Search This Blog

UKO WAPI MAMA? - 5

 





    Simulizi : Uko Wapi Mama?

    Sehemu Ya Tano (5)



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Basi siku zilisonga miaka nayo ikizidi kusogea wakati huo Kagaruki na dada yake Hamala wameshaacha shule ili kumuhudumia mama yao ambaye tayali mlemavu wa mgongo na upofu wa macho,Kiukweli maisha kwa upande wao yalikua magumu sana na hivyo Kagaruki akawa ndio kama mtu tegemezi kwa mama yake huku Hamala nae akiwa na kazi ya kumsafisha mama yake kila anapo jisaidia maana mama Kagaruki hukuwa na uwezo wa kukaa wala kusimama kwa sababu alivunjwa mgongo na yule nyoka aliyetokea kwenye kaburi la mama Nyanzala kwahiyo mama Kagaruki akawa anajisaidia ndani haja kubwa kwa ndogo..  Hapo ukatimia msemo usemao malipo ni hapa hapa duniani na kwa mungu ni hukum tu.

    Huzuni juu ya huzuni nyumbani hapo kwa mama  Kagaruki,na siku moja Hamala akamwambia kaka yake "Kagaruki nimemkumbuka sana dada Nyanzala sijui alienda wapi??

    Kagaruki akajibu.."sio wewe tu hata mimi maana nadhani laiti kama Nyanzala angelikuwepo basi mama angejisikia faraja sana kwa sababu siku haiishi  bila kumtaja Nyanzala "..Kagaruki alimjibu  dada yake  kwa sauti ya huzuni huku wakiwa chini ya mti wakila viazi vya kuchomwa,mara baada kumaliza kula hatimae Kagaruki alimwambia dada yake kuwa wamalizie kulima eneo ndogo lililobaki ili wawe wamemaliza kabisa kibarua walichopewa.

    Lakini Hamala alikataa katukatu kurudi tena shambani huku akisema kuwa anarudi nyumbani kumwangalia mama yake...

    "Hamala naomba unielewe dada tukimaliza hili eneo lililobaki tutapata hela yetu leo leo ili tuweze kununulia mahitaji ya nyumbani sawa" alisema Kagaruki akimwelekeza dada yake,ila Hamala baado alikataa huku akiondoka zake kitendo ambacho kilimuudhi Kagaruki mwishowe akampiga makofi ndipo Hamala  hakuweza kukubali  nae alimrudishia hivyo ikawa purugashani katika shamba la watu.

     Na wakati Kagaruki na dada yake wakiwa bado wanapigana hatimae mzee mwenye shamba alikuja kwa niaba ya kukagua mwenendo wa kazi unavyokwenda lakini cha ajabu aliwakuta mtu na dada yake wakipigana huku Hamala damu zikimtoka puani kama maji,basi yule mzee mwenye shamba aliingilia kati na kisha akasema "Nyie nimewapa kazi ili mpate hela ya kumsaidia mama yenu lakini jinsi mlivyokuwa wajinga mnaanza kupigana haya ondokeni hapa pumbafu zenu"

    Kwisha kusema hayo mzee huuo aliwakabidhi kiasi cha fedha kilicho lingana na eneo walilo fanya kazi Shani halafu akawatimua shambani kwake.

    Baada Kagaruki na dada yake kufika nyumbani,Hatimae walimkuta mama yao hali sio shwali na hivyo bila kuchelewa Kagaruki alikimbia kwa mwenyekiti wa kijiji ambaye nae alikuwa anafanya biashara ya kukodisha baiskeli,haraka sana Kagaruki alikodi baiskeli kisha akaelekea mjini kwenda kumnunulia mama yake dawa akijuwa labda mama yake kashikwa na malaria.

     Kwa muda wa saa moja Kagaruki alifanikiwa kuingia mjini na baiskeli yake,hivyo moja kwa moja alielekea mahali yalipo maduka ya madawa. Baada kununu dawa alichukua baiskeli yake kisha akaanza safari ya kurudi nyumbani,lakini  kabla hajaumaliza mji ili aingie kijijini mara ghafla Kagaruki alifinya brek ya  baada kumwona binti kama Nyanzala. Hivyo Kagaruki akawa ametulia akisubili yule binti ageauke ili amtazame usoni kama kweli ni Nyanzala au sio...Lakin mpaka yule binti anazama kwenye uchochoro flani hivi bila hata kugeuka nyuma..."daaah sijui ni yeye Nyanzala ??au nimemfananisha?

    Alijiuliza mwenye Kagaruki huku mapigo ya moyo wake yakimwenda mbio.. Ila yote kwa yote aliamuwa kumwachia mungu  akanyonga baiskeli yake kurudi nyumbani kwao huku akili yake yote ikimfikilia yule binti aliye mwona mjini akifanana mwendo  na Nyanzala kwahiyo maswali mengi aliweza kujiuliza kuhusu yule binti..na moja ya maswali.Tetesi kwamba Nyanzala alifariki mbona kaburi lake halionekani nyumbani?Wakati mila na desturi zetu zinadai kuwa hatakama mtu kafia wapi sharti ni lazima azikwe nyumbani alikozaliwa ..Sasa leo hii iweje waseme kwamba Nyanzala alifariki wakati hata mahali alipozikwa hapaonekani??...hapana ipo siku nitakuja tena mjini ili nifanye upelelezi kuhusu Nyanzala ".....Alijisemea mwemye kutoka katika ubongo wake Kagaruki ilihali muda huo huo akawa amefika nyumbani kwao lakini cha ajabu alikuta mlango umefungwa kwa ndani, aligonga kama mala tatu kisha Hamala akafungua mlango.

    "Kulikoni mbona unajifungia ndani mchana wote huu??....Kagaruki alimuuliza dada yake...nae akamjibu.."huwezi kuamini kaka,kwani muda ule ulivyokwenda mjini kumnunulia dawa mama..Alikuja mwanamke mmoja kumuulizia Nyanzala tena kibaya zaidi yule mwanamke nilipomtazama kwa umakini macho yake yalikua kama ya nyoka pia hata mikono yake kwa mbaali ilikuwa ngozi ya nyoka ingawa mwili na vingine vyote ni kama binadam"  Ni maelezo ambayo yalimwacha mdomo wazi Kagaruki huku asielewe cha kufanya.

    "enhee vipi uyo mama hajaacha ujumbe wowote au nia yeke alimtaka Nyanzala tu??"

    Alihoji Kagaruki huku akionekana kuwa na woga flani hivi..."mmh kasema atakuja baadae usiku kuja kumpa pole mama..

        CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/







    Kagaruki  alikastaajabu  kuambiwa  na dada yake kwamba kuna mwanamke amekuja nyumbani kwao ikiwa sehem  mbali mbali za mwili wake anafana na Nyoka,kibaya zaidi kilicho mchanganya Kagaruki  ni pale alipo ambiwa kuwa mwanamke huyo atakuja usiku kumpa pole mama yao. Hapo akawa mpole akionekana kana kwamba anawaza jambo fulani,mwisho akakata ukimya huo akamtazama dada yake akasema "Dada nakuomba leo  upike  chakula mapema ili tuwahi kulala . Pia  tafadhali endapo  ukisikia  mtu akibisha hodi  usifungue mlango  sawa dada? Kagaruki  alimwambia hivyo dada yake ambae nae wakati huo alikuwa    akichambua mboga za maboga  kwa niaba ya chakula  cha usiku. "Sawa  kaka nimekuelewa.. vipi lakini dawa umepata? " Hamala alihoji. "Ndio  nimepata, enhee  sasa sikia  hii  mpya  niliyotoka nayo mjini" Ghafla Hamala akastisha  zoezi la kuchambuwa mboga akawa makini kumsikiliza kaka yake alichotaka kuzungumza. "Dada leo  bwana  kwa macho yangu nimemwona dada mmoja kafanana  na Nynazala kila kitu" Hamala aliguna kusikia maneno hayo kisha akajibu" lakini kaka kweli? Au umemfananisha? "

    "Kweli  mimi sikudanganyi.. cha muhimu ngoja  nirudishe baiskeli kwa mwenyekiti kisha nije  nikupe  mkasa  wenyewe" " sawa kaka fanya hivyo wakati huu mimi naanda mboga.."  Kagaruki  alitengua stendi ya baiskeli. Moja  kwa moja akaanza safari  ya kuelekea kwa mwenyekiti wa kijiji ambako  ndiko  aliko kodi  baiskeli. Lakini  kabla Kagaruki  hajafika mbali, mara ghafla  dada yake alimuita nae Kagaruki  akaitika  "Kama  unahela  njoo na Mafuta ya kupikia "  Hamala alimwambia hivyo kaka yake lakini Kagaruki akasema " sina hata senti  dada yangu"  kwisha kumjibu dada yake, Kagaruki  akarudia kupanda baiskeli  hadi kwa mwenyekiti  ambapo akajikuta akitukanwa na mwenyekiti baada kupitiliza muda alio  pewa.

     Hatimae Kagaruki  alirejea nyumbani kwao.. akamkuta dada yake akisonga ugali, Kagaruki  alifurahi saana. Akasema "kweli dada yangu unamkono mwepesi yaani dakika kadhaa tayali unasonga ugali? Ila  angali usipike ugali mbichi  bwana" Alisema Kagaruki  huku akiingizia na utani  kidogo ulio mfanya Hamala kuachia kicheko. Kisha nae akajibu " Acha kunivunja mbafu  kaka embu andaa maji hapo sebuleni"  "sawa..mama umemchotea uji? " "ndio hilo ni jambo ambalo siwezi  kulisahau" Alijibu Hamala kwa sauti ya upole. Ukweli mama Kagaruki  kutokana na jinsi  hali yake ilivyokuwa hakuweza kula chakula chochote kigumu. kwahiyo chakula chake kilikuwa maji na uji mwepesi. " Mama uji tayali mama" Hamala alisema hivyo baada kumpelekea uji mama yake,Mama Kagaruki aliasama mdomo wake kisha mwanae akaanza kumnywesha. Hayo ndio yakawa  maisha ya  mama huyo. Kwani  alikuwa mtu wa kulala chali  pia hata kuona  mwanga  au Dunia jinsi ilivyo ilishindikana kwa maana  alikuwa kipofu,Hivyo mara baada Hamala  kumaliza kumnywesha uji mama,yake nae  na kaka yake walikaa  wakaanza kula chakula  wakati huo imeshatimia saa  kumi na  mbili jioni.  "Enhee niambie sasa kaka yangu.Ulisema  umemuona Nyanzala?   "Ndio  ila sina uhakika kama ni yeye ingawa nampa  asilimia nyingi huwenda yule akawa Nyanzala" Alisema  Kagaruki  kwa kujiamini kabisa"   "kaka kwani hujaipata habali kuwa Nyanzala  alifariki?.." Hamala alijibu kwa mshangao jibu lake likiambatana na swali.   "Mimi sikubaliani na hilo dada hadi nilione kaburi lake.. hivyo cha msingi ipo siku nitaenda mjini kumtafuata  dada Nyanzala  nimemkumbuka sana mimi" Kagaruki  alimwambia dada yake huku machozi yakimtoka,Hamala alimsihi  kaka yake apumguze munkali. Kagaruki akyafuta machozi kisha akainuka kuelekea chumbani kwake huku dada yake nae akielekea  chumbani kwake wote wakienda kulala. Kagaruki akarudia kumkumusha Hamala,akasema"Dada usisahau.. nakuomba usifungue mlango hata kama utasikia mtu unae  mfaham kagonga mlango"  "sawa kaka"  alijibu Hamala kisha akaingia  chumbani kwake kulala.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada watoto hao  kujichimbia vyumbani mwao,kweli punde si punde ilisikika sauti ya mwanamke ikimuita Hamala. Hamala alishtuka kutoka usingizi baada kusikia hiyo sauti,akajuwa  tayali yule mwanamke  aliye sema atakuja kumjulia hali mama yao tayali kafika. Hapo ndipo Hamala alipo nyamanza kimya huku ile sauti nayo ikiendelea  kumuita  mwishowe sauti hiyo aliisikia mama  Hamala,hivyo nae akapasa sauti ya kumuita Hamala lakini Hamala bado hakuweza kuitikia. Wakati  huo Kagaruki  nae alitelemka kutoka kitandani kisha akazipiga  hatua kuingia chumbani kwa mama yake. Baada kumfikia, kagaruki  alimziba mdomo mama yake kisha akasema "Mama kaa  kimya huyo sio binadamu wa kawaida" Mama Kagaruki alishtuka..

     "kwani saa hizi saa ngapi? Alihoji mama Kagaruki.  "Sijui  ila saa hizi usiku wa manane" Kagaruki  alimjibu  hivyo mama yake kisha akamuaga  kuwa anarudi chumbani kwake kulala.  Lakini  kabla Kagaruki  hajaondoka. Mama yake  alimuita " Kagaruki mwanangu"  "Naam mama"  "Hamala yuko wapi?  "Yupo chumbani kwake kalala"  alijibu Kagaruki . Mama Kagaruki  akashusha pumzi kwa nguvu Kisha  akasema "Muite na yeye kuna mambo nataka kuwaeleza maana mimi sio waleo wala wa kesho" Aliongeza kwa kusema hivyo mama Kagaruki maneno ambayo yaliweza kumshtua Kagaruki.  Hima  alizipiga hatua kuelekea chumbani kwa dada yake akamwamsha. Na  kwa Sababu Hamala alikuwa macho wakati wote,haraka sana aliitika moja kwa moja wakaelekea chumbani  kwa mama yao ambae kiukweli hali yake ilionekana  kuwa mbaya zaidi.

       Baada  Kagaruki  na dada yake kufika  chumbani kwa mama yao,Kagaruki  alipapasa mahali kilipo   kibiliti akakiona  akawasha kibatali wakati huo huo ile sauti iliyokuwa  ikimuita Hamala imeshapotea.  "Mama tupo  pembeni yako watoto wako" Alisema  Kagaruki kwa sauti ya upole. Mama Kagaruki alirudia kushusha pumzi kwa nguvu huku kijasho kikimtoka  kisha akasema. "Nampenda Nyanzala mtoto mwema kwangu hakika  najutia kwanini nilimtesa bila kuwa na hatia. .Leo hii wanangu mimi sio waleo wala wakesho  muda wowote  nakata  kauli.  Nawaza mtaishije wanangu kwenye hii Dunia hali ya kuwa mkiwa  yatima? Baba yenu alifariki kwa ajari ya gari,baba yenu pia mlezi ambae ni baba Nyanzala nae huko alipo sijui atarudi lini.  Wanangu nawonea huruma mimi" Alisema  Mama Kagaruki  huku akilia kwa uchungu kilio ambacho  kiliweza kuzua  simanzi kwa Kagaruki  na dada yake.

    "Mama  nisaidie chakula japo kidogo ili nipate nguvu za kunifanya  niende kuleta maji mtoni" Maneno hayo yalijirudia kichwani mwa  Mama Kagaruki.  Maneno  ya Nyanzala  alipokuwa akimuomba chakula. "Usiniombe mimi chakula, kamuombe Mama yako pale nyuma ya nyumba kwenye kaburi lake. Mama Kagaruki  alizidi Kulia maladufu  huku akijutia kwa kile alichokuwa akimjibu  Nyanzala  pindi alipokuwa akidai haki yake kama mtoto.

      Hivyo  kilio hicho  kiliweza kustisha  kile alichokuwa   akitaka  kusema Kagaruki ambapo watoto wake walimtuliza kisha wao wakarejea kwenye vyumba vyao kulala huku kila mmoja akiwa na sikitiko ndani ya moyo wake. 

       Na  asubuhi palipokucha,Hamala ndio alikuwa wa kwanza kuamka ambapo alishtuka kuona gamba  la nyoka  mlangoni kwao,Hamala akamuita kaka yake ambapo yeye  alikuwa bado amelala. Kagaruki alipo sikia akiitwa tena kwa mashasha,haraka aliamka akaenda kulishudia hilo gamba la nyoka. Hakika walioigwa na butwaa lakini mwishowe wakashauliana na dada yake kuwa walichome moto  hilo gamba. Kweli kagaruki  alilinyunyuzia mafuta  ya tataa kisha akaliwasha moto,ila wakati  gamba hilo likiwa limezungukwa na moto. Upande mwingine nako kule ndani ilisikika sauti ya mama Kagaruki akilia kwa kumtaja Nyanzala mtoto ambae alimnyanyasa kadri  awezavyo. Moto ulipokuwa ukizidi kukolea ndivyo mama Kagaruki nae alivyozidi kupasa sauti ya kilio.





    Mama  Kagaruki  alisikika akipiga kelele  ndani wakati huo lile gamba  la nyoka nalo likizidi kuzungukwa na moto. Lakini cha ajabu lile  gamba licha  ya kushikwa  na moto ila halikuweza  kuteketea. "Mama kuna  nini mama"Kagaruki  alimuuliza mama yake mara tu alipo ingia ndani kwenda kujuwa kitu kinacho msibu  Mama yake hadi afikie hatua ya kumtaja Nyanzala huku akilia.,ila licha ya Kagaruki  kuhoji kamwe Mama yake hakusema chochote zaidi ya kuangua kilio huku akiendelea kumtaja Nyanzala. Kiukweli Mama Kagaruki  alijutia  sana alitamani amuone  au amsikie Nyanzala  Kwa mala ya pili lakini ndio hivyo Nyanzala  hakuwepo tena mbele yake au pembeni yake.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

       Kilio kile cha mama Kagaruki  kilidumu ndani ya nusu  saa  wakati huo Hamala  na Kagaruki  nao wakiwa  wameshika tama  hawaelewi wamsaidieje mama yao  ambae kimwonekano alionekana sio waleo  wala wa kesho. Simanzi kubwa  ilitanda malangoni kwakina Kagaruki ila simanzi hiyo ghafla ikakatishwa na jopo  la wanakijiji walio onekana kuja  nyumbani  hapo wakiwa na siraha mbali mbali. Kagaruki  akatoka ndani baada kusikia fujo  nje. Akataharuki kuona  wanakijiji wakiwa na mapanga na mikuki huku baadhi yao  wakisema  "kijijini kwetu  hatutaki wachawi" "ndio ukingundulika kuwa wewe ni mchawi  adhabu  ni moja tu lazima uchomwe moto" Yalikuwa maneno ambayo yalimshtua  sana Kagaruki  akaogopa  sana akajuwa kuwa tayali kimenuka, Kagaruki  alimuita dada yake ili atoke ndani waweze  kujitetetea wote. Wakati huo huo wanakijiji hao walionekana kuwa na hasira  kali walikuwa tayali wamesha ikalibia nyumba yakina  Kagaruki.  "Unaona sasa? Hilo si gamba Nyoka? Aaah sasa huu uchawi wao umetosha hapa kijijini kwetu" Alisema mmoja wa wanakijiji waliokuwepo pale. Wakati huo Kagaruki  na dada yake wakijaribu  kujitetea bila mafanikio ya kusikilizwa. Hivyo punde si punde mzee mmoja aliye fahamika kwa jina moja aliitwa  Katabi,aliwaamulu vijana  wake waingie ndani ya nyumba ya baba Nyanzala  wakakague vitu  ambavyo  yeye alihisi  vimo  ndani. Kweli wale  vijana waliingia  ndani  wakatazama kila kona ya nyumba hadi uvunguni,hatimae wakafanikiwa kuapata tunguli ambalo lilikuwa  limefunikwa kwa kitamba chekundu.moja kwa moja vijana hao wakatoka nalo ndani. . wanakijiji waliokuwepo pale walistaajabu kuona kitu kile,hata Kagaruki  na dada yake wakajikuta wakipigwa  na butwa  "Ndio  maaana  huyo mama hakuwa na hata lepe la huruma kwa mtoto wa mwanamke mwenzake kumbe mchawi bwana" alisema hivyo balozi  wa  nyumba kumi. Hapo hapo yule mzee Katabi akakohoa kidogo kisha akasema "hili  pekee  ndilo  lililozidisha matatizo kwa yule mtoto alie fiwa na mama yake,kwani kwa kutumia tunguli hili ilimfanya baba wa mtoto kutojali kile mtoto asemacho hatakama kipo  kwenye ukweli" Alisema yule mzee Katabi  huku akiwa ameshikilia tunguli lilitoka  ndani ya nyumba ya mama Kagaruki. Na  wakati akisema hayo. Upande mwingine wanakijiji walionekana  kuwa na ham ya kufanya maangamizi kwa kuichoma moto nyumba ya yakina Kagaruki,na hivyo baada yule Katabi  kuongea  kwa kirefu zaidi hatimae alulitipa lile tunguli ambapo nalo  lilipo tua  chini alitokea ndege mweusi akiwa na uzi mweusi mguuni,ndege huyo akaruka  na kutoweka  zake. Kitendo hicho kilizidi  kuzua  taharuki,lakini yote kwa yote waligeuka upande mwingine,kwa sauti kali  kagaruki  akaulizwa "Mama yako yuko  wapi" Kagaruki akajibu kwa woga  "yupo ndani hali yake sio  nzuri" jibu hilo liliwapa nguvu wale wanakijiji kwa kuchukuwa hatua ya kuchoma  moto nyumba hali ya kuwa mama kagaruki  akiwa ndani. 

    "Mamaaaaa...mamaaaaaah!" Mayowe yalisikika  kutoka kwa Kagaruki  na dada yake wakimlilia mama yao huku moto nao ukizidi kutanda kwenye  nyumba,mama Kagaruki  alishtuka baada kuhisi  joto likiongezeka,na punde si punde kipande  cha fito  chenye  moto kilimdondokea kwenye mwili wake hivyo akajuwa tayali nyumba imeshika moto. Hapo sasa akipiga mayowe akiwaita wanae,Kagaruki  baada kusikia sauti ya mama yake alitaka kujitosa kwenye moto ili kumuokoa  mama yake lakini akazuiwa na mmoja ya wanakijiji. Kwahiyo hadi nyumba yote inateketea Kagaruki  aliitazama  huku akiishia  kulia  tu. Mama Kagaruki  na roho yake mbaya akawa amekufa  na ukatili wake kwa Nyanzala  pia dhambi  ya kumpa  mume wake limbwata akiwa na lengo  la kumteka kifikra,ilihali muda huo huo mama Kagaruki anakufa  gamba lile la nyoka nalo lilitoweka  kimaajabu.

        Maisha yakabaki ya Kagaruki  na dada yake ambae ni Hamala,ambao nao walitimuliwa kijijini baada ndugu zake baba Maria  kuja kuunza  kiwanja  ambacho kilikuwa na nyumba  ya kina Nyanzala. Kumbe marehem baba Maria  alimkatia  uwanja baba Nyanzala  kama ujirani mwema kwani baba Nyanzala  alikuwa akiishi shambani kwake na sio  kijijini,kwahiyo kitendo kile cha Baba  Nyanzala  kumuua  baba Maria  kiliwakera wanandugu wa baba Maria hadi ikafikia hatua ya kuuza eneo lili alilopewa  baba Nyazala.

      Kagaruki  na Hamala wakakimbilia mjini,ambapo huko walianza  kuingia katika shunghuli ya kuomba omba huku Kagaruki  akitamani japo siku moja akatune na yule binti aliye muona  kwa mbaaali akiwa kafanana na Nyanzala.



    ******



    Siku  zilisonga miezi nayo ikisogea. Hakika  maisha ni kama karata.  Ikimbukwe kuwa watoto hao hao Kagaruki  na Hamala ndio walikuwa wakimuona Nyanzala kama takataka  na hivyo Leo hii nao wanalionja joto la jiwe  baada kufiwa na mama yao mzazi ambae ndio alikuwa kikwanzo kwa kigoli  Nyanzala. Kiukweli Kagaruki  na Hamala walihangaika sana katika jua  kali wakiomba walau fedha ya  kununulia  chakula ili wapoze  njaa kitu ambacho ilizidi  kuwakondesha.   Na  siku moja asubuhi mapema Hamala alimueleza kaka yake kuwa anahisi  homa  na kweli punde si punde Hamala akaanza kutapika matapishi ya njano  wakati huo Kagaruki  akiwa hana  hata shilling  mia  mfukoni hivyo akawaza atamsaidiaje dada yake? Na  hatimae akaamua kutimua  mbio kuelekea mtaani kutafuta kibarua  chochote ili apate  fedha ya kumnunulia  dada yake dawa kwa Maana hali ya Hamala haikuwa  nzuri hata kidogo,lakini wakati Kagaruki akiwa katika heka heka ya kutaka  kuvuka  barabara,mara ghafla akagongwa na gari.



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Kagaruki  alipelekwa hospitali  baada kugongwa na gari. Wakati huo Hamala nae kule alipo achwa na kaka yake,hali ilizidi kuwa mbaya akaona  kama kaka yake kamuacha kwenye mataa  na ndipo alipo amuwa kujikongoja kutoka maskani walipokuwa  wakilaza  mbavu  zao,moja kwa moja akajivuta mpaka  kando kando ya barabara  ambako  napo  alishindwa kuendelea na safari akaanguka chini kwani hakuwa na nguvu za kusonga mbele kwa wakati ule. Hamala alilalama  huku akiomba  msaada kwa watembea kwa miguu,hatimae mama mmoja msamalia aliweza kumsaidi kwa kumpeleka  nyumbani kwake kuishi nae,na kwa bahati  nzuri mama yule hakuwa na mtoto hata mmoja licha  ya kuwa na mwanaume pamoja na mali nyingi za kutosha. Hivyo mama yule msamalia aliweza kumpa  uhuru Hamala ajisikie kama yupo nyumbani kwao wakati huo tayali amesha pelekwa kwenye matibabu kwahiyo akawa yupo kwenye  dozi.   Siku  ya kwanza iliisha ikafuata siku ya pili hadi ya tatu ambapo Hamala  akaanza kumkumbuka kaka yake kipenzi Kagaruki,chakula akawa hali kama inavyotakiwa kwani muda wote alikuwa akimuwaza kaka yake huku sintofahamu  ikiwa  ndio imetawaala kichwani mwake akishindwa kutambua hali aliyonayo Kaka yake kama ni mzima ama la!

       Na  wakati Hamala akiwa kwenye hali hiyo,Upande mwingine ilionekana  gari ndogo aina ya RAV4,gari hiyo ilionekana ikielekea  eneo la hospital na punde si punde ikaegesha eneo maalum la kuegeshea magari ya watu walioleta au kuja  kuwaona wagonjwa wao. Na  mara baada gari lile kuegeshwa ,ghafla  kunako gari hilo alishuka  binti wa makamo ambae alionekana mrembo kupita kiasi nae hakuwa peke yake bali  alikuwa na msichana mwingine ambae yeye alikuwa mkubwa kupita huyo binti aliyetangulia kushuka kwenye  gari. Hivyo mabinti  hao walizipiga  hatua kuingia hospitalini wakajieleza mbele ya wauguzi kumbe wao  ndio walio mgonga Kagaruki  kwahiyo walifika hospitalini hapo kwa niaba ya kughalamia ghalama zote kwa mgonjwa Kagaruki  ambae kiukweli hali yake ilikuwa mbaya sana. Lakini katika mabinti hao wawili mmoja ambae ndio mdogo alishtuka akajikuta akipigwa na butwaa  baada kumtazama  Kagaruki. kwa mshangao akasema "Huyu  mvulana kama  namkumbuka" alisema binti huyo ambae hakuwa mwingine bali ni Nyanzala  binti ambae ilisemekana amefariki   kumbe Nyanzala  hakufa bali baada kupoteza  fahamu kwa sababu  kutoka damu nyingi sehem ya siri alipo unguzwa na mama yake wa kambo,alipelekwa hospital  akaongezwa damu akapata faham. Alipo pata faham mwanakijiji mmoja alidokeza kwa kuwaambia  watu waliokuwa  maeneo ya hospital  kuwa mtoto  Nyanzala  mahali anapoishi hana amani  hata kidogo.Mwanakijiji huyo aliongeza kwa kusema "nibora nyie watu wamjini mumsaidie huyu mtoto kwa kumpeleka  kwenye kituo cha kulelea watoto yatima kuliko huyo mtoto arudishwe kwa mama yake wa kambo"Kweli kutokana na kitendo kile cha kinyama alicho tendewa Nyanzala wengi waliumia  sana ambapo alijitokeza mama mmoja  kumsaidi Nyanzala. Mama huyo alikuwa na mtoto mmoja wa kike ambae ndio huyo aliyekuja  na Nyanzala Hospital  kumuona  kagaruki  baada kumgonga na gari.



    Hakika  Nyanzala  alizidi kuvuta  kumbukumbu na mwishowe kumbukumbu ilimjia akaamini  kuwa yule ni Kagaruki  mtoto wa mama yake wa kambo.. kiukweli  Nyanzala  alilia saana,hali iliyomfanya yule binti aliekuja nae hospital  kumshangaa "Nyanzala  unalia nini mdogo wangu? Alihoji yule binti ambae alifahamika kwa jina Pendo. Lakini Nyanzala   hakusema chochote zaidi ya kujifuta  machozi.  Pendo baada kuona  hali ile kwa Nyanzala,alifungua  pochi yake akafungua  akatoa  kiasi cha fedha akamkabidhi muuguzi. Kisha akamwambia  Nyanzala  waondoke mule  hospital.  Nyanzala  alikubali kuondoka klakini alimwachia ujumbe muuguzi kuwa asimruhusu Kagaruki  kuondoka hadi pale atakapo rudi  tena kumuona.



     ~~~~~~~~~~~~~~~~~~



    Baada  ya siku nne  hali ya kagaruki  kidogo ilianza kuimalika,hivyo alipo pata faham alikumbuka kuwa ana  dada yake na pia mara ya mwisho alimuacha akiwa na homa  kali. Hapo Kagaruki  kwanza akijiuliza kafikaje fikaje pale hospital? alipokumbuka kwamba aligongwa na gari akaona sasa haina  haja ya kuendelea kukaa  hospital, hima aliafanya m pango wa kutoroka pale hospital kweli alifanikiwa japo kwa bahati nasibu kwani  wakati alipokuwa akitoroka  hakuna  muuguzi aliyekuwa  kwenye wodi yake.

      Mwendo wa polepole Kagaruki  alizipiga hatua kuelekea kule  alipo muacha dada yake akiugulia homa. Laikini kagaruki   hakumkuta kwani Hamala tayali alikuwa ameshapata msaada kutoka kwa mama msamalia. Kagaruki alilia sana kumkosa dada yake akajiona hana bahati katika dunia, wakati huo huo upande wa pili Nyanzala  alirejea hospital  kumuona tena kagaruki  ili waweze  kuzungumza japo mambo mawili matatu ikiwemo kuulizia hali ya kijijini tangu wapotezane,Nyanzala akajikuta akishtuka baada kuambiwa  kuwa mgonjwa wake katoroka. Kiukweli Nyanzala  aliumia sana lakini hakuwa na lakufanya  zaidi kuingia ndani ya gari kisha kuondoka zake.

          Japo Nyanzala maisha aliyokuwa akiishi ni mtu baki,lakini yalikuwa maisha matamu  alikuwa na uhuru wa kufanya  chochote chema  tofauti  na jinsi  alivyokuwa  akiishi na mama yake wa kambo hapo awali. Ila licha yakuwa  katika hali hiyo,  Nyanzala bado  moyo wake ulionekana kushiba  majeraha ya mateso aliyoyapata kutoka kwa mama yake wa kambo.  Hatakama akiwa na furaha ila ghafla furaha ile inatoweka kila akumbukapo Yale  yaliyowahi kukatisha Elimu yake.   Kwingineko Kagaruki alikuwa akihaha kumuulizia dada yake



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

       "Wapi ulipo  dada yangu? Alijiuliza Kagaruki  huku akipiga hatua kuelekea  mahali asipo  pajuwa kwa muda ule ambao  tayali ilikuwa saa  za jioni  muda ambao mji unakuwa umechangamka. Na  wakati Kagaruki  akitembea hana hilo wala  lile hatimae  aliingia kwenye  moja ya uchochoro ambako huko alikutana na kundi  la vibaka wakivuta bange. Kagaruki  aliogopa  sana akataka  kukimbia lakini ghafla akajikuta tayali kazungukwa na vibaka.  Vibaka wale walimkagua Kagaruki  kila kona  ya mwili wake wakidhania kuwa huwenda Kagaruki  ana  pesa ili wapate  kumtapeli lakini kagaruki  hakuwa na hata shilling  mia mfukoni mwake.. Vibaka wale baada kuona kagaruki  hana pesa,waluchukuwa uamuzi wa kumvutisha bange  Kagaruki. Kagaruki  alitaka  kukataa lakini wale vibaka wakamtishia kumchoma kisu. Hali  ambayo   ilimuogopesha sana Kagaruki ikabadi avute  japo kwa shida. Na wakati  akivutishwa bange mara ghafla walivamiwa na kundi la sungusungu. Na  moja kwa moja vibaka hao akiwemo  na Kagaruki walifikishwa kituo  cha police,ambapo taarifa hiyo ya kukamatwa kwa hao  vibaka ilirushwa mubashara katika kituo cha ITV.. Hivyo wakati taarifa hiyo ikiwa mubashara,Hamala nae alikuwa makini  mno  kufuatilia  taarifa ya habari kwahiyo akabahatika kumuona Kaka yake akiwa katika wale vibaka. Hamala alifurahi sana haraka kumwona kaka yake,haraka sana akamwambia mlezi  wake kuhusu taarifa hiyo,na kwakuwa mlezi huyo alimpenda saana Hamala akamwambia "Usijali Hamala kesho tutaenda kituoni kumtoa! " Hamala alifurahi kuambiwa hivyo hata chakula siku hiyo alikila  kwa furaha ya hali ya juu.

       Kesho yake asubuhi mama huyo msamalia akiambataba na Hamala walielekea  kituo cha police. Hatimae  kagaruki  akawa amekombolewa,furaha isiyo  kifani  ilitawala kwa watoto wale Kagaruki  pamoja na Hamala. Wakati huo Nyanzala  nae akiwa na Pendo walionekana kuja palepale kituoni kwa niaba ya kumkomboa  Kagaruki  kwani wao  pia walimuona  kwenye  taarifa ya habari  baada kukamatwa na police  kwa tuhuma za ukabaji. Hatimae Nyanzala akabahatika kuwaona wote wawili Kagaruki  na Hamala.  Kama  ilivyo ada  Nyanzala  alidondosha machozi huku akisema "Kila  lenye  mwanzo halikosi mwisho.. Hamala unanikumbuka? Je, Kagaruki unanikumbuka? Mimi Nyanzala nilikuwa kijakazi chenu  katika imaya ya Baba yangu..Mlininyima chakula mkitegemea nile  nini? Mama yenu akanikataza kwenda shule akitegemea nini katika maisha yangu? " Alisema Nyanzala kwa sauti ya upole iliyo jaa huzuni..Hamala na Kagaruki  walishtuka  kusikia maneno yale wote  wakaatazama wasiamini kama kweli yule ni Nyanzala. Hakika walidondosha machozi na punde  wakamuomba msamaha Nyanzala. Nyanzala  akasema "nimeumbwa na moyo wa chuma  nilisha  wasamehe kitambo,hata yule alienifanya dunia niione  chungu  nimemsamehe" alisema Nyanzala huku akilia na mwishowe  alipanda kwenye gari na Pendo  kisha wakondoka zao wakiwaacha Kagaruki  na Hamala wakilia  kwa simanzi nzito  ..lakini nao  mwishowe walipanda  gari ya yule mama msamalia alie jitolea kumsaidia  Hamala kisha wakondoka eneo lile la police.  Lakini  wakati Kagaruki  na Hamala pia yule mama msamalia walipo kuwa njiani wakirejea  nyumbani,ghafla walipata ajari  baada gari Yao kugongana uso kwa uso na Roli. Katika ajari hiyo hakupona mtu yoyote. Hivyo Hamala na kaka yake wakaaga dunia huku wakiwa  na huzuni kubwa  moyoni mwao.



        MWISHO



0 comments:

Post a Comment

Blog