Simulizi : Jini Wa Kuzimu
Simulizi : Safari Ya Kuzimu
Sehemu Ya Nne (4)
Mama Nyamizi
aliingia ndani ya gari huku
akilia kwa
kwikwi. Alijikuta akiujutia uamuzi
wao wa
kumpeleka binti yao kwa mganga wa
kienyeji.
Mzee Angu naye alikuwa akifungua
mlango wa
gari akahisi mkono wa mtu
ukimgusa begani.
Alipogeuka alipigwa na
butwaa baada ya
kumuona Dr,Kisonoko
amesimama nyuma yake.
Akajikuta
akitetemeka kwa woga na wasiwasi
wa hali ya
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
juu.
SASA
ENDELEA......
Alijikaza kiume na kutoa
kauli.
“wewe ni nani?”
“we una onaje?”
“mganga amekwisha kufa. Tena nimeshuhudia
kwa macho yangu” alisema mzee Angumbisye
huku akiwa na wasiwasi.
“mimi ni Dr. kisonoko”
“sawa. Kama wewe ni Dr.kisonoko, niambie
binti yangu yuko wapi?”
“unataka kujua alipo mtoto wako sio?”
“ndio”
“nifuate
ndani” alisema mganga huku
akielekea ndani.
Mzee Angumbisye alipumua
kwa nguvu huku
akitafakari cha kufanya.
Alipiga moyo konde
na kumfuata mganga.
Alipofika ndani mganga
alimtaka aje na mke
wake. Mama nyamizi
hakuwa anajua nje ya
gari kulikuwa
kunaendelea nini.
Alichokifahamu yeye kwa
wakati ule kilikuwa
ni kutoa machozi tu.
Mzee Angu alimchukua
mke wake na kuingia
nae ndani kwa mganga.
Mama Nyamizi
alipokutana na sura ya
mganga alidondoka na
kupoteza fahamu.
# * # * #
Kwa upande wa Mganga Ngoma moshi
uliendelea kufuka kwenye kile chungu. Ile
sauti iliyokuwa ikikwaruza ilisika ikiongea
“kijana wenu anamchumba anaitwa Husna. Au
sio?”
“ni kweli,
lakini sisi hatumkubali” Alisema
mzee
Shabani.
“kwanini?”
“kwasababu yupo mchumba ambaye
tumemtafutia sisi na tunamfahamu kiundani
kuliko huyo Husna”
“sasa basi, ili kijana wenu apone ni
lazima
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
mkubali amuoe Husna”
“inamana hakuna njia nyingine mbadala?”
“hiyo ni amri. Vinginevyo mnaweza
kumchukua kijana wenu na kuondoka nae”
“sawa mkuu tumekubali” mzee Shabani na
mkewake walijikuta wakijibu kwa pamoja.
“mmekubali?’
“ndio”
“basi
kazi imekwisha. Hivyo inabidi
tumsafirishe
kijana wenu leo hii akaonane na
wazazi wa
huyo binti”.
“sasa itawezekanaje, wakati
hali yake ndiyo
kama unavyoiona?”
“hilo sio tatizo. Akishaondoka tu haliyake
itakuwa nzuri, na atafika huko akiwa
bukheri
wa afya”.
“sasa wazazi wa huyo binti wanaishi wapi?
“KUZIMU”
“kuzimu….! Unamaana gani mganga?”. alihoji
mzee Shabani kwa mshangao.
“namaanisha kuzimu sehemu wanayoishi
mizimu na wafu”
“haiwezekani. Kijana wangu hawezi kuoa mfu”
“Husna sio mfu”
“kumbe ni nani?”
“Husna ni Jini”
“kwahiyo kijana wangu amuoe jini?
haiwezekani”
“unamtaka kijana wako au humtaki?”
“namtaka na nampenda, ndiomana sitaki aoe
jini”
Mzee
Shabani aliendelea kuwa na msimamo,
lakini
mganga naye alijitahidi kutumia
maneno ya
kumlainisha. Alimueleza kuwa
majini sio
viumbe wabaya kwa binadamu.
Isipokuwa watu
wanashindwa kutofautisha
kati ya majini na
mashetani. Mashetani ndio
viumbe wabaya na
walioahidiwa moto na
Mwenyezi Mungu siku ya
hukumu. Lakini
majini ni viumbe kama
walivyo binadamu. Upo
uwezekano wa kuishi
pamoja pasipo kuona
tofauti yoyote.
Aliwaambia kuwa hata Yasini
angewezaweza
kumuoa Husna na kusiwe na
tatizo lolote.
Akamalizia kuwa endapo
wangepingana na
maamuzi hayo kijana wao
angepoteza
maisha.
“mnakubali kumpoteza kijana wenu
kizembe
zembe?” Dr. Ngoma alihoji
“hapana mtaalamu”
“kwahiyo mnasemaje?”
“hatuna jinsi. Tumekubali”
“kazi imekwisha. Sasa tumuandae kijana kwa
SAFARI YA KUZIMU”
“kwahiyo atakwenda na usafiri gani?”
“tunakwenda naye hadi mzimuni, hapo ndipo
safari yake itakapoanzia” Mganga
alifafanua.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya maongezi hayo ule moshi wa
kwenye chungu uliongezeka na kusababisha
kiza kinene kutanda mle chumbani. Hakuna
hata mmoja aliyeweza kumuona mwenzake
kutokana na kiza kilichokuwa kimetanda.
Baada ya muda kidogo moshi ule unapungua
na kiza taratiibu kinaanza kutoweka. Nuru
ya
jua inaangaza na watu wanaonana.
Mazingira
waliyokuwepo ni tofauti nay ale
ya nyumbani
kwa mganga. Walikuwa katikati
ya msitu
mnene wameketi chini ya mti
mkubwa
uliokuwa umefungwa vitambaa
vyekundu
kwenye shina.
Dr. alifunika kile chungu kasha akaingiza
mkono kwenye kikapu na kutoa kibuyu kidogo
ambacho alianza kukipuliza. Kibuyu kile
kilitoa sauti mithili ya firimbi. watu wote
walikuwa kimya wakimuangalia mganga.
Upepo mkali ulianza kuvuma na kuyumbisha
miti huku na kule. Alitokea nyoka mkubwa
sana aliyejiburuza kuelekea pale walipokuwa
wamekaa. Mgongoni mwa nyoka kulikuwa na
mtu amekaa mithili ya mwendesha farasi. Mtu
Yule alikuwa ni mwanamke mweupe mno,
nyelezake nyeupe zilining’inia hadi kwenye
mabega, mikononi alikuwa na kucha ndefu
kuliko kawaida, macho yake makubwa
yaling’aa kama macho yap aka. Kiunoni
alikuwa amejifunga shuka jekundu
lililoburuzika hadi chini kiasi cha
kutoruhusu
miguu kuonekana.
Nyoka aliyekuwa amembeba mtu Yule
alisimama hatua chache kutokea pale
walipokuwa wamekaa. Yule mtu mweupe
aliteremka na kuwasogelea taratibu. Mganga
na wafuasi wake walipiga magoti na
kuinamisha vichwa vyao chini. Mtu mweupe
alifika na kuwashika vichwa mmoja badala ya
mwingine. alipomaliza alikwenda kwa Yasini
na kumpaka vitu vyeusi usoni. Akafungua
kibuyu cha mganga Ngoma na kutoa dawa
ambazo aliwapaka mzee Shabani na
mkewake. Dwa ile ilisemekana kuwa ilikuwa
ni
ya kuwaondoa hali ya woga.
Baada ya hatua za shughuli za hapa na pale
walitokea watu wafupi na weusi wengi mno.
Watu wale walikuwa wamebeba jeneza.
Walikwenda hadi pale chini ya mti na
kumbeba Yasini na kumtumbukiza ndani ya
Jeneza. Mtu mweupe alitangulia mbele na
watu wote wakaanza kumfuata. Walifika
sehemu iliyokuwa na shimo kama la kuzikia.
Walitumbukiza jeneza lile na kuanza
kulifukia.
Baada ya dakika kadhaa Yasini
alikuwa
amekwishazikwa akiwa hai…
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya mazishi ya Yasini watu wote
walirejea pale chini ya mti mkubwa
isipokuwa
wale watu wafupi walipotea
palepale
walipomaliza kufukia kaburi. Mtu
mweupe
aliwaambia kuwa walitakiwa warudi
pale siku
ya saba ili kuja kumpokea kijana
wao akiwa
mzima wa afya. Baada ya maneno
yale
alianza kuzungumza na mganga Ngoma
kwa
lugha ya kiganga kasha mtu Yule
alipanda
kwenye nyoka wake na kutoweka kwa
mwendo
wa kasi mno. Mganga alifunua chungu
chake
nacho kama kawaida kilianza kutoa
moshi
mzito uliosababisha kiza
kinene.
#*#*#
Kwa upande wa Dr. Kisonoko Mama nyamizi
fahamu zilimrejea. Alipofumbua macho
alikutana uso kwa uso na Dr. Kisonoko.
Hakuweza kuamini kilichokuwa kikiendelea
mle ndani, mambo yote yaliyotokea aliyaona
ni kama ndoto. Alichokuwa akikiamini ni
kuwa
binti yake pamoja na Mganga
wamekufa
kwenye maji na kuliwa na samaki wa
baharini.
Akajikuta akimuogopa na
kumkumbatia mume
wake kwa wasiwasi. Hata
hivyo mganga
alijitahidi kuwatoa
hofu.
“Hamna sababu ya kuniogopa mimi ni
Dr.
kisonoko yuleyule mnayemfahamu”
alisema
mganga.
“Na yule aliyekufa kule baharini ni nani?”
mzee Angumbisye alihoji.
“ni mimi…. Lakini sikuwa nimekufa. Samaki
aliyekula mwili wangu alikuwa ni mzimu
ambao ndio uliniokoa na kunirudisha
nyumbani”.
”kwahiyo binti yetu ndio amekwishakufa?”
“hapana binti yenu yupo hai”
“yuko wapi?”
“Kwa bahati mbaya amechukuliwa na jini
ambaye tulipanga kwenda kumuangamiza”
“kwahiyo unampango gani?”
“ondoeni wasiwasi. Mimi ndio Dr. Kisonoko
hakuna linalonishinda kirahisi kama hili”
“wacha masihara Dr. bado tunamhitaji binti
yetu”
“kwahiyo
hamniamini au?”
“Tunakuamini, lakini
hatukuelewi”
“najua mtanielewa. Ila
tunajiandaa sasahivi
kuelekea GAMBUSHI,
huko tutaweza kufika
kuzimu ambako Nyamizi
amefichwa”. Yale
maneno hayakuingia kabisa
akilini mwa mzee
Angumbisye. Aliyaona ni
kama mchezo wa
kuigiza. Hata hivyo alijipa
moyo na
kukubaliana na mganga
kwasababu
alimshuhudia akiliwa na samaki
lakini
anamuona mbele ya macho yake.
Kwahiyo
alitegemea muujiza mwengine
ungetokea kwa
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
mtoto wake.
Saa
kumi na mbili asubuhi walikuwa ndani ya
basi la AIR BUS lililokuwa likielekea mjini
Shinyanga. Kwenye mida ya saa tano usiku
walikuwa wamekwishaingia Shinyanga mjini.
Safari ilikuwa ndefu sana kutokana na basi
kubata hitilafu njiani. Walilazimika kulala
kwenye hoteli moja maarufu mjini pale
liyokuwa ikifahamika kama STAFF IN HOTELL
hadi kesho yake ndipo waendelee na safari.
Waliamka saa kumi na moja asubuhi na
kujiandaa kwa safari ya kuelekea Gambushi
kijiji kilichosifika kwa uchawi. Lakini
walipotoka nje hawakuamini kilichokuwa
kikiendelea. Walikuwa wamesimama nje ya
hoteli moja iliyokuwepo Raskazoni mjini
Tanga maarufu kama MKONGE HOTEL.
“Shit…” alitamka mzee Angumbisye na
kuelekea mapokezi. Alimkuta dada akiendelea
na shughuli zake za kikazi akamsemesha,
“samahani binti”
“bila ya samahani mzee wangu”
“hivi hii ni hotel gani na ipo mkoa gani?”
“ni MKONGE HOTELL na hapa ni mkoani
Tanga” msichana yula alijibu huku akuwa
ndani ya mshangao. Maneno yale
yalimchanganya sana mzee Angumbisye.
Alipumua kwa nguvu huku akikuna kichwa
asijue ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
Aliinua
macho na kumtazama yule dada
ambaye
alionekana bado
akimshangaa.
“kwani vipi mzee” msichana
yule alihoji
“ah….aa..h…usijali” alijibu na
kuondoka
kuelekea walipo wenzake.
Alipofika nje aliwakuta wenzake nao bado
wakiwa katika hali ya mshangao. Mzee
Angumbisye aliwagutusha kwa kuwasemesha.
“vipi Mganga ni kitu gani kinaendelea
hapa?”
“mambo ndio kama unavyoyaona”
mganga
alijibu.
“sasa tunafanyaje?” mama Nyamizi alidakia
“mambo ni magumu.. inabidi turudi Pangani
tukajipange upya” mganga alijibu kwa ufupi.
Mzee angumbisye na mkewake hawakuwa na
la kusema kwasababu maji wamekwisha
yavulia nguo hivyo hawana budi kuyaoga.
Walikuwa tayari kufanya jambo lolote ambalo
lingekuwa ni chanzo cho kupatikana kwa
binti
yao. Waliamini kuwa uwongo wa mganga
ni
nafuu kwa mgonjwa.
Walichukua kibasi kilichowapeleka hadi
stendi
ya mabasi ambako waliingia kwenye
basi la
Rahaleo iliyokuwa ikielekea
pangani. Dr.
kisonoko alikuwa amekaa siti
moja na mzee
wa makamo. Kabla basi
halijaanza safari yule
mzee alimsemesha
Dr.Kisonoko.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/-
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/-
“ kijana poleni sana kwa safari” maneno
yale
yalionekana kumkera mganga kisonoko,
hivyo
aliamua kugeuzia shingo dirishani
na
kumpuuza.
“kijana najua upo katika wakati mgumu na
mimi nimekuja kukusaidia” alisema yule
kikongwe na kumfanya Dr. kisonoko kushtuka
na kugeuza shingo kumtazama kwa makini.
Na kujikuta akimhoji.
“kwani wewe ni nani?”
“mimi ni mwanakijiji wa Gambushi. Wakuu
wamechukizwa na ujio wako na wageni pasipo
kuwafahamisha” alisema maneno hayo na
kukohoa kisha akameza mate na kuendelea
kuongea.
“hivyo
basi ili wewe na wageni wako muweze
kuingia
pale inabidi mtoe kafara la kondoo
watatu.
Tena shughuli zote za kutoa kafara
zifanyike pale hotelini mlipolala jana”
alimaliza yule kikongwe na kushika fimbo
yake kutaka kuondoka.
“sasa mzee…..” Dr. alitaka kuongea kitu
lakini
alichelewa kwani yule kikongwe
alitoweka
ghafla. Akawaambia wenzake
wateremke na
kurejea hotelini walikolala.
Suala lile
lilimchukiza sana mzee
Angumbisye na kutaka
kuongea kitu kwa
hasira lakini mkewake
alimtuliza.
Dr. aliwatuma vijana wake kwenye soko la
Tangamano kwenda kununua kondoo wa
kafara. Akaingia chumbani kwake kwaajili ya
maandalizi ya kutoa kafara, lakini
alichokiona
baada ya kufungua mkoba wake wa
uganga
alitamani kufa. Vibuyu vyake vyote
vya
uganga vilikuwa vimebadilika na kuwa
vifuu
vya nazi……
Alipokuwa akiendelea kushangaa akahisi mtu
anamshika kwenye bega. Alipogeuka alimkuta
yule kikongwe wa kwenye basi amesimama
nyuma yake. Safari hii alionekana
amekasirika
sana.
“hadi sasa mizimu imekasirika kwa kutakaka
kupeleka binadamu wa kawaida katika himaya
ya GAMBUSHI. Unafahamu wazi wanaofika
kule ni wafu, wachawi,na mizimu. Au hijui
hilo?” alihoji yule mzee kwa hasira.
“najua babu, lakini hawa watu wana matatizo
na huko ndiko pekee kwenye msaada” alijibu
Dr kisonoko kwa upole.
“sawa lakini tatizo lako ni kutokutoa
taarifa
kwa wazee”
“basi mzee naomba msaada wako”
“nitakusaidia. Ila kwa masharti”
“sawa mzee wangu”
“utakapomaliza kutoa kafara, utatangulia
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
wewe kwenda Gambusi, na wengine watakuja
nyumayako” alizungumza yule mzee na kutoa
kicheko kwa sauti.
“lakini babu, zana zangu zimebadilika na
kuwa vifuu vya nazi”
“hilo sio tatizo. mabo yatakuwa mazuri.
Nakutakia kazi njema” alisema mzee na
kutoweka machoni kwa mganga. Mganga
alipumua kwa nguvu mithili ya mtu aliyetoka
kubeba mzigo mzito. Aliusogelea mkoba wake
na kuufungua. Hakuyaamini macho yake,
vibuyu vyake vilikuwa vimerudi katika hali
ya
kawaida. Alijawa na furaha isiyo kifani.
Mara
alisikia mlango unagongwa. Akafungua
na
kuwakuta vijana wake mlangoni.
Walimueleza
kuwa tayari wamekwisha leta
kondoo.
Dr aliwaita mzee Angumbisye pamoja
na
mkewake ambao muda wote huo walikuwa
nje
wakitafakari mambo
yanayowatokea.
Walipofika Dr. kisonoko
alianza manjonjo yake
ya kiganga. Aliwasha
udi na kuzungumza
maneno ya kiganga. Baada
ya muda mfupi
hali ya hewa nje ilianza
kubadilika. Wingu
nene lilitanda, radi
ikiambatana na ngurumo
zilimulika, upepo
mkali ulivuma. Kutokana na
hali hiyo watu
wote waliokuwa wamepanga
hotelini pale
walijifungia vyumbani mwao.
Hapakuwepo na
hata mtu mmoja
aliyeonekana nje ya jengo
lile. Dr. kisonoko
aliitumia nafasi ile
kutoa kafara.
Walikwenda ufukweni mwa
bahari na
kuchimba shimo lenye urefu wa
kama futi
tano. Waliwavisha wale kondoo
vitambaa
vichwani. Mmoja alifungwa kitambaa
cheupe,
wa pili kitambaa cheusi, na wa tatu
kitambaa
chekundu. Wakawatumbukiza ndani ya
lile. Dr
kisonoko alivua nguo zote na
kubaki kama
alivyozaliwa kisha akaingia
kwenye shimo na
kuwashika vichwani wale
kondoo. Alianza
kutabana kwa lugha ya
kiganga. Hali ya hewa
nayo ilizidi kuwa
mbaya, mawingu yalizidi
kuwa meusi. Ilikuwa
ni saa tano asubuhi lakini
kiza kilifanya
kuonekane kama saa nane za
usiku. Mwanga wa
radi ndio uliwasaidia
kuona walichokuwa
wakikifanya.
@*@*@
Yasini alifumbua macho na kukumbana na
giza nene. Hakuelewa alikuwa wapi na nini
kilikuwa kinaendelea. Alitulia kama dakika
tatu akijaribu kutafakari alipokuwa lakini
hakupata jibu. Akaamua kusimaa lakini
alishindwa kwasababu alijigonga na
kurudisha kichwa chake. Alinyoosha mkono
wake wa kulia lakini hakufanikiwa kwani
alijigonga. Mkono wa kushoto nao ulikuwa
vilevile. Hapo ndipo alipogundua kuwa
alikuwa
amelala ndani ya kitu kilichofanana
na boksi.
Alijaribu kuvuta kumbukumbu jinsi
alivyoingia
ndani ya lile boksi lakini
kumbukumbu
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
hazikuja. Akanyoosha mikono yake na
kusukuma kwa nguvu upande wa juu ya lile
boksi, mara mwanga mkali ukampiga
machoni. Mfuniko wa lile boksi ulifunuka
hivyo alitoka haraka sana na kusimama
pembeni.Loo! kumbe alikuwa amelala ndani
ya jeneza. Macho yalimtoka mithili ya chura
mzee. Pumzi zikamjaa na kuanza kupumua
kwa harakaharaka.
Sauti kali za paka zilizotokea nyuma yake
zilimshitua na kumfanya ageuke. Walikuwa ni
paka wengi weusi waliokuwa na macho makali
kama tochi ya muwindaji. Wote walikuwa
wakimkodolea macho yasini. Walinyamaza
ghafla baada ya Yasini kuwageukia. Alitokea
paka mmoja ambaye yeye pekeyake ndiye
aliyekuwa na rangi nyeupe. Alitembea
kuelekea pale alipokuwa amesimama. Yasini
alivyogeuka nyuma lile jeneza halikuwepo.
Hakutaka kuwaza mara mbili, alitimua mbio
ns wale paka nao walimuunganishia na
kumfukuza. Kila alivyojitahidi kuongeza
mwendo paka nao waliongeza. Yasini akaona
huo ndio ulikuwa mwisho wa maisha yake.
Hakuweza kuamini macho yake baada ya
kugeuka nyuma kuwaangalia wale paka.
Hapakuwepo na hata paka mmoja. Alishindwa
kuelewa jinsi paka wale walivyokuwa na
spidi
kushindwa kumfikia. Alipohakikisha
kuwa
amewapoteza kabisa alipunguza
mwendo.
Alikuwa amechoka sana. Akakutana
na
msichana mmoja aliyekuwa
akitembea
mwendo wa kukazana, akamuomba
msada.
“naomba unisaidie dada” aliongea
Yasini
huku akihema mfurulizo
“vipi unatatizo gani kaka?”
“paka”
“Paka!...
wana nini?”
“wananikimbiza”
“wewe ni mgeni hapa?”
“mgeni! Kwani hapa ni wapi?” baada ya
Yasini kuhoji swali hili, yule dada alianza
kucheka
kicheko
cha kebehi. Alifungua pochi yake na
kutoa
kitu kama sarafu na kumkabidhi Yasini.
“Chukua hii”
“nini?”
“chukua
itakulinda” Yasini alinyoosha mkono
kutaka
kuchukua lakini kwa bahati mbaya
ilidondoka
chini. Wakati yasini anainama
kutaka
kuokota ile sarafu alijikuta akitamani
kuzimia. Miguu ya yule msichana ilikuwa ni
kwato za ng’ombe. Yasini alipoiona hali ile
aliiacha ile pete na kutimua mbio akimuacha
yule dada akicheka kwa sauti. Alipoona
amtefika mbali na hakukuwa na mtu
aliyemfuata akasimama huku akihema mara
mbilimbili. Hakuweza kuamini kama
amefanikiwa kumtoka yule mtu aliyekuwa na
kwato miguuni.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/--
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/--
Kitu kilichokuwa kikizidi kumchanganya ni
kuwa hakuwa anajua pale alipo ni wapi.
Mandhali yale hakuwa anayafahamu kabisa.
Hivyo alijikuta akikosa muelekeo maalum.
Hakuwa anajua anakoelekea wala anakotokea.
Kwa bahati nzuri alitokea mtu na baiskeli.
Ikambidi kuomba lifti kuelekea kule yule
mtu
alikokuwa anaelekea pengine
angeweza
kupata msaada. Yule mwendesha
baiskeli
alimpakia Yasini bila hiyana wala
kinyongo.
Yasini alitulia kwenye baiskeli
utadhani
alikuwa ana fahamu alipokuwa
akielekea.
Hakuona sababu ya kuvumilia
hivyo ilimbidi
kuhoji.
“samahani ndugu naomba kuuliza?”
“bila samahani kijana uliza tu”
“hivi hapa ni wapi?”
“kwani we umefikaje hapa?”
“kwakweli sifahamu. Nimejikuta tu niko hapa
na kukumbana na vituko mbalimbali. Hivi
ninavyokwambia nimekutana na mtu ana
kwato miguuni”
“kwato?”
“ndiyo,
tena kwato za ng’ombe”
“kama hizi” yule mtu
aliinua miguu yake na
kumuonesha Yasini
miguu yake iliyokuwa na
Kwato.
kama yule msichana aliyekuwa
anamzungumzia. Yasini hakusubiri kitu bali
aliruka kutoka kwenye baiskeli na kutimua
mbio. Alijiona ni mtu mwenye mkosi siku
hiyo.
Alitamani kupata msaada lakini
hapakuwepo
na mtu wa kumsaidia. Hakuwa na
imani tena
na mtu yeyote yule. Aliendelea
kukimbia bila
kujua alikokuwa
anaelekea.
Kwa bahati aliuona msikiti na
watu wakiwa
wanajitoharisha kwa kuswali.
Alifika pale na
kusimama huku akihema kama
mbwa
aliyeokoka mikononi mwa chatu. Kila
mtu
alikuwa bize kujiandaa na swala.
Akawaona
hao ndio watu pekee wa kumsaidia.
Hivyo
naye alinawa na kuingia msikitini.
Baada ya
ibada alisimama na kutoa salamu
kisha
akaongea kwa sauti.
maneno yaliwafanya waumini wote kutulia na
kumsikiliza kwa makini.
“kwajina ninaitwa Yasini Shabani. Nimefika
katika kijiji hiki pasipo kujitambua. Pili
nimekuwa nikikumbana na mambo ya kutisha
sana” alisema Yasini
“mambogani ambayo anakutisha wewe?”
alihoji mmoja wa waumini wale
“kwakweli yanatisha mno. Naogopa hata
kuyasimulia”
“sasa tutakusaidiaje?”
“hadi sasa nimeshakutana na watu wawili
wenye kwato za ng’ombe miguuni”
“kamahizi” wale waumini waliinua miguu yao
iliyokuwa na kwato na kumuonesha Yasini.
Alipotaka kukimbia mlango ulijifunga na
wale
waumini wakaanza kucheka kwa
dharau.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Yasini alibaki amesimama akitetemeka kwa
woga. Ghafla waumini waligeuka paka weusi.
Akawakumbuka wale paka aliowakimbia muda
mfupi uliopita. Mara yule paka mweupe
alijitokeza na kumsogelea tena. Aliongezeka
ukubwa kila alipopiga hatua. Hadi
alipomkaribia Yasini alikuwa na ukubwa wa
mbuzi lakini kichwa chake kilikuwa cha
binadamu. Hakuwa na la kufanya zaidi ya
kusubiria kifo. Aliwakumbuka sana wazazi
wake, akatamani wangeshuhudia kifo chake
lakini haikuwa hivyo alikuwa anakufa
pekeyake. Yule paka mtu alianza kucheka kwa
dharau kisha akamsemesha yasini.
“unajifanya unajua kukimbia sio?.....
kimbia
sasa” alizungumza yule paka
mtu...
“siwezi kuwakimbia kwasababu siwaogopi.
Ninamuogopa Mungu pekeyake” Yasini alijibu
kwa
jazba
akiamini kuwa hata kama akiwa mpole
hawezi
kupona, ni lazima angekufa tu. Majibu
ya
Yasini yalimchukiza sana Paka mtu.
“unajifanya unakiburi sio?”
“sijui”
“sasa
subiri.....utakiona chamoto” wakati
Yasini
akisubiri hiko chamoto alichoahidiwa
na
Paka mtu, radi ilipiga na kumfanya Yasini
kufumba macho. Alipofumbua hakuyaamini
macho yake. Alikuwa amesimama nje ya ule
msikiti na wale paka wote wakiwa pembeni
wamekufa. Lakini yule paka mwenye kichwa
cha binadamu alionekana yupo hai ingawa
haliyake ilikuwa mbaya sana huku damu
nyingi zilikuwa zimejaa mwilini mwake.
Alijitutumua na kutoa kauli kwa Yasini.
“bahati yako” baada ya maneno hayo yeye
pamoja na wale wenzie waliokuwa wamelala
pale chini wakatoweka. Yasini alibaki
ameduwaa asijue nini kinaendelea maeneo
yale. Hakuwa anajua baada ya pale
angeelekea wapi.
Alikuja njiwa mweupe na kutua begani mwa
Yasini. Alipogeuza shingo kumtazama yule
njiwa alikimbia. Alimtazama alivyokuwa
akipaa hadi alipotua kwenye tawi la mti
mrefu
uliokuwa jirani na pale
alipokuwa
amesimama. Alishusha macho yake
na
kuangalia pande zote kuhakikisha
usalama
wake kisha akayarudisha juu ya
mti
kumuangalia tena yule njiwa.
Alimuona
msichana amesimama kwenye lile
tawi
alilokuwa ametua njiwa. Moyo
ukampasuka na
kuhisi kuwa tayari kituko
kingine kilikuwa
kikimkaribia. Lakini
alipomtazama vizuri
alibaini kuwa alikuwa
ni Husna. Matumaini ya
kuendelea kuishi
yalimrejea tena kwani alijua
jinsi Husna
alivyokuwa na uwezo wa
kupambana na vituko
kama vile. Akanyoosha
mkono na kumuita aje
kumpa msaada.
“Husna njoo mpenzi nahitaji
msaada wako”
alisema Yasini huku ameinua
mkono kumtaka
Husna ateremke. Husna aliinua
mikono yake
na kupaa hadi pale alipokuwa
amesimama
Yasini.
“pole sana Yasini nimesikia kilio chako,
upo
salama sasa hakuna tena
kitakachokusumb
ua” alisema maneno hayo
Husna huku
amemshika Yasini
mabegani.
“samahani sana kwa kuchelewa
kukupokea.
Nilipata dharura” alisema
Husna
“kwani vipi Husna mbona
sielewi
kinachoendelea?”
“usijali, najua huu mji huufahamu kwasababu
hujawahi kufika. Sasa inabidi nikufahamishe
upo
wapi na
umekuja kufanya nini” aliongea
Husna huku
akiwa bado amemshika Yasini
mabegani.
Yasini alimtazama Husna usoni na
kisha
akameza funda la mate. Alikuwa na
hamu
kubwa ya kutaka kujua kilichokuwa
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kikiendelea. Husna alivuta pumzi na kuzutoa
nje kwa nguvu.
@*@*@
Dr.Kisonoko alibaki ndani ya shimo kwa
takribani nusu saa. Wakati huo maji nayo
yalikuwa yameshaanza kuingia kutokana na
chemchem za maji ya bahari. Alitoka na
kuwataka vijana wake kufukia shimo
lililokuwa na kondoo ndani yake. Vijana
walifanya kama walivyoagizwa. Kondoo
walikuwa wakilia sana wakitamani msaada
likini hakuna aliyewajali. Baada ya dakika
kadhaa walikuwa wamekwisha maliza.
Walirudi ndani na kuelekea moja kwa moja
chumbani kwa mganga, Dr. aliwaamuru mzee
Angu na mkewake wakae chini na kunyoosha
miguu. Alitoa nyembe na kuanza kuwachanja
chale katika sehemu mbalimbali za miili
yao.
Alichukua dawa kutoka kwenye moja
ya
vibuyu vyake na kuwapaka kwenye
majeraha
aliyochanja kwa nyembe. Alifungua
kibuyu
kingine na kutoa asali
iliyokuwa
imechanganywa na dawa zake
kisha
akawarambisha wote pamoja na
wasaidizi
wake. Alikamata pembe kubwa la
mnyama na
kumuwekea mzee Angumbisye miguuni
na
kichwani akamuwekea kibuyu
kikubwa
kilichokuwa kimevishwa ngozi ya
myama na
kuzungushiwa shanga. Alianza
kugongagonga
mfuniko wa kibuyu kile huku
akiongea
maneno ya kiganga. Alipomaliza
alihamia kwa
mama Nyamizi na kufanya kama
alivyofanya
kwa mzee Angumbisye.
Hali ya hewa huko nje tayari ilikuwa shwari
kabisa. Radi na upepo vilikoma, na kiza pia
kilikuwa kimetoweka. Dr.Kisonoko aliwataka
mzee Angu na mkewake wakajiandae kwa
safari ya kuelekea GAMBUSHI. Mganga
akawaambia kuwa kuanzi saa ile
hawakutakiwa kuonesha mshangao kwa
chochote ambacho wangekiona. Na endapo
wangevunja sharti basi wasingefanikiwa
katika safari yao.
Kila mmoja akilini mwake aliamini kuwa wapo
mjini Tanga, hivyo safari yao ingeanzia
kwenye stendi ya mkoa wa Tanga na kuelekea
mjini Shinyanga kwa mara ya pili. Kitu cha
kustaajabisha ni pale walipofika nje,
walikuwa
kwenye ile hoteli ya STAFF INN
HOTELL ya
mjini Shinyanga ambayo walifikia
siku
iliyopita. Kama maagizo ya mganga,
hakuna
aliyeonesha wazi kuwa hali ile
imemshangaza.
Wakaelekea kwenye kituo cha
daladala
zilizokuwa zikielekea Mchangani.
Kama
yalivyokuwa maagizo ya kikongwe,
Dr.
kisonoko alitangulia na basi la
kwanza,
wakafuatia wafuasi wake, na basi la
mwisho
walipakia mzee Angumbisye na
mkewake.
Mzee Angu na mkewake walipofika
Mchangani
walichukua vijana wawili ambao
waliwapeleka
kwa baiskeli kutokana na
kukosekana kwa
usafiri wa magari kuelekea
kwenye kijiji cha
Gambushi. Wale vijana
waliwapeleka lakini
walipofika kwenye eneo
lililofahamika kama
kikomo, wakagoma
kuendelea na safari.
Wakasema kuwa huko
mbele hakukuwa mahali
salama, kwani ni watu
wachache sana ambao
wakienda huko hurudi,
wengi wao hupotelea
hukohuko.
Mzee Angu na mkewake walianza kupiga
mwendo kwa miguu. Walitembea sana lakini
hawakuona dalili yoyote ya kufika.
Ilipotimia
mida ya saa tatu usiku walikuwa
wamefika
sehemu moja iliyokuwa na mbuga.
Kwakuwa
hakukuwa na mti ambao wangepanda
na
kulala kwa usalama wakatafuta kichaka
na
kujilaza hapo huku kila mmoja
akionekana
amechoka kupita
kawaida.
Kwambali waliona kama taa za gari
lilikuwa
likielekea kule walikokuwa wao.
Walishituka
na kusimama kuhakikisha kama
kweli lilikuwa
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ni gari au ni macho ya mnyama. Hata hivyo
mgurumo uliashiria wazi kuwa lilikuwa ni
gari.
Walijificha huku wakiliangalia kwa
makini,
lakini lilipofika karibu wakabaini
kuwa lilikuwa
ni basi la abiria. Hivyo
walijitokeza na
kulisimamisha. Lile basi
liliposimama taa za
ndani ziliwashwa. Hapo
watu wengi waliokaa
kama abiria walionekana
vizuri jambo ambalo
lilizidi kuwatia nguvu
na kuwatoa wasiwasi
mzee Angumbisye na
mkewake mama
Nyamizi.
“vipi jamani mnakwenda?” ilikuwa ni sauti
ya
kijana mmoja aliyekuwa amesimama
mlangoni
kama utingo.
“mnaelekea wapi?” mzee Angumbisye alihoji
“Gambushi”
“Ndio
tunakwenda” alijibu mzee Angumbisye
na
kuingia kwenye basi pamoja na mke
wake.
Walipofika ndani ya basi kulikuwa
kumebaki
viti viwili tu ambavyo havikuwa
pamoja.
Kimoja kilikuwa mbele na kingine
kilikuwa
nyuma. Mzee Angu aliketi na mtu
mmoja
ambaye alikuwa ni mzee sana, wakati
mama
Nyamizi naye alikuwa amekaa na
mwanamke
ajuza. Mzee Angu alimsalimia yule
babu
kikongwe lakini hakuitikiwa. Vivyo hivyo
kwa mama Nyamizi naye alimsalimia yule
Ajuza lakini naye hakuitika salamu yake.
Gari ilipoanza safari, taa za ndani
zikazimwa.
Ndani ya gari kulikuwa kimya
mno.
Hapakuwepo na mtu hata mmoja
aliyezungumza na mwenzie. Mama Nyamizi
na mumewake hakuna aliyepata usingizi kati
yao. Wote walizama kwenye dimbwi la
mawazo juu ya mtoto wao na jinsi
atakavyookolewa kutoka kwenye mikono ya
huyo jini hatari.
Gari liliendelea kuchanja mbuga kwa mwendo
wa kawaida. Ilikamata njia iliyokuwa na
mitimiti na kuiacha mbuga. Kila waliposonga
mbele miti iliongezeka na hatimaye
wakajikuta
wamo kwenye msitu mnene. Dereva
wa gari
alisimamisha na kuwa sha taa za
ndani. Sauti
ya utingo ilisikika ikiwataka
abiria
wakachimbe dawa. Mzee angu
alipomtazama
vizuri yule mzee aliyekaanae
hakuweza
kuamini. Alikuwa amekaa siti moja
na fisi.
Aliinuka na kujifanya anakwenda
kujisaidia
lakini alipofika kwenye siti
aliyokuwa ameketi
mke wake akazidi
kuchanganyikiwa. Mkewake
alikuwa amesinzia
huku naye akiwa ameketi
na fisi. Alitaka
kumuamsha lkini yule fisi
alimtazama usoni
na kufunua mdomo wake
kama vile anataka
kumng’ata……
Mzee Angu alitupa macho kwa mkewake na kumkuta bado amesinzia, lakini yule fisi hakuwepo bali alikuwa amekaa yule mwanamke mzee. Ajuza yule alimtazama mzee angu usoni kwa macho makali kisha akamsonya. Aliporudi kwenye siti yake alimkuta yule mzee naye amebadilika na kuwa binadamu. Aliketi lakini akili haikumtulia kabisa. Mawazo yake yote yalikuwa kwa mkewake ambaye muda wote alikuwa amelala fofofo. Akili ilimtuma kumchukua mkewake na kuteremka nae. Hivyo akajikuta anapaza sauti.
“kondaaaa?” dereva aliposikia sauti ya mzee Angumbisye aliwasha taa za ndani.
“tushushe hapo hapo tumefika” abiria wote waligeuza shingo na kumtazama kisha kwa pamoja
wakaguna. Mzee Angu hakujali miguno yao, alikwenda mojakwamoja hadi kwenye kiti alichokaa mkewake na kumkuta ameamka. Gari liliegeshwa chini ya mti mmoja mkubwa.
“vipi baba Nyamizi inamana tumefika?” alihoji mama nyamizi
“ndio”
“lakini mbona hapa ni porini?”
“Wacha ubishi mkewangu. Tuteremke” alisisitiza mzee Angu na kumshika mkono mkewake.
“unadai shilingi ngapi?” alihoji mzee Angu mara baada ya kufika nje. Hata hivyo utingo wa gari
hakujibu kitu zaidi ya kuingia kwenye gari na kuwatimulia vumbi pale chini. Mzee Angu alipumua kwa nguvu kwani hakuamini kama amefanikiwa kuwatoka wale fisi watu ndani ya gari. Lakini lile gari lilipoondoka tu ule msitu nao ukatoweka na kujikuta wamesimama palepale mbugani walipopandia gari. Hali ile iliwafanya washangae na kusahau masharti ya mganga Kisonoko. Walikuwa wamekwishachoshwa na vituko vya hapa na pale. Wakatafuta sehemu na kujilaza pale mbugani na kausingizi kakawapitia.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Sauti za paka ziliwagutusha kutoka usingizini. Walipoinua macho wakajikuta wamezunguukwa na kundi kubwa la paka. Paka wale walikuwa weusi na macho yao yalikuwa yanang’aa mno. Mama nyamizi akamkumbatia mumewake kwa woga. Wale paka walianza kuwazunguuka huku wakilia kwa sauti za watoto wachanga. Mara wakaungana na kutokea paka mmoja mkubwa sana. Paka yule alikuwa anatisha kuliko mnyama yoyote mkali. Alikuwa akiunguruma kwa sauti kali na nzito. Mwisho alitoa kicheko na kutoweka kwenye mazingira yale.
Ilipofika asubuhi mama Nyamizi alimsihi mumewake warudi mjini Tanga lakini mzee yule hakuwa tayari, hivyo waliendelea na safari yao kuelekea GAMBUSHI. Waliiacha mbuga na kuingia kwenye msitu wenye miti mirefu na mikubwa. Kwa mbali waliwaona wanawake watatu wakitembea tembea mle msituni. Wanawake wale walikuwa wamejifunga kaniki tumboni na matiti yao yalikuwa wazi. Mzee Angumbisye na mkewake wakaongeza mwendo hadi walipowafikia wale wanawake.
“ habari zenu kina mama” mzee angu aliwasalimia.
“salama baba shikamoo”
“marahaba”
“mnatafuta nini kwenye msitu hatari kama huu” alihoji msichana mmoja
“tunakwenda Gambushi”
“Gambushi…?”
“ndio”
“mnakwenda kutafuta nini kwenye kijiji cha kutisha na chenye hatari?”
“tumeongozana na mganga wetu. Lakini yeye ametangulia”
“anaitwa nani huyo mganga wenu?”
“ Dr. kisonoko”
“Dr Kisonoko!... yule mganga wa Pangani?”
“ndiye huyohuyo” mzee Angu alijibu na kuwafanya wale wanawake watazamane kwa mshangao.
“Dr. Kisonoko pamoja na wafuasi wake wote watatu wamefariki” aliongea msichana mmoja kwa
sauti iliyojaa masikitiko.
“wamekufa!...?” mama Nyamizi na mumewake walihamaki.
“ndio wamefarik, tena usiku wa kuamkia leo”
“mungu wangu…!” mama Nyamizi alidondoka chini na kupoteza fahamu
“kwani mna matatizo gani?”
“tumempoteza mtoto wetu. Mganga amesema huku ndiko tunaweza kumpata kiurahisi”
“Hakuna jambo kama hilo wazee wangu. Dr. Kisonoko hana uwezo wa kwenda kuzimu na kurudi. Alikuwa analazimisha tu, na hilo ndilo lililompoteza”.
“ninyi hayo yote mmeyajuaje?”
“sisi tunaishi huko”
“sasa humu msituni mnatafuta nini”
“tumetoroka”
‘kwanini?”
“sisi ni misukule”
“ina maana huko Gambushi wanaishi wachawi?”
“maswali yako ni mengi mno mzee na hayana msingi. Mnachotakiwa kukijua ni namna ya kuondoka maeneo haya” alidakia mwanamke mmoja aliyeonesha kukerwa na maswali ya Mzee Angumbisye.
“sawa tunahitaji msaada wenu”
“hakuna wa kutatua tatizo lenu zaidi ya Mwenyezu Mungu. Rudini Nyumbani na mtafute viongozi wa dini watawasaidia” alisema yule mwanamke.
Wakati huo mama Nyamizi alikuwa amekwishazinduka na kurejewa na fahamu hivyo aliweza kuyasikia kwa makini maneno ya wale wanawake.
“tutawapa dawa itakayowafikisha muendako kwa usalamat” aliongea yule mama na kufungua fundo lililokuwa kwenye nchaa ya kaniki yake. Alitoa ungaunga mweusi na kumkabidhi mzee Angumbisye. Mtajipaka dawa hii usoni huku mkitaja jina la sehemu mnakokwenda. Adui akitaka kuwadhuru hataweza kuwaona hivyo mtafika kwa usalama.
“tunaweza kujipaka sasahivi?” alihoji mzee Angumbisye.
“ndio, fanyeni hivyo sasahivi” alisema yule mwanamke kwa msisitizo. Mzee Angu na mkewake walijipaka ile dawa usoni, lakini walipomaliza walishangaa kuona wale wanawake wakiangua kicheko huku wakigongeana mikono kuashilia hali ya ushindi.....
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kitendo kile kiliwatia mashaka sana mzee angu na kewake, wakahisi wamenaswa na mtego wa watu wa Gambushi.
“mnaweza kujaribu kwenda juu ya ule mti” mwanamke mwengine aliwaambia.
Kwa wasiwasi mzee Angumbisye alimshika mkewake mkono na kutamka kama walivyoelekezwa na punde wakajikuta wapo juu ya ule mti mrefu. Walipokuwa kwenye ule mti waliweza kuona kila upande wa msitu. Kwa mbali waliweza kukiona kijiji cha Gambushi. Kulikuwa na watu wengi na wote walionekana kushughulika. Hapakuwepo na hata mmoja aliyekuwa amekaa kizembe. Pia kuna watu walikuwa wakicheza ngoma huku wakiwa uchi. Mzee Angu aliamuru warudi pale walipokuwa wale wanawake.
“hiyo dawa ni kiboko” alisema mwanamke mmoja
“mmeipata wapi?” alihoji mzee Angumbisye.
“Ilidondoshwa na wachawi” mwanamke mmoja alijibu.
Mara wakasikia sauti ya kitu kikivuma mle msituni. Kila sekunde ilipopotea ile sauti iliongezeka na kuelekea pale walipokuwa wamesimama. Wote watanao wakapaa hadi pale kwenye ule mti mkubwa. Waliweza kuona kundi kubwa la wachawi waliokuwa uchi likipaa kwa nyungo kuelekea kule msituni. Walifika kwa mwendo wa kasi na kutua pale walipokuwa wamesimama mwanzo kina mzee Angumbisye na wanawake.
Wachawi wale walitoka kwenye nyungo zao na kuonekana kama vile wanatafuta kitu. Walizunguka kila upande lakini walionekana kukosa walichokuwa wakikitafuta. Mchawi moja alisimama na kuangalia juu ya ule mti mrefu waliokuwa wamekaa wakina mzee Angumbisye na wale wanawake watatu. Alitazama kwa muda mrefu na kutingisha kichwa kama vile kuna kitu amekiona. Akapanda ungo wake na kupaa kuelekea juu ya ule mti.
“mungu wangu tumekwisha!” alihamaki mzee Angumbisye
“shiiiii!!” mwanamke mmoja akamnyamazisha.
Mzee Angumbisye alipomtazama mchawi yule alibaini kuwa tayari amewaona. Mchawi yule alifika na kutua kwenye lilelile tawi walilokuwa wamesimama. Taratiibu akaanza kuwasogelea. Mwanamke mmoja akawaonya mzee Angumbisye na mkewake wasizungumze wala kutikisika. Mchawi alifika na kumshika mzee Angumbisye begani na kumuegemea kama vile ameegemea tawi la mti.mzee Angumbisye alipomtazama kwa makini akabaini kuwa anamfahamu vizuri sana yule mchawi. Walikuwa wanaishi naye mtaa mmoja Muheza.
Yule mchawi alipuliza firimbi na mara wale wachawi wengine nao wakaanza kupaa kuelekea kule kwenye ule mti. Walifika na kuuzunguka mti ule mara kadhaa kabla ya kutua kwenye matawi. Walikuwa ni wengi mno kiasi cha kuonekana kama ndenge aina ya kwereakwerea. Mama nyamizi alikuwa amemkumbatia mama mmoja kati ya wale wanawake watatu. Alikuwa akitetemeka na kijasho chembamba kikimvuja. Alianza kuujutia uamuzi wao wa kumpeleka binti yao kwa mganga wa kienyeji. Wale wachawi walikuwa wanamtishia mno, kila alipomtazama yule aliyemuegemea mumewake alizidi kuchanganyikiwa.
@*@*@
Yasini alimeza funda la mate na kumtazama Husna usoni. Alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kufahamu kilichokuwa kikiendelea. Husna nae alivuta pumzi kwa nguvu na kuzitoa
“Yasini hapa ulipo ni KUZIMU”
“kuzimu!.. sasa mimi nafanya nini hapa Kuzimu?”
“umekuja kwa lengo la kuwaona wazazi wangu”
“inamaana wazazi wako wanaishi kuzimu?”
“ndio”
“kwanini?”
“ndiko kwetu”. Husna alijibu na kumfnya Yasini kubaki ameduwaa.
Aliinua macho yake na kumtazama tena Husna kwa makini. Kiukweli ni kwamba alikuwa akimpenda sana lakini matendo yake ndiyo yaliyokuwa yakimchanganya. Hata hivyo alikumbuka kuwa yaleyale matendo ya ajabu ya Husna ndiyo yaliyomfanya amalize elimu yake ya sekondari. Hivyo hakuona sababu ya kumchukia binti yule.
Husna alimshika Yasini mkono wa kushoto na kuanza kupaa nae angani kama tai huku Husna akiwa amenyoosha mkono wake wa kushoto juu. Baada ya dakika kadhaa alinyoosha mkono kuelekea chini na kusababisha waanze kutua. Walitua nje ya nyumba kubwa sana iliyokuwa na geti jeusi. Walipofika tu geti lilifunguliwa na msichana.
“karibu Yasini. Hapa ndipo ninapoishi” alisema Husna.
“ahsante sana” Yasini aliitikia na kuingia ndani. Lakini alipomtazama kwa makini yule msichana aliyewafungulia geti, akabaini kuwa alikuwa akimfahamu vizuri sana. Alisimama na kutaka mkumsemesha lakini Husna alimkatisha na kumvuta mkono kuelekea ndani. Walifika na kuketi sebuleni. Pale alipokuwa amekaa Yasini, aliweza kuona milango ya vyumba vyote vya ile nyumba.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Yule msichana aliyefungua geti alifika na vinywaji na kuwakaribisha Husna na Yasini. Yasini alikuwa akimtazama sana yule binti. Alionekana amechoka sana kutokana na kazi ngumu alizokuwa akizifanya. Yasini akataka kuuliza kitu lakini Husna aliweka kidole mdomoni kumuonya asiongee kitu. Yule msichana akatoka nje na kuwaacha Husna na Yasini pale sebleni. Lakini baada ya dakika kadhaa alirejea tena.
“dada maji ya kuoga tayari” sauti ya yule binti ilisikika na kumfanya yasini kuzidi kuwa na uhakika wa kumfahamu.
“twende tukakoge mpenzi” alisema Husna na kumshika mkono Yasini kuelekea bafuni. Baada ya kumaliza, Husna alimtia yasini mgongoni na kumpeleka chumbani ambapo alifika na kumuweka kitandani. Baada ya kumfuta maji, alifungua kabati na kutoa shati na suruali. Kama mtoto mdogo Yasini alivishwa zile nguo.
“Husna hao wazazi wako wakowapi?” Yasini alihoji huku akimtazama Husna ambaye alikuwa akichana nywele....
Huasna aligeuka na kuketi pale kitandani na yasini.
“Sikiliza mpenzi, wazazi wangu wanaishi kwenye nyumba nyingine mbali na hapa”
“inamaana hapa unaishi pekeyako?”
“ndiyo, hii ni nyumba yangu, lakini tukifunga ndoa tutakwenda kuishi pamoja Duniani” Yasini alitulia na kutazama huku na kule mle chumbani. Hakuweza kuamini kama Husna angeweza kumiliki nyumba ya kifahari kama ile. Ghafla akapata wazo la kuuliza juu ya yule msichana aliyekuwa akiwahudumia tangu wamefika.
“hivi huyu msichana anayetuhudumia ni nani?”
“wacha maswali ya mtego bwanaaa. Inamana humjui Nyamizi wewe?”
“Nyamizi!.... sasa hapa anafanya nini?”
“ni kijakazi wangu”
“kwanini sasa unafanya vitu vya kinyama kama hivi?”
“Wamenianza, namimi nimewamaliza”
“inamaana hukuwa na njia nyingine ya kufanya hadi umeamua hivi”
“vipi, unampenda sana mchumbaako?” Husna alihoji kwa hasira kidogo
“hata kama, lakini huu sio ubinadamu”
“sikiliza Yasini. Hawa walitaka kuniua lakini nimewawahi. Hii ni adhabu ndogo sana niliyowachagulia”
“inamaana sio suala la kutaka kuolewa na mimi?”
“hilo lilikwisha malizika. Lakini wakajipendekeza kwangu”
“wako wangapi?”
“wako wawili lakini mwenzie yupo kwa wazazi wangu anawatumikia huko”
“na yeye ni nani?”
“yeye ni msaidizi wa mganga aliyetaka kuniua”
Husna alimueleza Yasini kuwa kichaa alichokipata Nyamizi siku ya harusi kilikuwa kimesababishwa na yeye. Alisema kuwa baada ya kumsababishia yale wazazi wake wakampeleka kwa mganga wa kienyeji. Mganga alipomaliza kumponya, akataka kuja kupambana naye, lakini Husna alipata taarifa zile kupita kwa wazazi wake ambao walikuwa na uwezo kuliko yeye. Husna aliwafuata na kuanza kupambananao lakini kwa bahati mbaya mganga alifanikiwa kukimbia na kuwaacha wenzake. Hapo ndipo alipoamua kumchukua Nyamizi pamoja na msaidizi mmoja wa mganga na kuwapeleka Kuzimu kuwa vijakazi.
“kwahiyo nilipoingia hapa hakunifahamu?”
“kwanini asikufahamu wakti wewe ni mumewake. Ameniogopa mimi lakini angekusemesha”
“kwanini anakuogopa?”
“kwasababu ni adui yake”
“inaonekana unamtesa sana?”
“zaidi ya sana. Tena anastaili kifo na sio hii niliyompa”
“mnh!”
“vipi mbona unagumia?”
“ah! Hamna kitu”.
walibaki chumbani hadi mida ya saa mbili za usiku ndipo walipotoka na kukuta Nyamizi amekwishaandaa chakula cha usiku.
“Karibu chakula mpenzi wangu”
“ahsante sana mkewangu” alijibu Yasini na kufanya wote kutabasamu. Walikula huku wakiongea hili na lile. Walipomaliza hawakutaka kupoteza muda, walirudi chumbani kujipumnzisha.
“Husna” Yasini aliita
“sema mpenzi”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“unaweza kunipa siri ya maisha yako?”
“siri gani?”
“najua wewe sio binadamu wa kawaida. Nataka kujua ni kwanini upo tofauti”
“mbona una haraka sana. Mimi nipo na utanijua tu”
“naomba nikujue sasahivi” alisema Yasini.
Husna alimtazama yasini kwa kitambo kisha akaanza kumwagika. Alimueleza kuwa yeye ni binadamu wa kawaida kama walivyo binadamu wengine. Alisema yeye ni mtoto wa mwisho katika familia yenye watoto watatu. Kipindi mama yake anaujauzito wake, baba yake alimtishia kumuua yeye na mtoto endapo angemzalia mtoto wa kike. Kwa bahati mbaya ama nzuri mama yake alijifungua mtoto wa kike. Alipoona vile alimchukua mtoto na kwenda kumficha kwenye msitu mmoja uliofahamika kama msitu wa Mauaji ulioko kwenye kijiji cha Mkanyageni. Mtoto yule aliokotwa na majini ambao walikwenda naye kuzimu na kumlea. Mtoto huyoakapewa jina la Husna.
“na huyo Husna ndio mimi”
“kwahiyo unawafahamu wazazi wako?”
“hapana, hadi leo sijawajua. Na ndiomaana huwa napenda sana kuja duniani”
“na kule Kidutani ulikuwa unafuata nini?”
“kule ni kama njia. Kupitia kwenye lile bwawa ni rahisi sana kufika Duniani na kurudi Kuzimu”
“sasa umepata wapi uwezo wa kufanya mambo yasiyo ya kawaida kwa binadamu?” Yasini alihoji.
Husna badala ya kujibu swali, aliinua mkono wake wa kushoto na kumuonesha yasini vidole vyake. Kwenye kidole cha kati kulikuwa na pete ya Shaba. Yasini aliikumbuka ile pete kipindi yupo mwanafunzi na jinsi ilivyomsaidia kumaliza masomo yake.
“hii pete nimepewa na majini walionilea. Ninaweza kufanya jambo lolote kwa kuiamrisha”
“pole sana Husna. Lakini wasamehe wazazi wako”
“nimeshawasamehe na ndiomana nawatafuta nikaishi nao duniani” aliongea Husna na kujikuta akilia kwa kwikwi. Yasini alimbembeleza na kumtaka alale apumzishe mawazo. Hadi kufikia saa tano usiku wote walikuwa wamekwishalala fofofo.
Yasini alishituliwa na ubaridi mkali uliokuwa ukitembea mwilini mwake. Alipoinua macho alimkuta mtu mnene aliyekuwa anawakawaka mwilini mwake. Mtu yule alisogea nyuma hatua kadhaa baada ya kubaini kuwa Yasini ameamka. Mtu yule alikuwa akitoa nje ulimi wake mrefu ambao ulikuwa ukiwaka moto. Macho yake matatu yaliyokuwa yakiwaka kama tochi hayakufumba hata kwa sekunde moja. Yasini alitaka kumuamsha Husna lakini akabaini kuwa alikuwa pekeyake, Husna hakuwepo kitandani.......
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment