Search This Blog

NILIONGEA NA SHETANI ILI NIWE TAJIRI - 1

 





     IMEANDIKWA NA : STALLONE JOYFULLY





    *********************************************************************************





    Simulizi : Niliongea Na Shetani Ili Niwe Tajiri

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    wazazi waliniita Bella, shuleni nikajiita Bianka. Nilitunukiwa tunu ya urembo, yaani urembo haswa. Hapo mwanzo nilikuwa nikichukia macho ya wavulana waliokuwa wakinitazama kwa uchu. Ndio, nilifahamu ulikuwa ni uchu, kwa kuwa sikuwa najitambua wala

    kupevuka bado. Kioo changu mwenyewe pia sikukiamini kila nilipojitazama. Ni wachache walionifuata na kuniambia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Bella wewe ni mrembo uliyependelewa"

    hiyo ndio sababu ya kushinda kwenye kioo na kuutazama

    huo uzuri. Muda mwingine nilikaa nikijiuliza "inawezekana

    wanataka kunichezea? Huo uzuri uko wapi sasa?"

    nilicheka kidogo nikajigeuza geuza, nisione jinamizi lolote

    lililofanana na kitu kinachoitwa uzuri.

    Nikakiacha kioo na kukirudia kitabu changu. Ndipo

    nilisikia sauti ya mama, akiniita kutoka nyuma ya mlango

    wa chumbani nilioufunga. Kumbe mama alikwisha gonga

    sana mlango ila mimi sikusikia. Kitabu kilichoitwa KIVULI

    CHEUSI kiliuteka ufahamu wangu. Nilipenda sana simulizi

    za huyu kijana mwenye njaa, hata anaandika vitu

    vinavyogusa na kusisimua, Stallone joyfully. Niliendelea

    kusoma kitabu nikidhani huenda labda akiwa ananihitaji

    sana ataendelea kuniita mara ya pili. Aliita mara ya tatu

    ndipo na mimi nikaupata ulimi wangu.

    "bee mama"

    Nilinyanyuka na kwenda kuufungua mlango.

    Nilipoufungua, na kuutoa uso wangu. Nilikutana na uso

    wa mama ulioghafirika. Mama aliniangalia kwa dharau

    kabla ya kusonya. Sikujali kwa kuwa nilikwishamzoea.

    Mama yangu, alikuwa ni mama mwenye mashushu na

    ngebe za hapa na pale. Kwa mtu usiye mzoea utashangaa

    na roho yako. Aliingia ndani moja kwa moja na kwenda

    kukaa kwenye kitanda changu. Kama kawaida yake

    alianza kuniambia.

    "mwanamke mchafu wewe!" Nilicheka tu sikuongea

    chochote. Nilipokuwa nafunga mlango nikimfuata alipo,

    aliniambia. "yaani embu tazama kitanda kilivyo" aliinua

    ipod yangu, akakiinua kitabu nilichokuwa nasoma

    akairudia sauti yake "..yaani hata hakieleweki"

    Niliendelea kunyamaza nikitabasamu. Nilijua tu kuna

    jambo analotaka kunieleza, hivyo sikuwa na haraka

    niliendelea kumsubiri. Alianza.

    "mwanangu umekuwa"

    alikuwa akinisahili kuanzia juu mpaka chini, akanifanya na

    mimi nianze kujitazama.

    "miaka kumi na sita si midogo haswa uzuri ulio nao"

    nilishituka niliposikia neno hilo kutoka kwa mama, pia

    sikujibu kitu. Kisha aliendelea "mwanangu kuna jambo la

    muhimu nataka kukueleza ili ulifahamu kabla sijafa"

    "kufa!?" niliropoka kimoyomoyo. kiukweli mama

    alinichanganya sana, sikujuwa alikuwa na maana gani.

    Sikuweza kuongea chochote kwa kuwa sikuwa na lolote la

    kumwambia au kumuuliza. Nilihisi machozi yalitaka

    kunitoka. Lakini sikujuwa sababu ya mimi kutaka kulia.

    Nilimpenda sana mama yangu. "Ndiyo", nilikuwa na baba

    ila mama yangu ndiye alikuwa rafiki yangu wa karibu.

    Baba hakunijali kama alivyonijali mama. Nilikaa

    nikimsikiliza kwa makini alichotaka kuniambia. Aliniambia

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mwanangu, usikubali hata siku moja kuwa mchawi. Babu

    yako alinilazimisha kunirithisha mikoba yake, nikakataa.

    Amedai kuwa mizimu imekupenda. Yupo katika harakati

    za kuniua kwa sababu ya kumpinga wewe kuwa mchawi"

    Niliumizwa sana na taarifa hiyo. Mama alikuwa akiongea

    huku machozi yakimtoka.

    Nilimbembeleza mama huku nikimuhakikishia kuwa siwezi

    kuwa mchawi.

    Mama aliniambia.

    "mwanangu muheshimu sana huyu mzee unayeishi naye"

    nikamuuliza "mzee? Mzee yupi!?"

    Sikuweza kutambua kama alikuwa akimzungumzia baba.

    Aliniambia

    "Mzee Nyegezi, si baba yako, Bella. Ni mwanaume

    aliyeyaokoa maisha yangu baada ya mume wangu wa

    kwanza kutolewa kafara na babu yako"

    Nililia sana. Nililia kwa uchungu kwa sababu sikujua

    kama, babu yangu angekuwa na roho ya kinyama kiasi

    kile. Amuuwe mwanaye kwa sababu ya uchawi? Kafara?

    Kwa faida gani? Unyama ulioje? Nilimchukia babu kwa

    kuninyima haki ya kumjua baba yangu na mimi kulelewa

    na baba wa kambo.

    Mama aliniambia

    "mwanangu, mzee Nyegezi atakulea vyema kama baba

    yako mzazi. Nina uhakika sina siku saba zaidi duniani,

    lakini nitakapokufa usisahau kusoma kwa bidii na

    usikubali kuwa mchawi" Mama alinyanyuka na kuondoka.

    Nilichokuwa nikisoma kikatumbukia nyongo hata wimbo

    wa Ben Paul haukuwa mtamu kama nilivyokuwa

    nikiupenda siku zote. Niliitupa ipod yangu mbali na

    nilipolala, nikapitiwa na usingizi ulioletwa na kulia sana

    .............................

    Niliamshwa na upepo mkali uliovuma chumbani kwangu.

    Upepo niliodhani huenda ungeezua hata paa la nyumba

    yetu. Muda mwingine nilihisi kitanda nilichokilalia, kama

    kilikuwa kinabebwa. lakini hiyo ilitokana na nguvu ya

    upepo. Nilipotaka kupiga kelele za kuomba msaada,

    nilijifahamu kuwa napiga kelele kwa sauti ya juu, lakini

    sauti yangu mwenyewe sikuisikia. Jasho jingi likanitoka.

    Macho yakanitoka pima kwa uoga. Ile hali ilipotulia,

    nilitaka kunyanyuka; lakini sikuweza kusogeza hata

    kidole. Nikasikia sauti ya kicheko, kikicheka kwa dharau.

    Kicheko kilikuwa ni kicheko cha sauti ya juu sana.

    Nikaangalia mlangoni labda alikuwa ni mama, lakini

    hakukuwa na mtu. Machozi yalinitoka kwa uoga. Sauti ile

    ikacheka zaidi na kujirudia rudia kama mwangwi katika

    chumba changu. Hatimaye nikauona moshi mweusi

    ukitanda kutoka katika paa na kushuka mpaka usawa wa

    kitanda. Mbele yangu akasimama mwanaume ambaye

    sikumfahamu kabisa. Alikuwa amejifunga sanda nyeupe

    na kuonekana macho na pua. Puani aliwekwa pamba,

    mdomo ulikuwa hauonekani. Aliongea na mimi kwa sauti

    iliyokuwa ikijirudia rudia.

    "Bella lazima urithi lazima urithi mikoba"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kisha alisonya, sonyo lililonifanya nipige kelele kwa nguvu

    mpaka niliamka. Kumbe nilikuwa nimelala. Nilijikuta

    nikiwa mapajani kwa mama akinifuta jasho lililolowesha

    gauni yake aliyovaa. Aliniuliza "babu yako alikuwa

    anasemaje"

    nilishituka, kwa kuwa nilijua fika nilikuwa ndotoni. Sasa

    mama alijuaje? Nilihisi huenda mama alimuona babu.

    Nikamuuliza "mama umejuaje kama ni babu na mimi

    nilikuwa naota?"

    mama alinicheka kama niliyekuwa nikichekesha.

    Aliniangalia baada ya kusikitika na kuniambia.

    "mwanangu nafahamu yote"

    "unafahamu!?" nilishangaa

    "ndiyo" akanijibu

    "unafahamu nini?" nilimuuliza huku nikiwa ninakaa kitako

    kumsikiliza.

    Aliniambia kuwa alipokuja kuniamsha ili nikale chakula

    cha usiku, aliniona nikiweweseka. Akaja na kukipakata

    kichwa changu huku akiniombea. Ndipo akaisikia sauti ya

    babu ikiniambia "lazima niirithi mikoba" Aliisikia sauti ya

    babu katika ulimwengu wa roho. Nililia sana, huku

    nikimwambia mama kuwa sitaki kuwa mchawi. Mama

    alitabasamu na kuniambia

    "nakuombea Bella msimamo wako uwe hivyo hivyo"

    tulienda sebuleni kupata chakula cha usiku, kabla ya

    kulala tena mpaka kesho siku nyingine mpya. Baada ya

    kumaliza kula, nilimuomba mama aniombee kabla ya

    kwenda kulala. Tuliomba kwa muda mrefu sana. Mama

    alivunja nguvu za giza zote na uchawi wa babu yangu.

    Wakati nikiwa nimefumba macho, nilishituka kuhisi mama

    amenyamza ghafla. Nilipofungua jicho langu moja kwa

    kuibia, nilimuona mama kaanguka chini. Niliogopa. Mama

    alikuwa anatoa mapovu mdomoni na akigalagala pale

    chini kama mwenye degedege. Nilimuita baba, Mzee

    Nyegezi. Alikuja na tukasaidiana kumpeleka hospitali.

    Ulikuwa ni usiku mkubwa, hivyo ilikuwa rahisi kwetu

    kufika mapema na kupewa matibabu haraka. Baada ya

    daktari kumchukua na kuanza kumshughulikia mama,

    zilipita dakika 30 mpaka alipotoka.

    "anaendeleaje!" baba alimuuliza

    "nifuateni ofisini" Tulimfuata ofisini huku tukiwa na

    asilimia chache za mama kuwa mzima. Niliogopa sana.

    Tukiwa katika chumba cha daktari. Mimi jasho jingi

    lilikuwa likinitoka. Kiukweli sikuwa tayari kupokea habari

    za msiba wa mama. Baada ya daktari kumaliza kuandika

    vitu fulani katika kadi kadhaa zilizotapakaa katika meza

    yake, aliinua uso wake baada ya kikohozi kifupi kumpitia.

    "poleni sana" alisema

    mapigo ya moyo yalinilipuka na kwenda kasi sana.

    Yalienda mara tatu zaidi ya kasi ya kawaida. Nilihisi

    machozi yakianza kustahimili uvumilivu wake na kutaka

    kuniponyoka. Daktari aliendelea "ndugu yenu, amepatwa

    na homa kali sana lakini ni mzima. Tumemuwekea dripu

    ya dawa hivyo kesho asubuhi muje kumtazama

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    anaendeleaje. ila kama mngechelewa? Angekuwa katika

    hali mbaya zaidi ama mngempoteza kabisa" daktari

    akaturuhusu kuondoka. Kiukweli niliona kama muujiza

    mama kupona. Moyo wangu ukiwa na amani sasa na

    furaha. Tulikuwa njiani tukirudi nyumbani mimi na baba

    ndipo tulimuona mtu kasimama kando ya barabara.

    Alitupungia mkono. Baba alisimamisha gari na kumpa lift

    yule mtu. Baada ya kuingia ndani ya gari, alitusalimu.

    Baba aliendelea kuendesha gari kwa mwendo wa

    kawaida. Yule mtu tuliyempakia alikuwa mwanaume.

    Alikuwa muongeaji sana. Muongeaji mzuri aliyeleta

    mazungumzo ya hapa na pale

    "poleni na mgonjwa" Ghafla alituambia. Nilishituka sana.

    Nilishituka kwa kuwa hakuna ambaye alimwambia wapi

    tumetoka. Mimi sikuzungumza chochote, lakini kwa

    mshituko mkubwa, baba alisimamisha gari ghafla na

    kumuuliza

    "wewe umejuaje?" yule mtu tuliyempakia alijichekelesha

    bila sababu na kutuambia.

    "sikiliza mzee Nyegezi" moyo ukanilipuka kama ulitaka

    kunyofoka kifuani. "amelijuaje pia jina la baba?" likawa

    swali kichwani kwangu; lililokosa majibu. Nilibaki

    nikimsikiliza. Baba naye alimsikiliza macho yakimtoka

    kwa bumbuwazi.

    "nafahamu kila kitu kuhusu mama yake Bella" alinyamaza

    huku akiniangalia mimi siti za nyuma nilipokuwa nimekaa.

    "ubishi wake unamponza ubishi utampokonya maisha

    yake anayoyaringia ubishi unaweza kumletea matatizo

    makubwa katika kizazi chake na Bella" moyo wangu

    ulinienda mbio sana mwili ulininyong'onyea nikapoteza

    nguvu. Nilifikiri sana mtu huyu wa ajabu, alitujua vipi na

    kufahamu fika siri za familia yetu. Kicheko kikamlipuka na

    kurudia rudia kama mwangwi, kisha alisonya kabla ya

    kutoweka na kutuachia moshi mzito mweusi ndani ya

    gari. Sikujuwa nilifikaje nje ya gari, wala sikukumbuka

    kilichotokea. Nilijikuta katikati ya barabara nikikimbia

    kuliko kawaida. Mara chache nilistahimili kujikwaa

    nilipokuwa nikifanya uzembe wa kutazama nyuma, ndipo

    nilimuona baba naye akinijia mbio. Aliniita baada ya

    pumzi kumuishia akiwa amechoka hoi. Nilisimama na



    kurudi alipo

    "baba gari tumeiacha wapi..." sikujuwa tulikimbia umbali

    gani hivyo hata gari sikuiona. Baba alikuwa amechoka

    haswa, ilimbidi akae chini.

    "gari.. Gari ipo... ipo.. Kule" alikuwa amegeuka na

    kunionyesha tulipokuwa tumetoka, ndipo gari ilikuwepo.

    Baba akanishauri tupumzike kwanza. Baada ya dakika

    chache tulirudi nyuma lilipo gari. Milango ilikuwa wazi na

    taa zikimulika huku likiwa limewashwa "hukuzima?"

    nilimuuliza. "wewe unajitambua ulitoka vipi"

    Tulicheka kwa pamoja na kuingia ndani ya gari,

    tukaondoka kurudi nyumbani. Safari ilikuwa fupi tuliongea

    mengi ya hapa na pale tukicheka pamoja. Nilipokuwa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nikiingia chumbani kwangu, baada ya kufika nyumbani;

    baba alinishika mkono na kuniambia.

    "Hivi bella unafahamu wewe ni binti mrembo sana?"

    Baba alinishangaza sana. Sawa nilishaambiwa hata na

    mama, nilianza kuuhisi urembo wangu pale nilipokuwa

    nikicheka mbele ya kioo na pia rafiki zangu walinihusudu

    sana na kutamani wangekuwa kama mimi. Iweje baba

    anishike matiti yangu na kunitomasa kiuno changu? Hapo

    ndipo nilipoipata ile nguvu ya kuuputa mkono wake na

    kuutoa kiunoni mwangu.

    "baba nakuheshimu kama baba yangu"

    neno hilo likaniponyoka. Nilishuhudia mshangao wa

    kuigiza katika uso wa Mzee Nyegezi. Sikujali niligeuka na

    kutaka kuingia zangu chumbani. Alinishika tena mkono na

    kuniambia

    "hivi kama mama yako ameshakuambia, mimi si baba

    yako mzazi; huoni kama hakuna kinachotuzuia sisi kuwa

    wapenzi?" Alikuwa akicheka cheka kicheko kilichouudhi.

    Alinisogelea na kuanza kunitomasa tomasa na mdomo

    wake kuanza kuunganisha na papi zangu akiwa na nia ya

    kutaka tubadilishane mate. Nilirudi nyuma baada ya

    kumzaba kibao na kumuacha akiugulia maumivu na mimi

    niliingia ndani haraka. Niliufunga mlango kwa ufunguo

    nikimuacha nje akiropoka ropoka "mshenzi wewe huna

    adabu nimekulea mimi siku zote leo unanivunjia adabu

    mimi? Unanipiga kibao? Nitakuonesha mwanaizaya wewe"

    alipotelea chumbani kwake huku akiendelea kubwatuka



     "Baba nakuheshimu kama baba yangu"

    neno hilo likaniponyoka. Nilishuhudia mshangao wa

    kuigiza katika uso wa Mzee Nyegezi. Sikujali niligeuka na

    kutaka kuingia zangu chumbani. Alinishika tena mkono na

    kuniambia

    "hivi kama mama yako ameshakuambia, mimi si baba

    yako mzazi; huoni kama hakuna kinachotuzuia sisi kuwa

    wapenzi?" Alikuwa akicheka cheka kicheko kilichouudhi.

    Alinisogelea na kuanza kunitomasa tomasa na mdomo

    wake kuanza kuunganisha na papi zangu akiwa na nia ya

    kutaka tubadilishane mate. Nilirudi nyuma baada ya

    kumzaba kibao na kumuacha akiugulia maumivu na mimi

    niliingia ndani haraka. Niliufunga mlango kwa ufunguo

    nikimuacha nje akiropoka ropoka "mshenzi wewe huna

    adabu nimekulea mimi siku zote leo unanivunjia adabu

    mimi? Unanipiga kibao? Nitakuonesha mwanaizaya wewe"

    alipotelea chumbani kwake huku akiendelea kubwatuka

    ___________



    Niliamka asubuhi na mapema kwenda hospitali. Sikuona

    umuhimu tena wa kumsubiri baba ikiwa ameanza

    kunivunjia heshima. Amenivunjia heshima ya kunitaka

    kimapenzi. Nilipanda daladala, kwa mwendo mrefu

    ulioongezwa na msongamano, lakini nilifika. Mama

    alikuwa ameamka, amekaa katika kitanda alicholazwa.

    Baada ya salamu aliniuliza kiuchovu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "baba yako yuko wapi!?" sikumjibu. Sikujuwa cha kumjibu,

    kwa kuwa sikutaka mama atambue yaliyotokea jana

    usiku. Nilimpa uji niliotayarisha asubuhi. Aliunywa vibakuli

    viwili na kutosheka. Aliniuliza tena. "ina maana baba yako

    hajui kuwa nipo hospitali?"

    nilimjibu "atakuja baadaye mama. Huenda yupo njiani"

    mama akaniuliza tena "babu yako jana ulimuona tena?"

    Nilimuhadithia yote kuanzia yule mtu aliyepewa lift na

    baba na yote yaliyotokea na kutuambia kuhusu yeye

    kukataa mimi kurithi mikoba ya babu. Mama naye

    akaniambia

    "jana usiku hospitali nzima iliona cha moto. Hapa

    yenyewe leo nimelazimika kupewa discharge kutokana na

    mauzauza yaliyokuwa yanatokea jana, yaani ni makubwa"

    mama akaanza kunihadithia "Mwanangu jana wakati babu

    yako anakuja alianza kuja katika umbile la mnyama" Mimi

    mwili ulinisisimka na vinyweleo kunisimama. Ni nani

    ambaye asingeogopa kusikia binadamu kawa paka?

    Binadamu kuwa mnyama? Ni jambo la kushangaza.

    Mama aliendelea "muuguzi mmoja aliyekuwa

    akinihudumia alimpiga teke yule paka mwenye rangi ya

    kijivu. Mimi sikuwa na habari kama yule alikuwa babu

    yako. Alipomaliza kunifunga dripu ghafla alianza

    kulalamika maumivu ya mguu. mguu ukazaa kichwa.

    kichwa kichwa, kikazaa mauti ya ghafla" mama

    alinyamaza kuruhusu pumzi ya kumeza mate. Mimi

    nikabwatuka

    "akafa? Mbona ghafla? Ilikuwaje?" mama alicheka

    akaniambia

    "mwanangu uchawi upo na una nguvu sana usipokuwa

    mcha mungu. Nakumbuka yule muuguzi niliyemtambua

    kwa jina la Rebecca wakati anampiga teke yule paka

    aliropoka jambo" mimi nilikosa ustahimilivu, nikaropoka

    tena "alisema nini?"

    mama alitabasamu tena na kuniambia "usiwe na haraka

    Bella ni hivi alisema 'hawa paka wengine ni wanga' Mimi

    sikutilia maanani kwa kuwa nilimchukulia yule paka kama

    mtu wa kawaida. Mara nilishangaa hospitali nzima ilijaa

    paka wa kila aina. Madaktari na wagonjwa wenye nafuu

    walijaribu kuwafukuza, lakini hawakufanikiwa. Paka hao

    walikwishawauwa wagonjwa wawili na daktari mmoja.

    Wale waliokuwa wanapambana na wale paka walikimbia

    hovyo na wengine kuvunjika miguu. Kuna wengine

    walionusuru roho zao. Lakini kati ya wale paka alijitokeza

    paka wa kijivu yule aliyemuuwa muuguzi Rebecca na

    kusimama karibu na kitanda changu" mimi macho

    yakanitoka pima, nikamuuliza mama "sasa ulifanyaje"

    mama aliendelea "nywele zilinisimama kama nimepigwa

    na shoti ya umeme basi yule paka alijigeuza na kuwa

    katika umbile la binadamu mbele yangu. niliogopa sana.

    nilimsihi kwa machozi tele asinidhuru wala kuitoa roho

    yangu. alikuwa ni babu yako Mzee Matonde. alicheka

    sana na kuniambia, 'sijaja Kuitoa roho yako wala

    kukudhuru. hili ni onyo la mwisho acha kumkataza Bella

    kuirithi mikoba yangu'. kisha alinikumbusha ni jinsi gani

    alivyoila nyama ya mwanaye wa kiume ambaye ni baba

    yako. Pia kilikuwa ni kifo cha ghafla cha kuanguka bafuni.

    Baba yako aliumia mguu tu. Mguu ukaoza ukaanza kutoa

    harufu kali ya uvundo uliokera. Tukaliuza shamba la

    mihogo, alipe pesa ya kitanda cha hospitali, pesa

    hazikutosha. Akanishauri na kuniambia nisiliuze lile la

    michikichi na fenesi kwa kuwa alishajua.

    "umejua?" nilimuuliza mume wangu "umejua nini?" "baba

    anataka kuniua"alipumzika baada ya kumeza donge zito

    la uchungu. Chozi likamponyoka, likanyang'anya furaha

    yake "najua atamsumbua mwanangu Bella lakini

    nakuomba sana usiache kumuongoza mtoto wetu katika

    maombi" mume wangu hakusubiri hata nimfute chozi kwa

    kiganja changu wala hata hakutaka kuniaga, aliondoka

    kimya kimya. Ukimya ulioniumiza na kunifanya nilie sana

    na kusimama na msimamo wa kukataa kurithi mikoba ya

    babu yako. Mzee Matonde alikuja siku moja nikiwa Eda

    aliniambia kuwa 'nyama ya Jose tamu sana' nililia kwa

    uchungu lakini sikuwa na la kumjibu. Alitokomea

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alikokujua akicheka kifedhuli. Baada ya miaka mingi ndiyo

    akarudi tena, aliniambia asingeshindwa kuitafuna mifupa

    yangu kama nitaingilia harakati zake kama nilivyoingilia

    kwa baba yako na kumsababishia kifo mume wangu.

    Wakati Mzee Matonde anajaribu kunitisha, wale paka

    waliyekuja na babu yako walitokezea na maiti za watoto

    wadogo ambao walizaliwa kabla ya siku zao. sikujua nia

    na madhumuni ya kuzichukua maiti zile. Babu yako alirudi

    katika umbile la paka na kutoweka machoni mwangu

    katika hali ya kufumba na kufumbua" wakati mama

    anamaliza kunihadithia yaliyotukia jana, baba aliingia

    akiwa na tabasamu la kuudhi. Mimi sikumjali akili yangu

    ikawa imezama katika hadithi hiyo ya kusisimua hadithi

    iliyonitingisha moyo wangu na kuanza kuogopa.

    "Bella kumbe upo huku"

    "niliamua kuwahi kumletea mama uji" nilimjibu kwa

    karaha, kisha nilitoka nje. Baada ya muda mfupi naye

    alitoka na kunieleza

    "nimefurahi kwa kuwa, umenionesha umeanza kukuwa.

    Hukumueleza kabisa kuhusu yaliyotokea jana? inabidi

    nikupatie zawadi" sikumjibu. Japo yeye alicheka, mimi

    nilinuna. Alielekea ofisini kwa daktari kulipia gharama za

    matibabu ya mama, kisha tuliruhusiwa kurudi nyumbani.

    mama alitakiwa apate muda mwingi wa mapumziko na

    azimalize dawa zake za kunywa zitakazomsaidia

    kuongeza damu, kutokana na upungufu wa damu alio

    nao. Tulirudi nyumbani nikiwa na furaha ya mama kupata

    nafuu. Mama alionekana akiwa na huzuni, mzee nyegezi

    akiwa amepambwa na tabasamu la kishetani usoni

    mwake.

    Siku zikapita mpaka afya ya mama ilipotengemaa. Mimi

    sikuona mauzauza yoyote tangu siku ile, mpaka leo siku

    ya nane. Nilimuuliza mama "mama au babu kaamua

    kutusamehe"

    "we Bella omba Mungu tu mwanangu" mama aliamua

    kunijibu kiuchovu. Nilicheka kicheko kisicho na ladha ya

    kicheko. Nilimwambia tena mama "ameshindwa bwana na

    madude yake. Mbona haji tena?" Mama akanikatiza "Bella

    hufahamu wanapanga nini juu yetu.... Funga mdomo

    wako" Nilinyamaza huku nikiwa na hakika babu hatokuja

    tena. Hali ilikuwa shwari na siku saba alizozisema mama,

    kuwa anaweza asifike basi zilipita. Nilifurahishwa na hali

    hiyo na tuliishi kwa amani. Amani ya kutosumbuliwa na

    babu lakini usisahau, Mzee Nyegezi hakuacha

    kunisumbua. Alipopata upenyo wa kumtoroka mama

    chumbani alinijia chumbani kwangu na kunitomasa

    tomasa kimahaba. Nilipomtishia kupiga kelele, alikurupuka

    kutoka chumbani kwangu na kurudi chumbani kwao. Siku

    moja alipokuja chumbani kwangu mauzauza yakaibuka

    tena haya yalichachamaa zaidi.

    Baba aliingia kwa mwendo wake ule ule wa kuninyatia.

    Hakutumia muda mwingi wala umbali mrefu kunifikia.

    Alizipiga zile hatua ndefu ndefu zisizotoa sauti. Mimi

    nilikuwa nimelala fofofo, hivyo sikusikia. Alipotaka kuitoa

    khanga mwilini mwangu, nami nilishituka. Nilimuona baba

    akiwa uchi wa mnyama. Alikuwa anatabasamu, tabasamu

    la dharau. Nilipotaka kupiga kelele yeye alicheka kwa

    nguvu alininong'oneza jambo

    "mama yako ameifakamia wine niliyoweka madawa ya

    kulevya. Utadhani hakuwahi kunywa wine tangu

    amezaliwa?" alinicheka kwa kejeli. kisha aliongeza sauti

    ya kicheko huku akibinya binya matiti yangu. wakati

    akiendelea na mchezo huo mchafu ndipo niliusikia upepo

    mkali uliovuma kwa nguvu. ulikuwa ni upepo mkali sana.

    sauti ya kicheko cha dhihaka kikasikika kati kati ya

    kicheko hicho. nilifahamu alikuwa ni babu. baba

    alijidumbukiza ndani ya shuka kuificha aibu yake. alikuwa

    anatetemeka sana. mimi nilijibanza ukutani pia nikiogopa

    ile hali. mara mbele yetu akatokea joka kubwa lenye

    vichwa viwili. alikuwa ni nyoka mwenye mabawa. siwezi

    kusimulia kwa urahisi ni kiasi gani niliogopa lakini

    nilishangaa kumuona Mzee Nyegezi amepoteza fahamu.

    yule nyoka alizungumza

    "nitakulinda siku zote. popote uendapo"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilishajikojolea kwa uoga. Nilitetemeka haswa. yule nyoka

    aliufahamu uwoga wangu aliniambia

    "usiogope. mkuu wa ulimwengu huu amekuchagua"

    kisha kama alivyokuja, aliondoka vile vile. Upepo wa kisuli

    suli uliingia chumbani kwangu na kulimeza lile joka. Mimi

    pia nilizimia kanga ikiwa mbali nami. Nguo ya ndani

    ilisitiri maungo yangu huku mkono wa baba ukiwa kifuani

    kwangu.

    .........

    sikumbuki nilipoteza fahamu kwa muda gani, ila

    nilishituka kipindi ambacho kulikuwa kumeshakuchwa.

    Baba bado alikuwa amelala pembeni yangu. Nilikuwa

    nikiugulia maumivu ya kichwa. Maumivu ambayo,

    yaliyogonga kama niliyetaka kuzimia tena au nilipigwa na

    kitu kizito. Nilikumbuka usiku uliotisha. Usiku wa joka

    kubwa lenye mabawa. Upepo wa kisuli suli ukalibeba lile

    joka na kupotelea hewani. Hakika ilikuwa ni hali ya

    kumfanya yeyote kuzimia. Ndiyo hapo niliona kitu cha

    kushangaza mbele yangu. Mwili wa mama ukiwa

    umekumbatia sakafu. Mama alikuwa amedondoka karibu

    na mlango wa chumbani kwangu. Akiwa ameyalalia

    mapovu yaliyomtoka mdomoni. Kiukweli nilishituka sana.

    Sikujua nianze vipi kumsaidia mama ikiwa Mzee Nyegezi

    naye alikuwa hajiwezi. Nilitoka nje, nikarudi ndani.

    Nilipanda kitandani mara nikashuka. Nilimuita mama

    lakini hakusikia. Nilimuinamia kwenye kifua chake na

    kuyasikiliza mapigo yake ya moyo niliyasikia yakidunda

    kwa mbali sana. Nikapata uhakika kuwa bado alikuwa

    hai. Nilivaa nguo zangu haraka haraka. Nikafungua droo

    katika kabati yangu kutazama kiasi cha pesa nilichokuwa

    nacho. "shilingi elfu thelathini' zinatosha," nilijiambia.

    Nilitoka mpaka eneo la hifadhi ya barabara, nilienda

    kuchukua tax. Tax haikuchelewa, tulirudi nyumbani na

    yule mzee ambaye alikuwa dereva, ndiye alinisaidia

    kumbeba mama na kumuingiza ndani ya gari. Nilikuwa

    nimechanganyikiwa sana. Nilichanganyikiwa baada ya

    kufahamu kuwa, mama alipata mshituko wa kutuona mimi

    na Mzee Nyegezi, tukiwa tumelala pamoja. Mzee Nyegezi

    alikuwa kama alivyozaliwa, mimi nikiwa sina chochote

    kifuani na nguo ya ndani pekee ilihifadhi maungo yangu.

    Sikutaka niwe sababu ya kifo cha mama yangu. Sikutaka

    kumuumiza mama. Wala sikutaka mama atoe chozi kwa

    sababu yangu. Nilidondosha chozi nilipokuwa katika

    kuwaza.

    Yule dereva aliniuliza. "binti kuna nini?"

    "acha tu mzee, naomba unipeleke lugalo"

    "itakuwa elfu kumi"

    "nimekuambia nipeleke Lugalo hospitali" Nilimjibu kwa

    karaha. Sikujali kuhusu pesa, nilijali mama afike mapema

    hospitali; apate matibabu. Nilikuwa nikimpepea mama

    aliyelalia mapaja yangu, huku nikilia kwa uchungu. Nililia

    huku nikimlaani mzee Nyegezi kwa tamaa zake. Mwendo

    wa tax ulikuwa ukiridhisha. Mzee yule aliikimbiza tax

    huku akipiga honi za hapa na pale. Japo alikuwa

    akiendesha kwa kasi kama uwajuavyo madereva tax,

    hakuacha kunisumbua kuniuliza hili na lile. Aliniuliza "na

    Yule mwanaume aliyelala uchi pale kitandani ni nani?"

    nilitamani nimtukane, ila nilimuheshimu. Sikumjibu kitu

    niliendelea kuomba Mungu mama awe mzima. Foleni

    ilimpisha na yeye kupita bila matatizo. Punde si punde

    tulifika eneo la hospitali. Machela ikakimbizwa na

    kumbeba mama. Mimi nilimlipa Yule babu na kumfuata

    mama alipokuwa akipelekwa. Nilipofika katika wodi flani

    ambayo sikuitambua kwa haraka nilisimamishwa.

    "tafadhali naomba usubiri hapo nje" Muuguzi mmoja

    alisema na mama kuingizwa sehemu fulani hivi na

    kufunika pazia la kijani. Nilibaki nikiwa nimesimama.

    Nilizunguka kila sehemu. Kulia nilitaka, maombi nikaona

    yalichelewa. Kila muuguzi alipotoka katika chumba

    alichoingizwa mama, mimi nilitoka mbio kumfuata.

    "naomba unijuze hali ya mama"

    "tafadhali kuwa na amani, amepata mshituko wa kawaida

    yupo sawa" nilikaa kwenye benchi iliyopo katika baraza la

    hospitali. Daktari aliyekuwa akimuhudumia mama, alitoka

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akaniambia "wewe ndiye mwenye mgonjwa hapa?"

    "ndiyo"

    "nifuate ofisini" Nilimfuata ofisini nikiwa katika hali ya

    uoga sana. Sikujuwa nini alikuwa anaenda kuniambia,

    lakini sikupenda kupokea jibu lolote baya. Nilipoingia

    baada ya kukaa, aliniambia. "ilikuwaje huyu mama

    akafikia katika hali hii?"

    "nahisi alipoteza fahamu baada ya kupata mshituko,

    Daktari"

    "hilo ndiyo jambo baya lililomkuta" Nilishituka sana

    daktari aliposema hivyo. Nilianza kulia sikujua daktari

    alimaanisha nini. Yeye alininyamazisha na kunieleza yote

    sasa.

    "sasa unalia nini? Nimeshakueleza tatizo kwani?"

    Alinyamaza akavuta pumzi baada ya kumeza mate na

    kuniambia. "huyu mwanamke hana tatizo lolote la

    kimuonekano, ila ubongo wake umecheza na kusababisha

    kumpotezea kumbukumbu mara kwa mara hivyo watu wa

    karibu inabidi muizuie hali ya yeye kudondoka dondoka

    kila mara"

    "sawa dokta, ninaweza kumuona?"

    "bila shaka"

    Nilienda katika chumba ambacho daktari alinielekeza.

    Chumba ambacho mama alikuwa amewekwa kama

    mapumziko. Nilipomtazama mama, machozi yalikuwa

    yakinitoka tu bila sababu. Nilijisikia vibaya sana kwa hali

    aliyotukuta nayo na Mzee Nyegezi. Nilimsalimu na

    alionesha kunikumbuka. "marahaba Bella"

    Lakini hakuwa amechangamka wala hakuwa na furaha.

    Niliona chozi likimponyoka na kushuka mpaka kwenye

    mashavu yake. Nilmsogelea na kumwambia "mama

    naomba nikueleze" akaniambia "huna haja ya kunieleza

    lolote Bella inatosha"

    "mama sivyo kama unavyofikiria mama" Nilimsihi

    anisikilize, nilimuhadithia kila jambo lilivyokuwa mpaka

    mimi na Mzee Nyegezi kuwa katika hali aliyotukuta nayo

    asubuhi. Aliniambia "kwanini hukunieleza mapema?"

    "niliogopa wewe ungegombana na baba"

    mama hakuongea chochote mimi nilitoka katika kile

    chumba na kwenda kwa daktari. Nililipa kila gharama za

    uuguzi wa mama yangu na kuambiwa kuwa nimuache

    kwanza mpaka mchana ndiyo nitaweza kuondoka naye.

    Mama alitundukiwa dripu ya maji. Mimi nilirudi nyumbani.

    Sikumkuta mzee Nyegezi katika chumba changu tena.

    Nikatoka na kwenda jikoni. Ndipo nikasikia hatua za mtu

    akinyata niliposimama, akaniziba mdomo.



     "mama sivyo kama unavyofikiria mama" Nilimsihi anisikilize, nilimuhadithia

    kila jambo lilivyokuwa mpaka mimi na Mzee Nyegezi kuwa katika hali

    aliyotukuta nayo asubuhi. Aliniambia "kwanini hukunieleza mapema?"

    "niliogopa wewe ungegombana na baba"

    mama hakuongea chochote mimi nilitoka katika kile chumba na kwenda kwa

    daktari. Nililipa kila gharama za uuguzi wa mama yangu na kuambiwa kuwa

    nimuache kwanza mpaka mchana ndiyo nitaweza kuondoka naye. Mama

    alitundukiwa dripu ya maji. Mimi nilirudi nyumbani. Sikumkuta mzee Nyegezi

    katika chumba changu tena. Nikatoka na kwenda jikoni. Ndipo nikasikia hatua

    za mtu akinyata niliposimama, akaniziba mdomo.

    ****



    Nilijitahidi kujinasua, lakini mikono ya mwanaume huyo ilinishinda nguvu.

    Ilikuwa imejaa misuli, hakika alikuwa na nguvu za kutosha. Punde si punde

    nilianza kulegea. Macho yakakosa nguvu nikawa nimepoteza fahamu. Nilipoamka

    nilijikuta nina hali ya tofauti hali ya utatanishi juu ya mapaja yangu.

    "damu" damu zilikuwa zimetapaaka kwenye mapaja yangu na kiuno kilivuta

    haswa. Kengele ya hatari ikagonga kichani kwangu. "bikra yangu" imetoka?

    Nilijiuliza kwa huzuni. Bikra yangu imetoka bila kuridhika kuitoa kwa yule

    ampendaye. Nilishamuahidi mpenzi wangu Jordan kuwa, yeye ndiye atakuwa wa

    kwanza kuuona usichana wangu. Sasa sikuwa nao tena. Atanielewa vipi

    nikimueleza ukweli kuwa nimebakwa? "mama!"

    Nikakumbuka nilimuacha mama hospitali. Nilimuacha ikiwa nilimuahidi

    nitarudi kumletea chakula baada ya dripu aliyotundukiwa kwisha. Sasa

    atakuwa ametoka? Alisharudi nyumbani? aliniona mimi nikiwa katika hali hii?

    Nikajinyanyua tena kwa hasira. Maumivu makali yakazidi katika nyonga zangu

    na kunifanya nitembee kama binti niliyekeketwa. Miguu yangu ilikuwa kama

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    gulubaja na nililazimika kujipinda kidogo nikidhani huenda maumivu

    yatapungua. Nilioga na kubadilisha nguo zangu na kutoka. Sebuleni

    nikakutana na Mzee Nyegezi. Mzee Nyegezi alikuwa akitabasamu kinafki.

    Tabasamu la kishetani. Sikushitukia chochote kutoka katika tabasamu hilo.

    Nikataka kumpita bila kumsalimia. Mwendo wangu ukaniadhiri. Nilikuwa

    nikichechemea kutokana na maumivu. Mzee Nyegezi akaniuliza. "Bella vipi?

    Umeumia?"

    "nimejikata kucha vibaya kidole kinaniuma" Nilimjibu huku nikianza tena

    kupiga hatua kuelekea nje. Aliniambia "hali hiyo utaizoea Bella" alikohoa

    kidogo. Kikohozi alichokisindikiza na kicheko cha kinafki na kuniambia

    "usipokuwa mbishi na kunipa bila utata" Moyo wangu ulilipuka kutokana na

    hicho alichosema. 'hali hiyo utaizoea Bella' sauti yake ikajirudiarudia

    kichwani mwangu na kujenga kitu kama mwangwi. 'usipokuwa mbishi' Nikaupata

    ulimi wangu. "hali? Hali ipi?" Alicheka kifedhuli. Akacheka kwa sauti ya

    juu hata nikajisikia vibaya. Nikawa nimeshagundua nini kinaendelea na ni

    nani amenifanyia mchezo ule mbaya. Kitendo cha kinyama. Kufanya mapenzi na

    mimi bila ridhaa yangu. Ndipo akaanza kuniambia. "wewe ni binti mtamu sana.

    Niruhusu niwe wako, usinikatalie. siku nyingine nikatumia nguvu kama leo

    nikakusababishia maumivu zaidi"

    "ahsante sana shetani mkubwa wewe"

    "hata wewe na familia yako yote ni mashetani ndio maana mnashriki katika

    njama za kula nyama za watu" alicheka, kisha aliniuliza. "hivi mama yako

    yuko wapi? Sijamuona tangu asubuhi?" nilimjibu "ameshajua yote

    unayonifanyia na amekukuta chumbani kwangu asubuhi ukiwa uchi. Umesababisha

    mama yangu akapoteza fahamu na sasa yupo hospitali unataka kuniulia mama

    yangu" nilitoka nje nikiwa nalia. Nilimuacha Mzee Nyegezi akiwa anashangaa

    aamini alichosikia.

    nilirudi hospitali na kumkuta mama naye akijiandaa kutoka. Tulikaa tena kwa

    dakika chache zaidi mpaka alipomaliza kula. Aliniuliza "Bella, mbona

    umechelewa kurudi?"

    "mama nilipatwa na matatizo nikiwa narudi nyumbani"mama alidakia kwa

    mshangao "babu yako amekuja tena?"

    "hapana mama, nitakuhadithia yote" tuliondoka baada ya kuruhusiwa na

    daktari aliyekuwa akimuhudumia mama. Tulipofika nyumbani sikumuhadithia

    lolote.

    .......



    Nakumbuka ilikuwa ni usiku tukiwa mezani tunakula. Mzee Nyegezi

    hakuthubutu kuinua sura yake wala mimi sikuthubutu kumtazama mama. Kuna

    wakati nilikuwa nikimuibia mama kwa jicho la wizi wizi. Ni wakati huo ambao

    pia nilimkuta yeye akitutazama mimi na Mzee Nyegezi. Niliyarudisha macho

    yangu chini tena, kwa aibu wala sikuendelea kumtazama. Mama akakiacha

    chakula na kwenda kwenye makochi kutazama video. Chakula alichokipenda, leo

    alikigusa kwa kijiko kimoja tu. Mara nyingi alipendelea kutazama kwaya na

    kusikiliza mahubiri. Mahubiri ambayo aliinunua cd yake kanisani. Huko nako

    hakutumia muda mwingi kumaliza kile alichokuwa anakiangalia. Alirudi kwenye

    meza ya chakula tulipo mimi na Mzee Nyegezi. Mimi nilikuwa nimeshamaliza

    chakula changu. Nikawa nataka kuinuka, nilipomuona mama akirudi niliendelea

    kukaa kwanza kwa muda. Sikujua kwanini moyo ulinienda mbio na uoga

    ukaendelea kunitafuna.

    "Nyegezi kwanini unanitenda hivi" Mama alimuuliza Mzee nyegezi macho yake

    yakiwa yamefumba kwa lita za machozi. Mzee Nyegezi alijitutumua kiume

    kupotezea mada aliyotaka kuianzisha mama. Hakufanikiwa.

    Mama aliendelea kubwatuka kwa kilio chenye kwikwi na hasira ikaikamata koo

    yake. Sasa akawa anaongea kama vile alianza kujifunza kuongea.

    "Nyegezi, umekosa nini kwangu? Kwanini unathubutu kutaka kutembea na

    mwanangu? Au kwasababu si wako?" mimi nafsi moja ndani yangu ikanisuta,

    'kwanini hujamueleza mama kuwa ameshakubaka?' nilijaribu kupoteza sauti

    hiyo. Lakini ilikuwa king'ang'anizi kichwani mwangu. Ilirudi ikarudi

    ikaendelea kurudi zaidi. Ikanikera moyo. Nikataka kusimama mama akaniambia

    "Bella kaa chini" Nilikaa

    "Nyegezi sikutegemea kama wewe ungebadilika hivi." Mama alinigeukia mimi na

    kuniambia

    "Bella hata leo nikifa naomba usikae hapa tena. Nenda popote unapopafahamu,

    nenda popote pale lakini siyo na huyu mwanaizaya" Nilimuitikia mama kwa

    kumaanisha nimemuelewa alichoniambia.

    Baada ya muda kwenda na usiku kuzidi kuwa mkubwa, wote tuliiacha runinga na

    kwenda kulala. Mama aliingia chumbani kwangu ili tuweze kusali kabla ya

    kulala. Hiyo ilikuwa ni lazima ili kuilinda nyumba yetu na mzimu wa babu

    ambao hutusumbua kila mara. Nakumbuka siku hii tuliomba kwa muda mrefu sana

    na mimi niliomba pia na mama huku nikibubujikwa na machozi. Ndipo hapo

    likatokea jambo baya kati kati yetu mimi na mama. Chumba kilianza

    kutetemeka kama vile nje kulikuwa na trekta linalolima. Alikuja fisi mkubwa

    sana. Kama kisingekuwako kitanda na sisi kukikalia, basi angekuwa amekimeza

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    chumba chote. Yule fisi alikuja kama Yule nyoka mwenye mabawa alivyoondoka.

    Ulianza upepo wa kisuli suli, kisha kati kati yake akatokea fisi huyo. Yeye

    alikuwa na ukubwa kama wa farasi na meno kama ya ngiri. Miguu yake ilikuwa

    ni minene kama tembo. Niliweza kugundua na kusema alikuwa ni fisi kwa kuwa

    alikuwa na umbo la fisi. Hakuwa fisi wa kawaida alitisha sana. Cha ajabu,

    fisi huyu alizungumza lugha ambayo mimi na mama hatukuielewa. Kisha

    katikati yetu, Yule fisi alijigeuza maumbo mbalimbali ya wanyama na mwisho

    kuwa binadamu kabisa. Alikuwa ni babu. Alicheka kwa sauti kuu na

    iliyotetemeka. Kabla hajasonya alitoa kisu kilichong'aa sana. Lakini

    kilikuwa kinavuja damu. Alitoa na bakuli kubwa katika moja ya mifuko yake.

    Vitu hivi vyote vilikaa katka mfuko wa suruali yake lakini sikutambua

    kutokana na ukubwa wa vitu hivi ilkuwaje vilienea na kukaa bila shida. Muda

    wote mimi nilikuwa nikikemea chini kwa chini. Mama alikuwa anatetemeka kwa

    uoga kupitiliza. Babu aliendelea kucheka alicheka sana. Kisha aituambia.

    "msiogope"

    alimsogelea mama mpaka karibu na uso wake akamwambia "nilikuahidi

    ukiendelea kumpingia Bella urithi wake, roho yako ni halali yangu" Mama

    alitetemeka sana. Sikuwahi kumuona mama akilia kwa uchungu namna ile.

    Nilimsihi babu asimuuwe mama, lakini sikufanikiwa. Nilimsikia mama akikemea

    kwa sauti ya chini chini huku akinena kwa lugha ya roho mtakatifu(ile lugha

    ambayo huongea walokole)

    "Bella, wewe ni lazima uwe, hata kwa kuangamiza dunia nzima. Mkuu wetu

    ameipenda roho yako ya kishujaa na ujasiri. Sina jinsi ya kutekeleza

    ninaloagizwa"

    "mkuu?" Niliuliza kwa mshituko. Kwa nguvu alizo nazo babu, nilitegemea

    kusikia yeye ndiye shetani mwenyewe. Alikuwa na mambo makubwa ya kuogofya.

    Iweje yeye awe kibaraka wa huyo mkuu anayemtaja? Kama yeye yupo hivi? Huyo

    mkuu wao ana nguvu za kiasi gani sasa? nahisi babu aliyajua mawazo yangu.

    Akacheka sana kisha aliniambia. "utamuona"

    sauti yake ilijirudia rudia huku akiwa anacheka kwa sauti ya juu sana.

    Kicheko chake kilinifanya nihisi hata majirani ni lazima wangeamka. Aliendelea

    kuniambia "mkuu wetu, ni mkuu wa huu ulimwengu wote. Ana nguvu nyingi sana.

    Atakupa wewe endapo utakubali uwe mrithi wangu, usisahau kuwa mali na vitu

    vyote ni vyake hivyo utakuwa tajiri zaidi ya tajiri yeyote unayemfahamu

    hapa duniani"

    mama aliniambia "usikubali Bella, hata nikifa leo naomba usije kukubali

    kuwa mchawi"

    "mama siwezi kuwa mchawi kama nilivyokuahidi" mimi na mama wote tulikuwa

    tunalia sana. Lakini kitu cha kushangaza hatukuweza kusimama wala

    kusogeleana japo kuwa tulikaa katika kitanda kimoja. Nilijihisi nikiwa

    mzito sana. Sikuweza kunyanyua japo kidole wala mkono kumgusa mama.

    Kilichoweza kusogea katika mwili wangu ni jasho jingi lililokuwa likinitoka

    mfululizo pamoja na mkojo uliotoka bila mpangilio kwa uoga. Moyo wangu

    ulipiga mara nne zaidi ya mapigo yake ya kawaida. Ulipeleka damu kwa kasi

    katika kila kiungo cha mwili wangu na kunifanya nihisi kizunguzungu na

    mwili kukosa nguvu. Babu alikiinua kile kisu juu na kuongea maneno fulani

    ambayo mimi na mama hatukuyaelewa. Katika kuzubaa huko, kisu kile kilipita

    katika shingo ya mama na damu nyingi kurukia kwenye bakuli alilolishika

    babu. Babu alikinyofoa kichwa cha mama, na kuanza kukitafuna. Sura ya babu

    ilianza kubadilika na kuwa ya paka. Macho yake yaling'aa na kutoa mwanga

    mkali kama wa jua. Kiwiliwili cha mama kilikuwa kinarukaruka huku na kule

    pale kitandani tulipokaa mpaka damu ilipokatika yote na kuchuruzikia kwenye

    lile bakuli ambalo alilishika babu. Mimi nilizimia. Nikiwa katika usingizi

    mzito wa kuzimia, nilikuwa nikitumbukia katika shimo moja refu sana.

    Lilikuwa ni refu kupita kiasi. Siwezi kusema urefu halisi wa lile shimo,

    lakini lilikuwa ni refu kupitiliza. Ndani ya shimo hilo lililo na giza

    nene, Kulikuwa na hewa nzito na iliyoogopesha kila nilipokuwa nazidi

    kutumbukia.



    *******



    Sikuweza kuona chochote mbele wala chini nilipokuwa nikidondoka kwa mwendo

    wa kasi. Ulikuwa ni mwendo ambao sijawahi kudhani kama ningeweza kudumbukia

    katika katika shimo kama lile ikiwa mwili bado haujaiacha roho. Nilipofika

    mwisho sikuanguka wala sikuumia.

    Kumbe tulikuwa na babu pamoja na mama.

    Nilishituka kumuona mama akiwa mzima, lakini hakuwa na uwezo wa

    kuzungumza. Hakuwa na uwezo wa kuzungumza, kwa kuwa nilimuita hakuitika

    wala kuniambia chochote. Alibaki akinitazama kwa hudhuni. Alipojitahidi

    kuniongelesha niliona ulimi wake ukiwa umekatwa na kubaki kipande. Babu

    aliniambia "hapa panaitwa Gamboshi, nitakutembeza kila sehemu uweze kuona

    wabishi waliokuwa wakijaribu kukatisha mipango yetu duniani"

    "umemfanya nini mama na mbona haongei"

    wakati huo wote mama alikuwa akinitazama machozi yakimtoka. Hakuwa na

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    tofauti na wale mazezeta ninaowafahamu. Babu alicheka kwa kejeli kisha

    alikuwa akiongea huku akimtazama mama "huu ndiyo mshahara wa kukwamisha

    harakati za mkuu wetu. Huyu si mama yako tena, sasa hivi ni msukule.

    Atakuwa huku kwa muda mpaka siku yake ya kufa itakapofika"

    niliwahi kusikia kuhusu misukule, lakini nilichofahamu mimi kuhusu watu

    waliogeuzwa misukule nilidhani huenda ni wale walioishi katika maisha

    ambayo hayakumpendeza mungu. nilijiuliza sana iweje wawe na nguvu ya

    kumgeuza mama msukule? Wakati hadi wakati mama anakufa alikuwa akinena kwa

    lugha ya kimbinguni, lugha inayonenwa na watakatifu tu?

    wakati nikiwaza hayo, ghafla niliona kama sinema mbele yangu. Niliyaona

    maisha ya mama yote upande wa pili mbali na ulokole ambao nilikuwa

    nikiufahamu. Wakati mama akiwa duniani baada ya mume wake wa kwanza Joseph

    ambaye ni baba yangu mzazi kufariki, aliishi katika mazingira magumu sana

    kabla hajaolewa na mume wake huyu wa pili, Mzee Nyegezi. Aliwahi kushauriwa

    na rafiki yake waenda kwa mganga apate mume tajiri ambaye atamuowa. Mama

    alikubali. Masharti ya mganga yalikuwa ni vichekesho vitupu. Mganga yule

    mbilikimo, alimtaka mama wafanye naye mapenzi, kwa madai kuwa hiyo ni njia

    ya kumtumbukizia dawa katika mwili wake kupitia njia ya kujamiana. Mama

    hakukubali.

    Wa pili alikuwa ni yule mjukuu wa babu kutoka kigoma. Yeye alimshauri alale

    na maiti mbili usiku wa manane katika makaburi ya kisutu. Mama alikataa

    pia. Rafiki yake akawa amemchoka. "rafiki yangu mimi siwezi nikawa napoteza

    muda wangu kila siku halafu wewe unakataa masharti unayopewa"

    "sio hivyo rafiki yangu. yaani kweli unanishauri nilale na maiti jamani?"

    "maiti si alikuwa binadamu kama wewe tu? Embu usiniangushe bwana. Siku moja

    tu haidhuru jambo" nilisikitika sana picha ambayo ilioneshwa mbele yangu.

    Mama alilala na maiti zote zilizofukuliwa kichawi katika makaburi yale yale

    ya kisutu. Kisha baada ya kupata mume tajiri halafu kutokana na kushindwa

    masharti ya mganga ya kuendelea kulala na maiti kila mwisho wa mwaka, ndipo

    alipoamua kuokoka. Mama aliokoka akiwa na mume wake huyo huyo aliyempata

    kupitia kwa mganga kwa masharti ya kulala na maiti mbili.

    Chozi likaniponyoka. Ndipo nikaoneshwa saa chache kabla mama hajauwawa

    kichawi na babu, alikuwa na hasira juu ya Mzee nyegezi. Alikuwa na chuki

    ambayo alishindwa kumsamehe Mzee Nyegezi. Nikaogopa sana kufahamu kumbe

    hasira na kutomsamehe mwingine kunaweza kusababisha mimi nishindwe kwenda

    mbinguni. Nilimuonea huruma mama kila nilipomtazama. Babu alikuwa

    akitutembeza katika mitaa ya sehemu hiyo ambayo alinitambulisha kama ni

    Gamboshi. Ilikuwa ni mitaa ya kawaida kama mitaa ya duniani. Nilisema hivyo

    kwa sababu hapa kulifanana kabisa na ulimwengu Fulani wa siri. Ulimwengu

    ambao kulikuwa na viumbe vingine vyenye sura za binadamu lakini walipaa

    kama ndege. NIlimuona kiumbe kimoja kilichonguzwa Vibaya na moto. Sura yake

    ilikuwa imeharibiwa vibaya na kuwa iliyotisha. Nilimuuliza babu "huyu mbona

    yupo hivi?"

    Babu aliniambia "walokole duniani huwaharibu sana watu wetu huku Gamboshi

    kwa maombi ya wanayoyamba" kisha aliniinamia na kunionesha mtu fulani

    aliyekuwa mbele yetu, amevaa kaniki huku akipepeta unga katika ungo mkubwa

    sana. "unamuona yule?"

    Nilishituka sana. Alikuwa ni kijana fulani ambaye nilimfahamu kwa jina la

    Fikiri. Alikufa miaka miwili iliyopita. Tulikuwa tukiishi naye mtaani. Yeye

    alikuwa akiuza maji kwa kupitisha katika madumu kila nyumba. Watu wengi

    walinunua maji yake na kuwa maarufu sana. Hata kifo chake kilihudhuriwa na

    watu wengi sana. Lakini wengi walinong'ona msibani kuwa hakikuwa kifo cha

    kawaida.

    "alikuwa akicheza tu mpira akaanguka ghafla"

    "itakuwa bibi yake. Maana inasemekana yeye ndiye mchawi maarufu"

    rafiki zake Fikiri walifikiria hivyo na kunong'ona kwa nguvu kutokana na

    jazba iliyojaza mioyo yao. Nilimuuliza babu. "fikiri alifanya nini?"

    babu aliniambia "yeye hakuwa na tatizo. Ila alitolewa kafara na bibi yake."

    bibi yake alikuwa mchawi na alilazimika kumtoa yeye Fikiri kwa sababu zamu

    yake ya kutoa damu na nyama ilifika. Babu alinieleza kuwa hapo kuna kambi

    nyingi za wachawi na wa kila aina. Lakini Gamboshi ndiyo kilikuwa kijiji

    ambacho mkuu wao alikuwa akiishi. Nguvu zote za wachawi zilitoka katika

    kijiji hiki. Ilikuwa ni kijiji cha wachapakazi na watu walikuwa busy kuliko

    kawaida. Nilibahatika kuwaona watu wengi niliowafahmu huko duniani.

    Babu akaniuliza Swali "je upo tayari kuurithi ufalme wangu mara

    nitakapokufa?"

    aliniambia huku akiwa na anatokwa na machozi ya damu. Sikuelewa hali hiyo

    ilimaanisha nini ila nilishindwa kukubali haraka haraka. Lakini pia

    sikupenda kufa mapema kama alivyokufa mama. Nilitambua fika ule ndio

    ulikuwa mwisho wa kuonana na mama yangu. Mama aliondoka katikati yetu na

    kuvalishwa kaniki nyeusi kama walizovaa wengine wengi katika kjiji

    hicho. Baada

    ya kutafakari sana kwa dakika chache baadaye nilimjibu babu. "babu naogopa

    kuwa mchawi" Nilijibu kiuwoga. Nilijibu nikiwa namaanisha kweli ninaogopa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kuwa mchawi. Tuliendelea kutembea katika mitaa mbalimbali ya kijiji hiko

    cha wachawi.

    Babu alitabasamu na kunigeukia "mjukuu wangu uchawi hauna madhara yoyote"

    "babu hauna madhara?" Niliuliza kwa mshituko. Babu alicheka na kunijibu

    kifupi



    aliniambia huku akiwa na anatokwa na machozi ya damu. Sikuelewa hali hiyo

    ilimaanisha nini ila nilishindwa kukubali haraka haraka. Lakini pia

    sikupenda kufa mapema kama alivyokufa mama. Nilitambua fika ule ndio

    ulikuwa mwisho wa kuonana na mama yangu. Mama aliondoka katikati yetu na

    kuvalishwa kaniki nyeusi kama walizovaa wengine wengi katika kjiji

    hicho. Baada

    ya kutafakari sana kwa dakika chache baadaye nilimjibu babu. "babu naogopa

    kuwa mchawi" Nilijibu kiuwoga. Nilijibu nikiwa namaanisha kweli ninaogopa

    kuwa mchawi. Tuliendelea kutembea katika mitaa mbalimbali ya kijiji hiko

    cha wachawi.

    Babu alitabasamu na kunigeukia "mjukuu wangu uchawi hauna madhara yoyote"

    "babu hauna madhara?" Niliuliza kwa mshituko. Babu alicheka na kunijibu

    kifupi

    "ndiyo, hauna madhara yoyote"

    "babu mimi siwezi kula nyama ya mtu, kunywa damu ya binadamu wala mnyama,

    siwezi kuua. Babu sitaki kuwa mchawi"

    babu alizungumza na mimi kwa upendo hata nikajisikia faraja

    "mjukuu wangu, nafasi niliyo nayo ni kuwaadhibu wale wanaokiuka masharti ya

    mkuu wa ulimwengu huu hivyo wewe nawe utakuwa vivyo hivyo kama utakubali

    kurithi nafasi yangu"

    nilimuomba babu anipe muda nitafakari jambo hilo kwa muda. Babu alinipa

    masaa machache hivyo alidai kuwa angelifuata jibu lake usiku. Tulipokuwa

    tukiendelea kutembea tembea, nilishituka kumuona mtu ninayemfahamu kabisa.

    Alikuwa ni mtu mmoja maarufu huko duniani. Alikuwa ni mwanasiasa

    aliyeogopwa sana na vyama pinzani, pamoja na chama chake. Nilisikitika

    kumuona akiwa pale. Amechoka, amekuwa mweusi tofauti na alivyokuwa kule

    duniani. Nilipotaka kuzungumza naye, babu alinizuia.

    "hapana Bella, wewe bado hujawa na nguvu za kuweza kuzungumza na misukule"

    nikamuuliza babu "kwani huyu amefanya nini mpaka yupo mahali hapa?"

    "yeye alitolewa kafara na mume wake, mume wake ni mfanyabiashara maarufu

    lakini yupo katika chama kimoja maarufu kinachotoa kafara na kumwaga damu

    kwa sababu ya utajiri"

    nilitetemeka sana niliposikia hivyo. Baada ya muda, nikatamani kuzunguka

    zunguka tu mule katika kile kjiji cha Gamboshi ili niweze kuwaona watu

    mbalimbali ambao ninawafahamu.

    Tulipita katika kijiji duni ambacho niliwaacha wale misukule sasa tukaingia

    katika sehemu yenye uafadhali wa maisha katika shemu hiyo ya Gamboshi.

    Babu alinieleza "kule tulipopita mwanzo, ndipo wanapoishi misukule. Lakini

    huku ndipo ilipo ngome yangu na wachawi wengine wakubwa huko duniani."

    mbele ya majumba mbalimbali ya kifahari. Yaliyojengwa kiufahari. Niliuona

    mji Fulani ulikuwa uking'aa sana. Ulikuwa ni mji uliokuwa ukiwaka taa

    zilizotowa mwanga mkali hata kufanya niuone mji ule ukipendeza sana.

    Nikamuuliza babu "kule ni wapi na kuna nini?" Babu hakunijibu kitu na

    kunieleza ile si sehemu nzuri kuifikiria wala kutamani kwenda. Alinieleza,

    miaka mingi sana iliyopita ufalme wa falme ile ilijaribu kutaka kupindua

    tawala ya mkuu wao na kushindwa. hivyo ilijitenga nao na kuwa maadui

    wakubwa baada ya urafiki uliokithiri na kujikita katika ndani ya mishipa

    yao ya damu kabisa, kupoteza mvuto. Sikutaka kuendelea kuuliza zaidi lakini

    nilihisi jambo kuhusu mji ule niliouona. Mji ule na hapa Gamboshi tulipo,

    kuliteganishwa na shimo moja refu liliokuwa likitokota uji mzito wa moto.

    Tofauti ya mji ule na huu wa ngome ya babu ilipo. Japokuwa mji ule

    ulipendeza na uling'aa sana lakini huu wa babu ulififia na kuwa kama wenye

    giza Fulani lisiloeleweka. Babu alinitoa hapo na kunionesha sehemu ambayo

    mkuu wao alikuwa akiishi. Alinieleza "mjukuu wangu, sehemu hii ni takatifu

    sana. Watu wote maarufu uwajuao huko duniani, huja mahali hapa kumuomba

    mkuu wetu utajiri na kusafisha nyota zao ili waweze kukubalika zaidi na

    zaidi."

    "ninaweza kumuona?"

    niliuliza

    "hapana, bado hujafikia viwango vya kukanyaga sehemu ile" tuliondoka mahali

    hiyo na kurudi kule kwa awali. Kule kulipochosha. Kule niliposhuhudia

    misukule ikifanya kazi kwa bidii. Kule ambapo naamini ningemuona tena mama

    na nimuage kuwa ipo siku nitarudi kuja kumtoa. Nilimuuliza babu "hivi hawa

    hufanya kazi kwa muda gani" Babu alicheka sana na kunieleza kuwa "hawana

    mapumziko, hufanya kazi usiku na mchana na hupumzika mara moja tu kwa siku"

    alinyamaza baada ya kumeza mate kasha aliendelea kunieleza "wakati ambao

    umepangwa wa wao kula tu"

    "na huwa wanakula nini?" akanijibu "unga na funza, ndio chakula chao kikuu"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilishangaa sana, ghafla machozi yalinitoka. Nilihuzunika kwa kuwa

    nilifahamu mama yangu naye alikwisha kuwa msukule. Hivyo chakula chake

    nacho kingekuwa ni hicho hicho. Nilimlaumu babu kwanini alimuuwa mama

    yangu. Nililia kwa uchungu huku nikikimbia kusikojulikana. Nilikuwa sijuhi

    wapi naenda ila nilipishana na misukule na vile viumbe vilivyopaa kama

    ndege lakini wakiwa na maumbo ya binadamu. Ghafla Mbele yangu nilikutana

    babu akinicheka kwa sauti ya juu sana. Aliniambia "Bella huku huna pa

    kunikimbia" nilimjibu "babu nakuchukia, nakuchukia kuliko navyomchukia

    shetani"

    ghafla babu alinipiga kibao kilichonifanya nipoteze fahamu. Fahamu

    iliyonitoa katika ulimwengu wa Gamboshi na kunirudisha duniani. Nilijikuta

    nikiwa katikati ya watu wengi. Watu waliokuwa wakilia wakinamama

    wamejifunga kanga zao. Wengine wakinipepea huku wakilia kwa uchungu

    wakiliita jina la mama yangu.

    niliposhituka nilipiga chafya mara tatu mfululizo. Watu walijawa na

    mshituko. Niliwaona wengi wakiwa na maswali mengi sana juu ya kifo cha

    mama. Mimi pia nilianza kulia kwa uchungu. Nilifahamu fika sitoweza kumuona

    tena mama yangu katika ulimwengu huu wa kawaida. Watu walinibembeleza

    lakini niliona kama walikuwa wakiniongezea uchungu zaidi. Walimuita Mzee

    Nyegezi. Mzee Nyegezi alikuwa akizungumza na askari polisi waliofika eneo

    la nyumbani kwetu. Watu walikuwa wamejaa sana. Hakika kifo cha mama

    kilishitua wengi. Mzee Nyegezi na wale askari, walisubiri ninyamaze kulia

    kisha waniulize maswali kadhaa. "pole sana binti" Alizungumza askari mmoja

    aliyevalia sare zake.

    "salama" kwikwi ilinibana, lakini nilijibu hivyo hivyo. Wakati huo huo

    ambao askari wakiendelea kuzungumza, ghafla niliisikia sauti ya babu yangu

    ikizungumza na nafsi yangu

    "usiwaeleze chochote askari kuhusu kifo cha mama yako, wajibu hufahamu kitu"

    nilipopata kigugumizi cha kujibu kutokana na sauti niliyoisikia, macho

    yangu yakapata mshangao zaidi nilipomuona babu mbele yangu. Alikuwa kwenye

    msiba huo kama waombolezaji wengine wa kawaida. "unaweza kutueleza

    chochote ulichokiona?"

    askari mmoja akalirudia Swali aliloliuliza zaidi ya mara tatu. Sikulisikia

    kutokana na uwoga na nilijifanya sikuliskia kwa kuwa jibu walilotaka sikuwa

    tayari kuwajibu.

    walinipa muda wa kupumzika zaidi. Huku nikisikia kuwa, mwili wa mama upo

    hospitali kwa ajili ya uchunguzi. Bado nilikuwa katika woga zaidi. Watu

    mbalimbali waliingia katika chumba nilichomo kunipa pole. Nilimuona Jordan

    mpenzi wangu. Nilimuona Bertha rafiki yangu na wanafunzi wenzangu wa

    shuleni. Dakika chache baadae aliingia mwanamke fulani mwenye mwili mpana

    na uso wa mviringo. Uwazi Fulani katikati ya meno yake ukamfanya awe na

    mwanya hata akapendezesha kwa jino la dhahabu. Alijitanda kanga juu, chini

    akakivaa kitenge kutoka kongo.

    sikuwahi kumuona hata siku moja. Aliniambia "pole sana Bella" Nilikuwa

    nikimtazama kwa makini bila kukumbuka ni wapi niliwahi kumuona. Nilimjibu

    "asante, sijuhi niliwahi kukuona wapi?" akanijibu. "Gamboshi," hapo hapo

    nilipoteza fahamu na kuisalimia sakafu kwa kuibusu. Dakika chache baadaye

    niliamka kutoka usingizini. Nilijikuta katikati ya kundi kubwa la watu

    wakinisikitikia. Kila mmoja alisema lake

    "kufiwa na mama si kitu cha mchezo"

    "tena kuna tetesi alikuwa naye" mwingine alisema "mama yake amekufa kifo

    cha kinyama sana" Nikaanza tena kulia kwa uchungu. Nililia sana kwa sababu

    nilifahamu fika chanzo na sababu ya kufa kwa mama yangu ni kuzuia harakati

    za babu mimi kuwa mchawi. Nikiwa katika kulia huko sikujua nilipata hisia

    gani hata zikanigusa nitazame nyuma ya mlango wa chumba nilichomo.

    Nilimuona mama akiwa hana uwezo wowote wa kuongea.

    Nilizidi kulia. Mbele yangu akatokea babu na kunieleza kuwa. "sasa umeweza

    kuwa mchawi" Nilishituka sana. Sikujuwa ilikuwaje nikawa mchawi bila

    kukubali mwenyewe na ilikuwa saa ngapi nikawa mchawi. Babu aliongea na

    mimi bila mtu yeyote kufahamu kama nilikuwa nikizungumza na babu

    "uliniambia nikupe jibu jioni kama nimekubali, imekuwaje uniambie nimekuwa

    mchawi sasa?" Alicheka sana kisha aliniambia

    "mjukuu wangu unatamani utajiri na nyota yako inawaka sana"

    "hujajibu swali langu babu"

    "ipo siku utanielewa acha tuyamalize haya ya msiba kwanza"

    alipotaka kutoweka mbele yangu nilizishangaa nguvu nilizonazo. Niliweza

    kumzuia.

    "mama anafanya nini hapa?"

    nilimuuliza huku nikiangalia eneo la mlangoni. Babu naye aligeuka kuangalia

    alipo mama. Alinigeukia huku akitabasamu kifedhuli na kuniambia

    "atakaa pale mpaka mtakapomsalia katika mazishi yake. Ule mwili ambao

    wameenda kuufanyia uchunguzi si mwili bali ni mgomba. Usiogope, hana uwezo

    wa kufanya lolote pale na hakuna anayemuona"

    nilisonya kwa hasira na babu alitoweka hapo hapo. Nilisonya kiasi kwamba,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/-

    hata waombolezaji wengine walishituka. Mama mmoja aliniuliza "kuna nini

    Bella?"

    nilitingisha kichwa nikikataa kuwa hakuna kilichotokea. Nikatoka nje,

    nilishangaa kumkuta babu akiwa pale pale nilipomuona mchana akiwa na wale

    askari pamoja na Mzee Nyegezi. Mzee Nyegezi naye alinifuata na

    kuniuliza "unajisikiaje

    sasa Bella" nilimjibu tu, ilimradi

    "vizuri" akaniuliza "Nyama ya mama yako ni tamu?" alikuwa akinichekea kwa

    kunikejeli. Akaamsha hasira zangu. Nilimuangalia Mzee Nyegezi kwa jicho la

    chuki hata nikamuona akianza kutokwa na jasho jingi sana. Nilijihisi nikiwa

    na nguvu za ajabu, nguvu za kumuadhibu yeyote kwa kumtazama tu. Ilikuwa

    inashangaza.

    Muda wote huo babu alikuwa akinitazama. Alikuwa akitabasamu kwa raha sana.

    Nilimuona Mzee Nyegezi akilalamika. "Bella unaniunguza na macho yako". Nikampa

    onyo

    "ole wako umueleze yeyote kuhusu msiba wa mama"

    "nisamehe Bella usiniadhibu sintomueleza yeyote"

    taratibu za mazishi ziliendeshwa na famila ya mama mkubwa. Ndugu na

    marafiki wa mama walijumuika pamoja kumsindikiza mama katika safari yake ya

    mwisho. Watu walikuwa ni wengi sana. Siwezi kusema kuwa nilihesabu idadi

    yao, kwasababu nisingeweza. Misa takatifu ya kumuombea mama, ilifanyika

    katika kanisa la katoliki mule mule ndani ya hospitali ya muhimbili.

    Nilishituka kumuona yule mama aliyenitokea mule chumbani kichawi, akiwa

    kwenye madhabahu huku akitoa maelekezo

    "mwili wa mama yake Bella hautafunuliwa kutoka katika jeneza lake kutokana

    na wingi wa watu pamoja na kifo alichokufa. Hivyo tumeamua kuweka picha tu

    ambayo mtapita mkitoa heshima zenu za mwisho kwa kupita njia hii na

    kuelekea nje ambapo kuna magari ya kuwapeleka makaburini." Nilimgeukia Mzee

    Nyegezi aliye pembeni yangu, nikamuuliza

    "hivi huyu mama ni nani?"

    "nimetambulishwa na babu yako kuwa ni ndugu wa mama yako"

    "na babu si ni baba wa baba yangu? Imekuwaje yeye afahamu ndugu wa mama

    yangu?"

    "sifahamu Bella naomba uniache kidogo"

    tulienda kuaga kwa taratibu tulizoelekezwa na yule mama. Nilijaribu

    kumtafuta, lakini sikumuona tena eneo hilo la msiba. Mpaka tulipoingizwa

    kwenye magari ya kuelekea makaburini kuuzika mwili wa mama.

    Baada ya mazishi tulirudi nyumbani. Baada ya siku chache baadaye, msiba

    ulipomalizika maisha yalikuwa shwari wala babu na yule mama wa maajabu

    hawakutokea tena. Siku moja nikiwa shuleni pamoja na rafiki zangu, alikuja

    Berther na kunieleza kuwa "kuna mtu kule nje anakuita" nikamuuliza

    "mwanamke mwanaume?"

    "mmama mmoja hivi, ila niliwahi kumuona msibani kwenu"

    mimi nilitoka mbio mpaka getini kumtazama huyo mama. Mawazo yalijua fika ni

    yule mjumbe wa wachawi kutoka Gamboshi. Alifuata nini kwangu? alitaka nini?

    Nilipofika getini, sikukuta mtu. Nilipotaka kugeuza na kurudi ndani.

    Nilimuona babu amesimama pembeni ya ukuta wa shule akicheka "vipi mbona una

    wasiwasi?" aliniuliza ghafla. "babu yule mwanamke ni nani?" nilifahamu

    fika anafahamu ninachozungumzia. Alicheka bila kunipa jibu lolote.

    Nikamuuliza tena "umekuja kufanya nini hapa?" alinijibu "nataka ukadhuru

    Gamboshi mara ya mwisho kabla hujarithi kiti changu" moyo wangu ukaanza

    kwenda mbio sana. Ghafla mbele yetu tuliposimama, lilikuja gari la maajabu

    na ndani yake abiria walikuwa uchi wa mnyama. Nikisema gari la maajabu,

    namaanisha gari lile lilipita eneo la shule bila hata kufunguliwa geti na

    wala hakukuwa na barabara eneo hilo. Tulielekea gamboshi. Tulipoingia ndani

    ya lile gari la kichawi, sikuwa muoga tena. Niliwaona watu walio nadhifu

    kimavazi kuonesha walikuwa na uafadhali wa kifedha. Watu hao walijitundika

    ndani ya suti nyeusi mikononi walizibeba biblia. Nikajinong'oneza

    "wachungaji?" nilishituka sana. Ilibidi, nimuulize babu. "hawa si watumishi

    wa mungu?" Babu alinipiga kibao kikali sana na kunikataza kwa kuniambia

    kuwa, jina hilo halikuruhusiwa kutajwa eneo lile. Kisha aliniambia kuwa

    "hawa si watumishi wa huyo anayedhaniwa kuwa aliwaumba binadamu"

    nilimeza mate nikiugulia maumivu huku nikiwaangalia wale watu waliokuwa

    kimya muda wote. "sasa huku Gamboshi, wanaenda kufanya nini?"

    Babu alicheka kicheko kisicho na ladha ya kuitwa kicheko. Kisha aliniambia

    kuwa

    "hawa ni wachungaji maarufu sana huko duniani wanaolihubiri jina la mkuu

    wetu kupitia hizo dini zao. wachache huwafahamu kama wakiwa pamoja nasi

    katika ulimwengu huu wa Gamboshi" Nilikuwa nimetumbua macho muda wote.

    hakika ilikuwa habari ya kushangaza na kutisha muda wote. Kisha babu

    aliendelea kuniambia. "wengi wamepata nguvu ya uponyaji kutoka kwa mkuu

    wetu. Unapoponywa na mmoja kati ya wachungaji hawa, lazima wewe uwe mmoja

    wa wanachama wa kuleta watu wengine wengi katika ulimwengu wa mkuu wetu."

    sasa ndio nikakumbuka mama aliwahi kuniambia mwisho wa dunia yatatokea

    mambo mengi ya kutisha na kushangaza. Manabii wengi wa uongo wataponya.

    viwete wakatembea, viziwi wakasikia na mabubu kupiga yowe; nikiona ishara

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hizo nisihangaike katika kukimbilia miujiza nisimamie imani yangu. Mwili

    wangu ukasisimka hata vinyweleo vikasimama. Nilimgeukia babu na kumuuliza.

    "mbona gari imesimama na hawa wanashuka?" babu alinieleza kuwa "hawa ni

    wachawi ambao wanaenda kuongezewa vyeo kwa kazi walizofanya bada ya kutumwa

    na kuzifanikisha. Hupewa fisi wa kutembelea ama mnyama yeyote. Hongezewa

    nguvu pia kwa kujilinda na maadui na nguvu za walokole"



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog