Search This Blog

TAFADHALI MAMA USIWAUE WATOTO WANGU - 2

 







    Simulizi : Tafadhali Mama Usiwaue Watoto Wangu

    Sehemu Ya Pili (2)



    Mzee Edward alinyoosha bastola yake lakini kabla hajafyatua alishtukia macho yake yakiingia giza, hakuwaona tena na aliamini walipotea kimazingara. Yeye mwenyewe alitetemeka hakutaka tena kubaki kisiwani Kome aliamua kurejea Mwanza mara moja!

    Lililomtokea lilikuwa jambo la kutisha sana, alikata tamaa ya kuwapata mke wake na mwanae.

    ******

    Ulikuwa ni usiku wa kutisha sana Anne hakuamini alichokuwa akikiona mahali pale, alikuwa bado hajaamini kama mtu aliyemwona alikuwa ni Dioniz! Kabla hajakaa vizuri alimwona mtu kama mwalimu Catherine akiwa na shoka mikononi akipasua kuni! Alipozungusha macho yake upande wa pili alimwona mwanamke mmoja na alipomwangalia vizuri aligundua alikuwa na mama yake na Dioniz.



    “Huyu mama naye kaja huku lini?” Alijiuliza Anne lakini hakupata jibu.



    Alikimbia kwenda mahali alipokuwa amesimama Dioniz na kumkumbatia wakaanguka nae hadi chini huku akimmwagia mabusu mfululizo.



    “Dioniz nakupenda!” Alisema Anne.



    “Anne usitumie maneno hayo hapa si mahali pake! Utaiudhi mizimu yetu”



    “Sawa mama lakini ninampenda Dioniz na kwanini ulimuua? Je hatuwezi kumrudisha tena duniani?”



    “Hiyo haiwezekani tena mwanangu mtu akishafika huku hawezi kurudi duniani tena, sisi pekee yetu ndio tunaweza kufanya hivyo!”



    “Lakini kwa ninavyompenda Dioniz mama ni heri na mimi nibaki hukuhuku niishi naye!”



    “Haiwezekani mwanangu anakoishi Dioniz wewe huwezi kukaa kabisa kuna mateso makubwa mno!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nitavumilia mama!”



    Muda mfupi baadaye Dioniz, mwalimu Lutambi na mwalimu Catherine pamoja na watu wengine ambao hakuwafahamu wakatolewa eneo lile na kuzungushwa nyuma ya mbuyu ambako bibi mmoja alipiga kelele akiomba ardhi ifunguke na wote walidumbukizwa ndani ya shimo lililotokea chini ya mbuyu na kupotelea ardhini Anne alimlilia Dioniz.



    Baada ya tukio hilo la kutisha mama yake alimpiga Anne usoni kwa unyoya wa Jogoo, mazingira yakabadilika wakawa wamerejea katika dunia ya kawaida ambayo Anne aliizoea! Anne aliwaona watu wakitembea kuelekea mahali yeye na mama yake walikokuwa wamesimama wakiwa uchi.



    “Mama wale watu watatuona!”



    “Wao hawaoni ila sisi ndio tunawaona!”



    “Kweli?”



    “Kama huamini tukikaribia tuwatishie kwa kuwachoma na miti machoni, kama wakishtuka basi wanaona lakini kama hawaoni basi hawatafumba wala kushtuka!”



    Ili kuhakikisha maneno ya mama yake, Anne alipowakaribia alinyanyua kipande cha mwiba na kuanza kuwatisha kama anawachoma machoni lakini watu wale hawakufumba macho wala kushtuka! Anne akaamini kuwa kweli walikuwa hawawaoni akacheka.



    Njiani waliendelea kupishana na watu lakini wote waliokutana nao hawakuwaona kwa macho, walipofika nyumbani mama yake aligeuka na kuugusa mlango kwa matako, mlango ukafunguka bila hata kuguswa na mtu! Wote wakaingia ndani na kujitupa kitandani.

    *****

    Asubuhi kulipokucha Anne alikuwa mwenye mawazo mengi sana juu ya tabia ya mama yake, ni usiku wa siku hiyo ndiyo aligundua kumbe mama yake alikuwa mchawi. Kilichomsumbua zaidi akilini Anne ni vipi Dioniz na mwalimu Catherine walitoka katika shimo la maji machafu ya chooni alikowadumbukiza na kwenda hadi kwao.



    Anne na mama yake waliendelea kwenda kwenye sherehe za kichawi kila siku usiku, akiwa katika matayarisho ya kurithishwa Kiti cha Umalkia mara bada ya mama yake kufariki. Hatimaye Anne alizoea na kukubali kuwa mchawi! Alifundishwa kitu na mama yake.

    ****

    Pamoja na waganga wote aliokwenda kwao kumweleza kuwa mtoto wake Dioniz alifariki dunia kichawi bado mzee Edward hakuamini na aliendelea kuwasisitiza polisi wamtafute mwanae na pia mke wake, aliamini Anne na mama yake walikuwa wachawi.



    Kitendo cha yeye kuona giza alipotaka kuwashambulia kwa risasi kijijini kwao ndicho kilimfanya aamini Anne na mama yake walikuwa wachawi lakini pamoja na hayo bado aliendelea kuwashinikiza polisi wamtafute Dioniz mpaka apatikane.



    Kwa shinikizo hilo msako wa polisi ulikuwa bado ukiendelea tena kwa nguvu kuliko mwanzo lakini Dio hakupatikana, mzee Edward na polisi na hata watu wengine walikata tamaa na kuendelea na maisha yao mambo yote wakimwachia Mungu.



    “Yaani mke wangu na mwanangu hawapo tena? Mungu anajua na yeye ndiye atanilipia!”

    ****

    Baadaye Anne alirejea shuleni kuendelea na masomo, shule nzima ilimtenga si wanafunzi tu bali hata walimu pia walimwogopa, hakuna mwalimu ayediriki kumchapa Anne hata kama alikosea kitu! Ni msichana mmoja tu katika shule hiyo aliyetokea kumzoea Anne na kuwa rafiki yake.



    Msichana huyo aliitwa Grace mwenyeji wa Morogoro, yeye na Anne walikuwa marafiki wakubwa sana, walisoma pamoja, walikula pamoja na pia kucheza pamoja, wanafunzi wengine katika Shule ya Ngaza walimshangaa Grace na kuna wakati walihisi labda yeye pia alikuwa mchawi.



    Kila siku iliyopita Grace alimshauri Anne juu ya kujiunga na UKWATA, Anne alitamani sana kuingia katika umoja huo kusali kitu ambacho hakuwa kukifanya katika maisha yake, lakini aliogopa vitisho alivyopewa na mama yake kuwa siku yoyote ambayo angeingia kanisani angekufa sababu mizimu yao ilizuia!



    Siku zote aliendelea kumkatalia Grace bila kumwambia sababu, kila siku iliyokwenda kwa Mungu aliendelea kuteseka na siri aliyokuwa nayo moyoni mwake, hakuwa na mtu wa kumwambia jambo lililomsumbua ingawa moyo wake siku zote ulitamani kufanya hivyo.

    “Ipo siku nitaenaweza kusema jambo hili kwa mtu yeyote!” aliwaza Anne.

    ****

    Juni 26 Mkutano Mkubwa wa UKWATA ulipangwa kufanyika katika shule ya sekondari ya Ngaza, Grace ndiye alikuwa muandaaji wa mkutano huo kwa sababu yeye ndiye alikuwa mwenyekiti wa UKWATA katika shule yao, shule zote za sekondari mjini Mwanza zilitegemewa kutuma wawakilishi kwenye mkutano huo.



    Kijana Huggins alikuwa miongoni mwa watu waliotegemewa kuhudhuria mkutano huo na na kutoa mahubiri kwa wanafunzi wenzake, hilo lilikuwa moja ya malengo ya Huggins lakini lengo la pili la Huggins lilikuwa ni kumtafuta Anne, msichana aliyetamani kumwona siku zote. Alitaka amwone ili amsadie matatizo yake.



    “Safari hii ni lazima nimwone tu!” Aliwaza Huggins.



    Kila siku Grace aliendelea kumshawishi Anne pia ahudhurie mkutano huo, maneno ya Grace na yalimwigia lakini bado aliogopa kuingia kanisani!



    “Tuna kijana mmoja aitwaye Huggins ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Nsumba, atakuwepo na atakuwa mahubiri maalum tafadhali njoo usikie habari zake!”



    “Huggins?”



    “Ndiyo kwani unamfahamu?”



    Kabla Anne hajajibu swali hilo kumbukumbu zake zilimrudisha moja kwa moja hadi kituo cha polisi, siku aliyomsonta Emmaculata kwa kidole akaanguka chini,ni Huggins aliyemnusuru baada ya kumwombea maombi maalam!



    Kwa siku nyingi sana Anne pia alitamani kukutana na kijana huyo aliposikia alikuwa anakuja hisia za kutaka kumwona zilianza kumwingia tena upya.



    “Kweli atakuja au unamwongelea Huggins mwingine?”



    “Hapana ni Huggins yuleyule mmoja si ni mrefu mwenye sura nzuri hivi?”



    “Sawasawa kabisa Grace!”



    “Basi atakuwa hapa 26!”



    Walipoachana siku hiyo Anne aliendelea kumfikiria Huggins, sura yake ilimchanganya akili, yeye na Dioniz hawakuwa na tofauti sana! Lakini alipofikiria kasoro aliyokuwa nayo mwilini mwake alisita kwani hakutaka kuua tena!



    “Akija nitaonana naye lakini siyo kanisani kwao!”

    ****

    Mkutano ulijaa idadi kubwa sana ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali zilizopo mjini Mwanza, ilikuwa ni furaha kupita kiasi, wanafunzi waliimba, wanafunzi walifanya maombi na mambo mengine mengi ya kufurahisha, Huggins alimtafuta Anne bila mafanikio yoyote, Anne alikuwa amejificha hakutaka kabisa kuwa karibu na mkutano ule, aliigopa mizimu yao, kila aliposikia nyimbo za mapambio zikiimbwa alijisikia kupandisha mashetani.



    Ndani ya roho ya Huggins aliendelea kusikia sauti ikimweleza amtafute Anne kwani alijisikia kumsaidia, ndipo alipofikia uamuzi wa kumtafuta Grace na kumuuliza.



    “Tena nilikuwa naongea naye jana tu ni rafiki yangu sana!”



    “Sasa nitafanye nini ili nimpate?”



    “Subiri baadaye kidogo tukimaliza mahubiri nitakwenda nikamwite sawa?”



    Muda wa mahubiri ulipowadia wanafunzi walitulia kumsikiliza Huggins akihubiri, Anne alikuwa umbali wa kama mita mia nne hivi kutoka mkutanoni akiwa ameinama chini ya mti na vitabu vyake, alikuwa akiusikia mwili wake ukiwaka moto!



    Anne alishindwa kuelewa kabisa moto ule uliomuunguza ulitoka wapi, aliungua kama alikuwa ndani ya pipa la maji ya moto! Alikimbia bafuni kujimwagia maji lakini maji ya bafuni hayakutosha na kujikuta akichomoka uchi kuelekea ziwani ambako alijitupa majini na kuanza kuogelea lakini bado maji ya ziwani hayakuupoza mwili wake!



    Watu walimwona akikimbia kuelekea ziwani akiwa uchi walimtaarifu mwalimu wa nidhamu ambaye alitoka akiongozana na walinzi pamoja na baadhi ya wanafunzi hadi ziwani ambako walimkuta Anne ndani ya maji akilia kwa maumivu.



    “Moto! Moto! Moto! Unaniunguza!” Alimwambia mwalimu.



    “Moto upo wapi?”



    “Mwilini mwangu mwalimu nisaidieeeeeeeeee!” Anne alipiga kelele kwa maumivu.



    Walimkamata na kumtoa majini na kuanza kuongozana naye kwenda bwenini mwalimu mmoja wa kike alitoa khanga aliyokuwa amejifunga na kumfunga Anne kiunoni, kabla hawajafika bwenini upepo ulielekea upande wao na sauti ya kipaza sauti ilisikika vizuri masikioni mwao.



    “BABA WA MBINGUNI SHUSHA MOTO! MOTO! MOTO! MOTO !MOTO WA MBINGUNI UMETEKETEZE SHETANI!” Ilikuwa ni sauti ya Huggins.



    Kadri moto ulivyozidi kutajwa katika kipaza sauti ndivyo Anne alivyozidi kujirusha huku na kule akidai moto ulimuunguza, walipoingia bwenini sauti iliacha kutaja neno moto na palepale Anne alitulia.



    Wakati bado wanajadiliana kitu cha kufanya Huggins alianza tena kupaza sauti yake akimwomba Mungu ashushe moto kumteketeza shetani, Anne alianza kupiga kelele tena.



    “Mh!”Mwalimu aliguna.



    “Mbona kila mhubiri anapotaja moto ndio Anne anadai kuungua?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hata mimi nashangaa!”



    Wakiwa bado wanatafakari hilo ghafla macho ya Anne yalianza kutoka nje na mapovu mengi pia yalitoka mdomoni watu wote waliogopa.



    “Jamani mimi nafikiri huyu msichana ana mapepo!”



    “Hata mimi!”



    Mwalimu, walinzi na wanafunzi waliokuwepo walikubaliana kumpeleka Anne moja kwa moja kwenye mkutano huo!



    “Hapana msinipeleke!”



    “Kwanini?”



    “Nitakufa kabisa!”



    “Huwezi kufa huko ndiko utapata msaada!”



    “Mama! Mama! Msinipeleke huko!” Alilia Anne



    Baadaye alichomoka nakuanza kukimbia kuelekea ziwani, walipomfuata hawakumuwahi walimkuta ameshaingia majini na alizidi kuogelea kuelekea kwenye maji yenye kina kirefu zaidi, wanafunzi walizidi kuogelea kumfuata majini, kabla hawajamfikia Anne alizama majini na alipoibuka hakuwa yeye bali nyoka mkubwa aina ya chatu mwenye vichwa viwili! Wanafunzi na waalimu walikimbia na kutoka majini! Taarifa zilipelekwa kwa Huggins naye alishuka hadi ziwani kila mtu aliamini lile lilikuwa ni pepo.



    Bila kuchelewa Huggins alishuka jukwaani na kuongozana na wanafunzi wengine hadi ziwani, mkononi alikuwa na Biblia yake, alipofika alishangaa kuona nyoka mkubwa majini!



    “Mh! Huyu alikuwa mtu?”



    “Ndiyo ni mwanafunzi mmoja anasoma hapahapa!”



    “Anaitwa nani?”



    “Anaitwa Anne!”



    Alilikumbuka jina lakini hakusema kitu na bila kuchelewa alianza kuteremka kuingia majini, watu wote walimshangaa, alizidi kumsogelea yule nyoka huku akiwa amenyanyua mikono yake juu!

    Nyoka alizidi kuvimba kama vile alitaka kumrukia Huggins amuume, watu wote waliokuwepo ziwani waliingiwa na hofu kubwa mioyoni mwao, walijua Huggins angeumwa na nyoka na kufa!



    “Toka katika jina la …..!” Aliamuru Huggins huku bado hakukutoka kitu. Na watu wote walikuwa kimya kusikiliza.



    “Nakuamuru katika jina la Yesu toka, mwachie kiumbe wa Mungu shetani wewe mwachie nenda nyikani na usirudi tena!” Alizidi kukemea Huggins.



    Ghafla katika hali ambayo haikutegemewa na wengi nyoka yule alizama majini na alipoibuka hakuwa nyoka tena bali Anne, akilia machozi, watu wote walipigwa na butwaa.



    “Ahsante baba kwa sababu umemweka mtumishi wako huru!” Huggins alisema akiwa amenyanyua mikono yake juu.



    “Nisaidie Huggins nimeteseka kiasi kikubwa!”



    “Siyo mimi ila ni yeye aishie ndani yangu atakusaidia, upo tayari kutubu?”



    “Ndiyo!”



    Hapohapo majini alimwangoza Anne Sala ya Toba, alipomaliza wote waliondoka kuelekea juu mahali kulipokuwa na mkutano awali ambako Anne alipandishwa jukwaani na kuanza kutoa ushuhuda juu ya mambo aliyowahi kuyafanya.



    “Mama yangu alinifanya mimi mchawi bila kutaka, nasikitika nilisababisha kifo cha mwalimu Lutambi, Dioniz na mwalimu Catherine!” Aliposema tu maneno hayo wanafunzi wa Nsumba waliomfahamu Dioniz walianza kulia machozi.



    “Haijalishi alifanya nini, Mungu amemweka huru na sasa yeye ni safi! Haleluya!!



    “Ameeni!” Watu wote waliitikia kwa sauti kuu!



    Kumbe katika watu waliokuwepo katika mkutano huo wapelelezi wawili walijichanganya, aliposhuka tu jukwaani Anne alifikia mikononi mwa polisi na kutiwa pingu mikono yote miwili.



    “Tuonyeshe mahali ulipozika miili ya watu uliowaua umetusumbua sana!”Askari mmoja alimshambulia Anne na kumzaba vibao.





    Minong’ono ilitawala kila mahali watu wakijadiliana juu ya kitu ambacho Anne alikisema jukwaani kama ushuhuda wa maisha yake yaliyopita! Watu hawakuamini kama kweli Anne na jinsi alivyokuwa mzuri alikuwa mchawi na ndiye aliyemuua Dio na mwalimu wao Catherine.



    Mkutano haukuendelea tena palepale ulivunjika na Anne huku akifuatwa na kundi kubwa la watu aliongozwa na maaskari kupelekwa kituo cha polisi ambako ilibidi aandikishe maelezo yake juu ya nguvu aliyokuwa nayo ndani ya mwili wake iliyomwezesha kuwaua Dioniz na watu wengine akiwemo mwalimu Lutambi na Catherine!



    Kwa kila mtu aliyesikia tukio hilo na mpaka walimu wa shule ya Ngaza, ilikuwa si rahisi kuamini kuwa msichana mdogo na mwenye sura ya kuvutia kama Anne alikuwa na nguvu ya kichawi na za hatari kiasi kile, hata askari wa kike WP Jacqulline aliyekuwa akichukua maelezo ya Anne alitetemeka.



    “Bila msaada wa maombi ya leo mimi ndiye nilikuwa nimetayarishwa kuwa mrithi wa mama yangu katika uchawi!”



    ‘Mrithi wa nani?”



    “Ni habari ndefu sana ila fahamu tu kuwa kuna mzimu uitwao Lutego, upo katika ukoo wetu ni huu ambao hutumika kutulinda sisi watu na ukoo wote wa mzee Kamanzi! Mzimu huu hukaa ndani ya mwanamke mmoja katika ukoo!”



    “Kwa hivi sasa anao nani?”



    “Anao mama yangu na baada ya kufa yeye mzimu huo ungeniingia mimi na tangu siku hiyo ningekuwa na uwezo mkubwa mno kichawi na ni mimi ndiye ningekuwa malkia wa wachawi kanda ya ziwa!”



    Maelezo hayo ya Anne yalizidi kumtisha WP Jacqulline na maaskari wengine na kuwafanya wawe na wasiwasi zaidi, kwa hofu hiyo hakuna hata askari mmoja aliyethubutu kumpiga Anne, askari aliyemzaba kibao baada ya kumtia pingu kwenye mkutano aliingiwa na wasiwasi mkubwa maisha yake, ikabidi amfuate Anne kumwomba msamaha.



    “Nisamehe sana dada yangu!” Alisema baada ya kupiga magoti chini.



    “Usiwe na wasiwasi Afande hayo ni ya zamani, hivi sasa mimi ni kiumbe kipya kabisa! Sina tena mambo hayo nimeokolewa na kuwa huru!” Alijibu Anne.

    ****

    Baada ya maelezo hayo Anne alichukuliwa na maaskari na kupelekwa kwenye chumba cha mkuu wa kituo ambako pia alitoa maelezo yaliyomtisha sana mkuu huyo, bila kuchelewa alitoa idadi ya maaskari wapatao sita na gari la kunyonya maji machafu kwenda kuona kama kweli miili ile ilikuwa ndani ya shimo alilodai Anne au la!



    “Binti kweli una hakika miili hiyo ipo ndani ya shimo manaake usitupotezee muda wetu bure!”



    “Afande hauamini basi twende ukaone!”Anne alisema kwa ujasiri ingawa moyoni mwake alishindwa kuwa na uhakika zaidi kama kweli miili wangeikuta ndani ya shimo la maji machafu au la! Kitendo cha kuwaona akina Dioniz na mwalimu Catherine kisiwani Kome katika moja ya sherehe zao za kichawi zilizofanyika usiku kilimfanya akose uhakika!



    “Sina uhakika lakini acha twende tukaone, kama haipo sijui nitawaeleza nini!” Aliwaza Anne.

    ****

    Habari juu ya tukio la mwanafunzi na kukiri kuua watu kichawi na kutumbukiza maiti zao katika shimo la maji machafu zilivuma sana katika maeneo yote ya kuzunguka shule ya Ngaza na hatimaye yalifika shule ya sekondari ya Nsumba, wanafunzi walipopata taarifa kuwa gari la polisi lilikuwa likinyonya maji katika shimo hilo ili kuzitoa hizo wengi walimiminika shuleni hapo kushuhudia tukio hilo la ajabu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pamoja na kuwepo na watu wengine idadi kubwa ya watu waliokuwepo walikuwa ni wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nsumba, waliokuwa wakilia machozi kumlilia Dioniz rafiki yao mpendwa.



    Gari la majitaka lililomilikiwa na jeshi la polisi liliendelea kunyonya maji yote yaliyokuwemo ndani ya shimo hilo ili kuona kama kweli miili ya Dioniz na mwalimu Catherine ilikuwemo ndani ya shimo hilo kama alivyodai Anne.



    Watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali ya habari walikuwepo kushuhudia tukio hilo, walimpiga Anne picha nyingi zisizo na idadi na alijua wazi kuwa magazeti ya siku iliyofuata yangejaa picha na habari zake kwa kichwa cha habari ambacho wangetaka wenyewe.



    Anne hakuona aibu wala kujuta moyoni mwake kuitwa mchawi! Hiyo ni kwa sababu hakuwa hivyo tena hayo yote kwake yalikuwa mapito, hiyo ilikuwa historia yeye wakati huo alijisikia ni mtu mpya na mwenye mtazamo wa kimungu zaidi kuliko dunia.



    Wanafunzi wa Nsumba wenye hasira walimkuta Huggins akiwa pale na aliwasimulia kila kilichotokea na kuwaomba wawe wavumilivu mpaka mwisho wa tukio hilo, alihofia wangeweza kufanya jambo lolote kwa hasira ya kumpoteza Dioniz.



    Maneno ya Huggins hayakusaidia lolote kwani badala ya wanafunzi kuwa wavumilivu waliendelea kumshambulia Anne kwa maneno makali huku wengine wakimmwagia mchanga machoni na kumwita mchawi, wanafunzi wa Ngaza pamoja na polisi walijaribu kuzuia lakini haikuwezekana.



    “Tuue wote basi, ulimuua Dio unashindwa nini kutumaliza na sisi kabisa?”



    Anne alizidi kulia machozi, Huggins alimhurumia na akamsogelea na kuanza kumfuta machozi yake machoni.



    “Jamani! Jamani! Jamani!” Huggins alipiga kelele Huggins akiwaomba wanafunzi wenzake wamsikilize na kweli walitulia ili kusikia alichotaka kusema.



    Pamoja na Huggins kuwa kiongozi wa UKWATA katika shule ya Nsumba pia alikuwa kiranja mkuu hivyo wanafunzi walimheshimu sana.



    “Wanafunzi wenzangu nawaombeni sana tafadhali msimsumbue Anne kwani hana makosa, yaliyotokea yote si kwa mapenzi yake, tafadhali msimwagie mchanga wala kumwita mchawi, kwa taarifa yenu ndugu zangu hivi sasa Anne ni mpendwa mwenzetu amekwishaamua kumpokea kristo na kufanya ngome yake yaliyotokea nyuma katika maisha yake hayajalishi tena, hebu tushangilie!” Alisema Huggins lakini idadi ya watu walishangilia haikuwa kubwa sana wengi walionekana kutaka kuendelea kummwagia mchanga na kumpiga Anne.



    Muda wote Anne alikuwa akilia machozi, alizidi kumlaumu mama yake kwa alichomfanyia, alijilaumu kuzaliwa katika ukoo wa wachawi, katika maisha yake hakutaka kuua lakini tayari alishafanya hivyo bila mapenzi yake mwenyewe!



    “Kwa kweli simpendi mama ila nimemsamehe kwa sababu hivi sasa nimeokoka!” Aliwaza Anne.



    Wakati hayo yote yakiendelea mpira mkubwa wa gari la maji taka ulikuwa ndani ya shimo ukiendelea kunyonya maji machafu, watu wote walikaa kusubiri maji yaishe ili waone kama kweli maiti zilikuwepo chini.



    Dakika ishirini na tano baadaye kazi hiyo ilimalizika na wafanyakazi wawili wa gari hilo walichungulia ndani ya shimo kukagua, macho yao yalipambana na tope zito, hawakuona kitu chochote kile!



    Baada ya majadiliano na uongozi wa shule uamuzi ulifikiwa kuwa shimo hilo libomolewe ili maaskari waingie ndani kuangalia vizuri ndani ya tope ili kuona kama kweli kulikuwa na kitu chochote kimejificha humo.



    Ilikuwa ni lazima waangalie ndani ili kujua kama kweli yaliyosemwa na Anne yalikuwa kweli au la, Anne alikuwa pale na pingu zake mikononi akishuhudia choo kikipigwa nyundo na kubomolewa, ilipomalizika kazi hiyo maaskari wawili waliovaa mavazi maalum waliingia ndani ya shimo na kwa kutumia chepeo walianza kulichambua tope lililokuwepo chini wakiangalia.



    Ghafla chepeo la mmoja wao liligonga kwenye kitu kigumu kilichokuwa ndani ya matope, alipokibinua kilikuwa ni kipande kikubwa cha mgomba, kilichofungwa khanga na alipoivuta khanga aligundua ilifungwa kwenye jiwe kubwa lililokuwepo pembeni.



    Muda mfupi baadaye askari huyo huyo alipambana na kipande kingine cha mgomba kilichofungwa kwenye jiwe, alizidi kushangaa!

    Walipomaliza kazi hiyo hapakuwa na kitu kingine zaidi ya mgomba ndani ya tope hilo, Maaskari wote walishangaa na kuitoa migomba ile nje!



    ‘Tumekutana na migomba hii tu hakuna kitu kingine chochote ndani ya shimo hili!”



    “Kweli?”



    “Ndiyo!”



    “Binti uliwatupa wapi mbona hatuwaoni?”



    “Niliwadumbukiza humo humo ndani ya shimo! Sijui maiti zao zimepotelea wapi ila hiyo nguo ilikuwa ya mwalimu Catherine!”



    Waalimu na wanafunzi wote waliokuwepo pale waliitambua nguo ile, ilikuwa ya mwalimu Catherine na alipenda sana kuivaa baada ya saa za kazi.



    Maaskari walizidi kuchanganyikiwa lakini watu wa kanda ya ziwa waliokuwepo eneo lile walielewa migomba ile ilimaanisha kitu gani kuwepo ndani ya shimo hilo, miili yote ya watu waliochukuliwa msukule ilibadilika kuwa migomba.

    ****

    Pamoja na kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha kuwa kweli Anne aliwaua Dioniz, mwalimu Lutambia na mwalimu Catherine, tendo pekee la kukiri mauaji kilitosha kabisa kumfanya awekwe mahabusu! Huggins alijitahidi kuwaomba askari wasifanye hivyo lakini haikuwezekana kuwazuia walidai hata kama alitubu kwenye mkutano wa dini kisheria alikuwa bado ana kesi ya kujibu na kama ingethibitika alifanya mauaji hayo angehukumiwa kifungo cha maisha.



    “Jamani si mmwachie tu kwa sababu ametubu!”



    “Hapana hiyo haiwezekani hata kidogo ni lazima akae mahabusu mpaka upelelezi ukamilike!”



    Huggins badala ya kufurahia alilia machozi, wanafunzi wenzake walishangaa kuona akimtetea Anne mtu aliyemuua Dio rafiki yao kipenzi.



    “Ebwanae na wewe usilete ulokole wako hapa hebu twende zetu shule upesi si umwache akafie lupango, wewe inakuuma nini? Mbona Dio alikufa” Alifoka kijana mmoja.



    “Hapana jamani, Anne amekwishatubu hayo ina maana amekwishasamehewa mbinguni na duniani!”



    “Mbinguni na wapi?”



    “Duniani!”



    “Mbinguni sawa lakini duniani, anajidanganya ni lazima akanyee ndoo tu!” alijibu mwanafunzi mwingine.

    ****

    Mkutano wa wanachama wa Lutego ulikuwa umekutana kwa dharura kuliongelea suala la Anne kukiri kuua watu kichawi na kuokoka, jambo ambalo hakutakiwa kabisa kulifanya hata kama angekuwa amewekewa kisu shingoni, hilo lilikuwa mwiko kwa wanachama wote wa chama hicho! Kuamua kwake kumpokea Yesu Kristo lilikuwa kero kubwa sana kwa mama yake na wanachama wenzake ambao hatimaye walidhamiria kunywa damu yake kupunguza hasira zao!



    Uamuzi huo kwa maana nyingine ulimaanisha kifo cha Anne, ilikuwa ni lazima afe na damu yake inywewe na wanachama.



    “Mtoto huyu kanikosea sana na nitaamuru watu wanywe damu yake sasa hivi kwanini kaenda kuniadhirisha kiasi hicho?” Aliwaza mama yake Anne.



    Kikao kizima kilikuwa kimya watu wote wakifikiria ni nani angemrithi malkia kama mtu aliyetegemewa kufanya hivyo alikuwa ameamua kukiasi chama chao na kujiunga na Ukristo!



    “Ni lazima Anne afe!” Alipiga kelele mama yake na vibibi vizee vyote viligeuka kumwangalia kwa mshtuko mkubwa! Ilikuwa ni mara ya kwanza kumwona mama yake Anne akiwa katika hali hiyo hawakujua nini kingempata Anne huko alikokuwa.



    “Nileteeni damu ya mtoto mchanga hapa upesi!” Haikuchukua hata sekunde mbili damu ikaletwa katika kikombe cheupe.



    “Haya nileteeni kipande cha kamba aliyojinyongea mwanamke!” haikuchukua muda mrefu kamba hiyo ikaletwa!



    “Naomba mniletee kipande cha sanda ya zeruzeru pamoja na mchanga kutoka kwenye kaburi la mwendawazimu!”



    Vitu vyote hivyo alikabidhiwa, alichukua sanda, kamba na kuvichoma moto na majivu yake aliyamwaga katika kikombe cha damu ya mtoto na vyote kwa pamoja alivinywa.



    Aliposhusha kikombe mwili wake ulikuwa ukifuka moshi jambo kuwa alikuwa na hasira kubwa sana.



    “Nisikilizeni kwa makini leo nimekasirika kupita kiasi na nafikiri nimesikia mambo ambayo Anne ameyafanya huko shuleni kwao, ametusaliti vibaya mno hivyo nimeamua afe hukohuko mahabusu aliko na ninakwenda mwenyewe ninafikiri hatanisumbua, hivyo nitarudi sasa hivi nisubirini”



    Baada ya kusema hayo kiti alichokalia kilibaki tupu akawa amepotea ghafla katika kimbunga kilichotokea.

    ****

    Mpaka saa tisa hivi usiku Huggins alikuwa hajapata usingizi, mawazo yake yalikuwa kwa Anne aliyekuwa mahabusu akiteseka, alijishangaa ni kwanini alikuwa amevutiwa kiasi hicho na msichana huyo, kwa mara ya kwanza katika kipindi kirefu alihisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikitokea ndani ya moyo wake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Huggins alihisi kumpenda Anne, alimhurumia kwa mateso aliyokuwa akiyapata ingawa tayari alishaokoka na kubadilishwa! Usiku huo alikuwa katikati ya maombi akimwomba Mungu amlinde Anne huko mahabusu alikokuwa.



    Anne naye mpaka muda huohuo alikuwa akifanya maombi ya toba, alikuwa akitubu dhambi za kuua alizofanya na kumwomba Mungu amtie nguvu zaidi ili aweze kupambana na mzimu wa Lutego ambao alijua kwa vyovyote ungetumwa kwake.



    Ghafla akiwa katikati ya maombi hayo alishtukia anasikia kishindo kikubwa sana nje ya mahabusu, wafungwa wote walikuwa wamelala usingizi katika sakafu iliyolowa maji na mikojo! Ni yeye tu aliyesikia.



    Baada ya hapo aliendelea kusikia vishindo vikiendelea nje ya mahabusu, Anne alijua ni nini kilikuwa kikitokea nje, alijua huyo alikuwa mama yake na yeye alizidisha maombi akimwomba Mungu ampe ulinzi zaidi, alijua wazi bila ulinzi wa Mungu siku hiyo ndiyo ingekuwa mwisho wake.



    Ghafla alianza kusikia sauti ya bundi wengi wakilia nje na sauti ya mtu akiita jina lake ilisikika pia, sauti hiyo ilikuwa ya mama yake alijua alikuwa amekuja kumdhuru kwa sababu ya msimamo wake, Anne alizidi kumwomba Mungu amsaidie katika janga lililokuwa mbele yake.



    Baadaye sauti za bundi zilitulia lakini vishindo viliendelea kuwepo mpaka mwanga wa jua ulianza kutokea kwenye kidirisha kidogo kilichokuwa juu ya mahabusu, ilionyesha kuwa tayari kulikuwa kumekucha.



    Majira aliyoyakadiria kuwa saa kumi na mbili na nusu hivi alisikia sauti za watu wakipiga kelele nje ya mahabusu.



    “Jamani mwanga! Mwanga! Mwanga! Huyu hapa mwanga! Amekuja kuloga kituo cha polisi!” Anne aliisikia sauti hiyo na kujua kilichotokea, mama yake alikuwa ameshikwa wanga kituoni.



    Kelele ziliendelea na alianza kusikia kilio cha mama yake na watu wakimpiga, muda mfupi baadaye katika hali ambayo hakuitegemea Anne alishtukia mlango wa mahabusu ukifunguliwa na mama yake akitupwa ndani, alikuwa uchi wa mnyama akiwa amevalia mavazi ya kutisha ya kichawi Anne alipiga kelele kuomba msaada!



    “Kuniingiza humu wamenirahisishia kazi!” mama yake alitamka huku akicheka.





    “Ndiyo ni mama yangu lakini there is nothing I can do to help”(Hakuna ninachoweza kufanya kusaidia!) Alitamka Anne huku akitupa mikono yake huku na kule kwa hasira, alionyesha ni kiasi gani alimchukia mama yake, shetani alimwingia na kujikuta akilia machozi kwa hasira, madereva walishangaa.



    “Kwanini mmemleta hapa lakini?” Anne alimfokea dereva teksi.



    “Amesema yeye ni mama yako na kwa sababu ni mgonjwa tukashindwa kumwacha ukizingatia sisi tunakufahamu!”



    “Asanteni sana ndugu zangu lakini ninasikitika mimi siwezi kumpokea huyu mama!”



    “Lakini ni mama yako kweli?”



    “Ndiyo lakini……!”



    “Lakini dada hata kama alikukosea huyu ni mama yako tafadhali tunakuomba umpokee!”



    “Nasema haiwezekani!” Anne aliongea akiwa ametoa macho kumwangalia dereva.



    “Kwanini?”



    “Mimi ninajua kwanini sitaki kumpokea nyinyi hamuwezi kuelewa ni bora mniache niendelee na uamuzi wangu!”



    Mama yake Anne, Isabella alikuwa ndani ya gari hajiwezi mwili wake ukiwa umevimba kwa sababu ya kupigwa, ingawa hakueleza ni kwa sababu gani sungusungu walimpiga Anne alijua ilikuwa ni sababu ya uchawi wake na ni hilo hilo ndilo lililomfanya asiwasiliane na mama yake kwa miaka karibu kumi.



    “Sasa dada tutafanya nini na huyu mama yako?”



    “Kwa kweli mimi sijui labda mmrudishe mlipomchukua!” Alisema Anne bila huruma, ni kweli alikuwa mama yake lakini alimuogopa.



    “Na pesa yetu atatulipa nani?”



    “Kama ni pesa nitawalipa lakini sipo tayari hata kidogo kumpokea!”



    “Basi tulipe hizo pesa zetu sisi tuondoke!”



    “Nisubirini!” Alisema Anne na kuondoka kuingia ndani na aliporudi alikuwa na noti ya shilingi mia tano mkononi mwake na kumkabidhi dereva.



    Cha kushangaza baada ya dereva kuipokea pesa hiyo alifungua mlango na kuanza kumshusha mama yake Anne kutoka ndani ya gari, alipomfikisha chini alimuamuru kijana aliyekuwa naye aingie ndani ya gari na walianza kuondoka kwa kasi.



    “Mama yako huyo hapo chini bwana, hatuwezi kuzunguka nae tuache kufanya biashara utajua mwenyewe la kufanya naye ili mradi amekwishafika kwako!” Alisema dereva wakati gari lake likiondoka.



    Anne alimwangalia mama yake na roho ikamuuma kupita kiasi kweli Isabella alikuwa mama yake kabisa, lakini mambo ambayo mama yake alimfanyia katika maisha yake hakuyafurahia hata kidogo kwa sababu hiyo hakuwa tayari kumkaribisha ndani.



    Alijua kufanya hivyo lingekuwa kosa kubwa kwani ni lazima mama yake angesababisha madhara makubwa sana kwa familia yake hasa kwa watoto wake wakiwemo mapacha Patrick na Nancy waliokuwa na umri wa mwaka mmoja tu wakati huo.



    “Nisaidie mwanangu!” Isabella alilia akimwangalia mwanae Anne usoni, alishangaa kuona mtoto wake hakuwa na huruma kiasi kile lakini kwa aliyomtendea hakuhitaji kumlaumu.



    “Mama siwezi kukusaidia sababu tabia na mwenendo wako ni mbaya sana! Hebu nieleze kwanini umechapwa kiasi hiki?”



    “Wanadai mimi mchawi!”



    “Wanadai?”



    “Ndiyo!”



    “Yaani hata mimi unaniambia hivyo wakati kila kitu nakielewa cha muhimu mama uache tabia hiyo! Si unaona matatizo yake?”



    “Nimekwishaacha mwanangu na ninaomba tu unipokee nyumbani kwako unitibu mpaka nipone!”



    “Hapana mama siwezi kufanya hivyo mume wangu hatakubali hata kidogo kwani anaifaha....!” Kabla hajamaliza sentensi yake Anne alisikia mlio wa gari ikitokea upande wake wa kulia alipogeuka lilikuwa gari la Huggins! Alishangaa ni kwanini mume wake alirudi nyumbani muda huo kitu ambacho hakikuwa kawaida yake.



    “Vipi honey mbona umerudi saa hizi tena?”



    “Nimepigiwa simu kuwa hapa nyumbani kuna mgeni tena ni mgonjwa na umekataa kumpokea!” Alijibu Huggins baada ya kuteremka kwenye gari.



    “Ndiyo ni huyu mama yangu! Sitaki kabisa aingie ndani kwetu!”

    Huggins aliinama na kumwangalia mama mkwe wake aliyekuwa amelala chini huruma ilimshika moyoni mwake, alijua kilichomfanya mke wake asikubali mama yake aingie ndani!

    Aliuogopa uchawi wa mama yake lakini yeye Huggins hakuwa na hofu kwani alijua ile ilikuwa ndiyo nafasi nzuri ya kumbadilisha mama yake na Anne na kumfanya aachane na matumizi ya nguzu za giza!



    “Anne mruhusu tu mama aingine ndani tafadhali nakuomba!”



    “Haiwezekani! Sitaki! Sitaki Huggins, mimi namfahamu mama!”



    “Mwache mama Anne! Yasahau ya zamani wewe sasa unaifahamu nuru lazima uwe tayari kutoa msamaha!” Alisema

    Huggins lakini badala ya Anne kukubali alianza kulia machozi.



    Huggins aliendelea kumbembeleza mke wake mpaka akakubali na wote wawili walisaidiana kumbeba Isabella na kumwingiza ndani ya nyumba yao na dakika chache baadaye Huggins alitoka na kwenda kumtafuta daktari aliyekuja nyumbani na kuanza kumpa Isabella matibabu.



    Baada ya huduma hiyo Huggins aliondoka kurejea kazini kwake na kumwacha mke wake akimhudumia mama mkwe wake kwa chakula, Anne aliyafanya yote hayo akiwa na hofu kubwa, watoto wake wakubwa Frank na William walimuuliza maswali mengi wakitaka kujua Isabella alikuwa nani.



    “Ni bibi yenu ndiye mama yangu mzazi!”



    Watoto wake walifurahi sana kumwona bibi mzaa mama yao.

    ******

    Ilimchukua Isabella miezi miwili mpaka kurejea katika hali yake ya kawaida na katika muda huo wote Huggins na Anne waliendelea kumpasha mama yaojuu ya Mungu ili ageuke na kuyaacha mambo yake mabaya! Kwa juujuu Isabella aliwakubalia lakini ndani ya moyo wake roho ya uchawi iliendelea kumtawala na pamoja na wema wote aliofanyiwa mpango wake wa kumuua mwanae bado uliendelea.

    ******

    Baada ya Huggins na Anne kuwa wamekaa na mama yao kwa miezi sita bila matatizo, akiwa amewahakikishia kuwa tabia ya uchawi aliiacha, wote walimkubali na kuyasahau ya zamani.



    Anne alimsamehe kabisa mama yake ikawa ni familia yenye furaha tena,mama aliishi kwa raha na alikuwa kipenzi kikubwa cha wajukuu zake, ilikuwa si rahisi kuamini Isabella aliwahi kuwa mshirikina.



    Kasoro pekee aliyokuwa nayo mama yao ni kutokwenda kanisani! Hakuweza kwenda kanisani kwa sababu siku aliyojaribu kufanya hivyo alipoukaribia mlango wa kanisa alianguka chini akageuza macho na kuanza kutoa mapovu mdomoni.



    Kwa siku tano mfululizo Isabella alikuwa kama mwendawazimu akiongea peke yake na kuokota makopo, alitulia baada ya kufanyiwa maombi na wachungaji lakini tangu siku hiyo hakuthubutu kuingia tena kanisani, si kanisani tu bali hata nyumbani hakushiriki ibada yoyote kila mahali lilipotajwa jina la Mungu yeye hakuthubutu kusimama, kila mtu aliamini Isabella bado alikuwa na mapepo.



    Huggins na Anne pamoja na watoto wao walimwamini Isabella lakini kumbe hakufaa kuaminiwa, kwani roho yake bado ilijaa uchawi na nia ya kuua! Isabella alichukizwa sana na kitendo cha mwanae aliyetegemewa kuwa mrithi wake wa mzimu wa Lutego kujiunga na Ukristo kitu ambacho hakutakiwa kukifanya.



    Hapakuwa na mtu mwingine wa kuurithi mzimu wake isipokuwa Anne peke yake na kila siku iliyokwenda kwa Mungu Isabella alitamani sana Anne aanguke na kurejea katika imani yao lakini haikuwa hivyo.



    Hatimaye siku moja baada ya Isabella kuwa amevumilia sana alifikia uamuzi wa kumwita mwanae kwa maongezi siku hiyo Huggins hakuwepo nyumbani.



    “Anne nimejaribu sana kuvumilia lakini nimeshindwa na ninaomba niseme wazi nia yangu ya kuja hapa ilikuwa kukuua lakini nilipofika hapa kwa msaada ulionipa niliamua kughairi!”



    Moyo wa Anne ulilipuka na kujikuta akikubwa na hofu kubwa,

    lakini alijikaza hakutaka kuonyesha udhaifu wa wazi.



    “Asante mama!”



    “Sipendi hata kidogo kukua mwanangu, lakini wanachama wa Lutego wote walichukizwa sana na kitendo chako cha kuingia katika Ukristo na wote wanahitaji kunywa damu yako, siku zote nimejaribu kujitahidi sana kukutetea lakini siku zote imeshindikana, juzi nilipoongea nao walisema ili wakuache hai ni lazima uache dini yako na urejee na kuwa malkia nitakapokufa!”



    “Mama kumbe bado unahudhuria sherehe zenu usiku?” Anne aliuliza kwa mshangao hakuamini kabisa kama mama yake katika siku zote alizokaa nao alikuwa akitoka usiku na kwenda kwenye vikao vya wachawi!



    “Hilo usijali kitu cha muhimu wewe eleza unakubali kuacha dini yako au hapana!”



    “Mama hiyo haiwezekani tena!”



    “Kweli? Shauri yako yatakupata makubwa!”



    “Mama lolote na liwe!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Maongezi yao hayakuendelea tena, yaliishia hapo hapo Isabella alionyesha hasira kali.



    Jioni ya siku hiyo Huggins aliporejea kutoka kazini kwake hakuwa mtu mwenye furaha kama siku zilizotangulia, alionekana mnyonge na mwenye mawazo mengi, kwa sababu hiyo Anne alishindwa hata kumweleza kilichotokea siku hiyo nyumbani kati yake na mama yake na alipomchunguza mume wake vizuri usoni aligundua Huggins alikuwa akilia! Anne alishtuka na kumsogelea.



    “Vipi tena baba?”



    “Nina matatizo makubwa sana mke wangu!”



    “Matatizo gani tena?”



    “Nimepunguzwa kazi ofisini!”



    “Umepunguzwa kazini kwa sababu gani?”



    “Hata mimi sijui ila wafanyakazi kama kumi hivi tumepewa barua za kupunguzwa kazi na tutalipwa mafao yetu baadaye!”



    “Mh! Unasema kweli au unatania baba Patrick!”



    “Kweli ndiyo maana unaona nina hali hii nashidwa kuelewa maisha yetu yatakuwaje!” Alisema Huggins na kuendelea kulia huku mkewe akimbembeleza na kumpa moyo!



    “Usilie darling hayo ni majaribu tu, si ajabu Mungu amekutayarishia sehemu nyingine nzuri zaidi!”



    “Kweli?” Aliuliza kwa mshangao Huggins ilikuwa si rahisi hata kidogo kuyaamini maneno ya mkewe kwani kutokea kwa jambo hilo kulimaanisha mwisho wa kila kitu!Mwisho wa raha zote na mwisho wa furaha iliyokuwa katika maisha yao.

    *****

    Wakati Huggins anasimamishwa kazi ulikuwa ni mwezi wa kumi na mbili katikati na hayo yaliyotokea yalikuwa ni jaribu makubwa katika maisha yao, yalihitaji mtu imara kusimama.



    Huggins akawa haendi tena kazini akawa mtu wa kushinda nyumbani na familia yake na usiku ulipoingia alilala, hiyo ndiyo ikawa ratiba yake ya kila siku kwa mtu aliyezoea kazi yalikuwa ni mateso makubwa! Watoto wake walimsumbua sana wakimuuliza maswali ni kwanini alikuwa haendi kazini tena, hakuwa na jibu la kuwapa ila maswali hayo yaliuumiza moyo wake sana.

    ******

    Shule zilipofunguliwa Huggins hakuwa na pesa ya ada ya watoto wake kwani mafao yao hayakuwa tayari! Watoto walimsumbua kwa maswali wakitaka kujua ni kwanini walikuwa hawaendi shule wakati wenzao walikuwa wakisoma!



    Watoto hakuwakujua tatizo lilikuwa ni ada, Huggins hakuwa na akiba yoyote, akaunti yake haikuwa na pesa, pesa yote aliitumia kununulia shamba sehemu za Nyegezi mwezi mmoja kabla ya kupunguzwa kazi! Alishindwa kuelewa angepata wapi pesa za kulipa ada ya watoto wake.



    Ni usumbufu wa maswali ya watoto wake yaliyomfanya asiwe anashinda nyumbani na kurudi usiku watoto wakiwa wamelala ni mke wake aliyempa ushauri wa kuuza gari lao ili wapate pesa za kulipa ada ya watoto ! Huggins hakuwa mbishi mbele ya mke wake ilibidi aliuze gari lao na pesa iliyopatikana aliwalipia watoto wake ada katika shule ya kimataifa, waliyokuwa wakisoma na sehemu nyingine alilipa pango la nyumba yao lililokuwa limekwisha.



    Watoto walianza kwenda shule lakini bado waliendelea kumsumbua baba yao na maswali zaidi, kila jumapili walimuuliza gari lilikuwa wapi waende kanisani kuna wakati walikataa kwenda kanisani kwa kutumia daladala wakitaka gari la baba roho ya Huggins ilizidi kuuma zaidi, alitamani yaliyokuwa yakitokea yawe ndoto lakini uliendelea kubaki ukweli.



    Watu wengi kanisani waliyaelewa matatizo yake na walimpa pole wakifikiri ingesaidia lakini ndiyo alizidi kumfanya achanganyikiwe zaidi mwisho alianza kuona aibu mbele ya waumini wenzake taratibu akaanza kupunguza safari zake za kwenda kanisani mke wake peke yake na watoto wakawa wanahudhuria misa kila Jumapili, Anne alimshauri Huggins arejee kanisani lakini haikuwezekana.



    Kitendo hicho cha Huggins kilimfanya mke wake awe analia machozi na alilia zaidi siku Huggins aliporudi nyumbani akiwa amelewa pombe chakari, hakuwahi kumwona Huggins akiwa amelewa katika maisha yao ya ndoa hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kwanza na alijua wazi kuwa mumewe alikuwa amevurugikiwa.



    “Huggins umeanza kunywa pombe?”



    “Ni lazima nipumzishe mawazo mke wangu nitachanganyikiwa!”



    “Upumzishe mawazo kwa pombe badala ya kufunga na kuomba?”



    Huggins hakunywa pombe tu bali alianza pia tabia ya kuwa anampiga mke wake na kusumbua watoto! Ilibidi Anne apeleke taarifa hizo kwa wazazi wake na Huggins ambao pia walijaribu kumshauri mtoto wao bila mafanikio tabia ya Huggins ilizidi kuwa mbaya.



    Huggins alipoteza imani kwa Mungu katika muda mfupi tangu alipopunguzwa kazi, alishindwa kuelewa hayo yalikuwa majaribu ambayo ilikuwa ni lazima ayapitie, akawa mlevi kupindukia na watu wengi walishangazwa na mabadiliko hayo na kuna wakati akawa analala katika baa na kurudi asubuhi.



    Hali hiyo ilimvunja moyo sana Anne naye pia akawa haendi kanisani tena, imani katika familia yao ikapotea na uwepo wa Mungu ukaisha! Mama yake Anne aliifurahia hali hiyo kwa sababu jina la Mungu likawa halitajwi tena katika familia yao, shetani akatawala kila kona ya nyumba! Kwake huo ndio ulikuwa wakati mwafaka wa kufanya kazi yake iliyomleta mjini.

    ******

    “Mwanangu Anne hili sasa ni ombi la mwisho, jana tulikuwa kwenye kikao cha Lutego, wazee wametaka damu yako na nilipokataa sana walisema wanataka damu ya watoto wako wawili!”



    ‘MAMAAAA! UNANITAFUTA NINI? NINAAMINI NI WEWE UMENIHARIBIA NDOA YANGU NA UCHAWI WAKO!”



    “Unasemaje?”



    “Tena nasema ondoka kwangu leo hii nitakuitia polisi!”



    “Unanifukuza Anne?”



    “Ndio mama na ninajuta kukukaribisha hapa nyumbani!”



    “Naondoka lakini cha moto utakiona!”



    Siku hiyo hiyo mama yake alikusanya mizigo yake na kuondoka, ilikuwa yapata saa tisa za jioni na Huggins aliporejea saa sita usiku Anne alimsimulia kila kitu kilichotokea na kumwambia mama yake alikuwa ameondoka kurejea Kisiwani Kome.

    “Heri mama yako ameondoka labda ndiye anayenitia mikosi hii?” Alisema Huggins.



    Waliongea mengi baadaye walipitiwa na usingizi, masaa matatu baadaye walizinduliwa na kelele ndani ya chumba chao walipofungua macho kulikuwa na mwanga mkali kupita kiasi, wote waliogopa na miili yao ilitetemeka.



    “Baba Patrick nini?”



    “Hata mimi sijui!”



    Hali hiyo ilidumu kwa dakika ishirini ilipotulia walikwenda kwenye chumba cha watoto na kujikuta wakilia walipowakuta watoto wao wawili Frank na William wakiwa wamening’iniza vichwa pembeni mwa vitanda vyao damu zikiwatoka puani na mdomoni! Walikuwa wamekufa.



    “MAMAAAAA KWELI UMEUA WANANGUUUU!” Anne alipiga kelele.



    “Ni mama aliyewaua?” Huggins aliuliza.



    KWA kawaida wazazi wengi huwa na upendeleo fulani kwa baadhi ya watoto wao, mzazi anaweza kuwa na watoto kumi lakini akawa anampenda zaidi mtoto mmoja au wawili kati yao pamoja na kuwa wote ni watoto wake, katika familia nyingine hali hufikia mpaka watoto wengine kuelewa kabisa kuwa mtoto fulani ni kipenzi cha baba au mama na wengine sio!



    Hivyo ndivyo pia ilivyokuwa kwa Huggins, alikuwa na watoto wanne lakini kati ya watoto hao aliwapenda sana Frank na William, hawakuwa watoto wake tu bali marafiki zake wakubwa, ingawa umri wao ulikuwa mdogo ni wao waliomwambia aache tabia mbaya ya kunywa pombe kwa wingi na kurudi nyumbani usiku na wakati mwingine kumsumbua mama yao.



    Ni watoto hao kipenzi wa Huggins, ndiyo walikuwa wakining’inia darini damu zilichuruzika sakafuni.



    “Patrick na Nancy wako wapi?” Huggins alimuuliza mke wake.



    “Wako kitandani wamelala!”



    “Hawajashtuka?”



    Wangeshtuka wangelia!”



    Aliendelea kujibu Anne huku akilia.

    ****

    Ghafla bila kutegemea kibunga kikubwa na cha ajabu kiliibuka nje ya nyumba yao.



    “Anne ni nini hiki lakini, nini kimetupata jamani? Mbona mimi sielewi”



    “Huggins huyu ni mama tu hakuna mwingine na anafanya hivi kwa sababu ninamemwasi na kujiunga na Ukristo!”



    “Kweli ni mama yako?” aliuliza tena Huggins kwa mshangao.



    “Nakuambia hakuna mwingine huyu ni mama tu na nguvu zake za giza na ndiye kawaua watoto wetu Frank na William!”



    “Hivi kweli Frank na William wamekufa ehe?”



    “Nina hakika watoto wetu wamekufa Huggins!” Aliitikia Anne huku akilia.



    Pamoja na yote aliyoyaona kwa macho yake bado Huggins hakuamini kama kweli watoto wake walikuwa wamekufa, alichofanya ni kutafuta kitu cha kukanyagia ili apande juu na kuhakikisha kama kweli Frank na William walikuwa wamekufa au la!



    Alipata kiti kirefu na kukisogeza karibu na mahali mwili wa Frank ulipokuwa ukining’inia lakini kabla hajapanda ili kuangalia alisikia sauti ya kutisha ikitokea dirishani kwao.



    “Anne mwanangu ni mpaka ukubali cha dini yako ndipo tutaacha kuiteketeza familia yako na sasa bado wewe, mpaka tutainywa damu yako na usithubutu kuyasema mambo haya kwa watu!”



    Walipoisikiliza vizuri sauti hiyo waliigundua ilikuwa ni sauti ya Isabella mama yake Anne, ni sauti hiyo ndiyo iliyomfanya Huggins aamini maneno aliyoyasikia kwa mke wako.



    “Uchawi wa mama yako ndiyo umeua watoto wangu Frank na William?” alisema Huggins huku akimsogelea Anne.



    Katika hali ya kushangaza ambayo Anne hakuitegemea kabisa alishtukia mumewe akimkaba na kuanza kumpiga vibao, ngumi na mateke bila huruma.



    “Huggins kwanini unanipiga?”



    “Utanieleza kwanini wewe na mama yako mmewaua watoto wangu!”



    Anne alijaribu kadri ya uwezo wake kujitoa mikononi kwa Huggins lakini alishindwa kabisa, aliendelea kulia akiomba msaada wa majirani kwa sababu ya mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha hakuna jirani hata mmoja aliyeisikia sauti yake na kumfanya Huggins aendelee kutoa kipigo kwa mkewe bila huruma. Kilio cha Anne kiliwaamsha Nancy na Patrick na kuwafanya nao waanze kulia na kuzidisha kelele.



    “Yaani uchawi wenu ndiyo umeua watoto wangu wapendwa? Wewe na mama yako mtawala watoto hawa nyama!” Huggins alisema kwa hasira.



    “Siyo hivyo mume wangu ni mama pake yake, mimi nisingeweza kuwaua watoto niliowazaa mwenyewe! Niliwapenda mno Frank na William hata wewe unajua!



    “Haiwezekani, umewatoa wanangu sadaka kwani mimi sijui wachawi mnavyofanya!”



    Radi ilipiga kila mahali lakini Huggins hakuogopa, alitembea gizani huku mvua ikinyesha na kuyachukua machozi yote yaliyotiririka kutoka machoni pake, moyo wake uliuma mno!

    ****



    Anne alibaki pake yake ndani akiwa amelala sakafuni hajiwezi kwa kipigo alichopewa, damu nyingi ilimtoka puani na kuilowanisha blauzi yake, Huggins alimuumiza sana na hakuamini kama ni yeye aliyemfanyia ukatili huo.



    Hali ndani ya chumba chake ilitisha, giza lilitanda kila mahali sababu umeme ulikatika muda mfupi baada ya mvua kuanza kunyesha, kila wakati picha ya watoto wake wakining’inia darini ilipomwijia kichwani alipiga kelele kwa woga.



    Baadaye ilimbidi anyanyuke na kupapasa mezani kwake ambako alichukua kiberiti akawasha mshumaa akachukua pamba ambazo alizitumia kuziba pua ili damu isiendelee kutoka zaidi, alipomaliza kazi hiyo aliuzima mshumaa kwa sababu hakutaka kuiona miili ya watoto wake ikining’inia darini.

    ****

    Kama saa mbili hivi asubuhi Anne alisikia mlango wa mbele ya nyumba yake ukigongwa, alifikiri labda ni Huggins alikuwa amerudi kwa sababu tangu alipoondoka usiku wa manane mvua ikinyesha hakurudi tena.



    Alinyanyuka na kujikongoja hadi mlangoni ambako alifungua mlango, tofauti na alivyofikiria mtu aliyekuwa mlangoni hakuwa Huggins bali akinamama wawili wa nyumba za jirani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mama Patrick vipi tena mbona damu nyingi kiasi hiki zimechuruzika nje? Kuna nini humu ndani? Mmechinja mbuzi nini?” aliuliza mmoja wa majirani hao kwa utani.



    Badala ya Anne kujibu swali hilo aliangua kilio! Kitendo hicho ndicho kilichowashtua majirani hao na kuwafanya waanze kudadisi.



    “Mama Patrick nini? Hebu tueleze tafadhali? Una tatizo gani?”



    “Ni mambo makubwa mno na sijui nianzie wapi kuyaeleza!”

    “Nini?”



    “Ingieni wenyewe humo ndani mkaangalie!”



    Bila kusita majirani wale walimpita Anne pembeni na kuingia ndani walifuata michirizi ya damu hadi sebuleni hawakuona kitu!



    “Mbona hatuoni kitu?” Mama Mariam alisema kwa sauti.



    “Angalieni darini!” Anne alipaza sauti iliyochanganyika na kilio.



    Kauli hiyo ya Anne iliwafanya majirani wale wanyanyue shingo zao kuangalia juu, alichosikia Anne kutoka ndani ya nyumba kilikuwa ni kilio huku akinamama hao wakikimbia kurudi nje, walimpita Anne na kusimama.



    “Anne watoto wako wamepatwa na nini?”



    “Nimewaeleza ni stori ndefu sana!”



    “Na mumeo yupo wapi!”



    “Aliondoka usiku kwenye safari!”



    “Ni nini hasa kilichotokea mpaka watoto wakatundikwa darini?”



    “Majambazi walituvamia” Anne alidanganya.

    ****

    Hapakuwa na jambo la kufanya zaidi ya majirani kwenda kutoa taarifa polisi, kila mtu aliyeona miili hiyo darini alilazimika kumuuliza Anne juu ya kilichotokea lakini jibu lake lilikuwa majambazi.



    Polisi walipokuja wakiambatana na daktari waliishusha miili ya Frank na William darini na kuibeba miili ya marehemu kwenda nayo Hospitali ya Sekotoure ambako ulifanyika upasuaji kuichunguza vizuri miili hiyo.



    Baada ya kuchunguza kufanyika miili ilihifadhiwa chumba cha maiti wakati majibu yakisubiriwa, wazazi wa Huggins walishapata taarifa na walikuwa miongoni mwa watu waliofurika hospitali kutaka kujua ukweli.



    Siku iliyofuata majibu yalitoka na yalionyesha kulichoua watoto kilikuwa ni kupasukakwa mishipa kichwani lakini kitaalamu haikuweleweka ni kitu gani kilichowapandisha darini ingawa Anne alielewa.



    Baada ya majibu hayo majirani wakiongozwa na baba ya Huggins mzee Martin William waliruhusiwa kuchukua miili ya marehemu kwenda kuzika.

    ****

    vifo vya Frank na William viliwachanganya akili sana wazazi wa Huggins, walishindwa kuamini kama ni majambazi kweli walioua watoto ila walilazimika kukubali kilichosemwa na Anne, walichukua Patrick na Nancy na kuwahamishia nyumbani kwao.



    “Hivi baba yao yupo wapi?” mzee Martin aliuliza.



    “Aliondoka usiku!



    “Kwenda wapi?”



    “Hakuniaga!”



    “Hakukuaga kwanini? Je wakati anaondoka watoto walishafariki au la!”



    “Walishafariki!”



    “Sasa kwanini aliamua kuondoka?”



    Anne alikosa jibu na kubaki kimya na baadaye aliangua kilio.



    “Baba acheni kwanza kuniuliza maswali hivi sasa mimi bado nimechanganyikiwa!”



    lilikuwa ni ombo la msingi na baba wa Huggins alielewa alikuwa amevuka mpaka kuuliza maswali kwa mtu aliyefiwa.



    “Samahani sana mwanangu ni sababu ya uchungu!”



    Baadaye Anne alihitajika kituo cha polisi kutoa maelezo juu ya tukio hilo bado msimamo wake uliendelea kuwa huo huo kuwa alivamiwa na majambazi usiku walikuja kulipa kisasi.

    ****

    Mazishi hayakufanyika siku hiyo sababu Huggins hakuwepo na watu wote waliamini Huggins alikuwa safarini, ilibidi mazishi yaahirishwe hadi siku iliyofuata ambayo Anne alidanganya kuwa mume wake angeweza kurudi kutoka safarini.



    Kulipokucha asubuhi watu walianza kukusanyika msibani, kijana mmoja aliwashangaza waombolezaji alipoleta taarifa kuwa alimwona Huggins asubuhi hiyo akiwa amefunga taulo kiunoni akipiga mswaki nyumbani kwa mwanamke mmoja aliyejishughulisha na biashara ya kuuza pombe za kienyeji aina ya gongo.



    “Hakyanani nimemwona Huggins nyumbani kwa Delila!”

    Alisisitiza kijana huyo.

    “Nani labda umemfananisha!”



    “Nina uhakika nimemwona kama hamuamini nendeni mkahakikishe!”



    “Kweli?” baba yake Huggins mzee Martin aliuliza kwa mshangao ilibidi vijana watano wa mtaani waamriwe kwenda kuhakikisha, waliporudi dakika kumi na tano baadaye jibu lao liliwashangaza wazee na kuanza kuhisi vifo vya watoto wao havikuwa vya kawaida.



    “Tumemkuta nyumbani akiwa amelewa vibaya mno, tukampa taarifa za vifo vya watoto wake lakini amekataa kuja!”



    “Mna hakika mliyemwona kweli ni Huggins?” aliuliza baba yake na Huggins Mzee Martin.



    “Ndiyo baba ni yeye!”



    “Haya twendeni nikahakikishe mwenyewe sasa hivi!” Alisema mzee Martin na vijana kama ishirini hizi waliongozana nae hadi nyumbani kwa Delila, Huggins alipomwona baba yake alianza kulia.



    “Mwanangu vipi?”



    “Baba mke wangu na mama yake wamewaua watoto wangu!”



    “Akinanan?”



    “Mke wangu na mama yake!”



    “Wamewauaje?”



    “Kichawi na simtaki tena yule mwanamke ni mchawi nimemwambia awale nyama!”



    “Mh! Huggins unayosema ni kweli?



    “Ni kweli baba!”



    “Siamini hata kidogo twende kwenye msiba wa watoto!”



    “Baba niache tafadhali niache baba!” Huggins alikataa katakata pamoja na kubembelezwa na baba yake kwa masaa matatu!

    ****

    Taarifa za kugoma kwa Huggins zilisambaa mioyoni mwa majirani ikabidi watu wengi wajae nyumbani kwa Delila wakijaribu kumshawishi Huggins akubali.



    Taarifa hizo kuliwaudhi sana wakazi wa mtaa huo ambao mara nyingi walifiwa na watoto wao kimazingara na kujikuta wakimbebesha Anne lawama zote juu ya vifo vilivyotokea mtaani hapo, akimama waliokaa nae ndani walitoka nje na kumwacha chumbani peke yake na maiti mbili za watoto wake.



    “Anajifanya mlokole kumbe ni mchawi!” Sauti hiyo ilimuumiza sana moyo Anne.



    “Hatuwezi kuzika maiti ya mtu aliyeua watoto wake mwenyewe!” alisema kiongozi wa mtaa.



    Maneno hayo yaliwafanya wananchi waanze kusambaa kurudi majumbani kwao baba na mama yake Huggins walishindwa kuondoka na kumwacha Anne peke yake na maiti.



    “Mama hebu tueleze ukweli nini kimetokea?”



    Anne aliendelea kulia machozi huku akizidi kuzikumbatia maiti za watoto wake zilizokuwa pembeni yake.



    “Baba ninawapenda sana watoto wangu nisingewaua!”



    “Sasa ni nini kimewaua?”



    “Ni mama yangu, alitaka damu za wajukuu zake ili zikanywewe na wachawi wenzake siyo mimi wazazi wangu naonewa bure!”



    Ilibidi Anne achukue sana kuwaeleza wazazi wa Huggins juu ya mzimu na jinsi ulivyorithiwa kutoka kwa mwanamke mmoja hadi mwingine na pia alieleza jinsi ambavyo mama yake alimlazimisha yeye kuacha Ukristo ili awe mrithi wake atakapokufa.



    “Mwanangu kama ndio hivyo hatuwezi kukusaidia shauri yako, utabaki na miili ya watoto wako utawala nyama!” Alisema baba yake Huggins kwa hasira.



    “Baba!” aliita Anne lakini mzee Martin hakujibu kitu alimnyanyua mke wake na wote walianza kutoka nje ya nyumba.



    “Mama!” Anne aligeuka na kuanza kumwita mama yake Huggins lakini naye pia hakuitika wote walitoka nje na kuingia ndani ya gari lao na kuondoka, mbele walikatisha nyumbani kwa Delila na kumkuta mtoto wao akiwa amelewa chakali, Huggins alipomwona mama yake alianza kulia tena kwa uchungu akiita majina ya watoto wake.



    “Mama, amewaua watoto wangu!”



    “Pole sana mwanangu Mungu anayafahamu yote haya na atakupa faraja!”



    walimbembeleza kuondoka naye lakini alikataa alichofanya ni kuwaomba wamtunzie watoto wake.

    ****

    Mawingu yalikusanyika angani jioni ya siku ya jumapili baadaye mvua yenye radi kubwa ilianza kunyesha na kusababisha giza kila mahali, umeme ulikatika tena na kufanya kuwa kiza kabisa!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Katika hali kama hiyo Anne alikuwa ndani ya nyumba yake katikati ya maiti mbili za watoto wake katikati ya maiti mbili za watoto wake machozi ya uchungu yaliendelea kumbubujika, watu wote walishamkimbia mpaka wakati huo alikuwa haamini hata kidogo kama dunia ilikuwa imemgeukia kiasi kile, yote hayo kwa sababu ya mama yake, aliwatingisha watoto wake akifikiri yaliyotokea yalikuwa ndoto na labda wangeweza kurejewa na fahamu, ukweli haukubadilika.



    Asubuhi siku iliyofuata pia hakuna mtu aliyefika nyumbani kwake, Anne aliendelea kukaa peke yake na maiti za watoto wake akilia, hakuna mtu aliyefika kumpa pole, alitamani Patrick na Nancy wangekuwepo kumfariji lakini bibi na babu yao waliwachukua!



    Alikaa hivyo hivyo kwa siku ya nne na maiti zilianza kutoa harufu.



    Saa 12:45 asubuhi ya siku ya Jumatano ikiwa tayari ni siku ya tano tangu Anne asusiwe watoto na majirani zake pamoja na ndugu wote baada ya kuaminika kuwa aliwaua mwenyewe kichawi, alikuwa ndani nyumba yake akilia, mume wake hakuwepo alimkimbia baada tu ya watoto wake kufariki katika mazingira ya kutatanisha.

    “Hivi kweli Isabella ni mama yangu mzazi? Hivi ningekuwa mtoto wake kweli angenifanyia ukatili huu? Hapana si mama yangu na mimi nitamuua, ni lazima afe, kama siyo leo kesho na kama si kweli wiki ijayo lakini ni lazima Isabella afe tu!” Alisema Anne huku akilia.

    Harufu ilisambaa mtaa mzima na kuwaghasi watu wengine, baadhi ya majirani walitamani kwenda kumsaidia Anne lakini waliogopa kwa kitisho walichokipata kutoka kwa uongozi wa mtaa kuwa yeyote ambaye angejitokeza na kwenda nyumbani kwa Anne kumsaidia pia angetengwa!

    Kauli hiyo ilizidi kuwafanya majirani wote wabaki ndani ya nyumba zao kama vile hakukutokea kitu mtaani kwao. Taarifa za mateso hayo ya Anne ziliwafikia waumini wa kanisa la Praise And Worship ambalo Anne na Huggins walisali kabla ya kuasi na kuacha kwenda kanisani, habari hizo za Anne kufiwa ziliwasikitisha sana waumini wenzake.

    Kuna hata waliolia kanisani habari hiyo ilipotangazwa, kanisa zima waliazimia kwenda kumsaidia Anne katika mateso yake.

    “Pamoja na kwamba ameasi kuja kanisani lakini bado ni ndugu yetu tu katika bwana ni wengi waliasi na baadaye kurudi tena kanisani, ni lazima tumsaidie Anne!” Alisema mchungaji Aaron Mugabiro aliyekuwa kiongozi wa dhehebu hilo na waumini wote waliitikia Ameni!

    Hawakutaka kupoteza muda taratibu zote ziliandaliwa, mabasi mawili yalikodishwa pamoja gari dogo aina ya Landcruiser pickup lililokuwa mali ya mmoja wa waumini yalipeleka waumini kwenda nyumbani kwa Anne!

    Ukimya uliokuwepo nyumbani hapo wakati wanaingia uliwashangaza waumini wote hapakuwa na dalili yoyote ya kuwepo mtu, milango yote ya nyumba ilifungwa na hapakuwa na kelele yoyote, mchungaji aliteremka katika gari lake aina ya Musso na kwenda mlangoni kuanza kugonga lakini hakuna mtu aliyeitikia.

    “Labda walisafirisha?”

    “Hapana nilivyosikia mimi Anne alikuwepo hapa na maiti za watoto wake!” Alijibu muumini mwingine.

    “Sasa atakuwa wapi?”

    “Sifahamu!”

    Karibu kila muumini aliyekuwepo mbele ya nyumba ya Anne aliziba pua yake, sababu ya harufu kali iliyokuwepo mahali pale, iliyowafanya waendelee kuamini ni lazima maiti za watoto wa Anne zilikuwemo ndani!

    “Huyu huku nyumba!” Ilikuwa ni sauti ya mmoja wa waumii aliyezunguka nyuma ya nyumba waumini wote walitembea harakaharaka hadi nyuma ya nyumba wakiongozwa na mchungaji Aaron!

    Anne alikuwepo nyuma akichimba shimo ardhini, shimo lilishafika kiunoni mwake na alikuwa akilia machozi, alitia huruma sana.

    Anne alishajua kulikuwa na watu nyumba yake lakini hakuonyesha kujali, aliendelea kuchimba huku akilia machozi, alionekana kama mtu aliyekata tamaa kabisa, mchungaji alimfuata na kumgusa begani lakini hakugeuka, aliweka jembe lake chini na kukaa ndani ya shimo akilia.

    “Mwanangu Anne unafanya nini hapa?” Mchungaji aliuliza.

    “Ni..na…chi…mba…kaburi….la…watoto..wa..ngu!” Aliongea Anne huku kwikwi ya kulia imemkaba!

    Jibu hilo la Anne liliwafanya waumini wote waliokuwepo waanze kulia na hata mchungaji Aaron alishindwa kuvumilia akamwaga machozi.

    “Acha mwanangu nyanyuka na utoke shimoni, maombi yako Mungu ameyasikia!”

    Anne alijitahidi na kusimama waumini wakamsaidia kutoka shimoni akasimama nje ya kaburi na kusadiwa kuingia ndani ya nyumba yake ambako harufu ilizidi na kuwafanya hata baadhi ya waumini kushindwa kuvumilia kakaa ndani ya kutoka nje!

    Miili ya watoto wake ilikuwa imelazwa kitandani chumbani ikiwa imevimba na kuharibika vibaya, hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini kama binadamu wanaweza kufanya binadamu mwenzao kitendo cha kinyama kiasi kile!

    “Huu si ubinadamu hata kidogo na kwanini hukuja kwetu kututaarifu?”

    “Niliogopa!”

    ‘Uliogopa nini mwanangu?”

    ‘Nilijua msingenisaidia kabisa!”

    “Kwanini?”

    ”Sababu niliacha kuja kanisani!”

    Baadaye wakati waumini wengine waliondoka kwenda makaburini kuchimba makaburini, mchungaji alipata nafasi ya kumhoji Anne suala lililopelekea mpaka majirani zake wagome kuzika watoto wake! Annne alisimulia kila kitu mpaka kilichopelekea mume wake kukimbia nyumbani kwake na kuhamia nyumbani kwa kahaba, mchungaji alipigwa na butwaa!

    “Kwa hiyo kila mtu anaamini kuwa wewe ndio umeshirikiana na mama yako kuwaua watoto wako siyo?”

    “Ni kweli mchungaji lakini jambo hilo si kweli hata kidogo, ila mama yangu amefanya hivyo yeye peke yake, kama njia ya kunishinikiza mimi nikubali kurudi tena katika ushirikina kitu ambacho sipo tayari kukifanya ingawa hivi sasa nipo nje ya kanisa!”

    “Unajua kwanini lakini mama yako amefanikiwa kuua watoto wako?”

    “Hapana mchungaji!”

    “Kwa sababu wewe na mumeo mliacha kumtumaini Mungu! Kwanini unafikiri hakulifanya hili siku za nyuma?”Anne alikaa kimya kwa sababu alijua kilichosemwa na mchungaji kilikuwa kweli tupu!

    “Unasikia?”

    ”Nimekuelewa mchungaji!”

    Baadaye watu waliokwenda makaburini kuchimba kaburi walirejea na kutoa taarifa kazi hiyo ilikuwa tayari, mchungaji na watu wengine kama watano hivi waliingia ndani wakiwa wamevaa mipira mikononi na kusafisha miili ya Frank na William ilikuwa ni kazi ngumu lakini ulikuwa ni wajibu wao.

    Baada ya hapo kazi hiyo ibada fupi ilifanyika na miili ikachukuliwa kwenda makaburini kwa mazishi ambako mchungaji Aaron pia aliongoza ibada! Muda wote huo Anne alikuwa akilia, maisha yake tangu utotoni yalikuwa ni ya mateso mengi na kutengwa na jamii, hali iliyosababishwa na mama yake.

    “Sasa tunamwomba mama wa marehemu hawa aje mbele aweke mchanga kama ishara ya kuwaaga wapendwa wake!”

    Anne alishikwa mikono na akinamama wawili waliomwongoza hadi kaburini lakini kabla hajaweka mchanga alilegea na kuanguka chini, alikuwa amezimia, ilibidi ndoo ya maji iletwe haraka na kumwagia maji ili azinduke lakini haikuwa hivyo, ikabidi apakiwe katika gari na kurudishwa nyumbani akiacha mazishi yakiendelea, nyumbani pia alimwagiwa maji lakini hakuzinduka ikabidi achukuliwa na kupelekwa hospitali ya TMC iliyokuwa karibu na nyumbani kwao ambako alipewa matibabu ya kuzimia ikiwemo kuongezewa maji na kuzinduka masaa mawili baadaye.

    Alipozinduka kwa mara ya kwanza alifikiria yupo makaburini, hakujua mara moja kuwa alikuwepo hospitali.

    “Nipeni mchanga! Nipeni mchanga niwaage watoto wangu!” Watu wote waliokuwa karibu yake wakiwemo manesi walisikitishwa sana na kitendo hicho na walimhurumia sana Anne.

    “Hapa ni wapi?” Aliuliza fahamu zilipomrudia kichwani.

    “Hapa ni Hospitali ya TMC!”

    “Nimekukuja hapa saa ngapi?”

    “Ulizimia makaburini!”

    “Kweli haya nirudisheni makaburini upesi!”

    “Makaburini wameshatoka labda tukupeleke nyumbani!”

    ”Hapana nataka makaburini nataka niyaone makaburi ya watoto wangu!”

    Mchungaji Aaron na waumini wengine waliokuwepo hospitali walijaribu kumshauri waende nyumbani kwanza lakini Anne alikataa na kuendelea kusisitiza apelekwe makaburini, hapakuwepo na njia ya kulikataa hilo ikabidi watoke hospitali na kumpakia hadi makaburini.

    “Watoto wako tumewalaza kwenye kaburi hili!”

    Anne alianguka juu ya kaburi hilo na kuanza kulia akiita majina ya watoto wake.

    “Frank na William kweli mmekwenda? Kweli mmeniacha? Kwa sababu yenu mimi nitamuua mama yangu!”

    “Acha Anne acha usiseme hivyo tafadhali mwachie Mungu kila kitu!”

    “Mchungaji inauma sana!”

    Walimnyanyua kutoka kaburini na kumwomba waondoke, Anne hakutaka kuendelea kukataa huku akilia alitembea hadi kwenye gari nakupanda, alikuwa amekonda sana sababu ya kulia na kutokula.

    “Mchungaji sijui jinsi ya kukushukuru wema na waumini wa kanisa, Mungu atanilipia ila mmenisaidia katika wakati mgumu sana!”

    ****

    Walipofika nyumbani walikuta waumini wengi wakiendelea na shughuli za msiba, wengine wakipika chakula na wengine wakipasua kuni na wanakwaya wakiimba nyimbo mbalimbali za kumsifu Mungu, ilikuwa ni faraja kubwa sana kwa Anne, majirani walikuwa wamemtenga walishangazwa sana na kitendo kile, wengi walipita na kuchungulia na kutokuamini kama hatimaye watoto wa Anne walikuwa wamezikwa, wao pia walishukuru kwa kitendo hicho kwani walikuwa na mateso makali sana ya harufu nyakazi za usiku.

    ****

    Mchungaji Aaron na waumini wengine walikaa na Anne wiki moja wakimfariji siku ya nane nao walilazimika kumwaga ili warudi nyumbani kwao na kuendelea na shughuli zao, siku zote alizokaa nao zilikuwa za faraja kubwa kwa Anne mpaka wakati huo alishindwa kuelewa bila waumini hao mwisho wa tatizo lake lingekuwa nini? Ndiyo angezika halafu baadaye kingefuata nini, hakuwa na jibu la moja kwa moja.

    Shukrani zake kwa mchungaji na waumini wengine wote zilikuwa kubwa mno na hakujua jinsi ya kuzielezea kwa maneno, asingependa sana Frank na William waendelee kuishi naye lakini isingewezekana ilikuwa ni lazima sasa apambane na maisha peke yake!

    Katika siku zote waumini waliokaa kwake, hakuwahi kumwona Huggins akija nyumbani pale wale wazazi wake na watoto wake wawili Patrick na Nancy roho ilimuuma sana kujikuta katika hali hiyo, angependa kumbadilisha na kuirejesha tena katika wakati wa zamani alipokuwa na maisha bora lakini aliona kama ilikuwa si rahisi kabisa jambo hilo kutokea.

    Hapakuwa na njia ya kuwazuia waumini wasiondoke, ilibidi waondoke na kumwacha Anne peke yake, nyumba kubwa aliyoishi ilimtisha sana na ilimfanya asikie ukiwa zaidi.

    Siku hiyo alilala peke yake ndani na siku hiyo hiyo majira kama ya saa tisa hivi usiku alisikia dirisha la chumba alikokuwa amelala likigongwa alishtuka sana ana hakufahamu ni nani aliyekuwa akigonga usiku huo, baadaye alisikia sauti ya kiume ikiita dirishani, alipoisikiza vizuri sauti ile ilikuwa ni sauti ya Huggins, furaha kubwa ilimrejea moyoni na kujua kipenzi chake alikuwa amerejea kwake, hakutaka kuchelewa alisimama na kutembea hadi dirishani na kufungua.

    Alipofungua alishangaa kukutana na sura ya mama yake! Mwili wake ulitetemeka alikataa kufungua dirisha lakini alishindwa

    “Karibu mama!”

    “Unamkaribisha nani? Na bado nimekwishachukua watoto wawili sasa nimebakiza kuwajia hao wawili ulionao ndio utaelewa kuwa mimi nimekasirika mpaka utakapokubali kuwa upande wangu ndipo nitakapokuacha, umeuniudhi sana!” Mama yake alisema maneno hayo kabla Anne hajajibu kitu alishtukia kitu kama maji yenye harufu kali yakimwangika kuingia ndani na kumlowanisha mwili mzima!

    “Huo tayari ni mkosi watu watakuona kama mavi kuanzia leo!” Mama yake alisema na kupotelea katikati ya migomba.

    Anne alirudi na kuanguka kitandani kwao na kuanza kulia alishindwa kuelewa ni kwanini mama yake alikuwa akimfanyia unyama ule!

    “Watoto wangu hawaui nitawapeleka kwa mchungaji Aaron na halafu mimi nianze kazi ya kumtafuta mama hadi nimuue tu!”Asubuhi kulipokucha Anne alitoka ndani baada tu ya kunywa chai na kuanza kutembea kwenda nyumbani kwa wazazi wake na Huggins kabla hajafika alipita kwanza nyumbani kwa Delila kumwona Huggins!

    Aligonga mlango na mlango ulifunguliwa na Huggins mwenyewe.

    “Wewe mchawi umefuata nini hapa? Tokaa vinginevyo nitakua!” Alisema Huggins.

    “Huggins wewe ni baba wa watoto wangu acha kusema maneno hayo!”

    “Toka hapa kwanini umeua watoto wangu?”

    “Sio mimi Huggins nimekwisha kueleza juu ya jambo hilo!”

    Huggins alimwacha Anne mlangoni na kuingia ndani alipotoka alikuwa na panga mkononi na kuanza kumkimbiza Anne, watu waliokuwa wakiangalia walishangilia na kumzomea Anne! Kweli Anne aliamini mama yake alikuwa amempaka mkosi, kila alipopita watu walipishana nae hawakutaka akae karibu yao, harufu ya mwili wake haikuwa nzuri.

    “NITAMUUA MAMA!” Alisema kwa sauti alipofika nyumbani kwa wakwe zake walishangaa kwa harufu aliyokuwa nayo. Siku iliypfuatia, akaamua kuwapeleka watoto wake kwa mchungaji Aaron.

    Kwa mwaka mzima aliishi mbali na watoto wake na hakuona jambo lolote lililowapata Patrick na Nancy alimshukuru Mungu mama yake hakuja tena usiku.

    ****

    Januari 23 saa tisa ya usiku ikiwa ni miezi miwili tangu watoto wake wafariki alizinduliwa usingizini na sauti ya mtu akiongea dirishani ilikuwa ni sauti ya mama yake.

    “Kwa sababu umewaweka watoto wako kwa mchungaji sasa nitakupa adhabu nyingine, itabidi kila siku maisha yako yote!”

    Dakika mbili tu tangu asikie sauti hiyo alishangaa kusikia nguo zake za ndani zikilowa damu ilikuwa ikitoka kama maji!

    “Mungu wangu!” Alisema Anne kwa mshangao, hakuamini kama hali hiyo ingeendelea siku zote lakini alishangaa alipomaliza miezi sita ikivuja damu usiku na mchana wakati mwingine alilazimika hata kwenda kuongezewa damu na kupewa vidonge vya kuongezwa damu, nyumba yake ilijaa makopo ya vidonge vya Fero B’ alivyopewa hospitali kuongeza damu! Aliishi kwa mateso, inzi walimfuata kila alikokwenda, watu hawakumkaribia, kila mara alishindwa kukaa kitini sababu kila alipokaa alilowanisha kiti alichopewa katika daladala alisimama hata kama kulikuwa na viti.

    Hakuweza kumudu kununua ‘Always’ badala yake akawa anatumia taulo lakini nazo zilioza pia, yalikuwa mateso makubwa sana kwa Anne alilia na kumwomba Mungu amsaidie, hasira ya kumuua mama yake ilipanda kila siku.



    Anne alizidi kukimbia huku akilia machozi, Huggins alizidi kumfuata nyuma yake, akimpiga na ubapa wa panga! Watu wote walioshuhudia walizidi kupiga kelele wakishangilia kitendo kile na wengine walizomea!

    Taarifa za Huggins kuhama nyumbani kwake na kutoshiriki katika mazishi ya watoto wake kwa kile kilichoaminika kuwa ni mkewe kuwatoa sadaka watoto wake mwenyewe wafe kichawi!

    Wengi walimchukia Anne, hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa tayari kumsaidia Anne akipigwa na Huggins, hata alipoangushwa chini na kuanza kuchaniwa nguo watu wote walishangilia na kupiga mayowe.

    “Ua mchawi huyo! Ua mchawi huyo!” Wananchi walipiga kelele.

    Huggins alizidi kushusha kipigo kwa Anne huku watu wakizidi kushangilia, mwisho kabisa Huggins alilinyanyua panga lake na kumkata nalo Anne begani, damu nyingi sana ilimtoka, watu walipoona kitendo kile waliogopa na kuanza kukimbia kuondoka eneo lile, baadaye Huggins naye aliondoka.

    Anne alijitahidi akanyanyuka lakini alishindwa kwa sababu alikuwa nusu uchi, watu waliendelea kukusanyika wakimshangaa, baadhi ya akinamama walimhurumia lakini wengine walimlaani kwa kitendo chake cha kuwaua watoto.

    Baaaye alishtukia akifunikwa na khanga mwili mzima! Alishangaa ni mtu gani mwenye huruma, alinyanyua uso kuangalia juu, aliitambua sura yake!

    “Anne vipi?”Aliuliza

    “Mume wangu kanipiga dada!”

    “Kwanini?”

    “Wewe ni nani na unaishi wapi hujayasikia yaliyonipata?”

    “Mimi naitwa Victoria kama utakumbua tulisoma wote Ngaza!”

    Aliposema hivyo kweli Anne alikumbuka msichana huyo alikuwa miongoni mwa wasichana waliosoma katika shule ya wasichana ya Ngaza, ila Anne alikuwa mbele yake, msichana yule alimsaidia Anne kusimama wima.

    “Twende nikusindikize hospitali!”

    “Lakini nilikuwa nakwenda ukweni kwangu kuwafuata watoto wangu, baba mkwe aliwachukua!”

    “Hapana huwezi kwenda katika hali hii ya kuvuja damu twende kwanza polisi ukatoe taarifa kisha twende hospitali ukatibiwe, baada ya hapo ndipo utaweza kwenda ukweni kwako!”

    “Twende tukatoe taarifa wapi?”

    “Polisi!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapana Vicky siwezi kwenda polisi!”

    “Kwanini?”

    “Sitaki kumshitaki mume wangu, Huggins ni baba wa watoto wangu, akifungwa watoto wangu watakuja kuniuliza!”

    “Mh!” Vicky aliguna.

    “Kama ni hospitali twende lakini polisi sitakwenda, nisaidie kunifikisha basi!”

    “Hospitali hawawezi kukutibu bila PF3!”

    “Hilo nalifahamu lakini wee twende tu!”

    Walianza kutembea taratibu kuelekea hospitali ambako pia hapakuwa mbali sana na mahali tukio hilo lilipotokea, watoto wengi waliwafuta nyuma wakati wakitembea na watu wengine wakubwa walizidi kuwashangaa.

    ****

    “Binti kimetokea nini?”Daktari aliuliza.

    “Nimeangukia kisu jikoni!”

    “Pole sana na hayo majeraha usoni je?”

    “Ni jengo la jiko limebomoka ndiyo likasababisha niangukie kisu!’

    “Aisee pole tena!” Daktari alimpa pole Anne.

    “Itabidi tukushone kiasi cha nyuzi zisizopungua kumi na tano, sababu umeumia sana, itakugharimu shilingi elfu kumi na tano na baada ya hapo tutakuandikia sindano za PPF tano na chanjo ya pepopunda sawa, kwa hiyo gharama na matibabu yote itakuwa shilingi eflu ishirini na moja na mia tano!”

    “Daktari mie sina pesa kabisa!” Alisema Anne huku akilia.

    “Mimi nitalipa!” Vicky alisema na palepale alianza kufungua mkoba wake kutoa pesa!

    “Subiri kwanza basi utalipia pale dirishani kwa keshia!”

    Baada ya kulipia Vicky alirudi kwenye benchi na kukaa akimsubiri Anne amalize kuhudumiwa muda wa dakika thelathini baadaye, Anne alitoka chumba cha upasuaji akiwa amefungwa bandeji kubwa begani! Alishachomwa tayari sindano za PPF na Pepopunda.

    ****

    Walipotoka hospitali, Anne alimuomba Vicky waongozane kwenda ukweni kwake kuwachukua watoto, Vicky alikubali na walikwenda hadi nyumbani kwa mzee Martin.

    Walipowasili nyumba ilikuwa kimya kama vile hapakuwa na watu, Anne aligonga na mlango ukafunguliwa na mama yake Huggins!

    “Karibuni sana!”

    “Ahsante shikamoo mama” wote wawili waliitikia na baada ya salamu wote waliingia ndani ambako walikaa vitini na muda mfupi mzee Martin aliungana nao na wote wakamwamkia!

    “Vipi binti zangu?”

    “Baba nimekuja kuwafuata watoto, hawatakiwi kabisa leo kulala hapa, najua kitakachowapata!” Alisema Anne akikumbuka kitisho kilichotolewa na mama yake.

    “Nini kitawapata?”

    “Watakufa?”

    “Watakufa vipi?”

    “Mama amesema anawafuata!”

    “Sasa unataka kuwapeleka wapi kwenye usalama kuliko hapa nyumbani?”

    “Nataka niwapeleke kwa mchungaji Aron akakae nao, leo mama anakuja kuwadhuru watoto wangu!”

    “Hilo mwanangu haliwezekani, watoto hawaondoki hapa, baba yao amekataa kabisa!” mama yake Huggins aliweka mgomo.

    “Hapana mama nipeni watoto wangu, niondoke nao!”

    “Haiwezekani labda tumwite baba yao aje hapa umuombe!”

    “Sitaki kuonana na Huggins kabisa, kwani ni yeye aliyenifanyia hivi!”

    “Sawa na pole sana lakini sisi hatuwezi kuacha uondoke na watoto bila yeye kukubali!”

    Wakati maongezi yakiendelea, Patrick na Nancy waliokuwa wakicheza chini walimfuata Anne na kusimama mbele yake! Ikabidi Anne awapakate miguuni pake, alijisikia vizuri kuwa na watoto wake tena! Hakutaka kabisa kutenganishwa nao! Aliwapenda na hakutaka wapatwe na matatizo yaliyosemwa na mama yake!

    “Baba siwezi kuwaacha watoto wangu!” Alisema Anne huku akiwawekea watoto wake matiti mdomoni ili wanyonye! Watoto walionyesha furaha.

    “Mimi naondoka!”

    “Tafadhali waache watoto!” Baba yake Huggins alisema kwa sauti.

    “Hapana baba ni lazima niondoke nao

    Ulitokea mzozo mkubwa sana wa kunyang’anyana watoto hatimaye Anne alinyang’anywa Patrick na Nancy walilia kupita kiasi wakimlilia mama yao.

    “Ondoka hapa vinginevyo nitakuitia polisi”

    “Siondoki nipeni watoto wangu upesi!” alisema Anne huku akilia machozi.

    “We binti!” Mzee Martin alimwita Vicky!”

    “Naam mzee!”

    “Hebu mwondoe huyu mchawi hapa sisi hatuwezi kumpa watoto akawaue, ondokeni kabla sijawaita wezi!”

    Vicky aliogopa na kujikuta akimwomba Anne waondoke, Anne alikataa lakini Vicky alimbembeleza hatimaye alikubali na wote walianza kuondoka, watoto wakimlilia mama yao lakini mzee Martin na mkewe hawakujali walizidi kumfokea Anne kwa maneno machungu yaliyomuumiza moyo.

    ****

    Kwa msaada wa Vicky huku akilia machozi Anne alikwenda hadi nyumbani kwake , baada ya kufika Vicky aliaga na kuondoka kwenda nyumbani kwake, aliishi kwenye majengo ya shule ya Isamilo ambako alifanya kazi kama mwalimu!

    “Ahsante kwa msaada wako Vicky!” alisema Anne akitoa shukrani.

    ****

    Saa tatu usiku Anne akiwa amelala kitandani kwake alisikia sauti ya watoto wakilia nje ya nyumba yake, alishituka zaidi kusikia mlango ukigongwa! Aliogopa kwenda kuufungua lakini baadaye aliposikia sauti ya watu wakiongea na kuitambua sauti ya mama mkwe wake alinyanyuka harakaharaka kwenda mlangoni.

    Alisikiliza kwa muda na kugundua kweli waliokuwa nje walikuwa wakwe zake pamoja na watoto wake, ingawa aliogopa na hakujua kilichowaleta alifungua mlango, alishangaa kukuta Huggins na Delila pia wapo.

    “Karibuni ndani!”

    “Unamkaribisha nani ndani? Nani aingie nyumbani kwa mchawi” Delila alisema kwa nyodo.

    “Jamani ingieni ndani!”

    “Sisi ndani hatuingii, tangu umeondoka watoto wanalia tu na hawataki kula sijui umewaroga, sasa dawa ya mchawi ni kumpa mtoto alee! Tumekuletea watoto wako ili uwaue vizuri!”

    Baada ya kusema hayo tu waliwabwaga watoto chini na kuondoka, Anne alimshukuru Mungu na alichofanya pale kikawa ni kuwachukua watoto wake na kuanza safari ya kwenda nyumbani kwa mchungaji.

    Hapakuwa mbali sana ulikuwa kama umbali wa robo kilometa hivi, alipofika aligonga na kufunguliwa.

    “Nimewaleta watoto wangu mkae nao hapa nyumbani!”

    “Mchungaji na mke wake hawakutaka kuuliza kwanini bali waliwapokea watoto wale na kuagana na Anne, watoto walilia lakini hapakuwa na njia ilibidi wabaki kwa usalama wa maisha yao, Anne alikuwa na uhakika pale walikuwa salama kuliko nyumbani kwake.

    Aliporudi nyumbani aliendelea kulia akimfikiria mama yake na jinsi alivyomtesa tangu utotoni! Alikosa raha ya maisha na thamani ya kuwa na mama mzazi.

    Mpaka saa tisa ya usiku Anne alikuwa bado yupo macho, bila kupata hata lepe la usingizi, ghafla alishitukia kimbunga kikubwa nje na mwanga mkali ukafuata, alilifananisha tukio hilo na tukio la siku Frank au Henry, jina alilopewa na babu yake baada ya kuzaliwa na William walipokufa!

    “Ahaa! Umejifanya mjanja siyo, umewahamisha watoto eh! Sasa ni kazi kwako! Nakuambia tangu sasa utalowanisha hizo nguo zako hadi mwisho wa uhai wako!”

    Baada ya sauti hiyo tu, Anne alishitukia kitu kama maji mengi yakitoka sehemu zake za siri na nguo zake za ndani zililowa, alifikiri ni mkojo lakini hali ilipotulia na kuangalia vizuri aligundua haukuwa mkojo bali damu nzito iliyotiririka kushuka chini miguuni kwake!

    “Hili ni pigo jingine lakini ni heri hali hii kuliko watoto wangu kufa na ugomvi wangu na mama hautakwisha mpaka nimwondoe duniani!” aliwaza Anne.

    ****

    Asubuhi kulipokucha nguo zote alizovaa zililowa damu, damu iliyokuwa ikimtoka ilikuwa nyingi mno kiasi cha kushindwa kuvaa ‘pedi’ ili kuzuia isilowanishe nguo zake alilazimika kuchukua taulo ya kuogea na kulikunja akaivaa katika ya miguu yake lakini nalo muda mfupi tu lililowa!

    Pamoja na shida hiyo Anne alijitahidi kutembea hadi nyumbani kwa Mchungaji kuwaangalia watoto wake, aliwakuta wakinyweshwa uji aliwabeba na kuanza kuwanyonyesha.

    Walimweleza kila kitu kilichotokea usiku, kimbunga na mwanga mkali huku sauti za watu wakiwataka Nancy na Patrick, Anne alielewa kilichoendelea.

    “Ilibidi mimi na mchungaji tuanze maombi ndipo hali ikatulia!” Mke wa mchungaji alisema.

    *****

    Hayo ndiyo yakawa maisha ya Anne kila siku ilikuwa ni lazima aende kwa mchungaji kuwanyonyesha watoto wake, damu iliendelea kumtoka kila siku, kila alikokwenda kwa sababu ya harufu alifuatwa na inzi wengi, harufu hiyo ilimfanya atengwe na watu, kila alipokaa watu walimkimbia!

    “Aliishiwa damu mara tano katika kipindi cha miezi sita, safari zote alilazwa hospitali na kuongezwa damu chupa kadhaa! Madaktari walijaribu kumpa tiba lakini haikusaidia, ikabidi ajaribu tiba za jadi lakini nazo hazikusaidia, maisha yalimtesa na hakuona haja ya kuendelea kuishi alitamani kufa lakini aliwahurumia watoto wake Patrick na Nancy alijua bila yeye wangepata taabu kubwa maishani.

    “NITAMUUA MAMA HAWEZI KUNITESA HIVI” Anne aliwaza na siku hiyohiyo alichukua kalamu na karatasi kumwandikia mama yake barua akimweleza kuwa aliamua kuuacha Ukristo na kurudi tena katika uchawi ili awe mrithi wa mzimu wa Lutego.

    Mama yake alipoipokea barua hiyo alifurahi mno na kuisoma usiku mbele ya wanachama wenzake, walipiga makofi na kushangilia wakajua Anne alikuwa amenyooka.

    “Hivyo nitakwenda mimi na wengine wawili na tutakwenda kama binadamu wa kawaida!”

    “Lini?” wanachama wengine waliuliza!

    “Kesho asubuhi!”

    ****

    Ulikuwa mchana wa joto kali, Anne alikuwa amechoka sasa alidhamiria kumwondoa mama yake duniani! Hakuwa na kitu kingine cha kufanya, mateso aliyopata yalitosha kabisa hakutaka mengine zaidi, akiwa katika mawazo hayo ghafla alishitukia mlango wa nyumba yake ukigongwa, alikwenda moja kwa moja kufungua mlango, alikutana na sura ya mama yake na bibi vizee wengine wawili, alipowaangalia aliwafahamu walikuwa bibi vizee wa kijijini kwao.

    Hasira ilimkaba Anne kooni lakini hakutaka kuionyesha, aliazimia kuwaua wote watatu

    ****

    Anne alikuwa akitetemeka kwa hasira, tayari alishamchoma mama yake kwa kisu kifuani tena kwenye titi la mkono wa kushoto na alipohakikisha kuwa amekufa alikichomoa na kutembea hadi chumba cha pili ambako bibi kizee mwingine muumini wa Ushirikina aliyeongozana na mama yake alilala, huko nako aliikamilisha kazi yake kwa kukizamisha kisu kilekile kifuani kwa bibi yule naye akaaga dunia.

    Alikuwa amebakiza mtu mmoja tu ili alikamilishe zoezi zima, bibi kizee wa tatu aliyelala katika chumba kilichokuwa mkono wa kulia pembeni mwa chumba chake cha kulala, ni huyo ndiye aliyekuwa amesimama mbele yake!

    Tofauti na mama yake pamoja na bibi kizee mwingine aliyekwishawaua, bibi kizee huyo alikuwa macho amesimama katikati ya chumba huku tunguli mbili kubwa zikiwa mikononi mwake! Anne alitetemeka hali iliyokuwepo ilikuwa ni tofauti kabisa na picha aliyoitegemea, kwa hasira aliyokuwa nayo moyoni hakusita wala kuiruhusu hofu imtawale.

    “Nakuua! Amini usiamini wewe bibi kizee pamoja na uchawi wako mimi nakuua uwafuate wenzako kwanini mmenitesa kiasi hiki?”

    “Mimi huwezi kuniua, utajiua mwenyewe tu!”

    “Nakuambia wazi utakufa!”

    “Huwezi na jaribu uone!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akiwa na hasira kali na uchungu pamoja na nia ya kuua ambayo hakutaka kabisa izuiliwe, Anne aliruka juu huku kisu chake chenye ncha kali kikiwa mkononi, lengo lake likiwa kumchoma bibi kizee shingoni lakini kabla hajamfikia bibi alizirusha tunguli zake juu na zilipodondoka chini zilipasuka!

    Moshi mkubwa ulikifunika chumba na kumfanya Anne ashindwe kuona mbele baadaye mwanga mkubwa ulimulika kila kona ya chumba, Anne aliona kitu kama moto ukiwaka chumbani lakini cha kushangaza hakuhisi maumivu wala kuungua.

    Anne aliendelea kuzunguka chumbani akimtafuta bibi kizee lakini hakufanikiwa kumpata sehemu yoyote ya chumba! Ghafla alihisi kuanza kulewa na kupoteza fahamu na hatimaye akajikuta akianguka sakafuni, hakuelewa tena kilichoendelea na alipozinduka alishangaa kujikuta akiwa amelala nje ya nyumba yake akiwa uchi wa mnyama! Alishindwa kuelewa nini kilitokea mpaka akajikuta nje!



    Je nini kitaendelea?

    Je Anne ataweza kuwaua wengine?

    Je watoto wake watabaki salama?



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog