Search This Blog

BINTI WA PILI WA MFALME - 3

 







    Simulizi : Binti Wa Pili Wa Mfalme

    Sehemu Ya Tatu (3)



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alianza kuyafumbua macho yake kwa taratibu kabisa na hapo alikutana na sura ya Hancy.



    " Mozah, uko salama?? Unajisikiaje sasa???



    "Embu sogea" alizungumza Fancy na kumsogeza Hancy pembeni.



    "Embu inuka kama unaweza; alizungumza Fancy na Mozah alijitahid kuamka.



    " ammhhhh tumesharudi nyumbani, samahani kwa kuweza kuikatiza safari yenu " alizungumza Mozah.



    "Hivi wewe nimekuuliza Zaidi ya Mara ngapi kama unaumwa au lah na ukanijibu kuwa huumwi........ Kwanini lakini eti?? Aliuliza Hancy kwa hasira.



    "Samahani lakini" Alizungumza Mozah kwa sauti ya utaratibu.



    "Hiyo samahani yako inasaidia nini hivi unafikiri baba au mama yangu wangekuona katika halii hii si wangesema Mimi sikuwekei umakini......na kama ulikuwa mgonjwa kwanini nilivyoweza kukwambia twende wewe ukaja tu?? Aliendelea kufoka Hancy kwa hasira.



    " Samahani Hancy, nimeshakutaka radhi.... Naomba pia wote mnisamehe" alizungumza Mozah kwa sauti ya upole.



    "Hancy unaona unamfanya mpaka mtoto wa watu anaanza kulia?? Aliuliza Fancy kwa hasira na kusimama pale alipokuwa amekaa.



    "Sasa na wewe mbona Unataka kulia wakati wewe ndo umemgombeza mwenzako?? Aliyeweza Fancy na Hancy aliweza kutoka njee.



    "We Hancy si ninakusemesha...



    " Fancy.....nitaenda kuzungumza naye" aliongea Tom na kutoka njee katika kijumba walichoweza kufikia kwaajili ya kumtibu Mozah kabla ya kwenda nyumbani.



    Basi usilie mwaya alizungumza Fancy akimbembeleza Mozah huku Sarah na Sikitu wakiwa wanamtizama tu.



    "Hancy! Aliita Tom na Hancy aliweza kusimama huku akionekana kudondosha machozi.



    " Hancy...



    "Huyu Mwanamke ajui eti ananiumiza kiasi gani yeye anachukulia tu rahisi kwa kila jambo; hivi unajua alipodondoka nilishtuka sana nusura roho yangu initoke.. Nampenda sana Mozah sitaki kuona kitu chochote kibaya kikimtokea mbele yangu" alizungumza Hancy kwa hasira.



    "Sawa....sawa...nimekuelewa lakini punguza hasira kwanza..... Kisha tafuta muda mzuri uzungumze na Mozah kuhusu hili....... Sasa wewe unalia na yeye analia nani atambembeleza mwenzake?



    Muda ulienda na baadaye alionekana Mozah akiwa amepanda farasi mmoja na Hancy huku Hancy akiwa nyuma yake na kila mmoja akiwa kimya katika safari ile.



    " aaaaaahhhhhh me sijaipenda hii unafikiri tunaenda mazishini hata mazishini huwaga wanaimba nyimbo za mazishi alizungumza Fancy aliyeonekana kutopenda kabisa utulivu ule.



    "Mozah" aliita Fancy.



    "Abee"



    "Umeshamsemesha Hancy??



    Mozah hakujibu kitu zaidi ya kupandisha macho yake na kumtizama Hancy ambaye bado alionekana kuvimba kwa hasira.



    " aaaahhh kwani mnashida gani ninyi, si tumeshayamaliza" alizungumza Fancy



    "Kuna kitu nimesahau hivyo nitarudi nyie tangulieni alizungumza Hancy na kuanza kugeuka farasi.



    " Hancy si ungemtuma tu Tom" alishauri Sikitu.



    "Hapana nitafuata mwenyewe.



    " Sawa na Mozah na yeye?? Aliuliza Sarah aliyeonekana bado kuwa na wivu pindi awaonapo pamoja.



    "Nitapanda tu kwenye farasi wangu alizungumza Mozah na kutaka kushuka.



    " Unaenda wapi?? Aliuliza Hancy



    "Wewe si unarudi, sitaki kuwa mzigo kwako kwahiyo nitampanda farasi wangu hata hivyo naona Tom anapata shida kumuongoza.



    " Tom" aliita Hancy.



    "Wala sipati shida yoyote ile tena ninauwezo wa kuwaongoza farasi kumi nikiwa juu ya farasi wang" alizungumza na kucheka Tom



    Hancy alirudisha macho kwa Mozah ambaye alikosa cha kusema.



    "Haya sisi wengine twendeni Hancy anarudi na Mozah kule tulipoweza kutoka kasahau kitu kule....haya twendeni twendeni alizungumza na wote walianza kuvuta farasi zao kivivu kamba kwaajili ya Kuondoka.



    "Kaka aliita Fancy



    " Nini??



    "Ikumbukwe tu ya kuwa kitanda chenu kipo ngomeni" aliondoka kwa kuchka.



    "Mpuuzi huyu mtoto anadhubutuje kumwambia kaka yake maneno hayo" alizungumza Hancy na kuanza kumrudisha nyuma farasi.



    Alitembea kwa dakika Tatu kisha akasimamisha farasi.



    "Mbona umesimamisha hapa kwani haturudi tena?? Aliuliza Mozah na Ghafla alihisi mikono ya Hancy katika tumbo lake dogo.



    " Mozah......nahitaji unisamehe kwa kile nilichoweza kukifanya kwasiku ya Leo ila napenda utambue ya kuwa lile niliweza kulifanya kutokana na naumia sna pindi uwapo matatizoni na.......



    Kabla hajamaliza kuzungumza Mozah alimshika Mikono yake iliyokuwa katika tumbo lake kisha kukiegemeza kichwa chake katika kifua cha Hancy.



    "Haina haja ya kunitaka radhi Mimi pia ninamakosa katika hilo ila furaha sana baada ya kuona ya kuwa tumebaki wawili" alizungumza Mozah.



    "Nmhh alikohoa Hancy.



    " Kwanini kwani Kuna kitu ulitaka nipatia lakini ukashindwa kwasabab tuko wengi?? Aliuliza Hancy.



    "Ww unawaza nini wewe?? Aliuliza Mozah na kutoa kichwa chake katika kifua cha Hancy.



    " Hamna alijibu Hancy na kumkumbatia Mozah vizuri kabisa kisha kukilaza kichwa chake mgongoni mwake.



    "Twende basi tukachukue hicho kitu ulichoweza kukisahau.



    " Hmna nilichoweza kusahau, nilitaka tu tupate muda wetu wawili nikutake radhi" Alizungumza Hancy na kumfanya Mozah atabasamu kwa furaha na kuweza kuishika tena mikono ya Hancy kwa Mara nyingine.



    ***** katika kijiji cha Isambala *****CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Nzanza na Nzenze nahitaji muende katika mji wa Isadora na chochote kinachoendelea baina ya binti yangu na mtoto wa Mfalme basi mnitaarifu" alizungumza Mfalme Nuhu



    "Na mtamtumia ndege huyu katika kurudisha taarifa na mkumbuke mnahitajika kwenda kwa Siri sana mtu yoyote asiweze kuutambua uwepo wenu katika mji ule.



    " Ndiyo Mfalme " waliitika wote kwa pamoja na kisha wakakabidhiwa ndege kisha wakaanza safari.



    "Mtabiri Tambitambi, unafikiri hii itasaidia??



    " Kwanza tufahamu maisha anayoishi alafu kisha tuta tafuta njia nyingine ya kumsaidia Mozah kama itawezekana, kwani mpaka sasa sijapata kuona damu zozote katika maono yangu" alizungumza Mtabiri Tambitambi na Bi Lunde aliweza tu kushusha pumzi ndefu pasina kuongezea neno.



    Katika upande wa pili alionekana Mganga Kipande na Malikia Samela.



    "Imekuwaje sasa??



    "Bado kazi ni ngumu sana ila nitamsaidia kwa kiasi kikubwa Sikitu akapate kuolewa na Hancy kwani kama hataolewa basi hatapata chochote.



    " siyo hata pata chochote, hatutapata chochote kwasababu..... ni mtoto wetu mtoto wangu Mimi na wewe, kwahiyo akikosa kule na huku akigundilika siyo mtoto wa mfalme basi hatutapata chochote, hivyo lazima tuhakilishe anafanikiwa" alizungumza Malikia Maua.



    Error iliyoweza kutokea Malikia Maua ni mama wa Hancy na Malikia Samela ni mama wa Sikitu hivyo ni Malikia Samela.



    Tulipoweza kuishia tunaendelea.



    **** Katika kijiji cha Isadora *****



    "Ahaaaaa kwahiyo umeweza kurudi tena??



    " Sawa tuone utaendelea kubaki hapa mpaka lini?? Ilisikika sauti ya kike ikizungumza huku akimtizama Mozah aliyekuwa akija na Hancy na kupokelewa na Tom.



    "Natumaini safari yenu ya kurejea katika ufalme imekuwa nzuri sana" alizungumza Tom akimtizama Hancy.



    "Nzuri sana" alijibu Hancy na kumtizama Mozah



    "Naweza kutembea" alizungumza na kuanza safari ya kutembea lakini alishindwa na kudondokea Mkononi mwa Hancy.



    "Siipendagi ubishi wako kabisa" alizungumza Hancy na kumuinua Mozah kwa kum beba kisha kuelekea naye ndani.



    Watumishi waliwapa heshima huku wengine walicheka na kumtazama Mozah kwa uwivu.



    Mbele walikutana na Fancy ambaye alikohoa na kumtizama Mozah aliyekuwa akimuonea aibu.



    "Nipishe" alizungumza Hancy na kumsukuma Fancy aliyeweza kudondoka chini.



    "We Hancy,wewe inamaana nilikuwa sipishi amah" alizungumza Fancy na kuwafuata nyuma.



    "Kwanini umenidondosha eti?? Aliuliza Fancy akionekana mwenye hasira.



    "Ulisimama mbele yangu kwanini?? Aliuliza Hancy na kumuweka mkewe kitandani.



    " Kwahiyo kwaajili ya Mozah, ukanidondosha Mimi??



    "Ndiyo kwaajili yake naweza kufanya chochote" alizungumza Hancy akitania na ghafla aliweza kuyaona machozi ya Fancy.



    "Fancy, nakutania tu, siyo kwamba nilimaanisha hapana" alizungumza Hancy.



    "Kwaajili ya mwanamke wako ndo unanidondosha Mimi?? Aliuliza tena Fancy.



    " Fancy, nimeshakwambia nilikuwa nakutania na haikuwa nia yangu kukudondosha" alizungumza Hancy na kumshika Mkono Fancy.



    "Fancy......aliita Mozah ila alikatishwa na sauti kali kutoka kwa Fancy.



    " Usiongee chochote wewe mwanamke, kwasabab yako Hancy amenidondosha mimi.. Unafikiri nitakusamehe kwahili?? Aliuliza Fancy na kuachia kicheko.



    "Mmeogopa eeeeeee?? Aliuliza Fancy.



    " Mjinga wewe, umenishtua eti?? Alizungumza Hancy na kumsukuma kichwa Fancy.



    "Umeogopa eeeee aliuliza Fancy na kumsogelea Mozah aliyekuwa ameshtuka.



    " Ndiyo" alizungumza Mozah na kumtizama kwa wasiwasi Fancy.



    "Usiogope Fancy ni mtu mwenye utani sana" Alizungumza Hancy.



    "Na Mara kadhaa utani huo ndo uwaga ukweli tu" alizungumza Fancy.



    "Kamletee wifi yako maji ya kunywa kwanza, ameshtuka sana eti, na wakati mwingine usifanye hichi ulichoweza kukifanya Leo"



    "Ndiyo kaka samahani, Wifi samahani.... Alizungumza Fancy kwa sauti ya upole.



    "Nimekusamehe ila umeniogopesha eti"



    "Kamlete kwanza maji ya kunywa"



    "Ndiyo" alijibu Fancy na kutoka njee.



    Wakati anatoka aliweza kupishana na Stela ambaye aliweza kumtizama kwa macho ya mashaka na kuingia ndani ya chumba kile.



    ****** *** ******



    Sarah akiwa amekaa katika chumba alichoweza andaliwa aliingia mtu na kukaa katika kiti chake.



    " Mbona umekaa tu pasina kufanya chochote kitu juu ya Hancy na Mozah??



    "Nitafanya nini ilihali Hancy tayari kwasasa ni mume wa mtu na tayari ameshaweza kuvunja ahadi tuliyoweza kuiweka tukiwa wadogo, laiti ningelijua hichi ndicho ulichoweza kuniitia ningebaki zangu kwetu"



    "Kwahiyo umeshakata tamaa mapema yote hii?? Basi humpendi Hancy hata kidogo, Mimi nakusaidia wewe katika hili"





    "Nimeshazungumza naye na tumeshaelewana ya kuwa tutabaki kuwa marafiki tu na hakuna kingine kitakachoweza kuendelea. alizungumza Sarah.



    "Watu weupe wenzako wakijua umeweza kuzidiwa kiakili na mtu mweusi basi watakudharau sana" alizungumza binti yule na kutoka njee.



    "Njoo" aliita Sarah na hatimaye alionekena Zawadi akigeuka.



    Mozah!! Ilisikika sauti ikiita



    "Abeeee mama"



    "Ammmhhhh hivi Fancy ni......... Au acha tu"



    "Kuna kitu unataka kuzungumza mama?? Aliuliza Mozah.



    " hapana achana nayo,ntachunguza mwenyewe " alizungumza Stela na kuendelea kuchana nywele za Mozah.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Ila alionekana mtu mwenye wasiwasi na mashaka kidogo juu ya kitu fulani.



    "Hodi!! Ilikuwa sauti ya Hancy na Stela aliweza kucheka baada ya kumuona.



    "Karibu ndani mtoto wa Mfalme Kantala"



    Hancy alipiga hatua za kivivu na kuingia ndani ya chumba.



    "Hancy" aliita Mozah.



    "Mi nawapisha" alizungumza Stela na kutoka njee.



    "Mama sasa nani atanichana?? Aliuliza Mozah.



    Stela alimtizama Hancy na kutoka tu njee akiwa anatabasamu.



    " Kwanini ananitizama huku anacheka?? Aliuliza Hancy na kumfanya Mozah ageuke kumtizama.



    Baada ya Mozah kumuona Hancy na yeye alicheka.



    "Unanicheka kwanini?? Aliuliza Hancy na kumsogelea Mozah.



    Mozah alisimama na kumtizama usoni.



    " Kuna nini mbona unanitizama sana usoni?? Aliuliza Hancy na Mozah alimshika Mkono akampeleka kwenye kioo kisha akamkalisha.



    "Mama" alizungumza Hancy kwa kuogopa na kusimama juu.



    "Mpumbavu huyu ndo kanifanya Mimi hivi?? Alizungumza Hancy.



    " Nani huyo?? Aliuliza Mozah.



    "Hmna mtu alisema na kucheka tu Hancy kisha akamvuta Mozah katika mapaja yake



    " Nisafishe basi uso kwa mate yako" alizungumza Hancy.



    "Kwa mate yangu, kwanini mate yangu?? Aliuliza Mozah na kutaka kusimama lakini Hancy aliweza kumzuia.



    " Sawa basi Nisafishe kwa nguo yako" alizungumza Hancy na kumfanya Mozah amtizame usoni mwake kisha kucheka.



    "Nifute bana haya masinzi" alizungumza Hancy na Mozah alitoa kitambaa chake kisha akakiweka mdomoni mwake, na kuanza kumpangusa taratibu kabisa, aliweza kufika katika upande wa lipsi na Hancy alimshika Mkono.



    "Mozah naweza kukuomba kitu?



    Mozah alitikisa kichwa ishara ya Ndiyo.



    " Kote umenifuta na kitambaa chako kwa mate yako je hapa mdomoni unaweza ukanifuta na lipsi zako kwa mate yako?? Aliuliza Hancy na kumfanya Mozah akiwa amebaki katika mshangao.



    "Unaongea nini wewe?? Aliuliza Mozah na kumtupia kitambaa chake Hancy.



    " Mozah....... Aliita kwa sauti ya upole na kusimama kwa kumfuata Mozah aliyekuwa amesimama.



    "Namaanisha eti, unaweza ukazifuta lipsi zangu kwa kutumia lipsi zako na mate yako??



    Mozah alibaki akimtizama Hancy usoni mwake na kujikuta akishindwa kuongea kutokana na Hancy kumshika mikono yake na pia kuziweka pumzi zake Karibu na Mozah.



    "Mi sijawahi" alizungumza Mozah.



    "Sawa kama huwezi" alizungumza Hancy na kutoka Mikono yake katika mikono ya Mozah kisha kurudi kwenye kiti na kuanza kufuta lipsi zake.



    Mozah alimzuia kisha akachukua rangi ya mdomo nyekundu kisha kumpaka Hancy mdomoni.



    "Nmekwambia sijawahi siyo kwamba siwezi, hivyo funga macho yako ili nisione aibu" alizungumza Mozah na Hancy alichukua rangi ya mdomo na kuikoleza Zaidi sehemu zake za lipsi.



    Kisha akayafumba macho yake.



    Mozah alianza kupeleka lipsi zake taratibu kabisa kwaajili ya kumbusu lakini katika mlango wao alionekana mtu akishuhudia kitendo kile na kushikwa na hasira kwa kukwangua mlango ule kisha kudondosha kitu ili tukio lile lisiweze kuendelea.



    Ilipoishia ni baada ya kuonekana mtu ambaye hakuweza kupend kile kilichokuwa kinaelekea kutokea baina ya Hancy na Mozah.



    Mozah alijitoa mapajani mwa Hancy ambaye aliweza kumrudisha na kumrukia mdomoni mwake.



    Mozah alijitahid kujitoa lakini baada ya muda sasa, yeye ndiye aliyeonekana kutokutaka kumuachia Hancy.



    "Kaka" aliita Fancy ambaye aliweza kuingia ndani na baada ya kukuta hali ile aliweza kufumba macho yake.



    "Samahani jamani, nilikuja kuleta taarifa..........Hancy baba anakuita" alizungumza Fancy.



    "Ammmhhhh tumeshamaliza alizungumza Mozah na kutaka kuondoka.



    " Bado.....alijibu Hancy na kumvuta Mkono Mozah.



    "Hancy......... Aliita Mozah.



    " Bado....rangi ya mdomo haijaisha" alizungumza Hancy na kumshika kiuno Mozah kisha kumuweka karibu kabisa na kifua chake.



    "Baba anakuita" alirudia kauli ile Fancy.



    "Mwambie hujaniona.....au mwambie yuko chumbani na mkewe Mozah" alizungumza Hancy na kujilaza mgongoni mwa Mozah.



    "Muone hata Mimi nitapata mume wangu, unaniringishia nini sasa, na ninaenda mwambia uko ndani lakini hutaki kutoka" alizungumza Fancy.



    "Kamwambie vyovyote utkavyo, lakini nisikukamate" alizungumza Hancy na kumbusu Mozah mgongoni ambaye alionekana kuona aibu.



    "Lione" alizungumza Fancy.



    "Linani?? Aliuliza Hancy na kuanza kumtoa njee Fancy



    "Hancy niache....niache wewe nimekwambia"



    "Alafu hakikisha hakuna mtu anakuja kugonga tena hapa ukae hapo....sawa"



    "Sitaki, alizungumza Fancy.



    " Utaona kama nitakupa ile Zawadi yako Leo" alizungumza Hancy.



    "Umeniletea!? Aliuliza Fancy kwa mshangao.



    " Ndiyo ila sikupi maana hunisikilizi"



    "Wewe......na kusikiliza umesema nikae hpa na hakuna mtu yoyote yule kuingia ndani....... Na ninakuhakikishia hakun mtu yoyote atakayeweza hata kujisogeza karibu na hapa; we rudi ndani .....ila mfanye polepole" alizungumza Fancy akimtania kaka Yake.



    "We mtoto wewe?? Alizungumza Hancy na kutaka kumpiga Fancy. Fancy alimsukuma na kumrudisha ndani ya chumba chake kisha akafunga mlango.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pembeni aliweza kuonekena Zawadi akishuhudia tukio hilo, hakuna na furah wala huzuni bali alionekana wa kawaida tu.



    "Hancy......aliita Mozah.



    " nini tena.....aliuliza Hancy aliyekuwa akimvua nguo ya juu Mozah aliyeweza kumzuia.



    "Tusifanye Leo bhna tufanye siku nyingine" alishauri Mozah.



    "Siku kama ipi?? Aliuliza Hancy aliyeonekana kuendelea kufungua vifungo vya nguo vya Mozah.



    " yoyote lakini siyo Leo. ......kwa maana Fancy anajua kile tunachokifanya" alizungumza Mozah.



    "Kwahiyo unaogopa??? Aliuliza Hancy aliyeweeza kuacha kufungua vifungo vingine zaidi.



    Mozah alitikisa kichwa ishara ya Ndiyo na Hancy alivirudishia vifungo vyake na kusema



    "Sawa samahani kwahili"



    Hancy alitoka njee na kumuacha Mozah ndani aliyebaki akimuita.



    Fancy alisimama pale alipokuwa amekaa



    "Heeeeeee mmeshamaliza haraka haraka hivi?? Aliuliza ila Hancy alimpita pasina kusema lolote lile.



    "We Hancy........ Aliita ila kabla hajaweza kumfuata Mozah aliweza kumfuata nyuma akimuita wakati hay yote yakiendelea bado pia Zawadi alionekana akiyatizama.



    " Hancy...... Aliita Sarah lakini Hancy aliweza kumpita.



    Sikitu akiwa njee aliweza kumuona Hancy akieleka kupanda farasi kisha akaondoka eneo lile.



    "Mbona kama ana hasira? Alijiuliza na kutazama upande ambao alihisi aliweza kumuona Nzenze



    Alitizama upande ule na kuamua kuelekea upande ambao Hancy aliweza kuondoka.



    Mozah alifika eneo lile lakini tayari Hancy alishaweza kuondoka.



    Alivuta pumzi ndefu kisha akampanda farasi kwaajili ya kumfuata Hancy nyuma.



    Muda ulienda na masaa yakapita alionekana Mozah akiwa anazunguka njee ya geti la ngome ya kifalme akimsubiri Hancy ambaye hakuweza kugundua wapi alipoweza kuelekea.



    Aliweza kumuona Hancy akija na aliweza kumsubiria ashuke kwenye Farasi alipiga hatua mbili kwaajili ya kumfuata lakini aliweza kuacha baada ya kumuona Sarah aliyeweza kufika pale.



    Hancy aliita Sarah na kumkumbatia Hancy ambaye alionekana kuwa mwingi wa mawazo.



    " Nimekutafuta sana,Kuna kitu nahitaji kukuonyesha alizungumza na kuanza kumvuta Hancy kumpeleka mahali ambako alihitaji kumpeleka.



    Mozah aliweza kujificha nyuma ya nguzo ya nyumba ili asiweze kuonekana. Hancy alipita eneo lile alihisi kama Kuna mtu mahali pale lakini alipoweza kugeuka hakuweza kuona mtu, wakati huo nao alionekana Zawad akiwa anamtizama Mozah aliyeweza kuliona tukio lile.



    Mozah alifuta machozi yake kisha kuelekea katika chumba chake kwa hali ya utaratibu kabisa.



    "Hancy........aliita Sarah na Hancy aliutoa Mkono wake.



    " Sarah nafikiri ulishanielewa...sitopenda tena tabia yako ya kunishika Mkono wala kunileta katika chumba chako, mke wangu akiliona hili hatoweza kupendezwa nalo. Hancy aliweza kutoka katika chumba cha Sarah na kuelekea ndani kwake.



    Wakati huo aliweza kuonekena mtu akicheke na kusema



    "Sarah, hivi unafikiri unauwezo wa kuwa na Hancy ; au Mimi nakusaidia wewe uwe na Hancy, hapana nahitaji uiharibu ndoa ya Hancy na Mozah kisha baada ya hapo Hancy ataniowa Mimi" kiliweza kuonekana kicheko tena cha kebehi kisha kumfuata Hancy nyuma akitaka kujua kipi kitaendelea baina yake na Mozah.



    Aligeuka nyuma na macho yake yaliweza kukutana na Zawadi ambaye alionekana kumfahamu vizuri sana na kwa kila tendo analoweza kulifanya juu ya ndoa ya Mozah na Hancy.



    Baada ya Zawadi kuweza kuonekana , alitoa heshima na kuondoka zake.



    Mozah ilisikika sauti ya kike ikiita kabla ya Mozah hajaingia katika chumba chake.



    "Abee mama" ilikuwa ni sauti ya Stela ambaye aliweza kumsogelea Mozah.



    "Una shida gani mbona unalia??



    " Hapana ...ni mdudu ameingia machoni" alizungumza Mozah.



    'Nimekuelea Mimi hivyo Naelewa....niambie mchana nilikuona wewe na Hancy mkiwa katika hali ya kutokuwa na maelewano .......Hancy ndo anakufanya unalia sindiyo?? Aliuliza Stela.



    "Hpana mama siyo Hancy" alidakia kw haraka haraka.



    Stela alimtizama bila kusema neno lolote.



    "Sawa nitamuuliza Hancy mwenyewe"



    "Hpana.... Nàfikiri ni matatizo kidogo baina yangu na yeye hivyo tutayamaliza tu; nisingependa umwambie" alizungumza Mozah.



    "Sawa twende ukale" alizungumza Stela na kumshika Mozah kisha Kuondoka naye wakati huo nao Hancy ndo alikuwa anakuja eneo lile.



    "Hancy' aliita Fancy.



    " chakula tayari twnde tukale"



    "Nimeshiba"



    "Umeshiba umekula wapi, twende tukale" alizungumza Fancy na kumshika Mkono Hancy kisha kumfikisha mpaka Katika meza ya chakula alimkuta Mozah akiwa tayari mezani alimtizama tu bila kusema neno na ndivyo ilivyokuwa kwa Mozah.



    "Mozah, kwanzia umekaa hapo hujagusa hata kijiko kwanini, vipi unajisikia kuumwa au?? Aliuliza Malikia Maua.



    " hapana Malikia Maua, nakula" alizungumza na kushuka kijiko kisha kuchukuwa chakula na kuanza kula.



    Sarah alikuja na kukaa pembeni ya Hancy ,Mozah alimtizama chini kwa chini pasina kusema chochote.



    "Jamani tuleni, alizungumza Sarah na kuanza kula.



    " Hancy huwa unapenda, ndizi kula na hii ya kwangu " alizungumza Sarah na kumuwekea ndizi mdomoni Hancy ambaye alibaki akiwa katika hali ya kutotaka kuipokea.



    "Mwenzko si anakupa ndizi" alizungumza Fancy na Hancy aliweza kuitumia ndizi ile kwa kulishwa na Sarah.



    "Mozah unashida gani mbona hulii?? Aliuliza Fancy.



    " Nimeshiba" alizungumza Mozah na kutoka katika meza ya chakula.



    Hancy alimtizama tu na kujikuta akishindwa kumeza ndizi ambayo tayari ameshaiweka mdomoni.



    Stela na yeye alisimama.



    "Unaenda wapi???



    "Naenda kumtizama binti yangu"



    "Lakini haujala chakula" alizungumza Fancy.



    "Nimeshiba" alijibu na kuondoka zake.



    "Sidhani kama ulivyoweza kufanya ni sahihi mbele ya mke wako....hata Mimi nimeshiba" alizungumza Malikia Maua na kuondoka zake.



    Mfalme Kantala na yeye aliweza kusimama na kusema



    "Mke wangu hana hamu ya kula hat mimi nimeshapoteza hamu"



    Hancy alisimama na kuondoka mezani huku Sarah akimfuata nyuma.



    Sikitu na yeye aliweza kusimama na kuondoka akifuatwa na Tom, mezani alibaki Fancy na Kipande.



    "We hujapoteza hamu ya kula??



    "Sijawahi kupoteza appetite kutoka na jambo ambalo hata halinihusu" alizungumza na kuendelea.



    "Na kutokana na. wewe ndo chanzo cha haya yote bado tu uko mezani; vipi unajisikia kula?? Aliuliza kipande

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Na utaishiaga kula tu katika falme hii kwani unajali sana tumbo lako" alizungumza Fancy na kusimama lakini macho yake yaliweza kugongana na Zawadi aliyekuwa akimtizama tu.



    "Na wewe unamtizama nan? Aliuliza Fancy kwa hasira na kuondoka.



    Mozah akiwa ameketi ndani kwake aliweza kuingia Stela.



    "Basi usilie alizungumza Stela na kwenda kumshika Mozah mabegani kisha kumtuliza kwa kumpiga piga mgongoni.



    " Basi mwanangu basi" alizungumza na kuendelea kum bembeleza.



    Huko nako alionekana Sarah akiwa nyuma ya Hancy aliyeweza kuonekana mwingi wa hasira.



    "Ngoja nikwambie kitu kimoja, Mozah ni mke wangu Mimi na nimeweza kumuowa kutokana na kuwa nampenda; hivyo sitopenda tena ukaribu wowote na wewe kwanzia sana siwzi kumliza mke wangu, kwaajili tu ya furaha yako.....Mozah akitoa machzo na Mimi huwa nayatoa moyoni mwangu, hivyo nakuomba Tafadhali rudi kwenu, kabla sijawa mtu mbya kwa upande wako". Alizungumza Hancy na kuondoka huku akimuacha Sarah ambaye alishindwa kuelewa baada ya kumuona Hancy akiwa na hasira kwa Mara ya kwanza toka aweze kumfahamu.



    " Sarah.....unashida gani mbona unalia?????? Aliuliza Fancy na Sarah aliendelea kulia zaidi



    Fancy alimkumbatia na kuanza kumcheka kwa nyuma Sarah ambaye hakuweza kuona.



    "Fancy kwanini ulinipigia simu na kuniambia Hancy anahitaji kuniona?? Aliuliza Sarah na Fancy alizidi kucheka tu kisha kuonyesha anachuki juu ya Sarah baada ya kumtoboa na pete aliyoweza kuivaa Mkononi mwake.



    " Fancy...... Aliita Sarah baada ya kuhisi maumivu.



    "Samahani" alisema Fancy na kumcheka pasina Sarah kujua hilo wakati huo nao alionekana Zawadi akimtizama Fancy kwa sura ambayo haikuweza kufahamika kama ni furaha au huzuni.



    ****** ****** ******



    Katika kijiji cha Isambala



    ******** ********** ********



    Mfalme Nuhu aliweza kupokea ujumbe ulioweza kutumwa kupitia ndege ambaye aliweza kumkabithi Nzanza na Nzenze.



    "atukuzwe Mfalme wa kijiji cha Isambala maisha kati ya Mozah na Hancy, yanaendelea vizuri na Mozah anaonekana kuwa na furaha huku aliko"



    Huo Ndiyo ujumbe ulivyokuwa ukisomeka.



    "Narizika baada ya kuona sasa Mozah anaishi vyema katika mji wa Isadora, ila vipi kuhusu Sikitu mbona hajamuelezea?? Aliendelea kuzungumza Mfalme Nuhu.



    " Kweli hajaongelea lolote kuhusu Sikitu" alizungumza Bi Lunde.



    "Naweza nitakufanya wewe, ukamuona Mozah" alizungumza Mtabiri Tambitambi.



    Aliweza kukaa chini na kutoa kitambaa chake chekundu kisha akakimwagia mwagia unga ambao aliweza kuunenea maneno kabla ya kuumwaga .



    Hatimaye aliweza kuonekena Mozah na Stela aliyekuwa akimbembeleza.



    "Kwanini mwanangu analia?? Kipi kimetokea?? Aliuliza Mfalme Nuhu baada ya kuona.



    ****** **** *****



    Hancy aliweza kugonga mlango kwaajili ya kuingia ndani na Stela baada ya kumuona aliweza kumuaga Mozah na kuondoka.



    Mozah aliyafuta machozi yake na kwenda kukaa kitandan, Stela alipoweza kutoka alimtizama Hancy na kumwambia maneno machache tu.



    "Baba yake akilitambua hili basi atakuja kumchukua binti yake"



    Hancy alienda karibu na Mozah na alipoweza kufika alikohoa kidogo kisha akakaa kitandani. Mozah alisogea kitandani na Hancy na yeye aliweza kumsogelea karibu kila alipozidi kusogea karibu na Mozah ndipo Mozah alipozidi kusogea.



    Hatimaye alifika mwisho wa kitanda na mozah aliamua kuinuka.



    "Mozah aliita Hancy na kumshika Mkono.



    Alitaka kuongea jambo lakini alijikuta anashindwa kuzungumza chochote na kuweza kupiga magoti mbele ya mke wake.



    " Hancy aliita Mozah kwa uwoga.



    "Unafanya nini?? Amka! Simama watumishi wako wakiona hili watafikiria vibaya, Hancy!!



    " Mozah Tafadhali naomba unisikilize kile ninachoweza kuzungumza" alizungumza Hancy.



    "Lakini si vyema kupiga magoti mbele yangu; simama kwanza kisha tuzungumze"



    "Hapana nisikilize kwanza" alizungumza Hancy na Mozah aliweza kupiga magoti akimuomba asimame.



    "Mozah.....alizungumza na kumshika mikono yote kisha kuiweka mbele ya uso wake.



    " Mimi sina mahusiano yoyote Yale na Sarah, na samahani kwa kuweza kuondoka mchana pasina kukuagaa ya kuwa ninaenda wapi?? Na.............'



    "Hancy........ Ni sawa tu Mimi nakuelewa lakini Tafadhali amka watu wakiona.......



    " haijalishi kwani nimepiga magoti mbele ya mke wangu, Mozah Tafadhali naomba msamaha wako'



    "Sawa amka kwanza" alizungumza Mozah akiinuka na kutaka kumuinua Hancy.



    "Nijibu kwanza, umenisamehe?? Aliuliza Hancy



    " Ndiyo simama basi" alizungumza Mozah na Hancy aliuliza tena.



    "Huwezi nisamehe kirahisi rahisi hivyo, pia siamini kama kweli umenisamehe" alizungumza Hancy na Mozah aliweza kumuinua.



    "Hancy.... Hata Mimi nina uhakika ya kuwa nilikukosea mchana wa Leo na Nahitaji pia msamaha kutoka kwako; Hancy ...... Aliita Mozah na Hancy aliweza kumpiga busu mdomoni.



    ***** katika kijiji cha Isambala******



    " huyu anamfanya nini binti yangu?? Aliuliza Mfalme Nuhu



    "Kwani wewe ulimfanya nini binti yangu aliuliza Bi Lunde na kuondoka zake



    " Nafikiri tumeangalia vya kutosha sasa" alizungumza Mtabiri Tambitambi na kutoa kitambaa chake.



    "Upumbavu gani huo unaendelea?? Alizungumza Malikia Samela



    " huyu mpumbavuuuuuu Sikitu ameenda kufanya nini huko huyo mjingaaaaa?? Alilalamika Malikia Samela.



    ***** **** katika mji wa Isadora **** ****



    "Hancy" aliita Mozah ambaye kwa sasa alishaweza kufika ukutani na Hancy akiendlea kumfungua nguo ya juu.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Hancy aliita tena Mozah na Hancy aliweza kuacha kufanya kile alichokuwa akikifanya na Mozah aliweza kupandisha nguo yake kisha kumuonyesha ishara ya mlangoni.



    Hancy aligeuka na aliweza kumuona Fancy.



    " Ni wewe tena?? Aliuliza Hancy akionyesha kuchoshwa na tabia ya Fancy.



    "Sikujua kama mnaweza mkafanya mapema nmna hii" alizungumza Fancy.



    "Kwani Kuna shida gani ikiwa tayari ni wana ndoa wanaruhusiwa kufanya hata kwa siku Mara 100 kwasababu Hancy ni halali ya Mozah na Mozah ni halali ya Hancy, tena kwasasa unatakiwa uwe na adabu na utambue ya kuwa sasa hivi kaka yako ameweza kuowa hivyo huna ruksa ya kuja tena katika chumba chake, na watumishi hakuna ruhusa ya mtu yoyote yule kuweza kufika katika chumba hichi au karibu na eneo hili kwanzia Leo na siku zote za mbeleni. Alizungumza Malikia Maua na akionyesha kuchukizwa na Fancy.



    "Mama....



    "Toka ndani ya hicho chumba" alizungumza Malikia Maua na kwenda kumtoa Fancy kisha akaufunga mlango.



    "Mama aliita Fancy lkini ghafla alipigwa kibao na Malikia Maua kisha akaanza kumkokota na kumpeleka ndani ya chumba chake.



    " Kwanini ulimpigia simu Sarah na kumwambia aje Isadora..... Kitu gani Unataka tena kutoka kwa mtoto wangu, kukubeba wewe na baba yako bado tu haikutoshi Unataka tena kuniletea tabia za baba yako kwa kumtaka mtoto wangu. Cheo cha kuitwa binti wa mfalme bado hujaridhika nacho Unataka tena kumpokonya Mozah mume wake, Kaa mbali kabisa na kijana wangu Kaa mbali naye " alizungumza Malikia Maua na kutoka hapo.



    Fancy alishikwa na hasira kuanza kutupa tupa vitu ndani.



    "Ww mwanamke wewe, unakuwa na kiburi kwa kuwa sasa wewe ni mke wa Mfalme, usijali kwani umebakiza miaka michache sana na nafasi hiyo itakuwa yangu Hancy ataniowa Mimi" Alizungumza Fancy kwa hasira.



    "Nilikwambia Mara ngapi ya kuwa hutakuwa na uwezo wa kufanya vile utakavyo pasina uwepo wa baba yako??? Aliuliza Kisude na kutabasamu.



    " Mimi pekee ndiye mwenye njia ya kukufanya wewe uwe Malikia.



    "Umeshindwa kumfanya yeye mke wako, utawezaje kumfanya mtoto wake mume wangu?? Nitapambana mwenyewe na sitaki unisaidie kwalolote, na huyu mwanamke nitamuonyesha ya kuwa Mimi ni nani?? Alizungumza Fancy na kumtizama Kisude ambaye ali pandisha mabega juu na kumtizama mwanaye.



    Njee alikuwapo Sikitu ambaye aliweza kusikia kila kitu.....



    " Mungu wngu hii ni nini hii aliuliza Sikitu akionyesha kutokuweza kuelewa kile kilichoweza kuzungumzwa.



    "Hancy.....mama anaonekana anahasira eeeeehhh"



    "Ndiyo, ila hawezi kumdhuru Fancy kwani ni mdogo wangu hivyo atamkemea tu" alizungumza Hancy aliyekuwa akipanda kitandani.



    "Malikia ameongea kwa ukali sana, au Kuna ugomvi katikati yao??



    "Sidhani alizungumza Hancy na kujifunika na shuka kwaajili ya kulala.



    " Hancy..... Naweza nikawa Mimi Ndiyo chanzo cha ugomvi wao?? Aliuliza Mozah



    "Hapana mama hajapendezwa na tabia yake ya kuingia tu ndani ya chumba changu bila kupiga hodi, ilihali kwasasa ninamke" alizungumza Hancy na kumtizama Mozah aliyekuwa akibinya binya vidole vyake



    "Mozah" aliita Hancy na kuinuka kitandani kisha kwenda kumchukua Mozah na kumketisha kitandani.



    "Huna lolote lile uliloweza kutenda juu yangu, na juu ya Fancy wala Mama yangu hivyo sipendi ujilaumu kwa makosa ambayo siyo ya kwako, hivyo acha kufikiria kile kilichoweza kutokea dakika chache zilizopita"



    "Hancy...........



    " Naomba tulale" alizungumza Hancy na kumpandisha kitandani kisha kumfunika na shuka yeye akapanda na kugeukia upande mwingine kisha akalala.



    "Hancy.....aliita Mozah na kumshika bega.



    " vipi wewe uko salama?? Aliuliza Mozah.



    Hancy alitabasamu na kumbusu Mozah katika paji la uso



    "Niko salama" alizungumza Hancy na kutabasamu.



    Mozah aliweza kumsogelea karibu na kukilaza kichwa chake katika kifua cha Hancy.



    "Hancy eeeeeeee" aliita Mozah



    "Naaam"



    "Najisikia Amani sana moyoni mwangu, kwani kwa Mara ya kwanza kabisa nimeweza kulala katika kifua chako" alizungumza Mozah



    Hancy aliweza kumkumbatia barabara na kumbusu zaidi katika nywele zake.



    "Hata Mimi najisikia vizuri sana kwani kwasiku ya Leo sihitaji hata shuka kwaajili ya joto, kwani joto la mwili wako linanitosha kwa siku ya Leo" alizungumza Hancy na Mozah aliweza kujilaza vizuri kifuani mwa Hancy.



    **** ***** *****



    "Tom" aliita Hancy na kwenda kumkumbatia



    "Ulikwenda wapi pasina kunitaarifu aise, nilikutafuta sana eti; ndipo nilipoweza kupata taarifa ya kuwa umepata safari; vipi kwanini ulienda mwenyewe kutafuta dawa!?



    " Kwasababu sitaki mazoea na mme wa mtu, untaka niongozane nawe alafu mkeo alale na nani?? Aliuliza Tom na kumfanya Hancy acheke



    "Alafu wewe"



    "Shika kwanza hii"



    "Dawa ya nini hii?? Aliuliza Hancy



    " Hii unachemsha kisha unachanganya na Supu ya samaki; ukiwa kitandani Mozah hawezi lalamika ya kuwa haumridhishi na ukinywa hii alafu ukalala naye hata kwa dakika moja tu; Mozah lazima awe mjamzito " alizungumza Tom.



    "Kwani bila hii siwezi mridhisha mke wangu, muone huyu" alizungumza Hancy.



    "Hpana lkini ni nzuri pia kwa afya yako na itakuongezea nguvu zaidi" alizungumza Tom.



    "Basi wacha nikaifanyie kazi alafu niifanyie majaribio leo usiku alizungumza Hancy na kuondoka zake eneo lile.



    Tom aliweza kukumbuka siku ambayo Hancy aliweza kumuomba ya kuwa asiweze kumpenda mwanamke ampendaye yeye.



    Pia akakumbuka siku ambayo Hancy alimuuliza anampenda nani kati ya Mozah na Sikitu.



    Anakumbuka ya kuwa kabla hajamjibu anampenda nani Hancy aliweza kumuwahi na kumwambia Mimi nampenda Mozah.



    Alirudisha kumbukumbu yake na kusema.



    " Hancy natumaini ya kuwa utamfanya Mozah awe mwanamke mwenye furaha kuliko wanawake wote duniani kwni ndiye mwanamke nimpendaye nami nitafanya njia zote za kuhakikisha ya kuwa unamfanya Mozah awe mwenye furaha " alizungumza Tom na alikuja Zawadi kwaajili ya kumpokea alichukua baadhi ya dawa na kuanza Kuondoka



    "Zawadi" aliita Tom na kumshika bega Zawadi ambaye aliweza kupata hisia kali sana.



    "Kwanini unakuwaga mkimya sana na huwa unaongea Mara moja moja sana kwani unashida gani?? Aliuliza Tom akiwa bado amemshika Zawadi aliwez kutoa Mkono wa Tom kwa kugeuka na kutaka kumjibu ila kabla hajamjibu aliweza kumuona Fancy katika chumba chake akiwa dirishani huku akimtizama Zawad aliweza kunyamaza na kuondoka zake. Tom alitizama juu na hakuweza kumuona mtu.



    " anashida gani mbona kama alikuwa anahitaji kusema jambo fulani lakini aliweza kuacha baadatu ya kutizama juu?? Alijiuliza lakini hakutilia maanani.



    Muda kidogo alionekana Zawadi akitembea katika kasiri ya kifalme aliweza kuvutwa na mtu asiyeweza kujulikana na baada ya hapo alionekana Fancy akiwa ameshikilia kisu.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ulitaka kuzungumza nini juu ya Tom?? Aliuliza huku akiwa anampitishia kisu katika shingo yake.



    " hapana, hakuna chochote kile nilichkuwa nahitaji kukizungumza juu yake"



    "Nilishakwambia ya kuwa sihitaji uzungumze neno lolote lile kama sijakuruhusu, na kuwa makini sana au hutaki maisha ya mdogo wako"



    "Hpana muache mdogo wangu Tafadhali usimfanye chochote kile" alizungumza Zawadi akitokwa na machozi.



    "Basi kama unahitaji hilo; inabidi unisaidie kufanya kitu kimoja" alizungumza Fancy na kutabasamu.



    Wakati huo nao Mozah alikuwa ndani akivaa gauni lake na alikuwa akijitahidi kufunga zipu yake. Alivyoweza kusikia uwepo wa mtu ndani aliweza kumuomba amsaidie kufunga zipu huku yeye akiendelea kuvaa vaa bangili zake.



    Hancy alitizama nyuma yake na hakukuwa na mtu mwingine



    "Mbona unachukua muda mrefu hivyo; njoo nifunge nataka kutoka njee" alizungumza Mozah na Hancy aliweza kusogeza hatua kwaajili ya kwenda mbele na kufunga gauni la mkewe.



    Alishusha pumzi ndefu na kuanza kushika zipu kisha kuanza kufunga kwa kutetemeka bahati mbaya aliweza kumbana Mozah na zipu hali iliyoweza kumfanya Mozah apige kelele kidogo tu iliyopenya katikati ya ngome zake za masikio.



    "Umenibana" Alizungumza kwa sauti ndogo ilimfikia Hancy



    "Samahani" alizungumza Hancy na kumfanya Mozah ashtuke kisha ageuke na kumtizama Hancy.



    "Hancy ni wewe?? Aliuliza Mozah akijitahidi kujifunga zipu mwenyewe.



    " ammmhhhh samahani lakini nilitaka nikuulize kama utaniruhusu kufanya hivyo " alizungumza Hancy aliishika Mkono wake kwa wasiwasi.



    "Ha....ha....haina shida..... Nilidhani ni Fancy au Mama Stela ndo maana" alizungumza Mozah na kuendelea kujaribu kujifunga zipu.



    "Sawa me natoka njee nitarudi ukimaliza kuvaa" alizungumza Hancy na kuondoka kwa kuokota dawa zake alizoweza kupew na Tom.



    "Hancy.... Aliita Mozah.



    " Naomba unisaidie kufunga zipu kwamaana hakuna mtu mwingine hapa ndani" alizungumza Mozah na kuweza kumfuata Hancy kwa taratibu kabisa na baada ya kufika aliweza kugeuka nyuma na kutoa nywele zake hali iliyomfanya Hancy aweze kuuona mgongo wa Mozah vizur kabisa.



    Aliweza kuipeleka mikono yake katika nguo ya Mozah na taratibu kabisa akaanza kufunga nguo yake huku vidole vyake vingine vikiweza kuigusa ngozi ya mgongo wa Mozah ambaye aliweza kuweweseka kila alipoweza kuguswa na vidole vya Hancy.



    Baada ya kumaliza kumfunga aliweza kuzirudishia nywele za Mozah mgongoni mwake.



    "Mmhhhhh" aliguna Hancy Mozah na yeye aliweza kuguna.



    "Tayari" alisema Hancy na mlangoni alionekana Zawadi aliyeweza kuja na juice katika kikombe huku nyuma yake akiwa Fancy...



    "Wifi nimekuletea juice uweze kupata kabla ya kwenda kokote kule asubuhi hii" alizungumza Fancy na kuichukua juice ile kutoka kwa Zawad kisha kuanza kuipeleka kwa Mozah huku akitabasamu.





    Ilipoishia ni baada ya Fancy kuweza kuandaa juice na kwaajili ya kumpatia Mozah kupitia Zawadi.



    Sasa tuendelee



    "Ahsante alizungumza Mozah na kuipokea huku akimtizama Hancy.



    " ammmhhhh Me huwa naipendaga juice ya maembe kwahiyo naomba ninywe Mimi. Alizungumza Hancy na kuweza kuichukua juice kisha akainywa.



    "Hancy............ Aliita Fancy kwa mshangao mkubwa lakini tayari alishaweza kushindwa kumzuia Hancy kwani alishaweza kuimaliza.



    " Kuna shida gani, Zawdi anaweza kwenda kuiandaaa nyingine tu ila ukimuandalie mpe ya nanasi kama linapatikana alizungumza Hancy na kutoka njee



    Fancy alimtizama Mozah kwa hasira sana lakini aliishilia kucheka ili kumzubaisha na asiweze kutambua lolote lile linaloweza kuendelea katika moyo wake.



    "Siku nyingine nikikupatia kitu hakikisha ya kuwa unakunywa na kumaliza mwenyewe wala usimruhusu Hancy atie mdomo wake, Sawa wifi Mozah.



    " Ndiyo" alijibu Mozah akimtizama Zawadi ambaye alionekana mkimyaa sana na mwenye mawazo mengi sana.



    Fancy aliondoka akiwa ameikunja sura yake na mbele yake aliweza kugongana na Stela aliyekuwa akiongea katika chumba cha Mozah.



    "Anashida gani huyu?? Aliuliza Stela.



    " hamna'



    "Mimi huyu mtoto simpendi kabisa, na nahisi namchukia zaidi ya ninavyoweza kumchukia Sikitu.



    " Mama" aliita Mozah na Stela alimtizama.



    "Leo umependeza kweli" alizungumza Stela na kuweza kutoka ndani ya chumba kile na Mozah.



    ****** ****** *******



    "Sijisikii vizuri kabisa kwa siku ya Leo na nashindwa hata kutambua shida ni nini eti" alizungumza Mfalme Nuhu akimwambia Mtabiri Tambitambi.



    "Labd nimpigie Mtabibu aje akutizame" alizungumza Mtabiri Tambitambi.



    "Hapana sidhani kama shida itakuwa juu yangu, nawaza sana juu ya Mozah na nahisi Kuna jambo baya linaweza kumtokea kwa sasa" alizungumza Mfalme Nuhu.



    "Mara zote huwa unawaza kuhusu Mozah mbona sijawahi kukusikia unawaza kuhusu Sikitu?? Aliuliza Malikia Samela.



    " Tena yeye namuwaza sana kuliko Mozah, kama aliweza kutega nyoka ili aonekane mzuri kwa Malikia Maua vipi akiwa huko atamfanya nini binti yangu?? Aliuliza Mfalme Nuhu na kumfanya Malikia Samela aanze kuweweseka.



    "Au unafikiri sijui ya kuwa huo upumbavu uliweza kuufanya wewe na huyo mwanao mpumbavu?? Aliuliza Mfalme Nuhu kwa kugomba.



    " Hodi, hodi...... Atukuzwe Mfalme Nuhu wa kijiji hichi cha Isambala" alizungumza Mganga Kipande.



    Mfalme Nuhu aliweza kumtazama na kuzungumza



    "Unabahati ya kuwa hakumgusa Mozah laiti angaliweza kumgusa basi....kichwa chake kingekuwa halali ya ardhi ya Isambala. Alizungumza Mfalme na kutoka huku Mtabiri Tambitambi akitoka eneo lile lakini aliweza kusimama na kutizama juu ya anga baada ya kuhisi kitu alitizama kwa muda kisha akaondoka hata Mganga Kipande naye aliweza kufanya hivyo hivyo na kusema kama Kuna jambo baya linaenda kutokea juu ya Mozah.



    Malikia Samela alimtizama kisha akauliza " Jambo gani???



    Uliweza kuingia usiku na alionekana Mozah akiwa anaulizia kama Kuna mtu mahali alipoweza kuwepo yeye kwani kulikuwa giza sana.



    "Nani???.... We ni nani??? Hancy........Hancy...........ni wewe umenifuata huku?? Aliendelea kuuliza lakini kimya kiliendelea kutawala .



    Hatimaye viliweza kusikika vitu vikidondoka. Alishtuka na kutizama ghafla alisikia mlio wa paka na kuweza kumuona akitoka sehemu hiyo ya jiko.



    " haaaa nimeogopa sana" alizungumza na akimimina chai aliyoweza kumaliza kupika ghafla taa ziliweza kuzima na uliweza kuonekana Mkono wa mtu ukiwa umeshika kisu na ukiwa unamfuata nyuma Mozah aliyekuwa akipiga hatua za kutoka pale. Ghafla iliweza kusikika sauti ya Hancy ikimuita Mozah kwa shida na mtu yule aliweza kujificha maeneo yale.







    "Hancy.......mbona umekuja huku?? Aliuliza Mozah



    " Nilikusikia ukiniita na kuniomba msaada" alizungumza Hancy.



    "Hpana nilisikia michakacho jikoni nikahisi ni wewe kumbe alikuwa paka" alizungumza Mozah.



    "Unauhakika ni paka?? Aliuliza Hancy.



    " Ndiyo nimemuona akitoka" alizungumza Mozah.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sawa twende" alizungumza Hancy na kutizama upande ambao aliweza kujificha mtu ambaye alihitaji kumtoa uhai Mozah.



    Waliweza kufika ndani na Mozah aliweza kumkalisha Hancy kitandani.



    "Unauhakika lakini tofauti na paka hujaona kitu kingine?? Aliuliza Hancy.



    "Hapana, embu kunywaa kwnza hii chai unaweza jisikia vizuri na ukaacha kuelekea chooni kila Mara alizungumza Mozah na Hancy aliweza kukumbuka ya kuwa aliweza kuona kivuli cha mtu aliyekuwa ameshika kisu.



    Katika chumba kimoja aliweza kuonekena Fancy akitupa kisu chini kwa hasira.



    " upumbavu gani huu?? Nilikupa juice ili uweze kwenda chooni Mara kwa Mara nikuulie huko lakini ukampa Hancy, nataka kukuuwa bado tu unamuita Hancy......tutaona kama utaweza tena kukwepa mtego utakao fuatia" alizungumza Fancy na kutabasamu ila alihisi Kuna uwepo wa mtu nyuma yake alipoweza kutizama hakumuona mtu.





    Alielekea msalani kwake pamoja na kisu kile.



    Hakuwa amehisi vibaya ni kweli kulikuwa na mtu aliyeweza kumtizama na alikuwa Sikitu ambaye aliweza kutabasamu na kusema



    "Kazi hii itakuwa rahisi sana" alizungumza Sikitu na kutizma kama Kuna mtu aliyeweza kumuona kisha akaondoka pembeni ya moja kati ya nguzo zilizoweza kusimamisha Jumba lile la kifalme aliweza kutokeza Zawadi ambaye aliweza kujionea matokeo yote yanayoweza kuendelea katika Jumba lile la kifalme.



    Palikucha asubuhi na alionekana Mozah akiwa amelala katika Mkono wa Hancy.



    Hancy aliinuka na kuweza kumpandisha Mozah kitandani kisha akamfunika lakini aliweza kukumbuka kitendo cha kivuli kilichoweza kushika kisu kikiwa nyuma ya Mozah.



    "Ni nan huyo anayetaka kumuuwa Mozah; ni Mjomba Kisude au........hpna yeye amesafiri na bado hajaweza kurudi..... .sasa ni nani adui wa Mozah katika kasiri hii, au Sarah?? Sitamuacha huyu mwanamke hai alizungumza Hancy na kuinuka kutoka pale alipokuwa ameegema akimtizama Mozah.



    " Hancy aliweza kuita Mozah na kumshika Mkono



    "Vipi unaendleaje?! Aliuliza Mozah akijitahidi kuamka lakini alishindwa kufanya hivyo.



    " Naendelea Vizuri, kwanini Jana hukulala kitandani ukalala kwenye sakafu unaona sasa unavyo umwa sasa hivi?? Alizungumza Hancy na kumpima Mozah kwa kujishika kichwani na kumshika yeye.



    "Mwili wako ni wamoto zaidi, ngoja nikutafutie maji ya kuja kukukanda alitak kutoka njee lakini baada ya kukumbuka kile kivuli cha kisu alisita na kuanza kuita akiwa pale pale mlangoni kwa kupiga kelele na watumishi zaidi ya watatu waliweza kufika pale.



    Niletee maji ya baridi na kitambaa kisafi fanya haraka.



    " Ndiyo mtoto wa mfalme, ninyi wawili mtakaa mlangoni na wewe mmoja Kaa ndani na Mozah alafu msifunge mlango ili muweze kuonana" aliendelea kuzungumza Hncy na kuweza kutoka njee.



    "Mfalme mtaraji anatatizo gani?? Aliuliza moja kati ya wafanyakazi wale walioweza kupatiwa kazi baadye kidogo alionekana Tom akiwa ndani na Hancy huku Mozah akiwa amejipumzisha.



    " Hancy, unashida gani mbona kama una mawazo mengi hivyo "



    Hancy alimtizama Mozah kisha akamvuta Tom mbali kidogo na mahali alipo Mozah



    "Jana usiku niliweza kuona kivuli cha mtu kikiwa kimenshikia Mozah kisu kwa nyuma alipokwenda jikoni kunitengenezea chai.



    " una uhakika?? Aliuliza Tom.



    "Nina uhakika"



    "Lakini Mjomba Kisude bado hajarudi ndomaana nakuuliza una uhakika"



    "Nina uhakika bhna.... . na kivuli chenyewe nahisi ni cha mtoto wa kike "



    '"Wa kike??? Aliweza Kuuliza Tom kwa sauti ya juu



    "Kuna shida gani mbona umeshtuka?? Aliuliza Hancy



    " hapana" alijibu Tom



    "Me nahisi ni Sarah" alizungumza Hancy



    "Me na hisi ni Sikitu"



    Walitizamana wote kisha wakasema.



    "Fancy"



    "Na wewe unafikiri hichi ninachoweza kufikiria Mimi,?? Aliuliza Hancy na Tom alitikisa kichwa



    Ni baada ya Hancy na Tom kuweza kufikiria kitu juu ya Fancy.



    "Me nahisi ni rahisi kwa Fancy kuweza kumchunguza Sarah pamoja na Sikitu kwani ni wakike" alizungumza Tom na wote waliweza kukubaliana ila wakati wanaondoka na kuelekea kwa Fancy Zawadi alikuwa eneo lile na aliweza kuyasikia mazungumzo yale.

    Tom aliweza kumuona na kuendelea na safari zake huku akiwahi yeye pamoja na Hancy.



    "Hancy" aliita Mozah aliyekuwa amefika eneo lile.



    "Mozah" umefikaje.



    "Wewe......we..... Mbona umewahi kuamka mapema sana, vipi unaendleaje?? Aliuliza Mozah.



    " Naendelea vizuri kiasi" alizungumza Hancy na kumtazama Tom akimtaka aende kwa Fancy mwenyewe.



    Tom alitoa heshima na kuondoka zake.



    Tom aliendelea kwenda na mbele aliweza kukutana na Zawadi aliyekuwa amesimama mbele yake na kumtazama.



    "Zawadi, yuko wapi Fancy?? Umemuona wapi ?? Aliuliza Tom na kutaka kuelekea chumbani kwa Fancy Zawdi aliweza kumshika Mkono kabla hajamwambia kitu ulisikika mlango wa chumba cha Fancy ukifunguliwa.



    "Tom" aliita Fancy na kumuuliza.



    "Ulikuwa unazungumza na nani???



    " Na.....aligeuka na hakuweza kumuona tena Zawadi...... Hahahaha nilikuwa najiuliza kama uko ndani....vipi naweza kuingia aliuliza Tom.



    "Ndiyo karibu" alizungumza Fancy na kuingia ndani.



    Tom alitizama nyuma yake na hakuweza tena kumuona Zawadi.



    "Hii inastajabisha hii" alijizungumzia kimoyo moyo na kuingia ndani.





    ****** ******* ******



    "Nini nan huy aliyeweza kujaribu kutaka kumuuwa binti yangu?? Lazima niende huko lazima" alizungumza Mfalme Nuhu na kuweza kumuachia Ndege yule aliyeweeza kuleta ujumbe ule.



    "Lakini Mfalme Nuhu. Naamini yuko salama kwasababu Stela na Hancy wako upande wake watamkinga kwa kila jambo" alizungumza Bi Lunde.



    "Kama Sikitu yuko sehemu moja na Mozah siwezi kuwa na Amani nakwenda kumleta huyo mpumbavu huku kijijini nina uhakika ni kazi yake hii; kishoka....kishoka"



    "Ndiyo Mfalme Nuhu"



    "Andaaa farasi tunaelekea mji wa Isadora"



    "Ndiyo mfalme Nuhu" alijibu na Samela aliweza kuzisikia habari zile.



    "Kwanini anafanyaga ujinga huyu mtoto?? Alijiuliza Malikia Samela na kuingia katika chumba chake.



    ****** **** ******



    Alionekena Mozah akitembea huku akitizama nyuma yake na kuongeza mwendo zaidi huku akiendelea kutizama nyuma. Alisimama na kugeuka.



    " wa cheni kunifuata" alizungumza Mozah na Watumishi wale waliweza kusimama huku Mfalme Kantala na yeye akiwa amewasili eneo hilo.



    "Kuna shida gani binti wa mfalme Mozah?



    Wote waliweza kutoa heshima na kumsalimia Mfalme Kantal



    " Samahani mfalme wangu kama nimeweza kukusumbua kutokana na sauti yangu kupaa" alizungumza Mozah



    "Hapana nilikuwa napita maeneo haya ndipo nilipoweza kusikia sauti yako, kwanini mnamfuata mke wa mfalme mtaraji nyuma"



    "Samahani Mfalme lkini hii ni amri ya...........kabla hajaweza kutamka ya kuwa ni amri ya nani Tom aliweza kuyaingilia mazungumzo yale.



    " Mnaweza mkaenda"



    Wlitoa heshima kwa wote kisha wakaweza kuondoka zao.



    "Hii ni kazi yako na Hancy sindiyo, haya natoa amri kama mnahitaji kumlinda Mozah basi mlinde wewe au Hancy, ili asiweze kujisikia vibaya hata kidogo"



    "Ndiyo Mfalme wangu" alijibu Timo na Mfalme akaondoka huku Tom akimuonyesha Mozah njia ya kuelekea chumbani kwake.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Fancy alikuwa nyuma yao na aliweza kutabasamu huku akisema.



    "Tayari nilishaweza kucheza mchezo wa kumuwekea Sarah kisu kile katika begi lake na Hancy aliweza kumfukuza sasa, amebaki huyu Mozah na nitamtumia Tom na Sikitu kwani nawaona wanaanza kuelekea katika njia zangu. Alicheka na kugeuka nyuma ambako alihisi Kuna mtu lakini baada ya kuona Hamna mtu aliweza kuondoka zake, Zawadi aliweza kutoka katika eneo aliloweza kajificha na kumtazama Fancy aliyekuwa akieleka chumbani huko huko.



    Mozah aliweza kuingia ndani na Tom.



    " Naelekea Msalani alizungumza na kumtaka Tom aweze kutoka njee.



    Tom alitoa heshima na kuweza kutoka njee huku akiwa amesimama mlangoni.



    "Najua kwa sabuni niliyoweza kuipaka katika sakafu lazima udondoke na utapiga kelele kisha Tom ataweza kukufuata huko ndani nami nitaingia na kuwafungia mlango huko kwa pamoja na Hancy ataweza kuwakuta basi mchezo wangu umekwisha na Mozah utarudi kwenu huku Tom akifukuzwa katika kasiri hii ya kifalme aliweza kucheka na kama alivyoweza kutabiri ndivyo ilivyoweza kutokea baada ya Mozah kupiga kelele Tom aliweza kwenda ndani na Fancy aliingia kisha akaufungua mlango.



    " we toka njee unawezaje kuingia ilihali niko Msalani?? Aliuliza Mozah.



    "Samahani samahani alizungumza na kutaka kufungua mlango lakini tayri ulishaweza kufungwa. Alisukuma na kusukuma lakini mlango haukuweza kufunguka.



    Wakati huo nao Hancy alikuwa akija baada ya kutoka katika kazi ya kifalme aliyoweza kupatiwa na bab yake.



    Fancy aliweza kuzisikia hatua za mtu na aliamini ni Hancy hivyo alitafuta sehemu ya kujificha asiweze kuonekana kisha akaufungua mlango huku nako ndani walishaweza kukata tamaa.



    "Mozah aliita Hancy na wote waliweza kushtuka.



    " Ha...Ha.... Hancy " aliita Mozah kwa wasiwasi.



    "Uko bafuni sawa fanya haraka utoke huko na Mimi niingie kwni nimechoka au Unataka niingie hivyo hivyo aliuliza Hancy akiwa anatania na akiwa anavua shati lake.



    " Hancy " aliita Tom na Hancy alikomea hapo kuendelea kufungua vifungo vya shati.



    "Tom" aliita na kwenda kusukuma mlango ambao uliweza kusukumika kwa urahisi wakati huo nao Fancy aliweza kujitokeza akiwa amebeba matunda. Hancy baada ya kufungua mlango alibaki akitizama tu kwani Mozah aliweza kuvaa taulo tuu na juu yake aliweza kufunikwa na shati la Tom huku Tom akibaki kifua wazi.



    Hancy aliingia ndani na kwenda kumtoa Mozah akiwa amemshikilia Mkono kwa nguvu sana.



    "Tom ..Tom.... Mozah mlikuwa mnafanya nini huko bafuni watu wawili na mbona huna shati??: aliuliza Fancy akajifanya haelewi kile kinachoweza kutokea.



    Hancy alitoa shati la Tom na kumpatia kisha akamfunika Mozah kwa shati lake.



    " Siyo hivyo unavyoweza kufikiria Hancy .........Mimi na Mozah"



    "Tom najua huwezi kufanya kitu kama hicho wala Mozah pia kwasababu nawaamini wote wawili na Mozah akinielezea vile ilivyoweza kuwa Mimi nitaamini hata asipoweza kunieleza pia. Alizungumza Hancy



    Mlango uligongwa na kijakzi aliweza kusema.



    " Mfalme Nuhu kutoka katika kijiji cha Isambala ameweza kuwasili hivyo amri ya Mfalme Kantala ni muwende mkampokee kabla hajaweza kuingia katika kasiri hii ya kifalme. alizungumza Zawadi na kuweza kuwatizama.



    "Mozah harakisha vaa nguo tuendee, Tom Tafadhali andaa farasi" Fancy alishikwa na hasira baada ya kuona ya kuwa mpango wake wote haujaweza kufanikiwa.



    Baadye walionekana wakienda kwa pamoja huku njia nzima ikiwa kimya si kweli ya kuwa Hancy hakuweza kufikiria vibaya juu yao alikuwa ni mwenye hasira sana pindi amuonapo Tom na Tom aliweza kugundua hilo baada ya kuona mikono ya Hancy inatetemeka.



    "Mozah hakikisha unatafuta muda mzuri na muelezee Hancy kila kitu ili asiweze kuweka mawazo potofu juu yangu"



    "Ndiyo" alijibu Mozah kisha akaenda kwa kasi kidogo na kuzungumza na Hancy.



    "Hancy"



    "Naam"



    "Nimechoka kumuelekeza farasi naweza kupanda farasi mmoja na wewe?? Aliuliza Mozah na Hancy aliweza kumruhusu bado mikono yake ilikuwa ikitetemeka kwa hasira na Mozah aliweza kuona hilo.



    Aliishika mikono ya Hancy ambayo iliweza kuachaa kucheza baada ya tu kuguswa na Mozah.



    " Nataka kuzungumza na wewe punguza mwendo wafarasi aliweza kuzungumza Mozah na Hancy alifanya hivyo huku Tom akisema tuongeze mwendi kidogo Fancy na Sikitu wote waliweza kufanya hivyo na Fancy aliweza kupandwa na hasira kwani mchezo wake wote uliweza kuvurugika kwa mbali alionekana Zawadi ambaye alitabasamu Sana, tena siku ya Leo aliweza hata kucheka na meno yake yakaweza kuonekena.



    "Unafikiri kila Mara utageuka mshindi, hapana Fancy siyo kila Mara" alizungumza na kuendelea kucheka .



    Ulifika usiku na wote walikuwa mezani wakipata chakula cha pamoja huku wakiendeleaa kupiga stori.



    "Siku ya kesho nitaondoka na Sikitu hivyo jiandae na Hancy kabla sijaondoka nataka kuzungumza nawe; hivyo itakubidi kesho uwahi kuamka. Alizungumza mfalme Nuhu na kucheka.



    " nimekuja katika nchi ya watu na ninaanza kupanga masharti yangu "



    Mfalme Kantala Alicheka na kusema



    "Leo umekuja ukweni bhna, ila ujio wake umetushtua kweli ungetoa tu taarifa tufanye maandalizi" alizungumza mfalme Kantala.



    Wakati huo nao Fancy aliweza kuwaza Sikitu akiondoka mpango wangu utafeli hivyo sitaweza kumruhusu mtu aweze kufanya hivyo alizungumza na hatimaye macho yake yaliweza kugongana na Malikia Maua.



    "Unawaza nini?? Aliuliza Malikia Maua.



    " Hamna"



    "Nani bora iww Hamna kuliko uwaze upumbavu, kauli ile aliyoweza kuisikia ni Tom tu kwani watu wengine walikuwa busy na mazungumzo yao.



    Tom aliweza kumtizama Fancy kisha akamtizama na Malikia na kuanza kuhisi kitu juu yao.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Muda ule uliweza kupita na alionekana Sikitu katika chumba chake akiwaza sana.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog