Search This Blog

JUMBA LA WACHAWI - 4

 





    Simulizi : Jumba La Wachawi

    Sehemu Ya Nne (4)



    “Kwakweli yule kijana ni miaka mingi imepita sijamwona ila niliwahi kusikia kuwa hivi sasa yupo huko Mwanza japo sina uhakika,”

    “Wakati nimepotea yeye hakuwahi kujishughulisha kunitafuta?” niliuliza, japo sikujua kwanini niliuliza swali lile.

    “Hilo kwakweli sijui..sikuwahi kumwona toka ulivyo potea” alisema mama Leila.

    Tangu wakati huo Sikuwa na uelekeo maalumu, sikuwa na mbele wala nyuma katika hii dunia mpya, si mashariki wala magharibi, sikuona kama ninalolote muhimu katika maisha.

    **********************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilikuwa nikiishi nyumbani kwa mama Leila yapata wiki, pale katika ile nyumba yenye kuegama’ upande mmoja.

    Nilikuwa ni msichana mgeni kabisa katika jamii ile mpya, hata wale watu wachache waliokuwa wakinifahamu wengi wao hawakuwa tayari, kuamini kama mimi ndiye yule Zahara waliye mfahamu toka miaka ile, wengi wao kama sio wote waliamini kwa vyovyote vile mimi ni mtoto wa Zahara.

    “Mtoto wa marehemu Zahara anafanana na mama yake vilevile” mtu mmoja wa zamani alikuwa akiongea na mwenzake mtaani nilikokuwa nikikatiza.

    “Huyo binti mwenyewe anaitwa Zahara na nasikia anadai yeye ndiye Zahara”

    “Binti huyo anajitia umajinuni Zahara hawezi kuwa yeye, Zahara alikwisha fariki miaka mingi mno toka mwanzoni mwa mwaka themanini na tisa”

    Yalikuwa ni maneno niliyowahi kubahatika kuyasikia, kila mtu alikuwa akisema lake juu yangu kadri alivyo weza kunijua.

    Nilikuwa ni msichana wa miaka ishirini na nne tu, nilikuwa ni mtu mshamba katika mambo mengi mno, kila kitu katika maisha yangu kilikuwa kipya.

    Sikuwa mimi tena yule mwandishi wa magazeti maalufu hapa nchini, gazeti nililokuwa nikiandikia halikuwepo kabisa katika ulimwengu wa magazeti.

    Nilikuwa ni binadamu mpweke, marafiki ndugu na jamaa wengi wao niliwapoteza miaka mingi.

    Nilikuwa nikimsaidia kazi za kuuza chakula mama Leila. Kila mara nyakati za usiku tulikuwa tukibeba meza majiko na vyombo kisha tunauza chakula gengeni.

    Siku moja tulikawia kidogo kumaliza kuuza biashara, ilikuwa yapata kama saa tano kasoro za usiku, siku hii biashara haikuwa nzuri sana.hivyo kutokana na muda kuwa umekwenda ilitubidi tufunge na kurejea nyumbani.

    Kwakuwa usiku ulikuwa umekwisha kuwa mkubwa moja kwa moja tulifikia kitandani na kulala.

    Wakati nimekwisha pitiwa na usingizi, kwa mbali nilikuwa nikisikia sauti ya mtoto mchanga ikilia, ilinijia kama ndoto, lakini nikagundua haikuwa ndoto muda wote ilikuwa ikitengeneza karaha kichwani mwangu, nikafumbua macho kivivu nikihisi huenda alikuwa ni mtoto nyumba ya jirani aliyekumbwa na masaibu ya kuto kulala usiku ule.

    Lakini nilistuka nilipo gundua sauti ile haikuwa inatokea nyumba ya pili kwa jilani, isipokuwa sauti ile ilikuwa inatokea chumba cha pili mule mule ndani.

    Sasa vipi sauti hii ya mtoto itokee ndani ya nyumba ile wakati,ndani ya jumba lile tulikuwa tukiishi wawili tu!. Niliwaza.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sauti ile ilizidi kulia kwa kasi, nilipatwa na mashaka na woga mkubwa, nilianza kumwamsha mama Leila aliyekuwa akikoroma.

    “Mama Leila, we mama Leila” nilimwita huku nikimtikisa, ajabu ni kuwa mama Leila alikuwa akiendelea kukoroma na kutoonesha dalili za kuamka.

    Na nilivyokuwa nikizidi kumwamsha mama Leila kwa nguvu ndivyo sauti ya mtoto ilivyozidisha kasi ya kulia.

    Sasa nikawa natetemeka na jasho likinitoka kwani niliona dhahili mazingaombwe mengine yanakaribia maisha yangu. Niliona hilo ni tukio jingine ambalo linakuja katika maisha yangu na pengine ni tukio litakalo badilisha tena maisha yangu japo sikujua safari hii maisha yangu yatakuwa katika hali gani.

    Mara sauti ya kichanga ilinyamaza ghafla, halafu muda huo huo vikafuatia vicheko vingi.Yanii ilikuwa ni kana kwamba wale watu walikuwa wakinicheka mimi kutokana na namna nilivyokuwa na woga na wasiwasi uliotokana na kusikia sauti ya yule mtoto akilia.

    “Ninyi ni akina nani?” nilisema kwa sauti kali ya kushurutisha.

    Vicheko vikanyamaza na kukawa kimya, yanii kimya cha ghafla kama vile hakukuwa na vicheko. “Ninyi ni akina nani..eeh?” nilirudia tena kuuliza kwa ukali baada ya kuwa kimya.

    Kimya kingine..

    Sikusikia chochote wala chakara chakara yoyote, nilitega sikio kwa makini nikitegemea kusikia labda minong’ono ya wale watu lakini kulikuwa na ukimya wa ajabu, ukimya ambao hata sisimizi angetambaa chini ungeweza kumsikia, hali ya ukimya usiku ule ulikuwa ni eneo lote la mtaa ule wa buguruni malapa.

    Niliogopa sana, kwa muda wa dakika sita hadi kumi, nilibaki nimekaa pale kitandani nikitegemea kusikia chochote wakati wowote, lakini muda ulizidi kwenda bila kusikia chochote.

    “Inamaana hawa walozi wananiogopa ama?” niliwaza.

    Wakati huo mama Leila alikuwa akiendelea kukoroma. “Hii hali si ya kawaida vimbweka vyote hivi mtu anakoroma kama amekufa!”

    Baada ya kukaa kitako kitandani kwa muda mrefu pasina kusikia kituko chochote, niliamua kulala, wakati huo ilikuwa yapata saa saba na madakika za usiku.

    Nilijilaza huku nikifikiria suluhu ya matatizo haya yaliyokuwa yananiandama katika maisha.

    Nikiwa pale kitandani usingizi ukiwa umegoma wasiwasi ukiwa mwingi mara nikasikia kitu kingine, nilisikia sauti kama ya moto, tena moto mkubwa unao waka kwa kasi, moto ule ulikuwa ukiwaka nyumba ya pili.

    Nilikurupuka pale kitandani na kuwasha mshumaa, kisha nikasogea katika dilisha na kufungua kisha nikatupa macho nje.

    Sikuamini nilicho kiona moto mkubwa ulikuwa ukiwaka katika nyumba ya jirani, nyumba ile ilikuwa ikiungua kwa kasi kubwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Na mara nikasikia sauti nyingi kutokea nje “moto, moto, moto,moto” sauti za watu wengi zilikuwa zikipiga kelele.

    Ule moto ulikuwa ukiwaka kuelekea katika nyumba yetu, niliogopa mno, na hapo nikarejea kitandani na kumwamsha mama Leila kwa nguvu zaidi, lakini mama Leila hakuamka, alikuwa ni kama mtu aliye kunywa pombe nyingi mno na kuwa hajiwezi. Nilichukua maji ya baridi na kumwagia ili amke na tutoke nje ya nyumba ile ili kuokoa maisha yetu kwa kuungua na moto uliokuwa unawaka kwa kasi kuja nyumbani kwetu.

    Lakini wapi, mama Leila hakuamka.

    Akili yangu ilifanya kazi upesi upesi, niliona ni vema nitoke nje nikaombe msaada kwa watu waje kumtoa nje mama Leila hata kwa kumbeba ili kuokoa maisha yake kutokana na moto uliokuwa ukiwaka kuja katika nyumba ile.

    Nilifungua mlango na kutoka nje.

    Lakini ile natoka tu nje, sikuamini macho yangu, ajabu ni kuwa hapakuwa na kitu kile nilichokuwa nakiona wakati nimo mule ndani.

    Hapakuwa na moto uliokuwa ukiwaka na kuchoma nyumba, na hata zile sauti zilizo kuwa zikisema “moto, moto moto” HAZIKUWEPO TENA.

    Pale nje palikuwa hakuna mtu hata mmoja kulikuwa kimya na eneo lile lilikuwa shwari kabisa.

    Nilihisi mwili ukinisisimka kwa kituko kile, nilijikuta nikiwa nimeduwaa huko hofu kuu ikiwa kifuani mwangu, mate mepesi yalinijaa mdomoni na hapo nikajikuta napiga kelele nyingi na kupiga hatua kubwa kurejea ndani.

    Nilipo ufikia mlango wa kuingia ndani nilipo usukuma, haukufunguka, nikasukuma tena kwa nguvu lakini ulikuwa mgumu, ulifungwa kwa ndani, haukufunguka.

    Na wakati huo huo nikasikia vile vicheko vya awali vikitokea mule ndani.

    Niliendelea kutishaka pasina kifani.

    Sasa nikawa sielewi, aidha niingie ndani ambamo kuna viumbe visivyo onekana ama nibaki pale nje.

    Jibu rahisi likaja, ni kheri kubaki pale nje kuliko kuingia mule ndani ambamo kuna viumbe wa ajabu tena wasio onekana, wenye kutia wasiwasi na mashaka, lakini bado hofu yangu ilikuwa juu ya mama Leila aliyekuwa akikoroma mule ndani, sikujua nini hatma ya uhai wake mule chumbani ndani ya lile jumba.

    Nilisogea hatua kadhaa kutoka pale mlangoni vile vicheko kutokea mule ndani nikawa navisikia kwa mbali na badae kidogo vikayeyuka.

    Nikiwa pale nje nikawa nasogea katika ukuta wa jumba lile la mama Leila,nikawa ukingoni kabisa mwa ukuta ule, nikajikunyata, umeme wa tanesko uliokuwa ukiwaka wasaa ule mara ukakatika, na kufanya kuwa na giza zito, giza jeusi, nilizidi kuogopa lile giza kwakweli sikujua nikimbile wapi, moyo wangu haukuwa tayari kurejea mule ndani usiku ule.

    Nikaendelea kujikunya nyuma ya jumba lile katika ukuta, joto siku hii lilikuwa ni kubwa usiku ule. Kwa wakazi wa Dar wanaelewa hili.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikiwa pale ukutani, mbu walikuwa wakinishambulia vibaya mno.

    Bado mashaka yangu yalikuwa makubwa dhidi ya mama Leila mule ndani japo zile sauti sikuzikia tena kutokea ndani.

    Kukawa na kiupepo kidogo, joto likapungua kiasi, kiupepo kile kikaongeza kasi ya kuvuma, na joto nalo likawa linapungua, hata mbu pia wakapunguza kasi ya kuniuma.

    Ule upepo ulio anza kuvuma kama mzaha ukawa upepo mkubwa ukawa unapeperusha takataka nyingi mtaani na kuzisukuma hovyo, mapaa ya nyumba za uswahilini yalikuwa yakilalama kutokana na kuzongwa na upepo ule.

    mimi niliendelea kujikunyata katika ukuta wa lile jumba.

    Machozi yalikuwa yakinitoka na kulia, nilia sana kwa uchungu, sikujua nilimkosea nini Mungu katika maisha hata kukumbwa na mambo yale.

    Kila kilichokuwa kinatokea katika maisha yangu kilibakia kuwa kitendawili ambacho sikujua nani wa kunitegulia.

    Nilijiona ni mtu mwenye mkosi mkubwa katika maisha, siku zote niliamini Mungu ndiye mtatuzi wa mitihani yote migumu kwa waja wake. Bahati mbaya kuliko zote nilizowahi kuwa nazo katika maisha, sikuwa ni mtu mwenye kumcha Mungu.

    Sikumbuki mara ya mwisho kumsujudia Muumba wangu ilikuwa mwaka gani, hili halina maana kuwa sikuwa na dini ama kuamini katika uwezo wa Mungu lahasha.

    Isipokuwa ni kule kujiweka mbali na Mwenyezi wangu, kwani pamoja na mambo yote hayo bado sikuwa na misingi ama njia na taratibu sahihi ya kumuomba Mungu wangu kama ambavyo alivyo amrisha katika vitabu vyake vitakatifu.

    Mara ule upepo uliokuwa unavuma ulibadilika na kuwa kimbunga..kimbunga kilichokuwa kinavuma kwa kuzunguka, kilikuwa kikizunguka kuja katika uelekeo nilikuwapo mimi.

    Niliendelea kujikunyata, nikiwa naogopa mno hali ile, usiku ule ulikuwa ni usiku mwingine wa kutisha na kuogopesha.

    Kile kimbunga kilifika eneo lile nililokuwa nimejikunyata na kuvuma kwa kasi mbele yangu.

    Hata vile vitu vilivyokuwa vikizungushwa na kimbunga kile vilikuwa vikizunguka kwa kasi kama pangaboi .

    Hakikuwa kimbunga cha kawaida, hilo nililielewa, nikiwa nimejikunyata niliangalia vizuri mbele ya kile kimbunga japo kulikuwa na giza lakini niliweza kuona kiumbe kilichokuwa katikati ya kimbunga kile.

    “Uwiiii, mamaaa ,ooooiii” nilipiga kelele nyingi nikiwa nimetoa macho najiburuza kwa makalio kurudi nyuma, mkono wangu nikiwa nimeiweka mbele kuzuia kile kiumbe nilicho nilicho kiona, huku mkono wangu mwingine nikiwa nimeziba mdomo, macho yenye mshangao na hofu kubwa yamenitoka pomoni.

    Kilikuwa ni kiumbe cha kutisha mno, alikuwa ni kama kichwa cha nyati, huku umbo lake likiwa kama la ndege popo, alikuwa na rangi nyekundu umbo lake lote, Macho yake yalikuwa makubwa kama bundi huku zile mboni za macho yake zikiwa zinamg’ao wa rangi ya dhahabu.

    Na kadri nilivyokuwa nikijiburula pale chini ndivyo kiumbe yule alivyokuwa akipiga hatua ndogo kunisogolea akiwa katikati kimbunga kile, kwa hiyo hapo unaweza kuwa umeelewa, yanii kadiri nilivyokuwa nikijongea nyuma ndivyo kile kimbunga kilivyokuwa kikinisogelea taratibu.



    Nikafika mwisho wa kona ya ukuta ule sasa nikawa sina eneo la kusogea, yule kiumbe akazidi kunikaribia nilikuwa nikilia kama mtoto, nilijikojolea.

    Niligundua kitu kingine kwa yule kiumbe, alikuwa na miguu kama ya binadamu lakini katika kiganja cha mguu alikuwa na kwato kama za ng’ombe.

    Mikono yake ilikuwa ya binadamu lakini yenye manyoya mengi na kiganja kikubwa. “uwiiiii” nilipiga ukelele kubwa, akili yangu ilinambia kuwa jini alikuwa mbele yangu.

    Yule kiumbe aliniangalia kwa macho yake ya kuogopesha, mimi pia nikabaki nikiwa nimekodoa macho mbele ya kiumbe yule na kuwa kama mtu aliyenata katika lundo la ulimbo.

    Mara nikasikia sauti fulani niliyo wahi kuisikia mahala fulani, ulikuwa ni wimbo usio kuwa na maana ninayo weza kuielewa, na hata wakati ile sauti inaendelea kupenya masikioni mwangu nikawa nahisi nazongwa na hali fulani ya kupoteza fahamu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ni hapo nilipo kumbuka kuwa sauti ile nilipata kisikia katika lile jumba la ajabu kule mjini, Agrey Kariakoo.

    Nikazidi kuelekea kuzama katika kina kirefu cha bahari ya usingizi.

    Sikuwa tayari kwa hilo, nikakumbuka mbinu niliyo itumia kuepukana na ile sauti ya ajabu,

    Hapo nikasokomeza vidole masikioni mwangu, nikiziba masikio sauti ile isipenye ndani ya kichwa changu.

    Wakati napambana na tendo lile yule kiumbe alikuwa akinitizama huku sura lake baya likiniangalia kwa hasira kubwa.

    Sasa kukawa hakuna ninacho kisikia zaidi ya kuona yale yalikuwa mbele yangu.

    Upepo wa kimbunga uliendelea kuvuma kwa kasi na kadiri nilivyokuwa nikiziba masikio yangu ndivyo upepo ulivyokuwa ukiongeza kasi ya kuvuma, na yule kiumbe akitizima kwa jicho kali la hasira.

    Lakini wakati vile vituko vinaendelea kutokea mara nilistuka nilipo mwona mama leila akitokea nyuma ya nyumba ile.

    “Wee Zahara” aliniita huku akinitizama kwa mshangao. Nilipo mwona nilijiburuza pale huku nikijiweka mbali na yule kiumbe kusogea mahala alipo kuwa amesimama mama Leila.

    Wakati nafanya matukio hayo mama Leila alishikwa na mshangao mkubwa juu yangu, alionekana ni mtu mwenye kutahayari huku maswali yakiwa mengi kichwani mwake.

    Hapo nikagundua jambo moja, ama mawaili, kwanza mama Leila hakuwa anamwona yule kiumbe aliyekuwa mbele yangu, pamoja na kwamba kulikuwa na kimbunga kilicho kuwa kikizunguka kwa kasi hatua chache mbele yangu.

    Lakini jambo la pili nilielewa kuwa mama Leila alikuwa na maswali mengi juu yangu, vipi usiku ule mkubwa, usiku wa giza niwe nje kama mwanga, lakini vipi niwe ni mtu mwenye mashaka woga na wasiwasi kama mtu aliye ona jini mbele yake.

    “We Zahara una nini? Mbona hivyo? na mbona huku sasa usiku huu?”.

    Sikujibu lolote, isipokuwa nilijikuta nikipiga ukelele wa hofu na kusimama kiwazimu kisha nikatoka mbio kuelekea pale alipo kuwa mama Leila.

    Kitendo kile, kilimwogopesha mama Leila yeye pia aligeuka na kukimbilia ndani, alisukuma mlango wa ndani na kujichoma ndani hatua chache nyuma mimi pia linijitoma ndani kwa kasi kisha tukashindilia komeo kwa ndani.

    Tukawa tunahema kwa zamu huku mashaka makubwa yakiwa ndani yetu.

    “Nini kimetokea?” mama Leila alihoji.

    “Hata sijui..ila ni majini..humu ndani kuna majini na wachawi?”nilisema kimajinuni.

    Mama Leila hakunitizama ila alisikiliza kauli yangu kisha akatikisa kichwa kunikatalia. “Hayo majini humu ndani yameingia lini..miaka nenda rudi sijawahi kuona japo unyoya sasa mimi sikuelewi kwakweli Zahara”

    “Mama Leila nimekuamsha mno ila hukuweza kabisa kuamka, vituko vilivyo tokea humu ndani leo si vya kawaida” nilisema, japo uso wa mama Leila alionekana kuanza kujutia uamuzi wa kuishi na mimi ndani ya nyumba yake, uso wake ulizungumza zaidi ya kinywa chake.aliona kama mimi nimemletea mabalaa nyumbani kwakwe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tulibaki kimya kila mtu akiwaza lake, huku ule mvumo wa upepo huko nje ukiwa umepotea.

    “Nimeona kimbunga kikivuma kwa kasi mbele yako nini maana yake? Na kwanini muda huu ukawa nje?” mama Leila aliniuliza.

    Nilimweleza kila kitu kilivyo kuwa usiku ule, tangu vile vituko ndani ya nyumba kutokea chumba cha pili,moto kuwaka nyumba ya jirani na kisha kile kimbunga cha ajabu.

    Ilikuwa ni habari ya kutisha kwa mama Leila lakini bado ilikuwa ni kama hadithi ya kufikirika kwa upande mwingine.

    “Labda naweza kukuelewa kwa huo upepo kwakuwa nimeuona lakini nashndwa kuelewa maelezo yako kuhusu hiki chumba cha pili ulicho sema kuna sauti ya mtoto mchanga na vicheko, hii ni stoo na humo hakuna vitu vingi zaidi ya makorokoro yasiyo na kazi..”

    Nilinyamaza kwakuwa sikujua namna ya kuendela kueleza.

    “Haya mambo ya kiswahili tuwapelekee waswahili mwanangu au unaonaje?” alisema mama Leila baaada ya kifiri kwa muda wa nukta kadhaa.

    “Sijaelewa mama”

    “Ninamaana kuwa kesho kukicha twende kwa mtaalamu huko bagamoyo.”

    Niliifikiri rai hiyo, nikaona siyo wazo baya wala siyo wazo zuri.

    Baya lisilokuwa na madhala ni jema lisilo na faida, niliamini hivyo, nikalala kuisubiri kesho.

    *************



    Siku iliyofuatia alikuwa mama Leila aliyeanza kuamka.

    “Zahara” aliniamsha.

    “Abee ma..ma” niliitika usingizi ukiwa bado machoni mwangu.

    “Sasa mie itabidi nizungukie madeni yangu, ili tupate senti kidogo tutakayo iacha huko kwa mtalamu tuendako, maa na humu ndani sent iliyopo haitoshi.”

    Alisema mama Leila kisha akaondoka. mie nilibaki pale nyumbani nikifanya usafi wa nyumba na mwili wangu mwenyewe. Si unajua mwanamke mazingira, Saa saba juu ya arama mama Leila alirejea.

    “Pesa imepatikana mwanangu lakini safari ya bagamoyo itabidi iwe kesho maana sasa hivi muda umekwenda mno na hili foleni la Dar tunaweza kufika huko saa tatu usiku.” Alisema huku akiangalia saa ya kwenye simu yake na muda ulionyesha ilikuwa ni saa saba mchana.

    “Mie sina neno mama Leila, chochote usemacho ni sawa tu”. Nilisema, na atimae tukakubaliana kesho ndio iwe siku ya safari.

    Siku hiyo hatukwenda kuuza chakula usiku gengeni kwani hatukuwa tumetayarisha chochote.



    Nilitumia muda mwingi kuwaza maisha yangu, mambo mengi yaliyo pita katika kichwa changu yaliniumiza mno.

    Uhai wangu ulikuwa nusu duniani nusu kuzimu,.niliishi maisha ya dhiki japo kitaaluma nilikuwa mwandishi wa habari.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Usiku ulipo ingia muda wote nilikuwa nikifikiria safari ya kwa mganga huko bagamoyo, bado sikuwa na uhakika kama kuna binadamu anaeweza kuwa na uwezo wa kuzuia viumbe vilivyokuwa vimezingira maisha yangu.

    Ulikuwa ni usiku mwingine nikiutafuta usiingizi, huku tumaini langu likiishia mikononi mwa mganga tutakae kwenda kumwona kesho huko wilayani bagamoyo mkoa wa pwani.



    *************



    Asubuhi ya siku iliyofuatia, tuliamka mapema na kupata staftahi ya chai na maandazi kisha tukajiweka vema na safari ya kuelekea bagamoyo ikaanza.

    Tulipanda basi hadi makumbusho kituo kipya cha mabasi ya mjini awali ikiwa pale mwenge, hapo tukachukua gari jingine na sasa tukaanza safari ya kuelekea bagamoyo kwa mganga wa kienyeji.

    Siku hii ya juma pili hakukuwa na foleni kubwa kwa muda wa nusu saa tulikuwa tumekwisha pita tegeta na sasa tulikuwa tukiitafuta bunju.

    Mita kama hamsini mtu mmoja aliyekuwa na gari lake dogo, akionekana kama ni mtu aliye haribikiwa na usafiri wake, alilipiga mkono basi letu dogo aina ya costa.

    Mvulana yule aliingia ndani ya basi kisha safari ya kuelekea bagamoyo ikaendelea.

    Tulipo fika Kituo kimoja mbele abiria aliyekuwa ameketi siti moja na mimi aliteremka, na yule kaka aliye panda basi akiwa ameharibikiwa na usafiri wake njiani aliketi katika siti.

    “Habari yako ant?” alinisalimia. Hata sauti yake ilipo toka kinywani mwake tumbo langu lilipuka na moyo wangu ukapata mstuko, nikajaribu kuikumbuka ile sauti niliwahi kuisikia mahala gani.

    “Mambo vipi ant?” yule mtu alinisalimia tena

    Nilikuwa kama mtu aliyepigwa nusu kaputi,nikabaki nimemkaodolea macho yule mtu.

    “Wewe ni Thabit Talib?”

    “Nani…mimi?”

    “Ndio”

    “Hapana..ila mzee Thabit Talib ni baba yangu mzazi.

    Umemjua vipi baba yangu”

    Yule kijana alisema, Tumbo lilipata joto nikawa nahema kwa kasi, lakini wakati nafikiria maneno ya yule kijana tulikuwa tumefika katika kituo cha kijiji cha msata bagamoyo, na hapo ndio ilikuwa kituo anacho shukia yule kijana.

    “Any way, tumejuana juu juu..lakini labda siku moja tutafahamiana zaidi,..shika hii”alisema huku akitoa kadi yake ya biashara iliyokuwa na mawasiliano yake na kunipatia, kisha yeye akateremka katika gari.

    Nilibaki katika gari nikitafakari lile tukio na kuona ni kama mkanda wa sinema unaopita katika maisha yangu.

    Tuliendelea na safri na mwendo wa kilometa kadhaa tukawa katika mji wa bagamoyo.

    Tulivyo shuka katika gari nilimweleza mama Leila juu ya kukutana na mtoto wa Thabiti mvulana aliyekuwa mchumba wangu wa zamani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama leila pia alishangaa sana, lakini hatukuwa na namna ya zaidi ya kuacha maisha yaende kama yalivyo.

    Tulitembea mwendo kiasi sikumbuki ni eneo gani mama Leila alinipeleka pale Bagamoyo lakini ninacho kumbuka safari yetu ilishia katika kijumba kidogo cha makuti kilicho zingirwa na wigo mkubwa wa fensi ya mifenesi.

    “Karibuni jamani karibuni..”

    Tulikaribishwa na kijana wa miaka kati ya ishirini na nne ama tano, alikuwa mchangamfu mdada mzuri na mrembo wa kuvutia lakini uzuri wake ulipotezwa na matunzo duni aliyoyapata katika maisha yake.

    “Asante ..asante sana” mama Leila aliitikia huku tukiketi katika mkeka mkubwa uliokuwa chini ya mti wa mpogopogo.

    “Haya mtalaamu tumemkuta?”

    “mmh..hapana kaenda musikitini ila ndio mida yake hii”

    Alisema yule mdada chaurembo asiyekuwa na matunzo.

    Tulikaa kumngoja mtalaamu na baaada ya kama ya nusu saa alirejea babu akiwa katika kanzu nyeupee.

    “Mwenyewe huyoo anakuja” alisema yule dada chaurembo, na wote tuligeuza kichwa kumtizama.

    Alikuwa ni mzee wa miaka kati ya sitini ama sabini, alijikongoja taratibu kuja usawa wa pale mkekani tulipo kuwa tumeketi.

    Alipo karibia mita kama kumi na mbili kutoka pale mkekani, mara alisimama ghafla na akabaki ameduwaa huku macho ya uwaoga amenitumbulia, akawa anatetemeka huku ngurumo fulani ya vitu kama maruhani ikawa inamtoka.

    “Weweeee!” alisema kwa mshangao akinisonta na kidole.

    Kila mtu aliyekuwepo pale alibaki na taharuki kuu, hata yule dada niliye mpachika jina la chaurembo aliogopa.

    “Umebeba viumbe wabaya na hatari mnoo sogea mbali na eneo hili upesi..tokaaa..nasema tokenii hapa!.”

    Yule mganga alifoka akinitizama kwa hofu na mshangao akawa ananifukuza.

    Niliendelea kushangaa kile kituko huku yule mganga akiendelea kunitaka nipotee upesi eneo lile.

    Hatukuwa na namna zaidi ya kuondoka haraka pale kwa mganga, lakini si mimi wala mama Leila kila mtu alikuwa na hofu kubwa moyoni mwake.

    Na hata nilivyokuwa nikimwangalia mama Leila nilimwona kabisa kuwa alikuwa akiniogopa mno.

    “Sasa nikwambie kitu Zahara” alisema Mama Leila akitoa noti mbili za shilingi elfu kumi na kunikabidhi

    “Niambie tu mama Leila”

    “Naomba uniwie radhi sana kwa hili ninano kwenda kuliamua kwa sasa”

    “Lipi hilo?”

    “Kwakweli siwezi kuishi na wewe zaidi, niwe tu mkweli ndugu yangu, kwa sasa nakuogopa, kama mtaalamu ninaye mwamini ile kukuona tu kashindwa hata kusikiliza tatizo letu kwa vitu ulivyo navyo mwilini mwako.



    Vipi mimi niweze kubeba matatizo haya kiasi hicho, kwakweli ndugu yangu siwezi?”

    “Sasa mama Leila kama wewe ukiamua pia kuniacha wapi pawe kimbilio langu, kumbuka matatizo haya niliyo nayo sijapenda mie kuyapata.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Lakini pia kumbuka kwa sasa sina sehemu yoyote ni nayo weza kusema nitakwenda kuishi zaidi ya kwako mama Leila…tafadhali” nilisema kinyonge huku kamasi na machozi vikinitoka kwa pamoja.

    “Pole lakini sina wazo tofauti zaidi ya hilo nililokwisha amua, nafsi ya uhai wangu ni muhimu kuliko kitu chochote Zahara.. nasikitika sana lakini sina jinsi”

    Alisema mama Leila, kisha akasimamisha bodaboda na kumtaka dereva ampeleke stendi ya mabasi ya Makumbusho.

    Kwa Muda wa dakika tano nilibaki nimebunga’aa pale barabarani nikiona maisha yangu hayana thamani hata kidogo.

    Mfululizo wa matukio ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea katika maisha yangu yakawa yanapita katika fikra zangu mithili ya mkanda wa filamu.

    Nilifikiria kwa muda kisha nikaona sina namna zaidi ya kurejea Dar ili kuona kama nitaweza kumshawishi mama Leila ili aendelee kunipa hifadhi nyumbani kwakwe nikiwa natafuta ufumbuzi wa masaibu yangu.

    Nilifika jioni Buguruni, na nilipo fika nyumbani kwa mama Leila sikumkuta, zaidi ni kuwa nilikuta begi dogo lililokuwa na nguo zangu chache likiwa limewekwa pale mlangoni huku mlango ukiwa umefungwa kwa kufuri kubwa.

    Hali hiyo ilimaanisha mama Leila hakuhitaji kabisa kuendelea kushi na mimi pale nyumbani kwakwe.

    Nilishusha pumzi ndefu huku nikijaribu kufikiria wapi pa kwenda jioni ile.

    Nilibeba lile begi la nguo na kuondoka pale kwa mama Leila.

    Kwa mujibu wa saa yangu ya mkononi ilikuwa yapata saaa moja za jioni, giza lilikuwa limekwisha funika nuru ya jiji la dar es salam, nikawa nazipiga hatua kuelekea mjini, japo sikujua uelekeo ule hatma yake itakuwa ni wapi ila niliendelea kujisukuma kwa mbele vitendawili vingi katika maisha yangu vikiwa vimezingira ufahamu wa akili zangu.

    Kufumba na kufumbua nikajikuta nimefika mitaa ya jangwani, hapo nikastuka na akili yangu ikarudi kufikiria cha kufanya zaidi juu ya hatma ya maisha yangu kwa usiku ule wa siku hiyo.

    Nikawa mbele ya viwanja vya jangwani, katika nyasi kavu nikaketi kitako huku macho yangu yakielekea angani na kutizama nyota na mwezi huku nikiwa na wivu dhidi ya nyota zile, nikaona bora ningekuwa nyota pengine ningekuwa na furaha na maisha kuliko kuwa binadamu nisiye na mbele wala nyuma huku mitiahani mizito ikiwa imechukua nafasi kubwa katika maisha yangu.

    Wakti nikiwa katika mawazo yale mara nikajikuta nazungukwa na wavulana kama sita watatu kati yao wakiwa na panga na visu.

    “Leta begi hilo” mmoja alisema akinisogelea na kukwapua lile begi langu la nguo.

    Mara moja nikaelewa wale walikuwa ni wezi.wakati sijajua nifanye nini mwingine alinifikia na kunipokonya ile pesa niliyokuwa nimepewa na mama Leila.

    Lakini nilipo taka kupiga kelele nilijikuta napigwa vibao vikali na kutakiwa kutulia kama maji ya mtungini.

    Walipo ona wamemaliza kuninyang’anya kila kitu hawakuniacha hivi hivi.

    Wakanipiga na kunitaka nivue nguo zangu zoote huku kila mmoja akionekana kutaka kunibaka.

    “Hapana kaka zangu msinifanyie hivyo ni dhambi kwa Mungu kunifanyia hivyoo”

    “Unazijua dhambi wewe., hebu toa hicho kichupi chako upesi kabla sijakucharanga na panga sasa hivi”

    Jamaa alisema kwa ukali macho yake mekundu yaliyo athiriwa na bange yaliniogopesha sana.

    Nilivua lakini siku tayari kuona nafanya mapenzi na vijana wale wahuni.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa mnaonaje kama mkifanya kwa hiyari yangu kuliko kuniingilia kwa nguvu?”

    “Ni wewe tu utakavyo amua, ukipenda ukubali kwa hiyari yako na utukatie mauno na ukipenda ukomae kama gogo ni wewe na roho yako sisi tunacho taka ni uroda tu”

    “Sasa naombeni msinikabe kwa nguvu mtafanya mapenzi na mimi kwa zamu hadi hamu yenu iishe” nilisema kwa kwa sauti ya kubembeleza na huruma kidogo.

    Hata nilipo pata kusema hayo jamaa watatu katika wale sita wakaonekana kugutuka kidogo kutokana na rai ile.

    “Oyaa masela kama vipi tujikatae huyu demu inawezekana ana moto, vipi akubali kirahisi hivi tena bila hofu kufanya mapenzi na sisi sote kwa zamu?”

    Jamaa mmoja alisema akimaanisha inawezekana kuwa nikawa na ukimwi hata nikakubali kufanya nao mapenzi kwa zamu ili pengine na mimi niwaambukize huo ukimwi.

    “Eti wee una ukimwi?”

    “Kusema ule ukweli sitaki kuwaongepea kaka zangu,. Mimi kweli nina ukimwi, naishi na ukimwi huu mwaka wa pili sasa”

    Nilisema kwa kujiamini nikiona ile fikra ya yule jamaa hakika ndio njia pekee ya kujinusuru na tatizo lile la kutaka kubakwa na wale wahuni.

    Lakini baada ya kusema hilo nikidhani wale jamaaa wataniacha na kuondoka zao lakini kilicho tokea huwezi kuamini mpenzi msomaji.

    Nilikutana na kipigo cha haja kutoka kwa wale vijana wa kiume nilipigika hadi nikahisi safari ya kuelekea kuzimu inaninyemelea.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Fala wewe unataka kutuaa kwa ngoma kirahisi hivyo.” Nilisukumiziwa teke la tumboni na kutoa mguno mkali hapo hapo jamaa mwingine alinilapua konde la usoni na kunipasua mdomo huku damu zikawa zinanitoka puani na mdomoni.

    ****************

    ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog