Search This Blog

HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA - 5

 







    Simulizi : Hamunaptra - Mji Uliopotea

    Sehemu Ya Tano (5)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/





    §§§§§



    Zamarad aliendelea kumtazama huyo kiumbe akimkabidhi fuvu lile Sherhazad, naye akawa akilipokea huku akitabasamu.

    “Humsaing tuuunggg, seiduss seiduss” Zamaradi alitamka maneno hayo ambayo kwa kiwango chao katika ulimmwengu huo, ungeweza kujigeuza na kuwa kiumbe yoyote yule.. Mara upepo mkali ukaanza kuvuma ndani ya jengo lile. Zamaradi akageuka mwewe, akachomoka pale alipo na kulinyakuwa lile fuvu na kutoka nalo dirishani kwa kasi.



    Sherhazad alitamani kulia kwa kuona Zamarad amemzidi ujanja katika hilo, akanyoosha mkono wake na kupewa uta wake wa kichawi, akaweka mshale juu yake na kuuvuta kwa nguvu, akautuma kwa maneno yasiyoeleka kwa lugha yake ya kijini, ule mshale ukaondoka kwa kasi kumfuata yule mwewe.

    Seidon alikuwa katika hali mbaya sana, kama ni kupambana basi alikuwa kapambana na jitu la kutisha linalowaka moto kila upande. Ilikuwa ni wakati wa kumaliza kazi aliyotumwa, akasikia radi zikipiga huku na huko, yule malaika wa moto akashtuka na akajua kwa vyovyote mvua itapiga hapo muda si mrefu, na kweli alipogeuka ulikotokea mlio ule. Malaika wa moto anayetegemewa na Sherhazad katika shughuli ngumu kama hizi huwa hatakiwi kuguswa na maji hasa mvua kwani mwili wake umeumbwa kwa moto hivyo akiguswa na maji ndiyo mwisho wa uhai wake. Mara moja bila kuuliza, akamgeuza farasi wake na kuondoka, na kweli mvua kubwa ikanyesha eneo lile na kukatika kwa muda mfupi. Mbele ya Seidon akatua mwewe mkubwa aliyeshika fuvu la Cleopas miguuni mwake, akatua na alipoliacha lile fuvu na kuondoka hakufika hata mita 10 mshale wa kichawi uliotumwa na Sherhazad ukampiga yule mwewe na kisha ukageuka nyoka aliyekuwa akijiviringa mwilini kwa yule mwewe. Yule mwewe akaanguka chini na vumbi likatimka eneo lile.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Seidon akalichukua lile fuvu na kuondoka mahala pale haraka, alikumbuka maneno ya yule mzee ambaye alikufa kwenye bonde la mauti, kuwa akifika katika mstari wa Ikweta basi nguvu zote za majini haziwezi kufanya kazi, hakuwa mbali na eneo hilo. Seidon akiwa na upanga wa Vernad mkono wake wa kulia na ule wa kushoto amelishikilia lile fuvu, sasa halikuwa kwenye mfuko lilikuwa wazi mkononi mwake, akaanza kutimua mbio kuielekea Ikweta. Nyuma yake alisikia sauti za watu wanaomkimbiza lakini kila alipogeuka hakuwaonaa, aliendele kukimbia lakini bado aliona hafiki wakati mahali penyewe palikuwa karibu. Mara hii alipogeuka nyuma aliona kundi kubwa la watu waliokuwa wakimfukuza kwa miguu na farasi. Seidon alikimbia kwa nguvu zake zote, akakaribia kabisa Ikweta, ndipo alipoanza kuona maajabu ya lile fuvu alilolibeba, akajikuta amekuwa mwepesi, anakimbia akikanyaga hewani na si ardhini kama ilivyokuwa mwanzo, wakati huo vishindo na kelele za radi zilikuwa zikisikika na anga lote lilikuwa likikatwa kwa miali mikali ya radi. Seidon aliendelea kukimbia na alipoingia Ikweta alijikuta akikimbia zaidi kuliko mwanzoni, mwisho wake akaingia ndani ya pango na kujificha, lile fuvu likatengeneza mwanga wa kutosha uliopitia katika matundu ya macho yake.



    Seidon akawa anashangaa kila analoliona likifanyika sasa kutoka katika fuvu lile.

    “Amatagaimba, uko wapi?” akanong’ona Seidon. Mara akasikia sauti za watu wawili wakiongea, sauti zao zilikuwa zikisikika kutoka chini. Seidon akasimama na kuangalia huku na huko lakini hakuweza kuona mtu yeyote isipokuwa aliendelea kusikia sauti zile mbili, ya kike nay a kiume.

    Seidon akashtuka kidogo, kwani alikuwa akizisikia sauti zile kutoka chini ya ardhi, akapiga magoti na kutega sikio lake ardhini, akaisikia kwa uwazi kabisa sauti ya Amatagaimba.

    “Inatupasa tutoke humu, namtafuta rafiki yangu Seidon,” ile sauti ikasikika.

    “Amata gaimba!” Seidon akaita kwa sauti ya taratibu.



    §§§§§



    Amatagaimba akamzuia Anna kwa mkono wake wa kuume.

    “Vipi?” Anna akauliza.

    “Kuna mtu ananitafuta,” akamjibu. Baada ya kutulia kama dakika tatu hivi, akatazama kidole cha mkono wake, akaitazama pete ya ajabu aliyokuwa nayo kidoleni, akaongea maneno Fulani na mara upepo mkali ukavuma na kutimua vumbi jingi. Anna Davis kwa woga akajificha nyuma ya Amatagaimba akitetemeka kwa hofu.

    Amatagaimba akanyosha mikono yake na lile vumbi likatulia, katikati ya vumbi lile kukabakia farasi mkubwa aliyesimama kimya akimtazama Amatagaimba. Akamshika mkono Anna na kumwelekea yule farasi.

    “Mi naogopa kupanda farasi,” Anaa alikataa.

    “Endelea kuogopa, utabaki hapo hapo ulipo maisha yako yote!” Amatagaimba akamjibu huku akimtazama, “Twende! Tena wewe una kazi ngumu sana ya kufika huko ulikotoka”. Amatagaimba akakwea farasi, akamtazama tena Anna bado akiwa amesimama palepale.



    “Tazama nyuma yako!” akamwambia. Anna akageuka nyuma na kushuhudia moto mkubwa ukiwaka huku ukielekea kule walikosimama wao.

    “Mamaaaaaaaa…. Amatagaimba nisaidie!” Anna alipiga kelele za woga, akakimbilia pale kwenye farasi, mkono wake ukashikwa na ule wa Amatagaimba na farasi akaanza kuondoka kwa kasi huku Anna akijiweka vizuri mgongoni mwake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wanakuja Amatagaimba, watatuua wale kimbia!” Anna alikuwa akipiga kelele mgongoni mwa Amatagaimba. Farasi alikuwa akipiga mbio za ajabu, lakini Amata gaimba kila alipogeuka nyuma aliona jeshi lile linakuja kwa kasi kuliko yake. Vumbi lilikuwa likitimuliwa na miguu ya yule farasi, hakujali mchanga mwingi wa jangwani alizipiga mbio kwelikweli. Kwa mbali kidogo, Amatagaimba aliona kitu kama nyumba au mlima hivi hakuweza kujua haraka ni kitu gani kiuhakika.

    “Huyo atakuwa Dherhazad na swahiba zake!” Amatagaimba aliendelea kuongea.



    “Sherhazad?” Anna akauliza akiwa bado kamng’ang’ania Amatagaimba kiunoni.

    “Ndiyo ni Malkia wa majini katika milki ya Soria,” akamjibu. Baada ya mwendo wa muda kidogo wakakaribia kabisa ule mlima, mara zikaanza kusikika kelele za watu, watu wengi kana kwamba kuna kitu wanakifukuza. Kelele zao zilikuwa zinaumiza masikio, mara nyingi Anna alikuwa akijiachia na kuziba masikio na kuataka kuanguka, kelele zilizidi sana, Amatagaimba hakujali.



    “Anna!!! Jishike vizuri, tunaingia Ikweta!” Amatagaimba alipiga kelele huku akimwimiza farasi kupiga mbio, zile kelele sasa zilikuwa kali zaidi kiasi kwamba zilikuwa zikisumbua masikio ya wote. Alipogeuka nyuma aliona wale majeshi wanakuja na farasi wao tena hawakuwa mbali.



    “Amatagaimba., wanatufikia, hawa hapa!” Anna alipiga kelele za woga.

    “Tulia Anna, tukifika Ikweta tutakuwa tumekwishapona,” akajibu.

    Mara ghafla yule farasi akawakama amejipiga kwenye ukuta au jiwe, wakaanguka chini wote wawili na farasi wao, tayari walikuwa wameingia Ikweta, lakini farasi yule aliishia pale ambapo Ikweta inaanzia kwa kuwa hakuwa farasi wa kweli bali wa kutengenezwa. Amatagaimba aliinuka nharaka na kumshika mkono Anna aliyekuwa amechafuka kwa vumbi la janagwani kisha akaanza kukimbia naye mpaka kwenye kitu kama mlango, akaupiga teke ukafunguka wakaingia wote wawili na kuufunga mlango nyuma yao, kisha wakasimama kwa kujibanza kwenye pango hilo lenye kiza kinene.

    “Hamunaptra!” Amatagaimba alijisemea kwa sauti ndogo, kisha akaanza kufuatilia ngazi ndefu zilizokuwa zikiteremka chini.

    “Amatagaimba” Anna akaita kwa kunong’ona.

    “Shhhhhh!!!!! Usiamshe roho zimelala” Amatagaimba alaimwambia Anna. Amatagaimba akatazama zile ngazi zilizokuwa zikielekea shimoni, giza lilitanda, sauti ya vitu kama wadudu ndiyo iliyokuwa imetawala ndani humo, alikuwa akikanyaga kwa hatua za polepole ambazo hazikuwa zikitoa hata kelele, huku upanga wake ukiwa mikononi mwake barabara kabisa kwa hatari yoyote, mbele zile ngazi zikaisha pakabaki uwanda mkubwa lakini uliojazwa na giza totoro.



    Mara sauti za milango ikifunguliwa zilisikika, Amatagaimba akasimama ilhali upanga wake ulikuwa mikononi mwake, mara kitu kama jiwe kilimpitia jirani na kugondokea upande wa pili. Mara kelele kama za watu waliokuwa wakija kumshambulia zikaanza kusikika, aliutwaa upanga wake na kuanza mapambano, ilikuwa ni kazi ngumu sana kwani alikuwa havioni viumbe anavyopigana navyo kutokana na giza lililokuwa mahala hapo.

    Alijitahidi kuutembeza upanga wake wa nguvu zote alihisi kupiga vitu Fulani lakini hakuweza kuviona. Anna alibaki nyuma ya Amatagaimba akijikinga kupitia mgongo wake.

    “Amatagaimba, nisaidie!!!” Anna alipiga kelele alipohisi mguu wake kama unafungwa minyororo, amatagaimba aligeuka kwa wepesi na kuona japo kwa taabu, mwiliwa Anna ukivutwa, akaruka sarakasi na kukata ule mnyororo. Kelele zilizodo kuongezeka na viumbe hivyo vya ajabu vilizidi kumiminika ikawa taabu.

    Mara ardhi ya mule ndani ikaanza kuzunguka, taratibu na kueongeza kasi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Aiyaaaaaaa!!!!!” Amatagaimba alipiga kelele alipomuona Anna akitumbukia katika ufa mkubwa wa uliojitokeza ukutani na kufanya mwanga wa upande wa pili uking’aa, kwa haraka akawahi na kupenya katika ule ufa lakini kabla hajamaliza kuingia nguo yake ilibanwa na ule ufa.

    Sasa kelele za radi zikaanza kusikika, mvua kubwa ikaanza kunyesha.

    “Hapo sasa hauna ujanja, kama nilivyomkamata mwenzako sasa ni zamu yako,” sauti ya kike iliyoksikika kwa mwangwi ilikuwa inaongea sana, “Ingia, ingia wewe huko!” amatagaimba alianguka chini baada ya Anaa kukata ile nguo iliyonasa kwenye mwamba. Mara moshi mzito ukaanza kujaa mahala hapo.

    “Aaaaaaa ha ha ha ha ha, Aaaaaa hahahaha, zama zenu zimekwisha nipeni hilo fuvu, niutawale ulimwengu wote wa juu na wachini,” sauti kali ya Sherhazad ilisikika na kufanya kile chumba kiwe na vitu kama radi katika kuta zake, ilikuwa ni hali ya kuogofya sana, Anna alikuwa akipiga kelele huku akiziba masikio yake.



    Kwa mbali Amatagaimba akawa anasikia kana kwamba kuna ibada ilokuwa ikiendelea, kwani sauti za watu wengi zilikuwa zikisikika nkama watu wanaosali katika lugha isiyoeleweka.

    “Krusum krusum, sontum sontum …” ile sauti ilizidi kukaribi akana kwamba waliokuwa wakisali walikuwa wakitembea. Kwa sekunde kadhaa hawakusikia sauti ya Sherhazad. Amatagaimba alizidiwa na moshi ule wakati huo Anna alikuwa chini kaishiwa nguvu, mara radi kali na mngurumo ikasikika mara moja.

    “Amatagaimba… nifuate!” ilikuwa sauti ya Seidon.

    “Seidonnnnn!” Amata naye aliita huku akimtazama Anna aliyekuwa hajiwezi kwa moshi ule, akamvuta kwa mkono wake na kumburuza mpaka pale alipomkuta Seidoni ambaye alisimama katikati ya ufa mkubwa wa ukuta ule wa jiwe akiwa juu ya farasi wa ajabu.

    “Amatagaimba, pita!” akamwamuru, Amatagaimba akafanya hivyo, akapita na kutokea upande wa pili, nje ya lile shimo la mtego, Seidon akamwamuru farasi kurudi nyuma, naye alipoumaliza ule ukuta tu, ukajifunga kwa nguvu na kufanya mawe kutoka juu kuanza kudondoka huku na kule. Seidon akashuka juu ya yule farasi.



    “Huyu ni nani shujaa wangu? Si unakumbuka huku hatutakiwi kufanya lolote na mwanamke” Seidon akafoka huku akipiga magoti kumwangalia Anna.

    “Seidon, huyu ni mwnadamu sio jinni kama unavyofikiria, nimemkuta amenasa huko chini nikamsaidia kutoka, ni hadithi ndefu, tutaongea zaidi,” akamwangalia Seidon juu mpaka chini, “Fuvu liko wapi?” akamwuliza.

    “Amatagaimba bora nimekuona nalikuwa nakutafuta kila upande wan chi hii, fuvu limenidondoka katika shimo refu sana hata sikuwa na uwezo wa kulichukua, twende twende mara moja,” Seidon akamwambia Amatagaimba.

    Amatagaimba kabla ya kuondoka akachukua maji kutoka kwa Seidon na kumpa Anna, akayanywa kwa fujo na kuyamaliza. Nguvu zikamrejea. Anna akapanda juu ya farasi na Amatagaimba akatua nyuma yake, safari ikaanza.

    Seidon akapiga mbio kwa ustadi akipita vijilima vilivyo ndani yake, “Amatagaimba, Sherhazad na Wafuasi wake wamezingira eneo lote!” akamwambia.



    “Sasa tunafanyeje, inatubidi kutoka nje?” Amatagaimba akauliza.

    “Hapana, hatutoki nje kwani fuvu limedondokea humu ndani na tukilipata tu mlango wa kuifikia Klakos uko hukohuko chini,” akamjibu huku akimchochea farasi yule kusonga mbele, mote walimopita mlikuwa giza tupu, mara ghafla yule farasi akapiga ukelele na kupoteza muelekeo, akajipigiza katika jiwe na wote watatu wakaanguka chini. Yule farsi alilala chini kimya, Amatagaimba akachomoa nyoka kutoka usawa wa kifua cha farasi, akamshika mkononi, yule nyoka alikuwa ametumbukia kichwa ndani ya mwili wa huyo farasi. Akamsika mkia na kichwa akamvutaq kwa nguvu yule nyoka akakamaa kama mshale, Amatagaimba akautoa uta wake na kumpachika yule nyoka kisha akauvuta na kuufyatua gizani. Kitendo kile kilimuudhi sana Sherhazad ambaye alikuwa akitazama kila tukio kupitia dirisha lake la ajabu.



    §§§§§



    “Ni nani huyu anayeniuzi? Ana nguvu gani za kunifanya mimi mjinga, nilishamdhibiti sasa katoka vipi? Enyi Wachawi wa Soria, wazuieni njia, nataka sasa niende mwenyewe kwani fuvu lkile liko jirani kabisa na Klakosi, sasa hivi wanaweza kulirudisha, name sintokubali walirudishe,” Sherhazad alipiga kelele, akatoka dirishani na kuliendea joho lake kubwa la kung’aa, akakwea farasi wake wa kijini mwenye uwezo wa kupita angani, “Sasa sintotuma kivuli changu tena ila nakuja mwenyewe, naona mlipofika ni pabaya,”

    Sherhazad aliondoka kwa kasi kuelekea Hamunaptra, ilimchukua nukta kadhaa tu kufika katika mji huo, mji wa kale, mji ambao kwa macho ya kibinaadamu hauonekani kwa kuwa umepotea. Hasira zilimtawala Sherhazad, alikuwa akipiga mbio zisizo za kawaida na farasi wake, akitaka kuwahi kabla Seidon na Amatagaimba hawajaingia mle shimoni ambako huko ndiko kwenye njia ya kuifikia Klakos. Kwa kuwa hakuweza kuipita Ikweta, ilimbidi azunguke njia ndefu ambayo ingemtolea upande wa pili wa mji huo, huko angeweza kuingia kiurahisi zaidi.



    “Angusha tufani kubwa ya mvua yam awe ndani ya shimo hilo,” akasema huku akiwa mwendo wa kasi juu ya farasi wake. Wale wachawi wake walisikia ombi lake na kuanza kufanya linalowezekana. Sherhazad alikasirishwa na jibu la wale wachawi kuwa imeshindikana kuteremsha tufani katika shimo ile.

    “Nini, nini kimewashinda enyi wachawi Wapumbavu?” akawauliza kwa kuongea nao kwa hisia tu mawazoni mwao.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akajibiwa kuwa ndani ya shimo hilo kuna nguvu kubwa ambayo ipo kinyume na wao, ndiyo inayokinga yote hayo.

    “Shiit! Nikimpata huyu kijana namla nyama,” akajisemea huku akiendela na safari yake. Mbele yake alikabiriwa na bonde kubwa, kwa akili yake ya haraka akakumbuka kuwa bonde lile ni mto mkubwa wa maji ambao umekauka miaka mingi, karne na karne. Na alijua wazi kuwa mto ule ulikuwa ukiingia moja kwa moja chini ya mapiramid na kutokea kwenye kiti cha Klakos.

    Nitapita hapa, nitatokea moja kwa moja kwa Klakos, alijisemea na kumwamuru farasi wake aliyekuwa angani kulipita bonde hilo abadili njia na kurudi chini.



    §§§§§



    Wakati wale wachawi walipokuwa wakijaribu kuumba mvua yam awe ili kuwanyima njia Seidon na Amatagaimba, ndani ya shimo lile kubwa nako kulikuwa na jambo lingine, Amatagaimba akiwa na ile pete yake ya ajabu alikuwa akiomba iwafikishe salama waendako kwani ni kitambo kidogo tu kilichobakia wao kufika chini katika lile shimo.

    Kishindo kikubwa kikasikika na vumbi la wastani likatimka. Amatagaimba, Seidon na Anna Davis walidondoka katika udongo laini, chini ya shimo hilo lenye giza. Seidon aliamka haraka bila kujali maumivu aliyoyapata akaamua kuliwahi fuvu ambalo lilikuwa mahala hapo, alipoweka mkono tu kulinyanyua, akaona kitu kama upanga kinatua karibu na kiganja chake cha mkono, akawahi kuutoa, akatazama juu akamwona mwanamke mrefu mweupe mwenye nywele nyingi, nguo yake iliyofunikwa na joho kubwa ilikuiwa ikimetameta na kuyafanya macho ya Seidon yashindwe kuona sawasawa.



    “Amatagaimbaaaa!!!!” Seidon akaitwa kwa nguvu huku mikono yake ikiziba macho yake. Amatagaimba akashtuka na kumtazama Seidon aliyekuwa kajiinami ilhali lile fuvu limesogea mbali kidogo.

    “Seidon, Seidon!” akaitwa na kunyanyuka haraka kisha akamwendea Seidon lakini kabla hajamfiki, alihisi kama jiwe zito limempiga kifuani akatupwa upande wa pili na kujibamiza ukutani. Mara tu baada ya kujibamiza ukutani kishindo cha ajabu kikasikika, na ule ukuta ukapasuka katikati, radi kali iliyokata ule ukuta ilitisha na mwanga mkali kutoka ndani ya ule ukuta ilipenya na kung’aza lile shimo lote. Hakuna aliyeweza kutazama mwanga ule lakini Amatagaimba alihisi kua upande wa pili kulikuwa na kitu kama chumba kikubwa, kilichong’aa kwa dhahabu safi kutokana na miali ya kitu kama jua iliyokuwa ikipenya kupitia matundu Fulani. Hakuelewa sawasawa lakini aliona vitu kama viumbe Fulani vilivyojiinamia katika mtindo wa nusu duara na mbele yao akiwapo mwingine, lakini kwa jinsi miali ile ya mwanga ilivyopishanapishana mle ndani hakupata uhalisia wa kile anachokiona.

    “Klakos!” akatamka Seidon, na mara ileile ukatokea mngurumo mkubwa wa kutisha uliofuatana na ardhi kutetemeka. Seidon akajirusha kulichukua lile fuvu, lakini akapambana na upanga mkali wa Sherhazad.



    “Tulia Mpiga mbio, huna uwezo wa kulichukua hilo fuvu na wala huwezi kuingia pale kwenye kiti cha enzi cha Cleopas, kabla sijakuua, ulinifanya mimi mjinga ukanihadaa sio?” Sharhazad aliongea huku akimzunguka Seidon aliyekuwa bado pale chini kajiinamia.

    “Ewe mwanamke jinni dhalimu, kwa nini hupendi neema za wanadamu ilhali wanadamu hao hao unawatumia katika mambo yako mengi?” Amatagaimba akauliza huku akijiweka sawa, upanga wake ukiwa mkononi.

    “Kelele! Ewe kiumbe wa dunia, kwanza umeingilia vita isiyo yako na kwa hilo utaijutia nafsi yako,” Sharahazad akamwambia Amatagaimba na wakati huo akijibizana na Amatagaimba, Seudon alijinyanyua kwa haraka na kujirusha sarakasi akalikamata lile fuvu na kutaka kumpiga chenga Sherhazad, lakini lo, jinni ni jinni tu, Seidon aliona taswira nyingi za Sherhazad ndani ya lile shimo akashindwa kujua hasa yupi ni yupi.



    Amatagaimba akavuta hatu na kujirusha kumkabili Sherhazad, panga zao zikakutana hewani, wote wawili wakashuka chini na kutua kwa miguu yao. Sherhazad alitumia nguvu zote kumsukuma Amatagaimba ili apate nafasi ya kufanya shambulizi, lakini Amatagaimba alitulia palepale hakusogea hata milimita moja. Nguvu mbili zilizshindana, sherhazad akaingalia pete ya Amatagaimba, pete inayompa jeuri, akautoa upanga wake ghafla na kujizungusha kwa umahiri mkubwa. Amatagaimba akaitambua hila yake, akainama na Sherhazad akapita juu yake, alaipotua tu, upanga wa Amatagaimba ukapenya mbavu za Sherhazad.

    “Aaaaaaaaiiiiiggghhhhh!!!!!” kelele za Sherhazad zikapasua anga, mara kilicho kwenye kuta, paa, nje , ndani ya kaburi kikarudiwa na uhai.



    “Aisatuuum, Aisatuuum,” akaongea lugha isiyoeleweka, pale ulipochoma upanga pakawa panatoka moshi wa buluu, Amatagaimba alikuwa bado kashikilia upanga wake palepale na kumfanya Sherhazad asisogee popote, kwani alipochoma ndipo hasa penye uhai wa kiumbe huyo.

    Kelele za watu wa kutisha zikaanza kuzikika ndani ya shimo lile. Amatagaimba akaona hapo mambo yataharika wakati tayari wameshafika mwisho. Akauchomoa upanga wake haraka kutoka katika mwili wa Sherhazad.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Seidoooonnnn!” akaita huku akinyoosha upanga wake kule kwenye ule mlango uliojitokeza katika ukuta, Seidon akaruka na kujitupa upande wa pili kwenye ule mlango lakini hewani alikutana na kifua cha Sherhazad, Seidon akaanguka na kukohoa.

    Anna Davis, akarudiwa na fahamu akasimama haraka haraka akiwa anathema kama aliyekimbizwa na mbwa.

    Seidon alitambaa huku akiwa na maumivu, na fuvu likiwa mkononi mwake, Sherhazad alijitahidi kumshambulia lakini alijikuta anaishiwa na nguvu, anashindwa, viumbe wake aliowaita kijini nao walijikuta wanakosa nguvu ya kufanya lolote. Amatagaimba akamshika mkono Seidon na Anna, Seidon akajitahidi kunyanyuka na kuvuta hatua taratibu kuuelekea ule mlango.

    Sauti za watu waliokuwa kwenye ibada zikaanza kusikika kwa mbali zikitoka ndani ya kile chumba cha Klakos.



    Sherhazad akajitahidi kuruka ili amkamate Seidon haikuwezekana, alijikuta anashindwa kufanya lolote. Kila walipozidi kuufikia mlango walijikuta wakipata nguvu na kuanza kukimbiua kuelekea ndani, kelele za watu waliokuwa kama wakishangilia zilisikika. Kufumba na kufumbia, tena waligundua kuwa wanapita hewani nyanyo zao hazigusi ardhi. Punde si punde wakajikuta ndani ya chumba kile tulivu, mvumo wa kitu kama upepo ulikuwa ukisikika taratibu. Jinsi walivyokitazama kile chumba, kilionekana kama mji mkubwa sana, wenye magofu mengi nay a kutisha, masnamu ya wanyama mbalimbali mengine bado yamesimama kwenye nguzo zake na mengine tayari yamekwishaanguka.

    Hakukuwa na mmea wenye uhai, yote ilikuwa imekauka kwa ukame uliokithiri. Kwa ujumla ulikuwa mji uliopotea, ukungu ulijaa kila mahali, mvumo wa upepo uliendelea kufanya sauti tamu.

    “Hamunaptra!” Amatagaimba akatamka.

    Seidon na Anna wakageuka kumtazama, “Hamunaptra?” Anna akauliza.



    “Ndiyo, Hamunaptra,” Seidon akaongezea kumjibu Anna kwa ni alionekana kuwa na dukuduku juu ya hilo. Mara baada ya kutaja jina hilo wakasikia sauti hafifu ya kitu kama bembea inayobembea huku na kule na minyororo yake kufanya hiyo sauti kuashiria kuwa ni minyororo mikavu isiyo na kilainishi. Sauti hiyo ilisikika umbali mdogo tu kutoka pale waliposimama. Ukungu mzito uliwafanya wasiweze kuona hata mbele yao kuna nini, kwani hata wao wenyewe walikuwa wakionana kuanzia viunoni kuja juu. Ile sauti ya watu waliokuwa wakifanya ibada iliendelea. Dakika chache baadae walisikia kama mlango ukifunguliwa sehemu Fulani, kisha ukimya ukawakabili.



    Ule ukungu uliowazunguka ukaanza kupungua taratibu na wote wakaweza kuona ardhi iliyopo eneo lile, vito vya thamani vya dhahabu, almasi, yaspi, quartz, coral na vingienvingi vilikuwa viking’azwa na mwanga wa jua husio na joto la kuchoma bali la kuburudisha lakini kila walipoangali hawakuliona jua lenyewe isipokuwa mwanga tu.

    Mbele yao kulikuwa na kidaraja kidogo sana chini ya kidaraja hicho kulikuwa na mto lakini mto huo uliwashangaza kwani ulionekana kupitisha kitu kama uji wa buluu uliochanganyika na wekundu na weusi, uji huo ulikuwa ukichemka. Nyuma yao wakasikia kishindo cha ajabu, Amatagaimba akageuka na kumwona Sherhazad akija kwa kasi, mkononi mwake amekamata upinde wa ki-jini.



    “Tuondokeni haraka!” Amatagaimba aliwaambia Seidon na Anna.

    “Tuelekee wapi?” Seidon akauliza huku mkono mmoja ukiwa umemshika Anna na mwingine umekamata lile fuvu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Vuka hilo daraja,” Amatagaimba akawaambia.

    Seidon akaanza kuliendea lile daraja, lakini kabla hajaanza kulivuka Anna akaponyoka mkononi mwake na kubaki nyuma.

    “Anna!” Seidon akaita.

    “Naogopa kuvuka, daraja hilo minyororo yake imeoza, tutatumbukia,” kabla hajamaliza kujibu Anna, akajikuta akipigwa kikumbo kikali ambacho kilimsukuma mpaka darajani. Seidon akiwa tayari katikati ya daraja ambalo lilikuwa likinesa vibaya, na minyororo iliyoshika daraja hilo kuanza kushindwa kuhimili uzito, inayoanza kuachia mmoja baada ya mwingine, akamdaka Anna na kukimbia nae kuvuka. Walipokaribia mwisho mnyororo mmoja ukakatika na lile daraja likainama upande mmoja.

    “Mamaaaaaaaa!” Anna akapiga kelele na kutereza vibaya, miguu yake ikaliacha daraja, Seidon akawahi kukaza mikono na kumzuia, lakini miguu yake tayari ilikuwa imeacha daraja na sasa ikining’inia chini ya daraja. Anna akalia kwa uchungu sana, akijua kuwa mwisho wake sasa umefika.



    “Jipe moyo Anna, tumefika mwisho sasa,” Seidon alipiga kelele hukumkono wake mmoja tu ukiwa umemshika Anna, “Shika kwenye daraja kisha jivute juu,” Seidon akatoa maelekezo.

    “Seidon siweziiii !” Anna alilia.

    Wakati huo maopambano makali katika ya Amatagaimba na Sherhazad yalikuwa yakiendelea, Amatagaimba alikuwa akimzuia Malkia wa majini kulifikia hilo daraja, pia alitaka Seidon amalize kazi hiyo kwani baada tu ya daraja lile kulikuwa na ngazi ambayo juu yake kulikuwa na sakafu kubwa na Klakos ilikuwa hapo.

    Seidon akashindwa afanye nini, amuachie Anna na kwenda kurudisha lile fuvu au amshike Anna na achelewe kufikisha lile fuvu wakati huohuo hajui nini kitatokea.



    §§§§§



    Upande wa juu baada ya lile daraja kulikuwa na kitu kama jukwaa lenye ngazi zisizopungu ishirini na nne, na juu kabisa kulikuwa na kitu kama viti saba, vitatu upande wa kushoto na vitatu upande wa kulia, kisha kimoja kilikuwa mbele kabisa. juu ya hivi viti sita kulikuwa na viumbe sita vilivyokaa katika mtindo unaofanana, vyote vikiwa vimeweka viganja vyao magotini na sura zao zilikuwa zimenama na kuangalia chini. Kiti cha mbele kabisa kulikaa kiumbe kingine, hiki kilikuwa kikubwa zaidi ya hivi sita, hakikuwa na kichwa.

    Viumbe vyote vilionekana havina uhai,ngozi zao zilisinyaa kabisa vikaonekana kama vimepakwa vumbi.

    Sherhazad aliendelea kutembeza kichapo kikali kwa Amatagaimba ambaye alijitahidi kupigana kadiri ya uwezo wake. Sherhazad alionekana kuwa na nguvu sana ili kutimiza lengo lake. Amatagaimba aliona wazi kuwa wakileta mchezo hapo ndio mwisho wao kwani Sherhazad alikuwa anatumia mbinu kali za kichawi ambazo zilimfanya Amatagaimba kusahau kila kitu na kupumbazika.

    “Seidon, Seidon!” aliita kwa taabu, Seidon akamtazama Amatagaimba aliyekuwa akitambaa chini.

    “Muachie Anna, nenda kapachike hilo fuvu kwa kile kumbe kisicho na fuvu,” Amatagaimba alijitahidi kupiga kelele.



    Seidon alimtazama Anna akiwa bado ananing’inia na huku amemshika kwa mkono wake mmoja ambao ulikuwa unavuja jasho na ukitetemeka kuonesha kuwa umefikia mwisho wa kustahamili, macho ya Anna yalijaa machozi nay a Seidon yaliakisi hali ile.

    “Niache Seidon, niache uende, asante kwa yote,” Anna akafumba macho. Seidon hakuwa na lingine zaidi ya kumwachia Anna ili yeye amalize kazi iliyompasa kuifanya, hakupenda kumpoteza mwanadada huyo lakini ilimbidi.

    “Seidooooonnnn!!!!” Amatagaimba aliita, sauti ile ilimgutusha Seidon asliyekuwa akimtazama Anna kwa huzuni, akamwachia ili atumbukie kwenye ule mto wa ajabu. Seidon hakubaki mahala pale, alivuta hatu na kulimaliza lile daraja akaanza kupanda ngazi kuelekea juu ambako Klakos ilikuwapo. Mara ghafla upepo mkali ukaanza kuvuma na kumfanya Seidon kushindwa hata kunyanyua mguu wake. Ule upepo haukukoma uliendelea kumpa shida Seidon, nay eye hakukubali alijilaza chini na kupanda zile ngazi huku akitambaa kama nyoka.



    Wakati huo Amatagaimba alikuwa amesitisha mapambanao na Sharhazad ghafla baada ya kutoweka kwake, Sherhazad na Ujini wake lakini hakuwa na nguvu ya kupanda pale ilipo Klakos nah ii ilitokana na uovu mwingi uliomzunguka, hivyo alimwacha Amatagaimba na kuzunguka nyuma kisha kuanza kutengeneza upepo mkali kutoka katika kinywa chake kwa minajili ya kumpa kipingamizi, Seidon.

    Ilikuwa bado ngazi chache sana Seidon afike kwa viumbe vya kwanza vile ambavyop kimoja kipo kushoto kinaitwa Aminus na kile cha kulia kinaitwa Sagitarius. Bado viumbe vile vilikuwa vimetulia kimya hata havikutikisika; ni utando wa buibui tu uliokuwa umewazunguka hapa na pale.



    §§§§§



    Anna alipoanguka baada ya kuachiwa mkono na Seidon, alijigonga vibaya kwenye moja ya nguzo za lile daraja, ivyo mwelekeo wa mdondoko wake ukabadilika badala ya kwenda chini akasukumiwa kushoto na kudondokas jirani na jiwe kubwa lenye kung’aa sana, alifumbua macho aliyokuwa kayafumba muda wote huo na kujikuta kama umbali wa meta moja kutoka kwenye ule mto ambao maji yake mazito yalikuwa kama uji mzito wenye rangi mchanganyiko.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kizunguzungu kikamshika akajivuta pembeni na akulala kimya akipulizwa na ule upepo ambao hakujua hatima yake nini, maumivu makali yalikuwa katika eneo la mbavu zake ambapo alijgonga vibaya katika ile nguzo.



    §§§§§



    Amatagaimba akajibiringisha pale alipo na kujificha nyuma ya kitu kama ukuta mfupi, akachomoa uta wake mgongoni akautia mshale na kuuvuta kwa nguvu zake zote kuelekea kule ambako Cleopas alikuwa amekaa, alipouachia, ule mshale ukakata upepo kwa kasi na kuipita shingo ya Cleopas kwa nukta chache sana kambla haujapiga hewa na ule upepo ukakatika ghafla.



    Seidon akanyanyuka haraka na kupanda kazi iliyobaki akakanyaga eneo lile la Klakos, mara alimwona Sherhazad akiwa na mshale uliochoma kinywani mwake akija hewani kwa kasi na papo hapo, lile fuvu likamtoka mikononi. Vile viumbe sita bikawa kama vimepata uhai baada ya Seidon kukanyaga Klakos. Macho ya vile viumbe Aminus, Petrius, Segidus, Sagitarius, Hesmspitus na Sectogamus yakaanza kung’aa na vichwa vyao vikageuka kwa Seidon kisha vikageuka kwa ghafla kuelekea kwa Cleopas na ndipo lile fuvu lilipotoka mikononi mwa seidon na kwenda kunasa moja kwa moja kwenye shingo ya Cleopas.

    Viumbe sita vikainamisha vichwa vyao kama vinavyotoa heshima. Nukta hiyohiyo. Sherhazad alijikuta akipigwa na dharuba kali isiyoonekana, akapaisha juu na kujibamiza kwenye ukuta kisha akaanguka chini akihema, hakuweza hata kuvuta hatua.

    Vitu kama milipuko vikaanza kutokea kona mbalimbali za lile shimo au pango, vitu anuai vilivyotengenezwa kwa dhahabu safi vikaanza kung’aa na kupendezsesha mle ndani. Seidon aslipiga magoti, Amatagaimba palepale alipo naye alifanya hivyo. Mara Sherhazad kutoka pale alipo aliinuliwa juu na kitu kisichoonekana akashushwa mbele ya Klakos kwa kishindo, alipotua tu, vazi lake alilovaa likaanza kugandamana na ngozi yake.



    “Jostrutus, Jostrutus, loctus loctus, abilante sekretus …” yalikuwa maneno yaliyosikika kutoka kila kona lakini hakuna aliyeonekana kufungua kinywa chake. Sherhazad akatulia kimya sasa akiwa kiumbe wa ajabu kabisa, Seidon ambayew hakua mbali naye alikuwa akitetemeka kwa hofu.

    “Jostrutus, ulikuwa una nia gani na viumbe hawa?” Aminus na Sagitarius walimuuliza Sherhazad ambaye jina lake katika ulimwengu wao alijulikana kama Jostrutus.

    Hakujibu akabaki anathema, vile viumbe vikageuka kwa Cleopas ambaye sasa shingo yake ilikuwa ikinesanesa baada ya kupata uhai kwa lile fuvu.

    “Miaka 500 umekuwa ukisumbua viumbe hawa, umekuwa ukiwapumbaza wasijue nini maana ya Klakos, ulikuwa na nia gani?” Petrius na Hesmepitus nao wakauliza kwa pamoja. Siri kubwa ya viumbe hawa walikuwa wakitumia roho moja kila viumbe viuwili vilivyotazamana. Upepo ukaanza kuvuma tena lakini mara hii ulikuwa ni upepo mtulivu, wale vioumbe wakainama vichwa vyao kumwelekea Cleopas.



    “Cambialus Serpentus, Cmbialus Serpentus…” viumbe wale sita walianza kutamka kwa kurudia rudia maneno hayo.

    Macho ya Cleopas yakang’aa sana na kufanya kama mwali wa moto uliotua moja kwa moja mwilini mwa Sherhazad ambao wao walimtambua kama Jostrutus. Ukelele wa ajabu ukamtoka Sharhazad na mara mwili wake ukaanza kugeuka na kuwa chatu mkubwa wa kutisha, na rangi ya vasi lake ndiyo ikawa rangi ya ngozi yake.

    Seidon alihisi kuzimia lakini alijikaza akitetemeka, ule ukelele uliotoka katika joka lile sasa ulikuwa ukisikika hewani lakini haikujulikana ulitoka wapi, mara lile joka likatoka taratibu na kuingia katika ule mto wenye maji mazito, likaishia humo na yale maji yalionekana kama uji unaochemka kwa hasira. Mwisho wa Sherhazad ukawa ndani ya mto huo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    §§§§§



    “Mmetoka wapi?” sauti ilitoka kwa Cleopas na kufanya mwangwi mkubwa ndani ya pango lile.

    “Hamjui mlikotoka, lakini sisi tunajua mlikotoka, na kila mmoja atarudishwa salama kule alikotoka, lakini kila aliyefika mwisho wa mbio hana budi kupata zawadi,” ile sauti iliendelea. Mara vile viu,be vyote vikainama tena na mikono ta Cleopas ikatoka magotini na kuwekwa kifuani mwake.

    “Neema zote za ardhi na mbingu nakurudishieni kila mmoja na alikotoka, mvua zitanyesha, mito yenu itajaa maji, mazao na mashamba yenu vitarutubika na njaa itaondoka katika uso wa nchi, vita na matatizo vitakoma, lakini na alaaniwe kila aliyejaribu kuvuruga mpango wa kuirudishia Klakos uhai. Sisi ni viumbe tunaowapa uhai wa mimea na ninyi pia,” mwangwi wa ile sauti uliendelea na mara hii radi kali ilipasua anga kuashiria mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha huko duniani.

    Kisha Cleopas akaonesha ishara ya kuwaita pale juu wote watatu, Anna alihisi ghafla kutowekewa maumivu yake, akainuka na kufuatana pamoja na Amatagaimba na Seidon wakapiga magoti mbele ya Cleopas, katikati ya Klakosi.



    “Wewe ni shujaa wa Hamunaptra, na Msindikizaji wako pia, safari hii ya hatari imewagharimu na kuwapunguzia sehemu ya maisha yenu, Mnataka niwape nini?” Cleopas akauliza kwa sauti yake yenye mwangwi ambayo ilisikika pande zote lakini yeye mwenyewe hakuonekana kufungua kinywa.

    “Tunahitaji kurudi tulikotoka,” Seidon, Amatagaimba na Anna walijibu kwa pamoja.

    “Fumbeni macho, msiwaze lolote vichwani mwenu,” Cleopas akawaambia nao wakatii,

    Upepo Mwanana ulianza kuvuma, kila mmoja wao alijiona kama anapaa angani, hali ya utulivu ilitawala kwenye vichwa vyao.

    Hospitali ya Dar El Shefa – Cairo, Misri

    WAHUDUMU wa Hospitali walimshusha Anna Davis kutoka katika kitabda maalumu na kumlaza kwenye kitanda cha wosini, alikuwa hajitambui, fahamu zote zilimtoka kutikana na lile janga la kule kwenye mapiramidi. Wanafunzi wenzake walikuwa tayari wamekata tamaa ukizingatia mmoja wao alikuwa amepoteza maisha.



    “Ataamka muda wowote huyu!” sauti hio ilipenya kwa mbali sana ngoma za masikio ya Anna, hakuelewa nini kinatokea, akili yake ilikuwa ikirudi taratibu kutoka katika safari ya mbali, kutoka katika ulimwengu wa chini kabisa.

    Mara akakurupuka na kuanza kuhema kwa nguvu kama aliyekuwa anakimbizwa.

    “Ameamka, ameamka!” sauti ya muuguzi ilimshtua mawazo Anna.

    “Niko wapi hapa? Niko wapi? Amatagaimba, Seidon wako wapi? Wako wapi?” alikuwa akiongea kama mtu anayeweweseka.

    “Anna, Anna tulia Anna, unanifahamu mimi?”

    Anna akatulia kiasi na kumtazama mtu aliyekuwa mbele yake, “Ndiyo nakufahamu,” akajibu.

    “Mimi ni nani?” yule mtu akauliza.

    “Profesa Masati,” Akajibu, kisha akaanza kuwatazama mmoja baada ya mwingine, akamtambua na mwanafunzi mwingine aliyekuwa hapo.

    “Inaonekana alikuwa kwenye maono mazito sana katika mzimio wake, labda baadae tutamuuliza kwa tuo ili tujue nini alikiona,” Daktari bingwa wa magonjwa ya akili ambaye aliwaambia tangu mwanzo kuwa kutoka na vipimo, Ubongo wake umepata shida kidogo hivyo anweza kuamka akiwa hana kumbukumbu au nusu kichaa.



    Anna alilala kitandani, lakini mara alikuwa anacheka mwenyewe na mara alikuwa ananuna au kutajka majina ya vitu visivyoeleweka.

    “Akae hapa kwa wiki zaidi ili nimwangalie namna ya kumsaidia” yule daktari akamwambia Profesa Masati na wakakubaliana hilo.

    Jangwa la UajemiCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    JUA kali lilikuwa likiwaka, vumbi lilitimka kama limetumwa. Watu wawili waliokuwa juu ya ngamia walitazamana bila kuongea, lakini baadae mmoja alivunja ukimya.

    “Amatagaimba, Shujaa wa Msitu wa Solondo, Asante sana kwa kazi hii, Baraka za Klakos ziwe nawe,” Seidon akamwambia Amatagaimba.

    “Nawe pia, Mpiga mbio, Shujaa wa Hamunaptra, kama zilivyo mbali Mashariki na Magaribi nasi nafsi zetu hazitaonana tena,” Amatagaimba akashuka katika Ngamia na Seidon akafanya hivyo, wakakumbatiana na kuagana kisha kila mmoja akaenda upande wake.



    ˜ MWISHO ˜

0 comments:

Post a Comment

Blog