Search This Blog

666 NYAYO ZA KUZIMU - 3

 





    Simulizi : 666 Nyayo Za Kuzimu

    Sehemu Ya Tatu (3)





    "vipi tena si ulisema hutoki nje??"

    aliuliza mzee Patili,



    "eh! Yani mie nibaki peke yangu ndani??..wale mabibi si watanifuata!!"

    akajibu Julina huku macho ya uoga yakipendezesha uso wake mwembamba mweusi.Punde si punde mama Halima nae alitoka nje na kujumuika na Julina na mzee Patili aliembebelea mtoto,walianza kuteta kuhusu wale mabibi na pia bila kusahau ndoto ya

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mzee Patili iliyowashangaza na kuwaogopesha wakina Julina kwa kiasi kikubwa!

    "mito ilikua miekundu,haikuskika tena sauti za ndege,milio ya shida na malalamiko ndio iliyotawala,harufu ya kifo na umauti ndio iliyoshika hatamu,miti ilipendezeshwa na miili iliyoning'inia kwa kunyongwa,na mioyo ya binadamu ilikua ni ya wanyama,tena wanyama haswa!!!"



    alizidi kudadavua mzee Patili ile ndoto huku macho ya wakina Julina yakiwa yanakaribia kutoka kwa mshangao!!

    Akaendelea,

    "kila mmoja niliemuona alikua na chapa ya namba mwilini mwake!"

    "chapa!!..ipi tena??"

    Julina aliuliza kwa mjazo wa kutaka kujua,kwa masikitiko alijibu mzee Patili

    "chapa yenye namba tatu,sita zilizorudiwa mara tatu,yani 666!!!..cha kutofautisha tu kilikua ni wapi hiyo chapa



    ilipokuwepo,wengine kwenye mapaji ya uso,wengine mikononi,wengine mapajani na kadhalika! Maisha hayakua kama yalivyo,maisha hayakua kama tunavyoyajua,kila mtu muoga na maisha yake alikubali kubandikwa chapa itakayomuwezesha kuendelea kuishi,na wale wenye misimamo yao,walinyongwa kama kuku!!!"



    maneno hayo yalizidi kuteketeza amani ndani ya mioyo ya wakina Julina na pia kuzidi kupalilia roho ya uoga iliyochipukia kwa kasi!!....taswira ya kile kilichokua kinaelezewa na mzee Patili ilikua imejengeka ndani ya vichwa vyao hivyo kuipa mwanya hisia za uoga kukumbatia mioyo yao iliyokua inaenda mbio!!

    Udadavuaji wa ndoto ulizidi kutolewa na mzee Patili,lakini kabla ya kumalizika alikuja mama Tito kwa kasi huku akiwa kashikilia



    kichwa na anapiga ukunga,ilikua haiitaji vipimo kujua ya kwamba alikua kwenye matatizo!!

    "uuuuwwwiiiiiiii!!!!....Maamaaa weee!!! Mungu wangu eeeenhh!!!...jamaniiiiii!!!!"

    "mama Tito vipi tenaa???"

    aliuliza mzee Patili kwa hamaki huku wakina Julina wakiwa wameishiwa pozi kwa mshangao!!

    "mume wangu jamaniii!!!!...mume wangu..mungu wee!! Mume wangu Jamanii!!!!!"

    "sasa mume wako kafanya nini???"

    "nimemkuta mume wangu kanyongwa kule shambani,jamani baba Tito wanguuuuuwwii!! Mume wangu mie ntaishijeee!!!"

    sauti kali ya kilio ya mama Tito iligonga kwenye masikio ya wanakijiji,haraka lile eneo lilifurika watu,habari za kunyongwa Baba Tito zilihamsha taharuki,msururu wa watu ulianza safari na kuelekea eneo la tukio wakiwemo mzee Patili na wakina Julina ambao hawakutaka kabisa kubaki pale kijijini.



    Sauti za vilio vya wanawake ilipata kusikika vizuri,tahamaki ilimshika kila mtu,kuona mwili wa baba Tito ukiwa unaning'inia kwenye mti ule wa muembe halikua tendo la kawaida kabisa machoni mwao! Hisia za uoga zilitawala na baadhi yao wenye roho ndogo walizirai akiwemo Julina!!



    Nani amefanya haya?? Na amefanya kwa madhumuni gani?? Kila alieshuhudia lile jambo alijiuliza na kuwauliza wenzake pia,sauti ya kilio cha mama Tito iliyokua inazidi kupotelea kutokana na kukaukiwa sauti ilizidi kuchimbua na kumwagilia huzuni iliyodamiri lile eneo,na pia tukio la kumpepea Julina aliezimia liliendeleza hofu mioyoni.



    Mwili wa Baba Tito ulishushwa na kufunguliwa toka kwenye kile kitanzi,na taratibu ulibebwa kupelekwa kijijini kwa ajili ya shughuli za mazishi huku bado maswali mengi yakizaliwa ndani ya vichwa vya watu waliokua pale juu ya kipi hasa kinachoendelea.

    Wakati safari ya kurudi kijijini ikiwa inaendelea ghafla mjadala mzito ulianzishwa,mjadala uliokua unaongelea juu ya ujio wa Mzee Otongo na mama Kadogo kama sababu kubwa iliyopelekea ile hali,yani ujio wao ndio umeleta laana pale kijijini na ndio mana mambo ya ajabu yameanza kuchukua nafasi!!



    Asilimia kubwa ya watu walionekana kuafiki hilo jambo isipokua Mzee Patili aliesimama kidete kukanusha hilo kwa nguvu zote na kutetea tendo lake la kuwapokea wale watu kwamba lilikua sahihi.

    Mama Halima hakua na la kuchangia kwani hakushuhudia hayo mambo na pia Julina hakupata hiyo fursa kwani alikua bado hajazinduka,mtoto wake alikua amebebwa na mzee Patili na mwili wake ulikua mgongoni mwa Mama Halima!

    Je itakuaje? Na ni nani anahusika na hayo mauaji? Wakina mze Otongo watakua salama mbele ya wanakijiji?

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa mbali sauti za vilio zilifika kwenye masikio ya mzee Otongo,mwili wake bado ulikua unavuta kwa maumivu japokua fursa ya kuishi bado ilikuwepo mikononi mwake,tumbo lilikua linamuuma kwa sana ilihali na kichwa kutokana na dhoruba kali aliyokumbana nayo ya Jeshi! Jeshi! Jeshi la 666! Alitaka kujiinua,mungu wangu!! Alisikia mpasuko wa maumivu umepita mgongoni pahh!!...ka sauti ka kulalamika kakaitika..aaaahh!!! Kilichoashiria ya kwamba maumivu yamegota penyewe,aliurudisha mwili wake chini na kugeuza shingo kutizama pembeni alipomuona mama Kadogo ambaye bado fahamu hazikurudi kwenye makao yake,alipandisha na kushusha macho yake juu ya mwili wa mama Kadogo na kushuhudia jinsi gani majeraha yalivyoshika utawala,kila pande ya mwili wake ilikua na jeraha na hata alivyojiangalia mwilini mwake aligundua hilo,macho yake yakaanza kubarizi lile eneo alilokua,kuanzia juu chini na pembezoni,umbali wa hatua tano toka alipokua kulikua na jiko litumialo kuni,na sufuria ilikua juu ya mafiga.kilichomo ndani ya sufuria kilionekana kuchemka kwani sauti ya kutokota kupita kiasi na mvuke mkubwa kutoka kwenye sufuria zilithibitisha hilo,mzee Otongo alitambua hicho kitu lakini mwili wake usingeweza kumruhusu kusogea kutokana na mzigo wa maumivu aliokua nao,sauti za watu zilizidi kufika masikioni mwake na mwishowe alisikia mlango unafunguliwa,alikua ni mzee Patili,macho yao yaligongana na kidogo kamshangao kiliwapitia,taswira ya mzee Patili haikua ngeni machoni mwa mzee Otongo ila haikua hivyo kwa mwenzie ambae ilikua vigumu kumtambua kutokana na kile kipigo kumchakaza sura yake kwa kiasi kikubwa,hawakuongea kitu,mzee Patili alifunga mlango na mkono wake mmoja uliokua haujamshikilia mtoto na kufanya sauti za wanakijiji zilizokua bado zinaruruma kwa nje juu ya ujio wa wageni pale kijijini zififie kidogo,

    "vipi unaendeleaje??"

    mzee Patili aliuliza,

    "...mmm..kichwa kinanigonga mno,mgongo nao,vilevile tumbo!!!...issshh!!"

    alilalamika mzee Otongo,

    "usihofu,mpaka jioni utakua ushapata unafuu kwani hiyo dawa niliyokupaka ni nzuri sana kwa majeraha na kutuliza maumivu.."

    "ahsante sana!..eti,kwani hapa ni wapi??"

    aliuliza mzee Otongo ili kupata uhakika wa pale alipo baada ya nafsi yake kumtonya kwamba ni utowele,

    "upo kijiji cha Utowele kwa sasa,kwani nyie mlikua mnatokea wapi na mnaelekea wapi??"

    "tulikua tunatokea Igesambo,na safari yetu ilikua ni kuja hapa Utowele.."

    "mmmh...kufanya nini??"

    aliongezea swali lingine,mzee Otongo alijivutavuta huku akipambana na maumivu na mwishowe akakaa,kisha akajibu kwa tabu..

    "lengo letu lilikua ni kumuwahi mtoto aliezaliwa.."

    kauli hiyo ilimshtua mzee Patili! Hakuna mtoto aliezaliwa kijijini zaidi ya yule aliembeba,mtoto wa Julina!!!"

    kwa hamu ya kujua akaongeza swali lingine..

    "mtoto aliezaliwa?? Wa nini hasa??"

    "huyo mtoto ndie uhai wetu,ndie tumani letu na utawala wa giza ulilijua hilo na ndio mana walitujeruhi,kutudhoofisha na kufanikisha lengo lao la kumuwahi,na hata huku kuchomoza kwa jua ni ishara ya uzao wake....ila yu hatarini na inabidi alindwe kwa nguvu zote kwani jeshi! Jeshi! Jeshi la 666! Wanamsaka kwa hali na mali wamtokomeze!!"

    maneno yale yalipenya mpaka kwenye mishipa ya damu ya mzee Patili na hapo ndipo alipoanza kupata mwanga juu ya ndoto aliyoiota,lakini kuna kitu aligundua! Haraka akauliza

    "wewe ni Otongo??"

    "naam...ndie mimi!..bila shaka wewe ni Patili!"

    "haswaa mie ndie!"

    kile kitu kilimshangaza sana mzee Patili,ni muda mrefu umepita toka walipokua pamoja kutokana na uhusiano wao wa kikazi wa kiganga na hakutegemea kama wangekutana katika ile hali!!

    Ila bado mawazo yalizidi kumsonga kichwani!!!

    * * * *

    nje ya kijumba cha mzee Patili bado wanakijiji walionekana kuteta hasa juu ya kifo cha baba Tito ambaye mwili wake ulikua ushahifadhiwa ndani kwake,kutokana na ugumu wa kujua kinachoendelea kila mwanakijiji alitupia hisia zake juu ya wale wageni waliofika ya kwamba kwa njia moja au nyingine wanahusika,nani unadhani?? Ni hawa hawa tu!! Mbona hayajawahi kutokea tangu na tangu?? Hii ni laana!!! Hawa watu wametuletea laana!! Tutakwisha jamani!!! Wanakijiji walipayuka,ngebe za wanakijiji zilizopamba moto juu ya kukemea na kulaani tendo la ujio wa wale wageni bado hazikubadilisha kitu!!!

    ALINYONGWA MWINGINE MTU MWINGINE!!! NA TENA ALIKUA NI MAMA TITO!!!...PEMBENI YA MAITI YA MUMEWE!!! nani anafanya haya mauaji? Kwanini anaua?? Amedhamiria nini?? Nini hatma ya wakina Mama Kadogo mbele ya kiza cha jamii??



    Mama weee!!!..mama Tito kanyongwa jamaaanii!!! Mungu eeee!! Tunakwisha uuuwii!!! Ndivyo alivyosikika mama Kurwa alietoka kwenye nyumba ya mama Tito kwa lengo la kumpa pole kwa kifo cha mumewe,huku akikimbia mikono kichwani mithili ya mtu aliechanganyikiwa machozi na uoga ilionekana kuitawala sura yake!! Hakuna alieamini hizo habari mpaka walipoenda kushuhudia na kukuta jambo lile ni kweli limejiri!! Macho yao yalishudia Mama Tito akiwa kaning'inizwa na kamba nyekundu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kama ile iliyomnyonga mumewe muda si mrefu,ulimi ulikua nje na damu ilionekana kutoka puani na masikioni!!!!

    Mchanganyiko wa hasira na uoga ulitawala mioyoni mwa wanakijiji,kifo kwa mara ya pili mfululizo!! Hata masaa hayajapita,tena mume na mke!!!..ni nani anaeyafanya haya?? Jamani hii si bure...ni laana inatuua!!!...ni nani aliewaleta wale watu lakini?? Ni



    baba Madhifa!!...haraka wanakijiji wasiopungua idadi ya watu thelathini,wake kwa waume,watu wazima kwa watoto kwa jazba kubwa walianza kuelekea kwa baba Madhifa!!...chuki iliyokuwepo kati ya jamii ya wakulima na wavuvi juu ya wawindaji ilizidi kushamiri kwa kiasi kikubwa,baba Madhifa sasa ndie alieokana kama chanzo,kitendo chake cha kuwaokoa wakina mzee Otongo ilikua ni hukumu tosha!

    Mawe na dhana zingine kama mapanga mikononi mwa wanakijiji zilikua ni kipimo tosha cha kuonyesha kinachoenda kujiri,hakukua na amani tena!!



    Masikini baba Madhifa,hakua na hili wala lile,kuzaliwa kwake kwenye jamii ndogo ya wawindaji ndio kosa lake kubwa,hakuna wa kuwatetea mbele ya wanakijiji wengine,hakuna wa kuwasikiliza!!

    Walipowasili kwenye uwanja wa nyumba yake haraka shughuli za ubomoaji na uharibifu zilianza!! Mawe yalirushwa kama risasi kwenye nyumba ile ya udongo bila hata kuangalia na kuuliza kama mna watu ndani,sauti za kejeli matusi na kebehi zilisindikiza



    bara-bara shughuli hiyo na hatimaye waliamua waichome kabisa waridhishe roho zao zilizokua za kinyama baada ya kushuhudia mauaji ya wenzao wawili,je hilo ni suluhisho?? Hawakufikiria hicho!!

    Baba Madhifa na wanae hawakuwepo,walirudi msituni kuendelea na shughuli zao na hata Mama Madhifa vilevile alikua kisimani akichota maji,Mungu alikua upande wao kwani kama wangelikuwepo ni dhahiri wangelikua mishikaki!!

    Lile zoezi halikuishia pale tu kwa baba Madhifa,liliendelezwa kwenye nyumba zingine zote za jamii ya wavuvi zilizokuwepo karibu na kuwafanya wabakie mithili ya vifaranga waliokimbiwa na mama,hawakuweza kufanya kitu,hawakua na uwezo huo,ila waliumia sana rohoni! Kwanini wao?? Au ni kwasababu wao hawahesabiki ndani ya kile kijiji?? Walikua kama yatima,walishindwa kuyazuia machozi.



    Sasa wamebaki wakina mzee Otongo,je kipi kitawakuta?? Wale wanakiji baada ya kuridhika na walichokifanya hawakutaka kupoteza muda,miili ya Baba Tito na mkewe ilizikwa na kuhitimisha zoezi la kumuacha Tito yatima kamili,majonzi na simanzi zilitawala lile eneo bila kusahau na hisia za uoga,

    Julina na Mama Halima ni miongoni mwa watu waliokuwepo eneo la tukio japokua hawakuhusika kurusha hata jiwe moja kwenye nyumba ya baba Madhifa,chozi lilitiririka kwenye kila jicho la mmojawao ila hasa mama Halima,moyo wake ulikua umebeba siri



    nzito juu ya vile vifo,siri ambayo hakuna hata mmojawao anayoijua isipokua yeye,ni yeye pekee aliekua anafahamu ya kwamba mama Tito hakuuwawa bali alijiua kwani alimshuhudia mama Tito kwa macho yake akiichukua ile kamba iliyomnyonga mumewe kule shambani na ndio hiyo aliyoitumia kujimalizia na yeye pia,aliogopa kusema!! Na chozi lilizidi kumshuka haswa!!!

    * * * * *

    Mama Madhifa baada ya kuweka ndoo yake ya maji kichwani taratibu alianza kujivuta kuelekea nyumbani kwake,macho yake aliyoyatupia mbele ya safari yalimruhusu aone moshi mzito ukitokea kijijini,alipata mashaka,maswali yalikuja kichwani juu ya nini hasa kinachojiri huko kijijini,masikini hakufahamu ya kwamba nyumba yake na za wenzake ndo zinateketea.



    Aliongeza kasi kidogo inayoendana na umri wake wa miaka hamsini na tatu ili aweze kuwahi ila ghafla alikabwa na mtu tokea nyuma!!! Puuh ndoo ilidondoka na maji yakamwagika!!! Aliangaika kutetea uhai wake lakini hakufanikiwa!!..mara haraka akavishwa kitanzi chekundu tayari kwa KUNYONGWA!!!



    Alikabwa kwa nguvu mno akashindwa kupumua kabisa,macho na ulimi vilitoka nje!! Aliburuzwa kama zigo la maganda ya viazi na ile kamba shingoni mpaka ulipo mti mmoja mkubwa wa mkaratusi,akaning'inizwa mithili ya nyama buchani,maisha yake yakakomea hapo,kikatili mno aliuwawa,hakupata hata fursa ya kujua yaliyotokea kule kijijini,hakupata hata fursa ya kumuona mumewe tokea muda wa asubuhi,hata mwanae wa mwisho ampendae,Madhifa.



    Hakuna alieshuhudia chochote,hakuna jicho lililoona lolote hivyo bado ilikua ni siri juu ya nani anaeua na kwanini anaua vilevile,kwanini anatumia kamba nyekundu?? Pia lilikua ni swali ambalo bado wanakijiji walikua hawajalipa nafasi vichwani mwao,hali ilizidi kuwa tete na ya kuogofya...ndani ya masaa yasiozidi matano tayari watu watatu walikua washaenda na maji kwa kifo kinachofanana!!



    Baba Madhifa na wanae wawili walikua washawasili kijijini,hali ya kuona moshi mzito toka kijijini iliwafanya waache shughuli zao za uwindaji na kwenda kujua kinachojiri,walipofika kijijini hawakuona watu kama inavyokuwaga ni dhahiri walikua wameenda sehemu fulani ambayo wao hawakuifahamu,haraka walielekea ilipo nyumba yao,hawakuamini macho yao,hawakuamini

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    walichokiona,nyumba yao ilikua tayari gofu na nyumba zingine za wenzao nazo ndio zilikua zinamalizikia kwa moto,haraka waliwafuata wenzao waliokua wamejikusanya kihuzuni hatua kama kumi toka walipo kwa dhumuni la kuuliza ili kujua hasa kilichotokea,kiunyonge waliwajibu ya kwamba wanakijiji ndio wamefanya hayo,baba Madhifa alipata hofu kubwa moyoni!! Mke



    wangu yu kwapi?? Aliuliza haraka kwa taharuki akajibiwa ya kwamba alienda kisimani,bila ya kuchelewa aliwaagiza wanae wawili ambao walikua ni wa kiume;Madhifa na Khadhifa kwenda kumjulia hali mamayo huko kisimani,haraka walikimbia



    kuelekea huko! Masikini hawakujua ya kwamba mama yao tayari alishaning'inizwa ni ndege tu wa mizoga ndio wanaofaidi,walikimbia kwa kasi na nguvu zao zote huku mioyoni mwao wakiwa wanasali mama yao awe salama,Madhifa alishindwa kuzuia machozi na hofu kubwa ilishika wake moyo,alimpenda sana mama yake.



    Baada ya mwendo wa robo saa walikuta ndoo chini waliyoitambua ya kwamba ni ya kwao lakini hawakumuona mama yao!! Ilibidi waanze kufuatilia alama zilizoashiria ya kwamba mtu aliburuzwa toka eneo lile zilizowapeleka mpaka karibu na eneo ambapo mama yao alinyongwa,ndege wa mizoga walisaidia kuhitimisha zoezi.



    "Khadhifa!!!..yule anaening'inia pale mtini ni nani???...sio mama yule!!!"

    sauti iliyotepeta uoga ya Madhifa iliuliza,

    "He!! Mbona kama ni yeye!!!!"



    alijibu Khadhifa,haraka walisogea na kugundua ya kwamba walichobashiri ni kweli,alikua ni mama yao! Damu zilitawala dela lake kwa kiasi kikubwa kutokana na kunyofolewanyofolewa na ndege wa mizoga,macho yake yaliokua nje yalikua yashanyofolewa na hata ulimi pia,sura yake ilikua ngumu kutambulika!!!



    Haraka Khadhifa ambae ndie mkubwa alifukuza wale ndege na kupanda juu ya mti kwa ujasiri na kufungua ile kamba kuruhusu mwili wa mamaye kushushwa chini,walimshusha na kumbeba kisha safari ya kuelekea walipotoka ambapo baba yao anawasubiri ilianza,hawakua na mama wala nyumba tena,uchungu usioelezeka ulitawala mioyo yao,moja kwa moja walifahamu



    ya kwamba waliochoma nyumba yao ndio wanaohusika na kile kifo,yani wanakijiji!!

    Chuki kubwa ilipandikizwa mioyoni,roho ya kisasi ilikamata hasa vichwa vyao,hawakutaka kukubali lile jambo liende vile vile tu,hawakukubali roho ya mama yao iende peke yake yani bure kabisa kwa ule unyama aliofanyiwa,hisia za kuwa wawindaji wa watu badala ya wanyama zilizuka!!





    Baada ya muda kidogo waliwasili kwenye uwanja wa nyumbani kwao sura zao zikiakisi vya kutosha mioyo yao ilivyo na uchungu,walihisi kama wamekabwa rohoni tena hisia hizo zilizidi hasa baada ya kumuona baba yao,walishindwa kupata jibu juu ya nini watamueleza kwani walimuonea huruma,lakini ghafla walianza kulia kama watoto,kilio ambacho walijitahidi kukizuia tokea muda mrefu,kilio ambacho kilimfanya baba yao ashtuke,kilio kilichofanya baba yao aanguke kwa presha kama kiroba!!

    * * * * * * *

    upande wa pili wanakijiji waliokua kwenye mazishi ya baba na mama Tito walimaliza shughuli zao,walijiondoa toka kwenye lile eneo la makaburi huku bado habari za uoga juu ya ile hali zikitapakaa,bado hofu iliwashika na walishasahau kabisa dhambi waliyotoka kuitenda ya kuchoma nyumba za watu wanaowahisi wao ni chanzo,walikua kimakundi makundi lakini ghafla mama Halima alimvuta pembeni Julina na kumwambia kwa kumnong'oneza kiumbea..



    "mama Tito hakuuwawa!!"

    "unasema??"

    "ndio hivyo kama ulivyonisikia..!"

    "we umejuaje??"

    "nilimshuhudia kwa macho yangu akiichukua ile kamba iliyomnyonga mumewe,na ndio hiyo kajinyongea!"

    "weeeh!!"

    "we si ulizimia,ungeyaonea wapi?? Ila!!..uufunge huo mdomo wako,tena uufunge hasa!"

    "ntaweza kweli??"

    alidakia Julina.





    "kwanini usiweze??...ushaanza!!"

    kwa ukali kidogo mama Halima alitamka,

    "sawa mama nitajitahidi kadri ya uwezo wangu"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Julina alimtia moyo,waliendelea na safari yao ya kuelekea majumbani taratibu huku wakiwa washaachwa nyuma na wenzao,stori ndogo ndogo zilitawala maongezi yao hasa juu ya tendo lile la uchomaji moto wa nyumba zakina Madhifa kitu walichoonekana kupinga kupinga kabisa japokua walikua hawana uwezo wa kuongea mbele ya umati wa wanakijiji,wangeonekana wasaliti.taratibu walitembea bila hofu walishasahau



    kidogo mambo ya vifo kutokana na kupumbazwa na vijistori vidogo vidogo vya hapa na pale,ila ghafla Julina alisimama kisha akasema..

    "mama Halima,nina hofu"

    "nini tena Julina mwanangu? Mwanao si yupo kwa mzee Patili.."

    alisema mama Halima huku akirudi nyuma kumfuata,

    "sio juu ya mtoto wangu Mama,ni juu ya mume wangu Kitanzi!...ni muda sasa hajarudi,sijui nae atakua ashanyongwa??"



    "mh-mh,usiseme hivyo bwana kwanza embu twende nyumbani ukapumzike mana tokea usiku ulipojifungua upo kwenye heka heka tu hata mtoto wako atakua anakuhitaji mno kwa sasa,tafadhali twende!"

    kidiplomasia mama Halima alipooza jambo lililotaka kuzuka,alimshika mkono Julina na kumvuta waende.



    Nyuma ya mama Halima na Julina alionekana mtu anakuja kwa kasi! Pande la mtu,pande la mbaba! Mweusi tii kwa rangi na kichwani alikua hana nywele kabisa,yani upara!!



    Mikono yake miwili mikubwa iliyoshiba ilikua imeshikilia kamba nyekundu,macho yake makubwa mekundu yalisadifu hamu kubwa iliyo moyoni mwake,masikio yake yalizoea makelele ya kuomba msamaha ya watu mbalimbali na hata pia mikono yake ilizoea kunyofoa roho za watu,alikua ni mnyongaji!!!



    Ghafla mama Halima alihisi kitu akageuka nyuma haraka,hakuona kitu!! Wasiwasi ulimteka moyo,akamwambia Julina

    "nahisi kuna kitu!"

    huku akigeuka geuka nyuma,

    "nini tena hiko??"

    Julina mama uoga haraka aliuliza,

    "bado sijafahamu! Ila tuongeze mwendo Julina,twende!!"



    haraka mbio zikaanza,maumivu bado yalikua na Julina kwani si muda mrefu toka atoke kujifungua lakini uoga wake ulimsaidia mno kumkimbiza,tayari moyo wake ulishawasha jenereta,ulikua mbio mno kuliko hata wa yule aliehisi kitu,yani mama Halima!! Joto lilipanda mwilini mwake,kajasho kauoga kalimteremka! Mungu wangu nisaidie!! Alijiambia moyoni.



    Baada ya muda kidogo waliwafikia wenzao wakaungana nao,walishusha pumzi ndefu ya kutoamini kama wamefanikiwa huku mioyo yao ikianza kutulia taratibu,walijuta kwanini walibaki.

    Lile jitu lilitokomea,halikuonekana tena,halikujulikana lilielekea wapi!! Lilichokipanga hakikufanikiwa,wakina



    mama Halima waliponea chupuchupu watiwe kitanzini kama isingelikua hisia zao zilizowastua,hivyo nani anafuata?? Hiko kilikua ni kitendawili.

    Upande wa pili wa shilingi nyumbani kwa mzee Patili maongezi madogo madogo yalichukua nafasi,fahamu



    zilishamrudia mama Kadogo japokua majeraha bado mwilini yalimsumbua na pia vilevile kichwa kilikua kinamuuma,dawa alizopewa na yule mzee sio siri zilimsaidia vilevile mzee Otongo.



    Maongezi yao yaliokua yanaendelea yalishindwa kufikia hitimisho kwani kila walipojadili kuhusu vilivyotokea huko nyuma bado hawakupata jibu kwamba vimeishia wapi,ni ngumu kuamini kama lile jeshi limewaacha tu



    vilevile,walipata kidogo mashaka,walikua hawafahamu ya kuwa kuna mauaji yanaendelea kijijini,walikua hawajui kabisa juu ya hilo,walikua hawafahamu ya kwamba sasa jeshi la 666 limekuja kivingine!!

    Muda ulianza kuruhusu jua lizame,taratibu giza likaanza kuingia,wanakijiji kutokea kwenye mazishi walianza



    kuitia miguu yao ndani ya kijiji,mila zao na desturi haziruhusu kulaza maiti,hivyo mtu akifariki mapema tu anazikwa akapumzike kwa amani,kila mwanakijiji alielekea kwenye nyumba yake,tito aliekua yatima yeye alichukuliwa na mama Kurwa,mmama mmoja muongeaji sana mwembamba ambaye ni jirani yao,mama



    Halima na Julina moja kwa moja walielekea kwenye nyumba ya mzee Patili,kumpasha habari na kumchukua mtoto waliemuacha hapo kwa muda.Habari zile ziliwashtua sana! Mauaji ya watu wawili ndani ya kijiji kwa kunyongwa kilionekana kuamsha hisia ya kwamba ujio wa jeshi la 666 umewadia!

    Mama Kadogo na mzee Otongo pia walihisi vivyo hivyo!



    Upande wa pili mzee patili na wakina mama Kadogo walijisikia vibaya juu ya taarifa ya kuchomwa kwa nyumba za wakina baba Madhifa na walijiona wakosefu mbele zao.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ngo! Ngo! Ngo! Hodi iliita,mzee patili aliinuka na kwenda kufungua,alikua ni Khadhifa! Alikuja kumuita mzee patili akawasaidie kwani baba yao yupo kwenye hali mbaya!! Mzee Patili alishangazwa na zile habari na hasa alishangazwa zaidi baada ya kuambiwa hicho kitu kilijiri baada ya kuleta mwili wa mama yao waliokuta umenyongwa maeneo ya kisimani,haraka mzee Patili alichukua madawa fulani kisha mbio zikaanza kuelekea eneo la tukio!



    Kutokana na kaumbali kalichopo walichelewa,walipokaribia walisikia sauti ya kilio waliyoitambua ni ya Madhifa! Hofu zikajazwa mioyoni mwao! Nini tena hiki jamani?? Walijiuliza huku wakiongeza kasi!!



    kutokana na kaumbali kalichopo walichelewa,walipokaribia walisikia sauti ya kilio waliyoitambua ni ya Madhifa! Hofu zikajazwa mioyoni mwao! Nini tena hiki jamani? Walijiuliza huku wakiongeza kasi! Haraka waliingia ndani,mzee Patili bila kuchelewa alichukua madawa yake aliyoyabeba na kuanza shughuli ya kumpakaa dawa baba Madhifa alielazwa chini na kidogo alimmezesha kwa kumfungua kinywa,ilikua ni dawa ya kumrudisha kwenye fahamu,aliwaambia hivyo wakina Madhifa waliokua na hofu kubwa ya kumpoteza baba yao kama walivyompoteza mama yao,uzoefu wa mzee Patili kwenye yale matukio ulifanya jambo lisiwe gumu kihivyo,baada ya kupaka ile dawa aliwahitaji watulie ifanye kazi na baada ya muda kidogo itaonyesha matunda,aliutumia huo muda kwena kuangalia maiti ya mama Madhifa iliyokua imefunikwa gubigubi,ilimtetemesha mno na kumuogopesha,maiti ilikua haitamaniki na yenye kutisha kutokana na majeraha makubwa iliyonayo,shingoni kulikua na alama ya kamba iliyoashiria ya kwamba ilimkaba vilivyo,aliifunika kisha akayarushia macho yake kwa wakina Madhifa,hawakua na amani hata kidogo,roho ya chuki na kisasi ilichipukia mioyoni mwao,hofu ya kumpoteza baba yao na uchungu wa kumpoteza mama yao uliwafanya machozi yatiririke yakisindikizwa na kwikwi za kilio,aliwaonea huruma sana na kichwani akajiuliza leo hawa watoto watalala wapi?? Akatikisa kichwa kwa masikitiko kisha akaangalia anga lililokua kiza kuashiria giza lishaingia.

    Baada ya muda usiopungua robo saa baba Madhifa alianza kupiga chafya! Alirudi duniani!! Wakina Madhifa hawakuamini lile tukio,ilikua ni kama miujiza mbele ya macho yao!! Haraka walimkimbilia baba yao kwa kutaka kumjulia hali,tabasamu zilizoambatana na machozi zilionekana kwenye nyuso zao,walimkumbatia baba yao kwa nguvu huku wakilia! Walitia huzuni,mzee Patili nae chozi lilimshuka taratibu,lile jambo lilimgusa wake moyo.

    Hakukua na muda tena wa kupoteza,walifahamu hakuna msaada wowote wangeupata toka kwa wanakijiji na ukizingatia hawakuhuitaji hata kidogo,waliungana na wanakijiji wenzao na mzee Patili wakauzika mwili wa mama yao,hisia za kwamba alinyöngwa na wanakijiji zilifutwa baada ya mzee Patili kuwapa tahariri ya kua yale mauaji hayahusiki na mwanakijiji yoyote bali ni kwamba yanafanywa na jeshi la 666 lililowadhuru wale watu waliowaokoa japokua kwa kiasi kimoja yameleta mkanganyiko,hisia za uoga ziliwatetemesha na ukizingatia kwa ule usiku iliwabidi walale nje baada ya nyumba zao kuchomwa.

    * * * *

    pembeni ya nyumba ya mama Kurwa upande wa kushoto kulikua kuna mti mkubwa wa muembe ambao ukitoka huo nyumba ya mzee Yosso ndio ilikua inafuata,hali ya giza iliyokuwepo ilifanya mti ule kutoonekana vizuri na kutisha kidogo,pembeni yake alikua ameegemea mwanaume mmoja alieshikilia kamba mkononi akipiga mahesabu kichwani,ni lile jibaba pande la mtu lililowakosakosa wakina mama Halima,ni yule mnyongaji!!! Mungu wangu! Sasa lilikua ndani ya kijiji tena karibu na nyumba ya mama Kurwa na mzee Yosso au baba Matata,lilikua linafanya nini pale?? Hilo halikufahamika ila taratibu lilianza kujongea na kuusogelea mlango wa mzee Yosso au baba Matata,lilipokaribia liligonga mlango....ngo! Ngo! Ngo! Hodiiii! Kwa sauti ambayo haikuendana hata kidogo na mwili wake! Ilikua ni sauti ya kike tena ya mama Kurwa ambaye ni jirani!!... Karibuu! Alijibiwa tokea ndani,kwa kua halikua na lengo la kuingia ndani lilibakia pale nje likisubiri mlango ufunguliwe,mama Matata aliekua na mumewe ilihali na mwanae wakila ilimbidi ainuke taratibu na kuelekea mlangoni kumfungulia aliegonga,ni kosa kubwa alilitenda hakujua kama alipeleka nafsi yake kifoni!! Alipokwa kama pochi! Lile jibaba leusi kama giza lililokuwepo lilimbeba mama Matata na kuanza kupotelea nae maporini!! Makelele ya mama matata ya kuomba msaada yalisikika vizuri kutokana na utulivu wa mawimbi usiku hivyo kupelekea wanakijiji kushtushwa kwa kiasi kikubwa bila kusahau mumewe ambaye ndie aliekuwa wa kwanza kutoka nje kwa hamaki! Hakumuona mkewe! Alianza kukimbia kufuatilia sauti aisikiayo huku akiita jina la mkewe kwa nguvu! Ile sauti haikuskika tena! Ilitokomea na lile jibaba,ilitokomea porini!! Baba Matata hakuona kitu,mkewe akawa tayari ashakwenda!!

    Alieka mikono kichwani huku akilia kama mtoto,hakua na la kufanya aligeuza na kuanza kurudi kijijini kichwani mawazo yakimsonga na moyoni hofu ikimtinga!! Akili yake yote ikawa sasa ni kwa mama Kurwa kwani sauti ya yule aliekua anagonga ilikua ni yake,alikimbia,alipofika kijijini alikuta watu wameshajazana,sauti ya mama Matata iliwatoa majumbani mwao hasa ukizingatia hofu zao zilishawashwa tokea mapema siku ile,minong'ono ilitawala,baada ya kumuona baba Matata,walimfuata na kumuuliza kilichojiri,hakujibu kitu,alimfuata mama Kurwa huku akitoa macho,akauliza kwa ukali!

    "mke wangu yuko wapi???"

    huku akimnyooshea kidole! Mama kurwa alibanwa na kigugumizi,hakua na la kujibu! Ghafla mmama mmoja akaropoka..

    "jamani kuna mtu pale kwenye mti ananing'iniaa!!!"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alimnyookea moja kwa moja mama kurwa huku akitoa macho,kwa ukali akauliza!

    "mke wangu yuko wapi??"

    mama Kurwa alikosa cha kujibu,kigugumizi kilimbana,ghafla mmama mmoja aliropoka!

    "jamani kuna mtu ananing'inia pale mti!!!"

    Baba Matata aliachana na mama Kurwa na kukimbilia kwenye huo mti kushuhudia alichosikia,hakuamini macho yake kwa alichokiona! Alikua ni mkewe!! Alivishwa joho jekundu kitanzi kikimning'iniza! Damu zikiwa zinamtoka puani na masikioni! Aliishiwa nguvu za miguu akakaa chini na kuanza kulia!! Matata nae aliposhuhudia mwili wa mamaye unaning'inia katika ile hali kilio kilizidi kuchukua nafasi!! Baba na mwana wakawa wanalia kilio kilichoshindwa kutofautisha mkubwa na mdogo.Mwili wa mama Matata ulishushwa na kitanzi kikafunguliwa,wanakijiji walitawaliwa na hofu mara mbili ya ile iliyokuwepo mwanzoni,kushuhudia watu kunyongwa kwa siku mara tatu kama dozi haikua kitu cha kawaida,haikua kitu cha mzaha kabisa,ni kitu cha kuogopesha mno!! Kila mwanakijiji aliruhusu chozi la hofu na uchungu litoke huku wakiwa wanajiuliza mioyoni kwamba ni nani anaefuata sasa baada ya wale,miili ilikua inatetemeka na msamiati 'hamu ya kulala' haikua kabisa kwenye kitabu chao cha ile siku,nani alale kwa ile hali?? Hata mtu kukaa peke yake ilikua ni mtihani!!!

    Wakati baba Matata na mwanae wakiendeleza kilio baadhi ya wanaume waliokuwepo pale walijivuta pembeni na kuanza kuteta jambo,

    "sasa jamani ndio hivyo kama tunavyoona,tunazidi kutokomea! Sasa tunafanyaje sisi kama wanaume??"

    alieleza mzee Rama,baba wa watoto saba akaae nyuma ya nyumba ya mama Kurwa,alikua ni kiongozi mkubwa wa kuwashawishi wanakijiji wakachome nyumba za wakina Madhifa,

    "mh kusema ukweli hata mie naogopa hapa nilipo,ujue hiki kinatisha!"

    "ah-ah! Kila mtu anafahamu kuhusiana na hilo,sisi kama wanaume tumejivuta pembeni ili tuangalie ni jinsi gani tutakavyolikabili,hatuwezi tukakaa tu hivi,tutakwisha!"

    Mzee Rama alimdadavulia Tambwe alieonekana kutia mushkeli,

    "kusema ukweli hili jambo si la mchezo hata nukta,mimi nadhani ya kwamba si binadamu wa kawaida anaefanya haya!...Nilisikia kwa masikio yangu sauti ya mama Matata ikielekea msituni lakini cha kushangaza tumemkuta kaning'inizwa kwenye ule mti!!"

    mwalimu Baraka alichangia huku akiunyooshea kidole ule muembe,

    "hata mie nahisi hivyo,hiki kitu kitatuwia vigumu sana,kumdhibiti mtu asiye wa kawaida yataka moyo ukizingatia hatujui hata yupoje!"

    mzee Rama alisema,Lutiko aliekua kimya nae akachangia baada ya mzee Rama

    "mi nadhani mtu mkubwa ataetusaidia ni mzee Patili,yeye ana ujuzi na haya mambo!"

    "ni kweli! Hilo wazo zuri,nadhani mnaelewa ya kwamba nyumba ya mzee Patili ipo mbali na za kwetu na hata yaliyojiri hapa bado hayafahamu,sasa inabidi tumjuze!"

    wazo hilo lilionekana kuungwa mkono na wale waume,kazi ikawa ni nani atakaejitolea kwenda kumpa taarifa mzee Patili,kila mtu alikua anahofia kwenda kule kwa kale kaumbali mwenyewe ilikua ni kama kujitoa sadaka,hakuna alietaka,kila aliechaguliwa aliuliza kwanini mimi?? Hivyo ikawa ngumu kufikia hitimisho.

    Wakati hayo yanachukua nafasi Matata aliufata mwili wa mama yake na kuanza kuuangalia kwa kutoamini huku machozi yakimtoka,alijiuliza juu ya ile nguo aliyovishwa mama yake hakupata jibu,kuna kitu aligundua kwenye ile nguo haraka akaita Babaaa!! Sauti iliyowastua na kuwateka hisia wanakijiji wengine,baba Matata bila kuchelewa alifika eneo aliloitwa na mwanae akauliza

    "nini mwanangu??"

    huku macho yakiwa mekundu kama nyanya kwa kulia,

    "kuna kitu kimeandikwa kwenye hii nguo aliyovalishwa mama!!"

    "nini tena hiko??"

    aliuliza Baba Matata,kutokana na kutojua kusoma aliamuru mwanae amsomee,matata akasoma kisha akasema..

    "imeandikwa BADO KIDOGO!!!"

    * * * * *

    Baada ya shughuli ya mazishi kuchukua nafasi ilimbidi mzee Patili afunge safari ya kurudi kwake,aliwaaga wakina Madhifa waliokua wanatayarisha tayarisha kwa ajili ya usiku ule,walimshukuru kwa msaada na pia vilevile aliwahaidi atakuja kesho kuwasaidia shughuli za ujenzi,walifurahi kusikia hilo ila bado nyuso zao zilishindwa kujifungua kwa furaha,mioyo yao bado ilikua na huzuni.

    Ilikua ni tendo la ajabu kwa mzee Patili kuondoka na kuelekea nyumbani mwenyewe kwa ule muda ukizingatia vitu vya kutisha vilivyochukua nafasi kijijini,alikua na hofu lakini hakutaka iwe sababu ya yeye kubaki,aliamini kama siku imewadia hawezi likwepa hilo,mikono aliweka nyuma na kwa kasi kidogo alikua anatembea akipita miti na vichaka huku sauti za wadudu wa usiku zikigota masikioni mwake na kumfanya ageuke geuke mara kwa mara,baada ya muda kidogo alikaribia na kwake,macho yake aliyoyarusha mbele yalimruhusu aione nyumba yake ya udongo vizuri,ghafla alisimama!! Macho yake yalimshuhudia pande la mtu likiwa linasogelea mlango wake na mkononi akiwa na kamba,hofu ikagota moyoni,mtu yule alikua mgeni machoni mwake na alihisi vibaya juu yake,akasogea karibu huku akinyatanyata aweze kumuona vizuri,mara lile jitu likagonga hodi Na mtindo ule ule alioutumia kwa mama Matata!!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akasogea karibu huku akinyata aweze kumuona vizuri,mara lile jitu likagonga hodi kwa mtindo ule ule alioutumia kwa Mama Matata! Nini hiki? Alijiuliza mzee Patili,kutokana na uoga wa watu waliokuwepo mule ndani tendo la kufungua mlango lilichukua muda,mama Kadogo na mzee Otongo hawakuweza kufungua



    kutokana na miili yao yenye majeraha na maumivu kutowaruhusu,mama Halima na Julina walio wazima walikua na hofu hivyo kufanya lile zoezi lichukue muda kutendeka,lakini lile jibaba lililokuwepo mlangoni lilihisi kitu,lilipepesa macho yake huku likinusanusa na kugundua jambo,lilisikia harufu ya binadamu hivyo likafahamu ya kuwa haliko peke yake pale nje,haraka lilitoweka! Mzee Patili alijitahidi kufikicha zake mboni



    lakini hakuona kitu! Alishangazwa mno na lile jambo,haraka alikimbia mpaka mlango ulipo na kuanza kubisha hodi huku akitamka kwamba yeye ni mzee Patili! Maswali na hofu yalijazana vichwani mwa waliokua ndani,mara ya kwanza walipoisikia hodi iliambatana na sauti ya kike ila sasa hivi wanaisikia sauti ya kiume tena ni ya mzee Patili! Walisita kufungua.



    Tendo la busara lililofanywa na mama Halima la kuchungulia dirishani ndilo lililowashawishi kumfungulia mzee Patili baada ya kugundua ndie,aliingia ndani na kuwaeleza yote aliyoyashuhudia tokea alipotoka mpaka alipomuona lile jitu mlangoni,walishtuka sana na vilevile walishukuru hawakuifungulia hodi ile kwani ingekua



    ni hadithi nyingine sasa hivi,mzee Patili alizidi kulielezea lile aliloliona..

    "yule mtu alikua ameshikilia kamba nyekundu! Na hasa zinafanana na zile zilizotumika kuwanyongea wakina baba Tito! Hicho kitu kilinishangaza sana!"

    "mungu wangu! Jamani tuhame hiki kijiji tutakwisha!"

    kiuoga alinena Julina akiwa anamnyonyesha mwanae,

    mama Kadogo akasema,

    "sidhani kama hilo ni suluhisho,kila tutakapoenda watatufata mpaka pale watakapohakikisha ya kwamba lengo lao limefanikiwa!"

    kauli ile iliwashtua mama Halima na Julina waliokua hawajui kiendeleacho,haraka wote wakauliza

    "lengo! Lengo gani hilo??"

    mama Kadogo akazidi kunyumbua,



    "haya mambo yote yajiriyo ndani ya kijiji chenu yalitokea vilevile kijijini kwetu Igesambo,watu wetu wengi wa karibu wameuwawa na wengine wamejiunga kwenye jeshi la 666 lililo na itikadi moja tu ya kuusambaza utawala wa Ibilisi wao alieingizwa duniani,ilibidi tukimbie kuokoa maisha yetu kwasababu hatukutaka abadani kuungana na mashetani wale,lakini kuonyesha ya kwamba mungu yu upande wetu,alizaliwa mwana mwingine! Mwana ambaye ndie tumaini letu na vilevile anaweza akawa kifo chetu!"



    "nani huyo??"

    Julina aliuliza kwa papara huku akimtizamatizama mwanae,

    mama Kadogo akaendelea,

    "huyo mtoto ndie hasa lengo la hawa watutafutao na watuuwao,namaanisha jeshi la 666 kwani ni hatari kwao na huyo mtoto ndie hasa yatubidi tumlinde kwa hali zote kwani ndie tumaini na mwanga wetu,tukimruhusu afe,tumeruhusu utawala wa kiza!"

    mzee Otongo nae akadakia



    "mtoto huyo ana alama kwenye paja lake la kushoto kwa chini,alama ya nyota!"

    mama Halima na Julina walishtushwa na ile kauli! Kwani mtoto yule alikua na hiyo alama! Macho ya Julina yakatoka kwa uoga! Huku akitetemeka akasema

    "haiwezekani!! Ah-ah! Haiwezekani jamani,haiwezekani!!! Mtoto wangu! Hapana!"

    * * * *



    Bado wanakijiji walikua wamekusanyana mbele ya nyumba ya mama Kurwa na baba Matata,hakuna hata mmoja alieonekana na dalili wala hamu ya kurudi kwenye viota vyao na kulala,hali ilikua tete mno mioyoni mwao! Mada kubwa iliyokua inaongelewa ni juu ya ule ujumbe uliokutwa kwenye lile joho alilovishwa mama Matata baada ya kunyongwa uliosomeka BADO KIDOGO!! Hawakuelewa ulikua unamaanisha nini? Kila mtu alisema yake juu ya hilo.



    Kutokana na hofu kulowanisha nafsi zao waliamua kukaa pale pale mpaka usiku utakapokwisha na kuiona adhuhuri,hawakua na lingine la kufanya zaidi ya hilo waliloona ya kwamba ni salama kwa maisha yao.Baba Matata na mwanae walikuwepo sebuleni,huzuni iliwafanya wakose cha kusema na kuwa kimya,ilikua ni



    ngumu bado kuamini ya kwamba mtu waliekua nae muda si mrefu ni marehemu sasa hivi! Baba matata aliona mzigo wa majukumu waongezeka,Matata mwenye miaka tisa bado alikua anahitaji malezi ya mama yake na ukizingatia yeye si mkaaji nyumbani,kichwa kilivuruga.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ghafla upepo mkali ulipiga lile eneo!! Upepo usio wa kawaida kabisa!! Vibatari vilivyokua vinatoa mwanga vyote vilizima na kufanya giza totoro kushika hatamu!! Wakina mama walipiga makelele ya uoga na kila mtu hofu iliita ndani yake! Miili ilitetemeka kwa uoga,mioyo ilizizima kwa hofu!!



    Mchakato wa kuwasha vibatari ulipofanikiwa watu wawili hawakuonekana!! Hawakujulikana walielekea wapi...hawakujulikana walibebwa na nani!! Mtoto mmoja wa mzee Rama na mmama mmoja wa makamo walishabebwa!!!

    Mungu wangu! Sauti zao zilisikika zikiishilia kama ilivyokua kwa mama Matata!!

    Matumbo yalichemka,jasho liliteremka!! Wengine walizirai kwa uoga,na wengine walitamani kujimaliza!!!!



    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog