Search This Blog

JUMBA LA WACHAWI - 3

 





    Simulizi : Jumba La Wachawi

    Sehemu Ya Tatu (3)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilisimama kwa ungalifu nikavaaa raba zangu, kisha nikauendea mlango, wakati huo ilikuwa yapata saa kumi na nusu ya tarehe 29/3/1989, na majira hayo muadhini alikuwa akiadhini kule katika jumba la ibada.

    Nilitoka nje ya chumba kile na kunyata taratibu, nilitembea upesi upesi katika ile korido eneo lote bado lilikuwa kimya kabisa, niliongeza mwendo nikawa natembea kwa kasi kubwa,atimae nikawa nakimbia.

    Nilipopiga hatua kadhaa nikiwa mbali kidogo kutokea katika kile chumba, nikaona korido ndogo ambapo pembeni yake kulikuwa na lifti, nikaona hiyo inaweza kuwa njia nzuri ya kunitoa upesi katika lile jengo.

    Mara ghafla nikasikia ile sauti ya ajabu, lakini safari hii sikukubali kabisa kuendelea kubaki mule katika lile jengo, niliziba masikio nikatimua mbio.

    Nilikimbia kuelekea eneo lile, upesi nikajotoma ndani ya lifti moja katika tatu zilizo kuwa pale, kisha nikairuhusu inishushe chini, sekunde kumi tayari mlango wa ile lift ulifunguka na nilikuwa chini kabisa ya ghorofa lile..ile sauti ilikuwa ikipotea kwa mbali kabisa.

    Bila kuzubaa nikakimbia kuufuta mlango wa kunitoa nje, kama masikhara nikajikuta nipo nje ya jengo lile.

    Kwakweli ilikuwa ni furaha kwangu, nilijiona ni kama mfungwa niliyekuwa na kufungo kikubwa gerezani na sasa nimekuwa huru.

    Pamoja na kwamba nilikuwa ni mtu mwenye furaha ya kuwa nje ya jengo lile lakini nilijikuta nikisimama na kuduwaa hatua chache mbele ya jengo lile katika mtaa wa agrey kariakakoo kutokana na kile nilicho kiona mbele yangu.

    Nilikutana na mji mgeni mpya tena mpya kabisa mbele ya macho yangu, mji uliokuwa umejengwa ukajengeka maghorofa mengi, mazuri tena marefu kwenda juu.

    “Nipo wapi hapa” sauti moja iliniuliza mawazoni mwangu, japo mtaa ulikuwa ni ule ule nilio ufahamu miaka yote tena palikuwa ni Dar es salamu ninayo ijua kabisa.

    Lakini Asubuhi hii jiji hili lilikuwa tofauti kabisa, nilizipiga hatua kuelekea mnazi mmoja nikizidi kushangaa mandhali mazuri ya jiji la Dar es salam.

    “Kitu gani kinatokea katika maisha yangu huku nipo katika dunia gani tena?” nilijiuliza mwenyewe bila kuwa na majibu.

    Wakati naelekea mnazi mmoja tayari ilikuwa ni majira ya saa kumi na moja alfajiri katika Dar es salam hii mpya majira yale kulikuwa na watu wengi mno mida hiyo tofuati na Dar niliyokuwa ninaijua mimi. Watu hawa walionekana wako ‘bize’ kila mtu alikuwa ni mwenye kujali mambo yake.

    Nilifika mnazi mmoja na kuelekea katika kituo cha basi, bado niliendelea kupagawa na namna mandhali yalivyo badilika ghafla kiasi kile.

    Lakini pamoja na kuwa mji huu mpya machoni mwangu kuwa na majengo mapya yenye kuvutia bado kuna baadhi ya majengo niliona yako vilevile mathalani jengo la ushirika pale mnazi mmoja, jengo la chama cha mapinduzi, pamoja na nyumba za taifa{ nation housing} ambazo nyingi zilikuwa zikikaliwa wahindi.

    Hali ilinisukuma kuuliza tofauti ile ninayo iona mbele ya macho yangu kama na wezangu pia wanaona kama nionavyo mimi, ama ni maono yangu tu, kwani kusema ukweli toka hapo sikuwa najiamini hata kidogo, niliamini kwa vyovyote vile wale wachawi niliokutana nao katika lile jengo kuna namna watakuwa wamenifanya katika ufahamu wangu wa akili.

    “Kaka samahani”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Bila samahani dada yangu”

    “Hivi mbona naona leo mji umebadilika mno tofauti na siku nyingine za nyuma nini kimefanyika usiku wa leo?” niliuliza mkaka aliyekuwa anangojea usafiri kituoni.

    “labda sijalielewa swali lako dada yangu, mji umebadilika kivipi yanii uonavyo wewe?”

    “Kwani wewe huoni huu utitiri wa haya maghorofa?, huoni namna barabara zilivyo za kuvutia? Huoni kama leo watu ni wengi tofauti na siku zingine?..Huoni?” nilisema kwa kulalama kidogo, nikionyesha sura ya kumaanisha kile nilicho kuwa nakizungumza.

    Yule mtu alinitizama kwa kina kidogo kichwani mwake akahisi anazungumza na mlevi wa pombe aina ya mataputapu.

    “Ndivyo kulivyo kila siku” alinipa jibu moja kisha hakushughulika tena na mimi, nilimwona katika uso wake akinisoma mimi kama mlevi wa mataputapu.

    Upesi sauti moja ikanambia inawezekana ulikaa mule ndani kwa masiku mengi mno ndio maana kumekuwa na mabadiliko makubwa katika mji huu, lakini bado sauti nyingine ikaniambia hata kama nitakuwa nimekaa mule ndani kwa masiku kadhaa mji huu hauwezi kuwa umebadilika kwa kiwango hiki., mabadiliko yale hayakuwa ya miezi sita ukiachilia mbali hata kwa mwaka mmoja tu ingehitaji miaka zaidi ya ishirini ndio kuwe vile..

    Lakini sauti moja ikanijia ambayo niliona kidogo imenipa wazo la kujua utata ule, sauti ilinambia, angalia saa na tarehe ya leo, upesi niliangalia tarehe katika saa yangu ya mkononi.

    Sikuamini kile ambacho macho yangu yaliona,. “MWAKAA elfu mbili na kumi na sita..!.” Nilijikuta nibwata kwa nguvu huku nikibaki nimeduwaa.

    Hapakuwa na mtu aliye nijali pale kituo cha basi cha mnazi mmoja, nilihisi huenda saa yangu ilikuwa mbovu, kwani kabla ya kuitizama muda ule nilikwosha itizama wakati nipo ndani ya jengo lile na ikanionyesha ilikuwa ni tarehe 29/3/1989.,sasa vipi huku nje inionyeshe ni mwaka mwingine wa mbele kabisa, ambao sikuwahi kufikiria kama uhai wangu unaweza kufika huko.

    Mambo mawili yakawa katika ubongo wangu, jambo la kwanza inawezekana ile saa yangu niliyo kuwa nimeivaa mkononi ds ikawa ni mbovu, na jambo la pili inawezekana saa ile isiwe mbovu ila tu nikawa nipo katika ulimwengu mwingine kabisa wa kichwawi.

    Lakini bado wazo hilo nililipinga kabisa kwani pale nilikuwa katika mji ninao ufahamu sana, mji wa Dar es salam, japo ulikuwa umebadilika mno.

    “Samahani kaka yangu eti leo ni siku gani?tarehe ngapi? na mwaka upi?” niliuliza mshangao mkubwa ukiwa usoni mwangu,.nilisha anza kuhisi kuna bomu linaninyemelea katika maisha yangu.

    Yule mtu ambaye hakuwa anavutiwa na maswali yangu, alionekana kukereka kwa masawali yangu ambayo yalionekana ni ya kipuuzi kwakwe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nakujibu, lakini hili ni jibu langu la mwisho sintokujibu tena maswali yako ya ajabu.” Alisema yule jamaa.

    “Leo ni juma tatu ya tarehe nne mwaka 2016.”

    “Nini!. Siamini macho yangu.”

    “Shauri yako..Ni macho yako mwenyewe. Ukiyaamini sawa, usipoyaamini sawa, sitaki usumbufu zaidi.”

    Alisema yule jamaa na kuingia katika basi lililokwisha wasili pale stendi..

    Kwa mara nyingine nilijikuta nipo katika taharuki siyo na kifani, niliwauliza watu wengine kama watatu kuhusu tarehe ya siku hiyo. Kila mtu alinihakikishia kuwa ilikuwa ni mwaka wa elfu mbili na kumi na sita {2016} ya tarehe nne siku ya juma tatu.

    “Nimekuja kwenye dunia gani hii sasa mimi” niliongea peke yangu, kila mtu aliyekuwa pale stendi aliniona kama mwehu, kwani wakati mimi naishangaa hii dunia mpya na watu wao ambao walionekana ni watu walio endelea mno kuanzia mavazi yao hata mwonekano wao,lakini pia na wao pia walikuwa wakinishangaa mimi na kuona ni binadamu niliye tokea sayari ya mbali mno na kuangukia katika dunia yao.



    Wakati huo ilikuwa ni saa moja, watu walizidi kuwa wengi katika hili jiji jipya la Dar es salam asubuhi hio.

    Niliangalia katika lile jacketi langu na kuiona ile kadi yangu ya TTCL sasa nikaona njia nzuri ni kuwasiliana na ndugu zangu kwanza akiwa ni pamoja na mchumba wangu Thabit nikiamini angalau kutoka kwao nitaweza kupata suluhu ya matatizo yaliyokuwa yananikabili.

    Sasa kazi ikawa ni kutafuta kibada cha TTCL, kwakweli nilizunguka sana pale mnazi mmoja kutafuta kibanda cha TTCL lakini niliambulia patupu.. ilikuwa ni jambo jingine lilio nistajabisha awali kabla sijakumbwa na mazingaombwe yale vibanda vya Kampuni ya simu ya TTCL pale mnazi mmoja vilikuwa vimetapakaa tele kama uyoga ajabu ni kuwa mwaka huu nilio ambiwa ni elfu mbili na kumi na sita hapakuwa na kibanda hata kimoja.

    Japo sikuwa nataka kuuliza jambo lolote kwa mtu yeyote kutokana na kuonekana tahira, lakini ilinibidi niulize.

    “Vibanda vya kupiga simu vimehamishiwa wapi” Nilimuuliza fundi viatu aliyekuwa akifungua ofisi yake majira yale.

    “Vibanda gani?”

    “Vya TTCL”

    “Mmh!. sijahi kuviona hivyo vibanda maeneo haya” alijibu yule jamaa.

    Sasa nikaona nisizidi kuwapa watu faida ya kuonekana hamnazo kutokana na maswali yangu.

    Nilirejea stendi na kupanda basi lililokuwa likieleka buguruni., nikaona ni vizuri nifike nyumbani kwangu kwanza nioge, kisha nile chakula kwani toka chakula nilichokula kule Dodoma na wenzangu akina Lovenes na mr Magembe matiku sikuwa nimekula chochote hadi asubuhi hii, niliona hilo ni jambo zuri kulitekeleza kabla ya kuendelea kutafuta ufumbuzi wa masaibu niliyo kuwa nayo.

    Kwani hadi wakati huo ilibidi niamini kuwa huenda mimi pengine ndio nimekumbwa na jinamizi kichwani mwangu linalo nifanya nijione nipo katika karne ya 21 mwaka elfu mbili na kumi na sita.

    Hata basi lile la mjini lilikuwa ni basi la kisasa sana katika Dar es salamu hii mpya ukilinginisha na yele yetu.

    Nikiwa nimezama katika bahari ya mawazo nilistushwa na sauti ya konda aliyekuwa akidai nauli yake, niliingiza mkono katika lile jacketi langu na kutoa shilingi tano na kumpa konda.

    “Hii nini unanipa?” Konda aliniuliza kwa ghadhabu.

    “Si nauli ama unadai nini?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hiyo ndio nauli? Kitu gani hicho unanipa wewe sister?” alijibu yule konda kwa ukali huku akiwa amenitolea macho yake mekundu.

    Hata abiria aliyekuwa pembeni yangu pia alinishangaa, “hizo pesa za zamani sana ant hakuna anetumia tena pesa hizo we uko dunia gani” abiria wa pembeni alisema.

    “Oyaa lipa nauli we sister kama huna shuka chini,.. asubuhi hii.. tusianze kutiliana nuksi time hizi” alisema tena yule konda kwa ukali. Niliendelea kustajabu mazingaombwe yale yaliyokuwa yananitokea katika maisha yangu.

    Niseme tu, pengine hiki ninacho kieleza hapa wengi wenu mtafikiri ni hadithi za kubuni, lakini napenda nikwambie ndugu yangu unae soma maandishi haya, kwanza napenda uelewe kuwa uchawi upo kwani hata vitabu vyote vitakatifu vimeeleza juu ya uwepo wa uchawi, hivyo katika haya nikuelezayo hakuna neno hata moja nililoongezea chumvi katika hayo ambayo nimekwisha yaelezea, na nitakayo yaeleza yote yaliyo nitokea mimi Zahara katika maisha yangu.

    Kila kitu ni ukweli mtupu, na nimeona sina namna ya kuelezea haya katika jamii na jamii ikanielewa tofauti na kutumia njia hii ya maandishi.

    “Lipa pesa wewe sister” alinistua yule konda.

    “Sasa kama ndio hivyo mie sina pesa” nilisema kwa upole.

    “Suka eeh, zuia hapo mtu ashukie maana nisha ona naletewa za kuleta hapa” alisema yule konda akimtaka dereva asimamishe gari kisha nishushwe.

    Lakini yule abiria aliyekuwa kiti cha pembeni alitoa noti mpya mchoni mwangu, noti ya shilingi elfu moja na kulipia nauli za watu wawili, zogo la mimi na konda likaisha.

    Niliendelea kushangaa namna pesa ilivyokuwa haina thamani, kwenye hii dunia mpya . noti ya shilingi mia tano ni nauli ya mjini!. Pesa hiyo ilikuwa ndio posho yangu ya katikakati ya mwezi katika dunia yangu niliyotoka.

    Lakini sikujali sana kwani kadri nilivyo endelea kuwa na jamii ndivyo nilivyozidi kuonekana mtu wa zamani, hali ambayo nilianza kuchukia.

    Ilinichukua dakika ishirini na ushee kufika Buguruni malapa, napo huko kwa kiasi kikubwa mandhali yalikuwa yamebadilika mno, nyumba zilikuwa zimelundikana kila mahali mithili ya siafu.

    Taratibu nilianza kutembea kuelekea nyumbani kwangu, nilikuwa nikitembe lakini nikiamini muda wowote lolote linaweza kutokea mbele yangu na kuibua taharuki nyingine moyoni mwangu.

    *********************



    Mbele ya macho yangu, nilishuhudia jumba bovu lililokuwa limegemea upande mmoja, uchakavu wa jumba hilo ukiwa wa kiwango kikubwa, kulikuwa na nyumba nyingi mtaa ule ambazo zilijengwa bila mpangilio mzuri wa kiramani.

    Mtaa ule ulikuwa na nyumba nyingi ambazo sio nyumba bora, takataka zikiwa zimetapakaa eneo lote, kulikuwa na pitapita za watu wengi, kelele nyingi kila mahala.

    Ni uswahilini.

    Maeneo yaliyo kaliwa na watu wa kipato duni.

    Macho yangu yaliendelea kuganda katika lile jumba bovu ambalo pengine ndio lilikuwa jumba baya na bovu katika nyumba zote zilizo kuwa mtaa ule.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nyumba hii ndio ile nyumba iliyokuwa nyumba nzuri mtaa wote siku moja kabla ya siku hii,lakini leo ndio ilikuwa nyumba mbovu kuliko zote.

    Nilipiga hatua kusogea katika nyumba ile. Kulikuwa na watoto waliokuwa wakicheza pembeni ya nyumba ile hatua chache palikuwa na bibi aliyekuwa amejilaza katika mkeka, niliendelea kusogea pale kwa yule bibi.

    Moyo wangu ulikuwa ukipiga mkumbo nikiwa nimekata tamaa kwa kiwango cha mwisho,

    “Shikamoo bibi..mama” nilimwamkia yule mwanamke mzee, baada ya kumfikia, hakuwa mzee sana kama nilivyo mwona kwa mbali, alikuwa katikati ya umama wa makamo na uzee.

    “Marahaba mjukuu wangu hujambo” aliitikia, nilimwangalia vizuri yule bibi mama na kugundua jambo lililozidi kuustua moyo wangu, yule alikuwa ni mama mwenye nyumba wangu {mama Leila} ambaye jana kabla ya siku hii ndiye aliye nipatia namba ya mtu aliyekuwa ameokota vifaa vya ofisini kwangu vilivyokuwa katika jacket langu, mtu aliyeniingiza katika maisha ya mazingaombwe.

    Jana kabla ya leo alikuwa ni mwanamke wa miaka kati ya thelathini na thelathini na tano hivi, lakini siku hii ambayo kwangu ilikuwa ni siku ya pili tangu niachane nae, tayari alikuwa ni bibi wa miaka kama sitini ama sitini na tano.

    “Mama Leila kitu gani kinatokea katika maisha mbona sielewi, jana tu tumeachana ukiwa kijana, leo nakuona umekuwa mzee, nini kinatokea mama, eeh..kwanini mambo haya yanakuwa hivi,” niliuliza huku machozi yakinitoka, nguvu nazo nikihisi zinakwisha mwilini mwangu.

    Yule bibi alitayahari kwa yale maneno yangu, akakaa vizuri pale mkekani kisha akanitizama usoni vizuri.

    “Wewe ni nani..Za…Za..Zahara” alisema huku akinitizama kwa mshangao mkubwa. “ndio ni mimi mama Leila nimekumbwa na mambo makubwa mama..kila kitu katika maisha yangu kimeharibika..”

    “Ni wewe Zahara ama mwanawe na Zahara!!..”

    Yule bibi au mama Leila alizidi kuniuliza kwa mshangao…kisha akaendea kunisaili kwa maswali.

    “Wewe ni Zahara huyu aliye kuwaga’ mpangaji wangu?”

    “Ndio mama Leila ni mimi haswaa niliye ondoka jana baada ya kunipa namba ya yule baba aliye chukua Jacket langu lililokuwa na vitu muhimu vya ofisini.

    “Hata sio wewe,..japo ulicho kisema kuna ukweli kidogo lakini sio wewe..labda useme wewe ni mtoto wa Zahara nitakukubalia..ila sio Zahara huyu niliye kuwa namjua mimi..halafu hilo unalo lisema halikuwa jana” alisema yule bibi, akionyesha wasiwasi na mimi.

    Sauti moja mawazoni mwangu ikanambia, kama nisipo kuwa jasiri na imara katika kueleza ukweli juu ya mambo yaliyo nikuta kuna uwezekano wa kuonekana ni mtu majinuni.

    “Mama najua kuna vitu visivyo vya kawaida vimetokea katika maisha yangu, lakini nahitaji uwe makini kunisikiliza kile nitakacho kueleza kisha nione nitapata vipi msaada dhidi ya masaibu yangu, kwanza uwe na utayari wa kunisikiliza”

    Nilisema nikimkazia macho yaliyo onyesha kuwa sikuwa na mzaha na kile kilichokuwa kinatoka mdomoni mwangu.

    “Hebu ngoja… kwanza twende taratibu wewe mwana,.”Alisema yule bibi akionekana kutoafikiana na mimi moja kwa moja “unasema wewe ni Zahara mpangaji wangu?”

    “Ndio”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ulikuwa wapi miaka yote hiyo?.. Na kwanini umri wako unaonekana upo vilevile? Kama kweli wewe ni Zahara huyu nimjue mie..maaana ni miaka mingi mno imepita kama angalikuwa ni Zahara basi pengine sasa hivi ungekuwa mama wa miaka hamsini lakini.. Zahara wewe unaonekana bado mmbichi kabisa binti wa miaka ishirini na nne tu”

    Alisema yule bibi maneno yaliyo niingia kabisa ndani ya mtima wangu, na kwakweli niseme tu sasa nafsi yangu iliukubali ukweli kuwa katika maisha yangu uchawi wa ajabu uliusika kusimamisha umri wangu kwa kujiona nimeishi ndani ya nyumba kwa siku moja tu, kumbe nimeishi zadi ya miaka takribani thelathini.

    Nilifikiri kwa muda kidogo, kisha nikasema , “kama utakuwa tayari kunipa muda wako nieleze jambo, labda maswali yako na mashaka yako yote dhidi yangu yatajibiwa katika maelezo nitakayo yatoa kwako.”

    Mama Leila aitikisa kichwa kuonyesha ishara ya kukubaliana na ombi nililo omba, nilianza kumsimulia kila kitu kilicho tokea, nilimweleza toka mwanzo tukiwa safarini tukitokea kule katika mji wa geita, nilivyo mwona yule baba ambaye hadi wakati huo sikuwa nalijiua jina lake, kusahaulika kwa jacket langu, kurejea tena dodoma na kulikosa kisha kurudi Dar na yeye kunipa taarifa za uwepo wa mtu huyo aliyekuwa akinitafuta na kisha kuingia katika masaibu mkubwa.

    Hadi namaliza kueleza mama Leila alionekana kustajabishwa na mkasa huo wa ajabu kabisa, pamoja na kwamba alionekana kunielewa vema lakini bado alionekana kuwa na maswali lukuki ambayo hakujua ni kwa namna gani ayapangilie katika kuuliza.

    “Kwahiyo wewe unavyo ona mwaka ule ulivyondoka hapa kumfuata huyo mtu ilikuwa ni jana usiku?” aliniuliza mama Leila akiwa amechanganyikiwa kama tu ambavyo mimi nilivyokuwa katika mkalanganyiko wa kifikra siku ile nilivyo toka nje ya jengo lile kwa mara ya kwanza na kuona mabadiliko makubwa ya mandhali yaliyotokea mbele yangu kwa masaa machache niliyokuwa mule ndani.



    “Ndio mama ilikuwa ilikuwa ni jana usiku.. tena usiku wa saa sita ama saba kama sikosei.. yanii kwa namna nyingine naweza nikasema ilikuwa ni usiku wa kuamkia leo ama ni leo”

    Nilisema, na hapo mama Leila akazidi ‘kupalanganyika’ kwa mambo yale akatikisa kichwa kutokubaliana kabisa na jambo lile.

    “Mwanangu kwanza nikupe pole sana.” Alisema Mama leila, akisita kidogo kisha akaendelea.

    “kwakweli umenieleza tukio la ajabu ambalo sijawahi kulisikia katika maisha yangu yote hapa ulimwenguni, nalazimika kukubaliana na wewe kwa namna moja ama nyingine, lakini pia naweza nisikubaliane na wewe kwa upande mwingine vilevile..”

    Alisema mama Leila, sikuona tena haja ya kuendelea kumfanya yule mama anielewe maneno yangu kwani kwa vyovyote vile ingemchukua muda mwingi kunisadiki.

    “Sasa mama,kuna vitu nataka kujua, kitu gani kiliendelea kipindi chote ambacho ninyi mliona ni mimi sipo nyumbani kwa kipindi kirefu.” Nilisema.

    “Aagh..sasa huko unako elekea ni mapema sana, kwanza nataka nijilidhishe na maelezo yako Zahara” alinidakiza, akiwa ni mwenye kutaka kuelewa mambo mengi dhidi ya yaliyo nisibu.

    “Sawa mama uliza tu” nilimjibu.

    “Kwanini unafikiri huyo mtu alikupeleka wewe katika hilo jumba la kichwawi na si mtu mwingine.?”

    “Kwakweli hadi sasa hivi Mama Leila hilo swali bado kwangu ni kitendawili”

    “Na umesema ulibakwa?” nilijibu kwa kutikisa kichwa huku taswira ya tukio lile kuingiliwa kimwili na yule baba ikijidhihilisha tena mbele yangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Pole sana”

    “Asante”

    “Iliwezekanaje uingiliwe kimwili, muda huo huo upate mimba tena mimba kubwa na muda mchache ujifungue?”

    “Hilo pia sijui, nisime tu hata mie pia sijui mambo haya yaliwezekanaje kutokea, na labda tu nikwambie siku ile hata mimi nilishangaa kama wewe unavyo shangaa sasa” nilijibu, mama Leila alifikiri kwa muda kisha akaniuliza tena.

    “Kwani mwanangu uliwahi kuwa na ubaya na mtu katika maisha yako mama?”

    “Kivipi mama Leila?”

    “Agh..unajua Zahara katika hii dunia kuna watu wanavisasi vya ajabu usije kuwa uliwahi kukwaruzana na mtu akamua kukufanyia ushenzi huo”

    Nilifikiria kidogo maneno yale lakini hata hivyo sikuwahi kuwa na ugomvi na mtu yeyote katika siku za ukubwa wangu.

    “Hata sijawahi kuwa na ugomvi na mtu”

    Tuliendelea kuongea mengi na mama Leila hadi kiasi fulani akawa anaamini hadithi ile ya ajabu niliyo mpa.

    Ilikuwa ni zamu yake kujibu maswali yangu yote niliyo muhoji, kusema ukweli kila neno lililotoka kinywani mwake lilininyong’onyesha mno,

    Alisema; “mwaka 1989 baada ya wewe kuwa umepotea katika mazingira ya kutatanisha taarifa zako zilizagaa kila kona wakati huo, kulikuwa na uvumi mwingi juu ya kupotea kwako ghafla kiasi kile,”

    Aliendelea kusema; ndugu zako hususani wazazi wako walitumia muda mwingi katika maisha yako kukutafuta japo wapate hata mwili wako tu, lakini kadili siku zilivyo yoyoma ndivyo jambo hilo la wewe kupotea lilivyozidi kupotea katika vichwa vya watu wengi na kuhesabika kama ni miongoni mwa watu walio poteza maisha na mwili wako kutooneka, kila mtu anajua kuwa wewe ‘ulishakufaga’ siku nyingi tu.

    Mwazoni mwa mwaka 1999 nilipata taaarifa zisizo njema kwakweli” Alisema na kunikazia macho, moyo ulikuwa ukinienda kasi, nikaelewa kuna bomu linakuja masikioni mwangu na kwenda kuupasua moyo wangu, akaendelea kusema.

    “Taarifa zisizo njema, nilisikia wazee wako walifariki kwa kuangukiwa na nyumba, kutokana na mvua kubwa za alumino zilizo kuwa zikinyesha miaka hiyo..kibaya kuliko vyote..Alisema mama Leila. Akajiweka sawa pale alipo kuwa ameketi, halafu akanisogelea na kunishika bega kama ishara ya kunifariji kwa taarifa ile aliyokuwa akinipa. koo langu lilikuwa na donge zito, sikujua machozi yalinitoka muda gani kwani nilistuka tu pale matone ya machozi yalipo nichuruzika na kupenya hadi katika kinywa kilichokuwa wazi kwa mshangao wa taarifa ile, ni ile chumvi chumvi ya machozi ndio iliyonijulisha kuwa nilikuwa nikitiririkwa na machozi kwa kasi.

    “Kibaya kuliko vyote..” aliendela kusema mama Leila. “yule mdogo wako uliyekuwa ukimsomesha alikuwa akiitwaje vile?”

    “Nasri”

    “Naaam.. Nasri.. nilipokea taarifa za kijana huyo kwakweli hazikuwa taarifa njema..yupo Gerezani anatumikia kifungo cha miaka sitini jela.,inasemekana aliua kwa bunduki..alifanya uhalifu wa kuvunja na kuua..alikuwa jambazi..mwizi..mtumia madawa ya kulevya,.bange, na petrol”

    Alisema mama Leila. Kwakweli nililia sana siku ile, dunia niliiona ni kubwa mno huku mimi nikijona mdogo kama nukta..

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Inawezekanaje mtoto wa shule afanye hayo yote?” nililalamika mno, zaidi ya yote nilimlaumu yule baba mchawi kwani ndiye mtu aliye badilisha kabisa dira ya maisha yangu.

    Siku ile tuliongea mengi na mama Leila na niseme tu ilifikia hatua yule mama alinielewa vema juu ya masaibu yaliyokuwa yamenikuta, na niseme pia kwa kiwango kikubwa nashukuru yule mama alionekana kunielewa kadri nilivyokuwa nikiendelea kuzungumza nae..

    “Vipi kuhusu Thabit?” atimae nilimuuliza mama Leila juu ya mchumba wangu Thabit..

    “unamwongeleaThabit Talib mjukuu wa marehemu mzee mwaikimba?”

    “Ndio”

    “Kwakweli yule kijana ni miaka mingi imepita sijamwona ila niliwahi kusikia kuwa hivi sasa yupo huko Mwanza japo sina uhakika,”

    “Wakati nimepotea yeye hakuwahi kujishughulisha kunitafuta?” niliuliza, japo sikujua kwanini niliuliza swali lile.

    “Hilo kwakweli sijui..sikuwahi kumwona toka ulivyo potea” alisema mama Leila.

    Tangu wakati huo Sikuwa na uelekeo maalumu, sikuwa na mbele wala nyuma katika hii dunia mpya, si mashariki wala magharibi, sikuona kama ninalolote muhimu katika maisha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ******

    ITAENDELEA  

0 comments:

Post a Comment

Blog