Search This Blog

NILIONGEA NA SHETANI ILI NIWE TAJIRI - 2

 





    Simulizi : Niliongea Na Shetani Ili Niwe Tajiri

    Sehemu Ya Pili (2)



     "hawa ni wachungaji maarufu sana huko duniani wanaolihubiri jina la mkuu

    wetu kupitia hizo dini zao. wachache huwafahamu kama wakiwa pamoja nasi

    katika ulimwengu huu wa Gamboshi" Nilikuwa nimetumbua macho muda wote.

    hakika ilikuwa habari ya kushangaza na kutisha muda wote. Kisha babu

    aliendelea kuniambia. "wengi wamepata nguvu ya uponyaji kutoka kwa mkuu

    wetu. Unapoponywa na mmoja kati ya wachungaji hawa, lazima wewe uwe mmoja

    wa wanachama wa kuleta watu wengine wengi katika ulimwengu wa mkuu wetu."

    sasa ndio nikakumbuka mama aliwahi kuniambia mwisho wa dunia yatatokea

    mambo mengi ya kutisha na kushangaza. Manabii wengi wa uongo wataponya.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    viwete wakatembea, viziwi wakasikia na mabubu kupiga yowe; nikiona ishara

    hizo nisihangaike katika kukimbilia miujiza nisimamie imani yangu. Mwili

    wangu ukasisimka hata vinyweleo vikasimama. Nilimgeukia babu na kumuuliza.

    "mbona gari imesimama na hawa wanashuka?" babu alinieleza kuwa "hawa ni

    wachawi ambao wanaenda kuongezewa vyeo kwa kazi walizofanya bada ya kutumwa

    na kuzifanikisha. Hupewa fisi wa kutembelea ama mnyama yeyote. Hongezewa

    nguvu pia kwa kujilinda na maadui na nguvu za walokole"

    kisha aliendelea kunieleza kuwa, wale wachawi wanaelekea eneo ambalo

    kulikuwa na joka kubwa lenye vichwa vitatu. Joka hilo, ni kubwa sana. Joka

    linalotowa nguvu hiyo. Vichwa hivyo vina sura za binadamu zinazotisha. Kwa

    mtu wa kawaida huwezi kuzitazama zaidi ya sekunde tano bila nguvu za

    kichawi, utazimia au kufa kabisa. Babu aliponieleza hayo niliogopa sana.

    Siwezi kueleza kiasi nilichoogopa lakini hata wewe nikusimuliaye hadithi

    hii, bila shaka unatetemeka. Basi gari lilikuwa linaenda kwa kasi kama

    treni ya umeme. Tulipofika eneo Fulani, mimi na babu tulishuka na wale

    wachungaji waliendelea na safari.

    nilimuuliza tena babu "kumbe kule bado kuna safari nyingine ndefu?"

    Alinijibu "kule ndipo mwisho wa safari, kule ndipo alipo mkuu wetu, kule

    ndipo nilipokuonesha siku ile ya kwanza na kukuelekeza ile ni sehemu

    takatifu sana. Ipo siku utakwenda ukishakuwa na nguvu za kutosha na

    kukabidhi madaraka niliyonayo."

    lile gari halikuchukuwa muda mrefu likawa limeshapotea machoni pangu. "sasa

    mimi nimekuja kufanya nini huku ikiwa mimi bado sijawa mchawi?"

    babu alicheka kama kawaida na kuniambia "wewe ni mchawi tayari ila huna

    nguvu za kutosha za kukutana na mkuu wetu." Nilijiuliza mara kwa mara huyo

    mkuu anayetajwa na babu sana, atakuwa ni nani? lakini sikupata jibu. Katika

    kutembea na kuzuru eneo ambalo misukule walikuwa wakifanya kazi kulingana

    na kazi zao au vipaji walivyokuwa navyo huko duniani, tuliingia katika

    jengo moja ambalo babu aliniambia hiyo ni hospitali ya hapo Gamboshi.

    Niliuliza

    kwa mshangao "Hospitali? Kwani huku nako watu hupigania uhai?"

    babu alinieleza " hiyo ni sehemu ya kubadilishana viungo baina ya misukule

    na wachawi ambao huumizwa na nguvu za maombi ya walokole." Babu akanieleza

    jambo moja ambalo hata leo silisahau "wachawi hawaogopi biblia wala jina

    la huyo aliyekuja akasulubiwa msalabani(yesu) bali kwa hao wanaojifanya

    wanaomfuata huyo mtu wao" hapa babu alinieleza kwa maneno ya kashfa sana.

    Maneno ambayo yalimdhihaki Mungu. M Sikupenda niyaandike yote. Mara

    nikamuona msukule ambaye alikuwa akifanyiwa jambo kama operasheni.

    Alitolewa mguu na kubandikwa mtu mmoja aliyekuwa uchi akiugulia maumivu.

    Babu alinieleza kuwa yule ni mchawi aliyevunjwa mguu na nguvu za maombi. Babu

    akanigeukia na kunieleza "leo tutakuwa na safari ndefu kidogo huku

    Gamboshi. Lakini isiyochosha. Leo ni siku ambayo utakabidhiwa utawala wangu

    na utakuwa msichana wa kwanza tangu ulimwengu huu ulipoumbwa kwa kushika

    nafasi kubwa kama hii. Mkuu wetu amependezwa na mg'ao wa nyota yako hivyo

    ameamini akikutumia wewe atapata wafuasi wengi. Hakuna falme itakayoshinda

    mara itakapojaribu kujiinua kupigana na wewe. Utakuwa msichana mwenye nguvu

    za ajabu na utajiri usioelezeka. Ila kuna masharti utakayopewa ukiyatimiza

    hayo utakuwa umenifurahisha sana."

    Alinipiga piga mgongoni nikahisi kama nimeshikwa na nyaya za umeme.

    Nilitetemeshwa.

    Nilimuuliza babu nikiwa na tabasamu "babu sasa kwanini mkuu wenu ameamua

    kunichagua mimi ikiwa bado mimi ni binti mdogo? Na nisiye na uwezo wowote

    kifedha?"

    "swali zuri sana. wakati wote nakueleza kuwa mkuu wetu amependezwa na nyota

    yako hiyo ndio sababu iliyomvutia mkuu wetu" aliyameza mate kisha

    aliniambia "mkuu wetu ana utajiri mkubwa yeye haihitaji sadaka" kisha babu

    alicheka kifedhuli.

    niliacha kuuliza maswali na kuendelea kuzuru Gamboshi kama mtalii. Nikaona

    kikao kimoja klichohudhuriwa na watu wengi sana, kikiwa kinaongozwa na joka

    kubwa yaani joka lile lilikuwa kubwa kupitiliza. Joka lile lilikuwa

    likiwatemea wale watu mate yake. Cha ajabu mate yake yalikuwa mengi kila

    alipokuwa akiwatemea ikawa kama ilikuwa inanyesha mvua. hivyo kila mmoja

    aliye katika kikao kile alilowa chapachapa. babu alinieleza kuhusu joka

    lile.



    "yule ni mdogo sana kwangu, ni mtu wa heshima sana huko Nigeria yeye

    hugawa nguvu na kukubalika pamoja na kufunguka kwa milango yao ya pesa

    lakini bado hajafika katika wadhifa wangu yeye hapa ni sawa na waziri mkuu

    huko duniani" Nilijiuliza sana moyoni

    'sasa babu atakuwa ni nani ikiwa huyu nyoka mkubwa, anayetisha angekuwa yu

    chini ya babu?' ilibidi nimuulize "sasa wewe ni nani katika wadhifa wako?"

    Babu alicheka, wala hakuniambia wadhifa wake. Ila nilimuuliza tena "kwa

    hiyo babu wale ni matajiri wa wapi?" alinijibu kwa majivuni "wale ni

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    matajiri kutoka katika kila pembe ya dunia si wa Nigeria peke yake"

    hapo nikawa nimeelewa. Nilimuuliza swali lingine tofauti "hivi babu! yule

    mwanamke aliyekuja pale nyumbani siku ya msiba wa mama, akajitambulisha

    kuwa alitokea Gamboshi alikuwa ni nani?" hili nalo hakunijibu. Aliita jina

    moja nisilolifahamu kwa sauti iliyotetema kama radi. "Consolathaa!" Fumba

    na kufumbua mbele yetu akatokea yule mwanamke aliyekuja siku ile nyumbani

    kwenye msiba wa mama. Alikuwa ni mchafu na kunuka sana. Alikuwa ni huyo

    aliyeitwa na babu kwa jina hilo la Consolatha. Babu akanieleza hadithi fupi

    iliyomuhusu Consolatha. "huyu ni mwanangu wa kike wa pekee niliyemzaa

    baada ya baba yako kuacha ziwa katika miaka mitatu iliyopita kwenye uzao wa

    bibi yako. Mizimu ikapendezwa naye lakini alifanya kosa dogo la kijinga

    katika masharti aliyopewa na mkuu"

    wakati ambao babu alikuwa akinielezea hayo, Consolatha alikuwa amepiga

    magoti akiwa ameinamisha kichwa chini kwa heshima kama akisujudu mbele yetu.

    Babu aliendelea kunieleza "yeye aliambiwa ile damu iwatokayo kila mwezi

    ahiifadhi katika kikombe na kukiweka kwenye kitanda alaliacho na baada ya

    kukata, amletee mkuu wetu na iwe kama kiapo chake kwa kuinywa kikombe

    kimoja" babu alikohoa, akameza mate kisha aliendelea

    "yeye alishindwa kwa kuona eti ulikuwa ni uchafu" mimi mwenyewe nilikunja

    sura kwa kuona ni uchafu niliona kuwa ni jambo ambalo lisingewezekana.

    Kunywa uchafu uliotoka mwilini mwangu? Ni heri niukose huo umalkia.

    Nilimsalimia shangazi. Baada ya kuniitikia salamu yangu alitoweka. Babu

    akaniambia "hata wewe usithubutu kwenda kinyume na masharti ya mkuu.

    Utapata shida huku Gamboshi, duniani na popote utakapokuwa unaenda"

    niliteteeka kwa uoga sana. Niliitikia tu bila kumaanisha kama nimeelewa

    alichoniambia. Akaniambia tena "sasa muda wa kwenda kukuapisha na kukupa

    nguvu umefika. Lakini kama haupo tayari kupewa masharti utakayopewa ni heri

    usikubali."

    hapo ni kawa mzito kukubali. Sikujua niseme lipi kati ya "ndiyo ama hapana"

    lakini nilijipa moyo kuwa masharti ambayo ningepewa huenda ningeyaweza. Babu

    akaniamuru nivue nguo nilizovaa "vua zote ubaki kama ulivyozaliwa"

    Nilikataa.

    "usiogope, hutabaki uchi kila mahali utakapokuwa unaenda, kuna nguo ambazo

    nitakuvalisha kwa ajili ya utukufu mbele za mkuu" Bado nilikataa. Punde si

    punde dakika chache mbele nilijishangaa kuona nimevaa gauni lenye rangi ya

    zambarau. Kiunoni mshipi wa rangi ya damu ya mzee pamoja na viatu vya rangi

    ya dhahabu. Hakika nilipendeza sana. Nilipendeza kupitiliza. Nywele zangu

    zikawa laini kama sufi na ngozi yangu iliteleza kama mtoto mdogo. Ule uzuri

    niliokuwa nikisifiwa kule duniani, niliona kama uchafu, huku Gamboshi

    ulikuwa maradufu. Nilitamani kujitazama muda wote. Tabasamu likanipoyoka

    na kumzawadia babu lile maridhawa. Babu alikuwa akinitazama huku

    akitabasamu kiukweli.

    aliniambia. "nilikueleza huku hakuna kinachoshindikana" kisha tulipotea na

    kutokezea katikati ya kundi kubwa la watu. Wake kwa waume wakiwa wamefurahi

    kupita kiasi.

    Nilimuuliza babu "Hawa wamefurahi nini?"

    Babu alikuwa na furaha sana siku hiyo, alinishika mabegani na kuniambia

    "hawa wote wapo eneo hili kushuhudia msichana wa kwanza akikabidhiwa

    mamlaka makubwa na mazito ndani ya Gamboshi haijapata kuwahi kutokea tangu

    kuumbwa kwa ulimwengu msichana aliyechaguliwa na mkuu mwenyewe wa ulimwengu

    huu. hakika ni furaha iliyoje kwa ukoo wangu na watu wote wa Matonde" babu

    alicheka sana. Alicheka, akacheka kupitiliza. mimi nilijisikia ufahari

    kuona kila mtu akicheza na kunisujudia mbele yangu. Watu walikuwa ni wengi

    sana. Wengi walikuwa wamefunika sehemu zao za siri na ngozi ya mnyama. Fisi

    na wanyama wengine nao walikuwepo kila nyuso iliyokuwa mahali pale

    ilionesha uchangamfu na furaha iliyoje nilicheka usoni na moyoni tabasamu

    likachanua hakika. kikaja kiumbe cha ajabu. Kiumbe kilichotetemesha

    Gamboshi nzima.



    ulikuja upepo ukavuma kwa muda mrefu sana. Kabla ya kusikika kelele za hapa

    na pale, kulikuwa na radi iliyopiga na kutoa cheche kutoka kila kona ya

    sehemu zote za Gamboshi. Ufinyu wa mwanga haukuwepo tena, kiumbe hicho

    kiling'aa sana. Kilikuwa ni kiumbe kirefu na kikubwa sana. Kila kiumbe

    hapo Gamboshi kilisujudu mbele ya kiumbe kile, hata babu pia. Mimi

    sikufanya chochote kwakuwa nilikuwa nimekalishwa mbele ya kiti pembeni na

    ambacho angekaa yeye kiumbe huyo. Alikuwa na macho yaliyong'aa sana. Mfano

    wa macho yake yalivyong'aa ni sawa na paka uliyemmulika gizani sehemu za

    machoni. Hakuwa na macho mawili, jicho moja tu tena lilining'inia juu ya

    paji la uso. Mdomo wake ulikuwa mkubwa sana na kichwa chake kilikuwa kama

    ndege aina ya korongo. Wote waliosujudu waliongea vitu ambavyo haikuwa

    rahisi mimi kufahamu walizungumza nini. Lakini waliongea lugha ya tofauti

    na Kiswahili na wala haikuwa kiingereza. Niliendelea kuwatazama, wakati

    kiumbe yule wa ajabu mwenye mwili wa nyoka sehemu ya chini ya kiuno chake

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    baada ya kiwiliwili cha juu , kukaa sehemu aliyoandaliwa. Yeye alivaa joho

    la rangi ya dhahabu. Dhahabu iliyong'aa sana. Hata viatu vyake vilikuwa ni

    dhahabu tupu. Alikuwa anatoa ala za muziki kila atembeapo. Ala zile

    zilipendeza sana kuzisikiliza. Kichwani alikuwa na taji la dhahabu

    lililomeremeta sana. Alishika kitabu Fulani kikubwa ambacho sikukifahamu.

    Alionesha kuwa na furaha sana. Alipokuwa akinitazama muda wote, alikuwa

    akicheka kwa furaha.

    aliliita jina langu huku akicheka

    "Bella"

    kabla sijageuka kukitazama kile kiumbe, eneo lote la Gamboshi likalipuka

    kwa makofi yaliyokuwa yakipigwa kila kona ya mkutano huo. Niliogopa sana

    kukaa karibu na kile kiumbe. Kikiongea kilikuwa kinatema moto

    nikamfananisha na zile katuni za dragoni. Mwili wote ulijaa jasho kwa uoga.

    Kile kiumbe kilitamka

    "usiogope mwanangu Bella"

    kikacheka sana, kisha kiumbe kile kikaendelea kuniambia

    "mimi ni mkuu wa wakuu wa ulimwengu huu. Mimi ndiye baba wa wababa wa

    vizazi vyako vyote vilivyopita. Mimi ndiye niliyekuandaa wewe kuja kurithi

    falme atakayoiacha Babu yako Mzee Matonde, mimi ndiye Lucifer mtakatifu

    kuliko wote awaye"

    nilshituka kwa mshangao ambao sikutarajia. Sikuzimia kutokana na hali kuwa

    mbaya eneo hilo. Macho yangu yalipokuwa yakielekea eneo la usingizi mzito

    wa kupoteza fahamu, mimi nilishindwa kuzimia kutokana na uoga.

    Nilimkodolea macho.

    Sikuamini ambacho kilikuwa kikitokea kwa wakati huo, Niliona kama ndoto.

    Kiumbe kile kikabadilika kikawa binadamu aliyevutia sana. Alikuwa ni mzuri

    kuliko mvulana mzuri yeyote ambaye uliwahi kumuona duniani.

    Hakikutisha tena.

    kila kiumbe katika mji wa Gamboshi kilipiga kelele. Yule kiumbe wa ajabu

    akafura kwa sifa kwa heshima aliyopewa.

    Alisema

    "ninao utajiri wa kutosha pamoja na nguvu nyingi. Mimi si mchoyo kwa yeyote

    aniombaye. Hutoa vipawa na karama kwa kila mtu anifuataye. Mimi humbariki

    kila mmoja lakini kuna adhabu kali kwa yeyote akiukaye maagizo yangu"

    nilimuona yue mtu aliyejiita Lucifer, akiwa amefura kwa hasira na uso wake

    kujikunja sana. Hakika alikuwa na hasira na ghadhabu sana. Mimi sikuwa

    nikimsikiliza kwa umakini ila niliogopa sana kwa kuwa sikuamini kama

    nimekaa karibu kabisa na yule wanayemuita shetani. Niliwaza mengi sana.

    Nilitetemeka kwa uoga lakini haikusaidia.

    labda nikuambie kitu. Huyu kiumbe ndiye yule aliyewahi kuwa mmoja wa

    malaika wakuu huko mbinguni. Yeye alikuwa na kazi ya kumsifu na kumuimbia

    mungu.

    Aliitwa Lucifer.

    baada ya kujiona yeye ni mmoja kati ya malaika walioumbwa vizuri kuliko

    malaika wote, akapatwa na kiburi. Kiburi cha kutaka kumpindua mungu. Kama

    utakumbuka mwanzo wa safari yangu ya huku Gamboshi, nilimuuliza babu kuhusu

    ule mji ambao niliuona kwa mbali ukiwa unang'aa na kupendeza. Akaniambia

    kuwa ule si mji mzuri kufikiria wala kutamani kuingia. Akasema kuwa kule

    ndipo alipokuwepo mkuu wao hapo mwanzo. Basi eneo lile naweza kusema ndio

    mbinguni na yeye Lucifer akatupwa ulimwenguni katika ziwa la moto. Kutokana

    na adhabu kuwa kali, aliapa kuondoka na kila mwanadamu wa kumdanganya. Ila

    kipindi hiki ambacho nilikuwa Gamboshi sikuweza kuwa na ufahamu wa kutosha.

    Hivyo niliendelea kukaa nikifurahia utukufu niliopewa. Watu walianguka

    miguuni mwangu kwa kusujudu. Nilijisikia ufahari sana. Sikujuwa kuwa

    nilifungwa ufahamu wangu.

    yule kiumbe wa ajabu akaendelea.

    "leo nitakukabidhi utawala wa babu yako. Utawala wa kusimamia Gamboshi na

    kushika wadhifa mkubwa Duniani. Utakuwa mtu wa heshima hapa na huko

    duniani. Utajiri utakutafuta na si kuutafuta kwa jasho. Mdomo wako utakuwa

    Baraka kwa kila ukinenacho na kukitamka. Laana iwe juu ya kila mtu

    atakayekulaani"

    babu alisogea mbele yangu. Babu alikuwa amevaa joho la rangi ya zambarau

    pia, kama gauni langu. Alikuwa amevaa taji kubwa kichwani mwake. Alishika

    fimbo mkononi.

    yule kiumbe wa ajabu alipomuona babu, alicheka kwa sauti kubwa sana.

    hakucheka kwa karaha bali fedheha. Hapa nikagundua mbali ya ubinadamu

    halisi hakuna kiume kilichocheka kwa kumaanisha furaha halali. Babu

    alilivua taji lake na kunivisha mimi, pamoja na kunikabidhi pete yake.

    Fimbo yake pia alinipatia; yule kiumbe wa ajabu akapaza sauti

    "nakukabidhi rasmi utawala wa babu yako. Utawala uliotukuka Gamboshi na

    ulimwenguni kote. Upate heshima nchini mwako na nje ya nchi. Uwe na utajiri

    wa kutosha kwa kutumia pete hiyo. Fimbo hiyo itibu kila ugonjwa

    utakaosumbua kila mtu akuombaye msaada, taji hilo uwe malkia wa ulimwengu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mzima lakini hayo yote ni baada ya kutimiza masharti haya nikupayo"

    alinyamaza kwa muda kabla hajaendelea. Babu alinitazama kwa jicho la

    huzuni. Sikujua ilikuwa hivyo kwanini.



    Fimbo hiyo itibu kila ugonjwa

    utakaosumbua kila mtu akuombaye msaada, taji hilo uwe

    malkia wa ulimwengu mzima lakini hayo yote ni baada ya

    kutimiza masharti haya nikupayo"

    alinyamaza kwa muda kabla hajaendelea. Babu

    alinitazama kwa jicho la huzuni. Sikujua ilikuwa hivyo

    kwanini. Mimi nilitabasamu kumpa moyo babu kuwa

    ningeyaweza yote ambayo ningeambiwa. Yule kiumbe wa

    ajabu, alikohoa kisha alizungumza.

    "masharti hayo ni kwamba tunamuhitaji yule mpenzi wako

    kama kafara. Ndugu jamaa na raiki zako hapa Gamboshi

    wanywe damu yake na kuila nyama yake katika sikukuu

    ya kukabidhiwa utawala wako" nilifahamu kuwa huyu

    kumbe alikuwa akimaanisha Jordan. Nilinyamaza

    kumsikiliza. Aliendelea

    " Pia usiongee na mtu yeyote kwa siku nzima mara

    utakapoamka leo ukitoka hapa Gamboshi. Usithubutu

    kulowa maji kwa muda wa siku tatu ikiwa mvua ama

    kuoga kufanya hivyo utatoa utawala wako katika koo

    nyingine na adhabu yako itakuwa ni kuongea milele na

    kutoa siri zako ovyo kwa yeyote hata usiyemfahamu.

    Wewe na maji mtakuwa maadui mpaka unakufa"

    sikukubali haraka. Mkutano mzima ulikuwa kimya kusikia

    kama ningekubali kufuata masharti ya kiumbe huyo wa

    ajabu. nilinyamaza kimya kwa muda. Babu aliuinua uso

    wake na kupaza sauti "Bella mjukuu wangu tunasubiri jibu

    lako ili tuweze kutawanyika"

    niliendelea kunyamaza. "na kama hutajibu leo, usitarajie

    kuamka milele siku ya kesho ukitoka hapa Gamboshi"

    nikaipata sauti yangu kwa uoga wa kitisho cha kiumbe

    huyo wa ajabu nikasema. "nitatimiza kila ninalopaswa

    kulitimiza" mkutano mzima ukalipuka kwa shangwe. Kila

    mtu alifurahi sana, furaha ikazidi kupitiliza. Babu

    alipongezwa kwa kuimaliza kazi, kazi ya kunikabidhi

    mikoba. Kazi iliyomchukua muda mrefu kuikamilisha. Kazi

    iliyopingwa na mama kwa muda mwingi, sasa ikawa

    kama kumsukuma mlevi. Kile kiumbe kikapotea kikiwa na

    furaha ya ajabu. Niliwaona wale wachawi wa Gamboshi

    wakila na kunywa. Nilipotoka kitini na kwenda kujumuika

    nao, nilistaajabu sana. Nilistaajabu kuona wakinywa damu

    ya binadamu kwa furaha wakitafuna nyama ya mtu. Babu

    alinipongeza kwa kuniambia kuwa "umefanya jambo zuri

    sana" alinikabidhi nyama ya mtu ambayo niliikataa.

    Sikuwa mzoefu ghafla kiasi hicho kuanza kula nyama ya

    binadamu mwenzangu. Ila kutokana na jinsi ilivyochomwa

    na babu alivyonilazimisha niinywe, nilijishangaa nikikakata

    pande na kulitia mdomoni. Ama kweli ndio maana

    tulikatazwa tusimle binadamu mwenzetu. Nyama ilikuwa

    ni tamu kupitiliza. Hakuna mnyama yeyote iwe wa

    kufugwa ama wa porini, aliupita utamu wa Binadamu. ila

    babu alilinisisitiza sana nisifanye kosa katika masharti

    niliyopewa

    "nitakuwa sina jinsi ya kukusaidia katika hili ukifanya

    kosa. Kwa kuwa umekubali mwenyewe" aliniambia

    "Hakikisha unatimiza yote uliyoambiwa"

    nilimkubalia babu huku moyoni nikiwa na jambo

    ninalolifikiria. Mawazo yangu moyoni, hayakuwa juu ya

    utawala wala wadhifa niliokabidhiwa. Mawazo yangu

    yalikuwa kwa Jordani. Sura ya Jordani ilikuja kwenye akili

    yangu na kunipotea kila nikikumbuka sharti nililopewa na

    yule kiumbe. Jordan mwanaume niliyempenda kuliko kitu

    chochote katika hii dunia. Sikutaka nimpoteze Jordani, si

    kwenye kifo hata kwa mwanamke mwingine. Ndio maana

    nikachuma bibo kutoka katika mti wa mkorosho

    nyumbani, nikajichora jina lake 'JORDANI' kwenye mkono

    wangu kwa kutumia utovu wake. Nilimpenda sana Jordan

    baada ya mama yangu. Sharti hilo ndio nililiona lingekuwa

    gumu kuliko yote niliyopewa hapo Gamboshi. Nikiwa bado

    Gamboshi kila mtu alipepesuka kwa ulevi wa furaha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tulirudi lile eneo ambalo mimi na babu tulibadilishia nguo.

    Nilizivua zile nguo abazo zilikuwa maalumu kwa ajili ya

    shughuli ile ya kukabidhiwa mamlaka na nguvu, kisha

    nikazivaa zile nilizokuja nazo. Babu akanieleza kitu cha

    ajabu sana aliniambia

    "Bella nimeitumikia Gamboshi kwa muda mrefu sasa.

    Inabidi nilipe fadhila kwa kila jambo walilonifanyia nikiwa

    duniani. Miaka yangu ya kuishi duniani ilishakwisha muda

    mrefu sana, ila niliongezewa muda wa kuwakabidhi wewe,

    urithi mamlaka yangu. Sasa ninatakiwa kuja kuishi huku

    Gamboshi nikipewa nafasi nyingine baada ya wewe

    kuikaimu nafasi yangu. Nitaishi huku Gamboshi mpaka

    wakati wangu wa kuishi utakuwa umekwisha kabisa"

    nilishangaa sana. Sikujuwa kama kumbe kuna miaka ya

    kuishi duniani na miaka ya kuja kuishi huku Gamboshi.

    Nilimuuliza babu hii inakuwaje. "sijaelewa kabisa" babu

    alinieleza

    "kwa sisi huku Gamboshi tunaishi miaka nusu kwa nusu

    nikimaanisha kama duniani ulitakiwa kuishi miaka

    themanini, utaishi arobaini duniani arobaini huku

    Gamboshi. Kwa hivyo wakati mimi naanza kuhiji huku

    Gamboshi nilipimwa na kugundulika nina miaka mia na

    nne ya kuishi duniani" nilishituka, macho yakanitoka pima.

    babu akaendelea

    "hivyo ndio maana nimeishi miaka sitini duniani na

    iliyobaki yote nitakuja kuishi huku Gamboshi"

    hapo nikawa nimemuelewa babu. Tulipomaliza

    kubadilisha nguo babu aliniambia kuwa nisimueleze mtu

    yeyote, ila siku chache zijazo atalala usingizi wa milele

    akiwa kitandani kwake. Hivyo nisishitushwe na hayo

    yatakayotukia kwa sababu ni lazima yatukie.

    Nilitamani kulia lakini alinieleza "mjukuu wangu mimi na

    wewe tutakuwa tunaonana mara kwa mara hivyo

    usiogope" nilijipa moyo kwa kutabasamu kinafki. Nilikuwa

    nimeshamzoea Babu. Ubaya wake sikuuona tena na

    nilimpenda sana. Nilihisi kuupenda uchawi zaidi kwa

    kipindi hiko, ila kila nikifikiria kuila nyama ya mwanaume

    nimpendaye, niliona ni jambo gumu sana kulitimiza. mimi

    na babu tulitoka Gamboshi tukarudi katika ulimwengu wa

    kawaida. Babu aliishi magomeni usalama mimi nilielekea

    Sinza nyumbani nilipobakia mimi na Mzee Nyegezi baada

    ya mama kufariki.

    ..........................

    Nilijikuta nipo kitandani Mzee Nyegezi alikuwa

    akiniamsha. Nilipiga ukunga mkubwa sana

    "haiwezekaniiiiiiiii!!!" Mzee Nyegezi aliruka pembeni na

    kuniacha. Niliendelea

    "siwezi kumuua Jordani" nilipoamka kabisa niliuona

    mshituko wa dhati wa Mzee Nyegezi.

    aliniuliza "una tatizo gani" Nilinyamaza. Nilinyamaza kwa

    kuwa nilikumbuka sharti nililopewa Gamboshi. "usiongee

    na mtu yeyote mara kutapokucha baada ya kutoka hapa

    gamboshi" sauti ya yule kiumbe aliyejitambulisha kama

    Lucifer, ilijirudia kichwani mwangu. Mzee nyegezi

    hakutoka hata nilipokuwa nimenyamaza muda wote.

    Niliushika mdomo wangu wa uoga nikijiuliza kama, Mzee

    nyegezi alisikia nilichoropoka, ama hakukitilia maanani.

    "Bella una nini? Umeanza kupiga kelele muda mwingi

    sana. Tangu usiku mimi sikulala kabisa" Aliposema hivyo

    nilijiuliza, hivi mbona Gamboshi nilichukuwa muda mrefu

    katika kila jambo lililotokea kule? sasa iweje Mzee

    Nyegezi ahesabu kama ilikuwa ni siku moja tu?

    nikajisahau nikamuuliza swali.

    "kwani nimelala kwa muda gani?"

    "sasa hivi ni saa tatu asubuhi na ulilala jana mapema

    hata chakula cha usiku hukula"

    nikakumbuka hapo hapo kuwa nimeshavunja sharti moja

    wapo kati ya yale niliyopewa kule Gamboshi. Nililia sana

    hata Mzee Nyegezi asijue nilikuwa nalilia nini. Nilimpiga

    kikumbo mzee nyegezi na kuelekea chooni kunawa uso

    huku nikiwa nalia. Chooni ndipo nilikutana na babun Babu

    alikuwa akilia na yeye pia. Alilia machozi mfano wa damu.

    Aliniuliza

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ina maana mjukuu wangu yote niliyofanya kwako

    yamekuwa ni bure kabisa?"

    nilikabwa na kitu kooni hata nikashindwa kuongea nililia

    kwa uchungu ambao sikuwahi kuupata tangu nijitambue.

    Nilimuomba babu msamahan "nisamehe babu. Naomba

    uniombee anisamehe mkuu wa Gamboshi" Babu alinivunja

    moyo kabisa, aliniambia. "tazama jinsi Gamboshi

    ilivyohuzunika, tazama kwa macho yako" kwa kuwa ukuta

    wa choo chetu ulikuwa mweupe sana ikawa kama sinema

    nilipotazama aliponioneshea kwa kidole. Ilikuwa ni taswira

    ya Gamboshi.

    Mkuu wa Gamboshi ambaye ni yule Lucifer, alikuwa

    amekasirika sana. Babu alinionesha hadi kwenye makazi

    yake alipokuwa akiishi yeye lucifer. Kutokana na hasira,

    alikuwa akibadilika kila mnyama. Moto ulimtoka mdomoni

    kwa hasira iliyomzidi na kushindwa kujizuia kupunguza

    hasira zake. Hakika nikagundua nimefanya makosa

    makubwa sana.

    babu alinieleza "kuanzia sasa umepokonywa utawala na

    wadhifa wako wote umevuliwa kutoka Gamboshi.

    Hutakuwa na nguvu zozote, bali utakuwa na uwezo kama

    wa mchawi yeyote yule." babu alinyamaza kisha

    aliniangalia kwa huzuni. Mimi nilikuwa nalia sana, hata

    macho yalifumba kwa machozi. babu aliendelea "sijajua

    mkuu atakupa adhabu gani ila amekasirika sana sina cha

    kukueleza" babu akatoweka kabla sijamueleza chochote.

    siku hiyo nikawa nimeianza vibaya. Mzee Nyegezi

    hakuthubtu kuniuliza kitu kingine niliporudi chumbani na

    kupishana naye kibarazani. Alikuwa akinitazama tu,

    alipokuwa akielekea nje. Nilipokuwa chumbani, nilikaa

    kimtegomtego, nikimtegea babu nikidhani labda ningesikia

    ujio wake. Upepo ungevuma, kama siyo radi ingepiga

    baada ya mngurumo wa kutisha. Nilitamani kujua

    chochote kutoka Gamboshi. Niliumia sana kuukosa

    utawala niliokabidhiwa. Nikamuona mzee Nyegezi ni mtu

    mbaya sana kwangu. Nikamchukia kwa kuniamsha

    asubuhi na kunifanya nizungumze. Kuzungumza kule

    kulinifanya nivunje sharti. Moyo uliniuma kila nilipofikiria

    kuona kuwa sharti dogo nililodhani ningeliweza, kumbe

    hilo ndio lilikuwa gumu sana kwangu. Niliutamani tena

    ukuu na uwezo niliokabidhiwa kutoka katika kiti cha urithi

    wa babu. Mawazo yakanisonga, mawazo yakanifanya hata

    nisahau kufanya mambo mengine. Kwa sababu ya

    mawazo, nilisahau hata kula wala kupika. Kwa sababu ya

    mawazo, sikujua nilijilaza kwa muda gani hapo kitandani

    kichwa changu kikielea juu ya kidimbwi kidogo cha

    machozi. Kwa sababu ya mawazo, mawazo yakawa

    mawazo, nikapitiwa tena na usingizi. Niliamka saa nne ya

    usiku, tena si kwa kupenda ni Mzee Nyegezi ndiye alikuja

    kuniamsha. Alipatwa na wasiwasi jinsi nilivyolala. Nililala

    tangu jana mapema, lakini nilichelewa kuamka.

    Aliponiamsha saa sita mchana nilimuacha chumbani na

    niliporudi chumbani niliendelea kulala mpaka sasa.

    alizungumza na mimi kwa upole "Bella kama unaumwa

    sema. Kukaa kimya si vizuri" mimi sikumjibu kitu.

    Nilimchukia sana Mzee Nyegezi. Nilimuona Mzee Nyegzi

    hakuwa akinitakia mema. Alining'ang'ania kunibembeleza

    mpaka nilipoamua kuzungumza. "siumwi nipo sawa"

    nilimjibu kwa dharau sana. Lakini hakuweka ukali katika

    sauti yake. "sasa kwanini unalala lala oyo? Jana umelala

    saa moja jioni. Nimekuja kukuamsha leo saa sita mchana,

    nashitushwa kukukuta umelala tena. Umekula nini leo?"

    niliendelea kumjibu kwa dharau nikibetua midomo yangu

    kama shangingi.

    "ningesikia njaa ningeamka kupika" aliendelea "najua

    unajisikia vibaya kutokana na kifo cha mama yako,

    hakuna ambaye hajaguswa nacho. Tafadhali Bella usiwe

    mnyonge kiasi hicho nipo hapa kwa ajili yako" alitoa noti

    tano za elfu kumi na kunipatia baada ya kunibusu.

    Nilimsonya na kujilaza tena kitandani.

    nikiwa nimejilaza huko, kile ambacho nilikuwa nikikisubiri

    tangu mchana nilikisikia kikinijia. Ilikuwa ni sauti ya

    upepo mkali sana. Mngurumo mkubwa wa radi, ulisikika

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kila pande. Tetemeko la ardhi likatokea katika chumba

    changu na kukipasua chumba changu katikati. Wakati

    hayo yakitokea. Mlango wa chumba changu ukafunguliwa.

    Alikuwa Mzee Nyegezi.

    aliniambia "pipa halina maji hata kidogo, hakikisha

    unayakinga haya ya mvua kisha urudi tena kulala" wakati

    akiyaongea hayo, mimi nilikuwa nikipatazama pale

    palipopasuka. Kulikuwa vile vile na moshi mzito ulikuwa

    ukifuka kutoka katika shimo hilo. Nilikuwa nikimuangalia

    Mzee Nyegezi, hakuonesha kama aliona kile ambacho

    mimi nilikuwa nikitazama. Niljifanya kumskiliza kwa

    makini na kumkubalia alichoniagiza.

    Alipoondoka nilijiuliza. Nilijiuliza ina maana hakuona

    kilichotokea chumbani kwangu? Chumba changu

    kilipasuka na kuweka mfano wa bonde la ufa. Ndani yake

    akatokea kiumbe aliyetisha sana. Nilianza kutetemeka

    kwa uoga uliopitiliza. Kiumbe huyo alikuwa na uso wa

    babu, Mzee Matonde. Babu alikuwa akilia machozi ya

    damu. Sikujuwa machozi hayo yalikuwa yakimaanisha

    nini. Mara kwa mara babu alikwa akilia hivyo. Alikuwa na

    mwili wa mnyama. Babu alikuwa na mwili wa fisi, fisi

    mwenye miguu mikubwa sana kama ya tembo. Fisi huyo

    hakuwa wa kawaida. Alikuwa na mabawa kama ndege na

    meno marefu kama ngiri. Shimoni alipotoka, kulikuwa

    kukifuka moshi mzito sana. Moshi huo ulisindikizwa na

    harufu kali ya uvundo. Joto la chumbani lilizidi na

    kunifanya nihisi kama nipo karibu na moto mkali wa

    jikoni. Nilivuja jasho japo sikujua lilikuwa ni jasho la

    uwoga ama hili la joto kali.

    Kiumbe kile kikapata sauti yake iliyotisha. "mjukuu

    wangu" nikajuwa kuwa alikuwa ni babu

    "kesho asubuhi utapata habari za msiba wangu. Lakini

    hakikisha mwili wangu haufanyiwi maombi wala kuagwa

    na watu wengi." nilishitushwa na habari hizo. Japo

    nilikwishajua kiumbe yule ni babu, sikuwa na uhuru nafsini

    mwangu. Alikuwa akitisha sana. Nilimuuliza

    "kwanini hayo?" akaniambia "mimi nitakuwa sijafa ndiyo

    sababu ya kukueleza ufanye hayo"

    "sasa babu, mimi nitawezaje kuzuia watu wasiuage mwili

    wako au wasiuombee?"

    Aliniambia "nitakupa uwezo huo wa kuongea chochote

    ukakubalika bila kupingwa kwa swali lolote" hiyo

    iliniduwaza pia nilikubali bila kumpinga. Nilimuuliza babu

    kwa kuropoka "babu"

    alikuwa tayari anataka kuondoka, akasimama alipokuwa

    akitaka kuingia shimoni alipotokea.

    "Nataka kufahamu mkuu anasemaje?" akanijibu

    "tutazungumza baada ya msiba wangu"

    kisha babu alidumbukia shimoni humo. Mzee Nyegezi

    alikuja tena chumbani kwangu

    aliniuliza kwa ukali "bella umekuwa na tabia gani sasa

    hivi?" nilishitushwa na swali hilo mara tu alipoingia.

    "kwanini baba" akanijibu kwa hasira "si nilikueleza uamke

    ukinge maji"

    nilishangaa sana ile hali. Ni kweli mvua ilikuwa kubwa,

    lakini cha kushangaza mara tu babu alipotoweka, mvua

    ilikatika. Hata lile joto lililonivujisha jasho jingi, likapotea.

    Nilimjibu baba

    "si imeshakatika?" akaniamba "sasa nataka kesho uamke

    mapema ukakinge kwa mama Tunnu" nilimkubalia na yeye

    akaondoka. Nililala kwa usingizi wa mang'amung'amu.

    ..........

    Hata asubuhi ilipofika, bado sikujuwa nililala saa ngapi.

    Mzee Nyegezi, alikuja mbio chumbani kwangu "Bella

    amka... we Bella.. bella" alikuwa amevaa singlendi na

    bukta nyepesi. Niliogopa sana. Nilijifuta uso kutoa

    tongotongo kwa kiganja cha mkono.

    alikuwa ameshika simu "shangazi yako anataka kuongea

    na wewe" Baba alikuwa na wasiwasi sana. Ila niliipokea

    simu kutoka kwake na kuongea "shikamoo shangazi"

    nilichokisikia kutoka upande wa pili, sikutamani kusikia

    mara ya pili. Ilikuwa ni sauti ya shangazi akiwa analia.

    Alikuwa analia huku akimtaja babu. Ndipo nilipomuuliza

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "shangazi kuna nini kwani? Babu kafanya nini?" kwa sauti

    ya kilio alinijibu "babu yako amekufaaa Bella" shangazi

    aliongea kwa huzuni sana "Bella babu yako Mzee Matonde

    amekufa kiajabu mwanangu. Mzee Matonde kipenzi

    chako. Kwanini sisi. Kwanini Bellaaaa"

    simu iliniponyoka na kudondoka chini. Midomo yangu

    ilianza kucheza shere kwa kugongona gongona ya juu

    ikaipiga ya chini. Nikabubujikwa na machozi. Mzee

    Nyegezi alikuwa akinitazama muda wote, sasa

    alinisogelea. "pole Bella" aliniambia kwa sauti iliyopwaya.

    mimi nililia sana, kwasababu babu Mzee Matonde hakufa.

    Ukweli nilioufahamu kuhusu babu, uliniongezea

    machungu. Hicho ndicho kilichoniumiza sana.

    nikakumbuka babu alivyoniambia jana usiku "kesho

    asubuhi utapokea habari za kifo changu. Hakikisha mwili

    wangu hauombewi wala haugwi na watu wengi" ilinibidi

    nifanye haraka kuelekea alipokuwa akiishi babu, si mbali

    sana na nyumbani; Japo ilinilazimu kupanda gari kwanza.

    Mzee Nyegezi naye alitoka chumbani na kwenda

    kujiandaa aliniambia "nitaelekea kwanza ofisini, kisha

    nitakuja baadaye msibani" nikajibu "sawa" nilizivua nguo

    zangu nikajitundika taulo langu safi jeupe. Nikachukuwa

    sabuni na kwenda kuchota maji kwenye jaba lililopo jikoni.

    Nilipomaliza kujipimia maji niliyoona yanatosha, niliinua

    ndoo yangu mswaki mdomoni na kuingia bafuni. Nilianza

    kwanza kupiga mswaki. baada ya kumaliza kupiga

    mswaki, nikalivua taulo langu na kuliweka pembeni.

    Nikausahili mwili wangu kwenye kioo kilichopachikwa

    ukutani. Hakika niliumbika. Ukubwa ulioanza

    kuninyemelea ukanitunisha mapaja yangu na kuwa

    mrembo haswa. Nikatabasamu kidogo kisha nikairudia

    ndoo yangu ya maji. Nilichota kopo moja la maji ile

    kujimwagia tu usoni, nilianza kuwashwa. Sikuanza

    kichwani, kwasababu kama ujuavyo wanawake

    kujimwagia maji kichwani kwetu ni sumu. Uso ulianza

    kuwashwa sana, mara ukafuatia mwili mzima. Niliwashwa

    kupitiliza kama nimejimwagia upupu. Nikawa najikuna

    hapa, mara pale. Chini ya matiti yangu, mara mgongoni.

    Kucha pekee hazikutosha. Nikajipeleka ukutani. Najikuna

    lakini wapi. Muwasho ukazidi. Nikaendelea kuwashwa

    zaidi. Muda wote huo sikushituka mapema kama nilikuwa

    sioni kitu chochote. Sikujuwa kama macho yangu

    yalikuwa yamefumba. Sikujuwa kama nilikuwa nikitembea

    kwenye giza nene.



    Chini ya matiti yangu, mara mgongoni.

    Kucha pekee hazikutosha. Nikajipeleka ukutani. Najikuna

    lakini wapi. Muwasho ukazidi. Nikaendelea kuwashwa

    zaidi. Muda wote huo sikushituka mapema kama nilikuwa

    sioni kitu chochote. Sikujuwa kama macho yangu

    yalikuwa yamefumba. Sikujuwa kama nilikuwa nikitembea

    kwenye giza nene.

    "nimekuwa kipofu" nilijiuliza kwa uoga. nikapapasa

    ukutani kwa shida na kulitwaa taulo langu. Nikajifunga

    mpaka eneo la kifua na kulifanya liwe fupi kidogo. hapo

    hapo nikausikia mguso wa mkono ukiugusa mgogo

    wangu. Niliuputa ule mkono kwa uoga na kugundua

    ulikuwa ni mkono wa mnyama. Mkono ulikuwa na

    manyoya manyoya kila sehemu. Nilipiga kelele za kuomba

    msaada "baba nakufaaa" sauti yangu haikufika popote

    kumbe aikuwa ni babu. Nilimgundua ni yeye baada ya

    kunitibu na kupata kuona tena. Alinitibu kwa kunishika

    macho yangu huku akiongea maneno Fulani ambayo

    sikuyaelewa kwa urahisi. Alikuwa akiyafikicha fikicha

    baada ya kupaka mate kiganja chake. baada ya kufumbua

    macho, niliona mwanga mkali sana. Kisha ukapotea. babu

    aliniuliza. "umefanya nini?"

    sikumuelewa babu alimaanisaha nini hivyo ilinibidi

    nimuulize. "babu kuna nini?"

    babu hakunijibu chochote. Aliniangalia kwa huzuni kisha

    linionesha kwa kidole chake katika kioo. Ilikuwa ni taswira

    ya Gamboshi. Hapa alinionesha ile siku ambayo nilikuwa

    nikikabidhiwa mamlaka yake. Yule kiumbe wa ajabu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alikuwa akinipa masharti ya kuyafuata.

    "hakikisha maji hayagusi mwili wako, iwe ya mvua ama

    ya bomba. Iwe hivyo kwa muda wa siku tatu" hapo

    nikalijua kosa langu. Sikuongea chochote mbele ya babu.

    Nilitazama chini kwa aibu. babu aliniuliza tena. "Bella

    kama hukuwa tayari, kwanini ulikubali kupewa masharti

    haya?" nililia "babu nisamehe" babu alinikatisha kwa sauti

    ya ukali "nikusamehe? Nikusamehe vipi?" alikuwa

    amekasirika sana. kadiri babu alivyokuwa amekasirika,

    ndipo alikuwa akiongezeka urefu. Alikuwa mrefu.

    Akaongezeka zaidi. Alikuwa mrefu kupitiliza hata unyayo

    wa miguu yake tu, ndiyo iliyobaki bafuni. Vidole vyake

    vikagusa bati na kulitoboa kabisa. Kisha alirudi kwa

    nguvu za ajabu. Alikuwa akitoa moto alipokuwa akirudi

    katika hali yake ya kawaida. Alikua kama yule muhusika

    wa kwenye filamu ya ghost rider. akaniambia kwa sauti

    iliyotetemeka "umeniuzi sana, umemuuzi mkuu. Siwezi

    kusema nimekusamehe ikiwa sio mimi niliyekupa yale

    masharti." hapo akaacha kuongea kwanza. Alikohoa,

    akakohoa sana kama aliyepaliwa na chakula. Akaniambia

    "acha niende. Nimekuja kukuponya upofu ulioupata ili

    uende katika msiba wangu ukawaonye wasiuombee mwili

    wangu" aliniangalia kwa huzuni kisha aliniambia "Bella

    una kazi ngumu na adhabu kali mbele za mkuu" babu

    alitoweka kisha akauacha moshi mzito sana bafuni.

    Sikuoga tena Nilitoka bafuni na kurudi chumbani. Nilivaa

    nguo za kawaida tu ndani kisha nilijitanda kanga mbili za

    aina moja. Hatimaye nilitoka kulekea msibani. eneo la

    msiba lilifurika watu wengi na kujaa simanzi nzito. Rafiki

    zake babu walikuwepo ndugu na wengine ambao

    sikuwafahamu, wote walikuwa wana huzuni kubwa. Ndugu

    waliponiona walilia kwa sauti ya juu sana. Naweza

    kusema kwa upande wa baba yangu mzazi, babu

    alinipenda sana mimi kuliko hata watoto wake aliowazaa.

    Alinipenda kuliko kitu chochote au mtu yeyote. Hakuna

    mtu ambaye alikuwa hajui kwamba babu alikuwa

    ananipenda kiasi kile. Tuliingia chumbani ilipo maiti ya

    babu ikioshwa.

    shangazi mkubwa aliyebaki, akasema "hajafa katika

    mapenzi ya mungu. Hapa kuna jambo. Inabidi tumuite

    mchungaji kabla hajazikwa" mimi niliogopa sana. Sauti ya

    babu ikajirudi kichwani mwangu kama mwangwi.

    "hakikisha mwili wangu hauombewi" Nikapata nguvu ya

    kuzungumza "hapana shangazi. Huyu asiombewe wala

    kuagwa ninaomba iwe hivyo"

    sikuwa na hakika kama shangazi angekubali kile

    nilichomueleza kwa sababu aliniangalia kwa jicho kali

    sana kisha alisema. "Bella!?" alinishangaa kwa tuo. Mimi

    macho yalinitoka nisijue nitafanya nini akaendelea.

    "kwanini hutaki babu yako asiombewe, wala kuagwa?"

    Nilijua ni lazima mtu yeyote angeuliza swali kama hilo.

    Mtu yeyote mwenye akili timamu, angeniona kama

    niliyeanza kurukwa na akili. Hivyo nikashikwa koo na

    kigugumizi cha ghafla. Kigugumizi nisijue nitajibu nini? Si

    shangazi pekee aliyeshangazwa na jambo hilo! Hata mimi

    pia sikuelewa nilipoambiwa kwa mara ya kwanza. Mimi

    pia nilijiuliza sana, kwanini mwili wa babu usiagwe wala

    kuombewa?. "mimi sijafa katika mpango sahihi, Hivyo

    katika kuagwa huko, kuna watu ambao wanaweza kutoa

    siri kuwa mimi sijafa na sipo katika lile jeneza"

    nikaikumbuka sauti ya babu. Nilichoambulia kukifahamu

    kutoka kwa wachawi, yaani wanapoua mtu kabla siku

    zake za kufa hazijafika, basi humchukuwa na kwenda

    kumuhifadhi sehemu ambayo humtumikisha kazi nyingi

    sana. Kama vile kulima shamba kubwa sana, ambalo

    huchosha hata kikundi Kikubwa cha watu lakini msukule

    mmoja hulima ndani ya dakika chache. Hubeba mizigo ya

    wachawi au kwenda kuleta damu, baada ya kusababisha

    ajali katika barabara kuu iendayo mikoani. Na pale katika

    jeneza wanaweka mgomba ambao humuwakilisha yule

    mtu ambaye amechukuliwa msukule. Watu ambao

    hawana uwezo wa kichawi hawawezi kugundua kama ule

    ni mgomba. Bali mchawi pekee au mwenye nguvu kweli

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    za kimungu. Wazazi ndugu jamaa na marafiki zake

    marehemu, Wanaweza hata kulia kwa kumshika mshika

    kwa huzuni, lakini wasione tofauti yeyote na mwili wa

    kawaida. Ila kwa babu hakuwa msukule. Babu alikufa ili

    kwenda kuitumikia Gamboshi baada ya mkataba

    walioafikiana kutimia. Hivyo alikuwa analipa fadhila.

    Fadhila ya kipumbavu, fadhila ya kijinga, fadhila ya

    kishenzi kutoa uhai wako kwenda kuishi katika mji wa

    kichawi Gamboshi.

    Nilipokuwa katika kuwaza nisijue nini nimjibu shangazi.

    Ghafla mbele yangu nilimuona babu. Babu alikuwa

    akitabasamu. Aliniambia "usijali nitakusaidia" Kisha

    alipotea.

    nilimgeukia shangazi mara baada ya tukio hilo la

    kushitukiza. Nikataka nimjibu, akaniambia huku

    akitabasamu. "Bella umeanza kuwa na akili sana

    mwanangu" alinishika shika kichwani na kutabasamu kwa

    raha. Nilijiuliza shangazi alikuwa akimaanisha nini?

    Nilibaki katika bumbuwazi ya ajabu, nisijue nini shangazi

    alimaanisha. Aliendelea "basi nitapinga mwili wa babu

    yako usiagwe wala kuombewa, ila ni ngumu sana

    kueleweka kwa watu timamu"

    nilishangaa sana. Kukubali huko kwa shangazi. Lilikuwa ni

    jambo la haraka, wakati mimi sikujibu chochote!

    Kulinifanya nijiulize maswali mengi. 'babu alitumia kinywa

    changu kumjibu shangazi, bila mimi kufahamu? Alimfunga

    akili shangazi hata asikumbuke kuwa hilo ni jambo la

    kushangaza? Mwili usiagwe wala kuombewa? Ni ajabu na

    inayoshangaza?'

    mshituko wangu haukuwa na madhara yoyote kwa

    shangazi. Hakuniuliza jambo lolote, tukatoka chumba cha

    kuoshea maiti ya babu. Ndugu waliokuwa wakisubiriwa

    kutoka katika kila pande ya visiwa vya ukerewe. Visiwa

    ambavyo babu ndipo alipozaliwa, walikwishafika baada ya

    siku tano za msiba baadaye. Shangazi aliwaeleza

    nilichomueleza. "naona ni vyema tukamsikiliza kama

    alivyosema" nilishangazwa na kaka zake babu,

    walivyounga mkono hilo jambo. Ila mmoja aliweka

    pingamizi. Hapo ndipo palinigusa, nikataka nifahamu. "ila

    nyinyi jamani mbona tunataka tuishangaze jamii?"

    alikuwa ni shangazi aliyemfuata yule niliyekutana naye

    kule Gamboshi, kuzaliwa. Ndugu wa baba niliwafahamu

    kutokana na babu kunitambulisha kwa sauti ya kawaida

    bila mtu yeyote kusikia. Babu alikuwa eneo hilo la msiba

    bila mtu yeyote kumuona. "wewe dada Suzi embu

    nyamaza. Wewe ufahamu kuwa Bella ndiye mrithi wa

    mizimu ya ukoo wetu?" nilipigwa na butwaa. Hata hawa

    walifahamu kuwa mimi tayari nimekwisha zuru

    Gamboshi? Yule aliyemnyamazisha shangazi Suzi,

    alinigeukia na kuniambia. "mwanangu sawa tumekuelewa.

    Usijali kuhusu hilo, tutafuata kila ulichotuelekeza." kikao

    cha familia kikavunjwa baada ya lile nililoliongea

    kupitishwa bila kupingwa zaidi. Msiba ulienda kimipango

    bila kuvunjika hata moja. Babu akazikwa katika makaburi

    ya kigogo mburahati.

    .........................................

    Baada ya msiba, ndugu wa baba ambao hatukuwahi

    kuonana kabisa walijitambulisha kwangu na mimi kwao.

    Wengi walipendezwa sana kuniona na mimi sikuzificha

    hisia zangu kuwa pamoja nao. Nilifurahi sana. Shughuli

    nyingine zikaendelea. Siku moja mimi na baba mkubwa

    Christopha tulikuwa nje ya nyumba chini ya mti wa

    mchikichi tukizungumza.

    Baba mkubwa aliniuliza "sasa Bella ilikuwaje ukavunja

    masharti?" kikohozi kikavu kikanipitia. Nilikohoa sana

    kabla sijamjibu lolote, aliniambia tena."unafahamu sababu

    ya kifo cha babu yako?" nilimjibu kwa wasiwasi. Hii

    ilitokana na kudhani kuwa huenda kuwa sababu ya kifo

    chake ilikuwa ni siri yangu pekee yangu. Nilimwambia

    "hapana sifahamu baba" nilinyamaza kidogo kumeza

    mate kisha niliongeza "ninachofahamu ni kifo cha ugonjwa

    wa ghafla tu. Nadhani inaweza ikawa ni uzee?" nilijitia

    kuuliza swali ili nimchimbe alichotaka kunieleza.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    aliniamba yote yaliyohusu kifo cha babu yangu. "babu

    yako amejitoa kafara baada ya wewe kushindwa

    masharti. Kifo chake kimesababishwa na wewe.

    Hakustahili kufa, ila wewe" mshangao ulikuwa wazi katika

    macho yangu na uso wangu. Midomo yangu ilitetemeka

    sana kwa uoga. Nikamuuliza. "nahisi sijakuelewa baba?"

    alitabasamu kwa kejeli na kuniambia "ulipopewa masharti

    yale matatu na ukashindwa kutimiza, babu yako

    aliambiwa kuwa baada ya siku tatu ungekufa, ungekufa

    kinyama. Ndipo alipobatilisha adhabu hiyo na kuongea na

    mkuu wake na kuomba adhabu hiyo apewe yeye." bado

    nilikuwa nikishangaa nisijue chochote anachonieleza kati

    ya hivyo. Nilikuwa gizani, hata babu alinificha. Sikujua

    sababu ya babu kunificha jambo kama hilo.

    baba mkubwa alinieleza jambo lingine "umewahi kujiuliza

    kwanini babu yako hutoka machozi ya damu kila

    alipokuwa akikutokea?" macho yangu yakapata nuru ya

    ajabu na kuwa na shahuku ya kutaka kujua sababu.

    Jambo hilo la machozi ya damu lilinichanganya sana.

    Nilijibu kwa shahuku ili nifahamu ilikuwa inasababishwa

    na nini. "hapana sifahamu. kwanini alikuwa anatoa

    machozi ya damu?" akaniambia "inatokana na..."

    ghafla sauti yake ikaishia mdomoni kwake. Nadhani hata

    masikio yake mwenyewe hayakuisikia sauti yake vyema.

    Hili likanishangaza. Nikamuuliza "baba una nini?"

    macho yalinitoka kwa uoga. Yeye alikuwa akijitahidi

    kupiga kelele lakini sauti haikutoka. Nilitoa mbio

    tulipokuwa tumekaa na kwenda kuwaita ndugu zetu

    wengine. Walipofika tulipokuwa tumekaa, baba mkubwa

    hakuwepo. Nilishituka sana. Shangazi Suzi aliniuliza

    "we Bella! Yuko wapi sasa?" kwa kuwa bado sikuelewa

    kilichotokea, niliwaeleza kwa kunyoosha kidole. Mara

    nikaipata sauti yangu "alikuu..wa alikuwa hapa jamani"

    kila mtu alikuwa katika hali ya kutaharuki asijue nini

    kimetokea. "kwani mlikuwa mnazungumza nini na nini

    kilitokea" Shangazi Suzi aliniuliza "tulikuwa tumekaa hapa

    na yeye alikuwa ananieleza sababu ya kifo cha babu"

    kabla sijamaliza kuongea, sauti ya babu ikasikika

    masikioni mwangu. "usimueleze yeyote kuhusu ulilosikia"

    nilipokuwa nikiitafakari ile sauti. Yule shangazi mkubwa,

    aliniuliza "bella una nini? Mbona umenyamaza" Nilimjibu

    yule shangazi "alikuwa akinieleza jinsi ambavyo babu

    alikuwa akinipenda sana. Alinieleza ambavyo baba yangu

    mzazi alikuwa ni mtu wa watu na kifo chake kilisikitisha

    wengi"

    Ilibidi nidanganye. wengine walifahamu hila zangu na

    kuondoka nilipo. Mimi mahali pale nikabaki nikiwa na

    shangazi mkubwa na Suzi, wakinidadisi hili na lile. Macho

    yangu muda mwingi yalikuwa yakiangalia juu ya mchikichi

    huenda angekuwa amebebwa na babu, lakini hakuepo.

    Nikatazama njia ielekeayo barabarani labda nilidhani

    angekuwa akija, napo kukawa patupu. Wote tukaingia

    ndani kwa kuwa tayari ilikuwa jioni. tukiwa tunasimuliana

    hadithi mbalimbali, tulishituswa na sauti ya uoga aliyoitoa

    shangazi Suzi. Shangazi alikuwa ameenda chooni. Hivyo

    alitoka mbio mpaka sebuleni tulipo sisi. Alikuwa na jasho

    jingi usoni na uoga uliujaza uso wake. "kuna nini?" baba

    mdogo Joseph, alimuliza shangazi. Shangazi alikuwa

    ametoka chooni, chupi ikiwa chini, sketi akiwa

    ameishusha kama kawaida, macho kayatoa pima. Bila

    shaka yale maji maji niliyoyaona yakichuruzika miguuni,

    ulikuwa ni mkojo uliomtoka ghafla. Wachache tukamcheka

    kwa kuwa shangazi huyu, ndiye alionekana kuwa mtundu

    katika familia yote ya watoto wa Babu. "nimekutana na

    James chooni" alizungumza macho kayatoa isivyo

    kawaida. Alikuwa akituangalia sisi kisha akigeuka

    akiitazama njia ielekeayo choooni. Wote kwa pamoja

    tukaanza kushituka na kukaa kwa uoga. Wachache

    tulisimama kama tulikuwa na ujasiri wa kuelekea chooni

    vile.

    shangazi mkubwa akauvunja ukimya "chooni?" ghafla

    kicheko cha baba mkubwa James, kikasikika kikija eneo la

    sebuleni. Nilimshuhudia shangazi Suzi akitaka kukimbia,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    lakini kukawa hakuna njia zaidi ya kuelekea popote. Hivyo

    akawa akiwasukuma ndugu wengine. Alikuwa baba

    mkubwa James mwenyewe. Alikuwa kama vile ambavyo

    nilikuwa naye mchana. Alikuwa akitabasamu kama

    hakuna lolote lilitokea. Alinitazama kwa furaha na

    kuwaangalia wengine zamu kwa zamu. Kila mtu

    alishangaa kwa kujiuliza maswali kadha wa kadha.

    Maswali ambayo yalijionesha dhahiri juu ya nyuso zao.

    Hakuna ambaye alipata ujasiri wa kumsogelea wala

    kuongea naye chochote. Ni mimi peke yangu nilitoka

    nyuma ya shangazi yule mkubwa na kumfuata baba

    mkubwa Nilimuuliza. "baba mkubwa" kabla sijaendelea

    kuongea chochote, aliniziba mdomo na kuniambia

    ninyamaze. Alikuwa akitabasamu, hakika alitabasamu kwa

    furaha. Baba mkubwa, alizungumza sasa "kwanini

    mnaniogopa sasa?" nilimsikia yule shangazi mkubwa

    akicheka. Naye alitoka alipo na kumsogelea baba

    mkubwa. Alimuuliza "hivi wewe James" hawa walipishana

    kuzaliwa. Alianza Shangazi kisha Baba mkubwa james.

    shangazi akaendelea "huoni hata mdogo wako ametoka

    na chupi chooni kwa uoga?" alikuwa akimuoneshea

    Shangazi Suzi. Kwa kweli hakuna ambaye alijizuia

    kucheka siku hiyo. Tena walicheka kwa nguvu hata

    shangazi akaona aibu. Nadhani hata yeye mwenyewe

    hakujijua kuwa chupi ipo chini. Aliivaa haraka haraka

    kisha shangazi mkubwa aliendelea "ulikuwa wapi?" baba

    mkubwa James akacheka, kisha alisema. "nilikuwa

    chooni, kwani nimetokea wapi?" nikauliza ghafla

    "umewazaje kuongea tena? Kila mtu akashangaa

    "kuongea?"walinyamaza kwa pamoja. Nilipowatazama,

    shangazi Suzi aliuliza "kwani alikuwa haongei huyu?"

    baba mkubwa James alinishika mkono wangu kisha

    alinibinya binya ninyamaze kuongea na kuwaeleza "wakati

    nipo na Bella pale chini ya mti nilikabwa na tunda ambalo

    nilimeza mbegu zake, sasa ndipo alipokuja kuwaita ninyi

    na mimi nikawa nimetoka kuelekea chooni" kila mtu

    alicheka kwa kuudhika. Shangazi mkubwa akasema.

    "wewe James usitufanye sisi wajinga. Ni masaa mawili

    yamepita sasa, tangu wakati ambao hujaonekana. chooni

    kote tumekutafuta, mpaka chini ya uvungu hukuonekana.

    Sasa huko chooni ulienda choo kipi" shangazi aliuliza kwa

    ukali kidogo.



     Nilipowatazama,

    shangazi Suzi aliuliza "kwani alikuwa haongei huyu?"

    baba mkubwa James alinishika mkono wangu kisha

    alinibinya binya ninyamaze kuongea na kuwaeleza "wakati

    nipo na Bella pale chini ya mti nilikabwa na tunda ambalo

    nilimeza mbegu zake, sasa ndipo alipokuja kuwaita ninyi

    na mimi nikawa nimetoka kuelekea chooni" kila mtu

    alicheka kwa kuudhika. Shangazi mkubwa akasema.

    "wewe James usitufanye sisi wajinga. Ni masaa mawili

    yamepita sasa, tangu wakati ambao hujaonekana. chooni

    kote tumekutafuta, mpaka chini ya uvungu hukuonekana.

    Sasa huko chooni ulienda choo kipi" shangazi aliuliza kwa

    ukali kidogo. Baba mkubwa james bado aliendelea

    kucheka na kusema. "ili hali nimeshaoonekana hakuna

    sababu ya kuniuliza maswali yasiyo na msingi acheni

    nipumzike" aliondoka na kuelekea nje. Alikaa kibarazani

    katika kiti kile cha kunesa nesa. Kilikuwa ni kiti cha babu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alinesa kuelekea nyuma kisha alirudi mbele. Alikuwa

    ameshaichomoa sigara yake na kuipachika mdomoni.

    Alikuwa akiuvuta moshi wake taratibu na kuwa katikati ya

    tafakuri nzito. Alikuwa akitazama mawingu na nyota

    chache zilizojitutumua angani. Nilimnyatia taratibu mpaka

    alipo na kukaa mbele yake. Nilimuuliza. "Unaweza

    kunieleza kilichotokea?" alikisimamisha kile kiti kwa

    kushusha miguu yake chini na kunishangaa "umefika saa

    ngapi hapa?" sikutaka nicheke ndio maana nilicheka kwa

    hasira. "sasa baba mkubwa hukutaka niwepo hapa? Au

    kuna mtu ulikuwa naye" nilimuuliza nikiwa naangalia huku

    na huko kana kwamba nilikuwa nikimtafuta mtu ama kitu.

    "hapana Bella sijasikia hata ukija hapa nilipo. Nilikuwa

    mbali sana kimawazo" nilimuuliza "huko mbali nataka

    nipafahamu baada ya kuniambia ulikuwa wapi baada ya

    kupotea pale mtini?" baba mkubwa alicheka na kutingisha

    kichwa. Aliniambia

    "una msimamo kama baba yako" nilitabasamu tena kwa

    kukereka. Nilifahamu baba mkubwa hakuwa tayari

    kuzungumza lakini nilikuwa na shahuku pia ya kujua wapi

    alipokuwa na walimfanya nini mpaka alishindwa

    kuzungumza "baba mkubwa, tulikuwa wawili tu mimi na

    wewe. Ulishindwa kuongea nikikuona na si tunda kama

    ulivyodanganya. Ukapotea katika mazingira ya

    kutatanisha." nilinyamaza kuyaruhusu maneno hayo

    niliyoyazungumza yamuingie vizuri. Nilifanikiwa kwa kuwa

    nilimuona akitaka kunieleza yote yaliyomkuta. Aliizima

    sigara yake huku akinisikiliza kwa umakini. "naomba

    unieleze ilikuwaje sikukuta pale na ulienda wapi?"

    alinieleza "mwanangu, babu yako hakupendezwa na mimi

    kukueleza yale yote niliyokueleza na kuniambia kuwa

    endapo nikikueleza pia sitochukuwa muda mrefu nitakufa"

    Niliuliza kwa mshangao "utakufa" akanijibu "ndiyo,

    nitakufa tena katika kifo cha utatanishi kama nilivyopotea"

    alinieleza yote sasa, kama vile hakuogopa kifo

    alichoahidiwa.

    "babu yako ndiye alinifunga mdomo nisikueleze kuwa kwa

    nini huwa analia machozi ya damu. Machozi yale Bella

    humaanisha umwagikaji wa damu au kufa kwa mtu ama

    watu wengi. Lile hutokea pia kama kuna kitu ambacho

    hakipo sawa katika uwezo wake machozi yake ya damu

    humaanisha uangamivu" mimi moyo ulikuwa ukinienda

    mbio sana. Jasho likanitoka taratibu kana kamba

    kulikuwa kuna joto, kumbe wala. Baridi lilipuliza vizuri tu.

    Wakati nikiendelea kumsikiliza baba mkubwa. Ghafla

    nilimuona akikohoa. Alikohoa sana. Damu zikawa

    zinamtoka mdomoni kila akikohoa. Nilipiga kelele za

    kuwaita shangazi na baba wadogo. Baba mkubwa James

    aliniambia "mwanangu nakufa, nakufa kwa ajili yako"

    wakati akiyasema hayo shangazi Suzi alikuwa akisikia

    yote. Alikuwa ameshafika na kuniona nikiwa nimemshika

    baba mkubwa kichwa. Aliropoka "mchawi mkubwa wewe.

    Mchawi kama baba yako. Umemuua kaka yangu?"

    nilishituka sana hilo alilolisema shangazi. Nilishindwa cha

    kusema kwa kuwa kila mtu alikuwa tayari ameshafika na

    kuniona nikiwa nimekishika kichwa cha baba mkubwa,

    damu zikimtoka mdomoni. Yule shangazi Suzi alinisogela

    akanipiga kikumbo kikubwa pale nilipokuwa nimekaa,

    nikiwa nimemshika baba mkubwa, James. Nilianguka

    upande wa pili, nikiwatazama wale wengine. Baba

    wakubwa kwa wadogo walinitazama kwa hasira na yule

    shangazi mkubwa alikuwa akilia. "mkosi gani huu jamani

    katika familia yetu?, Dah!" shangazi mkubwa alisema.

    mimi machozi yalinitoka nisijue nijitetee vipi. Yule

    shangazi mkubwa aliniambia neno lliloniumiza sana nafsi

    yangu. "nyamaza mnafki mkubwa wewe, unalia nini

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wakati umemuua baba yako? Tena ondoka hapa

    nyumbani hatukutaki tena usije ukatuua na sisi mchawi

    mkubwa wewe"

    linibidi niondoke nikiwa bado siamini kilichotokea. Ilikuwa

    ni saa tano ya usiku nikiwa naelekea nyumbani peke

    yangu kutokea Magomeni kwa babu ulipokuwa msiba.

    Sasa kukawa na msiba wa pili wa mjomba wangu. Nikiwa

    katika kukatiza kichochoro hiki na kile, niliwaona vijana

    wakija nilipokuwa nikielekea. Walikuwa wanakuja kwa

    mbele yangu. Walikuwa vijana sita niliwahesabu kwa

    msaada wa mwanga wa mbalamwezi. Nilijipa ujasiri kuwa

    wasingeweza kunifanya chochote. Niliendelea kutembea

    kwa mwendo wa kawaida lakini nilikuwa nikitetemeka

    sana. Ulkuwa ni usiku na nilikuwa ni msichana, ikawa

    hatari zaidi. "vibaka!" Ilikuwa ni sauti ambayo

    ilizungumza ndani ya fikra zangu. Walikuwa hawana sura

    za kuwaamini hata kidogo. Nilipowasogelea, mmoja

    alinitolea tabasamu la kejeli. Wanne wakanipita wawili

    wakasimama mbele yangu. "we binti unaenda wapi?"

    waliuliza huku wakicheka kibabe. Mimi nilikuwa naogopa

    sana hivyo hata sauti yangu ilikuwa ni ya chini. "naenda

    nyumbani" mmoja alinicheka kwa nguvu huku akiyashika

    matiti yangu.

    "nyumbani? umetoka kwa bwana wako huku?" Huyu

    akadakia "da! ana kifua kizuri aisee! moyo umenienda

    mbio sana" mimi nikamputa mkono yule aliyekuwa

    akinishika matiti yangu. Nikaponyokwa na sonyo.

    Nikaropoka "sitaki bwanaa!" walicheka kwa pamoja na

    wale wengine wanne waliokuwa wamenipita, walirudi pale

    tulipo na wale wenzao. Kuna sauti iliyonijia kichwani

    haraka "Bella kimbia" nilipopata upenyo nikawachomoka

    wale wawili, katikati yao. Nilikimbia kwa kasi ya ajabu.

    Kabla hata sijafika, mbali walinikamata. Ilikuwa ni kabla

    sijafika kituoni, walikuwa wote sita kwa pamoja. "tena

    afadhali umejisogeza mwenyewe huku kwenye giza"

    alisema yule mmoja aliyeanza kuniongelesha. Niliwaomba

    wasinifanye chochote kibaya, lakini hawakunisikiliza wala

    hawakuwa na muda huo. Mmoja wao alinipiga mtama

    nikaisalimia ardhi iliyojaa michanga, mawe na vitu

    vingine. Walinivutia kwenye kijichaka kidogo ilichopo eneo

    hilo. Nikapata wazo la kupiga kelele. Hapo hapo nikapiga

    yowe la nguvu. "wananibakaa!!!" yule ambaye tayari

    alikuwa akiishughulikia sketi yangu, akanipiga ngumi ya

    uso. Maumivu ya ngumi ile, nikayasikilizia kwenye pua na

    mdomo wangu. Nikahisi maji maji mazito yakishuka

    kutoka katika pua zangu. Nilipojipangusa nikafahamu

    "damu" mmoja akasema "na bado ukituzingua tunakuua

    nani anatufahamu" "fanyeni faster" ilinibidi niwe mpole

    kwa kuwa tayari walikwisha nitolea, visu pamoja na sime

    zao walizozihifadhi viunoni mwao. Alianza yule aliyenipiga

    ngumi. Alinibaka alivyotaka mpaka alipochoka hakutumia

    zana yeyote. Aliingia wa pili, wa tatu mpaka wa nne.

    Kutokana na maumivu niliyokuwa nikiyapata, nilizimia.

    niliamka baada ya muda kadhaa mbele. Ulikuwa ni usiku

    mkubwa sana. Nilikuwa nimechafuka kupita kiasi. Damu

    zilikuwa zikinioka sehemu zangu za siri. Nilipotaka

    kunyanyuka, nilishindwa kutokana na maumivu. Nilipiga

    kelele za kuomba msaada.

    "nisaidieni jamani!" nashukuru mungu kuna kaka mmoja

    alikuwa ametoka kuchoma maindi barabarani, alikuwa

    akipita karibu na eneo hilo. Alikuja mbio. "kuna nini dada?

    Kuna nini?"

    mimi nilikuwa nikilia nikisikilizia maumivu katika kiuno

    changu. "wamenibaka kaka yangu naomba unipeleke

    hospitali sina nguvu" yule kaka alinisaidia kuninyanyua

    "inabidi twende kwanza polisi kupata pf3 halafu Rb kisha

    ndio twende hopitali" kwa kuwa kituo cha polisi cha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    magomeni hakikuwa mbali, alinikokota kwa miguu mpaka

    hapo. Damu zilikuwa zimekuka ila nilikuwa nikisikia

    maumivu makali sana. Sikutamani kuendelea kukaa japo

    dakika nyingine nyingi zaidi hapo polisi. Waliniuliza

    maswali kadhaa nikayajibu kama ilivyokuwa na kuwaeleza

    walikuwa ni wangapi kisha tuliruhusiwa twende hospitali.

    Yule kijana aliita taksi iliyo nje ya kituo hicho "tupeleke

    mwananyamala" dereva taksi alijibu "elfu kumi na tano".

    yule kijana aliniingiza ndani ya gari bila kuzungumza naye

    chochote. Taksi ilikuwa ikienda kwa mwendo wa kawaida

    kwa kuwa usiku ule hakukuwa na magari mengi

    barabarani. "kwani sasa hivi saa ngapi?" niliuliza huku

    nikigugumia kwa maumivu. Yule kijana alinijibu "Saa nane

    usiku sasa hivi" niliendelea kulia kutokana na maumivu

    niliyoyapata. Hatimaye tuliingia katika hospitali ya

    mwananyamala. Kutokana na uchovu wa hospitali hii,

    sikupata msaada wowote wa haraka. Ilikuwa ni yule

    kijana ndiye aliyenisaidia mpaka katika chumba cha

    daktari alinikokota hivyo hivyo huku aipishana na

    wauguzi.

    "dokta nina mgonjwa wangu" dokta alikuwa akiniangalia

    katika hali ya ukinyaa akauliza "usiku huu imekuwaje tena

    na damu hizo mapajani" mi sikujali nikajitupa katika

    kitanda kilicho karibu na kiti alichokaa daktari. Yule kaka

    akampatia pf3 tuliyo tuliyoandikiwa kule polisi na daktari

    kumwambia atoke nje ili aweze kunihudumia. Yule kijana

    alitoka nje akiwa ananiambia "usiwe na wasiwasi dada

    nipo hapa nje" nilijihisi faraja sana. Yule dakatari alirudi

    pale nipo baada ya kuufunga mlango na kuanza kunisaili

    kwa maswali. "kumbe yule ni kaka yako?" nikajibu

    "hapana ni msamari mwema tu" akaniambia nipanue

    miguu. Kutokana na maumivu na hali niliyo nayo

    unadhani ningebisha? Basi ndivyo nilivyofanya mwenzenu.

    Akiwa anatazama sehemu zangu za siri na msaada wa

    tochi yenye mwanga mkali akaniuliza "ulipatwa na nini?"

    nikajibu "nimebakwa. Nimebakwa na vijana sita mpaka

    nikapoteza fahamu" nilimsikia daktari akisikitika.

    Alisimama na kunieleza "hali ya huku chini si nzuri hata

    kidogo" nilishituka sana macho yakanitoka, daktari

    alikohoa kisha akaniambia

    "inaelekea baada ya kukufanyia huu mchezo walikuingiza

    vitu vyenye ncha kali na kukutoboa vibaya hivyo

    umechanika sana sehemu hizi na pia kizazi chako sina

    hakika kama hakijaharibika" alinitazama akiniangalia

    akiwa amenishika begani huku akinipiga piga kwa liwazo.

    Nililia sana haikuwa habari njema hata kidogo kwangu

    kwa wakati huo. Nilisikia uchungu mkubwa sana. Mimi ni

    msichana wa miaka kumi na nane tu duniani leo

    ninakikosa kizazi changu jamani? Kwanini mimi? Nilijikuta

    nikiropoka "dokta kwa hiyo sitozaa?"

    dokta alitabasamu kunipooza alielewa machungu na

    huzuni niliyojisikia baada ya kupewa taarifa ile. Alinieleza

    "hii ni kwa uchunguzi wa macho binti, sijawa na hakika

    kama ni kweli au lah lakini kesi kama hizi mara nyingi

    matokeo yake ni hayo" nikawa nalia "sasa dokta

    utanisaidiaje mwenzio mimi jamani?" nilikuwa nikilia kwa

    uoga na uchungu. Niliwachukia wale vijana na kuwaona ni

    watu waliotumwa kuaribu maisha yangu na ndoto zangu.

    Dokta akaniambia "tutakupeleka sasa sehemu ya

    kukufanyia uchunguzi zaidi na kama upo sawa

    tutakusafisha tu na kukushona pale ulipochanika" niliitikia

    kumuonesha kuwa nimemuelewa. Nilijikokota kutoka

    kitandani kisha mimi na daktari tulitoka katika chumba

    hicho na kwenda katika chumba cha upasuaji. Nilimkuta

    yule kijana amekaa kwenye benchi la mapokezi.

    Alipotuona, alisimama "vipi daktari?" akajibiwa "tulia

    endelea kusubiri"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    yule kijana aliendelea kukaa pale akisubiri. Daktari aliingia

    chumba fulani na kuwaita wauguzi watatu. "nawahitaji

    chumba cha upasuaji" nilipofika niliambiwa nilale kama

    nilivyolala kule kwa daktari chumba cha mwanzo. Wale

    wauguzi walioitwa waliingia na visu mikasi pamba na

    madawa madawa. Niliogopa sana. Hali ya hospitali

    ilitisha sana. Wale wauguzi walivaa gloves na kuanza kazi

    yao wa kuchunguza kizazi changu pamoja na daktari.

    Mimi nilichomwa sindano ya ganzi hivyo sikujua nini

    kilikuwa kikiendelea huko chini. Zilipotea zaidi ya dakika

    arobaini na tano kisha daktari aliibuka na kunieleza "pole

    sana kizazi kilikuwa kimesogea ila sasa kipo sawa na pia

    tumelazimika kukushona kutokana na ulichanika kwenye

    mashavu na pia tutakuapa dawa kwa ajili ya kusafisha

    uchafu wote ulioingiziwa japo mara kwa mara tumbo

    litakuwa likikusumbua hiyo hali isikutie hofu"

    nikajibu kwa kukunyekea "nashukuru sana dokta" yule

    daktari alitabasamu tu kisha alinieleza "unapaswa upate

    muda wa kupumzika labda kama ni ruhusu utapata

    kesho. Leo kuna dripu utatundukiwa kwa ajili ya

    kuongezewa damu iliyopotea" nikamuuliza "kwani

    mmeshanifanyia vipimo vya damu yangu" "hiyo ndiyo kazi

    yetu tumekupima ukimwi upo sawa tumekupima pia na

    group yako tumefahamu kuwa wewe ni group AB huna

    tatizo hivyo utapata damu hiyo sasa" nikauliza kwa

    kudadisi "kwanini labda nisingepewa dawa za kuongeza

    damu au nile nini na nini niongeze damu?" akaniibu

    kiufasaha "wewe damu yako imepotea kwa wingi saa ndio

    maana unajisikia hivyo unavyojisikia hata sisi hatuna

    damu ya kutosha ila tunalazimika kuigawa kwa watu

    waliopoteza wingi wa damu kama wewe"

    moyo wangu ulifarijika sasa. Kitanda changu

    kikasukumwa mpaka kwenye wodi nyingine ambapo huko

    nilipewa kitanda na kutundukiwa dripu iliyokuwa ikiingia

    taratibu katika mishipa yangu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog