Search This Blog

NILIONGEA NA SHETANI ILI NIWE TAJIRI - 4

 





    Simulizi : Niliongea Na Shetani Ili Niwe Tajiri

    Sehemu Ya Nne (4)



    "amediriki kunywa pombe ikiwa hairuhusiwi kuwa mlevi

    katika ukoo wetu. Sikumuadhibu mimi ila ameadhibiwa na

    kiongozi mkuu atupaye nguvu sisi mizimu ya koo zenu.

    Mkuu huyo amemuadhibu kwa kitendo cha kutaka

    kumbaka binti malkia wa Gamboshi"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    babu alinitazama akitabasamu. Mimi nikawa sijaelewa

    nikamuuliza babu

    "kwani yule kiumbe alimaanisha nini?"

    babu sasa akacheka zaidi akaniambia

    "ni nani basi aliyekutoa katika kiti cha umalkia wa

    Gamboshi?"

    he! hapo nikashituka zaidi.

    "babu ina maana mimi bado nina nafasi Gamboshi?

    Kwanini basi napata amteso ya kuhangaika huku na

    huko?"

    "siku utakapotimiza masharti ya mkuu"

    neno lile likawa sawa na kuniaga. Babu alipotea na mimi

    niliamka. Nilipoamka nilijikuta katikatia ya watu wengi

    wamenizinguka wakinishangaa. Nikawauliza kwa

    mshangao pia

    "kuna nini?"

    mmoja kati ya wale alikuwa mmama aliyekuwa

    ananifahamu. Alikuwa ni jirani akasema

    "bella unaumwa?"

    "hapana kuna nini kwani?"

    "ulikuwa unaweweseka umetokwa na jasho jingi pamoja

    na kuwa na joto kali sana. Tumejaribu kukuita muda

    mrefu lakini hukuamka"

    Nilijichekelesha kuwapoteza lengo. Na wakapotezeka

    kweli, wakaendelea na shughuli zao. Msiba uliisha na

    matanga tukaanua. Upweke ukamtawala mama yake na

    schola. Upweke uliomkosesha raha, hata mimi na schola

    hatukuweza kumpa tulizo la nafsi kama tulikuwa tukijaribu

    kufanya. Nachoshukuru mungu, nilifanikiwa kuianza shule

    nikiwa mwanafunzi wa bweni kwa msaada wa mama

    schola. Nilijiapia ntasoma, nikauahidi moyo wangu

    ntasoma kupitiliza. Uchungu wa shule nilionao niliuweka

    kwenye masomo peke yake. Nilihudhuria kwa mara

    nyngine tena masomo darasani nikiwa nina furaha tele.

    Furaha ya kumuona tena Jordan na furaha ya kuwa

    katika sare pamoja na wenzangu. Nlitumia muda wangu

    mwingi kumsikiliza mwalimu na kujisomea pale

    nilipoupata muda. Niliutumia ule muda wa prepo vizuri ili

    niweze kuelewa pale nilipokuwa sipaelewei. Nakumbuka

    siku moja nikiwa prepo majira ya saa mbili usiku. Mimi

    nilikuwa peke yangu na meza nyingine walikuwa

    wanafunzi kadhaa. Wavivu wachache wakaondoka kulala

    baada ya nusu saa kupita. Mimi na kikundi cha rafiki

    yangu Hilda ndio tulioendelea kukomaa zaidi. Punde

    nikasikia nikiitwa.

    "bella"

    nilipotazama sauti iliyotoka upande wa dirishani,

    sikumuona mtu. Mara ya pili ikaita upande wa kulia.

    "bella"

    nilipogeuka nako kukawa kama awali pale dirishani.

    Nilipokuwa nikijiuliza ni nani. Bla kujua.ghafla nilisikia

    kicheko kikilipuka kwa nguvu mbele ya ubao. Niliyaelekeza

    macho yangu kule niliposikia kicheko kile. Alikuwa ni

    babu. Nikawatzama wakina hilda kama walikuwa

    wamemuona. Lakini wao walikuwa wanaendelea na

    shughuli zao. Waliendelea kuinamia madaftari yao huku

    sehemu yote ikiwa kimya kabisa. Nilipokuwa nikimtazama

    babu, akili yangu ikahama. Nakiri akili yangu ilihama

    kutokana na mawazo yangu ya kibinadamu hayakuwepo

    tena. Akili ikachotwa nikafanya kile alichokuwa

    akinielekeza babu kule ubaoni aliposimama. Babu aliniita

    kwa kidole chake na mimi nilinyanyuka na kumfuata pale

    alipo. Niliwapita wakina hilda. Nakumbuka nilimsikia hilda

    akiniita

    "bella"

    sikuitika kwa kuwa sikujitambua zaidi ya kusikia na kuona

    tu. Akaniuliza bila kujali kama niliitika au lah!

    "leo umechemka mama uanenda kulala"

    pia akaambulia patupu. Nilipofika eneo la ubaoni tu na

    kumpa mkono babu, tukapotea. Tulipotea na babu katika

    mazingira ya kushangaza wala sikujuwa nini kikundi cha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hilda cha kujisomea wangenchukulia vipi. Mimi na babu

    tulielekea Gamboshi. Tulipofika huko nikiwa bado

    sijitambui, babu alinilaza kitandani kama vile vitanda vya

    hospitali. Na kuchukuwa beseni la maji mengi lakini

    yalikuwa meusi sana na kipande cha khanga aina ya

    kaniki. Alianza kunikamulia mahi yale machoni mwangu

    na kunilazimsha nipanue mdomo wangu. Nilipopanua

    akaniambia niyanywe yale maji machafu nikatii. Kisha

    alikuwa akiongea maneno ambayo sikuaelewa kabisa

    wala sikujuwa ilikuwa ni lugha ya wapi. Kila

    nilichofanyiwa sikuweza kuzuia kutokana sikuwa na nguvu

    za kutosha wala kutambua kitu gani nilikuwa nafanyiwa.

    Baada ya kunimalizia hayo babu aliniamsha.

    "bella amka"

    japo nilikuwa macho nikiona kila kitu lakini nilijikuta

    nikihisi nimetoka katika usingizi mzito sana. Nilikumbuka

    kila kitu. Na nilipoamka nilijikuta nipo ndani ya darasa lile

    lile la prepo lakini sasa hakukuwa na mtu hata mmoja.

    Wakina hilda na wenzake walikwishaenda kulala. Babu

    aliniambia

    "bella"

    nilishangaa tena kumuona amekaa pembeni yangu baada

    ya kuniona nikianza kufunua daftari na kutaka kuanza

    kusoma. Aliniambia

    "huu si muda wa kusoma, unapaswa ukalale"

    alikohoa kidogo kisha akameza mate

    "huna sababu ya kusoma kwa kuwa nimekupa nguvu ya

    kutosha . Nguvu ya kufanya miujiza mikubwa sana hapa

    shuleni. Hakuna anayeweza kushindana na wewe tena

    katika masomo. Utakuwa kichwa hata usipogusa daftari

    kwa muda mrefu cha msingi cha kuzingatia usije ni hili

    sharti lingine ninalokupa utakuwa ukiamka usiku na kuiba

    akili za wenzio kila siku usiku wa manane na usimwambie

    mtu yeyote kuwa wewe huwezi kusoma lakini utafaulu tu

    yaani wewe ni genious usijisifie hata siku moja kuna

    ambao wataharibu akili yako pia"

    aliniambi hayo na kutoweka. Niliyakusanya madaftari

    yangu na kurudi bwenini. Nilipokuwa nikipata karibu na

    mlinzi, alikurupuka kutoka katika usingizi mzito. Nilicheka

    kumkuta amesinzia.

    "ulizani bosi nini?"

    nikaendlea kucheka

    "majura bwana!"

    yeye hakucheka wala kutabasamu. Aliniangalia kwa

    makini na kuiangalia saa yake. Mimi pia nikakosa pozi

    nikawa namuagalia. Nikamuuliza

    "vipi?"

    alitingisha kichwa kwa kusikitika kisha aliniuliza kwa

    kutoamini

    "hivi unajua sasa hivi saa ngapi?"

    nilibetua midomo yangu kumwambia kuwa nilikuwa

    sifahamu. Akaniambia kwa manjonjo

    " sasa ni saa kumi kasoro alfajiri"

    alikohoa kidogo na kuniambia

    "kusoma gani huku sasa bella? Nilikujwa kukuomba

    nizime jenereta lakini ukanisihi kuwa unataka kusoma

    kweli ndiyo mpaka saa kumi?"

    aliniuliza ten akiipiga piga saa yake akiwa ananiangalia

    kwa mshangao. Nilimjibu kivivu

    "niache bwana mi nikalale Majura tutazungumza kesho"

    aliniangalia akisikitika nilipokuwa nikiondoka. Akawa kama

    anajiambia mwenyewe

    "yaani kama watoto wangu wangekuwa na uchungu wa

    kusoma kama wewe? Leo nisingekuwa mfungua geti mimi

    hapa leo"

    kisha akcheka kicheko cha kuudhika akasema kwa nguvu

    kidogo, huku sauti yake ikinisindikiza kushuka ngazi.

    "haya bella na mungu akulinde ufanikishe ndoto zako"

    Niliingia bwenini na kuwaamsha wawili watatu ambao

    walikuwa bado hawajazama moja kwa moja usingizini.

    Walishitushwa sana kuniona nikiwa na madaftari usiku

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    huo nikitoka prepo.

    "he makubwa watoto mliotumwa na kijiji mna kazi kweli"

    huyu alikuwa na mdomo sana nikamsonyo nikampita hilda

    aliyekuwa akijigeuza geuza kitandani kwake chini juu

    akiwa amelala Schola.

    "bella"

    aliniita kama hakuamini kuniona mimi nkiwa ndiyo nakaa

    kwenye kitanda changu cha chini jirani yake. Aliamka

    akakaa kitako. Aliniuliza

    "tangu muda ule umeenda chooni mpaka sasa ulikuwa

    prepo?"

    kiukweli alishangaa sana alishangaa kwa kuwa hakikuwa

    kitu cha kawaida. Mimi nilimpa tabasamu tu kisha nilivua

    shamba dress zangu na kulala. Sikuchukua walao zaidi ya

    robo saa nikatekwa na usingizi. Usingizi wa leo ukawa

    mtamu mtamu zaidi. Nililala bila ndoto yeyote mbaya.

    Nikalala zaidi kwa kuwa babu hakuja kunitembelea tena

    usiku huu. Nilalala kwa amani mpaka kengele ya asubuhi

    ilipopiga kuitwa paredi. Kengele hiyo ilinikuta nikiwa

    nimeshamaliza kujiandaa nimeshavaa sare zangu nikilekee

    paredi.

    ....

    Usiku wa siku ya pili nikawa siendi tena prepo kama ilivyo

    kawaida yangu wakina hilda wakaniita tuongozane lakini

    mimi sikuwa tayar kwenda tena

    "bella jamani mbona hatukuelewi?"

    "nyie nendeni tu jamani mi sijisikii poa"

    niliwajibu nikijichekelesha kisha wakaondoka. Ila hilda

    hakuridhika kuniacha mimi nikilala bwenini kwa kuwa

    alifahamu uchungu wangu wa kusoma. Nikajisemea

    "laiti angejua asingenionea huruma"

    mtu kama mimi sasa sikupaswa kuonewa huruma tena.

    Nilikuwa nimeuvaa umalkia nje ndani nikiwa ni kiumbe

    kinachotisha. Kiumbe kisicho na huruma. Kiumbe

    kinachosubiri kuchukuwa matilio ya wenzangu yote

    waliyoyasoma niyahamishie jwangu kiuchawi. Nakumbuka

    babu alinipa dawa ya kufanya haya yote yatimie. Aliipa

    kinyesi cha ndama yaani ng'ombe mtoto kisha

    akakichanganya na mchanga wa kaburi. Babu aliniambia

    "mchanga wa makaburini una nguvu sana katika kazi zetu

    za kichawi"

    kisha alinielekeza jinsi ya kuichanganya dawa hiyo.

    "ichanganye na mafuta ya mgando kisha ipake kwenye

    makalio yako na paji la uso hii itakusaidia wakati ukiwa

    uchi kabisa unaweza kumsotea makalio yako juu ya

    kichwa cha muhusika ambaye umepanga kumuibia

    masomo yake kichwani kwake ukishafanya hivyo msonye

    sana yaani sonyo kubwa kisha asubuhi uanpoamka

    usimuangalie usoni hata akikusalimia angalia chini na

    uepuke sana kukutanisha macho ya mtu mwingine na

    yako iwe unamfahamu au humfahamu"

    nilipokumbuka maelekezo ya babu, nilitabasamu

    "kazi rahisi sana"

    nilijisemea kimoyomoyo. Nikapitiwa na usingizi wa

    mang'amang'amu mpaka maira fulai niliposikia kelele za

    wanafunzi wakirudi kutoka prepo. Niliamka bila kufungua

    macho. Nikamsikia schola na hilda wakizungumza

    "masikini kabella ketu kamelala"

    alikuwa hilda, schola akajibu

    "muacheni dada yangu jamani apumzike si mnakumbuka

    aliwahi kusoma hadi sa kumi ya alfajiri!?"

    wakacheka kwa pamoja kisha kila mmoja nikamsikia

    akipanda kitandani wake kulala. Sikusubiri muda upite

    sana wauzoe usingizi. Ilinibidi wakati huo huo niipulize ile

    dawa ya usingizi. Ile dawa iliyoitwa mpiyuru. Mti mmoja

    ambao sikujua jina lake vizuri ulichomwa na kukaushwa

    juani majivu yake kisha ikalowekwa na unga unga fulani

    mweupe ndani ya damu ya mtoto mchanga. Vitu hivyo

    vyote vikawekwa kwenye jua kali kali sana yaani kisha

    vikawekwa juua ya dari kwa siku saba ikawa dawa kamili.

    Dawa iliyotimia kwa kunuia maneno ambayo ulikuwa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ukitaka. Dawa hii kama ungekuwa ukitaka watu hawa

    walale muda wako wote mpaka utakapomaliza shughuli

    basi wangetii. Kamakumvuta aliye mbali au hata kuvuta

    mvuto na bahati ya kitu chochote katika maisha yako

    kienda sawa dawa hii hutimiza. Ina nguvu ya kutosha.

    Basi mimi niliipuliza dawa ile niliyoichota kidogo kutoka

    katika kikopo nilichopewa na babu kule Gamboshi.dawa

    ilikuwa imejaa mimi nikaiweka kwenye karatasi na kuanza

    kuipulizia darasa zima. Wote wakakoroma hata ambaye

    alikuwa analala kimya kimya. Nilisaula nguo zangu na

    kubaki uchi wa kuzaliwa yaani sikuwa na nguo yeyote

    mwilini mwangu. Nilimfuata Hindu. Huyu msichana

    alikuwa na akili sana darasani. Nilimkalia kwa juu na

    kuanza kujisugua sugua makalio yangu niliyojipaka ile

    dawa kisha nikamsonya na kumfuata schola, naye

    nilijisugua sugua juu ya kichwa chake mpaka nilipomaliza

    kunuia yote niliyokuwa nikiyataka kutoka kwake na

    kumaliza nusu bweni zima. Wengine ambao hata mimi

    niliwapita sikuwa na haja nao. Nilirudi kulala baada ya

    kuanza kuona kunakaribia kukuchwa. Sikutaka mtu

    anikute nikiwa katika hali ile.

    ....

    Hali ile ikaendelea bila kuonesha madhara yeyote kwangu

    yaani kushitukiwa lakini kwa wahusika walipata tabu

    sana. Tabu ya kujaribu kukumbuka sana kila mara

    walipokuwa wakikutana na maswali kadhaa ambayo jana

    waliyasoma usiku na leo walikutana nayo darasani lakini

    majibu yalikuwa yanakuja na kupotea. Mimi nilikuwa

    nikiwacheka kichinichini pale niliokuwa nikikaa na

    mwalimu kunipongeza kuwa nimejibu sahihi. Wale ambao

    walikuwa wakienda kusoma prepo wakaanza kuona uvivu.

    Walichoshwa kuona walikuwa wakifanya juhudi nyingi

    katika kusoma lakini walikuwa wakisahau yote mara tu

    walipokuwa wakigusa vitanda vyao. Ni hapo mmoja

    mmoja alianza kumuuliza mwenzake.

    "yaani mwenzenu inanishangaza yaani mi nasoma usiku

    lakini asubuhi nikiamka kila kitu nimesahau ni nini siku

    hizi?"

    mwingine aliitikia vivyo hivyo na kuonekana hali hiyo

    iliwakatisha tamaa. Lakini sasa wakaniona mimi ni kama

    kimbilio lao wale walioniona sasa nimekuwa mzembe

    kutosoma kwangu kabisa prepo. Schola alikuwa mmoja

    wao kuniuliza ile na lile ambalo hakulielewa.

    "hivi bianka siku hizi umebadilika sana"

    nilishangaa kubadilikaje? Yeye akanijibu

    "yaani huingii prepo kabisa lakini unatukimbiza sana

    aisee"

    alikuwa akitabasamu na kutamani kujua siri yangu.

    Akaniuliza

    "embu nipe mbibu mpya shosti uliyoigundua maana hata

    sielewi siku hizi nna nini mwenzio"

    mimi nilicheka tu kumpoteza maboya kisha nilimwambia

    bila kuwa na ukweli wowote katika yote niliyomueleza

    "msikilize sana mwalimu. Labda huwa unasoma kitu

    ambacho mwalimu hajakizungumzia"

    nilimuona yeye akiridhika na kuahidi atasoma kile

    ambacho mwalimu amemuelekeza darasani kuachana na

    vitabu vya nyambari nyangwine.

    Babu alikuja kunipongeza sana kwa kazi jinsi ambavy

    nilikuwa nikiitekeleza. Sikuchoka na niliifanya kwa bidii.

    Niliwachosha wanafunzi wasiipende shule, nikawachosha

    walimu wacukie kufundisha. Sikuishia tu katika bweni

    langu. Nilienda katika mabweni tofauti tofauti na

    kuwachezea wanafunzi wengine. Wengi walianza

    kulalamika kuwa wanachoka sana siku hizi. Walipiga

    mihayo wakiwa darasani na wengine waliombea mwalimu

    amalize haraka waende kulala.



    Babu alikuja kunipongeza sana kwa kazi jinsi ambavy

    nilikuwa nikiitekeleza. Sikuchoka na niliifanya kwa bidii.

    Niliwachosha wanafunzi wasiipende shule, nikawachosha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    walimu wacukie kufundisha. Sikuishia tu katika bweni

    langu. Nilienda katika mabweni tofauti tofauti na

    kuwachezea wanafunzi wengine. Wengi walianza

    kulalamika kuwa wanachoka sana siku hizi. Walipiga

    mihayo wakiwa darasani na wengine waliombea mwalimu

    amalize haraka waende kulala. Jordan sikuwahi

    kumchezea wala kumfanyia chochote nilimpenda sana

    jordan nilimpenda kwa moyo wangu wote. Nilidirika

    kujichora jina lake kwene mkono wangu kwa kutumia

    utovu wa korosho. Sikujali maumivu ila nilifanya kwa

    watu niwepandao. Mama yanagu pamoja na jordan

    wangu. Nilijisikia fahari sana kuwaonesha kila mtu ni kiasi

    gani nampenda Jordan. Nikavunja agano nililopewa kule

    Gamboshi. Pete niliyopewa na mkuu wa Gamboshi

    nikampa Jordan aivae kama urembo kwa kuwa aliipenda.

    Ilikuwa ni pete ya dhahabu. Pete nzuri yenye urembo wa

    kila aina. Siku moja babu alinifuata na kunieleza kuwa

    kesho jumapili inabidi niende mjini na schola. Na

    nitakutana na mchungaji fulani ambaye ni mtu wao na

    kuna jambo atakaloniambia nilitekeleze. Nilikubwali.

    Alinisisitiza nitumie mbinu zote mpaka nihakikishe

    nimeenda na schola. Nikamwambia

    "usiwe na shida babu ni lazima akubali"

    pale shuleni kumbe kuna watu ambao walishaanza

    minong'ono. Walikuwa wakinijadili chinichini kuwa mimi ni

    mchawi. Sikujua walihisi vipi ila hili swala lilianzia ofisini

    kwa walimu. Ile pete ambayo nilimpa Jordan

    walikwishaivaa rafiki zake wote. Wa mwisho kuivaa

    alikuwa ni Kelvin. Aliitwa ofisini na mwalimu wa nidhamu

    na kuulizwa

    "hiyo pete umeipata wapi?"

    kelvin alikuwa ni kijana mtundu na uoga ulikaa pembeni

    naye hivyo alijibu haraka kwa kutumia uongo alioufikiria

    haraka haraka.

    "ni ya kwangu mwalimu"

    mwalimu yule wa kike alitabasamu na kumwambia kelvin

    "hiyo pete si ya kwako. Mumeshaivaa kundi lenu wote na

    wewe ni wa mwisho imetoka kwa jordan aliyepewa na

    mpenzi wake bianka. Nimeongopa?"

    kelvin alishituka sana aliyatoa macho yake kutokana na

    bumbuzwazi iliyomkumba ghafla asijue mwalimu alijuaje.

    Asijue kuwa mama yake na shola alikwisha kuja hapo

    shuleni na kutoa malalamiko kunihusu mimi. Siku kadhaa

    nyuma niliwahi kumfuata kimazingira mama schola na

    kumueleza

    "naomba usisali muda wasiku kumuombea schola"

    nilimaanisha kweli. Sikupenda anaposali. Alikuwa

    akiharubu kazi zangu na kunufanya nisitishe kuwafanyia

    wengine. Mama yake aliwaomba walimu wanitzame kwa

    makini kwakuwa nilikuwa nina ishara zote za kichawi.

    Habari hivyo ikasambaa kutoka katika ofisi za walimu na

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    minong'ono kuwafikia wanafuni kutoka katika kinywa cha

    kelvin. Jordan alifahamu kuwa mimi naitwa mchawi naye

    akaniogopa sana ila ni mtu mmoja tu ambaye hakunijua

    mimi vizuri hakunijua upade wangu wa pili mimi ni nani.

    Yaani mimi ni mtu wa aina gani ndani ya moyo wangu.

    Aliupenda umalaika nilio nao nje lakini aliti angefahamu

    kuwa mimi ni mtu wa aina gani ndani asingethubutu kuwa

    karibu na mimi. Huyu alikuwa ni schola sikuwa na nia ya

    kumdhuru, ila babu na uongozi mzima wa gamboshi;

    ulivutiwa naye. Ulinishauri nikae aye karibu kwa ukaribu

    sana.

    Jumapili hii nikamtafuta schola sikumuona, nilimuulizia

    kwa kila mtu; hakuna ambaye alikuwa na jibu. Nilipochoka

    kumtafuta, nilimuona kwa mbali maeneo ya getini.

    Alikuwa na tabasamu mdomoni mwake, mkononi akiwa

    ameibeba biblia. Alikuwa amependeza sana. Sikumsubiri

    anifikie pale nilipo nilimfuata mpaka hapo. Alionesha

    kushangaa kitendo cha mimi kumkimbilia isivyo kawaida.

    "bella!?"

    aliniita baada ya kusimama. Mimi nilisimama pia

    nikaanza kutembea mwendo wa kawaida mpaka

    nilipomfikia. Nikamwambia jambo lililosindikizwa na

    tabasamu pana.

    "schola mama, naomba unisindikize kwa mtu mmoja hivi"

    alionesha kushangaa. Alishangazwa na kitu ambacho

    mimi sikukifahamu ila aliniuliza

    "hivi bella huoni kuwa nimetoka kanisani jamani?"

    "sikia rafiki yangu hii ni emergency naomba unisaidie

    mwenzio"

    nilimlainisha schola akaingia mkenge. Alirudi bwenini na

    kuitupa biblia yake juu ya kitanda, tukatoka vile vile

    alivyoingia. Hakubadilisha chochote. Tulielekea mjini kwa

    kumpa kitu kidogo yule mlinzi rafiki yangu. Tulitoka na

    kuelekea kwa mzee mmoja aliyeitwa shekhe Majid.

    Shekhe huyu alikuwa anasomea watu kisomo cha kuwatoa

    watu majini na kuwatoa watu katika matatizo

    yanayowasibu. Babu alinielekeza kuwa Majid hakuwa

    hivyo kama vile wengi ambavyo walimfahamu. Majid

    alikuwa ni jini kamili. Jini lililovaa mwili wa binadamu na

    kusambaza ubaya juu ya watu wema. Alikuwa akiroga na

    kuwafanyia mabaya. Huyu alikuwa ni jini aliyetengenezwa

    na moto. Huyu ni jini mbaya sana. Alikuwa akiishi katika

    mbuyu ambao watu wa kawaida walikuwa wakiona kama

    sehemu nzuri na ya kawaida. Tulipofika maeneo ya

    mwananyamala kisiwani, huko kwa Majid, schola alianza

    kuingiwa na wasiwasi. Aliniuliza

    "huku tunaenda wapi bella jamni mbona vichochoroni

    sana?"

    nilimzawadia tabasamu pana, na kumwambia kwa asijali.

    Nilimuonesha nyumba moja ya kifahari iliyo pembezoni

    mwa makaburi. Schola akanisimamisha

    "we bella! Nyumba yenyewe ndiyo ile?"

    alikuwa akiuliza kwa mshangao uliomsawajisha uso wake

    "ndiyo schola yule ni rafiki wa babu yangu na ana jambo

    muhimu la kuniambia. Kwanini umeniuliza hivyo?"

    "yaani ile nyumba sijuhi kwanini"

    alipatwa na kigugumizi cha ghafla. Alikuwa akitetemeka

    sana. Kisha aliendelea

    "hapana bella ile sio sehemu nzuri nimepatwa na

    msisimko mkubwa nilipoiona ile nyumba na haswa

    uliponieleza kuwa ndiyo sehemu ambayo tulikuwa

    tunaenda nywele zangu zimenisisimka sana"

    nilicheka kisha nikamueleza kuwa asipatwe na wasiwasi.

    Majid ni mtu mzuri na asiwe na wasiwasi naye. Nilimsifia

    kuwa majid alikuwa ni mpole na mwenye upendo wa

    kushangaza. Nilimpa hadithi za uongo za kutunga

    kumuhusu majid. Nilijifanya kumfahamu fika majid kumbe

    nilikuwa simfahamu hata anafananaje. Kwa mwendo wa

    taratibu huku bado uoga ukimtawala. Nilimpa tu moyo

    mpaka tulipoifikia nyumba ya majid. Nyumba hii babu

    alinielekeza kabla sijaifikia hivyo haikunipa shida kupajua

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wapi. Babu alinieleza kuwa majid alikuwa anafahamu kila

    kitu kuhusu ujio wangu na Schola. Babu alinieleza kuwa

    walikuwanahitaji kivuli cha schola kivuli kilicho na nguvu,

    nguvu ya kuwaharibia kazi zao. Yaani kazi yao ikiharibika

    na mimi nisingefanikiwa chochote katika mambo yangu ya

    kichawi. Mimi sikuwa tayari kupoteza nguvu zangu kwa

    ajili ya kujilinda. Nilikuwa tayari kutoa kumtoa kafara

    kulinda nguvu zangu zisipotee. Tukaugonga mlango sauti

    ya mwanaumeikatupokea bila kuchelewa. Alikuja kufungua

    mzee mmoja mfupi mwenye upara lakini ndevu nyingi

    zilitawala kidevu chake. Alikuwa na asili ya kiarabu.

    Alitabasamu kutuona. Mimi nilipomtazama hakuwa na

    kiwiliwili cha binadamu chini yaani kuanzia kiunoni mpaka

    kushuka miguuni, alikuwa ni moto tu. Kwa mtu mwenye

    macho ya kawaida usingeweza kuona kile ambacho

    nilikiona. Aliniita jina langu

    "bella umekuwa mama"

    nilikuwa katika mshangao lajini sikutaka schola afahamu

    chochote. Alitukaribisha ndani huku Majid akiwa na furaha

    sana ya kuniona. Tulipofika sebuleni ndipo kila kitu cha

    ajabu bila kutarajia kikatokea. Niliiona miale fulani

    iliyofanana na utandu wa buibui. Ulimvaa schola na yeye

    kujigawa mara mbili. Yaani schola sasa walikuwa wawili.

    Yule niliyekuja naye nilikuwa naye akishangaa mazingira

    ya sebule ya majid. Lakini yule aliyemtoka schola

    ninayemfahamu alikuwa akilia akielekea katika chumba

    ambacho majid aliingia. Nllijiuliza maswali mengi sana

    lakini sikupata jibu sahihi. Majid alitoka akiwa

    amepambwa na tabsamu lisilo na raha yeyote. Alikuwa

    amebeba jag lililobeba maji ya matunda. Alituambia kwa

    ukarimu

    "karibuni jamani. Msiishangae sebule yangu haina viti

    kama mlivyozoea"

    alipotusogelea aliliweka lile jag katia stuli iliyoa na vitairi

    na kuisukuma kidogo na kutuelekeza pa kukaa

    "hii mito ndiyo kama makochi yangu karibuni jamani"

    nilimuona schola akitabasamu na yeye ndiye alikuwa wa

    kwanza kukaa. Aliniita

    "bella kaa basi"

    majid naye alitabasamu na kuniambia

    "mtazame mwenzako ameshakaa. Embu nawewe ukae

    basi tuzungumze"

    sikukaa kwa sabbu eti sikuyazoea mazingira ya aina ile.

    Nilichoshangaa uoga wa ghafla uliomtoka schola

    alipazoea hapo na kuwa kama mwenyeji nilipokaa majid

    alianza kuzungumza

    "karibu bella"

    "asante anko huyu hapa ni rafiki yangu anaitwa schola"

    alimgeukia schola na kufanya kitendo cha kushangaza.

    Aliutoa ulimi wake na kumtoa kitu mfano wa moshi mzito

    mweusi ulimtoka mdomoni mwake schola. Nilikuwa

    nikistaajabu sana linalotokea. Schola hakuonesha

    wasiwasi wowote wale kufahamu kile alichokuwa

    akifanyiwa. Nilimtazama majid kwa makini kisha wote

    walitoleana tabasamu. Tabasamu la heri ya kujuana.

    Walishikana mikono na hapo ndipo schola akamsalimia

    majid kwa mara ya kwanza. Tuliongea mengi na hadthi

    zisizo za kweli kuhusu mambo mbali mbali kumpoteza

    schola. Baada ya muda kwenda mimi na schola tuliaga

    na kuondoka. Majid alinishukuru akanishukuru sana. Kisha

    tulirudi shule. Tulipofika shule kama kawaida yangu mimi

    nililala nikamuacha schola yeye aeleke kusoma. Huko

    ndipo schola naye akawa anasikiliza hadithi zilizotapakaa

    shuleni hapo. Kwa bahati nzuri waliokuwa wakihadithia

    kunihusu mimi ni mchawi walikuwa hawanifahamu. Hivyo

    wakahadithia kinadharia jinsi nilivyo

    "tena anakaa katika bweni lenu kabisa, humfahamu

    jamani?"

    alikuwa akimwambia schola. Schola bado akawa

    hajanijua mpaka pale mmoja aliposema kitu

    kilichomshitua

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "tena leo mwalimu karim ametuambia kuwa alimuona

    akiwa na msichana mwingine maeneo ya mwananyamala

    kisiwani mwalimu karin alivyokuwa mbea jamani

    aliwafuatilia mpaka huko"

    schola alishitushwa sana baada ya kusikia hilo jambo.

    Alianza kutetemeka na kusikiliza kwa makini.

    "basi yule mwalimu akawa anatuambia kuwa walipokuwa

    wanaenda ni maeneo ya makaburini chini ya mbuyu

    mmoja mkubwa"

    schola alibwatuka

    "mbuyu?"

    wote walimtazama schola kwa mshangao. Schola alikuwa

    analia. Hapo ndipo schola alisema

    "jamani huyu aliyekuwa na huyo dada ni mimi jamani

    nakufa mie jamani mungu wangu bella mchawi bella wee

    unaniua"

    walimbembeleza na kushauriana kwa pamoja kwenda

    kumuamsha matroni kumueleza swala hilo. Kutokana na

    usiku ulikuwa mkubwa. Matroni hakuwa na la wa

    kuwajibu. Aliwashauri waende kulala na kesho asubuhi

    atazungumza na walimu na kujua nini watanifanya. Mimi

    sikutishwa kwa kuwa niliwasikia kila kitu walichokuwa

    wakizungumza. Nilikuwa pale tu wakati wote nilioufahamu

    kuna watu walianza kunifuatilia. Kuna watu walikuwa na

    nia mbaya na mimi. Nilijinyanyua kutoka kitandani na

    kuliacha gogo la kuwapumbaza wengine kama mimi

    nilikuwa nimelala bado. Nilikuwa nikisikia kila kimoja

    walichokuwa wakizungumza na matron matilda na

    walichoelezwa na matroni. Waliporudi mabwenini mimi

    nilirudi kulala pia. Sikumfanya chochote yule matroni kwa

    kuwa nilimuona hana hatia nilirudi kulala nikisubiri hiyo

    kesho itakuwaje. Nilitaka nifahamu nini wataongea na hao

    walimu kunihusu mimi.

    Asubuhi tuliamka kama kawaida, paredi tukajumuika

    pamoja wanafunzi wote. Kisha ule wakati wa kila mtu

    aliutamani ukafika. Nilipoingia darasani, kila mtu

    alinikwepa. Yaani walinikwepa kama waliniona

    nimejimyea. Sikujjali kwa kuwa kila nilichokifanya ni kwa

    ajili yangu na niliona fahari kufanya hivyo nilichojali ni

    furaha ya Jordan yaani nilijisikia raha sana nikimuona

    Jordan akitabasamu mbele yangu na kuniambia lile neno

    Nakupenda kutoka kinywani mwake. Hakika nilimpenda

    sana Jordan. Nilimpenda kupita kiasi na nilitambua hilo.

    Nikawa nimekaa kwenye kiti changu darasa zima likiwa

    kimya. Ni sauti za watu wachache walikuwa wakikohoa

    na wengine wakinong'ona. Ni wawili watatu ambao

    walinitupia jicho la wizi wizi. Mimi niliwatazama pia huku

    nikitabasamu tu bila kuwaonesha kuwa nilikuwa

    nikiwaangalia. Nilipotazama pale ambapo schola alikuwa

    anakaa siku zote, hakuwepo. Nikaangaza angaza kila

    sehemu ya darasa, sikumuona pia. Nikahisi huenda bado



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hakuwa ameamka. Lakini mbona nilimuona paredi?

    Nikaamua nimpotezee nikiendelea kufunua dftari

    nikipitisha pitisha macho nikijifanya nasoma. Haukupita

    muda mrefu aliingia schola na mwalimu wa zamu wiki

    hiyo alikuwa ni mwalimu karim. Yule ambaye niliwasikia

    wanafunzi wakisema kuwa alituona mimi na schola

    tukienda kwa majid. Schola alipoingia alitazama moja kwa

    moja pale kwangu nilipokaa. Nilipoiona sua ya schola

    nilishitushwa. Ulikuwa ni uso uliovimba na alikuwa akilia.

    Ulivimba kutokana na kulia kwa muda mrefu sana. Schola

    hakuja kukaa, alisimama pale mbele mpaka alipoingia

    mwalimu Karim na Bushiri. Walikuwa wamebeba fimbo.

    Nikafahamu fika wote walikuja kwangu baada ya kikao

    cha kunijadili kuhusu tuhuma zinazendelea kunihusu mimi.

    Mwalimu bushiri ndiye aliongea. Huku mwalimu karim

    akiniangalia mara moja moja

    "wanafunzi hamjambo"

    wote kwa pamoja tukamsalimia. Kisha tulikaa chini baada

    ya kusimama kwa heshima. Aliirekebisha sauti yake

    baada ya kikohozi kifupi kumpitia, kisha aliendelea

    "sasa wanafunzi labda tuwaulize ni wangapi

    wamekwishawahi vaa pete ya aina hii?"

    aliitoa ile pete niliyopewa na babbu na mimi nilimpitia

    Jordan. Mimi nikamtazama jordan, mwalimu karim na

    schola wakanitazama mimi. Jordan alikuwa ameshituka

    sana na yeye akanitazama mimi.’



    Walikuwa wamebeba fimbo.

    Nikafahamu fika wote walikuja kwangu baada ya kikao

    cha kunijadili kuhusu tuhuma zinazendelea kunihusu mimi.

    Mwalimu bushiri ndiye aliongea. Huku mwalimu karim

    akiniangalia mara moja moja

    "wanafunzi hamjambo"

    wote kwa pamoja tukamsalimia. Kisha tulikaa chini baada

    ya kusimama kwa heshima. Aliirekebisha sauti yake

    baada ya kikohozi kifupi kumpitia, kisha aliendelea

    "sasa wanafunzi labda tuwaulize ni wangapi

    wamekwishawahi vaa pete ya aina hii?"

    aliitoa ile pete niliyopewa na babbu na mimi nilimpitia

    Jordan. Mimi nikamtazama jordan, mwalimu karim na

    schola wakanitazama mimi. Jordan alikuwa ameshituka

    sana na yeye akanitazama mimi. Bushiri akarudia tena

    "nauliza kwa ulinzi wenu mathubutu ni nani ambaye

    ameshaivaa hii pete?"

    walinyoosha mikono yao wavulana wawili akiwemo Kelvin

    wakiongozwa na Jordan wangu, jumla waki watatu.

    Bushiri akatabasamu kifedhuli kisha aliniita mimi Bella

    simama na kila kitu chako. Nilikusanya madaftari yangu

    niliyoyafungua na kuyaibeba nikawa nimesimama. Bushiri

    akaniambia kwa sauti aliyoitia ukali kidogo

    "njoo huku"

    nikaenda mpaka pale mbele walipokuwa wamesimama.

    Tukawa tumetoka. Nyuma tukaacha mzozo mkubwa,

    yaani minong'ono ilianza kwa sauti ya chini hatimaye

    darasa likageuka soko la kariakoo. Nikawa naelekea

    ofisini kwa walimu wote wanapokaa. Nilipofika huko

    nilikuta kuna kikao kikubwa cha siri. Walikuwa wavulana

    wengine wanne ambao walikwisha vaa pete ile. Mama

    yake na schola alikuwa amekaa mbele akiwahadithia

    jambo. Jambo la kushangaza na jambo lililowavutia kila

    mmoja aliyekuwa eneo hilo waliponiona naongozana na

    schola pamoja na walimu na wale wakina Jordan,

    walinyamaza kuongea. Nilimsalimia mama yake schola

    hakuitika. Nikawa nimeelekezwa pa kukaa kisha nikawa

    nawatazama kila mmoja aliye katika kikao hiko kwa

    awamu. Mama yake na schola alikuwa amefura kwa

    hasira akinitazama kwa chuki. Kifua chake kilipanda na

    kushuka kana kwamba alitamani kunimeza muda wowote

    kama angekuwa na uwezo huo. Mwalimu mkuu ndiye

    alianza kunisemesha.

    "wanakuita nani hapa shule?"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alianza kuniuliza kwa kejeli, tabasamu liloudhi likiuharibu

    uso wake. Na mimi nikatabsamu vivyo hivyo nikamjibu

    jibu la kipumbavu kama alivyotaka.

    "jina langu ni Bella"

    akacheka kidogo kisha akaipaza sauti yake kwa hali ya

    kukereka

    "bianka"

    akayatoa macho yake kama aliyejaribu kunitisha lakini

    uoga ulikuwa mbali na moyo wangu mimi pia nilimkazia

    macho. Akaniuliza

    "hii pete ni ya nini? Na ilikuwaje ikaingia shuleni na

    unafahamu haturuhusu vitu kama hivi hapa?"

    aliitoa ile pete akaitupa juu ya meza kwa dharau.

    Niliitazama ile pete bila kujibu chochote. Niliitazama zaidi

    ya dakika ishirini. Mkuu wa shule alisimama akawa

    anazungukazunguka nyuma ya viti vya walimu wengine na

    waliojumuika katika kikao hicho. Alizungumza.

    9aomba utujuze hii pete ina lengo gani hapa shuleni?"

    alikuja nyuma yangu na kuniinamia kwenye sikio langu na

    kuniuliza

    "pete ile ndiyo urithi wa kichawi au ya kumroga

    aliyeivaa?"

    akatabasamu na kucheka kimaudhi. Kisha alinigeukia na

    kunitoa katika lile nililokuwa naliwaza kwa kugonga meza

    kwa nguvu na kuniambia.

    "hii pete ni yako na siku zote ulikuwa unaivaa huna

    sababu ya kuitazama kama ndiyo leo mara ya kwanza

    umeiona. Naomba utujuze hii pete ni ya nini?"

    nikapata la kumjibu. Niliuinua uso wangu na kumwambia

    "ni ya urembo wa kawaida tu"

    alinitazama kwa muda akawa amesimama

    kuzungukazunguka alikokuwa anakufanya na kuniambia.

    "pete ya kawaida? Urembo? Na kwanini basi waivae

    wavulana na si wasichana wenzio?"

    "niliyempa nafikiri ndiye ana jibu hilo"

    nikawa nimemtazama Jordan aliyekuwa amenuna mithili

    ya kutaaka kupasuka. Mwalimu mkuu na wengine nao

    walimgeukia Jordan. Mkuu hapa akawa amelegeza ukali

    akawa aamuuliza Jordan kwa sauti ya upole.

    "jordan embu tujuzue imkuwaje umegewa ete

    usiyeifahamu? Pete ya maajabu isiyovutia kwa lolote.."

    hasira zikanipanda, zilinipanda toka ndani. Yaani nilisikia

    kitu cha ajabu kikilpuka ndani ya moyo wangu na kutaka

    kumfanyia mwalimu mkuu lakini nikajizuia. Kisha nikawa

    namsikiliza alikuwa akiendelea

    "ukaichukua wewe ukaivaa ikaanza kutembea kwa

    wengine na ni wavulana wenzio tu na si wasichana?"

    jordana akawa anatokwa na jasho jingi hata nikaanza

    kumuonea huruma. Ule upendo nilio nao juu yake

    ukanitafuna moyo wangu nikajihisi kumtupia mpira mpenzi

    wangu asiye na hatia. Nikiwa nimeyatoa macho kutoka

    kwake nikaiangalia meza ndipo Jordan akaipata sauti

    yake.

    "ni mimi ndiye niliiomba kutoka kwa Bianka"

    akawa ananiangalia kwa jicho la chuki huku akimjibu

    mwalimu mkuu swali. Akawa anaendelea

    "lakini siku aliyonipa, hazikupita siku kadhaa ikapotea

    katika mazingura ya kushangaza pale nilipoihifadhi. Lakini

    cha kushangaza mara ya mwisho nilimkuta nayo Kelvin"

    hapo ndipo akanyamaza na kumwangalia mwalimu mkuu

    aliyenyamaza kimya muda wote na kumwambia

    "mimi sifahamu chochote zaidi ya haya niliyokueleza

    mkuu"

    mkuu aliitikia kwa kuonesha kumuelewa. Kisha mkuu

    alituambia wote kwa pamoja baada ya kurudi katika kiti

    chake kilichokuwa kikitazamana na changumimi ila kwa

    umbali mrefu sana kutokana na meza iliyo katikati yetu.

    Akasema.

    "nina kila sabbu ya kuwaruhusu wote muende darasani

    lakini hapa abaki schola na bella peke yake"

    kila mmoja ainyanyuka akawa anaelekea darasani. Mimi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nikawa naichezea chezea mikono yangu mara nishike

    daftari mara vidole sikujua kitu gani sahihi cha kufanya.

    Mkuu akasema

    "bella nimesikitika sana kwa hali iliyopo kwako sasa"

    mimi nikawa namtazama tu tena kwa makini.

    "nilipopata taarifa umefiwa na mama yako nilisikitika sana

    nikadhani huenda ungeanza kuwa na uchungu wa kusoma

    kwa bidii"

    akameza funda la mate kisha aliendelea.

    "lakini haikuwa kama nilivyotarajia. Wewe umekuwa na

    sifa mbaya zaidi kuliko mwanafunzi yeyote shuleni. Wewe

    umekuwa na mambi ya ajabu ajabu"

    mkuu wakati anasema hayo alitokea yule mlinzi Majura.

    Nilishangaa sana kumuona kati ya watu wanaohusika

    katika kikao hicho. Mwalimu alimgeukia majura na

    kumueleza

    "embu Majura kabla hatujachukua muda wako mwingi

    naomba utujuze chochote kuhusu rafiki yako Bella"

    nilipomtazama Majura, nikaiona sura ya usaliti na kicheko

    cha kebehi. Nikamchukia Majura na kumuona kama adui

    yangu mpya. Nikaitamani nguvu yangu mbaya niweze

    kumsambaratisha Majura. Nikamtazama kwa dharau

    nikamsonya. Yeye akacheka kidogo kisha akaanza

    kuzungumza.

    "mwalimu ninachoweza kusema huyu si mwanafunzi"

    macho ya kila mmoja katika kikao hicho yakang'aa kwa

    kustaajabu. Yeye akaendelea kuzungumza

    "hapo kabla naanza kumjua bianka kabla ya kumjua bella,

    nilimuona ni msichana mzuri tu mwenye utii wake kwa

    kila mtu. Lakini baada ya muda ndipo nilianza kuona

    vituko"

    mwalimu Bushiri akakohoa kidogo nilipomtazama naye

    alinitazama. Nikaona hana la maana huku nikiendelea

    kumsikiliza Majura

    "mimi nimechanjwa chale"

    alianza kuonesha chale zake mikononi na kila sehemu ya

    mwili wake kwa kutuonesha zile za mgongoni na kila

    sehemu.

    "hizi chale hunisaidia mimi kuona wacawi na kila kitu

    wanachokifanya. Siku moja bella akiwa na wenzake huko

    darasa la kule juu wanajisomea alitoweka ghafla bila

    wenzake kuonesha jambo lolote la kushangaza lilotokea.

    Lakini pale alipokuwa amekaa bella, aliuacha mgomba

    uliyomuwakilisha. Hivyo kama hukuwa na ile dawa ya

    kukufanya kuona wachawi basi usingeweza kutambua

    kama yule si bella"

    kila mtu alikuwa anashangazwa na hadithi hizo za

    majura. Japo ilikuwa ni kweli mimi nilikaa kimya.

    "bella alikuja akachukuliwa na babu mmoja mzee sana na

    anayeonesha ni ana nguvu nyingi sana za kichawi.

    Alimchukua bella mpaka sehemu ambayo mimi

    sikufahamu walielekea wapi lakini baada ya muda mimi

    nikapitiwa na usingizi. Hivyo sikutambua kuwa bella

    alirudi muda gami kwa kuwa ilikuwa yapata majira ya saa

    kumi kasorobo alfajiri ndipo bella alirudi akiwa anaelekea

    darasani. Mimi sikuonesha hali ya kujua chochote kwa

    kuwa bella hakugundua kuwa mimi nilkuwa nawaona"

    kila mmoja akawa amenikazia macho akinitazama kwa

    kutokuamini kile ambacho alikuwa akikisikia. Majura

    akanyamazishwa na kkohozi cha mwalimu mkuu

    aliyemtaka asimame kisha akamruhusu kuondoka. Mimi

    nilibaki nimeshika kichwa nikajuwa kila kitu kimeharibika.

    Mwalimu mkuu akaanza kuzungumza

    "sasa kutokana na join instruction yetu haituruhusu kuwa

    na mtu mwenye vitendo vya kichawi hivyo tumevumilia

    mambo mengi sana ambayo tumekuwa tukiyasikia kutoka

    kwa watu waliokushuhudia kabisa na sio kukuonea.

    Mfano mwalimu Bushiri kukuona ukienda maeneo ya

    makaburini ukiwa na mwanafunzi mwenzio Schola

    mkiingia ndani ya mbuyu pamoja na kumtokea mama

    yake na schola usiku wa manane ukimtisha kumuua

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    endapo akiendelea kumuombea mtoto wake ulinzi sasa

    basi tunakufuta shule kuanzia leo hatukuitaji tena"

    machozi yalinitoka ghafla na kitu cha uchungu kikapiga

    ndani ya moyo wangu hakika nililia kwa uchungu sana. Ni

    kweli niliadhibiwa kwa jambo la kweli lakini iliniuma

    kuachishwa shule. Ningeenda wapi? Ningekuwa mgeni wa

    nani mimi? Sina baba wala mama? Sina pa kwenda.

    Mama schola asingeniruhusu hata chembe hata

    ningemlamba miguu yake kwa ulimi wangu. Nimeumbuka

    mimi nitaenda wapi mimi? Mwalimu mkuu akanigukuza

    ofisini hapo na kuniambia nirudi bwenini kujiandaa ili

    niweze kutoka eneo hilo la shule. Yaani sikuhitajika

    kabisa. Nililia bila mtu yeyote kunionea hutuma wala

    kunitazama nilitoka nikiwa nimeshikwa na aibu

    nikimtazama kila mmoja wao wakiwa wananitazama kwa

    hasira

    Nilitoka nikaelekea bwenini nikachukua kila kilichokuwa

    changu. Nilipokuwa napita kurudi ofisini kwa ajili ya

    kuchukua barua yangu ya kufukuzwa shule, kila

    mwanafunzi alinyanyuka kutokea madirisha ya darasani

    akawa anazomea. Jina kubwa waliloniita ni

    "mchawi huyoo.. Mchawi huyo..."

    iliniuma sana. Lakini sikuwa na jinsi nilizidi kulia.

    Nilikutana na Jordan nilimsimamisha ili nizungumze naye

    alinikimbia kama kinyaa. Niliumia sana. Niliumia Jordan

    kunikwepa na kuiona mimi ni mbaya kwake. Sawa mimi

    nilikuwa mchawi mbona hakuwa akijua siku zote hizo

    ubaya wangu hakuwahi kuuona lakini nilikuwa mzuri na

    aliniambia mimi ni msichana mzuri kuliko wote duniani,

    kwanini leo anione mimi ni mbaya? Jamani Jordan

    wangu? Ina maana hanitak tena? Mapenzi yangu na yake

    ndiyo yamekufa? Vipi ningemuangamiza yule christina

    aliyezini naye chooni na mimi nikiwashuhudia bila wao

    kuniona? Ni mara ngapi jordan alikuwa akisaliti penzi

    langu lakini mimi nilizidi kumpenda? Ina maana upendo

    wangu wote bella mimi umekuwa bure? Nilikuwa

    nikijiuliza hayo nikimtazama Jordan aliyekuwa akitembea

    haraka haraka kuelekea darasani. Mimi machozi

    yalinitoka kila nikimuangalia. Leo nimebaki peke yangu.

    Peke yangu bila mama na baba. Kila mtu alinipiga teke

    nilipokuwa nikimuomba msaada. Uchawi wangu

    ukaniponza. Lakinisipo tayari kuuacha. Nikaanza

    kutembea kuelekea ofisini kwa mkuu wa shule. Nilimkuta

    mama yake na schola. Alikuwa akilia sana mbele za mkuu

    wa shule

    "mtoto wangu mimi sijuhi hata wamemfanyaje jamani..

    Upole wangu na huruma ndiyo imeniponza"

    nilimsikia yote aliyokuwa akizungumza nikajisikia vibaya

    sana. Alinyamaza aliponiona mimi akawa anafuta

    machozi yake na kuvuta kamasi jepesi lililokuwa linamtoka

    kila wakati

    "shika hii barua kaa ukifahamu kuwa usije kufikiria

    utaenda shule yeyote ukapata shule iliyokuvumilia zaidi ya

    hii. Nakuombea maisha mema huko uendako na cha

    msingi uache hizo tabia za kichawi."

    alinipatia barua yangu. Nikaipokea kisha nilitoka humo

    ofisini. Mama schola alikuwa akinisindikiza kwa macho

    yaliyojaa machozi. Mimi nilitoka mpaka getini kwa

    Majura. Majura sikumkuta. Niliondoka zangu popote pale

    ambapo pangenipokea. Sikujua wapi naelekea wala vipi

    ningeishi. Nikahisi babu amenidhulumu. Ameidhulumu

    sana nafsi yangu. Mateso haya ninayoyapata ni yeye

    anayasababisha. Kwanini anaruhusu watu kufahamu vitu

    vyangu? Yeye si ana nguvu? Kwanini hakujitokeza katikati

    ya kikao kile na kunitetea mimi kwa kuwapumbaza wote?

    Jamani dunia imenielemea. Nitaenda wapi sasa? Nilikaa

    kwa muda mrefu kituoni mpaka nilipopata akili ya kwenda

    kwa majid kule mwananyamala kisiwani. Nikachukuwa

    gari mpaka magomeni mikumi kisha nikaunganisha

    mpaka mwananyamala kisiwani. Nilivipita vile vichochoro

    tulivyopita mara ya kwanza nikiwa na schola kisha

    nikaibukia katika kichochoro cha mwisho kilichounganisha

    njia ielekeayo kwa majid nilipakumbuka vizuri. Lakini

    kilichonishangaza nilipofika katika ule uwanja ambao

    ulitakiwa niuvuke nifike kwa majid nilikuta makaburi

    matupu. Na nilipotazama mbele zaidi nilipozani labda

    ningeiona nyumba ya majid nikaambulia kuuona mbuyu

    mmoja mkubwa. Nikahisi labda nimepotea au nimeanza

    kuwehuka mama mmoja alipopita eneo hilo nikamuuliza

    "samahani kwa usumbufu mama ati aya makaburi

    yamejengwa lini hapa"

    alinicheka sana yule mama alinicheka mpaka nikaona

    machozi yakimtoka akaniambia.\

    "dada yangu hii ni sehemu ya makaburi miaka yote

    napafahamu hapa ni makaburini mimi nimezaliwa

    nimeyakuta na hata mengine yameanza kupotea lakini hili

    ni eneo la makaburi"

    nikaanza kuchukia kutokana na junicheka huko lakini

    haikunizuia kumuuliza

    "sawa lakini kwanini unacheka?"

    alinyamaza kisha akanijibu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "si wewe tu hii sehemu inaonesha ina mauza uza ya peke

    yake kwa sababu wengi huja hapa na kubaki

    wakishangaa. Wanashangaa na kutuuliza sisi wenyeji "hivi

    hapa haya makaburi yamekuja lini?" sasa ndio hapo pa

    kujiuliza makaburi yanabebwa na kuletwa sehemu moja

    na nyingine?"

    aliendelea kucheka huku akijipiga piga mapajani baada ya

    kupiga magoti chini. Nikamuuliza swali lingine

    "unamfahamu Majid?"

    nilimuona kushituka sana. Alishitua haswa na kuyatoa

    macho kwa mshangao. Aliniuliza kwa kubwatuka huku

    akiwa amesimama wima



    "unamfahamu Majid?"

    nilimuona kushituka sana. Alishitua haswa na kuyatoa

    macho kwa mshangao. Aliniuliza kwa kubwatuka huku

    akiwa amesimama wima

    "shekhe majid?"

    niliitikia kwa kumtingishia kichwa kuonesha ndiye

    niliyemmanisha. Kitu cha kushangaza alianza kulia. Alilia

    haswa tena alilia kupitiliza kama mtoto mdogo kamasi

    jepesi likamtoka na nilipombembeleza kwa muda mrefu

    alinieleza

    "huyo si binadamu dada yangu"

    mimi nikajitia kushituka nikauliza kwa mshangao

    "si binadamu!? Umejuaje?"

    kutokana na kilio ilinipa shida kumuelewa kiufasaha

    alichokuwa akizungumza. Ilimbidi nimkatishe kwanza

    alichokuwa akiongea ndipo nilimuomba arudie alichokuwa

    akiongea nimuelewe zaidi. Aliniambia

    "huyo ni jini aliyekuwa akimlinda mjomba wangu. Ni jini

    aliyetengenezwa kwa moto ni mweye nguvu sana.

    Alisababisha matatizo makubwa sana nyumbani. Ni jina

    aliyenunuliwa mascut lakini mjomba alipovunja masharti

    alimnyonya damu mjomba pamoja na kumuweka ukilema

    wa maisha bonamu yangu alitoroka katika chmba

    alichomowekwa na kuanza kuzagaa mitaani"

    alizidi kulia akalia sana. Mimi nilimpooza baada ya

    kunyamaza tena aliniuliza

    "wewe umemfahamu vipi Majid?"

    na mimi nikamueleza kila lililonikuta. Nilimueleza kuanzia

    mwanzo wa kuingia Gamboshi mpaka nilipofukuzwa

    shule. Ni siku hiyo ndiyo niliamua nije kumtafuta majid ili

    niweze kupata nguvu ya utajiri na mvuto wa biashara.

    Niliona jambo la kufanya na la kunipatia pesa kwa haraka

    ni kutumia nguvu hizo za kichawi kupata pesa. Sikujua ni

    biashara gani nitafanya ila sikuumiza sana kichwa

    kuchagua aina ya biashara. Hiyo ni kutokana na elimu

    yangu ndogo kunituma nifikirie kuwa hata mfanyakazi wa

    ndani lakini kwa kutumia nguvu za kichawi niwe na mvuto

    wa kupata mshahara mkubwa. Ndipo hapo yule msichana

    aliyejitambulisha kwa jina la zamda akaniuliza

    "una sehemu ya kukaa sasa?"

    nilipata shida kumjibu moja kwa moja lakini ilibidi nimjibu

    ili nisikose sehemu kama alikuwa na nia ya kunisaidia.

    "sina sehemu yeyote ya kukaa zamda naomba unisaidie

    dada yangu"

    alinikaribisha nyumbani kwake. Chumba kimoja kisicho na

    kitanda bali godoro kubwa la sita kwa sita likiwa

    limetandazwa chini kuonesha kuwa hiyo ndiyo ilikuwa

    sehemu yake ya kulaza mbavu zake. Nilipokuwa

    nikishangaa chumba hicho ni hapo aliponieleza kuwa

    "hatupo peke yetu sehemu hii kuna wenzangu wawili

    ambao wameelekea kazini mimi natokaga saa nne"

    nilijiuliza kazi gani ya jioni? Kazi ya usiku asubuhi

    mahesabu ndiyo hii? Nikahisi nilikuwa nikizungumza na

    dada poa dada anayeuza mwili wake kujipatia kipato.

    Nikaanza kuingiwa na uoga nikatetemeka. Zamda

    aliniambia

    "usiogope utakaa hapa kwa muda na utazoea tu ata

    wewe mwenyewe utatamani kazi yetu. Inalipa sana"

    alinieleza uzuri wa kazi yao.

    "yaani kwa siku unalala na wanaume hata kumi kila

    mmoja anaklipa buku kumi na kondomu wale wanaopenda

    kavu kavu unawachomoa hata 50"

    macho yakanitoka pima nisiamini kile ninachokisikia.

    Ilikuwa ni sauti ya zamda iliyokuwa ikitoka bila mzaa na

    uso wake ukiwa umepambwa kwa tabasamu pana.

    Aliyakatisha maongezi na kulirudia jiko lake na kuanza

    kupika. Lilikuwa ni pishi la wali wa nazi na samaki.

    "dada yangu hii ni sehemu ya makaburi miaka yote

    napafahamu hapa ni makaburini mimi nimezaliwa

    nimeyakuta na hata mengine yameanza kupotea lakini hili

    ni eneo la makaburi"

    nikaanza kuchukia kutokana na junicheka huko lakini

    haikunizuia kumuuliza

    "sawa lakini kwanini unacheka?"

    alinyamaza kisha akanijibu

    "si wewe tu hii sehemu inaonesha ina mauza uza ya peke

    yake kwa sababu wengi huja hapa na kubaki

    wakishangaa. Wanashangaa na kutuuliza sisi wenyeji "hivi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hapa haya makaburi yamekuja lini?" sasa ndio hapo pa

    kujiuliza makaburi yanabebwa na kuletwa sehemu moja

    na nyingine?"

    aliendelea kucheka huku akijipiga piga mapajani baada ya

    kupiga magoti chini. Nikamuuliza swali lingine

    "unamfahamu Majid?"

    nilimuona kushituka sana. Alishitua haswa na kuyatoa

    macho kwa mshangao. Aliniuliza kwa kubwatuka huku

    akiwa amesimama wima

    "shekhe majid?"

    niliitikia kwa kumtingishia kichwa kuonesha ndiye

    niliyemmanisha. Kitu cha kushangaza alianza kulia. Alilia

    haswa tena alilia kupitiliza kama mtoto mdogo kamasi

    jepesi likamtoka na nilipombembeleza kwa muda mrefu

    alinieleza

    "huyo si binadamu dada yangu"

    mimi nikajitia kushituka nikauliza kwa mshangao

    "si binadamu!? Umejuaje?"

    kutokana na kilio ilinipa shida kumuelewa kiufasaha

    alichokuwa akizungumza. Ilimbidi nimkatishe kwanza



    alichokuwa akiongea ndipo nilimuomba arudie alichokuwa

    akiongea nimuelewe zaidi. Aliniambia

    "huyo ni jini aliyekuwa akimlinda mjomba wangu. Ni jini

    aliyetengenezwa kwa moto ni mweye nguvu sana.

    Alisababisha matatizo makubwa sana nyumbani. Ni jina

    aliyenunuliwa mascut lakini mjomba alipovunja masharti

    alimnyonya damu mjomba pamoja na kumuweka ukilema

    wa maisha bonamu yangu alitoroka katika chmba

    alichomowekwa na kuanza kuzagaa mitaani"

    alizidi kulia akalia sana. Mimi nilimpooza baada ya

    kunyamaza tena aliniuliza

    "wewe umemfahamu vipi Majid?"

    na mimi nikamueleza kila lililonikuta. Nilimueleza kuanzia

    mwanzo wa kuingia Gamboshi mpaka nilipofukuzwa

    shule. Ni siku hiyo ndiyo niliamua nije kumtafuta Majid ili

    niweze kupata nguvu ya utajiri na mvuto wa biashara.

    Niliona jambo la kufanya na la kunipatia pesa kwa haraka

    ni kutumia nguvu hizo za kichawi kupata pesa. Sikujua ni

    biashara gani nitafanya ila sikuumiza sana kichwa

    kuchagua aina ya biashara. Hiyo ni kutokana na elimu

    yangu ndogo kunituma nifikirie kuwa hata mfanyakazi wa

    ndani lakini kwa kutumia nguvu za kichawi niwe na mvuto

    wa kupata mshahara mkubwa. Ndipo hapo yule msichana

    aliyejitambulisha kwa jina la Zamda akaniuliza

    "una sehemu ya kukaa sasa?"

    nilipata shida kumjibu moja kwa moja, lakini ilibidi nimjibu

    ili nisikose sehemu kama alikuwa na nia ya kunisaidia.

    "sina sehemu yeyote ya kukaa Zamda naomba unisaidie

    dada yangu"

    Alinikaribisha nyumbani kwake. Chumba kimoja kisicho na

    kitanda. Lilikuwepo godoro kubwa la sita kwa sita likiwa

    limetandazwa chini kuonesha kuwa hiyo ndiyo ilikuwa

    sehemu ya kulaza mbavu zake. Nilipokuwa nikishangaa

    chumba hicho, ni hapo aliponieleza kuwa

    "hatupo peke yetu sehemu hii kuna wenzangu wawili

    ambao wameelekea kazini mimi natokaga saa nne"

    Nilijiuliza kazi gani ya jioni? Kazi ya usiku, asubuhi

    mahesabu; ndiyo hii? Nikahisi nilikuwa nikizungumza na

    dada poa. Dada anayeuza mwili wake kujipatia kipato.

    Nikaanza kuingiwa na uoga, nikatetemeka. Zamda

    aliniambia

    "usiogope utakaa hapa kwa muda na utazoea tu hata

    wewe mwenyewe utatamani kazi yetu. Inalipa sana"

    alinieleza uzuri wa kazi yao.

    "yaani kwa siku unalala na wanaume hata kumi kila

    mmoja anakulipa buku kumi na kondomu wale

    wanaopenda kavu kavu unawachomoa hata 50"

    macho yakanitoka pima nisiamini kile ninachokisikia.

    Ilikuwa ni sauti ya Zamda iliyokuwa ikitoka bila mzaa na

    uso wake ukiwa umepambwa kwa tabasamu pana.

    Aliyakatisha maongezi na kulirudia jiko lake na kuanza

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/---

    kupika. Lilikuwa ni pishi la wali wa nazi na samaki.

    Mimi sikuona cha kumsaidia, hivyo niliendelea kutalii

    ndani ya hiko chumba kwa macho. Dakika chache

    baadaye nikiwa bado nimezubaa, waliingia wasichana

    wawili. Hawakuwa bado wamefikia umri wa kuitwa

    wanawake kwa kuwa hawakufika huko. Walikuwa

    wamevaa vivazi vilivyoacha maungo yao wazi kwa

    asilimia kubwa. Niliwatazama kwa aibu kidogo sikutarajia

    kama kuna binadamu mwenye uwezo wa kutembea

    barabarani namna ile. Wale wasichana walishituka sana

    kuniona. Wote walikuwa weupe lakini mmoja alionekana

    kuwa mweupe zaidi kutokana na kujikoboa. Niliwasalimu

    nao walinisalimu huku wakiwa wamezubaa kwa

    kunishangaa. Mmoja alikuwa anavuta sigara mwingine

    akiwa na chupa ya wine. Zamda aliwauliza

    "hoya mbona mmerudi mapema leo? Tusizinguane mjue"

    Wale mabinti walicheka kilevi levi huku wakiwa

    wameshajitupa kitandani. Mmoja wao ndiye aliipata sauti

    yake

    "leo tumepata lizungu hilo, lina mihela kibao. kila mmoja

    kamganjia laki mbili mbili"

    wakawa wanachomoa noti za elfu kumi kumi. Nyuso zao

    zikiwa zimepambwa na tabasamu pana sana. Zamda naye

    alionekana kuchanganyikiwa kupita kiasi. Aliwarukia

    wenzake na kuanza kushangilia kwa pamoja. Mimi

    sikuelewa kilichoendelea hivyo nikatulizana katika kochi,

    nikiwatazama tuli.

    Baada ya muda kidogo chakula kikapakuliwa tukala.

    Wakati huo wa chakula mabinti wale waliolewa chakari,

    ndipo walipaza sauti zao

    "we zamda"

    zamda alimgeukia yule aliyezungumza

    "hivi mbona haututambulishi huyu ni nani?"

    zamda alinigeukia mimi na kutabasamu, kisha kicheko

    kidogo kikampitia. Alisema

    "huyu ni mdogo wangu tutakuwa naye hapa geto"

    alinigeukia mimi na kuniambia

    "Bella hawa ndiyo wafanyakazi wenzangu na ndio

    tutakuwa nao hapa siku zote hii ni hali ya kawaida tu

    isikushangaze"

    mimi nilisikitika tu, huku kicheko kisicho na ladha ya

    kicheko kikinipitia. Wakati ambao mimi naenda kulala

    zamda alitoka akiwa amevaa baibui na kujifunika kama

    ninja. Lakini nilishangazwa na alichovaa ndani. Kilikuwa

    ni kituko na kitu cha kushangaza. Alivaa kipensi cha jeanz

    na kitopu kilichoziba matiti yake tu. Aliondoka na wale

    mabinti alionitambulisha kwao kuwa ni Caro na Prisca.

    Pombe zilikuwa zimewaisha kidogo, hiyo ilikuwa yapata

    saa 7 usiku. Nililala zangu lakini kwa uoga kidogo.

    Nilikuwa muoga kutokana na ugeni nilionao katika hicho

    chumba. Akili yangu ilianza kutafakari kuhusu kulala

    nyumba moja na wasichana waliokuwa wakiuza miili yao.

    Hiyo ilinitisha sana. Nikajisikia vibaya na kuapa kuwa

    sitoingia katika kazi hiyo hata kama nina shida kiasi gani.

    Nikiwa katika kuwaza huko, sikujua usingizi ulinipitia saa

    ngapi. Nilishitushwa na mlango uliogongwa kwa ghadhabu

    na sauti ya kilevi zile za Caro na Prisca ndio zilipiga

    kelele sana. Yeye Zamda aliniita jina langu kabisa

    "bella fungua bwana"

    nilijinyanyua kivivu na kwenda kuwafungulia, huku

    nikipikicha macho yangu nikiwa nimenuna. Nilipotupia

    jicho saa iliyopachikwa ukutani, katika chumba hicho;

    ilikuwa imetimu saa 12 asubuhi. Wote walikuwa

    wamelewa chakari. Zamda alikuwa anapepesuka sana.

    Caro hakujiweza kabisa, Prisca ndiye akaropoka uozo

    ulioniudhi

    "halafu Zamda sisi hatulei watoto yatima humu ndani.

    Sisi tukauze miili yetu, yeye alale asubiri kupakua tu.

    Hapa kama vipi mimi nahamia geto la kina Sandra, sitaki

    unafki mimi mtoto mzuri kabisa huyu"

    alinishika matiti yangu akiyabinya binya. Nilimputa mkono

    wake na kutoka nje. Nilikuwa nikilia. Sikutaka kuwa

    changudoa sikutaka niuze mwili wangu. Hivyo nikiwa nje

    zamda alinifuata. Alinishika bega langu kwa upole na

    kunipa moyo

    "Bella mdogo wangu sisi haya ndiyo maisha yetu hapa

    geto. Mimi mwenyewe nilipotoka kijijini nililelewa na

    mama mmoja huko kinondoni, yeye ndiye aliyeniingiza

    katika hii biashara. Nilikuwa nikifanya kazi za ndani

    kwake kumbe yule mama alikuwa anauza mabinti.

    Sikupenda kama wewe, lakini hivi sasa nimezoea. Na

    wewe utazoea tu mdogo wangu"

    nilimuangalia kama nilikuwa nikitazama kinyesi kilichotoa

    harufu iliyokera. Nilimjibu kwa hasira

    "siwezi.. Siwezi kuwa changudoa zamda"

    alinicheka kwa sauti ya kilevi. Kisha alinyanyuka kwa

    kutumia muhimili wa bega langu kujinyanyua. Akaniambia,

    huku akipepesuka pepesuka.

    "sina lingine la kuzungumza, umetaka sawa hujataka

    sawa. Lakini kama hauhitaji, unaweza kuchukuwa njia

    zako"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alimaanisha. yaani alichoongea kilikuwa ni kile ambacho

    kilimtoka ndani ya moyo wake. Nilijishika kichwa nikiwaza

    sana. Sikujuwa nitaishi vipi baada ya kutoka hapa kwa

    zamda. Nililaani kila maisha niliyoyapitia baada ya mama

    kufariki. Niliyachukia maisha ya Gamboshi. Nikamchukia

    babu kunipeleka huko. Yeye ndiye alinisababisha mimi

    kuwa mnyama na ubinadamu unikae pembeni. Niliikosa

    shule, na nikawapoteza wale waliojitolea kunisaidia

    kuyasongesha maisha yangu kwenda sehemu fulani.

    Machozi yakanitoka. Yakaniponyoka kwa uchungu nikiwa

    hapo nje. Niliingia ndani baada ya kuutokomeza muda wa

    zaidi ya dakika thelathini hapo nje. Nilipoingia ndani,

    niliwakuta wote wakikoroma kwa pamoja. Walilala ovyo

    hakika walikua wamechoka.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog