Search This Blog

BINTI WA PILI WA MFALME - 5

 







    Simulizi : Binti Wa Pili Wa Mfalme

    Sehemu Ya Tano (5)

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Embu toka hapa maana sikuelewi unachokizungumza" alisema Hancy na kuondoka zake.



    Alionekana Fancy, akicheka pembeni na kusema Hancy sasa itabidi uanze kuamini maneno niliyoweza kumwambia Sikitu akwambie... Mpaka sasa mchezo wangu unaendelea vizuri nataka kujua sasa utaishiaje? alizungumza na kumtazama Kipande ambaye aliishia tu kutabasamu.



    Malikia aliweza kutoka na hapo hapo Hancy alitokea katika kordo nyingine kwaajili ya kuelekea chumbani mwake na Mozah ndani aliweza kuifungua kabati yake na kuitafuta ile cheni hatimaye aliweza kuiona na kuiokota baada ya kuiona aligeuka na kusema nimeipata.



    Macho yake yaliweza kukutana uso kwa uso na Hancy ambaye aliweza kuiona ile cheni Mozah aliwahi kuificha akiamini ya kuwa Hancy hajaiona.



    "Hancy" aliita kwa kujichekesha.



    Hancy na yeye aliweza kucheka na kujifanya ajaona kitu



    "Unafanya nini ?? Aliuliza Hancy akimsogelea.



    " Hamna alijibu Mozah na kuweza kuirudishia ile cheni katika kabati kisha akageuka na kulifunga.



    "Nilikuwa napanga panga nguo" alizungumza Mozah na kumfuta Hancy.



    "Mbona uliniambia utachelewa kurudi" aliuliza Mozah na kuweka mikono yake katika kiuno cha Hancy.



    Hancy alimshika katika shavu na kumuuliza.



    "Kwani umeuchukia uwepo wangu kwasasa?? Aliuliza Hancy na kumsogeza Mozah zaidi.



    " au kuna jambo ambalo ulilitaka kulifanya pasina uwepo wangu?? Aliuliza Hancy na Mozah Alicheka tu.



    "Hapana.....hakuna ambacho nitaweza kukifanya pasina uwepo wako" alizungumza Mozah na Hancy aliitoa mikono ya Mozah kisha kuanza kulisogelea lile kabati kwaajili ya kwenda kulifungua.



    "Hancy" aliita Mozah na kujitokeza mbele yake.



    "Nini??



    " Unataka kuchukua nini kwenye kabati?



    "Nataka kubadilisha shati" alizungumza Hancy na kuanza kusogeza hatua.



    "Ngoja Mimi ndiye mke wako uniambie Unataka shati lipi nikuchukulie" alizungumza Mozah.



    "Hapana nataka kuchukua mwenyewe" alizungumza Hancy na kumpita Mozah.



    Mozah alimuwahi mdomoni na kumpiga busu Hancy kisha kuanza kumsogeza mbali na kabati lile.



    "Mozah unashida gani wewe?? Aliuliza Hancy na kujitoa mwilini mwa Mozah.



    Mozah aliweza kukumbuka ya kuwa Fancy alimwambia ahakikishe Hancy hatoweza kuiona hiyo cheni kwani ingeweza kuleta shida.



    " hapana siwezi kumfanya Malikia Maua aweze kugundulika" alizungumza Mozah na hatimaye alimuita Hancy.



    "Nini aliuliza Hancy na kugeuka nyuma ambako aliweza kumuona Mozah akifungua kamba za gauni lake na kuweza kulidondosha chini.



    " Mozah!! Aliita Hancy kwa kigugumizi na Mozah aliweza kumsogelea taratibu kabisa kisha akaanza kumfungua vifungo vya shati na kumpiga mabusu.



    "Mozah" aliita Hancy na kumtoa katika mwili wake.



    "Ni nini Unataka kufanya eti?? Aliuliza Hancy na kumpisha Mozah kisha kwenda kuokota gauni la Mozah na kumvisha.



    Hancy alitoka njee na kuondoka zake. Mozah alibaki kitandani akiwa ameshika kichwa chake na kujiuliza " kwanini alitumia njia ile"



    Lazima Hancy atakuwa amenifikiria vibaya alizungumza na kuanza kutoka njee kwaajili ya kwenda kuzungumza



    Alipofungua mlango tu aliweza kukutana na Hancy akirudi kwa speed ndani.



    Hancy aliita Mozah na Hancy alimrudisha ndani kisha akaanza haraka haraka kumvua nguo na kumtupia kitandani.



    "Bora tumalizie kile ulichoweza kukianzisha" alizungumza Hancy na kuanza kuvua nguo zake .



    Wakati huo Fancy alikuwa njee, sawa sawa ila nakuhakikishia ya kuwa hii ni mara ya mwisho kuushika mwili wa Hancy, kwani itabaki kama kumbukumbu tu alicheka sana na kuyafuta machzo yake.



    Ni baada ya Fancy kula kiapo ya kuwa hiyo ni mara ya mwisho Mozah kuushika mwili wa Hancy.



    Waliweza kufanya kile ambacho walihisi ni sahihi kwa upande wao.



    Usiku ulikuwa mwingi na Mozah alikuwa wa kwanza kuamka kutoka kitandani alielekea moja kwa moja hadi kwenye kabati aliloweza kuficha Cheni ile kisha akaitoa.



    Aliitizama na kumtizama Hancy ambye alikuwa amelala.



    Alijisikia vibaya sana jinsi anavyoweza kumdanganya Hancy lakini hakutaka Malikia Maua aingie kwenye matatizo kwani Furaha ya Hancy ni mama yake, hivyo asingependa kuona Hancy akiingia katika huzuni.



    Aliichukua cheni ile kisha akafungua kisanduku chake kidogo na kuweza kuiweka cheni ile. Akimini ya kuwa hakuna mtu aliyeweza kumuona basi alielekea bafuni.



    Hancy aliyafumbua macho yake na kuelekea moja kwa moja hadi sehemu ambayo aliweza kuihifadhi ile cheni aliifungua na kuitizama ile cheni.



    Aliirudishia na kuelekea kitandani huku akiwa mwingi wa mawazo.



    Palipambazuka asubuhi na Mozah alikuwa wa mwisho kuamka kitandani. Hakuweza kumuona Hancy kama kawaida yake kwani Mara nyingi Hancy humuamsha na kumtaka aende akaoge.



    Alihisi Hancy atakuwa ameelekea bafuni alisimama na kwenda kugonga bafuni mlango uliweza kufunguka na hakukuwa na uwepo wa Hancy mahali pale.



    "Ameelekea wapi?? Alijiuliza na baada ya muda kidogo alitoka ndani ya chumba chake na kwenda kumtafuta Fancy.



    Akiwa anamtafuta Fancy aliweza kumuona akiwa amekaa na Hancy huku akiwa amemshikilia Mkono na wakiwa wanacheka.



    Alikuja Sikitu na kusimama pembeni yake.



    " hivi unafikiria nini eti, kwamba Hancy na Mozah ni mtu na dada yake; labda wewe Ndiyo unafikiri hivyo, lakini wewe ni ndugu yangu Mimi hata kama nakuchukia vipi kwakuwa umeolewa na Hancy ila nataka nikwambie ukweli ya kuwa Fancy na Hancy siyo ndugu na kuwa makini sana na Fancy kwani siyo mtu mzuri kwa upande wako"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Unajua sijaweza kukuelewa" alizungumza Mozah na Sikitu alimsogelea na kumwambia.



    "Fancy anamahusiano ya Siri sana na Hancy na Fancy siyo Dada wa damu wa Hancy" aliondoka Sikitu na alikumbuka ya kuwa Fancy alimtaka aseme maneno yao ili kuharibu ndoa baina yake na Hancy na Hancy hatoweza kukubali kuona ya kuwa Kuna ugomvi baina yake na Mozah hivyo atamfukuza mozah na atachukua muda huo kumshawishi amuowe yeye. Sikitu akiwa anaamini kbisa ya kuwa anafanya yote kwaajili ya kuisaidia nafsi yake lakini lah hakuwa hakijisaidia bali kuharibu ndoa ya ndugu yake na kujitengenezea Kaa la moto.



    Mozah alibaki akiwa amesimama pale na akiwatizama wakati huo nao Fancy aliweza kumuona na aliendelea kumshika Mkono Hancy huku wakicheka.



    Hancy alipokuwa akicheka aliweza kumuona Mozah



    Aliutoa Mkono wa Fancy kisha kuelekea mahali alipo Mozah na kumshika Mkono.



    "Hii ni mara ya mwisho Hancy nakuapia ya kuwa hutauacha tena Mkono wangu kwaajili ya kwenda kuushika Mkono wa Mozah.



    Hancy alienda na kutabasamu.



    "Ndo umeamka? Aliuliza Hancy.



    Mozah alitikisa kichwa na kumtazama Fancy aliyekuwa akiwatizama.



    "Leo niliona nisikuamshe kwani inaonekana Jana usiku ulichoka sana" alizungumza Hancy na Mozah hakuwa akimjibu kitu.



    Aliweza kukumbuka maneno ya Sikitu lakini aliona ni upuuzi tu.



    "Huu ni upuuzi nafikiria nini" alizungumza na Hancy aliweza kumsikia akinung.unika.



    "Nini??



    " Hamna alijibu Mozah na kuanza Kuondoka na Hancy.



    Tom akiwa katika pita pita zake aliweza kumuona Fancy akizungumza jambo na Sikitu tena likionekana la Siri sana



    "Hawa wameanza lini kuzungumza?? Alijiuliza Tom na ghafla kwa mbele aliweza kumuona Zawadi.



    " Zawadi?? Aliita Tom na kuacha kuwafuatilia Fancy na Sikitu kisha akaanza kumfuata Zawadi.



    Alipofika alimgeuza na kumuuliza.



    "Wewe" aliita Tom na kumgeuza lakini aliweza kuona aliyeweza kumgeuza siyo Zawadi.



    "Samahani alizungumza Tom na kusema kwanini namfikiria huyu mwanamk alijiuliza na aliweza kupata wazo la kurudi alipofika hakuweza kumuona yoyote yule.



    " Kwanini Leo naona naona vibaya, nafikiri mfalme ataweza kumsamehe Zawadi kwa kumpitishia adhabu ndogo juu yake. Alijiaminisha kihivyo Tom na kuondoka zake.



    "Mozah hicho unachoweza kukifanya usifikiri ya kuwa unamsaidia huyo mtu asigundulike lakini fikiria kuhusu nafsi yako na nafsi ya Hancy hivi unafikiri Hancy atajisikiaje pindi atakapoweza kuusikia ukweli kutoka kwa mtu mwingine tofauti na wewe; ilihali alikubali kupata adhabu zote ili aweze kukuokowa wewe, kama huwezi kuniambia Mimi ukwli basi mwambie hata Hancy ili ajue atakusaidiaje kwani kutaja watu ambao siyo sahihi hakukufanyi wewe uaminike katika ufalme huu na ukumbuke kila mahali Kuna sheria na kanuni zake; nakuomba uzungumze ukweli nani kaweza kukupatia ile cheni" alizungumza Stela na kuondoka zake huku akiweza kumuacha Mozah katika mawazo tele.



    Muda ulikwenda na Hancy alikuwa akirudi ndani, huku akiweza kukumbuka ya kuwa alimuuliza Fancy kuhusu cheni yake.



    "Fancy ile cheni niliyoweza kukukabidhi siku ya kuzaliwa iko wapi??



    " kaka Hancy, ile cheni niliogopa kukwambia ila iliweza kupotea pamoja na ile cheni ya kifalme, nilijua utakasirika Ndiyo maana sikuweza kukwambia" alizungumza Fancy



    Hancy aliacha kuwaza na aliweza kuingia ndani ya chumba chake na kumkuta Mozah akiwa mwingi wa mawazo Hancy aliweza kwenda kukaa upande wa pili kisha akajilaza kitandni na yeye mawazo yakiwa yanamzonga hakutaka kuamini ya kuwa Mozah anaweza akawa anahusikia na tukio lile la kuiba cheni ya kifalme, katika upande wa pili Mozah alikuwa akiwaza atawezaje kumwambia Hancy ya kuwa mama yake anahusika na hilo.



    "Hancy"



    "Mozah"



    Waliweza kuitana kwa pamoja na kila mmoja akionyesha kutaka kusema jambo.



    "Unataka kusema nini?? Aliuliza Hancy.



    " Kuna jambo nataka kukwambia .... Na wewe??? Aliuliza Mozah.



    "Kuna swali nataka kukuuliza" alizungumza Hancy na kusema ila wewe anza kuzungumza.



    Mozah alivuta pumzi ndefu kisha akamgeukia Hancy vizuri na kuvut tena pumzi.



    "Malikia Maua........



    Kabla hajaongeza neno mlango ulifunguliwa na aliingia Malikia Maua aliyeonekana kutoka kwa jasho



    " Mozah binti yangu,alizungumza na kuanza kujichekesha hali iyoweza kumfanya Mozah ashindwe kuzungumza zaidi.



    "Mama unashida gani?? Aliuliza Hancy na kusimama kisha akamfuata mama yake.



    " Hamna; Mozah tunaweza tukaenda kuongea kidogo katika chumba changu sasa hivi" alizungumza Malikia Maua na kuanza safari huku akimtizama Mozah nyuma.



    "Mozah" aliita Malikia Maua na Mozah aliweza kutoka kitandani akiwa anatetemeka baada tu ya kushuka alipiga hatua Tatu lakini kutokana na hofu iliyoko moyoni mwake alijikuta anajikanyaga na kutaka kudondoka.



    "Mozah kuwa makini" alizungumza Hancy na kushindwa kuelewa kitu gani kinaendelea baina yao.



    "Wanashida gani hawa?? Alijiuliza lakini hakutaka kuwaza sana.



    Baada ya muda alionekana Mozah akitoka katika chumba cha Malikia Maua akiwa amepoza sana.



    Aliyakumbuka maneno ya Malikia Maua.



    " Mozah Tafadhali nipe muda kidogo zaidi na nitasema na kuuweka ukweli wazi mwenyewe "



    "Lakini Malikia Maua kwanini unafanya hivi??



    " Mozah yote haya niyafanyayo ni kwaajili ya kuilinda ndoa yangu pamoja na mtoto wangu na heshima ya falme hii hata wewe Kuna wakati utafika na utaweka kila kitu pembeni kisha uipiganie ndoa yako; na Mozah nataka nikwambie ya kuwa wewe ndiye furaha ya mwanangu Hancy; hakikisha uipotezi furaha yake kwani akosapo furaha na Mimi huudhunika zaidi "



    Baada ya Mozah kuweza kuyakumbuka maneno hayo tayri alishafika ndani na Hancy alikuwa akimsubiria.



    "Nilitak kuondoka lakini nilikumbuka Kuna jambo wahitaji kuniambia hivyo nikasema nikusubirie.



    " Ammmhhhh nilikuwa nataka kukwambia tu ya kuwa ukienda huko uendako uniletee chochote kitu' alizungumza Mozah na Hancy alimtizama tu.



    "Una uhakika?? Aliuliza Hancy na kumsogelea Mozah.



    " Ndiyo" alijibu Mozah akiweweseka.



    "La Ndiyo hivyo, kwanini unatetemeka mikono?? Aliuliza Hancy na Mozah alibaki akimtizama tu.





    "Aaauuhh unashida gani wewe?? Aliuliza Tom pasina kumtizma usoni



    " Fancy!! Samahani alizungumza Tom na kumuinua.



    Hancy aliweza kurejesha kumbukumbu zake juu ya alivyoweza kuambiwa na Fancy kuhusu cheni ile.



    Mozah akiwa ndani aliweza kulia sana kwani alijua anafanya makosa kwa kutoweza kumwambia mumewe.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akiwa katika hali ile aliweza kuingia Fancy na kumkuta akilia.



    "Fancy., nashindwa kwanini nashindwa kumwambia Hancy ukweli najiona mdhulumaji mbele ya Hancy siwezi hata simama nikamtizama kwa zaidi ya Mara mbili usoni mwake; nahitaji kumwambia juu ya Malikia.



    " hapana huwezi kufanya hivyo " alizungumza Fancy kwa ukali na hatimaye alijishtukia.



    "Namaanisha hupaswi kufanya hivyo kwani hata Mimi mambo yote Yale Malikia aliyoweza kunifanyia sijamwambia chochote kile nipe siku ya Leo na kesho Utamwambia Hancy kila kitu. Alizungumza Fancy akimkumbatia Mozah aliyekuwa analia na kusema leo tu nitasababisha dhoruba na hakuna kati ya wewe na Hancy atakayeweza kuhitaji kumuona mwenzake wala kumsemesha hiyo ni ahadi yangu.



    Hancy alikuwa amechukua vito vya dhamani zikiwemo cheni hereni na bngili za kike kwaajili ya kwenda kumpatia Mozah akiamini ya kuwa Mozah anatamaa na vitu vya thamani.



    Akiwa anaviweka ndani ya kimkoba chake aliweza kutokea Sikitu ambaye alimshika bega na kumlalia katika bega hilo kisha kumwambia.



    "Mozah hawezi ridhika na hivi, kwani atatamani zaidi na zaidi na atajifanya hataki hivi ili asionekane ni mwenye tamaa juu yako, na Kama aliweza kukupa wewe mwili wake ili tu usiweze kuiona ile cheni embu fikiria amewapa wanaume wangapi mwili wake kwa kuficha uhalifu wake usiweze kufika kwa mfalme, tena alianza na Tom.



    Hancy aligeuka na kumshika shingoni Sikitu.



    " unafikiri nitmuacha Mozah na kukufuata wewe, unafikiri nitayaamini maneno yako ?? Aliuliza Hancy na kumwambia.



    "Hii ni mara ya mwisho ukijaribu tena kuongea vibaya juu ya Malikia mtaraji wa Isadora nitakurudisha nyumbani kwenu Isambala ukiwa marehemu.



    Alizungumza Hancy na kuanza Kuondoka.



    " Mozah siyo mtu mzuri kwako na anamahusiano ya Siri na Tom; wote wale wanakufanya tu mjinga " aliropoka Sikitu na Hancy alitupa vitu vile chini kwa hasira kisha akamgeukia Sikitu na kumnyooshea Mkono kwa hasira sana.



    Sikitu aliogopa na kurudi nyuma baada ya kuona Hancy amevimba kwa hasira.



    Aliinama chini na kuokota vitu vyake baadhi kisha akaondoka zake.



    Huku nako alionekana Tom akiwa anatembelea katika kasiri ile ya kifalme huku akiwa mwingi wa mawazo aliweza kugongana na Fancy.



    "Oohh fancy samahani" alizungumza Tom na kumuinua Fancy kisha kutaka kuendelea na safari zake.



    Fancy alijifanya hawezi kutembea na kudondoka chini.



    "Nahisi mguu wangu umeshtuka nenda chumbani kwa Hancy utamkuta Mozah akupe dawa uniletee.



    Tom aliwahi haraka haraka kwaajili ya kwenda kuleta dawa pasina kufikiria wakati huo nao Fancy aliinuka na kujikung.uta kisha akatabasamu na kuondoka zake.



    " huyu siyo mtu mzuri" alizungumza Nzenze na kuwaz kitu gani kinaweza kutokea juu ya Tom na Mozah wakati huo nao aliweza kumuona Hancy akipita na kuelekea chumbani kwake akiwa amejawa na hasira sana.







    "Kipi kinaenda kutokea huko" alizungumza Nzenze na kuanza kumfuata nyuma nyuma Hancy.



    Tom alifika na Mozah alishngaa.



    "Dawa huku ndani??



    "Ndiyo ameniagizia huku"



    "Hapana Hamna dawa mbona huku ila subiri kidogo nina dawa yangu huwa nimeihifadhi cjui kama itaweza msaidia" alizungumza Mozah kisha akasogeza stulli na kupanda kabla hajaweka mguu wa pili vizuri aliweza kuweweseka na kujikuta anataka kudondoka Tom aliweza kumuwahi kwa kumdaka sehemu ya kiuno na kumfanya Mozah alaze kichwa chake katika kifua cha Tom.



    Hapo hapo Hancy aliweza kuingia na kuwaona katika hali ile.



    Baada ya Tom kumuona Hancy aliweza kushtuka na kumuachia Mozah ambaye aliweza kumshukuru ila alishngaa wapi anapoweza kushangaa aligeuka na alikutana uso kwa uso na Hancy.



    "Hancy" aliita Mozah na Tom alishaweza kujua kabisa ya kuwa Hancy ameshikwa na hasira na hawezi kujicontrol tena.



    "Hancy; hatujafanya chochote namaanisha Mozah hajafanya chochote" alizungumza na kumshika Mkono Mozah akimuweka nyuma yake kitendo kile kiliweza mkumbusha Maneno ya Sikitu na kujikuta akitupa kile kimkoba alichoweza kuja nacho na kudondoka chini.



    Alimtizama Tom kwa hasira aliyekuwa amemshikilia Mkono Mozah



    "Unadhubutuje kumshika Mwanamke wangu Mkono mbele yangu?? Aliuliza Hancy na Tom aliuachia kisha akamwambia Mozah kimbia.



    " Hancy!! Aliita Mozah na ghafla Hancy alichukua chupa ya Maua na kuirusha ukutani.



    "Hancy usiwaze chochote cha kijinga na unatambua ugonjwa ulionao usitake urejee katika hali ya mwanzo zi control hasira zako"



    Hancy alizidi kutupa vitu ndani na kumuelekea Tom.



    Alimpiga Tom ngumi na kumfanya adondoke chini.



    "Tom" aliita Mozah na jina lile liliweza kujirudia zaidi ya Mara 7 katika kichwa cha Hancy.



    "Mume wako niko mbele yako na unadhubutuje kumtaje mwanaume mwingine mbele yangu?? Aliuliza Hancy na kumchapa kibao Mozah.



    Mozah alidondokea kitandani na Hancy alianza kumfuata.



    " kitu gani ambacho sikupi au sikuridhishi tukiwa kitandani haya Leo nitakuridhisha alizungumza Hancy na kuvua shati lake la juu.



    "Hancy unashida gani wewe?? Aliuliza Mozah



    " Unaniogopesha eti?? Alizungumza Mozah huku akilia.



    Tom aliamka na kumshika Hancy kwa nyuma.



    "Mozah kimbia nenda kaite walinzi waje wanisaidie Hancy amerudia hali yake ya ukichaa"



    "Ukichaaa!!! Aliuliza Mozah kwa hamaki na Hancy alimsukuma Tom kule kisha akachukua chungu cha uwa na kumpasulia Kichwani.



    Alimgeukia Mozah ambaye alishindwa kupiga hta hatua moja baada ya kuyasikia maneno kutoka kwa Tom ambaye tayari ameshalowa damu.



    " Mimi na kuweka kitandani ili nikuridhishe wewe unatoka na kutaka kwenda kutafuta mwanaume mwingine wa kukuridhisha. Inamaana Mimi sikutoshelezi?? Aliuliza Hancy na kutupa meza karibu na mozah alitizama pembeni na kuona upanga aliuvuta na kuanza kumsogelea Mozah.



    "Ha....ha....Hancy umekuwaje!? Alibaki kuuliza Mozah ambaye hakuwahi kuiona hali hiyo kwa Hancy. Watu walishafika mlangoni na kuanza kugonga wakimtaka Hancy afungue mlango.



    " Mozah aliita Malikia Maua.



    "Kaa mbali naye" alizungumza Mfalme Kantala na kutaka walinzi wafungue mlango.



    "Mozah" aliita Hancy akitaka kumsogelea kwa ukaribu zaidi.



    Mozah alianza kukimbia ndani na kumfanya Hancy apatwe na hasira zaidi.



    "Msizungumze wala kupiga kelele; mtamchanganya Hancy ndani alizungumza Mfalme na wote walikaa kimya.



    Fancy alitabasamu na kusema sasa Mfalme hawzi vumilia kwa ulichoweza kukifanya Mozah wala Hancy hatokutambua tena kwasasa kwani tayari amesharejewa na ugonjwa wake na huwa hapatani na mtu tofauti na Mimi na hiyo itakuwa nafasi yangu Mimi kuingiliwa kimwili na Hancy kisha kuwa mke wa Hancy wakati huo wewe na dada yako mtakuwa kijijini kwenu"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mozah kwanini unanikimbia eti?? Hunitaki Mimi sindiyo unamtaka huyu hapa chini?? Aliuliza Hancy na kuanza kumpiga Tom.



    " Hancy aliita Mozah na kutizama mlangoni ambako palikuwa pamefungwa na Hancy.



    "Hancy aliita Mozah kwa sauti ya utaratibu Sana.



    "Unaniogopesha" alizungumza Mozah akionekana mwenye wasiwasi.



    Hancy aliushika ule upanga na kuutupa chini kisha akaenda kuokota cheni alizoweza kuingia nazo.



    "Mozah nimekuletea vito hivi vya thamani ili usiweze kwenda kumuibia tena Fancy vito vyake; na Fancy ameweza kuniambia Mimi ukweli wote sitopenda tena uende ukachukuwe vito vyake nikaenda kukuletea wewe vito vya thamani lakini umeona havina maana na unakumbatiani na Tom ndani ya chumba changu. Alizungumza Hancy na kugeuka akiwa na sura nyingine alivirusha vile vito vya thamani na kumpiga Mozah sehemu za bega na kumchubua kwa kiasi kidogo kisha damu kuanza kumtoka.



    " ohhh damu; aliuliza Hancy na kuendelea kuyasikia makelele ya mlango.



    "Sitaki kelele alizungumza Hancy na kukamata tena panga lake na kuanza kupiga piga kila mahali huku akionekana kama kichaa.



    Mlango ulifunguliwa na mwanga ulimpiga machoni.



    Hancy alipiga kelele na kuonekana kuzidi kuwa kichaa kwa kuendelea kupiga kelele na kukata kata vitu ndani.



    Walinzi kadhaa waliweza kufika kwaajili ya kupambana naye lakini hawakuweza kumkabili.



    Timo aliinuka nyuma yake na kuweza kuokota kitu kizito.



    " Hancy aliita Mozah lakini tayari alishaweza kuchelew alipigwa na kitu kizito kichwani na aliweza kudondoka chini.



    "Hancy!! Aliita Mozah kwa sauti na kumfuata Hancy aliyekuwa amedondoka chini.



    Malikia alianza kufunga madirisha ya ndani pale.



    " funga madirisha na milango rudishia pazia Hancy asipigwe na mwanga"



    "Ni nani huyo anahusika na huu ujinga namtaka huyo aliyesababisha yote haya" alizungumza Mfalme Kantala kwa hasira sana.



    Baada ya muda kidogo kilionekana chumba kikigungwa na Mfalme Kantala huku kila mtu akiwa njee.



    "Mozah upo salama??



    " kwanini Hancy amekuwa hivyo?? Aliuliza Mozah na Malikia Maua alimtaka waende kuzungumza ndani ya chumba chake.



    "Kwanza tungependa kukutaka radhi kwani hatukuweza kujua ya kuwa Hancy hali yake hii itaweza kumrudia tena. Nilijifungua Hancy akiwa mzima kabisa na mwenye afya nzuri alikuwa vizuri na baada ya kufikisha miaka7 Hancy alikuwa kila akiona mwanga basi huwa anauogopa sana hivyo alikuwa akitoka njee ya kasiri kipindi cha mvua tu siku moja akiwa ametoka njee tulimtafuta sana na tulishindwa kujua wapi kaweza kuelekea, tulimtafuta kwa takribni siku 2 na siku ya Tatu tuliweza kumkuta Hancy akiwa amejificha na kujifunika na majani mengi ili asipatwe na jua lakini Mara hii hali yake ilizidi kuwa mbaya kwani hakutaka hata kelele na alikuwa akipiga kelele akisema wtu waweze kunyamaza tu ilituchukua muda mpaka tukaweza kumrudisha ngomeni tulimfungia katika kile chumba na alikaa huko kwa miaka 4 na alitimiza miaka 10 akiwa hapatani na mwanga wala Sauti yoyote.



    Fancy aliweza kuingia katika chumba kile na Hancy aliweza kuanza kurejea katika hali yake......niliamini amepona kbisa kwani hakuwa akiogopa tena mwanga wajua wala hakuwahi akiogopa kelele, ilipita miaka kadhaa na Hancy aliweza kufungua sungura wake katika banda lake siku moja asubuhi aliweza kutoka katika chumba chake na kutaka kumletea sungura chakula chake lakini hakuweza kumkuta sungura bali alimkuta mbwa akimalizia kumla sungura wake Hancy aliweza kushikwa na hasira na alimuuwa yule mbwa kwa kutumia mikono yake damu ilimtapakaa mwili mzima niliogopa sana na hapo watu walikuja na kuanza kuzungumza tena kwa sauti, sauti zile ziliweza kumdhuru Hancy na alianza kupiga kelele na kuanza kuyaficha macho yake ilituchukua muda kuweza kumkamata na kumrudisha katika chumba kile tena, Fancy aliweza kuingia na hakuweza kuletewa shida yoyote na Hancy japokuwa kwa Mara ya kwanza ilikuwa ngumu kufanya hivyo; sasa nawaza ni kipi umemfanyia Hancy mpaka akawa katika hali ile?? Aliuliza Malikia Maua.



    "Fancy!!!!!! Aliita jina lile na aliweza kukumbuka ya kuwa Hancy alimwambia " Fancy amenambia wewe ndiye uliyechukua vito vyake,pia akakumbuka Tom aliingia ndani ya chumba chake na aliweza kumwambia "Fancy kamuagizia dawa; lakini akakumbuka pia alimuona Fancy akitembea kwa kawaida kabisa"



    "Fancy!!!! Aliita Malikia Maua na kusema.



    " huyu shetani huyu

    Sintamvumilia kwa michezo yake michafu" alizungumza na kuondoka katika chumba chake

    Mozah alisimama na kutaka kumfuata lakini alishangaa baada ya kumuona mtu aliyeweza kusimama mbele yake.



    "Nzenze???? Aliita kwa hamaki



    " atukuzwe binti wa pili wa mfalme wa kijiji cha Isambala "



    "Wewe" alirudia tena kwa mshangao.



    ***** ***** *****



    "Sina imani na Nzenze nina uhakika Kuna jambo aliweza kulificha mbele yangu, kurudi andaaa safari ya kurudi Isadora" alizungumza Mfalme Nuhu na Nzanza aliweza kutikisa kichwa ishara ya sawa.







    Mtabiri Tambitambi aliweza kutazama na kusema wakati umefika sasa ila kwa maombi ya Bi Lunde miungu yetu imeweza kumsikia na imerudisha majibu Mtabiri Tambitambi alitupa kete zake chini na kutabasamu akiwa katika nyumba yake



    Huku nako aliweza kuonekena Bi lunde akiwa katika sehemu wanazoweza kuabudu huku akitaka miungu yao iweze kumlinda mjukuu wake.



    Kwa upande wa Malikia Samela alionekana akijitengenezea nguo zake vizuri.



    "Malikia wangu kila siku unazidi kuwa mzuri tu kitandani"



    Malikia Samela aligeuke na kumtizama Mganga Kipande.



    "Kama haujaweza kumpa Sikitu umalikia kule Isadora basi muuwe Mozah naamini Mozah akifa hakuna msichana mwingne mzuri kumzidi Sikitu"



    "Malikia Samela tukifanya hivyo lazima itahitaji kafara kubwa sana upo tayri kulipia?? Aliuliza mganga kipande na Malikia Samela alikubali akisema hata kama ni kwa kifo chake.



    ****** ******* ******.



    Alionekena Sikitu akipanga nguo zake na Fancy aliweza kumfuata



    " unafanya nini??

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kilichoweza kunileta hapa ni Hancy kama Hancy mwenyewe ndo huyo kichaa nakaa hapa kufanya nini?? Aliuliza Sikitu.



    " kwahiyo Unataka kuondoka zako?? Aliuliza Fancy.



    "Ndiyo naondoka"



    "Unafikiri nani anaweza kukuruhusu wewe uondoke!?



    " hakuna aliyeweza kuniambia Mimi nije hapa wala hakuna mtu atakayeweza kuniambia Mimi nisiondoke hapa"

    Alizungumza Sikitu na ghafla alihisi Kuna kitu kimeweza kuingia katika mgongo wake.



    Aligeuka na alikutana na Fancy Akicheka.



    "ukiondoka ukiwa hai sina uhakika kama utaweza kutunz Siri yangu, nanikwambie tu nilikuwa nakutumia wewe ili uweze kuwaweka mbali Hancy na mozah kisha Mimi niwe na mahusiano naye"

    Alitoa kisu na kumchoma tena Sikitu huku akiwa anacheka.



    Aligeuka nyuma na macho yake yaliweza kukutana uso kwa uso na Baba yake Kisude aliyeweza kumwambia



    "Huku umefika mbali sana huyo unayemuuwa ni binti wa kwanza wa mfalme wa kijiji cha Isambala sidhani kama kesi yake inaweza isifuatiliwe kwa umakini kama jinsi ulivyoweza kumuuwa mdogo wake na Zawadi, na kumdanganya Zawadi kwamba upo na mdogo wake na siku akitambua ulishamuuwa basi itakuwa mbaya sana kwani Zawadi anasiri zko nyingi sana nani mbaya kwa upande wako Zawadi kuwa adui wako



    "Usijali kuhusu hilo kwani baada ya siku mbili utakuwa Mfalme na Mimi nitakuwa mtoto wa mfalme na Hancy ataendelea kuwa Mfalme mtaraji tu"



    "Kivipi" aliuliza Kisude.



    Na Fancy alimuuliza.



    "Huwezi nisaidia kuja kuibeba hii maiti tukaitupe au mpaka nikamatwe"



    Wakiwa pale waliweza kusikia vishindo nani Malikia Maua alikuwa akija eneo lile.



    Kuna mtu anakuja huku walianza kumficha Sikitu lakini kabla hawajaweza kumficha vizur tayari alishaingia Malikia Maua



    "Umemuuwa Sikitu?? Aliuliza kwa hamaki na kabla hajamka pale alipokuwa akimtizama Sikitu aliweza kupigwa na kitu kizito kichwani mwake àlidondoka na damu zilianza kumtoka ghafla alitulia kabisa



    Fancy aliinama na kumpima pumzi.



    " hii ni mbaya kwani huyu ni Malikia wa hapa na mke kipenzi wa Mfalme Kantala"



    Walibaki wakitizamana tu na muda kidogo alionekana Mozah akiwa anamtafuta Malikia.



    "Mmenionea wapi Malikia Maua?? Aliuliza Mozah na wafanyakazi wote waliweza kusema hawajamuona.



    " alisema anaelekea kwa Fancy, mbona Hamna mtu katika chumba kile?? Alijiuliza na hatimaye alimuona Fancy mbele yake



    "Fancy Malikia Maua yuko wapi???



    Fancy alishtuka sana na akamuuliza kwa wasiwasi.



    " Sijakuelewa "



    "Nimekuuliza Malikia yuko wapi, kwamaana aliniaga anakuja chumbani kwako"



    "Hapana sijapata kumuona kabisa wala hajaja chumbani kwangu" Alizungumza Fancy na kuondoka akiwa anawasiwasi.



    "Fancy" aliita Mozah na kumsogelea Fancy akionekana mwingi wa hasira.



    "Kuna jambo aliloweza kuniambia Hancy na nimeshindwa kumuelewa; alikuuliza swali lolote lile juu ya ile cheni uliyosema Malikia Maua alikuwa anakutaka wewe uilete chumbani kwangu?? Aliuliza Mozah na Fancy alijibu kwa wasiwasi.



    " hapana" aliongea kwa harak na kurudi zake ndani.



    "Sawa endelea kujifanya ya kuwa wewe ni mtakatifu na ninakuonyesha kwanza nimpate mahali ulipoweza kumpeleka Malikia Maua.



    Ilipoishia ni baada ya Mozah kula kiapo ya kuwa atapambana na Fancy pale atakapoweza kumpata Malikia Maua.



    Nzenze sijapata kumuona Malikia Maua lakini nakumbuka ya kuwa mara ya mwisho alisema lazima aelekee kwa Fancy, na pia nimeongea na Fancy anaonekana mwenye wasiwasi sana hapa nawaza atakuwa amempeleka wapi Malikia Maua??



    "Mnaongelea nini hapa?? Aliuliza Tom ambaye hakuweza kuelewa kinachoongelewa pale.



    Mozah alimtizama tu bila kusema neno.



    Baada ya muda alionekana akilitaja jina la Fancy kwa hasira.



    " kumbe yeye ndo chanzo cha yote haya yeye ndiye chanzo cha kila kitu; sitamuacha mzima naapa"



    "Tom, hata Mimi natamni kumpoteza kwa haraka zaidi lakini nahofia kwasababu bado hatujaweza kutambua mahali alipoweza kuwepo Malikia hivyo kitu cha kwanza ni tumpate kwanza Malikia Maua.



    Nzenze alikubaliana na Mozah na sasa akabaki Tom tu aliyekuwa na mashaka.



    " nawaza sana juu ya Hancy sasa, ameshaweza kugeuka na kuwa kichaa nafikiri hata hili nalo liko juu ya mpango wa Mozah na Mfalme anamuamini sana Mozah hata tukiongea lipi hawezi kutuafiki kwasababu hataweza kutuamini afadhali Hancy angekuwa katika hali yake ya kawaida.



    "Mimi nitamrudisha Hancy katika hali yake" alizungumza Mozah



    "Mozah si kirahisi hivyo kama uongeavyo akishashikwa na hali hiyo huchukuwa miezi hata 9 kuweza kupona na ninahofu kubwa sana kwani siku zake za kukaribia kutawadhwa na kuwa Mfalme ni siku baada ya kesho sidhani kama itawezekana hilo, ila nahisi naye huyu Mjomba wake Kipande kuna jinsi anahusika kwani mara nyingi anaonekana kuwa kama mtu mwenye tamaa za madaraka. Alizungumza Tom.



    " Kipande siyo Mjomba wake bali Baba yake mzazi na hilo ndilo kosa pekee lililoweza kumfanya Malikia Maua atumikishwe katika kuiharibu ndoa ya Hancy na Mozah" Wote waligeuka na walikutana uso kwa uso na Zawadi.



    Zawadi aliitoa heshima yake kwa Mozah pamoja na Tom. Aliyekuwa akitabasamu tu na kusema.



    "Zawadi, aliendelea kutabasamu na Nzenze ndiye aliyebaki akishangaa



    " we... We......we si umeshakufa nilishuhudia kabisa ukizikwa na Fancy "



    "Eeeeeeeee" alizungumza Mozah na kumtazama Zawadi.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Amezikwa aliuliza Tom kwa mshangao.



    " nimezikwa aliuliza hata Zawadi ambaye hakumuelewa nzenze.



    "Ndiye Nina uhakika ni wewe, ila mbona kule ulikuwa mdogo mdogo na hapa umekuwa mkubwa?? Aliuliza Nzenze.



    " Zawadina"!! Alizungumza Zawadi na Tom alimdakia.



    "Unamaanisha yule pacha wako???



    " pacha??????!!!! Aliuliza Nzenze na Mozah.



    Zawadi miguu ilimuishia nguvu na aliweza kudondoka chini.



    "Mbona Mimi sielewi" alizungumza Nzenze na Tom alisema



    "Inamaana Fancy alimkuwa na mdogo wako kwa muda wote huo ndo maana ulikuwa ukifanya kazi chini yake kama ndiyo hivyo kwnini sasa akamuuwa pacha wako hiyo inamaanisha hata wewe huna dhamani tena kwake sasa kabla hajamteketeza mtu mwingine yoyote yule basi nitamteketeza yeye" alizungumza Tom na kuchomoa panga kiunoni mwa Nzenze kisha akaanza safari.



    "Tom" aliita Mozah na kumkimbilia lakini tayari Tom alishaweza kuzamiria jambo lile akiwa karibuni kuingia katika chumba cha Fancy aliweza kuzuiliwa na Zawadi aliyeweza kuja mbele yake na kulala katika kifua chake.



    "Endapo nitakupoteza wewe tena katika maisha yangu basi nitajiuwa mwenyewe baada ya kumuuwa Fancy" alizungumza na kujilaza vizuri katika kifua cha Tom.



    Tom aliutupa upanga wake chini na aliweza kumkumbatia Zawadi huku na yeye alitokwa na machozi.



    Mozah aliweza kujisikia vibaya sana kwa kumuamini Fancy ambaye ndiye chanzo cha mambo yote mabaya katika kasiri ile ya kifalme. Aliweza kuifikiria hali ya mumewe Hancy na kujikuta akilia tu.



    Nzenze yeye alibaki kustaajabu tu inawezekanaje mtu aliyeweza kumuona akizikwa yuko hai tena?



    ***** ****



    Huku nako alionekana Fancy akiwa anazungumza na Mfalme Nuhu ambaye alionekana mwingi wa mawazo na aliyeshindwa kujua afanye maamuzi yapi sahihi.



    "Bab kesho kutwa unatakiwa uachie kiti cha kifalme na umfanye Hancy awe Mfalme najua ndicho kinachoweza kukuhuzunisha kutokana na hali ya Hancy ila Baba nakuhakikishia nitafanya kwa haraka zaidi na upesi mpaka apone Hancy ndani ya siku ya kesho.



    "Yuko wapi Malikia Maua?? Aliuliza Mfalme na kumtolea macho makali sana Fancy ambaye alianza kujing.atang.ata.



    " Mfalme nani amekwambia Mimi nilikuwa na Malikia Maua Leo Mimi sijamtia hata machoni" alizungumza Fancy na Mfalme alimuuita Mfanyakazi aliyekuwa akipita eneo lile.



    "Yuko wapi Malikia Maua?? Aliuliza Mfalme na Fancy alishusha pumzi ndefu sana akijua kuwa Mfalme hakuwa akifahamu jambo lolote lile wala kujua kipi kinachowez kuendelea.





    Ni baada ya Fancy kuweza kutambua ya kuwa Mfalme hajui chochote kile.



    Sasa aliamini amebakiza siku moja tu kabla ya mipango yake kutimia.



    Wakati huo nao shida iligeuka kwa Mozah, Zawadi; Nzenze pamoja na Tom waliokuwa wakimtafuta Malikia Maua katika kasiri ya kifalme mwishoni walikutana katikati na kila mmoja hakuwa anajua mahali Malikia Maua alipo.



    "Tufanyaje sasa?? Aliuliza Mozah akiwa hajui kipi cha kufanya.



    Wakiwa eneo lile wakiwa wanajadili juu ya Malikia Maua aliweza kupita Fancy na aliwaona.



    " wameweka kikao chanini hawa?? Alijiuliza na kusogea mbele pale walipo



    "Zawadi!! Aliita kwa mshangao baada tu ya kumuona kwani aliamini ya kuwa Zawadi hakuwa na uwezekano wa kutoka katika gereza aliloweza kufungiwa.



    " imekuaje uko hapa??? Aliuliza na Zawadi alibaki akijiishika nguo yake kwa nguvu ili asiweze kuharibu mipango yao.



    "Nakusalimu binti wa Mfalme alizungumza na kuweza kukilaza kichwa chake chini.



    " mbona uko hapa?? Umetokaje kule???



    "Malikia Maua ameweza kunitoa Leo, baada ya kugundua ya kuwa sina hatia" alizungumza Zawadi na kumfanya Fancy ashtuke kidogo.



    "Malikia??? Aliuliza kwa kurudia



    " ndiyo "



    "Yuko wapi?? Aliuliza baada ya kutoweza kumuelewa Zawadi.



    " ameondoka hapa na kuelekea katika chumba chake " alizungumza Zawadi na watu wote walibaki wakimshangaa.



    "Unasema?? Aliuliza kwa hamaki na kwasauti ya juu.



    "Mbona umeshtuka hivyo, kun tatizo kwani?? Aliuliza Mozah na Fancy alibaki kinywa wazi.



    " ammmhh hata na hivyo; embu wewe kijana twende nikupeleke kwa Malikia kwani kuna kazi anahitaji umfanyie" alizungumza Mozah na kuondoka na Nzenze.



    Hali hiyo ilimchanganya sana Fancy na alikumbuka yeye ndiye aliyeweza kumpima na kugundua ya kuwa apumui.



    "Au alijifanya ya kuwa hahemi?? Alijikuta akijiuliza kwa sauti na Zawadi aliweza kulinasa neno hilo.



    " mbona unazungumza mwenyewe aliuliza Zawadi akiwa anamtizama kwa hasira sana Fancy.



    "Hapana" alijibu Fancy na kutoka eneo lile haraka haraka.



    Baada tu ya kuondoka Zawadi aliweza kuachilia kilio cha kwikwi na Tom alijisogeza karibu na kumkumbatia kisha kumlaza katika kifua chake.



    "Jizuie hivyo hivyo, mpaka tufahamu wapi alipoweza kumpeleka Malikia Maua; pia umetumia njia nzuri sana kwani Fancy ataelekea hiyo sehemu aliyoweza kumpeleka Malikia Maua.



    " Nzenze inabidi tufanye kazi ya ziada na kwa haraka sana kwanza kamtafute mama Stela yeye pia anaweza kutusaidia kwa hili" alizungumza Mozah na Nzenze alitikis kichwa.



    "Lakini kwanini ukasema ya kuwa Malikia Maua ananitaka Mimi wakati wote hatui mahali Malikia Maua alipo?? Aliuliza Nzenze



    "Na ndiyo maana nakwambia tunamuhitaji Mama Samela" alizungumza Mozah na Nzenze alitoa heshima kisha akaondoka.



    ******* ******** ********



    Uku nako katika kijiji cha isambala alionekana Mganga kipande akiendelea kufanya yake kwaajili ya kuweza kumtoa uhai Mozah.



    "Malikia Samela sidhani kama tunaweza tukafanikiwa nahisi kabisa kwahili tutashindwa"



    "Na ndiyo neno ambalo silitaki kutoka kwako wewe ni Baba yake kwanini unashindwa kumsaidia mwanao??



    "Sawa ila inabidi tukubaliane na matokea yatakayoweza kutokea" alizungumza Mganga kipande na kuendelea kufanya shughuli zake ila wakati akifanya hivyo Kibonge aliweza kumuona na aliweza kupeleka taarifa hivyo kwa mtabiri Tambitambi.



    "Hivyo wanataka sasa kumuuwa Mozah?? Aliuliza mtabiri na Kibonge aliweza kukubali kwa kutikisa kichwa.



    " tufanyaje sasa?? Aliuliza Mfalme na mtabiri Tambitambi alisema.



    "Katika mji wa Isadora wewe ndiye unayeweza kutegemewa kwani mji huo mkuu ukiingia matatizo basi yataadhiri na vijiji vya karibu, na hiyo itakuwa hata rahisi kwa Mganga kipande kumuuwa Mozah pasina mtu kumuhisi kama ni yeye" alizungumza Mtabiri Tambitambi na Mfalme Nuhu aligeuka na kulitizama jeshi lake la maaskari alioweza kuwaaandaa.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sawa, ila pia nakukabidhi maisha ya binti yangu Tafadhali, muweke katika hali ya usalama alizungumza Mfalme nuhu na kuanza safari ya kuelekea katika mji wa Isadora.



    Wakati wakiwa njiani Malikia Samela aliweza kuwaona



    Kwani huyu Mfalme anaelekea wapi na jeshi kubwa hivi, au kuna vita?? Lakini mbona hajapata weza kuniambia?? Lazima nifuatilie mpaka niweze kutambua ya kuwa ni wapi anapoweza kuelekea.alizungumza Malikia Samela na kuamua kulifuata jeshi lile nyuma nyuma.



    ***** ****** ********



    " Nashindwa kuelewa hata Mimi hapo" alizungumza Fancy akiwa na Baba yake Kisude.



    Itawezekanaje na Malikia tuliweza kwenda kumtupa mbali sana na kijiji hichi?? Amewezaje kurudi pasina kuwa na farasi kwanza tayari tulishamuuwa" alizungumza Kisude na Fancy alimdakia kwa juu.



    "Siyo tulisha wewe ndiye uliyeweza kumuuwa " alizungumza Fancy na Kisude alimtizama kisha akasem.



    "Kama atanitaja mimi basi hawezi kukuacha na wewe; kwani tulikuwa wote kwa pamoja"



    Fancy alitizamana na Kisude na Kisude akasema.



    "Na je kama hii ni trick wanataka kujua mahali alipo Malikia Maua"



    "Kivipi???



    " nahisi ya kuwa labda tumeshaweza kugundulika ya kuwa sisi siyo watu wazuri katika kasiri hii"



    "Ingelikuwa hivyo basi tungeshakuwa hatuna ulimi sasa"



    "Sidhani kama wanaweza kufanya hivyo shida yao ni Malikia Maua endapo watafanya hivyo juu yetu basi watashindwa kutambua wapi alipo Malikia Maua" alizungumza Kisude ambaye alianza kuhisi kitu.



    Ghafla wakiwa pale waliweza kusikia sauti za wafanyakzi wakitoa heshima kwa Malikia.



    Wote waliweza kukimbilia dirishani na kutaka kutizama kama ni kweli ni Malikia Maua.



    Waliweza kushangaa kwani mavazi aliyoweza kuyavaa ni ya Malikia.



    "Haiwezekani' alisema Fancy na kutaka kutoka njee.



    " unaakili wewe, unatakaje kutoka Njee?? Mimi sitaki matatizo tena?? Alizungumza Kisude kwa haraka haraka.



    "Nataka kwenda kudhibitisha kama ni Malikia Maua kweli?? Nilihakikisha hakuwa akihema alikuwa amekufa itawezekanaje akawa yuko hai tena" alizungumza Fancy akionekana mwenye stress nyingi.



    "Je ukienda na ukikuta ndiye,utafanya nini?? Aliuliza Kisude na kutizama njee ambako Malikia hakuwepo tena.



    Lazima nikamuone na kama ndiye basi nitamuuea kabla hajaweza kufikisha habari hii kwa Mfalme kantala na kila anayejua kuhusu mimi, kwani ni kesho tu kesho ndiyo unatakiwa kuwa Mfalme wa Isadora na Mimi kuwa mtoto wa Mfalme halali wa Isadora mpaka pale Hancy atakapoweza kupona na kuwa Mume wangu na Mfalme" alizungumza Fancy na kutoka ndani ya chumba chake akimtafuta Malikia Maua.



    Akiwa anaendelea kamtafuta alionekana mtu akiwa nyuma yake na akiwa ameshika kisu kwaajili ya kumteketeza.



    Fancy alihisi kitu na aliweza kusimama akiwa katika hali ya uwoga ila wakati anageuka tu tayari mtu yule alishaweza kushikwa na mtu mwingine na kufichwa katika kordo moja ili asipate kuonekana.



    Fancy alivuta pumzi ndefu na kuondoka eneo lile.



    Wakati huo alionekana katika kordo moja Tom akiwa amemshikilia Zawadi na kuushika mkono uliokuwa na kisu.



    Alimshika Zawadi kwa nguvu na kuanza kumvuta huku akiwa amekishika kile kisu.



    "Unataka kufanya upumbavu gani kila kitu tumekipanga vizuri lakini wewe unataka kuharibu mipango yetu, unawezaje kufanya hivyo?? Aliuliza Tom na Zawadi alijitoa mikononi mwake.



    "Kamuuwa mdogo wangu Mimi; kaniulia Zawadina wangu, kamfanya nini mdogo wangu mpaka akamuuwa sitamuacha mzima" alizungumza na kuanza kuondoka

    .

    Tom alifika na kumzuia kwa kuufunga mlango wa chumba chake.



    "Unajua ukifanya hivyo hakutakuwa na tofaut baina yako na yeye; Zawadi hata Mimi Fancy kanifanya mengi mabaya sana lakini navuta subra kwaajili ya kufikia lengo, Tafadhali kuwa na subra" alizungumza Tom na kwenda kumkumbatia Zawadi aliyekuwa analia.



    Wakiwa ndani ya kile chumba kwa njee waliweza kumuona Fancy akihangaika na kuhaha ha-ha.



    "Zawadi husikii raha ukimuona Fancy anavyoyangaika huku na kule" aliuliza Tom akiamini ya kuwa Zawadi aliweza kumuelewa ghafla alisikia mlango ukijigongeza na mbele ya macho yake aliweza kumuona Zawadi akimfuata kwa kisu Fancy.



    Alimkaribia na kutaka kumchoma kisu lakini nyuma yake aliweza kuja Mozah na kumshika mkono ule wenye kisu Fancy aligeuka nyuma na aliweza kuwaona wote wawili.



    Kuna shida gani mbona Zawadi yupo katika hali hii?? Alizungumza Fancy akimtizama Zawadi aliyekuwa amejawa na hasira.



    Zawadi alitaka kuzungumza lakini alizibwa mdomo na Tom aliyekuwa ameshafika eneo lile.





    "Kuna nini? Aliuliza Fancy na Tom alimjibu.



    "Malikia Maua anakuitaji katika chumba chake cha kimalikia"



    "Mimi?? Aliuliza Fancy kwa hamaki na wakati huo kisu sasa kilikuwa mkononi mwa Tom na Zawadi.



    " ahaaaaaaa kelele hizo zilitoka kwa Tom na hakuna mtu hata mmoja aliyeweza kuzielewa kelele hizo zimetoka wapi.



    Fancy nitakupeleka Kwa Malikia Maua " alizungumza Mozah na kuanza kuonyesha wapi pa kuelekea.



    Tom alimshika kwa nguvu Zawadi na kumrudisha tena chumbani kwake.



    "Zawadi acha ujinga eti" alizungumza Tom na Zawadi alisema.



    "Hata iwaje lazima nitumie hiki kisu....... Alizungumza na kukivuta akiamini kipo mikononi mwa Tom lakini alishangaa baada ya kuona kisu kile tayari kina damu alishusha macho yake chini na hapo alikuta damu zikimtoka Tom tumboni mwake.



    'Tomimo" alijikuta akishngaa na kumuita Tom jina lake kabisa kwa kulirefusha huku nako Mozah akiwa njiani alikuwa anaomba litokee jambo lolote la kumzuia Fancy asiende naye kwani alimtumia mama yake kujifanya ndiye Malikia Maua.



    Ghafla mbele ya macho yake alimuona Mfalme na yeye akielekea katika chumba kilekile cha Malikia Maua.





    Mfalme aliita Mozah kwa mshangao.



    Mnaelekea kwa Malikia Maua?? Aliuliza Mfalme na Mozah alijibu kwa wasiwasi.



    "Ndiyo"



    "Unaumwa au, mbona unatetemeka?? Aliuliza Mfalme kantala akimtizama Fancy aliyekuwa anatetemeka.



    " ha....ha.....hamna" alijibu akiwa anatetemeka.



    "Sawa twende" alizungumza Mfalme kantala na kuanza safari yake tena.



    Ikiwa imebaki hatua kadhaa kabla ya kuingia katika chumba cha Malikia Maua alichokuwapo Samela.



    Alibakisha hatua kadhaa lakini ghafla zilianza kusikika kelele za Hancy.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kuna nini tena?? Aliuliza Mfalme kantala na kuanza kukimbia mbio mbio.



    " Hancy " aliita Mozah na kuanza safari wakati huo nao Fancy alitaka kwenda mahali alipo Hancy lakini aligeuka na kuutizama ule mlango tena.



    Alisimama na kuanza kurudi kwa utaratibu kabisa ili kuweza kutizama kama ndiye Malikia Maua au lah.



    Alisogelea mpaka mlango na kuanza kuufungua taratibu kabisa aliufungua mpaka alipoweza kuumaliza alivuta pumzi ndefu na kuanza kusogeza hatua zake kidogo kidogo.



    Fancy" ilisikika sauti ikiita na Fancy aliogopa sana kwa uwoga kisha akaanza kugeuka nyuma kwa uwoga zaidi



    'Ma.. Ma....Malikia?? Aliita kwa mshangao na mbele yake alimuona Malikia Maua akiwa na damu mwili mzima.



    "Kwanini umeniuwa"



    'Hapana hapana ...hapana " alisema Fancy na kuanza kupiga kelel ghafla alisikia tena anaitwa nyuma alipogeuka alimuona tena Malikia Maua.



    "Ha....ha....pana....... Hapana" alizungumza Fancy na kuanza kupiga kelele.



    Yote Yale yalikuwa ni mawenge hakukuwa na mtu yoyote mbele yake aligeuza safari na kuanza kurudi ndani aliingia ndani ya chumba chake na kuanza kusema hapana hapana hawezi kuwa Malikia Maua lazima nikadhibitishe kesho kama ndiye au lah! Alizungumza Fancy na kujilaza kitandani pake.



    Palikucha asubuhi na maandalizi yalianza kwaajili ya kuweza kumfanya Hancy Mfalme mtaraji.



    "Kuna nini?? Aliuliza Mozah baada ya kuona watu wakipamba maeneo Yale.



    " nini kinaendelea?? Aliuliza Mfalme kantala na mfanyakazi mmoja aliweza kumjibu.



    "Tumepewa maagizo ya kupamba kasiri nzima"



    "Na nani??



    "Na mimi" alizungumza Kisude.



    "Mfalme wangu umesahau ya kuwa Leo ni siku ya kumvika Ufalme Hancy?? Aliuliza Kisude na Mfalme alimjibu.



    "Na unatambua hali ya Hancy ya kuwa hana uwezo wa kuliona jua kwa wakati huu itakuwaje ufanye sherehe hiyo Leo?? Aliuliza Mfalme kantala na Kisude alimtizama na kusema.



    " lazima Hancy hasimikwe Leo kwani ndiyo siku ambayo anatakiwa kupatiwa Ufalme akipewa siku tofauti na Leo basi hatakuwa Mfalme bora "



    Mfalme alikosa cha kuzungumza na kuhema tu



    "Malikia Maua yuko wapi?? Aliuliza Mfalme kantala na Kisude alishangaa.



    " Kwanzia Jana hatujapata kumuona" alizungumza mfanyakazi mmoja na Kisude alianza kuwaza inamaana Jana walipata kumuona nani.



    Alimtizama Mozah na Mozah alimtizama pasina kusema neno lolote



    "Huu ni mtego huu" alizungumza kimoyo moyo na kuanza safari wakati huo nao Fancy alikuwa akikata msitu mdogo uliokuwa karibu na mji wa Isadora na kutizama mbele na nyuma kama kuna uwezekano wa mtu kuwa anamfuata.



    Alidhibitisha hamna mtu na aliendelea na shughuli zake



    Ila nyuma yake alikuwapo Nzenze.



    Katika chumba cha Tom alionekana Tom akiwa amejilaza kitandani huku chumba kikiwa na moshi wa kushoto pamoja na vyungu vilivyokuwa vikitoa moshi huo. Pembeni yake aliluwa Zawadi aliyekuwa akimtizama tu na kujiuliza saa ngapi anaweza akaamka.



    "Tom aliita Zawadi na bado hakupata jibu lolote lile kutoka kwa Tom.



    " Tom; unajua nitajisikia vibaya San kama utaendelea kulala hapa chini kwaajili yangu....... Najisikia kuumia sana Tom........ Tafadhali amka" alizungumza Zawadi na kuendelea kulia wakati huo nao alionekana Tom akiyafumbua macho yake.



    "Nakupenda Tom, sitaki ulale hapa kama unavyolala hivyo Tafadhali fungua macho yako" aliendelea kulalama Zawadi ambaye hakuweza kutambua kama tayari Tom alishaweza kuamka na anamsikia kwa kila jambo analoliongea.



    "Tom; endapo ukiamka basi nitakwambia ukweli ya kwamba nakupenda na sitako nikupoteze kwaajili ya ujinga wangu tena,na kama hautaamka alizungumza na kusimama wakati huo nao Tom aliyafunga macho yake.



    " Nitaenda kumuuwa Fancy mara moja" alizungumza na kuanza kuondoka.



    "Zawadi" aliita Tom na Zawadi aliweza kuisikia sauti hiyo .



    "Nimeshaamka usiende tena mahali" alizungumza Tom na kuanza kujiinua.



    "Tom" aliita Zawadi na kumrudia Tomimo.



    "Tom" aliita tena na kuendelea kumpapasa papasa mwili wake.



    "Ahhhhh we vipi, hauoni aibu kunishika shika hivyo Mimi mtoto wa kiume" aliuliza Tom na kutaka kujiinua.



    "Unataka kwenda wapi lala kwanza"



    "Hapana hatuwezi kumuachia vita hivi Mozah mwenyewe lazima tupambane wote" alizungumza Tom na alishngaa baada ya kuona wafanyakazi wengi wakihangaika huku na kule.



    "Kuna nini Leo??



    " Hancy ndiyo siku ya kusimikwa na kuwa Mfalme"



    "Itawezekanaje iwe Leo na wakati hali ya Hancy bado ipo matatani"



    "Nafikiri mchezo mzima huu ilikuwa ni juu ya Ufalme huu Fancy na Baba yake wanataka wamiliki Ufalme"



    "Baba yake??? Aliuliza Tom kwa mshangao.



    Muda kidogo ulienda na alionekana Kisude akiwa na wafanyakazi wachache.



    " kabla hajaweza kunitaja jina langu hakikisha ya kuwa mnautoa uhai wake" alizungumza Kisude na vijana wale walitoa ishara ya sawa kisha wakaweza kuondoka



    "Fancy, siwezi kukubali kukikosa kiti hichi cha kifalme kwaajili yako kwani nimekipambania sana takribani miaka 19, nilipomteka Hancy na kumpa mateso ili tu kusiwe na Mfalme tena na nije niiuchukue Mimi lakini ilishindikana baada ya Hancy kupona ila kwa mara hii hata kama ni kumuuwa Hancy Leo lazima nikichukue kiti hiki cha kifalme" alizungumza Kisude na kujitizama katika kioo kikubwa.



    "Hatimaye nimebakiza masaa machache sana kabla ya kuwa Mfalme wa mji wa Isadora" alizungumza Kisude na kuanza kucheka sana akimini ya kuwa ushindi ni wake na hakuna atakayeweza kumzuia.



    "Mnachokiongea ni nini mbona Mimi sielewi" alizungumza Mfalme kantala na hapo alirudi Nzenze.



    "Wapi amempeleka Malikia Maua?? Aliuliza Mozah.



    Nzenze alikumbuka ya kuwa baada tu ya kufika mahali alipoweza kufika Fancy; basi Fancy alianza kushangaa na kusema ya kuwa haiwezekani wakawa hai nahakika walikufa wote wawili.



    " wawili??? Aliuliza Tom na kushangaa.



    "Huyo wa pili ni nani??? Aliuliza Mozah.



    " ngoja mbona siwaelewi nani kafa?? Aliuliza Mfalme kantala ambaye alishindwa kuelewa ni kipi kinaendelea.



    "Inamaana mtu wa pili lazima awe Sikitu" alizungumza Zawadi na wote walimgeukia.



    Muda ulifika na alionekana Mfalme kantala akiwa amekaa katika kiti chake cha Kifalme huku akiishika mikono yake kwa hasira pembeni yake alikaa Kisude na upande mwingine alikaa Fancy.



    "Ndugu wana kijiji wa mji huu wa Isadora Leo ninafuraha kubwa sana kwani ni siku ya kuweza kumsimika mwanangu Hancy kuwa Mfalme wa mji huu; hivyo basi naomba tule na tunywe kabla hatujaanza utaratibu huo. Alizungumza Mfalme kantala na kukaa chini.



    Wakati huo nao Kisude alikuwa akicheka tu akiamini Ufalme ni wake.



    Alimtizama Fancy na kumpa ishara ya amfuate.



    Walitoka pembeni na Kisude alimuuliza



    " ulienda wapi?? Aliuliza Kisude.



    "Malikia wala Sikitu pale tulipoweza kuwaficha hawapo hivyo kabla mambo hayajaweza kuharibika basi tuharakishe kuuchukua huu ufalme" alizungumza Fancy na Kisude alimwambia.



    "Unauhakika ya kuwa hawajamchukua hao waliokuwa wakikufuatulia nyuma??



    " wakina nani hao??



    "Huu ulikuwa ni mtego wala siyo kweli ya kuwa Jana tulimuona Malikia Maua hakuwa yey"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Unamaanisha wameshaweza kunitambua?? Aliuliza Fancy kwa hamaki.



    " kabisa" alijibu Kisude na kumwambia.



    "Sihitaji kuukosa Ufalme huu kwaajili yako hivyo hakikisha huniletei madhara katika hili" alizungumza Kisude na kuondoka zake



    "Wamenionaje"



    Wakati huo nao alionekana Mozah akiikifungua chumba anachokaa Hancy kwasasa kwaajili ya kwenda kuzungumza naye"



    Alivua viatu na kutembea taratibu pasina kupiga kelele na pia alihakikisha ya kuwa hakuna mwanga wowote ule utakaoweza kupenya na kuingia ndani.



    "Hancy". Aliita kwa utaratibu na kukaa pembeni ya Hancy aliyekuwa amejikunyat zake



    " Hancy " aliita tena na kutaka kuzungumza naye jambo lakini kabla hajasema lolote lile mlango uliweza kufunguliwa kwa nguvu na kuingiza mwanga kule ndani .



    Hancy alianza kuweweseka kwa kupiga kelele za huku na kule.



    Njee alionekana Fancy ambaye alitabasamu na kuondoka zake.



    Fancy aliita kwa hasira Mozah huku akiendelea kupambana na Hancy aliyekuwa analeta shida kwaajili ya ule mwanga.



    Ghafla Hancy aliweza kumsukuma Mozah na Mozah alidondoka chini kisha kimya kikatawala.



    Huku nako katika kiti cha kifalme Mfalme aliweza kufuatwa na Kisude kisha kumtaka amtangaze yeye kama Mfalme kwani Hancy hana uwezo wa kupona tena.



    "Siwezi kukupa Ufalme wangu" alijibu Mfalme kantala



    "Sawa basi hutaweza kuuona mwili wa mke wako wala huyu mtoto wako" alizungumza Kisude na Mfalme kantala alimtizama.



    Alipewa ishara ya kukaa kwenye kiti kisha akakaa tena na kumtizama Kisude.



    Kisude alimpa ishara ya aongee.



    Mfalme alinyoosha mkono na NGOMA Zote ziliweza kuachwa kupigwa.



    "Umefika muda wa kumtawadha atakayekuwa Mfalme baada yangu" alizungumza Mfalme na Kisude aliendelea kutabasamu huku akimtizama Fancy aliyekuwa amefika eneo lile.



    Mfalme alitoa kofia lake la kifalme na kuanza kwa kusema



    "Kwa kuwa mwanangu hali yake siyo nzuri basi nitampa Ufalme kwa muda kwanza Mjomba wake Kisude na hali yamwanangu itakapo tengamaa basi Ufalme huu utarudi tena kwake" alizungumza Mfalme kantala akiwa na hasira juu ya Kisude



    "Haaaaa" wanakijiji ndiyo waliyobaki wakishangaa.



    Mfalme alianza kupiga hatua za kusogea mbele lakini mzee mmoja aliweza kukataa.



    "Siku ya Leo ilikuwa kwaajili ya Hancy kama atavikwa mtu mwingine Ufalme kwa siku ya Leo basi mji huu utatapaka damu"



    "Lakini Hancy anaumwa" alizungumza Kisude na alisikia sauti nyuma Yake.



    "Ila pia ameshapona" alizungumza Hancy ambaye alitokea nyuma ya Kisude na kumpita alitoa heshima kwa Baba yake na kuweza kupokea kofia ile ya kifalme.



    Aliivaa kisha akageuka na kumtizama Kisude



    "Kwanzia sasa Mimi ndiye Mfalme wa Isadora. Kisude pamoja na mwanao Fancy mnahukumiwa kunyonga walinzi kamateni hao na mkawanyonge"



    Kisude alicheka na kumwambia.



    Walinzi wote wapo chini yangu Leo ni siku yangu tu lazima niwe Mfalme.



    "Sidhani kama hilo litawezekan" alizungumza Mfalm Nuhu aliyekuja na maaskari zake walikwisha washindwa walinzi wote wapinzani na kuwabeba baadhi yao.



    "Mimi sijafanya chochote alizungumza Fancy na ghafla alisikia sauti ikimtaka anyamaze.



    Alikuwa akija Sikitu huku akiwa amembeba Malikia mgongoni mwake aliyekuwa tayari amekwisha fariki.



    Wewe na Baba yako ndiye mliyeweza kumfanya Malikia Maua hivi" alizungumza Sikitu na kuudondosha mwili wa Malikia akiwa anajikongoja taratibu kabisa wakati huo nao alionekana Mganga kipande akituma kombora lake la kumfuata Mozah.



    Wakati huo nao Mozah alikuwa amesimama pembeni ya Fancy na Zawadi aliyekuwa amemshikilia



    "Kombora lilienda moja kwa moja na kabla halijaweza kumfika Mozah tayari Sikitu alikuwa amesimama mbele ya Mozah na kumbora lile liliweza kumpata Sikitu aliyemdondokea Fancy na kuchomoa kisu alichokuwa amekificha kisha kumchoma nacho



    Wakati huo nao Kisude alitaka kukimbia lakini alipigwa mshale na aliweza kufia pale pale hivyo habari ya Fancy, Sikitu na Kisude zikawa zimeishia hapo



    Huku nyuma nako alionekana Mganga kipande kupigwa na kitu na kuweza kudondoka huku damu zikimtoka naye Malikia Samela baada ya kuona hivyo alianza kukimbia lakini na yeye hakufika mbali alijikwaa na kudondokea kwenye kiski kilichomchoma tumboni



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/





    MWISHO



0 comments:

Post a Comment

Blog