Search This Blog

NYAYO ZA DAMU - 3

 







    Simulizi : Nyayo Za Damu

    Sehemu Ya Tatu (3)





    Alijilaumu kwa kushindwa kuwa msikivu na matokeo yake kuishi kama nguruwe tena kwenye banda chafu lisilostahili mwanadamu kuishi. Alijiuliza ataishi vile mpaka lini na kukumbuka kauli ya Nargis ya yeye kuchinjwa mwishoni mwa wiki akichanganywa na nguruwe wengine.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


    Kufika hapo alilia huku sauti yake ikiwa kero masikioni mwa watu kutokana na kusikika zaidi kutokana na hali ya hewa ya usiku kuwa imetulia. Ubaridi wa usiku nao uliendelea kumtesa kwa kumpiga bila huruma.


    Njaa na kiu baada ya kumshika sana na kumfanya aanze kuona kizunguzungu na kiza kinene. Miguu haikuwa na nguvu alijilaza kwenye tope huku baridi likizidi kumuingia mwilini. Kila dakika alimuomba Mungu amchukue kwani mateso yalikuwa makubwa sana maishani mwake.


    Sehemu chafu inanuka asiyostahili mwanadamu kuwepo, njaa kali na kiu hakuna chakula zaidi ya chakula kichafu cha nguruwe wale. Akiwa amejikatia tamaa alishtuka kujiona ametolewa nje ya banda akiwa katika umbile lake halisi la kibinadamu.


    Alishangaa na kujiuliza nani aliyemtoa na hali ile ni kweli au ni kiini macho, kabla hajapata jibu alimuona Nargis amesimama mbele yake. Mke wa Sule alichanganyikiwa na kuamini ile ni nafasi pekee ya kuomba msamaha, alipiga magoti mbele ya Nargis.


    “Nargis najua nimekosa naomba unisamehe.”
    “Mariamu sicho kilichonileta, nimekuletea chakula na maji kwa kujua huwezi kula chakula na maji yake ya nguruwe.”


    “Ni kweli Nargis nateseka mwenzio naomba unisamehe sirudii tena,” Mke wa Sule aliomba msamaha akiwa amepiga magoti huku akilia kilio cha majuto.


    “Mariamu kuwa muelewa, sikufuata ujinga wako bali nimekuletea chakula usife na njaa na utakuwa ukila mara moja kwa siku mpaka siku utakayochinjwa na nyama yako kuliwa na watu,” Nargis alisema kwa sauti isiyo na mzaha hata kidogo.


    “Nargis najua kiasi gani nimekukosea, nipo chini ya miguu yako sitarudia tena.”
    “Mariamu wewe si wa kusamehewa na ukizidi kuniudhi nitaongeza mateso ya kuutia madonda mwilini wako na kukufanya utolewe kwenye banda na kukufanya utangetange kwa kupigwa mawe kila atakapo kimbilia na kifo chato kitatokana na kipigo cha wanadamu.”


    “Usifanye hivyo Nargis, nakuahidi siwezi kurudia na nikirudia nifanye lolote.”
    “Kama uliweza kutaka kuniangamiza na dawa ulibeba pamoja na kukutisha kila kona bado dhamila yako ya kuniangamiza ilikuwa pale pale. Wewe ni kenge huwezi kusikia mpaka utoke damu masikioni.”
    “Basi niue kabisa kuliko kunitesa hivi.”


    “Sina uwezo huo ndio maana kifo chako kitakuwa cha kupigwa na kuzilai kisha utachinjwa.”
    “Na leo sikuachi mpaka uniue nifanye lolote sikuachi,” mke wa Sule alijitutumua.
    “Kabla hujanigusa nitakutengeneza kiumbe wa ambabu afadhari nguruwe, kwanza usinipotezee muda wangu kula chakula niondoke zangu.”


    Mke wa Sule kutokana na njaa aliyokuwa nayo hakuona umuhimu wa kubishana zaidi ya kukishambulia kile chakula kilichokuwa kitamu na maji matamu ambayo hakuwahi kula na kunywa maishani mwake. Baada ya chakula hakujua Nargis amepanga kumfanya nini, baada ya kula alimshukuru Nargis ambaye hakuihitahi shukurani ya kinafiki.
    “Sina haja ya shukurani zako mwanaume shetani usiye na huruma.”
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Hapana Nargis ni mawazi mabaya ya kuamini majini ni viumbe vibaya lakini wewe umeonesha kumbe ni viumbe wapole na wenye huruma. Nimejifunza kupitia kwako nisamehe usinifanye kitu chochote kibaya mateso ya muda mfupi nimetamani kufa lakini sikuwa na uwezo huo.


    Chonde Nargis usinitese tena inatosha Nargis nateseka kumbuka mimi ni mwanadamu sifai kukaa na wanyama tena wachafu kama nguruwe.”


    “Nimekuleta huku na maana yangu, wewe si ulikuwa ukitafuta maji na mifupa ya nguruwe ili uniangamize nimeamua nikulete kabisa ukae nao ili uweze kuniteketeza vizuri”
    “Nisamehe Nargis ni shetani tu kanipitia nipo chini ya miguu yako.”




    “Nafikiri umeshiba, rudi katika umbile lako la kinguruwe ili urudi kwa wenzako, naona unanipotezea muda sicho kilichonileta. Nimekusamehe husameheki, nimekutisha hutishiki, bado unaitaka roho yangu bado unaomba nikusamehe.


    Nargis baada ya kusema vile alinyooshea kidole mke wa Sule ambaye kabla hajasema kitu alibadilika na kuwa nguruwe na kurudishwa kwa nguruwe wenzake.


    Mke wa Sule alipojaribu kumuomba msamaha lakini alitoa mlio wa nguruwe, hakuwa na jinsi zaidi ya kunyamaza kimya.


    Sule alichanganyikiwa baada ya mkewe kutoonekana kwa siku tano, wasi wasi wake mkubwa ulikuwa kwa Nargis mpenzi wa Thabit lakini alishindwa kutibitisha kuwa Nargis ndiye chanzo cha matatizo ya mkewe kwa vile hakuwa na ushahidi japo aliamini hivyo.
    Na aliogopa kumuuliza Thabit kwa kuwa ataulizwa ilianzaanzaje mpaka kufikia hatua ile. Wazo la haraka lilikuwa kwenda kwa mtaalamu wa tiba za asili mwenye uwezo wa kushindana na majini ili kujua mkewe siku tano alikuwa wapi. Kama siku tatu alizopotea alikuwa Morogoro kwa kutembea kwa miguu baada ya kukutana na Nargis.


    Siku aliyopanga kwenda kwa mganga ilikuwa ndiyo siku baadhi ya nguruwe kuchinjwa kwenye banda alilomo mke wake. Mke wa Sule aliendelea kuteseka kuishi maisha magumu na nguruwe katika banda moja na kula mara moja kwa siku.
    Siku hiyo ilipofika aliingia mtu bandani na kuhesabu nguruwe wa kwenda kuchinjwa na mke wa Sule alikuwa katika idadi ile. Walipakiwa kwenye gari kupelekwa sehemu ya kuchinjia, mke wa Sule alitamani atoe sauti kuwa yeye si nguruwe lakini kila alipotoa sauti ilitoka ya nguruwe.
    Sule naye alidamka asubuhi kuwahi kwa mtaalamu ambaye hakuwa mbali alikuwa Mtoni kwa Azizi Ali. Kwa kuwa mganga huwa na watu wengi alipandia gari Buguruni-Chama.


    Ilikuwa ajabu ya Mungu alipotelemka alijikuta yupo Kisarawe mkoa wa Pwani, hakuamini kwani alipanda daladala iliyopigwa debe Buguruni Mtoni-Mtongani. Ilibidi apande daladala nyingine iliyokuwa ikirudi mjini.
    Baada ya kupanda daladala alitulia kitini akiwa haamini kama kweli alipanda gari la kuelekea Kisarawe na si Mtoni kwa Azizi Ali. Baada ya muda gari lilirudi mjini ili aelekee Buguruni kwa mganga kuulizia habari za mkewe. Gari lilirudi hadi Buguruni ambako Sule alipanda gari liendalo Mtoni kwa Azizi Ali.


    Gari lilipoanza kuondoka alipitiwa na usingizi mzito mpaka linafika mwisho wa safari Mtoni Mtongani alikuwa bado amelala. Kutokana na ugumu wa usafiri gari lilipofika abiria waliwahi kuingia na kukaa kwenye siti, hakuna aliyejua kama Sule alitoka na daladala ile Buguruni.
    Safari ilianza tena kuelekea Buguruni, Sule alishtuliwa na konda kumdai pesa.
    “Mzee acha kulala nipe nauli.”
    “Mara ngapi?”
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Mzee sijadai nauli kwa mtu yoyote toka abiria waingie.”
    “Kaka si nimekupa mia tano ukanirudishia mia mbili na hamsini muda mfupi uliopita?”
    “Mzee wangu sijachukua hata senti ya mtu.”
    Mara konda alitoa shingo nje kuita abiria baada ya daladala kusimama Vetenari kwa kupaza sauti.
    “Buguruni mia mbili,” kauli ile ilimshtua Sule na kuhoji.
    “Konda tunatoka Buguruni au tunarudi Buguruni?”
    “Mzee tunatoka Mtoni tunakwenda Buguruni.”


    “Mungu wangu ina maana gari mpaka linafika na kurudi mimi nilikuwa nimepitiwa na usingizi?”
    “Kwani ulikuwa unakwenda wapi?” abiria mwenzake aliyekuwa pembeni yake alimuuliza.
    “Mtoni kwa Azizi Ali na nilipandia Buguruni, ajabu usingizi wa ajabu ulinipitia na kujikuta narudi nilipotoka.”
    “Ooh, pole unaweza kushukia hapa ili upande gari lingine.”
    Sule alitelemkia Vetenari kwa hasira ya kupotea na gari mara mbili aliamua kutembea kwa miguu kwani aliamini kwa njia ya mkato ya kupitia Mwembe Yanga hawezi kuchelewa. Alitembea kwa mwendo wa kasi kuokoa muda, lakini alijikuta akitembea mwendo mrefu bila kufika. Kitu kilichomfanya achoke sana, kingine kilichomshangaza mazingira aliyokutana nayo yalikuwa mageni kwake.


    Sule alitembea mpaka ikafikia hatua akawa haoni anapokwenda kiu ya maji ya kunywa na njaa kali vilimshika na kiza kilianza kuingia. Hakuamini kutoka Vetenari kwa miguu hadi Mtoni kwa Azizi Ali kunaweza kuchukua masaa kumi.
    Alitafuta mti wa mwembe uliokuwa mbele yake na kujipumzisha.
    Hayo yalikuwa kwa Sule, mkewe naye baada ya kuchanganywa katika kundi la nguruwe wa kuchinjwa, walifikishwa kwenye machinjio na kupangwa foleni kwa kuuawa mmoja mmoja. Mke wa Sule alikuwa wa tatu katika nguruwe kumi waliokuwa wakichinjwa siku ile.
    Alishuhudia nguruwe wa kwanza akitandikwa nyundo nzito kichwani na kupoteza fahamu kisha alichinjwa, wa pili ilikuwa vile vile alipokea kipigo kizito na kuchinjwa.


    Ikafuata zamu ya mke wa Sule ambaye haja ndogo na kubwa vilimtoka pamoja na kulia kilio huku akiomba msamaha kuwa yeye si nguruwe bali mwanadamu. Lakini kauli yake hakuna aliyeisikia zaidi ya kutoa mlio wa nguruwe.
    Alisogezwa kwenye sehemu ya shuruba kwa mtoa ufahamu wa nguruwe, aliinua nyundo nzito juu tayari kuishusha kwenye kichwa cha mke wa sule.
    Mke wa Sule alifumba macho kusubiri kipigo kile, lakini kabla nyundo haijashushwa mtu aliingia bila hodi na kusema.
    “Samahani ndugu usimuue huyo nguruwe.”
    “Kwa sababu gani?” mpiga nguruwe aliuliza.
    “Nilikuwa namtaka huyo nguruwe.”
    “Aah, bwana mbona wapo wengi kumbe ni hilo usinipotezee muda.”
    “Huyu ndiye niliyempenda, na nitamnunua kwa kiasi chochote nimempenda kwa kuwa ni jike, kwani mimi ninaye dume msumbufu nikimpelekea jike litapunguza usumbufu pia ninataka nguruwe wengi.”
    “Hakuna tatizo.”


    Mke wa Sule hakuamini kupona katika kifo kile japo aliamini yule atakayemchukua atampeleka katika banda lingine la nguruwe na kumfuga. Kibaya zaidi ni kupandwa na nguruwe dume ili azae watoto ambao yule bwana atatunza kwa ajili ya biashara.
    Mke wa Sule alisogezwa pembeni na kuchukuliwa nguruwe mwingine ambaye alimuona akichukua kipigo kimoja na kutulia. Moyoni alijisemea “Nilikuwa mimi nakutwa na yale, eeh Mungu niepushe na shari hii na nyingine tena.”
    Baada ya yule bwana kulipa pesa alitoka sehemu ya machinjio na nguruwe wake, alimpandisha kwenye gari na kuondoka naye. 
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Wakati akiwa ndani ya gari usingizi mzito ulimpitia mke wa Sule, aliposhtuka alijikuta kwenye umbile la kibinadamu, sehemu iliyokuwa ngeni kwake, ghala harufu ya manukato ya Nargis ilisikika nyumba yake.
    Alipogeuka alimuona akiwa amesimama ameshika mikono yake kwa mbele kwa sauti ya upole alisema.
    “Mariamu.”
    “Abee.”


    “Nina imani baadhi ya viumbe hawajui thamani ya maisha yao na mmoja wapo ni wewe, nilikutoa kwa muda kwenye kifo kile cha kuchinjwa lakini baada ya mazungumzo haya ukinijibu vizuri toka chini ya moyo wako nitakusamehe na kukurudisha kwa mumeo ambaye kutwa nzima hajui anakwenda wapi.


    La utashindwa nitakurudisha kabla nguruwe wale hawajachinjwa na wewe uwe mmoja wapo. Mariamu kipi kinachokukera mimi kuwa na Thabit?”


    “Hakuna basi tu upumbavu.”
    “Upumbavu, roho mbaya?”
    “Roho mbaya.”


    “Shida yako nini kwangu?”
    “Nilikuwa na wasiwasi huenda wewe ni jini.”
    “Baada ya kujua mimi ni jini?”


    “Najua majini ni viumbe wabaya hivyo ungeweza kutudhuru.”
    “Kwa hiyo ukaamua kunidhuru mimi?”
    “Ni kweli nilitaka kufanya hivyo.”


    “Kwa hatua hiyo mwanadamu na majini yupi kiumbe mbaya?”
    ”Mwanadamu.”
    “Mbona mimi sijakudhuru?”


    “Nisamehe Nargis, sirudii tena kumbe ninyi ni viumbe wema sana sikujua.”
    “Sasa sikiliza hili ni onyo la mwisho, kama hutasikia nitajua cha kukufanya ila sitakuwa na simile wala kuuliza zaidi ya kutenda.”


    “Nimekuelewa dada yangu sirudii tena tamu ya ukaidi wangu nimeiona kama nisiposikiliza sitakuwa mwanadamu mwenye akili timamu.”
    “Yangu yameisha rudi nyumbani kwako.” 
    “Asante Nargis”


    “Mariamu sihitaji asante zako za kinafiki zaidi ya kuyatekeleza yote niliyokwambia.”
    “Niamini Nargis huyu ni Mariamu mpya msikivu na nyenyekevu.”
    “Mmh, haya tutaona.”


    Baada ya kauli ile Nargis alipotena na kumuacha mke wa Sule akishangaa yupo wapi na atarudije nyumbani. Baada ya kutuliza akili alijishangaa kujiona yupo nyuma ya nyumba wanayoishi. Alizunguka na kutokea upande wa mbele, alishangaa kukuta mlango wa chumba chao umefungwa.


    Kwa vile alijua funguo wanapoweka alifungua mlango na kuingia ndani, kutokana na uchovu alipitiwa usingizi mzito.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Sule naye alishtuka usingizini saa saba za usikukutokana na mvua kali ya upepo iliyokuwa ikinyesha, alichanganyikiwa asijue pale alipokuwa ni wapi na wapi akimbilie kutokana na kiza kinene na mvua kali. 


    Yalikuwa mateso mazito kwa Sule ambayo hakuwahi kukumbana nayo katika maisha yake. Kingine kilichokuwa kikimchanya ni kilio cha mtoto mdogo mwenye sauti kama ya mtoto wake aliyeonesha naye ananyeshewa na mvua na kuomba msaada wa baba yake.


    Sule alijikuta akitapatapa kuifuata sauti ya mtoto yule ambayo hakujua inatokea wapi. Alijikuta akisahau mateso yake na kuanza kuifuatilia sauti ile kwa kuamini akifanya uzembe wowote mtoto wake anaweza kupoteza maisha kwa mvua ile kali iliyoambatana na upepo mkali.


    Sauti ya mtoto ulizidi kutanda katika ngoma za masikio ya Sule na kumfanya azidi kuifuata ili ajue mwisho wa sauti ile. Alizidi kuifuata ile sauti huku akimuomba Mungu amsaidie amuone mtoto wake akiwa hai.


    Katika kumbukumbu zake alikumbuka aliamka asubuhi kuwahi kwa mganga ili ajue sababu ya kupotea kwa mke wake. Lakini alijikuta akitokewa na mambo ya ajabu ya kupotea kila alipotaka kwenda kwa mganga kitu ambacho hakikuwahi kumtokea toka azaliwe.


    Sauti ya mtoto iliendelea kulia huku akiendelea kuifuata na mvua nayo ilizidi kumpiga huku baridi la usiku nalo likimuingia mpaka kwenye mifupa. Ajabu nyingine alijiona akitembea umbali mrefu mpaka aliposhtuka kulikuwa kumepambazuka nakujishangaa kujiona yupo karibia na nyumbani kwake miguu ikiwa amejaa tope kwa kutembea peku kwenye mvua.


    Ajabu alipofika nyumbani kwake sauti ile ya mtoto wake ilisikika ikitoka ndani kuashilia mwanae ndani analia. Alipofika aliingia ndani kwani mlango ulikuwa umefunguliwa, ndani alimkuta mtoto kitandani peke yake. Mara aliingia mkewe aliyetoka msalani.


    “Vipi tena mwenzetu mbona hivyo?” Mkewe alimuuliza baada ya kumuona mumewe alivyokuwa hoi nguo ilikuwa imebaki nusu shati suruali nayo kama alivamia msitu wa chui na kumnyambua chini miguu ilikuwa na tope kama alikuwa akilima jaruba.


    “Mmh, weee acha tu safari yako ya Morogoro leo ilinipata.”
    Kauli ili ilimshtua mke wa Sule na kuamini aliyefanya vile huenda ni Nargis ili asifike alipokuwa amedhamilia kwenda. 


    “Mmh, kwani leo uliamka kwenda wapi?”
    “Si unajua mke wangu ulipotea katika mazingira ya kutatanisha, jana alfajiri niliamka ili niende kwa mtaalamu kujua huenda yule mt...”


    Kabla hajamalizia sentesi yake mkewe alimshika mkono mdomoni kumzuia aseseme na kusema.
    “Mume wangu komea hapo hapo.”


    “Kwa nini au una ajenda yako.”
    “Nakuomba unisikilize mimi nipo chini ya miguu yako, kuanzia leo tufanye kila linalotuhusu sisi wenyewe lisilotuhusu tuachane nalo.”


    “Mke wangu mbona sikuelewi hata la kupotea kwako pia hata hili na mimi kupotea siwezi kukaa kipya.”
    “Atiii,” Kopi zito lilitua kwenye shavu la Sule.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Wee mwanamke imeanza lini na leo iwe mara ya pili kunipiga.”
    “We ni kiumbe gani usiyesikia unajua mimi nilikuwa wapi, ungejua usingethubuti kunyanyua hata unyayo wako kunitafuta.”


    “Basi inawezekana unanidanganya una mwanaume.”
    “Mume wangu unaupungufu gani wa ufahamu muda mfupi unasema yapi yamekukuta, kama mbishi fuatilia nyayo za damu utarudi jina.”


    “Wewe ni mwanamke tu huwezi kunishauri upumbavu, lazima nijue sababu ya wewe kupotea na pili, itakuwaje mji niliozaliwa nipotee sikubali hata kidogo.”


    “Mume wangu ungejua maisha niliyokuwa naishi usingethubutu kusema hayo, chonde chonde mume wangu yote yaliyopita tuachane nayo.”


    Mke wa Sule alimpigia magoti mumewe kumuomba mumewe asitake vita na Nargis kwa kuamini kupotea kote kule ni kwa Nargis na hakutaka kumzuru zaidi ya kumtisha.




    Lakini Sule bado alionekana mbishi na kutaka kujua mwisho wa yote lazima aende kwa mtaalamu kwa vile mateso aliyoyapata yalimtisha.


    “Mke wangu kwani tatizo nini?”
    “Ubishi ndiyo ulionifikisha hapa sina hamu ya kuvifuatilia visivyonihusu, naweza kusema sisi wanadamu ni wabishi pia tuna roho mbaya pengine kuliko viumbe vyote.”
    “Kwa nini unasema hivyo?”
    “Bila huruma ya yule niliyetaka kumtenda ningekuwa kiumbe wa ajabu na maisha niliyoishi kwa wiki nzima yasikie si ya kuomba uishi,” mke wa Sule alimsihi mumewe huku akitokwa na machozi.
    “Basi nielezee ilikuwaje ili nami nijue.”


    Kabla hajasema kitu alisikia sauti ya Nargis nje, hofu ilimtanda na kutoka nje ili kupata uhakika. Alipotoka nje alimuona Nargis akiwa amesimama nje ya mlango wa Thabit, kwa hofu alimsalimia.
    ‘Za saizi dada?”
    “Mmh, nzuri tu shemu hajambo?”
    ”Hajambo, e.e..ti,” mke wa Sule alipatwa na kigugumizi alipotaka kuuliza kitu.


    “Ulikuwa unasemaje?”
    “Mume wangu analazimisha nimueleze nilipokuwa, nimweleze?”
    “Mweleze tu.”
    “Ni hayo tu dada.”
    Mke wa Sule alirudi ndani na kumueleza mume wake yote yaliyomtokea mpaka kufikia siku ile kuwepo pale.
    “Utani huo mke wangu.”


    “Kweli kabisa mume wangu, bila huruma yake sijui ningekuwa katika hali gani. Ila nakuomba siri hii usimwambie mtu yeyote zaidi yangu mimi na wewe, la sivyo atakacho tufanya Mungu anajua.”
    “Mh! Lakini kweli ulichokifanya kilikuwa hakikuhusu, bora tuachane naye pia hapa tuhame.”
    Wakiwa katikati ya mazungumzo mlango uligongwa, alimruhusu aingie. Alikuwa Thabit.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Ooh, best karibu.”
    “Asante.”
    “Shemeji yupo?”
    “Yupo ulikuwa na shida naye?”
    “Walaa, nilikuwa namuulizia tu.”
    “Jamani mi si mkaaji ila nimekuja kuwaaga leo ninahama.”
    “Una hama, unahamia wapi?”
    “Nitawajulisha kwa kuwa bado mpo wala msihofu nitawajulisha.”
    Thabit baada ya kusema hayo aligeuka na kuondoka akiwaacha mtu na mkewe wakitazamana.


    ****
    Nargis baada ya kumkomesha mke wa Sule na mumewe aliamua kurudi chini ya bahari na mpenzi wake Sule kupumzika kwani muda mwingi aliutumia kushindana na mke wa Sule. 
    Hata wazazi wake hali ile waliiona ilikuwa ikijionesha katika uso wake uliochoka na kukata tamaa.
    “Vipi Nargis mbona upo hivyo tumekuruhusu uwe na mwanadamu mbona unaonekana huna raha?” Mama yake alimuuliza.
    “Hakuna kitu mama nipo sawa.”
    “Mh! Upo sawa kweli mwanangu?”
    “Nipo sawa mama.”


    “Mh! Sawa.”
    Mama Nargis hakuridhika na majibu ya mtoto wake alimtuma mtoto wake mkubwa wa kike ambaye ni shoga na mdogo wake Nargis ili kumchunguza mtoto wao ana tatizo gani. 
    Hairat dada yake mkubwa Nargis alimfuata mdogo wake ambaye alionekana mtu mwenye mawazo kila alivyofikiria kiburi cha mke wa Sule kilimkosesha raha kwani hakuamini kama kweli vitisho vyote vile ataogopa.


    Alimkuta akiwa amezama kwenye dimbwi la mawazo juu ya kitimtimu cha wiki mbili cha kumdhibiti mke wa Sule hata kushindwa kulifaidi penzi lake kwa Thabit. Alipofika kutokana na mawazo hakuweza kumuona dada yake mpaka alipomshtua.
    Alishangaa kumuona mdogo wake akibubujikwa na machozi tena akiwa sehemu ya peke yake kitu kilichouumiza moyo wake.
    “Nargis mdogo wangu unalia nini?”
    Nargis alishtuka na kumtazama dada yake huku akijitahidi kufuta machozi yaliyokuwa yakitoka bila kizuizi.
    “Hapana dada kawaida.”
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Nargis kawaida unalia, sijawahi kukuona ukilia haiwezekani wewe ni kipenzi changu tena ni kipenzi cha familia. Tumekuruhusu uolewe na mwanadamu ili kuupa furaha moyo wako lakini imekuwa kinyume.
    Nargis mdogo wangu najua Thabit kakutenda, hili nililijua mapema ndiyo maana nilikuonya na wazazi nao walikuonya lakini umekuwa kichwa ngumu, matokeo yake kuikosesha furaha nafsi yako.
    Nakuahidi kumkomesha Thabit kwa mkono wangu wewe najua si mama huruma, sasa niachie hiyo kazi na kwa vile umemleta mwenyewe humu ndani hatoki,” Hailat alisema kwa hasira baada ya kumuona mdogo wake akiteseka kwa ajili ya wanaume wa kibinadamu.


    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog