Simulizi
: Baba Kiumbe Wa Ajabu
Sehemu Ya Nne
(4)
ILIPOISHIA
Baada
ya kusema yale aliondoka kipande cha mti wa mnyaa sikioni na kuutupia kwenye
kapu la dawa lililokuwa pembeni
yake.
“Umesikia?”
“Ndiyo.”
“Yaliyozungumzwa yana
ukweli?”
“Ndiyo.”
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Unajijua kuwa
wewe ni maiti?”
“Maiti?” Kauli ya mganga ilinishtua
sana.
“Hujijui?”
“Sijijui.”
“Mpaka sasa hivi upo
sawa kama nduguzo?”
“Kivipi?”
“Viungo vyako vipo
sawa?”
“Vipo sawa.”
“Kipi kilichokuleta
hapa?”
“Mambo mengi.”
“Moja wapo?”
“Ni mengi ila
kubwa ni hii hali iliyojitokeza hivi karibuni ya kufa nguvu za
kiume.”
“Hujui sababu zake?”
“Najua.”
“Sasa nini
kimekuleta huku?”
“Mwenzangu alinieleza unaweza
kunisaidia.”
“Nikusaidie nini?”
”Kuitoa hali
hii?”
“Kidonda umeridhika nacho?”
“Nasikia nikikitoa
panaweza kutokea matatizo katika familia yetu.”
“Kama unajua hivyo kwa
nini unataka dawa ya nguvu za kiume?”
“Kama utajiri ni wao lakini
mapenzi ni haki yangu ya msingi.”
“Sikiliza kijana usijitoe akili,
kwa jinsi alivyokuelekeza dada yako mkubwa juu ya kupona nguvu zako za kiume,
nini kitampata baba yako?”
“Kwa hiyo nibaki na hali hii
milele?”
“Ni uamuzi wako, kupona upoteze watu au uendelee kuwa maiti
inayotembea ili kuiokoa familia yako. Na hiyo mosi familia yako sasa hivi
itakutuliza ndani kwa kupooza miguu, utakuwa wa kula na kulala wao wanaponda
maisha.”
“Eti?”
“Ukweli ndiyo huo mpango huo utatekelezwa
mara moja baada ya kuonekana umekuwa
mkaidi.”
“Sikubali.”
“Kama hukubali utafanya
nini?”
”Nitatibiwa kila kitu nihakikishe napona na litakalowatokea
watajijua wenyewe.”
“Usiseme kwa hasira, upo tayari kuisambaratisha
familia yako?”
“Nipo tayari.”
“Kwa kukupa mfano mdogo, dawa
utakayokunywa itarudisha nguvu zako za kiume, lakini ukirudi nyumbani utamkuta
baba yako yupo hoi kitandani.”
“Kitakachofuata?”
“Siku
ukifanya mapenzi ndiyo siku ya kifo chake.”
“Mmh!”
Niliguna.
“Ukweli ndiyo huo, chagua kusuka ama
kunyoa?”
Nilibakia kimya kwa muda nikiwaza nitakachokifanya na
matatizo ambayo yangeikuta familia yangu. Nilikuwa radhi kuendelea na kidonda
changu na kukosa nguvu za kiume. Lakini maelezo ya mganga kuwa wanataka
kunigeuza msukule kwa ajili ya kuendeleza mali kilinichanganya
sana.
Kufikia pale nilijikuta nikichanganyikiwa na kushindwa niegemee
upande gani, lakini niliamini maisha yangu ni muhimu kuliko kitu chochote chini
ya jua. Vilevile sikuwa tayari kumhurumia mtu aliyepanga kuniangamiza kwa ajili
ya tamaa zake za mali.
Uamuzi nilioamua ni kujitengeneza mimi na
lolote litakalotokea kila mmoja ataubeba msalaba wake.
Baada ya kukaa
kimya kwa muda mrefu mganga alinishtua.
“Vipi umeamua nini maana naona
umekaa kimya?”
“Mzee wangu mambo ni mazito kila ninalofikiria naliona
zito.”
“Kwa hiyo tuache kama ilivyo?”
“Mzee wangu huna
ufumbuzi mwingine usio na madhara?”
“Sikiliza kijana wewe unajua
matatizo ya familia yenu kuliko mimi, hebu nisaidie nifanye
nini?”
“Wewe si ndiye mtaalamu ninayekutegemea?”
“Hutaki
kunisikiliza, kwani mimi napenda kuona matatizo, lakini mambo yenyewe yamekaa
vibaya.”
“Kwa hiyo?”
“Nimekueleza yote una uamuzi wako
mwenyewe wala siwezi kukuingilia lakini ukweli ndiyo huo.”
“Basi fanya
unavyoweza.”
“Vipi?”
“Utakaloliona
linafaa.”
“Kijana acha kujitoa akili, mimi sipo hapa kwa ajili ya
kuwachagulia wateja jinsi ya kufanya.”
“Mzee wangu kwa vile mpango wao
ni mbaya kwangu naomba unisaidie mimi.”
“Kwa hiyo upo tayari kwa
lolote litakalotokea?”
“Nipo tayari.”
Leo nitaanza kukupa
dawa ya kurudisha nguvu za kiume, lakini usishtuke kusikia taarifa
zitakazokufikia ambazo zitajenga uadui mkubwa kati yako na
nduguzo.”
“Siwezi kushtuka kwa viumbe wasio na huruma na mimi, wewe
nipe hiyo dawa kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe.”
“Haya
nisubiri.”
Mganga alinyanyuka na kutoka nje, akiniacha na uamuzi mmoja
ambao nilikuwa tayari kwa lolote. Baada ya muda aliniita nje, nilitoka na
kuelezwa nisubiri kwenye kigoda. Baada ya muda nilimuona mpenzi wangu akiwa
amebeba ndoo kutoka kwenye kisima kilichokuwa pembeni ya nyumba ya
mganga.
Alipofika, mganga alimueleza ayapeleke nyuma ya nyumba na
kuyaweka kwenye beseni. Alifanya vile, aliporudi mganga alizunguka nyuma na
baada ya muda aliniita. Nilimfuata na kukuta kuna beseni lililokuwa na maji
yaliyochanganywa na dawa ya unga na majani mabichi kama ya
mnyonyo.
“Oga haya maji, kisha haya majani utajisugua sehemu zako
zisizofanya kazi, sawa?”
“Sawa.”CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Haya, ukimaliza
kuoga vitu vyote viache hukuhuku.”
“Hakuna tatizo
mzee.”
Mganga aliondoka na kuniacha nikivua nguo na kuanza kujimwagia
maji kwa mikono huku nikijisugua kwa majani yale mabichi sehemu zangu za siri
zilizokwisha nguvu. Baada ya kumaliza kuoga nilirudi kwa mganga, alinielekeza
nikae kwenye kigoda kisha alizunguka nyuma ya nyumba, sikujua anakwenda kufanya
nini, mara alirudi akiwa ameshikilia majani niliyojisugulia na kuingia kwenye
kilinge chake. Baada ya muda aliniita.
Niliingia kibandani na kuketi
kwenye ngozi ya ng’ombe, baada ya kuketi mganga alinipa maji yaliyokuwa kwenye
kikombe cha plastiki. Nilikunywa maji yale kisha nilimrudishia kikombe, baada ya
kukipokea alisema:
“Sasa nafikiri kazi tumemaliza, weka hapo kwenye
kikapu kiasi chochote kama sadaka kwa mizimu.”
Nilichomoa pochi na
kuweka elfu hamsini, baada ya kuweka mganga alisema:
“Mpaka sasa kwenu
kuna hali ya sintofahamu, inaonesha hapa baba yako ameanguka dukani na
anarudishwa nyumba. Ukitaka kumuua haraka baba yako ukikutana na mpenzi wako
haimkopeshi, salamu utasikia.”
“Sasa mganga kama ni hivyo kuna faida
gani ya kuja kwako?”
“Nilikuwa nakujulisha tu, litakalotokea
usishangae, kesho asubuhi njoo haraka maana kuna vita nzito itakayotokea.
Itakuwa mara mbili ya leo, ningeweza kukutengenezea zindiko lakini siwezi
kufanya kazi mbili kubwa kwa wakati mmoja.”
“Hakuna
tatizo.”
“Basi wewe nenda nyumbani, kama unaweza usionane nao
watakutafuta sana ili kuhakikisha baba yenu anarudi katika hali ya kawaida. Na
kurudi kwa afya ya baba yako, huchukui muda unakuwa msukule wa familia wa
kuwaingizia pesa.”
“Siwezi kukubali, kama nimepona nitaendelea na
mpenzi wangu kwa vile bila yeye nisingeweza kupona.”
“Pia kuna kitu
cha ajabu kitamtokea baba yake, sumu ya uchawi itamgeuza kiumbe cha
kutisha.”
“Vyovyote atakavyokuwa mimi hainihusu, yule sasa ni adui
yangu na si mzazi wangu,” pamoja na maneno yale kuwa ya kutisha sikuingiwa
huruma kwa vile wao walitafuta uhai wangu.
“Hiyo ni juu yako kwa vile
yote nimekueleza bila kuacha kitu.”
*****
Baada ya maelezo ya mganga, nilitoka na
kumpitia mpenzi wangu na kuondoka, tulipofika Pasiansi tulitafuta sehemu kupata
chakula kutokana na njaa iliyokuwa ikituchonyota.
Wakati wa kula
nilijikuta mtu mwenye mawazo mengi, kitu kilichomshtua mpenzi wangu na kutaka
kujua kulikoni.
“Masalu kuna nini mbona unaoneka una mawazo
mengi?”
“Ni kweli, nina mtihani mzito.”
“Upi
huo?”
“Kuhusiana na hali yangu, kama nilivyokueleza, kuna mambo mazito
yamejitokeza.”
Sikuwa na jinsi nilimueleza kila kitu, sikutaka
kumficha kwa vile msaada wake ndiyo uliofichua yote. Baada ya kunisikiliza
alishtuka sana.
“He!”
“Ndiyo hivyo nikubali ili nigeuzwe
ndondocha au niokoe maisha ya baba na familia kukutwa na matatizo
mazito.”
“Mmh! Huo mtihani, lakini maisha yako ni muhimu kuliko kitu
chochote.”
“Nami ndiyo nimefanya hivyo, ila mganga ameniomba leo
nisionane nao ili kesho turudi mapema kwake.”
“Hakuna haja ya
kuhangaika, tutafute gesti yoyote nzuri hapahapa Pasiansi ili kesho turudi kwa
mganga mapema.”
“Kweli wazo zuri, basi tufanye
hivyo.”
Nilikubaliana na mpenzi, wangu baada ya chakula tulitafuta
nyumba ya wageni yenye hadhi na kupanga pale.
Siku ile tulishinda na
kulala pale, majira ya saa tano za usiku dada alinipigia simu, nilitaka kuacha
kuipokea lakini niliamua kuipokea.
“Haloo.”
“Haloo
Masalu.”
“Shikamoo”
“Marahaba.”
“Unasemaje?”
“Masalu
upo wapi?”
“Una shinda gani?”
“Masalu umefanya
nini?”
“Kuhusu nini?”
“Unataka kumuua
baba?”
“Kumuua kivipi?”
“Masalu baba akifa utamla
nyama.”
“Kama mlivyo mla nyama dada
Monika?”
“Nini?”
“Umenisikia vizuri.”
“Wee fanya
mzaha, lakini ole wako baba afe.”
“Na wewe ole wako siku ukisogeza
pua yako kwangu utanitambua mimi ni nani mwanga mkubwa we, kwanza nilikuwa
nakuchekea sasa hivi sikupendi nakuchukia ni adui yangu namba moja na taarifa
zako nazipeleka polisi.”
“Polisi! Utawaambia nini?”
“Kwamba
wewe na wenzako ni wauaji.”
“Tumemuua nani?”
“Dada Monika na
mtoto wako na ushahidi wa sehemu ulipoziweka hizo maiti ninao na lazima
mtanyongwa mwaka huu.”
“Masalu usifike huko hali ya baba ni mbaya
sana, hebu rudi nyumbani tujue tufanye nini,” ilibidi arudishe sauti
chini.CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nirudi
mnimalize.”
“Tukumalize?” Alijifanya kushtuka.
“Eeh, baada
ya kuniua nguvu za kiume sasa mnataka kunigeuza msukule.”
“Ha! Masalu
nani kakudanyanya hivyo?”
“Dada hakuna siri duniani, yaani pamoja na
kunipa kidonda hamkuridhika pamoja na utajiri na maisha mazuri kupitia mwili
wangu. Mkaamua kuniua nguvu za kiume ili nisiwe na thamani yoyote dunia.
Haitoshi mmeniandalia pigo zito la kunimaliza kabisa la kunigeuza msukule ili tu
muwe na maisha mazuri.
“Ninyi ni viumbe gani mnaojali fedha kuliko utu
wa mtu, mmemtoa kafara dada Monika kwa tamaa zenu, hamkuridhika umemtoa mtoto
wako ili uwe na pesa nyingi vile vile hamkuridhika mmenigeukia mimi. Kwa vile
hakuna mtu mwingine wa kumpa kidonda hiki mmeamua mnigeuze ndondocha wa
familia.”
“Masalu umejuaje?”
“Si kujuaje, kwa nini umeamua
kunifanya hivyo?”
“Si kweli,” dada alijifanya
kushtuka.
“Sawa si kweli, basi baba anakufa.”
“Umeamua
kuuana?”
“Masalu bila wewe baba atakufa, unakubali baba yetu afe
kweli?”
“Mimi na ninyi nani kaamua kumuua mwenzake?”
“Masalu
kumbuka baba yetu ni huyuhuyu, akifa hatutampata mwingine.”
“Kwani
kuna mbadala wa dada Monika, baba ni huyo huyo, dada Monika mwingine yupo
wapi?”
“Masalu makosa yamekwisha fanyika rudisha moyo uokoe maisha ya
baba.”
“Kwanza mnaniambia hivyo mimi nimemfanya nini baba?”
niliwauliza swali gumu.
“Inaonekana umekwenda kwa mganga kurudisha
nguvu zako za kiume.”
“Mlitaka niwe hivihivi milele kwa raha zenu,
mbona ninyi mna watoto na wanaume?”
“Kwani Masalu upo
wapi?”
“Tokea lini mlinitafuta?”
“Basi zungumza na mama,”
baada ya muda nilimsikia mama akiniita.
“Masalu.”
“Naam
mama, shikamoo.”
“Marahaba mwanangu upo wapi? hali ya baba yako ni
mbaya sana.”
“Anaumwa nini?”
“Ameanguka kwenye mishughuliko
yake, kama ni kweli umefanya wewe njoo umsaidie baba yako, hali inatisha
hajitambui anakoroma tu.”
“Mama sihusiani na lolote kuhusiana na
matatizo ya baba, naomba mumpeleke hospitali.”
“Ugonjwa huu si wa
hospitali.”
“Kwa hiyo mimi ndiye niliyemroga?”
“Hapana
Masalu, ila inawezekana ulichokifanya ndicho kilichomuathiri baba
yako.”
“Kipi hicho?”
“Unakijua Masalu, hebu rudi haraka
nyumbani.”
“Mama ni nani kwako?”
“Mtoto.”
“Nina
haki gani kama mmoja wa watoto wako?”
“Haki zote kama walizonazo
wenzako.”
“Sasa kama kila mtu ana haki hiyo kwa nini unataka kushiriki
katika kunigeuza ndondocha wa familia?”
“Masalu! Wakugeuze kivipi?”
mama alishtuka.
“Mama, unajua vizuri sana si suala la siri, mpango
wenu wa kunimaliza nimeugundua lakini nawahakikishia kila atakayenigusa
nitampoteza.”
“Upo tayari baba yako afe?”
“Mimi situnzi uhai
wake bali Mungu aliyetuumba wote, kama wakati wake umefika basi atakufa, kama
alivyokufa mtoto wa dada na dada Monika.”
“Kwa nini umekosa
huruma?”
“Kwa vile ninyi mnanionea huruma eeeh.”
“Kama
ulivyosikia hali ya baba yako ni mbaya kifo chake
kitakuhusu.”
“Sishangai hata wewe mama niliyekuwa nakutegemea ni mmoja
wapo. Asante sana nashukuru, Mungu yupo
atanilinda.”
“Masalu...Masa..,” nilikata simu na kuizima
kabisa.
******
Baada ya mazungumzo nilijikuta nikilia peke yangu jinsi
familia yangu ilivyokuwa ikijijali yenyewe na kuwa tayari kupoteza uhai wa mtu
ili tu ipate mali.
“Masalu nyamaza mpenzi wangu,” mpenzi wangu
alinibembeleza, kipindi kile yeye ndiye aliyekuwa mfariji
wangu.
“Inaniuma.”
“Kweli inauma, lakini kwa nini umekubali
kuzungumza nao? Ungezima simu yote haya yasingetokea.”
“Ilikuwa lazima
nizungumze nao ili wajue kuwa naelewa kila kitu, pia hata kujua kama kweli hali
ya baba ikoje.”
“Kwa hiyo utakwenda kumuona baba
yako?”
“Nikitoka kwa mganga nitakwenda.”
“Pole sana
inasikitisha, familia yako ina dhambi kubwa.”
“Wee waache sijui kwa
Mungu watasema nini?”
“Ulisema wewe ndiye chanzo cha utajiri
kilichoachwa na marehemu dada yako Monika, ukipona itakuwaje?”CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Sijui, watajua
wenyewe, mimi nitaangalia afya yangu.”
“Mmh! Pole sana mpenzi wangu,
kupona lazima uwe na roho ngumu ili umeze mfupa.”
“Nimekwisha umeza
lolote na liwe, siwapendi mashetani wale.”
Kwa vile muda ulikuwa
umekwenda tulipanda kitandani kulala, usiku nilijikuta nikipatwa na hamu ya
mapenzi. Lakini nilikumbuka kauli ya mganga kuwa nikikutana kimwili na mwenzangu
ndiyo kifo cha baba, hawezi kuomba hata maji.
Pamoja na hasira
kutokana na roho mbaya ya familia yangu juu ya mambo waliyotaka kunifanyia
nilijikuta nikiingiwa na imani ya kutofanya tendo lile kuokoa maisha ya baba.
Tulilala mpaka asubuhi bila kufanya tendo la ndoa, asubuhi tuliamkia kwa
mganga.
Hatukuchelewa kufika kwa vile hapakuwa mbali kutoka
tulipokuwa tumepanga, ulikuwa mwendo wa dakika ishrini. Ilionesha sisi ndiyo
tulikuwa wateja wa kwanza toka nje kufika pale kwa siku ile, tuliowakuta pale ni
wale waliokuwa wakitibiwa na kulala palepale.
Mganga alitukaribisha,
kama kawaida niliingia ndani peke yangu na mpenzi wangu alibakia nje. Nilipofika
hakunisemesha lolote, aliendelea na kutoa chupa za dawa kwenye kikapu na
kuziweka juu ya ngozi kisha alichukua karatasi ya kaki na kuanza kumiminia unga
wa dawa kidogo kidogo kutoka katika kila chupa.
Zilikuwa chupa zaidi
ya tano, baada ya kuukusanya unga wa dawa katika karatasi moja, alichukua chupa
iliyokuwa na mafuta kama sikosei ya ng’ombe, yalikuwa meupe na mazito.
Aliyamiminia yale mafuta na kuyachanganya na mchanganyiko wa dawa kisha alitoka
nje.
Baada ya muda alirudi na kunionesha kwa ishara nimfuate,
nilimfuata mpaka kwenye kichuguu kimoja ambacho alinielekeza. Kabla ya kupanda
juu ya kichuguu alinielekeza kwa ishara nivue shati. Nami nilifanya kama
alivyonielekeza.
Baada ya kupanda juu ya kichuguu kifua wazi, alipanda
na yeye na kuanza kunichanja kila kona ya mwili huku akinipaka ile dawa
aliyochanganya na mafuta mazito. Alipomaliza tuliteremka na kurudi hadi ndani ya
kilinge, ndipo aliponisemesha.
”Habari za toka jana?”
“Nzuri
mzee wangu, shikamoo.”
“Marahaba, kuna habari gani
mpya?”
“Jana walinipigia simu usiku na kuniomba ninusuru maisha ya
baba.”
“Uliwajibu nini?”
“Niliwaambia siwezi kujiteketeza
mwenyewe.”
“Wao walisemaje?”
“Walinitishia kama baba akifa
nitamla nyama.”
“Akawajibu nini?”
“Niliwaeleza kama
walivyokula nyama ya dada Monika.”
“Wakasemaje?”
“Walishtuka
na kunieleza kuwa habari nimezijulia wapi?”
“Mh, ukawajibu
nini?”
“Niliwambia nitawapeleka polisi na kuwafungulia mashtaka ya
uuaji na kukaa na maiti za watu ndani?”
“Enhee!
Wakasemaje?”
“Walishtuka na kuniomba ninusuru maisha ya
baba.”
“Ukawajibu nini?”
“Niliwaeleza sipo
tayari.”
”Wakasemaje?”
“Waliendelea kunibembeleza niende kwa
vile uliniahidi nikitoka hapa nitakuwa kamili, nimewaeleza nitakwenda
leo.”
“Wakasemaje?”
“Tumekubaliana, nikitoka hapa
niende.”
“Sikiliza, una bahati kama usingekuja hapa na kujipendekeza
jana ukaenda ungekwisha palepale.”
“He!” Nilishtuka kusikia
vile.
“Unashtuka, kama nilivyokueleza familia yako haina mapenzi na
wewe kwa ajili ya mali.”
“Mmh! Sasa nikienda leo
itakuwaje?”
“Leo usiende, nenda keshokutwa ila kuna kitu kitatokea si
cha kawaida, kuwa tayari kukabiliana nacho.”
“Kitu gani
hicho?”
“Wee nenda, ila majibu utayapata kujua kinga niliyokukinga
inafanya kazi kiasi gani.”
“Niambie ili nijue ikiwezekana
nisiende.”
“Lazima uende ili kuwaumbua wabaya wako.”
“Mmh!
Sawa.”
“Baada ya kesho kwenda rudi tumalizie tiba, kwa vile
hawatakubali kuona umewashinda.”
“Sawa
nimekuelewa.”
“Nilitaka kusahau kitu kimoja, leo usioge wala kukutana
na mwanamke kimwili ikiwezekana leo kila mmoja alale chumba chake au kitanda
chake.”
“Sawa nimekuelewa.”
“Ndoto utakayoiota ndilo jibu la
safari yako.”
“Nashukuru kwa msaada wako.”
******
Baada ya mazungumzo, tulirudi
hoteli tuliyokuwa tumepanga kwa ajili ya mapumziko, siku ile sikukaa kutokana na
kuwa na alama nyeusi za kuchanjwa na mganga.
Kwa vile hatukuruhusiwa
kulala pamoja, tulichukua chumba cha vitanda viwili na kila mtu alilala kitanda
chake. Usiku niliota ndoto nafukuzwa na kichaa mmoja ambaye katika kunifukuza
aligongwa na gari, hapohapo nilishtuka usingizini na kujiuliza kichaa yule ni
nani na ndoto ile inaashiria kitu gani.
Siku ya pili nilimueleza
mpenzi wangu ambaye alinishauri heri nisiende nyumbani ili kuepusha
nilichokiota.
“Masalu kama mganga alikuambia utakachokiota ndicho
kitakachotokea, kwa nini uende?”
“Hilo wazo hata mimi nilikuwa nalo
lakini mganga alisema lazima niende, ili nirudi na kupata dawa ya
mwisho.”CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kwa nini asikupe
hiyo dawa?”
“Alisema lazima niende ili kuonesha uwezo wa kile
alichokifanya jana.”
“Mmh! Mtihani mzito kweli.”
“Lakini
kwetu hatuna kichaa.”
“Basi inawezekana utakutana naye
njiani.”
“Kama ni hivyo bora nikodi gari mpaka
mlangoni.”
“Bora ufanye hivyo.”
“Sawa, basi tuongozane, wewe
uende kwenu najua wamekutafuta sana.”
“Hata wakinitafuta mimi mtu
mzima, kuna mdogo wangu anajua kila kitu sidhani kama watasumbuka sana. Mbona
tuliishasafiri zaidi ya wiki hakuna kilichoharibika?”
“Si
uliaga?”
“Basi taarifa zangu watazipata kwa mdogo wangu na leo
nikifika watapata jibu.”
“Mmh! Haya.”
Niliongozana na mpenzi
wangu hadi kwao, nilimteresha na mimi kuendelea na safari yangu. Nilikwenda na
gari hadi mlangoni na kuteremka, wote waliokuwepo walishtuka. Baba aliyekuwa
amelazwa sebuleni aliponiona alipiga kelele.
“Mtoeni...mtoeni
ataniua...ataniua.”
“Baba siwezi kukuua, utajiua mwenyewe,” nilimjibu
baba.
“Jamani mtoeni ataniua,” baba alizidi kupiga
kelele.
“Masalu hebu toka nje,” dada alinifokea.
Niligeuka
kutoka nje, kaka yangu alikuja kwa nyuma na kunishika kisogoni, mara alianza
kupiga kelele kama mtu aliyepagawa, akachukua jembe na kutaka kunipiga nalo,
alinikosakosa mara mbili, nilipoona hatanii nilitimua mbio, alinikimbiza mpaka
barabarani huku akidhamiria kuniumiza.
Ilinibidi nivuke barabara bila
kuangalia baada ya kuona nakufa najiona, baada ya kuvuka nilisikia kishindo
nyuma yangu na kelele za watu. Nilipogeuka nilimuona kaka yangu akiwa chini
akivuja damu kichwani.
Japo ajali ile ilifanya moyo uume na kupatwa na
huruma, lakini sikutaka kurudi kuangalia, wakati huo watu walikuwa wakijaa
kwenye tukio la ajali na kumzunguka kaka. Nilikodi teksi iliyokuwa ikipita
kuwahi nyumbani. Nilipofika nyumbani nilimpigia simu mpenzi
wangu.
“Vipi Masalu mbona kama kuna
tatizo?”
“Ndiyo.”
“Tatizo gani?”
“Si la
kulizungumzia kwenye simu.”
“Upo
wapi?”
“Nyumbani.”
“Nakuja sasa hivi.”
Baada ya
kukata simu nilibaki nimejilaza kwenye kochi nilijiuliza vita nzito niliyoelezwa
na mganga ndani ya familia yangu nini hatima yake. Nilijiuliza kaka yangu bila
kugongwa na gari alitaka kunifanya nini. Au alikusudia kuniua?
Njozi
ile baada ya kuuona ukweli nilijuliza nini kitafuata.
Niliamini kama
vita ya nguvu za giza itashindikana basi watatumia nguvu za kawaida ili
kunitokomeza duniani. Nilijiuliza kama itakuwa hivyo nitawezaje kuwaepuka?
Nilipanga kuukimbia Mji wa Mwanza ili kuokoa maisha yangu kwa kuliuza duka
langu.
Wazo lile nilitaka nishauriane na mwenzangu kabla ya kutoa
uamuzi, nilipanga akija nitamgusia suala lile ambalo kwa upande wangu lilichukua
sura mpya ya kutishia maisha yangu. Wakati nikiwa kwenye dimbwi la mawazo mpenzi
wangu aliingia kwa hali aliyonikuta nayo ya kujilaza mikono kichwani ilimshtua
sana.
“Vipi?”
“Masalu?”
“Mambo
mazito.”
“Kivipi?”
Nilimueleza niliyokutana nayo nyumbani,
alibakia mdomo wazi asiamini nilichomueleza.
“Sasa bila kugongwa na
gari ingekuwaje?”
“Hata sijui.”
“Sasa kwa nini mganga
hakukuambia?”
“Aniambie nini wakati aliniambia nitakayoyaota ndotoni
ndiyo nitakutana nayo?”
“Sawa, lakini alitakiwa akupe
tahadhari.”
“Mganga hawezi kukuambia kitu kijacho kabla ya kutokea ili
usije sema uongo.”
“Pole sana mpenzi wangu sasa tutafanya
nini?”
Mara simu yangu iliita nilipoangalia nilikuta ni dada,
niliitazama bila kupokea kitu kilichomfanya mpenzi wangu
kuuliza.
“Mbona hupokei ni nani?”
“Dada”
“Anataka
nini si alikufukuza?”
“Hata mimi
nashangaa.”
“Usipokee.”
Kweli sikuipokea, iliita mpaka
ikakatika, baada ya kukatika haukupita muda iliita tena. Vilevile sikuipokea,
ikaita mpaka ikakatika. Nilitaka kuizima lakini mpenzi wangu alikataa kwa
kuniambia:
“Simu za ndugu zako usipokee, lakini zingine ziache
ziingie.”
“Kutokana na vita hii nzito nilikuwa nimepanga kuuza duka
langu niondoke Mwanza, ulikuwa na wazo gani?”
“Mmh! Ni haraka sana kwa
nini tusirudi kwa mganga tumsikilize atasema nini?”
“Mganga kazi yake
ni kunizindika ili nisidhurike na nguvu za wachawi, lakini si kuwazuia kunidhuru
kwa silaha za kawaida.”CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Sawa, lakini kabla
ya kufanya hayo tukamsikilize mganga, si alikuambia urudi.”
“Mmh!
Kweli, kuna umuhimu wa kwenda muda huu.”
“Hakuna tatizo ni muda
mzuri.”
Nilikubaliana na mwenzangu kurudi kwa mganga, tuliongozana
hadi kwa mganga, tulimkuta akihudumia wagonjwa. Ilitupasa kusuburi kwa zaidi ya
saa nne. Ilipofika zamu yangu niliingia kwa mganga, aliponiona alitabasamu na
kusema:
“Umeona?”
“Ndiyo.”
“Sasa ule ndiyo ubaya
uliokuwa umekuzunguka, bila kupitia hapa alipokushika ungeanguka chini na
kupooza, kuanzia muda ule ungewekwa kwenye chumba chenye mwanga hafifu na hayo
ndiyo yangekuwa maisha yako mpaka unakufa.”
“Mmh! Na kaka yangu
aliyegongwa na gari
hakufa?”
“Hakufa.”
“Atapona?”
“Atapona, lakini
itachukua muda mrefu sana kupona, alipogongwa hakuumia. Lile halikuwa gari la
ukweli kama ulivyodhania ni kinga yako mwilini hakuna wa kukuchezea. Atakayetaka
kukuchezea atapatwa na mazito kuliko yaliyompata kaka yako.
“Kila
tatizo litakalokutokea utaliota usingizini kabla ya kukutokea.”
“Kwa
hilo nashukuru, lakini wakitumia silaha?”
“Zindiko nililokuwekea
hawawezi kukudhuru kwa kitu chochote.”
“Nilikuwa na wazo la kuuza duka
ili nitoroke.”
“Wala usiende popote, hakuna wa kukugusa, watakuogopa
kama ukoma, ila inabidi duka lako lifanyiwe zindiko bila hivyo mali zako zote
zitamomonyoka na kukufanya ubaki kuwa maskini wa kutupwa.”
“Na ndugu
zangu?”
“Nao wana wakati mgumu, si muda mrefu watakuwa na maisha
magumu, labda wahangaike tena la sivyo kwa kutegemea ndagu ya kidonda
wataadhirika.”
“Kwa hiyo unataka kuniambia kaka hakupata
ajali?”
“Hakupata ajali ila amepata kichaa baada ya kutaka kukudhuru
na kumrudia mwenyewe.”
“Lile gari na watu waliokuja walitokea
wapi?”
Kile ni kiini macho tu lakini ile ndiyo kinga inayokulinda,
baada ya kumzuia ulipata nafasi ya kukimbia na kurudi kwako.”
“Na hali
ya baba?”
“Mmh! Hali ya baba yako ndiyo hivyo imeshikiliwa na uhai
wako, kubali uteseke baba yako apone.”
“Sipo tayari wacha afe, siwezi
kuwaonea huruma tena ni watu wabaya wasionitakia mema.”
“Basi leo
nitamalizia kazi yangu, ukitoka hapa fanya mambo yako bila hofu, atakayekugusa
atapotea.”
Mganga baada ya kusema vile alichukua dawa nyeusi iliyokuwa
kwenye chupa na kuichanganya na asali kisha alisema niachame mdomo, akanichanja
kwenye ulimi na kunipaka dawa kwa kutumia simbi. Chale zingine alinichanja
katikati ya utosi, kifuani na mgongoni na sehemu zote za maungio ya mwili kisha
alinipa ruhusa ya kurudi nyumbani na kunipa masharti yaleyale ya kutolala na
mwanamke kwa siku ile.
“Kijana kazi imekwisha, unaweza kuendelea na
shughuli zako kama kawaida.”
“Asante, na kuhusu hali ya
baba?”
“Yangu nimemaliza, utaamua mwenyewe.”
“Hawezi kupona
tena?”
“Akipona ujue unakufa wewe.”
“Hata akipelekwa kwa
mtaalamu mwingine?”
“Kwangu nimemaliza na kazi yangu naiamini
haijawahi kutokea kama itatokea basi ujue ndiyo kifo chako.”
“Na
asipopona?”
“Utakufa.”
“Sasa itakuwaje, ndugu si watajua
mimi ndiye niliyemuua?”
“Kijana niondolee upumbavu, niambie unataka
nifanye nini, ufe baba yako apone au afe baba yako wewe upone?” Mganga
alikasirishwa na maswali yangu.
“Basi mzee nisamehe,” niliomba
msamaha baada ya kuona nimemuudhi mganga.
“Sjawahi kuona mtu mpumbavu
kama wewe, unanipotezea wakati wangu nakuomba uondoke,” mganga alikuja juu na
kunifukuza.
“Samahani mzee wangu,” nilijikuta nikichanganyikiwa baada
ya kumuudhi mamba kabla sijavuka mto.
“Samahani nini, nilikuita hapa
nikutibu?”
“Hapana.”
“Nilikuomba
nikusaidie?”
“Hapana.”
“Sasa kwa nini unanitia ujinga kwa
kazi nzito niliyoifanya ya kuokoa maisha yako?”
“Nisamehe mzee wangu
nipo chini ya miguu yako sitakuuliza tena swali lolote kuhusiana na familia
yangu.”
“Kazi nimemaliza nipe changu kilichobaki kisha uende zako
utaamua chochote kwenda kwa mganga yeyote akusaidie. Ila ukiondoa mguu wako hapa
usije tena.”
“Mzee wangu najua nimekukosea naomba usifike huko,”
nilizidi kumuomba msamaha mganga baada ya kubaini kosa langu.
“Lazima
nifike nimekufafanulia mangapi yaliyotaka kukupata na leo umepata jibu bado
unajitoa akili nikufanye nini? Wewe mtoto?”
“Hapana, nimekosa mzee
wangu nipe adhabu yoyoye lakini usinikataze kuja hapa,” nilipiga magoti mbele ya
mganga kuomba msamaha.
“Nimekuelewa kijana lakini usirudie tena
kuingilia kazi za watu.”
“Nashukuru mzee wangu.”
******
Baada ya kusamehewa na
mganga, tuliagana na kunieleza ninapotokewa na tatizo niende kwake bila tatizo.
Baada ya kutoka pale sikutaka kurudi nyumbani ambako niliamini lazima ndugu
zangu watanitafuta.
Kama kawaida tulirudi kwenye hoteli yetu
tuliyolala jana yake, tulilala pale mpaka siku ya pili. Usiku wa siku ile mpenzi
wangu alitaka kujua nini hatima ya maisha yangu baada ya kutoka kwa
mganga.
“Mh, Masalu mganga amesemaje juu ya uamuzi wako wa kukimbia
mji?”
“Amesema hakuna kitakachonitokea nikae hapahapa.”
“Na
kuhusu ile ajali?”CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Anasema haikuwa
ajali bali kinga aliyoniwekea ndiyo iliyonilinda nisidhuliwe na
kaka.”
“Masalu! Unataka kuniambia kaka yako hakugongwa na
gari?”
“Mganga ndivyo alivyonieleza.”
“Mmh! Makubwa, lakini
mganga huyu kiboko, sifa zake ni kubwa.”
“Lakini alitaka
kunitimua.”
“He! Kivipi?”
“Nilitaka kumuulizia hatima ya
hali ya baba yangu.”
“Akakujibu nini?”
“Wewe, kumbe
niliwasha moto wacha anifukuze kama mbwa aliyeiba mayai.”
“Ehe!
Ikawaje?”
“Mmh! Ilibidi nimuombe msamaha huku
ninalia.”
“Mkaishiaje?”
“Alinisamehe na kunionya nisirudie
tena kuuliza maswali ya kijinga.”
“Lakini nawe umeyataka, unamuombea
dhamana mtu uliyemfunga mwenyewe?”
“Pamoja na hayo, lakini yule ni
mzazi wangu.”
“Haya sasa, chagua mzazi apone uumie
wewe.”
“Japo inaniuma lakini kisu kimegusa mfupa, kungekuwa na njia
mbadala nisingekubali kuona baba yangu anateseka kwa ajili
yangu.”
“Lakini ningekuwa ni mimi nisingekuwa na huruma na mtu
anayenitoa kafara kwa tamaa zake. Tena ningemuulia mbali hata kwa
sumu.”
“Lakini kumbuka pamoja na yote ni mzazi
wako.”
“Siwezi kumuonea huruma mzazi mwenye nia mbaya na mimi, akitaka
kuniua nikigundua na mimi namfanyia kitu kibaya.”
“Lakini si kila baya
lazima ulipe baya kuna lingine unatakiwa kulisamehe.”
“Kwa upande
wako utasamehe vipi, ili kupona lazima mtu aumie, kibaya zaidi pamoja na yote
waliyokufanyia bado wanataka kukupoteza kwenye sura ya dunia bado watu kama hao
unawaonea huruma?”
“Kwa kweli nimechanganyikiwa.”
“Sikiliza
Masalu, unapofanya kitu kibaya kisha ukaona huruma basi lazima litakurudia na
halitapata tiba mpaka unakufa.”
“Wewe nani
kakwambia?”
“Masalu mpaka nakupeleka kwa yule mganga nayajua mengi
kwa hiyo jiepushe kukingia kifua unayoyafanya, bora ungeacha kabisa kuliko
kuingilia kazi ya mganga hasa wakikusaidia katika matatizo yako.”
“Kwa
hiyo nikiendelea kusikitika itakuwaje?”
“Usishangae ugonjwa wa baba
yako ukakurudia.”
“Lakini sasa hivi si nimeachana
nao.”
“Basi ndiyo hivyo, siku zote usioneshe huruma pale unapoamua
kutenda jambo zito, huruma yako hugeuka sumu na kukurudia
mwenyewe.”
“Nimekuelewa.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda
tulikubaliana tulale ili mengine tuzungumze kesho yake kwa vile bado tulipanga
kuendelea kuwa pale kwa siku moja zaidi. Kila mtu alilala kitanda chake kama
tulivyoelezwa na mganga, ilionesha wazi kabisa mpenzi wangu alikuwa akiumia
kutokana na kumnyima haki yake ya msingi.
Lakini bado sikuwa tayari
kumuua baba yangu kwa kulifanya tendo lile, hata hali aliyokuwa nayo ilitokana
na kuyaokoa maisha yangu yaliyofikia hatua mbaya. Pia hakukuwa na njia mbadala
ya kuweza mimi kupona bila baba yangu kuguswa.
Japo mpenzi wangu
alionekana hana huruma na familia yangu na kuwa tayari kuiona inapotea baada ya
kugundua walikuwa na mpango mbaya kwangu lakini nilijitahidi kutafuta njia ya
kumueleza kwa makini ili anielewe, sikupenda hata siku moja kifo cha baba yangu
kitokane na mimi kwa kufanya tendo la ndoa nikijua kabisa ndilo litakalomaliza
uhai wake.
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment