Search This Blog

JUMBA LA WACHAWI - 2

 





    Simulizi : Jumba La Wachawi

    Sehemu Ya Pili (2)



    Nikiwa bado pale, shoka langu likiwa mkononi, nilitupa macho yangu kule chini nilikokuwa naelekea, nilicho kiona kilinitisha sana.

    Watu wanne wanaume walikuwa uchi wa mnyama, walikuwa wamebeba mwili wa mtu aliyekuwa kama mtu aliye ungua na moto,mwili wa yule mtu aliye kuwa amebebwa katika machela ulikuwa na nyama nyekundu iliyoonyesha kama mtu yule amebabuliwa na mafuta ya moto, wale watu walikuwa wamejipaka masizi meusi usoni mwao na kufanya waonekane kama vinyago vya kimakonde. Walikuwa wakizipanda ngazi kuja juu nilikokuwa mimi huku wakiimba nyimbo Fulani kwa lugha ambayo sijawahi kuisikia hapa duniani.

    Kwakweli nilijikuta nikipiga kelele nyingi na kutoka mbio huku nikitupa kile kishoka na kupanda juu mradi nijiweke mbali na jambo lile la kutisha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliendelea kwenda kasi, atimae nikafika mwisho kabisa wa ghorofa lile, nilikuwa niko juu kabisa ya lile jengo pale juu kukiwa na eneo kubwa la wazi, kulikuwa na mitambo mbali mbali ya vitu kama setelite pamoja na antena.

    Nilisogea mwisho wa ukuta na hapo niliweza kuona mandhali ya jiji la Dar es salam, jiji lilikuwa kimya, mataa ya umeme yakifanya mji kunga’aa na kuvutia. Kwakweli machozi yalinitoka.

    Nilijikuta nalia kama mtoto mdogo, sasa niliona kama ndio naiona nchi kwa mara ya mwisho na badae kushikwa na wale watu na kufanywa mbuzi wa kafara.

    Niliangalia chini nikaona niko umbali mrefu kutoka ardhini kiasi kwamba kama ikitokea umeanguka kutoka kule juu basi ukifika chini mifupa yote huna.

    Nililia mno, sikujua kwanini yote haya yananitokea mimi, nilijiona ni mwanamke mwenye bahati mbaya katika siku za ukubwa wangu.

    Niliikumbuka familia yangu, nikawakumbuka wafanyakazi wenzangu hususani timu nzima niliyokuwa nayo kule safarini geita. Kwakweli nilihuzunika mno, nilitamani nipaze sauti yangu na iwafikie watu ambao wangeweza kuja kunipa msaada lakini sikuweza.

    Na mwisho mawazo yangu yakakita kwa Thabiti Talib Mwaikimba ni mpenzi tuliye kuwa na ndoto kubwa ya pamoja, ndoto ya kufunga ndoa ndogo tu ya mkeka, tuwe na biashara yetu ndogo itakayo leta matokea makubwa,

    kisha tuzae mtoto mmoja mzuri ambaye tutamsomesha hadi chuo kikuu.

    Lakini kila kitu hadi wakati huo, niliona kinaeleka kubaki kuwa hadithi tu kama zile za mwandishi Adam Shafi.

    Nikiwa bado nafikiria mambo yale mara nikasikia vishindo, nilikurupuka upesi nikajisogeza karibu na lilipo kuwa sinki kubwa la maji aina ya sim tank kwa lengo la kujificha.

    Nilipo sogea tu pale katika lile sinki mara moyo wangu ukapiga mkumbo na kujikuta naruka hatua moja kwa pembeni kisha nikabaki nimebung’a.

    Yule mwanamke niliyekutana nae kule ndani alikuwa amejificha pale, alikuwa amejikunyata miguu yake ameikumbatia karibu kabisa na kifua chake huku kichwa chake akiwa amekiegemeza katika magoti yake.

    Ajabu ni kuwa yule mama alikuwa ameganda hatikisiki wala hasemi lolote, wakati huo huo wale watu waliokuwa uchi huku wamebeba machela iliyokuwa na mwili wa mtu aliyekuwa amebabuka mwili wote waliwasili eneo lile.

    Hapo hapo nilikurupuka na kusogea upesi pale alipokuwa amejikunyata yule mwanamke. “wa..wa.me..fika” nilisema kwa kunong’ona kumwambia yule mwanamke.

    Nilikuwa natetemeka vibaya mno, nilichungulia kidogo, nikaona wanashusha mwili wa yule jamaa aliyekuwa katika machela ambaye bila shaka alikuwa amekwisha fariki na kuuweka chini.

    “uu..wiii leo..mama..ya..ngu weeee!!” nililia, mwili wote ukiingiwa ubaridi,ila yule mwanamke alibaki akiwa vile vile ameganda hasemi wala hajibu lolote hata ile hofu yake haikuwepo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikahisi kitu kisicho cha kawaida kwa yule mwenzangu, nilimtizama nikamwona uso wake ukiwa ni wenye hofu kubwa ila macho yake yamekodoa sehemu moja bila kope za macho yake kupepesa.

    Hakuna kiungo katika mwili wake kilichokuwa kinatikisika. “Hey..hey” niliiita.

    Kimya.

    “Hey wee ma..ma” niliita tena kwa kunongo’na.

    Kimya tena, hakukuwa na jibu.

    “Wewe..mbo..na hu,.semi ki..tu?” nilimsemesha kwa kunongo’ona.

    Kimya kwa mara nyingine.

    Nilimsogelea nikamgusa, hapo hapo yule mama akaanguka chini kama mzigo.niliruka hatua moja nyuma kwa woga.

    Hapo nilipata kujua kuwa yule mama alikuwa amekufa. Nilichanganyikiwa sana. Nililia nikifinya sauti yangu kwa chini ili wale watu wasinisikie.

    “Wewe mama sasa unafanya nini hivyo!” nilisema kibweege huku nikitetemeka kama mtu mwenye degedege, yule mtu alikuwa amekufa huku akiwa amekodoa macho kama kwamba kabla ya kifo chake aliona tukio baya la kuogopesha.

    “Hellow Zahara”, ghafla..sauti ilitokea nyuma yangu…nilistuka, “uwiii”,niliruka kwa hofu huku nikiachia ukulele kisha niligeuka, macho kwa macho nikakutana na yule baba,. “uwiiiiiiiiiiiii” nilipiga kelele nyingi za hofu.

    Na bila ya kutarajia nikajikuta nazungukwa na wale watu wanne waliokuwa na masizi usoni mwao mithili ya vinyago vya kimakonde.

    “Toka..to..ka..to..ka” nilisema kwa fadhaa kama kwamba nafukuza nyani shambani. Wale watu wakawa wananisogelea taratibu huku wakiwa wamekodoa macho yao na vidole vya mikono yao wamevichanua kama majini, lakini yule baba mchawi mwenye shuka jekundu yeye alikuwa amesimama vilevile.

    Kadri walivyokuwa wakinisogelea ndivyo nilivyo ona kifo changu kinazidi kuwa karibu yangu.

    “Mamaaaaaaa” nilipiga ukulele mkubwa wakati wale watu wanne walipo nifikia, na sauti yangu ikasambaa katikati ya jiji usiku ule, huku mwangi ukiniitikia kwa mara ya pili masikioni mwangu.

    Sasa mikono ya wale viumbe ikanikamata, ikaushika mwili wangu kwa pamoja, nilihisi mwili wote unakufa ganzi punde baada ya kuguswa na wale viumbe. Lakini wakati huo huo nikabebwa kwa nguvu ya ajabu na wale watu wakawa wameni-ning’iniza juu juu kunipeleka mahala nisipo pajua.

    Nilipiga ukulele mwingi kujaribu kufurukuta na kujinasua kutoka katika mikono ya wale watu lakini mikono yao ilikuwa na nguvu za ajabu kadri nilivyo zidi kufurukuta ndivyo mikono ile ilivyozidi kunibana kwa nguvu hadi nikawa napata maumivu.

    Walinipeleka ndani ya lile jengo kisha wakaniingiza ndani ya chumba kimoja miongoni mwa vyumba vingi vilivyokuwapo katika nyumba ile ya ghorofa

    Bila kutarajia nikajikuta narushwa hewani, niliachia ukulele wa kuogofya baada ya tukio hilo lakini nikajikuta naangukia sehemu laini yenye kunesa nesa. Ilikuwa ni kitandani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Waiiii..uwiiiii” nilipiga kelele nyingi huku nikikurupuka pale nilipo angukia na kujiweka sawa.akili yangu niliona kama inazunguka kwani nilikuwa ni mtu mwenye mashaka makubwa vibaya mno.wale watu wanne walisimama kukizunguka kile kitanda kisha sura zao wakazielekeza juu huku macho wameyatoa vibaya.

    “Ninyi ni akina nani na mnataka nini kwangu?” nilijikaza na kuuliza jasho likinitoka katika maungo yangu.

    Hapakuwa na majibu niliyoyapata, wote waliniipuza kama kwamba hawakusikia swali langu. “nini hii? Kitu gani kinatokea katika maisha yangu mimi? Kwanini yote haya yananisibu mimi?” nilijiuliza mwenyewe lakini sikuwa na majibu na sikuona mtu wa kunipa majibu yale.

    Wale watu wakiwa wanatizama juu na kuwa kama wanazungumza maneno Fulani kwa kunong’ona mara mule ndani ulianza kutoka moshi mweupe, niliona moshi mzito mweupe lakini sikujua ni wapi moshi ule unatokea,ule moshi ukasamba mule ndani na kuacha halafu Fulani nzito nisiyoweza kuielezea.

    Aisee haya mambo endelea kuyasikia tu yanahadithiwa katika riwaya kwakweli ni mambo yenye kutisha si kawaida.

    Kwa Dakika nilikuwa nimejikunyata katika kona ya kitanda kile kilichokuwa kimetandikwa mashuka mekundu huku rangi ya kuta za chumba kile ikiwa ni rangi ya maziwa.



    Nilijaribu kukisaili kile chumba haraka haraka nikaona kile kilikuwa ni chumba kikubwa tu kilichokuwa na vitu vichache tu, kabati la nguo, televisheni ndogo ya Hitachi, saa ya ukutani aina ya Ajanta, meza ndogo ya kioo iliyo beba simu ya mezani, na panga boi lililokuwa limefungwa ukutani ambalo lilikuwa likizunguka kwa kasi na kutoa upepo mkali mule ndani.

    Kwakweli nilikuwa ni mtu mwenye hofu kuu, niliendelea kujikunyata pale katika kona ya kitanda huku nikilia na kumuomba Mungu wa mbinguni kimya kimya.

    Mara macho yangu yakashuhudia tukio jingine lililonifanya nipige kelele nyingi,

    Alingia yule baba akiwa na vazi lake lile lile,sura lake amelichafua kwa mikunjo mikunjo iliyo jipinda kama mkeka wa kisukuma huku akionekana ni mtu mwenye hasira kubwa, lakini kubwa kuliko vyote alikuwa ameshikilia kichwa cha yule mwanamke niliyekutana nae katika ngazi kabla ya kumkuta akiwa amekufa pale mafichoni.

    “Mme..mchi..nja mtu.. na kumnyofoa kichwa?” nilisema kwa kitetemeshi, uzito wa kile nilicho kiona kilinielemea na kuniwia vigumu kuamini, nilikuwa nimeduwaa macho nimeyatumbua kwa yule baba huku mdomo wangu ukijikuta unaachama mshangao uliochanganyikana na hofu vikishika hatamu, kwakweli tukio lile lilikuwa kubwa mno kwangu.

    Toka nizaliwe sikuwahi kushuhudia tukio baya na la kuogopesha kama lile, akili yangu haikuwa tayari kuamini tena kama wale walikuwa ni binadamu walio zaliwa na mwanamke, “bila shaka ni majini haya, mashetani, mizuka”, sikuona sifa stahiki za wale viumbe.

    Mwisho niliishia kulia kwa uchungu na kusubiri zamu yangu ya kuchinjwa na ile mizuka.

    Yule baba alisogea na kile kichwa kilichokuwa kinatiririsha damu kisha ile damu akawa anainyunyuzia katika kile kitanda nilichokuwa nimekalia.

    Nilijikuta najitapikia hovyo huku nikihisi kichefu chefu cha hali ya juu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya kufanya tukio lile yule baba aliwapa wale watu kile kichwa na mara wale watu wakaanza kukigombania kile kichwa kwa kukitafuna na kunyonya damu iliyokuwa inatoka katika shingo.

    Kwa mara nyingine nikajikuta natapaika hadi nikahisi nguvu zikiniishia.wale watu wenye masizi na miilini mwao wakiwa uchi walitoka mule ndani huku wakiendelea kukishambulia kile kichwa cha binadamu.

    Nikaelewa kitu,.

    Kwa tukio lile nikapata kunga’amua kwa wale viumbe wenye masizi ndio vile viumbe vyenye kuitwa misukule, ama wengine wanaita ndondocha, lakini pia nikapata kuelewa kuwa yule baba mchawi wale misukule walikuwa ni viumbe vyake anao wafuga.

    Kwa faida ya wale wasio elewa, Misukule ama mandondocha ni wale binadamu walioaminika kuwa wamefariki dunia lakini badala yake wanakuwa wamechukuliwa kichawi na wachawi kwa dhumuni maalumu.,

    Nililifahamu hili upesi kutokana na habari za viumbe wa namna hii niliwahi kusoma katika vitabu hasa vile vya Ally Mbetu na pia hata kupata bahati ya kusikia hadithi zao kutoka kwa watu tofauti tofauti.

    Sasa mule ndani tulibakia wawili tu, mimi na yule baba.

    “Sijawahi kufanya jambo lolote baya” nilisema huku nikimtizama yule mtu kwa huruma,mtu ambaye muda mfupi ulio pita tulikuwa marafiki tena rafiki aliyenisaidia kuvipata vitu vyangu, lakini sasa kawa mtu mbaya na hatari kwa maisha yangu.

    Yule mtu hakujibu kitu, alinyanyua mikono yake juu na kuanza kuzungumza vitu Fulani kwa lugha nisiyo ijua wala kuwahi kuisikia katika ulimwengu. Na kadili alivyokuwa akizungumza maneno Fulani hali yangu ilikuwa ikibadilika.

    Nilikuwa nikijisikia kitu kama usingizi mzito ukizikumba mboni za macho yangu. “Mungu wangu ndio nakufa hivyo..” usigizi mzito ulikuwa ukinijia kwa kasi, wakati yule mtu akikazana kutamka maneno yale kwa nguvu tena kwa kuyarudia rudia. “kumbe ndivyo hivi mtu akitaka kufa inavyo kuwa” niliwaza wakati giza la ajabu likinipitia katika ufahamu wangu.

    ******************

    Siku moja katika maisha nilidhani kubadilisha ndoto zangu na kuvurugikiwa ilihitaji miaka mingi jambo hilo kutokea. Nilidhani kuisha kwa uzuri wangu na kila nilichokianzisha toka nilipokuwa mdogo ilihitajika miaka mingi kama ile niliyokuwa nayo sasa. Nilikuwa msichana wa miaka 24 tu mwenye ndoto kubwa ambazo tayari sasa zilikuwa zinaeleka kutimia asubuhi ya siku inayo fuatia. Nilitarajia Kendesha gari zuri la kifahari na familia yenye furaha mchumba mzuri nitakea funga nae ndoa ndogo tu ya mkeka itakayo jumuisha watu wachache sana, ndicho kitu nilichokiwaza katika muda wote wa maisha yangu. Kwakweli Hatima ya maisha yetu anayeijua ni Mungu na kamwe huwezi kumuona na kumuomba muda zaidi maisha yafikapo tamati, kila kitu huvurugika pale jioni ya maisha yako ifikapo. Milango ya ndoto zako hufungwa na giza nene hutanda mbele, hata fimbo ya kukuongoza njia hupotea. Mwanga hufifia na woga hukusonga. Hiyo ndiyo hali iliyonipata katika usiku wa giza ni baada tu ya kupoteza jacket langu lililokuwa na vitu muhimu vya ofisini ambalo liliokotwa na mtu wa ajabu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kichwa changu kilikuwa kizito, nilipo fumbua macho, hata macho nayo yaalikuwa mazito, kwa mbali niliona ukungu mbele yangu huku nikiona kufifia kwa vitu vilivyoonekana mbele yangu.

    Nikiwa nimelala, chali macho yangu yakiwa yanitizama katika dari ya chumba nilicho kuwepo huku fahamu zangu zikiwa hazija kaa sawa nilihisi chakara chakara ubavu wangu wa kulia. Nikageuza shingo yangu.

    Mtu mwanaume alikuwa uchi huku akichezea sehemu zake zilizokuwa wima kama ukuni mkavu, alikuwa akiniangalia huku akilamba lamba lips za midomo yake.

    Sasa mtiririko wa matukio yote yaliyo tokea kabla ya kupitiwa na usingizi mzito yakarejea tena upya, nikajikuta nataka kupiga kelele, lakini ajabu sikuwa na nguvu hata ya kufumbua mdomo.

    Ni wakati huo huo pia nilipogundua kuwa hata mimi pia nilikuwa uchi wa mnyama pale nilipokuwa nimelala chali.

    “Nataka kubwakwa ‘Yaillah’, uko wapi wewe Mungu? Basi mungu fanya miujiza yako,.sitaki kubakwa na mashetani mimi” niliomba kimoyo moyo huku nikijaribu kujitikisa pale kitandani, lakini nilikuwa kama mtu aliyepigwa nusu kaputi.

    Machozi yalinitoka baada ya kugundua sina namna ya kuzuia kile kinacho onekana kutaka kutokea muda mfupi ujao.

    Kama nilivyo tegemea yule baba alipanda kitandani akawa mbele ya mapajaa yangu huku sehemu zake zikinitizama kwa uchu!.

    Yule mtu alichukua chupa ndogo nyeusi, kisha akafungua mfuniko na kutoa dawa fulani iliyokuwa na mafuta kama ya griselin ila yale yalikuwa ya njano. Kisha akayanuia kwa sauti ndogo yale mafuta, kisha akajipaka katika lile jogoo lake kubwa.

    Baada ya hapo akanisogelea na kunitanua mapaja yangu,.kwakweli ndugu msomaji huwa kila nikifkiria tukio hili, akili yangu inashindwa kabisa kulifuta na kusahau jambo hili la kinyama.

    Niseme tu kuwa huwa najihisi haya{aibu}kuelezea eneo hili, lakini kwakuwa nahitaji ulimwengu wote utambue juu ya maisha yangu na ukweli kuhusu mimi sina budi kuficha jambo hata moja katika yale mengi yaliyo nisibu.

    Mara zote nimekuwa ni mtu ninae hitaji uhuru wangu, labda kuna watu wanaweza kuona ninajidhalilisha katika hili na niseme tu nimekuwa mwanamke ninae amini katika zile falsafa za mr Sankara nilizo wahi kusoma katika vitabu nilipokuwa chuo kikuu pale mlimani alisema “ili kuleta mabadiliko na mitazamo chanya ni lazima kuwa na hali fulani ya uendawazimu. Ila tusiufikirie uendawazimu huu wa kuokota makopo bali ule ukichaa mzuri wa kuamini katika mambo au misingi fulani na kuisimamia kwa dhati pamoja na changamoto nyingi. Kwa kuamini kwa dhati katika mabadiliko haya na kutaka kuboresha maisha,” hivyo sina budi kueleza ukweli mtupu bila kujali nani ataniona mwendawazimu.

    Wazungu wana msemo usemao, to be healthy you have to share your problems with others!”



    Yule baba alipokuwa akiniingilia kwakweli nilihisi maumivu makali mno kiasi kwamba niliona kama utumbo unataka kutoka.maumbile ya yule mwanaume yalikuwa ni makubwa mno.aliniumiza.

    Alikuwa akiingiza na kutoa upesi upesi, huku pumzi zake zikimtoka kwa kasi, alikuwa katika mahaba mazito juu ya mwili wangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Na mara zote wakati ananizini nilikuwa nikiona dunia inazunguka kwa kasi huku mimi nikiwa ndani yake, yalikuwa ni mateso yasiyo mithilika.

    Yule mtu alinibaka hadi hamu yake ilipokwisha, nilikuwa nasikia sehemu zangu zote zinawaka moto.

    Sikujua kama yule mtu aliningiza katika maswahibu yale yote kwa sababu ya tendo lile, lakini pia sikuwa na uhakika wa asilimia zote kama mtu yule anaweza kuishia kunifanya vile kisha akaniachia uhai wangu.

    Nilikuwa nikitweta huku maumivu makali yakinisulubu, hasira zilikuwa zimenipanda vibaya mno, lakini sikuweza kuongea kila nilivyo hitaji kufanya hivyo.

    Yule mtu alikuwa ameniroga na kunifanyia ukatili ambao sikustahili kabisa, sikuona kama nilikuwa na kosa la kutendewa unyama ule.

    Kwakweli sikuona hata faida ya kuishi.

    Yule mtu alipotoka mwilini mwangu, alifungua kabati lililokuwa mule ndani na kutoa shuka jekundu kisha akajifunika, halafu akasogea mbele ya kitanda changu kisha akaanza kufanya vitendo vile alivyokuwa anafanya kisha nikapitiwa na usingizi wa ajabu.

    Namna nilivyokuwanimelala chali machozi yalikuwa yakinichuruzika pembeni ya macho yangu na kutiririka hadi masikioni.

    Yule mtu alikazana kuzungumza maneno yale ya ajabu, na hata yale maneno yake yalipoingia ndani ya ngoma za masikio yangu nilianza kukumbwa na hali ile kama ya awali.

    Usingizi mzito ulikuwa ukininyemelea kwa kasi, hazikufika sekunde kumi na tano tayari nilikuwa nimekwisha zama katika bahari ya usingizi.

    -

    ******************



    Sikujua fahamu zilinirudia baada ya muda gani au baada ya siku ngapi kwani kichwani mwangu nilikuwa nikipitiwa na taswira nyingi za ajabu ambapo zilifuataiwa na vipindi virefu vya kiza na utupu mrefu akilini,miongoni mwa yale yaliyo pita ni tukio la kuingiliwa kimwili na yule baba, nilikuwa nikimwona namna alivyokuwa akikazana kuniingilia huku akitokwa na pumzi nzito za huba huku mimi nikipatwa na maumivu yasiyoweza kuelezeka.

    Nakumbuka, kuna wakati nilijihisi kuchoka mno kutokana na kulala muda mrefu nilifumbua macho na kuona mwanga hafifu,. Mule ndani kulikuwa kimya hakuna kilichosikika zaidi ya mishale ya saa ya ukutani iliyokuwa ikizunguka taratibu huku ikilia “ta,ta, ta, ta” nilijaribu kuamka nikaona nina nguvu za kutosha.

    Niliamka pale kitandani na kukaa kitako, nilikuwa myonge mithili ya teja wa madawa ya kulevya mwenye kuhudhurua clinic.

    Macho yangu yalitizama ile saa ya ukutani kwakweli sikuamini kile nilicho kiona.

    Ile saaa ilionyesha ilikuwa yapata saa kumi usiku. “Inamaana kulala kote kule bado hakuja kucha asubuhi” nilijiuliza huku nikijikagua mwili wangu uliokuwa umevalishwa tena nguo zangu zote ikiwa ni pamoja na lile jacketi lililokuwa na vitu vya ofisini vyote.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Au nimelala siku mbili humu ndani huyu baba akiwa amenigeuza mkewe” niliendelea kujiuliza, lakini sikuwa na jibu kamili japo nilihisi kuwa kunauwezekano niliishi mule ndani kwa muda wa siku mbili nikiwa usingizini.

    Nilipokuwa najikagua mwili wangu ndipo nilipo ona jambo jingine lililonifanye nitishike vibaya mno.

    Tumbo langu lilikuwa kubwa kama kwamba nilikuwa na ujauzito wa mizezi tisa na muda wowote naweza kujifungua. “Mungu wangu nini hii tumboni mwangu.,nina mimba! Nimebakwa na nimepata mimba.. Lakini..hii mimba inakuwaje iwe kubwa kwa siku mbili tu.!”

    Nilinong’ona peke yangu machozi yakinitoka, “ni ukatili wa kiwango gani natendewa mimi Zahara..nabakwa hadi napewa mimba..kwanini msiniue tu..kwanini sijafa ..kwanini mniacha hai hadi sasa.. fuck you” nililia mno, jambo lile lilikuwa ni kubwa mno. Nilijiona ni kiumbe nisiye na faida ya kuishi duniani tena.

    Mwili wangu ulikuwa mnyonge mno, nilihisi kabisa ndani ya tumbo langu kuna kiumbe. Lakini jambo lililokuwa la kustajabisha ni kuwa ile mimba iliwezaje kukuwa kiasi kile kwa siku mbili tu ambazo niliamini nilikaa mule ndani.

    Nilinyanyua mkono wangu na kutizama saa yangu ndogo niliyowahi kupewa zawadi na mpenzi wangu Thabit Talib Mwaikimba, kwa mujibu wa saa yangu ya mkononi ilinionyesha ilikuwa ni saa kumi kama ambavyo ile ya ukutani ulivyosema, lakini katika kutaka kupata uhakika zaidi nilibofya ile saa ili nione ilikuwa ni siku gani na tarehe ngapi maana siku ya mwisho kuingia mule katika lile jengo ilikuwa ni usiku wa saa saba siku ya alhamisi ya tarehe 29/3/1989.

    Saa yangu ilinionyesha kitu kilicho nifanya kuanza kupata hisia kuwa huenda nipo katika ndoto mbaya usingizini.

    Ile saa ilinionyesha kuwa ilikuwa ni siku ya alhamisi ya tarehe ya tarehe hiyo hiyo 29/3/1989. yanii ilikuwa ni usiku ule ule.

    “Sasa hii miujiza gani tena jamani yanii kulala kote kule kumbe hata masaa matatu hayajaikwisha!.” Lakini hilo lilikuwa ni dogo katika kubwa lililoumiza mtima wangu.

    Vipi niwe na mimba kubwa kama ya miezi tisa ilihali niliingiliwa kimwili lisaa limoja tu lililopita.

    Niliona ninalo bomu kubwa ambalo linalokuja kulipuka katika maisha yangu muda mchache ujao.

    “Sasa nifanye nini” nilijiuliza, wazo la kutoroka mule ndani lilinijia, nilisimama wima nikasogea pale mlangoni, bado ukimya wa ajabu uliendelea kushika hatamu.

    Nikashika kitasa na kukinyonga kushoto, kitasa kiliachia “kwachaa” nikatoka kwa kunyata nikiwa na tahadhari kubwa.

    Niliangalia kulia na kushoto nikaona nipo katika kikorido kirefu kilichokuwa na vyumba vingi vilivyo fungwa pembeni yake.

    Nikatizama mazingira yale kisha nikashika uelekeo ambao nilihisi ni uelekeo sahihi wa kunitoa nje ya jumba lile.

    Tumbo langu lililokuwa na kiumbe ndani yake lilikuwa zito na lilikuwa likiuma, nilikuwa nikisikia kitu kilicho kuwa tumboni ambacho bila shaka alikuwa ni mtoto akicheza cheza tumboni.

    Niliendelea kujisukuma kwa mbele huku nikiwa na tahadahli kubwa, sikuwa na woga tena, sikuogopa kifo kwani hata hivyo sikuona faida ya kuishi katika dunia ilihali nikiwa ni binadamu niliye na kovu baya moyoni mwangu ambalo siwezi kulisahu hadi siku naingia kaburini.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikiwa nazipiga hatua mara ghafla nilianza kusikia sauti kwa mbali.

    Ile sauti ilipenya masikioni mwangu na kunifanya nipate kizunguzungu, sauti ya yule baba akizungumza maneno ambayo huwa yananifanya nizingirwe na usingizi mzito.

    Yale maneno yalizidi kupenya katika masikio yangu pasina kuelewa mzungumzaji yupo sehemu gani, lakini kwa namna nilivyokuwa nikisikia ilikuwa ni kama mzungumzaji yupo maili nyingi kidogo kutoka pale nilipokuwepo mimi, kwani ile sauti ilingia katika masikio yangu kama mwangwi.

    Nilianza kupepesuka nguvu zikiniishia huku Giza la ajabu likivaa mboni za macho yangu.

    Na wakati huo yule mtoto tumboni mwangu alikuwa akicheza,giza liliendelea kutanda mbele yangu na kujikuta nguvu zinaninishia na kuanguka chini kama mzigo.

    Baada ya muda mrefu kupita nikiwa katika dimbwi la usingizi, mara nilistuka nilipohisi sauti kali ikililia masikioni mwangu, ilikuwa ni sauti ya mtoto mchanga.

    Nilifumbua macho yangu na kujikuta nipo katika kile kile chumba mtoto mdogo wa mwaka mmoja akiwa pembeni yangu katika kitanda.

    Na nilipo rejewa tu na fahamu zangu, tukio baya la kubakwa na yule baba ndio ilikuwa kitu cha kwanza kupita katika ubongo wangu.

    Nilijinyanyua kitako na kuketi pale kitandani. Mtoto mzuri wa kike alikuwa pembeni yangu.

    Yule mtoto hakuwa analia tena baada ya mimi kuamka.nilijiangalia tumbo langu na kuona mabadiliko, sikuwa na mimba tena, nilijiona niko tofauti katika maungo yangu.

    Matiti yangu yalikuwa makubwa na yaliyo lala ilihali awali matiti yangu yalikuwa wima.



    Lakini hata sehemu zangu za siri, kwakweli vile nilivyokuwa najiskia awali si sawa na muda ule. Hapo nikaelewa kuwa ile mimba iliyoingia kimaajabu nilikuwa nimejifungua tena kimaajabu, na inavyo elekea nilijifungua wakati ule nimepoteza fahamu.

    Lakini ajabu nyingine mbele yangu ni yule mtoto pembeni yangu. Alikuwa ni mtoto mkubwa wa mwaka mmoja ambaye swali kuu likawa yule mtoto amewezaje kukua upesi kaisi kile. Wakati nalifikiria hilo saa yangu ya mkononi bado ilinionyesha ilikuwa ni tarehe 29/3/1989. siku ya alhamisi.

    “Inamaana haya mambo yanenda halaka hivi kwa dakika ama ni kwa kutegema siku miezi na miaka”

    “No lazma niondoke eneo hili, leo lazma niondoke siwezi kuishi humu! Nini hatma ya maisha yangu?.kama kufa na acha nife tu, lakini siwezi kuendela kuishi kifungoni kiasi hiki” nilendelea kuwaza nikiwa nimeketi kitako mule ndani tukiwa wawili tu, mimi na yule mtoto mchanga.

    Sasa nikawa nafikiria namna ya kukabiliana na mazingaombwe yale ambayo yamekuwa yakindelea kutokea.

    Kitu kingine ambacho nimesahau kukueleza mpenzi msomaji, ni kuwa toka siku ile nibakwe na yule mbaba sikuwahi kumwona yeye wala mtu mwingine yeyote mule ndani hadi siku nilipo amka na kujikuta nipo na yule mtoto mchanga wa miaka miwili.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikaendela kuwaza namna ya kutoroka katika lile eneo nililo amini ni kifungo kwangu. Swali dogo likaja kichwani mwangu. Je nitoroke na yule mtoto ambaye niliamini ni wangu?

    Nikapata kidogo kigugumizi katika hilo lakini sauti fulani ikanambia na kunitahadhalisha kuwa sitakiwi kuondoka na yule mtoto kwani kufanya vile ni kutengeneza mazingira ya kuandamwa na wale viumbe kwani kwa namna yoyote ile kupewa kwangu ujauzito ilikuwa ni mipango yao.

    Lakini sauti nyingine ikanambia kamwe nisimwache mtoto wangu, kwani pamoja na kwamba upatikanaji wake haukuwa mwema lakini bado yule malaika atabakia kuwa damu yangu, na ni mimi mwenye jukumu la kuhakikisha usalama wa yule mtoto unakuwepo kwani mimi ndiye mama yake mzazi.

    Sasa nikawa nakinzana na nguvu mbili, kuondoka na yule mtoto ama kumwacha.

    Nilifikiria kwa muda mwisho nikazimia kumwacha yule mtoto mchanga.

    “Sikuja na mtoto hapa, vipi niondoke na mtoto, kwanza si mtoto huyu, mtoto gani anaingia tumboni siku hiyo hiyo na kuzaliwa siku hiyohiyo kisha anakuwa siku hiyo hiyo..no siwezi kubeba matatizo haya.” Nilinong’ona peke yangu nikiteremka kitandani.

    Msomaji pengine haya nikuelezayo unaweza kuhisi kabisa ni hadithi za kubuni, lakini amini nakwambia hakuna hata moja la kubuni katika hayo niliyokwisha kueleza.

    Kuna wakati hata mimi sikuwa naamini wakati yananitokea lakini amini nakwambia katika huu ulimwengu kuna mengi ya ajabu ambayo yanatokea katika jamii ya siri

    [secret society] ambayo ukisimuliwa unaweza usiamini asilani.

    Sasa nikiwa pale, nilipo angaza chini nikaona raba zangu zikiwa chini ya kitanda, upesi nikavaa na kuwa tayari kuondoka.

    Lakini ghafla.

    Nilisikia ile sauti, sauti ya yule baba, alikuwa akizungumza yale maneno yenye kunifanya nipatwe na usingizi wa ajabu.

    Sauti ile kama ilivyo kuwa awali, ilitokea maili nyingi, ilifika pale kama mwangwi

    Na mara ilipopenya katika masikio yangu nikahisi kizungu zungu, nikaelewa kitu gani kinaenda kutokea, safari hii sikuwa tayari kabisa kuendela kulala lala pale huku wale wachawi wakinichezea kama shangazi yao, nilidhamiria kabisa kuondoka mahala pale, ile sauti ikakazana kuyatamka yale maneno, hali yangu nayo ikaendela kubadilika, kizunguzungu kikazidi kunielemea huku giza la ajabu likinizingizira.

    “No no siwezi kuendelea kubaki hapa..” nilijikuta kinibwata kwa hasira wakati ile sauti ikizidi kugonga ngoma za masikio yangu.

    Sasa akili yangu ikafanya kazi upesi upesi, kwakuwa ile sauti ikisikika masikioni mwangu ndio huleta madhala ya kupoteza fahamu nikaona njia pekee ya kuzuia hali ile ni kuziba masikio ile sauti nisiisikie.

    Niliingiza vidole vya shahada ndani kabisa ya masikio yangu na kukandamiza kwa nguvu kuzuia ile sauti kupenya katika masikio yangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sikusikia chochote zaidi ya mvumo fulani katika masikio ambao huwa unasikika pale unapoziba masikio. {Wanazuoni wa tauhidi husema ule ni mvumo wa moto wa jehanamu}.

    Kwa muda wa dakika mbili niliendelea kuziba masikio pasina kusikia yale maneno, niliondoa taratibu vidole katika masikio, sikusikia kitu chochote zaidi ya sauti ya yule mtoto aliyekuwa akilia kwa nguvu.

    Nilibaki nimesimama nisijue kitu gani nifanye, mara nikiwa bado nimesimama nilihisi nyayo za mtu akija kutokea nje akielekea mule ndani.

    Akili yangu ikaendela kufanya kazi upesi upesi, niliruka kitandani na kulala gubigubi na kujifanya nipo katika usingizi mzito.

    Zile nyayo ziliendelea kusogea mule ndani na hatimae nikahisi kitasa cha mlango kikiguswa na kisha akaingia mtu, kupitia pembe ya jicho niliweza kumwona mwanaume mzee mno akiwa amevalia kanzu nyekundu.

    Nilipo mtizama vizuri mtu yule nikagundua mtu yule alikuwa ni mzee kati ya miaka themanini, lakini nipo mtizama kwa uzuri zaidi nikagundua yule mzee alikuwa akifanana mno na yule baba aliye nibaka,nikahisi pengine huenda wale watu walikuwa ni watu wa familia moja, famili gani hii washenzi wa tabia kiasi hiki, niliwaza.

    Alikuwa amekamatilia vibuyu viwili vilivyo fungwa hirizi nyeusi na nyekundu.

    Yule mtu alisogea hadi pale kitandani kisha akazungumza maneno fulani nafikiri ya kichawi kisha akafungua vile vibyu vyake, mara moshi mweusi ulitokea katika vile vibuyu na kusamba mule ndani, baada ya hapo alimsogelea mtoto kisha akambeba na kutoka nae nje.

    Nilitaka kufanya kitu baada ya tukio lile lakini nafsi nyingine ikanionya juu ya hilo.

    Niliendelea kutulia kwa namna ile ile kwa muda wa dakika tano nikitegemea yule babu anaweza kurejea. Lakini dakika tano nyingine zilipita yule babu hakutokea, nikajiongeza dakika tano nyingine za ziada ili kujilidhisha kuwa yule mtu hawezi kurejea, zilipita tano nyingine lakini hakurejea.

    Nilisimama kwa ungalifu nikavaaa raba zangu, kisha nikauendea mlango, wakati huo ilikuwa yapata saa kumi na nusu ya tarehe 29/3/1989, na majira hayo muadhini alikuwa akiadhini kule katika jumba la ibada.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog