Search This Blog

NYUMBA YETU,NYUMBA YA WACHAWI - 1

 







    IMEANDIKWA NA : DENIS BENARD



    *********************************************************************************



    Simulizi : Nyumba Yetu, Nyumba Ya Wachawi

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Ni asubuhi na mapema kijana Faluu amelala huku manyunyu yakiwa yanapiga kwa mbali,ilikua ni asubuhi iliyojaa mvuto saana maana ilitokea kupamba usingizi wa Faluu na kufanya iwe ngumu sana kwake kuachia shuka na kuingia katika mahangaiko ya maisha,wakati akiwa katikati ya ndoto Faluu    aliamshwa na mama yake ili awahi shambani,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Faluu mwanangu kumekucha sasa amka uende shambani’’



    (kwa sauti ya uchovu Faluu alijibu)



    ‘’Mmh!!,sawa mama ngoja niamke ila mwili wangu umechoka sana’’



    ‘’Jitahidi mwanangu maana kadiri unavyowahi kwenda shambani,ndivyo utakavyowahi kurudi’’ mama aliongea kwa upole sana na kumtia moyo mwanae



    ‘’Sawa mama..’’aliongea Faluu.



    Baadae aliamka na kujiandaa na kisha alimuaga mama yake huku nafsi yake ikiwa na wasiwasi sana..

    ‘’Haya mama yangu mimi naenda shambani,ubaki salama..Ilaa! Basi tutaongea baadae’’aliongea Faluu.



    Kitendo kile kilimfanya mama yake kutomuelewa Faluu juu ya nini anachokimaanisha,ilibidi amuulize…

    ‘’Usiondoke kwanza,embu niambie kulikoni mbona sikuelewi??’’ aliuliza kwa shahuku kubwa sana ya kutaka kujua nini mwanae anafikiria..



    ‘’Hamna mama kawaida,tutaongea baadae ,ngoja niende shambani’’Faluu alijibu



    Maneno yale yalimfanya mama yake Faluu kua na wasiwasi juu ya nini mwanae anamaanisha,hivyo ikambidi aendelee kumdadisi mwanae..CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ‘’Embu nieleze mimi mama yako ilinijue nini unafikiria mwanangu,kwa sababu unanifanya niwe na wasiwasi sana mama yako’’

    (kwa uchungu sana,Faluu alijibu)

    ‘’Sawa mama yangu najua,lakini naomba usiwaze sana,ni hivi najikuta akili yangu haiko sawa sana  kukuacha wewe peke yako mama yangu mpendwa’’



    (Mama alicheka sana)

    ‘’Yaani mwanangu  unakua na wasiwasi kwa sababu ya kuniacha hapa nyumbani mimi peke yangu??kwani leo ndio mara ya kwanza,embu usiwe hivyo,nenda tu mimi nitakua salama sawa mwanangu’’



    (Huku akiwa na tabasamu,Faluu alijibu)

    ‘’Sawa mama,mimi naenda,ubaki salama eeh mama yangu’’aliongea Faluu na baadae aliondoka.

    Kutokana na maongezi yale,yalimfanya Faluu achelewe kufika shambani ,maana mpaka jua la saa moja na nusu asubuhi linatoka alikua bado hajafika shambani.Lakini pamoja na faraja zote za mama yake,alijishangaa sana pale ambapo alijikuta akiingiliwa na mawazo mabaya katika kichwa chake.



    ‘’ Hivi mbona nakua katika hali hii??,kitu gani kinaendelea?? Na mwili wangu unakua mchovu hivi??’’ alijikuta akiwa na awazo sana.Alifika shambani na bila kupoteza muda alianza kufanya kazi yake.



    Ilipofika saa nane mchana,alijikuta kichwa chake kikiwa kizito sana na macho yake yaliacha kuona mbali, ghafla alipoteza fahamu .Wakati akiwa amepoteza fahamu katika shamba lile walitokea viumbe wa ajabu wakamchukua na kumpeleka  barabarani na katikati ya viumbe kulikua na kiongozi wao ambaye



    (aliongea maneno haya kwa sauti ya kutisha sana )

    ‘’Baada ya mambo yote ya msiba kuisha hakikisha unaenda kwa mjomba wako,hayo ndiyo maneno ya mwiso nilioachiwa na mama yako” huyo kiumbe aliongea na baada ya hapo walipotea na kumuacha Faluu pale barabarani peke yake. Baada ya muda wa dakika kadhaa alipita jamaa mmoja katika eneo lile,alishangaa sana alipoona mtu kalala mbele yake na hivyo ikamfanya asogee ili ajue nini na ni nani kimemkuta mtu Yule…



    ‘’ Nani Yule na kwa nini kalala pale ?? ‘’alijiuliza na kuongeza mwendo ili afike haraka katika eneo lile alipokua amelala na alipokaribia alishtuka sana kumuona Yule…



    ‘’ Heeee! Kumbe ni Faluu rafiki yangu, sasa kafanyaje ?? ‘’ alijiuliza na kumkimbilia ili ajue nini kimemkuta.



    ‘’ Faluu ! Faluu! Faluu rafiki yangu nini tena kaka?? ‘’ aliongea Yule kaka kwa sauti ya uchungu sana. Baada ya muda kidogo Faluu alishtuka sana..



    (Kwa mshtuko mkubwa sana ,Faluu aliongea)

    ‘’ Mama yangu , Mama yangu ! “ aliongea  Faluu na  baadae alikimbia kutoka eneo lile na  kumuacha Yule kaka pale………CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Baada ya Faluu kukimbia,alimuacha Yule kaka pale huku akibaki kumshangaa asijue nini cha

     kumsaidia.



    ‘’ Huyu nae kawa kichaa nini ? Mbona anafanya mambo ya ajabu? ,aah! Shauri yake ! ‘’ alijiongelea Yule kaka na baadaye aliondoka kuelekea kwao.



    Baada ya Faluu kukimbia akielekea kwao, alikua kama mtu aliyechanganyikiwa na kwa wakati huo wote ile sauti aliyoisikia wakati akiwa amepoteza fahamu ilikua ikimrudia katika mawazo yake..

    ‘’ Hapana !! Itawezekana vipi yale maneno niliyoyasikia ?? , Haiwezekani !! “ alijiongelea na kutokana na maneno yale,Hasira ilimpanda na kujikuta akiongeza mwendo ili akajue ukweli wa kinachoendelea. Wakati akiwa njiani,alikutana na watu wengi na wengi wao walikua wanamfahamu  Faluu,walijitahidi kumzuia ili waongee naye..



    (Walitanda njiani ,huku sura zao zikiwa zimetawala uzuni )



    ‘’ Na nyie hapo shida yenu nini?? Mbona mmezuia njia mimi nisipite ??’’ Faluu aliwauliza…



    ( Mmoja wao alisogea mbele na kisha akapiga magoti )



    ‘’ samahani ndugu yetu, tunaomba utuisikilize japo kidogo ‘’ yule mtu aliongea



    ( Kwa pamoja wote waliobaki , walijibu)



    ‘’  Kweli kaka tunaomba utusikilize ‘’



    Kutokana na maombi ya wale watu , Faluu ilibidi atulie na awasikilize wale watu shida yao..

    ‘’ Enhe nawasikiliza , mnaweza kuongea ….’’ Alijibu Faluu



    Baada ya Faluu kuongea vile , alijikuta Jadhiba ikipungua na kutaka kuwasikiliza wale watu nini shida yao.

    ‘’ Tunaomba tusogee pembeni kidogo ili tuongee, si unajua hapa njiani ‘’ aliongea mtu mmoja. Lile swala la kusogea pembeni lilimpa wasiwasi kidogo Faluu , maana sehemu aliyokua akielekezwa wasogee waongee ilikua ni porini .



    ( Faluu Akiwa na wasiwasi aliwaeleza)



      ‘’ Kwanini tusiongelee hapa hapa ?? ‘’ Faluu aliwauliza



    ( Huku wakiwa wanatabasamu mmoja alijibu )



    ‘’ Hamna kaka hapa naona tunaongea tukiwa hatuna uhuru , mimi naona tusogee pembeni kidogo ‘’

    Wakiwa wanajibizana katika ile njia , wale watu walianza kuhisi kama kuna mtu atapita muda si mrefu katika eneo lile , hivyo walipeana ishara na bila kupoteza muda Faluu alijikuta akiwa amebebwa juu juu na wale watu na wakaingia katika pori hilo..



    ( Faluu alianza kupiga kelele akihitaji msaada )



    ‘’ Jamani nisaidieni , nisaidieni sana jamani ! Nakufa mimi!! ‘’



    ( Wale watu walimjibu kwa jeuri )



    ‘’ Utajua tu ! ‘’ waliongea huku wakiwa wanazidi kuingia naye katika pori hilo..

    Kumbe wakati Faluu akipiga kelele , kuna mtu msamalia mwema alimsikia , alikua ni yule mtu aliyemkuta amelala pale njiani..



    ‘’ Mmh ! ni nani huyu ?? nah ii sauti mbona kama inafanana na ya Faluu ?? ‘’ alisogea mpaka karibu na sehemu walipokua wamesimama, kabla hawajaingia naye katika pori..



    ‘’ Halafu inaonekana hii miguu walikua wamesimama hapa na kama sio kusimama , basi walipita eneo hili  ,  sasa mimi nitafanyaje ??kumsaidia‘’ yule kaka alikua akijiongelea na baadae mawazo yalimjia aingie ndani ya lile pori..



    Wakati yule kaka mawazo yakimjia afatilie ili ajue nini kinaendelea , na wale watu hisia ziliwapelekea kama kuna mtu anakuja kuwafatilia , hivyo walijikuta wakiwa makini sana..

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ‘’ Oya sasa tunafanyaje ? maana hapa kuna mtu anakuja nyuma anatufatilia ‘’ aliongea mmoja.



    ‘’ Hatari sana ,maana inaonekana mtu mwenyewe yuko kasi sana ‘’mwingine alijibu.



    ‘’ Mimi naona tuongeze mwendo hadi katika lile shimo letu kule ‘’ kiongozi wao aliongea



    (Kwa pamoja walijibu)



    ‘’ Sawa mkuu ,inabidi tuwahi ‘’



    Wakati maongezi yao yakiendelea , Faluu alikua akiwafatilia sana na kumfanya kua na hofu sana na maisha yake na kitu kikubwa zaidi ilikua ni hali ya mama na taarifa alizozipata..



    (Kwa unyonge alijibu )



    ‘’ Hivi jamani mimi nimefanya nini ?? , huku mnanipeleka wapi ?? na nini maana yenu ? ‘’



    ‘’Unajifanyab unaongea kinyonge , wewe subiri hata usiwe na haraka utajua tu sawa , punguza maneno ,kwanza sehemu yenyewe tumeshafika mshusheni hapo ‘’aliongea mtu mmoja. Baada ya huyo mtu kuongea hivyo hawakumchelewesha ,walimshusha na moja kwa moja walimtupa katika shimo moja kubwa sana na kiongozi wao aliongea neno moja…



    ‘’ Wachawi ! wachawi ! na huo ndio mwanzo tutajua tu ,twendeni ‘’ Wakati wanageuka na kuondoka ,walikutana uso kwa uso na yule kaka Msamalia mwema………..



    Wakati watu wale wanageuka walikutana uso kwa uso na Yule kijana akiwa anafatilia ni sehemu gani yule mtu atakua anapelekwa.Kitu kile kiliwashtua sana na sio wao tu hata yule kijana naye alipata mashaka kutokana na mazingira yao na pande zote  mbili zilijikuta zikishindwa kufanya kitu chochote kwa wakati ule.



    (Wale vijana walibaki wakijinong’oneza )



    ‘’Mkuu tunafanyaje sasa?, maana tunaona kama huyu mtu sio salama sana kwetu,embu sema kitu chochote’’

    (Mkuu wao alitikisa kichwa na kuongea neno moja tu)



    ‘’Hana lolote huyu,nyie muacheni ‘’ aliongea na baadae waliendelea na safari yao, huku wakiwa na maongezi binafsi.



    Katika kipindi chote hicho,Yule kijana alikua akiwaangalia huku nguvu zikiwa zimemuisha na zaidi wasiwasi ulikua ni juu ya mazingira waliyokutana  kule msituni,hivyo hakua na namna nyingine ya kufanya pale.



    (Huku akitetemeka alijiongelea)



    ‘’Mmmh! Hawa ni akina na nani na mbona nimewakuta huku porini ,halafu ndiko sauti ile ilikoelekea?, bila shaka huku kutakua na namna tu! Mh!,ila bora wameondoka,maana ilikua hatari sana hapa”alijiongelea huku akiwa anapumua sana.



    ‘’Ila hapa cha msingi nianze kumtafuta huyu mtu na nina amini hawa hawa ndio watakua wanafanya,lakini pia watakua wametoka wapi?,maana sura zenyewe ngeni sana katika macho yangu na ninafikiri hata kwa kijijin ni wageni pia’’ alikua akijiongelea tu mwenyewe huku asijue jibu gani ni sahihi kutokana na maswali aliyokua akijiuliza mwenyewe na mwisho wa siku aliyapuuzia na kuendelea kusonga mbele huku akimtafuta Faluu huku na kule ili ajue hatima yake.



    “Faluu !Faluu! Faluu!Faluu!....’’ na kwa mbali alihisi kama kuna mtu aliitikia sauti sauti yake na wakati huo Alikua anatembea huku akiita.Lakini kipindi hicho alikua amesonga mbele kwa muda mrefu sana huku akiita jina la Faluu yeye ,kutokana na mabadiriko ya hali yake,alianza kuhisi kama kuna mtu alikua anamfatilia kwa nyuma huku akimpulizia upepo kwa nyuma.Kitu kile kilimfanya ageuke nyuma,Alipogeuka nyuma hakuamini maana alikutana na lile kundi la wale watu,kumbe muda ule hakuondoka na badala yale walifika mbele na kurudi huku wakimfatilia ili wajue lengo lake nini katika msitu ule.



    (Alitetemeka sana pale)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ‘’Sasa wakubwa mimi nimefanya nini ?mbona mnanifatili?’’aliuliza huku haja ndogo ikimtoka.

    Wenyewe walibaki wakimshangaa tu huku wasimjibu kitu chochote,



    ‘’Mkuu embu ongea tumfanye nini huyu?’’mmoja aliuliza



    Mkuu wao hakumjibu kitu na badala yake alimsogelea huku yule jamaa akirudi nyuma na alipomkaribia alimpuliza kama karatasi akajikuta akipeperuka angani na baada ya dakika mbili alijikuta akitokea kwao,Alijishangaa sana maana hakuamini yale yaliyotokea kule na hayo aliyofanyiwa,hicho ndicho kilichompa hofu sana na wakati akijishangaa alisikia sauti ikimueleza.



    ‘’Sikiliza wewe!leo umepona ila onyo kwako,uliyoyaona huku usimueleze mtu yeyote,tena sikiliza!Usimueleze mtu yeyote!!, sina mengi ila ni matumaini yangu umenielewa,huwasirudii mara mbili,sasa ukitaka kuona kitu gani nitafanya katika maisha yako,wewe fanya hivyo”Mara baada ya muda ile sauti ilikata katika masikio yake.



    Kutokana na Sauti ile,ilimfanya aanze kukuna masikio yake,maana hakuelewa maana yake nini na ndipo alipoamua kutoka nje ya nyumba yao ili ajichanganye na watu walau apunguze mawazo yaliyokua katika kichwa chake.Wakati anatoka nje alianza kusikia sauti za watu wakilia,sauti zile zilimfanya aanze kua na wasiwasi sana maana hakujua nini sababu za watu hao kulia na ndipo aliposogea kwa watu waliokua karibu na maeneo ya nyumbani kwao ili awaulize kulikoni.



    (Kwa shauku kubwa aliuliza)



    ‘’Enhe jamani za samahani nasikia kuna watu wanalia,wapi huko ??’’huyo kijana aliuliza



    ‘’Tulia dogo Elly,wenzio wanapofika maeneo yoyote kabla hawajaanza kuongea chochote,huwa wanasalimia ,kua na heshima mdogo wangu”mtu mmoja aliongea,Kutokana na majibu yale yalimkata usemi kidogo hasijue kitu gani cha kujibu .



    (Kwa sura ya upole alijibu)



    ‘’Samahani sana kaka,si unajua maisha na kuchanganyikiwa, naomba unisamehe sana , Shikamoo !”alijibu Elly



    (Huku akitabasamu mtu yule aliongea)



    ‘’Hayo ndio maneno mdogo wangu , sasa hapa ndio tunaweza kuongea sasa , Huko kwenye msiba ni kwao rafiki yako “alijibu yule mtu.



    (Kwa sura ya mshangao ,Elly aliongea)



    ‘’Kwao rafiki yangu ? , Rafiki yangu gani huyo ?’’aliuliza Elly



    ‘’Usijifanye hujui bhana ,’’ aliongea yule mtu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ‘’Kweli tena kaka , ni nani?’’ aliongea Elly



    ‘’Inawezekana hajui, wewe mueleze tu”alidakia mtu mwingine aliyekuwepo maeneo yale. Wakati huo maongezi yale yakiendelea, Mwili wa Elly ulikua ukizidi kupanda joto kwa kasi sana.



    ‘’ Ni hivi punguza presha , mama yake na rafiki yako Faluu amefariki dunia kwa kuchomwa na moto katika nyumba yake na watu wasio julikana kwa kisingizio cha uchawi’’ yule mtu aliongea.



    (Kwa mshtuko mkubwa sana Elly aliongea)



    ‘’ Unasemaje wewe? Mama yake…! Na Faluu..! kafariki dunia kwa kuchomwa na moto, inawezekana vipi ?’’aliongea Elly



    ‘’Ndio hivyo bhana ! ‘’ alijibu yule mtu pale.

    Kutokana na presha upande wa Elly kupanda , nguvu zilimuishia na pale pale alianguka na kupoteza fahamu…………..



    Machozi ya Elly yaliwafanya watu wote watulie na kubaki wakimuangalia yeye, kwa maana aliwashangaza sana na kila mtu alijikuta akiwa na maswali sana katika ufahamu wake,ya kwanini Elly analia?



    ‘’Elly mwanagu mbona hatukuelewi?kulikoni?’’ mama mmoja alimuuliza.



    ‘’Mmmh, hamna mama’’ alijibu Elly huku akifuta machozi



    ‘’Hapana mwanangu unatuongopea sisi wakubwa wako au awepo mama yako? ,mbona unaonekana kama kuna kitu kinaendelea katika mawazo yako?’’aliongea yule mama.



    Wakati akitaka kujibu,alitokea  mama yake pale, Elly alijikuta akisimama na kumfata mama yake mlangoni alipokua anaingia huku akilia…



    ‘’Mama yangu hapana! Mama mmh! Mama hapana!’’aliongea Elly huku akilia sana baada ya kumuona mama yake.



    ‘’Mwanangu kulikoni?mbona sikuelewi?nini kinaendelea? Nini kimekusibu mwanangu,embu niambie mwanangu’’ aliongea mama yake.



    Wakati huo Elly akiwa anaongea na mama yake kitendo cha yeye kulia na kuanza kuongea yale maneno,kilifanya wale watu waliokua mle katika chumba alichokuwepo Elly kuzidi kupata wasiwasi maana walishindwa kumuelewa Elly nini anachokimaanisha..



    ‘’Elly embu ongea chochote basi unajua hapa tulipo unatupandisha presha tu’’aliongea yule kaka aliyekuwa amempeleka hospitali.. Lakini Elly aliishia kumuangalia tu huku akilia.



    ‘’Elly baba si uongee tu mwanangu ,embu sema chochote basi tunakusikiliza’’aliongea mama yake.

    ‘’Mama na ndugu zangu wote hapa.. mmh…’’aliongea Elly huku akitaka kuwaeleza nini kinachoendelea, lakini ghafla ilimjia ile sauti ya yule mtu kule porini



     ‘’Sikiliza wewe!leo umepona ila onyo kwako,uliyoyaona huku usimueleze mtu yeyote,tena sikiliza!Usimueleze mtu yeyote!!, sina mengi ila ni matumaini yangu umenielewa,huwasirudii mara mbili,sasa ukitaka kuona kitu gani nitafanya katika maisha yako,wewe fanya hivyo’’



    Maneno haya yalimfanya ashindwe kuendelea kuongea nini alichotaka kuongea, watu walibaki wakimshangaa nay eye akiwashangaa..



    ‘’ Ndugu yetu mbona huongei sasa na sisi tunakusikiliza wewe hapo’’ aliongea mtu mmoja



    ‘’Ni kweli Elly embu sema kitu basi,ndugu zako tunakusikiliza ‘’alidakia mtu mwingine pale



    ‘’Mwanangu vipi mbona huongei sasa? Embu ongea mama yako na kusikiliza, sema kitu baba yangu’’ aliongea mama yake.



    Katika kipindi chote hicho Elly hakuwajibu kitu chochote  zaidi ya kugeuka kwa kila mtu aliyekua anaongea wakati huo. Baada kama ya dakika 5 hivi alikuja yule muuguzi pale..

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ‘’Jamani saa hizi nafikiri mgonjwa wenu yuko salama, mnaweza kuondoka nae na ninaomba mpunguze sauti kidogo maana kuna wagonjwa wengine wamelala humu ndani’’ aliongea yule muuguzi.



    ‘’Sawa daktari asante sana kwa matibabu ya mtu wetu’’ aliongea yule kaka.



    Baada ya yote hayo hakuwa na jinsi ilibidi waondoke pale hospitali na kuelekea nyumbani huku wakiwa wanataka sana kujua nini anachofikiria Ellyn a baada ya hapo watu wengine walipungua na kuelekea msibani na wengine walifatana kwao Elly huku wakiwa wanamuuliza maswali ya hapa na pale lakini ilikua ngumu sana kwa Elly kuyajibu.



    Siku ile ilipita huku wakiwa bado hawajazika kwa lengo la kumsubiri mwanae Faluu ambaye walikua wakijua ameelekea shambani,lakini pia kutokana na hali iliyokua ikiendelea walianza kupata wasiwasi sana,siku ya tatu Elly alimuuliza mama yake..



    ‘’Mama hivi sababu ya kutokuzika mwili wa mama,mama yake Faluu ni nini?’’



    ‘’Wanamsubiri Faluu arudi,maana watu walisema alienda shambani’’ mama yake Elly alijibu.



    Baada ya Elly kusikia hivyo,alijikuta akilia sana na asiwe na kitu chochote cha kuongea..

    ‘’Wewe Elly mwanangu,ndio nini sasa?mbona unalia?kuna nini kinaendeleaa?’’aliongea mama yake Elly

    ‘’Mama samahani naomba uniitie Mwenyekiti na wajumbe wakijiji’’aliongea Elly



    ‘’Mwenyekiti? Na wajumbe? Kuna nini?’’ aliuliza  mama



    ‘’Wewe naomba uniitie tu mama yangu’’ Aliongea Elly huku akilia tena kwa sauti saana na watu waliokua wakipita nje ya nyumba yao walikua wakisikia na kujikuta wakiingia ndani..



    Nakutokana na majibu hayo,ilibidi mama awaite mwenyekiti na wajumbe wa kijiji ili waje kusikia  nini wanchoitiwa.Bila kuchelewa walifika pale ilikusikia sababu ya kuitwa,kulikua na watu wengi sana nyumbani kwa akina Elly..



    ‘’Enhe Elly tunakusikia kijana ..’’aliongea Mwenyekiti



    ‘’Mwenyekiti na ndugu zangu hapa,samahani sana kwa kuwapotezea muda ,nilichowaitia hapa nataka kuwaeleza wapi aliko Faluu’’aliongea Elly



    (Watu kwa mshangaoo)



    “Aaaaah,aliko Faluu!!!!’’



    ‘’Ndio ,juzi wakati natoka shambani juzi nilimkuta amelala barabarani,huku akiwa amepoteza fahamu, nilimuamsha lakini cha ajabu aliposhtuka alianza kutaja Mama! Mama! Mama! Na baadae akakimbia,nilimshangaa sana’’

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Enhe!ikawaje”aliongea Mwenyekiti.



    ‘’Nilimshangaa sana na baadae nikaendeleaa na safari yangu kuja huku nyumbani,nilipotembea mbele kidogo nikasikia sauti ya mtu anasema Wachawi! Wachawi            ! wachawi !,mimi nikatulia kufatilia sauti baada ya kusikia kwa makini ilikua nisauti ya Faluu,sikujua watu waliokua wamembeba na baadae ile sauti ilianza kupotelea Porini nikaanza kuifata’’aliongea Elly



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog