Search This Blog

JINI WA DARAJA LA SALENDA - 1

 







    IMEANDIKWA NA : ALLY MBETU

    *********************************************************************************



    COMPLETE - IMEKAMILIKA YOTE



     Simulizi : Jini Wa Daraja La Salenda

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Majira ya saa nane za usiku msichana Suzana alikuwa akitoka kujirusha katika ukumbi wa Bilicanas. Kilichomshtua kilikuwa kutoweka kwa mpenzi wake Sammy ambaye aliondoka bila kumuaga. Wazo lake la kwanza lilikuwa Sammy kaondoka na msichana mwingine akijua kabisa yeye ndiye mchumba wake.Akiwa amekasirika kwa kitendo cha Sammy kuondoka na kumuacha peke yake, kila alipopiga simu yake iliita bila kupokelewa kitu kilichoonesha dharau. Aliamua kurudi nyumbani kwake japo alipanga siku ile kwenda

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

     kulala kwa Sammy. Aliendesha gari akiwa amefura kwa hasira huku machozi yakimtoka kutokana kitendo alichotendewa na mpenzi wake ambaye ndiye aliyemtoa kitandani alipokuwa amekwisha kulala. Suzana awaliza mengi juu ya kitendo cha mpenzi wake kumwita klabu na kumkimbia.Wakati akitoka Bilicanas mvua ilianza kunyesha, hakutaka kuisubiri aliamua kwenda nayo ili awahi kunyumba angalau alale kwa muda mchache ili asubuhi awahi kanisani misa ya kwanza.Mvua ilikuwa kubwa iliyoambatana na upepo mkali kitu kilichomfanya ashindwe kuona mbele ilimbidi alisimamishe gari pembeni ya daraja ya Salenda ili kusubiri upepo upungue ndipo aendelee na safari yake. Upepo ule haukuchukua ulitulia na mvua ilikuwa imekatika.Alipowasha gari liligoma kuwaka, alirudia zaidi ya mara tano kuzungusha funguo lakini liligoma kuwaka. Kuteremka kwenye gari alishindwa kutokana na hali ya kiza cha kutisha nje. Wasi wasi ulimtawala na kujiuliza atatokaje pale au ndio atalala mpaka asubuhi.Hasira zilizidi kumpanda Suzana kutokana na kukimbiwa na mpenzi wake na kuharibikiwa na gari. Kutokana na hofu aliyokuwa nayo alihakikisha milango na vioo vyote vimefungwa vizuri. Alijikuta akipiga dua kumuomba Mungu amuokoe la janga lile kwa kupata msaada wa watu wenye gari kumsaidia kuwasha gari lake. Lakini kwa muda ule hakukuwa na dalili ya gari lolote kupita.Akiwa ameinama mikono ameikutanisha kifuani kwake alishtushwa na upepo makali uliovuka toka baharini na kulifanya gari lake kuyumba na kusogea kidogo. Kwa woga uliompata Suzana alijikuta akitokwa na haja ndogo bila kuelewa. Alitamani kulia lakini aliamini sauti yake haitasaidia lolote kwa vile hakukuwa na wakumsaidia.Aliinama kwa woga hakutaka kuangalia popote zaidi ya kusubiri chochote kitakachomtokea. Baada ya muda hali ile ilitulia, Suzana alinyanyua kichwa taratibu ili achukue simu ampigie baba yake amfuate eneo lile ambalo lilikuwa limemuweka katika hali ya hatari.Aliponyanyua uso achukue simu iliyokuwa kwenye kwenye dash board, alishtushwa na mwanga mkali kama jua la saa saba mchana. Aliangalia katikati ya bahari palipokuwa kunatoka mwanga ule. Alituliza macho baada ya kumuona mwanamke aliyekuwa amevaa gauni jeupe lilikuwa liking’aa kutokana na mapambo yake.Hali ile ilimfanya asahau yalitomtokea muda mfupi na kutuliza macho kumuangalia yule mwanamke aliyekuwa akitembea juu ya maji huku nyuma akisindikizwa na wasichana walikuwa wamebeba vikapu vidogo vilivyokuwa na maua ambayo walimwagia kila hatua ilivyopigwa huku wakiimba nyimbo nzuri.Suzana alijikuta akipata ujasiri wa ajabu kwa kufungua dirisha kidogo ili aweze kusikia watu wale walikuwa wakiimba kitu gani. Zilikuwa sauti nzuri kama za kaswida zilizoibwa kwa lugha ya kiarabu. Nyimbo zile zilimvutia na kujikuta akiwa na hamu ya kuwaona watu wale waliokuwa wakitembea juu ya maji huku kwa mstari mbele akitangulia yule mwanamke ambaye usoni kwake kulikuwa kunawaka kama taa na kushindwa kuiona sura yake vizuri.Suzana alijikuta akisahau kama wale watu walikuwa wakitembea juu ya maji zaidi ya kushangazwa na sherehe ile ambayo toka azaliwe hajawahi kuona sherehe ya aina ile ya mtu mmoja kutangulia mbele wengine kumfuata nyuma huku wakimuwagia maua na kumwimbia nyimbo nzuri.Baada ya muda watu wote walikaa mstari mmoja, kisha yule mwanamke aliyekuwa amepeneza kuliko wote alipita katikati yao na kupigiwa vilegele huku akitupiwa maua. Manukato ya maua yalisambaa mpaka ndani ya gari la Suzana alilokuwa amefungua kioo kidogo kusikia nyimbo alizokuwa anaimbiwa yule mwanamke ambaye alionekana kama bibi harusi lakini muda wote hakumuona bwana harusi wala mwanaume kwenye kundi lile.Yule mwanamke alipita kwenye mstari mpaka mwisho alitembea peke yake bila kufuatwa na mtu kisha aligeuka na kuwapungia mkono wenzake ambao nao walimpungia huku wakimrushia maua. Baada ya kutembea kidogo Suzana alimshuhudia yule mwanamke alikunja gauni lake usawa na kifua na kushangaa kumuona akitembea ndani ya maji yaliyokuwa yamemfika tumboni.Suzana alijikuta akishtuka na kujiuliza yupo ndotoni au anaona kweli, kilichomshangaza ni umbali aliotoka yule mwanamke akitembea juu ya maji. Lakini cha kushangaza alipokaribia ufukweni alionekana yupo ndani ya maji yaliyomfikia tumboni.Aliendelea kumtazama amuone anakwenda wapi, yule mwanamke baada ya kutoka ndani ya maji alitembea juu ya mchanga kulifuata lile gari. Kila hatua ilivyokuwa akipiga ilizidi kumtisha Suzana, alijikuta akimshangaa kutaka kuijua sura yake. Alituliza macho yake kwenye uso wa yule mwanamke aliyekuwa akiisogelea gari huku manukato makali yakizidi kujaa ndani ya gari.Kilichomshangaza zaidi ni sura ya yule mwanamke alikuwa akifanana naye kwa kila kitu umbile na sura. Suzana alishtuka na kufunga kioo haraka ili mtu yule ambaye yeye alimuona wa muujiza asiingie kwenye gari. Yule mwanamke alisogea kwenye gari na kuligusa, ajabu baada ya kuligusa lile gari alitoweka ghafla.Suzana akiwa anatetemeka alijaribu kuwasha gari kwa mara nyingine, ajabu ya Mungu gari liliwaka aliondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Alipofika nyumbani kulikuwa kumekucha, alikwenda kuoga haraka ili awahi kanisani kwani muda ulikuwa umekwenda.Baada ya kuoga alirudi ndani, lakini

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alishtushwa na harufu ya manukato ambayo aliyasikia muda mfupi darajani gari lake lilipozima na kuenea hadi ndani ya gari lake. Hakutaka kulifikiria sana lile kwa muda ulikuwa umekwenda, alikwenda kwenye kabati kubadili nguo ili awahi kanisani.Baada ya kumaliza kubadili nguo alijikuta akiingiwa na uvivu na kwenda kukaa kwenye kitanda haikupita muda. Usingizi mzito ulimshika na kulala bila kujielewa, aliposhtuka usingizini alishtuka kuiona familia yake yote imesimama mbele yake. Alijiuliza kuna nini, alipojiangalia alijiona alikuwa amevaa nguo za kuendea kanisani.“Suzana upo sawa?” Mama yake alimuuliza. “Mbona unaniuliza hivyo? Halafu mbona kama wote mlikuwa mnalia kuna nini mbona mnanitisha?

    LIPOISHIA; Yule mwanamke alipita kwenye mstari mpaka mwisho, alitembea peke yake bila kufuatwa na mtu kisha aligeuka na kuwapungia mkono wenzake ambao nao walimpungia huku wakiendelea na zoezi la kumrushia maua. Baada ya kutembea kidogo Suzana alimshuhudia yule mwanamke akikunja gauni lake usawa wa kifua na kushangaa kumuona akitembea ndani ya maji yaliyokuwa yamemfika tumboni. Suzana alijikuta akishtuka na kujiuliza yupo ndotoni au anaona kweli, kilichomshangaza ni umbali aliotoka yule mwanamke akitembea juu ya maji. Lakini cha kushangaza alipokaribia ufukweni alionekana yupo ndani ya maji yaliyomfikia tumboni. Aliendelea kumtazama amuone anakwenda wapi, yule mwanamke baada ya kutoka ndani ya maji alitembea juu ya mchanga kulifuata gari lake. Kila alivyopiga hatua Suzana alizidi kutishika, alijikuta akimshangaa na kutamani kuijua sura yake. SASA ENDELEA... Alituliza macho yake kwenye uso wa yule mwanamke aliyekuwa akiisogelea gari huku manukato makali yakizidi kujaa ndani ya gari. Kilichomshangaza zaidi umbile la yule mwanamke ambaye mwanzo alionekana kama mrefu tena mweupe lakini kila alivyomsogelea sura na umbile la yule mwanamke lilibadilika na kufanana naye kwa kila kitu. Suzana alishtuka na kufunga kioo haraka ili mtu yule ambaye yeye alimuona wa muujiza asiingie ndani ya gari. Yule mwanamke alisogea kwenye gari na kuligusa, ajabu baada ya kuligusa, alitoweka ghafla. Suzana akiwa anatetemeka alijaribu kuwasha gari kwa mara nyingine, ajabu ya Mungu gari liliwaka aliondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Alipofika nyumbani kulikuwa kumekwisha pambazuka, alikwenda kuoga haraka ili awahi kanisani kwani muda ulikuwa umekwenda sana. Baada ya kuoga alirudi ndani, lakini alishtushwa na harufu ya manukato ambayo aliyasikia muda mfupi darajani gari lake lilipozima na kuenea hadi ndani ya gari lake. Hakutaka kulifikiria sana lile kwa sababu muda ulikuwa umekwenda, alikwenda kwenye kabati kubadili nguo ili awahi kanisani. Baada ya kumaliza kubadili, alijikuta akiingiwa na uvivu na kwenda kukaa kwenye kitanda haukupita muda usingizi mzito ulimshika na kulala bila kujielewa, aliposhtuka usingizini alishtuka kuiona familia yake yote imesimama mbele yake. Alijiuliza kuna nini, alipojiangalia alijiona alikuwa amevaa nguo za kuendea kanisani. “Suzana upo sawa?” Mama yake alimuuliza huku akifuta machozi. “Mbona unaniuliza hivyo? Halafu mbona kama wote mlikuwa mnalia kuna nini mbona mnanitisha? “Suzana,” mama yake alimwita tena akiwa bado anamshangaa.. “Abee mama.” “Upo sawa?” Mama yake alimuuliza huku akimkagua mwanaye kwa kumshika kila kona ya mwili. “Nipo sawa mama, kwani vipi?” “Siamini kweli Mungu wa ajabu.” “Mama mbona sikuelewi nilitokewa na nini?” Suzana alizidi kushangaa. “Hebu nyanyuka kwanza.” Suzana alinyanyuka kitandani kuonesha yupo sawa, wote waliokuwa mule ndani walishukuru Mungu. “Kwani muda huu ni saa ngapi?” “Saa kumi na moja.” “Jamani ina maana sikwenda kanisani?” Suzana alizidi kujishangaa. “Kwani ilikuwaje?” Mdogo wake wa kike alimuuliza huku akionesha kumshangaa dada yake. “Hata najua, nashangaa kuwaona mpo mbele yangu mkitokwa na machozi kwani nilikuwa kwenye hali gani?” “Mmh, haielezeki.” “Mbona mnanitisha.” “Ulitaka kwenda kanisani misa ya ngapi?” “Ya kwanza, ooh, nimekumbuka nilihisi uchovu na kuja kujilaza kilichoendelea sikujua, kwani mama nini kimenitokea?” “Tumepigiwa simu na shoga yako kuwa upo katika hali isiyoeleweka, ndipo tulipozoana na wadogo zako kuja hapa. Tulipofika tumekukuta umepoteza fahamu hujitambui hata mapigo yako ya moyo yalionesha kusimama.” “Mungu wangu!” Suzana alishtuka sana. “Basi tulichanganyikiwa, lakini sikutaka kuamini kama kweli utakuwa umekufa, ndipo tulifanya maombi ambayo yamekufanya unyanyuke na kuonesha kama ulikuwa katika usingizi mzito. Hatuamini kama huna tatizo lolote.” “Ni ajabu kulala muda mrefu kiasi hicho sijawahi kutokewa na kitu kama hicho, lakini nipo sawa kama uchovu ni wa kawaida tu.” “Mmh, haya ni maajabu makubwa sana, kuna umuhimu wa kwenda kwanza hospitali kuichunguza afya yako.” Suzana hakutaka kubishana na familia yake, walimchukua na kumpeleka hospitali ya TMJ. Walipofika walimueleza daktari hali waliyomkutana nayo na baada ya maombi kuamka kama alikuwa usingizini. Alichukuliwa vipimo vyote ambayo havikuonesha ugonjwa wowote, waliruhusiwa kurudi nyumbani. Siku ile alichukuliwa kwenda kulala kwa wazazi wake, usiku kwake ulikuwa mrefu kuwaza yote aliyokutana nayo na hali iliyomtokea. Mpaka siku ya pili inaingia hali ya Suzana ilikuwa nzuri hakuonesha mabadiliko yoyote. Siku hiyo aliondokea kwa wazazi wake kwenda kazini, alipofika kazini alikuwa mtu mwenye mawazo mengi juu ya matukio yaliyomtokea toka alipokimbiwa na mpenzi wake kwenye ukumbi wa Club Bilicanas, matukio ya ajabu aliyoyaona baharini kwenye sherehe ya ajabu. Kingine hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki, na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani, akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi Sharifa aliingia. “Vipi shoga mbona leo sikusomi?” “Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.” “Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda club usiku.” “Yepi tena hayo shoga?” Suzana alimueleza yote aliyokutatana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa. “Haa! Shoga unayosema ni kweli?” “Kweli kabisa.” “Huyo mtu unasema umemuona wapi?” “Daraja la Salenda” “Mmh!” Sharifa aliguna. “Mbona unaguna?” “Mbona tukio linafanana kama langu.” Sharifa naye alikutana na tukio gani linalo fanana na Suzana?







    @@@@@@@@@@@@@@





    ILIPOISHIA; Kingine, hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki dunia na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani. Akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi, Sharifa aliingia. “Vipi shoga mbona leo sikusomi?” “Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.” “Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda klabu usiku.” “Yapi tena hayo shoga?” Suzana alimueleza yote aliyokutana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa. “Haa! Shoga unayosema ni kweli?” “Kweli kabisa.” “Huyo mtu unasema umemuona wapi?” “Daraja la Salenda” “Mmh!” Sharifa aliguna. “Mbona unaguna?” “Mbona tukio linafanana na kama langu.” SASA ENDELEA... “Lako?” “Eeeh.” “Tukio gani?” “Unajua kuna mtu nilimueleza akasema eti ni uongo na uzushi, si unakumbuka kuna tukio moja lilitamba katika vyombo vya habari?” “Tukio gani?” “Lile la msichana kuota manyoya baada ya kumpa msaada ombaomba kwenye Daraja la Salenda?” “Ndiyo.” “Mimi nilikuwa mmoja ya watu walio kataa katakata kuwa ni uzushi, Suzana mimi ni mbishi sana kukubaliana na jambo linaloonekana ni la kusadikika.” “Mh.” “Basi wiki iliyopita katika majira ya saa kumi na mbili jioni nikiwa narudi nyumbani, si unajua foleni za Dar. Toka pale Palm Beach magari yalikuwa yakienda taratibu sana, tulipofika katika Daraja la Salenda magari yalisimama. Niliendelea kusubiri huku nikisikiliza nyimbo za Injili. “Nje ya magari kulikuwa na ombaomba wachache, sikushughulika nao, niliendelea kusikiliza muziki nikisubiri foleni isogee. Nilishtushwa na dirisha kugongwa kwa nje, niliponyanyua macho nilimuona ombaomba wa kike akitaka msaada kwangu. “Huruma iliniigia, nilifungua dirisha kidogo na kumpa noti ya elfu moja, halafu nilifunga dirisha na kuendelea kusikiliza muziki. Nilishtushwa tena dirisha kugongwa, nilipoangalia nilimuona yule yule ombaomba wa kike. Nilijiuliza ana shida gani ya kugonga tena, safari hii nilijikuta nimefungua kioo mpaka chini na kumuuliza: “Una shida gani tena?” Yule ombaomba aliyekuwa ameinama na uso wake kuzibwa na nywele nyingi alinyanyua uso wake na kunitazama, alionesha kama kunishangaa. Nilijiuliza mbona amenishangaa huenda kanifananisha na mimi nilikaza macho kumwangalia. Kilichonishangaza zaidi ilikuwa sura yake iliyofanana sana na yangu kama pacha. Moyo ulinilipuka ajabu, kuna kitu nilikiona kikitoka kwenye macho yake na kupiga kwenye macho yangu na ghafla alitoweka.” “Weee!” Suzana alishtuka. “Ndiyo maana nikasema tukio kama langu japo tofauti yake ni ndogo sana. Baada ya foleni kuanza kutembea, niliondoa gari na kwenda moja kwa moja nyumbani. Amini Suzana tukio lile wala sikulitilia maanani kwa vile sikulielewa na pia sikuwa muumini wa mambo ya kishirikina.” “Mh!” “Basi shoga, siku ile nyumbani nilikutana kimwili na mume wangu. Kama kawaida mzunguko wa kwanza ulikwenda vizuri, ajabu wa pili hakuwa na nguvu. Kila alivyojitahidi nguvu zake za kiume ziligoma.” “Mmh!” Suzana aliguna na kujitengeneza vizuri kwenye kiti chake. “Tokea siku ile mpaka leo mume wangu hana nguvu za kiume.” “Usiniambie!” “Kweli kabisa.” “Sharifa unataka kuniambia ombaomba yule ndiye aliyesababisha yote hayo?” “Sasa napata picha kuwa sehemu ile kweli kuna kitu kinafanyika.” “Kwa hiyo unataka kusema ni kweli pale kuna jini kama watu wanavyoamini?” “Sina uhakika kama ni jini lakini kuna kitu kibaya.” “Kwa hiyo hata ya mwanamke kuota manyonya ni kweli?” “Inawezekana.” “Mmh! Kama ni kweli basi tuna hatari, kwani yule mwanamke alipatikana?” “Nilisikia alionekana ufukweni akiwa uchi na akili zake kama chizi.” “Unataka kuniambia ndiye aliyetutokea?” “Huenda.” “Basi kuna umuhimu wa kulifanyia kazi jambo hili.” “Ngoja tutafute ushauri wa watu wazima.” “Kwani mumeo ulimueleza uliyokutana nayo?” “Sikumueleza kwa kuamini hali ile imetokana na yeye kutoka nje ya ndoa.” “Una uhakika gani?” “Suzana, sasa naingiwa na imani hiyo kutokana na tukio lililokutokea wewe.” “Sharifa kabla ya kutafuta ufumbuzi mbadala kwa nini usikae chini na mumeo kutafuta sababu ya yeye kuwa vile?” “Suzana mume wangu namfahamu vizuri, hata kama anatembea nje haijawahi kutokea, ninaye mwaka wa kumi sasa.” “Mmh! Bado haijawa sababu, kwani yeye anasemaje?” “Kwa kweli nyumba yetu imeingia matatizo ya kulaumiana huku nikimlaumu mume wangu na yeye kusema haelewi sababu ile inatokana na nini.” “Mmekwenda hospitali?” “Suzana wazo hilo sikuwa nalo, akili yangu yote niliielekeza kwenye lawama.” “Sharifa hasira siku zote haijengi ulitakiwa kumsikiliza mwenzako.” Wakiwa tukiwa katikati ya mazungumzo Brighton mpenzi wa Suzana aliingia. Baada ya kusalimiana Sharifa aliwaaga na kuwaacha wapendanao wazungumze. Baada ya kuondoka Sharifa alimuangalia Brighton kwa jicho la hasira. “Vipi sweet, mbona unaniangalia hivyo?” “Brighton wewe wa kunifanya hivyo, nimepungukiwa nini mwilini mwangu kufikia hatua ya kunidhalilisha kiasi hicho,” Suzana alimlalamikia mpenzi wake. ILIPOISHIA;

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sikumueleza kwa kuamini hali ile imetokana na yeye kutoka nje ya ndoa.” “Una uhakika gani sababu ya mumeo kuwa hivyo ni kutokana tukio lile?” “Suzana sasa naingiwa na imani hiyo kutokana na tukio lililokutokea.” “Sharifa kabla ya kutafuta ufumbuzi mbadala kwa nini usikae chini na mumeo kutafuta sababu ya yeye kuwa vile?” “Suzana mume wangu namfahamu vizuri, hata kama anatembea nje haijawahi kutokea ninaye mwaka wa kumi sasa.” “Mmh! Bado haijawa sababu, kwani yeye anasemaje?” “Kwa kweli nyumba yetu imeingia matatizo ya kulaumiana huku nikimlaumu mume wangu na yeye kusema haelewi sababu ile inatokana na nini.” “Mmekwenda hospitali?” “Suzana wazo hilo sikuwa nalo, akili yangu yote niliielekeza kwenye lawama.” “Sharifa hasira siku zote haijengi ulitakiwa kumsikiliza mwenzako.” Wakiwa katikati ya mazungumzo Brighton mpenzi wa Suzana aliingia, baada ya kusalimiana Sharifa aliwaaga na kuwaacha wapendanao hao wazungumze. Baada ya kuondoka Sharifa alimuangalia Brighton kwa jicho la hasira. “Vipi Sweet mbona unaniangalia hivyo?” “Brighton wewe wa kunifanya hivyo, nimepungukiwa nini mwilini mwangu kufikia hatua ya kunidhalilisha kiasi hicho?” Suzana alimlalamikia mpenzi wake. SASA ENDELEA... “Suzana nimekufanya nini tena mpenzi wangu?” “Hujui...hujui eeh, juzi umenifanya nini Bilicanas?” “Sasa Suzana nani wa kulaumiwa kati yangu na wewe?” “Brighton unachukua mwanamke unaniacha club peke yangu, nilikulazimisha kuwa na wewe siku hiyo, si ni wewe ndiye uliyenipigia simu nije tujumuike wote kisha nikalale kwako. Kama ulijua una miadi na mwanamke mwingine kwa nini uliniita?” Suzana alijisahau kama yupo ofisini na kujikuta akitokwa na machozi ya uchungu. “Mimi?” “Kwani nazungumza na ukuta?” “Suzana juzi si nilikuacha unakunywa mimi nikapanda juu kuzungumza na Shakoor, nilipoteremka nilishangaa kukuta meza nyeupe na vinywaji vipo kama nilivyoviacha. Nilijua umekwenda msalani lakini muda ulipokwenda sana ilibidi nitoke nje kukutafuta. Kilichonishangaza sikukuta gari lako ilibidi nikodi teksi hadi nyumbani kwa kuamini umekwenda huko. “Kila nilipopiga simu yako iliita bila kupokelewa, nilipofika nyumbani kwangu sikukuta, nilisubiri kwa saa moja mpaka saa tisa na nusu. Baada ya kutokukuona niliamua kukufuata kwako, nilikuta mlango umefungwa. Nilipomuuliza mlinzi aliniambia hujarudi. “Hapo nilichanganyikiwa, nilijiuliza utakuwa wapi? Huwezi kuamini mpaka kunakucha nilikuwa sijapata jibu. Simu yako kila nilipopiga iliita bila kupokelewa, nilirudi nyumbani na kuamua kujilaza kidogo niende kanisani misa ya pili kutokana na uchovu wa kutopumzika. “Amini usiamini nimeamka saa tatu usiku toka saa moja asubuhi nilipoweka ubavu, toka nizaliwe na kuwa na akili zangu timamu sijawahi kutokewa na usingizi wa ajabu kama ule. Hata nilipoamka nilikuwa kamsa mlevi niliyekunywa pombe nyingi, sikunyanyuka kitandani niliendelea kulala, huwezi kuamini nililala bila kula kwa saa 24 na nilipoamka leo asubuhi nilikuwa na nguvu kama sijatokewa na kitu chochote. “Nilipitia kwako mlinzi alinieleza kama ulirudi, lakini kuna kitu kilitokea kilichoonesha kuna jambo limekupata na kuchukuliwa na familia yako. Mimi kiguu na njia mpaka kwenu, nilipofika niliambiwa umekuja kazini na afya yako ni salama. Kwani ulitokewa na nini?” “Yangenitokea bila wewe?” “Bila mimi kivipi Suzana?” “Eeh, kama ningekwenda kwako unafikiri ningekutana na mauzauza, Brighton uliondoka na mwanamke unajitetea tu,” Suzana alizidi kulakamika. “Suzana mpenzi wangu tuna muda gani juzi nifanye hivyo?” “Si umenichoka.” “Suzana naapa kwa jina la Yesu Kiristo uliniacha juu sikutoka na mwanamke muulize hata Shakoor kama nilitoka na mwanamke au muulize mlinzi wako nimefika kwako saa ngapi?” “Itanibidi nikubali kwa vile nakupenda.” “Suzana mpenzi wangu niamini siwezi kwenda kunyume na ahadi yetu, nakupenda na sitakusaliti hata siku moja.” “Basi yamekwisha lakini uliniumiza sana.” “Mh, eti ulipatwa na nini?” “Samahani Brighton toka niingie ofisini sijafanya kazi yoyote, naomba unipe muda baada ya kazi nikitoka hapa nikakuja kwako moja kwa moja tuzungumze, ni mazungungumzo marefu.” “Nigusie hata kidogo” “Ni kuhusu nilipotoka Bilicanas na mambo niliyokutata nayo njiani.” “Mambo gani?” “Nimekueleza nitakueleza au unataka nifukuzwe kazi?” “Basi mpenzi wangu nimekuelewa.” Waliagana Brighton na mpenzi wake Suzana na kumuacha akifanya kazi. Baada ya kuondoka Brighton, Suzana alijikuta akihamia kwenye maelezo ya Brighton juu ya hali iliyomtokea ya kulala zaidi ya saa kumi na nne. Alijiuliza kama yeye alikutana na maajabu yale, Brighton alikutana na kitu gani. Kazi kwake ilikuwa nzito siku ile, aliomba ruhusa na kurudi nyumbani kupumzika, kabla ya kutoka alimjulisha mpenzi wake kuwa anatangulia nyumbani kwake. Baada ya kutoka kazini alikwenda moja kwa moja nyumbani kwa mpenzi wake, kwa vile alikuwa na funguo za nyumba alifungua na kuingia ndani. Alipoingia alishangaa kukuta chumbani kumesafishwa tofauti na siku zote, mara nyingi usafi wa nyumba ile alikuwa akifanya yeye. Ile haikumsumbua akili yake aliamini kutokana na msongo wa mawazo hali ya usafi ya nyumba ingemfanya asisumbue mwili wake zaidi ya kwenda moja kwa moja chumbani kujilaza. Hali ya hewa ndani ilikuwa nzuri tofauti na siku zote huku harufu ya manukato aliyowahi kuyasikia alipokutana na maajabu ya dalaja la Salenda. Upepo mwanana uliompuliza ulimfanya apitiwe na usingizi bila kujijua, katikati ya usingizi alishtushwa na Brighton akimpapasa. “Aah, mpenzi umerudi zamani?” “Kama robo saa.” Kwa vile Brighton alikuwa amekwishaoga Suzana naye alikwenda kuoga na kujumuika wote kitandani. Kama kawaida walisafiri katika meli ya wapendanao, safari ya kwanza ilianza vizuri kila mmoja aliifurahia. Baada ya safari ya kwanza kwisha Suzana hamu ilikuwa bado haijamuisha alitaka asafiri safari moja zaidi ndipo wapumzike. Ajabu kila alipomgusa mwenzake jogoo alikataa kuwika kitu kilichomshtua Suzana. “Vipi mpenzi mbona hivi?” “Hata mimi nashangaa.” Nini kimempata Brighton? Au ndiyo yaliyompata mume wa Sharifa?





    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    @@@@@@@@@@@@



    ILIPOISHIA: Kwa vile Brighton alikuwa amekwishaoga, Suzana naye alikwenda kuoga na kujumuika wote kitandani. Kama kawaida walisafiri katika meli ya wapendanao, safari ya kwanza ilianza vizuri kila mmoja alifurahia safari ile. Baada ya safari ya kwanza kwisha, Suzana hamu ilikuwa bado haijamuisha, alitaka asafiri safari moja zaidi ndipo wapumzike. Ajabu kila alipomgusa mwenzake, jogoo alikataa kuwika kitu kilichomshtua Suzana. “Vipi mpenzi mbona hivi?” “Hata mimi nashangaa.” SASA ENDELEA... “Au umeanzia kwa mwingine?” “Lakini kwa nini kila linapotokea tatizo unanifikiria vibaya kuwa nilikuwa na wanawake? Siku hizi sina kazi, kazi yangu kutembea na wanawake,” Brighton alilalamika. “Mbona leo imekuwa hivi?” “Hata mimi nashangaa.” Suzana alijitahidi kumkanda mpenzi wake kumrudisha kwenye hali ya kawaida lakini hakukuwa na mabadiliko, jogoo alikataa kuwika. Aliamua kumwacha ajipumzishe waendelee baadaye. Alijilaza pembeni ya Brighton aliyeonekana mwingi wa mawazo. Suzana akiwa amejilaza alikuwa na yake aliyokuwa akiwaza, ghafla mazungumzo yake na Sharifa yalijaa kichwani na kuyakumbuka maneno aliyoelezwa juu ya tatizo la mume wake. “Basi shoga, siku ile niliporudi nyumbani nilikutana kimwili na mume wangu kama kawaida mzunguko wa kwanza ulikwenda vizuri, ajabu wa pili hakuwa na nguvu kila alivyojitahidi, nguvu za kiume ziligoma.” Sauti ile ilijirudia kichwani mwake na kumfanya atishike na kuamini huenda tatizo la Sharifa limempata na yeye. Bila kujielewa, alijikuta akikaa kitako na kumshtua Brighton aliyekuwa katika dimbwi la mawazo. “Brighton,” alimwita kwa sauti ya juu japo alikuwa pembeni yake. “Unasemaje?” “Hali hii imekutokea mara ngapi?” “Suzana swali gani hilo, toka niwe na wewe hali hii imeshanitokea?” “Hapana, basi utakuwa na tatizo la muda mrefu.” “Lakini siamini huenda ni uchovu ngoja nipumzike kidogo tutaendelea,” Brighton alimtoa hofu Suzana. “Mmh! Sawa,” Suzana aliguna akiwa na wasiwasi na maneno aliyoelezwa na Sharifa ya mpenziwe kuwa amekufa nguvu za kiume. Kila mmoja alilala upande wake, mchana waliamka na kwenda kupata chakula cha mchana. Wakiwa wamekaa wanakula, Brighton akamsifia Suzana kwa usafi aliofanya na kuifanya nyumba ipendeze. “Mpenzi umetumia muda gani kufanya usafi ule?” “Usafi gani?” “Wa nyumba,” kauli ile ilimshtua Suzana na kuamini kabisa tayari nyumba yao imeingia kwenye tatizo lakini hakutaka kulikubali mara moja ili kuficha kila anachokiwaza, alijikuta akikubali pongezi zisizo zake. Baada ya kupata chakula walirudi nyumbani kupumzika, kwa vile kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake baada ya kuoga walipanda kitandani kujiachia kwa raha zao. Lakini hali ilikuwa mbaya zaidi Brighton hakuwa na nguvu za kiume. Hali ile ilizidi kumweka Suzana kwenye hali mbaya, hakukubaliana nayo, aliendelea kumsaidia mpenzi wake lakini hali ilikuwa ile ile. Suzana alijikuta akiangua kilio kitu kilichomshtua Brighton na kuhoji: “Suzana mbona unalia?” “Brighton unajiona upo sawa?” “Sijajua nikujibu nini?” “Hujioni haupo sawa?” “Hali ya leo inanishangaza hata mimi si kawaida yangu.” “Inawezekana kuwa ndiyo yenyewe,” Suzana aliropoka. “Yenyewe nini?” “We acha tu, kesho nitakwenda kumweleza Sharifa.” “Kumweleza nini?” Brighton alizidi kuyashangaa maneno ya mpenzi wake. “Naomba leo tuachane na hilo.” “Kwani umegundua nini kuhusu tatizo langu?” “Brighton sijagundua lolote.” “Mbona unasema utanijibu kesho?” “Sijajua nini tatizo, linafanana na la Sharifa.” “Sharifa ana tatizo gani?” “Brighton tutazungumza kesho, naomba niondoke.” “Si ulisema utalala?” “Kwa hali hii siwezi kulala niache tu niwahi nyumbani.” Brighton hakuwa na la kusema zaidi ya kumruhusu Suzana akalale kwao. Suzana akionekana amechanganyikiwa, aliwasha gari na kurejea kwake. Alijikuta akilia njia nzima juu ya hali ya mpenzi wake huku akijiuliza kama itakuwa hivyo mpenzi wake amekufa nguvu za kiume atafanya nini? Alipoingia ndani kwake alijitupa kitandani hata usingizi ulivyomchukua hakujua. Suzana alishtuka siku ya pili, alijiandaa kwenda kazini huku akiwa na shauku ya kuonana na Sharifa kumwelezea yaliyomsibu kama yake. Alipofika kazini kiti alikiona cha moto, hakukaa, alikwenda moja kwa moja ofisini kwa Sharifa. Sharifa alipomuona alishtuka na kumkaribisha: “Mmh! Dada mbona asubuhi asubuhi?” “Wee acha tu, ukiona hivyo ujue kuna jambo.” “Karibu, mi ndo naingia sasa hivi hata vumbi sijafuta kwenye kompyuta.” “Yaani wee acha tu,” Suzana alisema huku akiketi kwenye kiti. “Mh, kuna kipi kipya?” “Kuna mapya! Yale yaliyokutokea yamefika na kwangu.” “Yapi hayo tena?” “Si yaliyomtokea mume wako.” “Unamaanisha jogoo kushindwa kuwika?” “Ndiyo.” “Ehe!” Suzana alimwelezea Sharifa yaliyomkuta, baada ya kumsikiliza alishusha pumzi na kusema: “Unajua unaweza kuona nakutania .” “Kwa kipi?” “Jana usiku nilipokutana na mume wangu huwezi kuamini, nimefurahia tendo kama kawaida.” “Wewee! Mara zote?” “Tena ajabu lilikuwa penzi tamu ajabu hata asubuhi nimeamka nilihisi kama siku ya kwanza kuonana na mume wangu.” ILIPOISHIA; Suzana alimuelezea Sharifa yaliyomkuta, baada ya kumsikiliza alishusha pumzi na kusema: “Unajua unaweza kuona nakutania!” “Kwa kipi?” “Jana usiku nilipokutana na mpenzi wangu huwezi kuamini nimefurahia tendo kama

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kawaida.” “Wewee! Mara zote?” “Tena ajabu lilikuwa penzi tamu ajabu hata asubuhi nimeamka nilihisi kama siku ya kwanza kuonana na mume wangu.” “Usiniambie,” Suzana alishika mkono kwa mshtuko. SASA ENDELEA... “Hata nashindwa kuelewa hali ya jana inatokana na nini?”?”Au alikwenda hospitali?” “Walaa, hata yeye anashangaa.” “Sasa kwangu imetokana na nini?” “Hapo ndipo nashindwa kujua hali hii inatokana na nini.” “Yaani nashindwa kuelewa na kubakia njia panda, niliamini lililonitokea jana ndilo lililokutokea wewe wiki moja iliyopita. Leo imekuwa tofauti kabisa uliponieleza hali imebadilika.” “Suzana hebu nawe angalia kwa wiki tuone mabadiliko, huenda vyakula tunayokula vimesababisha upungufu wa nguvu za kiume.” “Lakini Sharifa upungufu gani hata kunyanyuka kidogo.” “Suzana hata kwangu ilikuwa hivyo hivyo, jana sikuamini, tena mume wangu ndiye aliyeniamsha usingizini.” “Basi inawezekana tatizo hili limeingia, kwani hujawahi kusikia mwingine zaidi yetu mwenye tatizo kama hili?”?”Mmh! Sijawahi.” “Kama lako limekwisha huenda langu bado nalo litakwisha.” “Ondoa wasiwasi nina imani litakwisha.” “Mmh! Sawa.” Suzana alimuaga Sharifa na kurudi ofisini kwake, alipofika alijikuta akicheka peke yake na kuamini huenda tatizo lile huondoka bila dawa. Siku hiyo Suzana alishinda akiwa bado yupo njia panda, baada ya kuamini alichokiona Daraja la Salenda ndicho kilichosababisha hali ile. Lakini ilikuwa tofauti baada ya kukutana na Sharifa na kumueleza kuwa hali ya mumewe kukosa nguvu za kiume imekwisha. Pamoja na kusikia nguvu za mume wa Sharifa zimerudi katika hali yake bado alikuwa na maswali juu ya hali ile kuwatokea wanaume wawili tofauti ilitokana na nini? Suzana naye alijipa moyo kuwepo na mabadiliko kwa mpenzi wake, lakini walipokutana zaidi ya mara tatu hakukuwa na mabadiliko yoyote. Bado alijipa moyo kwa vile wiki ilikuwa bado haijakatika. Akiwa ofisini kwake akiendelea na kazi alimuona Sharifa akiingia kwa mwendo wa kujivuta. Alipomuona alishtuka na kumuuliza: “Vipi shoga mbona hivyo?” “Wee acha tu, hata sijui hili ni balaa gani?” “Kwa nini? Hebu kaa kwanza.” Baada ya kuketi Sharifa alishusha pumzi huku akiuma meno kuonesha kuna kitu kilimuuma sana. “Vipi shoga kulikoni?” “Mmh! Hata nashindwa nianzie wapi.” “Kivipi tena Sharifa mbona unanitisha.” “Hebu ngoja,” alisema huku akijiweka vizuri kwenye kiti. Suzana alimuangalia Sharifa kwa huruma alivyokuwa akiugulia maumivu. “Jamani Sharifa si uende hospitali?” “Hata sielewi ugonjwa huu ni wa hospitali au vipi.” “Kwa nini?” “Hadithi bado inaendelea?” “Hadithi gani tena Sharifa?” “Si ile niliyokueleza.” “Ya?” “Kuhusu mume wangu na matatizo yake.” “He! Yamerudi tena?” “Tena sasa hivi hata kuielezea siwezi.” “Sharifa mbona unanitisha au bado ni yale yale ya Daraja la Salenda?” “Inaweza kuwa hivyo.” “Mmh! Ehe, kwa hiyo tatizo limejirudia?” “Hapana, ila limezuka lingine.” “Lipi hilo?” “Basi shoga siku ile baada ya kukueleza raha nilizipata kwa mume wangu usiku wake vilitokea vitu vya ajabu. Nilipokutana na mume wangu nilishangaa kuhisi maumivu makali kama vile maumbile yake yameongezeka hata kuingia ilikuwa shida.” “Weweee!” “Basi shoga wacha nipige kelele za maumivu ambazo zilimshtua mume wangu na kuniuliza hali ile imeanza lini la kuyaona maumbile yake yananiumiza. Nilivumilia lakini sikuona raha yoyote zaidi ya maumivu. Mpaka tunamaliza sikuwa na hamu tena sehemu za siri zilikuwa zikiniuma sana. “Siku ya pili sikuwa tayari kuendelea kuumizwa, lakini mume wangu alikuwa akinishangaa na kusema mbona yupo kawaida. Siku ile tulifanya gizani, lakini jana tuliwasha taa na kuyaona ya kawaida. Hata tulipokuwa kwenye zoezi sikuhisi maumivu yoyote. “Baada ya kufanya mapenzi na mume wangu kila mmoja aligeuka upande wake kulala, katikati ya usingizi niliota kuna mtu kaingiza mkono sehemu zangu za siri na kuanza kukoroga, kitu kile kilifanya nihisi maumivu makali sana chini ya tumboni. Niliposhtuka usingizini nilishtuka kumuona mume wangu akiwa juu yangu, kutokana na maumivu niliyokuwa nikisikia nilimsukuma kwa miguu. Baada ya kumsukuma tumbo lilinikata kwa muda kisha lilitulia.” “Jamani kama angekuwa na shida na wewe kwa nini usikuambie kuliko kukuingilia bila taarifa?” Suzana alichangia. “Hata mimi nashangaa mume wangu toka anioe hajawahi kufanya vile.” “Wewee!’” Suzana alishtuka kusikia vile. “Hebu ona ajabu nyingine baada ya kumsukuma mume wangu na miguu na kuanguka upande wa pili, aliendelea na usingizi mzito na asubuhi nilipomuuliza alishangaa huku akiapa kwa miungu yote hakuniingilia usiku.” “Weweee!” “Yaani nilimueleza yote lakini alibisha na kusema labda nilikuwa naota. Nilimueleza kuwa alikuwa juu yangu na hali niliyosikia, bado alikataa. Basi shoga yangu tokea hapo nilishangaa kuiona damu yangu ya hedhi, ilikuwa ajabu kuingia hedhi mara mbili kwa mwezi. Hata kutembea sitakiwi kuharakisha, nikiharakisha chini ya kitovu pananivuta sana.” “Sharifa unajua tunafanya uzembe, tukija shituka tumekwisha umia.” “Na kweli hili jambo siwezi kuliacha lipite hivi hivi, sasa hivi mapenzi nayaogopa kwani yamekuwa mateso.” “Si ulinieleza kuna mtu unayemfahamu tulifanyie kazi, nipo tayari kukusaidia Mpaka hatua ya mwisho.” “Nimekuelewa acha nikapumzike, kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute nyumbani.” Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka shoga yake Suzana alizidi kuchanganyikiwa. Alijiuliza ni kitu gani tena kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amuelezee matatizo ya mpenzi wake.





    @@@@@@@@@@@

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ILIPOISHIA; “Nimekuelewa, acha nikapumzike nyumbani kwani kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute.” Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka, Suzana alizidi kuchanganyikiwa juu ya hali ya shoga yake. Alijiuliza ni kitu gani kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amwelezee matatizo ya mpenzi wake. SASA ENDELEA... Sharifa akiwa na maumivu makali ya chini ya tumbo, alitembea taratibu kurudi nyumbani. Suzana alipata wazo la kumsindikiza shoga yake ambaye aliamini kabisa alihitaji msaada wake. Alitoka haraka nje na kumkuta akimtafuta dereva wa kampuni ampeleke nyumbani. “Sharifa acha nikupeleke mimi.” “Suzana endelea na kazi, acha tu nitafika.” “Haiwezekani, lazima nikusindikize.” “Mmh! Sawa.” Suzana alikimbilia kwenye gari lake na kuligeuza haraka kisha akasimamisha pembeni ya Sharifa na kumfungulia mlango. Sharifa aliingia na kufunga mlango. Alimpeleka kwake kupitia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Ajabu walipokaribia Daraja la Salenda, Suzana alipunguza mwendo na kumfanya Sharifa aliyekuwa amejilaza kukaa kitako. Wote walijikuta wakitupia macho maeneo ya baharini labda wataona kitu chochote lakini hawakuona kitu walichokikusudia zaidi ya kuwaona watu wakitembea juu ya mchanga baada ya bahari kupwa. Baada ya kila mmoja kuwa na uhakika hakuna kitu, Suzana aligeuza uso wake na kubadili gia ili waendelee na safari yao. Sharifa alikuwa wa kwanza kushtuka na kupaza sauti yake... “Suzana umemuona yule mwanamke pale pembeni ya barabara?” Suzana aligeuza shingo tena kuangalia sehemu aliyooneshwa na rafiki yake, kweli alimuona mwanamke mmoja mrefu aliyekuwa amevalia gauni la rangi nyekundu na mtandio wake mwepesi ulioziacha nywele zake nje. Ajabu wakati huo gari lao lilizimika ghafla. “Suzana vipi, mbona hivyo?” “Hata mimi nashangaa gari limezimika ghafla.” “Makubwa, sasa yule dada ni nani?” “Hata najua, muone jinsi alivyo mzuri, tena anatuchekea labda anatujua.” “Mmh! Lakini mbona sielewi, nausikia mwili wote ukinisisimka.” “Siyo wewe tu, hata mimi nasikia nywele zikinisisimka.” “Mmh! Inawezekana mtu yule si mzuri?” “Na kweli Suzana, hebu yaone macho yake! Mbona siyaelewi... Mungu wangu! Ona miale inatoka machoni kwake, Suzana washa gari tuondoke.” Suzana alijaribu kuwasha gari lake lakini liligoma kuwaka, walijikuta wakizidi kupagawa na kutamani kupiga kelele. Sharifa alishtuka kuona mabadiliko kwa yule mwanamke aliyekuwa bado amesimama sehemu ile ile chini ya mti. “Suzana haya ni maajabu!” “Ya nini?” “Muone yule mwanamke, si alikuwa amevaa gauni jekundu na mtandio?” Suzana alinyanyua uso kumuangalia yule mwanamke na kumuona akiwa na gauni lingine la rangi pinki lililokuwa limempendeza zaidi ya mwanzo, nywele zake zikiwa zimetengenezwa vizuri na kuongeza urembo wake. “Mmh! Kweli! Kama sikosei alikuwa na gauni jekundu.” “Unajua yule si kiumbe wa kawaida, huenda ni jini.” “Jini?” Kauli ile ilifanya wasikie msonyo mkali ambao ulifanya tumbo la Sharifa livurugike ghafla, baada ya muda lilitulia na kurudi katika hali ya kawaida. Yule mwanamke waliyekuwa wanamshangaa aliwapungia mkono kama anawafahamu, wakajikuta wote wakimpungia mkono, aligeuka na kuondoka kuelekea baharini. Walijikuta wakimsindikiza kwa macho yule mwanamke aliyeanza kuelekea katikati ya bahari na kupotea machoni mwao. “Mmh! Suzana hii nini?” “Hata sijui.” “Sasa yule atakuwa nani?” “Yaani nazidi kuchanganyikiwa, ulisikia ule msonyo?” “Nisiusikie vipi wakati umelifanya tumbo langu lingurume na kutulia.” Ajabu nyingine, Suzana alipojaribu kuwasha gari liliwaka, wakaamua kuendelea na safari yao huku kila mmoja akijiuliza yule mwanamke mzuri aliyevalia gauni lenye mshono mzuri ambao hawakuwahi kuuona. “Jamani haya ni maajabu, sasa yule mwanamke ni jini?” “Lakini jini gani anavaa nguo nzuri kama zile tena za gharama?” “Mmh! Makubwa, hata sielewi eneo hili lina nini. Kuna umuhimu wa kuulizia zaidi kwa watu ili tupate ufumbuzi.” Suzana aliendesha gari mpaka nyumbani kwa Sharifa, bahati nzuri walimkuta mama yake ameshafika nyumbani kwake. Hali ya Sharifa ilikuwa tofauti na muda mfupi uliopita akiwa ofisini. Alishangaa kujiona akiwa mzima kabisa, wala hakutembea kwa kupinda mgongo kwa maumivu ya tumbo tena. Hali ile ilimshangaza hata Suzana kumuona shoga yake yupo katika hali nzuri. “Sharifa vipi maumivu yamekwisha?” “Huwezi kuamini sasa hivi sijambo kabisa, siumwi chochote mwilini.” “Mmh! Mbona mwaka huu wa maajabu, kila dakika kinazuka kitu kipya machoni mwangu.” “Shoga karibu ndani umsalimie mama uwahi kazini.” Suzana aliingia ndani kwa Sharifa kumsalimia mama yake. Alipoingia nusura akimbie kwa mshtuko, aliyeambiwa ni mama yake Sharifa alikuwa ni yule mwanamke mrembo waliyemuona maeneo ya Daraja la Salenda. “Karibu mwanangu.” “A..a..sante.” Alishangaa kumuona akitabasamu lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake. “Sharifa huyu ndiye mama yangu.” Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amtambulishe kuwa ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa, muda ule alivaa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi. Suzana aliaga na kutaka kuondoka baada ya kushindwa kumuelewa mama. Ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kuelewa alichokiona mbele yake. Kila dakika imekuwa ikimshangaza Suzana, ni kweli aliyemuona mbele yake ni yule waliyemuona baharini na aligeuka na kuwa mtu mwingine?ILIPOISHIA; Alishangaa kumuona akitabasamu, lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake. “Sharifa huyu ndiye mama yangu.” Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amfahamishe ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa muda ule lilikuwa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kumuelewa mama, lakini ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana alishindwa kuelewa alichokiona mbele yake. SASA ENDELEA... Akiwa njiani alijiuliza maswali yasiyo na majibu juu ya mambo aliyokutana nayo ya kumuona mwanamke

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mzuri aliyebadilika nguo, pia kutambulishwa tena kuwa ndiye mama yake Sharifa. Alijikuta akijiuliza Sharifa huenda naye ni jini lakini wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Sharifa, mtu aliyemfahamu muda mrefu hakuonesha kitu chochote cha kumfanya amdhanie kuwa si mtu wa kawaida. Alijiuliza ilikuwaje amuone akifanana na mwanamke waliyemuona pembeni mwa Barabara ya Ali Hasani Mwinyi karibu na Daraja la Salenda na baadaye kumuona mtu tofauti. Aliamua kurudi ofisini kuendelea na kazi. ****** Jioni akiwa nyumbani alipigiwa simu na Sharifa, aliipokea na kuzungumza. “Vipi shoga za muda?’ “Nzuri tu, vipi unaendeleaje?” “Huwezi kuamini sijambo kabisa kama siyo mimi niliyekuja ofisini nikitembea kwa shida, kingine kilichonishangaza ni kukatika ghafla kwa damu yangu ya hedhi.” “Wewee!” “Yaani Suzy siamini kila dakika kwangu ni miujiza.” “Mmh! Makubwa.” “Halafu Suzy eti kuna kitu gani kisicho cha kawaida ulikiona tulipofika nyumbani?” “Kitu gani?” “Kisicho cha kawaida ambacho kilikutisha,” swali lile lilimshtua Suzy na kujiuliza kwa nini ameulizwa. “Kwa nini umeniuliza swali hilo?” “We nijibu kuna kitu nataka kukuambia.” “Ni kweli, we umejuaje?” “Hivi nd’o nimeingia toka kwa mtaalamu mama alinipeleka.” “He ! Amesemaje?” “Mmh! Shoga mazito si ya kuyazungumza kwenye simu.” “Kwa hiyo?” “Kama unaweza kuja nyumbani njoo, maana hapa nilipo niliyoelekezwa yamenichosha.” “Mmh! Lazima nije?” “Basi shoga njoo usikie mambo ya dunia.” Taarifa zile zilimfanya Suzana ajiandae haraka haraka na kuingia ndani ya gari lake, tayari kwenda kwa Sharifa akiwa na shauku ya kutaka kujua kitu gani kilichomfanya aseme vile. Alimkuta Sharifa akimsubiri kwa hamu. “Karibu shoga yangu.” “Asante.” “Naona ndiyo unatoka kuoga?’ “Wee acha mwili ulikuwa umechoka kila kona, karibu.” “Asante,” Suzana alijibu huku akikaa kwenye kochi. “Mh! Shoga lete habari,” Suzana alianzisha mazungumzo. “Basi shoga baada ya kuondoka nilibakia na mama na kumueleza yote yaliyonitokea hata tukio la kuonana na yule mwanamke leo.” “Ehe.” “Mama alinieleza lazima yule atakuwa jini.” “Ehe.” “Basi alinichukua na kunipeleka kwa mzee mmoja mtaalam wa majini, tulipofika tulikaribishwa kwenye chumba kilichokuwa na mkeka na nyuma yake kulikuwa shuka nyekundu, pia kulikuwa na picha za kuchora za simba na viumbe visivyoeleweka.” “Mmh.” “Basi mganga huyo kijana akachukua kioo kidogo na kunitaka niweke mkono juu yake na kuniuliza matatizo yangu. Baada ya muda akatanitaka nitoe mkono na kunitaka nikitazame kile kioo kwa muda kisha alishusha pumzi. “Huwezi kuamini wakati akikitazama kile kioo jasho lilianza kumvuja yule mganga kama kamwagiwa maji, kitu kilichonishtua sana. Baada ya kushusha pumzi alichukua kitambaa na kukifuta na kutuuliza.” “Mnataka mtatuliwe matatizo yenu au unataka kujua sababu ya yote yaliyotokea?” “Wewe utakavyoona inafaa,” Mama alijibu. “Mama si huwa nasikia eti waganga wanajua kila kitu kilichotokea kabla ya kutibu?” Niliuliza. “Ni kweli tunajua na yote nimeyaona hapa,” mganga alinijibu. “Sasa si ungeniambia ili nijue natibiwa kitu gani?” “Hakuna tatizo, kwa hiyo upo tayari kuyasikia yaliyokusibu?” “Nipo tayari,” nilimjibu. “Haya vizuri,” Baada ya kusema vile alichukua unga na kuumwaga mbele yake huku akisema maneno kwa sauti ya chini. Baada ya kusema vile alikichukua kioo na kuangalia tena kwa muda wa kama dakika kumi kisha alitugeukia na kusema: “Kama nitakuwa nasema uongo naomba ukatae, sitaki nionekane nazungumza tofautina ukweli.” “Sawa.” “Unaitwa Sharifa, sawa?” “Ndiyo” “Umeolewa?” “Ndiyo.” “Ndani ya wiki tatu kumetokea matatizo ndani ya ndoa yako?’ “Ndiyo.” “Wasiwasi wako ni tukio lililokutokea katika Daraja la Salenda?” “Kweli.” “Basi ni kweli tatizo lako lilitokana na tukio la darajani ambalo lilipelekea kukuingizia mgogoro ndani ya ndoa yako. Yule uliyekutana naye ni Jini Balikis, kazi yake kubwa ni kuvuruga ndoa za watu. Si wewe tu kuna watu wengi wamekumbwa na mgogoro huu hata kufikia hatua ya kuachana. “Hata rafiki yako kipenzi ana tatizo hilo, tena yule ndiye chaguo la Jini Balkis kwa vile ni mwanadamu pekee aliyeshuhudia sherehe ya kuagwa kwake kuja duniani. “ Tuachane na hayo ya shoga yako najua naye ana yake, ila tatizo la mumeo kukosa nguvu za kiume linatokana na kufanya mapenzi na Jini Balkis. “Kila mnapofanya mapenzi, jini huyo hufika katika eneo la tukio hilo na kuziondoa nguvu za mumeo ili asiweze kukuridhisha vyema. “Anafanya hivyo makusudi ili aweze kufanya naye mapenzi yeye wakati wa usiku mkiwa mmelala. “Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri kiasi cha kufikia kukuona wewe hufai tena kwake.” Huu ni mwanzo wa siri ya Jini la Daraja la Salenda. Nini kiliendelea?





    @@@@@@@@@@@@@@@@@



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ILIPOISHIA: Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri usingizini hadi kufikia hatua ya kukuona hufai tena kwake.” SASA ENDELEA... Kauli ile kwa kweli ilinishtua sana, basi mganga akaendelea kuchimbua mambo na kusema: “Baada ya kufanya vile kitu kile kilikutia wasiwasi kiasi cha kufikiria kutafuta ufumbuzi baada ya kupata tatizo kama hilo kumtokea shoga yako. Kumbuka mwanzo uliamini kabisa tatizo lile linatokana na mwenzako kutokuwa mwaminifu ndani ya ndoa yako kweli?” “Kweli.” “Baada ya kupanga mipango ya kutafuta ufumbuzi wa mumeo kupoteza nguvu za kiume na shoga’ako kukutwa kama mtu aliyekufa, pale shoga’ako kama wangechelewa alikuwa anabadilishwa kwa kuchukuliwa maiti yake ambayo ingepelekwa chini ya bahari na yeye Jini kukaa na mchumba wake.” Kauli ile ilimshutua sana Suzana na kujikuta akishika mdomo kwa mshtuko. “Mungu wangu, ina maana pale nilikuwa nakufa?” Suzana alimuuliza Sharifa. “Shoga hebu tulia kwanza unisikilize utaniuliza maswali mwisho japo nina imani maelezo nitakayokupa hutahitaji kuniuliza swali.” “Mmh! Inatisha sana, haya endelea.” Basi mganga akaendelea kunieleza: “Kilichomrudisha shoga yako duniani ni maombi yaliyofanywa na familia yake bila hivyo maisha yake yote yangekuwa chini ya bahari na jini yule kuishi na mpenzi wake kwa kuwa shida yake ilikuwa kusambaratisha ndoa za wanadamu au uhusiano wa watu waliopendana. Baada ya shoga yako kurudi katika hali yake ya kawaida na wewe mumeo akapoteza nguvu za kiume. “Mlipokutana na kuhadithiana juu ya kilichotokea Daraja la Salenda na matukio yaliyowatokea. Alihamia kwa shoga yako kumtoa nguvu za kiume mpenzi wake. Mwanzo shoga yako hakuwa na imani kuwa kuna vitu kama hivyo vinatokea, vilipomtokea kama ulivyomuhadithia mumeo kutokewa na hali ile, hapo ndipo akaamini kabisa ni kweli tatizo lipo katika Daraja la Salenda. “Jini Balkis aliwachezea akili kwa kumrudishia mumeo nguvu za kiume ili taarifa za shoga zako zipingane na ukweli ambao ungepata picha ya tukio la Daraja la Salenda. Kumbuka usiku wa siku ile ulipokutana kimwili na mumeo kulikuwa na tofauti kubwa na siku zote tangu muoane, kweli au uongo?” Mganga aliniuliza. “Kweli,” nilijibu huku nikiona aibu kutamka maneno yale mbele ya mama. “Unajua ni kwa nini?” Aliniuliza. “Hata sijui.” “Majini wanapotaka kufanya mapenzi na wanadamu huwapaka mafuta sehemu za siri ili asipungukiwe nguvu za kiume ili waweze kumpa raha kwa muda mrefu. Hawapendi kukatishwa raha, huchukia sana. Mwanzo walikuwa wakifanya mapenzi na wanadamu bila kutumia kitu chochote. “Lakini tatizo la nguvu za kiume ndilo lililowakasirisha na kutafuta njia ya kustarehe na mwanadamu kwa muda mrefu. Njia ilikuwa ni kutafuta dawa ya kumwezesha mwanaume awe na nguvu muda wote wa kufanya mapenzi chombo kisilale, nina imani umenielewa kusema chombo?” Mganga aliniuliza. “Ndiyo nakuelewa endelea mzee wangu,” nilimjibu huku nikihisi mwili ukinisisimka kwa yale niliyoyasikia. Basi mzee akaendelea huku akiangalia kioo kama anasoma kitu. “Basi baada ya kujua kesho yake shoga yako naye yamemtokea kama yako na kuamini kabisa mtaamini kilichotokea kinatokana na tukio la Darajani Salenda. Usiku mkiwa mmelala, Jini Balkis alikuja na kumpaka mafuta yale mumeo sehemu za siri ambayo yalizifanya sehemu zake zinyanyuke. Mumeo alikuamsha usingizini kutaka haki yake, kweli au si kweli?” Mganga aliniuliza. “Kweli,” nilimjibu kwa aibu mbele ya mama aliyekuwa ametulia akisikiliza kwa makini. “Najua hukuamini kuikuta hali yake tofauti na siku zilizopita za kukosa nguvu za kiume, ulishtuka, hukushtuka?” “Nilishtuka.” “Hata ulipokubali kufanya naye mapenzi bado hukumuamini, ulijua ni yale yale ya siku zote, lakini ilikuwa tofauti na siku zote. Pia kulikuwa na tofauti kubwa siku za nyuma ulipofanya mapenzi kwa muda mrefu ulikuwa unachoka sana lakini siku ile ilikuwa tofauti, kweli au si kweli?” “Kweli.” “Usijibu kwa kuniogopa, nijibu kwa uhakika siyo ukubali hata la uongo.” “La uongo nitakuambia lakini yote unayosema ni kweli.” “Najua asubuhi ulipoamka ulijishangaa kuwa na nguvu za ajabu huku ukikumbuka penzi tamu la mumeo ambalo hakuwahi kukupa tangu akuoe.” “Ni kweli.” “Ni kwa nini hukuchoka kama siku zote?” “Hata sijui, nilifikiri labda kutokana na kukaa muda mrefu bila kukutana na mume wangu.” “Unataka kuniambia kipindi hiki ndicho kirefu kuchelewa kukutana na mumeo?” “Hapana.” “Unajua sababu ya kufurahia penzi la siku hiyo na asubuhi kuamka na nguvu za ajabu hata kazi siku hiyo ulifanya ukiwa na furaha tele moyoni?” “Hata sijui.” “Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi. Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi ya nguvu kila siku.” “Mmh! Kumbe.” “Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea wewe siku za nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shoga yako alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini. “Baada ya Jini Balkis kuwachanganya, wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumuhakikishia tatizo lake linaweza kwisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi Jini Balkis kufanya mapenzi na mpenzi wake usingizini hadi kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye. Siri ya Jini Balkis imewekwa hadharani, je, ufumbuzi utapatikana au ndiyo kumwagia mafuta kwenye moto? ILIPOISHIA; “Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi. Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi kila siku bila kuchoka.” “Mmh! Kumbe.” “Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea siku za

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shogayo alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake, lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini. “Baada ya jini Balkis kuwachanganya wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumhakikishia huenda tatizo lake likaisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi jini Balkis kufanya mapenzi na mpenziwe usingizini kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye. SASA ENDELEA... “Baada ya kuweza kukuchanganyeni akili, penzi mlilofanya na mumeo lilirudisha mapenzi yaliyoanza kutoweka. Kitu kile kilimuudhi sana jini Balkis na kuamua kukukomoa. Najua alichokufanya nikikueleza utaogopa lakini kwa vile umetaka mwenyewe sina budi kukueleza,” kauli ya mganga ilinitisha lakini kwa vile maji nilikwisha yavulia nguo nilikuwa sina budi kuyaoga. Basi mganga akaendelea. “Usiku mlipokuwa mkifanya mapenzi bila kuzima taa jini Balkis alishindwa kufanya kitu chochote, kosa kubwa mlilofanya japo msingeweza kujua madhara yake. Nina imani mapenzi uliyofanya wakati wa giza na mwanga kuna mabadiliko yalitokea ulipofanya mapenzi?” “Ndiyo.” “Mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani ulihisi maumbile ya mumeo kuwa makubwa na kusababisha uumie sana badala ya raha ikawa maumivu.” “Ni kweli kabisa.” “Basi wakati mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani, mumeo aliondolewa juu yako na jini Balkis aliingiza mguu wake uliokuwa na kwato kama mbuzi na kuanza kukusukumia ndani.” Kauli ile ilinifanya nisijikie vibaya mpaka tumbo likaanza kunikata chini ya kitovu, nikiwa navuja jasho la hofu. Mganga aliendelea kunieleza maneno niliyohisi yananikata maini. “Basi ulijikuta ukivumilia huku ukiumia, ilifikia hatua kutotamani tena kufanya mapenzi na mumeo kwa kuamini maumbile yake yameongezeka ukubwa. Lakini ulipowasha taa ulishangaa kuyaona ya kawaida uliyoyazoea, kweli si kweli?” “Kweli,” nilijibu huku nikizidi kumuogopa mganga kuwa na uwezo wa ajabu kuyajua mambo ambayo hakuyaona lakini utafikiri alikuwepo. “Ajabu hukumwambia mumeo, kwa nini?” “Hata sijui,” nilimjibu. “Baada ya kuamua kutofanya mapenzi na mumeo kuogopa kuumizwa badala ya kupewa raha, uliamua kutafuta visingizio ili usikutane naye kimwili, uongo kweli?” “Kweli.” “Jana kuna kitu cha ajabu kimekutokea ndiyo sababu ya kumpigia simu Bi mkubwa wako?” “Ni kweli.” “Basi, baada ya kuona hufanyi tena mapenzi na mumeo, jana ulipolala uliota ndoto kuna mtu anakuingiza mkono sehemu zako za siri na kuanza kukukoroga kama anavuta kitu toka sehemu zako cha siri na ulipoamka ulijikuta ukitoka damu ambazo uliamini ni za hedhi japo ulishangaa kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi kitu ambacho hakikuwahi kukutokea maishani mwako.” “Ni kweli.” “Unajua madhara yake?” “Hapana!.” “Naomba uwe na moyo mgumu kwa vile alichokifanya kwa tiba ya kubabaisha hutapona milele.” “Mungu wangu,” kauli ilitushtua mimi na mama na kujiuliza ni ugonjwa gani tena huo Yaillah. “Baba ni ugonjwa gani tena huo?” Ilibidi mama aulize baada ya mimi kuwa katika wakati mgumu nilishika mikono kifuani, nilimuomba Mungu aniepushe na balaa linalotaka kunikumba. “Jina Balkis alijiulaumu kwa kuamini alifanya kosa ambalo aliliona limempotezea mapenzi ya mumeo kwake,” mganga alimjibu mama. “Mapenzi yapi hayo?” Mama aliendelea kuuliza. “Kosa kubwa alilofanya ni kumpaka mafuta ya kuongeza ladha ya mapenzi mwanao, kumbuka maumbile ya jini na mwanadamu yanatofautiana, kwa vile yako ya kibinadamu baada ya kukupaka ilizidi raha mara dufu na thamani yake kwa mumeo ilishuka. Alichokifanya kilikuwa kukutoa kizazi kitu ambacho ndicho kitakacho vunja ndoa yenu. Katika ndoto ulichokiota ndicho kilichotendeka usiku wa jana. Jini Balkis alikutoa kizazi na sasa hivi huwezi kuzaa tena maishani mwako.” “Mungu wangu,” kauli ya mganga ilinikata maini. “Sasa baba utatusaidia vipi?” Mama bado alikuwa na ujasiri kutaka kujua nini hatima ya ukatiri wa jini Balkis kwangu. “Mmh! Ndiyo maana nikasema ipo kazi tena kazi kubwa sana si ya kitoto na tukifanya mchezo tutapotea wote.” “Jamani, tupotee kivipi?” “Vita yake ni kubwa sana, kumdhibiti naweza lakini kama nitakufanyia kinga ya kukufunga huwezi kupona tena. Na kosa lolote linaweza kuhatarisha maisha yetu. Hawezi kukubali kuona anazuiwa kutimiza dhamira yake, kwa kutumia nguvu zake anaweza kututeketeza wote.” “Unataka kutuambia kuna uwezekano wa kupona?” “Upo, lakini ndiyo mzame sana.” “Baba wewe huwezi?” Mama aliuliza tena kwa vile mimi nilikuwa nimechanganyikiwa kwa niliyoyasikia. “Uongo mbaya, mimi siwezi kukirudisha kizazi chake, si yeye ni wanawake wengi wametolewa na yote kaenda kuiweka chini ya bahari kwenye mwamba wa maji yaliyotulia pia hayafikiwi na kitu chochote kitakachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda hospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo na wengi maradhi yao kwa tiba ya kisasa hayaonekani lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa kizazi na kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yameweka migogolo lakini mabwana hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.” “Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza. “Hakuna sababu nyingine ni ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kupata tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akiisha maliza kazi yake ya kupata vizazi mia, ambao walipata bahati ya kutokutana naye. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa tasa milele.” Siri nzito za jini Balkis zinazidi kufunguka, nini hatma ya yote je kuna tiba sahihi ya tatizo hilo?



    @@@@@@@@@@@@@@@@

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ILIPOISHIA: Eneo hilo halifikiwi na kitu chochote kinachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda mahospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo. Wengi maradhi yao hayaonekani kwa vipimo vya kisasa lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa vizazi. Kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yamesababisha migogoro mikubwa. Wanaume hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.” “Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza. “Hakuna sababu nyingine zaidi ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kutafuta tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akishamaliza kazi yake ya kupata vizazi mia. Watakaokuwa na bahati ya kutokutana naye watasalimika. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa matasa milele.” SASA ENDELEA... “Unafikiri ni mganga gani anaweza kutusaidia?” Nilimuuliza nikiwa nimekata tamaa. “Mmh! Nendeni Bagamoyo kwa mzee mmoja maarufu sana maeneo ya Mlingotini, anaitwa Ustaadh Sudi Makata.” “Una uhakika?” “Japo sina uhakika kwa asilimia mia, lakini yule bwana namwamini sana.” “Tutamjuaje?” “Mkifika pale Bagamoyo maeneo ya Mlingotini muulizeni mzee Njiwa Manga.” “Ni tofauti na ustaadhi Makata?” “Hapana ndiye huyo huyo Makata, jina la Njiwa Manga kapewa na watoto aliokuwa akiwatuma wamkamatie njiwa manga kwa ajili ya kazi zake za majini. Kila mtoto aliyetumwa akimuona alimwita babu wa njiwa manga. Basi ikawa njiwa manga, njiwa manga mpaka leo.” “Mmh! Tutajitahidi twende haraka.” “Wala msiwe na haraka, jipangeni kwani tatizo limekwishatokea,” mganga alitutuliza. “Sawa tutafanya hivyo.” “Ila leo nitakupa dawa ya kuoga na kufukiza ndani mwako, lakini hapa naona itakuwa vigumu kwa vile mumeo haamini ushirikina. Kwa hiyo dawa ya kufukiza iache ila utaoga hii ambayo itakusaidia kumfukuza jini Balkis asikusogelee. Pia kuna kitu nilisahau kuwaeleza, leo wakati mnarudi nyumbani kutoka ofisini, mlipofika daraja la Salenda mlimuona mwanamke mmoja mrembo sana akiwa amesimama pembeni ya barabara chini ya mti?” “Ndiyo.” “Baada ya hapo gari lilizima ghafla?” “Ndiyo.” “Yule mwanamke mlimuona akibadilika mavazi?” “Ndiyo.” “Basi yule ndiye jini Balkis, ni mwanamke mzuri sana ambaye hakuna mwanaume yoyote anayemtaka akamkataa. Lakini ana roho mbaya, kwa sababu ana matatizo ya uzazi, dawa aliyoelezwa ni kutafuta vizazi vya wanawake mia moja ili atengenezewe dawa ya kupata mtoto.” “Mungu wangu, kama ni hivyo unafikiri nitaweza kupona kweli?” Niliuliza kwa sauti ya kukata tamaa. “Ukiwahi utapona! Mpaka sasa inaonesha ana vizazi ishirini na mbili, bado vingi na havipati kwa urahisi namna hiyo.” “Mbona mzuri sana, jini gani anavaa nguo kama binadamu, si huwa nasikia wana mabawa?” “Wenye mbawa si majini bali malaika, wao ni kama binadamu kabisa, wanaishi maisha kama watu ila wamepewa uwezo wa kujibadili kuwa katika umbile lolote watakalo, pia wana nguvu za ajabu walizobarikiwa na Mungu za kuonekana wanapopenda wao.” “Kumbe!” “Alifanya vile ili mmuone, baada ya hapo aliondoka na ninyi gari lenu liliweza kuondoka, kitu ambacho kiliwahi kumtokea shoga yako siku aliyohudhuria sherehe ya kuagwa jini Balkis kuja duniani rasmi. Mlipofika nyumbani kwako kuna kitu kimoja kilitokea ambacho shoga yako ilifikia hatua ya kukufikiria vibaya na kuamini huenda na wewe ni jini.” “Mungu wangu, kitu gani hicho?” “Alipoingia ndani taswira ya sura ya jini Balkis ilitanda kwenye uso wa mama yako, kitu kilichomshtua sana. Baadaye alijiondoa na bi mkubwa kuwa katika hali yake ya kawaida. Shoga yako aliondoka akiwa hakuamini kabisa. Kama unabisha ukirudi nyumbani muulize kaona nini.” Basi baada ya maelezo yale tulirudi, huwezi kuamini kidogo gari linishinde kuendesha kutokana na mshtuko nilioupata. Lakini mama alinipa moyo kwa kuniambia ili nipate ukweli wa kile nilichoambiwa na mganga lazima niende kwa waganga zaidi ya mmoja. Lakini nilimweleza mama mbona yote aliyoyasema yana ukweli kwa asilimia mia? Lakini mama alinieleza inawezekana ni kweli kwa asilimia kumi, mengine tusiyoyajua huwa ni uongo wa waganga ili kujipatia pesa. Nilimueleza mbona hakutaka pesa zaidi ya kutueleza twende kwa mganga mwenye uwezo zaidi yake. Mama alinikata maini kwa kunieleza kuwa waganga wana tabia ya kutafutiana wagonjwa na kugawana pesa kwa kuufanya ugonjwa uonekane mkubwa usioweza kutibiwa. Tukienda kwa mganga mwenzake tutaambiwa pesa nyingi ambazo hatutaweza kukataa. “Kwa hiyo mama hata kutolewa kizazi ni uongo?” Nilimuuliza. “Uongo, nilishindwa kumkatalia angeona namuingilia kwenye kazi yake.” “Kwa hiyo mama nisiwe na wasiwasi?” “Ondoa wasiwasi, kitu kama hicho hakipo.” Basi shoga niliporudi kidogo moyo ulitulia japo maelezo yote kila nilipoyafikiria mwili ulisisimka. Niliporudi hata bila kupumzika nikakupigia simu. Basi shoga habari ndiyo hiyo tumekamatwa na jini sijui Balkis,” Sharifa alimueleza Suzy aliyekuwa ametulia kama sanamu asiamini alichokisikia toka kwa shoga yake. “Sharifa acha kuligeuza jina lake si umesema anaitwa Balkis.” “Kweli, Balkis.” “Mmh! Mbona kama...” “Kama nini?” “Sijaelewa basi inaonekana hata mimi ana mengi juu yangu, kuna umuhimu kesho kunipeleka na mimi,” Suzy alimweleza shoga yake huku wasiwasi ukiongezeka moyoni mwake kwa kuamini mpenzi wake anaweza kumuacha kwa penzi la ndotoni na jini Balkis linalotumia dawa ya kuongeza ladha ya mapenzi na yeye kuonekana si mali kitu. “Sawa tutakwenda.” Waliagana kwa Suzana kurudi nyumbani kwake kutafakari aliyoelezwa na Sharifa, moyoni alikuwa na mambo mawili; kukubali na kukataa. Akili yake ilikuwa kwenye kukataa na kuamini hakuna vitu kama vile. Basi shoga niliporudi kidogo moyo ulitulia japo maelezo yote kila nilipoyafikiria mwili ulisisimka. Niliporudi hata bila kupumzika nikakupigia simu. Basi shoga habari ndiyo hiyo tumekamatwa na jini sijui Bakils,” Sharifa alimueleza Suzy aliyekuwa ametulia kama sanamu asiamini alichokisikia toka kwa shoga yake. “Sharifa acha kuligeuza jina lake si umesema anaitwa Balkis.” “Kweli, Balkis.” “Mmh! Mbona kama...” “Kama nini?” “Sijaelewa basi inaonekana hata mimi ana yangu mengi juu yangu, kuna muhimu kesho kunipeleka na mimi.” Suzy alimueleza shoga yake huku wasiwasi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ukiongezeka moyoni mwake kwa kuamini mpenzi wake anaweza kumuacha kwa penzi la ndotoni na jini Balkis alinalotumia dawa ya kuongeza ladha ya mapenzi na yeye kuonekana si mali kitu. “Sawa tutakwenda.” Waliagana kwa Suzana kurudi nyumbani kwake kutafakari aliyoelezwa na Sharifa, moyo alikuwa na mambo mawili kukubali na kukataa. Akili yake ilikuwa kwenye kukataa na kuamini hakuna vitu kama vile. sasa endelea... Tatizo la Brighton kukosa nguvu za kiume lilimnyima raha na kuamua kwenda hospitali kutafuta ufumbuzi wa tatizo ambalo hata yeye hakuelewa limetokana na nini. Alikwenda hadi katika hospitali ya TMJ kwa rafiki yake, baada ya kumuelezea tatizo lake daktari alitaka kumpima ili ajue tatizo ni nini. Brighton aliingizwa kwenye chumba maalumu na kuvua nguo zote na kubakia na nguo ya ndani, kisha alielelezwa apande kwenye kitanda nilichokuwa mule ndani na kujilaza kusubiri kufanyiwa uchunguzi. Baada ya daktari kuingia chumbani na boksi la gloves kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi wa awali. Alichukua gloves ili aanze kufanya uchunguzi hata kabla hajamgusa sauti ilisikika toka nje. ilimwita: “Dokta kuna mgonjwa yupo serious sana.” “Sorry Mr Brington, nakuja mara moja,” daktari alisema huku akigeuka na akitoka chumbani kumuwahi mgonjwa. “Hakuna tatizo,” Brighton alijibu akiwa bado amejilaza kitandani. Baada ya muda mchache alishangaa kumuona muuguzi wa kike akiingia chumbani mule bila hodi. Brighton alishtuka kumuona muuguzi wa kike mwenye asili ya kiarabu akiingia bila hodi wakati yeye amelala kitandani na nguo ya ndani tu. “Wee vipi?” Brighton alishtuka na kutaka kuziwahi nguo zake. Lakini muuguzi alikuwa ameishawahi kuingia na kumshika kifuani kumrudisha kitandani. “Brighton hebu tulia.” Kauli ile ilimshtua Brighton na kujiuliza yule muuguzi amejuaje jina lake, lakini bado alitaka kuamka ili achukue nguo zake. “Brighton mbona unakuwa si muelewa, nimetumwa nije nikusaidie tatizo lako.” Kauli ilimshangaza sana Brighton na kuamua kutulia, lakini hakupenda mwanamke yule aliyeonekana ni muuguzi kumchunguza matatizo yake. Baada ya kutulia yule muuguzi ambaye alikuwa mrembo kupindukia huku akinukia manukato mazuri sana ambayo hakuwahi kuiyasikia alisema: “Sikiliza Brighton, tatizo lako si la dawa za kizungu, si lilitokea wakati ukifanya mapenzi na mpenzio?” “Ndiyo,” Brighton alikubali huku akijiuliza taarifa zile nani kamwambia. “Basi nitakupa dawa ya kupaka, wala usikubali dawa za kizungu italala moja kwa moja.” “Hiyo ni dawa gani?” “Dawa ya asili ya mafuta mazuri,” Alisema huku akitoa kichupa kidogo kwenye matiti na kujipaka mkononi, bila kuvaa gloves alitelemsha nguo ya ndani kidogo na kuanza kumchua sehemu za siri. Ilikuwa ajabu sehemu zake zilisimama na kumfanya Brighton azidi kushangaa. “Sasa hii dawa nitakuachia, kwa vile muda huu natoka, tutaonana siku nyingine. Ila hapa hospital sitakuwepo naacha kazi.” “Kwa nini mrembo?” “Nimeamua tu.” “Nikitaka kukuona?” “Si rahisi, la muhimu umepona kampe raha wifi?” “Umeolewa?” “Ukitaka mazungumzo mengi utanikuta nje, sasa hivi vaa nguo zako akija daktari mwambie umekwishapona na usikubali kumjibu zaidi ya kuondoka.” Baada ya kusema vile yule muuguzi mrembo alitoka na kumuacha Brington akivaa nguo. Akiwa anamaliza kuvaa viatu daktari aliingia na kumkuta anataka kuondoka. “Vipi best, mbona unataka kuondoka, samahani nimechelewa hata mgonjwa mwenyewe nimemuona?” “Una maana gani?” “Hata hao wauguzi nawaelewa wanasema alikuja dada mmoja wa Kiarabu, alipofika katikati ya korido alidondoka na kuanza kutoa povu, ndipo waliponifuta ili nikampe msaada wa haraka. Lakini ajabu mgonjwa mwenyewe sikumkuta.” “Sasa kaenda wapi?” “Hata wanajua.” “Labda kapata nafuu kaondoka.” “Si rahisi kwa hali aliyokuwa nayo si rahisi kuondoka.” “Mmh! Sasa atakuwa amekwenda wapi?” “Hata najua, hebu tuendelee na matibabu yetu.” “Nimepona,” Brighton alijibu kwa mkato. “Mr Brighton najua nimekuchelewesha, samahani sana hebu rudi nikufanyie uchunguzi.” “Mr Paul nipo sawa.” “Si kweli, najua umekasirika.” “Sijakasirika Mr nipo sawa, nimeshangaa kujiona nipo sawa nikiwa nimelala kitandani, kama itarudia nitakueleza.” “Heri tungejua tatizo ili lisije likarudia tena.” “Halitatokea tena.” “Si kweli najua umekasirika.” “Niamini Mr Paul wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu, kwani umetumia muda gani wa kunifanya nikasirike. Na kwa nini nikasirike wakati ulikimbilia kuokoa maisha ya mtu.” “Kama hujakasirika sawa.” Brighton aliagana na Dokta Paulo na kutoka nje ya hospitali, alipofika nje aliingia kwenye gari lake na kuamua kurudi nyumbani. Ili kuiamini dawa yake kabla ya kuondoka alimpigia simu mpenzi wake Suzana. “Mpenzi naomba leo uje nyumbani nina imani tiba ya tatizo langu imepatikana.” “Tiba ya nini?” “Kwani nasumbuliwa na nini?” “Lile tatizo la kitandani?” Ni kweli Brighton amepona? Yule aliyempa dawa ni muuguzi kweli?



    @@@@@@@@@@@

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

     Hilo hilo.” “Brighton hebu acha utani.” ”Kweli mpenzi wangu, huwezi kuamini ugonjwa ulivyopona.” “Au ulikwenda kwa Babu?” “Walaa, tukikutana nitakueleza maajabu yaliyonitokea, ilikuwa kama bahati ya mtende.” “Basi leo mtoto hatumwi dukani nina usongo na wewe ile mbaya.” Baada ya Suzana kukata simu alijikuta akizidi kuchanganyikiwa na maelezo ya mganga kuhusu mpenzi wake na taarifa za kupona kwake. Alijikuta akianza kuamini maneno ya mama Sharifa kuwa waganga wengi ni waongo, kazi yao kuwatisha wagonjwa ili wapewe pesa nyingi. Alijikuta akifuta wazo la kwenda kwa mganga ili na yeye akaangaliziwe mambo yake. Aliona kuna uongo mkubwa kati ya maneno ya mganga na mpenzi wake, alipoambiwa kuwa mpenzi wake hamhitaji tena kwa vile anafanya mapenzi na jini Balkis kwenye ndoto. Ujumbe wa mpenzi wake kumhitaji kimapenzi ulidhihirisha jinsi mganga alivyowadanganya. Aliona kwenda kwa mganga ni kupoteza muda na kumpa pesa za bure. Muda ule ule alimpigia simu Sharifa kuahirisha safari ya kwenda kwa mganga. “Shoga, kesho safari ya kwa mganga imekufa.” “Vipi shoga, mbona hivyo?” “Aah! Basi tu, tutakwenda siku nyingine.” “Mmh! Sawa.” Wakati Suzana akiahirisha kwenda kwa mganga kuangalia matatizo yake, Brighton baada ya kutoka ndani ya hospitali alipepesa macho labda atamuona muuguzi aliyemtibu. Lakini hakumuona, alitaka kwenda kumuuliza ndani ya hospitali, lakini alikumbuka kauli ya yule muuguzi ambaye hata jina lake hakulijua, alimkataza asimuulize mtu yeyote habari zake. Aliingia ndani ya gari yake na kuondoka huku akiwa na shauku ya kumuona yule dada mrembo mwenye roho ya huruma. Mpaka anaondoka eneo la hospitali hakumuona. Alijikuta akiwa na shauku ya kumuona yule mrembo ambaye alisema mengi wangezungumza nje ya hospitali. Alipokaribia maeneo ya Makumbusho alishtuka kumuona yule dada akiwa katika vazi refu zuri lenye mvuto, lililoongeza uzuri wake akilipungia mkono gari lake. Alilisimamisha mbele yake kidogo, yule mwanamke mrembo alisogea hadi kwenye gari na kufungua kisha aliingia ndani na kukaa kwenye siti. Baada ya kukaa na kufunga mlango wa gari, Brighton aliondoa gari bila kujua mrembo anaelekea wapi. Baada ya mwendo mfupi aliitwa jina lake. “Brighton.” “Naam.” “Za muda?” “Nzuri.” “Unaelekea wapi?” “Nilikuwa narudi nyumbani, lakini nitakusikiliza wewe unakwenda wapi.” “Umeoa?” “Bado.” “Na Suzana?” “Suzana! Umemjuaje?” “Jibu swali,” yule mwanamke alisema huku akimuangalia jicho lililolegea. “Ni mchumba wangu, si mke wangu.” “Ina maana ukipata mtu mwingine utakuwa tayari kumuoa na kumuacha Suzy?” “Itategemea.” “Itategemea nini, wakati tayari Suzana ni mchumba wako?” “Itategemea uwezo wake katika ufahamu wa maisha, Suzana mchumba wangu pamoja na kunipenda, tatizo lake anapenda sana starehe. Kwangu namuona kama si mwanamke anayefaa kuwa mke wangu.” “Kwa mfano mimi nikitaka unioe itakuwaje?” “Mmh! Nitakuweza?” “Kivipi?” “Unaonekana unatoka katika familia ya watu wenye uwezo.” “Familia yangu ingekuwa na uwezo ningefanya kazi pale hospitali?” “Hata mimi nashangaa.” “Niambie kweli kama utakuwa tayari kunioa niwe mkeo, kila kitu nitashughulikia mimi, nakuahidi kuyabadili maisha yako.” “Mmh! Nipe muda.” “Brighton sina muda mwingine zaidi ya huu.” “Nimekubali.” “Kama umekubali naomba leo nikalale kwako.” “Mmh! Kwa nini tusifanye siku nyingine?” “Au kwa vile umemwita Suzana?” “Umejuaje?” Brighton alishtuka tena. “Brighton, nimekueleza sitaki maswali ninapokuuliza swali nataka jibu.” “Ni kweli, leo nilimualika aje tulale pamoja.” “Tatizo nini?” “Sasa itakuwaje wewe uwepo na yeye aje?” “Wee mwache aje alale, mimi nitalala chumba kingine.” “Si atakuona?” “Hawezi kuniona, labda umwambie wewe.” “Kwa hiyo utaingia nyumbani saa ngapi?” “Muda wowote, usiwe na wasiwasi.” Brighton alielekea nyumbani kwake akiwa na wasiwasi wa kugonganisha wanawake. Brighton anakutana na mtihani mzito wa kuvunja uchumba wake na Suzy, Suzy atakubali kirahisi kumpoteza mpenzi wake?

      Walipofika nyumbani yule mwanamke aligundua wasiwasi wa Brighton, alimgeukia na kumuuliza: “Mbona una wasiwasi?” “Bado siamini kama Suzana akija hawezi kukuona, kwa nini nisimzuie asije?” “Hapana Brighton, kwa vile umemuita, mwache aje tu.” “Anaweza kuja chumba utachokuwemo itakuwaje?” “Naomba uwe mwelewa, wee mwache aje na mimi hawezi kuniona.” “Mmh! Sawa.” Brighton alikubali kwa shingo upande, lakini moyoni alikuwa na kiburi cha ajabu, kama Suzana atamuona mgeni wake, atakuwa tayari kwa atakachokiamua. “Brighton bafu lipo wapi?” Mgeni aliuliza. “Lipo ndani ya chumba cha kulala.” “Naomba nikaoge.” “Ruksa.” Mwanamke mrembo alielekea chumbani ili aende bafuni kuoga, kila hatua aliyopiga kuelekea chumbani ilimchanganya sana Brighton, alijiuliza imekuwaje mwanamke mzuri kama yule kumpenda yeye kwa haraka. Katika maisha yake aliwahi kuona wanawake wazuri lakini yule alikuwa ni zaidi. Baada ya mgeni kuingia chumbani, wazo la haraka kwa Brighton lilikuwa kumpigia simu Suzana kumzuia asije. Ili mgeni asisikie alitoka nje lakini ilikuwa ajabu simu ya Suzana haikupatikana, kitu kilichozidi kumweka kwenye wakati mgumu wa kuweza kumzuia asifike nyumbani kwake. Akiwa bado anatafakari jinsi ya kutatua tatizo lile, sauti ndani ilimwita. “Mpenzi upo wapi?” “Nipo nje.” “Njoo basi.” Brighton aliingia ndani huku akijitahidi kuficha hofu yake, picha aliyoiona mbele yake ilimfanya afikiche macho kujiuliza anachokiona ni kweli au yupo ndotoni. Mbele yake alikuwa amesimama mwanamke mrembo ajabu akiwa amejifunga mtandio mwepesi sehemu ya makalio na kifuani. Sehemu nyingine ya mwili wake ilikuwa wazi. Lilikuwa umbile lenye kumtia msisimko mwanaume yeyote rijali. Alijikuta akipigwa na butwaa kama ameona meli ikitembea barabarani. “Mbona unanishangaa?” Mgeni alimuuliza. “Lazima niseme ukweli, wewe ni mwanamke mzuri sana.” “Asante, hata wewe ni mwanaume mzuri sana.” “Nashukuru.” “Brighton mbona unajiweka roho juu, hebu mwache Suzana aje.” “Umejuaje?” Brighton alishtuka kusikia vile. “Unaniuliza nimejuaje, ina maana ninachosema ulifanya siri?” “Hapana, sipendi litokee tatizo lolote, unaweza kuniona sina maana.” “Aliyekueleza umruhusu Suzana aje nani?” “Wewe.” “Sasa tatizo nini, nimekueleza mwache aje kwani chumba nitakachokuwa hawezi kuingia.” “Wewe unajiamini nini?” “Utajua baadaye sasa hivi ni haraka, mimi si mkeo mtarajiwa?” “Ndiyo.” “Kipi kimekufanya ukubali niwe mkeo?” “Hata sielewi lakini kitendo chako cha kujitolea kunitibu bila gharama ugonjwa ambao ulinisumbua sana, imeonesha jinsi gani ulivyo muhimu sana kwangu.” “Kingine?” “Nimetokea kukupenda na kila dakika mapenzi yangu kwako yanazidi kuongezeka.” “Nashukuru kusikia hivyo, nina imani kuna vitu umehisi kuvikuta kwenye mwili wangu, basi nakuhakikishia kukufurahisha katika maisha yangu yote.” “Nitashukuru.” “Brighton nipo chumbani, Suzana amekaribia kufika.” “Umejuaje?” “Brighton mbona kila ninachokizungumza kwako kinakushangaza?” “Unanishangaza kuzungumza vitu ambavyo kwa mtu yeyote ni vigumu kuvijua.” “Brighton najua una hamu kunifahamu kwa undani, hata jina langu hulijui?” “Ni kweli, hebu niambie jina lako unaitwa nani?” “Sasa mbona mpaka nimekueleza mimi au hukupenda kulijua jina langu?” “Huwezi kuamini, jinsi nilivyopagawa kukupata, hata kuuliza jina niliona kazi, najiona kiumbe mwenye bahati ya mtende.” “ Naitwa Balkis Bakilas, naomba nikuache Suzana anaingia sasa hivi, nakusihi usioneshe wasiwasi wowote.” “Umejuaje?’ “Kuwa mwelewa,” baada ya kusema vile aligeuka na kuelekea chumba cha wageni. Kila hatua aliyopiga kuelekea chumbani huku akimuachia Brighton sehemu za nyuma ambazo ziliumbwa kwa mpangilio. Alijikuta akimeza mate huku akimsindikiza kwa macho. Hata alivyoingia mpenzi wake Suzana hakumuona, alishtuka alipoulizwa swali. “Brighton mbona umeshangalia huko hadi naingia wewe huna habari, kuna nini?” Suzana aliuliza huku macho yake yakiangalia alipoelekea Balkis. “Aa..aah,” Brighton alibabaika kujibu. “Brighton kuna nini?” “Ha..ha..kuna kitu.” “Au ulifikiri siwezi kuja?” Suzana alisema huku akimbusu na kukaa pembeni

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    yake. “Wala.” “Mbona kama haupo sawa?” “Nipo sawa.” “Nakuja.” Suzana alisema huku akinyanyuka na kuelekea chumba alichoingia Balkis, Brighton alijikuta akipatwa na mshtuko, wasiwasi wake ulikuwa huenda Suzana alimuona akiingia hivyo alikwenda kumfumania. Alitaka kumkataza lakini mdomo ulikuwa mzito. Ni kweli Suzana kamuona Balkis? Na kama kamuona nini kitatokea?



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog