Search This Blog

THE STRANGER - 5

 







    Simulizi : The Stranger

    Sehemu Ya Tano (5)



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sam aliporudiwa na hali yake ya kawaida. Alianza kulia na kujilaumu mwenyewe kwa kushindwa kuzizuia hisia zake baada ya kuona damu ya mama mkwe wake.

    Aliamua kwenda hospitali alipoenda Jane kumpeleka mama yake baada ya kufumba macho na kuendeleza kilichotokea baada ya yeye kutoweka.

    “samahani , namuulizia mama yangu anaitwa Suzana Jackson.” Aliongea Sam baada ya

    Kufika kwenye mapokezi ya ile hospitali.

    “pole sana kaka, mama yako amefariki masaa mawili yaliyopita.” Aliongea dada mmoja aliyekuwa kwenye ile mapokezi baada ya kuangalia Jina kwenye computer maalumu.

    “duh.. sasa ndugu zangu wengine waliokuja huku wapo kwenye chumba cha maiti?” aliuliza Sam lengo lake kujua Jane yupo wapi.

    “ kuna mdogo wako peke yake alikua analia sana . yupo chumba cha mapumziko namba 29” alijibu yule dada na kumuelekeza Sam hicho chumba.

    Alipofika, alimkuta Jane akiwa macho huku akiwa mwekundu na macho yamevimba kutokana na kilio cha muda mrefu.

    Jane alipomuona tu Sam alianza kucheka kwa sauti kubwa mpaka Sam mwenyewe akashangaa. Aliendelea kucheka na kushuka kitandani. Alimsogelea Sam na kumtekenya kisha akakimbia na kujificha chini ya kitanda uvunguni. Alianza kulia na kuongea maneno yasiyoeleweka. Alitoka kitandani na kuanza kucheka tena. Daktari alikuja mbio na kumchoma Jane sindano ya usingizi.

    “imekuwaje dokta??” aliuliza Sam baada ya daktari kumuomba amuache na amfuate yeye ofisini kwake.

    “ amechanganyikiwa baada ya taarifa za kifo cha mama yake.” Alitoa majibu hayo daktari huku akimuangalia Sam kwa jicho la huzuni.

    “ tufanye nini daktari ili arudi katika hali yake ya kawaida?” aliuliza Sam huku akionyesha wazi kuchanganyikiwa.

    “kuna uwezekano mkubwa asipone kabisa kwa jinsi vipimo vinavyoonyesha.”

    Alijibu daktari na kumfanya Sam kuishiwa nguvu na kukaa chini.



    Majibu yale yalimfanya apagawe na kuondoka pale hospitalini. Alijua kuwa uwezekeno wa kuwa na Jane kimapenzi ni mdogo sana.

    Alijua kuwa kutokuwa karibu na Jane ndio mwanzo wa kutafuta damu yeye mwenyewe. Hivyo kumfanya aishi maisha ya kutanga tanga. Mawazo yalimsonga Sam na hakujua afanye nini.

    Siku ya pili yake akaenda tena hospitalini kumuangalia mpenzi wake. Alikuta amehamishiwa katika ward ya vichaa.

    Alienda na kumuangalia. Jane alikua anamshangaa tu, muda mwingine anamuogopa na wakati mwingine anacheka na hapo hapo anaanza kulia kitoto.

    Yalikuwa maumivu mazito kwa Sam kila akimuona mpenzi wake akiwa katika hali ile.

    Aliondoka na kurudi kule kwenye hotel na kuchukua card ya benk.

    Alidroo hela ambazo zilimuwezesha kupanga chumba na kununua vitu vya ndani.

    Alinunua kitanda na godoro lake. Kwake vilikua vitu vya muhimu sana. Maana alikua hapiki kutokana na chakula chake anachokula.

    Hapo alijaribu kuanza maisha peke yake bila kujua hatima ya maisha ya kujitafutia mwenyewe.

    *************************************************

    Haiba akiwa chumbani kwake alikaa na kumuwaza sana Bakari na alijikuta amekuwa mwepesi sana kumsaidia. Hata ule usiku tu ulikuwa mrefu sana kwake na alitamani kukuche ili aende kuonana na Beka na familia yake.

    Asubuhi alifunga safari na kwenda tena kwa Bakari.

    “leo nimekuja mara moja tu, nataka kukupeleka kwenye duka utakalolitumia kuendesha maisha yako.” Aliongea Haiba baada ya kukaa kawa muda wa nusu saa.

    “ poa, ngoja nikajiandae”.

    Aliongea Bakari na kungia ndani. Hakuchukua muda mrefu alitoka akiwa amependeza sana. Zilikua ni moja kati ya nguo nyingi alizonunuliwa jana yake na Haiba.

    “ safi” aliongea Haiba na kumuonyeshea dole gumba.

    Walitoka na kuingia ndani ya Tax aliyokuja nayo Haiba.

    “ndiye yule pale shoga umemuonaje?” aliuliza yule dada wa jana baada ya kumfata shoga yake na kumuonyesha.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “dah!..kwanza unamuona Beka anavyo shine dada… mama Hassani kaacha mbachao kwa msala upitao.” Aliongea yule dada mwingine na kuendelea kuwaangalia mpaka walipopotea katika upeo wa macho yao.

    Walifika maeneo ya kariakoo na Haiba akamuonyesha Frem iliyokuwa imefungwa na kumwambia kuwa lile ndio duka lake.

    “kuna kila kitu ndani, unaweza kuanza kazi siku yoyote.” Aliongea Haiba na kumkabidhi funguo Bakari.

    “waooooooooooooooooooh”

    ulikuwa mshangao mkubwa baada ya kuona duka likiwa limejaa makabati ya thamani na ndani yake kukiwa na simu aina mbalimbali. Rangi na taa za ajabu ambazo hajawahi kuziona toka siku anayozaliwa, ziliku kivutio kikubwa. Alikuta bidhaa nyingine zikiwa kwenye kichumba kidogo alichotambulishwa kama Store.

    Alishindwa kuizuia furaha yake na kumkumbatia Haiba huku analia kwa furaha.

    “ooooooooosh”

    ulikuwa mguno mkubwa uliosikika kutoka kwa Haba. Alikua mgonjwa kila akiguswa na Bakari. Mpaka yeye mwenyewe alijishangaa na hakujua kuna nini katika mikono ya Bakari. Alijisikia raha kila akiguswa na kujihisi yupo katika wakati wa tendo.

    “usijali…. Lini utaanza?” aliuliza Haiba na kumtoa mikono Bakari haraka baada ya kumuona anampa ashki kila akimpapasa.

    “ leo hii hii” alijibu Beka na wote wakacheka

    “basi mi naenda, nitakupitia jioni” aliiongea Haiba na kumuacha Bakari dukani.

    Aliendelea kulikagua lile duka jipya kabisa. Bakari alifikicha macho yake labda aliku anaota. Lakini haikuwa ndoto. Zaidi alikuta amerahisishiwa kazi. Kila bidhaa ilikua imebandikwa bei yake.

    Alitafakari jinsi ya kutafuta wasaidizi. Aliwakumbuka marafiki zake waliokuwa wamevunjiwa vibanda vyao na kuwapigia simu.

    “ kaka, umejiunga na free mason nini??” aliuliza mmoja kati ya marafiki zake kwa mshangao baada ya kuliona duka la Beka.

    “ hamna kaka, ni story ndefu. Achanane na hayo, nimewaita tufanye kazi washikaji…au mmeshapata vitengo??” aliongea Beka.

    “tumepata wapi, tulikua tunachakaa tu kitaa.” Alijibu yule mwengine aliyekua kimya muda mrefu.

    “ basi msijali, tutapiga kazi pamoja. Ngojeni bosi mkuu aje niongee nae kuhusu mishahara yenu.” Aliongea Bakari na kuwaangalia marafiki zake kwa zamu. Walionekana kufurahi na kumpa tano rafiki yao.

    Ilipofika saa kumi na moja, Haiba alirudi na kukutana na wageni.

    “dada hawa ni marafiki zangu, tulivunjiwa wote pale kijiweni kwetu.” Aliongea na Haiba akawapa mikono.

    “huyu anaitwa Salumu na huyu mwengine anaitwa Fabi.” Aliendelea na utambulisha Bakari.

    “basi waambie kesho waje waanze kazi, au ulikuwa unatakaje Beka?” aliongea Haiba baada ya kutambua ujio wa wale vijana pale.

    Aliwapa elfu ishirini kila mmoja na kuwaruhusu waondoke.

    Walifunga duka na kuondoka zao.



    Haiba alirudi chumbani kwake na kwenda kuoga. Aliporudi alijilaza kitandani na usingizi ukachukua nafasi yake.

    Baada ya kuzama sana usingizini. Alianza kuota yupo pamoja na Bakari. Mara wanaingia ndani na kuanza kupakatana. Mara akaanza kumuona Beka akivua shati na kumsogelea. Alipapaswa kila kona ya mwili wake. Joto lilipompanda, akajikuta anajibu mashambulizi kwa kuanza kumtomasa Beka. Vilio vya mahaba vilisikika kwa wote wawili. Baada ya hapo walianza kupata raha za dunia bila kujua nguo za chini zilichojokaje. Kwa ufundi wa Beka, ulimfanya Haiba aheme jujuu wakati wate.

    “ooh gosh!!!”

    Alishtuka Haiba na kujikuta amelowana. Alinyanyuka kitandani na kwenda kuoga. Alipokua anaoga, mawazo juu ya beka yalizidi kumuandama. Alimuwaza sana. Na kubwa zaidi kwa wakati ule ambao alikua na hamu kabisa ya kufanya mapenzi. Hakuwahi kujisikia hali hiyo alipokua kwao. Lakini toka alipokaribia kubakwa siku ya kwanza. Yule mtu japokua alimuua, lakini ndio aliyemjengea hisia nzito katika ubongo wake. Sasa alijisikia kabisa kushiriki hilo tendo. Ukijumlisha na ile ndoto ndio kabisa, aliouna utamu japokuwa haukua halisi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alitamani kwenda kwa Beka usiku ule ule. Lakini alianza kujihisi mkosaji baada ya kutupa macho yake kwenye dressing table na kuiona picha ya mke wa Beka.

    “hii kazi nitaweza kuifanya kweli?” alijisemea na kuichukua ile picha.

    “lakini huyu ni msaliti…anastahili adhabu,” aliongea na kuuendea mkoba wake na kutoa cheni.

    Aligundua hela zimemuishia. Alifumba macho na kuongea maneno yasiyoeleweka na alipofumbua tu. Alikuta mabunda ya hela yamemzunguka.

    “safi, bado kufanya kazi ya huyu dada.” Aliongea na kuunyanyua tena ule mkufu na kuuelekezea kwenye ile picha.

    Ilikuja kitu kama Tv na kumuonyesha matukio ya nyuma kuanzia mapenzi yao mpaka mwanamke huyo alipoitoroka familia yake na kumfata huyo bosi mwenye hela.

    Alipomuangalia kwa vizuri huyo bosi, aligundua kitu.

    “kumbe mwanaume anayetembea naye ameshaathirika??....YES!!”

    Alijikuta Haiba anashangilia baada ya kugundua ukweli kuwa hata mke wa Beka naye ameathirika na virusi vya ukimwi.

    “ nipo huru na sina makosa nikimchukua Beka kwakua siwezi kumuacha afe kizembe.”

    Aliongea na kuanza kuichana chana ile picha.





    Usingizi haukua na nafasi kabisa kwa Haiba mpaka jua la asubuhi likapanda.. Alimpitia Beka kwa tax na kwenda naye kariakoo. Waliwakuta marafiki zake Beka wapo nje ya duka.

    “safi sana, naona mmewahi?” aliongea Haiba baada ya salamu. Baada ya kufungua duka, aliwaachia duka wale vijana baada ya kuwapa maelekezo machache na wao wakaingia kwenye tax na kutoka tena.

    Walienda hotelini na kumuachia Beka aagize anachohitaji kwa kua hakua amekunywa chai.

    “samahani, naomba nikuulize kitu?” aliongea Beka wakati anapata kifungua kinywa.

    “uliza tu.” Alijibu Haiba huku akimuangalia kwa umakini.



    “huwa unakula nini?... maana sijawahi kukuona kula wala kunywa chochote.” Aliuliza Beka na kuendelea kunywa chai.

    “huwa sipendi kula kula. Mi nikishakula mara moja tu kwa siku basi sili tena mpaka kesho yake.” Alijibu Haiba huku akiendelea kumuangalia Beka .

    “duh?...ndio balance diet au?” aliuliza Beka kwa mshangao.

    “basi tu, huwa sipendi kula.”

    Alijibu Haiba na Beka akaridhika na majibu ya Haiba.

    Kimya kikatawala kwa dakika kadhaa bila yeyote pale kunena kitu mpaka Beka alipomaliza kula.

    “ hivi ukigundua kuwa mkeo nimeshindwa kumrudisha kwako utachukua hatua gani?” hatimaye Haiba alifungua mjadala uliomfanya Beka ataharuki kidogo. Hakulitegemea lile swali.

    “ sitakulaumu, sana sana kwa sasa nakushukuru kwa kuyabadilisha maisha yangu kwa kiasi kikubwa.” Alijibu Beka na kuonyesha kutojali.

    “ nikikushauri uwe na mwanamke mwengine na umsahau kabisa mkeo. Utakubali?” aliongea Haiba na kumkazia macho kidogo Beka kuonyesha umakini wake na kutaka jibu kutoka moyoni.

    “ yule ni mzazi mwenzangu tu, na kama yeye mwenyewe alinikimbia kwa kuwa nilikua na hali duni. Basi kavunja ahadi na viapo vya ndoa kwa kuishi maisha yote ya dhiki na faraja, shida na raha. Hata mimi simfikirii na nipo tayari kuoa msichana mwengine kama atakubali kuwalea watoto wangu.” Alijibu Beka na kumfanya Haiba avute pumzi ndefu kuashiria ameyakubali mawazo na mtazamo wa Beka.

    “kuna kitu nimekigundua kutoka kwa mkeo, sio kitu kizuri na hafai kuwa wako tena” aliongea Haiba na kumuangalia Beka usoni ili asome riactions zake.

    “vitu gani, na umemuona wapi?” aliuliza Beka kwa mshangao.

    “mwanaume anayeishi na mkeo si anaitwa Philipo the don?” aliuliza Haiba ili kupata uhakika kutoka kwa Beka kama anamjua mume mwenzake.

    “umejuaje?” aliendelea kushangaa Beka.

    “ndio maana niliomba picha ili nimlinganishe huyo dada anayetembea na Mr. Philipo kama ni mke wako.” Aliongea Haiba kwa kujiamini.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ‘ kipi kilichompata?” aliuliza Beka na kukaa vizuri kutaka kujua kitu kinachoendelea pale

    “unajua kua Mr Philipo huwa ana tabia ya kubadili wasichana kama nguo, hivyo mkeo kaingia mkenge na hivi sasa anaishi na virusi vya ukimwi bila yeye mwenyewe kujua.” Aliongea Haiba na kumuacha Beka akiwa katika masikitiko makubwa.

    “inaweza ikawa adhabu kutoka kwa mungu kwa kosa la kuisaliti ndoa yake.” aliongea Beka huku akonyesha wazi kuwa ile taarifa imemuhuzunisha kupita kiasi.

    walirudi dukani na Haiba akarudi kwake. Ilimchukua dakika kadhaa beak kuamini maneno ya Haiba. Pia alitafakari ukaribu wake na yule dada ni nini, hata hilo swali halikuwa na majibu lililomridhisha. Akaamua kuacha ili ajue hatima yake.



    “dada muda wako wa kukaa hotelini umeisha toka saa nne asubuhi.” ilikua kauli ya mtu aliyekua Reseption baada ya kumuita Haiba.

    “ oh gosh!!siku tano tayari??” aliuliza Haiba kwa mshangao.

    “tayari dada.” alijibu na kumtajia siku aliyoingia mpaka muda ule

    Haiba alifungua pochi yake na kutoa noti nyingi na kumkabidhi. Aliingia chumbani kwake na kukaa. Hapo mawazo juu ya kazi ya mfalme yakamjia. Aliwaza juu ya muda alioupoteza kwa ajili ya Beka. Alijilaumu kidogo na kuchukua mkufu wake na kuanza kumtafuta Sam alipo. Aligundua alipo na hapakuwa mbali na pale. Alicheka na kuchukua kibegi chake na kutoka tena.



    ****************************



    akiwa chumbani kwake Sam huku mawazo juu ya Jane yakichukua sehemu kubwa ya akili yake. Wakati akiwaza na kuwazua ni nini afanye ili amponyeshe mpenzi wake, alisikia mtu akibisha hodi katika mlango wake. Alishtuka kidogo kwa kua hakua na rafiki wala ndugu aliyekua anapajua pale alipopanga.

    alinyanyuka kivivu na kwenda kufungua mlango kwa umakini mkubwa.

    Hamadi! alikutana na msichana mwenye sura nzuri sana. Alikua kavaa nguo nyekundu ya moja kwa moja, masikioni akiwa ametoga na dhahabu zikiupamba mwili wake kila sehemu.

    Sam mwenyewe alibaki amepigwa na bumbuwazi baada ya kukiona kile kifaa. Alimkaribisha ndani na kumsikiliza shida yake.

    “naweza kukaa kitandani kwako?” aliuliza yule dada baada ya kuona kile chumba kikiwa na kitanda na godoro peke yake. chini kukiwa na tires na juu feni ndio lilikua linaleta upepo mule ndani. Harufu nzuri ya asili ya mwili wa Sam ndio kilikua kivutio kingine mule ndani.

    “kaa tu usijali!” aliongea Sam huku akiendelea kuutathmini mwili wa mgeni wake huyo ambaye hajawahi hata kumuona. Tabasamu la mgeni lilizidi kujaza maswali kichani kwa Sam bila kujua yule mgeni alikua anamfahamu au la.

    “bila shaka wewe ndio Sam?” aliuliza yule mgeni na kumfanya Sam kutumbua macho kwa mshangao. Alimuangalia yule mgeni na kuvuta picha labda ni wapi alishawahi kumouona yule msichana lakini jibu la haraka lilikosekana.

    “vipi?......umeshanisahau kwani?” yule mgeni alizidi kuumiza akili ya Sam. alipomuangalia yule msichana bado kumbukumbu zake ziligoma kabisa kurudi nyuma. Ziliishia tu pale mpenzi wake alipokua kichaa.

    Hakika Jane alimuathiri Sam kwa kiasi kikubwa. Mpka uwezo wake wa kufikiri pia uliathirika.

    “naitwa Candy…. Mara ya mwisho tulikutana club tukacheza pamoja na baadae kukatokea vurumai na kiumbe cha ajabu kikatokea……..hukumbuki?” aliuliza yule dada na kumfanya Sam atabasamu baada picha ya yule dada kujichora tena ubongoni.

    “mambo mengi……….umepajuaje hapa?” aliuliza Sam



    “mi nakaa nyumba ya pili kutoka hapa. Leo nimekuona ukiingia ndio maana nimekuja coz nimekumiss sana” aliongea yule dada na kuanza kujichekesha chekesha.

    “ karibu” aliongea Sam na kumuangalia yule dada

    “nishakaribia, nilijua nitamkuta wifi?” aliuliza yule dada baada ya kugundua kuwa hakukua na dalili zozote za kuishi mwananmke pale. Kutokana na vitu muhimu kama juko na ndoo za maji. Hakukua na hata kijiko wala nguo yoyote ya kike mle ndani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “naishi peke yangu humu.” alijibu Sam na kumuangalia yule dada aliyekuwa bize kukikagua kile chumba.

    “jamani kwanini huishi na mwanamke??” aliendelea kudadisi yule dada.

    “ni maamuzi ya mtu tu kwani kuna ulazima wa mtu kuishi na mwanamke?” aliuliza Sam na kuonyesha wazi kuchoka na maswali ya yule dada.

    “sio lazima ila nilitaka kujua kama una mwenyewe au upo single” aliongea yule dada huku aking`ata vidole vyake kimahaba.

    Ile harufu ya manukato ya ajabu ndio iliendelea kummaliza yule dada. Alijihisi anakunywa kilevi Fulani aina ya Amarula kinachomfanya ajisikie hamu ya tendo. Wakati mwengine mpaka sauti ya yule dada ilianza kubadilika.

    “sijakwambia kuwa nipo single, ila sikai na mwanamke kwa sababu hayupo karibu na mimi kwa wakati huu” alijibu na kumkata maini yule dada aliyeonekana anataka kujiletaleta kwa Sam.

    Sam alimuangalia na kunyanyuka na kuuendea mlango

    “nahitaji kupumzika dada tutaonana baadae.” aliongea Sam na yule dada akatii amri na kuondoka zake.



    Usiku wa siku ile yule dada alitoroka kwao na kwenda kwa Sam na kumgongea mlango.

    Sam alifungua na yule dada akaingia ndani na kufunga mlango.

    “sipati usingizi kwa ajili yakoSam, naomba uniokoe kwenye hili gharika la mahaba lililonikumba mwenzio kwa kulala na mimi japo usiku mmoja wa leo tu” aliomba yule dada na kumvaa Sam aliyekuwa kifua wazi huku akiwa na boxer peke yake.

    “naomba uondoke, dada sijisikii vizuri” aliongea Sam baada ya kuona kizunguzungu kimempata mara tu baada ya kuguswa na damu changa ya yule mtoto mzuri.

    “naomba nionee huruma Sam, nipe hata kamoja tu nitasuuzika moyo wangu” aliongea yule dada na kuupapasa mwili wa Sam alifanya hayo na Sam hakuongea kitu tena zaidi alianza kulegea miguu na kuangukia kitandani.

    Yule dada alianza kusaula nguo zake baada ya kumuona Sam kalegea kwa kujua alikua ammempatia kwa kumshika Sam sehemu zake zenye mihemko mikali.

    Alimfata na kumkalia juu huku akiendelea kuchezea vinyweleo vidogo vilivyokua kifuani kwa Sam.

    ghafla aliona vile vinyeleo vinaongezeka na mwili wa Sam unabadilika rangi na kuwa wakijani. Mara Sam akabadilika na kuwa mnyama wa ajabu.

    yule dada aliruka pale kitandani na kuanza kupiga kelele. Alikimbilia kufungua mlango lakini hakufanikiwa. Kwani tayari Sam alishamrukia na kuanza kumnyonya damu yake shingoni. Hakua na uwezo wa kupiga kelele tena sana sana alianza kupapatika kama kuku aliyechinjwa na kuachiwa. Dakika moja baadae akaaga dunia





    “Sam, nakuomba usighairishe safari!” aliongea Haiba baada ya kumuona Sam akiwa haeleweki.

    “ siwezi kwenda popote mpaka nimshuhudie mwanangu” aliongea Sam huku akimuangalia Jane aliyekua anacheka cheka bila kujua kinachoendelea.



    Haiba alijitahidi sana kumbembeleza, lakini Sam alikataa katu katu. Mida ikazidi kuyoyoma mpaka usiku ulipoingia. Haiba jasho lilimtoka mpaka machozi lakini wapi. Hazikufua dafu kwa Sam. Mida ilipokaribia, Haiba alimuaga Sam na na kutangulia kwa safari maana chombo kilishafika. Alipofika na kupanda, kwa mbaali alimuona Sam akija huku anakimbia. Alifurahi na Sam akapanda kile chombo na safari ya kuelekea katika sayari ya Mars ikaanza.

    Walitumia usiku wote angani na mchana wa siku yapili chombo kilitua kwenye uwanja maalumu uliofurika watu wote wa jamii ya Baikiri. Watu walianza kushangilia na milango ikafunguliwa na watu wawili muhimu walishuka. Watu hao ni Haiba na Sam.

    Walikaribishwa kwenye viti malumu na mfalme ambaye alidhoofu kwa mawazo juu ya mwanaye, alisaidiwa kwa kushikwa mkono na Msemaji mkuu na kupelekwa kwenye kiti cha enzi na kukaa.

    Haiba na Sam walimsogelea mfalme na kupiga goti na kuinamisha vichwa vyao kama ishara ya kumuheshimu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mfalme aliwakumbatia wote wawili na na kuanza kulia. Wote wakaungana naye na kuanza kulia. Aliwaangalia kwa zamu na kutoa shukurani kwa Haiba kwa kumletea mwanae wa kiume.

    “Sam mwanangu” aliongea mfalme huku machozi yanamtoka.

    “naam baba” Sam aliita baba kwa mara ya kwanza. Uwanja woote ukashangilia na furaha iliyotoweka kwenye jamii yote ya Bikiri ikarudi tena.

    ******************************

    Haiba na mama yake walipewa nyumba moja kati ya nyumba za ikulu kama zawadi yake. Alipewa cheo kikubwa na mali nyimgi. Yalichongwa masanamu mawili makubwa yenye sura ya Sam na Haiba kama maashujaa wapya wa jamii ya Bikiri.



    Baada ya miezi miwili mfalme Josh akaaga dunia na Sam akatawazwa kama mfalme mpya akiwa na umri mdogo. Ilikua ngumu kuongoza bila kuwa na mke. Akaambiwa achague mke na kuamua kumchagua Haiba kwakua alikua anampenda pia.

    Harusi ya aina yake ilifungwa kwa mashujaa hao walioishi sayari ya tatu bila kupata madhara yoyote.

    Haiba alishika mimba na kujifungua mtoto wa kike. Wakaenda kupima na kukuta Sam hawezi kuzaa tena maana watoto waliisha.

    “sina budi mke wangu, natakiwa nirudi duniani nikamchukue mtoto wangu” aliongea Sam na kumwangalia Haiba.

    “sina neno mie, ila tutaenda wote. Maana nakujua jinsi unavyompenda yule msichana unaweza kubaki huko huko.” Alitania Haiba na wote wakacheka.



    *************************

    Safari ya kuelekea duniani ilitimia na Sam na mkewe walitua salama duniani. Haiba alichukua mkufu wake wa ajabu na kuanza kuangalia maisha ya Jane kuanzia pale walipomuacha Hospitali.

    Walimuona Jane akijifungua mtoto wa kiume na huyo mtoto kulelewa katika kitua cha watoto yatima. Cha ajabu huyo mtoto alikua anakula vyakula vya duiani bila shida. Alifanana kabisa na Sam. Haiba alikatisha na wakaamua kwenda kituo cha kulea watoto yatima.

    “mtoto mnayemuulizia anaitwa nani?” aliuliza mlezi baada ya salamu na utambulisho.

    “ jina hatulijui ila mama yake anaitwa Jane James” alijibu Sam na kumfanya yule mlezi kumuangalia usoni. Alistaajabu kumuona anafanana sana na mtoto wake.

    “bila shaka wewe ndio baba yake, ulikua wapi siku zote?” aliuliza yule mlezi swali lililochelewa kujibiwa.

    “ nilisafiri na nimerudi ndio nimepata taarifa kuwa mtoto wangu analelewa humu.” Aliongopa Sam.

    “huyo mtoto anaitwa SAMJE. Hilo ndilo jina alilokua analiimba mama yake toka alipokua anajifungua”.

    Sam alicheka baada ya kugundua kua japo Jane alikua hana akili kabisa, lakini aliunganisha jina lake na lakwake na kutoa jina la mtoto. Alijisemea moyoni kuwa Jane alikua ana mapenzi ya kweli moyoni mwake juu yake.



    Walipewa maelekezo na kumchukua mtoto na kwenda naye hospitalini.

    Jane alipomuona tu Sam alinyanyuka alipolala na kumuita.

    “SAM!!” Aliita Jane kwa sauti kubwa.

    “JANE!!” aliongea Sam na kumuangalia machoni Jane.

    Jane aliamka na kumkumbatia Sam. Sam alishangaa kumuona mpenzi wake akiwa amerejewa na fahamu. Daktari alikuja mbio na kushangaa kumuona mgonjwa wake karudiwa na akili zake. Alimchukua na kwenda kumpima. Akagundua kua amepona.



    Waliongea mengi sana ikiwemo kumwambia ukweli kuwa kaoa mwanamke mwengine nay eye kurudi kwao. Pia walimwambia Adhma yao ya kuja kumchuku mtoto.

    Mwanzoni Jane alikataa, lakini walipompa mkufu wa ajabu utakaomuwezesha kupata mawasiliano ya moja kwa moja na wao wakati wowote. Akakubali kwa shingo upande. Pia walimuelekeza jinsi ya kuomba hela na chochote anachokitaka.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Waliagana kwa vilio wapendanao wa zamani na kabla hawajaondoka, walipitia anapoishi Beka kwa sasa. Alikua kanunua ghorofa tatu na magari kama uchafu. Pia alikua na kituo cha kulelea watoto yatima na watoto wenye vichwa vikubwa walifanyiwa operation bure kwenye hospitali yake kubwa.

    Haiba alimpa mkono wa pongezi na kumsifia mke wa Beka wa sasa hivi kwa kuwajali watoto wa Beka. Waliaga na kurudi kwao ambapo waliishi kwa furaha. Walizidi kuwasiliana na Jane.

    Waliamua kurudi tena Duniani kuhudhuria Harusi ya Jane na tajiri mkubwa afrika nzima. Jane alifurahi ugeni huo kutoka Sayari ya Mars wakiwa na mwanae na kuwashukuru. Maisha yaliendelea na walizidi kuja na kuondoka Duniani kama wageni wengine bila kudhuru watu.

    MWISHO…………



    Naamni mtakua mmepata elimu ndani ya burudani. Mi ni binaadamu. Sijakamilika. 

0 comments:

Post a Comment

Blog