Search This Blog

URITHI WA BABU - 4

 





    Simulizi : Urithi Wa Babu

    Sehemu Ya Nne (4)



    Macho ya watu wote yakaelekea kwenye mwili huo. Polisi hao waliufungua uso wa marehemu huyo. Ingawa ngozi yake ilikuwa nyeusi kwa sababu ya kukaa ndani ya kaburi kwa muda mrefu haikuwa imeharibika.

    Uso wake ulikuwa mwembamba na uliosinyaa lakini haukunizuia kugundua kuwa ulikuwa na sura ya Ummy.

    “Hebu mtazameni, huyu ndiye maiti wenu?” Inapekta Amour akawauliza wazazi wa Ummy.

    “Ndiye yeye” Mzee Nasri akajibu haraka.

    Polisi mmoja aliyekuwa na kamera ya kuchukua alama za vidole alipiga picha alama za viganja vya Ummy. Polisi mwingine aliupiga picha uso wake. Daktari naye aliuchunguza mwili huo na kukata kipande cha ngozi yake ya mkono.

    Baada ya uchunguzi huo kumalizika, mwili huo ulirudishwa kwenye kaburi na kufukiwa tena

    Daktari akawambia watu kwamba atakuwa na matokeo kamili ya uchunguzi wake baada ya saa sita. Polisi walioupiga picha mwili huo wakasema watakamilisha uchunguzi wao baada ya saa tatu.

    Tukaondoka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Inspekta Amour alinirudisha nyumbani kwangu akanitaka nifike kituo cha polisi asubuuhi ya kesho yake ili nionanne naye.

    Baada ya kuagana naye, Inspekta huyo aliondoka. Niliridhika sana na hatua alizochukua. Alikuwa ni miongoni mwa makachero wa polisi niliowakubali sana. Alikuwa akitambua wajibu wake kama polisi mpelelezi.

    Hata hivyo bado niliona kitu kama ukungu katika uchunguzi huo wa polisi. Dalili kwamba huenda tukajikuta tupo njia panda katika uchunguzi huo ni kule kukuta maiti ya iliyoonekana kuwa ni ya Ummy kwenye kaburi lililofukuliwa.

    Nilijiambia kama itathibitika kuwa aliyezikwa ni Ummy Nasir, moja kwa moja yule msichana anayenipigia simu atakuwa ni mzuka wa Ummy na ndio uliokwenda kusajili namba ya simu kwa ajili ya kunipigia mimi.

    Na kama itathibitika kwamba yule si Ummy, basi Ummy atakuwa yupo hai na ndiye aliyeuawa watu waliokuwa wakidaiwa na babu yangu, na ndiye

    huyo huyo aliyekwenda kusajili namba ya simu.

    Kwa vyovyote itakavyokuwa, niliendelea kujiambia, huenda Ummy huyo asiwe na nia njema na mimi. Kama amedai anaijua siri ya mali ya babu yangu huenda anataka kuniua ili aweze kumiliki mali hizo.

    Shaka hii ilinijia baada ya kuona ameshaua watu waliokuwa wanadaiwa na babu yangu bila kueleweka dhamiri yake ilikuwa nini.

    Lakini kama utakuwa ni mzuka, suala litakuwa zito zaidi.

    Usiku wa siku ile sikupata usingzi kwa kuwaza. Niliwaza mengi yaliyonikera moyo wangu lakini hatimae kulikucha salama.

    Saa tatu asubuhi nikawasili kituo cha polisi cha Kinondoni na kuonana na Inspekta Amour.

    Inspekta Amour alinikaribisha kwenye kiti akaniuliza.

    “Yule msichana hajakupigia simu?”

    “Hajanipigia”

    “Tumeanza kupata utata kuhusu suala lake. Tumefanya uchunguzi wa kutosha jana na leo lakini matokeo yamekuwa ni ya kutia shaka”

    “Kwanini?”

    “Uchuguzi wa madaktari wa Muhimbili kwa kutumia chembechembe za mwili wa marehemu na vielelezo vingine umebaini kuwa ule ulikuwa mwili wa Ummy…”

    Nilikuwa niimemkodolea macho Inspekta huyo kumsikiliza. Akaendelea.

    “Sasa utata unakuja kwa sababuni hata uchunguzi tuliofanya sisi unaonesha kuwa mtu anayekupigia simu ni Ummy huyo huyo ambaye ameshakufa. Alama zake za vidole zilizoko katika usajili wake

    na alama tulizozichukua jana katika

    viganja vyake zinafanana. Hii inaonesha kuwa ni Ummy huyo huyo!”

    “Una maana kwamba alama za vidole za watu hazifanani?”

    Inspekta Amour akatikisa kichwa.

    “Alama za vidole za binaadamu hazifanani kabisa. Kila mtu ana alama zake”

    “Hata kama watachunguzwa watu milioni moja, watakutwa na alama za vidole tofauti?”

    “Hata watu milioni kumi, wanaweza kufanana sura tu lakini alama zao za vidole hazifanani. Kila binaadamu anakuwa na alama zake mwenyewe”

    “Hicho ni kitu cha ajabu sana”

    “Ndiyo maumbile yetu binaadamu. Na wataalamu waligundua hilo. Ndiyo maana alama za vidole zimekuwa kielelezo muhimu cha kumkamatisha mhalifu”

    “Mungu ni muweza sana”

    “Unaiona ile mistari ya pundamilia?”

    “Ndiyo, niimeshawahi kuiona”

    “Unaweza kuiona kama inafanana lakini ile pia haifanani. Kila punda milia ana

    aina yake ya mistari, hata wawepo pundamilia milioni kumi, watakuwa na mistari tofauti”

    “Hilo sijawahi kulisikia”

    “Ndiyo nakueleza mimi ili uone maajabu ya Mungu, si katika alama za vidole za binaadamu tu bali tofauti zipo hata katika alama za wanyama”

    “Nimekuelewa Inspekta. Sasa hili suala la Ummy unalifikiriaje?’

    “Ndiyo nilikuwa nataka kukueleza kwamba limekuwa suala lenye utata. Mtu ambaye imethibitika kuwa amekufa na kuzikwa miaka mitano iliyopita lakini kunakuwepo na ushahidi kuwa yuko hai. Hili jambo ni la ajabu sana”

    “Niliwahi kukwambia kwamba inawezekana kuwa ni mzuka wa Ummy”

    “Suala hilo la kiimani hatuwezi kuliingiza

    katika uchunguzi. Kazi yetu haiamini kuwepo kwa mizuka”

    “Sasa atakuwa ni nani yule?’

    “Siwezi kusema ni nani kwa sababu hatujamthibitisha ila wewe utakuwa ni nguzo muhimu katika uchunguzi wetu wa awamu ya pili. Nisikilize kwa makini”

    “Ndiyo”

    “Wakati wowote atakapokupigia simu, kubali kukutana naye halafu tupigie simu ili tufike mahali hapo. Pale mtakapokutana tu tunamkamata hapo hapo”

    “Nafikiri hilo litakuwa wazo zuri. Hapo mwanzo nilikuwa sitaki kukutana naye kwa sababu ya hofu lakini kama polisi mtakuja nitaweza kukutana naye”

    “Tutakuja. Muulize angependa mkutane wapi”

    “Mara nyingi anapenda tukutane mahotelini”

    “Basi muache ataje yeye hoteli ambayo angependa mkutane”



    “Alikuambia hivyo?”

    “Ndiyo. Kwa kweli nilishangaa sana”

    “Wewe ulimjibu nini?”

    “Nilinyamaza kimya. Sikuwa na jibu”

    “Milizungumzia mahali pa kukutana?”

    “Ametaka tukutane Lux Hotel, kule Masaki”

    “Saa ngapi?”

    Saa nne, asubuhi hii”

    “Sasa acha tujiandae tuje huko”

    “Lakini Inspekta huu si utakuwa ni mzuka wa Ummy? Amejuaje kuwa tulifukua kaburi lake?”

    “Hapo tutakapomkamata kila kitu kitajulikana”

    Kama nitakutana naye ni lazima niwe karibu na polisi, nilijiambia kimoyomoyo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa wewe wahi kufika hapo heteli kabla ya saa nne umsubiri yeye” Inspekta aliniambia kwenye simu.

    “Mimi ndiyo najiandaa. Nitahakikisha ikifika saa tatu na nusu niko pale”

    “Tafadhali usikae katika eneo lililojificha. Tunataka tukifika tukuone. Kama mtakaa katika eneo la wazi la hoteli itakuwa vizuri sana”

    “Sawa”

    Baada ya kumaliza kuzumngumza na Inspekta Amour. Sikungoja ifike saa tatu na nusu, niliondoka muda ule ule kwa gari langu.

    Niliendesha kwa mwendo wa taratibu huku nikiwaza. Niliwaza kwamba endapo polisi watafanikiwa kumkamata yule msichana, kitendo hicho kitafichua mengi yaliyojificha.

    Mengi yaliyojificha ni pamoja na mali za babu yangu ambazo zimekuwa ni kitendawili ambacho nimeshindwa kukitegua.

    Kingine ambacho kingefichuka ni kuhusu Ummy mwenyewe ambaye mpaka muda ule tulikuwa hatujui kama alikuwa ni mzuka au alikuwa binaadamu.

    Wakati niko njiani Inspekata Amour akanipigia simu.

    “Umeshakwenda huko Masaki au bado?”

    akaniuliza.

    “Ndiyo niko njiani, ninakwenda”

    “Ukifika tu utanipigia simu kunijulisha kuwa umekaa sehemu gani”

    “Lakini na nyie msichelewe sana, msije mkamkosa. Mimi nimekubali kukutana naye kwa sababu yenu”

    “Usiwe na wasiwasi. Tayari makachero watatu wameshatangulia huko”

    “Sawa”

    Inspekta akakata simu.

    Haukupita muda mrefu nikaingia Masaki. Niliutafuta ule mtaa uliokuwa na hoteli ya Lux, nilipoupata nikalielekeza gari ilipokuwa hoteli hiyo.

    Baada ya dakika tatu tu hoteli hiyo ikawa upande wangu wa kushoto. Wakati

    nakata kona kuelekea kushoto, simu yangu ikaita tena. Kwa vile nilikuwa katika mwendo wa taratibu niliichukua na kutazama namba iliyokuwa inanipigia.

    Nikaona namba ya Ummy!

    Wakati naipokea ile simu nikamuona Ummy mwenyewe amesimama katikati ya njia mita chache tu mbele ya gari langu.

    Alikuwa ameshika simu sikioni. Kumuona kwake kukanigutusha. Nikasema “Hello” kwenye simu huku nimemkodolea macho.

    Vile alivyokuwa amesimama katikati ya njia, nilihofia kwamba ningeweza kumgonga kwa vile nilikuwa nimeshamkaribia. Nikafunga breki kusimamisha gari.

    “Utaona leo! Utaona leo!” nikaisikia sauti yake ikisema kwenye simu.

    Kumbe sikuwa nimekanyaga breki. Nilichokanyaga ni pedali ya mafuta. Gari lilifyatuka na kumgonga Ummy. Ummy akatoweka ghafla mbele ya macho yangu. Badala yake nikaona nimegonga nguzo mbili za umeme zilizokuwa zimebeba transfoma.

    Mlipuko uliotokea hapo ulinizibua masikio. Nakumbuka kwa mara ya mwisho niliona moto mkali ukiwaka kama umeme. Hapo hapo fahamu zikanipotea.

    Sikuweza kujua gari langu lilisesereka na kwenda upande gani lakini nilizisikia kelele za watu waliokuwa wakikimbia huku na huko. Baadaye nilisikia king’ora ambacho ama kilikuwa cha gari la zima moto au cha gari la hospitali kama si cha gari la polisi.

    Nilikuja kuzinduka nikiwa katika chumba cha hospitali. Nilikuwa nimefungwa

    bendeji sehemu mbali mballiza mwilli wangu kuanzia kichwani hadi miguuni.

    Wakati nazinduka wauguzi na daktari, walikuwa wakishughulika na mimi. Karibu yangu niliona polisi mmoja alliyekuwa na bunduki.

    “Oh umezinduka!” Daktari alipoona nimefumbua macho aliniuliza.

    Sikumjibu kitu. Bado nilikuwa nikjiuliza nimefikaje pale hospitalli.

    “Unajisikiaje?” akaendelea kuniuliza.

    Nikatikisa kichwa changu.

    “Sijisikii vizuri. Mwili wote unaniuma” nikamwambia.

    “Maumivu yako sehemu gani zaidi?”

    “Hizi sehemu zilizofungwa bendeji zinaniuma sana”

    “Kuna baadhi ya sehemu umeshonwa baada ya kukatwa na vioo vya gari na kuna sehemu nyingine hazikushoneka, zina majeraha makubwa ya kukatwa na

    vioo” Daktaria akaniambia.

    Nikanyamza kimya na kuanza kuitafakari ile ajali.

    “Tutakupatia tenbe za kutuliza

    maumivu. Utajisikia vizuri” Daktari akaniambia.

    “Nitashukuru”

    Mara nikamuona Inspekta Amour akiingia katika chumba hicho.

    Alipoona namtazama alimuuliza daktari kama angeweza kuongea na mimi.

    “Mnaweza kuzungumza” alipata jibu kutoka kwa daktari.

    “Pole sana” Inspekta akaniambia.

    “Asante”

    “Nini kimetokea pale”

    “Kwa kweli palitokea kitu kama miujiza….”



    Mara nikamuona Inspekta Amour akiingia katika chumba hicho.

    Alipoona namtazama alimuuliza daktari kama angeweza kuongea na mimi.

    “Mnaweza kuzungumza” alipata jibu kutoka kwa daktari.

    “Pole sana” Inspekta akaniambia.

    “Asante”

    “Nini kimetokea pale”

    “Kwa kweli palitokea kitu kama miujiza….”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilimueleza inspekta huyo hali iliyotokea pale. Inspekata Amour akashangaa.

    “Una uhakika kwamba aliyekupigia simu ni Ummy na alikwambia kwamba utaona?”

    “Nina hakika”

    “Na una uhakika kwamba ulimuona amesimama mbele yako wakati unafika pale hoteli?”

    “Nina uhakika”

    “Tangu tulipooanza uchunguzi wa Ummy, namba ya Ummy imetegwa na kila anapopiga au kupigiwa simu inarekodiwa. Tutakwenda kampuni ya simu ili tuhakikishe kwamba ni namba ya Ummy iliyokupigia na pia tuhakikishe wakati alipokuwa anakupigia alikuwa karibu na wewe”

    “Nilimuona mbele ya gari akiwa ameshika simu. Nikafunga breki ili nisimgonge. Kumbe nilikanyaga pedeli ya mafuta, nikamgonga. Nilipomgonga alitoweka pale pale, nikaona nimegonga nguzo ya umeme” nikamwambia Inspekta Amour kwa mkazo.

    “Ni kitu kisochoeleweka lakini nitakwenda kwenye kampuni ya simu kufanya utafiti. Laiti tungeuona mwili wake uliogongwa tusingepata utata lakini mwili wa Ummy haukuwepo!”

    “Alitoweka kimiujiza. Yule kweli si binaadamu, ule ni mzuka. Ulitaka

    kuniua!” nikasema kwa jazba.

    “Tulia upate matibabu. Tukio lililotokea ni kubwa”

    “Nimekuelewa Inspekta”

    Inspekta huyo akaniaga na kutoka.

    Yule daktari pamoja na wauguzi wake nao waliondoka. Akabaki yule polisi aliyekuwa na bunduki ambaye sikujua alikuwa akisubiri nini.

    Baadaye kidogo muuguzi mmoja alikuja na chano cha dawa. Akanipa tembe za kumeza kisha akanipiga sindano na kuondoka.

    Tukio lile lililotokea lilikuwa limeushitua moyo wangu na kuniacha katika hali mbaya. Kila wakati ile picha ya kumuona Ummy akiwa amesimama mbele ya gari huku akiniambia.

    “Utaona leo...utaona leo!” ilinijia akilini ikifuatiwa na ile picha ya kumgonga kisha ghfla akanipotea na kuona nimegonga nguzo ya umeme.

    Zilikuwa picha zilizonisisimua na kunitia hofu ya kufa. Kama nilinusurika kufa pale, nilijua si muda mrefu Ummy ataniua kama alivyowaua wadaiwa wa babu yangu.

    Nilijua kikubwa kilichompa hasira ni kugundua kuwa nilishirikiana na polisi kumuwekea mtego wa kumkamata. Bila shaka Ummy aligundua kuwa polisi walitaka kumkamata ndipo akaona

    anikomoe.

    Sikuweza kujua gari langu liliharibika kiasi gani na lilikuwa wapi. Na pia sikuweza kujua ule moto uliendelea kuwaka hadi muda gani na ulisababisha hasara ya kiasi gani.

    Laiti ningejua kuwa tukio lile lingetokea, katu nisingekwenda kule Lux Hotel wala nisingekubali kumuwekea mtego Ummy wakati nikijua fika kuwa alikuwa mzuka.

    Lakini nikajiuliza, Mzuka huo ulikuwa

    una lengo gani na mimi?

    Sikuweza kupata jibu mara moja.

    Baada ya muda kidogo niliona polisi watatu wa usalama barabarani ambao walikuja kuchukua maelezo yangu.

    Walitaka kujua jinsi ile ajali ilivyotokea, nikawaelezo lakini niliona wazi kuwa polisi hao hawakuamini maelezo yangu yote. Nusu waliyamini lakini nusu hawakuyaamini.

    Kwamba yule msichana ambaye nilipanga na Inspekta Amour tumuwekee mtego alitokea mbele ya gari langu na kisha nikafunga breki na yakatokea yaliyotokea, polisi hao hawakuamini.

    Lakini walitimiza jukumu lao la kuandikisha maelezo yangu kama

    nilivyoyatoa wakaniambia niweke saini,

    nikaweka saini.

    Walipokuwa wanataka kuondoka niliwauliza hali ilivyokuwa baada ya ajali hiyo. Polisi hao walinieleza kwamba ajali hiyo ilikuwa kubwa na kwamba transfoma iliyokuwa katiika nguzo za umeme ililipuka moto na kusababisha nyaya za umeme kutoa cheche za moto na moto kusambaa katika eneo kubwa.

    Walinieleza kuwa baadhi ya nyaya zilikatika kwa mlipuko na kuanguka chini.

    Patashika iliyotokea ilisababisha shughuli kusimama kwa muda katika hotelli ya Lux ambapo wateja walikimbia ovyo kwa hofu.

    Ile habari nayo ikazidi kunifadhaisha.

    Nikajiambia huo mpango ulipangwa na polisi, mimi nilifuatisha tu maelekezo ya polisi.

    Baada ya kupita kama saa nne hivi, Inspekta Amour akarudi tena pale hospitali.

    “Ni kweli ulivyosema” akaniambia na kuongeza.

    “Sauti ya Ummy imenaswa na amesikika akisema “Utaona leo!” Alikuwa akipiga simu kwenye namba yako. Vile vile mionzi ya simu yake ilionesha kuwa ilirushwa katika mnara mmoja na mionzi ya simu yako. Watu wa kampuni ya simu wameniambia hii inaonesha kuwa ni kweli mlikuwa karibu au mllikuwa katika eneo lile lile”

    Inspekta huyo aliponiambia hivyo nikamuuliza kwa pupa.

    “Umeamini sasa…umeamini sasa….? Yule msichana ni mzuka! Kama alikuwa pale, sasa yuko wapi? Mbona hakuonekana

    tena?”

    Inspekta Amour akanyamza kimya.

    Nilikaa pale hospitali kwa siku tatu. Polisi aliyekuwa na bunduki alikuwa akibadilishana zamu na mwenzake kila baada ya saa nane. Baadaye niligundua kuwa polisi hao walikuwa wakinilinda mimi kwani nilikuwa chini ya ulinzi.

    Asubuhi ya siku ya tano nilitolewa hapo hospitali. Nikapelekwa mahakamani moja kwa moja. Huko nilifunguliwa mashitaka ya kuendesha gari kwa uzembe, kugonga nguzo ya umeme na kusababisha hasara ya karibu shilingi milioni hamsini.



    Kwa kweli nilishangaa kuona polisi wamenigeuka na kunifungulia mashitaka. Maelezo yalikuwa yamegeuzwa. Badala yake nimeshitakiwa kwa kuendesha kwa uzembe wakati

    hapakuwa na uzembe wowote. Kilichotokea kilikuwa miujiza tu.

    Kadhalika nilikuwa nimemgonga Ummy na polisi wamekwenda kampuni ya simu na kuthibitisha kuwa Ummy alinipigia simu na alikuwa mbele ya gari langu lakini hakutajwa kuwa nilimgonga.

    Inspekata Amour sikumuona tena. Kweli polisi hana rafiki. Anakuwa rafiki yako pale anapotaka lake.

    Baada ya kusomewa mashitaka hayo na kuyakana, upande wa mashitaka ulisisitiza kuwa nisipewe dhamana kwa sababu ninaweza kuingilia na kuharibu uchunguzi wao kwani uchunguzi wa tukio hilo ulikuwa bado unaendelea.

    Nikapelekwa rumande.

    Ile kesi iliendelea kuunguruma kwa miezi minne. Wakati wote huo nilikuwa nimewekwa mahabusi. Japokuwa uchunguzi wa polisi ulikuwa umekamilika, nilinyimwa dhamna kwa madai kuwa hasara niliyoisababisha ni kubwa na ningeweza kutoroka kama nitaachiwa kwa dhamana.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Inspekta Amour alikuwa ndiye shahidi wa kwanza aliyekuja kutoa ushahidi dhidi yangu. Aliieleza mahakama kuwa alinifahamu nilipokwenda katika kituo cha polisi anachofanyia kazi na kuripoti kuhusu msichana anayeitwa Ummy ambaye alikuwa ananisumbua.

    Alieleza kuhusu uchunguzi wake na jinsi alivyogundua kuwa msichana huyo alikuwa ameshakufa lakini kulikuwa na vielelezo na ushahidi kuwa alikuwa hai.

    “Kwa vile tulitaka kumkamata tulimwambia mshitakiwa kuwa atakapopigiwa simu na msichana huyo apange naye mahali pa kukutana na atuarifu ili twende tukamkamate” Alieleza Inspekata Amour.

    Huku akiongozwa na Mwendesha Mashitaka, Amour aliendelea kueleza jinsi nilivyowaarifu kuwa Ummy alinipigia simu na nilipanga kukutana naye katika goteli ya Lux saa nne asubuuhi ambapo Amour aliandaa mtego wa kumkamata msichana huyo.

    Lakini wakati polisi wanajiandaa kwenda hukohoteli ya Lux ndipo walipopata taarifa ya ajali ya gari iliyogonga nguzo ya umeme na kusababisha moto mkubwa kuwaka.

    “Tulipofika hapo hoteli tulikuta aliyesababisha ajali hiyo alikuwa mshitakiwa. Tulikuta gari lake likiwa pembeni mwa nguzo zilizokuwa zinawaka huku mwenyewe akiwa amezirai. Tukafanya jitihada za kuokoa maisha yake” Inspekta Amour alisema.

    Aliendelea kueleza kuwa baada ya kufanikiwa kunitoa kwenye gari na kunipakia kwenye gari la hospitali, kikosi cha zima moto kiliendelea na jitihada ya kuuzima moto huku wafanyakazi wa shirika la umeme wakiwa wameingia kazini kuzima umeme katika eneo hilo.

    “Uchunguzi wetu umeonesha kuwa ajali ile ilitokana na uendeshaji wa kizembe wa mshitakiwa ambaye bila kuwa muangalifu na kujali sheria za usalama barabarani aligonga nguzo za umeme zilizokuwa zimebeba transfoma na kusababisha mlipuko wa moto” Inspekta Amour alimalizia hivyo maelezo yake.

    Baada ya inspekta Amour, alikuja polisi wa usalama barabarani ambaye alionesha vipimo vya jinsi ajali ilivyotokea na kueleza kwamba niliacha njia sahihi na kwenda kugonga nguzo za umeme.

    Shahidi mwingine alikuwa afisa mmoja wa shirika la umeme ambaye alieleza kuwa kugongwa kwa nguzo za umeme kulisababisha transfoma ya shirika hilo kulipuka na kuwaka moto.

    Afisa huyo aliendelea kueleza kuwa hasara waliyoipata kutoka na tukio hilo ilifikia shilling milioni hamsini.

    Wakati mashahidi hao wakitoa ushahidi wao, kichwa kilikuwa kinaniuma na kilikuwa kizito kwa mawazo yaliyochnaganyika na fadhaa hasa nilipowaza kwamba kesi ile ingenifunga

    miaka mingi.

    Baada ya mashahidi hao kutoa ushahidi wao, kesi iliahirishwa na kupangiwa tarehe nyingine ya usikilizaji.

    Nilirudishwa mahabusi ambako

    niliendelea kusota na kuwazia maisha yangu ambayo niliona yalikuwa yameshafikia kikomo kwani nilijjua kuwa nitafia jela.

    Tarehe ya kuendelea kwa kesi hiyo ilipowadia nilipelekwa mahakamani nikiwa na hali mbaya ya kiafya kwani nilikuwa nimekonda. Kule mahabusi nilikuwa sili chakula vizuri kutokana na fadhaa.

    Vile vile nilikuwa nikimlaani Inspekta Amour aliyekuwa amenigeuka ili kulinda kazi yake. Amour alifahamu fika kuwa ajali ile ilitokea kimiujiza na si mimi niliyeisababisha lakini alitoa maelezo ya kunitia katika hatia.

    Kesi iliendelea kwa mashahidi mbalimbali kuja kutoa ushaidi wao. Katika kipindi chote wakati ushahidi unatolewa nilipewa nafasi ya kuuliza maswali kama kulikuwa na kitu sikubaliani nacho. Lakini ukweli ni kwamba nilishindwa kuuliza chochote.

    Nilishindwa kwa sababu ya kutojua sheria na pia kupatawa na hofu.

    Pale nilielewa ni kwanini hata wanasheria wanapokabiliwa na kesi wanaweka mawakili wa kuwatetea. Ni kwa sababu wao wenyewe licha ya kujua sheria wasingeweza kujitetea vizuri kwa sababu ya hofu.

    Baada ya upande wa mashitaka kumaliza kuleta mashahidi wake, hakimu alisoma muhutasari wa kesi na kueleza kuwa nina kesi ya kujibu, kwa hiyo nilitakiwa nijitetee.

    Niliulizwa kama nilikuwa na mashahidi, nikajibu kuwa sikuwa na shahidi yeyote.

    Baada ya kujibu hivyo nilitakiwa niandae utetezi wangu ili kesi itakapoitishwa tena niweze kujitetea.

    Baada ya hapo kesi ikaahirishwa na kupangiwa tarehe nyingine.

    Siku hiyo ilipofika nilipelekwa tena mahakamani ambako nilijitetea kwa kuieleza mahakama kuwa tukio lile la ajali lilitokea kimiiujiza na kwamba ajali ile sikuisababisha mimi.

    Hakimu aliandika maelezo yangu na kupanga tarehe ya kutoa hukumu.

    Usiku wa siku ile ya kutolewa hukumu niliota ndoto mbaya sana. Niliota ninahukumiwa kifungo cha miaka thelathini jela na kutakiwa nililipe shirika la umeme shilingi milioni hamsini.

    Nilikuwa sina pesa hizo nikajikuta nimetupwa jela. Baada ya kusota jela

    kwa mika thelathini, eti nikaona ninatoka jela nikiwa mzeee ninayetembea kwa mkongojo!

    Ndoto ile ilinishitua sana nikajua ndio

    mambo yatakavyokuwa.

    Asubuhi nilipelekwa mahakamani kwenda kusikiliza hukumu yangu.

    Jalada langu lilipoitishwa nilipanda kizimbani na hakimu akanisomea hukumu aliyokuwa ameniandalia.

    Alianza kuyataja mashitaka yaliyokuwa

    yananikabili na akaeleza kuwa niliyakana mashitaka yote niliyosomewa.

    Baada ya hapo akaanza kuuchambua ushahidi uliokuwa umetolewa na upande wa mashitaka. Alianza kuuchambua ushahidi wa Inspekta Amour.

    Akaeleza kuwa ushidi huo anaukubali kwa vile mimi kama mshitakiwa nilishindwa kumhoji shahdi huyo chochote ikimaanisha kuwa nilikubaliana nao.



    Akaja kwenye ushahidi wa polisi wa

    usalama barabarani ulioonesha jinsi ajali ilivyotokea. Akaeleza kuwa pia amekubaliana na ushahidi huo uliokuwa na vipimo vya polisi ambao walipima

    ajali hiyo.

    Ushahidi wa afisa wa shirika la umeme uliotaja tathmini ya hasara iliyotokea nao ulichambuliwa na kukubaliwa.

    Wakati wote niliokuwa nikisikiliza hukumu hiyo, moyo wangu ulikuwa ukienda mbio

    kama saa. Na mara moja moja miguu yangu ilikuwa ikitetemeka.

    Hakimu alipomaliza kuuchambua ushahidi wa mashahidi wote alisema

    kuwa mashitaka yote matatu

    niliyoshitakiwa yalikuwa yamethibitishwa bila kuacha shaka yoyote.

    “Kutokana na ushidi huo, mahakama hii inakutia hatiani kwa makosa yote matatu.…”Hakimu aliniambia huku akinitazama.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ingawa nilijua kuwa ningetiwa hatiani, nilishituka. Uso wangu ulionesha wazi kupigwa na butwaa.

    Sasa hapo ilikuwa ni kutiwa hatiani tu, bado adhabu. sikujua ningekula miaka mingapi. Nikapatwa na kihoro kilichofanya nimkodolee macho hakimu.

    “Adhabu” Hakimu alisema baada ya kuyageuza macho yake kutoka usoni kwangu na kulitazama jalada alilokuwa akilisoma.

    “Baada ya kukutia hatiani ninakuhukumu adhabu ya kulipa faini ya shilingi laki tatu au kifungo cha miezi mitatu kwa kosa la kwanza ambalo ni la kuendesha kwa uzembe”

    Hakimu alipenua ukurasa mwingine akaendelea kusoma.

    “Pia ninakuhukumu kifungo cha miaka miwili kwa kosa la kugonga nguzo za umeme au ulipe faini ya shilingi milioni kumi”

    Hakimu alisita akanitazama kabla ya kuendelea.

    “Kwa kosa la tatu ambalo ni kulitia hasara ya shilingi milioni hamsini shirika la umeme, ninakuhukumu kifungo cha miaka mitatu jela au ulipe faini ya shilingi milioni kumi na tano pamoja na fidia ya shilingi milioni hamsini ambayo unatakiwa uwalipe shirika la umeme”

    Hakimu alimaliza kupigilia msumari kwenye moyo wangu. Msumari huo ulikuwa umenimaliza kabisa.

    Ilikuwa hukumu ambayo sikuitarajia kabisa. Nilijiuliza.

    “Nitapata wapi pesa hizo za kulipia faini pamoja na fidia ya shilingi milioni hamsini?

    Hapo ilikuwa ni kukubali tu kufungwa, hakukuwa na jingine.

    “Kama utaweza kulipa faini na kulipa fidia utakuwa umeepukana na adhabu ya kifungo” Hakimu aliendelea kunifahamisha.

    “Na kama utatumikia kifungo bado utalazimika kulipa fidia baada ya kifungo chako” hakimu alimaliza hukumu yake.

    Nilihisi kijasho chembamba kikinitiririka kwenye uti wa mgongo wangu. Yalikuwa ni matokeo ya joto lililofumka ghafla mwilini mwangu.

    Baada ya kusomewa hukumu hiyo nilikuwa kama niliyepatwa na wazimu. Nilikuwa nikisema peke yangu huku nikiwalaumu polisi hususan Inspekta Amour..

    “Mshitakiwa utalipa faini na fidia au utatumikia kifungo ambapo utakapomaliza kifungo chako utalazimika kulipa fidia ya shilingi milioni hamsini” Hakimu akaniuliza baada ya kimya kifupi.

    Sikuwa na jibu. Akili yangu ilikuwa imeruka. Pakapita ukimya wa karibu sekunde tatu kabla ya kuisikia sauti ya mwanamke ikisema.

    “Mheshimiwa nitamlipia fainii pamoja na fidia ili asitumikie kifungo”

    Maneno hayo yalinishitua, nikageuza uso wangu kuelekea upande sauti hiyo ilikotokea.

    Ilitokea kwenye safu za watu waliokuwa wakisikiliza ile kesi. Kulikuwa na msichana mmoja aliyekuwa amesimama akimtazama hakimu. Nikahisi yeye ndiye aliyesema atanilipia faini pamoja na fidia.

    “Hebu tokea hapa mbele” hakimu alimwambia.

    Msichana huyo alitoka na kusimama karibu na meza ya mwendesha mashitaka. Nilipomtazama vizuri nilishituka nilipogundua kuwa alikuwa Ummy!

    Alikuwa amevaa wigi lililompendeza na alipachika begani mkoba wa ngozi ya pindamilia uliokuwa umeendana na vazi allilokuwa amevaa.

    “Hebu rudia ulichosema” hakimu akamwambia.

    “Nimesema kwamba nitalipa faini na fidia aliyotozwa mshitakiwa”

    “Umeisikiliza kesi vizuri?” hakimu akamuuliza.

    “Ndiyo, nimeisikiliza”

    “Umeisikia na hukumu niliyoitoa hapa?”

    “Nimeisikia”

    “Utamlipia faini ya kiasi gani na fidia ya kiasi gani?”

    “Kiasi chote kitakachohitajika”

    “Fidia peke yake ni shilingi milioni hamsini!”

    “Ninajua mheshimiwa”

    “Haya nenda kalipe”

    Hakimu akamtaka polisi aliyekuwa akinilinda kufuatana na Ummy pamoja na mimi kwenda kulipa faini na fidia.

    Sikuamini na sikujua kama Ummy angeweza kulipa kiasi cha pesa kilichohitajika. Lakini katika hali ya kushangaza Ummy alitoa katika mkoba wake maburungutu ya noti nyekundu ambayo aliyakabidhi kwa karani wa mahakama.

    Taratibu za kulipa faini na fidia pamoja na kuachiwa huru zilichukua karibu saa moja. Wakati ule Ummy akinilipia pesa hizo nilijikuta nikimheshimu na kumchukulia kama mkombozi wangu ingawa ndiye yeye aliyekuwa ameniangamiza.

    Nilipoachiwa huru na kutoka nje ya mahakama nikakutana na Imspekta Amour, akanipa mkono na kunisalimia.

    “Pole sana na hongera” akaniambia kwa uso mkavu usio na aibu.



    Baada ya kuachiwa huru na mahakama nilimshukuru Sana ummy kwa kuniokoa na kifungo kile japo nilijua wazi msababishaji ni yeye.

    Ummy alinitaka tukutane saa 11 jioni ya siku ile japo sikua tayari ila niliogopa kumkatalia.

    Naomba tukutane kwa mazungumzo zaidi Leo saa 11 kwenye bustani ya mnazi mmoja.

    Nilimwitikia sawa ningefika mahala hapo kwa mda aliopanga.

    Niliagana na ummy na kurudi nyumbani.Niliendelea na kazi za nyumbani masaa nayo yalikatika haraka nikifikiria kuhusu kukutana na ummy tena kutokana na visa na makubwa yaliyonikuta kutokana na ummy nilijikuta na kuwa mzito Sana kukubaliana na wazo la kukutana naye tena. Niliamua nipuuzie wito wake wa kukutana naye kwa kuepusha makubwa zaidi. Mda alioutaja tukutane ulifika na ukapita nilitegemea ningepokea hata simu au ujumbe wa simu kuniuliza kwanini sikufika lakini haikua hivyo.Usiku uliingia Niliendelea na mambo mengine ya nyumbani mda wa kulala ukafika nikalala japo nilikua na mfikiria Sana Ummy ila sikuchukua mda nilipitiwa na usingizi wakati nikiwa nimelala kunakitu nilikisikia nje Nikatega masikio yangu kusikiliza vizuri ili nijiridhishe kuwa mlango wa nje

    ulikuwa unabishwa. Mlango huo ukabishwa tena.

    “Hodi! Hodi!” Sauti ya mwanamke ikasikika.

    Nikanyamza kimya huku nikijiuliza ni nani abishaye mlango usiku ule. Ile sauti iliporudia tena kupiga hodi nikaigundua kuwa ilikuwa sauti ya Ummy.

    Nikashituka. Ummy ameamua kunifuata nyumbani usiku?

    Wakati najiuliza hivyo nikasikia mlango wa nje unafunguliwa. Nikasikia kama viatu vya Ummy vikitembea ukumbini hadi kwenye mlango wa chumba changu. Kitendo hicho kilinishangaza kwa sababu sikujua ule mlango uliwezaje kufunguka wakati hakukuwa na mtu aliyeufungua.

    Ndani ya ile nyumba nilikuwa ninaishi peke yangu.

    Sasa mlango wa chumbani mwangu nao ukaanza kubishwa!

    Nikaisikia sauti ya Ummy ikipiga hodi.

    “Hodi! Hodi!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hapo ndipo nilipoanza kutetemeka nikijua kuwa sasa Ummy ananiingilia chumbani mwangu.

    Nilikuwa nimejifinika shuka shuka gubigubi huku nimetega masikio yangu kwenye mlango. Jinsi nilivyokuwa nikitetemeka sikutofautiana na mgonjwa wa homa ya baridi aliyekuwa amefinikwa shuka.

    Licha ya kuisikia waziwazi sauti ya Ummy ikipiga hodi kwenye mlango wa chumbani kwangu sikuthubutu kujibu chochote.

    Nilijua kuwa maana ya Ummy kuopiga hodi ni kutaka nimkaribishe chumbani mwangu lakini wakati huo huo alishaingia ndani ya nyumba yangu bila

    kumkaribisha.

    Nikajiambia hata kama sitamfungulia mlango wa chumbani, ataingia mwenyewe kama alivyoingia ukumbini.

    Kunyamza kimya kwangu kusingesaidia kumzuia msichana huyo asiyeeleweka kuniingilia chumbani.

    Nikajikuta nikijuta kwa kutotimiza ile ahadi tuliyowekeana ya kukutana saa kumi na moja jioni kwenye bustani ya Mnazi Mmoja. Kama tungekutana, Ummy asingekuja nyumbani kwangu usiku huo. Nilijua kuja kwake kulitokana na mimi

    kutotimiza ahadi yangu.

    “Hodi! Hodi!” Sauti ya Ummy iliendelea kusikika mbele ya mlango.

    Alipoona simjibu aliniambia.

    “Kama hunijibu, naingia chummbani mwako!”

    Maneno hayo ndiyo yaliyonipasua moyo wangu, nikawa nahema kama niliyemuona Ziraili akiniambia amekuja kuitoa roho yangu.

    Mara ile ile nikausikia mlango wa chumbani mwangu ukitoa mlio wa kufunguliwa.

    Nikafungua shuka kwenye usawa wa macho yangu na kuchungulia. Nikamuona Ummy Nasri akiingia chumbani. Alikuwa amevaa viatu vya mchcumio vilivyokuwa vikitoa mlio wakati akitembea.

    Alipoingia chumbani kwangu macho yake yalikwenda kwenye kitanda nilichokuwa nimelala. Akawa anakisogelea kitanda hicho huku akinitazma jinsi nilivyokuwa nimejifinika shuka. Ili asione kuwa niko macho nilifumba macho yangu niikajifanya nimelala.

    Ummy alitembea kwa mwendo wa taratibu akafika kando ya kitanda

    changu. Akasimama na kukitupia macho chumba changu kisha akakaa kwenye pembe ya kitanda changu ambapo palikuwa na nafasi ndogo.

    Akaniita kwa kulitaja jina langu. Nikanyamaza kimya.

    “Mimi najua kuwa uko macho na umesikia wakati naingia ndani ya nyumba hii” akaniambia lakini mimi niliendelea kunyamza.

    “Umenyamza lakini mwili wako unatetemeka, inaonesha kuwa uko macho na umeshaniona” Ummy aliendelea kuniambia kwa kunisuta.

    Mtetemeko ulikuwa umeniumbua lakini sikuwa na namna ya kujizuia nisitetemeke.

    “Inuka tafadhali”

    Nikaitenga shuka na kuinuka, nikakaa kitandani.

    “Mimi ni Ummy Nasri” Ummy akaniambia mara tu alipoona nimeketi kitandani.

    “Nimeamua kuja nyumbani kwako baada ya kuona umekuwa ukinikwepa sana. Kama ungejua usingenikwepa kwani nina habari zenye manufaa kwako wewe” Ummy aliendelea kuniambia.

    Ummy akanyamaza kidogo na kunitazama kisha akaendelea.

    “Nataka kukupa hadithi fupi kuhusu marehemu babu yako. Babu yako alimpenda sana Ummy Nasri mpaka alimuachia mali zake, lakini Ummy hakumtaka babu yako zaidi ya kutaka kumla pesa zake kwa sababu babu yako alikuwa mzee”

    Ummy aliendelea kuniambia.

    “Kuna mwanamke wa kijini ambaye alimchunuka babu yako. Mwanamke huyo alitaka aolewe na babu yako na aliahidi kumpa utajiri. Alimfuata babu yako mara kadhaa lakini babu yako hakuwa tayari kukubaliana na jini huyo na sababu kubwa ni kuwa moyo wa babu yako ulikuwa kwa Ummy Nasri.

    “Huyo jini akachukua uamuzi wa kumuua Ummy Nasri kisha akavaa sura ya Ummy na hapo akamfuata babu yako na kumwambia yeye ni Ummy anataka waoane. Ndipo babu yako alipooana na jini huyo akijua ameoana na Ummy Nasri. Babu yako akapata utajiri mkubwa sana.

    “Jini huyo alimuonesha babu yako mahali ambapo angepata madini ya Tanzanite ambayo aliyauza nje ya nchi na kumpatia pesa nyingi”

    Maneno ya Ummy sasa yakaanza kuniingia vizuri kichwani mwangu kwani ni kweli babu yangu alikuwa akiuza madini hayo nje ya nchi na mara kadhaa niliwahi kujiuliza babu yangu alikuwa akiyapata wapi madini hayo.

    Ummy aliendelea kuniambia.

    “Jini huyo aliendelea kuishi na babu yako. Babu yako alipokufa yule jini alichukua mali yote aliyompa na ndiyo

    maana wewe hukupata mali yote ya babu yako na umekuwa ukijiuliza utajiri wa babu yako umekwenda wapi”

    Maneno hayo sasa yalianza kuzindua akili yangu. Sasa nikaanza kufahamu asili ya utajiri wa babu yangu na jinsi utajiri huo ulivyotoweka mara tu mwenyewe alipokufa.

    “Umekuwa ukinidhania kuwa mimi ni mzuka wa Ummy. Ukweli ni kwamba mimi ndiye huyo jini niliyevaa sura ya Ummy ambaye nilikuwa mke wa babu yako. Mimi ndiye niliyempa utajiri babu

    yako na mimi ndiye niliyeupoteza utajiri huo mara tu baada ya babu yako kufa” Ummy aliendelea kuniambia.

    Nikainua yangu yangu na kumtazama mwanamke huyo usoni.

    “Niangalie vizuri. Mimi ni mwanamke wa kijini” Mwanamke huyo akaniambia na kuongeza.

    “Jina langu ninaitwa Maimun. Usilinganishe na Maimuna. Mimi ni Maimun binti Hashhash”



    Nikainamisha uso wangu na kuanza kuwaza kwamba kumbe yule mwanamke aliyekuwa akitusumbua alikuwa jinni na si mzuka wa Ummy.

    “Nilikuelekeza uende nyumbani kwa kina Ummy uniulizie, lengo langu ni kutaka kukuonesha miujiza. Baada ya Miujiza ile nilitaka tukutane nikueleze ukweli lakini ulikuwa ukinikwepa hadi hii leo nilipofanya uamuzi wa kukufuata nyumbani kwako” Maimun aliniambia.

    Akaendelea. “Najua kilichokutisha ni jinsi nilivyowaua wale watu kule Botswana, Zimbabwe na Afrika kusini. Wale watu baada ya kugundua kuwa aliyewapa mali alikuwa amekufa walipanga njama za kukuua. Ndipo nilipochukua uamuzi wa kuwaua wao mmoja baada ya mwingine. Wewe hujui tu lakini mimi nipo na wewe tangu babu yako alipofariki”

    Wakati wote huo nilikuwa kimya nikimsikiliza kwa makini mwanamke huyo.

    “Nilikwambia kuwa ninaijua siri ya mali ya babu yako, siri yake ndiyo hiyo. Utajiri wa babu yako ninao mimi na ninakusudia kukupa wewe. Lakini nisingekupa mpaka nikutane na wewe kama tulivyokutana hii leo na unirithi mimi”

    Nikainua uso wangu na kumtazama mwanamke huyo huku nikimfananisha na jini. Hakuonesha ishara yoyote ya kuwa jini zaidi ya ile miujiza yake alionionesha siku ile katika eneo la hoteli ya Lux. Ile miujiza pekee ilitosha kunipa imani kuwa alikuwa jini kweli.

    “Nikurithi kivipi?” nikamuuliza.

    “Unirithi kama mke wa babu yako na uendelee kuishi na mimi kama mke wako”

    “Mimi sijui mlikuwa mnaishi namna gani?”

    “Tulikuwa tunaishi kama mke na mume. Tofauti ilikuwa mimi ni jini, yeye ni binaadamu”

    Nilijaribu kuwaza kwamba ninaishi na mwanamke ambaye ni jini nikaona jambo hilo haliwezekani.

    Nikatikisa kichwa.

    “Naona kama haiwezekani kuishi na mwanamke ambaye ni jini”

    “Inawezekana. Mbona babu yako aliweza”

    “Sijui alikuwa akitumia mbinu gani kuishi na wewe”

    “Haihitaji mbinu. Tunaishi tu kama mke na mume. Vile ambavyo utamtumia mke wako ndivyo ambavyo utanitumia mimi. Na vile ambavyo mimi nitamtumia mume wangu ndivyo ambavyo nitakutumia wewe”

    “Unaweza kunipa muda wa kufikiria jambo hilo na kunipa muda wa kujiandaa”

    “Ninaweza. Niambie nikupe muda wa siku ngapi?”

    “Nipe muda wa wiki moja tu”

    “Sawa. Nitakupa muda wa wiki moja. Lakini nitakuwa na masharti yangu

    ambayo ni lazima uyafuate”

    “Masharti gani?”

    “Kwanza sitataka ujihusishe kimapenzi na mwanamke mwingine. Pili kila jambo ambalo utalifanya ni lazima utake ruhusa kutoka kwangu. Na mimi kila jambo ambalo nitalifanya ni lazima nitake ruhusa kutoka kwako”

    “Sawa. Na kuhusu huo utajiri nitaupataje?”

    “Utaupata wakati tutakapokuwa tumekubalina kuwa wanandoa”

    “Sawa”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pakapita ukimya wa karibu sekunde kumi. Maimun alikuwa akikikodolea macho chumaba changu.

    “Sasa mimi nakwenda zangu” akaniambia baada ya sekunde hizo.

    “Sawa, tutawasiliana”

    Maimun akainuka kutoka kitandani na kuniambia.

    “Kwaheri”

    “Karibu sana”

    Akageuka na kuelekea kwenye mlango. Alifungua mlango akatoka. Nikainuka na kumfuatia ukumbini. Sikumuona tena. Nilikwenda kwenye mlango wa mbele

    nikaukuta umefungwa kwa ndani.

    Sikuweza kujua alitoka vipi. Nikarudi chumbani mwangu na kufunga mlango.

    Nilijitupa kitandani na kuanza kuwaza. Kile kitendawili cha Ummy alikuwa nani, kilikuwa kimeshateguka. Sasa nilikuwa nikifahamu kuwa Ummy ni jini na siye yule Ummy tuliyekuwa tukimdhania aliyekuwa amezikwa kaburini.

    Kile kitendo cha kuvaa sura ya Ummy ndicho ambacho kilinichanganya na kumdhania alikuwa mzuka wa Ummy.

    Sasa suala la Ummy ni nani lilikuwa limeshapata jibu. Ummy ni jini na jina lake ni Maimun binti Hashhash. Suala sasa ni la kufikiria kuishi na mwanamke huyo kama mke na mume.

    Awali sikuwa nikijua kama babu yangu alikuwa na mke wa kijini. Kwa vile nilikuwa nikiishi Morogoro sikuwahi kumuona hata siku moja na babu yangu hakuwahi kuniambia. Jambo hilo alilifanya kuwa siri yake.

    Sasa babu ameshakufa, nilijiambia, jini huyo amenifuata mimi na ametaka

    nimrithi.

    Amenipa siku saba za kufikiria ama kumkubalia ama kumkatalia.

    Nikajiuliza endapo nitakubali kumrithi Maimun na kuwa mke wangu faida yake itakuwa ni nini?

    Jibu nililipata mara moja. Faida yake ni

    moja tu, kupata utajiri ambao kila mwanaadamu katika ulimwengu huu anauwania.

    Nikimrithi Maimun nitakuwa tajiri. Nitaishi katika jumba la kifahari na nitakuwa na gari kama sio magari ya gharama. Vile vile nitaishi maisha ya hali ya juu.

    Na je kama sitataka kumrihi athari yake itakuwa nini? Nilijiuliza.

    Jibu hilo lilipaswa litolewe na Maimun mwenyewe lakini nililijibu mimi kwamba endapo sitamrithi Maimun sitapata utajiri. Nitendelea kuishi katika umasikini. Hilo ndilo jibu la haraka haraka nililolipata.

    Usiku ule nilikesha macho nikiwaza hadi asubuhi. Wazo ambalo niliamka nalo ni la kwenda kwa yule mganga wa marehemu babu aliyeko Chanika ili anipe ushauri wake.

    Ilipofika saa nne nikaliwasha gari na kwenda Chanika kwa yule mganga.

    Nilipofika nyumbani kwake nilimkuta akikatakata vipande vya mzizi.

    “Habari za siku nyingi?” akaniuliza.

    “Nzuri. Habari za hapa?”

    “Hapa ni kwema. Karibu sana”

    “Asante. Niimekuja nina tatizo moja. Nataka kupata ushauri wako”

    “Tatizo gani hilo?”

    Nikamueleza kuhusu yule jini aliyekuwa mke wa babu yangu.

    Baada ya kumpa maelezo yangu mganga alishituka na kushngaa. Akaacha kukatakata vipande vya mizizi.



    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog