Search This Blog

NILIONGEA NA SHETANI ILI NIWE TAJIRI - 5

 





    Simulizi : Niliongea Na Shetani Ili Niwe Tajiri

    Sehemu Ya Tano (5)



    Niliingia ndani baada ya kuutokomeza muda wa

    zaidi ya dakika thelathini hapo nje. Nilipoingia ndani,

    niliwakuta wote wakikoroma kwa pamoja. Walilala ovyo

    hakika walikuwa wamechoka.

    Mimi nilijiandaa kufanya usafi

    japo nilikuwa mgeni, nilitaka niwaridhishe wasije

    kuendelea kunighasi niingie katika kazi hiyo ya kuuza

    mwili wangu. Nilifanya kazi kwa bidii nilifua nguo zao zote

    na kuosha vyombo na kufagia uwanja. Nilichukuwa muda

    mrefu pia kuchota maji kutoka umbali mrefu. Nilipomaliza

    niliwakuta tayari Caro Prisca na zamda wamekwishaamka

    na wamekaa kibarazani wakicheza karata. Zamda

    aliponiona aliniambia

    "mdogo wangu unaonyesha wewe ni mchapakazi sana?"

    sikumjibu lolote nilinyamaza kimya kisha nikaingia ndani.

    Nilipotoka tena ndani nikitaka kujumuika nao, prisca

    akaropoka

    "acha upuuzi wewe unakaa umeshapika?"

    nilijinyanyua bila hiyana nikaenda kuandaa chakula. Kwa

    kuwa sikuwa na hela niliwaomba hela ya kwenda gengeni

    kununua viungo vya mboga.

    "nani akupe hela? Wote si wanawake humu ndani? Kuna

    bwanako humu? Nenda kanunue hivyo viungo kwa hela

    yako hatuuzi mwili kulisha watoto yatima sisi"

    maneno ya caro yalinichoma sana, ila sikuwa na jinsi

    nilienda kuchukua senti iliyobaki kwenye akiba yangu na

    kununua viungo na vipaja vya kuku vilivyouzwa kwa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mafungu. Siku hiyo tulikula tukashiba. Hakuna ambaye

    alithubutu kunikaripia wala kunigombeza usiku ulipotimu

    kila mmoja alishika njia yake kwa wakati wake wakiniacha

    mimi nimelala. Asubuhi ikawa vile vile wamerudi wakiwa

    wamelewa na kama kawaida ya prisca alirudi na maneno

    yake ya maudhi. Ikawa vile kwa muda wiki nzima mimi

    ndiye nilitoa pesa yangu iliyobaki kutoka shule

    nilipofukuzwa na kuwalisha wao, hiyo iliokana na kuogopa

    kushinda njaa ama kufukuzwa kwa sababu ya kukataa

    kujiuza yaani kufanya biashara ya uchangudoa. Ni katika

    siku hizo pia nilijitahidi kutafuta kazi mbali mbali sehemu

    mbalimbali lakini ni nani angenipokea ikiwa sikuwa hata

    na cheti cha form four? Ni nani alikuwa anahitaji mtu

    ambaye alikuwa hajui hata chuo ina rangi gani? Ni hapo

    ndipo nilipokata tamaa ya maisha na kuona nimepewa

    adhabu kubwa sana nisiyoweza kuistahimili. Nilimlilia

    sana mama yangu usiku na mchana na kumuuliza mungu

    kwa nini amemchukua wakati nikiwa bado namuhitaji

    mama. Wakati ambao alikuwa na umuhimu mkubwa

    katika maisha yangu. Mtu pekee aliyekuwa na uchungu na

    mimi. Mtu pekee niliyefahamu kuwa alikuwa ananipenda

    na kunihangaikia ili niwe na maisha mazuri. Ni hapo chozi

    likanitoka nikiwa nje ya chumba cha zamda nikiwaza

    mengi. Ni siku hiyo ndiyo nilimuahidi zamda kuwa

    nitaianza kazi hiyo. Kazi ya kuuza mwili wangu. Zamda

    alifurahi sana. Alifurahi huku akiniambia kuwa

    "utapata wanaume wengi sana mdogo wangu hadi

    naogopa utanipora mzungu wangu"

    alisema huku akicheka, mimi moyoni nikilia. Nikalitoa

    tabasamu la hudhuni nikiwa nalia ndani kwa ndani.

    Nilirudi ndani nikamkuta Zamda ndiyo anajiandaa.

    Alishangaa kunikuta bado nipo ndani ya midabwada

    yangu isiyotamanisha kuitazama

    "we bella ha!"

    alikuwa amesimamisha zoezi la kuivaa ile pensi iliyokuwa

    imembana haswa. Kisha alikuwa ananishangaa mimi

    niliyekuwa namshangaa yeye.

    "mbona bado umevaa hiyo matambara yako? Si nimekupa

    nguo wewe uvae?"

    nguo alizonipa zilikuwa bado kitandani nimeziweka.

    Nilipoziangalia, nilishindwa kulizuia chozi lililoniponyoka.

    "unalia nini sasa?"

    nikamjibu "zamda sijajua itakuwaje siku ya kwanza katika

    hii biashara mimi si mwenyeji zamda naumia moyo

    wangu unaniuma"

    alinicheka kwa dharau kisha aliniuliza

    "hivi kuna mtu ni mwenyeji katika kila jambo? Acha

    upumbavu au unapenda unavyotukanwa tukanwa na

    prisca? Unajua ni kiasi gani wanaudhika kukuona

    ukiwategemea humu ndani? Nimeshachoka kukutetea mtu

    hubebeki"

    alikuwa anaivaa nguo yake kwa ghadhabu. Na mimi

    ikanilazimu nivae nguo hiyo kwa juu nikajitupia khanga

    zangu. Moja nilijifunga kwa chini ya pili nikajitupia kifuani.

    Niliumia sana. Nilianza kujiona ni msichana mchafu

    asiyefaa katika jamii. Lakini kutokana na shida

    inayonikabili, ilinipasa kufanya hivyo. Niliingia barabarani

    kule maeneo ya ubalozi wa ufaransa ndiyo ilikuwa windo

    letu. Tulipoona kulipooza mimi na zamda tulihama kijiwe

    tukaelekea maeneo ya jolly club huko tulikuwa tumekaa

    barabarani tukisimamisha kila gari la kifahari lililokuwa

    likitupita. Mimi sikuwa mzoefu na wala moyo

    haukunisukuma kufanya hayo. Nilikaa chini huku baridi la

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    usiku likinipiga. Nilikuwa nalia sana, nililia kupita kiasi.

    Nasukuru mungu siku hii hakukuwa na wateja kabisa

    hivyo mimi sikupata mtu wala zamda hakupata mtu.

    Zamda alinieleza kuwa siku ya jumanne mara nyingi huwa

    mbaya katika vijiwe vyote anavyoibukaga. Mimi kwangu

    ikawa afadhali sikuona kama hiyo ilikuwa ni mbaya au

    nuksi kwangu. Siku ikapita vizuri. Kutokana na tabia

    yangu ya kukataa wateja waliokuwa wananihitaji, Zamda

    alikerwa nayo. Yeye akaniambia wazi.

    "sikia bella, mimi siwezi nikawa nakuhudumia bure

    unakula na kulala bure. Naomba uchukuwe ustaarabu

    wako"

    alikuwa hana mzaha kwa kile ambacho alikizungumza.

    Mimi nilianza kuogopa. Nilfikiria ni wapi nitaenda endapo

    kama zamda pia naye amenichoka? Niliamua kukubali.

    Nikamuahidi zamda

    "nitafanya na nitaleta pesa nyumbani Zamda naomba

    unisamehe"

    alitabasamu baada ya kuridhishwa na jibu langu. Kisha

    tukaingia kazini.niliingia kazini kwa mara ya kwanza

    nikalala na wanaumewawili. Moyo wangu uliniuma sana

    siku hii lakini sikuwa na jinsi. Nikawa changudoa mpya.

    Wanaume wale waligundua mimi si mzoefu kutokana na

    ugeni wangu katika mambo ya kitandani. Hata katika

    kuwavalisha zana sikufanya kama wengine waliozoea.

    Waliponiingilia nilikuwa nalia machozi yakinishuka. Sikulia

    kwa sababu nilisikia raha au nilifurahia tendo hilo ila nililia

    kwa uchungu. Uchungu wa kuwa changudoa bila kupenda.

    Nilirudi nyumbani na noti mbili za shilingi elfu kumi ikawa

    sawa kwao wakatabasamu na prisca ndiye aliniambia

    "utazoea tu dogo usilie kama una mama vile"

    caro akampokea

    "ndiyo hivyo bella cha msingi jitahidi tu utundu usije

    ukakimbiwa bila kuachiwa chochote maana wateja wetu

    wengine ni wehu"

    kisha siku hii pia nilijaribu pombe. Sikuijaribu tu niijue ina

    ladha gani kwa kuwa nilifahamu ilikuwa ni chungu kama

    silki. Lakini nilijaribu nikidhani ni njia sahihi ya kukata

    mawazo niliyo nayo. Jinamizi la mawazo lililonikaba na

    hatia ya mimi kutembea na wanaume nisiowafahamu hata

    kwa majini. Hakika nilijihisi fedheha. Aibu na

    kudharirishwa sana ila glass ya kwanza ya pombe ile aina

    ya value brandy niliyoichanganya pamoja na maji ya uhai

    ilitosha kuuteka ufahamu wangu. Nilianza kuwa

    mchangamfu na muongeaji sana. Wote kwa pamoja

    tukawa tupo bwi mimi na wenzangu. Tulirudi nyumbani

    tukiwa tunapepesuka. Tulikokotana mpaka eneo la

    barabara baada ya kuiacha bar ya Q bar maeneo ya

    masaki tulimoenda kupata kilaji. Tukakutana na bajaji

    kadhaa pale katika kituo cha macho. Ikatupeleka mpaka

    katika geto letu la mwananyamala. Sikukumbuka ni nani

    alikuwa na akili kidogo kati yetu aliyemlpa yule dereva wa

    bajaji pesa yake na kutufungulia sisi kuingia chumbani.

    Ninachokumbuka ni mimi nilijikuta nikiwa juu ya godoro

    asubuhi iliyoanza kupitisha jua lake kali chumbani humo

    huku nikimtusi Caro kwa kunipandishia miguu nadomo

    lake lililotoa harufu kali ya pombe na kukoroma kwa hali

    ya juu katika sikio langu. Nilimsukumuzia upande wapil

    akakutana na uso wa zamda wakakumbatiana baada ya

    zamda kujizaba kibao kumpiga mbu aliyekuwa

    amemng'ata na hapo ndipo nilimtazama Caro kwa hali ya

    uvivu nilishitushwa kumkuta yeye alilikataa godoro na

    kwenda kulala chini kabisa akiibusu sakafu. Nilijinyanyua

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    taratibu lakini kichwa kikakataa. Kilikuwa kikiniuma kupita

    kiasi. Nikaijutia pombe niliyoinywa kwa furaha jana usiku.

    Niliamka nikaenda kupigwa mswaki na kuuweka mwili

    sawa na kuanza kuandaa chai ya chapati za maji yaani

    na mayai pia. Hapo mmoja baada ya mwingine wakawa

    wanaamka wakiwa na uchovu mwingi. Zamda ndiye

    alikuwa wa kwanza kunyanyua chapati moja kuitia

    mdomoni

    "mnhh mwanamke wewe ni mjuzi haswa wa jiko"

    akaimeza moja ya ile chapati niliyoitia iliki inukie

    akaendelea kunipa sifa zangu

    "yaani ningekuwa na kaka ningekupa hata usipate hizi

    shida zote. Mtoto tashtiti wewe"

    nilimuangalia kisha nikaangua kicheko jinsi

    alivyonitingishia sehemu zake za nyuma. Hakika zamda

    alikuwa amebarukiwa mzigo mkubwa sana sehemu zake

    za huku nyuma na juu ya kiuno alikatika ki kike. Unywele

    uliomdondoka mpaka mgongoni nikajiuliza kimoyo moyo

    "mungu jakunyima nini wewe dada mpaka ujiuze mwili

    wako ulivyo wa thamanu hivyo?"

    nikajisonyea taratibu nikimuangalia alipokuwa akijitingisha

    huku akiingia ndani. Mimi niliugeuza geuza mkaa na

    kuendelea kumwaga unga wa ngano uliojaa mayai na maji

    kidogo na iliki nyingi kikaangoni.

    Pishi lilipokuwa tayari nikalitupa juu ya sahani nikaliweka

    kati gombania goli ya mikono ikawa imeanza. Kila mtu

    alikuwa akiguna alipokuwa akishushia na maziwa ambayo

    sikuacha kuweka kila kiungo. Kama mdalasini, tangawizi

    na iriki. Hakika chai ikawa imekolea. Furaha ikawa kubwa

    ndani ya geto hili la machangudoa wenzangu. Ila kipindi

    hiki chote hakuna ambaye alifahamu upande wangu wa

    pili. Upande ambao ulinifanya kuikosa shule na kumkosa

    mwanaume wa maisha yangu, Jordan. Kila nilipokuwa

    nikimkumbuka yeye machozi yaliniponyoka. Hakika nilihisi

    huzuni sana kumkosa Jordan. Si Caro wala Prisca

    ambaye hakunipenda tena ndani ya ile nyumba. Siku za

    usoni nikawa mzoefu na mtundu kazini. Kutokana na pesa

    nilizokuwa nazipata, nikaongeza nakshi katika vifaa

    vyangu vya kazi. Nikwa na maana kuwa kiuno changu

    nikakipamba na mkufu wa dhahabu. Nikaingia unyagoni

    nikafunzwa jinsi ya kumkatikia mwanaume. Zamda

    alinieleza

    "bibi wewe mwibie kihisia akuongeze mkwanja"

    alikuwa akisema hayo huku akikatika. Nakiri kusema

    zamda alifuzu chuo cha mapenzi. Sikupata picha

    wanaume ambao anakutana nao yeye katika shughuli zetu

    za uchangudoa. Ila nilipomuuliza hakuwa tayari kunijibu.

    Mahudhurio mazuri kazini yakazidi kuleta manufaa zaidi

    katika kazi na maendeleo katika chumba chetu. Chumbani

    kwetu kukawa na vitu vingi vya kifahari. Ni hapo ndipo

    tukapatwa na wazo la kuhama katika chumba kimoja na

    kutafuta vyumba viwili yaani sebule na chumba.

    Tulipokipata, tukanunua sofa set, runinga ya kupachika

    ukutani, friji na zuria la manyoya ikaipamba sebule yetu

    iliyoibeba meza kubwa ya duara. Chumba kikapuliziwa air

    fresh pakanukia vizuri na kubeba kitanda cha kifahari

    nilichopata kukiona kwenye tamthilia mbalimbali

    walizoigizia katika vyumba vya mahotel. Nilijihisi raha siku

    zote na kuifurahia kazi yangu. Siku nyingine nililazimika

    kuwawekea madawa wale ambao nilifahamu kuwa

    walikuwa na pesa za kutosha ili niwaibie wakiwa

    usingizini. Nilifanikiwa kwa kuwapagawisha kwa viuno

    vyangu. Uzuri ule niliokuwa naukataa zamani sasa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nikajitamani mwenyewe nilipojitazama kwenye kioo.

    Ikafika ile siku ambayo nilipatwa na mshituko mkubwa

    sana moyoni yaani ni mshituko wa ajabu. Mimi nilikuwa

    pale pale kwa siku zote ambapo huwa nakaa nikitege

    mingo zangu yaani wateja. Ndipo likatoke gari ya kifahari.

    Siwezi kukambuka ilikuwa ni gari ya aina gani kwa

    sababu mimi si mjuzi mzuri wa magari. Sikupata shida

    kulikimbilia kwa kuwa lilinifuata mpaka pale nilipo

    likiwaacha wenzangu watatu pale mwanzo. Lilipopiga

    breki mbele yangu kioo cha mbele kilifunguliwa na

    kukutana na kijana ambaye alikuwa anaonesha fedha

    kwake haikuwa tatizo. Alinipatia shilngi elfu hamsini bila

    kuongea naye chochote kisha aliniambia ingia ndani ya

    gari. Kwa kuwa nilihitaji pesa niliingia bila wasiwasi.

    Humo ndani ya gari nikakutana tena na watu watatu..

    Watu hao sikuweza kuwafahamu wala kuona nyuso zao

    kutokana na giza zito lililopo ndani ya ile gari. Gari hilo

    likaanza kutembea kwa mwendo wa kawaida huku wale

    vijana wa kule nyuma wakiwa wameniweka katikati yao

    wakianza kunichezea chezea kila sehemu yangu ya mwili.

    Kwa kuwa tayari walikwisha nilipa, mimi niliwaachia

    wafanye wanachotaka. Walinishika sana mpaka pale

    waliponihitaji tukiwa humo humo ndani ya gari nikahisi

    kuifahamu sauti ya mmoja wa watu hao. Yeye alikuwa

    akilazimisha sana kuanza yeye.

    "niacheni nianze bwana masela mimi ndiye nimetoa pesa

    nyingi"

    alikuwa akikoroma. Sauti hiyo ikawa inaniadhibu

    ikaniadhibu sana. Nikajiuliza wapi nimeiskia? Wale watu

    wakaanza kuniingilia mmoja baada ya mwingine wakiwa

    wamevaa zana zao. Walipomaliza wakanishusha pale pale

    waliponichukua na mmoja kati ya wale watu alishuka na

    mimi kwa nia ya kuongea. Alpokuwa akishuka mimi

    sikujuwa lengo lake. Ula nilifahamu kuna uwezekano labda

    huduma yangu ilimpagawisha. Tulipofika eneo lenye

    mwanga ni hapo nilipoanza kuukosa mhimili wa

    kusimama na kutaka kuzimia. Lakini nilijitahidia hilo

    lisitokee. Aliyekuwa amesimama mbele yangu hakuwa

    mwingine bali ni Jordan. Jordan mpenzi wangu alikuwa

    amesimama mbele yangu naye akiwa ameshitushwa sana

    Nilimuita huku midomo ikiwa inatetemeka

    "jordan"

    hata maneno nayo hayakusikika sawia. Naye aliniita kama

    alikuwa akijifunza kuzungumza.

    "bella? Ni wewe tulikuwa ndani ya lile gari"

    alikuwa kama amewehuka akaniuliza tena

    "unafanya nini hapa?"

    nilimjibu kwa ujasiri huku machozi yakinitoka

    "jordan mimi ni changudoa sasa"



    "Bella? Ni wewe tulikuwa ndani ya lile gari"

    alikuwa kama amewehuka akaniuliza tena

    "unafanya nini hapa?"

    nilimjibu kwa ujasiri huku machozi yakinitoka

    "jordan mimi ni changudoa sasa"

    Nilipouinua uso wangu jordan alikuwa akimalizia

    kuufunga mlango wa gari na lilipotiwa ufunguo gari

    likachomoka kwa mwendo wa kasi. Siku hii nilikosa raha

    sana sikuamini kama Jordan pia alikuwa akifanya upuuzi

    wa namna ile. Alikosa mwanamke wa kutembea naye

    hata aanze kutafuta machangudoa? Nikaishusha thamani

    nikamuona jordan alikuwa ni mwanaume mchamu

    aliyepitiliza. Amewamaliza wale wanafunzi wa pale

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    shuleni na sasa ameamua kuja na huko kwa

    machangudoa? Niliumia sana. Nikajilaumu kwa nini

    nililaghaika ni ile shilingi lakimoja waliyonipatia? Kwanini

    sikutaka kuwashwa kwa taa za ndani ya ile gari ili

    nisikubali kufanya mapenzi na jordan? Si kwamba

    sikuwahi kufanya mapenzi na jordan ila iliniuma yeye

    kufahamu pia nimejiingiza katika uchangudoa. Hapo moyo

    wangu ukaniambia kuwa jordan si wangu tena. Yaani

    mimi na jordani ni watu wawili tofauti wanaoishi katika

    maisha mawili tofauti hakika nisingeweza kuwa na jordan

    tena. Iliniuma nikalia machozi yakanikauka. Ukawa msiba

    ulionizika mwenyewe. Nikajipa moyo lakini bado uchungu

    ulining'ang'ania. Kumpoteza jordan kukawa ni sawa na

    kumpoteza mama yangu. Nakumbuka siku hii nililewa

    kupita kiasi.nilikunywa sana kupita kiasi. Nililewa hata

    sikujitambua. Niwale wasichana wa geto la kina sandra

    ndiyo waliompa taarifazamda kuwa sijitambui. Siku ya pili

    nilijikuta kitandani nikiwa nyaka nyaka lakini pochi yangu

    ilikuwa salama. Zamda alikuwa akinitazama jinsi

    nilivyokuwa najigeuza geuza pale kitandani nilipoamka

    akaniuliza

    "vipi mwenzangu? Wamekuweza jana?"

    kwa kuwa nilikuwa nina pombe nyingi kichwani bado,

    nikamjibu kilevi levi.

    "anhaa! Achana na mimi"

    baada ya muda waliniletea supu iliyojazwa ndimu na pili

    pili nyingi. Niliinywa haraka haraka kutokana na njaa kali

    iliyoniyafuna. Kisha nilitapika sana siku hii. Baada ta

    kupata nafuu niliwaelezea kila jambo lililotokea mpaka

    nikakutana na jordan. Caro alicheka sana prisca akadakia

    huku naye akiwa anapasuka mbavu kwa kucheka. Alisema

    "wewe bella hayo ni mambo ya kawaida kazini, wengine

    tuliwahi kukutana na wajomba zetu tukaliana buyu hivyo

    hayo mambo ni ya kawaida sana kazini chukulia poa

    halafu ngoma isambe"

    siku za usoni nikawa sawa na mawazo ya jordan

    yakaniisha. Ni hapo ndio nikauona mwezi huu ulikuwa ni

    mwezi mbaya zaidi kwangu. Kwa kuwa likatokea jambo

    baya zaidi ambalo sikuwahi kudani kama lingewahi

    kunitokea nikiwa kazini. Ni jambo nililoapa nitaacha kazi

    hii ya uchangudoa. Ni siku hiyo ndipo niliutafuta mzimu

    wa babu ulipo na kumuomba nafasi yake ya mimi

    kuongea na mkuu wa nitimize sharti lolote analotaka ili

    niwe tajiri. Sasa nikautamani utajiri kwa nguvu zote.

    Yaani sikuona pibgamizi lolote la mimi kutimiza sharti

    lolote ili mradi tu niwe tajiri. Ni siku hiyo nilipokutana na

    mzungu mmoja aliyekuja akiwa ndani ya gari nyeupe aina

    ya discovery. Alikuwa akivuta sigara zao zile kubwa

    walizoziita siga. Alivutiwa na mimi kama ilivyo kawaida

    ya wanaume wenye macho ya tamaa ya mwanamke

    mwenye mvuto. Uso wake ulipambwa na tabasamu lauchu

    huku akilamba lamba midomo yake. . Alishusha kioo cha

    gari yake nikapulizwa na kiyoyozi cha ndani ya gari hiyo

    kisha aliniambia.

    "nitakupa shilingi laki tano"

    nilishituka sana kwanza nilishituka kiasi hicho ca pesa na

    pili nilishitushwa jinsi alivyoongea kiswahili fasaha. Lakini

    tamaa haikunikaa mbali na moyo wangu. Nilitabasamu

    lakibi nikijitia kuwa na wasiwasi nilimuuliza

    "kwanini kiasi kikubwa hivyo?"

    "wewe ni binti mrembo sana hivyo sipo peke yangu

    nitakuwa na mwenzangu ambaye anatusubiri nyumbani."

    hapo nikawa nimemuelewa nikaingia ndani ya gari kisha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    safari ya kuelekea kwake ikaanza. Zile fedha alinikabidhi

    shilingi laki mbili kwanza na nyingine kuniahidi kuwa

    atanilipa nikishafika hapo kwake.

    Nyumba yake ilikuwa ni ya kifahari sana. Nakumbuka

    hakuwa na shida ya mlinzi amfungulie geti japo alikuwepo

    askari wa kumlinda. Alilifungua geti kwa remot baada ya

    kubonyeza tarakimu kadhaa ambazo sikujisumbua

    kuzinakili kichwani. Gari likaingizwa sehemu ya parking.

    Mimi na yule mzungu tulishuka baada ya kuja

    kunifungulia mlango akakikamata kiuno changu. Nilikuwa

    nashangaa jisni ya utajiri wa huyu mzee kweli alishindwa

    kuwa na mke huyu? Iweje apende kuja kuchukuwa

    machangudoa na kuwalipa kiasi kikubwa namna ile? Basi

    nilifahamu jibu fika ningelipata ndani ya nyumba hiyo.

    Sebule ya kifahari ikatupokea kwa makochi ya thamani.

    Runinga pana yenye ukubwa zaidi ya nchi 42 ilipachikwa

    ukutani ni zile zinazoitwa plasma. Jokofu lenye milango

    miwili lililofunguka kama kabati la nguo. Hakika nilijihisi

    kusimama katika moja ya sebule za ghali duniani ambazo

    niliwahi kuingia na ambazo sijawahi. Nilikuwa nikiangaza

    huku na huko nikitazama ufahari wa mzee huyu wa

    kizungu. Alipoona nikitazama kila kona ya nyumba yake

    bila kuchoka. Alikohoa kuupata uwepo wangu, kisha

    aliniambia

    "karibu kochini ili niweze kumuita ndugu yangu basi

    tuanze biashara yetu"

    mimi nilitabasamu huku macho bado yakiwa katika kila

    kona nikitazama hiki na kile. Nilikaa lakini bado macho

    yangu hayakuridhika kutazama nilichokuwa nakiona mbele

    yangu. Nikiwa nimekaa, yule mzungu alikuja na mbwa wa

    kizungu. Yale majibwa makubwa yenye mashavu

    yaliyoshuka. Huyu alikuwa mnene sana na mwenye afya.

    Huwa wanaitwa bull dog. Moyo wangu haukushituka

    sana. Nilisimama na kuanza kumchezea chezea yule

    mbwa bila uoga. Mimi nilikuwa mpenzi mkubwa wa mbwa

    hivyo nilimshika mshika yule mbwa manyoya yake

    yaliyonivutia. Nilipoona yule mzungu naye amekaa,

    nikamuuliza

    "yuko wapi rafiki yako? Muda unakwenda ninahitaji

    kuondoka?"

    yule mzungu akatabasamu. Kwa kuwasikumuelewa

    niliendelea kusubiri nifahamu atajibu nini. Aliniambia

    "nadhani damu zenu zimependana. Wengi humuogopa

    bobby lakini wewe hukuwa na haja ya kukuelekeza nini

    cha kumfanyia"

    nikawa bado sijamuelewa nikawa katika kumshangaa.

    Nikamuuliza

    "sijaelewa. Rafiki yako yuko wapi?"

    nilimuona akinyanyuka kwa hasira akija kiti cha jirani na

    nilipokaa mimi. Aliniambia kwa hasiara kidogo

    "wewe malaya. Huyu ndiye rafiki yangu. Anaitwa bobby ni

    mbwa anayejua zaidi ya binadamu hivyo hutajisikia

    vibaya. Nahitaji ufanye naye mpaka aakaporidhika"

    nilihisi sikusikia sawia alichoongea. Nilimuuliza ili nipate

    hakika

    "huyu ndiye rafiki yako uliyeniambia!!?"

    akatingisha kichwa huku tabasamu likiwa usoni mwake.

    Tabasamu lililoanza kunikera. Nilipomtazama yule mbwa

    alikuwa akitoa ulimi wake kwa uchu. Sehemu zake za siri

    zikawa zimeanza kusimama. Jasho likanitoka nikawa

    nikimuangalia mbwa na yule mzee kwa zamu. Sikuamini

    kama leo nilikuwa natakiwa nilale na mbwa yaani mimi

    nitembee na mnyama? Niliona kitu ambacho



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hakikuwezekana hata chembe. Niliutazma mkoba wangu

    ulio na pesa zote ulikuwa karibu. Nikatazama umbaii wa

    mlango ulipo na nilipokaa,nikapima hazikuzidi hatua kumi

    kwa kukimbia. Chozi likaanza kunitoka ilipomuona yule

    mbwa akianza kunisogelea akinilamba lamba mapaja

    yangu. Nakumbuka nilichomoka kama mshale kwenye kile

    kiti ila nilifanya kosa dogo. Wakati nikikimbia niliuweka

    mguu wangu sambamba na mdomo wa yule mbwa.

    Hakuaacha kunipitishia meno yake na kuniparua kwa

    makucha yake. Yule mzungu alikuwa akicheka sana huku

    akimuambia vitu fulani yule mbwa ambavyo sikuvielewa.

    Nilianguka bila kukosa mhimili mzuri. Yule mbwa akawa

    ameshalipata titi langu na kucha zake zikiwa zipo juu ya

    kifua changu. Aliichana sehemu kubwa ya titi langu la

    kushoto lakini ikawa sawa na kunipa nguvu ya kumpiga

    ngumi moja nikausikia mlio mmoja tu aliutoa kwa

    uchungu na kumuona akiwa ameanguka mbali kidogo na

    mimi. Nilianza tena harakati za kukimbia nje kuokoa

    maisha yangu. Yule mzungu hakunipata hata alipojaribu

    kunikimbiza. Nilikuwa tayari nimeshafika nje ya geti

    baada ya kumpita yule mlinzi wake aliyekuwa akikoroma.

    Ilikuwa yapata saa kumi alfajiri. Nilirudi hadi lile eneo

    ambalo alinitoa yule mzungu.

    Kutokana na titi langu moja kuwa wazi na nguo zangu

    kuchanika nilishindwa kurudi nyumbani moja kwa moja.

    Nilirudi eneo lile ili niweze kupata msaada wowote kwa

    wenzangu. Nilipofika sikukuta mtu, nilimkuta kaka mmoja

    ambaye alikuwa akifungua duka lake eneo hilo.

    Nilimuomba hifadhi kwa kumueleza kila kitu bila kumficha

    chochote akaniweka ndani ya kiduka chake kidogodogo

    kisha nilimpatia shilingi elfu ishirini ili aweze kuninunulia

    doti za kanga. Alikubwali kwenda kunitafutia. Nashukuru

    alirudi akanipatia khanga hizo ambapo damu zilikuwa

    zimeanza kukauka juu ya titi langu. Nikajifunika moja juu

    na nyingine chini hakuna ambaye angefahamu kama ndani

    nilikuwa uchi kabisa. Nilikuwa nikilia njia nzima. Wengi

    walizani kuwa nilifiwa kutokana na uvaaji ule wa khnga

    na jinsi nilivyokuwa rafu. Mmoja wa watu waliopishana na

    mimi alinipa pole mwingine alisikitika

    "masikini inawezekana amefiwa na mtu wake wa karibu"

    ilikuwa tayari asubuhi mpaka niliofika katika geto letu.

    Nilianza upya kulia baada ya kuwakuta wote wapo.

    Niliwahadithia kila kitu na kuwaonesha majeraha ya

    mbwa aliyening'ata. Waliniapa pole na kuanza taratibu za

    hospitali. Mimi moyoni nikaapa siwezi kuwa changudoa

    tena. Niliichukia kazi ile nikaichukia zaidi. Niliumia sana

    kwa yaliyonikuta. Baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali

    tulirudi nyumbani nikiwa nimeambiwa na daktari nipate

    muda mwingi wa kupumzika.hiyo ikawa tiketi ya kuaga

    biashara hiyo. Usiku ulipofika wenzangu waliniaga na

    kuniambia kuwa kama nikipata nafuu nisiache kwenda au

    hata kama nilihisi hali ilikuwa ni mbaya zaidi niwataarifu

    wao watakuja kunitazama. Niliwaitikia kwa kichwa

    nikiwaigizia kua nimezidiwa. Baada ya kuniacha na mimi

    nikapitiwa usingizi. Katikati ya usingizi nilisikia sauti za

    ajabu zikizungumza ndani ya hiko chumba nilicholala.

    Niliamka nikiwa nimelowa sana jasho. Nilipoitazama feni,

    ilikuwa ikifanya kazi yake kama kawaida. Nikajiuliza

    "sasa hili joto linatoka wapi?" nikajifuta hilo na kujilaza

    tena juu ya mto. Nikiwa hata kabla sijafunga macho

    yangu nilisikia kelele za bati lililopasuka na mwanga mkali

    mweupe kupenya ndani. Ilikuwa ni hali iliyotisha lakini

    miujiza ya namna hiyo ikawa ni kawaida kwangu. Kiumbe

    cha ajabu kikawa kimeshuka mfano wa ndege aina ya tai

    kikanikwapua kutoka kitandani kwangu nilipolala na

    kuanza kupaa na mimi kunipeleka nisipopajua. Hatimaye

    kiumbe kile kilicho na umbo kama la ndege huyo

    kikanitupa chini ya mti mkubwa aina ya mbuyu yaani

    ulikuwa mkubwa sana huku moto ulikuwa umewashwa na

    watu kadhaa wakiuzunguka moto huo. Niliwasikia

    wakiimba nyimbo mbalimbali nisizozijua wala kufahamu

    zilikuwa ni za lugha gani. Ule mti ukapasuka katikati na

    kutoka kiumbe kingine cha ajabu yaani lilikuwa ni joka

    lililotisha na kuwameza kila mmoja aliyekuwa katika eneo

    hilo. Lilinimeza na mimi pia. Sikuhisi madhara yeyote

    nilipokuwa ndani ya tumbo la huyu nyoka. Ila nilihisi

    tulikuwa tunashuka kwa kasi sana yani kasi iliyonifanya

    nihisi huenda ningeuacha mwili wangu na roho pekee

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ndiyo ingedondoka huko nilipokuwa nikielekea. Wale

    wengine walikuwa uchi wakishangilia tukio hilo. Sikuweza

    kumtambua hata mmoja ila nilikuwa nikisubiri kutazama

    kitakachotokea. Moyo haukuwa na uoga sana kwa kuwa

    nilishi tu ni lazima ilikuwa ni safari nyingine ya Gamboshi.

    Lakini nilipata sana shida kila nilipojiuliza binafsi kwanini

    babu hakuwa tayari kunisaidia nilipokuwa katika tatizo

    kama la kung'atwa na mbu? Safari ikaishia katika kijiji

    nilichokitarajia, Gamboshi. Nilipoangaza huku na huko

    nikahisi kugongwa bega. Nilipogeuka alikuwa ni babu.

    Alinikumbatia na kunipa pole. Kisha alinieleza

    "usiku ule ule hakuweza kuliona japo jua la asubuhi"

    babu alimuongelea yule mzungu aliyetaka nitembee na

    mbwa wake

    "mlinzi wake alistaajabu kumuona yule mbwa akimtafuna

    mpaka mifupa huku kichwa pekee kikiwa kimelalia damu

    yake nzito iliyoanza kuganda"

    nikatamanu kuona hiko ambacho baba alikuwa

    akinihadithia japo nilitabasamu kwa raha. Babu

    akaniambia

    "safari hii ni ya kukupa tena nafasi yako uliyopokonywa

    baada ya kushindwa masharti na kukupeleka kwa mkuu

    mwenyewe na umueleze shida zako"

    Nikamuuliza swali babu

    "shida zangu? Nimueleze nini babu?"

    babu alinicheka akaniuliza

    "ina maana wewe huna shida? Huna chochote unachotaka

    kuomba mbele za mkuu?"



     Nikamuuliza swali babu

    "shida zangu? Nimueleze nini babu?"

    babu alinicheka akaniuliza

    "ina maana wewe huna shida? Huna chochote unachotaka

    kuomba mbele za mkuu?"

    Kiukweli si kwamba sikuwa na shida au sikumuelewa babu

    alichonieleza ila ni jinsi ambavyo nilikuwa nahitaji mambo

    mengi na makubwa nikahisi nitapewa masharti mengine

    ambayo nitayashindwa kabisa kuyatekeleza. Nilimjibu

    "nahitaji utajiri babu nataka niishi maisha mazuri nikiwa

    na familia yangu"

    "hayo ndiyo yakumueleza mkuu sasa"

    tulipotea pale tulipokuwa kisha tukatokezea sehemu

    ambayo sikuwahi kuingia tangu nianze safari zangu za

    huku Gamboshi. Mahali hapa palikuwa ni pazuri sana.

    Kulikuwa na watu wengi wakicheza ngoma na kuimba

    nyimbo mbalimbali. Babu aliniambia kuwa.

    "mkuu wetu ni mkuu sana. Hupenda kuabudiwa na

    heshima hivyo hata ukiwa unazungumza naye hakikisha

    kichwa chako kinasujudu mbele zake"

    niliitikia kwa kutingisha kichwa huku nikiendelea kutazama

    wale watu walivyokuwa wakicheza. Nyimbo zile

    zilionekana kuwafurahisha sana jinsi walivyokuwa

    wakiendana na midundo ya ngoma ilivyo kuwa ikipigwa.

    Nilianza kutabasamu kidogo kidogo kutokana na mimi pia

    nilianza kuvutiwa na ngoma hizo. Baada ya muda kidogo

    watu wote wakainama zaidi hata babu pia alipoinama

    alipiga kelele na mimi niiname pamoja naye. Niliinama pia

    huku nisijue nini kinaendelea. Nilimtazama babu

    nikimuuliza nini kinatokea

    "mkuu ndiyo anakuja" Alininong'oneza. Baada ya muda nilisikia kicheko kikali

    kutoka ule upande wa kaskazini yaani mbele nilipokuwa

    nikiatazama. Sikuinua kichwa changu. Wakati hu uo

    nikasikia sauti y a mkuu ikiita jina langu kwa sauti ya juu

    "bella mwanangu karibu tena Gamboshi"

    babu alinionesha ishara ya kusimama. Nilisimama

    nikainamisha kichwa mbele zake

    "ahsante mkuu"

    nilimjibu kwa sauti ya juu iliyomfikia kutokana na eneo hili

    lilirudisa sauti na kutengeneza mwangwi uliokera. Yule

    mkuu alikua ni kile kiumbe cha ajabu kilichonipatiamashar-

    ti niliyoyashindwa kipindi kile. Fumba na kufumbua

    nilijikuta pembeni yake akichezeachezea nywele zangu.

    Alikuwa anavuja damu na macho yake yaliudhi sana. Vile

    vinanda vilikuwa vikitoa ala nzuri ya mziki kila alipokuwa

    akicheka. Yule kiumbe aliniambia

    "unataka nini kwangu? Sema nini nikufanyie?"

    nilihisi furaha ya ajabu moyoni mwangu na wepesi kiasi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    fulani. Nilipoipata sauti yangu nilimuambia

    "nahitaji maisha mazuri na niwe mwenye mamlaka yaani

    utajiri wa kuogopwa na kila mtu hata wale viongozi wa

    serikalini"

    yule kiumbe kikacheka mpaka kikatoa ceche za moto na

    kusema

    "inawezekana"

    neno hilo likajirudia mara nyingi nyingi. Kisha aliniambia

    tena

    "sharti letu kubwa tunaitaka roho ya jordan. Pia usizae

    mpaka utakapofikisha miaka 30 na usiwe mwenye

    kumueleza mtu kila kitu usiyemjua"

    nilitabasamu na kumjibu harakaharaka

    "usijali mkuu nitatekeleza kila unaloniambia. Kama ni roho

    ya Jordan hata sasa nitakuletea kama utahitaji"

    alicheka sana yule kiumbe aliyetisha na kuniambia tena

    "nenda nenda nenda utajiri upo nyuma yako ukikufuata.

    Utakuwa tajiri mwenye viwanda vingi ndani na nje ya

    nchi. Bidhaa zako zitapendwa na kugombewa kama

    njugu. Ni utajiri utakaowashangaza wengi lakini

    usimueleze yeyote na kumwambia chochote yeyote.

    Nimekubariki wewe na uzao wako endapo utafuata

    masharti hayo" kisha nilitoweka eneo hilo la gamboshi na

    kujikuta nikiwa tena kitandani. Nilipowasha taa na

    kutazama ilikuwa ni saa ngapi

    "saa tisa?"

    nikajilaza tena nikiwa nina mipango mipya ya kuitafuta

    roho ya Jordan. Hii ilikuwa ni usiku wa siku ya pili.

    Kutokana na kila mtu kuwa mzoefu, mimi niliwaaga

    wenzangu kuwa naenda kijiwe kingine kutafuta wateja.

    Walinikubalia bila kujua hila zangu. Wao waliniacha mimi

    bado nikiendelea kujivuta vuta.

    Nilikuwa nina uhakika kuwa wakati huu ni wakati ambao

    kule shuleni ni lazima wangekuwa wameshalala. Niliwaza

    jinsi nitakavyoitoa roho ya Jordani. Mwanaume ambaye

    nilimpenda kuliko mwanaume yeyote katika hii dunia. Ila

    sasa sikuona uchungu tena wa kuitoa roho yake.

    Nilijaribu kuitafuta huruma lakini ilikuwa mbali na roho

    yangu. Sikujuwa sababu ya kumchukia Jordan lakini

    nilichojua sikumpenda tena wala sikuwa na huruma juu ya

    kifo chake. Nilishuka mpaka juu ya bati la bweni ambalo

    alikuwa akilala Jordani. Nakumbuka nilipata uwezo wa

    kulipasua bati na kuingia mpaka alipo yeye. Alikuwa

    akikoroma kwenye usingizi mzito uliomdondosha udenda..

    Nilimnakuwa na kuanza kupae naye. Nilikuwa nimeota

    mbawa na kugeuka kiumbe cha ajabu. Nilielekea mpaka

    ulipo ule mbuyu ambao ulinidumbukiza mpaka ilipo

    Gamboshi. Kama siku ile ya mwisho ndivyo ambavyo ule

    mbuyu ulipasuka. Nikiwa bado nimembeba Jordan

    sikumuona kama ni mzito tena. Ulembuyu ulipasuka na

    lile joka likatokeza mbele yetu likanimeza mimi pamoja na

    Jordan. Lilitumeza na kudumbukia mpaka Gamboshi.

    Umati mkubwa ulikuwa ukitusubiri kwa hamu huku ngoma

    mbalimbali zikiwa zinapigwa. Waliponiona watu wale

    nikiwa na Jordan umati ule wote uliripuka kwa furaha ya

    ajabu wakiwa wanapiga nduru na vifijo vigele gele vikiwa

    juu. Nilielekezwa sehemu ya kumlaza Jordan mimi nikiwa

    nimerudi katika hali yangu ya kawaida. Yule mkuu wa

    Gamboshi alikuja kujumuika nami pale nilipokuwa

    nimemlaza Jordan akiwemo na babu yangu. Kisha babu

    ndiye alinipa kisu, akaniambia

    "tunauhitaji moyo wa Jordan"

    nikakipokea kile kisu. Mikono ikawa inanitetemeka.

    Sikufahamu sababu ya mikono kunitetemeka ila nilijua ni

    uoga uoga wa kuitoa roho ya binadamu? Nilishatoa za

    wangapi? Nikauinua mkono ulioshikilia kisu na

    kukichomeka upande wa moyo ulipo. Nilikipasua kifua

    chake kwa kisu kilichopenya sawia kwenye moyo wake.

    Jordan aliamka na kuanza kutapa tapa huku macho

    kayatoa pima. Baada ya tukio hilo umati ule ulilipuka tena

    kwa furaha na mkuu naye aliongeza shangwe hizo kwa

    kicheko chake kilichokera. Nikaunyofoa moyo wake

    uliokuwa ukidunda dunda na kumkabidhi babu. Kile

    kiumbe kilizungumza

    "umeweza bella umewezaa"

    alikuwa ni mwenye furaha sana. Kisha mimi nikatoweka

    na kujikuta juu ya kitanda changu. Sikulala siku hii,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nikikumbuka vile ambavyo niliutoa uhai wa jordan.

    Nikiyakumbuka macho ya Jordan yaliyokuwa

    yakinitazama kwa huruma. Nilitamani kulia lakini machozi

    hayakunitoka. Ni hapo nilipoamua kuwasha taa ili niweze

    kutoka nje nikakutana na begi lilotuna pembezoni mwa

    kitanda nilichokaa. Nikavuta kumbukumbu kama niliwahi

    kuliona humo ndani hapo kabla,

    "hapana sijawahi kuliona"

    nlipotaka kulisogelea nikaiangalia saa kutazama ilikuwa ni

    saa ngapi. Ilikuwa yapta saa 8 usiku. Nikajiuliza.

    Inawezekana kati ya Caro Prisca ama Zamda ni nani

    alikuja na mgeni ambaye sijamuona? Nilipotaka

    kulifungua niliusikia upepo uliovuma kwa nguvu sana

    kisha nikaisikia sauti ikiniongelesha. Ilikuwa ni sauti ya

    babu akiniamba

    "huo ndiyo utajiri wako bella"

    alijitokeza mzima mzima mbele yangu na kuniambia

    "umemfurahisha sana mkuu wetu kwa kafara

    uliyoifanikisha mbele yetu kuitoa roho ya mpeniz wako

    umeuonesha ujasiri wa hali ya juu kama ambao ulinfanya

    akuchague wewe. Utakuwa tajiri usiyefilisika katika

    maisha yako na ukoo wako unachopaswa kuzingatia ni

    kufuata masharti mkuu aliyokupa ndio kitu muhimu na

    cha kuzingatia"

    katika begi lile kulikuwako na pesa nyingi sana.

    Maburunguta ya pesa zakigeni yaani dola mia mia.

    Kuanzia siku hiyo maisha yangu yakabadilika. Sikuwa

    changudo tena na wala sikuwa na maisha ya kutanga

    tanga tena. Kila mtu akanijua na kunizungumzia kati ya

    mmoja wa matajiri wa kutetemekewa ndani ya tanzania

    na nje furaha yangu ikawa imetimia ya KUONGEA NA

    SHETANI MPAKA KUUPATA UTAJIRI sifikiri kuyavunja

    masharti wala kukiuka agano nililoweka mbele ya mkuu.

    Nitawapeleka mamia Gamboshi na kuwaangamiza wale

    waliokuwa wakimpinga mkuu wa Gamboshi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MWISHO.

0 comments:

Post a Comment

Blog