Search This Blog

UTAJIRI WA DAMU - 3

 





    Simulizi : Utajiri Wa Damu

    Sehemu Ya Tatu (3)



    "Aliniambia kazi yangu ni kusimamia magari yake.

    "Kwani yule mzee hana watoto au mke?"

    Moyo wangu ulienda mbio kwa sababu niliona kama askari yule aliyekuwa akinihoji pale kwenye kituo cha polisi kama alikuwa ananitega.

    Lakini pia nilikuwa nawaza kwamba kama wakiamua kwenda kuikagua nyumba ya mzee Mitimingi ni wazi mbwamtu watamuona na kile kiganja cha mtu watakiona.

    Nikawa najiuliza ikitokea hivyo moja kwa moja nitaingia matatani. Sikujua hawa polisi waliambiwa na nani kuhusu ushirikina wa yule mzee.

    "Kwani nyinyi nani amewaambia kuwa mzee Mitimingi ni mshirikina?" Nilijikakamua kumuuliza yule askari.

    Aliacha kuandika, akaniangalia kama vile alikuwa akitafakari kitu. Unajua askari wa upelelezi wana akili ya kwenda mbele zaidi kwa kila kitu.

    "Nakuona kama una wasiwasi."

    "Wasiwasi wa nini? Nakuuliza ili niwez

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/e kujua na mimi, mbona wewe unanihoji."

    "Kwa kawaida mtuhumiwa ndiye anayehojiwa polisi na kazi yake kujibu siyo kuuliza tena suala linalohusu alichoitiwa. Unaweza kunihoji ili nikikupa jibu ukwepeshe ukweli."

    "Haya endelea kunihoji." Nilisema huku nikibongesha simu yangu ya kiganjani, nilipolifikia jina la mzee Mitimingi nikabofya ili iite, iliita akaipokea. Nilifanya hivyo ili asikie yale mahojiano. Simu yangu nikaiweka kwenye shavu kama vile nilikuwa naitumia kukuna shavu langu.

    "Mzee Mitimingi alikuambia kazi yako ni kusimamia magari yake, kwani wewe ni fundi makenika?"

    "Hapana, hakuniambia kusimamia mambo ya ufundi."

    "Sasa alikuambia usimamie nini kama wewe siyo fundi makenika."

    "Mimi kazi yangu ni kukusanya fedha zake, yaani kwenye mabasi na kwenye malori nilikuwa nakusanya fedha na kuzipeleka benki."

    "Ahaaa kwani wewe umesomea uhasibu?"

    "Hapana. Kazi yangu hiyo nilijifunza nyumbani tu na pale nimepata uzoefu zaidi."

    "Sawa. Hujawahi kusikia lolote kuhusu mzee Mitimingi kuua watu?"

    "Ningesikia kuwa anaua watu nisingeweza kukaa pale na kufanyanaye kazi."

    "Niambie pale nyumbani kwake ni nani hasa wanaopenda kwenda na kwa muda gani?"

    "Pale wanaofika ni madereva wake na mara nyingine hawamkuti wananikuta mimi."

    "Anakuwa amekwenda wapi?"

    "Ana mambo mengi, siwezi kujua labda siku ambazo ananiaga."

    "Siku ambazo amekuwa akikuaga, huwa anasema anakwenda wapi?"

    "Huwa anasema anakwenda kutembea au anakwenda kwenye mipango yake."

    "Mipango gani?"

    "Huwa haniambii."

    "Mke wa mzee Mitimingi yupo wapi?"

    "Aliniambia ni mgonjwa na amelazwa."

    "Wapi?"

    "Hospitali ya Dk. Mei Chilungoli."

    "Kwa nini ameamua mkewe alazwe huko?"

    "Daktari yule ni mtu wa kwao, tena ana utaalam wa hali ya juu kwa magonjwa ya akina mama."

    "Wewe unamfahamu Dk. Mei?"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Namfahamu kwa kuwa siku nyingine huwa anakuja nyumbani kumtibia huyo mama."

    Baada ya mahojiano hayo yule askari alikwenda kumuona mkuu wake ambaye ni Inspekta Ado.

    "Subiri nikamuambie afande haya uliyoyasema tuone atashauri nini."

    Aliinuka na kuniacha nikitafakari, kisha nikakata simu.

    Baada ya dakika chache niliitwa kwenye ofisi ya Inspekta Ado. Niliingia nikamkuta akipekuapekua lile jalada lenye maelezo yangu.

    "Binti nimesoma maelezo yako hapa nadhani subiri tumuhoji mlinzi wenu. Nimetuma askari wamemleta hapa."

    Baada ya dakika mbili niliona mzee Chambilecho akiingizwa katika ofisi ile. Shati lake lilikuwa limelowa jasho kama vile alikuwa anafanya mazoezi ya viungo na alikuwa na wasiwasi.

    Sikujua kwa nini alikuwa na wasiwasi kiasi kile kama kwamba kaambiwa ana kesi ya kujibu inayohusu mauaji. Aligeuka kuangalia nilipokuwa nami nikajifanya kutabasamu ili kumuondoa hofu.

    Hakuonekana kubadilika muonekano wa sura yake kwani bado alikuwa kama vile ananishangaa kuwepo pale. Nilihisi inawezekana yule mzee wa Kimakonde alikuwa anajua siri za mzee Mitimingi.



    Mzee Chambilecho aliingizwa moja kwa moja kwenye ofisi ya Inspekta Ado na aliyemuingiza humo ni yule askari ambaye alikuwa ananihoji mimi.



    "Chepriska nisubiri hapa ofisini kwangu. Nampeleka mlinzi wenu Mzee Chambilecho kwa afande."

    Sikuitikia kwa kutoa sauti isipokuwa niliitikia kwa kubetua kichwa tu, polisi yule alinielewa.



    Baada ya muda mfupi yule askari alirudi kwenye ofisi yake na kuniambia nahitajika kwa Inspekta Ado. Nilijiuliza maswali mengi kwamba kwa nini nami niitwe tena au kuna jambo amelisema yule mzee kuhusu mimi?





    Moyo ulinidunda wakati nasindikizwa na askari yule hadi kwenye ofisi ya afande Ado.

    "Karibu tena Chepriska. Nilihitaji unisaidie wakati wa kumuuliza maswali huyu mzee. Anajibu lakini baadhi ya maneno siyaelewe anachanganya na lugha ya kwao ambayo wewe nimeambiwa unaijua vyema."

    "Ni kweli, sisi ni kabila moja."Nilimjibu huku nikitafakari jambo.



    Nilimuona askari yule kuwa siyo makini kabisa. Nilijiuliza kama majibu ya yule mzee nikiyapotosha atajuaje?

    Hata hivyo, kati ya maswali yote aliyomuuliza sikuona hata moja la kumpotosha kwa sababu yalikuwa hayahatarishi usalama wangu au wa bosi wangu, Mzee Mitimingi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliulizwa alianza kazi lini na analipwaje pale, akajibu. Alihojiwa pia kama anahafamu biashara nyingine anayofanya Mzee Mitimingi ukiacha ya magari na nyumba za wageni.

    Hata hivyo, mzee huyo aliwaeleza kwamba mambo ya kazi za bosi wake hayajui na anachojua yeye ni kuja kazini saa kumi na mbili jioni na kutoka saa kumi na mbili asubuhi.



    Aliwachekesha maofisa wa polisi kwa kusema kuwa asubuhi mara nyingi huondoka saa moja na nusu au saa mbili kwa sababu maalum.

    Alipoulizwa sababu gani hiyo maalum inayomfanya ashindwe kuondoka kwenda nyumbani kulala japo kwa mchana huo alisema.

    "Achubuhi mara nyingi huwa nagoja chai. Nikinywa tu huyoo nachapalika kwendaga nyumbani."

    "Ina maana kinachokufanya uchelewe ni chai tu."

    "Wewe unaona kitu kidogo hicho? Wenchako bila chai kichwa kinauma."

    Baadaye tuliruhusiwa kuondoka kituo cha polisi kurudi nyumbani. Tulipotoka nje Mzee Chambilecho aliniuliza maswali mengi ya haraka haraka.

    "Tumeletwa hapa polichi kwani kuna nini?"

    "Nikuulize."

    "Uniulize mimi wakati nimekukuta wewe polichi?"

    "Wamekuuliza habari za Mzee Mitimingi, umesema hujui lolote, labda mzee ana tatizo."

    "Najua ana mataticho, si mgonjwa? Chacha ugonjwa na polichi wapi na wapi?"

    "Ngoja baada ya siku chache tutajua kwa nini wametuita huku.Wakinijulisha nitakuarifu." Niliyakatisha mazungumzo baada ya kulifikia gari ambalo lilikuwa pembeni ya kituo, mbali kidogo lakini ndani yake alikuwepo mzee Mitimingi.

    Alitoa macho kwa wasiwasi alipotuona tukitoka kituo cha polisi. Hakujua kama mlinzi Chambilecho naye alikamatwa.

    "Wewe umekuja kufanya nini hapa polisi?" alimhoji kwa ukali yule mlinzi.

    "Nzee chi wale polichi walikuja tena na gari lao, wakanichukua, chijui kuna nini kabichaaaa!!!"

    "Sawa. Chepriska, wewe una akili sana maana mazungumzo yenu kati yako na polisi nimesikia kila kitu baada ya kunipigia simu, Nilipoipokea nikawa nasikia kama nami nilikuwa ndani ya kituo cha polisi. Wewe ni mbunifu sana."

    "Nakushukuru mzee."

    Tulitoka pale polisi na kwenda moja kwa moja sokoni kununua mahitaji.Tulinunua mchele, unga wa mahindi na ngano, sukari, nyanya, vitunguu, mchicha na nyama ya kusaga.

    Baadaye tulipitia kwenye nyumba zake za wageni mbili, nadhani alikwenda kuchukua fedha kwani hakuishia hapo, tulikwenda pia kwenye mabasi yake, stendi kuu na kukuta manne yamefika isipokuwa moja ambalo madereva walisema limeharibika njiani.

    Tulitoka na kufika nyumbani kwa Mzee Mitimingi ajabu ni kwamba tulikuta polisi wamejaa tele nje ya geti. Wote tulianza kutetemeka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Polisi baada ya kuona gari tulilokuwamo walionyesha kana kwamba walikuwa wakitutii kwani waliweka gari lao kando na kutupisha.

    Tukiwa ndani ya gari tuliangaliana tusijue la kufanya, haraka haraka nikamtazama mzee Mitimingi, sura yake ilijaa uoga.

    “Kwani kile kiganja kimo ndani?” nilijikuta nimemuuliza.

    “Kimo ndani, kwani wewe uliwaambia chochote kuhusu hilo?”



    “Hata kichaa hawezi kuwaambia kwa sababu kama ningewaambia ina maana ningejiweka matatani mimi na wewe ndiyo maana nakuuliza kama kiganja kipo ndani au ulikitoa.”

    “Kiganja kimo ndani, tena sehemu mbaya sana,”

    “Tumekwisha.” Nilisema huku nikimuangalia mzee Mitimingi.

    “Kuna mtu una ugomvi naye?” nilimuuliza.

    “Sisi wafanya biashara tuna maadui wengi, si unajua watu wana wivu?”

    “Sasa sijui tutafanya nini kuokoka na haya majanga. Endela kujifanya mgonjwa,” nilimshauri huku nikiwaza jinsi ya kuwafanya polisi wasiwe na wasi wasi na sisi. Nilishuka kwenye gari nikaenda pale walipokuwa.

    “Jamani kulikoni tena? Naona mmetufuata huku nyumbani?”

    “Tumeambiwa na Inspekta Ado kwamba tuje kupekua nyumba.”

    “Lakini mnapekua nyumba kwa sababu gani? Au mnatutuhumu nini?” niliuliza huku moyo wangu ukidunda.

    “Sikiliza Cheprisca. Polisi ukiona wanafuatilia jambo ujue kuna ukweli fulani. Sisi tumeambiwa huyu mzee wako Mitimingi ndiye anayehusika na vifo vingi sana vinavyotokea hapa mjini. Ni vigumu sana kuamini au kupata ushahidi kwa sababu ni mambo ya kishirikina.”

    Geti lilifunguliwa na Mmakonde mzee Chambilecho.

    “Chacha dada Cheprishika, hawa polichi wanataka nini kwetu hapa?” aliuliza yule mzee mlinzi.

    Sikumjibu chochote. Polisi waliingia ndani ya ua na gari lao na mimi pamoja na mzee Mitimingi tukatangulizwa mbele. Kulikuwa na polisi wenye silaha wanne na ambao walikuwa wamevaa kiraia watatu akiwemo yule mama aliyekuwa akituhoji, walivalia magwanda ya polisi.

    Tulipoingia ndani walituonyesha hati ya upekuzi yaani search warrant na walikuwa na mtu mwingine ambaye raia aliyeishi katika ule mtaa kama shahidi.

    “Tumekuja kusachi nyumba hii kwa sababu tumeambiwa kuwa kuna vitu vipo ambavyo hairuhusiwi kisheria wananchi kuvimiliki,” alisema yule mama huku akimuangalia mzee Mitimingi.

    “Mzee umenielewa?” aliuliza baada ya kuona hakuna mtu aliyemjibu.Walianza upekuzi wao jikoni kwa kufunua makabati yote lakini hawakukipata hicho walichokuwa wakikitafuta.

    Baadaye waliingia chumba cha wageni wakapekenyua vitanda, makapeti, makabati na hata magodoro mawili yaliyokuwa kwenye vitanda viwili chumbani humo, lakini hawakuona kitu walichokuwa wakikitafuta ambacho mimi nilikuwa sikijui.

    “Wewe Cheprisca, hiki ni chumba chako?” Yule askari wa kike aliniuliza. Nilikataa kwa kutikisa kichwa.

    “Wewe unalala wapi?”

    “Mimi nina chumba changu.”

    “Kipi kati ya hivi hapa ndani?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Niliposema nina chumba changu nina maana siyo humu ndani, nina maana kuwa nimepanga huko mtaani.”

    “Kwa nini upange wakati mzee wako ana nyumba kubwa hapa na haina watu wa kuishi?”

    “Niliamua tu kukaa kivyanguvyangu, najitegemea.”

    Baada ya polisi hao kupekua chumba cha wageni waliingia katika stoo. Humo walikaa muda mfupi sana kwa sababu hakukuwa na makorokoro mengi, kulikuwa na kigunia cha mchele na unga kilo kumi, maharage na njugumawe kama nusu salfeti.

    Lakini wakati maofisa makachero hao wa upelelezi wanatoka katika chumba hicho juu ya kabati waliona gunia likiwa limetundika juu ya waya. Walilifungua na kukuta ndani kuna ngozi za chui mbili.

    “Mzee una kibali cha kumiliki ngozi hizi?”

    “Sina,” alijibu mzee Mitimingi.

    “Hujui kuwa na vitu kama hivi ni kosa kisheria? Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Hamisi Kagasheki kila siku anatangaza vita dhidi ya wanaoua wanyama pori, hujasikia vita hivyo?”

    “Nimewahi kusikia.”

    “Sasa wewe unambishia siyo?”

    ”Hapana.”

    Waliendelea na ukaguzi wao, waliingia hadi vyooni baadaye walihamia chumba cha mzee Mitimingi. Wakati makachero wale wanaingia katika chumba cha mzee, alianza kutetemeka kama vile amemwagiwa maji ya barafu.

    Walipoingia na kufungua kabati la nguo walikumbana na kiganja cha mtu kilichokaushwa.Wakapekua sanduku wakakutana na fuvu la mtu na mifupa ya mkono ikiwa imezungushiwa nguo nyeupe.

    Ndani ya sanduku hilo walikuta tunguri mbili zilizokuwa zimevishwa mavazi yaliyokuwa yametapakaa mafuta.

    “Mzee hivi vitu vya kwako?” aliuliza kiongozi wa wale polisi, Mzee Mitimingi hakujibu kitu badala yake mkojo ukawa unamtoka.





    Upekuzi wa polisi katika chumba cha mzee Mitimingi ulichukua muda mrefu hasa baada ya kukuta viungo hivyo vya binadamu ambavyo vilionesha dhahiri kwamba vinahusiana na mambo ya kishirikina.

    "Cheprisca, unajua vitu hivi ni vya nini?"

    Nilikataa kwa kubetua mabega bila kutoa sauti.

    Baadaye walifunua kapeti jekundu chumbani mle na kukuta furushi la nywele. Mwili ulinisisimka kwa kuwa nywele zile nilivipeleka mimi kwa mzee Mitimingi.

    Niliingiwa na woga kwa kuwaza kwamba kama mzee huyu atasema aliyezileta nywele zile ni mimi ni wazi ataniingiza katika matatizo mazito.

    Polisi wanaweza kuamini kuwa hata kile kiganja na fuvu nimemletea mimi. Niliwaza kuwa makachero wataweza kunitesa ili niseme ni kiganja cha nani wakati sijui chochote kuhusu vitu hivyo.

    Baadaye yule kiongozi mkuu wa polisi katika upekuzi ule aliviandika vitu alivyovikuta kuwa amevikuta ndani ya chumba cha mzee Mitimingi kisha akamtaka yule raia ambaye alijitambulisha kwa jina la Ben Mtwanga, mjumbe wa nyumba kumi , atie sahihi maelezo kama shuhuda.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Bwana Ben Mtwanga wewe ni mjumbe wa nyumba kumi katika mtaa huu na nimekuandika na umetia sahihi kama shahidi wa polisi. Nikufahamishe tu kwamba ukihitajika kutoa ushahidi mahakamani, tutakuarifu. Umeelewa?"

    "Nimeelewa," alijibu Mtwanga.

    Polisi waliingia chooni kwa mzee Mitimingi kusachi lakini hawakupata kitu chochote cha maana na baadaye wakaingia katika chumba chakuhifadhi spea za magari yake.

    Ndani ya chumba hicho walitoa meno kadhaa na kucha za simba ambazo zilikuwa zimewekwa kwenye kibuyu. Ajabu ni kwamba kila akiulizwa swali kuhusiana na vitu hivyo, mzee Mitimingi alikuwa hajibu badala yake akawa ananiangalia mimi.

    Nilizidi kuingiwa na woga kwa kudhani kwamba anaweza kunisukumia mimi msala huo wa kukutwa na viungo vya binadamu na nyara za serikali, jambo ambalo sasa serikali inalipiga vita sana.

    "Koplo John, nenda na Bwana Mtwanga mkakague mabanda nje," aliamuru kiongozi wa polisi. Moyo ulinipasuka paa'. Ulinipasuka kwa sababu nilijua kuwa siri ya mbwa mtu itabumburuka.

    Walianza kuingia katika banda la kuku lakini hawakukuta chochote kisha wakaingia katika banda la ng'ombe.

    Wakati wakiendela kukagua vyumba hivyo mbwa mtu akawa anabweka kama ishara ya kuwaita polisi.

    "Inaelekea mbwa huyo anayebweka ni mkali sana. Tusikaribie banda lile, anaweza kuchomoka akang'ata watu. Muda wa kuchomwa sindano za tetenasi saa hizi hatuna," alisema yule askari kiongozi wa upekuzi.

    "Lakini kule kwetu wazee wanasema ukiona mbwa anabweka sana ujue kuna kitu," alidakia askari mwingine na kunifanya nisikie tumbo langu likinguruma kwa woga maana nilijua kuwa wakienda na kumkuta mbwa mtu, mambo yatakuwa mazito zaidi.

    "Hizo imani zimepitwa na wakati. Mbwa yule ni mkali na anatamani ararue mtu," alisisitiza yule bosi wa polisi.

    Majibu hayo yalinifanya nipate faraja na hata nilipomuangalia mzee Mitimingi alionekana kufurahia uamuzi wa kuachana na wazo la kwenda kupekua kibanda cha mbwa.

    ;Wangejua kuwa banda lile lina kiumbe wa ajabu kamwe wasingeacha kwenda kupekua na kujua siri ya mbwa yule kuwa na sura za binadamu,' niliwaza kimoyomoyo.

    Mimi pia nilitamani sana kujua ilikuwaje mbwa yule awe na sura ya binadamu. Lakini tamaa yangu ya kujua hayo ilikatizwa na vile vitu hasa nywele kwa sababu nilijua kuwa mzee Mitimingi akibanwa anaweza kunitaja mimi kuwa ndiye mletaji.

    "Sasa mzee Mitimingi, hebu tueleze, hivi vitu ni vya nini na umevipata wapi?" alihoji askari mmoja huku akiwa na daftari lake alilokuwa akitumia kuandika vitu vilivyokutwa ndani ya nyumba ya mzee huyo, alikuwa akingoja jibu aandike.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MZEE Mitimingi alishindwa kutoa jibu badala yake alikuwa akitetemeka huku akitokwa na jasho jembamba usoni.

    Ilibidi awe anatumia leso kuondoa jasho lililokuwa likivuja usoni mwake.

    Baadaye askari walielekea kwenye banda la mbwa na wakati huohuo mbwa huyo akawa anabweka kwa nguvu sana.

    "Huyu mbwa ana jambo, haiwezekani awe akibweka namna hii," alisema askari mmoja aliyeonekana kuwa ni kiongozi wa oparesheni hiyo ya upekuzi.

    "Tuhamie kwenye banda la mbwa," aliamuru.

    Umati wote ulianza kuelekea kwenye lile banda ambalo mbwa alikuwa akibweka.

    "Mzee Mitimingi au wewe Cheprisca mtangulie, mumtoe mbwa kibandani ili tukague ndani."

    Maneno hayo yalimfanya mzee Mitimingi azidi kuingiwa na wasiwasi na kunyong'onyea. Ilikuwa karibu adondoke kutokana na wasiwasi aliokuwa nao.

    Alilisogelea banda la mbwa na kulifungua. Mbwa haraka sana alichomoka bandani na kuanza kugalagala chini kabla ya kuketi na kutukodolea macho.

    Watu wote walipigwa na mshangao kuona mbwa huyo ana sura ya binadamu. Mbaya zaidi alikuwa akitokwa na machozi kama afanyavyo mtu ambaye ameteswa sana na sasa anataka huruma ya mtesaji.

    "Mzee Mitimingi, huyu ni mbwa au jini?" aliuliza askari mmoja.

    "Naam," aliitikia mzee Mitimingi.

    "Unaitikia nini? Jibu swali huyu ni mbwa au jini? Mbwa gani ana pua na macho kama ya binadamu, tena analia machozi kama mtoto wako?"

    Hakuweza kujibu na badala yake akawa ameinamisha kichwa chini kwa aibu ya kugundulika siri zake.

    Yule askari baada ya kuona mzee Mitimingi hajibu lolote aligeuka na kuniangalia mimi. Alipiga hatua kama tatu na kufika karibu kabisa na niliposimama.

    "Chepriska, unaweza kutusaidia, huyu ni mbwa au jini?"

    "Mimi sijui."

    "Hujui wakati mbwa mtu huyu yupo hapa kwenu? Ina maana wewe hujawahi kumuona humu?"

    "Niliwahi kumuona, lakini chochote kuhusu mbwa mtu huyo anajua mzee, mimi sina ninalolijua."

    "Unataka kutuambia wewe mara baada ya kumuona mbwa huyu wa ajabu ambaye dunia nzima hayupo kama huyu hukumuuliza mzee wako?"

    "Nilimuuliza, mimi pia siku ya kwanza kumuona nilishangaa."

    "Alikujibu nini mzee wako?"

    "Aliniambia kuwa hadithi ya mbwa huyo ni ndefu."

    "Hebu tusimulie hadithi yake maana kama ulivyoona mzee Mitimingi ameshindwa kujibu maswali yetu ya awali."

    "Hakunisimulia chochote bila shaka alikuwa akitafuta nafasi ya kufanya hivyo."

    Askari aliyekuwa akinihoji aliandika mambo fulani kwenye daftari lake kisha akaniangalia usoni.

    "Wewe Cheprisca baada ya kumuona mbwa huyu kuwa ni wa ajabu, uliripoti popote?"

    "Hapana."

    "Kwa nini?"

    "Niliogopa."

    "Uliogopa kudhurika na jini au ulimuogopa mzee Mitimingi?"

    "Niliogopa vyote, kudhurika na hata mzee kwani alishawahi kunionya."

    "Aliwahi kukuonya kuhusu nini?"

    "Kuhusiana na huyu mbwa."

    "Ilikuwaje mpaka akakupa onyo."

    "Siku moja nilimuona mbwa huyo akiwa anamchapa, akanionya kuwa nisimuambie mtu na kama nitakiuka basi kilichompata mbwa huyo kitanipata na mimi."

    "Alikuambia kuhusu kilichompata huyo mbwa?"

    "Hapana hakuwahi kuniambia."

    "Kwa nini usimuulize."

    "Sikumuona mbwa huyu siku nyingi, nilimuona juzi tu na leo ndiyo tulipanga anielezee historia yake ambayo alisema ni ndefu sana."

    Askari yule alitulia kidogo, akachukua daftari lake na kalamu na kuanza kuandika, bila shaka alikuwa akiandika yale niliyomuambia.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Umesema siku ya kwanza ulimuona akimchapa mbwa huyu, ilikuwaje? Fafanua kidogo."

    "Siku hiyo nilifika hapa nyumbani kama saa kumi na mbili jioni. Nikasikia mbwa akilia, nilichungulia kwenye tundu la geti nikamuona mzee huyu akimchapa huyu mbwa huku akitamka maneno."

    "Alikuwa anasemaje?"

    "Alikuwa anasema, nakupiga kutokana na kutotimiza masharti niliyokupa."

    "Wafunge pingu," yule afisa wa polisi aliamuru, tukafungwa.





    Baada ya kufungwa pingu mimi na mzee Mitimingi, yule askari aliyekuwa akihoji alitulia kidogo, akachukua daftari lake na kalamu na kuanza kuandika, bila shaka alikuwa akiandika yale niliyomuambia.

    Askari walikagua ndani ya banda la mbwa lakini hawakuweza kuambulia chochote.

    Yule askari aliyekuwa akionekana kama kiongozi wao alimgeukia mlinzi korokoroni wa mzee Mitimingi ambaye ni mzee wa Kimakonde aitwaye Chambilecho, alikuwa haelewi kinachoendelea kutokana na yeye ;kuganda' getini.

    "Wewe askari, njoo," aliitwa kwa sauti kama ya amri ya kijeshi na akatimua mbio kwenda kwa bosi wa askari huyo ambaye alikuwa na redio call mkononi.

    "Wewe uliitwa polisi ukahojiwa, kweli au si kweli?"

    "Kweli."

    "Unajua chochote kuhusu mbwa huyu?"

    "Chijui kitu."

    "Aliletwa lini?"

    "Chijui kabichaa, nilishitukia akibweka."

    "Lini?"

    "Nimechahau chiku."

    "Huyu mbwa umewahi kutumwa kumpa chakula kwenye banda lake?"

    "Nzee aliniambia ni malufuku kuchogelea banda lile."

    "Alikupa sababu?"

    "Hakuchema."

    "Uliwahi kumuona?"

    "Nimuone wapi? Nilikuwa nachikia akibwekabweka tu."

    Yule askari hakuona sababu ya kuendelessa kumhoji korokoroni huyo bila shaka kutokana na kutojua kila analoulizwa.

    "Sasa mzee Mitimingi funga nyumba yako kwa funguo na mkabidhi lindo mlinzi wako. Tunakwenda Kituo cha Polisi Nyasa, mambo mengine ataenda kuamua Afande Ado,"aliamuru askari yule.

    "Koplo Anjela utakaa na Chepriska nyuma na mzee Mitimingi pia atakaa nyuma ya gari na askari wengine," alizidi kufafanua.

    Nilisaidiwa kuingia kwenye Defender' na yule askari wa kike, haikuwa kazi kubwa kwangu kuingia nyuma ya gari hilo isipokuwa shughuli pevu ilikuwa kwa mzee Mitimingi.

    Kutokana na utu uzima wake na unene alishindwa kupanda mwenyewe na hata askari mmoja alipojitahidi kumpandisha alishindwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilibidi askari watatu wafanye kazi ya kumpandisha kwenye gari mzee huyo. Mmoja alikuwa ndani na wawili walikuwa nje ya gari wakawa na kazi ya kumpandisha garini.

    "Mzee Chambilecho usisahahu kumpa chakula mbwa," alisema mzee Mitimingi huku akimuangalia mlinzi wake.

    "Chacha nzee chakula umiweka wapi?"

    "Angalia nyuma ya banda kuna chakula maalum cha mbwa cha kwenye makopo. Kuna katoni moja, utakuwa unampa asubuhi na jioni na maji yasikauke kwenye banda lake. Sawa?"

    "Chawachawa."

    Askari ambaye alikuwa kiongozi wa msafara alimsifu mzee Mitimingi kwa kukumbuka mbwa kulishwa chakula.

    "Umefanya vizuri sana kukumbuka hilo maana hii kesi yako inaweza kuwafanya tukawashikilie kwa siku kadhaa."

    "Mtanishikilia siku ngapi?"

    "Itategemea! Hii kesi imeingilia majanga ya nchi," alisema askari yule.

    "Hii kesi ina majanga, mbona sikuelewi?"

    "Hunielewi nini? Ndani ya nyumba kuna kiganja cha mtu, hatujui ni cha mtu wa kawaida au ni albino kutokana na kubadilika rangi na kukaushwa na kuwa cheusi."

    "Lakini

    "Lakini nini? Hata kama mtu aliyekatwa siyo albino bado kukutwa na kiganja ni kesi nzito sana kwa sababu ni jinai. Ni majanga kwa sababu kuna kesi mbili."

    "Ipi na ipi afande!" alihoji dereva wa askari.

    "Kuna kesi ya kiganja na kuna kesi ya kukutwa na ngozi za chui. Kule kukutwa na nywele siyo kitu sana kwa sababu hata mahakamani anaweza kusema ni zake au za nduguye."

    "Sawa afande na huyu dada Chepriska je?"

    "Huyu anaweza akawa na kesi nyepesi sana kama ataweza kujieleza vizuri."

    "Kwa nini?"

    "Kwa sababu hata katika mahojiano hapa sikuona kama ana kesi ."

    Gari liliwashwa na hatukuchukua muda mrefu, tulifika kituoni na moja kwa moja tukaenda ofisini kwa Inspekta Ado.

    "Afande tumekuta kiganja, ngozi ya chui na nywele, pia kuna mbwa mtu nyumbani kwa mzee huyu."

    Afande Ado aliviangalia vitu vilivyotajwa na kumuangalia mzee Mitimingi na mimi.

    "Mzee kwa usalama wako tuambie ukweli."alisema Inspekta Ado akiwa amekunja sura.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog