Search This Blog

KISIWA CHA HARISHI - 2

 







    Simulizi : Kisiwa Cha Harishi

    Sehemu Ya Pili (2)



    “Mimi nasikia harufu ya binaadamu humu ndani. Kumbe ni wewe!” akamwambia yule mwenzetu aliyemshika shati. Suati yake ilikuwa ya kuunguruma kama gari bovu.

    Wakati anasema meno yake yalitoka nje. Yalikuwa meno marefu kama ya nyani!

    Alipomshika mwenzetu shati alimvuta karibu yake.

    “Umeingiaje humu ndani na umefuata nini….kwanza umetoka wapi?” akamuuliza kwa hasira.

    Ghafla Yasmin akatoka.

    “Ni nani?” akauliza huku akimtazama yule mtu ambaye alikuwa akitetemeka.

    Yasmin alipomuona alimgundua.

    “Itakuwa ni wavuvi walioharibikiwa na chombo chao, wameona nyumba wameingia wakidhani watapata msaada” Yasmin akaliambia lile jitu.

    “Anaingia humu anamfuata nani. Huyu simuachi ng’o!” jitu hilo lilisema na kumshika yule mwenzetu kwenye kiuno kisha likamuinua juu kwa mkono mmoja na kumgeuza kichwa chini. KIchwa cha mwenzetu kikawa chini ya kichwa cha jitu lile jitu.

    Ndipo jitu hilo lilipokita utosi wa yule mtu kwa ncha ya upanga wake. Mwenzetu huyo alipiga ukulele mmoja tu “Nakufaaa!” kisha akawa kimya. Damu ikaanza kuchuruzika kutoka kwenye utosi wakei jitu hilo likakinga mdomo wake na kuanza kuifyonza!.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliendelea kuinywa ile damu iliyokuwa ikitoka kama maji ya bomba. Mwisho alibandika mdomo wake pale kwenye utosi na kuanza kufyonza.

    Nilikuwa nikitetemeka kwa hofu kama niliyepatwa na homa ya baridi ya ghafla. Nilijua akimalizwa yule mwenzetu itaanza zamu yetu sisi kwani sote tulikuwa ndani ya lile jumba.

    Midomo ya Harishi ilitapakaa damu. Damu nyingine ilikuwa inavuja midomoni mwake na kuingia kwenye ndevu zake na kisha kutiririka hadi kwenye kanzu yake.

    Yasmin alikuwa ameshika kichwa chake kwa huzuni na alikuwa amekiinamisha kichwa chake chini ili asiangalie lile tukio.

    Pamoja na huzuni na uchungu vilivyompata Yasmin bila shaka alikuwa akijiambia “Wameyataka wenyewe. Nilishawambia waondoke, kumbe wamerudi tena”

    Nikaona mafunda ya Harish yanafutuka huku akitafuna kwa haraka haraka na kumeza. Kumbe alikuwa alikuwa anafyonza ubongo wa mwenzetu na kuula. Aliula kwa ulafi. Mwingine ulimvuja midomoni na kuingia kwenye ndevu zake.

    Alipotosheka alitupa chini ile maiti akaanza kujirambaramba midomo na kujifuta kwa mkono. Alipomaliza aliinama akaushika mguu wa yule mtu aliyemuua.

    “Sasa nimeshiba vizuri, ngoja niondoke” alijisemea peke yake akiuinua ule mguun na kuuburuza kuutoa ule mwili nje. Aliuburuza huku akiendelea kujirambaramba. Alipofika kwenye mlango aliufungua na kutoka na ile maiti nje.

    Yasmin alikuwa bado amesimama akimtazama.

    “Lakini mimi niliwambia ila hawakunisikia” akajisemea peke yake huku akitikisa kichwa.

    Kwa sababu ya kuzidiwa na hofu na kujua kuwa sote tutakufa nilijitokeza pale nilipokuwa nimejificha. Nikamfuata Yasmin.

    Yasmin alishituka aliponiona.

    “Na wewe umetokea wapi?” akaniuliza kwa kutaharuki.

    “Nilikuwa nimejificha chooni” nikamjibu kwa sauti ya kutetemeka.

    “Unaiona damu hii ya mwenzenu?”

    Yasmin akanionesha damu iliyokuwa imedondoka chini.

    “Nimeiona na nimeona pia alivyouawa”

    “Si niliwambia mwendezenu?”

    “Tulirudi huu usiku tulipoona kuna mvua na hatukuwa na mahali pa kujisitiri”

    “Sasa mmerudi na Harishi ametokea. Mwenzenu ameonekana”

    “Kwani atarudi tena usiku huu?”

    “Usiku huu hatarudi tena lakini kama ameshasikia harufu zenu anaweza kurudi hata kesho akijua atapata mlo mwingine. Yule hali kitu isipokuwa damu na ubongo. Watu wa kisiwa chote hiki amewamaliza yeye na ana nguvu zisizo za kawaida. Yule mtu amemuinua juu kwa mkono mmoja tu”

    “Na amempeleka wapi?”

    “Amekwenda kumtupa nje ili asubuhi aliwe na kunguru”

    “Sasa sijui sisi tutakimbilia wapi kwani chombo chetu kimekataa kabisa kuwaka”

    “Mimi sina la kuwambia kwani popote mtakapokwenda ndani ya kisiwa hiki atawagundua na atawamaliza mmoja mmoja”

    Nilibaki kuduwaa na kutikisa kchwa. Kwa mara ya kwanza niliona kazi ya uvuvi ilikuwa mbaya. Laiti kama ningejua kuwa chombo chetu kingeharibika baharini nisingeshiriki katika safari ile.

    “Wenzako wengine wako wapi?” Yasmin akaniuliza.

    “Nikwambie ukweli Yasmin, sisi tulirudi mapema huu usiku tukaigia jikoni na kula chakula chako kwa sababu tulikuwa na njaa. Tukaingia vyumbani kulala. Sasa tulitoka watu wawili kuja kujisaidia. Huku nyuma mwenzetu mmoja naye alitoka peke yake, Ndiye yule aliyekamatwa na kuuawa”

    “Wenzako wengine wako wapi?”

    “Mmoja amejificha chooni na wenzetu wengine wako vyumbani”

    “Sasa na nyinyi nendeni mkalale, asubuhi mtafanya maarifa. Yule jini hatarudi kwa leo, ameshashiba”

    Yule mwenzangu aliyekuwa chooni aliposikia maneno yale alitoka haraka. Yasmin akamtazama.

    “Nyinyi mna bahati sana. Angeweza kushikwa mmojawenu”

    “Ni kweli kwa sababu sisi ndio tuliotoka kwanza” nikamwambia Yasmin.

    “Basi nendeni mkalale”

    Tukarudi kwenye vile vyumba. Yasmin alikuwa bado amesimama akituangalia hadi tulipofungua mlango na kuingia chumbani’

    Wala hatukulala kamwe. Mimi nilikaa macho usiku kucha nikimuwaza yule mwenzetu aliyeuawa kikatili.

    “Nyinyi mna bahati sana. Angeweza kushikwa mmojawenu…” nikawa nayakumbuka maneno ya Yasmin huku mwili ukinisisimka kwa hofu.



    Mara kwa mara nilikuwa nikitupa macho kila upande wa chumba hicho kwa hisia kwamba Harishi angeweza kutokea mle chumbani.

    Asubuhi kulipokucha Yasmin alikuja kutugongea mlango.

    “Amkeni. Kumeshakucha” Alikuwa akituambia wakati akigonga. Tukatambua kuwa alikuwa ni yeye.

    Tukafungua mlango.

    “Mmeamkaje?” akatuuliza.

    “Tunashukuru tumeamka salama” nilimjibu kwa niaba ya wenzangu.

    Wenzetu waliolala chumba kingine walikuwa hawana habari ya tukio lililotokea usiku. Nikawaeleza mbele ya Yasmin. Wakasikitika sana na kupata hofu.

    “Sasa nendeni mkaoge halafu niwaandalie chai” Yasmin akatuambia.

    Tukaenda kuoga. Kwanza waliingia watu wanne kwa vile vyoo vilikuwa vine. Walipotoka nikaingia mimi na mwenzangu.

    Yasmin akatuandalia chai pale sebuleni. Ilikuwa chai iliyotengezwa kwa maziwa ya unga na iliyoungwa kwa iliki, tangawizi na bdalasini. Pia alitupa mikate iliyotengezwa kwa mayai.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yeye mwenyewe alikunywa chai pamoja na sisi. Nikamuona amefurahi na kuchangamka licha ya kwamba usiku wa jana yake tu tulishuhudia machungu ya kuuawa mwenzetu.

    “Ningekuwa nakula na wageni kila siku namna hii ningechangamka, lakini mh!” Yasmin alisema kama aliyekuwa akisema pek yake.

    “Ni kweli Yasmin lakini tutafanyaje? Tunapenda kukusaidia lakini hatuna uwezo. Kama hivyo umeona mwenzetu ameshauawa na sisi hatujui maish yetu yatakuwaje!” nikamwambia Yasmin kwa huzuni.

    “Kusema ukweli napenda niendelee kuwa na nyinyi hapaili nipate wenzangu wa kuzungumza nao. Lakini haitawezekana nyinyi muwepo hapa mkiwa hai.”

    “Na pia hatuna mahali pengine pa kwenda” nikamwambia Yasmin.

    “Huu ni mtihani. Sijui mtatumia mbinu gani muwe salama”

    “Labda tuendelee kujifichaficha humu ndani” Mwenzetu mmoja akaingilia yale mazungumzo.

    “Humu ndani atawagundua tu” Yasmin akamjibu.

    “Sasa tutakwenda wapi jamani!”

    “Mimi sijui niwambie nini ndugu zangu!” Yasmin akatuambai.

    Tulipomaliza kunywa chai Yasmin aliondoa vyombo. Alituacha tumekaa tukiendelea kujadiliana. Baadaye kidogo alirudi akiwa na karata.

    “Hizi karata ziko siku zote. Huyu mwendawazimu ananiletea. Lakini sina mwenzangu wa kucheza naye”

    Tulipoona karata tukazunguka duara. Yasmin akakaa na kutugawia.

    “Tunacheza mchezo gani?” nikamuuliza Yasmin.

    “Tunacheza mchezo wa arbasitini”

    Mchezo huo ulikywa maarufu kule Zanzibara na Comoro.

    Tukaanza kucheza karata. Tukasahau kabisa habari ya Harishi. Mchezo ulinoga sana. Kelele zetu zikawa zinasikika hadi nje.

    Ilipofika saa tano Yasmin akavunja mchezo na kutuambia tukatembee tembee. Tukiona jua la saa saba ndio turudi kula chakula. Mda ule alitaka kwenda kupika chakula.

    “Niwapikie nini?” akatuuliza.

    “Tupikiechochote tu utakachopenda” nikamwambia.

    “Basi nitawapikia pilau”

    “Tutashukuru sana”

    “Sasa mtakapokuja, kwanza mchungulie na kusikiliza. Mkimuona Harishi msiingie ndani, rudini huko huko mtakakotoka. Anaweza kuja ghafla”

    “Tumekuelewa” nilimjibu.

    Baada ya hapo tulitoka tukarudi kule kwenye boti letu.

    Ni tabia ya maumbile ya binaadamu kutokata tama na kujaribu kubahatisha kila mara hasa kwa watu kama sisi ambao tulikuwa katika hatari. Kwa mara nyingine tulijaribu tena kuliwasha lile boti. Kila mmoja wetu alijaribu kuliwasha bila mafanikio.

    Tukakaa chini ya mti na kuanza kujadiliana. Hata hivyo mjadala wetu ulikuwa kama usio na maana yoyote kwani haukutupa ufumbuzi wa jinsi ya kusalimisha maisha yetu.

    Kikubwa tulichokizingatia ni kujaribu kumkwepa Harish kadiri itakavyowezekana. Tuliona kama tutafanikiwa kumkwepa tunaweza kuendelea kuishi.

    Tuliendelea kukaa pale chini ya mti hadi saa saba tulipoamua kurudi kwa Yasmin. Tulimtuma mmoja wetu aingie akachunguze kama Harishi yuko ndani aje atuambie.

    Mwenzetu huyo akaingia ndani. Sisi tukawa tunamchungulia kwenye dirisha. Alinyata hadi ndani. Tukawa hatumuoni tena. Tukahamia kwenye dirisha jingine. Tukamuona amesimama pembeni mwa ukumbi akiangalia huku na huku. Akaenda jikoni kuchungulia kisha akatoka.

    Alipotoka jikoni alikwenda moja kwa moja kwenye mlango wa chumba cha Yasmin na kutega masikio yake kwenye mlango. Alisikiliza kwa muda kidogo kisha akaanza kugonga mlango taratibu.

    Mlango ukafunguliwa ghafla. Aliyetoka alikuwa Yasmin. Alitoka haraka haraka akaufunga mlango kisha akamuashiria yule jamaa aondoke. Nikajua kuwa hapakuwa salama.

    “Moshi unajaa kwenye chupa, Harishi anakuja!” Yasmin alimwambia.

    Yule mwenzetu aliposikia vile aligeuka ili aondoke lakini ghafla tena mlango ukafunguliwa. Harish akaibuka mbele ya yule mtu. Alikuwa ameshika upanga wake. Akamshika yule jamaa kwa mkono mmoja.

    “Unataka ukimbie wapi wewe?” akamuuliza akiwa amemtolea macho.



    Mwenzetu aliishiwa na nguvu kabisa. Akawa amemkodolea macho Harishi.

    “Mimi nasikia harufu zenu tangu jana”

    Mwenzetu kimya. Sasa mwili wake ulikuwa ukitetemeka waziwazi.

    “Sheikh nisamehe sana…” Sauti yake ikasikika kwa mbali ikiomba.

    “Chombo chetu kiliharibika jana”

    Harisha alikuwa akimtazama kama vile alikuwa hamuelewi.

    “Wasemaje?”

    “Nisamehe sana…nakuomba” jamaa alikuwa analia.

    “Kwani wewe huna damu?. Ngoja nione”

    Hapo hapo Harishi akamuinua juu mwenzetu huyo kwa mkono mmoja tu. Akamgeuza kichwa chini.

    Kiasi cha kufumba na kufumbua tu alishamtoboa utosi kwa ncha ya upanga wake.

    Yasmin alipoona hivyo alikimbilia nje. Akatuona tumeinamia dirisha.

    “Jamani balaa gani hili?” akajisemea peke yake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Idadi yetu sasa tulikuwa watu watano, wenzetu wawili walikuwa wameshauawa. Na sisi pia hatukuwa na matumaini kuwa tungebaki.

    Tulijua kuwa kama hatutakufa kwa njaa, tutauliwa na lile jini la Yasmin. Kila mmoja wetu alikuwa ameshikwa na hofu na fadhaa. Tulitamani angalau kipite chombo kituokoe kuliko vile tulivyokuwa matumatu tukisubiri kufa.

    Tulitamani tusifike tena katika lile jumba la Yasmin lakini tungekula nini, wakati kwa Yasmin ndiko tunakotarajia kupata riziki yetu. Kusema kweli tulichanganyikiwa na hatukujua la kufanya.

    Tulikaa pale chini ya mti kwa karibu saa mbili. Ghafla tuliona mwanamke akiambaa na ufukwe wa bahari akija upande wetu. Mkono mmoja alikuwa ameshika kapu.

    “Jamani ni nani yule?” Mwenzetu mmoja akauliza.

    “Naona ni kama Yasmin” nikajibu.

    Mjadala ukaanza.

    “Ni Yasmin kweli!”

    “Amefuata nini huku?”

    “Labda anatutafuta sisi”

    “Mmoja wetu atokeze ili atuone au aende akampokee lile kapu. Labda anatuletea chakula”

    “Hatujui Harishi yuko wapi. Unaweza kujitokeza ukajikuta unakamatwa!”

    “Bila shaka Harishi ameshaondoka, Yasmin asingeweza kuja huku. Ngoja nimfuate” Mimi ndiye niliyesema hivyo. Nikanyanyuka na kuanza mwendo kuelekea upande ule aliotokea Yasmin.

    Yasmin akaniona.

    “Nawatafuta nyinyi, mko wapi?” akaniuliza tangu akiwa mbali.

    “Tuko huku chini ya mti. Tumekuona tangu ukiwa mbali”

    “Nimewaletea chakula”

    Nilikuwa nimeshamfikia. Nikampokea lile kapu.

    Tukawa tunatembea pamoja kuelekea kule waliko wenzetu

    “Lile shetani limeshaondoka, ndio maana nimeweza kutoka” Yasmin akaniambia’

    “Halitarudi tena kwa leo?”

    “Halitarudi labda kwa kesho”

    “Yule mwenzetu ndio ameuawa?”

    “Ndio aliuawa. Si mliona wenyewe akikamatwa”

    Nikatikisa kichwa changu kusikitika.

    “Wakati anabisha mlango niliona ile chupa ya Harishi inajaa moshi. Nikajua kuwa Harishi anakuja. Nikawahi kutoka ili niwambie muondoke. Wakati nasemeshana na yule mwenzenu, Harishi akasikia akawahi kutoka na kumkamata” Yasmin aliendelea kunieleza.

    “Sasa yule jinni atatumaliza sote. Tulikuwa watu saba sasa tumebaki watano tu”

    “Basi msije kule”

    “Sasa tusipokuja utatuletea chakula?”

    “Nitawaletea. Na leo ameshakula mtu mmoja harudi tena hadi kesho”

    Tukawa tumefika walipokuwa wenzetu.

    “Leo tumepata msiba mwingine” Mtu mooja akamwambia Yasmin.

    “Nilishawambia tangu mapema kuwa usalama hapa ni mdogo sana kwa sababu ya Harishi. Sasa mnaona wenyewe, na ijui mtafanya nini ndugu zangu”

    “Jamani kwanza tuleni chakula. Yasmin ametuletea chakula. Tukanawe mikono kwa maji ya chumvi. Mazungumzo baadaye” nikawambia wenzangu.

    Tukaenda kunawa maji ya bahari kisha tukarudi pale chini ya mti, tukaketi. Yasmin naye akaketi.na sisi. Tukaanza kula.

    “Kwani Harish ameshaenda zake?” Mtu mmoja akamuuliza Yasmin.

    “Ameshaondoka” nikamjibu mimi. “Angekuwepo Yasmin asingeweza kuja huku”



    Tulikula pilau ikiwa ndani ya kapu. Tukashiba na kupata nguvu.

    “Nimesahau kuwachukulia maji ya kunywa” Yasmin akatuambia.

    “Na maji tuliyokuwa nayo yamekwisha” nikasema.

    “Lakini kwa leo Harishi hatarudi, mnaweza kuja nyumbani” Yasmin akatuambia.

    “Mh!. Nyumbani kwako kunaogopesha” nikamwambia Yasmin.

    “Tunaweza kwenda mnywe maji halafu mtarudi huku huku”

    Tukajadiliana na Yasmin, mwisho tukaamua turudi katika lile jumba. Tukarudi.

    Tulipofika alitupatia maji ya kunywa. Tukamshukuru kwa wema wake.

    “Bado mna wasiwasi?” Yasmin akatuuliza.

    “Kuwa na wasiwasi ni lazima” nikamjibu na kuongeza. “Tunajiona kama tuko kwenye vita”

    “ Kwa leo msiwe na wasiwasi. Yule jini hatarudi tena. Kama ni kurudi ni kesho. Tunaweza kukaa tukaongea hadi usiku mkaenda zenu”

    Tukashauriana na kukubaliana tukae hadi usiku kwa vile mwenyeji wetu ameshatuhakikishia kuwa tutakuwa salama. Pia tulikuwa tunamuhurumia Yasmin aliyekuwa mpweke katika jumba lile. Tukaona tukae tumchangamshe.

    Tukakaa kwenye ule ukumbi pamoja na Yasmin na kuanza kuzungumza.

    “Yasmin alitupa hadithi ya jinsi alivyofikishwa katika jumba lile na jinsi alivyokuwa akilia katika siku za mwanzo mwanzo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    .

    “Lile jini hata ukilia, halijali. Linakwambia utazoea tu. Na ni kweli kadiri siku zilivyokwenda nilijikuta nikizoea” Yasmin aliendelea kutuhadithia.

    “Sasa mnaishije, wakati wewe ni mtu na yule ni jini?” Mwenzetu mmoja akamuuliza.

    “Tunaishi kama mke na mume ingawa mwenzangu ni jini lakini ndio nimeshamzoea. Ameshaniambia kwamba nitaishi naye hadi kufa kwangu”

    “Je kama akifa yeye?” nikamuuliza.

    “Amesema yeye hatakufa haraka. Umri wa majini ni mrefu sana. Pale alipo ana miaka mia tatu na anaweza kuishi hadi miaka mia tano”

    “Loh!. Wewe utakufa, yeye ataendelea kuishi kwa miaka mingi sana” Mtu mmoja akamwambia Yasmin.

    “Lakini mimi ningependa kujua hisia zako. Unajisikiaje unapohisi kuwa utaishi ndani a jumba hili hadi ufe wakati bado ni msichana mdogo” Mimi nilimuuliza Yasmin swali hilo.

    Yasmin akabetua mabega.

    “Nasikia vibaya lakini nitafanyaje sasa. Nimelia nimechoka, sasa silii tena”

    “Kwa hiyo ndio unaishi ukisubiri kifo chako kitokee humu humu ndani?” Mtu mwingine alimuuliza. Lilikuwa si swali zuri. Sikulipenda. Lakini Yasmin alimjibu.

    “Wakati mwingine najidanganya kwamba iko siku yaweza kutokea miujiza nikaokolewa kwa namna nisiyoijua.

    “Na tangu uishi humu hakujatokea watu kama sisi wakaingia katika jumba hili?” nikamuuliza.

    “Nyinyi ndio watu wa kwanza kuwaona tangu nianze kuishi katika jumba hili”

    Tukaendelea kuzungumza na Yasmin hadi alipotuambia kuwa anakwenda kupika chakula cha usiku.

    Tukabaki sisi peke yetu na kuendelea kuzungumza na kujadiliana kuhusu maisha ya Yasmin na maisha yetu wenyewe.

    Jua lilipokuwa limekuchwa nilimfuata Yasmin jikoni nikamwambia kwamba tunaondoka.

    “Kwanini…subirini mle chakula. Nimepika chakula kingi kwa ajili yenu” Yasmin akaniambia

    “Giza linaingia. Tuna hofu yule jini anaweza kutokea. Acha tuondoke tu”

    “Jamani mkiwepo mnanichangamsha na mimi. Sasa mnataka kwenda wapi?”

    “Tunarudi kule kule ulikotukuta”

    “Kwanini jamani? Nimewambia Harishi hawezi kurudi leo labda kwa kesho. Mnaweza hata kulala hapa na mkawa salama. Muhimu ni kuamka kabla hakujapambazuka mwende zenu”

    “Unajua tuna hofu na wasiwasi, wenzetu wawili wameshauawa humu humu ndani”

    “Sasa kule mtakaaje usiku huu na baridi? Je mvua ikinyesha usiku huu mtafanyaje. Si bora mlale hapa hapa”

    “Ngoja nikawashauri wenzangu” nikamwambia Yasmin na kurudi kule ukumbini. Yasmin naye akanifuata.

    “Yasmin amesema tusubiri chakula na pia tunaweza kulala hapa hapa” nikawambia wenzangu.

    “Tulale hapa hapa?” Mtu mmoja akaniuliza kwa mshituko.

    “Hakuna neno. Mnaweza kulala tu ilimradi muamke alfajiri kabla ya kupambazuka mwende zenu” Yasmin akawambia.

    “Una hakika kwamba Harish hatakuja usiku huu?’

    “Hatakuja tena kwa leo ila kesho anaweza kuja. Sasa kwa vile sijui atakuja saa ngapi ndio maana nninawambia muondoke alfajiri”

    Yasmin alipoona wenzangu wameduwaa wakitazamana kutafakari yale maneno yake akatuambia.

    “Jamani kuweni na mimi. Hivi nashukuru kupata wenzangu wa kunichangamsha. Harish hatakuja tena leo”

    “Mimi naona tumsikilize mwenyeji wetu, acha tukae” Nikawambia wenzangu kwa kumuonea huruma Yasmin.

    Pia huko tulikotaka kwenda hakukuwa salama. Tungeweza kushambuliwa na wanyama usiku ule au kunyeshewa na mvua.

    Tukakubaliana kuwa tubaki na Yasmin.

    “Hakuna lolote litakalotokea, kaeni kwa roho moja. Mimi ndiye ninayejua kawaida na nyendo za Harishi. Mnachotakiwa ni kujihimu wakati wa alfajiri muondoke humu ndani ili kama kesho atatokea asiwakute” Yasmin akatusisitizia kabla ya kurudi jikoni.

    Baada ya muda kidogo alituletea chakula, tukala pamoja na yeye.

    Tulipomaliza kula Yasmin aliondoa vyombo. Aliporudi tena alikuwa ameshika karata. Akaketi na kutuambia. “Sasa tuchezeni karata, tukichoka tunakwenda kulala”





    Akagawa karata, tukacheza hadi usiku mwingi. Wenzangu wengine walikuwa wameshaanza kusinzia. Tukavunja mchezo na kwenda kulala.

    Tuliingia katika vyumba viwili. Chumba kimoja waliingia watu wawili na chumba kingine waliingia watu watatu. Mmoja aliweka godoro chini. Mimi nilikuwemo katika kile chumba walichongia watu watatu. Nililala kitandani. Na mwenzetu mmoja ndio alilala chini.

    Licha ya Yasmin kututoa wasiwasi kuwa Harishi hatatokea usiku ule, hatukulala kwa raha. Mara kwa mara nilikabiliwa na hofu. Nilipolala kidogo nilijikuta ninagutuka na kutupa macho huku na huku.

    Wakati inakaribia kuwa alfajiri ndipo nilipopata usingizi wa uhakika. Nikalala moja kwa moja. Sikuzinduka mpaka kumekucha. Kilichonizindua ni hisia zangu. Niliona kama mlango wa mle chumbani unafunguliwa na mtu aliyekuwa nje.

    Nilipofumbua macho niliona kweli mlango unafunguliwa na kulikuwa kumeshakucha ingawa Yasmin alituambia tuamke alfajiri na kuondoka.

    Nikajiuliza ni nani anayefungua mlango. Nikaona kanzu yenye madoa ya damu ikiingia ndani.

    Alikuwa harishi!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilishituka sana nilipogundua kuwa aliyefungua ule mlango alikuwa ni jini Harishi. Tulipaswa kujilaumu kwa uzembe wetu wa kulala hadi muda ule wakati Yasmin alituambia tuondoke kabla hakujapambazuka.

    Na kwa kweli haukuwa uzembe bali tulipitiwa na usingizi, tena wakati mimi nazinduka wenzangu wote walikuwa bado wamelala.

    Harishi aliingia ndani ya kile chumba. Sasa niliweza kuuona vizuri uso wake. Alikuwa na macho makubwa yenye makengeza.

    Nikajifanya kama nimelala lakini nilikuwa nikimuangalia kwa pembeni na kwa makengeza huku mwili wangu ukitetemeka kwa hofu.

    Pengine ni kutokana na ale makengeza yake, Harishi alipoingia mle chumbani macho yake yalikwenda kwa yule mtu aliyelala chini.

    Mara moja aliinama na kumshika shingo yake kisha akamuinua na kutoka naye ukumbini.

    Nikaisikia sauti ya Harishi akiuliza.

    “Hii nyumba ni yako?”

    Sikusikia jibu bali nilimsikia mwenzetu akipiga ukulele mmoj tu.

    “Jamani nakufa!”

    Halafu sikusikia kitu tena.

    Hapo nilijua mwenzetu huyo alikuwa ameshatoolewa utosi na alikuwa akifyonzwa damu.

    Ule ukulele aliopiga ulimuamsha mwenzangu niliyelala naye. Akainuka na kuketi kitandani.

    “Kitu gani?” akaniuliza.

    Nikaweka kidole changu cha shahada kwenye midomo yangu kumkataza asitoe sauti.

    “Nini kwani?” Sasa sauti yake ilikuwa ya chini. Uso wake ulikuwa umeanza kushituka.

    Nilishuka kitandani nikamnong’oneza “Harishi!”

    Akagutuka. Uso wake ukabadilika na kuvamiwa na hofu.

    “Yuko wapi?” akauliza kipumbavu

    Sikumjibu. Nikamwambia “Tuingie mvunguni mwa kitanda”

    Akakurupuka na kujiingiza kwenye mvungu huku akiburuza shuka aliyokuwa amejifinika. Tulipoingia kwenye mvungu huo tukanyamaza kimya.

    Tuliamua kujificha humo japokuwa hatukuwa na uhakika kuwa tutapona. Bada ya muda kidogo tuliona mlango unafunguliwa tena.

    Nilimuona mwenzangu anatikisa kichwa kwa hofu. Tuliona miguu ya Harishi ikiingia. Ilikuwa miguu mikubwa iliyochafuka na yenye vidole vyenye kucha ndefu. Ilikuwa pekupeku.

    “Kumbe alikuwa ni yule peke yake!” Tukamsikia akisema Peke yake.

    Ile shuka ya mwenzangu aliyokuwa akiiburuza ilitokeza nje ya mvungu wa kitanda. Harishi akaiona!

    Tukaona mkono wake ukishika ncha ya shuka na kuivuta. Jamaa akaiachia. Shuka yote ikavutwa na kuchukuliwa na Harishi.

    “Hizi ni shuka zangu ninazoziiba kwa Wahindi. Imewekwa na nani huku mvunguni?’ akajiuliza mwenyewe kisha akaitupa chini.

    Tukaona miguu inageuka na kutoka. Alipotoka tulishukuru. Mimi nilitambaa hadi kwenye mlango, nikaufungua na kumchungulia.

    Nilimuona akiinama na kuushika mguu wa mwenzetu aliyemuua, akamburuza kuelekea kwenye mlango wa kutokea.

    Mwenzangu alikuwa amebaki mvunguni akinitazama. Nikaufunga mlango taratibu kisha nikarudi mle mvunguni.

    “Mwenzetu ameuawa” nikamwambia mwenzangu. “Harishi amemburuza na kutoka naye”

    “Alimuona wapi?”

    “Mara ya kwanza aliingia ndani, wewe ulikuwa umelala, Akamsomba pale kwenye godoro na kutoka naye kwenda kumuua. Ndio pale ulipoamka”

    “Kumbe Yasmin alitaka tufe alipotuambia tulalae humu?”

    “Ni makosa yetu sisi. Yasmin alituambia tutoke Alfajiri, sisi tumelala hadi saa hizi kumekucha”

    “Lakini ni kweli”

    Wakati tunazungumza kwenye mvungu, Yasmin akaingia.

    Tulipoona miguu yake tulitoka mvunguni.

    “Jamani niliwambia nini?” akatuuliza kwa kutaharuki.





    Hakukuwa na aliyemjibu. Sote tulikuwa tumeshikwa na fadhaa.

    “Si niliwambia mtoke alfajiri, mmelala hadi saa hizi wakati niliwambia kuwa Harishi atakuja leo”

    “Ni kweli ulituambia” nikamkubalia.

    “Sasa mbona hamkutoka alfajiri?’

    “Tumepitiwa”

    “Mtanilaumu mimi bure jamani!”

    Hatutakulaumu hata kidogo. Umetufanyia wema sana”

    “Harishi alikuja mapema sana akaniambia anasikia harufu ya kimtumtu. Nikamwambia mtu ni mimi. Akaniambia hebu ngoja. Akatoka kuja kuwatafuta”

    “Siku hizi atakuwa anakuja kila siku kwa sababu ameona anapata mlo anaoutaka. Ni lazima mjihadhari”

    “Mimi naona tuondoke tu humu ndani” Mwenzangu akasema kwa woga.

    “Lakini amekwishakwenda zake. Kwa leo hatarudi tena” Yasmin akatuambia.

    “Itabidi tuondoke tu” Mwenzangu alizidi kusisitiza.

    “Kwani wenzenu wengine wako wapi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Bado wamelala hadi sasa?” Yasmin akauliza kwa mshangao.

    “Naona bado wamelala” nikamjibu.

    “Kumbe nyinyi hamuwezi kuamka alfajiri?”

    “Tatizo ni kuwa usingizi wenyewe unakuja wakati wa alfajiri” nikamwambia Yasmin.

    “Basi ni balaa. Sasa itabidi usiku mwende mkalale sehemu nyingine, mjaribu bahati yenu”

    “Tutafanya hivyo”

    “Kuna nyumba nyingi hazina watu. Mnaweza kutafuta nyumba nzuri yenye vitanda mfanye makazi yenu. Hapamtakuwa mnakuja mchana tu, muda ambao nitawambia mimi”

    “Tumekue;lewa, ngoja niwaamshe hawa mabwana”

    Tukatoka pamoja mle chumbani. Tulipotoka tukawaona wenzetu nao wametoka.

    “Hivi ndio mnaamka jamani?” Yasmin akawauliza.

    “Dadayetu si unajua usingizi hautabiriki?” Mtu mmoja akamjibu.

    “Hamkumbuki jana niliwambiaje? Si niliwambia muamke alfajiri muondoke?” Yasmin akawauliza.

    “Ni kweli ulituambia lakini ndio tumepitiwa”

    “Shakiri ameuliwa leo na Harishi!” nikawambia.

    “Unasema kweli?” wakaniuliza kwa pamoja kwa mshituko.

    “Ni kwa sababu ya kuchelewa kuamka. Sisis tumeponea chupuchupu baada ya kuingia mvunguni mwa kitanda”

    “Basi utakwisha!”

    “Yasmin ametupa wazo. Badala ya kulala hapa tutafute nyumba nyingine tuweke makazi yetu. Hapa tutakuwa tunakuja kula chakula mchana katika muda atakaotuambia Yasmin”

    “Hivyo itakuwa vizuri” Mmoja wa wenzetu hao akasema.

    “Sasa mjitayarishe, ninaenda kuwaandalia chai” Yasmin akatuambia.

    Wakati Yasmin anakwenda jikoni, wenzetu wawili waliokuwa wamelala chumba cha pili ilivyokuwa hadi mwenzetu akauliwa.Tukawaeleza.

    Kwa kweli walipata hofu.

    “Sasa tukishakunywa chai tutoke tukatafute hiyo nyumba” nikawambia wenzangu.

    Ilipofika saa nne tayari tulikuwa tumeoga na kunywa chai. Tukamwambia Yasmin tunataka kwenda kutafuta nyumba ya kukaa kwa maana tayari tulishakuwa wakazi wa kisiwa kile na hatukuwa na mategemeo ya kuondoka.

    “Kwani mpaka mwende nyote”Yasmin akaniuliza.

    “Unataka twende wangapi?” nikamuuliza.

    “Mnaweza kwenda wawili, wawili mkabaki”

    Mimi na wenzangu tukatazamana lakini sote tulionekana kutoliafikiwazo la Yasmin.

    “Acha tu twende sote” nikamwambia Yasmin.

    “Basi ngoja niwasindikize, msiniache peke yangu”

    “Tukizunguka na wewe itakuwa vizuri” nikamwambia.

    “Kwanini?’

    “Kwa sababu wewe ndiye mwenyeji wetu, utaweza kutuongoza vizuri”

    “Haya basi twendeni”

    Tukatoka na Yasmin. Yasmin alikuwa akikijua vyema kisiwa hicho. Alituzungusha mitaa mbalimbali tukiangalia nyumba. Mwisho alitupeleka katiaka nyumba moja ambayo alituambia ilikuwa ya mtu mmoja tajiri wa kisiwa kile.ambaye naye naye aliuawa na Harishi.

    Ilikuwa nyumba nzuri lakini ilikuwa imechakaa kwa vile ilikuwa haiishi watu. Tulipoingia ndani tulikuta mavumbi yalikuwa yameenea nyumba nzima.

    Tukaanza kazi ya kuisafisha nyumba. Yasmin alitusaidia kufanya usafi. Ilikuwa kazi iliyotuchukua saa kadhaa.

    Tulipomaliza tulichota maji kwenye kisima tukaoga kisha tukapumzika. Hapo ndipo tulipoanza kugawana vymba

    Nyumba yenyewe ilikuwa ya vyumba vine na sisi wenyewe tulikuwa wanne. Kila mmoja alijichagulia chumba chake alichokipenda. Tulifungua makabati tukatoa mashuka na kutandika vitanda tulivyovikuta humo ndani.

    Wakati ninatandika kitanda Yasmin aliniambia nimpe shuka atandike yeye. Nikampa.

    “Natamani sana ningekuwa hapa pamoja na nyinyi” Yasmin akaniambia wakati anatandika.

    “Ukiwa hapa utatuponzea sote”

    “Ninasema tu lakini najua haitawezekana. Unajua katika nyinyi nyote nimekupenda wewe zaidi. Ninatamani ungekuwa mume wangu”

    “Hata mimi natamani ungekuwa mke wangu lakini ndio tupo jela. Uhai wetu unahisabika”

    “Ni kweli. Usikumbushiie hayo. Tuswali tuombe nusura itufikie”

    “Wewe unaswali?” nikamuuliza Yasmin.

    “Ninaswali lakini kwa siri sana. Harishi hataki niswali. Swala ndiyo inayonipa matumaini ya kuishi”

    “Umenikumbusha jambo zuri sana na sisi tutaanza kuswali”

    “Kila mara ninaota kunamtu atakuja kumuangamiza Harish na mtu huyo atakuwa mume wangu”



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog