Search This Blog

UFALME WA NUGUTU - 2

 







    Simulizi : Ufalme Wa Nugutu

    Sehemu Ya Pili (2)



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mdidi kusikia vile akashtuka sana, akahisi labda wanamuadaha tuu ili wammalize, mwili wake ukahisi hatari ya kifo.

    "Jamani kwani nimewakosea nini hadi mtake kunimaliza, mimi sina hatia yeyote niacheni niende," alisema Mdidi.

    Hakuna aliyemuelewa Mdidi alichokisema, nyimbo zikaendelea yule mzee akamkabizi kifurushi kilichofungwa kwa magome ya miti na kusujudu tena na wengine wakafanya kama alivyofanya mzee. Mdidi akavipokea hatimaye usiku ukawa mzito na kila mmoja akalala isipokuwa mdidi ambaye hakuruhusiwa kutoka katika hiko kiti hadi jua litakapochomoza. Watu wote walishikwa na usingizi mzito sana, Mdidi akahisi kuwa ndio muda sahihi wa yeye kuondoka, akachukua vitu alivyokabidhiwa na kwa tahadhari kuu akapiga hatua ndefu na kutokomea msituni, hakujua anaelekea wapi hivyo ikamlazimu asubiri hadi jua litakapochomoza ili limpe muelekeo.



    ******************



    Katika jumba la kifalme mambo yanaonekana kuanza kuharibika waganga na wanajimu wakakusanyika kwa dhumuni la kutoa taarifa kwa mfalme Msongo,

    "Mtukufu mfalme! Jua na mwezi wa ufalme wako vinaonekana kuzingirwa na wingu zito, na hii inaashiria kuna mfalme mpya wa Nugutu atakaye kuja kukuvua na kujivika yeye"

    "Kwa hiyo nini kifanyike kuzuia ilo lisitendeke?" mfalme akauliza.

    "Unahitaji kuipata hazina ya Nugutu kabla ya huyo mwenzio hajaipata".

    "Na huyo mwenzangu ni nani?".

    "Mtukufu mfalme! huyo anayetishia ufalme wako ana damu sawa na ya kizazi chako ila tofauti yeye ana nguvu kukuzidi".



    Mfalme akazidi kuchanganyikiwa kutokana na maneno ya wale waganga ni wazi mtu anayeutishia ufalme wake ni ndugu yake, swali linalomjia je ni nani kati ya wadogo zake au watoto zake.

    "Nataka mniletee wazee wote waliokuwepo kipindi cha utawala wa baba yangu," Mfalme Msongo akatoa amri kwa washauri wake.

    "Mtukufu mfalme! Wazee waliokuwepo kipindi cha utawala wa baba yako tumewaangamiza na waliosalia wamekimbia hawapo ndani ya Nugutu, hivyo sio rahisi kuwapata kwa haraka".

    "Nahitaji kujua hazina ya Nugutu ilipo, japo nimekuwa mfalme lakini hazina ya kifalme siijui natakiwa niipate kabla ya mtu mwingine kuipata. Piteni nyumba kwa nyumba, kijiji kwa kijiji, hakikisheni kesho jioni mnanipa habari kamili kuhusu Hazina ya Nugutu".

    "Mapenzi yako yatimizwe eeh Mfalme!"

    Wakakubali agizo la mfalme na kuanza kupeleleza kama walivyoagizwa.



    *****************



    Jua lilivyoanza kuchomoza Mdidi naye akaanza safari yake, sababu alijua Nugutu ipo upande wa mashariki ivyo akaamua kulifata jua lilipotokea. Akatembea sana hatimaye akatokea katika mto ule aliokotwa akaangalia vizuri akajikuta amerudi eneo lile lile la kina Nkalo. akachoka kwa kweli ikabidi asogee hadi mtoni na kunywa maji, kwa mbali akaona kundi la watu kikifanya maombi na kutoa sadaka, moshi wa ubani na udi ulionekana kupaa, akaendelea kutazama vizuri lakini hakumtambua yeyote kati ya wale, akazidi kukodolea macho kwa nguvu lakini akashtushwa na maaskari waliokuwa wanazunguka maeneo hayo.

    "Wewe ni nani, na unataka nini?".

    "Mimi ni mtu wa Nugutu, nimepotea njia na nahitaji kurudi kwetu" Mdidi akawajibu.

    Maaskari wakatazamana kisha wakamshika na kuondoka naye, wakamfikisha kwa chifu wa kijiji hiko,

    "Mtukufu kiongozi wetu! Uishi miaka mingi, tumemkuta kijana huyu akiranda randa katika milki yako takatifu, na tulipomuhoji amesema yeye ni mtu wa Nugutu".

    Chifu alivyosikia kijana yule anatokea Nugutu, akasimama kwa hasira sana, na kusogea alipo Mdidi,

    "Sema ni nini mfalme Msongo amekutuma uje kuchunguza katika milki yangu, je hakutosheka na mali na mifugo aliyoichukua?"

    Swali lilikuwa gumu sana kwa Mdidi, hakujua lolote lililotokea au lolote lililopangwa na kufanyika kwa kivuli cha mfalme Msongo.

    "Mtukufu chifu! Mimi sifahamu lolote..,"

    Kabla hajaendelea kuongea akamuona Nkalo, moyo wake ukashtuka mno ndio hapo akili ikafunguka kuwa anayeongea nae hapo ni chifu Mzovu baba yake na Nkalo. Akaanza kubabaika kuongea, chifu akaamuru wamweke kwenye jela za wahalifu.



    Mawazo yakawa mengi sana, matumaini ya kutoka yakawa madogo akafikiri jinsi alivyo mkatili Nkalo leo, yupo kwenye himaya yake asee sijui nini kitatokea. Akamkumbuka sana mama yake hakujua hali yake iko vipi kwani ni muda mrefu toka aonane nae, akailaani ile siku aliyekubali kuingia jeshini akajuta sana.

    "haya yote yasingali nikuta kama ningekuwa mtu wa kawaida, rafiki niliowapenda na kuwaeshimu ndiyo hao walionisaliti na kutaka kuniangamiza, kwanini nakutana na haya yote, mimi ni nani hasa mbona sielewi!"

    Mdidi akajiuliza maswali mengi ambayo alikosa majibu, giza lilipoanza kuingia Nkalo akaja sehemu aliyofungwa. Wafungwa wote wakasimama na kuinamisha vichwa vyao, kasoro Mdidi ambaye hakuwa anaelewa lolote,

    "Wewe ndiye kiburi eenh! Nani aliyekupa mamlaka ya kutokutoa heshima kwa mtoto wa chifu," alisema askari ambaye alipewa jukumu la kulinda sehemu hiyo.

    Mlango ukafunguliwa na Mdidi akatolewa nje ya jela, akasogezwa aliposimama Nkalo,

    "Samahani mkuu sikua naelewa taratibu zozote za hapa?" alisema Mdidi.

    "Kutojua sheria hakuna maana utaepuka adhabu, umeonesha dharau kwa mtoto wa chifu na lazima uadhibiwe".

    "Sawa ni tayari kufanya lolote"

    "Mlete kwenye nyumba yangu" Nkalo akasema na kuondoka.

    Mdidi akachukuliwa hadi kwenye nyumba ya Nkalo na kusubiri adhabu toka kwa mtoto huyo wa chifu,

    "Utakuwa ukifanya kazi na kusikiliza kila ntakachokuamuru kwa muda wa siku 3, na usifikirie kutoroka sababu kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha yako" Nkalo akasema.

    "Lakini kwa usiku huu sioni kazi yeyote ya kuifanya niache niende kesho asubuhi nitakuwa hapa" Mdidi akasema.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nkalo akamruhusu mdidi arudi, huku akimsisitizia kuwahi asubuhi na mapema kwa ajili ya kuianza adhabu yake.

    "Duuh! Wee dogo umerudi mzima?"

    "Mhm! unabahati sana mdogo wangu hakuna aliyefanya kosa kama lako akabaki hai".

    "Daah! Bila shaka binti wa chifu amempenda huyu jamaa, nafasi hiyo dogo itumie vyema ila baba yake hakigundua umeisha".

    Kila mfungwa akaongea lake lakini Mdidi akawa anafikiria tofauti kabisa na wao. Asubuhi na mapema Mdidi akawasili na kusikiliza maagizo toka kwa binti chifu,

    "Kazi yako kabla ya jua la utosi ni kupalilia bustani iliyo hapa"

    Mdidi akainamisha kichwa kutoa heshima zake kisha akachukua jembe na kuanza kufanya kazi, kadri alivyozidi kufanya kazi ndivyo nguvu zilizidi kuongezeka tofauti na wengine huwa wanachoka kadri wanavyofanya kazi, akuchukua muda akawa amemaliza kazi aliyopewa. Chifu Mzovu akapita kumtazama binti yake akashangazwa na kazi aliyoifanya Mdidi.

    "Mhm! kuna kitu ambacho si cha kawaida kwa huyu kijana" Chifu akasema pindi alipofika kwa binti yake.

    "Ni kweli baba hata utendaji wake ni watofauti mno"

    "Atakuwa ni nani hasa huyu kijana?" chifu aliuliza.

    "Baba mimi naona tumuache aende zake sababu sioni hatia yeyote juu yake" alisema Nkalo.

    "Mchunguze nahitaji kumjua kiundani zaidi, tumia kila njia uijuayo hakikisha anakwambia ukweli"

    Agizo hilo la baba yake lilikuwa kama kumkabizi fisi bucha, Nkalo alitamani sana nafasi hiyo, na sasa akaipata hivyo hakutaka kufanya uzembe.

    "Sitokuangusha baba"







    Chifu akatabasamu na kuondoka. Nkalo ikabidi aende alipo Mdidi na kumita,

    "Mdidi...!"

    "Naam malkia"

    "Nifuate!"

    "Sawa malkia"

    Nkalo akaenda hadi pembezoni mwa mto kisha akakaa na kumtaka Mdidi akae nae akafanya kama alivyoambiwa na binti huyo.

    "Hivi kwanini haukuitikia nilivyokuita ile siku?"

    "Samahani! Naomba tusiongee kuhusu hayo".

    "Kwanini? basi tuu sitaki kukumbuka",

    "Hivi Mdidi wewe kwa nini ni jeuri, kwanini hutaki heshimu hisia za wengine?"

    "Nkalo japo sijawahi kuingia katika mapenzi lakini macho yangu yameshuhudia, mapenzi huwa matamu na yenye bashasha pindi yanapoanza lakini kadri ya muda unavyozidi kwenda ile furaha ubadilika na kuwa huzuni," alisema Mdidi.

    "Unawezaje kuyapima maji usiyoyavuka?  Mdidi! Siwezi kuishi bila ya wewe, uwepo wangu ni kwa sababu yako tuu, Mdidi natamani kukuacha uende lakini siwezi, sitamani umbali kati yako na yangu, nakukabidhi moyo wangu tafadhali naomba uupokee," alisema Nkalo.

    Nkalo aliendelea kuongea maneno matamu ambayo kiukweli yalivutia kuyasikiliza, akatumia pia viganja vyake kumkoleza zaidi mdidi ambaye ni wazi alionekana si lolote si chochote kwenye ulimwengu wa huba, mapigo ya moyo yakaongeza kasi, damu ikazunguka kwa haraka mno, kwa mara nyingine tena Mdidi akahisi hali ya utofauti mwilini mwake.

    "Nkalo samahani.......!"

    Lakini mwanadada yule aliyeo

    nesha amefundwa akafundika akaujua udhaifu wa Mdidi akazidi kumchawisha kwa maneno mwanana, kabla hajafika popote Mdidi akamsukuma Nkalo na kunyanyuka pale walipokaa,

    "Nkalo mimi ni mfungwa wako sikatai, nipe adhabu yeyote nitafanya lakini hii siiwezi," akasema Mdidi.

    Nkalo akapandwa na hasira mno kutokana na kitu alichokifanya Mdidi, akafikiri jinsi wanaume wengi wanavyotafuta nafasi ya kuwa naye na kuikosa. Akamuangalia mdidi kwa jicho la ghazabu Zaidi.

    "Mdidi ondoka na usirudi tena huku, la sivyo shingo yako itakuwa halali yangu," akasema Nkalo.

    Kukataa kitu ambacho mtoto wa chifu anakitaka ni sawa na kugomea mamlaka ya chifu na hamna adhabu nyingine yeyote zaidi ya kifo cha aibu. Mdidi kumkataa Nkalo ni kosa kubwa ambalo lingeweza kutoa uhai wake lakini kwa kuwa Nkalo anamhusudu Mdidi akaamua kumuacha aende zake. Mdidi akufikiri mara mbili akaanza kupiga hatua ndefu na kuondoka, lakini kabla hajatokomea zaidi akakumbuka amesahau kifurushi chake kwenye sehemu aliyofungwa ikabidi arudi kwa kasi akakutana na Nkalo uso kwa uso,

    "Kuna kitu nimekisahau tafadhali naomba nikakichukue ni muhimu sana"

    Mdidi akamwambia Nkalo nae akamwambia asubili, akamuagiza kijakazi wake akakifata baada ya muda mfupi akawa amerudi na kumkabidhi, Mdidi akamshukuru na kuondoka.



    ********************



    "Mfalme mtukufu, uishi miaka mingi...! Tumebahatika kudodosa na kupata taarifa kuhusu hazina ya Nugutu, Mfalme mtukufu Hazina hiyo haiwezi kufikiwa na mtu yeyote asiye kuwa mfalme, hazina ina siri nzito kuhusu Nugutu na kuna ramani moja tuu itakayo kuwezesha uifikie hazina hiyo, ramani iyo ipo miongoni mwa wananchi wako".



    Kiongozi aliyeagizwa na mfalme kufatilia swala la hazina ya Nugutu akasema hayo, mfalme akafikiri kidogo kisha akasema,

    "Toa taarifa kwa machifu wote nawaitaji wafike hapa kesho asubuhi na mapema..."

    "Matakwa yako yatimizwe eenh mfalme.

    Taarifa ikasambaa kwa machifu wote na viongozi wote wa Nugutu, hivyo asubuhi na mapema wakawa tayari katika ukumbi ambao wanautumia kwa ajili ya vikao mbali mbali vya nchi.

    "Kitu kimoja nahitaji mkifanye pindi mkitoka mahala hapa, hakikisheni mnaipata ramani yenye kuonesha hazina ya Nugutu, nimesikia ipo miongoni mwa wananugutu, hivyo waambieni mfalme anatoa siku 3 tuu, yeyote atakayekutwa nayo basi kifo halali yake".

    Mfalme msongo akafunga mkutano wake na machifu kwa maneno hayo, kisha wakatawanyika. Tangazo likawafikia wananchi wote wa Nugutu na kila mtu akaanza kupekua na kuitafuta ramani iyo, lakini hadi siku 3 zinaisha hakuna aliyefanikiwa kuiona, Mfalme akachukia mno, hakuamini kama angeweza kuikosa ramani ndani ya milki yake, akaamuru jeshi lake lifanye upekuzi kwa kila aingiaye na atokaye Nugutu, na akatoa amri kwa yeyote ambaye atakutwa na vitu vyenye kuhusiana na Miungu ya Nugutu akamatwe na kuhojiwa, Jeshi likatii amri ya Mfalme na kujipanga katika mipaka yote ya Nugutu.



    **********************

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mdidi akiwa amechoka baada ya kutembea umbali mrefu mno hatiamye akatokea kwenye mpaka wa kuingia Nugutu, akashangaa kuona jeshi kubwa likiwa limezagaa pale mpakani. Hakuelewa nini kinaendelea kwa bahati akapita kijana wa rika lake akamsimamisha

    "Habari yako ndugu!"

    "Nzuri tuu sijui wewe..!"

    "Kwangu pia ni njema, Samahani naomba kukuuliza!"

    "Bila samahani ndugu yangu"

    "Kuna nini mbona wanajeshi ni wengi kuliko kawaida pale mpakani...!"

    "Aah! Ndugu yangu wewe ni mgeni?"

    "Hapana ila nina muda mrefu toka nitoke Nugutu".

    Yule kijana kabla hajajibu akaangalia huku na huko, alipojiridhisha akavuta pumzi ndefu na kusema

    "Nugutu imeingia katika sintofahamu, mfalme anahisi kuna mtu anakuja kunyakuwa mamlaka yake, hivyo kabla ya yote kutimia anaitaji kupata ramani itakayomuwezesha kufika katika hazina ya Nugutu"

    Mdidi aliposikia hazina ya Nugutu akashtuka mno akaupeleka mkono wake kwenye kifurushi alichobeba akakumbuka kauli aliyoisema yule mzee pindi alivyokabidhiwa kile vifurushi.

    "Vipi mboni umeshtuka kusikia hazina, je unajua lolote kuhusu hazina?"

    "Hapana sina nilijualo" Mdidi akajibu,

    "Haya na wanajeshi unaowaona pale wanafanya msako wa ramani hiyo au kitu chochote kitakachohusishwa na hazina ya Nugutu!"



    Mdidi akamshukuru sana jamaa kwa kumjuza, ikabidi akae chini na kuanza kutafakari jinsi atakavyo pita bila kukamatwa sababu alijua wazi kuwa lazima atashikwa na kile kifurushi alichokuwa nacho,

    "Kwani mimi ni nani, nini natakiwa nifanye, mboni sijielewi" akajikuta akijipa maswali mengi ambayo alikosa majibu yake.



    Baada ya muda akaona kundi kubwa la wafanya biashara za nafaka wakiingia Nugutu, akaamua kuungana nao ili kupunguza ukali wa msako, akaongea na mkuu wa msafara kuwa hakuwa na kibali cha kuingia Nugutu na anahitaji kuingia. Mkuu wa msafara akamuelewa na kumkabidhi moja kati ya mizigo abebe, wakatembea na kulifikia lango la kuingia Nugutu wakasimamishwa na kuanza kupekuliwa mizigo yote. Hawakupatikana na kitu wakaruhusiwa kupita, hapo moyo wa mdidi ukatulia walivyokaribia kulimaliza lango la kuingia Nugutu wakasimamishwa tena.

    "Samahani mkuu, tulipekuwa vifaa vyenu na tukasahau kuwafanyia ukaguzi watu wako," akasema mmoja kati ya askari aliyeonekana kuwa kiongozi.

    "Kwa hiyo unawasiwasi na msafara wangu?" yule mkuu wa msafara akauliza kwa hasira.

    "Ni wajibu tuu mkuu"

    Alipomaliza kuongea ukaguzi ukaanza kwa mmoja hadi mwingine, hadi kufika hapo mdidi akaamini kuwa tayari ashashikwa, ikafika zamu yake akafumba macho sababu aliamini awezi kuponyoka hapo.





    "Bang'ala! Waache waende hao njoo huku kuna wengine wakuwakagua" ilikua amri ya mkuu wa pale juu ya askari aliyekuwa akimkagua Mdidi.

    Askari akamuachia mdidi na kwenda eneo aliloitwa, Mdidi akashukuru Mungu mno, maana alijua wazi kuwa asingeweza kuponyoka pale. Msafara ukaendelea walipoingia kijijini kabisa mdidi akamshukuru yule mkuu na kuendelea na safari yake.



    Ni muda mrefu toka Mdidi aondoke hapo Nugutu wengi waliamini amefariki kama taarifa ya wanajeshi wenzie ilivyowafikia kipindi kile walivyokuwa mafunzoni. Mdidi akajongea hadi alipokuwa akiishi mama yake, alipofika akakuta kuna msichana mrembo sana, alipomtazama akamfananisha na Nkalo, Mwenye kiuno cha nyigu, macho ang'avu, tabasamu la hamu. Wakati Mdidi akiendelea kuutafakari uumbaji wa mungu kwa yule msichana, akashtusha na sauti yake,

    "Wewe ni nani na unataka nini hapa?"

    "Labda nikuulize wewe mwenzangu ni nani, sababu hapa ni kwetu," alijibu Mdidi. 

    "Kwenu! kaka samahani sana, naomba uende kabla sijapiga kelele za kukuita mwizi," alisema yule Msichana.

    "Mwizi! utawezaje niita mwizi ndani ya nyumba yangu mwenyewe, hata hivyo sina muda wa kubishana nawe, nambie mama yangu yukwapi?"

    "Eeh! Mama yako wewe mimi ananihusu nini au nitamjua vipi?".

    Mdidi alipoona maelewano yamekuwa madogo akaingia kila kona ya nyumba na kumuita mama yake lakini hakukuwa na dalili yeyote ya uwepo wa wake, Kipindi hiko chote yule msichana akabaki akimtazama tuu,

    "Nambie mama yangu yukwapi?"

    Mdidi akamsogelea yule msichana na kumuuliza lakini kabla hajajibiwa akasikia sauti ya kiume ikiita,

    "Balanoga! Balanoga! Njoo umpokee mama yako mzigo".

    Mdidi akatazama kule sauti inapotokea akakutana uso kwa uso na mzee mmoja wa makamo, ambaye hakuwa anamfahamu, wakati akiendelea kuduwaa akatokea yule mama ambaye alifikiri anaweza kuwa mama yake lakini haikuwa vile.

    "Wewe ni nani? Unataka nini nyumbani kwangu?”

    Swali lile lilimchanganya Mdidi kwani aliamini kabisa pale ndipo alipokuwa akiishi miaka 4 iliyopita.

    "Samahani mzee wangu! Nyumba hii nilikuwa nikiishi na mama yangu, lakini sasa ni miaka 4 imepita toka niondoke Nugutu, na niliamini kuwa nitamkuta mama yangu hapa"

    "Mama yako anaitwa nani?"

    "Mlali"

    Yule mzee akashtuka aliposikia jina la Mlali,

    "Ndiyo mzee wangu",

    "Kwani wewe ndiye Mdidi?" mzee akauliza tena kwa mshangao.

    "Ndiyo ni mimi"

    Wote mle ndani wakapatwa na mshangao mkubwa zaidi ya wa mara ya kwanza,

    "Maskini Mlali kumbe alikuwa sahihi na hisia zake" mama yake Balanoga akaingilia kati maongezi.

    "Unamaana gani kusema hivyo mama?"

    Yule mama akavuta pumzi ndefu na kumtazama mumewe kisha akamtazama Balanoga, machozi yakamtoka, Mdidi alivyoona hivyo kengele ya hatari ikagonga kichwani mwake, naye akajikuta akitoa chozi.

    "Sasa mboni unalia, nambie kitu kuhusu mama yangu!"

    Yule mama akashindwa kusema lolote, alipomgeukia Balanoga nae akaondoka huku machozi yakitoka, akazidi kukosa nguvu alipomtazama mzee nae akawa na huzuni kubwa, Mdidi machozi yakaongezeka.

    "Tafadhari naomba msiniache njia panda, niambieni nini kimemkuta mama yangu"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *************



    Jioni ya siku hiyo mwezi wa Nugutu ukafifia nyota zikawa hazina nguvu, wingu zito lilitanda,

    "Njooni muone ukombozi wa Nugutu, tuliokuwa tukiisubiri ishara hii kwa zaidi ya miaka 20 sasa, hatimaye leo tumeiona na mkombozi wetu yu karibu, itukuzwe miungu ya Nugutu, Itukuzwe........"

    Itukuzwe..!"

    Watu wote wakaitikia na kusujudu, ni kijiji kimoja kilichopo upande wa kaskazini na nje kidogo ya nchi yaNugutu, ni kijiji pekee ambacho kwa siri kinaendeleza miiko na ibada kwa miungu ya Nugutu.

    "Ni lazima tuikabidhi ramani hii kwa uyo mrithi ambaye miungu ya Nugutu imetuletea" akasema mzee ambaye alionekana kuwa kiongozi katika eneo hilo, watu wakajawa na furaha na tumaini la ukombozi likachipuka mioyoni mwao.

    "Hakikisheni hamna yeyote anayetoa siri juu ya haya mambo hadi pale yule mrithi atakapo pewa mamlaka kamili juu ya milki hii ya Nugutu. Wote tutashuhudia anguko la ufalme wa Msongo lakini tunaitaji kulinda siri hii kwa nguvu zote na nimesikia kuna msako wa ramani yenye kuonesha hazina ilipo hivyo tunahitaji kuwa makini kwa kila tulifanyalo," aliongea Kiongozi wa kijiji hiko ambacho kwa sehemu kubwa kimezungukwa na msitu na majabali makubwa akaongea na wote wakatii.



    ***********



    "Mdidi taarifa ya kifo chako ilimfikia mama yako miaka 4 iliyopita, alihuzunika sana na akawa mtu wa kulia na kujilaumu kila kukicha, akapoteza hamu ya kula na afya yake ikadhoofika,” alisema mzee huyo ambaye ni baba yake Balanoga.

    "Mboni umalizi maelezo! Niambie nini kilitokea baada ya kudhoofika, tafadhari usinambie mama yangu amefariki, hiyo ni taarifa nzito ambayo katu sitoiweza kibeba ndani ya moyo huu dhaifu,” Mdidi aliongea kwa kwikwi huku machozi yakitengeneza mifereji kwenye mashavu yake.

    "Mdidi mama yako yupo hai....!"

    "Unasema..!?, mama yangu yuko hai na yuko wapi?"

    Mdidi hakuamini alihisi kama anaota vile lakini alizidi kushangaa ile hali ambayo wenyeji wake wanaionesha nyusoni mwao, kila mtu alionekana kuhuzunika sana, maswali mengi yakatiririka kichwani mwake, kama mama yuko hai kwanini watu hawa wawe na huzuni.

    "Jamani nielezeeni basi kinaga ubaga juu ya hali ya mama yangu kama mzima yuko wapi saa hii?".

    "Mdidi mama yako ni nusu mfu na nusu hai, kwani kwa miaka 4 sasa hazungumzi chochote yeye muda wote ni mtu wa kulia tuu"

    Mdidi akahisi kuchanganyikiwa akaona kama wanachelewa kumpa taarifa nusu nusu,

    "Kesho nitakupeleka alipo mama yako," alisema mzee yule.

    "Lakini japo mmenijuza kuhusu mama yangu sijawatambua nyie ni akina nani?"

    "Mama yako alituuzia nyumba na kwenda kuishi huko alipo sasa na akatupa simulizi kukuhusu huku akiamini siku moja utarejea".

    Ikabidi Mdidi aoneshwe chumba ambacho atalala kwa usiku huo, na kwakuwa alichoka sana haikuchukua muda usingizi ukampitia. Wakati akiwa usingizini akahisi kama kuna kundi kubwa la wanajeshi likija kuizingira nyumba ile, ghafla akashtuka na kukaa kitako akawaza kile alichokiona ni ndoto au kweli, akiwa katikati ya mawazo Balanoga akaingia huku akiwa anahema sana, mdidi akashtuka mno.

    "Nyanyuka tuondoke hapa, baba anauwawa huko nje, tupitie njia hii ya nyuma.."



    Taarifa ile ikamchanganya sana mdidi alipochungulia akaona kweli jeshi likibishana na yule mzee, akaona jinsi yule mzee anavyopokea kichapo, hakupoteza muda akachukua kifurushi chake na kumshika balanoga mkono na kuanza kukimbia kupitia mlango wa nyuma. Walikimbia sana ikafika mahali balanoga akawa hana uwezo tena wa kukimbia, ikabidi mdidi aangaze huku na huko ili aone kama kuna mahali pa kujificha, lakini kabla ya kufanya lolote akaona kundi kubwa la jeshi walio juu ya farasi huku wakishika mienge ya moto wakija upande wao kwa kasi.

    Mdidi ikainama chini na kumziba mdomo Balanoga asipige kelele itakayowashtua maaskari wale, msafara wa maaskari ukapita Mdidi akamwachia Balanoga ambaye alionekana kuchoka mno.

    "Hivi kwanini wamemuua baba yako na wanahitaji nini kutoka kwangu?" Mdidi akauliza.





    "Nugutu imekuwa na sheria kali kwa siku za hivi karibuni, kosa alilofanya baba ni kukubali wewe ulale nyumbani bila kutoa taarifa kwa maaskari na kama unavyojua dunia haina siri wakagundua kuwa kuna mtu mwingine ndani ya nyumba yetu hivyo wakaamua waje wathibitishe. Baba alikuwa akibisha ili kukulinda ndipo nami nilipopata nafasi ya kuingia chumbani kwako," alisema Balanoga.

    Mdidi alishusha pumzi baada ya kusikia yale akamsogelea Balanoga na kumkumbatia huku akimpa pole kwa yaliyomkuta baba yake.



    **************



    Ni asubuhi tulivu iliyopambwa kwa kila aina ya hali, kwenye kilele cha mlima jua la mawio laonekana kung'ara na kutoa mwanga uliovutia Zaidi. Sauti tamu za ndege wa mwituni zilitengeneza ala tamu ya muziki, mawimbi ya mtoni yalinogesha zaidi kwa kugonga kwenye miamba na kutoa sauti nyingine ya namna yake. Harufu nzuri ya maua ya asubuhi yaliwafanya Mdidi na Balanoga kusahau shida zao kwa muda mfupi, Mdidi akawa wa kwanza kuamka na kuang'aza huku na huko hakika ile sehemu ilivutia sana machoni pake akasogea hadi mtoni na kuanza kunawa, alipomaliza akageuka na kutazama sehemu aliyokuwa amelala balanoga lakini hakumuona akapepesa macho yake huku na huko atimaye akamuona. Uzuri wa Balanoga ulichagizwa zaidi na ule mwanga hafifu wa jua la asubuhi, urembo uliongezeka zaidi pale alipokuwa akipita katikati ya maua.



    "Kwanini mama aliniambia nikae mbali na wasichana, mboni wanaonekana wenye kupendeza na kuvutia, Nkalo kwanza na sasa Balanoga mhm! Ashukuriwe mungu," alisema Mdidi kwa sauti ya chini.

    "Eti unapajua alipo mama yangu?" Mdidi akauliza.

    "Utafanyaje kama nitasema sijui!"

    "Mhmhm! ata sijui nitafanya nini ila tumaini langu lipo juu yako naamini utaniepeleka alipo mama yangu".

    Balanoga akacheka, safari hii Mdidi akaona kitu kingine kipya ambacho hakukiona kwa Nkalo, akaona vishimo vidogo vidogo pindi binti yule alipokuwa akicheka, mwili ukaanza kushindana na nafsi yake, akahisi kuanza kupoteza muelekeo juu ya msimamo wake.

    "Twende ni njia hii tunahitaji kutembea kwa haraka kabla ya saa 4 tuwe tumefika kwenye msitu uliopo kaskazini”, alisema Balanoga.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ***********



    "Mkuu kuna mtu mme na mtu mke wanakuja upande wetu...!"

    Taarifa ikapita kwa watu wa 5 na kumfikia kiongozi wa kijiji hko, watu wote wakakusanyika kushuhudia ni nani wanaokanyaga ardhi hiyo, walikuwa ni Mdidi na Balanoga ambao walionekana kuchoka baada ya safari ya muda mrefu. Mdidi alipokanyaga tu kwenye lango la kuingilia, hali ya hewa ikabadilika, wingu zito likatanda, ardhi ikatetema, upepo mkali ukavuma na kusababisha miti kuvunjika hovyo. Mkuu wa kijiji hiko alipoona hayo yanatokea akaamuru watu wote wainame na kusujudu, Mdidi akabaki ameduwaa hakujuwa nini kinaendelea. Upepo ukaongeza kasi zaidi na ukamueka Balanoga matatani ikabidi Mdidi amkumbatie ili kumkinga asikutwe na baya lolote.



    Baada ya muda upepo ukatulia na mvua nyepesi ikaanza kunyesha, wengi wakaamini kuwa mvua hiyo ni ishara ya baraka, mvua ikanyesha kwa muda wa dakika 30 kisha ikakata, na hapo ndipo Mdidi alipopata fursa ya kusogea karibu na makazi ya eneo hilo,

    "Tumeona nguvu ya miungu ya Nugutu hii juu yako!"

    "Unamaanisha nini..?"

    "Karibu Mdidi bado kitambo kidogo utaelewa kila kitu"

    Mapokezi yalikuwa makubwa sana kila mmoja alionekana kuwachangamkia na kuwafurahia tofauti na alivyotegemea Mdidi.

    "Samahani mzee wangu, sina raha hadi pale nitakapomtia machoni mama yangu," alisema Mdidi.

    "Usijali mama yako yupo utamuona lakini kwa sasa naomba upumzike"

    "Hapana mzee wangu, siwezi kufanya lolote bila kumuona mama yangu, tafadhali niambie alipo," alisisitiza Mdidi.



    Mzee akafikiri mara mbili kisha akamwambia amfate, Mdidi bila kupoteza muda akamfata, wakaongozana hadi kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa pekee tofauti na nyingine wakaingia humo, wakafika sehemu wakasimama mzee akamwambia tazama kwenye kitanda kile. Mdidi akatazama lakini hakuona kitu, mzee akamwambia sogea na utazame vizuri, akasogea na kuangalia tena kwa umakini, machozi yakamtoka akuweza jizuia kutoa sauti ya kilio na uchungu. Mama yake alidhoofika sana, alikonda mno kutokana na ugonjwa uliomsibu, yule mzee akamsogelea na kumwambia,

    "Wewe ndiye tiba pekee kwa mama yako, hakuna dawa yeyote duniani itakayomtoa mama yako katika hali aliyokuwa nayo sasa na kurejea hali yake ya kawaida".

    "Sasa nini napaswa nifanye juu yake.?"

    "Upendo na ukaribu wako tuu"

    "Sawa mzee wangu nashukuru unaweza kwenda mimi nitabaki hapa na mama yangu"

    Mzee akakubaliana na Mdidi akaondoka, Balanoga naye akaungana na Mdidi kuhakikisha mama anarejea katika hali ya kawaida.



    Baada ya siku 2, mama akafungua macho yake na kukutana uso kwa uso na Balanoga, Balanoga alipoona mama yake Mdidi amefungua macho akapaza sauti na kumuita Mdidi, Mdidi akaja kwa kasi hadi alipo mama yake, Mama akatabasamu, Mdidi akamsogelea na kumkumbatia mama yake.

    "Mwanangu niliambiwa umeuawa nami sikuona faida ya kuendelea kuwepo duniani lakini kila nilipojaribu kukatisha uhai wangu ilishindikana hapo nikapata hisia kwamba mwanangu bado unaishi na ipo siku utakuja kwangu, na leo hisia zangu zimetimia," alisema mama.

    Wote wakajikuta wakikumbatiana huku machozi yakiwatoka, muda ambao Mdidi alikuwa akiongea na mama yake Balanoga alitoka na kuandaa uji mwepesi kwa ajili ya mama yake Mdidi, akauleta Mdidi akaupokea, mama yake Mdidi akamtazama sana msichana yule, mdidi alipomtazama mama yake akagundua kuwa anamuangalia Balanoga.

    "Aah! Mama huyu anaitwa Balanoga ndiye aliyenisaidia hadi mimi nafika huku"

    Mama akatabasamu na kunyoosha mikono ishara ya kutaka kumkumbatia Balanoga, basi Balanoga naye bila hajizi akafanya kama mama alivyotaka, Furaha ikawa kubwa mioyoni mwao

    "Akhsante sana mwanangu..!" mama akamshukuru Balanoga ambaye alionesha kujali sana matatizo ya Mdidi.

    Wakati hayo yakiendelea huku nje ukunga wa kuomba msaada ukasikika, Mdidi akashtuka, Balanoga akasema

    "Bila shaka hilo ni jeshi la mfalme Msongo"

    "Mfalme msongo! Wamepajuaje huku?" Mdidi akauliza

    "Hata mimi sifahamu" Balanoga akajibu, Mdidi akatoka nje akakuta mpambano ukiwa mkali mno, akarudi ndani.

    "Balanoga naomba ubaki na mama yangu acha mimi nikasaidie mapambano"

    Balanoga akaitikia na Mdidi akaanza kutoka nje lakini kabla hajatoka mama yake akamuita.

    "Mdidi wape watu hawa furaha wamenifanyia hisani kubwa sana" Mama akanyoosha mkono na kumkabidhi Mdidi Jambia kisha akamwambia

    "Miungu ya Nugutu iwe nawe"

    Baada ya maneno yale Mdidi akawa kama amepigwa shoti ya umeme na kuanguka chini, Balanoga alivyoona hayo akasogea kwa upesi kutaka kujua nini kimemkuta Mdidi Lakini mama akamkataza. Baada ya dakika mbili Mdidi akainuka akamtazama mama yake kisha akasema,

    "Sitokuangusha mama"

    Akatoka nje na kukuta idadi kubwa ya watu wa upande wake wameangamizwa, akaingia katikati kabisa ya mapambano akachomoa jambia lake na kutoa amri kwa watu wake

    "Wote simameni nyuma yangu" Sauti ile ikawa kubwa zaidi ya ilivyotegemewa kuwa na ndani ya dakika kadhaa watu wote wakawa nyuma yake, yeye katikati na mbele ni jeshi la Msongo,





    "Sitaki niwaangamize, nawapa nafasi ya kuishi ondokeni hapa"

    Mdidi kwa sauti ya mtetemo akaamuru, lakini kiongozi wa jeshi la Nugutu akacheka na wenzake wote wakacheka kisha akasema

    "Shambuliaaaaaaaaa!!!!!!"

     "yeaaaaaaaaah! Ushindi kwa mfalme Msongo"

    "Shambuliaaaaaaa"

    Jeshi la msongo likaja kwa kasi kuelekea upande aliposimama Mdidi, akaamuru jeshi lake lirudi nyuma zaidi kisha akachomeka jambia chini papo hapo ardhi ikapasuka na kutengeneza mfano wa shimo kisha lile kundi lilioagizwa kwanza kushambulia likazama lote, kisha Mdidi akachomoa jambia na ardhi ikafunga,

    "Mhmh mkuuu huyu si mtu wa kawaida....!"

    "Acha kuzubaa wewe shambuliaaaaa"



    Jeshi likasogea kwa nguvu kuja upande wa mdidi, Mdidi akanyoosha jambia angani ukungu mweupe ukatanda na kuwanyima jeshi la mfalme msongo kuona Vizuri apo akatoa nafasi kwa watu wake kushambulia na kazi ikawa rahisi mno, Mdidi akapita katikati ya jeshi la msongo na kumteka Kiongozi wa jeshi lile kisha akasafisha wingu na kutoa nafasi ya watu kuonana

    "Wekeni silaha zenu chini, mkuu wenu yupo mikononi mwangu," alisema Mdidi.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Jeshi la mfalme msongo lilipoona hayo likanyanyua mikono juu na kuwekwa mateka. Kwa mara ya kwanza watu wa pale wakawa na furaha isiyo na kifani baada ya miaka mingi kuangaika huku na huko kukimbia unyanyasaji wa Msongo ndani ya falme za Nugutu. Ngoma zilipigwa watu wakasherehekea ushindi ule.

    "Mwanangu ameleta ushindi kwetu...!"

    "Amewezaje kulishinda jeshi kubwa vile peke yake?" Balanoga akauliza.

     Mama akashtuka kidogo kisha akamtazama Balanoga

    "Wewe na mimi tulikuwa hapa umewezaje kutambua kuwa lilikuwa jeshi kubwa au la?" mama akauliza.

    "Aah! Mama namjua vizuri mfalme Msongo huwa anatuma jeshi kubwa sana katika kutekeleza jambo lolote linalohusu maslahi yake...!" alijibu Balanoga.

    "Umejuaje kama amepambana nao wote peke yake?"

    "Ulimwambia Mdidi awape furaha watu wa hapa apo ndipo nlipojua kuwa amepambana nao peke yake"



    *************************





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog