Search This Blog

MALAIKA? AU SHETANI? - 3

 





    Simulizi : Malaika? Au Shetani?

    Sehemu Ya Tatu (3)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ujasiri ulikufanya ujikaze huku ukilia kwa sauti hafifu, lakini kadiri maumivu yalivyokuwa yakiongezeka, ndivyo sauti ikaanza kupanda, kilio cha uchungu na maombolezo kikawafikia wapangaji wenziyo na kuwafanya waje kukugongea mlango. Ukajizoazoa kitandani, ukautwaa mlango na kuwafungulia, kisha ukajibwaga sakafuni na kuendelea kuugulia maumivu huku ukiwa umeushikilia mkono kama kwamba unayazuia maumivu yasisambae mwilini.

    “Muga!” mama mwenye nyumba akaakuita, “umeumwa na mdudu?”



    “Bora hata angeniuma,” ukamjibu huku jasho la uchungu na maumivu likikutiririka, “ameniingiia kabisa mkononi!”

    Mama mwenye nyumba, pamoja na wapangaji wenziyo, waliojumuika chumbani mwako, walikumbwa na taharuki. Na badala ya kukusaidia, wakaanza kukuhofia. Vihoro na alama za mshangao vikajidhihirisha kwenye nyuso zao.



    “Mbona hatukuelewi Muga?” Salum mdananda, kijana aliyepanga chumba cha pili kutoka cha kwako, akaakusaili huku akikuinamia. Ukatamani kuwasimulia, walakini maumivu makali hayakukupa pumzi za kutosha kufanya hivyo. Badala yake, ukaazidi kulia kwa uchungu.



    Wakaamshwa majirani, wajuvi wa dawa za kuondosha sumu za wadudu mfano wa Nyoka, Nge, Tandu, nk. Kuamshwa kwa majirani, kukaaongeza idadi ya watu chumbani mwako.”

    “Enhee, amekuuma wapi?” mmoja kati ya wazee walioleta dawa, alikusaili.



    Ukatamani kumwambia kwamba hakukuuma, bali alikuingia mwilini, lakini hilo litachukua muda na kucheleweshea tiba–ukamwonesha mkononi, huku ukiendelea kulia.

    Si tu kwamba dawa hazikufaa kitu, bali kadiri walivyokuwa wakikupaka dawa, ndivyo sumu ilivyozidi kutambaa ndani kwa ndani na kuzalisha maumivu mara dufu. Kwa uchungu ukajikuta ukiwaondoa wasikuguse. Hilo nalo likawashangaza majirani na wapangaji wenziyo.



    “Ja–ma–ni nau–mia–” Kila ulipohitaji kuelezea namna maumivu yanavyozidishwa na dawa zao, kauli haikufika mwisho kwa maumivu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Majadiliano ya wakubwa, yakapitika kwamba uwahishwe hospitali. Na, kwakuwa hapo unapoishi si mbali na hospitali ya Amana. Mzee Lawalawa, mmoja wa majirani, akajitolea gari yake, ukapandishwa kwa kubebwa, na msafara wa kuelekea hospitali ukaanza.



    Kilichowastaajabisha madaktari ni kauli kutoka kwa wapangaji wenziyo kwamba, kuna mdudu amekuingia mwilini, kutokana na maelezo yako ya awali. Kesi nyingi huwa mni tu kuumwa na mdudu mwenye sumu, na si mdudu kuingia mwilini kupitia sehemu isiyo na tundu. Kama kawaida ya matabibu, matibabu yakaanza.



    Taarifa za maradhi zinawafikia nduguzo mjini Bukoba. Kwa uzito wa aina ya ugonjwa, hawakufanya zohali, walijikusanya na kuianza safari ya kuja jijini Dar es Salaam. Pia, taarifa zikawafikia watu wa Bukoba waishio Dar es Salaam, walakini wakagoma kujumuika nawe, kwa sababu tangu awali uligoma kujumuika nao wakati wakianzisha umoja wa kusaidiana.



    Majira ya saa kumi na mbili jioni, waliowasili kutoka Bukoba ni; mama yako, Bi Mwanakatwe; dada yako, Shella; Na, kaka yako, Kamugisha. Wakati huo, ule uchungu usababishwao na sumu ya kijidudu ndani ya mkono, ulikuwa umepungua, maumivu yakabaki kwa mbali.

    Salum Mdananda na mzee Lawalawa, wakawapokea nduguzo na kuwapa kwa muhtasari, taarifa za tangu hali ilivyobadilika usiku hadi kufikia muda huo. Nduguzo pamoja na mama yako, wakawashukuru waungwana wale kwa namna walivyoshughulika hadi muda ule.



    Baada ya kumalizana na akina mzee Lawalawa, mama yako alikusogelea, na kuanza, “Pole sana, unaendeleaje kwa sasa?”



    “Ahsante mama, naendelea vyema, namshukuru Mungu.”

    Shella akadakia kwa wahka, “Haya, ilikuwaje hasa na kipi kimekukumba?”



    “We nawe, hata hatujajuliana hali!” Muganyizi akamshushua Shella.



    “Ni vyema akatusimulia mapema kama hali yake imetulia, kuliko kukaa tu halafu hali ibadilike ashindwe hata kuzungumza!” Shella akasema.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ukajiinua kitandani na kuketi, kisha ukaanza kusimulia mkasa mzima, tangu awali ya mkasa wa Ombaomba na sauti ya ajabu, hadi akhiri ya usiku wa uvamizi wa Ombaomba chumbani kwako. Simulizi za kubandikwa jino na kuingiziwa kijidudu, iliwaacha hoi nduguzo, kila mmoja akiingiwa na ubaridi wa hofu.



    “Hapa, kuna namna, si bure,” bi Mwanakatwe akasema, “na sioni haja ya kuendelea kupoteza muda hapa hospitali!”



    “Kabisa!” Kamugisha akayasadiki maneno ya mama yake.



    “Mwiba uingiliapo ndipo utokea. Kamwe, uchawi hautolewi hospitali,” bi Mwanakatwe aliendelea. “Leo hii, nitakwenda kwa Nyahinga kumuelezea.”



    Nyahinga, mama wa rika la bi Mwanakatwe. Ni mganga wa kuogopwa kutoka Bukoba japo anaishi Dar es Salaam. Amejitengenezea umaarufu mkubwa kwa uwezo wake wa kupambana na wachawi na kuwaangamiza. Makazi yake ni Gongo la Mboto.



    Bi Mwanakatwe na Nyahinga, walifahamiana tangu enzi za utoto wao huko Bukoba, kabla ya Nyahinga kuhamia jijini Mwanza na baadaye Dar es Salaam kwa shughuli zake za kiganga. Kwa fikra za bi Mwanakatwe, zilizoungwa mkono na watoto wake, tatizo linakwenda kuhitimishwa na mtaalamu wao.



    Ilitokea kama bahati, pale bi Mwanakatwe alipokwenda kuomba ruhusa kwa madaktari, kumwondoa mwanawe hapo hospitali ili kumtibu kienyeji, alikubaliwa. yamkini madaktari nao, walikuwa njia moja kutoa ushauri kama huo, baada ya kusikia kisa cha mdudu wa ajabu aliyemo ndani ya mkono wa mgonjwa.



    Nyote kwa pamoja mkaondoka hospitalini hadi kwako. Baada ya kufika nyumbani, majirani na wapangaji wenziyo wakaajumuika kukujulia hali. Walipokwisha, wakasambaa kila mmoja na shtighali zake za dunia. Baada ya kupata chakula na maji ya kuoga, kwa kutumia gari ya Kamugisha, mkaianza safari ya kuelekea Gongo la Mboto kwa Nyahinga.



    __________

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    BAADA ya Nyahinga kukuoneni, kwa bashasha na taadhima, akawaacha wateja, akatoka kumlaki shoga yake, “Oh, Mama Kamu, karibu sana shoga yangu–sikujua kama mko nje, nisingalikuweka muda wote huo ndugu yangu!”



    “Aah, usijali swahiba, ndivyo kazi inavyotaka hivyo,” bi Mwanakatwe akajibu.



    “Kweli unenayo, lakini si kwa mtu kama wewe bwana–we ni mwanafamilia!”

    Baaada ya kupokeana; bi Mwanakatwe akakutambulisheni nyote kwa Nyahinga.



    “Hata ningekutana nao barabarani, haki vile, nisingaliwakumbuka. Niliwaacha wangali wadogo mno,” Nyahinga akasema. “Kama huyu Muga ndo alikuwa mwembamba kama chelewa!”

    Nyote mkacheka kwa pamoja.



    “Na huyo ndo ametufanya kwako muda huu,” bi Mwanakatwe akaanzisha mjadala.



    “Kumbe–basi vyema–karibuni!”



    Kabla bi Mwanakatwe hajasimulia chochote, mabadiliko ya hali yako yakaanza kutoa picha ya tatizo lililokupelekeni hapo. Mdudu akaanza kutambaa mithili ya moto mkononi mwako na kukuachia sumu kali ya maumivu kiasi cha kukufanya uanze kulia na kuomboleza kwa uchungu. Hali ika tafrani, Nyahinga akashirikiana na wasaidizi wake kukutuliza kwa ufundi wa kiganga bila mafanikio. Hila zote zikamwisha Nyahinga, bila ya kuweza kuzuia maumivu wala kujua kiini cha tatizo.



    Zinaletwa dawa za kupaka–hazikufua dafu! Dawa za kunywa–hazikufaa kitu! Maumivu makali mtindo mmoja!

    Mara, Nyahinga akapandisha mizimu, na kuanza kuongea lugha zisizoeleweka kwa mtu wa kawaida. Wasaidizi wake ambao walikuwa wakimsaidia kusikiliza maelekezo ya mizimu, nao ghafula wakapandisha mizimu. Nyumba ikakuwa ya mizimu–utulivu ukavurugika–hakuna wa kutafasiri wala kuwaelewa mizimu waliopanda vichwani mwa wataalamu. Almanusra wazimu umpande bi Mwanakatwe.

    *****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mara, Nyahinga akapandisha mizimu, na kuanza kuongea lugha zisizoeleweka kwa mtu wa kawaida. Wasaidizi wake ambao walikuwa wakimsaidia kusikiliza maelekezo ya mizimu, nao ghafula wakapandisha mizimu. Nyumba ikakuwa ya mizimu–utulivu ukavurugika–hakuna wa kutafasiri wala kuwaelewa mizimu waliopanda vichwani mwa wataalamu. Almanusra wazimu umpande bi Mwanakatwe.



    Hali hiyo ilidumu kwa takribani nusu saa kabla ya mizimu kumruka Nyahinga, na kustaajabu kuona wasaidizi wake nao wakiwa wamepandisha mizimu vichwani. Akawasikiliza huku akiwahoji hadi walipomaliza na kuruka.

    Utulivu ukarejea kwa wastani.



    “Fanya upesi, kalete nghusha,” Nyahinga akamwagiza msaidizi wake, “lete ile nyekundu!”

    Nghusha ni dawa ya mitishamba, ambayo aghalabu hufungwa kwa kuzungushwa kwenye kitambaa chekundu au cheusi.



    Ngusha Ilipofika, Nyahinga akakufunga mkononi na kuanza kukupunga huku akiimba nyimbo za kiganga kwa lugha ya kihaya. Alifanya hivyo huku akikuzunguka mduara hadi maumivu yalipopunguza kasi na kwisha kabisa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog