Search This Blog

JINI HUSNAT - 1

 





    IMEANDIKWA NA : ZUBERI MARUMA



    *********************************************************************************



    Simulizi : Jini Husnat

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    UTANGULIZI



    JOHN VERGAN kijana anayemiliki kampuni kubwa na mwenye mafanikio makubwa katika maisha yake anadondokea katika penzi la mtoto mrembo mwenye asili ya kishombeshombe HUSNA ambaye ni jini!



    VERGAN akubali kuwa na HUSNA baada ya kugundua si binadamu heka heka,vituko,uzuni vinamuandama je atafanikiwa kuokoka katika kisanga cha jini huyo mpole na mwenye hasira za karibu?



    fuatana nami mwanzo mpaka mwisho wa riwaya hii itakayokuburudisha-..,..



    TUANZE



    1

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ulikuwa ni ukumbi mkubwa ulojaa watu wenye hela zao, kila starehe iliyopo katika dunia hii ilikwepo hapo kasino ilo lilijaa wadachi,waindi,

    walokuwa wakijiuza.



    mziki mkubwa ulikuwa ukiendelea kuwaburudisha wateja wa club hiyo



    kulikuwa kuna walinzi wa kutosha,walokuwa tayari kupambana na kiumbe chochote kitakachotaka kuleta shida



    gari aina mbali mbali za kitajiri ziliingia na kutoka na wasichana warembo ni ukumbi ulosifika kwa matanuzi yote uyatakayo



    JOHN VERGAN kama mwenyewe alivyopenda kujiita alikuwa counter akitupia pombe yake taratibu!



    machangudoa wachache walijipitisha mbele yake lakini ilo wala akulijali wengine awakuishia kujipitisha tu kwani walimfata na kutaka kutoa company



    lakin VERGAN hakuwa tayari, mawazo yalitawala kichwa chake aligubia bia kwa fujo aikujulikana kipi kilichomtesa kijana huyo mwenye umbo la wastani



    si mrefu sana wala si mfupi sana,maji ya kunde mwenye body sex mwili wa mazoezi alikuwa na kila mvuto wa kimapenzi kwa mwanamke amwangaliaye!



    wanawake wengi sana walimmezea mate lakin moyoni mwake alikwepo mwanamke mmoja tu MOURINE



    huyu ndo alomfanya VERGAN Agubie ile bia kwa hasira na hisia tele MAPENZI yalimtesa alimpenda mtu asiyempenda tena secretary wake



    macho yake makubwa yaliyozungukwa na nyuzi nyembamba nyeusi yalitua mkononi mwake alivaa saa ya dhahabu iliyosomeka ni saa sita na nusu usiku akashusha pumzi taratibu ni wazi alishachoka na usingizi ulishaanza kuyanyemelea macho yake kilevi kilishaanza kumlevya



    Akaishika simu yake na kuibonyeza tarakimu kadhaa akaiweka maskioni....



    "simu unayopiga haipatikani tafadhali jaribu tena badae"



    ndiyo kauli ilojibu upande wa pili JOHN VERGAN akakunja sura kwa hasira,akaachia mguno wa fedheha



    Akashika chupa yake na kugubia kile kinywaji alipoishusha chini ilikuwa tupu



    Kwa vyovyote muda ule MOURINE asingeweza kuja



    Akaamua kujinyanyua zake akiwa anapepesuka taratibu na kuelekea nje kwa hatua fupi aliendea gari yake na kujipakia ndani



    toka jioni alikwepo katika hoteli ile mpaka muda ule aliiwasha gari na kuiondoa kwa kasi.



    *************



    MOURINE msichana mrembo kiumbo na secretary wake VERGAN akiwa ndani ya gari yake jioni hii moyoni mwake alikuwa na raha sana! kitendo cha BOSI wake kumuitaji hotelini kilimpa faraja,ni kweli alimpenda bosi wake yule, na bosi wake alishamwonesha ishara zote za kumpenda,



    Hakutaka kumkubali kwa kutopenda kuonekana mrahisi ila siku hii ya leo alijihisi hali flan si ya kawaida alijihisi KUMPENDA na kuitaji kuwa pamoja naye kimapenzi hisia zile zikamfanya aongeze mwendo wa gari lake kumuwai mwanaume yule



    Lakini ghafla akiwa katika mwendo mkali akakatisha mwanamke mrembo mbele ya gari,



    MOURINE akajaribu kupiga break huku akiachia yowe ns kufumba macho yake ila breki ikakataa na gari likamvaa dada yule



    MOURINE akiwa kachanganyikiwa huku alitetemeka baada ya kujiisi kumgonga mtu yule akashuka kwa speed mpaka mbele ya gari lake



    AKUKUWA NA MAITI WALA MDADA MOURINE akashtuka!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kwa haraka akarudi garini na kujaribu kuwasha gari GARI LIKAGOMA, akazidi kuchanganyikiwa



    Akashika simu yake nayo kwa ajabu ikawa imezima chaji,safari ya MOURINE ikawa imefia hapo.



    ************



    BADO JOHN VERGAN moyo wake ulijaa simanzi ghafla akiwa kwenye mwendo wa wastani mbele yake akamuona msichana mrembo,



    msichana alozivuta na kuziamisha HISIA zake akazidi kupunguza mwendo wa gari na alipo mfikia dada yule kabla ajamsemesha dada yule akamuwahi



    "kaka naomba lifti"



    VERGAN akujibu swali lile kwani akili yake ilikuwa katika umbo zuri la mrembo yule!



    umbo namba nane,mwenye asili ya kiindi akika alikuwa na mvuto wa ajabu,



    "mimi naita JOHN mwenzangu sijui unaitwa nani?"



    dada yule ndani ya gari alikaribishwa na swali



    "MIMI NAITWA HUSNAT"....



    Macho ya VERGAN yalikuwa katika mapaja mazuri yalokuwa wazi wakati huo,



    binti yule aliyejitambulisha kama HUSNAT alivaa kimini kidogo kilicho acha mapaja yake wazi! kutokana na msukumo wa pombe VERGAN alijikuta akishindwa kuzizuhia HISIA zake nzito kwa dada yule!



    akamtongoza!



    dada yule akuwa na kizuizi VERGAN akimchukulia kama changudoa akaelekea naye katika nyumba yake,



    akiwa na mwanamke yule ndani ya gari alipania kulala naye usiku mzima katika jumba lake lile akilifaidi penzi lake!



    Akazidi kuongea mwendo kurudi afike haraka!...



    LAITI ANGEJUA!?....



    **************



    Ilikuwa ni nyumba kubwa na ya kifahari gari aliyepanda VERGAN na msichana mrembo HUSNAT iliingia mpaka parking

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    VERGAN akiwa kamshika mkono binti yule wakatoka na kuelekea sebuleni ambapo awakukaa sana wakaelekea chumbani



    wakapanda kitandani kila mmoja akionekana kumuitaji mwenzake zaidi!



    VERGAN katu akuziona kwato zilizokuwa katika miguu ya bibie yule!



    Pia hakuyaona macho yake ya kung'aa katika giza kwa macho yake ya kawaida aliyaona kawaida!



    wakazama penzini!



    penzi ambalo katu VERGAN hakuwai kulipata kwa binadamu wa kawaida,



    penzi liliyomlevya na kumpa usingizi mzito,baada ya VERGAN kulala jini HUSNAT akuwa na muda wa kupoteza akavaa nguo zake zote akanyoosha mkono wake juu barua ikatokea akaiweka pale kitandani na GHAFLA AKATOWEKA!!!



    Ilikuwa ni alfajiri tulivu ilojaa kibaridi VERGAN alipapasa mbele yake hapakuwa na mtu, akafumbua macho yake taratibu kajua cha asubuh kalitokeza kutarifu sasa kumepambazuka,



    VERGAN alishtuka na kucheki mlango



    "UKUFUNGULIWA"



    Akakumbuka juu ya kukutana na HUSNA jana



    "au nilikuwa naota?! hapana!"



    bado VERGAN alikuwa katika hali za sintofahamu akakurupuka kitandani pale akiita kwa nguvu kama mweu



    "HUSNA! HUSNA! HUSNA!" Bado hakukuwa na jibu! akaingia chooni,bafuni ndani kwa ndani bado akukuwa na mtu!,



    vergan akiwa kama kachanganyikiwa akafungua mlango na kutoka nje alipomkuta mlinzi wake kipele



    "umemuona msichana katoka humu ndani asubuhi hii?" Akauliza kwa wahka



    "msichana? msichana yupi bosi?" Kipele akasaili....



    "yule nlokuja naye jana usiku!"........



    " Jana usiku?!"



    Kipele akaoji huku bumbuwazi likimbumbukia usoni pale....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ndiyo yule binti nloshuka naye kwenye gari?!"



    "No Bo's!,nliona ukishuka mwenyewe hukuja na mtu kaka"



    "What?!"



    "Ndiyo!,tena ulikuwa full ukipepesuka ukuja na mtu bosi"



    "Mfyuuuuu!"



    Vergan akaachia msunyo ulosindikizwa na mguno hafifu wa mfadhaiko



    Ni wazi alizidi kuchanganyikiwa

    !,akaenda sebuleni akajitupa sofani!,mawazo yakaanza kupishana kama mishale ya saa!!!



    "uyu binti atakuwa kaenda wapi yarabi?! mbona mlango ukufunguliwa? mlinzi naye anasema sikuingia na mtu jana usiku au nilikuwa naota? hapana hapana hapana nilimpa binti lifti HUSNA alinambia anaitwa HUSNA nikampenda! nkamchukua nkaja naye akanipa penzi tamu ambalo sijawai kulipata alafu! alafu ikawaje? HUSNA! HUSNA! hapana si ndoto kuna kitu"



    alijiuliza VERGAN na kujijibu mwenyewe akajinyanyua na kurudi tena chumbani



    macho yakadondokea kitandani



    Kitanda kilikuwa shaghala baghala kuonesha kwamba usiku kucha kilitumika,hilo likazidi kumpa picha sahihi kwa kile akiwazacho



    macho yake yakatua mezani akakuta barua imefungwa vizuri



    Akastaajabu!!!...



    Kwa hatua fupi fupi akasogea pale kitandani huku mkono ukiwa unatetemeka akaifata barua ile na kuishika ilinukia harufu nzuri!,



    harufu ya manukato,alikumbuka manukato hayo ni ya HUSNA



    akaichukua ile barua na kuifungua na kuanza kuisoma naaam macho yalimtoka pima



    "DEAR SAMAHANI! KWA KUONDOKA BILA KUKUTA HARIFU NILIHITAJIKA HARAKA NYUMBANI NA WAZAZI WANGU WAKWE ZAKO HASUBUHI NJEMA WAKO KIPENZI HUSNA NTARUDI"



    VERGAN akashangaa!,ilikuwa lazima ashangae!



    "aliitajika nyumbani!?,alipitia wapi?! aliondoka saa ngapi?!!"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    bado maswali mfululizo yalizidi kumuandama akairudia tena kuisoma ile barua yenye hati nzuri ila akupata majibu aloyaitaji akaikunja barua yake na kuirudisha pale mezani alitoka akaenda kuoga, kuswaki, kuvaa nguo za kazini dakika chache zilizofatia zilimkuta mezani akinywa chai aloandaliwa na mfanyakazi wake aliyetambulika kwa jina la Jasmin.



    alipomaliza alinyanyuka na kuliendea gari lake akapanda na kuelelea kazini alipofika alimpita secretary wake MOURINE bila salamu na kuingia ofisini kwake.



    Dakika chache baadaye Mourine akaingia ili kumuuliza kama aliitaji amletee chai tofauti na matarajio yake VERGAN akaanza kushusha lawama



    "hivi MOURINE kwa nini unantesa hivi? kwa nini jana ulin'danganya na ukuja? kama ulikuwa utaki si ungenambia kuliko kuniweka mahali namna ile mapenzi ayalazimishwi Mou sotokulazinisha......



    MOURINE huku akiwa anatetemeka akamwangalia bosi wake!



    "hapana bosi niliaribikiwa na gari"



    "comon MOURINE kwa nini ukunambia kwa simu nikajua?"



    "simu nayo iliisha chaji bosi...."



    Wakati wakiendelea kuongea ghafla simu ya VERGAN ikaita alipoangalia kwenye scrini ilisomeka HUSNAT.



    Ubongo wake ukatingishika! akampa ishara MOURINE aondoke



    Kabla ajaipokea maswali yakaanza kutiririka katika kichwa chake!



    "nani kampa namba zangu?"



    aliwaza alikuwa na uhakika akumpa wala akuserv namba zake, ili kupata jibu akaamua kuipokea simu ile....



    "alooo!" VERGAN alisema



    "vipi sweet za kazi" sauti nyororo kama kinanda iliuliza VERGAN akaipuuza Na kwa hasira akamuuliza



    "nani kakupa namba zangu?"



    "si wewe sweet umenipa jana?"



    "mimi sijakupa namba zangu"



    "umenipa beby"



    "sijakupa"CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "umenipa!"



    "ok ulikuwa unasemaje?" VERGAN aliuliza kwa hasira



    "nilikuwa naitaji tuonane" HUSNA alisihi



    "siwezi kuonana na wewe" VERGAN alijibu kwa jeuri akapokewa na kicheko kitamu kisha sauti laini ikafatia



    "basi my love ntakuja hapo kazini jioni tuondoke wote!"



    hapo hapo akakata simu ubongo wa VERGAN kwa mara nyingine ukatingishika idadi ya maswali yasiyo na majibu yakatiririka!



    "uyu ni binadamu au jini?,anapafahamu hapa kazini?"



    bila kujielewa akaanza kusarch namba ya HUSNA kusudi azipige



    NO AZIKWEPO!!!



    hakuweza kujizuia kutetemeka akaziangalia kwenye recevid



    kwenye recevd azikwepo!!!



    wakati akiwa katika mawazo ya sintofahamu ghafla meseji ikaingia katika simu yake



    "usiwaze sana dear utaumwa na kichwa"



    namba zilikuwa na jina tu



    JINA BILA NAMBA?



    akazipiga zikakataa!



    Azikutambulika na mtandao ule wa simu!



    Lakini si ndo hizo zilizomtumia msg,?!



    moyo ukaanza kumwenda mbio akaishika simu ya mezani na kumpigia secretary wake MOURINE



    "naomba mwambie ZUBERI namwitaji ofisini kwangu" baada ya maneno Yale akakata simu



    dakika chache badae ZUBER aliingia

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Vergan akamwonesha ishara aketi



    alikuwa ni kijana mrefu,alikuwa ndo meneja baada ya yeye ZUBER ndo alikuwa chini yake alimwamini kijana yule alikuwa ndo mshauri wake,siri zake ZUBERI alizijua,siri za ZUBER naye alizijua



    Kwa kivipi walikuwa ni zaidi ya marafiki waloshibana,waloshauriana....



    Zuberi akupata tabu kugundua bosi wake yule au rafiki yake yule yupo katika matatizo makubwa



    Hiyo ni baada ya kuisoma simanzi ilotawaliwa na majonzi pamoja na woga katika uso wake ule



    "Nimeitikia wito bosi"



    Zuberi akatamka kwa sauti ya upole,akimwangalia kwa mashaka Vergan



    VERGAN alimweleza ZUBERI kila kitu!,akimwacha kijana yule katika mshangao wa hali ya juu wa kutokuamini Yale aelezwayo....



    Mwisho akatoa ushauri wake akitanguliza pole,



    ,"dah pole bosi huyo atakuwa ni jini tu! kubali ukatae! kwanza embu nioneshe hizo msg zake! maana siamin kabisa!"



    VERGAN akatii na kuchomoa simu yake mfukoni akaanza kutafuta zile meseji inbox



    'MESEJI HAZIKWEPO'



    na anakumbuka akuzifuta kabisa! bumbuwazi likauvaa uso wake



    "kah meseji azipo kak!"



    "nini?" ZUBER akaoji kwa mshangao



    "sijazifuta lakini nashangaa kutoziona!"



    "basi BOSI jibu ndo ilo huyo atakuwa ni jini mahaba!"



    "sasa nfanyeje rafiki yangu?"



    "kuna mtaalamu namfahamu ntakupeleka"



    "hapana best mim ni msomi siamini hao watu wengi wao matapeli....."



    Katika vitu ambavyo JOHN VERGAN akuvipenda ni kuamini ushirikina

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mganga wa kienyeji!"



    ZUBER alijaribu kumbembeleza lakin VERGAN akuwa tayari,mwisho akakata na tamaa!



    Zuberi akaaga akihaidi kurejea baada ya kupata wazo lengine, akamwacha bosi wake katika mawazo Yale....



    "ina maana uyu ni mtu au jini?" bado maswali yasiyo na majibu yaliambaa katika kichwa chake.



    "sura ya HUSNAT ikamjia kichwani mwake wakati walivyokuwa wakifanya mapenzi"



    miguno ya kimapenzi na hata sura yake alivyoikunja,utamu alokuwa nao,HISIA zikampanda,na ghafla tabasamu likamponyoka.



    "atakuwa ni binadamu anacheza na akili yangu tu!"



    akajifariji upendo moyon mwake ukafumuka kama mvua za masika



    ALIANZA KUMPENDA!.



    Akashangaa kumpenda ghafla kiasi icho! moyo wake aliujua vyema.



    Aukuwa wa mtu aliyeyaendekeza mapenz akupenda kujiumiza kichwa kama kwa MOURINE aliyepanga kumuoa,lakini MOURINE anamzingua,



    alipobahatika kumuona HUSNA akajua jibu lake limepatikana lakini vitabia tabia vyake vinamshangaza naye ni jini?



    aoe jini?!!



    "no siwezi kumpenda HUSNA!"



    akapingana kwa nguvu na HISIA zake



    ilipofika jioni wakati anajiandaa kuondoka ghafla mlango ukafunguliwa na HUSNAT akaingia na tabasamu pana usoni



    Uzuri wake ulikuwa mara mbili ya mwanzo bumbuwazi likauvaa uso wa VERGA akutegemea kama angekuja kweli



    mbona secretary wake ajampgia simu?



    Na alikuwa kawaida mgeni kuingia bila 'secretary' wake kumpigia naye ndo amruhusu!



    Lakini huyu!!!......

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Verga alijawa na khofu ulochanganyikana na woga



    ilikuwa lazima aogope alikuwa kavaa gauni jekundu refu lililo mkaa vyema, akaenda kuketi kwenye viti vya wageni na kumpa mkono Vergan aliyekuwa bado akitetemeka....



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog