Search This Blog

BABA KIUMBE WA AJABU - 3

 





    Simulizi : Baba Kiumbe Wa Ajabu
    Sehemu Ya Tatu (3)


    ILIPOISHIA
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Kwani anaumwa sana?”

    “Toka asubuhi analia tu.”

    “Kafanya nini?”

    “Mmh, nenda ndani ukamuone.”

    “Masalu,” baba aliniita.

    “Naam baba.”

    “Eti kuna nini?”



    “Kuna vitu ambavyo sielewi.”

    “Vitu gani?” Baba alisema huku akiingia ndani.

    Alipoingia ndani alinikuta nimeshikilia mguu.

    “Kuna nini?”

    “Baba sehemu hii inaniwasha sana kufikia hatua ya kunikosesha raha.”

    “Hebu nione,” nilimuonesha baba, baada ya kuona alisema:

    “Kumbe hiki?”

    “Ndiyo baba.”

    “Sasa tatizo nini?”

    “Kinaniwasha.”

    “Usikikune kitapoa chenyewe.”

    “Hapana baba bora niende hospitali.”

    “Masalu usiende hospitali, ugonjwa juu si wa kawaida.”

    “Wa nini?”

    “Utajua tu baadaye, lakini chonde usiende hospitali.”

    “Au ndiyo kama wa dada Monika?”

    “Eti?” Kauli yangu ilimshtua baba na kunitazama mara mbili kama ndiyo siku yangu ya kwanza kuniona.

    “Eti umesemaje?”

    “Baba mbona umeshtuka hivyo?”

    “Sijakuelewa, hebu rudia swali lako.”

    “Nauliza, kisiwe kidonda kama cha dada Monika.”

    “Mama yako ndiyo kwakwambia? Leo atanitambua,” baba alikuja juu.

    “Baba badala ya kunijibu swali langu unakimbilia kutaka kumpiga mama au ndiyo umemuona gunia lako la mazoezi,” nilizidi kumchanganya baba na maneno yangu ambayo hakufikiria hata siku moja nitayatamka.

    “Masalu mbona unanikosea heshima?”

    “Sijakukosea heshima ila nataka kujua ukweli wa muwasho huu kwa vile nilibashiliwa kipindi kirefu.”

    “Na nani?”

    “Na dada Monika”

    “Alikubashiria nini?”

    “Alinieleza kuwa kifo chake kimetokana na kukikataa kidonda hiki, na ulichomuahidi ndicho kilichotokea.”

    “Muongo, unamsingizia Monika wakati uongo wote kakupa mama yako.”

    “Baba utamuonea mama bure, mama hajanieleza chochote zaidi ya kunifanya mtoto mdogo mambo ninayoyajua.”

    “Mambo gani?”

    “Kuhusu chanzo cha utajiri kidonda cha dada Monika mpaka kifo chake kilisababishwa nini na utabiri wake kidonda kikitoka kwake kinakuja kwangu.”

    “Mmh,” baba aliguna, kisha alinitazama kwa muda na kuangalia juu kabla ya kushusha tena pumzi.

    “Masalu.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Naam.”

    “Niambie ukweli mama yako kakuambia nini juu ya huu muwasho?”

    “Kaniambia ni muwasho wa kawaida, utapoa wenyewe.”

    “Hakukuambia kitu kingine?”

    “Hajaniambia, ndiyo maana nilijua ananidanganya, dada Monika alinipa siri nyingi, zingine hata mama hajui na bahati mbaya wakati anakufa nilikuwa mbali lakini kuna mengi mazito alitaka kunipa juu ya familia yetu.”

    “Monika alikuambia nini?”

    “Alinieleza jinsi kidonda chake kilivyoanza kama muwasho na mwisho kilikuwa kidonda kisichouma zaidi ya kutoka maji na kukatazwa asiyafute.”

    “Mmh, pamoja na uongo wake nakuomba usimuamini ni mfitini yule.”

    “Baba unataka kunihakikishia kidonda hiki sio kama cha dada Monika?”

    “Nimekueleza usimfuate Monika ni muongo.”

    “Kama muongo naomba na mimi uniondolee masharti ya kuwa na mke.”

    “Masalu, umri wako bado.”

    “Baba mimi si mdogo, ukweli ni kwamba huu muwasho mwisho wake ni kidonda ambacho kitaingiza pesa kwa njia ya kumwagika maji. Baada ya dada Monika kuyashindwa masharti yako uliamua kumuua na mimi nahofia utaniua.”

    “Narudia tena kukueleza Monika ni muongo.”

    “Baba nasema kama ndicho kidonda hiki basi nami nitakufa kama dada Monika.”

    “Masalu kuna sababu ya kuzungumza kwa kituo.”

    “Sawa baba lakini kaa ukijua kama muwasho huu mwisho wake ni kidonda cha utajiri sikitaki nakuomba unirudishe shuleni.”

    “Nikurudishe shuleni fedha za shule utazipata wapi?”

    “Kwani lazima nipate kidonda ili nisome?”

    “Utasoma, lakini kumbuka fedha zinatafutwa na njia zake pesa zipo nyingi.”

    “Moja wapo ni kidonda changu?”

    “Masalu tutazungumza, hebu vaa kuna mali mpya nimeituma dukani mwako twende ukaiangalie.”

     “Sawa baba,” nilikubali shingo upande na kukubali kuondoka na baba kwenda dukani kwangu. Nilipanga kutokwenda dukani baada ya kupata uhakika wa muwasho wangu.

    Niliondoka na baba hadi dukani ambako alinionesha baadhi ya bidhaa alizoniagizia toka China, vilikuwa vitu vingi sana ambavyo vilifanya duka langu liongezeke. Kwa muda mfupi hata ndugu zangu walianza kunionea wivu. Wazo la haraka lilikuwa huenda aliyoyafanya dada Monika ya kutaka naye awe na maisha yake ndiyo yaliyosababisha hali ile.

    Hali ya muwasho iliendelea kupungua na kuweka kitu kama gamba kwenye weusi ule. Siku moja asubuhi ilipoamka nilikuta lile gamba limetoka kutokana na kujigeuza na kuweka kidonda. Moyo wangu ulilipuka na kujua kazi imeanza, kutokana na maelezo ya awali kidonda kile hakikutakiwa kutibiwa.

    Nilijikuta nikikosa raha pamoja na mali zote alizonipa baba  sikuwa na furaha yoyote moyoni mwangu kuishi na kidonda kisichowekewa dawa mpaka mwisho wa maisha yangu. Nilipoamka na kukuta hali ile nilimweleza mama, naye alinipa jibu jepesi.

    “Aliyokueleza dada yako yametimia.”

    “Mama nitafanya nini, nitaishi hivi mpaka lini?”

    “Masalu, ondoa wasiwasi kama nilivyokueleza toka mwanzo usishtuke sana kwa vile hali hii nilishakueleza mapema uishi vipi baada ya kutokea kwa hali hii.”

    “Mama kusema ni rahisi, lakini haivumiliki, nitaishi vipi na watu wakijua nina kidonda kama cha dada Monika nitauweka wapi uso wangu?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nani atajua, labda utawaonesha wewe.”

    “Duniani hakuna siri.”

    “Ukitaka iwe siri itakuwa siri.”

    “Lakini kwa nini umenifanya hivi si mngeniuliza kuliko kunipa kidonda bila idhini yangu?”

    “Mimi utanilaumu bure wa kumlalamikia ni baba yako.”

    “Mama nami nitakufa kama dada siwezi kuishi maisha ya mipaka.”

    Nilimuhakikishia mama sitakubali kuishia maisha yale bali nitakayoamua mwenyewe.

    Siku ile mama aliniomba nisivae viatu na soksi bali nivae sandoz ili nisikibughudhi kidonda ambacho kilikuwa kimeanza kutoa maji. Ugumu wa  kuishi maisha ya kidonda nilianza kuuona kwa kuamini mabadiliko yangu ya mavazi lazima watu watataka kujua kumetokea kitu gani kilichosababisha hali ile.

    Siku ile nilishinda ndani nikilia japo  mama alijitahidi kunibembeleza, sikuweza kumkubalia niliamini ule ulikuwa uonevu wa kupewa kitu nisichokipenda tena chenye masharti ya kumdhalilisha mtu.

                                                                 *****

    Taarifa zilimfikia baba aliyekuja kunipoza, alipofika alinikuta nimejifungua ndani kwani sikuwa na hamu ya kuonana na mtu. Alinigongea mlango kwanza nilikaa kimya bila kujibu lolote.

    “Masalu hebu fungua tuzungumze.”

    Sikumjibu nilikaa kimya, lakini aliendelea kunibembeleza mpaka nilipofungua mlango. Nilipomuona tu niliangua kilio.

    “Baba mmenifanya nini?”

    “Masalu mwanangu hebu tulia nikueleze jambo.”

    “Kitu gani baba utachonieleza nikuelewe?”

    “Najua umeshtuka kuona kidonda hicho, nataka kukueleza kila kitu ulichoelezwa na Monika kina ukweli. Lakini nakuomba utusamehe kwa uamuzi wa kidonda hiki kuhamia kwako.”

    “Lakini kwa nini hamkunishirikisha mwenyewe?”

    “Hatukuwa na jinsi, pia hakuna mtu mwingine katika familia yetu ambaye angeweza kukaa na kidonda hiki baada ya Monika kufa.”

    “Baba mimi nitaweza wapi maisha ya mipaka?”

    “Unaruhusiwa kufanya lolote kasoro kulala na mwanamke tu.”

    “Baba huoni kunikataza kulala na mwanamke ni sawa na kuiondoa furaha yangu moyoni?”

    “Kwani usipolala na mwanamke unapungukiwa nini?”

    “Vingi baba, vingi sana hakuna raha ya mwanadamu kamili bila kuwa na mwenza.”

    “Ni mawazo yako, ukiizoea wala haitakusumbua.”

    “Na nikitembea na mwanamke?”

    “Utamfuata dada yako Monika.”

    “Bora nimfuate,” nilimjibu kwa hasira.

    “Hapana usifanye hivyo kuna vitu vingi nilivyopanga kukufanyia kuliko watoto wangu wote, huoni hata sasa hivi wanakuonea wivu? Nakuhakikishia kukufanyia mambo mazuri. Nakuomba usiwe kama dada yako Monika.”

    “Sawa baba,” nilikubali kwa shingo upande.

    Kukubali kwangu baba alikufurahia sana na kunikumbatia, hakujua jinsi gani mwenzake nilivyoumia. Tuliondoka pamoja kwa maelekezo yaleyale ya mama ya kutovaa viatu na soksi ili kukiacha kidonda kipumue. Nilikubaliana na baba ambaye hakutaka niwe kwenye mawazo sana muda wa siku ile kuwa nami karibu muda wote.

    Nilijilazimisha kuikubali hali ile kwa vile sikuwa na jinsi, hata ningefanya nini isingebadilika. Siku zilikatika huku nikipata maswali mengi kutokana na kubadilika na kuonekana mtu mwenye mawazo mengi. Watu wangu wengi wa karibu walitaka kujua sababu ya mimi kuwa katika hali ile.

    Niliwaeleza nipo sawa, lakini hawakukubali na kunikubalia kwa shingo upande,  siku zilikatika huku nikiendelea kuficha siri zangu. Tatizo lililonisumbua lilikuwa kwa mpenzi wangu ambaye siku za nyuma nilikuwa nikifanya naye mapenzi hadi kufikia hatua ya kumuahidi kumuoa.

    Mwanzo nilijitahidi kumkwepa ili asijue sababu ya mimi kufanya vile, lakini kila siku nilipozua uongo alinikubali mwisho uongo uliisha.

    “Masalu mbona siku hizi sikuelewi?”

    “Kivipi?”

    “Kila siku umekuwa mtu wa visingizio.”

    “Lakini si nimekueleza sababu?”

    “Sababu gani hizo?”

    “Kwa hiyo unatakaje?”

    “Nina hamu na wewe mpenzi wangu.”

    “Si nimekueleza subiri mpaka tutakapooana.”

    “Masalu usinitanie, si ni wewe uliyenilazimisha tufanye mapenzi kabla ya ndoa?”

    “Ni kweli, lakini nimegundua tulifanya kosa.”

    “Masalu niambie moja unanipenda hunipendi?”

    “Nakupenda.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Basi nataka leo tulale pamoja.”

    Kwa kweli kwangu ulikuwa mtihani mgumu wa kumkwepa mpenzi wangu nisifanye naye mapenzi. Jioni nilipotoka kazini alinipitia na kwenda La Kailo Hoteli, nilishindwa kumkatalia. Kumbe alikuwa amekwishachukua chumba kabisa, tulipofika tuliingia moja kwa moja ndani.

    “Vipi mbona huku?” Nilimuuliza.

    “Swali gani hilo Masalu?”

    Nilishindwa tena kumueleza kitu chochote, nilibakia kupelekwa kama mkokoteni usio na breki. Tulipoingia ndani mpenzi wangu alionekana na shauku kwa kunivamia kutaka mapenzi. Nilijiuliza nitawezaje kumkatalia tusifanye mapenzi ikiwa tayari ameishalipia chumba?

    Nilijiuliza kama nikifanya mapenzi itakuwaje, nilijikuta nikisemea mwenyewe “Liwalo na liwe” niliamua kufanya mapenzi siku ile. Kilichomshtua mpenzi wangu ni kitambaa nilichokuwa nimejifunga mguuni.

    “Masalu nini hiki?”

    “Niliumia,” nilidanganya.

    “Sasa mbona umejifunga kitambaa badala ya dawa?”

    “Natumia dawa za asili.”

    “Ulifanya nini?”

    “Niliumwa na nyoka wa maajabu.”

    “Una maana gani?”

    “Nilikuwa nimelala ndani nikaota naumwa na nyoka.”

    “Enhee.”

    “Nilipoamka si ndiyo nikakuta natokwa damu.”

    “Mungu wangu, baada ya hapo ikawaje?”

    “Nilikimbizwa hospitali, lakini kila dawa niliyowekewa ilizidi kulifanya donda kuzidi kuchimba.”

    “Jamani ni nyoka gani huyo akuume kitandani?”

    “Hata sijui.”

    “Mmekwenda kwa wataalamu wa jadi?”

    “Nilikwenda ndiyo natumia tiba yao kidogo sasa sijambo.”

    “Walikuambia nini kuhusiana na tatizo lako?”

    “Nilielezwa kuwa nitatibiwa hadi nipone.”

    “Mmh! Masalu pole sana mpenzi wangu, mbona hukuniambia mapema?”

    “Sikupenda kukuumiza moyo mpenzi wangu, nilijua tatizo ni dogo kumbe kubwa.”

    “Mmh! Pole sana,” mpenzi wangu aliniambia kwa sauti ya huruma.

    “Asante.”

    Pamoja na mazungumzo yale, mpenzi wangu alilazimisha tufanye mapenzi kwa vile alikuwa na hamu na mimi sana. Nilijikuta sina jinsi zaidi ya kukubali kufanya naye mapenzi na kukiuka masharti ya baba. Siku hiyo sikurudi nyumbani, nilala hotelini na mpenzi wangu mpaka asubuhi.

    Siku ya pili nilirudi nyumbani majira ya saa tatu, mara moja kwenda kubadili nguo kisha niende dukani kwangu. Mama aliponiona alishtuka na kuniuliza:

    “Masalu ulikuwa wapi?”

    “Nilikwenda kwenye sherehe ya rafiki yangu.”

    “Kwa nini hukurudi?”

    “Iliisha muda mbaya.”

    “Mmh! Sawa baba yako leo hajalala, ninavyozungumza na wewe, ameondoka asubuhi kwenda kukutafuta.”

    “Sasa ananitafuta mimi mtoto?”

    “Hayo hayajui baba yako, si unajua wewe ndiye mtoto wake wa mwisho.”

    “Naelewa, lakini mimi sasa hivi ni mtu mzima.”

    “Ina maana jana ulilala na mwanamke?”

    “Mama kusema mtu mzima namaanisha kulala na mwanamke?”

    “Sina maana hiyo, kulala nje siyo tija, wasiwasi wangu pengine ulimaanisha hivyo.”

    “Lakini kumbukeni mnaninyima haki yangu ya msingi.”

    “Ni kweli, lakini ndivyo ilivyo, unatakiwa kuvumilia.”

    “Hayavumiliki.”

    “Tutafanyaje?”

    “Ipo siku nami nitapata ufumbuzi wa tatizo langu kama dada Monika.”

    “Unataka kufanya kama dada yako? Usifanye hivyo bado tunakuhitaji.”

    “Hamna shida na mimi, wenye thamini kwenu ni hao wanaoishi maisha mazuri yasiyo na masharti.”

    “Hapana Masalu, utanifanya mama yako nife kwa mawazo. Hujui kiasi gani nilivyokuwa nawapenda wewe na Monika, ndiyo watoto pekee mnaonijali. Baada ya kifo cha Monika umebakia wewe na wewe ukifa nami sitachelewa kufa, sitakuwa na mtetezi wangu wa karibu.”

    “Mama nakupenda sana, lakini baba hatutendei haki.”

    “Najua tuvumilie, hata wewe si unajua maisha yangu yalivyo?”

    ”Nayajua mama.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa kwa nini unakuwa hivyo, hebu tuvumilie.”

    ”Sawa mama.”

    Nilimkubalia mama lakini moyoni nikiwa na siri nzito ya kitendo nilichokifanya na mpenzi wangu usiku kucha.

    Baada ya kujiandaa nilikwenda zangu dukani kwangu, nilipofika nilikuwa tayari wameishafungua. Wahudumu wangu waliponiona walinieleza:

    “Bosi mzee alikuja kukutafuta.”

    “Amesemaje?”

    “Kwa kweli haeleweki, sijui hukulala nyumbani?”

    “Kama sikulala nyumbani mimi mtoto?”

    “Tutajuaje, tumemkuta kabla ya kufungua duka, alipotuona tu alituuliza upo wapi, sisi tukamjibu tangu jana tulipoachana hatujui upo wapi?”

    “Mzee yule anazeeka vibaya, sasa kasemaje?”



    “Tumemuona akitembea kona moja hadi nyingine kisha alitoweka bila kuaga.”

    “Achaneni naye.”

    Nilisema huku nikikaa kwenye kiti changu, ajabu wafanyakazi walinishangaa jinsi nilivyoonesha sijali lolote. Haikuchukua muda baba aliingia huku akitweta.

    “Masalu.”

    “Naam baba, shikamoo.”

    “Marahaba, hebu njoo nje mara moja.”

    Nilitoka nje kuzungumza na baba, baada ya kusogea pembeni baba aliniuliza.

    “Masalu jana ulilala wapi?”

    “Kwenye sherehe.”

    “Sherehe ya nani?”

    “Ya rafiki yangu.”

    “Masalu kuna sherehe gani katikati ya wiki?”

    “Birthday.”

    “Hukulala na mwanamke wewe?”

    “Mbona unaniuliza hivyo?”

    “Masalu umelala na mwanamke,” baba alinilazimisha.

    “Baba nimekueleza nilikuwa kwenye pati unanilazimisha nimelala na mwanamke,” nilijitia kujitetea.

    “Masalu tusije kulaumiana, ukirudia tena shauri yako.”

    “Hivi baba kwa nini unanilazimisha kitu nisichokifanya, ulinikataza nisitembee na mwanamke si kufanya mambo mengine kama hili la jana, nakushangaa unanitafuta kama mwizi.”

    “Mmh sawa.”

    “Baba mbona unataka kuninyima uhuru, niliyajua haya toka mwanzo ukabisha, ona sasa unanifuata kila kona,” nilijifanya kulalamika.

    “Siyo hivyo, sipendi uingie kwenye matatizo.”

    “Baba mi mtu mzima sasa, vilevile najijali.”

    “Kama ni hivyo itakuwa vizuri, nisamehe kama nimekukwaza.”

    “Nimekusamehe ila naomba uhuru sipendi nifuatwefuatwe.”

    Kauli yangu ilimfanya baba azidi kuomba msamaha, tulikubaliana asinifuatilie mambo yangu kwa vile nitajilinda mwenyewe.

                                                                  *****

    Tangu siku ile hata nilipolala nje baba hakunifuatilia, aliniacha niishi nitakavyo, mpenzi wangu alinishawishi nihame nyumbani ili tuweze kuwa naye siku zote. Nilifikisha wazo kwa baba ambaye mwanzo alipinga lakini  baada ya kumlazimisha alinikubalia kwa shingo upande. Nilipanga chumba maeneo ya Isamilo ambako nilipanga nyumba nzima. Niliendelea na tabia zangu za kufanya mapenzi na mchumba wangu ambaye alihamia kwangu kwa siri.

    Siku moja baba alinifuata dukani na kuniita pembeni, baada ya kusogea pembeni aliniuliza:

    “Masalu kwa nini hujihurumii?”

    “Kivipi?”

    “Hebu nione kidonda chako.”

    Nilimuonesha, kidonda changu, baada ya kukiangalia alisema:

    “Si unaona!”

    Nilishangaa, sikujua alisema vile kumaanisha nini? Nilijikuta nikijiuliza kipi kilichomuonesha kitu kilichomshangaza.

    “Kuona nini baba?”

    “Ina maana huoni kidonda chako kinaonesha hujionei huruma maisha yako.”

    “Bado sijakuelewa.”

    “Kidonda chako kinatoa maji?”

    “Hapana.”

    “Unajua kwa nini?”

    “Hata sijui.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Masalu unatembea na mwanamke wewe.”

    “Baba mbona unang’ang’ania neno hilo?”

    “Nakuomba uache, shauri zako.”

    “Niache vipi wakati sifanyi?”

    “Masalu mimi baba yako nimewahi kuona jua kabla yako najua kila kitu, na sababu kubwa ya kuhama nyumbani ni kufanya uchafu wako. Huoni hata biashara sasa hivi zinadoda?”

    “Baba tafuteni tatizo lingine siyo mimi.”

    “Mmh, haya mama yako asiye kunililia.”

    Baba aliondoka akiwa amechanganyikiwa, nami sikuwa tayari kuachana na mpenzi wangu, katika maisha niliamini raha ya mwanaume ni mwanamke na si wingi wa pesa. Siku hiyo hiyo ndugu zangu wote walikuja na kuniweka chini juu ya mimi kuwa na mwanamke.

    “Masalu kwa nini hutaki kumsikiliza baba?”

    “Nimsikilize kwa lipi?”

    “Juu ya wewe kuwa na mwanamke.”

    “Mna uhakika gani?”

    “Sisi hatuna uhakika ila kasema mwenyewe.”

    “Ninyi mna wapenzi?” Niliwauliza.

    “Tunao.”

    “Sasa mimi nazuiwa na nini?”

    “Si unajua hali yako haitaki uwe na mwanamke?”

    “Kwa hiyo kidonda niwe nacho mimi maisha mazuri muwe nayo ninyi, sikilizeni kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe.”

    “Masalu utakuja kuijutia kauli yako.”

    “Sijutii, mbona dada Monika hakuijutia na mkiniua na ninyi mnafilisika, kazi kwenu.”

    Maneno yangu yaliwazima midomo, waliondoka na kuniacha wakiwa hawana hamu na mimi. Tangu siku ile nikawa adui yao mkubwa, niliwashangaa kunikasirikia mimi kuwa na mwanamke wakati wao walikuwa na kila kitu. Kama mateso ya kidonda  nimeyakubali bado hawaridhiki walitaka nikose na raha za dunia.

    Ukali wa baba uligonga mwamba, akamtumia mama kunibembeleza, nani msimamo wangu ulikuwa palepale wa kukataa kuwa nalala na mwanamke.

    “Masalu jihurumie usije kufa kama dada yako Monika.”

    “Mama mkiniua nani atakayebeba kidonda? Dada Monika alinieleza kuwa wote mliotaka kuwapa kidonda mizimu iliwakataa.”

    “Ni kweli, lakini unatakiwa uionee huruma familia yako.”

    “Mama ninyi hamnionei huruma, mimi nitawaonea vipi?”

    “Kumbuka kama utaendelea kufanya kama usipokufa wewe basi utampoteza baba yako.”

    “Mama kila mwanadamu hufa kwa ahadi ya Mungu na wala si kwa ajili yangu.”

    “Kwa hiyo una mwanamke?”

    “Nilikuwa naye lakini sasa hivi kabakia rafiki.”

    “Mbona baba yako kaelezwa kuwa unautia mwili wako uchafu ndicho chanzo wa kidonda chako kukauka na kufanya mambo yote yaanze kusimama?”

    “Lakini mama kama kidonda nimekubali kwa nini mniwekee vikwazo kwenye maisha yangu?”

    “Si vikwanzo bali masharti ya mizimu.”

    “Kama ni masharti ya kunyanyasana mimi siyawezi, kama mali zenu chukueni na mimi niacheni na maisha yangu.”

    “Masalu unajiamini nini mwanangu?”

    “Sina cha kujiamini bali ukweli ndiyo huo.”

    “Basi baba nakuomba, nipo chini ya miguu yako, kama una mwanamke achana naye.”

    “Nikueleze mara ngapi kuwa sina?”

    “Najua tumekufanyia kitu kibaya lakini mabadiliko ya kidonda chako ni hayohayo.”

    Niliachana na mama ambaye niliona na yeye ananizingua, sikutaka kukosa vyote, mavazi nilibadilika kuvaa siku zote nilivaa suruali za kitambaa ili kuogopa kukitonesha kidonda, sikuruhusiwa tena kuvaa viatu zaidi ya sandozi. Kila mmoja alinihoji uwezo wangu wa kifedha na mavazi yangu.

    Nilikuwa na duka kubwa kuliko ndugu zangu, lakini wao ndiyo walionekana wana maisha mazuri. Nami sikutaka kushindana nao, kwa vile kidonda nilijua hakitoki mwilini mwangu nami niliamua kutumia kilicho ndani ya uwezo wangu.

    Nilianzisha tabia ya kumhonga pesa mpenzi wangu ili naye afaidi kama ndugu zangu kutokana na kuonekana wao ndiyo wenye thamani. Siku moja niliamka asubuhi nyumbani kwangu kama kawaida na kushangazwa kukuta baba yangu na ndugu zangu wakiwa nje ya nyumba yangu.

    Eti shida yao kubwa ilikuwa ni kunifumania na mwanamke, niliwashangaa watu wazima kama wale kuacha kazi zao za msingi kutaka kunifumania mimi. Ajabu ya Mungu siku ile mpenzi wangu hakulala nyumbani, sikutaka kupigizana nao kelele. Niliwaruhusu wamtafute, walifanya upekuzi bila kuona lolote.

    “Jamani kama bado hamjaridhika semeni niwafungulie wapi mkatafute?”

    “Wee chonga lakini lazima utakumbuka siku moja kuwa sisi tulitangulia kuzaliwa.”

    “Hilo ni dua la kuku ambalo halitanipa asilani.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wote waliondoka na kuniacha nikijiuliza kama wangenikuta na mwanamke wangenifanya nini maana walionekana kabisa walikuja kishari.

    Baada ya kuondoka niliapa kufanya ninachokiweza, sikuwa tayari kugeuzwa kitega uchumi cha watu. Niliendelea kufanya mapenzi na mpenzi wangu kama kawaida japo hata biashara kwenye duka langu zilidoda, hazikwenda kama mwanzo.

    Yote hayo sikuyafikiria zaidi ya kusubiri litakalotokea japo mama alijitahidi kunibembeleza niachane na yote yanayoonekana yanaharibu biashara za familia yetu ikiwemo na yangu. Baada ya kuona maneno yamezidi nilianza kuwa mlevi, kila muda nilikuwa nimelewa kitu kilichozidi kuichanganya familia yangu.

    Siku moja nikiwa faragha na mpenzi wangu nilishangaa kuziona sehemu zangu za siri zimeingia ndani, nilishtuka sana. Hali ile ilinifanya nikose raha kwa kuamini zile zilikuwa njama za familia yangu kutaka kuona sifanyi mapenzi na mwanamke.

    Katika kumbukumbu zangu, nilikumbuka siku moja kabla ya kutokea kwa tukio lile nilipokuwa na mpenzi wangu kuna kitu alinipaka kilichofanya nihisi kama kuwashwa baada ya kumaliza kufanya mapenzi. Na siku ya pili nilitokewa na tatizo lile, ilibidi nimbane kutaka kujua alinipaka kitu gani.

    “Masalu juzi nilikutana na dada yako mkubwa aliniomba nikupake dawa hii, nilikataa lakini alinitishia kuniua. Unajua familia yako imeniandama sana kumbuka kuna wakati nikawa nakukimbia nawe ukaamua kutafuta mwanamke mwingine.

    “Kitendo kile kiliniuma sana na kuamua kurudiana na wewe, ndipo juzi nilipokutana na dada yako aliyenipa dawa hii nikupake kabla ya kufanya mapenzi itasaidia kupunguza madhara yanayotokana na matatizo ambayo yangekupata.

    “Nilikubali kuipokea kwa vile sikudhania kama dada yako angekufanyia kitu kibaya, kumbe nia yake ilikuwa hii ya kukufanya hivi.”

    “Lakini kwa nini amenitenda hivi?” Nilijikuta nikilia kwa uchungu kwa kitendo cha dada yangu.

    “Mpenzi sikuwa na nia mbaya, kama ningekuwa na nia mbaya leo ningekuwepo hapa?”

    “Ona jinsi ulivyonimaliza, hujui ugomvi wangu na familia yangu umekuwa kama mgeni unakubali kunimaliza, ona sasa,” nilisema kwa uchungu huku nikimuonesha sehemu zangu za siri zilizokuwa zimerudi ndani.

    “Nisamehe Masalu sikujua yatatokea yaliyotokea.”

    “Wameniweza,” nililalamika kwa uchungu.

    Nilijikuta nikiapa kupambana nao, nilipanga sitakwenda tena dukani na nilikuwa nipo tayari kufa kwa njia yoyote ili tu niwaachie maisha yao.

    “Masalu kwa nini usiende hospitali kuangalia afya yako kuliko kujikatia tamaa,” mpenzi wangu alinishauri.

    “Hospitali haitasaidia kitu wameishaniweza kwa msaada wako, ona tena sina thamani ya uanaume, kimebakia kichwa kama kobe. Haya ni maisha gani ya kukoseshana raha?”

    “Kama mambo ya kienyeji twende kuna babu mmoja namfahamu anaweza kazi hii.”

    “Unanifikiri atanisaidia nini?”

    “We, twende yote tutayajua huko huko.”

    Nilikubaliana na mpenzi wangu niende kwa mtaalam aliyekuwa akikaa Pasiansi kuvuka kota za benki. Sikutaka kupoteza muda tuliondoka muda uleule kwenda kwa mtaalam kuangalia kama tatizo langu kama linatatulika.

    Kabla ya kwenda kwa mganga nilitulia ili nitafakari kama nitapata ufumbuzi wa tatizo langu bila kwenda huko. Baada ya sehemu zangu za siri kukosa nguvu nilipata mabadiliko mwilini kwa kidonda kuanza kutoaji maji upya huku biashara nazo zikifunguka.



    Nilimtolea uvivu dada yangu kwa kumfuata kwenye duka lake na kumshutumu mbele ya wafanyakazi wake kwa kitendo chake cha kishrikina cha kumpa dawa ya kuniua sehemu za siri mpenzi wangu.

    Dada alikimbia dukani huku watu wakinishangaa, ugomvi wangu haukuishia pale nilimfuata kwake usiku akiwa na mume wake na kuendelea kumshtumu. Lakini dada alinisihi suala lile tukalizungumze kwa wazazi.

    “Masalu utanilaumu bure mpango huo ni wa watu wengi si wangu peke yangu.”

    “Kwa hiyo baada ya kunipa kidonda hamkuridhika mmeniua nguvu za kiume?”

    “Lakini Masalu si ulielezwa madhara ya wewe kutembea na mwanamke?”

    “Kuna madhara gani? Mbona ninyi mna wanaume na watoto au mnataka niwe shoga?”

    “Hapana usifanye hivyo.”

    “Nakuhakikishieni baada ya kuniua nguvu za kiume sasa natafuta mwanaume wa kufanya naye mapenzi,” nilisema kwa hasira.

    “Masalu maneno gani hayo?”

    “Tena kawaambie na wanga wenzako.”

    “Masalu ukifanya hivyo utatudhalilisha.”

    “Heri niwadhalilishe kuliko kunidhalilisha kuna faida gani ya mimi kuitwa mwanaume si bora niolewe?”

    “Najua tumekukosea lakini unatakiwa ujue madhara yanayoweza kukupata, tumefanya vile kuokoa maisha yako.”

    “Maisha yangu hamuwezi kuyaokoa ninyi si Mungu.”

    “Hapana, kutokana na kafara iliyofanywa ya utajiri, ukifanya kosa kama la Monika lazima wewe au baba mmoja wenu atakufa.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wacha nife mimi kwani nina faida gani?”

    “Hapana Masalu una faida kubwa kosa lako litagharimu mambo mengi katika familia yetu. Hatukuwa na jinsi imetubidi tufanye hivyo bila hivyo hali ilikuwa mbaya sana, muda wote huo baba alikuwa mgonjwa mahututi alikwishaanza kupooza sehemu moja.

    “Amini usiamini kuacha kwako kufanya mapenzi sasa hivi baba ndiyo ameanza kupata nafuu hata chooni anakwenda peke yake. Masalu hebu kuwa na huruma na baba hana nia mbaya sema ni kiburi cha Monika wala kidonda hiki kisingekuja kwako.”

    “Ina maana Monika yeye alikuwa hana haja ya maisha mazuri au kuwa na mtoto?”

    “Maisha mazuri angeyapata tu, kidonda hiki kina muda wake ukikaa nacho kwa miaka ishirini hupotea na wewe kufanya mambo yako bila kipingamizi, mtoto utapata tu mdogo wangu wala usijigeuze mwanamke.”

    “Dada yaani nikae miaka ishirini bila kuwa na mwanamke nina mkataba na Mungu wa kuishi miaka yote hiyo?”

    “Masalu usipofanya mapenzi utapungukiwa na nini?”

    “Si swali la kuniuliza, kama unaona sipungukiwi na kitu mbona umemhonga mwanaume gari?”

    “Masalu sasa hayo maneno gani?”

    ”Huo ndiyo ukweli wenyewe, kila mwanadamu ameumbwa kufurahia mapenzi pia kupata watoto.”

    “Najua ni kweli , lakini kumbuka lililotokea lilihatarisha maisha ya baba, hatukuwa na jinsi.”

    “Basi kama hamna jinsi niacheni niishi maisha niyatakayo.”

    “Hapana mdogo wangu, hebu punguza munkari tukae kikao cha familia   

    ili tutafute ufumbuzi wa tatizo lako.”

    “Hakuna ufumbuzi wowote zaidi ya kuniongezea machungu, nakueleza ukweli sikupendi wewe na wote walionizunguka.”

    “Masalu utatulaumu bure, kila kitu baba ndiye anayefahamu.”

    “Sasa kama anafahamu kwa nini mnanitesa mimi, si mgemuacha akafia mbali.”

    “Masalu kuwa na huruma.”

    “Niwe vipi na huruma wakati ninyi hamna huruma na mimi, mmemuua dada Monika bila kosa.”

    “Masalu Monika kajiua mwenyewe, amekiuka masharti aliyopewa.”

    “Muongo mkubwa, nina kila kitu mlichomfanyia, hivi dada kwa Mungu utamwambia nini ikiwa ulimtoa mtoto wako kafara ili upate mali?”

    “Nani kakwambia?” Dada alishtuka kusikia vile.

    “Nina siri ambazo hata wewe huzijui juu ya familia yetu inayoendekeza ushirikina.”

    “Masalu una siri gani?”

    “Ya wewe kumtoa mtoto wako ili upate utajiri na kuwekwa ndani ya chumba.”

    “Masaluu! Habari hizo umezitoa wapi?”

    “Unaweza kuamini kuwa ni siri, kuna siri gani ikiwa dada Monika ndiye aliyekuwa akiipaka mafuta maiti ya mwanao.”

    “Wewee!” Dada alizidi kushangaa.

    “Kibaya zaidi mmemuua dada Monika mmeshindwa kumzika na kumuweka ndani kama mwanao. Na wewe siku hizi ndiye unayempaka mafuta, hivi kwa mtindo huo kwa Mungu mtasema nini?”

    “Masalu nani kakueleza yote hayo au mama?”

    “Utamsingizia bure mama kama wewe, ninayo mengi ambayo wewe huyajui.”

    ”Masalu mambo gani?”

    “Siwezi kukueleza muulize baba si ndiye anayefanya yote haya, hata hiki kidonda nilielezwa mapema kitanipata.”

    “Na nani?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Na dada Monika, hata kifo chake alinieleza kitakavyompata.”

    “Alijuaje?”

    “Siku alipoondoka baba alimwambia lazima atakufa.”

    “Monika muongo.”

    “Kweli kabisa na hata alipotaka kufa alinieleza sema siku ya kufa nilikuwa shule kuna siri nzito alitaka kunipa lakini bahati mbaya sikuwepo. Hata mwanaume aliyekuwa akikaa naye hakumpa siri hiyo dada yangu amekufa na siri nzito hata sijui ni siri gani?”

    “Wewe unamuamini?”

    “Nisimuamini vipi hata bwana’ake mmemuua?”

    “Nani kakwambia tumemuua?”

    “Najua kila kitu, mimi si mtoto ndiyo maana nimekueleza najua unayoyajua na usiyoyajua.” 

                                                                ******                       

    Kila nililokuwa nikimueleza dada aliona kama maluweluwe, niliamua kuondoka huku nikiwa na akili kichwani mwangu.

    Wazo la kwenda kwa mganga sikulitupa mbali japo lilikuwa mtihani kwangu. Lakini niliamini maisha yangu yananitegemea mimi mwenyewe si mtu mwingine. Siku ya pili nilimpigia simu mpenzi wangu ili anifuate na anipeleke kwa mtaalamu huyo. Alinifuata na kunipeleka kwa mtaalamu mmoja aliyekuwa maeneo ya Pasiansi nyuma ya kota za benki.

    Tulipofika eneo la mganga tulikuta kuna wagonjwa wengi kiasi, ile ilinipa moyo kuwa huduma za mganga ni nzuri. Ilibidi tukae chini ya mti kusubiri wagonjwa wahudumiwe. Baada ya saa tatu ndipo tulipoitwa sisi, ilikuwa ni majira ya saa kumi jioni. Tuliingia ndani na kuketi kwenye mkeka.

    “Huyu ni nani?” Mganga aliniuliza.

    “Mchumba wangu,” nilimjibu.

    “Mbona inaonesha kwenu hawamfahamu?”

    “Ni kweli kwetu hawamfahamu.”

    “Sasa kama kwenu hafahamiki mizimu haiwezi kuzungumza mbele yake.”

    “Kwa hiyo?”

    “Akatusubiri nje.”

    “Sweet kanisubiri nje,” nilimueleza mpenzi wangu ambaye alionesha hakupenda kutoka nje.

    Mpenzi wangu alitoka nje na kuniacha na mganga ndani ya kilinge, baada ya kutoka nje, mganga naye alitoka nje na kurudi na kipande cha tawi la mti wa mnyaa na kuushikilia mkononi. Alipoingia alikaa kwenye mkeka kisha alinipa kipande cha mnyaa ambacho nilishika kwa muda kisha aliniambia nikiachie. Baada ya kukiachia alisogeza karibu na sikio kama anasikiliza simu kisha alianza kuzungumza kama mtu anayezungumza peke yake:

    “Masalu mimi jamani mbona kila siku matatizo sifai chini sifai juu, kiuno kinaniuma mgongo unaniuma miguu inaniuma kifua kinaniuma shingo inaniuma kichwa kinaniuma macho hayaoni vizuri choo sipati vizuri, jamani ni kwa sababu gani?

    “Masalu mimi nina tatizo gani jamani, mbona kila siku matatizo yanaongezeka ni kweli mganga atanisaidia mbona mimi ni maiti inayotembea ninayesubiri kufa. Ni kweli mganga atanisaidia? Mbona sina thamani ya dunia kifo changu kashikilia baba kama cha dada Monika.

    “Maisha haya mpaka lini kidonda mimi na sasa wamechukua nguvu zangu za kiume. Nini kimebakia kama si uhai wangu, kweli mganga atanisaidia?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya kusema yale aliondoka kipande cha mti wa mnyaa sikioni na kuutupia kwenye kapu la dawa lililokuwa pembeni yake.

    “Umesikia?”

    “Ndiyo.”

    “Yaliyozungumzwa yana ukweli?”

    “Ndiyo.”



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog