Search This Blog

NILIFANYA MAPENZI NA MAITI 20 ILI NITAJIRIKE - 2

 







    Simulizi : Nilifanya Mapenzi Na Maiti 20 Nitajirike

    Sehemu Ya Pili (2)



    Mwanaume yule akachukua kibegi changu na kuanza kuelekea ndani ya basi moja, sikumbuki liliitwaje. Nikaingia ndani, akanipa mzigo wangu na kisha kutulia kitini. Sikuwa nikiamini kilichokuwa kikiendelea, eti Zakia mimi, leo hii nilikuwa njiani kuelekea Dar. Safari ikaanza.



    Kumbuka kwamba sikuwa na ndugu yeyote ndani ya Jiji la Dar es Salaam, nilikuwa nikienda mimi kama mimi, sikujua ningefikia wapi lakini hamu yangu ilikuwa ni kufika ndani ya jiji hilo tu. Njiani, sikutaka kulala, nilikuwa macho japokuwa nilichoka sana, nilitaka kuona huko mwanzomwanzo wa jiji hilo kulionekanaje.



    MWAGIKA NAYO HAPA….



    “Hivi Dar kuzuri?” nilijikuta nikimuuliza mwanamke niliyekuwa naye.



    “Ndiyo! Kwani hujawahi kufika?”



    “Hapana kwa kweli…”

    “Una ndugu huko?”

    “Hapana!”



    “Eeeh! Sasa unakwenda kufanya nini?”



    “Nakwenda kutafuta utajiri!” nilimwambia yule mama, kwa mbali akaonekana kushangaa.



    “Unakwenda kutafuta utajiri?” aliuliza kwa mshtuko.



    “Ndiyo!”



    Hakuuficha mshangao wake, aliniangalia kwa macho yaliyoonyesha kuwa na maswali mengi mno, sikujua alijiuliza nini lakini hata kwa kuniangalia usoni, aligundua kwamba nilimaanisha nilichokuwa nikikisema kwamba nilikwenda Dar kutafuta utajiri tu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakutaka kuniuliza swali jingine tena, akanyamaza na kuendelea na mambo yake huku nikipata muda zaidi wa kuangalia dirishani. Baada ya saa moja na nusu, nikahisi kwamba ndiyo nilikuwa nikiingia ndani ya jiji hilo, nyumba nzuri zilianza kuonekana, hisia zangu zikaniambia kwamba tayari tulikuwa tukiingia ndani ya jiji hilo.



    “Ndiyo tumefika?” nilimuuliza baada ya ukimya mkubwa.



    “Ndiyo! Ila tunaelekea Ubungo, hapa kunaitwa Kibamba…” aliniambia.



    Japokuwa sikuwa nikipafahamu huko na wala kufika sikuwahi lakini nilikuwa na hamu kubwa ya kuliona jiji hilo. Kipindi cha nyuma nilipokuwa kijijini, kila mtu alitaka kwenda huko, hawakujali kama walikuwa na ndugu au la, walichokitaka ni kujiona wanaingia ndani ya Jiji la Dar es Salaam na kufanya biashara kwa kuamini watafanikiwa.



    Baada ya dakika arobaini, basi likaanza kuingia ndani ya kituo kikubwa cha Ubungo, huko, idadi kubwa ya watu ilinishangaza, haikuwa kama Morogoro, watu walionekana kuwa wengi huku wengi wao wakionekana kuwa bize wakifanya mambo yao.



    Niliteremka na mwanamke yule kuondoka, sikuwa na pa kwenda, begi langu mikononi, kwa sababu humo kulikuwa na watu wengi, wa rika zote tena mbele nikiona kuna mikeka, nikasema pia ua, ilikuwa ni lazima na mimi niishi humohumo, hata kwenda huko nje, sikutaka kabisa, kama kula, nitakula humohumo, kama kufanya biashara, acha nifanye humohumo, ila kutoka ndani ya kituo cha Ubungo, nisingeweza, kwani hata kama ningetoka, ningekwenda wapi? Sikuwa na sehemu, hivyo kuishi humo niliona kuwa sulkuhisho. Na humohumo ndipo ningepata huo utajiri.



    Nilipokuwa nikiingia ndani ya kituo hicho, moyo wangu uliniambia kwamba inawezekana nilikuwa peke yangu ambaye sikuwa na makazi, niliamini kwamba unapoingia usiku basi watu hao wote wangeondoka na kuelekea nyumbani kwao hivyo kubaki peke yangu kumbe kile nilichokuwa nikikifikiria hakikuwa sahihi kabisa.



    Muda ulizidi kwenda mbele, ilipofika saa moja usiku, badala ya watu kupungua ndiyo kwanza walizidi kuongezeka. Nilijiuliza kilichokuwa kikiendelea ni kitu gani lakini nikashindwa kufahamu chochote kile. Mabasi kutoka mikoani yaliendelea kuingia kwa zamu, nilichoka sana, nilihitaji kulala lakini sikujua wapi pa kulala kwani kila sehemu niliyoiangalia pale kituoni ilikuwa na mizigo ya watu hivyo kuwa na wakati mgumu.



    “Wewe dada!” nilimsikia mwanaume mmoja akiita nyuma yangu, nilipogeuka, macho yangu yakagongana na macho ya mwanaume huyo.



    “Abee..” niliitikia, akanisogelea.



    “Wewe ni mgeni mahali hapa?” aliniuliza huku akiwa amenikazia macho.



    “Ndiyo!”

    “Umetoka wapi?”

    “Morogoro!”

    “Unaitwa nani?”



    “Naitwa Zakia!”



    Kwa jinsi nilivyomwangalia mwanaume yule, nilijua tu kwamba alitaka kunizoea na kulikuwa na kitu kingine alichokihitaji kutoka kwangu. Kiukweli nilifanya mambo mengi mabaya, yasiyopendeza mbele ya jamii lakini wakati mwingine nilitakiwa kuyafanya hayo kwa sababu hali niliyokuwa nayo kipindi hicho, ilinilazimu kufanya hivyo.



    “Utalala wapi sasa?”



    “Sijajua, sina ndugu yeyote yule…” nilimjibu.



    Kwanza akaonyesha tabasamu pana, lilinishangaza lakini kitu nilichokumbuka, mwanaume huyu alifanya kama alivyofanya Mudi kwamba kama sina ndugu, basi yeye angejifanya ndugu ila mwisho wa siku alihitaji penzi.



    Akaniambia twende sehemu kuzungumza, kwanza niliogopa lakini sikuwa na jinsi, ningefanya nini na wakati nilihitaji msaada mkubwa kutoka kwake? Hivyo nikakubaliana naye. Tukaenda sehemu, ilikuwa pembeni ya duka moja la vinywaji, pale niliona kukiwa na mikeka zaidi ya thelathini ikiwa imekunjwa, sikujua ilikuwa ni ya kazi gani.



    “Unajua mpango mzima wa kulala humu?” aliniuliza swali.



    “Kulala humu? Kwani kuna watu wanalala humu?” nilimuuliza huku nikionekana kushtuka.



    “Ndiyo! Wanakodisha mikeka na kulala, saa kumi na mbili wanairudisha..” aliniambia.



    “Wanakodisha wapi?”

    “Hapa kwangu…ukitaka nitakupa…”

    “Wanakodisha kwa shilingi ngapi?”

    “Elfu moja, ila wewe, nitakufanyia bure kabisa…” aliniambia.



    Jibu lake lilinipa uhakika juu ya kile nilichohisi juu yake. Sikutaka kukataa, nilikuwa na uhitaji mkubwa wa kukaa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuutafuta utajiri hivyo nilikubaliana naye. Akanipa mkeka na kunionyeshea sehemu ya kulala, nikaenda, nikautandika na kulala huko.



    Maisha yangu mapya yakaanza ndani ya kituo hicho, nilishinda nikiwa huko, sikutoka kwani mambo mengine nilikuwa nikiyafanya humohumo ndani. Mwanaume huyo aliyeitwa Dickson akanitafutia biashara ya kuuza ya kuuza magazeti, kweli nikaanza kuifanya na kuingiza kiasi kidogo cha fedha, hichohicho ndicho nilichokitumia kwa matumizi mengine.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dickson alinionyeshea upendo wa ajabu, alionekana kuwa miongoni mwa wanaume waliokuwa na uvumilivu mkubwa. Hakuniambia suala lolote la kimapenzi, wakati mwingine nilikuwa nikijiuliza sababu ya yeye kunisaidia, kwa nini mimi? Je hali ingeendelea hivyohivyo au mwisho wa siku angebadilika.



    Mwezi wa kwanza ukapita, nilikuwa nikiendelea kuishi ndani ya kituo hicho na kwa kweli sikuwa nimetokea. Ninayokuandikia hapa unaweza ukashangaa lakini ukweli ulikuwa huo. Ulipoingia mwezi wa pili, Dickson akashindwa kuvumilia, akaniambia ukweli kwamba alikuwa akinipenda na alitaka kunioa.



    “Kunioa mimi?” niliuliza.



    “Ndiyo!”



    “Hapana! Haiwezekani…”



    “Kwa nini?”



    “Dickson, nipo tayari kwako kwa kila kitu isipokuwa mambo mawili tu,” nilimwambia pasipo kumuonea aibu.



    “Mambo gani?”

    “Sitaki unioe na sitaki uzae nami, ila mengine yote ruksa…” nilimwambia bila kupepesa macho.



    Akatabasamu kidogo na kuniangalia kwa macho yaliyoonyesha kama mtu aliyetaka nirudie kauli zangu. Hakuniambia kitu zaidi ya kuondoka kuendelea na shughuli zake huku mimi nikiendelea kuuza magazeti.



    Ilipofika usiku, akaniita alipokuwa akilala na kunitaka nimpe kampani kwani usiku huo ulikuwa na baridi kali hivyo nikakubaliana naye na kwa mara ya kwanza kukutana naye kimwili. Moyoni sikuumia, sikujuta kwani tangu nimeingia Dar es Salaam ndiye aliyeonekana kuwa msaada wangu mkubwa.



    “Zakia…” aliniita kwa sauti ya uchovu.



    “Abee mpenzi…”



    “Nataka uwe tajiri kama unavyosema, upo tayari?” aliniuliza huku akiuweka mkono kifuani kwangu. Kabla ya kujibu, nikaachia tabasamu pana.



    “Nipo tayari!”

    “Kweli?”

    “Ndiyo mpenzi! Nimesafiri kutoka Morogoro kuja hapa kwa ajili hiyo tu…” nilimwambia.



    “Basi subiri..kesho kuna mtu atakuja, mwambie kila kitu,” aliniambia.



    “Anao utajiri?”

    “Hana ila ukitaka, anakupa?”

    “Kweli?”

    “Hakika!” aliniambia huku akiongeza tabasamu usoni mwake. Nikawa na uhakika wa kuuupata huo utajiri.



    Nilikaa pale Ubungo na kuanza kumsubiria Dickson ambaye aliniambia asingechukua muda mrefu mpaka kurudi mahali hapo. Kama nilivyokwambia kwamba nilikuwa na presha kubwa, hakukuwa na kitu kingine nilichokifuata jijini Dar es Salaam zaidi ya utajiri tu, hivyo kuniambia kwamba angerudi akiwa na mtu ambaye angenifanya nitajirike, kwangu ilikuwa furaha tele.



    Nilikuwa na presha kubwa, kila wakati nilikuwa nikiangalia saa yangu, hakukuwa na siku ambayo niliona mshale wa dakika ukienda taratibu kama siku hiyo, nilikuwa na presha kubwa na kitu nilichokitaka kwa wakati huo ni kuonana na huyo mtu na kumwambia kile nilichokitaka.



    Baada ya kusubiri kwa saa tatu ndipo Dickson akarudi huku akiwa na huyo mtu. Alikuwa mwanaume mtu mzima, mwenye ndevu nyingi ambaye alionekana kuwa wa kawaida sana kiasi kwamba nikashangaa, iweje mtu huyo anipe mimi utajiri na wakati yeye mwenyewe alionekana kuwa mtu wa kawaida sana.



    Wakati nikijiuliza hayo yote, mwanaume huyo, hata kabla ya kuzungumza nami, akatoa tabasamu pana usoni mwake, tabasamu lililoonyesha matumaini makubwa kwamba nisiwe na wasiwasi kwani tayari nilipata nilichokitaka.



    “Naitwa bwana Hassani Mudi…” alijitambulisha huku akiniangalia kwa uso wenye tabasamu hilo pana.



    “Naitwa Zakia…” nilimwambia, na mimi nikatoa tabasamu pana vilevile.



    Dickson akaanza kuniambia kwamba huyo ndiye alikuwa mtu aliyeniambia kwamba ningepata utajiri kupitia yeye, nilipomwangalia, bado nilikuwa na maswali mengi ambayo yote hayo hayakuwa na majibu yoyote yale.



    Huyo mzee akaniambia niende naye pembeni kwani suala ambalo nililitaka halikuwa la kulizungumzia juujuu, ilitakiwa tutulie sehemu na aniambie kila kitu, nikakubaliana naye hivyo Dickson kutulia pembeni akitusubiri.



    “Kweli unataka kuwa tajiri?” lilikuwa swali lake la kwanza kuniuliza.



    “Ndiyo!” nilimjibu huku nikionekana kumaanisha nilichomwambia.



    “Kweli?” aliniuliza.



    “Ndiyo!”

    “Sidhani kama unataka utajiri…” aliniambia.



    “Kweli tena, nataka kuwa tajiri…” nilimwambia kwa sauti yenye msisitizo kabisa.



    “Zakia, huna moyo, huna moyo, unaonekana tu…”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Moyo ninao, nipo tayari kwa lolote lile.”



    Niliposema hivyo, yule mzee akaanza kucheka sana, sikujua alikuwa akicheka nini, sijui kama alifurahishwa na jibu langu au la. Nilibaki nikimwangalia kwa mshangao, yeye mwenye aligundua kwamba nilikuwa nikijiuliza mengi kuhusu kicheko kile.



    “Eti una moyo! Moyo gani na wakati unaogopa hata mende?” aliniuliza.



    “Siogopi mende…nimetoka Morogoro mpaka hapa kwa ajili ya kutafuta utajiri tu, jua kwamba nina kiu ya kuwa tajiri, nipo tayari kufanya lolote ili nipate huo utajiri,” nilimwambia.



    “Hata kuua?” aliniuliza.



    “Sidhani, ila nikiambiwa kwamba nikimuua huyu napata utajiri, nitaua tu, sitokuwa na budi,” nilimwambia.



    Nilichokuwa nikikiongea, nilimaanisha kutoka moyoni mwangu, kwa wakati huo nilikuwa tayari kwa lolote lile, kiu kubwa ya kuwa tajiri ilikuwa imenikamata. Mzee Hassani akaniambia kwamba jioni ya siku hiyo angenifuata hivyo nijiandae kwani kuna sehemu nilitakiwa kwenda naye, hilo halikuwa tatizo, nikakubaliana naye, akazungumza kidogo na Dickson kisha kuondoka, ndiyo kwanza muda huo ilikuwa saa saba mchana.



    Aliniacha na mawazo tele, kichwa changu kilivurugika kabisa, wakati mwingine nilikuwa namuamini huyo mzee kwamba angenifanya kuwa tajiri mkubwa lakini wakati mwingine nilikuwa na wasiwasi kwamba asingeweza kufanya hivyo.



    Kama kweli yeye alikuwa akitoa utajiri, kwa nini yeye mwenyewe hakuwa tajiri? Kama alikuwa akitoa utajiri, kwa nini Dickson hakuwa tajiri na wakati alikuwa rafiki wake wa karibu? Kila nilichojiuliza, nikawa na uhakika kwamba inawezekana mzee huyo alikuwa muongo.



    “Dickson…unamuamini kweli huyu mzee?” nilimuuliza Dickson.



    “Ndiyo!”



    “Kweli atanisaidia?”



    “Sana tu…kuna marafiki zangu kama watano, kawasaidia na sasa hivi ni matajiri wakubwa hapa mjini,” aliniambia.



    “Sasa kama yeye anatoa utajiri, kwa nini na wewe asikupe? Au hutaji kuwa tajiri?” nilimtupia swali.



    “Nataka!”



    “Sasa kwa nini hujamwambia akupe?”



    “Basi tu, nataka utajiri ule wa kuutafuta kwa nguvu zangu ili baadaye niwe na ushuhuda jinsi nilivyosota,” aliniambia huku macho yake yakionekana kuwa na jambo lililojificha.



    Sikutaka kujali sana, nilichokuwa nikikiangalia ni maisha yangu tu kwani kwenye ridhiki za kuwa na maisha mazuri, Mungu aliwapa wale waliokuwa na kiu kubwa kama niliyokuwa nayo kipindi hicho.



    Basi baada ya saa kadhaa, mzee Hassani akarudi mahali hapo na kukutana naye. Akanichukua na kuanza kuondoka naye mahali hapo. Kumbuka kwamba kwa kipindi chote tangu nifike Dar es Salaam sikuwa nimetoka ndani ya kituo kile, hivyo kutoka humo ndipo nikaanza kuona mazingira halisi ya jiji hilo.



    Lilikuwa zuri, lililopendeza machoni mwangu.



    Mzee Hassani alifika na gari lake na kulipaki nje. Tulipotoka, tukapanda na kisha kuondoka, tulipoelekea kwa kipindi hicho sikuwa nikipafahamu ila kwa sasa, ninapajua mno, palikuwa ni Bunju.



    Njiani tulikuwa tukizungumza mambo mengi, katika kila sentensi aliyoongea ilionyesha alikuwa miongoni mwa watu waliojiamini kwa kila walichokuwa wakikifanya. Sikutakiwa kuwa na hofu hata kidogo.



    Tulikwenda mpaka tulipofika sehemu iliyokuwa imeunganishwa na barabara moja ya vumbi, tukaingia nayo, tulikwenda zaidi mpaka tukaanza kuingia sehemu iliyokuwa na miti mingi.



    Sikuwa na uhakika kama huko kulikuwa na watu walikuwa wakiishi, kulikuwa kimya sana, hatukusimama, tuliendelea kuifuata barabara hiyo ya vumbi mpaka kufika sehemu ambayo barabara ilifika mwisho, sasa tukaanza kuelekea katika njia ambayo hakukuwa na njia rasmi, nikaanza kushikwa na hofu, nikahisi kuna hatari mbele yangu! Mzee Hassani hakutaka kuzungumza tena, naye alikuwa kimya, macho yake yalikuwa mbele, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, ila kwangu, nilitamani nirudi. Eti huko ndipo kulipokuwa na utajiri! Nikasubiri nione nini kingetokea.



    ****

    Tuliendelea na safari mpaka tulipofika sehemu fulani ambayo ilikuwa na miti mingi na kwa mbali kulikuwa na nyumba ndogo ya udongo. Nilibaki na mshangao, sikuamini sehemu kama hiyo kungekuwa na mtu anaishi, niliogopa, wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa kwenye sehemu mbaya, yenye kutisha ambayo ingenifanya nitekwe na watu wenye roho mbaya.



    “Ila si natafuta utajiri, haina jinsi..” nilijisemea.



    Mzee Mudi akaniambia niteremke na tuanze kwenda kule kwenye kile kijumba, wakati natembea, mwili wangu ulikuwa unatetemeka mno na wakati mwingine nilihisi ningeweza hata kuanguka.



    “Mbona unatetemeka?” aliniuliza.



    “Hakuna kitu.”



    “Kweli?”



    “Ndiyo!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Japokuwa nilimficha lakini nilikuwa na uhakika kwamba alinigundua. Tuliendelea kusogea mbele mpaka tulipokifikia kijumba kile ambapo akaniambia kwamba hatukutakiwa kuingia moja kwa moja bali tulitakiwa kusubiri nje, tukafanya hivyo.



    Baada ya dakika kama mbili, tukasikia sauti ndani ikitukaribisha, tukasimama na kuanza kuingia ndani. Huko, tulimkuta mzee mmoja, kwa kumwangalia harakaharaka, alikuwa na miaka kama sabini ila alikuwa amechoka sana kimaisha.



    Kichwa changu kikaanza kujiuliza, je, mzee yule angeweza kunifanya niwe tajiri kama nilivyotaka? Wakati najiuliza hayo, nikashangaa mzee yule akisimama na kunishika kichwa changu.



    “Usijiulize swali hilo, nitakufanya kuwa tajiri mkubwa sana,” aliniambia huku akiwa amenikazia macho.



    Kwanza nikashtuka, ilikuwaje ajue kile nilichokuwa nikijiuliza, mpaka hapo, nikajua kwamba huyo mzee alikuwa na nguvu za ziada. Nikatulia na kumwangalia usoni. Kwa jinsi chumba kile kilivyokuwa, kiliniogopesha mno, kulikuwa na tunguli kila kona, harufu mbaya ambayo ilinifanya kutamani kuziba pua zangu.



    “Unataka kuwa tajiri?” aliniuliza mzee huyo.



    “Ndiyo!”



    “Una uhakika?” aliniuliza.



    “Ndiyo mzee!”



    “Utayaweza masharti?” aliniuliza.



    “Nitayaweza tu..”



    Mzee yule akasimama na kuanza kuimba nyimbo ambazo sikuwa nikizielewa kabisa. Hakuishia kuimba tu bali akaanza kucheza pia. Nilibaki nikimwangalia, sikutaka kuzungumza kitu chochote kile kwani hata nguvu ya kufanya hivyo sikuwa nayo.



    Akanisogelea na kunipaka unga fulani machoni mwangu. Ulikuwa na rangi nyeusi, alipoyapaka macho yangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti moyoni mwangu, furaha kubwa ambayo sikuwahi kuipata maisha yangu yote.



    “Unajisikiaje?” aliniuliza.



    “Najisikia vizuri….”



    “Unahitaji utajiri wa aina gani? Wa kuku na mahindi au wa milele?” aliniuliza swali ambalo sikuwa nikilijua kabisa.



    “Sijajua upo vipi!”



    Mzee Mudi ndiye akachukua nafasi hiyo na kuanza kuniambia tofauti ya utajiri hiyo aliyoniambia mzee huyo. Utajiri wa kuku ulikuwa ni kwamba kuku anatupiwa mahindi chini, anaanza kula, kama akila mahindi matano, basi utajiri wako utakuwa ni wa miaka mitano, kama akila mahindi ishirini, basi utajiri wako utakuwa wa miaka ishirini, baada ya hapo unafilisika na kufa.



    “Hapana huo siupendi!” nilimwambia mzee Mudi.



    “Kwa nini? Huo ndiyo mzuri!”



    “Mimi nautaka huo mwingine.”



    “Unaujua upo vipi?”



    “Sijui, ila nautaka huohuo!” nilimwambia.



    Utajiri niliosema kwamba niliutaka ulikuwa ni wa masharti makubwa. Niliambiwa hilo lakini nikasema kwamba nautaka huohuo na kama ni masharti nitayafanya yote lakini si kukubali ule wa mwanzo wa kuwa tajiri kwa kipindi fulani kisha kufa.



    “Huu una masharti makubwa mawili,” aliniambia mganga.



    “Yapi?”



    “Moja, unatakiwa kuwaua wazazi wako wote wawili,” aliniambia huku akikishika kitunguli kidogo kilichokuwa pembeni yake.



    “Kuwaua wazazi wangu?”



    “Ndiyo!”



    “Na sharti jingine?” niliuliza huku nikionekana kuchanganyikiwa.”



    “Kufanya mapenzi na maiti ishirini..” aliniambia.



    ****



    Kwanza nikashtuka, sikuonekana kuamini kile alichoniambia, nikamuuliza mara mbilimbi alisemaje, yeye akaniambia vilevile kwamba nilitakiwa kufanya mapenzi na maiti ishirini kama nilitaka kuwa tajiri, hivyo nilitakiwa kuchagua.



    “Umechagua nini?”



    “Kati ya nini na nini?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kuwaua wazazi wako au kufanya mapenzi na maiti ishirini?” alinijibu kwa kuniuliza swali.



    “Bora nifanye mapenzi na maiti ishirini…” nilimwambia japokuwa niliogopa mno.



    Alichokifanya mzee yule ni kuchukua unga mwingine na kunipaka usoni kisha kuniambia nitulie kwa muda. Nilitulia hapohapo, sijui nini kilitokea, ghafla, nikajikuta nikitokea katika hospitali moja kubwa hapa jijini Dar es Salaam, nilishangaa, nilijiuliza nilifikikaje mahali hapo lakini sikuwa na jibu lolote lile.



    Kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakiendelea na shughuli zao, wagonjwa waliokuwa wakiingia na kutoka. Ghafla, nikasikia sauti ya yule mzee ikiniambia kwamba nilitakiwa kwenda mochwari, sikujua ilikuwa wapi lakini nikajikuta nikijiongoza mpaka kufika katika mlango ambao uliandikwa MOCHWARI kwa nje.



    “Subiri hapo mpaka usiku,” niliisikia sauti hiyo.



    Nilifanya kama nilivyoambiwa, nikasubiri mahali hapo. Ilikuwa jioni kama saa kumi na moja hivi. Hakukuwa na mtu aliyeniona, wengi walinipita bila kunisalimia. Ilipofika saa moja usiku, nikasikia sauti ile ikiniambia niende ndani ya mochwari ile, maelekezo mengine angeniambia, nikafanya hivyo na kuanza kuingia humo ambapo kulikuwa na masanduku mengi yaliyokuwa na maiti nyingi. Nikaambiwa nisubiri. Nakuja kutahamaki, eti ilikuwa saa sita usiku. Nikabaki nikitetemeka tu.



    *****



    Ulikuwa usiku mkubwa, nakiri kwamba hakukuwa na sehemu iliyokuwa inatisha kama ilivyokuwa mochwari. Ndani ya mochwari ile, kulikuwa na majeneza ya maiti ambazo zililetwa humo ndani na nyingine tayari kwa kuchukuliwa lakini pia kulikuwa na masanduku mengi ambayo ndani yake kulikuwa na maiti, baridi lililokuwa humo ndani, lilikuwa kubwa mno.



    Humo kulikuwa na walinzi wawili, walikuwa wakilinda, nilijiuliza walipata wapi ujasiri wa kuwa ndani ya chumba kile, tena usiku mzima huku wakionekana kutokuwa na hofu hata kidogo.



    Mimi, sikuwa nikionekana, yaani hata niliposogea karibu yao, hawakuwa wakiniona zaidi ya kufanya vitu vyangu. Humo, ndipo nilipojifunza kwamba kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa yakitokea.



    Niliwaona watu wakija usiku huohuo, walikuwa wakizungumza na walinzi hao na kuwaambia shida zao, wengine walifika kwa kuwa walihitaji baadhi ya viungo kutoka kwa maiti ili waende kufanya mambo yao ya kishirikina.



    Nilimuona mlinzi mmoja akitoka na kwenda kwenye sanduku moja, akalivuta kisha kuanza kuitoa maiti iliyokuwa humo ndani. Mwili wangu ulisisimka mno, sikuamini nilichokuwa nikikiona, hofu ilinijaa moyoni mwangu.



    Mlinzi yule akaivua nguo maiti ile, sikujua alichokuwa akikihitaji, yale mambo ambayo nilikuwa nikiyasoma kwenye vitabu vya kusisimua, siku hiyo nilikuwa nikiyaona kwa macho yangu.



    Akachukua kisu ambacho alikihifadhi sehemu maalumu, nyuma ya mlango na kisha kuanza kukata kifundo cha mguu cha maiti ile kwani ndicho kilichokuwa kikihitajika kwa hali na mali.



    Ninayoyazungumza hapa, niliyashuhudia kwa macho yangu. Mapigo yangu ya moyo yalikuwa juu mno, japokuwa kile kilikuwa kikifanywa kwa maiti lakini niliogopa na kuionea huruma, niliona kama ilikuwa ikionewa.



    Alipomaliza, mlinzi akakichukua kifundo cha mguu ule na kisha kumpa mwanaume aliyekuwa amekifuata na kuondoka nacho. Walinzi waligongesheana mikono, kila mmoja alionekana kuwa na furaha.



    Wala haukupita muda mrefu, nikaona mlinzi mmoja akitoka nje. Sikutaka kubaki ndani, wakati namsubiria yule mganga, nilitaka kujua ni kitu gani kingine kilichokuwa kikitokea.



    Nilimfuata mlinzi, alikwenda moja kwa moja kwenye gari moja ya kifahari, Range SUV nyeusi na kuongea na mtu aliyekuwa humo ndani. Nilisogea kwani nilitaka kuyasikiliza mazungumzo yao.



    “Nahitaji maji ya maiti,” alisema mzee aliyekuwa humo ndani ya gari.



    “Laki mbili! Hela ipo?” aliuliza mlinzi yule.



    “Ipo! Naomba ukaniwekee humu!”



    Yule mzee sikuweza kumfahamu kwa kipindi kile lakini sauti yake, hapo baadaye nilimfahamu kwani nilikutana naye mara kwa mara. Baada ya kuzungumza hivyo, akatoa kidumu na kumpa mlinzi yule ambaye akakichukua na kuondoka nacho.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sikutaka kubaki hapo nje, nikamfuata mlinzi mule mochwari alipokwenda. Nilipoingia, nikakuta akimwambia mwenzake kwamba kulikuwa na dili jingine, kuna mtu alifuata maji ya maiti.



    “Hakuna tatizo! Twende kule kwenye maiti za wiki iliyopita!” alisema mlinzi aliyeletewa taarifa.



    ****





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog