Search This Blog

URITHI WA BABU - 5

 





    Simulizi : Urithi Wa Babu

    Sehemu Ya Tano (5)



    “Kumbe babu yako alikuwa na mke jini, ndiyo maana alipata utajiri ghafla! Lakini hakuwahi kunieleza hata siku moja. Alikuwa msiri sana”

    “Huyo jini sasa amejitokeza kwangu na anataka nimrithi ili anipe utajiri aliokuwa nao babu yangu”

    “Sasa ulitaka nikupe ushauri gani?”

    “Nimkubalie au nimkatalie?”

    Mganga baada ya kutafakari aliniambia.

    Umefanya vizuri kuja kwangu. Mimi nitakupa ushauri mzuri”

    “Nitakushukuru sana”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Usikubali. Huyo jini atakusumbua sana na pengine atakuja kukuua. Sasa nimeanza kugundua kuwa hata babu yako aliuawa na huyo jini”

    Maneno ya mganga huyo yakanishitua.

    “Kumbe hivi viumbe vina madhara makubwa?” nikamuuliza

    “Wewe hujui tu. Hawa viumbe si wazuri. Uliona wapi jini akaolewa na binaadamu?”

    “Sijawahi kuona”

    “Sasa ujue kuwa hicho kitu hakiwezekani. Huyo jini anakilazimisha kwa nia mbaya. Amemuua babu yako, sasa anataka kukuua wewe”

    Nikabaki nimepigwa na butwaa la mshangao.

    “Wewe angalia vituko na miujiza aliyokufanyia ndipo utajua ana madhara ya kiasi gani”

    “Sasa nifanye nini ili niweze kuepukana naye?”

    “Njoo kesho asubuhi, nitajua jinsi ya kukusaidia. Huyo hawezi kuondoka mwenyewe mpaka nimuondoe mimi”

    “Sasa hapo kesho utakuja kumuondoa?”

    “Nitamuondoa na utaishi kwa usalama. Wewe ni binaadamu, wajibu wako ni kuoa binaadamu mwenzako mzae watoto na sio jini. Kama utaoana na jini mtazaa watoto gani? Mtazaa binaadamu au majini?”

    Mganga aliniuliza swali hilo lakini sikuwa na jibu. Nikaona kweli ushauri wa kumrithi yule jini haukuwa na maana.

    “Kama ulivyoniambia nitakuja kesho unishighulikie” nilimwambia mganga huyo kabla ya kuagana naye.

    Nilipoondoka nyumbani kwa mganga huyo niliona mawazo yake yalikuwa sahihi. Si tu ningejitafutia matatizo

    mimi mwenyewe kwa kukubali kuishi na jinni bali pia sikuwa na uhakika tungezaa watoto wa aina gani.

    Kama tungezaa watoto wa kijini wasingekuwa na manufaa kwangu na hata kama watoto hao wangekuwa ni binaadamu bado wasingekuwa binaadamu kamili, wasingeweza kuishi na watu wengine.

    Lakini kulikuwa na kitu kilichojificha ambacho nilikuwa sikijui. Nilikuwa sijui

    kwamba yale maneno ya yule mganga yalikuwa ni ya roho mbaya. Alikuwa akitia fitina ili mimi nisimrithi yule mwanamke wa kijini kwa kuona kwamba nitaidi utajiri wa bure.

    Lengo lake la kuniambia niende kesho lilikuwa ni kutafuta mbinu ili amchukue yeye jini huyo.

    Asubihi ya siku ya pili yake nikaenda tena kwa mganga huyo.

    “Sasa mwanangu unajua hii kazi haitafanyika hapa. Itafanyika shanbani kwangu. Itabidi twende shamba” akaniambia.

    “Sawa. Tunaweza kwenda. Gari lipo”

    Mganga akaandaa vifaa vyake. Akawachukua wasaidizi wake wawili ambao bila shaka alishawaeleza tunakwenda shamba kufanya nini.Tukaondoka na gari.

    Shamba hilo lilikuwa kule kule Chanika lakini lilikuwa mbali kidogo. Akaniambia tuingize gari ndani ya shamba hilo. Nikaliingiza gari na kulisimamisha mbele ya nyumba yake ya miti na udongo iliyokuwa katikati ya shamba.

    Tukashuka na kuingia kwenye ile nyumba.

    Kwa jinsi nilivyofahamu baadaye ni kuwa ili aweze kumchukua Maimun alitaka kwanza aniue mimi na ndiyo madhumuni ya kunipeleka huko shamba.

    Baada ya kuniua alitaka achukue damu yangu na kuioga mwilini mwake kisha ajipake mafuta ya waridi.

    Tulipoingia kwenye ile nyumba nikaambiwa nikae chini. Kwanza kilianza kisomo. Nilisomewa na watu watatu bila

    kuambiwa ninasomewa nini.

    Baada ya kisomo hicho mganga alikoroga dawa kwenye kikombe akanipa ninywe.

    “Kunywa hii dawa” alinaimbia kisha akaongeza.

    “Nitakupa na dawa nyingine ya kuoga”

    Kumbe ile haikuwa dawa. Ilikuwa sumu! Alitaka niinywe ili nife pale pale na kisha wanitoe damu kabla haijakauka.

    Kile kikombe nilikipokea nikakisogeza midomoni mwangu ili ninywe ile dawa niliyoambiwa. Hapo hapo niliona kikombe kinabetwa. Kikanitoka mkononi na kuanguka chini. Sumu iliyokuwamo ikamwagika. Yule mganga na wasaidizi wake walikuwa wameshangaa. Aliyenibeta kikombe hakuonekana!

    Ghafla nikasikia mganga anapigwa kibao

    cha nguvu na kuanguka chini. Alivyoanguka alinza kutokwa na povu mdomoni. Wale wasaidizi wake walipoona hivyo walitimua mbio.

    Nikabaki nimekaa nikiwa sijui kinachoendelea. Ikabidi niinuke na kumtazama yule mganga. Nikaona amekauka. Tukio hilo likanishitua.

    Nikatoka nje ya ile nyumba kuwatazama wale waliokimbia lakini sikuwaona.

    Nikasikia ninaitwa ndani ya gari langu. Niliposogea kwenye mlango nikamuona Maimun amekaa kwenye siti ya upande wa pili wa dereva.

    “Ingia twende zetu” akaniambia.

    Nikafungua mlango wa gari na kujipakia.

    “Washa gari tuondoke”

    Nikawasha gari.

    “Umeuona upuuzi wako?” Maimun akaniuliza.

    Kwa vile nilikwenda pale kwa ajili ya kumfukuza yeye, sikujibu kitu. Nilihisi pengine upuuzi aliokusudia ulikuwa ni huo.

    “Sisi tunakubaliana kitu vizuri halafu wewe unakwenda kwa mganga! Ulikwenda kwa mganga kufanya nini?” Maimun akaniuliza.

    Kwa kweli nilitahayari aliponiuliza hivyo. Nikaendelea kubaki kimya.



    “Mwenzako amekudanganya. Amekwambia mimi ni mbaya kwa maana yake. Alikuleta huku ili akuue. Ile dawa aliyokupa kwenye kikombe haikuwa dawa. Ilikuwa ni sumu. Kama

    ungekunywa ungekufa pale pale! Mimi ndiye niliyekibeta kile kikombe”

    Hapo ndipo nilipogutuka.

    “Kumbe alikuwa ananipa sumu?”

    “Alikuwa anakupa sumu akuue. Ukishakufa alitaka anichukue mimi

    niwe mke wake ili apate utajiri”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo maana aliniambia tuje huku shamba!”

    “Sasa ndiyo ujue kuwa ulichofanya kilikuwa ni upuuzi. Kwanini ulikuja kumueleza siri ya mimi na wewe?”

    “Nilikuja kumtaka ushauri, ndio akaniambia kuwa wewe ndiye uliyemuua babu yangu na utaniua na mimi. Kwa hiyo alitaka akuondoe”

    “Shiit…! Mimi nimuue babu yako kwa kosa gani wakati nilimchunuka mwenyewe. Babu yako alikufa kwa sababu alikuwa mzee. Angeendelea kuishi hadi lini?”

    “Basi alinaimbia umemuua wewe”

    “Yale yalikuwa maneno ya uchochezi yenye lengo la kutaka unichukie mimi na ukatae kunirithi” Maimun aliniambia kwa huzuni kisha akaongeza.

    “Ni mganga mwenye roho mbaya sana. Kama mimi ni mbaya mbona alinitaka yeye?”

    Nikanyamaza kimya nikifikiria kwamba kama si mwanamke huyo ningekuwa nimeshauawa kwa sumu.

    “Unajua hukupaswa kuwaeleza watu kila kitu. Babu yako alikuwa msiri sana. Hakuwa na mtu yeyote aliyejua kama alikuwa na mke jini. Hata yule mganga wake hakumwambia”

    “Ni kweli nilikosea”

    “Sasa acha tabia ya kuwaeleza watu habari zangu. Utakuja kuuawa bure”

    “Yule mganga sitamuamini tena”

    “Kwani nani alikwambia kwamba ataamka tena?”

    Nikashituka.

    “Hataamka tena?”

    “Ile ndiyo safari. Nilikubeba wewe kile kikombe kisha nikampiga kibao. Alijiona anapigwa lakini hajui anapigwa na nani. Hataamka tena. Ile ndiyo safari!”

    “Niloimuona amekakamaa”

    “Hivi ndivyo ninavyomfanya mtu mpumbavu. Kama ni mganga kweli mwenye majini, mbona hawakunizuia nisimpige? Yule hawezi kunichukua mimi. Mimi ni jini wa kweli kweli. Sio vijini vyake ochwara!”

    Kikapita kimya cha sekunde kadhaa nikiyawazia maneno ya Maimun.

    “Sioni haja ya kusubiri ujiandae au ufikirie. Unajiandaa kwa lipi au unafikiria nini? Leo utanirithi na ninakuwa mke wako. Sasa twende madukani tukanunue nguo kwa ajili ya sherehe yetu ya usiku” Maimun akaniambia ghafla.

    “Tutakuwa na sherehe leo usiku” nikamuuliza.

    “Ndiyo, sherehe ya kuoana kwetu”

    “Itafanyika wapi?”

    “Itafanyika nyumbani kwako usiku”

    “Itakuwa ni sherehe ya namna gani?”

    “Sherehe kama sherehe yoyote ya ndoa. Nitawaalika wageni wangu kutoka kwetu lakini wewe usialike mtu. Itakuwa sherehe ya majini”

    “Kwani haitaki maandalizi?”

    “Mimi mwenyewe nitaandaa kila kitu”

    Nikabaki nimeduwaa. Ningemjibu nini Maimun anayeua watu kwa vibao? Ilibidi nimkubalie kila alichosema.

    Nikampitisha katika maduka makubwa ya nguo. Akanunua vitu pamoja na nguo zake na zangu. Alijaza masanduku mawili ya nguo zenye thamani na kuyapakia kwenye gari. Pesa

    zilizomtoka zilikuwa karibu shilingi milioni ishirini na tano!

    Ile ‘shopping’ ilinitisha hata mimi. Kununu nguo zenye thamani kubwa kiasi kile kwa wakati mmoja halikuwa jambo dogo. Niliamini kuwa kweli yule mwanamke alikuwa na utajiri, si mchezo.

    Tulirudi nyumbani kwangu na yale masanduku. Maimun akaniambia siku ile nisiondoke kwenda popote. Nikatii agizo lake nikashinda nyumbani hadi jioni lakini yeye aliondoka. Usiku nilitoka mara moja kwenda kula chakula halafu nikarudi kulala.

    Yapata saa nae usiku, mlango wa chumba changu ukabishwa. Nikasikia sauti za watu ukumbini. Sikupata hofu kwa vile Maimun aliniambia sherehe zitafanyika usiku. Nikaamka na kwenda kufungua mlango.

    Niliona wasichana wawili waliokuwa mbele ya mlango. Sikuwa na shaka kwamba wasichana hao walikuwa majini kwani walikuwa wazuri sana.

    “Wakati umewadia. Unatakiwa uoge uvae joho lako alilokununulia dada, ujifunge na kilemba halafu ujitie manukato” Mmoja wa wasichana hao wakaniambia.

    Nikarudi chumbani na kuingia bafuni. Nilioga na nilipomaliza nilitoka nikavaa ‘Panjabi’ aliyoninunulia Maimun kisha nikajitia manukato.

    Nikatoka bila kuvaa kilemba kwani nilishindwa kukifunga. Nilikuwa nimekishika mkononi.

    Wale wasichana wawili walikuwa bado wako kando ya mlango kama maaskari. Waliponiona ninatoka, mmoja alinishika mkono akanirudisha chumbani.

    “Usitoke hivi hivi, dadada atagomba” akaniambia na kunifunga kile kilemba.

    Baada ya kufungwa kilemba hicho nilijitazama kwenye kioo. Nilijiona nilikuwa kama ‘Mpakistani’ anayejiandaa kwanda kuswalisha.

    Nyumba yangu ilikuwa imepambwa vilivyo. Mapazia yalikuwa yamewekwa mengine. Taa zilikuwa zimebadilishwa na kuwekwa taa za rangi mbalimbali na zisizo na mwanaga mkali.

    Niliona watu mbalimbali, wake kwa waume, wakishughulika. Maimun aliniambia mchana kuwa ataalika wageni kutoka kwao. Nikahisi wageni wenyewe ndio wale niliowaona hapo.

    Nikapelekwa sebuleni. Sebule ilikuwa imebadilishwa. Makochi yangu yaliondolewa na kuwekwa makochi mengine ya chini chini. Nilikuta watu wawili, mmoja akiwa mzee mwenye ndevu nyeupe ambaye alikuwa amevaa joho na kilemba cheupe.

    Pembeni yake palikuwa na chetezo kilichokuwa kinafuka moshi uliokuwa unanukia ubani uliochanganya na udi wa mawaridi, wengine huuita udi wa Unguja.

    Sebule nzima ilikuwa ikinukia udi wa mawaridi.

    “Kaa hapa” yule mzee aliyekuwa amevaa joho akaniambia akinionesha sehemu iliyokuwa mbele yake.

    Nilipokaa tu akaniambia.

    “Lete mkono wako”

    Nikampa mkono.

    “Unaitwa nani?” akaniuliza.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Nikamtajia jina langu.

    “Nikilitaja jina lako utaitikia labeka”

    “Sawa”

    Mzee huyo akaniita. Nikamuitikia “labeka”

    “Ninakuozesha Maimun binti Hashhash kwa mahari mliyokubaliana. Unakubali?”

    “Nimekubali”

    “Sema nimekubali kumuoa Maimun binti Hashhash kwa mahari tuliyokubaliana”

    Nikasema kama vile alivyonifundisha. Akarudi kunaimbia hivyo mara tatu.

    Hapo hapo nikasikia sauti za wanawake waliokuwa wamekaa ukumbini ziking’ara kwa vifijo.

    Yule mtu aliyekuwa amenichukua kutoka mlango wa chumbani kwangu, akaniambia niinuke. Nilipoinuka akanirudisha chumbani kwangu. Nilipoingia nilikuta chumba hicho kimebadilishwa.



    Hakikuwa kile chumba changu kabisa. Kitanda kilikuwa kimewekwa kingine. Kabati lilikuwa jingine na mapazia pia

    yalikuwa mengine. Kwa kweli kilikuwa kimependeza sana. Hata taa zizokuwa zinawaka zilikuwa ni za rangi mbali mbali.

    Nikamkuta Maimun binti Hashhash amekaa kwenye kitanda. Pale kwenye kitannda palikuwa pametandazwa maua ya mawarisi, asmini, vilua, mlangilangi na vitu vingine ambavyo vilikuwa vikitoa

    harufu nzuri mle chumbani.

    Maimun alikuwa amepambwa na kupendeza kama malkia wa Habesh. Alikuwa akinukia manukato ya kila aina. Mwili wake ulikuwa umejaa mapambo ya dhahabu. Kuanzia kwenye shingo yake ambapo palikuwa na mkufu mzito wa thamani. Masikioni mwake alikuwa amewekwa vipuli vilivyokuwa vikimeremeta. Kwenye mikono yake alikuwa amevaa aina ya bangili za dhahabu.

    Kadhalika katika mguu wake wa kulia alikuwa amefungwa mkufu mwembamba uliokuwa ukimeremeta.

    Kwa kweli alikuwa amependeza na kutamanisha.

    Alikuwa amefunikwa mtandio uliokuwa unaonya. Hivyo niliweza kuyaona macho yake yaliyokuwa yamepakwa wanja mzito mweusi huku yakiwa na kope ndefu mithili ya kope za bandia.

    Nyusi zake pia zilikuwa zimeongezewa msitari wa wanja uliopinda juu ya macho yake mithili ya pindi za mvua.

    Aliniomba nimfunue ule mtandio, nikaushika kwa uoga na kuufunua. Akaniambia.

    “Asalaam alaykum mume wangu” Wakati akinipa salaam hiyo alikuwa akinipa mkono.

    “Wa alayka salaam” nikamjibu na kushikana naye mkono.

    Mkono wake ulichorwa maua kwa kutumia piku na hina. Ulikuwa umeota malaika marefu yasiyo ya kawaida.

    “Salaam yako ina kasoro, sikuipenda” Maimun akaniambia wakati tumeshikana.

    “Kwanini?” nikamuuliza.

    “Nimekusalimia asalaam alaykum mume wangu. Ulipaswa kujibu wa alayka salaam mke wangu”

    “Samahani. Ni kweli nimekosea”

    “Sasa nijibu kwa usahihi”

    “Wa alayka salaam mke wangu”

    Maimun akakibusu kiganja cha mkono wangu kisha akaniambia.

    “Karibu chumbani”

    “Asante” nikamjibu.

    Kusema kweli nilikuwa nimenywea kama vile kile chumba hakikuwa changu.

    Yule mtu aliyenisindikiza mle chumbani akaniambia.

    “Kama umeshaonana na mke wako, mimi nakwenda zangu”

    “Wewe nenda, muache” Maimun akanijibia.

    Yule mtu alipotoka Maimun akajilaza kitandani na kuniambia.

    “Huu ni wakati wako. Karibu tujipumzishe…..”

    **********

    Mkono wenye ngozi laini kama ya mtoto mchanga uliokuwa ukipapasa kifua changu ndio ulioniamsha kutoka usingizini.

    Nikafumbua macho yangu na kuisikia sauti ya Maimun ikiniambia.

    “Amka mume wangu, kumekucha”

    Maimun alikuwa amesimama kando ya kitanda mkono wake ukiwa kwenye kifua

    changu. Sikuweza kujua alikuwa ameondoka muda gani hapo kitandani lakini wakati ule ananiamsha kulikuwa kumeshakucha.

    “Amka ukaoge, nimeshakuandalia kifungua kinywa” akaniambia.

    Nikaitenga shuka na kushuka kitandani.

    “Utaoga maji ya moto?” Maimun akaniuliza.

    “Hapana, ninaoga maji baridi tu”

    Niliingia naye bafuni tukaoga pamoja. Baada ya kuoga Maimun akanikaribisha mezani nipate kifungua kinywa alichokuwa ameniamndalia. Ile vurugu pale nyumbani haikuwepo tena.

    Nyumba ilikuwa kimya na hakukuwa na mgeni yeyote aliyekuwa amebaki. Sikuweza kujua wageni wale waliokuwepo usiku waliondoka saa ngapi.

    Kitu kilichoonesha kuwa usiku uliopita kulikuwa na sherehe ni mapambo yaliyopambwa mle ndani ambayo bado yalikuwepo.

    Baada ya kupata kifungua kinywa pamoja na Maimun tulirudi chumbani ambapo Maimun alifungua kabati. Hilo kabati lilikuwa moja ya vitu vilivyoletwa usiku uliopita. Halikuwa lile kabati langu.

    Maimun alipolifungua kabati hilo, upende mmoja ulikuwa umepangwa nguo zake, upande mwingine ulipangwa nguo zangu.

    Katika sehemu ya chini ya kabati hilo kulikuwa na sanduku la chuma. Maimun akanipa funguo na kuniambia nilifungue

    sanduku hilo. Nikalifungua na kupatwa na mshituko.

    Sanduku hilo lilikuwa na tabaka tatu. Tabaka ya kwanza ilikuwa imepangwa maburungutu ya noti nyekundu za Kitanzania. Zilikuwa noti nyingi na mpya zilizozonesha kama zilitoka benki kwani bado zilikuwa zimefungwa mfungo ule

    ule wa kibenki.

    Tabaka la pili lilikuwa limejaa mapambo ya dhahabu, mikufu, bangili, vipuli na vitu vngine.

    Tabaka la tatu lilikuwa na maburubgutu

    ya noti lakini hazikuwa za Kitanzania. Zilikuwa ni dola za Kimarekani.

    Nikamtazama Maimun kwa mshangao.

    “Hizo ni za kutumia hapa nyumbani. Zikiisha ninaweka zingine” Maimun akaniambia.

    Nikageuza tena uso wangu na kuzitazama zile noti nilizoambiwa kuwa ni za kutumia.

    “Bado kuna pesa za miradi ambazo nitakupa” Manuna aliendelea kuniambia.

    Akilini mwangu niljiambia kuwa nimeshakuwa tajiri.

    “Chukua kiasi unachotaka uweke mfukoni mwako”

    “Nichukue dola au hizi za Kitanzania?’

    “Chukua unazotaka”

    “Kuna miradi mingi ambayo ninataka kuianzisha”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nimekwambia hizo si za miradi. Hizo ni za kutumia tu. Pesa za miradi nitakupa baadaye”

    “Sawa. Ngoja nichukue milioni moja”

    “Chukua hata mbili”

    Nikatia mkono na kuchukua burungutu moja ya zile noti za Kitanzania.

    “Si unataka milioni mbili, chukua mawili”

    Nikatia tena mkono na kuchukua burungutu jingine.

    “Sasa funga hilo sanduku”

    Nikalifunga. Maimun akanipa ufunguo wa sanduku hilo.

    “Funguo utakaa nayo mwenyewe” akaniambia.



    Aliponiambia hivyo, kwa bumbuwazi lililonipata kufuatia kuwa na pesa nyingi kiasi kile nikabaki nikimuangalia Maimun.

    “Vipi mume wangu, mbona umetulia unaniangalia?”

    “Unajua siamini macho yangu. Kwa hiyo pesa zote hizi nizitumie?”

    Nilipomuuliza hivyo Maimun alitoa

    kicheko laini akaniambia pesa zote zile zilikuwa zangu. Hivyo naweza kuzitumia kununua chochote nitakachotaka.

    “Nakushukuru sana mke wangu”

    Maimun aliachia tabasamu kabla ya kuniambia kuwa kulikuwa na jambo muhimu alinieleza.

    “Sijui kama unalikumbuka?”

    “Nimesahau mke wangu ni jambo gani hilo?”

    “Mume wangu jamani! Naona furaha yako imepita kiasi mpaka umesahau jambo muhimu nililokueleza. Kweli umesahau au unataka tu nikueleze tena?”

    “Siyo hivyo mke wangu, ningekumbuka ningekwambia. Naomba unikumbushe maana umeniacha njia panda mwenzio”



    “Haya njoo hapa kitandani nikueleze tena” Maimun akaniambia. Kidogo nilipatwa na wasiwasi. Nikamfuata.

    “Mbona hujafunga kabati?” Maimun akaniuliza na kuongeza.

    “Funga kabati kwanza ndio uje”

    Nikarudi kunako kabati. Nikalifunga kisha nikaenda pale kitandani ambako

    Maimun alikuwa ameketi.

    Maimun akauzungusha mkono wake mmoja kwenye shingo yangu, mkono mwingine ukawa unapapasa kifua changu.

    “Kassim una manyoya marefu kifuani!” akaniambia halafu akawa anacheka kama mtoto

    Aliendelea kunipapapasa huku akiendelea kusema peke yake.

    “Utadhani jini…!”

    Aliposema hivyo aliangua kicheko kabisa.

    “Hivi majini wanakuwa na manyoya marefu?” nikamuuliza.

    “Hunioni mimi?” akaniambia huku akinionesha mikono yake ambayo ilikuwa na malaika marefu.

    Akaendelea kunionesha miguu yake.

    Ingawa alinionesha miguu na mikono lakini kifuani kwake kulikuwa na manyoya zaidi. Niliyaona usiku uliopita.

    “Nilidhani ni wewe tu” nikamwambia.

    “Hapana, hivi ndivyo tulivyo. Tena mimi ni mafupi lakini majini wenzangu wana manyoya marefu sana”

    “Kwa hiyo unapenda malaika marefu?”

    “Sana”

    Maimun aliposema neno ‘sana’ aliurudisha mkono wake kwenye kifua changu.

    Mbona hujaniambia hilo jambo muhimu ulilotaka kunieleza”

    “Ni kukukumbusha tu, nilishakwambia jana kwamba sitaki siri yangu uitoe nje. Hizi pesa ninazokupa ziwe siri yako na bado nitakupa nyingi zaidi. Sitaki nikuone unamueleza mtu kwamba mke wako ni jini na anakupa pesa. Umenielewa?”

    “Nimekuelewa”

    “Siku nikikusikia ukimwambia mtu habari zangu ujue umenivunjia mwiko wangu. Sawa”

    “Sawa mke wangu. Sitamueleza mtu.

    Kwanza nimueleze mtu ili iweje?”

    “Mimi nazijua tabia za binaadamu. Wengine wanapenda sifa sana. Na sifa haifai”

    “Ni kweli lakini mimi sina tabia hiyo”

    “Nataka nikukumbushe kitu kiingine kwamba usiwe na mahusiano na mwanamke yeyote na kama ulikuwa naye umuache”

    Hapo nikanyamaza kidogo. Nikamfikiria msichana wangu mmoja ambaye ndiye niliyekuwa nimepanga kuoana naye.

    “Mbona umenyamaza?” Maimun akaniuliza.

    “Sikufichi. Kuna msichana mmoja ambaye nilikuwa na uhusiano naye na tulikuwa tumepanga kuoana…”

    Nilikuwa sijamaliza sentensi yangu,

    nikauona uso wa Maimun ukiwa mwekundu mpaka niliogopa.

    “Unasemaje?” akaniuliza huku akiwa amekunja uso.

    “Nilikuwa nataka kukueleza kwamba huyo msichana itabidi niachane naye…”

    Maimun akabaki kunitazama. Hata hivyo kwa vile nilikuwa nimeshamzoea nikamshika kiuno chake na kumvuta upande wangu. Wakati namvuta alikuwa laini kama si yeye aliyekuwa amekasirika.

    “Unakasirika nini” nikapata ujasiri wa kumuuliza nikiwa nimemkumbatia.

    “Sitaki shirika. Siku nikikufuma naye ujue ninamuua” akaniambia kwa sauti ya kudeka kama ya mtoto mdogo. Hasira zilikuwa zimeshamtoka.

    “Hutonifuma naye ila itabidi nimueleze kuwa sitaoana naye tena”

    “Kwa hilo ninakuruhusu”

    “Yaani Maimun unafikiri mimi ni mjinga sana, nikupate wewe mrembo ambaye unanipa utajiri halafu nitafute mwanamke mwingine wa kunifilisi!”

    Maneno hayo yakamfurahisha Maimun ambaye bado nilikuwa nimemkumbatia.

    “Si kukupa utajiri tu, pia nakupa mapenzi adhimu” akaniambia kwa kunilegezea sauti.

    “Ni kweli. Sasa baada ya hayo yote nitafute nini tena kwa mwanamke mwingine?”

    Sikujua Maimun alipandwa na mori gani, akanipindua kitandani kisha akanikalia juu.

    “Hutatoka humu chumbani leo. Nakwambia tutashinda humu humu nikuoneshe mahaba ya kijini” akaniambia.

    Ni kweli siku ile siikutooka nje. Kumbe babu yangu alikuwa akifaidi! Majini wanajua mapenzi ya kweli. Kuoana na Maimun kuliniingiza katika enzi mpya katika maisha yangu, enzi ya mapenzi adhimu.

    Mapenzi yetu hayakuwa chumbani tu, yalikuwa mahali popote, kwenye chakula, kwenye kuoga na hata kwenye mazungumzo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kitu ambacho niliokiona kilikuwa kero ni wivu wa mwanamke huyo. Alikuwa na wivu wa kupindukia. Siku akiamua nisitoke nyumbani, sitoki. Nitashinda naye chumbani mchana kutwa.

    Siku ambayo ninapomuudhi anakasirika mchana kutwa. Anakuwa hataki kusema na mimi lakini siku akifurahi atakuenzi mpaka basi.

    Saa moja asubuhi Maimun anakuwa ameshanitayarishia kifungua kinywa. Saa sita mchana ameshatayarisha chakula cha mchana. Chakula cha usiku kinakuwa tayari saa mbili.

    Vyakula ambavyo Maimun alikuwa akivipenda ni uji uliochanganywa na nyama ya mbuzi, anauita ‘shurba’ Pia hupenda chai ya maziwa, chapatti, mkate wa mchele, pilau ya kuku, biriani na wali kwa maziwa ya mgando.

    Vitu ambavyo alipenda kuvinunua kila siku ni aina za manukato. Kwenye kabati letu kulikuwa na chupa karibu ishirini za manukato tofauti tofauti.

    Alikuwa akipenda kuoga. Mchana mmoja alioga karibu mara sita na akiingia bafuni huchukua muda mrefu kutoka. Ngozi yake ilikuwa safi na laini kama ngozi ya mtoto mchanga.

    Kuna kitu kimoja nilikuja kukigundua kwamba Maimun alikuwa halali usingizi. Ninapolala naye usiku anafanya geresha tu. Ninapopitiwa na usingizi mwenzangu anabaki macho akiwa na kazi ya kuniamgalia tu. Wakati mwingine hushuka kitandani na kwenda kukaa sebuleni usiku kucha.



    Siku nilipogundua hilo nilimuuliza.

    “Hivi wewe Maimun hulali usiku?”

    “Sisi majini hatulali, tunakuwa macho tu” akanijibu.

    “Kwaninini?”

    “Ndiyo maumbile yetu”

    “Kumbe usiku nalala peke yangu?”

    “Ukilala mimi nakulinda”

    Kuna siku moja aliniamsha saa nane usiku akaniambia nichukue shepe kisha nitoe gari. Baada ya kulitia shepe kwenye gari nililitoa gari. Maimun akajipakia na kukaa kando yangu.

    “Twende Kigamboni” akaniambia.

    “Kuna nini?” nikamuuliza.

    “Wewe twende tu”

    Nilikwenda kukutana na maajabu ambayo sitayasahau katika maisha yangu.



    Tulifika Kigamboni kama saa nane na nusu hivi. Ilielekea Maimun alikuwa akilijua vizuri eneo hilo kwani aliniongoza hadi sehemu ambayo ilikuwa na pori.

    Akaniambia niingize gari katika pori hilo. Sikumuelewa halafu pia nilipata hofu kidogo. Nikafunga breki na kumuuliza.

    “Kwani tunakwenda wapi?”

    “Wewe twende tu”

    “Lakini huku unakoniambia twende hakuna njia”

    “Mimi pia nina macho, ninaona kuwa hakuna njia. Ingiza gari hivyo hivyo”

    “Unataka tutokee wapi?”

    “Kassim mbona mbishi sana?”

    “Mahali kuna pori, unaniambia niende! Njoo uendeshe wewe”

    “Kumbe huniamini?”

    “Ninakuamini. Tatizo nini kuwa siwezi kuendesha gari kwenye pori na pia sijui tunakwenda wapi”

    “Kwahiyo turudi?”

    “Tusirudi. Nimekwambia njoo uendeshe wewe”

    “Inaelekea wewe ni muoga sana!”

    Hapo sikumjibu. Nikanyamaza kimya kwani ukweli ni kuwa uoga pia nilikuwa nao.

    “Shuka unipishe hapo kwenye sukani” Maimun akaniambia.

    Nikafungua mlango na kushuka.

    Kulikuwa na gari ambayo ilikuwa nyuma yetu ikatupita na kusimama mbele yetu.

    Wakati ule nafungua mlango nikaona ninavamiwa na mtu mmoja miongoni mwa wanne waliotoka kwenye lile gari. Mtu huyo alinishikia bastola na kunitia kabari kwa nyuma. Mtu mwingine alifungua mlango wa upande aliokuwa Maimun akamwambia.

    “Shuka haraka!”

    Maimun akashuka kwenye gari.

    “Mnataka nini?” Maimun akiwauliza.

    Mimi nilikuwa nimeshadhibitiwa. Mkono ulionitia kabari ulikuwa ukinikaza na kunifanya nisifurukute hata kidogo. Mdomo wa bastola ulikuwa ukitekenya shavu langu la kulia.

    Sikuweza kujua watu wale walikuwa kina nani na walikuwa wanataka nini.

    Kulikuwa na watu wengine wawili ambao walikuwa wamefungua milango ya ile gari kama vile walikuwa wakitafuta kitu.

    “Mnakwenda wapi?” Yule mtu aliyemtoa Maimun kwenye gari akamuuliza Maimun.

    “Nyinyi ni majambazi sio?” Maimun akawauliza.

    Yule mtu alitaka kumpiga Maimun kibao, bila shaka kwa vile alivyowambia ni majambazi. Maimun akatoweka ghafla mbele yake. Kibao kikakata hewa. Maimun akaibuka tena mahali pale pale. Nikamsikia akitoa mlio kama wa fataki inayopaa juu huku na yeye akirefuka kwenda juu.

    Wakati ule mmojawao, alikuwa ameshajipakia kwenye gari kwenye siti ya dereva. Nikahisi walitaka kutupora lile gari.

    Lakini kitendo cha Maimun kurefuka kiliwashitua. Maimun aliendelea kurefuka akafikia kimo cha mnazi!

    Nikawasikia wale watu wakisema kwa fadhaa. “Ha! Ha1 Ha!”

    Yule aliyenitia kabari aliniachia akakimbilia kwenye gari lao. Yule aliyetaka kuendesha lile gari letu alitoka kwenye gari na kukimbia lakini yule aliyetaka kumpiga Maimun kibao alinata pale pale.

    Wale waliokimbilia kwenye gari walikwama baada ya Maimun kupiga hatua moja na kutinga mbele ya gari hilo. Mtu mmoja alianguka hapo hapo. Wengine wakakimbia kwingine na kuliacha gari.

    Baada ya tukio hilo nikauona mwili wa Maimun umerudi vile vile kama ulivyokuwa mwanzo.

    Akaja kwenye gari letu upande wa dereva na kuniambia.

    “Ingia garini twende”

    Nikazunguka kwenye mlango wa upande wa pili na kujipakia. Yule mtu aliyenata alikuwa bado amesimama pale pale, mkono wake mmoja akiwa ameunyoosha mbele kama vile anampiga mtu kibao.

    Maimun alikuwa ameshaingia kwenye gari akaliondoa na kuliingiza kwenye pori.

    Kile kitendo cha Maimun kujirefusha, hata mimi kilinishitua kwani katika maisha yangu sijawahi kuona mtu akirefuka kwenda juu akafikia kimo cha mnazi.

    Mpaka wakati ule nilikuwa bado nikitweta.

    “Umewaona wapumbavu wale?” Maimun akaanza kuniambia akionekana alikuwa amekasirika.

    “Nimewaona lakini sikujua walikuwa ni kina nani”

    “Wale ni majambazi, walitaka kulipora hili gari. Walitufuata kuanzia mbali sana. Nilishawaona lakini sikukwambia”

    “Kwa hiyo walitaka watuue?”

    “Sasa kama walitutolea bastola, unadhani walikuwa wana maana gani nyingine?”

    “Lakini wametishika!”

    “Walivyonuona ninakuwa mrefu sio?”

    “Ndiyo. Hata mimi nimetishika”

    “Wewe mume wangu pia unatishika?”

    “Sijawahi kukuona ukiwa vile!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Acha vile naweza kujirefusha mpaka ukawa hujui nimefikia wapi!”

    “Sasa unafanyaje?”

    “Ni namna yetu. Naweza pia kujigeuza mnyama kama vile punda au joka kubwa”

    “Lakini sitapenda ufanye hivyo mbele yangu”

    “Nikifanya mbele yako ndipo utakaponizoea”

    “Eh! Nitaogopa sana”

    “Utazoea tu. Utaogopa mwanzo, mwisho utakuwa huogopi tena”

    “Sasa yule mtu aliyetaka kukupiga kibao, ataendelea kubaki pale hadi lini?”

    “Atajua mwenyewe, achana naye”

    Maimuna aliendesha gari huku akikata kona ndani ya msitu hadi tukatokea mahali ambapo palikuwa na mawe makubwa sana yaliyotokea ardhini.

    Akalisimamisha gari na kuniambia tushuke. Tukashuka. Palikuwa ni mahali panapotisha usiku huo lakini kwa vile nilikuwa na Maimun sikuwa na hofu sana. Nilijua kama kutatokea tatizo atanisaidia.

    “Toa lile shepe nyuma ya gari” akaniambia.





    Nikaenda nyuma ya gari na kulitoa lile shepe.

    “Njoo hapa” akaniambia akiwa amesimama mahali fulani kando ya lile gari.

    Nilipofika karibu yake akaniambia.

    “Chimba mahali hapa”

    Alinionesha pale aliposimama kisha akaondoka na kusimama kando yake.

    Nikaanza kupachimba mahali hapo kwa kutumia lile shepe. Bahati nzuri mchanga ulikuwa laini, sikutumia nguvu nyingi. Niliendelea kuchimba mpaka shimo likafikia urefu wa wastani wa futi mbili.

    “Nichimbe hadi wapi?”

    “Bado. Endelea kuchimba” Maimun akaniambia.

    Nikaendelea kuchimba. Mwili wangu ukaanza kutoka jasho. Nikaacha kuchimba na kuvua shati.

    “Lete nikushikie” Maimun akaniambia.

    Nikampa lile shati na kuendelea kuchimba.



    Niliendelea kuchimba lile shimo mpaka likanifikia usawa wa kifua. Nilikuwa nikimwaga mchanga juu ya shimo hilo. Ghafla nikaona ninapiga kitu kama mwamba au jiwe lililokuwa chini ya ardhi.

    “Sijui nimepiga nini hapa?” nikamuuliza Maimun kwa mshituko.

    “Huo ni mwamba, upige tena” Maimun akaniambia.

    Nikaupiga tena kwa shepe.

    “Piga tena”

    Nikaupiga kwa mara ya tatu. Ule mwamba ukapasuka.

    “Umepasuka” nikamwambia Maimun.

    “Hebu washa kitochi cha simu yako umulike hapo palipopasuka” Maimun akaniambia.

    Nikajipapasa mfukoni na kutoa simu yangu. Niliwasha kitochi nikamulika pale chini.

    Mama yangu! Niliona vipande vya madini yanayomeremeta vikiwa vimetawanyika!

    “Nini hii?” nikamuuliza Maimun kwa mshituko.

    “Kwani umeona nini?”

    “Sijui ni madini haya. Huu mwaba ulikuwa na madini!”

    “Ndiyo ni madini”

    “Sijui ni madini ya aina gani?”

    “Ni Tanzanite, ni yale aliyokuwa akiuza babu yako”

    “Niyachukue”

    “Ndiyo yachukue”

    Nikainama haraka na kuyachukua yale madini.

    Vilikuwa vipande saba vya madini.

    “Huu ni utajiri hasa! Nikajiambia kimoyomoyo kisha nikamshukuru Mungu.

    “Mungu anipe nini tena!”

    Yakiwa mikononi mwangu madini hayo yalikuwa yakiakisi rangi mbali mbali za dunia. Zile rangi zilikuwa kama zinazunguka. Ilikuwa ni furaha hata kuyatazama.

    “Ni vipande vingapi?” Maimun akaniuliza.

    “Viko saba”

    “Haya sasa toka kwenye hili shimo”

    “Ngoja niendelee kuupiga huu mwamba”

    “Hapana, usirudie tena. Toka kwenye shimo” Maimun akanionya.

    Nikayatia yale madini mifukoni mwangu kisha nikalitoa lile shepe na kuliweka juu ya shimo hilo.

    “Lete mkono wako nikutoe” Maimun akaniambia.

    Nikampa mkono wangu Maimun, akaushika na kunivuta. Mara moja

    nikjioan niko juu ya lile shimo.

    “Anza kulifukia haraka haraka”

    Nikalichukua shepe hilo na kufukia lile shimo.

    “Tutakuja lini tena kuchimba?” nikamuuliza Maimun kwa tamaa huku nikiendelea kufukia shimo hilo.

    “Baada ya miezi sita”

    “Ah kwanini! Mbona mbali sana?”

    “Ndiyo masharti yake. Haya madini yanakaliwa na majini. Huwezi kuja kienyeji tu na kuyachimba na hata ukija hutoyaona. Masharti yake ndiyo haya ninayokupa. Kila baada ya miezi sita tunakuja kuchimba tena”

    “Sawa”

    Niliendelea kulifukia lile shimo mpaka nikaliweka sawa.

    “Watu wengine hawatakuja kufukua?” nikamuuliza Maimun.

    “Ni nani atakayethubutu?”

    “Wanaweza kutokea watu wakaja kufukua”

    “Hawatapata kitu chochote. Chukua shati lako tuondoke”

    Nililichukua lile shati alilokuwa amelishika Maimun nikalivaa.

    “Twenzetu” akaniambia.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nililiweka shepe nyuma ya gari.

    “Utaendesha wewe?” Maimun akaniambia.

    “Sawa” nikamjibu haraka haraka na kwenda kufungua mlango wa gari wa upande wa dereva.

    Maimun alifungua mlango wa upande wa pili wa dereva na kujipakia.

    “Washa gari tuondoke. Muda umekwenda sana”

    Nikaliwsha gari na kuliondoa. Nilipokuja na Maimun mahali hapo nilikuwa nimefadhaika lakini wakati tunaondoka moyo wangu ulikuwa na furaha iliyopita kiasi.

    “Hivi babu yangu ulikuwa unakuja naye hapa hapa kuchimba haya madini?”

    “Ninajua mimi kama tulikuwa tunakuja hapa au mahali pengine”

    “Hutaki kuniiambia”

    “Si lazima kila kitu ukijue kwa sasa Kasim”

    “Sawa mke wangu”

    Nikabaki kimya mpaka tulipotokea pale mahali ambapo majambazi walitaka kulipora gari langu. Yule mtu aliyenata huku mkono wake mmoja ukipiga ngumi kwenye hewa alikuwa bado amenata vile vile na yule aliyeaguka alikuwa bado yuko chini. Lile gari lao pia lilikuwa pale pale.

    “Kumbe hawa watu bado wapo?”nikamuuliza Maimun.

    “Si uwaache tu. Majambazi wanakuhusu nini?”

    “Nilikuwa nasema tu”

    “Sema maneno yenye maana. Achana

    na watu hao”

    “Inaonekana walikuudhi sana



    Maimun hakunijibu chochote na mimi nikanyamaza. Mawazo yalikuwa yakipita akilini mwangu

    Niliwaza si muda mrefu nitakuwa mmoja

    wa matajiri wakubwa hapa nchini. Nitakuwa ninazungka kwa ndege katika nchi mbalimbali kama alivyokuwa babu yangu.

    Huku nikiliendesha gari kwa mbwembwe, nilijiambia fedha itakaponikubali sawasawa, nitamshawishi Maimun ninunue jumba jingine la kifahari eneo la Masaki ambalo nilikuwa niikitamani sana kuishi.

    Pia nilitaka ninunue gari jingine la gharama kutoka Ulaya. Ikiwezekana magari mawili la Maimun na la kwangu.

    Tulipofika nyumbani Maimun aliniambia niyatoe yale madini. Nikayatoa mifukoni.

    Aliyashika shika na kuyaangalia kisha aliniambia.

    “Kuwa makini sana, wewe bado ni kijana mdogo. Nakuomba uwe msikivu. Ujue kuwa ukifanya papara utakwenda na maji”

    “Kwanini?”

    “Si lazima kila kitu nikwambie, unapaswa kutumia akili yako. Mimi sitaki uwe mtu wa papara”



    “Kwani umenionaje mke wangu?” nikamuuliza Maimun baada ya kutomuelewa.

    “Nimekuona una papara. Jicho limekutoka kwenye haya madini. Unajiona tayari umeshakuwa tajiri. Nataka nikukumbushe kuwa hii mali yote ni yangu mimi. Wewe ninakupa uimiliki tu, wakati wowote utakapovunja masharti yangu nninaichukua mwenyewe”

    “Sitavunja masharti yako, wewe acha tu niimiliki. Kila mara unapenda kunituhumu lakini mimi sina tatizo”

    “Sasa sikiliza. Tafuta wanunuzi wa haya madini hapa hapa nchini. Sitaki uende nje ya nchi kama alivyokuwa babu yako. Na pia huwezi kuyauza madini yote kwa pamoja. Uza moja moja”

    “Kwanini hutaki niende nikayauze nchi za nje wakati huko nitapata bei nzuri kuliko ya hapa?” nikamuuliza.

    “Uhitajji kupata pesa nyingi. Pesa yoyote utakayopata itakutosha kwa sababu kila baada ya miezi sita utapata madini mingine, una wasiwasi gani?”

    “Mimi nilitaka niende nje lakini kama unataka tuyauze hapa hapa, sawa”

    “Wewe unajua jiwe moja litakupatia kiasi gani?”

    Pesa nyingi sana. Naweza hata kujenga jumba moja la ghorofa”

    “Sasa kiherehere chako ni cha nini?”

    Nikacheka kidogo kisha nikamwambia.

    “Sina kiherehere. Sasa nitakwenda kuyauza lini haya madini?’

    “Ni wewe tu”

    Basi kesho nitaanza kufanya utafiti wa wateja”

    “Sawa”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Naam, hivyo ndiyo nilivyoanza kutajirika. Nilifanikiwa kuviuza vipande vyote saba. Nikapata kiasi kikubwa cha pesa. Maimun aliniambia pesa hizo nisiziweke benki, niziache pale pale nyumbani atazilinda mwenyewe.

    Badala ya sanduku moja la pesa tulilokuwa nalo kabatini, tukawa na masanduku mawili. Kila baada ya miezi sita nilienda na Maimun kuchimba madini mengine ambayo niliyauza. Nikapata utajiri mkubwa.

    Maimun aliniruhusu ninunue nyumba jingine Masaki. Nikanunua jumba la kifahari ambalo alikuwa akiishi mzungu mmoja. Nililinunua kwa bilioni tatu.

    Nikaagiza magari mawili kutoka

    Uingereza aina ya Benz. Moja nilitaka nimpe Maimun lakini akaniambia hataki kuwa na gari la peke yake ila tuyatumie yote mawili kwa pamoja.

    Pia nilifungua miradi mbali mbali ya kibiashara. Nikawa mmoja wa watu maarufu katika jiji la Dar na pia nikawa mmoja wa matijiri wakubwa Afrika.

    Baada ya kuishi na Maimun kwa miaka

    mitatu aliniambia yale madini yamekwisha, kwa hiyo tutumie fedha tulizonazo na kwamba atakapoona inafaa atanionesha mahali pengine pa kuchimba madini mengine ya Tanzanite.

    Siku za mwanzo mwanzo nilizoanza kuishi na Maimun nilikuwa nikimuogopa lakini kidogo dogo nikaanza kumzoea na kumuona wa kawaida. Ilifikia mahali nilikuwa ninabishana naye kupinga maamuzi yake na kumwambia kwamba mimi ndiye mume, kwa hiyo anapaswa kunisikiliza mimi.

    “Nimekupa mali sasa imekulewesha”

    alikuwa akiniambia baada ya kuona sitaki kumsikiliza.

    “Sio hivyo Maimun, amri zako nyingine zinanikera”

    “Mimi najua kinachokupa kiburi ni huu utajiri lakini ujue kwamba ninaweza kuufyeka kwa siku moja tu”

    “Hapana, usifanye hivyo Maimun. Nipe uhuru wa kushauriana na wewe. Kwanini ninapokushauri kitu unatishia kuchukua mali yako?”

    “Ni kwa sababu ninataka unitii mimi”

    “Basi yaishe. Naogopa kurudi katika umasikini”

    Hivyo ndivyo nilivyokuwa ninaishi na Maimun. Alikuwa na wivu mwingi pamoja na kufuatilia mambo yangu kwa karibu. Wakati mwingine nilikuwa nachukia.

    Kwa maisha ya nyumbani, Maimun alikuwa mke wa kweli aliyenionesha upendo na alinipa mamlaka ya kuimiliki nyumba vile ninavyotaka mimi. Wakati mwingine nilimtolea ukali, Maimun akaniomba msamaha kwa kuwa nilikuwa mume wake.

    Jamani huu ndio mkasa wa urithi wa babu yangu. Nilikiona cha moto lakini mwishoni nikaja kupata mke wa kijini na kupata utajiri ambao sikuutarajia.

    Kilichokuwa kinanipa uchungu ni kuwa Maimun alipata ujauzito wangu mara tatu lakini alikwenda kujifungulia kwao. Wale watoto alikuwa akiwaleta nyumbani usiku. Inapofika alfajiri anawarudisha kwao.

    Nilipomuuliza ni kwanini anafanya hivyo aliniambia anataka watoto hao wawe majini kama yeye. Hakutaka wazoeane na watu na kwamba watoto hao hawataenda shule ila watasomea huko

    huko ujinini.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Watakapokuwa wakubwa watakuja kukusaidia, watakuwa kama binaadamu na utaweza kuwatuma popote” Maimun aliniambia.

    Mtoto wangu wa kwanza niliyemzaa na Maimun, hivi sasa ana miaka saba. Wa pili ana miaka minne na wa tatu bado ni mchanga. Nilikuwa kiona jinsi anavyonyonyeshwa na mama yake ifikapo usiku anapokuja naye nyumbani pamoja na wale watoto wengine.

    Sijui nitakapokufa Maimun atakwenda kwa nani kwani sikuwa na mrithi. Huenda atakwenda kwa mtu mwingine atakayemchunuka.

    Hadi hii leo niko na Maimun huko nyumbani kwangu Masaki lakini wageni ni marufuku nyumbani kwangu.



    MWISHO

0 comments:

Post a Comment

Blog