimamisha Roda,, Roda akasimama,, mwanamke huyo ni yule nesi mwenye pete yenye uwezo wa kupambana na majini.. pia pete hiyo ni adui mkubwa wa majini!

    nesi huyo akasema najua huwezi kunikumbuka kwa sababu ulipoteza fahamu wakati unajifungua,, mimi ni nesi kwenye ile hospitali.

    Roda akatabasam,kisha akasema,, "asante sana mimi naishi maeneo haya haya.......kama hautojali twende ukapafahamu pia nashukuru sana kwa msaada wenu nimejifungua salama,, bila kuchelew. a wakaongozana kurudi nyumbani kwa Roda.

    walipofika Nesi huyo akambeba mtoto,, akashtuka akamtazama kwa makini mtoto huyo,,akaona anabadilikabadilika,,  anakuwa mtoto wa kutisha mwenye manyoya na masikio marefu,!!!, pia anaonekana kurudi katika umbile la mtotonwa kawaida!

    Roda akauliza,, unatumia kinywaji gani?

    nesi huyo akainua uso wake na kumtazama Roda,, akasema,, "usijali kwa sasa sijisikii kunywa kitu chochote. kwani ulikuwa unaenda wapi?

    Roda akajibu,, "nilikuwa naenda kanisani kwa mchungaji... lakini hakuna shaka nitakwenda tu kwa sababu hakuna umbali kutoka hapa nyumbani kwangu..

    Nesi huyo akasema,, "inaonekana unatatizo na tatizo hilo sina uhakika kama unalijua!

    Roda akashtuka,, akahisi huenda huyo ni Tobi kajibadilisha kwenye umbile la kike!

    mqcho yakamtoka akauliza kwa mshangao!  wewe umejuaje?

    nesi huyo akasema,, "mumeo yuko wapi? namaanisha baba wa mtoto huyu!

    Roda akazidi kuchanganyikiwa,, akabaki mdomo wazi!

    Roda akasema,, "yupo lakini katoka atarejea baadae.

    nesi huyo akasema,, "huyu mtoto wako anachembechembe za damu ya binadamu iliyochanganyikana na damu ya jini!

    Roda akaingiwa na hofu kupita kiasi! akasema,, "najua wewe ni Tobi kwanini unaninyima furaha katika maisha yangu?

    Nesi huyo akashtuka!  akauliza,, "Tobi ni nani?

    Roda akazidi kuchanganyikiwa.. akasema kama wewe sio Tobi ni nani?  na umejuaje haya yote?



    wati huo huo,,upande mwingine alionekana Tobi na mama yake wakijitokeza kwenye nyumba ya yulez mume na mke waliomsaidia Roda kumpeleka hospitali!

    wakawakuta wanandoa hao wamejilaza chumbani wamepumzika!  Tobi akaingia kwenye kiwiliwili cha mwanaume huyo huyo,, na Malkia wa bahari akaingia kwenye kiwilwili cha yule mwanamke...

    pumde si punde wakashyuka kutoka usingizini kwa wakati mmoja,, wakawa na wazo la kwenda kumtembelea Roda ke nyumbani kwake!

    bila kuchelewa wakajiandaa na kuingia ndani ya gari,, safari ya kwenda nyumbani kwa Roda ikaanza!

    walipofika wakaingia wakashuka kutoka ndani ya gari na kugonga mlango wa Roda.

    wakati huo Roda alikuwa anamsimulia nesi kila kitu kilichompata.. Roda akashtuka kusikia mlqngo unagongwa akajisemea moyoni,, "ni nani huyo anayegonga mlango?



    kule nje Malkia wa bahari akaanza kuhisi hali ya hatari,, akasema,, "bila shaka sehemu hii kunaadui yetu!

    pia Tobi akahisi harufu hiyo ya hatari... wakatoweka kimiujiza kutoka kwenye miili ya wana ndoa hao wawili!

    punde si punde wanandoa hao wakajishangaa, kujikuta hapo!

    wakaangaza angaza macho yao wakaliona gari lao!  mwanamke huyo akamuuliza mumewe,, "tumefikaje hapa?  mbonw kila nikivuta kumbukumbu sikumbuki kitu,, zadi ya kukumbuka kuwa tulikuwa nyumbani tumelala.

    punde si punde Roda akafungua mlango,, akashtuka kuwaona watu hao.. kisha akasema,, "karibuni.

    wanandoa hao wakatazamana usoni hawakuongea neno lolote wakaondoka zao na kuingia ndani ya gari kurudi nyumbani! huku wakiwa wametawaliwa na hofu kupita kiasi!



    Malkia wa bahari pamoja na Tobi wakajitokeza kwenye ufukwe wa bahari!

    pia jua lilikuwa tayari limeanza kuzama hivyo mpango wao ukashindikana.. wakatoweka kimiujiza kurudi ujinini kule chini ya bahari!

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati huo huo kule nyumbani kwa Roda alionekana bado akiendelea kumsimulia,, yule nesi mkasa wote uliompata.. nesi huyo akamuonea huruma sana,, kisha akasema hili ni tatizo usipokuwa makini utampoteza mtoto,, kwa sababu ni lazima waje kumchukua mtoto wao!

    kisha nesi huyo akanyanyuka na kumuaga Roda,, akamrudishia mtoto wake!

    Roda hakuwa na kipingamizi,, akaongozana na nesi huyo mpaka nje ya nyumba..nesi akaondoka zake Roda akaelekea kanisani kwa mchungaji... kwa bahati nzuri akamkuta mchungaji,, anatoka kwenye ofisi iliyokando ya kanisa lake.

    Roda akamsalimia mchungaji,, kisha akasimulia mkasa mzima..

    bila kuchelewa mchungaji akasema,," tuingie kanisani,, wakaongozana mpaka ndani ya kanisa,, Mchungaji akasema,, "mlaze mtoto huyo hapo juu ya meza.. nianze maombi.

    Roda akafanya kama alivyoagizwa na mchungaji, akamlaza mtoto pale juu ya meza.

    Mchungaji akaanza kufanya maombi......akiwa katikati ya maombi.. mtoto akaanza kulia kwa sauti kali kupita kiasi akaanza kubadilika na kuwa mtoto wa kutisha... punde si punde ukatoka mwanga mkali ndani ya mwili wa mtoto huyo... akarudi katika umbile lake la kawaida.. mchungaji akaendelea kufanya maombi kwa imani kali nila kusita.

    na baada ya dakika kadhaa kupita mchungaji akahitimisha kwa kusema,, "Amen.

    Mtoto akanyamaza,, kisha mchungaji akasema,, "sasa waweza kwenda lakininusisahau kusali mara kwa mara,, usisahau kumkumbuka Mungu wako!.

    wakati huo Roda alikuwa kabaki mdomo wazi juku macho yamemtoka akimtazama mtoto wake,, yani alikuwa aamini kile alichokishuhudia... mchungaji akasema,, "ondoa shaka Mungu yu pamoja nawe,, ukimuamini na kumtumikia yeye atakulinda kwa kila jambo..kisha mchungaji akazipiga hatua akachukua biblia moja na kumkabidhi Roda huku akisema,, "mara kwa mara jifunze kusoma maandiko ya kwenye biblia.....utajifunza mabo mengi ya kumtumainia Mungu muumba.

    Roda akaipokea biblia hiyo kisha akamchukua mwanae.. na kuondoka zake kurudi nyumbani!



                           **************************************



    Upande mwingine kule ujinini, alionekana,, Malkia wa bahari pamoja na Tobi...

    Malkia wabahari akasema kwa lugha ya kijini akimaanisha,, " tumechelewa na jua limeshazama! kule duniani usiku umeanza kuingia ambavyo huku kwetu ndio panaanza kukucha,, hivyo tutaifanya kazi hii kesho,,

    kama ilivyo kawaida viumbe wa kuzimu,, wanaishi tofauti na maisha ya binadamu! 

    huku duniani,,nyakati za mchana,, lakini huko kuzimu ni usiku wa manane..

    na huko kuzimu nyakati za mchana,,,, huku duniani ni nyakati za usiku wa manane..



    Kesho yake mipango ukaendelea wakajipanga kwenda duniani kumchukua mtoto wa Roda wampeleke ujinini.



    Kule nyumbani kwa Roda alionekana yupo sebuleni akiwa anasali kwa imani huku kashikilia biblia.. alipomaliza akaingia jikoni kuandaa chakula wakati huo mtoto alikwa kalala usingizi juu ya sofa.

    punde si punde Tobi na Mama yake(Malkia wa bahari akasema wakajitokeza ndani ya nyumba ya Roda upande wa sebuleni,, wakastaajabu kumuona mtoto haonekani kuwa na chembechembe zozote za ujini!  Malkia wa bahari akasema bila shaka hapa kunajambo limetendeka! haiwezekani iwe hivi.. punde si punde mtoto akashtuka kutoka usingizini akaanza kulia,, Roda akatoka jikoni haraka kuelekea sebuleni.

    akashtuka kumuona Tobi pamoja na Mwanamke mzee sana ambaye ndiye

    mama Tobi(Malkia wa bahari) Roda akakumbuka maneno ya mchungaji,, kuwa afanye maombi kwa imani mara kwa mara,

    bila kuchelewa Roda akaanza kusali huku akikemea kwa imani.. Tobi na Malkia wa bahari wakaanza kuhisi wanaunguzwa na moto mkali,, walipojaribu kutoweka kimiujiza ikashindikana.. wakaanza kupiga kelele za maumivu makali!

    Roda akaendelea kusali bila kusita.. punde si punde wakaanza kuwaka moto.. hatimae wakateketea kabisa na kubaki majivu... ikawa ndio mwisho wa Tobi ma Malkia wa bahari.

    Roda,,akamchukua mwanae haraka akambeba.. kisha akaichukua biblia na kuikumbatia.

    akaamua kufanya mpango wa kuhama ndani ya nyumba hiyo siku hiyohiyo.. akahamia Temeke,,

    siku zilizidi kusonga,, Roda hakuona mauzauza tena.. akaishi kwa amani na furahmiaka ikazidi kusonga hatimae mtoto akatimiza umri wa miaka kumi na nane(18) binti huyo anaitwa

    SIMA. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akashindwa kuvumilia kuificha siri kwa mwanae.. kwa sababu kila kukicha binti huyo alimuuliza mama yake kuwa baba yake mzazi yuko wapi... Roda akamsimulia mkasa wote... binti huyo akastaajabu sana,, lakini akajipa moyo kwa kumtumainia Mungu... huku akijisemea moyoni,, "Mungu ndiye muweza wa yote,, amenileta duniani kwa namna hii,, MUNGU ndiye baba yangu pekee.

    maisha yaliendelea,,wakaishi kwa amani na furaha.



                      ******************MWISHO******************

     

BAHARI YA HINDI - 4

 







    Simulizi : Bahari Ya Hindi

    Sehemu Ya Nne (4)





    Roda akashtuka akaingiwa na wasiwasi! Tobi akasema,,"jisikie huru mimi siwezi kikudhuru tatizo wewe ulienda kinyume na matakwa ya majini! katika safari yako uliyokuwa unasafiri kwenye meli...ulibeba kitu ndani ya begi lako..kitu hicho kilikuwa kinahabari kuhusu majini na viumbe wa kimiujiza!CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akashtuka! akajaribu kuvuta kumbukumbu,ilikuwa hivi!

    Siku moja Roda alidamka asubuhi,,akajiandaa haraka haraka kwenda kazini....Siku hiyo alidamka kachelewa...... .alikuwa anahitajika aende kwenye jumba la makumbusho ya kale,,akaandike habari inayohusiana na mambo ya yanayosadikika ya kimiujiza!!

    alipofika katika jumba hilo la makumbusho aliendelea kuhoji wahusika wanaohusika na kutunza historia ya makumbusho hayo...

    akiwa ndani ya jumba hilo katika pitapita zake akaona kipande cha sanamu! kipande chicho cha sanamu..kilikuwa kimetengenezwa kwa madini ya Rubi nyekundu.  akakiokota kipande hicho akakiweka kwenye mfuko wa suruali yake ya jinsi(kitambaa kigumu) aliyokuwa ameivaa..

    akaendelea na utafiti wa kuchambua habari zinazohusiana na majini na viumbe wa kimiujiza!



    wiki moja baadae,,akiwa kazini katika kituo cha habari ambapo alipokuwa anafanyia kazi..akaletewa barua kuwa anatakiwa aende zanzibar kukamilisha taarifa ambazo anatakiwa aziwasilishe kazini zikiwa kamili.

    pia akakumbuka kuwa siku ambayo alisafiri...aliweka nguo zote ndani ya begi lake kwa sababu safari yake ya kwenda Zanzibar..angebaki huko kwa wiki nne(4) mwezi mzima..miongoni mwa nguo alizoziweka ndani ya begi,,,ni ile suruali ya jinsi ambayo inakipande cha sanamu iliyotengenezwa kwa madini ya Rubi! kipande hicho alisahau kukitoa ndani ya suruali hiyo....

    akashtuka akasema,,"nimefanya nini mimi? kosa langu ni lipi? au tatizo ni kile kidubwasha nilichokiokota kule kwenye jumba la makumbusho?

    kitendo cha Roda kuita Rubi kidubwasha! kilimkasirisha Tobi!!!! akabadilika na kuwa na sura ya kutisha!!! meno yake ya mbele yakarefuka ndani ya sekunde moja....

    Roda akaingiwa na hofu kubwa kupita kiasi! hakuwahi kumuona Tobi katika muonekano huo!...

    Tobi akamsogelea Roda akamwambia,,"unanikosea heshima mbele ya Malkia wa bahari..ambaye ni mama yangu mzazi!

    kutokana na hasira Tobi akajikuta anamkaba shingo Roda kwa mkono wake...

    Malkia wa bahari akagundua kuwa mwanae Tobi kakasirika kwa sababu Roda kadhalilisha Rubi!!

    akamzuia Tobi asifanye jambo lolote baya kwa kusema,,"huyu ni mpenzi wako,,chaguo langu mimi pamoja na miungu wa bahari.nakusihi mwanangu isimdhuru binti huyu!

    Ghafla Tobi akabadilika na kurudi katika hali yake ya kawaida....akashtuka akamwambia Roda,,"samahani,haikuwa kusudio langu wewe ndiye amani ya moyo wangu....

    Roda alibaki kimya bila kujibu kitu chochote akimtazama Tobi kwa macho ya mshangao!

    Tobi akasema,,"nisamehe mpenzi..Roda akabaki akimshangaa Tobi!! kisha akamuuliza,,"kwa nini unaniita mimi mpenzi wako?

    Tobi akageuka nyuma na kuzipiga hatua kadhaa,kisha akajibu,,"nakuita mpenzi kwa sababu nakupenda na wewe ndiye chaguo langu..pia ni chaguo la Malkia wa bahari!

    Roda akashtuka akasema,,"mbona mimi sina hisia zozote za kimapenzi na wewe?

    Tobi akasema,,"kumbuka masaa kumi na sita yaliyopita tulikuwa kitandani ukasema kuwa umekubali kuwa wangu!

    Roda akaingiwa na wasiwasi akajilaumu kwa ule mpango wake aliodhani kwamba ni sahihi,,kwa kumkubalia Tobi ombi lake la yeye kuwa mpenzi wake!!!!



    Tobi akacheka kicheko cha sekunde tatu kisha uso wake ukawa kama mtu ambaye hajacheka!! akasema ,,"mimi siwezi kukudhuru bali wewe ndiye unataka kujiletea mauti.

    Macho yakamtoka Roda! baada ya kusikia kauli hiyo..akauliza kwa mshangao,,"Mauti?? mimi nimefanya kosa gani litakalosababisha uniuwe?

    Swali hilo lilimfadhaisha Tobi akajikuta amtazama Roda kwa macho ya huruma!

    Malkia wa bahari akatoweka kimiujiza! akamuacha Tobi na Roda wakiwa peke yao.

    Tobi akaongea kwa sauti ya chini,,"nakukupenda sana Roda..na sihitaji kukukosa..

    Tobi aliendelea kuongea maneno matamu yenye ushawishi wa asilimia mia moja(100%) Roda akajikuta anamuamini Tobi kwa asilimia zote!

    Roda akasema,,"nakupenda pia!...

    Tobi akafarijika na jibu la Roda lenye hamasa ya mahaba mubashara!!!! kisha akasema,,"haupo kwenye kifungo! mimi ndiye mkombozi wa maisha yako..Malkia wa bahari alitaka kuondoa uhai wako..kwa sababu ulibeba Rubi nyekundu ndani ya begi lako na ukapita juu ya himaya yake!!!

    lakini alishindwa kufanya hivyo kwa sababu wewe ni mtu muhimu kwangu..adhabu amboyo ulitakiwa upate wewe  akaamua kuwapa abiria wenzako....kwa kunywa damu yao.

    Roda akauliza,,"mama yako anakunywa damu ya binadamu?

    Tobi hakutaka kuongea ukweli kuhusu hilo akajibu kwa kudanganya,,"hapana aliwapa adhabu tu ya kawaida..CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akauliza kwa msisitizo,,!!"wewe umesema alikunywa damu ya abiria wenzangu!?

    Tobi akaamua kufanya miujiza ya nguvu za giza ilimradi Roda asiendelee kumuuliza maswali na asifahamu ukweli wowote kuhusu hilo!

    akatazama kando yake pakabadilika na kuonekana ni mbuga ya wanyama! kisha akamsogelea Roda na kumkumbatia..pumde si punde wakajikuta wamo ndani ya mbuga Ya wanyama! Roda akafurahi sana..mawazo yake yote yakatoweka yakahamia kutazama wanyama aliowaona mbele yake....

    Tobi akagumdua kuwa Roda amesahau kila kitu..akaamua kufanya jambo ili asije kukumbuka chochote..akamtazama machoni..ukatoka mwanga wenye rangi nyingi.ukaingia machoni mwa Roda...ukafuta kumbukumbu zote..

    Roda akawa hakumbuki kitu chochote alichokiona kabla.



    Tobi akamgusa Roda kichwani..pasipo Roda kujua kuwa Tobi analengo gani! Ghafla Roda akajikuta yupo nyumbani kwake akiwa chumbani.Roda hakuweza kugundua kitu chochote kilichotokea juu yake! kwa sababu Tobi alifuta kumbukumbu ya matukio yote yaliyotokea aliyoyashuhudia Roda machoni mwake..akanyanyuka kutoka kitandani,,akajiandaa kuelekea kazini...kabla hajatoka akasikia mlango wa sebuleni unagongwa!







    akaenda kuufungua...akamuona Tobi..Roda akatabadam na kusema,,"karibu.

    Tobi akajibu,,"asante nimekuja kukupitia twende kazini..

    Roda akasema,,"nilikuwa namalizia kujiandaa..

    Tobi akasema,,"sawa hakuna shaka wacha nikusubiri ndani ya gari...

    Roda akafunga mlango na kuendelea kuweka vitu vyake sawa.....



    Kule ndani ya gari alionekana Tobi,, uso wake ulikuwa umejaa tabasamu..punde si punde Roda akatoka ndani ya nyumba na kuufunga mlango wake..akazipiga hatua kulifuata gari la Tobi.

    safari ilaanza...walipofika kazini kazi zikaendelea kama kawaida,

    mmoja kati ya wafanyakazi wenzake akamfuata na kumuuliza jambo fulani...Roda akaonekana kishangaa baada ya mfanyakazi mwenzake kumuuliza mambo ambayo hayajui...

    Roda akasema mbona sikumbuki! kitu chochote kuhusu jambo uliloniuliza!

    yule mfanyakazi akaamua kuondoka kwa kuhisi kuwa Roda amemdharau!

    Roda akawasha kompyuta anayoitumia kuhifadhi kumbukumbu ya kazi zake! akastaajabu kuona ni mwaka 2017...akashtuka akahisi huenda kompyta yake imeharibu mpangilio(setting's)

    kumbe ni miaka kumi imepita tangu apelekwe kule ujinini..

    kumbe Tobi alifanya jambo la kimiujiza..miaka hiyo yote nafsi ya Roda ambayo ni kivuli chake ilikuwa inakwenda kazini kama kawaida..lakini ilikuwa ndani ya mwili wa mtu wingine...Roda halisi alikuwepo kule ujinini kwa kipindi cha miaka yote hiyo....

    Roda hakujali akaendelea kufanya kazi,bila kutambua yaliyotokea.



    siku zilizidi kusonga kusonga,,maishau yakaendelea...lakini Roda akilala nyakati za usiku.Tobi alikuwa anamtokea na kumuingilia kimwili,,pasipo Roda kujua chochote. Roda akawa anahisi ni ndoto,,lakini akajiuliza maswali mengi pasipokupata jibu,,"kwa nini  kila siku naota nafanya mapenzi na mtu ambaye siioni sura yake.na nikwanini ndoto hii ijirudie kila siku?



    siku zilizidi kusonga,,na miaka ikasogea.,,,,siku moja Tobi alikwenda nyumbani kwa Roda,,ilikuwa ni siku ya mapumziko ya kazi..

    Tobi akaanza kumchombeza Roda....

    Roda akaishia kutabasamh tu bila kujibu kitu chochote..wakaendelea kubadilisha mawazo kwa maingezi mbalimbali..

    Baada ya masaa mawili kipita Tobi akamuaga Roda na kuondoka zake.

    siku zilizidi kusonga..Tobi aliendelea kumtokea Roda nyakati za usiku na kifanyanae mapenzi pasipo Roda kufahamu...

    siku ya leo majira ya usiku wa manane..Tobi altokea Roda na kufanyanae Mapenzi...ghafla Roda akashtuka kutoka usingizini...akahisi kama kalowana sehemu zake za siri! akanyanyuka na kuwasha taa akashtuka kukuta kweli kalowana..alipojishika kwa mkono wake akagundua kuwa ni manii..macho yakamtoka akajisemea moyoni,,"ndoto gani ya namna hii...akaanza kuingiwa wasiwasi..akaamua kusali..kisha akaingia bafuni na kujisafisha mwili.

    alipomaliza akarudi chbani akapanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

                           ************************



    Asubuhi palipokucha,Roda akadamka akajiandaa na kuelekea kazini ....alipofika akaingia ofisini..Tobi akamfuata wakasalimiana kisha akamuuliza ,,"umeamkaje?

    Roda akasema niko njema..lakini kunajambo linanitatiza,

    Tobi akatabasamu akajua kile ambacho Roda anataka kumwambia.

    Roda akaanza kumwambia Tobi kuhusu ndoto anayoiota  kila siku! Tobi akacheka kisha akasema,,"hiyo ni ndoto tu, yawezekana kunamwanaume unampenda sana...na kama hayupo basi inaonekana umeishi muda mrefu pasipo kushirikiana kimwili...mawazo yako ndio yanakufanya wewe uote ndoto kama hizo!

    wakati huo Roda alikuwa anamsikiliza Tobi kwa umakini...kisha akasema,,"labda ni kweli kwa sababu ninamida mrefu sana sijashirikiana kimwili..sikumbuki mara ya mwisho ilikuwa ni lini!     

    Tobi akauliza swali la kimitego,,"bafo hujafikiria kuolewa?

    Roda akatabasamu kisha akajibu,,"kwa sass bado sijampata mtu ninayempenda..

    Tobi akadakia! akasema lakini kumbuka nilishakuambia kuhusu mahusiano baina yangu mimi na wewe laki hukunijibu chochote..uliishia kitabasamu tu....kwanini usinipe nafasi hiyo..nikumiliki....Tobi aliongea maneno hayo huku akimtazama Roda machoni..

    Roda akauliza,,"tangu nimekufahamu sijawahi kukuona ukipiga kope! unatatizo gani machoni mwako?

    Tobi akashtuka kwa sababu alijua kuwa majini hawana uwezo wa kupiga kope kama walivyo binadamu wakawaida!! akajibu kwa kudanganya,,"mimi ndivyo nilivyozaliwa hivi..

    Roda akastaajabu lakini hakujali..



    Ilipofika jioni ,,muda wa kazi ulikwisha,Roda akaondoka na kuelekea nyumbani kwake....akajilaz akabaki anatafakali,,kuhusu yale maneno ya Tobi..akajikuta anapitiwa na usingizi akasinzia!

    baada ya masaa kadhaa kupita akashtuka usingizini..alipotazama saa ilikuwa ni saa tano za usiku..akanyanyuka na kuingia jikoni..akachulua mayaianne akayakaanga ...kisha akachukua juisi ndani ya friji..akaanza kula na kunywa juisi hiyo..akaingia bafuni akaoga kisha akapanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi....

    ilipofika saa saba za usiku,,,Tobi akajitokeza mdani ya chumba cha Roda..akamtazama kwa macho ya matamanio akavua kofia yake aliyokuwa ameivaa kichwani..akafungua mkanda,,akapanda kitandani na kuanza kumuinhilia kimwili Roda....alipomaliza tu..Roda akashtuka kutoka usingizini..Tobi akatoweka kimiujiza....akasahau kofia yake juu ya meza iliyokuwemo ndani ya chumba cha Roda..

    Roda akajisemea moyoni,,"hivi ni kwanini huwa naota naingiliwa kimwili na mtu asiyeonekana sura yake? na nikwanini mdoto hii inajirudia kila siku?

    Roda akanyanyuka nabkuwasha taa...akashtuka kuona kofia ipo juu ya meza!!

    akaitambua kofia hiyo kuwa ni ya Tobi! akajiuliza moyoni,,"kofia hii imefikaje chumbani kwangu?

    nani kaileta humu..







    Roda akaingiwa na wasi wasi hofu ikazidi kuongezeka.. akatoka chumbani,, akaelekea bafuni,, akaoga kisha akarudi chumbani,, akashtuka,, macho yakamtoka alipotazama pale juu ya meza hakuiona tena ile kofia,, akajiuliza moyoni,, "hivi hii ilikuwa ni ndoto

    au niliona kwa macho yangu!!?  mbona akama niliona kofia hapa juu ya meza na nikaishika kwa mikono yangu! 

    basi kama ilikuwa ni ndoto,,,nahisi naanza kuchanganyikiwa.!

    Roda hakujali akapanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi..

    baada ya lisaa limoja kupita Roda alisinzia usingizi mzito.. Tobi akajitokeza chumbani kwa Roda,, akachukua shuka ndani ya kabati akamfunika Roda.. kisha akamvusu shavuni....

    Tobi akasimama wima,, akatoweka kiujiza. 



                      ************************

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Asubuhi palipokucha,, Roda alidamka na kujiandaa kwenda kazini,,

    baada ya nusu saakupita Roda alimaliza kujiandaa, kisha akaondoka zake, kuelekea kazini.

    alipofika akamuona Tobi anaingia ofisini kwake,, wakasalimiana,, lakini Roda alikuwa anaitazama kofia ya Tobi aliyoivaa kichwani.

    Roda akasema,, "usiku wa kuamkia leo,nimeota kofia yako,, imo chumbani kwangu juu ya meza kisha sikuiona tena,, Tobi akacheka akasema,, "inaonekana kuna habari njema kuhusu ombi langu kwako.. Roda akatabasamu akabaki kimya pasipokuongea neno lolote! 

    Tobi akasema wacha nikaendelee na majukumu ya kazi Tutaonge baadae.



        ******BAADA YA WIKI MOJA KUPITA******



    Roda akaanza kujisikia tofauti.. akawa anapenda kulala pia mwili wake ulikuwa na uchovu muda wote,, akaanza kupoteza hamu ya kula!!

    siku zilivyozidi kusonga Roda akawa anatapika mara kwa mara,, akahisi huenda anamaralia, akaamua kwenda hospitali kufanyiwa vipimo vya damu! 

    lakini majibu ya vipimo vya damu yakathibitisha kuwa hana tatizo lolote mwilini mwake,,

    Roda akaamua kurudi nyumbani kwake,, lakini bqdo hali hiyo ilijitokeza mara kwa mara,, akawa anatamani kula vitu vyenye uchachu, kama maembe mabichi na ndimu...

    hali hiyo ilizidi kumtesa kila siku,, akaamua kurudi hospitali..

    akafanyiwa vipimo vya mkojo na haja kubwa... majibu yalipotoka yakathibitisha kuwa Roda ni mjamzito!  anamimba ya mwezi mmoja!



    Roda akasema,,"wahusika wa kitengo cha maabara hawapo makini na kazi yao! yawwzekana wamechanganya vipimo vyangu na vya mtu mwingine mimi wina ujauzito na ninamwaka mmoja sijashirikiana kimwili! daktari akabaki mdomo wazi... Roda akazipiga hatua na kuondoka zake..

    akarudi nyumbani....



                     ***********************



    ilipofika majira ya saa sita za usiku.. alionekana Tobi akijitokeza kule ujinini,,, akamwambia mama yake ,,"nina habari njema,, Mchumba wangu anaujauzito!  Malkia wa bahari akafurahi sana akampongeza kijana wake, kisha akasema,,, sasa fanya haraka iwezekanavyo siku atakayozaliwa mtoto huyo hakikisha haupotezi dakika wala sekunde,, kumleta huku ujinini,, vinginevyo hawezi kuwa mwenzetu kqma akivuta hewa ya duniani kwa sekunde kumi na mbili(12).

    Tobi akasema sawa nimekuelewa ewe Malkia wa bahari,  kisha akatoweka kimiujiza kurudi duniani..

    miezi ilizidi kusonga Roda akawa haoni mzunguko wa siku zake kila mwezi,, akaona tumbo lake linazidi kukuwa kadri miezi ilivyozidi kusonga,, Roda akaanza kuingiwa na wasiwasi akafanya iwe siri yake.. lakini tumbo la mimba halifichiki,, hatimae wafanyakazi wenzake wote wakajua kuwa Roda ni mjamzito!! 

    Tobi akawa na ukaribu wa hali ya juu kwa Roda..

    akawa anamuuliza maswali ambayo majibu yake anayajua,, "hivi baba wa mtoto aliye tumboni mwako yuko wapi?

    Roda alikosa jibu, kwa sababu kila akijaribu kukumbuka mahusiano yake,, ni mwaka mmoja uliopita,, akilinganisha na umri wa ujauzito wake hakuna uwiano!!  kitendo hicho kilimfanya roda awe na hofu pia wasiwasi,,



    Siku moja nyakati za usiku wa manane,, Roda alikuwa kalala chumbani mwake,,, ghafla Tobi akajitokeza akaanza kulipapasa tumbo la Roda,, kisha akalibusu akanyanyuka na kuzipiga hatua

    Punde si punde Roda akashtuka kutoka usingizini,, akashtuka kumuona mtu anaishirizia ukutani,,, mtu huyo alioneka kavaa viatu na nguo zinazofanana na nguo na viatu vya Tobi..

    Roda akanyanyuka haraka kutoka kitandani... akachukua simu yake na kumpigia Tobi.... ukasikika mlio wa simu ikiita sebuleni kwake,, Roda akakata simu haraka kisha akapiga tena... simu ya Tobi ikaita kule sebuleni,,, Roda akaingiwa na wasiwasi.. hofu kubwa ikatanda juu yake,, akafungua mlango taratibu akatoka nje ya chumba chake,,, akazipiga hatua huku macho yake yakitazama kwa umakini mkubwa..... alipofika sebuleni,,  akahisi kamuona mtu anakatisha kuufuata mlango wa kutokea nje,,, hofu ikazidi kuongezeka... akachungulia,, hakuona mtu.. akaamua kurudi chumbani kwake.... alipogeuza shingo yake akaona tena miguu ya yule mtu inaishirizia kuingia chumbani kwake!!!!





    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akaingiwa na wasiwasi,hofu ikazidi kuongezeka,, akazipiga hatua za kunyatia kuufuata mlango wa chumba chake !  akaufungua lakini hakuona mtu yeyote kuwemo ndani ya chumba chake. Roda akaingia akaketi kitandani.. akajiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu,, akapanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi...

    lakini hakupata usingizi akabaki macho wazi mpaka pakakucha !!! akadamka na kujiandaa kwenda kazini......

    siku ya leo Tobi hakuja kumpitia Roda nyumbani kama ilivyo kawaida yake ! Roda akaamua kupanda daladala,,, alipoingia ndani ya daladala hilo akastaajabu kumkuta Tobi kaketi kwenye kiti ndani ya gari hilo,,,,akaamua kuketi kando yake kisha akamsalimia na kumuuliza,, "gari lako likowapi ? 

    Tobi akajibu,, "limepata hitirafu nimelipeleka kwa fundi...

    bqada ya nusu saa kupita wakafika mjini,, wakashuka kutoka ndani ya daladala na kuzipiga hatua kuelekea kazini ! wakiwa njiani Roda alimsimulia Tobi kuhusu matukio aliyoyaona usiku wa jana !

    Tobi akasema pole sana yawezekana unamawazo,, Roda akadakia na kusema,, "pia tumbo langu silielewi kadri miezi inavyozidi kusonga linakuwa kubwa !!

    nimeenda hospitali mara kadhaa,,vipimo vi. ethibitisha ninaujauzito !!  yani hata sielewi,, mimi sijashiriana kimwili takribani mwaka mzima ! 

    Tobi akacheka kisha akasema sio kweli kuhusu hilo ! mbona kila siku unashiriki kimwili,, pamoja na mwanaume unayemthamini na kumuheshimu !

    Roda akashtuka akamtazama Tobi kwa macho ya mshangao ! kisha akauliza,, "wewe umejuaje ?  kwa upande wangu mimi sijashirikiana kimwili mwaka mzima !!

    Tobi akasema siku ya leo ni siku maalumu kwangu,, nataka twende tukale chakula cha usiku pamoja ! Roda akauliza,, "mbona unakwepa swali langu ?

    Tobi akajibu,, "hapana nimeongea tu,, lakini ninauhakika na ulichokisikia,

    baada ya dakika kadhaa wakafika kazini..kila mmoja akaanza kufanya majukumu yake ya kazi !



    Ilipofika jioni,, muda wa kazi ukawa umekwisha, Roda akazipiga hatua kutoka nje ya jengo analofanyia kazi,, akakodi bodaboda impeleke nyumbani !

    akiwa njiani likaonekana gari la kubeba wagonjwa likiwa kwenye mwendo wa kasi.. gari hilo lilikuwa limewakaribia,, Roda akapiga kelele,," NAKUFAAA !!!

    punde si punde akaonekana Tobi akinyoosha mkono wake pikipiki ikainuka kama imebebwa ikatuwa kando ya barabara....watu wakatoka ndani ya magari yao wakatimua mbio,,,wakihisi pikipiki hiyo ni ya kichawi... Pia yule dereva bodaboda akashuka kutoka kwenye pikipiki akatimua mbio akihisi kuwa kabeba jini,, pia kitendo hicho kilimshua Roda.. akabaki mdomo wazi huku akiangaza angaza macho yake,,,kwa mbali akamuona Tobi anaishirizia kwenye ukuta wa jengo refu,, (ghorofa)

    Roda akatimua mbio kumfuqta Tobi.. alipolifikia jengo hilo hakumuona Tobi.. Roda akahisi kuchanganyikiwa !  akaamua kutembea kwa miguu mpaka nyumbani kwake !  alipofika akajilaza kitandani,, akasikia mtu anagonga mlango,, akanyanyuka kwenda kufungua... alipoudungua mlango hakukuta mtu yeyote kuwepo hapo nje !

    akafunga mlango na kurudi chumbani... akajilaza kitandani... alilala usingizi mzito kupita kiasi.... mpaka saa nne za usiku Roda alikuwa bado kalala,, Tobi akajitokeza chumbani kwa Roda, akamvua nguo zote kisha akamuingilia kimwili alipomaliza akaamua kujionyesha mbele ya Roda... akamuamsha Roda !

    Roda akashtuka kutoka usingizini.. alipofumbua macho akamuona Tobi kalala kitandani kando yake... akauliza kwa mshangao !!  umefikaje humu ???

    wakati anauliza swali hilo akagundua kuwa yupo uchi wa mnyama akakurupuka kutoka kitandani akaficha maungo yake kwa kutumia shuka lililokuwa kitandani.

    akahisi kalowana sehemu zake za siri akamtazama Tobi kwa macho ya uwoga wahali ya juu.. kisha akauliza,,, wewe ni nani ?

    Tobi akasema,, "unamaanisha hunijui ?  mimi ndiye baba wa kiumbe kilichomo tumboni mwako ! kamq unakumbuka nilikwambia kuwa siku ya leo ni siku maalumu kwangu ?

    leo nimeamua ufahamu ukweli kuhusu mimi.. mimi sio binadamu wa kawaida kama ulivyozoea kuniona,, mimi ni JINI.. lakini sina nia mbaya na wewe mimi nimekupenda.. na nimekumiliki kwa kipindi cha miaka kumi na moja sasa,

    Roda akastaajabu sana akauliza kwa mshangao !  ,,"unamaanisha wewe ni jini na si binadamu ?  Tobi akacheka kisha akajibu,, "ndio ni kweli kabisa uyasemayo !

    Roda akataka kufungua mlango atimue mbio.. kabla hajagusa kitasa Tobi akajitokeza mbele yake !  ni kitendo cha sekunde..

    Tobi akasema,, "usiniogope,, mimi ndiye baba wa mtoto aliyetumboni mwako.. sina nia ya kukudhuru.. nimekulinda kwa miaka yote hiyo pia muda na wakati umewadia !!  utazaa mtoto wa kike,,,.kisha Tobi akatoweka kimiujiza !



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

BAHARI YA HINDI - 3

 







    Simulizi : Bahari Ya Hindi

    Sehemu Ya Tatu (3)





    Piaa madhari ya nyumba hiyo ikabadilika na kuonekana ni ndani ya nyumba ambayo imechakaa kupita kiasi..yani kama nyumba ambayo imetelekezwa miaka mingi bila kuishi mtu ndani yake....Roda akaingiwa na hofu akatamani kupiga kelele lakini alishindwa!!

    Tobi akasema..mimi ninamiaka zaidi ya mia moja(100)tangu nizaliwe..lakini ninaishi katika umbile la binadamu wa kawaida tangu miaka arobaini iliyopita...

    Roda alishtuka kusikia maneno hayo aliyoyaongea Tobi.

    Roda akauliza kwa mshangao!!! ,,"inamaana miaka hiyo yote tuliyokuwa tunafanya kazi pamoja ulikuwa ni jini katika umbile la binadamu?

    Roda aliongea maneno hayo huku akimtazama Tobi kwa macho ya uwoga! mapigo yake ya moyo yalipiga kwa kasi zaidi.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tobi akajibu,,"ndiyo ni kweli kabisa hayo usemayo.

    Roda akageuza shingo yake kutazama huku na kule ili atimue mbio..lakini alishindwa hakuweza kuona sehemu ya kukimbilia...kwa sababu kila kona palionekana kutisha sana. punde si punde Tobi akanyoosha mkono wake,,ghafla muonekano wa nyumba hiyo ukabadilika..pakaonekana ni ndani ya jumba la kifahari..pia Tobi akajibafilisha na kuonekana muonekano wake wa kawaida!

    macho yakamtoka Roda! nisu atimue mbio..

    Tobi akasema..usiogope,,wala usikimbie kwa sababu hakuna sehemu ambayo utakimbilia.

    naomba unisikilize kwa makini, kuna jambo ambalo nataka nikueleze ujue..

    Tobi akaanza kusimulia..



    Ilikuwa hivi....Siku moja majira ya saa kumi jioni, ulikuwa na marafiki zako Coco beach..ukaingia bafuni kwenda kubadilisha mavazi...wakati unatika bafuni,,uliokota mkufu, ukauvaa mkufu huo wa dhahabu shingoni mwako,,ukaingia baharini kuogelea...mkufu huo ulikuwa ni mtego ambao Mama yangu Malkia wa Bahari aliutegesha..ili mimi niweze kurudi duniani na kuishi kama wanavyoishi binadamu wengine,,hii ni baada ya mimi kuuwawa na Binadamu aliyekuwa ni Mchungaji..

    wakati nipo kwenye mawindo yangu ya kutafuta chakula(Damu) mchungaji huyo aliniona akaniangamiza kwa maombi..nikafa na kurudi ujinini nikawa sina uwezo tena wa kurudi kuishi maisha ya Duniani..Mama yangu akatumia mkufu huo wa Dhahabu kuutegesha,,ili mtu yeyote atakayeuokota mkufu huo na kuuvaa shingoni mwake,,, mimi nitaweza kutoka ujinini na kuishi maisha ya Duniani...CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    lakini wewe ulipouokota mkufu huo na kuuvaa,,nikatokea kukupenda sana,, nikalazimika kukufatilia kila sehemu unakokwenda,, nikapajua kazini kwako..nikaja kuomba kazi ili tufanye kazi pamoja na kutengeneza ukaribu zaidi...

    nimekuwa nikishirikiana nawe kimwili kila nilipokuhitaji..pasipo wewe kujua...mara nyingi nilikuwa nakutokea usiku ukiwa usingizini,,lakini wewe ulikuwa ukiamini ni ndoto...La! hasha haikuwa ndoto, bali mambo hayo yalitendeka kweli....na nilikufunga kimiujiza ili usipendwe na mwanaume yeyote wala usimfikirie mwanaume mwingine zaidi ya mimi kuwa karibu yako kikazi.



    macho yalimtoka Roda akadakia,,"kwa nini ulinifanyia hayo yote?

    Tobi akasema,,"ni kwa sababu nakupenda sana.

    Roda akauliza kwa mshangao,,"UNANIPENDA!!!?

    nitawezaje kuwa na mpenzi jini?

    Tobi akacheka kwa sekunde kadhaa kisha akajibu,"inawezekana na ndio maana nimekuwa na mahusiano na wewe kwa miaka mingi pasipo wewe kujua,, nilitamani ujue lakini ungeniogopa na ndio maana nikafanya iwe siri yangu.



    **********************



    Roda akasema,,"naomba kurudi nyumbani kwangu tafadhali..kama kweli unanipenda naomba ufanye jambo hilo..

    Tobi akasema,,"hilo tu ondoa shaka lakini inabidi utimize masharti yafuatayo..

    kabla Tobi hajaanza kueleza masharti hayo..ghafla akaonekana yule Bibi kizee akiingia ndani ya jumba hilo la kifahari..

    Roda akaingiwa na hofu akasema,,"tafadhali nawaomba msinidhuru..nitafanya chochote mtakachokitaka..

    bibi kizee huyo(Malkia wa Bahari) ambaye ni mama mzazi wa Tobi akaongea maneno yaliyofanan na lugha ya kiarabu akimaanisha,"hakuna atakaye kudhuru,,lakini kuna kosa kubwa ambalo umelifanya,,na siku ya leo ndiyo imgekuwa mwisho wa uhai wako..umenusurika kwa sababu wewe ni chaguo la mwanangu wa pekee..amekuchagua ili akuoe..

    Roda akashtuka sana kusikia maneno hayo..pia alistaajabu ameweza kuelewa maneno aliyoyaongea bibi kizee huyo bila kujifunza lugha hiyo.

    Bibi huyo akazipiga hatua na kupita kwenye mlango bila mlango huo kufunguliwa!!



    Roda akauliza kwa mshangao! ,," unamaanisha kunioa niwe mke wako?? na itawezekana vipi wakati wewe si binadamu bali ni jini!

    Tobi akajibu,,"inawezekana hakuna tatizo kabisa.

    Roda akatumia ujanja akakubali ili Tobi asimdhuru

    lakini akilini mwake alikuwa makini sana,,huku macho yake yakimtazama Tobi muda wote..



    **********************



    upande mwimgine kule nje ya bahari(nchi kavu) palionekana ni mchana wa saa saba hivi.

    lakini kule chini ya bahari (ujinini) palionekana ni usiku wa manane,,masaa ya huko ni tofauti na masaa ya duniani...hivyo wakati binadamu wamelala usiku..Majini hutumia muda huo kufanya shughuri zao za kutafuta chakula(damu)

    kwa sababa kwa masaa ya ujinini inakuwa ni nyakati za mchana..



    Tobi akasema,,"nifuate,,aliongea hivyo huku akizipiga hatua kukifuata chumba kimojawapo kati ya vyumba vilivyokuwemo ndani ya jumba hilo la kifahari.

    Roda akamfuata Tobi kwa nyuma hukua akionekana kuwa na wasiwasi mkubwa,,wakaingia ndani ya chumba hicho kilikuwa kinanukia marashi,,

    Tobi akasema,,"Penzi la kweli halifi,,likifa haliozi,,na kama likioza harufu yake hupendeza

    Roda akauliza ,,"unamaanisha nini?

    Tobi akamsogelea Roda akambeba na kumlaza kitandani...

    Roda alikuwa makini sana kutazama Tobi anataka kufanya nini?



    ********************CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Roda akauliza swali la kimitego ili ajue namna ya kutoka huko ujinini  kurudi  duniani.

    Tobi akajibu..inawezekana lakink ni lazima kuzingatia masharti..

    Roda akauliza kwa kudadisi zaidi,,"masharti gani hayo? sasa hivi Roda aliuliza huku akitabasamu kumtega Tobi atoboe siri.



    Kama ilivyo kawaida mapenzi yana nguvu kuliko kitu chochote..Tobi akajikuta anaelezea siri ambayo haitakiwi binadamu yoyote wa kawaida ajue.

    Tobi akasema,,"ni lazima uvae pete maalumu..kisha akanyanyuka na kufungua droo akatoa pete iliyokuwa na jiwe la RUBI NYEKUNDU

    akasema,,"pete hii itamfanya binadamu wa kawaida atoke ujinini na kurudi Duniani ndani ya sekunde moja...naomba usiniogope sasa hivi sipo katika hali ya ujini mpaka nitakapokunywa damu ya mtoto mchanga..mimi ni yule Tobi uliyemzoea siku zote. kwa hiyo usiku wa leo tutalala wote kama binadamu wa kawaida kabisa..tafadhali usiniogope..

    Roda akamuita Tobi kitandani huku akitabasamu,,Tobi alikuja haraka,.akamkumbatia ..kisha akasema,,"tafadhali Tobi naomba tusifanye chochote usiku huu...na ninaomba uniahidi kuwa autanifanya chochote!

    Tobi akakubali kwa sababu alikuwa anampenda sana Roda..wakalala usingizi bila kugusana..

    Roda hakuweza kulata usingizi..akili yake yote ilikuwa inawaza juu ya pete ile aliyo onyeshwa na Tobi..



    Baada ya lisaa limoja kupita...wazo likamjia Roda akamtazama Tobi akamuona kalala usingizi mzito! Roda akanyanyuka kitandani taratibu,,akazipiga hatua za kunyatia akafungua droo na kuichukua ile pete ili aivae,aweze kutoroka na kurudi Duniani. ghafla yule bibi kizee (malkia wa bahari) akajitokeza..







    Roda akaivaa pete hiyo harakaharaka..punde si punde akatoweka!! ni kitendo cha sekunde moja akajikuta yupo ufukweni mwa bahari..akastaajabu kuona miamba mikubwa na miti mingi midago midogo!! akapanda juu ya miamba na kuanza kutafuta njia...lakini kila akitazama huku na kule..aliona kazungukwa na miti..Roda akaanza kuingiwa na wasiwasi akajisemea moyoni,,"hapa ni wapi? mbona hapaoneshi dalili ya mtu yeyote kuwahi kufika eneo hili!!

    Sehemu hiyo palionekana kutisha sana,,zilisikika sauti za ndege warukao...na ngurumo za upepo uvumao kwa kasi..

    Roda akaingiwa na hofu kubwa...



    *********************



    Upande mwingine kule chini ya bahari,,alionekana Tobi akiandaa mikakati ya kwenda kumnasa Roda amrudishe kwenye himaya yake..

    Yule bibi kizee (Malkia wa bahari) ambaye ni mama mzazi  na Tobi..akaamua kumuamuru jini mmoja aende duniani..akalete damu ya mtoto mchanga aliyezaliwa dakika hiyohiyo ili Tobi anywe aweze kurudi katika hali ya ujini...arudi duniani kwenda kumtafuta Roda.



    ****************



    upande mwingine kule Duniani lilionekana gari la wagonjwa(ambulance) likiingia ndani ya geti la Hospitali ya Muhimbili..gari hilo lilikuwa limebeba mama mjamzito..ambaye alikuwa ametimiza siku ziku ya kujifungua(kuzaa) manesi walimpokea mama hiyo harakaharaka na kumkimbiza kwenye chumba cha uzalishaji. mama huyo alijaribu kusukuma mtoto lakini ikashindikana....alitumia nguvu nyingi sana..akaishiwa nguvu akapoteza fahamu....

    madaktari wakaamua kumpeleka haraka kwenye chumba cha upasuaji ili wamfanyie upasuaji wanusuru maisha ya mtoto...CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ni kitendo cha sekunde kadhaa upasuaji ukaanza.

    apunde si punde akajitokeza mwanamke mmoja aliyevalia mavazi ya kidaktari huku kafunika pua na mdomo wake kwa kifaa maalumu wanachokivaa madaktari na manesi kwa ajili ya kutokuvuta hewa chafu wakati wa ulasuaji.

    mwanamke huyo akazipiga hatua hatua kadhaa akafungua mlango wa chumba cha uoasuaji akaingia upande wa ndani...wale madaktari waliokuwemo ndani ya chumba hicho wakashtuka..wakashangaa ni nani kaingia humo wakati upasuaji unaendelea!!

    yule mwanamke hakuongea neno lolote akakifuata kitanda maalumu kwa ajili ya upasuaji..akaanza kushirikiana na madaktari hao...mwanamke huyo kumbe ni yule jini aliyetumwa akalete damu ya mtoto mchanga aliyezaliwa dakika hiyohiyo..

    mwanamke huyo akazibadilisha akili za madaktari..wakajikuta wanamkata mtoto kwenye shingo pasipo wao kujitambua..

    damu nyingi zikaanza kutoka shingoni mwa mtoto huyo mchanga hatimae akafa...yule mwanamke jini..akaitazama damu hiyo ghafla damu hiyo ikatoweka....

    punde si punde mwanamke huyo naye akatoweka kimiujiza na kurudi ujinini..

    Ghafla akili za madaktari zikarudi katika hali ya kawaida...wakastaajabu kuona mtoto huyo kakatwa shingoni na ameshapoteza uhai..wakamtoa haraka tumboni na kuanza kuishona ile sehemu iliyopasuliwa ya mama wa mtoto huyo...

    madaktari walisikitika sana...tangu waanze kufanya upasuaji hawajawahi kufanya upasuaji wakamkata mtoto!!



    Baada ya lisaa limoja kupita..mama huyo alipata fahamu akawa na shauku ya kutaka kumuona mwanae...akauliza,,"mtoti wangu yuko wapi??

    nesi akasema,,"pole sana dada nasikitika kukwambia kuwa mtoto kafariki wakati unafanyiwa upasuaji.

    Yule mama akapata mshtuko wa moyo.. akapoteza fahamu...madaktari walijitahidi kumfanyia huduma ya kwanza lakini ilishindikana..tayari alikuwa amepoteza maisha dakika chache zilizopita..



    ************************



    Upande mwingine,,kule chini ya bahari ,alionekana

    Tobi akinywa damu..

    damu hiyo ni ya yule mtoto mchanga aliye uwawa kule hospitali, dakika chache zilizopita.

    Tobi alipomaliza kunywa damu hiyo akapata uwezo wa kurudi Duniani..akafumba macho yake akagundua ni wapi Roda alipo!!!,,akatabasamu..ghafla akatoweka kimiujiza



    Wakati huo huo alionekana Roda akiendelea kutimua mbio,,alikimbia bila kujua ni wapi aendako...

    Baada ya lisaa limoja kupita akatokezea kwenye barabara,,,akaanza kupata amani...akazipifa hatua za harakaharaka huku macho yake yakitazama huku na kule..

    Kwa mbali akaona gari limeegeshwa!! akaamua kulifuata gari hilo,,alipolikaribia akamuona mwanaume mmoja kafungua boneti analitengeneza gari hilo....Roda akamuongelesha mwanaume huyo...,,"habari yako kaka!!

    mwanaume huyo hakujibu kitu chochote aliendelea kulitengeneza gari lake!

    Roda hakuweza kuona sura ya mwanaume huyo kwa sababu alikuwa ameinamisha uso wake...

    Roda akasema,,"kaka nakusalimia...

    mwanaume huyo akageuza shingo yake,, na kumtazama Roda..

    Roda akashtuka akaanza kutimua mbio...





    Nibaada ya kumuona mtu huyo anafanana na Tobi kwa kila kitu..kuanzia sura mpaka mavazi!!

    Roda alikimbia huku analia...

    baada ya kukimbia umbali mrefu..akahisi kuchoka akaamua kutembea.....akaanza kuhisi njaa kali,,akiangaza macho yake huku na kule hakuina mtu hata mmoja kwenye barabara hiyo.....wasiwasi na hofu ikazidi kuongezeka!!

    akajikuta ametokezea kwenye makazi ya watu..akastaajabu baada ya kuona shamlashamla za watu wakisherehekea mwaka mpya!! Roda akamfuata mtu mmoja  akauliza,,"samahani dada,,nauliza eti haya ni maeneo gani?yule mwanamke akajibu..hapa ni kisiwani mpakani mwa Unguja na Pemba..

    Roda akashtuka sana,,akauliza tena,,"kwani kuna sherehe gani inaendea??

    yule mwanamke akashtuka akamtazama Roda kwa macho ya mshangao..akamuuliza,,"inamaana haujui kuwa leo ni mwaka mpya?CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akasema,"mwakampya kivipi?..mbona huu ni mwezi wa sita(6) !!

    yule mwanamke akasema leo ni tarehe 1/1/2017

    Roda akashtuka!...akajisemea moyoni inamaana tangu mwaka 2007??? ghafla kumbukumbu ikamjia akakumbuka Tobi alimwambia kuwa siku moja ya kule ujinini ni miaka kumi ya Duniani!!

    Roda akaingiwa na uwoga...kwa mbali akaona machinga anatembeza vioo vya kujitazama...akamfuata machinga huyo..akachukua kioo na kujitazama uso wake...akashtuka kuona uso wake unaonekana kama mama wa makamo kiasi!!! Roda akazidi kuogopa zaidi...akarudi kwa yule mwanamke..kisha akasemaa,,"mimi nimepotea...na wenzangu wote wamekufa baharini..baada ya meli tuliyokuwa tumepanda kuzama baharini...mimi niliogelea nikabahatika kufika nchi kavu..Roda aliongeaaneno hayo..yaliyokuwa na ukweli pamoja na uwongo kiasi ndani yake!!!

    mwanamke huyo akasema,,"pole sana kwa majanga yaliyokupata..nitakusaidia kukupa sehemu ya kujihifadhi wakati unafanya mipango ya kurudi nyumbani kwenu..

    Roda akafurahi sana kupata msaada...

    mwanamke huyo alikuwa anauza bidhaa ndani ya duka lake...lakini alionekana kumtazama Roda kwa macho ya msisitizo!!!

    Roda hakulitambua hilo...mwanamke huyo akasema,,"itabidi ukae hapa mapaka nitakapofunga duka tuelekee nyumbani kwangu.

    Roda akasema,,"sawa dada hakuna tatizo nakusikiliza wewe.

    yule mwanamke akauliza,,"umekula?

    Roda akajibu,,"hapana sijala nahisi njaa kali..

    wakati huo Roda alikuwa nje ya duka hilo kasimama...

    Mwanamke huyo alikuwa upande wa ndani ya duka akainama..alipoinuka akawa ameshikilia sahani yenye chakula...ilikuwa ni Chipsi kuku..

    Roda alipokea chakula hicho akaanza kula...

    lakini mwanamke huyo aliendelea kumtazama Roda kwa macho ya msisitizo...kisha akatabasamu..

    Roda alikishambulia chakula hicho mdani ya dakika tano tu..sahani ikawa tupu..akasema,,"asante sana dada yangu kwa msaada wa chakula.



    *************************



    Upande mwingine alionekana Tobi akijitokeza barabarani,,barabara hiyo ilikuwa tulivu...haikuonekana hata gari moja kupita kwenye barabara hiyo!!!akazipiga hatua kadhanaa akatoka kwenye barabara hiyo...akasimama kando kabisa.akanyoosha mkono wake..ghafla ikajitokeza ya nyumba moja iliyozungushiwa uzio akatoweka kimiujiza na kujitokeza mdani ya nyumba hiyo...



    ************************



    ilipofika majira ya saa kumi na moja za jioni..yule mwanamke akafunga Duka..

    Roda akajisemea moyoni,,"eneo hili hakuna biashara kabisa..yani tangu nimekaa hapa masaa yote hayo,sijaona mtu hata mmoja akija kununua hata kiberiti..mmh!!!

    Yule mwanamke alipomaliza kufunga milango ya duka lake akasema,,"tuondoke twende nyumbani.

    Roda akaongozana na mwanamke huyo..walitembea mwendo wa dakika saba,,hatimae wakafika nyumbani kwa mwanamke huyo..akatoa ufunguo kwenye pochi yake akafungua geti....wakaingia ndani ya uzio wakazipiga hatua kuufuata mlango wa kuingia ndani ya nyumba....akafungua mlango wakaingia ndani...akamkaribisha Roda,na kusema,"hapa ndio nyumbani kwangu...naishi na kaka yangu...nahisi atakuwa amelala wacha nimuamshe ili nimtambulishe kwako...

    Roda akatabasam,,kisha akasema,,"sawa hakuna shaka..

    Mwanamke huyo akazipiga hatua kuifuata korido ya kuelekea kwenye vyumba vya kulala ili amuamshe kaka yake akamtambulishe kwa Roda..

    Punde si punde akaonekana mwanamke huyo akija sebuleni huku kaongozana na Tobi...

    Roda alipogeuza shingo yake akashtuka kumuona Tobi..ghafla nyumba hiyo ikabadilika.....na yule mwanamke pia akabadilika akawa ni ye bibi kizee(malkia wa bahari) ambaye nia yake Tobi!



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

BAHARI YA HINDI - 2

 







    Simulizi : Bahari Ya Hindi

    Sehemu Ya Pili (2)

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wakati Roda anajiuliza maswali hayo..ghafla ikasikika sauti ya mtoto wa kiume ikiongea kwa lugha ya kiarabu,, sauri hiyo ilijirudia rudia(mwangwi) Roda akastaajabu..akachungua tena....lakini hakumuona mtu anayetoa sauti hiyo!!!

    akaingiwa na hofu akageuza shingo yake kutazama mbele ili atimue mbio kurudi kule sehemu ya abiria,, akashtuka kumuona yule mtoto akizipiga hatua kutokea kule sehemu ya abiria akija upande ambao Roda kasimama!!!Roda akaingiwa na hofu kwa sababu alimuona mtoto huyo kaingia chooni alafu sasa hivi anamuona anatokea kwenye sehemu ya abiria...

    yule mtoto akazidi kuzipiga hatua kumsogelea Roda...wakat huo  Macho yalikuwa yamemtoka Roda akataka kupiga kelele kutokana na mauzauza aliyoyaona....ghafla akaonekana abiria mmoja wa kiume akija upande huo huo kwa lengo la kwenda chooni kwa ajili ya kujisaidia haja ndogo,,,

    wasiwasi ukaanza kupungua kwa Roda....akamtazama yule mtoto kwa macho ya uwoga.

    yule mtoto akafungua mlango na kuingia chooni huku akimtazama Roda kwa macho ya msisitizo,,,,Roda akaamua kuzipiga hatua kutoka kwenye korido hiyo,,na kuelekea kule kwenye sehemu ya abiria...

    yule abiria wa kiume akafungua mlango na kuingia chooni....

    kabla Roda hajafika mnali akasikia sauti ya mtu akipiga kelele huku akigonga gonga mlango ufunguliwe atoke nje..ghafla sauti hiyo haikusikika tena...

    Roda akatimua mbio na kuelekea kwenye kiti chake..akaketi,,huku akipumua kwa mfululizo,,aliogopa hata kugeuza shingo yake kutazama kushoto wala kulia...ghafla wingu likatanda nda mvua ikaanza kunyesha.



    ***************************



    wakati huo huo upande mwingine walionekana mabaharia kadhaa wakiingia kwenye moja ya chemba inayoelekea kule kwenye injini za Meli...bila kuchelewa ukaletwa mtungi wa gesi maalumu kwa kuchoma(kuunganisha) chuma chepesi..na kazi ikaanza mara moja.

    wakaiziba paipu hiyo kisha baharia mmoja akatoka na kupandisha kule juu kumpa taarifa Sam kuwa tayari wameshamaliza kufanya matengenezo,,hivyo awashe mitambo Meli iwake na safari iendelee.....

    upande wa nje mvua kubwa iliendelea kunyesha mfululizo,,Ghafla!!! likaonekana wimbi kubwa kupita kiasi likiifuata meli hiyo...likaizonga na kuifunika Meli  ikatoweka kimiujiza..







    Hakuna abiria yeyote aliyefahamu nini kimetokea!

    Kwa sababu kilikuwa ni kitendo cha sekunde moja tu...Meli hiyo ikajitokeza kwenye sehemu tofauti kabisa...hata Sam(Nahodha) alishangaza sana kila akiangalia muelekeo ulionesha tofauti katika kifaa maalumu (DIRA) (COMPASS) cha kuangalia muelekeo wa meli inapokwenda..kilionesha meli hiyo inaelekea magharibi mwa bahari ya hindi..akashtuka akatazama nje ya meli hiyo kwa kupitia kioo cha Meli hiyo,,kilichokuwa maalumu kwa Nahodha kutazama ulande wa nje.

    Sam akashuka kuona bahari nyingine tofauti ma muonekano wa bahari aliyoizoea siku zote akiwa anakiendesha chombo hicho majini..

    akaamua kufungua mlango akatoka na kuelekea kwenye chumba cha abiria..akastaajabu kuwaona abiria hawana wasiwasi kabisa...wametulia tuli..

    Sam akaamua kuelekea  kwenye chemba inayotokezea ke chini kwenye injini za meli hiyo.

    alipofika akastaajabu kuwaona mafundi wa meli hiyo(mabaharia) wakiwa wanapiga stori bila wasiwasi! Sam akauliza,,"jamani mbona kama mimi naona meli inaelekea magharibi na bahari inaonekana tofauti kabisa inatisha kupita kiasi..wale mabaharia wakashtuka wakaamua kuingia kwenyechemba inayotokezea nje kabisa ya meli hiyo(upande wa juu)



    **********************

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    upande mwingine alionekana Roda akiwa bado kaketi kwenye kiti chake..lakini alionekana kuwa na wasiwasi na hofu kubwa...akanyanyuka na kuzipiga hatua kuelekea kwenye korido inayotokezea nje ya meli....kwa mbali akamuona yule Bibi kizee akiishirizia kwenye kona...Roda akashtuka akageuka ili arudi kwenye kiti chake..ghafla akakutana uso kwa uso na yule mtoto akiwa amesimama mbe yake..Roda akaingiwa na hofu,,macho yakamtoka huku mapigo yake ya moyo yakipiga kwa kasi ya ajabu..

    punde si punde taa zikazimika na kujiwasha zenyewe,, Roda akatazama ile sehemu aliyokuwa kasimama yule mtoto,,hakumuona tena...hapo Roda akagundua kuwa ile ndoto aliyoiota sio ya kawaida..na hicho anachokiona sasa hivi sio ndoto tena bali ni kweli,anashuhudia kwa macho yake...akatimua mbio kurudi kule sehemu ya abiria. ghafla taa zikazimika tena...

    abiria wengine hawakuwa na wasiwasi,,walijua huenda radi zilizokuwa zinapiga nje..zinasababisha,,mgusano wa nyaya (shot) ndio sababu taa zinazimika na kujiwasha zenyewe..

    Roda akashindwa kuvumilia akapaza sauti na kusema,,"JAMANI TUSIKILIZANE. humu ndani ya Meli kunamauza uza na nimeyashuhudia kwa macho yangu...

    kabla Roda hajaongea neno lingine ukasikika mngurumo wa kutisha sana..kisha taa zikazimika.

    sasa hivi taa hazikuwaka tena,,giza likatawala...ghafla ulengurumo ukatoweka..na ukimya ukatawala..

    taa zikawaka abiria wote wakaanza kupiga mayowe ya uwoga baada ya kuona baadhi ya abiria wakiwa wameuwawa na mtu asiye fahamika !! ni kitendo cha sekunde ikawa ni mtafutano ndani ya Meli hiyo..kila abiria alikimbia kutafuta sehemu ya kujificha lakini ikashindikana...kelele za vilio zilitawala ndani ya Meli hiyo..punde si punde..taa zikazimika tena!!!!

    abiria wote wakabaki kimya bila kujua hatma yao ni ipi?

    ikasikika sauti ya milango ya chuma ikijifunga...ghafla taa zikawaka....abiria walipojaribu kufungua milango haikufunguka ilikuwa imefungwa..hakuna aliyeweza kutoka nje ya Meli hiyo...



    *************************



    Upande mwingine,,walionekana mafundi wa meli hiyo(mabaharia)kule kwenye chemba ya kutokezea nje ya Meli hiyo wakiwa wanazipiga hatua mdani ya chemba....ghafla mlango ukajifunga...wakatimua mbio kuufuata mlamgo wa kutokezea nje kabisa,,walipoukaribia pia ukajifunga...kisha taa zikazimika...giza likatawala..lilikuwa ni giza totoro ambalo huwezi kuona kitu kilichopo mbele yako.. ghafla ikasikika sauti ya Baharia mmoja akipiga mayowe ya kuomba msaada...wale mabaharia wengine wakaingiwa na hofu!! punde si punde ikasikika sauti ya baharia mwingine akivurutwa na mtu asiyeonekana akapiga kelele ghafla sauti ikanyamaza na maji yakawarukia wale mabaharia wawili waliobaki ndani ya chemba hiyo..

    baharia mmoja akashtuka kumwagikiwa na maji usoni mwake..akajifuta maji yale akanusa...akashtuka kusikia harufu ya damu mbichi na sio maji!!! akamwambia mwenzake kuna hatari! hatupo sehemu salama..wakaanza kupiga kelele za kuomba msaada..



    kule kwenye upande wa injini zilipo alibaki baharia mmoja alikuwa ni mtumiaji wa kilevi aina ya bangi!

    alishindwa kuongozana na wenzake akabaki hapo kumalizia kuvita kipisi cha bangi..ghafla akasikia sauti za mabaharia wenzake wakiomba msaada..

    akaamua kuufuata mlango ili awafungulie wenzake..

    alipoufungua kikarushwa kiwiliwili cha mmoja kati ya mabaharia walioingia kwenye chemba hiyo..kikiwa nusu,,kuanzia kiunoni kushuka chini..

    kiwiliwili hicho kikadondoka mbele yake..akashtuka akajisemea moyoni,,"bila shaka hizi ni bangi zimenilevya, Binadamu gani anakuwa nusu!! akachuchumaa na kugusa damu,alipozinusa akagundua kuwa ni damu..akili ikamkaa sawa,,akanyanyuka haraka huku akiwa na hofu kubwa kupita kiasi..akaifuata chemba inayotokezea kule kwenye ulande wa abiria..gjafla akamuona ye Bibi kizee akiwa anazipiga hatua kuja upande wake..lakini alipomtazama kwa makini akaona Bibi kizee huyo miguu yake haikanyagi chini..anatembea hewani..

    alipogeuza shingo yake ili atimue mbio kutafuta chemba nyingine akakutana uso kwa uso na yule mtoto..wakatazamana machoni!! ghafla damu zikaanza kutoka machoni mwa Baharia huyo huku akihisi kukabwa shingoni..akakosa pumzi akashindwa kupumua akadondoka chini ma kupoteza maisha..CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    **********************



    kule juu sehemu ya abiria,,alionekana Roda akiwa anatafuta sehemu ya kujificha..kwa mbali akaona kuna  chumba kipo wazi hakijafungwa mlango akatimuabio kukifuata chumba hicho akajifiche..akaingia haraka ndani ya chumba hicho akaufunga mlango haraka.....akasimama kando..ghafla akasikia mlango huo unafujinga wenyewe kwa ufunguo. punde si punde taa iliyokuwa inamulika ndani ya chumba hicho ikazimika na giza likatawala....Roda akaingiwa na hofu kubwa kupita kiasi baada ya kusikia vishindo vya mtu akitembea ndani ya chumba hicho..





    Hofu ikazidi kuongezeka! akapiga kelele ghafla taa ikawaka.na mlango ukafunguka wenyewe.Roda akaogopa hata kutoka nje ya chumba hicho,akabaki kasimama,,

    Kelele za abiria wakipiga mayowe ya kuomba msaada zilitawala ndani ya meli hiyo..

    Roda akazipiga hatua za taratibu kutoka ndani ya chumba hicho huku macho yake yakitazama kwa umakini wa hali ya juu...alipotoka  ndani ya chumba hicho..akatimua mbio..kutafuta uwezekano wa kujificha...



    *************************



    Upande mwingine alionekana Sam akiwa amejifungia katika kile chumba maalumu cha kuiongoza meli...Sam alikuwa na wasiwasi kupita kiasi..akatazama upande wa nje,kwa kupitia kile kioo cha nahodha kutazama upande baharini.

    Sam akashtuka kuona Giza limetanda ndani ya sekunde moja...Sam akaogopa akafungua mlango na kutimua mbio kuelekea sehemu ya abiria,,akashtuka kuina abiria wote wanatafuta jinsi ya kutoka nje ya meli hiyo,,huku abiria wengine wakiwa chini wameuwawa...damu zilionekana kutapakaa kila kona ndani ya meli hiyo!! utadhani ni uwanja wa vita.



    *******************



    upande mwingine alionekana Roda akiendelea kutafuta sehemu ya kujificha.......alipoangaza macho yake kwa mbali akaona chemba moja ikiwa wazi..akaamua kuifuata chemba hiyo akaingia haraka akajifiche...akapita ndani ya chemba hiyo akajikuta anatokezea kule chini kwenye injini za meli hiyo.akatereza nakudondoka akaangukia juu ya maiti ya mmoja kati ya mabaharia waliouwawa...Roda akapiga kelele kwa sauti kalinmfululizo..akanyanyuka haraka akatimua mbio pasipo kujua ni wapi anaelekea...akaingia kwenye chemba nyingine..akapita humo akajikuta anatokezea nje ya meli(upande wa juu) akastaajabu kumkuta ye bibi kizee akiwa amesimama peke yake.bila kuonekana mtu mwingine yeyote...Roda akajificha akaendelea kuchungulia ili aone Bibi kizee huyo anafanya nini..

    akamuona ananyanyua mikono yake juu ghafla Bibi kizee huyo akageuza shingo yake haraka akatazama ule upande aliokuwepo Roda..

    sura ya Bibi huyo ikabadilika na kuinekana kutisha sana kisha bibi huyo akamfuata Roda huku anazioiga hatua hewani hewani..Roda akajikuta anapiga kelele akatimua mbio kuridi ndani ya chemba ghafla Roda akamuona ye bibi kizee ndani ya chemba hiyo akiishirizia mguu wa mwisho kutoka ndani ya chemba hiyo..

    Roda akahisi kuchanganyikiwa akaitimua mbio kurudi upande wa nje ya meli..akaufunga mlango wa chemba hiyo kwa komeo la nje..

    akaangaza angaza macho yake pande zote..kwa mvali akaona taa inawaka baharini..akagundua kuwa ni boti ndogo inakuja upande huo..akaanza kupata matumaini...

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ******************************



    upande wa ndani ya meli hali ilizidi kutisha zaidi..yule bibi kizee alijitokeza mbele ya Sam akakutanisha macho na Sam...ghafla Sam akabadilika  akuingiwa na roho ya kikatiri kupita kiasi...bibi kizee huyo akatoweka kimiujiza..

    Sam akaingia ndani ya meli akabadilisha muelekeo wa meli ikawa inaelekea mashariki mwa bahari ya hindi...aliiongoza meli hiyo pasipo yeye kujitambua mpaka ukingoni mwa bahari..kwenye sehemu iliyoonekana kuwa na mapango na miamba mikubwa kupita kiasi...Kwa mbali akaonekana mwanamke amelala nchi kavu akiwa.nusu binadamu nusu samaki...mwanamke huyo akajivuruta akaingia ndani ya bahari na kutokomea kusikojulikana..

    Roda alishuhudia tukio hilo kwa sababu alikuwa kule nje juu ya meli hiyo.pia taa kubwa ya meli hiyo ilimulika vyema ulande wa nje...hofu ikazidi kuongezeka akakosa pa kukimbilia..aliogopa kurudi ndani ya meli kwa sababu alishuhudia mauzauza na mauwaji ya kutisha..ghafla meli hiyo ikaanza kuzama taratibu kuelekea chini ya bahari...Roda akaingiwa na wasiwasi!! macho yakamtoka akatafakari nini cha kufanya lakini alishindwa akaamua kuruka kutoka juu ya meli na kujitosa baharini...akastahajabu maji hayamgusi..huku akizidi kuelekea chini zaidi..akaanza kupiga kelele..lakini kelele hizo hazikumpa msaada..akazidi kuelekea chini..akiwa ndani ya maji hakuweza kuona kitu chochote kwa sababu ya giza kuwa totoro...lakini alizidi kustaajabu akajiuliza,,"mbona maji hayagusi mwili wangu? yani kama nipo angani..wakati anajiuliza maswali hayo yasiyokuwa na majibu..ghafla akaanza kuona mwanga  chini ya bahari..mwanga huo ulimulika pakawa kama mchana...akaanza kuona majengo na magari ya kifahari huku watu wakiendelea na shughuri zao kama wapo nchi kavu....alipoangaza angaza macho yake akashtuka kumuona yule bibi kizee....

    Macho yakamtoka Roda ghafla akaangukia juu ya paa la nyumba..akashtuka akaingiwa na hofu kubwa kupita kiasi... punde si pundeikasikika sauti ikisema..ebu katazame nini kimedondika juu ya bati... Roda akajaribu kupiga mbizi akadondika kutoka juu ya paa la nyumba hiyo..akaanguka chini..wakati anatahamaki...yule mtoto akajitokeza mbele yake akagusa mwili wa Roda....yule mtoto akaanza kubadilika...ngozi yake ikaanza kujivua yenyewe mwilini..kumbe ni mwiko kugusa mwili wa binadamu wa kawaida..kitendo hicho kikamshtua Roda macho yakamtoka..ghafla akasikia sauti ya kitu kikidondoka kutoka juu..aliponyanyua shingo yake alishtuka kuiona meli ikiangukia hiyo sehemu aliyosimama..ni ile meli iliyozama muda mchache uliopita yeye akajitosa baharini..

    Roda akatimua mbio ghafla akavutwa na mtu asiyeonekana......







    Akajikuta yumo ndani ya jumba la kifahari.akashtka sana hakujua amefikaje fikaje ndani ya nyumba hiyo..akaangaza angaza macho yake. hakuina mtu hata mmoja kuinekana ndani ya jumba hilo la kifahari...akazipiga hatua za haraka haraka akaufuata mlango alipojaribu kuufungua mlango haukufunguka ulikuwa umefungwa kwa nje.,,,akaamua kuchungulia dirisha..akastaajabu kuona ile meli imegota chini..huku bahari imebadirika rangi na kuonekana ni damu tupu..damu hiyo ilizunguka kwenye eneo la meli hiyo pekee..Roda akaingiwa na hofu,,akajiuliza,,"hivi mimi naota! au naona kweli mambo haya yanatendeka!!!?

    Roda akanyanyua mkono wake akajipiga kofi..akahisi maumivu..akagundua kuwa hayupo katika ndoto bali anayaona mambi hayo yanatendeka kweli!!! macho yalimtoka..ghafla akamuona Mwanamke mrembo kupita kiasi..mwanamke huyo alikuwa anatokea upande wa ndani ya meli..huku mdomo wake ukiwa umezungukwa na damu...

    Roda akastaajabu kuona zile damu mdomoni mwa mwanamke huyo hazisambai wakati maji ya bahari yamemzunguka mwanamke huyo!!!.lakini mwanamke huyo alikuwa anazipiga hatua kama anatembea nchi kavu...Roda akatazama miguu ya mwanamke huyo haikuonekana ilikuwa imefunikwa na gauni refu lililokuwa linaburuza chini. ghafla mwanamke huyi akatoweka kimiujiza haikujulikana ni wapi kaelekea..

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akazidi kuchanganyikiwa..akajikuta anaangua kilio bila kujua hatma yake ni nini...

    kwa mbali akamuona yule bibi kizee akizipiga hatua kuifuata nyumna hiyo..Roda akaingiwa na wasiwasi,,hofu ikazidi kuongezeka..akatimua mbio akaingia kwenye chumba kilichokuwa karibu na sebule...akajifungia humo..akaangaza angaza macho yake akastaajabu kuona vitu vingingi vya thamani..vitu hivyo vilitengenezwa kwa madini ua dhababu tupu...ghafla kumbukumbu ikamjia! akakumbuka marehemu babu yake aliwahi kumsimulia kuhusu majini...pia akakumbuka kuwa makazi yao ni baharini sehemu yenye kina kirefu sana..ghafla akahisi kunusa marashi..marashi hayo yalinukia vyema kupita kiasi...

    akashtuka akajisemea moyoni,,"bila shaka nipo kwenye himaya ya majini.Eee Mungu ninusuru nitoke salama..



    Punde si punde akabmuona yule Bibi kizee kaingia ndani ya chumba hicho pasipo mlango kufunguliwa...bibi kizee huyo alioenda kwenye ukuta kama upepo na kujitokeza upande wa ndani.

    Roda akapiga kelele..lakini kelele hizo hata yeye mwenyewe hakuzisikia!!! ingawa alikuwa anapaza sauti kali lakini sauti haikutoka..

    yule bibi kizee akaketi kwenye kiti kilichokuwa ndani ya chumba hicho,, akaanza kumuongelesha Roda kwa lugha iliyofanana na maneno ya lugha ya kiarabu..Roda akabaki mdomo wazi huku amekodoa macho kumtazama bibi huyo...

    Ghafla Roda akanza kusikia na kuielewa lugha hiyo!! akajisemea moyoni,,"mbona sijawahi kujifunza lugha hii!!! iweje nasikia na kuelewa kile anachokiongea huyu bibi kizee!!?

    wakati Roda anawaza hayo yote..

    bibi kizee huyo akaonge tena kwa ligha hiyo..

    Roda akaelewa kilicho ongelewa bibi huyo alimaanisha kuwa,,"umefanya kosa kubwa ambalo ni vigumu kuepuka adhabu ambayo unastahiri kuipata..kulingana na kosa ulilolifanya.

    Roda akashtuka kusikia hivyo..hofu ikazidi kuongezeka,,mapigo yake ya moyo yakaanza kupiga kwa kasi zaidi huku jasho likimtoka kwa uwoga wa hali ya juu.

    ghafla bibi kizee huyo akatoweka kimiujiza!

    ikasikika sauti ya milango ikijifungua yenyewe..kila baada ya sekunde..

    Roda akatimua mbio kutoka ndani ya chumba hicho akaelekea sebuleni akashtuka kumuona Tobi ameketi kwenye sofa,,Roda akastaajabu sana akauliza kwa mshangao,,"na wewe wamekuleta huku??

    Roda aliuliza swali hilo huku akimtazama Tobi..lakini Tobi alionekana kutokuwa na wasiwasi kuwepo sehemu hiyo..

    furaha ya Roda ikaanza kurejea taratibu,,kwa sababu kamuona mtu wake wa karibu anaye fanya nae kazi katika kituo cha habari.

    (uandishi wa habari),,,Roda akazipiga hatua za haraka haraka mpaka kwenye sofa alilokuwa amelikalia Tobi..akamuuliza,"kulikoni mbona upo hapa!? hivi unaweza kuitambua sehemu hii?

    Tobi akatabasamu tu,bila kujibu kitu chochote.

    Akabaki kimya kwa sekunde kadhaa kisha akanyanyuka kutoka pale alipokuwa ameketi.akazipiga hatua kadhaa,,akasimama akageuza shingo yake na kumtazama Roda..

    Roda akaanza kuingiwa na hofu..alishangazwa na kitendo cha Tobi kutokuwa na wasiwasi kabisa..yani Tobi alionekana kama hapo ni nyumbani kwake..au sehemu anayoijua..

    Tobi akasema,,"Roda...mbina unaonekana kuwa na wasiwasi? kuwa huru jisikie upo nyumbani.

    Machi yakamtoka Roda baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kinywani mwa Tobi!!

    Roda akaingiwa na hofu akauliza kwa sauti ya msisitizo,,"nijisikie nipo nyumbani??

    Tobi acha utani hii ni sehemu ya majini!! wewe huogopi??

    Tobi akacheka kwa sekunde nyingi. kisha akasema,,"bila shaka haujakosea..hapa ni nyumbani kwetu nilipozaliwa..na yule bibi kizee uliyekuwa unaongea nae ni mama yangu mzazi..na yule mtoto uliyekuwa unamuona mara kwa mara ndani ya meli ni mimi..

    Rose akaanza kumuogopa Tobi!! akajisemea moyoni,,"inamaana Tobi kayajuaje haya yote wakati nilimuacha Mombasa pale bandarini baada ya yeye kusahau tiketi yake nyumbani!!!

    kumbe Tobi alikuwa anajua kila kitu anachokiwaza Roda akilini mwake..

    Tibi akasema,,"ni kweli uliniacha lakini tulisafari safari moja pasipo wewe kujua...lakini kini ulifanya kosa kubwa ambalo limemfanya mama yangu ambaye ni Malkia wa bahari kukasirika sana.

    Roda akadakia,,akauliza kwa mshangao,,"KOSA!!! KOSA GANI HILO?

    Tobi akajibu,,"kunakitu ulibeba ndani ya begi lako..

    pia kuna kitu umekivaa mwilini mwako..vitu hivyo ni adui wa Malkia wa Bahari.ambaye ni mama yangu.

    Roda akauliza kwa mshangao,,"mbona sikuelewi Tobi!! inamaana wewe ni jini??? na mbona haukuniambia miaka yote hiyo tuliyofanya kazi pamoja,,na wewe ni rafiki yangu wa karibu!!

    pia kwa nini usinge niambia tangu jana kabla sijaianza safari?

    Tobi akasema sio jani..ni miaka kumi imepita..sisi kwetu huku ujinini.siku moja ni miaka kumi kwetu.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roda akashtuka sana hofu ikazidi kuongezeka akamtazama Tobi kwa macho ya uwoga...

    Tobi akasimama akasema humu ndani,,hivi vitu vyote uvionavyo sio vipya kama uonavyo kwa macho yako,, wala hii siyo nyumba ya kifahari..Tobi  alipomaliza kuongea maneno hayo ghafla muinekano wa ndani ya  nyumba hiyo ukawa wa kutisha kupita kiasi..Punde si punde Tobi akabadilika na kuwa na muonekano kama mzee wa miaka tisini(90)





    ITAENDELEA

Blog