Search This Blog

DHAHAMA - 3

 







    Simulizi : Dhahama

    Sehemu Ya Tatu (3)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    RASKAZONE

    TANGA



    Siku iliyofuata katika jiji la Tanga ilikuwa ni siku nyingine iliyobeba tukio la ajabu jingine ambalo lilistahiki kuingia katika matukio ya ajabu yaliyowahi kutokea nchini Tanzania, ilikuwa ni siku ya pili imepita baada ya kutokea tukio la kuungua zile nyumba za kampuni Hamid kule Duga maforoni. Majira ya saa nne asubuhi wafanyakazi wa kampuni ya mafuta ya Matro ambao hawakumalizia kazi zao kutokana na tukio lililotokea hapo ofisini kwao la kuuawa kwa mmiliki wa kampuni hiyo walihitajika kufika mapema kumalizia viporo vya kazi yao ili waweze kwenda mapumzikoni kutokana na kifo cha mmiliki wa kampuni hiyo, ilipotimu saa tano asubuhi wafanyakazi wote walikuwa kwenye ukumbi wa mkutano wakimsikiliza msemaji wa kampuni hiyo baada ya kumaliza viporo vya kazi vilivyosalia siku iliyopita.

    "Natumai wote ni wazima wa afya na mpo hapa kusikiliza jambo nililowaitia, kikubwa kilichonifanya niwaite hapa ni juu ya kutokea kwa msiba wa bosi wetu kipenzi na wote mnalitambua hili. Sasa basi kwa taarifa zilizonifikia ni kwamba kumetokea vifo viwili ndani ya siku moja ambacho kimoja ni cha bosi wetu kipenzi na kingine ni cha kaka yake mmiliki wa kampuni ya Extoplus nadhani wote mnamfahamu. Hivyo misiba hii yote miwili itafanyika nyumbani kwa baba yao mzazi mzee Buruhan maeneo ya Sahare jijini hapahapa, ikiwa sisi ni miongoni mwa wafanyakazi wake tuliyempenda inabidi wote twende tukamfariji mjane wa marehemu pamoja na familia nzima ya mzee Buruhan. Hakika sisi ni wa....." Msemaji mkuu wa kampuni ya Matro alitoa maelezo kwa wafanyakazi wa kampuni aliyoyapata ambayo hayakuwa yamefika kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo, alipokuwa anataka kuhitisha maelezo hayo alisikia mlango mmojawapo wa chumba cha mkutano ambao hautumiki ukifunguliwa kwa nguvu na ikaonekana aliyefungua ni mtu mwenye ubavu mkubwa kwa jinsi ulivyotoa kishindo hadi kitasa chake kikaanguka papo hapo. Macho ya kila mmoja aliyepo eneo hilo yalielekea kwenye mlango huo na hapo ndipo wakapigwa na butwa baada ya kumuona mtoto mdogo wa kike mwenye takribani miaka sita akiingia huku kabeba mdoli mdogo mwenye umbo la dubu mweupe, macho ya baadhi ya wafanyakazi yalionesha kumtambua huyo mtoto ila baadhi hawakumtambua hata kidogo. Mtoto huyo wa kike mzuri alizidi kumfanya Msemaji mkuu wa kampuni hiyo apagawe zaidi, mtoto huyo alipiga hatua hadi alipo Msemaji mkuu wa kampuni hiyo kisha akamuangalia usoni huku akitabasamu.

    "Annet mwanangu umekuja na nani?" Msemaji mkuu alijikuta akiuliza huku akiwa ameduwaa na hata wengine waliduwa kwa jinsi mlango aliopitia huyo mtoto ulipotoa kishindo kizito sana hadi kitasa chake kikaanguka.

    "nimekuja mwenyewe baba" Mtoto huyo anayeitwa Annet alijibu kwa lafudhi ya kitoto ambayo ilisikika na kila mmoja humo katika chumba cha mkutano.

    Msemaji wa kampuni aliposikia hilo jibu la mtoto wake alichuchumaa chini akamshika mashavu huku akitabasamu kwa ishara ya upendo wote anaotakiwa kuuonesha baba kwa mtoto wake kisha akamuuliza, "ni nani aliyeufungua mlango kwa nguvu hadi kitasa kikaharibika?"

    "Mimi hapa nimeugusa tu kwa mkono mmoja nikausukuma ukafunguka" Annet alijibu na akazidi kuwashangaza watu waliomo humo ndani hadi Msemaji mkuu wa kampuni naye akazidi kushangaa majibu anayoyatoa binti yake huyo mdogo.

    "Samahani kwa kuwavamia mkutano wenu na kuwakatisha, nimetumwa tu kuwaeleza ujumbe niliopewa ambao unawahusu nyinyi na ujumbe hamtakaa kuusambaza wala kusimulia kwa wengine kwani mlipewa nafasi mkaichezea. Ni hivi siku iliyopita baada ya kufa kwa bosi wenu nyinyi mlipoondoka hapa kwenye kampuni hii ilikuwa ndiyo salama yenu ila kwakuwa mmerudi, nimeambiwa niwaambie kuwa hili ndiyo kaburi lenu" Annet aliongea kwa sauti nzito tofauti na ile ya kitoto aliyokuwa anaongea tena akatoa maneno yaliyozidi kuwachanganya.

    "We Annet unasemaj..?" Msemaji wa kampuni hiyo alishindwa kumalizia kauli yake baada ya Annet kupotea katika mazingira yasiyo ya kawaida, jengo zima lilianza kutingishika kama limekumbwa na tetemeko la ardhi vioo vya madirisha vikaanza kuvunjika na kuzidi kuwatia wafanyakazi wote hofu. Wafanyakazi walipojaribu kukimbilia mlangoni ili watoke walikuta milango ikiwa imejifunga, mtetemeko wa jengo hili ulizidi kuwatia hofu na wakajikuta wakitaja jina la muumba kwa mara ya kwanza baada ya kutaja majina ya mama zao kwa muda mrefu.



    ****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    LAS VEGAS

    MAREKANI



    Wakati wafanyakazi wa kampuni ya Matro wakikumbana na janga lililotokea hapo kwenye makao makuu ya kampuni hiyo, upande mwingine wa bara la Amerika ya kaskazini katika mji wa Las Vegas nchini Marekani majira ya saa nne usiku kwa masaa ya huko ambapo yapo masaa kumi nyuma ya Tanzania. Kijana mwenye mavazi ya anasa zaidi alionekana akiingia ndani ya klabu maarufu ya usiku ya jijini humo, Falzal ndiyo jina lake huyu kijana mwenye kila aina ya majigambo na mwenye jeuri ya kuchezea pesa katika starehe. Ingawa bado ni kijana msomi na aliyekuja nchini humo kwa ajili ya masomo, aliishi mithili ya mtu maarufu wa jijini humo.

    Alipoingia ndani ya klabu hiyo ilikuwa kama kawaida yake lazima aende kwenye meza ya wacheza kamari kama kawaida, hiyo ndiyo ilikuwa starehe yake nyingine ambayo ilimuingizia pesa nyingi na kumfanya aishi maisha ya kifahari sana jijini humo. Aliwasalimu watu anaocheza naoo kamari kila siku akiwemo Miliver mcheza kamari maarufu hapo La vegas kisha akaketi, alimuangalia Miliver akatabasamu kisha akasema, " naona leo umekuja kunikuzia mtaji kama kawaida yako"

    "Ha! Ha! Ha! Leo unaliwa wewe ngoja utaona tu"Miliver aliongea huku akicheka.

    Faiz alipotaka kuchukua kete alishtushwa na mlio wa simu kutoka kwenye suruali yake na ikamlazimu awaombe radhi wachezaji kamari wenzake halafu akasogea pembeni sehemu isiyo na sauti nyingi na akaipokea simu.

    "Baba vipi mbona usiku hivi?" Falzal aliongea baada tu ya kumsalima aliyekuwa anaongea naye kwenye simu.

    "kuna tatizo gani baba mpaka nirudi nyumbani si uniambie tu nielewe hapahapa"Falzal alizidi kulalamika akiona anaharibiwa starehe zake.

    "Sawa baba nakuja kesho asubuhi" Falzal alikata simu kisha akionekana ni mwenye uso wa masononeko kisha akaondoka humo kwenye klabu ya usiku pasipo kumsemesha yeyote na uso wake ulikuwa unalengwa machozi, aliingia ndani ya gari na akaondoka hapo akionekana ni mwenye kuchanganyikiwa sana baada ya kupokea simu kutoka kwa baba yake.



    ****



    RASKAZONE

    TANGA



    Wakati Faizal akiondoka kwenye klabu ya usiku majira ya saa nne usiku kwa saa za Marekani, huku Tanzania majira kama hayo ya saa nne ila asubuhi kuna kitu kingine kabisa kigeni ndani ya nchi hii kilikuwa kinaanza kutokea. Tukio la aina yake ndiyo lilianza kuonekana kwa watu waliopo karibu na jengo lenye ofisi za makao makuu ya kampuni ya mafuta ya Matro, jengo hilo lilianza kutetemeka na taratibu likaanza kuporomoka kuelekea chini likivunjika vioo pamoja na kuta zake zikiporomoka. Lilikuwa ni tukio la kustajaabisha sana kwani eneo la chini ya ardhi lenye msingi wa jengo hilo lilipasuka kisha likafunguka na jengo zima likaingia chini ya ardhi huku eneo zima linalomilikiwa na kampuni ya Matro likiwa lunatetemeka kama kuna tetemeko la ardhi, tetemeko hilo lilipokuja kutulia eneo lenye msingi wa jengo la Matro lilibaki kama urefu wa kaburi lililojengewa. Jambo la namna hiyo halikuwahi kutokea nchini Tanzania ingawa huwa inakumbwa na matukio makubwa, tetemeko la ardhi lililoikumba eneo lenye ukubwa wa ekari moja ambalo ndani yake ndiyo zilipo ofisi kuu za kampuni ya Matro halijawahi kutokea hata katika nchi nyingine ndani ya dunia hii.

    Baada ya muda mfupi kikosi cha uokoaji kilikuwa kimeshafika katika eneo hilo ambapo walibaki wakishangaa tu kwani hawakuwa na kifaa chenye uwezo wa kuchimba chini lilipodidimia ghorofa hilo wakati linavunjika, kikosi hicho kilichokuja kwa ajili ya uokoaji na chenye ari ya kufanya uokoaji kilijikuta kikishindwa kufanya uokoaji kutokana na ugumu walioukuta eneo hilo lililohitajika kufanyiwa uokoaji.

    Wakiwa wamesimama hapo mlio wa mkoromo wa simu ys upepo ya kiongozi wao ilisikika na ikamlazimu kiongozi huyo atoe simu hiyo ya upepo na kuiweka mdomoni kisha akazungumza kwa kutaja eneo alipo halafu akajitambulisha, sauti yenye kukoroma ilisikika ikiongea ambapo ilisikika vyema kwa kiongozi ambaye alibaki akiwa amepigwa na butwa halafu akawaangalia wenzake huku akihema kwa kasi.

    "Jamani sheli zote za Matro zinaungua sasa inahitajika timu kubwa ya msaada ya kusaidia uokoaji, sasa hatuwezi kukaa hapa mpaka mashine ya uokoaji kutoka Dar es salaam iletwe. Team twendeni tukasaidiane na wenzetu kwenye uwezekano wa kutoa msaada na sio kubaki" Kiongozi huyo aliongea kisha akaanza kukimbia yalipo magari yao na wenzake wakawa wanafuata nyuma, magari ya kikosi cha uokoaji yaliondoka eneo hilo la Raskazone kwa kasi yakiacha mamia ya raia kutojua sababu ya wao kuondoka eneo hilo



    ****



    SURA YA TANO



    Siku iliyofuata nyumbani kwa Mzee Buruhan tayari turubai kubwa lilikuwa limeshafungwa katika eneo la wazi la nyumba hiyo pamoja na maeneo jirani na eneo hilo, hadi muda huo tayari watu walishajaa nyumbani hapo kutokana na umaarufu wa watoto wa mzee Buruhan waliofariki katika vifo vya kutatanisha. Upande wa kinamama kulisikika vilio kutoka kwa watu wa karibu ambao walikuwa na uchungu wq kuondokewa watu hao, ilikuwa ni siku ya kuhuzunisha kwa familia nzima ya Mzee Buruhan kutokana simanzi iliyowakumba.

    Watoto wa mzee Buruhan waliosalia ambao ni ,Ally,Hassan na Falzal tayari walikuwa wapo msibani wakiwa na huzuni sana huku kaka yao mkubwa Shafii akiwa yupo hospitali kutokana na ajali aliyopata. Taratibu zote za mazishi ziliendelea kama zilivyopangwa na baada ya adhuhuri ndugu wawili wa damu walizikwa kwa wakati mmoja, baada ya mazishi watu walitawanyika na kuwaacha watu wa karibu wa marehemu wakiwa hapo msibani kuendelea na taratibu zingine zilizokuwa zimewekwa hapo awali katika ratiba ya msiba huo uliowagusa wengi kutokana na vifo vilivyowapata ndugu hao wawili wa damu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ****



    HIMAYA YA MAJINI YA MAJI CHUNGU



    Wakati mazishi ya Hamid na Hussein yakiwa yanaendelea yalikuwa yakishuhudiwa kwenye kioo kikubwa mithili ya sinema kilichopo katika chumba maalum ndani ya kasri la himaya ya Majichungu, Zalabain na Salmin walikuwa wakishuhudia kila kitu hadi maziko yanakamilika, baada ya kumaliza kuangalia tukio hilo waliangalia pia tukio la kuanguka kwa ghorofa la kampuni ya Matro na kuungua kwa sheli zote za kampuni hiyo.

    "kazi nzuri ewe mjukuu wa mfalme nadhani bado magugu makuu manne ili kazi yetu ikamilike na hakikisha kila mmoja anaondolewa kwenye ardhi waliyokufanyia ubaya yaani Tanga na ukimmaliza yeyote nje ya Tanga utakuwa umefanya kazi bure tu" Salmin aliongea

    "Nashukuru kwa kunifahamisha ewe jini mwenye nguvu uliyezaliwa milenia moja na robo tatu iliyopita, naishukuru sana nafsi yangu iliyonizuia kumuua yule mmoja wao anayesoma Marekani. Usiku kwa masaa ya Marekani tayari nilikuwa nimeshafika kwenye eneo maarufu analochezea kamari yule binadamu kwa lengo moja tu la kummaliza. Nilitumia njia ya kujigeuza Miliver ambaye ni mchezaji kamari maarufu jijini Las Vegas ambaye nilimlaza usingizi ili asije kucheza kamari siku hiyo. Nilikuwa na kila njia ya kumuangamiza lakini nafsi ilinizuia kufanya hivyo na mimi nikaacha, nafikiri nisingeisikiliza nafsi ningekuwa nimejipa hasara" Zalabain aliongea

    "ungejipa hasara haswa kwani ufalme ungeupata kwa njia ya kafara ya ndugu yako wa damu kama ungefanya uzembe huo" Salmin alisisitiza kisha akaendelea kusema, "hakikisha yule binadamu harudi tena Marekani yaani kwa lugha rahisi ni kwamba anahitajika awafuate ndugu zake"

    "Hilo ondoa shaka nitalifanyia kazi haraka iwezekanavyo na inabi......." Zalabain alimuambia Salmin na alipotaka kuendelea kuongea Salmin alimzuia huku macho yake yakibadilika rangi na kuwa mekundu yaliyokuwa yanawaka kisha yakarudi katika hali ya kawaida.

    "vizuizi vya kuingia vya kuingia kwenye himaya hii vinavyozuia tusivamiwe vipo wazi" Salmin aliongea huku akisimama kwa haraka.

    "Ndiyo ni kweli vimefunguliwa maana kuna mfalme wa himaya ya jirani ana ziara hapa kwenye himaya yetu" Zalabain aliongea

    "Ni mtego huo hao ni watu wa jamii ya kishetani ya KAKIN wametuma majini yao kulipa kisasi, wale wabaya wako mmoja wao ni mwanachama wa jamii hiyo na hao majini wameshaingia inabidi tuwazuia kabla hawajaleta madhara sasa hivi" Salmin aliongea kisha akapotea hapohapo na Zalabain naye akapotea akatokea nje ya Kasri akamkuta Salmin akiangalia juu ya anga la himaya yao ambalo limebadilika rangi kutoka ile rangi nyekundu hadi nyeusi isiyopendeza kiasi cha kuleta giza.

    "tangu Dainun iibiwe hatujawahi kupata giza sasa jiulize giza hili linatokana na nini kama sio kuvamiwa huku, agiza askari wa baragumu apulize baragumu la hatari ili raia wote waingie majumbani mwao na hii vita ni yetu wasihusike" Salmin aliongea huku akimtazama Zalabain ambaye alipiga kofi moja akatokea kiumbe wa ajabu mbele yake.

    "Ndiyo mtukufu mfalme mtarajiwa" Yule kiumbe aliongea kwa utiifu.

    "puliza baragumu la hatari haraka iwezekanavyo raia wote waingie majumbani mwao" Zalabain alitoaamri kwa kiumbe huyo, kiumbe huyo aliitikia kwa ishara kisha akapotea papo hapo na baragumu la hatari muda huo huo likaanza kulia.

    Salmin na Zalabain walipaa juu huku macho yao yakiwaka kama nuru ya nyota angani, walipofika juu walitanua midomo yao wakapuliza na ukatoka upepo mzito sana ambao uliliondoa giza lote kama unavyoondoka ukungu na mwanga ukarudi. Mbele yao walikuwa wakitazamana na viumbe wenye sura za ajabu tena wenye rangi nyeusi, miili ya viumbe hao haikuwa ikieleweka ilivyo ilikuwa na umbile kama tambara bovu jeusi. Viumbe hao walikuwa wamebeba silaha za aina mbalimbali za kijini wakiwa na hasira za dhahiri, viumbe hao wakihema walikuwa wanatoa moto mdomoni kwa jinsi hasira zilivyokuwa zimewazidi.

    "Jisalimisheni kwa usalama wa jamii yenu yote hii" Mmoja wa wale viumbe aliongea.

    "Ondokeni kwa amani kwa usalama wenu na si mpaka tutumie nguvu" Salmin aliongea kwa upole sana

    "Naona jeuri sasa ngoja tuanze na wewe" Yule kiumbe alisema kisha akamnyooshea silaha yake Salmin iliamuangamize lakini alijikuta anaangamia yeye baada ya shoti kali zilizotoka kwenye macho ya Salmin kutua mwili mwake.

    Wenzake waliosalia walijiandaa kuwashambulia Salmin na Zalabain lakini walichelewa kwani walijikuta wakizungushwa na upepo wa ghafla uliotengenezwa na Zalabain ambao uliwafunga kama wamefungwa na kamba ngumu kisha waliangamizwa wote kwa pamoja kwa kuunguzwa na moto uliotoka mdomoni kwa Salmin uliowaunguza wote wakawa majivu.

    "Habari yao imekwisha funga kizuizi" Salmin aliongea kisha akashuka chini taratibu na Zalabain akaenda juu zaidi akanyoosha mkono mmoja uliotoa mwanga wa ajabu ulioelekea juu halafu akashuka chini taratibu baada ya kumaliza kazi yake.

    "hakuna atakayeweza kuivamia himaya ya majichungu nikiwa mimi nipo na himaya hii itadumu mpaka mwisho" Salmin aliongea kumuambia Zalabain kisha akainama chini kiutiifu akapotea mbele ya macho ya Zalabain.

    Baragumu la kuashiria hakuna hatari tena katika himaya hiyo lilipulizwa na raia wa himaya hiyo wakatoka majumbani mwao kuendelea na shughuli nyingine za kawaida na Zalabain akarudi ndani ya Kasri la ufalme.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ****



    Wakati majini waliotumwa kuleta maafa wanauawa upande mwingine kwenye chumba chenye watu waliovalia majoho meusi ambacho kilionekana kwa muonekano kilikuwa kipi chini ya ardhi. Kilikuwa kimetawaliwa na jazba miongoni mwa watu waliomo humo ndani, kiongozi wa watu ndiyo alionekana kuwa na jazba za wazi hadi akavua kofia ya joho lake akasema kwa hasira, "Haiwezekani! Haiwezekani! Hussein wamuue na majini yetu wayaue, lazima! Lazima! Tulipe kisasi kwa ajili ya Hussein mwanachama wetu".

    Sauti ya kiongozi huyo ilisikika kwa nguvu na kusababisha tetemeko zito litokee kwa sekunde kadhaa na lilipotulia ilisikika sauti ikisema, "Dalipso Londo usiingie kwenye vita isiyokuhusu hata kidogo, Hussein alikuwa ana janga lake tofauti alilolichuma kabla hajaungana nanyi,nimetumwa na mkuu wa wakuu nikuonye ukae mbali na tukio hilo na uhakikishe unamtia nguvuni Qwanta Alfred Lumaki aliyetutia hasara".

    Wote walikuwa wameinama kiutiufu na waliinua vichwa vyao baada ya sauti hiyo kuacha kuzungumza.

    "ndiyo mkuu" Dalipsol Londo alitii.



    "kazi ianze sasa hivi ili dunia iwe chini yetu tukiipata damu ya Alfred Lumaki na Qwanta wenzake,ndiyo furaha ya mkuu wa wakuu ni ushindi kuwa upande wetu na si vinginevyo" Sauti ile iliendelea kusikika kama mwangwi kisha ikapotea haraka sana, Dalipsol Londo aliwageukia wenzake akawaambia, "vita ya mamba kiboko haimtii wahka kwani amani hutawala hata bila kuingilia hiyo vita hivyo haina haja ya yeye kuingilia, ndiyo hivyohivyo vita ya Hussein na familia yake haitufai sisi kuingilia ile inawahusu yeye na familia yake na wala haivurugi hata kipengele cha kazi yetu".

    Baada ya Dalipsol Londo kusema maneno hayo alipiga kofi mara moja na mlango wa eneo walilopo ukafunguliwa, aliingia mtu aliyevaa joho jeusi akiwa anavuta kitoroli kidogo kilichofungiwa kondoo mweusi na pembeni kulikuwa kuna kifaa chenye ncha kali. Toroli hilo lilivutwa hadi mbele ya Dalipsol Londo kisha yule mtu akamkabidhi kifaa chenye ncha kali huku akiwa ameinamisha kichwa kwa heshima, Dalipsol Londi alikipokea kifaa hicho kisha akasema, "ni muda kuanza ibada kuu zaidi ya zote kwa mkuu ambaye ndiye mungu yetu mkuu, hatuna Mungu mkuu zaidi yake mkuu wa wakuu".

    Alipomaliza kutamka maneno hayo alimtoboa yule kondoo shingoni kisha chombo kikubwa kikakingwa chini, damu ya yule Kondoo iliingia ndani ya chombo hicho hadi kikajaa na Kondoo aliondolewa na yule mtu aliyemleta akiwa bado anatapatapa kutokana na jeraha lililotobolewa na Dalipsol Londo. Damu ile ya Kondoo ilitiwa kwenye kwenye bilauri zilizotengenezwa na madini ya fedha na zikasambazwa kwa watu waliokuwa wapo humo ndani, kila mmoja alikamata bilauri yake na wakazinyanyua juu kwa pamoja huku vichwa wakiviinamisha.

    "Kwa jina la mkuu wa wakuu mwenye mamlaka kuu ya kutupa nguvu pamoja na pumzi kuu" Dalipsol alitamka maneno hayo huku bilauri akiwa ameinua juu kama wengine, alipomaliza kutamka maneno hayo aliinywa damu ile huku wenzake wakifanya hivyo hivyo.



    Kakin ni jamii ya watu wanaoabudu nguvu za giza ambayo ilianzishwa miaka mingi iliyopita huko mashariki ya mbali na iliingia Afrika miaka mingi iliyopita kupitia waziri mkuu wa utawala wa Roma aliyetoroka katika himaya ya Roma kuepuka kuuawa na mtawala wa himaya hiyo aliyekuwa anaitwa Miltonus baada ya kubainika ni mwanajamii wa Kakin. Bwana huyu aliitwa Hilainus aliingia barani Afrika na akapokelewa kwa ukarimu sana kama ilivyo kawaida ya Waafrika kupokea wageni kwa ukarimu, aliingiza falsafa za jamii ya Kakin kwa siri sana hadi akajipatia wafuasi kutoka pande mbalimbali za Afrika. Hadi anafariki tayari alikuwa na familia yake na jamii hiyo ya siri ilikuwa imeshasambaa mhalimbali na ilikuwa inaendeshwa kwa siri mno kwani habari za uovu wa jamii zilikuwa zishasambaa barani kote ingawa haikujulikana ni nani aliyeileta Afrika.

    Usiri wa ibada za jamii hii ulizidi sana pale mtawala wa himaya ya Soghai Sunni Ali alipowaua kwa kuwakata vichwa watu waliobainika ni watumishi wa jamii hiyo, asilimia kubwa ya himaya za kiafrika tayari zilikuwa zimeufuata uislamu baada ya kufanya biashara na waarabu kwa muda mrefu kipindi ambacho himaya ya roma bado inanyanyasa watumwa. Hadi imani za Kakin zinaingizwa barani hapa tayari Uislamu ulikuwa umeshasambaa sana, juhudi za upambanaji dhidi ya jamii haramu ziliwahusisha wanajamii wote wa Afrika bila kujali tofauti ya kiimani iliyokuwa ipo kati ya waislamu na ambao walikuwa wana imani za kizamani za kuabudu miti na mapango ambao walitofautiana sana kiimani na Kakin ingawa walitegemea majini walioiita mizimu. Wote kwa pamoja walipambana sana na udhalimu na Kakin na baadaye hatimaye waislamu walijitoa baada ya kuzaliwa mtoto aliye na mchanganyiko wa mashariki ya mbali na Habaishi waliokuwa wafuasi wa Waothodoksi, mtoto huyu alipewa jina cheo cha Qwanta ambaye katika uzao wake walishirikishwa majini weupe wanaojulikana kwa jina la majini wa nuru. Majini hao walikuwa wametengana na wale wa giza waliokuwa wako pamoja na Kakin, majini hawa walikuwa wapo tayari kuona jamii nzima ya Kakin inaangamia ili dunia iwe huru na walimpatia nguvu za ajabu mtoto huyo ili alete mapinduzi katika, kisa hicho kilichoelezewa na mwandishi wa mkasa huo aitwae Hassan Omar Mambosasa alichokipa jina la KUANGUKA KWA KAKIN kuanzia kitabu cha kwanza na hadi cha mwisho ndiyo kinaelezea kinagaubaga juu ya jamii hii na kuanguka kwake.



    ****



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya siku kadhaa tangu mazishi ya Hamid na Hussein yafanyike Falzal alipanga arudi Marekani na alienda kukata tiketi katika ofisi za shirika la ndege la Ermirates za jijini Tanga lakini alijikuta akishindwa kuondoka baada ya kuambia kuwa hakuna ndege hata moja iliyokuwa ikiingia Marekani kutokana na hali ya ukungu iliyokuwa imetanda katika bahari ya Antalantiki, habari hiyo ilimnyong'onyesha sana na akajikuta akibakia kwenye jiji la Tanga na hata alipojaribu kwenda jiji la Dar es salaam ili akaendelee na starehe napo alijikuta akishindwa kutokana na kukosa gari linaloenda huko. Alipouliza juu ya chanzo cha kuvunjika kwa safari hiyo alijibiwa kuwa daraja la mto Wami lilikuwa limevunjika na hata alipojaribu kwenda uwanja wa ndege wa Majani mapana wa jijini Tanga kukata tikeri ya ndege alikosa vilevile akaambiwa ndege za mashirika mbalimbali zilizokuwa zinarusha ndege zake kuja Tanga zimevunja safari zao. Hali hiyo ilimfanya Falzal ajihisi ana mkosi baada tu ya kurejea nyumbani akiwa ili ahudhurie msiba wa kaka zake, maisha ya anasa aliyoyazoea kuishi kule marekani ndiyo yalimfanya ashindwe kukaa jijini Tanga kwani akiishi maisha hayo alikuwa anamtia aibu baba yake mzazi.

    Heshima ya mzee Buruhan ndani ya jiji la Tanga kutokana na busara alizonazo kwa kuwaongoza wanae zilimfanya aheshimike kwani wanae ni watu maarufu sana ndani ya jiji hilo, hivyo laiti Falzal angeishi hivyo hapo Tanga angetia doa heshima ya baba yake. Falzal alijiona ni kama yu kifungpni kwa kukosa maisha anayoyapenda na aliyoyazoea, alivumilia kukaa hivyo kwa muda wa takribani siku mbili na hatimaye siku ya tatu akachukua mizigo yake akaiweka kwenye gari na akaazimia kuondoka mbali na jiji la Tanga ili akaishi atakavyo hadi pale atakapoondoka tena Marekani. Eneo alilofikiria kwenda ni Arusha tu kwani ndiyo ambapo hapakuwa na kikwazo chochote, aliamua kutumia usafiri binafsi ili awe huru zaidi.

    Hakika hakutambua kama alikuwa anajaribu kukwepa jambo lisilokwepeka labda akukwepeshe muumba ndiyo linaweza kukwepeka lakini si kwa nguvu za kawaida kuweza kulikwepa, hakujua na alikuwa ameshasahau juu ya janga walilolifukia ambalo limejifukua bila ya wao kujijua. Hakutambua kama vikwazo vya safari vinatokana na jambo ambalo lisilokuwa na la kawaida.

    Falzal aliwaaga ndugu zake pamoja na mzazi wake kisha akaingia kwenye gari binafsi anayoitumia aina ya toyota landcruiser, alianza safari vizuri huku akiwa na shauku kuu ya kuliacha jiji la Tanga ili aende kuendelea na maisha yake ya anasa aliyoyaacha hapo awali.

    Aliendesha gari kwa mwendo wa wastani hadi alipoanza kukaribia Majani mapana ndipo alipozidi kuongeza mwendo wa gari ili aendane na mwendo unaotakiwa katika barabara aliyopo, alipokaribia eneo ambalo kuna njia iendayo kwenye mzani wa magari makubwa wa Majani mapana aliona mzee mwenye mizigo akumpungia mkono njiani ili amsimamishe lakini alimpita kwa mwendo mkali sana huku akisonya.

    "Vizee vingine bhana vinadhani kila gari ni ya kubeba watu masikini kama wao, akapande basi huko asinisumbue mimi" Falzal aliongea kwa dharau kisha akaongeza mwendo zaidi.

    "vijana wengine bhana wanadhani kila mali inaweza ikadumu bila kujali imepatikana kwa njia gani, wakatafute kupitia jasho lao wenyewe" Ilisikika sautu ikitoka kwenye kiti cha nyuma cha gari hilo na ikamfanya Falzal ageuke nyuma huku akiwa ameachia usukani, loh! Sallaleh alimuona yule mzee aliyempita pale barabarani akiwa amekaa kwenye kiti cha nyuma akiwa amekunja nne akiwa na mavazi yake machakavu aliyomuona nayo pale njiani wakati anampita. Falzal alizidi kupatwa na uoga sana kwani haiwezekani mtu akiyempita njiani tena kwa mwendo wa kasi amkute ndani ya gari yake, alibaki akimtazama huku akitetemeka kwa uoga hasa alipoona tabasamu la yule mzee.

    "Kijana kamata usukani utagonga huoni kama tupo kwa Minchi tunaelekea kwenye ule mzunguko tena kuna tuta mbele, dereva gani usiyekuwa na umakini uwapo barabaranu wewe tena punguza mwendo maana tunaingia katikati ya jiji magari ni mengi" Yule mzee alimwambia Falzal huku akutabasamu na mahali alipomtajia Falzal palikuwa ni mahali ambapo ni mwanzo kabisa alipapita hata kabla hajafika Majani mapana, Falzal alipoangalia mbele kweli aliona anakaribia kwenye tura na alipunguza mwendo haraka sana na akalipita tuta kisha akashika usukani vizuri akawa anaingia kwenye mzunguko wa kwa Minchi. Falzal alilizungusha gari kwenye mzunguko huo ili arudi alipotokea katika barabara kuu iendayo Segera, alipotaka kunyoosha tairi kisha akate kidogo aingie barabara ya hiyo ambayo alitokea kuingia mzunguko huo wa kwa Minchi alijikuta akishindwa baada ya usukani kugoma na hivyo akazunguka tena ule mzunguko na gari ikaingia katika barabara kuu iendayo Mombasa.

    " Huwezi ukatoka nje ya Tanga hata kwa namna gani , ulidhani ukimaliza hiyo roundabout ya Kwa Minchi utaweza kurudi kule ulipokuwa unaelekea. Sasa umeula wa chuya kijana" Yule mzee aliongea huku akitabasamu.

    "we...we.....wewe ni nani?" Falzal aliuliza huku akitetemeka na alikuwa akimuangalia huyo mzee pamoja na kuangalia mbele ili asipate ajali, uoga uliokuwa umeibugika nafsi yake ulimfanya ashindwe kutambua kama gari hiyo ilikuwa inaenda yenyewe kwa mazingira ya ajabu pasipo yeye kuiendesha.

    "Achia usukani kijana maana unajisumbua gari hiyo inaenda yenye na si wewe unaiendesha na si unataka kunijua mimi ni nani sio?" Yule mzee aliongea kisha akaongea akajibadilisha akawa na sura ile ya mtoto ambayo iiliwatokea kaka zake muda mfupi kabla hawapoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha.

    "Jamadin! Ha..pana siyo we..we" Falzal aliongea huku akitetemeka kwa uoga kwani hakutarajia kumuona aliyemuona hapo.

    "Unashangaa kuniona mimi? Ha! Ha! Ha! Kwanini usijishangae kwa kuhusika kufanya maisha ya mwenzako aliyeumbwa kama wewe kuwa duni" Yule mtoto aliongea kwa sauti yenye kukwaruza tena alicheka kicheko kisichokuwa kinaashiria furaha kwani machoni alishaanza kutoa damu.

    "Kutumia nguvu za wenzenu kujitajirisha mliona raha sana sasa leo ni zamu yako Falzal ambaye hupaswi kuitwa baba mdogo kwa mabaya uliyonifanyia" Yule mtoto aliongea huku akilia kwa machozi ya damu

    "Si.....siyo mimi Jamadin ni kaka ndiyo aliyekukosea na ndiyo aliyepanga kila kitu" Falzal aliongea kwa uoga.

    "Huna cha kujitetea kwa sasa kitachoweza kufanya nikusamehe wewe mwanaharamu, kwanza nipe ukitaka ufe kistarabu la si hivyo nakurarua kama Simba anavyorarua nyama ya swala" Yule mtoto aliongea kwa hasira hadi miale ya moto ikawa inamtoka mdomoni mwake.

    "Ni...nikupe nini Jamadin?" Falzal aliuluza huku akiwa anazungusha macho yake kuangalia kama anaweza kupata upenyo wa kukimbia lakini hakukuwa na upenyo wa kutokea kwani milango ilikuwa imefungwa na vioo vimebanwa hadi mwisho.

    "Mmmhu! Yaani hilo suala la kunitoroka usifikirie kabisa, nimesema nipe kile kinachowafanya muwe matajiri kila kukicha na kile kinakufanya uwe na bahati kila ukicheza kamari" Yule mtoto aliongea kwa hasira sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "sinacho mimi Jamadin anacho..." Falzak alijitetea na alipotaka kumtaka mwenye kitu kinachotafutwa na huyo mtoto lakini alijikuta akikabwa kooni baada ya huyo mtoto huyo kumnyooshea kidole.

    "sijakuambia umtaje huyo aliyenacho, sasa nilikuambia nakurarua ukiwa huna na sitengui kauli yangu" Yule mtoto aliongea kisha akatoa makucha mikononi akaanza kumrarua hadi mwili wa Falzal ukawa ni damu tupu tu na vidonda kila sehemu ingawa roho yake haikuachana na mwili na maumivu ndiyo yalitawala mwili wake wote, alipiga makelele akilia kama mtoto mdogo lakini hakukuwa na mtu aliyesikia kulio chake kwa muda huo.

    "Sasa wasalimie ndugu zako waliokuwa wametangulia kaburini nadhani watakuwa wanakungoja huko walipo" Yule mtoto aliongea kisha akatoa moto mkubwa wenye mlipuko mithili wa bomu ambao ulisambaa gari zima

    Hadi muda huo tayari gari la Falzal lilikuwa limeshafika maeneo ya Kisosora kwenye matanki ya mafuta ya kampuni ya BP iliyopo jirani na bahari ya hindi, yule mtoto alipopuliza ule moto gari lote lilipuka na likarushwa juu hadi ndani ya maji na hu ndiyp ukawa mwisho wa maisha ya Falzal ndani ya dunia na ukawa mwanzo wa maisha mengine nje ya dunia hii katika ulimwengu usionekana kwa macho ya kawaida.



    ****

    Hali ya Shafii kiafya iliendelea kuwa nzuri na hadi muda huo alikuwa tayari amesharuhusiwa na yupo nyumbani akiuguzwa na mke wake, huzuni kubwa ilkuwa ni sehemu iliyoutawala moyo wake hasa akikumbuka vifo vya wadogo zake. Hakuwa na la kufanya kwa muda huo kwani yeye alikuwa ni mtu wa kutembea na baiskeli ya walemavu kwani kiuno kilikuwa ni sehemu iliyopatwa na kadhia katika ajali ile iliyomkuta na ingemchukua muda mrefu mpaka kutengemaa na kuwa na hali ya kawaida kama ilivyokuwa hapo awali. Hadi muda huo si yeye wala familia yake waliokuwa na habari na jambo lililomkuta Falzal tangu alipowaaga anasafiri kuelekea Arusha akitumia gari binafsi, hawakujua akama falzal ni mmoja wa marehemu kwa muda huo.

    Kusononeka, kuhuzunika na kuumia moyo ndiyo jambo ambalo lilikuwa likimsumbua Shafii kila siku hasa alipowakumbuka ndugu zake na jambo lile aliloambiwa na sauti asiyoitambua kuhusu mwanae wa pekee Zayina kuwa ametekwa na yupo chini ya adui yake ambaye hamtambui hadi muda huo aliwahi kumfanyia ubaya upi kwani hakuna dui yake mwenye ubavu wa kumfanyia mambo hayo kwa mujibu wa mganga wake marehemu Sauti ya radi kama alivyomuambia. Alikuwa akimiliki cheni yenye kidani chenye kito kisichofahamika hapa duniani ambayo ndiyo ilifanya awe na nguvu miongoni mwa maadui zake na pia kidani hicho kilikuwa na uwezo wa kuwalainisha mioyo wanadamu wenzake ambao walitaka kufanya jambo baya kwake au kwa jamaa zake. Fikra zilizokuwa zipo kichwani ni kuwa adui aliyekuwa anamfanyia ubaya alikuwa ni mwanadamu wa kawaida na hakuwahi kuwaza kama kuna jini anayeweza kumfanyia hivyo kwani fikra zake zilimpa asilimia mia moja kuwa hajawahi kumfanyia ubaya jini katika maisha yake zaidi ya kuwafanyia ubaya wanadamu wenzake tu.

    "ni nani huyu na ana shida gani na mimi kwani hata cheni niliyokuwa nayo inashindwa kumtambua hata kidogo.Jamadin,gasper,Hilson na wengine wengi niliowahi kuwafanyi ubaya tayari wametangulia mbele za haki" Shafii alijiuliza katika nafsi juu ya utata wa tatizo linalomsumbua la kuondokewa na watu anaowapenda.

    "Eeeh! Mungu nimekosa nini mja wako nipo njia panda mja wako" Kwa mara ya kwanza Shafii alijikuta alijikuta akimtaja muumba baada ya kukaa kwa kipindi kirefu akimuasi mwenyezimungu kwa kumtegemea mwingine tofauti na yeye, maneno yake yalisikiwa nyema na mke wake ambaye alikuwa yupo nyuma yake akimtazama mumewe wake kwa masikitiko makuu jinsi anavyolalalmika kwa Mwenyezi mungu. Bi Farida muda wote huo akimtazama mumewe kwa jinsi anavyolalamika alijua ni kutokana na vifo walivyokufa wadogo zake, wala hakutambua kama mumewe alikuwa akiteswa na sauti ya mbaya wake ambaye alikuwa hamtambui. Machozi yalipoanza kutiririka katika macho ya Shafii. Hali ya Shafii ilimfanya Bi Farida amkumbtie kwa nyuma kisha akambusu shavuni kwa upendo halafu akamwambia,"Baba Zayina kazi ya Mungu haina makosa yapasa kumshukuru katika kila hali kwani amekujalia uzima katika ajali mbaya uliyoipata, haipaswi kumlaumu kwakuwa ndugu zako wamepoteza maisha mpenzi wangu"

    "Mke wangu inauma sana nahisi dunia yote nimeangushiwa mimi inauma.....inauma sana" Shafii aliongea huku machozi yakimtiririka machoni mwake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ha! Ha! Ha! Ha! Nadhani unatambua ule msemo wa waswahili waliosema kwamba jeraha la kujitakia halihitaji pole, sasa usitegee pole kwa mtu ambye baadaye akija kukujua upande wa pili wa maisha atakuacha na janga lako mwenyewe. Ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Mwanao Zayina najiandaa kuwapikia supu mbwa wangu wamle nikishamchinja" Sauti ileile iliyompa taarifa ya kuwa kuna jambo baya lnalotaka kutokea kwa mtoto wake ndiyo ilimpa taarifa iliyomfanya ashtuke

    "He! Baba Zayina kuna nini mbona unashtuka hivyo hadi unanitisha mume wangu" Bi Farida aliuliza

    "Nimejitonesha sehemu ya mgonogni mke wangu kutokana na kusononeka huku" Shafii aliamua kudanganya huku akiuma meno kwa maumivu kana kwamba alijitonesha kweli kumbe alishtushwa na sauti ya adui yake mkuu ambaye aliyewahi kumlea mwenyewe kwa mikono yake bila kujua ambye alimwambia jambo baya ambayo ameazimia kwenda kulifanya kwa binti yake kipenzi aliyempenda. Laiti kama wanadamu tungalipewa uwezo wa kuona yaliyojificha katika mioyo ya wenzetu basi Bi Farida angeliomba talaka mapema sana lakini Mungu muumba hakutupa uwezo huo wa kuona yaliyo katika mioyo ya wenzetu ndiyo maana Bi Farida hakutambua jambo linalimtatiza. Ama kweli moyo wa mtu ni kiza nene zaidi hata ya giza nene lililotanda kwenye pori nene katika usiku mnene, mungu muumba alikuwa na maana yake sana kutuumba wanadamu kwa kuficha yaliyopo mioyoni kwani hadi muda huo tayari wanadamu tungekuwa tushafarakana kama tungebaini yaliyopo kwenye mioyo ya wenzetu.





    ****



    "ngoja nikuwahishe ndani mume wangu ukanywe zile dawa na upumzike" Bi Farida aliongea huku akianza kuburuza kiti cha matairi cha mumewe huku akiita, "Jamali! Jsmali!".

    "naam!" Sauti kutoka ndani ya chumba kimojawapo ilisikika ikiitika.

    "njoo unisaidie kumuweka kitandani mjomba wako" Bi Farida alimuambia yule mtu aliyemuita huku akikisukuma kiti cha matairi kuelekea chumbani kwake, muda huo Shafii alikuwa bado ameuma akiweka maumivu yake ya kuigiza ili azidi kumchota mke wake akili ajue ni kweli ameumia.

    "Sawa shangazi nakuja sasa hivi" Sauti ya Jamal ilisikika kisha mlango wa chumba kimojawapo ukafunguka na akatoka kijana aliyefanana sana sura na Hamis kaka yake Bi Farida na shemeji yake Shafii, Jamal alitembea upesi akamfikia shangazi yake akachukua kiti alichokalia Shafii akaanza kukiburuza yeye kukiingiza katika mlango wa chumba kimojawapo ambacho kimejitenga sana na vyumba vingine ndani ya nyumba hiyo, alipoingia ndani alikiburuza kiti hadi mahali kilipo kitanda cha kisasa kilichotengenezwa kwa mtindo wa kipekee na kunakshiwa kwa mapambo mbalimbali. Jamali alipofika hapo alimbeba mjomba wake kwa uangalifu akamlaza kitandani halafu akatoka chumbani kwa mjomba wake upesi kutokana na heshima aliyonayo kwao ambayo haimpasi kukaa humo ndani muda mrefu kama alikuwa tayari amemaliza kile kilichomfanya aitwe.

    Bi Farida alichukua dawa za kutuliza maumivu akampatia mumewe pamoja na maji, Shafii alizinywa hizo dawa kisha akajilaza huku akiuma meno vilevile na baada ya muda alijifanya kapitiwa na usingizi ili kutuliza wahka aliyokuwa nao mkewe juu yake kwani wasiwasi ulikuwa mkubwa sana kila akimuangalia anavyouma meno kwa hasira. Bi Farida baada ya kumuona Shafii kalala alimfunika na shuka vizuri halafu akambusu usoni, alitoka chumbani akaelekea sebuleni akamkuta Jamali anaongea na simu ya mezani ambapo alipofika tu mpwa wake huyo alisema, "eeh huyu hapa ongea naye".

    Jamal alimkabidhi mkonga wa simu shangazi yake kisha akaenda kukae sebuleni kwenye kochi, Bi Farida alichukua mkonga wa simu akauweka sikioni na kuongea " ndiyo ni mama yake hapa.......hapana hajarudi nyumbani tangu muhula wa masomo ulipoanza.......nyinyi mnasema tulimtuma mtu aje kumfuata sisi hatukutuma ingawa ni kweli kulikuwa na matatizo huku nyumbani.....sawa toa taarifa ya kutoonekana kwake nyumbani wala chuoni".

    Baada ya kuongea hayo maneno kwa njia ya simu aliikata simu kisha akaanza kulia kwa sauti ya chini kutokana na taarifa aliyopewa, Jamali aliinuka akaenda kumbembeleza shangazi huku akimuuliza jambo lililomfanya alie.

    "Jamal binamu yako hajaonekana chuo tangu siku ile ya msiba wa wajomba zako na huko chuoni kwao walikuja watu wakasema wametumwa na baba Zayina kumfuata arudi kwa ajili ya msiba jambo ambalo siyo la kweli kabisa" Bi Farida alieleza huku akilia kwa uchungu sana.

    "Shangazi usilie sasa inabidi wewe ndiyo upange mkakati wa kumtafuta kwani mjomba hali yake ndiyo hiyo unaiona na hii taarifa akipewa itamletea matatizo zaidi, naamini Zayina yupo salama tu na hajadhurika hivyo tuanze kumtafuta haraka iwezekanavyo bila hata kumuhusisha mjomba"Jamal alimuambia shangazi yake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Jamali mwanangu mimi jamani, sijui wamemkosea nini mpaka wamafanyie hivyo. Oooh! Yarrabi nisaidie mimi" Bi Farida alizidi kulalamika kwa sauti tofauti na awali.

    "Shangazi sauti hiyo mjomba ataamka na asikie iwe mengine nafikiri unajua jinsi anavyompenda sana Zayina, hebu fikiria akiamka utamuweka katika hali gani kama akijua. Inabidi tutoe taatifa kwa wajomba wengine na baba ila yeye tu asiambiwe ili wasaidie katika hili" Jamali aliongea kwa upole tena kwa kusihi hadi Bi Farida akatulia akawa anafuta machozi hadi aliponyamaza.

    "Sawa nimekuelewa anko, ngoja nimpikie baba yako na shemeji Hassani ili tuje tujadili hili suala" Bi Farida alimuambia Jamali halafu akanyanyuka akaenda mezani alipoiacha simu yake ya mkononi akawapigia wahusika aliowahitaji katika kujadili hilo suala.



    Baada ya nusu saa Hamis na Hasaani walikuwa tayari wameshawasili nyumbani kwa Shafii na kikao cha watu wanne kikawekwa eneo la bustanini na wahusika wa kikao hicho wakawa ni Bi Farida, Hamis, Hassani na Jamali. Kikao kilianza kwa Bi Farida alifungua kikao kwa kueleza kils kitu juu ya taarifa aliyoipata kutoka kwa uongozi wa chuo kikuu cha Dar es salaam kisha akaeleza ushauri alioupata kutoka kwa Jamali wa kuwaita wao ili waweze kulitatua tatizo hilo.

    "Umefanya vizuri sana mwanangu kwa kumshauri shangazi juu ya hili suala" Hamis alimpongeza Jamali kisha akaendelea, "dada hili suala kwa jinsi unavyolieleza ni zito sana na linahitaji tufikirie kwa kina haswa maana huyo mtu aliyemfuata Zayina akamwambia mnamuita nyumbani anajua nini anafanya na ametumia taarifa ya msiba huu kuwa ni njia ya kumnasa".

    "Shemeji Hamis naungana na wewe katika suala hili itakuwa huyu mtu ni adui namba moja wa kaka sasa inabidi huu msako tutume watu wenyewe wauendeshe kwani tukitumia vyombo vya dola itakuwa tunaharibu tu maana hatuwezi jua huyu mtu ana nguvu gani katika serikali. Kumbuka Zayina kusoma chuo kile tulifanya siri kwa wanafamilia tu kwani tunatambua mtu maarufu ana maadui sana ndiyo maana tukawaambia watu wengine kwamba Zayina anasoma Ulaya ili tuwapoteze njia ya kumtafuta, sasa tujiulize huyu mtu ana ni nani na ana lengo gani mpaka amejua Zayina alipo na akafanya hilo alilolifanya" Hassani naye aliongea kwa mara ya kwanza katika kikao hicho.

    "Shemeji tayari mimi nishawaambia uongozi wa chuo kikuu cha Dar es salaam watoe taarifa juu ya suala hilo hivyo tayari lipo kwenye vyombo vya dola, sasa tufanyeje?" Bi Farida aliongea

    "Aaaah! Shemeji umekosea sana kufanya hivyo huoni huyo aliyemshikilia Zayina atazidi kuwa makini ili tusimjue" Hassani alimlaumu shemeji yake kwa kuwaambia uongozi wa chuo kutoa taarifa.

    "Dada hapo umekosea sana kufanya hivyo kwani alichokuwa anaongea Shemeji hapa ni sahihi kabisa kukifanya katika suala hili kwani haitakiwi kuwashirikisha wanausalama inatakiwa tutumie pesa yetu mtoto apatikane" Hamis naye alimlaumu dada yake.

    "Jamani nilikuwa nimechanganyikiwa haswa kutokana na kupokea taarifa hiyi, sasa tutafanyaje?" Bi Farida aliongea akionekana kutambua alichokifanya sicho katika kutoa taarifa ya kuwaambia uongozi wa chuo.

    "Hukutakiwa kufanya hivyo dada" Hamis alimlaumu dada yake.

    "Baba na mjomba hili suala limeshatokea na haliwezi kuwa halijatokea yaani tukubali Shangazi alikosea kuwaambia uongozi wa chuo kuto taarifa polisi lakini tusimlaumu kwa kufanya hivyo maana huo muda wa kulaumiana hamna, cha msingi ni kukaa na kujadili hilo tufanye nini ili Zayina apatikane jamani" Jamali kwa mara ya kwanza aliongea baada ya kuwasikiliza wakubaa zake, maneno yake yalionekana kuwaingia mjomba wake na baba yake hadi wakakaa kimya kwa muda wakijifikiria halafu wakatazamana na wakapeana ishara ambayo hakuna yoyote aliyeiona.

    "Sawa mwanangu nimekusikia tuachienu hili suala tulishughulikie naamini Zayina atapatikana ndani ya muda mfupi tu" Hamis huku baada ya kushusha pumzi, Hassan naye alikubaliana na maneno naye.

    "nafikiri hili suala lipo kwetu na tutalifanyia kazi sasa naomba Kaka asijue juu ya hili" Hassani naye aliongea kisha akasimama pamoja na Hamis.

    "Shemeji yupo wapi tukamjulie hali kidogo kwani kuja huku bila kumjulia hali si jambo jema" Hamis aliuliza

    "Yupo chumbani kapumzika baada ya mgongo kushtuka, nafikiri atakuwa kashaamka twendeni mkamuone" Bi Farida aliwaambia huku akinyanyuka kwenye akaelekea ndani, Hamis na Hassani walikuwa nyuma wakimfuata.

    Wote kwa pamoja walielekea chumbani kwa Shafii ambapo walimkuta akiwa tayari ameamka.

    "Karibuni jamani" Shafii aliwakaribisha

    "Asante Chumbio" Hamis aliitikia ukaribisho huku akikumbushia jina la utani la Shafii, Hassani na Bi Farida wacheke.

    "hilo jina husahau tu Bonoeza" Shafii naye aliongea huku akitia jina la utani la Hamisi nakupelekea wote wacheke humo ndani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Bonoeza siku hizi umelizoea si ulikuwa ukiitwa unarusha mawe kaka" Bi Farida naye aliongea huku akicheka na kupelekea wote humo ndani wacheke sana.

    "Ila hilo jina umenikumbusha mbali sana niliwahi kumpiga mwenzangu tukichunga mbuzi kisa hilo jina, ila toka naingia kwenye ujana hadi utuzima naona kawaida tu" Hamis aliongea huku akicheka.

    "Haya jamani ngoja niwaache na soga lenu la kiutuzima" Bi Farida aliongea kisha akatoka humo chumbani akiwaacha Kaka yake, mume wake na shemeji yake.

    Alipofunga mlango wa chumbani mwake mada ikabadilika papo hapo na ikaongelewa mada inayowahusu hao wanaume watatu waliokuwa na ukaribu tangu utotoni, mambo yao mengi ya siri walikuwa wakiambizana na hata mengine mazito walishirikiana.

    " kajua Zayina anashikiliwa na mbaya wetu ambaye bado hatujamtambua" Hamis alimuambia Shafii

    "Natambua sana kama anajua hilo kwani wakati anaongea na simu sikuwa nimelala kama anavyofikiri na hata alipolia kwa sauti na kulalamika nikawa namsikia" Shafii aliwaambia.

    "Hiii ni balaaa haswa inabidi tumtafute mtaalamu mwenye uwezo wa kudhibiti majini maana anayefanya haya si mwanadamu wa kawaida" Hassani aliongea.

    "Hilo ndiyo la kufanya inabidi atafutwe mtaalam ila asiwe mzee Mahmud maana yule mzee atatuvua nguo tuaibike kwanza halafu ndiyo atusaidie maana tiba zake hufanya kazi ukiongea ukweli tu, sasa sisi hatuko tayari kuvuliwa nguo" Shafii aliongea

    "Kweli kabisa bwana Shemeji ni bora kufa na matatizo yetu shingoni kuliko kukubali kuvuliwa nguo" Hamis alidakia baada tu ya Shafii kumaliza kauli yake.

    "Jamani hili suala tupiganeni hadi kufa maana wataalamu ni wengi hapa Tanga tena leo hii nimepata taarifa kuna mtaalam mwingine anaitwa Mafindo yupo Pangani nasikia huyo ni kiboko ninahisi ndiyo itakuwa mwisho wa matatizo" Hassani aliongea

    "Enhee Hassani umenena haswa naona mkitoka hapa muanze huko au mnasemaje jamani na ningekuwa mzima ningeungana nanyi" Shafii aliafikiana na Hassani.

    "Sawa naona tusipoteze muda bali twende huko ili mambo yasiwe mabaya" Hamis alisema kisha akanyanyuka akampa mkono Shafii na Hassani naye akafanya hivyo hivyo.

    "Kila la heri jamani" Shafii aliwaambia kuwatakia heri katika mpango huo wanaoenda kuufanya, Hamis na Hassani waliondoka upesi ili wawahi kurudi kwani Pangani kulikuwa mbali na muda ulikuwa umeenda sana.







    SURA YA SITA

    Hali ya hewa ilikuwa ni tulivu sana na mawingu ng'amba yalikuwa yamepamba anga zima na kulifanya jua lisionekane kabisa na kuweka hali ya kivuli na kuwafanya wakazi wa jiji la Tanga kuwa na ahueni ya joto haswa kwa wale wanaotembea kwa miguu pembeni mwa barabara. Hamis na Hassani walikuwa wapo ndani ya gari binafsi wakielekea Pangani na muda huo tayari walikuwa wanaimaliza barabata ya Taifa wakiingia katika mzunguko wa magari unaounganisha barabara nne zikiwemo barabara ya Taifa, barabara ya Pangani, barabara ya jamhuri na barabara iendayo kukutana na barabara ya Chuda. Waliuzunguka mzunguko huo wa unaounganisha barabara hizo na wakafuata barabara ya pangani kwa mwendo wa wastani kutokana na uwepo wa baiskeli nyingi zikiwa zimebeba wasafiri, walitembea kwa mwendo huo hadi walipofika jirani na duka la dawa la Mang'ombe. Hapo walijikuta wakiingiwa na moyo wa huruma na kusimamisha gari baada ya kijana mwenye asili ya kisomali aliyekuwa amevalia kinadhifu alipowapungia mkono kuwasimamisha, waliegesha gari pembeni na kijana huyo aliwaomba wamsaidie afike Pangani kwani alikuwa ameibiwa pesa yake yote ambayo ingemtosha kuifanya nauli ya kuelekea huko. Kijana huyo alikubaliwa kwa moyo mkunjufu kupanda gari hilo kutokana na moyo wa kusaidia watu alionao Hamis, alipanda kwenye gari akakaa kiti cha nyuma na safari ikaendelea kama kawaida. Njiani maongezi yalitawala kwenye gari hilo kutokana na ucheshi mkubwa aliokuwa nao huyo kijana ambao uliwavutia sana kwani alitokea kuchangamsha safari yao isionekane imepooza, Hamis ndiye alikuwa dereva wa gari hilo na alionekeana kutendea gia za gari hiyo kwa kubadilisha gia moja na kwenda nyingine na mwendo wa gari aliuzidisha kutokana na uchache wa magari.

    Baada ya mwendo takribani saa moja wakiwa njiani mvua kubwa ilianza kunyesha na ikamlazimu Hamis apunguze mwendo ili kuepuka ajali kwani mvua hiyo ilifanya kioo cha gari kiweke ukungu kwa ndani na kusababisha iwe tabu kuona mbele, ukungu ulipozidi Hassani aliufuta kwa kitambaa kilichopo ndani ya gari.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Dah hili eneo kila nikipita huwa nakuta mvua" Yule kijana aliongea

    "Labda ulipita kipindi cha mvua tu ila si kila muda tu linakuwa na mvua, hivi unaelekea Pangani sehemu gani?" Haasani aliongea kisha akamuuliza swali huyo kijana.

    "ninaelekea Kuani kumuona babu yangu maana ni muda sijamtembelea" Yule kijana alimjibu.

    "Imekuwa kama bahati na sisi tunaelekea hukohuko sasa nafikiri utafika moja kwa moja hadi huko, si tunaenda kumuona mzee Mafindo nafikiri unamfahamu" Hamis naye aliongea huku akibadilisha gia ya gari.

    "Said Humud au ukipenda gaza wa mafindofindo, ndiye babu yangu ninayeenda kumtembelea imekuwa kama bahati yaani ila bahati hii imeingia dosari" Kijana huyo alianza kuongea kwa uchangamfu hayo maneno yake lakini mwishowe akamaliza akiwa amekunja sura na macho yakawa mekundu.

    "Kijana unamaanisha nini?" Hassani aliuliuza huku akimtazama yule kijana lakini alijikuta na hofu zaidi baada yakuona sura ya yule kijana imebadilika na kuwa ya hasira"

    "Unataka kuelewa siyo? Haya ngoja nikueleweshe" Yule kijana alisema kisha akajibadilisha sura na kuwa ya mtoto yule aliyewatokea watoto wa mzee Buruhan muda mfupi tu kabla hawajafa kwa kuuawa na mikono yake.

    "Ushaelewa au bado unataka uelewe zaidi" Yule mtoto alimuambia Hassan ambaye alipatwa na mshtuko sana baada ya kuiona sura ya yule mtoto.

    "Jamadin! Hapana siyo wewe" Hassan alisema na kupelekea Hamis naye ageuke aangalie kwani aliona kama ameangalia vibaya alipotumia kioo cha kati, Hamis alijikuta akikanyaga breki ya gari lakini gari halikusimama bali ndiyo lilizidi mwendo.

    "Hamuwezi kunikimbia nyinyi wanaharamu na huu ndiyo mwisho wenu" Yule mtoto wanayemtambbua kwa jina la Jamadin aliongea kwa hasira kisha akamuangalia Hassani akamuambia, "nipe kile ".

    "Si....sina"Hassani aliongea kwa uoga huku akiweka mikono ishara ya kuomba msamaha lakini alijikuta akipigwa shingoni na mkono wa yule mtoto hadi kichwa chake kikakatika na kuruka kwenye mapaja ya Hamis na damu zikawa zinatoka kwa wingi, Hamis alijikuta anatoa yowe la woga baada ya kichwa cha Hassani kutua kwenye mapaja yake hadi akajikojolea papo hapo.

    "Mjomba leo ndiyo unakuwa na uoga siyo wakati mlipokuwa mkifanya yenu wala hakuwa unaogopa, nadhani umetambua kuwa ubaya huzikwi nao bali unalipwa hapahapa na leo ndiyo hukumu yako" Yule mtoto aliongea kisha akampiga Hamisi ngumi ya kichwa iliyotoboa kichwa chake hadi ubongo na mabonde ya damu yakaruka kwenye kioo cha mbele.

    Huo ndiyo ukawa mwisho wa Hamis na Hassan katika dunia hii baada ya kupatiwa malipo kwa kila walichokitenda kwani ndiyo mwisho wa yoyote afanyaye balaa kana walilolifanya wao, hakika mshahara wadhambi ni mauti kama wahenga walivyonena tangu zamani na ndiyo kilichowapata Hassani na Hamis.

    Siku zote mchimba kaburi huingia mwenyewe ndiyo atafanikiwa kulichimba haitotokea mchimbaji wa kaburi akachimba kaburi na kulimaliza pasipo kuingia yeye mwenyewe, Hamis na Hassani hivyo hivyo ni wachimba kaburi waliochimba kaburi na wakaingia ndani yake na matokeo yake wakakutwa na kisanga kizito kilichosababishwa na uchimbaji wao wenyewe. Walichimba kaburi pasipo kujua kama kaburi hilo litakuja kuwazika wenyewe na wamekuja kujua kuwa kaburi hilo ni kaburi lao wenyewe na wamekuja kujua tayari wameshachelewa, laiti wasingefanya hivyo tangu awali wangekuwa ni miongoni mwa waliosalimika hadi muda huo.



    ****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya dakika takribani kumi tangu Hassani na Hamisi waiage dunia, hali ilikuwa shwari katika jiji la Tanga na hakuna aliyekuwa na habari ya kutokea kwa tukio la kinyama katika barabara ya Pangani likiwahusisha watu maarufu waliouawa kinyama kutokana na kisasi kizito cha mabaya waliyoyafanya kipindi cha nyuma. Nyumbani kwa mzee Buruhan muda huo alitembelewa na rafiki yake kipenzi aitwae Mahmud ambaye anafahamika sana huko Mkinga kama mganga maarufu sana na aliyetatua matatizo mengi yaliyowakumba watu na familia zao na hata yenye utata. Mzee huyu alikuja kwa lengo la kumpa pole rafiki yake kipenzi kutokana na vifo hivyo kwani hakuwepo ndani ya Tanga kipindi msiba unatokea na ndiyo amerejea na ameamua kupitiliza nyumbani kwa rafiki yake moja kwa moja baada tu ya kupumzika nyumbani kwake. Mzee Mahmud alikaribishwa kwa utiifu na rafiki yakr kipenzi na akapatiwa kinywaji anachokipendelea kila awapo nyumbani kwake, alikaribishwa kahawa na rafiki yake huyo kisha wakachukua bao wakaenda kwenye kibaraza cha nyumba ya mzer Buruhan wakakaa na wakaanza kucheza kama ilivyo kawaida yao.

    "Mzee mwenzangu unajua kazi zetu hizi za kuagua zilinitoa huku Tanga nilipozaliwa na kukulia hadi Mombasa nikaenda kumuagua bwana mmoja aliyetupiwa jini zito, basi hiyo shughuli ilinichukua mwezi na nusu na hadi namaliza huku mshazika ndiyo maana hukuniona" Mzee Mahmud aliongea huku akiwa na kikombe cha kahawa mkononi.

    "pole na majukumu mzee mwenzangu ndiyo kama nilivyokueleza yaliyonifika na hata sijui chanzo chake nini?" Mzee Buruhan aliongea kwa unyonge.

    "haina haja ya kuhuzunika mzee mwenzangu bali inabidi uwalaumu wanao na janga hili mzee mwenzangu limeanzwa na wao na sasa mwenzao wanalimaliza" Mzee Mahmud aliongea kisha akanywa kahawa funda moja bila hata kumtilia maanani Mzee Burhan aliyeonekana kutoielewa kauli hiyo.

    "Mzee mwenzangu mimi ni rafiki yako wa muda mrefu sana na kuhusu hili suala jua mwanao mkubwa analielewa fikra, na kama yupo tayari kuliweka bayana utabaki na nguzo tu lakini kama hataki kuliweka bayana hutabaki na nguzo hata moja" Mzee Mahmud alizidi kuongea maneno yaliyomfanya Mzee Buruhan abaki akimtazama kwani anamtambua fika ni mganga mwenye uwezo mkubwa wa kujua yaliyojificha.

    "Sijakuelewa mzee mwenzangu" Mzee Buruhan alisema huku akimtazama Mzee Mahmud kwa umakini, Mzee Mahmud alipotazamwa alitoa tabasamu tu kisha akasema, " zamu yako kucheza mimi nishalala mzee mwenzangu".

    Mzee Buruhan aliacha kumtazama akaliangalia bao kisha akachukua kete akaanza kucheza huku akiwa njia panda kutokana na kauli ya Mzee Mahmud ambaye huwa hafafanui akishaeleza mambo kama hayo halafu akabadili mada ghafla.





    ****





    Maneno ya mzee Mahmud bado yalibaki ndani ya kichwa chake ingawa yalikosa ufafanuzi wa kutoka kwa mzee huyo aliyebobea katika uganga, Mzee Buruhan aliendelea kucheza bao huku akiwa na mawazo sana juu ya  maswali ya maneno ya utata aliyoambiwa  na mzee Mahmud. Hadi alipolala katika mchezo huo wa bao bado mawazo lilikuwa juu ya maneno hayo, mzee Mahmud alipoanza tena kucheza bao huku ameinamisha kichwa chake  akitazama kwenye bao kwa umakini hakujua kama mzee mwenzie alikuwa akimtazama sana kichwani mwake na alitamani hata akione ndani hicho kichwa chake ili atambue ni nini anachowaza lakini suala hilo lilishindikana kabisa kwani yaliyomo katika ubongo wa mtu huwezi kuyaona hata ukipasua kichwa chake na kuangalia ndani.

    "Kuna kisa cha zamani sana mzee mwenzangu nakikumbuka hadi leo hii katika kichwa changu, hakika wahenga hawakukosea kukitunga kwani ni kisa kinachohusu vijana wawili waliompenda msichana mmoja kigori huko mashariki ya mbali" Mzee Mahmud alianzisha mada nyingine huku akiendelea kucheza bao na safari hii alikuwa anamtazama mzee Buruhan usoni mwake akiwa na tabasamu hafifu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mzee mwenzangu kama kawaida hukaukiwi visa vyenye mafunzo na kuburudisha, hebu nipe habari bwana" Mzee Buruhan alimuambia mzee mwenzie ili apate kusikiliza kisa kutoka kwake kwani mzee Mahmud alikuwa akijulikana kwa jinsi alivyokuwa hodari kwa kusimulia visa na hadithi zenye kufundisha, hakika taaluma ya fasihi simulizi ya wakati wa zamani bado ilikuwa ipo ndani ya halmashauri ya ubongo wake ingawa alionekana kuzeeka sana.

    "Katika kijiji kimoja cha jamii ya wastarabu alizaliwa binti mmoja mrembo sana aliyeitwa Giguna katika familia yenye hadhi duni sana katika Jamii ya Watarabu, binti huyo alianza kuwa gumzo kijijini happ tangu akiwa mdogo kutokana na uzuri aliokuwa nao uliokuwa wa ajabu sana. Hadi anavunja ungo  ilikuwa ni habari nyingine katika kijiji hicho kwani vijana wa rika lake walikuwa wakimtamani kila kukicha kutokana na umbo maridadi alilokuwa nalo, haikuwahi kutokea binti mwenye umbo kama lake ambalo lilijaa utata mtupu tena alijaliwa kuwa na kiuno kilichojitenga kama mdudu Mavu. Usoni alikuwa na sura  yenye mvuto wa ajabu sana na jicho lenye umbo la nusu mwezi,  Giguna alikuwa ni binti mrembo haswa na kila alipokuwa akiwatazama wavulana wa rika lake walidhani kuwa wanaitwa lakini haikuwa hivyo bali asili ya jicho lake ndiyo lilimchengua sana kila mvulana. Ilipotimia majira manne ya mwaka katika kijiji hicho walihamia familia ya wasafiri kutoka mbali ambao walipenda sana kuweka makazi katika kijiji hicho na walipewa ukaribisho mkubwa kutoka kwa kiongozi wa kijiji hicho, familia hiyo nayo ilikuwa gumzo kijiji hapo kutokana na kuwa na kijana aliyekuwa na mvuto wa ajabu na usafi uliopitiliza kuliko hata vijana wengine wa kijiji hicho.  Kijana huyo alijulikana kama Mufedi ambaye alikuwa na asili mchanganyiko iliyomfanya awe na nywele za kipekee sana ambazo hata angeishi bila chanuo basi zingeonekana ni nzuri sana na zipo  kama zimechanwa. Mufedi alikuwa ni mtu wa kukaa na vijana wenzie wa rika lake hadi wakamzoea kutokana na ucheshi wake alionao ambao uliwafanya vijana wenzake wafurahi kila kukicha, ndani ya muda mfupu tu katika kijiji hicho tayari Mufedi alikuwa yupo midomoni mwa mabinti wa kijiji hicho kama ilivyo kwa Giguna alivyokuwa yupo katika midomo ya wavulana wa kijiji hicho. Ilifika kipindi hata wasichana wa kijiji hicho wakawa wanakuja nyumbani kwao Mufedi na kumsaidia mama yake Mufedi kazi mbalimbali wakiwa na lengo tu la kuiona sura ya Mufedi jinsi ilivyokuwa ni nzuri na yenye kuvutia, baadhi ya wasichana waliokuja hapo nyumbani kwao Mufedi na kumuona akiwa sehemu kubwa ya kifuani mwake haijastiriwa walikiri kwamba alikuwa ni mvulana mwenye uzuri wa ajabu. Maneno ya chini kwa chini juu ya uzuri wa ajabu alionao kijana huyo yalienea hapo kijijini kama ilivyokuwa akisemwa Giguna na wavulana wa kijiji hicho, muda wote huo si Giguna wala Mufedi aliyewahi kumuona mwenzake kwa macho na kila mmoja alisikia sifa za mwenzake kupitia marafiki zake. Siku moja ambayo ndiyo ilikuwa chanzo cha kuanzishwa kitu ambacho hakikutarajiwa kuanzishwa ndiyo siku ambayo wawili hawa kwa mara ya kwanza walionana, siku hiyo Mufedi alikuwa akiongea na marafiki zake vipenzi walioitwa Nikeze na Nunele. Giguna siku hiyo aliagizwa kupeleka mzigo nyumbani kwao Mufedi baada ya wazazi wake na mufedi kufanya biashara ya kubadilisha mali kwa mali kwani kipindi hicho bado fedha zilikuwa hazijaanza kutumika. Ilikuwa ni muda mrefu Giguna alikuwa hajaonekana kutokana na kuwasaidia sana wazazi wake na bibi yake kazi za hapo nyumbani kwao, eneo alilopita ndiyo walikuwa wamekaa Mufedi, Nikeze na Nunele wakipiga soga na kuchia vicheko. Giguna alipokaribia Nikeze alimuita lakini hakuitikiwa ndipo Nunele alipomuita akasimama kutokana na heshima aliyokuwa nayo, Nunele na Giguna walikuwa ni ndugu wa damu na Nunele ndiyo mkubwa kwa Giguna. Hivyo Giguna alijongea hadi walipo akiwa amejitwisha furushi kichwani  lililokuwa na mzigo aliotumwa kuupeleka, hapo ndipo kwa mara ya kwanza Giguna alimuona Mufedi na Mufedi alimuona Giguna na wakaongea kwa lugha ya macho na nyoyo pasipo wengine kutambua wanachozungumza.

    "Giguna u waitwa wanyamaza si vizuri hivyo" Nunele alimuambia Giguna baada ya kunyamazia salamu ya Nikeze.

    "Kaka nataka wahi nilipotumwa niweze wahi rejea" Giguna aliongea kwa sauti nyororo huku akimtazama Mufedi kwa jicho la kuibia.

    "hapana dada sifanye hivyo muache wslau akusindikize kidogo tu hutachelewa kurudi" Nunele alimuambia kisha akampa ishara Nukeze amfuate Giguna, Nukeze hakufanya ajizi alimfuata Giguna na taratibu akaanza kwenda huku akiongea kwa maneno ambayo hayakusikiwa na yoyote zaidi yao wenyewe. Huo ndiyo mwanzo uliozua safari nyingine kabisa isiyosafiriwa kwa umbali mrefu, ilikuwa kama ukurasa ila haukuwa na karatasi. Siku na siku zilisogea na hatimaye dalili za dhahiri kabisa zikachipuka na kuonesha kila mmoja alikuwa akimuhitaji mwenzake, katika msogezo huo wa  siku ndipo ikafika siku ambayo haitasahaulika kwenye ukurasa mpya wa upendo ulioanza kuchipuka katika mioyo yao"   Mzee Mahmud aliweka kituo hapo katika kusimulia na kumuangalia Mzee Buruhan  ambaye alionekana kuwa na hamu ya kuendelea kuisikiliza hicho kisa anachosimuliwa.

    "Aaaah! Mzee mwenzangu wakatisha pasipo stahiki kukatishwa" Mzee Buruhan alimlaumu mzee Mahmud kwa kukatishiwa uhondo mwanana uliokuwa unapita kwenye masikio yake na kujenga taswira kwenye ubongo wake kama vile alikuwa anaangalia sinema ya kile anachosimuliwa na kusikiliza simulizi tu.

    "Weka mafuta kwanza tuendelee na safari huoni kikombe kitupu hicho na birika lina mafuta tele ya kunifanya niendelee kutoa burudani" Mzee Mahmud alimuambia mzee Buruhan huku akimpa kikombe chake cha kahawa ili aongezewe kahawa aweze kuendelea kusimulia.

    "simulia walau kidogo basi mzee mwenzangu huku nakuongezea kahawa"  Mzee Buruhan alimuambia Mzee Mahmud akiwa amenyanyua birika la kahawa ili amuongezee kahawa.

    "Basi bwana siku hiyo si wakaombana namba za simu ili waweze kuongea vizuri maana ya vijana unayajua" Mzee Mahmud aliamua kusimulia kitu kingine kabisa tofauti kabisa na kufanya Mzee Buruhan amtazame kwa mshangao.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ushaanza visa vyako tayari mzee mwenzangu, sasa umesema zamani na hizo namba za simu zimeingia vipi" Mzee Buruhan alimuambia Mzee Mahmud huku akianza kucheka.

    "Sasa si wewe  unalazimisha gari kwenda wakati mafuta yamekwisha, umeona wapi likatembea  huku likisubiri mafuta" Mzee Mahmud aliongea huku akicheka kidogo na kusababisha Mzee Buruhan acheke kwa nguvu kutokana na vituko vya mzee mwenzake.

    "Yaani mzee mwenzangu hubadiliki kabisa tangu upo kijana tabia ni zile zile tu" Mzee Buruhan aliongea huku akimtilia kahawa mwenzake.

    "ewaaa! Mambo si hayo sasa twende kazi" Mzee Mahmud aliongea huku kisha akinywa kahawa kidogo.

    "sasa endelea mzee mwenzangu usikatishe habari" Mzee Buruhan alimuambia.

    "Siku hiyo ilikuwa ni majira ya jioni baads ya jua kuzama, Giguna alicheleewa kuchota maji mtoni na ikambidi akimbie mara moja mtoni ili walau apate maji ya kuoga kwa usiku wa siku hiyo kwani ilikuwa ni kawaida kulala akiwa nadhifu usiku. Alipofika mtoni ndipo akakutana na Mufedi akiwa na kabeba  vazi lake la juu lilionekana kuloa na alibakiwa na shuka kubwa aliyojifunga kiunoni iliyofika juu ya kitovu, kitendo cha wao kuonana tu walibaki wakitazamana tu kwa muda mrefu bila hata kusema chochote. Walikuwa wapo kwenye njia nyembamba iliyochongwa baada ya miguu ya watu kukanyaga nyasi hizo kwa muda mrefu hatimaye baadhi zikakauka na kufanya njia, ilikuwa lazima mmoja ampishe mwenzake kwenye  hiyo njia ili apite kwani haikuwa inatosha kupishana. Kwa ufinyu wa njia hiyo hakuna aliyefanya hivyo wote walisimama tu wakizamana tu hatimaye Mufedi akajikaza akamshika Giguna bega, walisogeleana karibu zaidi  na muda huo hakuna yoyote aliyetambua nini wanafanya kwani walijikuta wamefikwa na hisia za ajabu kila mmoja kutokana upendo walionao kwa mwenzake. Ule usemi aliousema nabii wa Mungu kwamba kwenye watu wawili wa jinsia tofauti basi watatu wao atakuwa ni ibilisi ndiyo ulijidhihirisha hapo na wakajikuta wameingia sehemu isiyotakiwa kuingilika, tangu siku hiyo ndiyo ukurasa haswa wa mapenzi ya dhati baina yao ukafunguliwa  na mapenzi ya siri  baina yao yakawa yanaendelea. Katika kipindi hicho ndipo Mufedi alipokuja kubaini kwamba Nukeze alikuwa akimtaka Giguna kwa muda mrefu lakini hakukubaliwa kabisa ndiyo maana hata siku ile alipomuita hakuitika kutokana na kuchoka  usumbufu wake, mapenzi baina yao yaliendeshwa kwa usiri mkubwa na hawakumueleza yoyote hadi pale siku moja mmoja wa watu hapo kijijini alipokuja kubaini uhusiano huo. Ginota rafiki kipenzi wa Giguna ndiye mtu aliyekuja kufahamu uhusiano huo baada ya kuwakuta wakitoka kuvuja ile amri sijui ya ngapi  ya imani ya wenzetu hao, siku hiyo ilibidi Giguna amuambie ukweli juu ya uhusiano wao na akamuapiza kumtunzia hiyo siri pasipo kujua anamuaminisha nyoka. Giguna jambo ambalo hakuwa analijua ni kwamba Ginota ni mmoja kati ya wasichana  waliokuwa wamezama kabisa katika kumpenda Mufesi lakini hakuwahi kumuambia Giguna kwasababu ana mahusiano na Nunele na laiti angemwambia ungekuwa ugomvi kati yao kwani Giguna asingekuwa tayari kuona kaka yake Nunele anasalitiwa. Pia katika jambo ambalo Giguna hakulitambua ni kwamba Nukeze alikuwa akimtumia sana Ginota katika kumshawishi  Giguna amkubali lakini jitihada hizo ziligonga mwamba kwani macho ya Giguna hayukutamani hivyo moyo wake haukuhitaji, kumbuka macho yasipotamani moyo hauwezi kuhitaji. Ginota hakuweza kustahimili kuona rafiki yake kampata mwanaume aliyekuwa anagombewa hapo kijijini na wasichana wote kama vile ni lulu yenye thamani, Ginota aliifikisha habari hiyo kwa mpenzi wake Nunele na kupelekea taarifa hiyo ifike kwa Nukeze. Hapo ndipo vita mpya ya mapenzi ilipoanza chini kwa chini, Nunele na Nukele walikuwa wanacheka na Mufedi kwa jino pembe tu lakini walikuwa wakipanga kumuua Mufedi kila muda lakini ilishindikana na kila walipoenda kwa waganga  ili wamuue kazi yao ilikataliwa na mwisho wake wakafanya kitu ambacho kilimuumiza sana Mufedi na ikawa ndiyo mwisho wa mapenzi ya Giguna na Mufedi. Waliamua kwenda kwa mganga wakafanya dawa ili ambayo walimtilia Giguna kwenye maji ambayo alikuwa anakunywa na alipoyanywa ndiyo ikawa mwanzo wa Giguna kumpenda Nukeze na Mufedi kukosa penzi lake baada ya kukataliwa wazi na kutolewa maneno yasiyofaa na Giguna. Mufedi alidhani utani lakini alikuja kujua ni kweli baada ya kutaka penzi mtoni wakati Giguna alipoenda kuchota maji, Giguna alipiga kelele ya kuwa anavakwa na kusababisha watu wajae na Mufedi aliambulia kipigo nusura afe. Tangu siku hiyo Mufedi hakumgusa tena  Giguna na alipopona tu aliondoka kijijini hapo akiiacha familia yake baada ya wanakijiji kutomuhitaji, huo ndiyo mwisho wa kwanza wa simulizi hii na muendelezo utaujua mzee mwenzangu tuombeane uzima tu" Mzee Maud aliishia hapo kuelezea simulizi hiyo.

    "Mzee mwenzangu unajua ninamuonea huruma sana huyo kijana yaani naona kama nimefanyiwa mimi hivyo" Mzee Buruhan aliongea baada ya kuisikiliza hiyo simulizi kwa umakini.

    "Fahari yetu waswahili kujaliwa sanaa inayokuteka akili zako ukaona kama tukio ni la kweli" Mzee Mahmud aliongea huku akimalizia kikombe cha kahawa.

    "Yaani hata bao nimesahau kulicheza" Mzee Buruhan aliongea huku akitabasamu.

    "Mzee mwenzangu huku leo silali naondoka maana narudi Mkinga leo leo nimekuja kukupa pole tu ujue sijakutupa rafiki yako wa toka utotoni" Mzee Mahmud alisema huku akinyanyuka kivivu.

    "Haya mzee mwenzangu ngoja nikuitie kijana akutoe na usafiri hadi Makorora ukapate gari ya  kurudi nyumbani" Mzee Buruhan alimuambia mzee  Mahmud.

    "Hasbuk mzee mwenzangu shukran sana muache kijana apumzike mimi nitatumia sehewa  hapo tu niende chapuchapu haina haja ya gari" Mzee Mahmud aliongea huku akitembea na Mzee Buruhan akawa anamsindikiza, walitoka hadi nje ya nyumba  eneo linaloegeshwa baiskeli nyingi za kukodisha. Mzee Mahmud alikodi moja na dereva wake akamuaga Mzee Buruhan akaondoka.





    ****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog