Search This Blog

KIJIJINI KWA BIBI - 1

 









    IMEANDIKWA NA : ALEX KILEO



    *********************************************************************************



    Simulizi : Kijijini Kwa Bibi

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    "njoo uingie bado gari iko wazi hii,

    mama kaa vizuri hapo mnatosha

    watu wawili",ilikua sauti ya mpiga

    debe aliyekuwa anaita abiria katika

    stendi kuu ya daladala mkoani Dodoma(Jamatini).

    Ni dhairi kabisa mpiga debe huyo alikuwa amechoka kutokana na njaa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    na jua kali, pia muonekano wake ulijidhirisha alivyochoshwa na



    maisha. Mdomoni alikuwa na sigara iliyokuwa inawaka na aliipeleka



    mdomoni kila alipogida kipakiti cha konyagi kilichokuwa na nembo ya



    kichwa cha jogoo, na kila alipogida konyagi hiyo aliimeza kwa tabu



    huku sura yake akiwa anaikunja kama anaumia koo. Alivaa shati na



    suruali ya rangi ya bluu iliyopauka na zaidi suruali yenyewe



    aliivalia chini ya makalio na kufanya kuonekana kwa nguo yake ya



    ndani iliyokuwa na rangi isiyoeleweka kutokana na kuvaliwa kwa muda



    mrefu au kukosa maji yenye sabuni ya unga kwa muda mrefu.

    Na kichwani alikuwa na kofia ya kapelo yenye picha ya mmea kwa



    mbele na uso wake ulipambwa na macho makubwa malegevu yenye rangi



    nyekundu, alikuwa na pua pana ilienea vizuri juu ya mdomo wake



    uliokuwa mwekundu kama umeunguzwa na kemikali au moto, na masikioni



    alikuwa amevaa heleni ya duara kama mtoto wa kike na miguu ilikuwa



    na raba nyekundu ya kupanda iliyonakshiwa na mchoro wa nyota



    uliozungukwa na neno lililoandikwa "allstars".



    Ndani ya daladala mojawapo pale

    stendi anaonekana kijana mmoja

    mtanashati, ingawa sio sana ila

    mpangilio wake wa mavazi na usafi

    ndo vimemfanya aonekane wa kipekee kuliko vijana wengine

    ndani ya ile daladala.

    Mpangilio wake mzuri wa mavazi ilitosha kumjua kabisa huyo kijana



    ni aina ya vijana wa kileo wanaokwenda na wakati. Alikaa kiti cha



    nyuma kabisa cha daladala huku masikioni akiwa amevaa headfones



    kubwa kama mpigaji mziki wa disco.



    Baada ya muda wa dakika ishirini, ile daladala ilijaa kabisa na



    Dereva akaiwasha na safari ikaanza.



    Ilitumia mwendo wa dakika 30, ile

    gari ilisimama mbele ya majengo

    marefu(ghorofa) yaliokuwa

    yameandikwa UNIVERSITY OF

    DODOMA.



    kijana akatelemka na kumlipa konda nauli kisha akashika njia



    iliyokuwa ikielekea kwenye ghorofa lililokuwa na rangi nyeupe,



    alipolifikia alipanda ngazi mpaka ghorofa ya tatu na kuingia katika



    chumba ambacho inaonekana anaishi humo,



    'niaje kayoza,? vipi umepata body

    spray ya chastity,'" wenzake ndivyo

    walivomlaki namna hiyo,hakujibu

    kitu akawatupia begi,



    "Alafu sio ustaharabu huo, muwe mnajifunza kusalimia ndipo muulize



    shida zenu" Kayoza aliongea huku akitoa shati

    lake akabaki na vest iliyoruhusu kifua

    chake kionekane kwa ufasaha zaidi, alafu akajitupa kitandani



    akachuaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    simu yake aina ya HTC desire,

    akaenda upande wa ujumbe mfupi

    wa maneno ambao kulikuwa na ujumbe mfupi uliongia muda mrefu



    uliopita ila hakuonekana kuujali, akaona huo ndio muda wa kuangalia



    huo ujumbe, alipousoma aliishia kutabasamu kwa dharau huku



    akisikitika, kisha akaandika

    "usipoteze

    muda wako kunifikiria, sina mpango

    wa kuwa na mahusiano ya kimapenzi

    muda huu" akautuma ule ujumbe katika jina alilosevu

    KICHECHE.



    "Vipi umekula" Rafiki yake mmoja alimuuliza huku alivaa fulana,



    "Tayari, sasa nitaendaje mjini alafu nisile?" Kayoza alijibu huku



    akiutupia mto chini ya kitanda,



    "Poa basi, mimi ndio naenda kutafuta msosi" Rafiki yake huyo



    aliongea huku akifungua mlango,



    "Haina noma, Acha nijipumzishe kidogo" Kayoza alijibu.



    Siku iliyofuata ilikua sikukuu ya

    kitaifa, kwa hyo wanafunzi wengi

    hawakuwa na ratiba ya kuingia

    darasani.



    Kayoza alichelelewa

    kuamka hiyo siku, aliamka saa nne

    asubuhi, akaingia bafuni, alipomaliza

    kuoga akarudi katika chumba chao, ile kuingia ndani akakunja sura

    ghafla baada ya kumkuta ndani msichana ambaye hakuwa akimpenda,



    "mambo kayoza", ilikua sauti ya binti mrembo ambae

    anawakimbiza wanawake wenzake

    kwa uzuri wa umbo na sura, alikua

    katika tatu bora katika shindano la urembo lililoshirikisha vyuo



    vyote vilivyopo Dodoma.



    Huyu binti anaitwa Stellah

    Malingumu, ni msichana wa miaka ishirini na moja ambaye alikuwa



    mwanafunzi chuoni hapo akichukua shahada ya ualimu katika masomo ya



    sayansi.



    "poa, umeamkaje?",Kayoza akajibu

    huku akijilazmisha kujua hali ya stellah ingawa hakutaka,



    "aah safi, mbona meseji yako uliyonitumia jana sikuielewa?",



    Stellah nae akamtupia swali,



    "kwani niliiandika kwa kutumia lugha

    ya kichina?", Kayoza badala ya kujibu

    nae akauliza, tena kwa jeuri,



    " Ok, yaishe", stellah akaamua

    kukatisha mabishano,



    "Samahan naomba utoke nje mimi

    nataka kuvaa", kayoza akaongea kwa

    ustaharabu wa kinafki,



    "mimi naondoka moja kwa moja, ila

    naomba jioni tukutane mjini katika

    maeneo ya nyerere square", Stellah

    akamwambia Kayoza,



    "kuna ishu gani?, alafu jioni, si bora

    ingekua mchana ningekuja",Kayoza

    akajibu. ,



    "usiwe na wasiwasi mpenzi, kama

    unahofu njoo hata na marafiki

    zako",Stellah akamalizia huku akitoa tabasamu murua.



    "Mimi sio mpenzi wako Stellah, rekebisha kauli zako" Kayoza



    alimuonya Stellah huku akiwa amekasirika,



    "Sawa, nisamehe kwa hilo. Kwa hiyo jioni utakuja ama?" Stellah



    aliuliza tena,



    " Jioni ya saa ngapi?", Kayozaakauliza,



    " saa moja na nusu tutakua pale tunawangojea, nitakua na Tausi",



    "Poa, haina noma, nitakuja", Kayoza

    akakubali mwaliko. Kama angejua



    "Peke yako au?" Stellah aliuliza,



    "Vipi kwani, mbona maswali mengi?" Kayoza aliuliza huku akiwa



    amehamaki,



    "Inatakiwa nijue ili nipange ratiba zangu za matumizi vizuri"



    Stellah alijibu kwa upole,



    "We panga unavyojua wewe, maana mimi nije peke yangu au na wenzangu



    hayo hayakuhusu na gharama zangu au wenzangu pia hazitokuhusu"



    Kayoza aliongea macho yakiwa makavu,



    "Basi baba, hatugombani hapa" Stellah aliongea huku akitabasamu,



    "Haya nenda nje mimi nivae" Kayoza alimwambia stellah,



    "Kwani ukivaa mbele yangu kuna ubaya gani?" Stellah aliuliza kwa



    utani,



    "Wewe mpumbavu nini?" Kayoza aliongea huku akimsukumia Stellah nje



    na kubaki ndani peke yake akisonya kwa hasira huku akiufikiria



    mualiko aliopewa na Stellah..CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Ila angejua ambacho kitamtokea, basi asingekubali ule



    mwaliko.......



    "Mpuuzi kweli huyu manzi" Kayoza aliendelea kuongea peke yake huku



    akivaa kaptula kabla hajashtuliwa na mtu aliyekuwa anasukuma mlango



    ili aingie ila alishindwa kutokana na ule mlango kufungwa kwa



    ndani,



    "Bado hujaondoka tu?" Kayoza aliuliza kwa hasira,



    "Fungua bwana" Sauti nene ya kiume iliongea kutoka nje na ndipo



    Kayoza akauendea mlango na kuufungua na wakaingia rafiki zake



    wawili, mmoja aliitwa Omary na mwingine alitambulika kwa jina la



    Denis,



    "Vipi wewe unajifungia fungia mchana, au ulikuwa na Stellah?" Denis



    alimuuliza Kayoza,



    "Umejuaje?, alikuwepo hapa muda si mrefu" Kayoza alijibu huku



    akijitupa kitandani,



    "Kwa hiyo mlikuwa mnafanya mambo flani nini?" Omari aliuliza huku



    akicheka,



    "Muda wote unawaza ujinga tu, hivi ni lini utakuwa wewe?" Kayoza



    alimuuliza Omary kwa hasira,



    "Huyu sio bure, zile tetesi hata mimi naanza kuziamini" Omary



    aliongea huku akimgeukia Denis,



    "Tetesi gani?" Kayoza aliuliza kwa hamaki huku nae akimgeukia



    Denis,



    "Maneno tu ya watu" Denis alijibu huku akionekana hataki



    kulizungumzia hilo,



    "Maneno gani sasa, si uniambie" Kayoza aliongea huku akiwa bado



    anamuangalia Denis,



    "Mchane, usiogope, huyu ni rafiki yetu na ni lazima chochote



    kinachosemwa juu yake tumwambie" Omary alimsisitizia Denis,



    "Niambie hata wewe kama Denis hataki kuniambia" Kayoza aliongea



    huku akimgeukia Omary,



    "Bwana mimi sipendi kuficha, uko nje habari zimeenea kuwa wewe ni



    shoga, eti haiwezekani tokea uanze kusoma hapa mwaka wa tatu huu



    haujawahi kuonekana na mwanamke sehemu yoyote ile" Omary aliongea



    huku akitazama chini na kumfanya Kayoza nae ainame chini huku akiwa



    na huzuni sana,



    "Mimi siamini kama wewe unaweza kuwa shoga, ila nahisi labda una



    tatizo jingine, tueleze rafiki yetu, usiogope" Denis aliongea kwa



    lengo la kumfariji Kayoza ambaye bado alikuwa kichwa chini huku



    akiwaza,



    "Tunasaidiana mambo mengi. Sisi ni ndugu sasa na sio marafiki tena,



    tatizo lako ndio tatizo letu, kwa hiyo Sema kama una tatizo tuone



    kama tutaweza kukusaidia" Omary nae alimsihi Kayoza awaeleze,



    "Sina hamu ya kuwa na mwanamke wala kufanya mapenzi na sijui ni kwa



    nini?" Kayoza aliongea kwa huzuni huku akiwa bado kichwa chini,



    "Ila ulishawahi kufanya mapenzi kipindi cha nyuma?" Omary



    alimuuliza,



    "Tokea napata akili sijawahi na wala sina hamu kabisa" Kayoza



    alijibu,



    "Umeshawahi kwenda hospitali?" Denis alimuuliza,



    "Nimeenda mara nyingi sana na naonekana sina tatizo" Kayoza



    alijibu,



    "Na kwa waganga wa kienyeji umeshawahi kujaribu?" Omary aliuliza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kila nikipanga Mipango ya kwenda kwa waganga, uwa siku ikifika



    najikuta napuuza au kinaweza kutokea kitu kingine kitachoharibu huo



    mpango" Kayoza aliwaeleza wenzake,



    "Basi ilo jambo tutalifuatilia vizuri, sio bure" Denis aliongea



    huku akisikitika,



    "Stellah alikuwa anasemaje?" Omary aliamua kubadilisha maada,



    "Alafu nilishasahau, amesema jioni tuonane mjini" Kayoza alijibu,



    "Kwa hiyo leo unatuacha, utalala huko huko au utarudi?" Omary



    aliuliza,



    "Amesema tuende wote watatu" Kayoza alijibu,



    "Aisee mimi leo sina hela, kwa hiyo sitoenda, si unajua leo



    wikiendi so ukienda mjini inabidi ujipange" Denis aliongea huku



    akitabasamu,



    "Amesema gharama zote zake, sisi tuende kama tulivyo" Kayoza



    aliongea na kufanya wenzie wafurahi,



    "Basi poa, ngoja nilale kidogo ili chakula kishuke" Denis aliongea



    huku akijilaza kitandani,



    "Ila usiku tutarudi, hatutalala mjini" kayoza alisema,



    "Mimi sitorudi, nitaunganisha clab moja kwa moja, leo wikiendi



    bwana. Au wewe Denis nawe utarudi?" Omary aliuliza huku nae



    akipanda katika kitanda chake cha juu,



    "Tutajua uko uko" Denis alijibu kivivu huku akiwa amesinzia.



    ********************



    Mida ya saa moja kasoro jioni, Kayoza,

    Omary na Denis walikua maeneo ya

    mjini katika foleni ya ATM. Ilipofka

    zamu yao kayoza akaingia ndani,

    akatoa pesa, kama elfu hamsini

    akatoka na kuungana na wenzake,



    "oya wakubwa, mi naona twendeni

    kwanza tukale kwa sababu huyu

    demu mimi simuamin amini,

    anaweza kuwa katenga bajeti ya

    kunywa tu, akijua sisi tumekula", Kayoza alikua anawaambia wenzake,



    "acha uboya we mtoto wa mama, alipokwambia uje saa moja alitaka



    tuje tupige nae msosi wa jioni, huyo du si

    anajua ratiba zetu za msosi wa

    usiku, kuwa tunakula saa tatu, kwa hiyo alijua saa moja tutakuwa



    bado hatujala" Omary aliongea huku akiwa anatafuna karanga.



    Mara simu ya kayoza ikaanza kuita mfukoni,

    akaitoa mfukoni kisha akaiangalia

    kwenye kioo cha simu, jina lililoonekana wakati huo lilisomeka



    KICHECHE.



    'huyo Stellah anapiga" Kayoza aliwaambia

    wenzake ambao walikuwa

    wanamuangalia,



    "usilembe bishoo wewe, pokea simu uongee na mtoto mzuri", Omary

    alimsisitiza Kayoza baada ya kuona anajishauri kupokea simu.



    Kayoza akaipokea ile simu, kisha

    akaweka sura ya umakini,



    "Mambo..",Kayoza alimsalimia Stellah,



    "poa, mko wapi?",Stellah alimuuliza Kayoza kupitia simu,



    "tupo hapa benk, tunakuja",Kayoza

    alijibu,



    "mbona simu ilikuwa inaita muda mrefu hivyo?",Stellah alianza

    kulalamika namna hyo,

    "nimeiweka sauti ndogo mno, alafu

    hapa ATM kuna utulivu sana na watu wako wengi sana, kwa hiyo



    ilinibid nisogee mbali kidogo ili niipokee simu yako" Kayoza

    akamdanganya Stellah,



    "ok.. poa, sisi tumeshafika

    tunawasubir nyinyi" Stellah

    akamtaharifu Kayoza,



    "sisi tutachelewa kidogo kwa sababu tunaenda kula kwanza", Kayoza

    akatoa udhulu,



    "mambo gani sasa, nyie njooni tu, hivyo vyote



    nimevitayarisha",Stellah akawaka,



    "poa, ndani ya dakika kumi tutakuwepo hapo" Kayoza akaongea kisha



    akakata simu.



    "Haya waungwana twendeni

    tukawachune hao vicheche, mida ya

    saa nne tuwateme tukajiachie clab

    mpaka kuche" Kayoza akawaambia wenzake,



    "Vicheche? Kwani yuko nani?" Omary aliuliza,



    "Yuko na Tausi" kayoza alijibu,



    "Basi twendeni tukakae nao alafu baadae tunaenda zetu clab" Omary



    aliongea,



    'nyie nendeni tu uko club mimi lazma nikalale

    na mmoja wao" Denis aliongea na wenzake wakacheka.



    "Jamaa mroho kweli" Omary alimtania Denis huku akiendelea kucheka,



    "Wamekwambia wapo wapi?" Denis alimuuliza kayoza,



    "Wapo Nyerere squarre" kayoza alijibu huku wakivuka barabara



    inayoelekea wanapokwenda.



    Walipofika nyerere square,

    wakamuona kwa mbali stellah na rafiki yake aitwae Tausi,



    "Leo kazi ipo" sauti nzito ilipita kwenye masikio ya Kayoza na



    kushindwa kuelewa inatokea wapi, na cha ajabu Denis na Omary



    hawakuweza kuisikia sauti hiyo....



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Jamani hamsikii sauti yoyote ya kutisha?" kayoza aliwauliza



    wenzake baada ya kuwaona kama hawasikii anachokisikia yeye,



    "Sauti gani?" Denis aliuliza,



    "Sauti nzito inakwaruza masikioni" Kayoza alijibu na wenzake



    wakaishia kucheka,



    "Acha mawenge wewe, au unapata uoga kukutana na Stellah?" Omary



    aliongea huku akimcheka kayoza,



    "Acha ujinga, mimi sijamuongelea Stellah hapa, naongelea ishu



    nyingine" Kayoza aliongea baada ya kutofurahishwa na maneno ya



    Omary,



    "Yaishe basi, kifupi sisi tunasikia sauti za magari tú na hatusikii



    sauti nyingine. Au sio Ommy?" Denis aliuliza huku akimgeukia Omary,



    "Ndio maana ake" Omary alijibu huku akicheka.



    Wakiwa wanaendelea na mwendo, kwa mbali waliweza kuwaona Stellah na



    Tausi , ila walikua nje ya sehemu husika.



    "Sasa mbona wapo nje?" Omary aliuliza kwa mshangao,



    "Labda wamekaa nje ili tuwaone kiurahisi" Denis alijibu.



    wakina kayoza walipowafikia

    wakapeana salamu,



    "jaman twendeni sehemu

    nyingine, hapa hata hapaeleweki" Stellah aliongea baada ya salamu,



    "kwani hapa kuna nini?, kayoza akauliza?" Kayoza aliuliza kiubabe



    ubabe,



    " Jamani shem hapa

    wamesema mda umeisha" Tausi

    ndivyo alijibu namna hyo,



    "We mpuuzi nini, nani Shemeji yako?" kayoza aliuliza kwa hasira,



    "Nini wewe, Acha fujo Kayoza, huwezi jua labda Shemeji yako kwangu"



    Omary aliongea huku akimcheka Kayoza,



    "Huyu mwenzenu vipi, mbona ana hasira za karibu hivyo?" Stellah



    aliuliza huku akimtazama Dennis,



    "Mzoeeni tu huyu mshkaji wetu" Denis alijibu huku akitabasamu,



    " sasa tunaelekea wapi?" Kayoza akauliza,



    "Mhm...mi hata cjui ni sehemu gani nzuri kwa hapa mjini usiku huu"



    Stellah akajibu,



    "Mi naona twendeni hapo

    Saturnight bar" Denis akatoa mwelekeo,



    "Bar tena?" Kayoza aliuliza kwa mshangao kwa maana yeye hatumiagi



    kilevi,



    "Bar hata soda zipo" Omary alijibu huku akionekana kumpuuza Kayoza,



    " hiyo Saturnight ni mbali kwani ili tuchukue taxi?" Stellah



    aliuliza,



    "Ahaa wapi ni hapo tu nyuma ya TRA" Denis akajibu na mwisho wote

    wakakubaliana waende hapo Suturnight Bar.



    Walipofika wakakuta

    watu wengi sana na hii ni kutokana na mpira wa ligi kuu ya



    uingereza

    ilikua inaonyeshwa pale nyakati za usiku,



    "Kwa hiyo tufanyaje? Maana naona kote kumejaa na hakuna nafasi"



    Tausi aliuliza,



    "Ebu subirini kidogo" Denis aliongea

    kisha akaingia ndani akatumia mda

    kama wa dakika kumi hivi hivi, kisha akatoka,



    "jamani eee, nimeongea na wahusika

    wakasema kama tunahitaji sehemu

    tulivu, tunaweza kuchukua chumba

    kimoja tukawa tunakitumia ila lazima

    tukilipie, wenzangu mnasemaje?" Denis aliongea baada ya kutoka



    ndani,



    "haina shida tena ndo vizuri" Stellah

    akajibu,



    "Mhm, kwani jaman

    tutatumia mda gani kula na hayo maongezi kiasi kwamba mpaka



    tuchukue chumba?" Kayoza akauliza,



    "Boy acha maswali ingia utengeneze shavu, leo tuifanye siku kuu"



    Omary akasema.



    Baada ya mvutano

    wa hapa na pale, wakakubaliana

    kuingia mule ndani, wakaagza

    chakula cha kutosha na vinywaji pia,

    so ikawa kula na kunywa, paka

    wakawa wako hoi kwa ulevi. Ila wakati wote huo Kayoza alikuwa



    anakunywa soda. Ila mwisho wenzake walimrubuni na kujikuta akionja



    bia moja, katika hali ya ajabu kabisa, alijikuta anazima kwa bia



    moja tu mpaka wenzake wakamshangaa.



    Baada ya wote vilevi kuwakolea, vibweka vikaanza mara Stellah



    amkumbatie

    kayoza, mara omari amtukane denis

    kisa tausi.



    Ilipofika saa 7 usiku, mhudumu

    akawaambia anataka kufunga kwa

    hiyo waondoke, ila wao wakadai

    watalala pale pale na waongezewe

    chumba kingine, Mhudumu akawapa

    ufunguo wa chumba kingine ambacho kwa makubaliano yao hicho chumba



    wangeenda kulala Denis, Omary na Tausi.



    Stellah akawaomba wote watoke abaki yeye

    na kayoza, kipindi hicho kayoza hajielewi amepoteza kujitambua



    kutokana na bia moja aliyokunywa, tena ukizangatia ndio ilikua mara



    yake ya

    kwanza kunywa pombe.



    Walipotoka tu wakina Denis, stellah akafunga

    mlango haraka, akajitahidi kumbeba

    kayoza paka kitandani, alafu Stellah

    chap chap akavua nguo kisha akawa

    anamvua kayoza, huku akiamini hiyo siku ni moja kati ya siku bora



    kabisa ya kutimiza moja ya ndoto zake, kulala na mwanaume



    anayempenda.



    Alitumia dakika

    tano kukamilisha zoezi zima, kisha akapanda kikatandani na kuanza



    kumchezea Kayoza kimahaba, ila kuna hali aliiona, kila baada ya

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    dakika moja mwili wa Kayoza uliongezeka ubaridi kiasi kwamba akawa



    kama chupa ya soda iliyotoka ndani ya friji.



    Stellah aliliiona hilo ila alitaka kupuuzia kutokana na hamu zake



    za kimwili. wakati akiwa bado anaangaika, ghafla bin vuu kayoza



    aliamka mithili ya mshale huku macho yake yakiwa meupe na kiasi



    kwamba mboni hazikuonekana, macho yakawa

    yanang'aa tena kama tochi, Stellah ndipo akapata mshtuko,



    "Vipi tena Kayoza?" Stellah aliuliza huku hofu ikianza kumtawala,



    lakini kayoza hakujibu kitu na badala alitoa tabasamu moja la ajabu



    na kufanya meno yake yaonekane na kwa kasi ya ajabu yale meno



    yakaanza kurefuka na kuwa makubwa kama ya mnyama anayefahamika kwa



    jina la ngiri.



    Stellah akiwa kama amepatwa na

    mshango au bumbuwazi, alijikuta ameganda Pale pale kwa kihoro huku



    akiwa hana nguvu kutokana na tukio analoliona.



    Mwishowe akajikaza na kuanza kujiondoa ndani ya shuka kwa lengo la



    kukimbia,



    "Unaenda wapi usiku huu, huogopi kutoka nje na giza hili?" Kayoza



    alimuuliza huku akiwa katika hali yake ile ile,



    "Naenda chooni mara moja" Stellah alijikuta anajibu bila kutegemea



    huku mwili ukiwa unamtetemeka,



    "Nisubiri nikusindikize" Kayoza akaongea huku nae akiwa anashuka



    kitandani, Stellah akahisi ni bora kukimbia kuliko kumuamini huyo



    kiumbe wa ajabu. Akiwa anaanza kukimbia, Kayoza aliruka na kutua



    mbele yake, Stellah akataka kupiga kelele, ila alichelewa, tayari



    mkono wa Kayoza ulikuwa mdomoni kwa Stellah kumziba asipige kelele



    na huku mdomo wa kayoza ukiwa shingoni mwa Stellah na yale meno



    makubwa yalitumika kuung'ata mshipa mkubwa wa damu na Kayoza



    akaanza kuinyonya hiyo damu huku akitoa muungurumo wa ajabu



    uliosikika kwa sauti ya chini. Alipomaliza kazi ya kufyonza damu ya



    mwili wa Stellah, aliuachia ule mwili na kudondoka chini ukiwa



    hauna tena uhai, ndio ukawa mwisho wa Stellah, mwanaume aliyedhani



    wa ndoto za maisha yake ndiye mwanaume aliyempotezea ndoto za



    Maisha yake.



    Kayoza aliuangalia ule mwili kwa dakika chache na yeye nguvu



    zikamuishia akapoteza fahamu na kuanguka chini pembeni ya mwili wa



    Stellah.



    Asubuhi Kulipokucha, Kayoza aliamka huku akiwa na uchovu usio wa



    kawaida, ila alijishangaa akijikuta amelala chini huku akiwa mtupu



    hana nguo na pia alihisi mdomoni ana harufu ya damu ila alipuuza



    huku akiamini labda alijing'ata usiku, kitandani hakukuwa na mtu.



    Akapeleka mikono chini ili ainuke, hapo ndipo alipohisi amegusa



    mwili wa mtu, akapeleka macho yake Pale alipohisi amegusa mtu,



    ndipo alipoweza kumuona Stellah akiwa amelala tena akiwa mtupu na



    shingoni alikuwa na damu, hapo akashtuka, akajivika ujasiri na



    kumgeuza, akakuta alama ya meno kwenye shingo ya Stellah, Kayoza



    akajikuta anatema mate kutokana na zile alama za meno



    zilizotengeneza kidonda kikubwa shingoni kwa Stellah. Kayoza



    alipotema mate alishangaa kuona mate yake yametapakaa damu, akaona



    sasa hiyo kesi ni yake.



    "mama yangu, kumeshaharibika hapa" kayoza aliongea baada ya kuhisi



    kuwa inawezekana Stellah amekufa na hakuna mwingine atayekamatwa



    zaidi yake.



    Akaona njia sahihi ni kukimbia hakutaka kujua hata wenzake wapo



    wapi.



    Akaamua kuvaa fasta ili

    akimbie mule ndani kabla mtu yoyote hajajua tukio alilolifanya,



    mara akasikia

    sauti ya mtu akigonga mlango,



    _________________

    Kayoza akakaa kimya, sio kwamba hakuisikia hodi inayopigwa, ila



    alipigwa na ganzi kutokana na kuhisi kuwa mtu yoyote atakayeingia



    ni lazima amuhisi kuwa yeye Kayoza ndiye aliyemuua Stellah.



    Mgongaji akaongeza nguvu ya ugongaji.



    "Nani?" Kayoza aliuliza kwa sauti ya juu kidogo iliyoambatana na



    kitetemeshi,



    "Mimi Tausi" Mgongaji mlango alijibu huku akiacha kugonga kwa



    kuamini amesikiwa na watu waliopo ndani,



    "subiri kidogo au sema una shida gani?" Kayoza akauliza,



    "Niruhusu niingie bwana, maswali ya nini?" Tausi aliongea,



    "Ongea shida yako bwana, sio lazima uingie ndani" Kayoza aliongea



    huku akiwa hataki Tausi aingie ndani,



    "mwambie Stellah anipe hela nikanunue mswaki na dawa" Tausi



    akasema, Kayoza akakimbilia suruali

    ya stellah akaikota kisha akaisachi,



    "mh..hamna kitu'' Kayoza akajisemea peke yake, kisha akasogea



    mlangoni CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "kasema hana" Kayoza aliongea kwa sauti ya juu kidogo,



    "khaa jamani hela

    zote zile za kwenye pochi kazimaliza jana!?, Tausi aliuliza kwa



    mshangao.



    Kayoza ndio akagutuka na kupepesa macho mule chumbani, ghafla



    akainama chini ya meza ilipokuwa pochi ya Stellah, akaichukua pochi

    akatoa noti ya shilingi elfu kumi, akaenda hadi mlangoni,



    akaufungua mlango kidogo,



    "mambo" Kayoza

    akamsalimia Tausi,



    "safi, vipi stellah

    bado kalala?" Tausi aliuliza baada ya kujibu

    salamu huku nafsi yake ikiwa na amani,



    "yuko macho ila anaona

    uvivu kuinuka kitandani" Kayoza alijibu huku akitabasamu.



    "Na wewe uko poa?" Tausi alimuuliza Kayoza,



    "Niko Poa, unaweza kuniambia nini kiliendelea baada ya mimi kunywa



    pombe jana?" Kayoza alimuuliza Tausi,



    "Jana ndio nimejua kuna watu wana vichwa vibovu" Tausi aliongea



    huku akicheka,



    "Unamaanisha nini?" Kayoza aliuliza,



    "Yaani wewe ulikunywa bia moja tú na ukazima kabisa. Yaani kabia



    kamoja tu?" Tausi aliongea huku akiendelea kumcheka Kayoza,



    "Baada ya hapo?" Kayoza aliuliza,



    "Sisi tuliondoka na kuwaachia chumba. Sasa labda wewe ndio uniambie



    baada ya hapo mlifanya nini?" Tausi aliuliza ila kiutani,



    "Na wakina Omary walielekea wapi?" Kayoza aliuliza,



    "Jana tulichukua chumba kingine baada ya wewe kuzidiwa" Tausi



    alijibu,



    "Kwa hiyo wewe ulilala na wakina Denis?" Kayoza aliuliza,



    "Ndio, ila hatukufanya kitu" Tausi alijibu huku akijisikia aibu,



    "Poa, Acha mimi nirudi kulala kidogo" Kayoza aliongea,



    "Inaelekea mlikuwa na shughuli nzito jana usiku" Tausi aliongea



    huku akicheka,



    "Ebu fuata kilichokuleta, kama huna cha kuongea ni bora uondoke"



    Kayoza aliongea huku akifunga mlango na kumuacha Tausi akiendelea



    kucheka.



    "Hutaki kusifiwa?" Tausi aliuliza huku akiwa amefungiwa mlango kwa



    nje,



    "Kwanini usijisifie wewe uliyelala na wanaume wawili?" Kayoza



    aliuliza huku akiwa ndani,



    "Acha maneno yako ya kipuuzi" Tausi aliongea kwa hasira,



    "Kwani yako ndio ya maana?" Kayoza nae aliuliza,



    "Ebu muamshe Stellah nimsalimie shoga yangu" Tausi aliamua kubadili



    mada,



    "Nimekwambia amelala, Kwanini huelewagi wewe?" Kayoza aliuliza kwa



    hasira huku akiwa ndani,



    "Nilijua amelala na ndio maana nikakwambia muamshe, au mtu



    anayeamshwa ni wa aina gani?" Tausi alihoji huku akiwa nje,



    "Ebu nenda bwana, mtaongea baadae akiamka" Kayoza aliongea,



    "Ujue mimi ni shoga yake?, ebu muamshe nimuulize kitu" Tausi



    alikazania utasema alikuwa anajua kuwa Stellah hayupo tena duniani,



    "Mimi boyfriend wake, nimesema muache apumzike" Kayoza aliongea kwa



    mamlaka,



    "Umesema wewe nani wake?" Tausi aliuliza,



    "Boyfriend wake" Kayoza alijibu,



    "Leo ndio umekubali kujiita boyfriend wake, si ulikuwa unajifanya



    humtaki?" Tausi aliuliza huku anacheka,



    "Hayakuhusu" Kayoza alijibu na kufanya kuwa kama wanasutana,



    "Kwa hiyo ndio umegoma kumuamsha?" Tausi aliuliza huku akimcheka



    Kayoza,



    "Nenda dukani, ukirudi utakuta nimemuamsha" Kayoza alijibu ili tu



    Tausi aondoke.



    Baada ya tausi kuridhika na majibu ya Kayoza aliondoka na kuelekea

    dukani.



    Kayoza akaona hiyo ni nafasi nzuri ya kuuficha mwili wa



    Stellah,Akauchukua mwili wa

    stellah na kuuingiza chini ya kitanda, na kisha akaenda bafuni na



    kukuta kuna taulo zimetundikwa ukutani, akaichukua moja kwa ajili



    ya kwenda kufutia damu iliyomwagikia sakafuni.



    Akaichukua na kurudi nayo chumbani, sasa wakati anaangaika

    kufuta damu sakafuni mara mlango

    ukafunguliwa ghafla, alikua ni Tausi, alipoziona zile damu sakafuni



    alionekana kushtuka sana,



    "vipi kuna usalama kweli?" Tausi aliuliza,



    "upo shem" Kayoza alijibu huku akizuia hasira zake kutokana na



    Tausi kuingia bila hodi,



    "Hizo damu za nini sasa?" Tausi aliuliza,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Stellah alijigonga kidogo ukutani ndio damu zikawa zinamtoka



    puani"

    Kayoza akatumia uongo kujibu,



    "stellah mwenyewe kaenda wapi?" Tausi akauliza tena,



    "kaenda kuoga" Kayoza akadanganya tena.



    "Acha na mimi nikaoge" Tausi aliongea huku akinyanyuka ili aondoke,



    wakati ananyanyuka akadondosha dawa ya

    meno, ikabidi ainame ili aiokote, ile kuinama tu, kwa ajili ya



    uchovu pia

    na hangover alizoamka nazo akajikuta anapiga mweleka mtakatifu

    puh, hadi chini, sasa akawa anajigeuza geuza pale chini, mara

    macho yake yakagota chini ya uvungu wa kitanda,



    "khaa naota au?" Tausi akajikuta amelopoka.

    Ni kitendo bila

    kuchelewa, Kayoza akaruka hadi

    shingoni kwa tausi, ila hapa hakumnyonya damu ila alimkaba

    shingoni kisawa sawa mpaka binti wa

    watu akatoa shuzi zito alafu akatulia

    kimya, hakutaka kumuua ila alitaka kumzuia tú asipige kelele na



    matokeo yake yakawa ni kuua bila kukusudia. Kayoza akazidi



    kuchanganyikiwa, Akauchukua mwili wa

    Tausi nao akauingiza chini ya kitanda, Kayoza akawa kama chizi kwa



    maana alikuwa anazunguka tú ndani bila kujua anachofanya.



    Baada kama ya dakika ilisikika hodi nyingine,



    "Nani?" Kayoza aliuliza huku jasho la uoga likimtoka,



    "Mimi muhudumu" Sauti ya kike ilijibu kutoka nje,



    "Unasemaje?" Kayoza aliuliza,



    "Nauliza kama mnajitaji kufanyiwa usafi chumbani kwenu" Mhudumu



    aliongea huku akiwa nje,



    "Hapana hatuhitaji" Kayoza alijibu,



    "Pia kama mtahitaji supu au chai vinapatikana pia" Mhudumu alizidi



    kuongea,



    "Tukihitaji tutakuja wenyewe kuagiza" Kayoza alijibu huku akikereka



    kutokana na maswali ya huyo muhudumu,



    "Alafu pia kama chupa za soda au bia chumbani kwenu, naziomba"



    Mhudumu aliongea pale nje ya mlango,



    "Acha ujinga msichana, ujue huo ni usumbufu unatufanyia katika



    starehe zetu, au ndio mmefundishwa hivyo na bosi wenu ili nikitoka



    nikamuulize?" Kayoza aliongea kwa hasira baada ya kuchoshwa na



    maswali ya Mhudumu,



    "Basi samahani kaka yangu, usiende kumwambia bosi wangu" Mhudumu



    aliongea huku akiondoka haraka haraka mlangoni mwa chumba



    alichokuwamo Kayoza.



    Mhudumu wakati anaondoka, koridoni akapishana na Denis na Omary



    ambao nao walikuwa wanaelekea katika chumba alichokuwepo Kayoza,



    walifika mlangoni na kuingia bila hata kupiga hodi.



    "bishoo vipi unambonji paka saa tano,

    au binti kakupa vitu hadimu?" Omary

    aliingia kwa staili hyo, ila kayoza hakujibu, alionekana ana mawazo

    sana,



    "vipi kaka mbona hivyo? Sie tuliechangia demu tuko poa hatuna

    mawazo, we uliejilia mzigo wa peke

    yako umeshika tama" Denis akaongeza neno tena, pia kayoza

    hakujibu na wenzie wakawa wanaishangaa hiyo hali na mwisho wote



    wakakaa kimya. Mwishowe baada ya

    ukimya mrefu,



    "tunaweza kwenda au kuna kitu mnangoja?" Kayoza aliuliza,



    "warembo wako wapi?" Denis nae akauliza,



    "nimeua" Kayoza akajibu kwa kifupi,



    "tunajua umeua Stellah, Tausi tumeua sisi"

    Denis akasema uku neno kuua akijua kayoza kamaanisha ni kitendo cha



    kufanya mapenzi,



    "au wameenda kupata supu moto?" Omary akatupia swali tena,



    "wako chini ya kitanda" kayoza akajibu huku dhahiri uso wake



    ulionesha amechanganyikiwa.



    Kwa kuwa Omary alikaa kwenye kochi, yeye

    ndio akawa wa kwanza kutupia macho chini ya kitanda, aliona Stellah



    na Tausi wakiwa chini ya kitanda, ila hakuamini alichokiona,



    ilibidi asogee mpaka ilipo miili ya wakina Stellah na kuhakikisha



    mwenyewe kwa macho yake kuwa wale wanawake wawili tayari ni



    marehemu.



    "Mungu wangu, umeua kweli" Omary aliuliza huku akiwa anasimama,



    Kayoza kuona hivyo nae allisimama na kwenda alipokuwa Omary na



    kumkaba shingo....







    Denis akanyanyuka haraka mithili

    ya gari inayowaisha mgonjwa

    mahututi hospitalini, lakini kayoza

    alikua na kasi mara mbili, akawai

    mlangoni.."please Denis na Ommy, nawaomba

    mtulie rafiki zangu, nahitaji msahada

    wenu" kayoza aliongea kwa upole,



    Denis ikabidi arudi na kufunua godoro na

    kuziangalia zile maiti, huku akionekana ni mtu mwenye maswali

    mengi kichwani, baada ya muda

    kidogo akagutuka,



    "imekuaje kaka?" Denis

    akauliza huku akiwa bado anaziangalia zile maiti,



    "Kwanza kubalini kuwa upande wangu, alafu nitawaambia ukweli" Kayoza aliongea huku akiwatazama wenzake kwa zamu,



    "Tuambie kwanza nini tatizo?" Omary aliongea huku akijishika shingo kutokana na kabali alipigwa na Kayoza muda mchache uliopita,



    "Mimi niko upande wako, na nitakuwa upande wako" Denis aliongea huku akimuangalia Kayoza aliyeonekana kuchanganyikiwa,



    "Hata mimi niko upande wako, haya tuambie ilikuwaje?" Omary aliuliza,



    "jamani nitawaambia tu,

    cha muhimu tuondoke eneo hili haraka iwezekanavyo" Kayoza

    akaongea kwa kuwasisitizia wenzake,



    "Ok, fasta basi" Omari

    akawaharakisha wenzake huku akionekana mwenye wasiwasi.



    Wakavaa haraka, na wakawa wanaelekea nje. Wakanyoosha moja kwa moja mpaka mapokezi,



    "Mbona Mpo peke yenu, wenzenu wako wapi?" Dada wa mapokezi aliwatania,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Bado wanajipodoa, si unajua tena mambo ya wanawake?" Omary alijibu huku akicheka,



    "Haya, nawasikiliza" Dada wa mapokezi aliongea,



    "Tumekuja kulipia chumba" Omary aliongea huku akimkabidhi pesa Mhudumu,



    "Sasa mbona ya chumba kimoja?" Dada wa mapokezi aliuliza baada ya kuzihesabu zile pesa,



    "Hicho kingine watalipia wadada" Denis alijibu,



    "Na wakikataa?" Dada wa mapokezi aliuliza ila kwa utani,



    "Wakikataa itabidi muwazuie na wawasaidie kufua mashuka" Omary nae alitania huku wakianza kuondoka na kumuacha yule dada wa mapokezi akicheka.



    Njiani kila mmoja

    alikua anafikiria lake,



    "Tunaenda wapi sasa?" Kayoza aliuliza huku akiwa hana muelekeo,



    "Itabidi turudi kwanza chuo" Denis alitoa jibu lililomfanya Kayoza asimame ghafla,



    "Hamuoni hatari iliyopo mbele yetu? Sasa tukirudi chuo si naweza kukamatwa?" Kayoza aliuliza huku akiwa bado amesimama,



    "Acha ujinga wewe, hakuna hata mmoja atayetuhisi sisi tunahusika na vifo vile" Denis alimwambia Kayoza,



    "Kwa hiyo?" Kayoza aliuliza,



    "Kwa hiyo turudi chuo, alafu tuangalie upepo unaendaje na tukiona mambo yanaweza kuharibika basi ndio tutaangalia namna ya kupambana" Denis alimueleza Kayoza,



    "Alafu hili suala ni letu sote, sio lako peke yako" Omary nae akaongezea maneno yalimpa nguvu kidogo Kayoza na kukubali kurudi kwanza chuo.



    Walienda mpaka jamatini ambapo ndipo zilikuwa coaster za kuwapeleka chuo, wakatafuta usafiri ambao ulikuwa upo tayari kuondoka na wakaingia, baada ya muda mchache gari iliondoka.



    Walipofika eneo la chuo wakaingia kwenye chumba chao, Denis na Omari wakaingia kuoga,

    Kayoza akajitupa kitandani ila sio kwamba alitaka kulala, hapana, mawazo ndio yaliutawala ubongo wake muda wote.



    Ilipofika mida ya saa 10 jioni, habari zikaenea

    chuo chote kuwa kuna wanafunzi

    wawili wa kike wamekutwa wamekufa

    Katika nyumba ya kulala wageni, kwa denis na Omari hiyo habari kwao

    haikuwa ngeni ila hofu waliyokuwa nayo mwanzo sasa iliwazidia kupita kiasi.



    Usiku wa siku hiyo, Kayoza hakulala kabisa kila dakika

    alikua anazunguka chumbani tu huku tukio la kumuua Tausi likimrudia kichwani mara kwa mara pamoja na sura ya Stellah, wakina Omary pia hawakulala ni

    kutokana na uoga, walikua

    wanaogopa kulala wakijua kuwa

    kayoza anaweza kuwaua pia.



    ********



    Kesho yake asubuhi wanafunzi

    wakatangaziwa waende wakaage miili

    ya wenzao, na utaratibu mzima

    utakuwa katika hospitali kuu ya mkoa

    wa dodoma inayoitwa jenero hospital(general).



    "Jamani mimi nitaenda kuaga pia, maana ni watu ninaowafahamu" Omary aliwaambia wenzake baada ya kupata ratiba kamili ya kuiaga miili ya Tausi na Stellah,



    "Kayoza na sisi itabidi tuende, haina haja ya kuogopa kitu ambacho hatujahisiwa nacho" Denis alimshawishi Kayoza,



    "Hapana, nyie nendeni tu, mimi siendi" Kayoza aliwaambia wenzake,



    "Ilo futa kichwani kwako, watu wote wanajua ulishawahi kuwa na uhusiano na Stellah, sasa usipoenda watu watakuchuliaje?" Denis alimwambia Kayoza,



    "Hivi nyie hamuoni hatari iliyo mbele yetu?" Kayoza aliuliza huku akisikitika,



    " hakuna hatari yoyote kwa sababu hakuna atayejua ni nani amewaua wakina Stellah" Denis alizidi kumueleza Kayoza,



    "Na pia usipoenda haitakuwa picha nzuri kwa watu wanakufahamu" Omary alichangia na mwisho Kayoza alikubali kuambatana na wenzie ifikapo saa kumi jioni.



    ___________________

    SAA KUMI JIONI

    ___________________.



    Wanafunzi wengi walijitokeza eneo la hospitali, pia Kayoza na

    wenzake walifika kuaga miili ya wenzao. Eneo lote lilitawaliwa na vilio vya wasichana wa chuo pamoja na walimu wao wachache walioguswa na vile vifo.



    * * * * * * * *



    Baada ya wahudumu kukaa mda mrefu bila

    kuona wakina stellah wakitoka, walipata wasiwasi kidogo na waliitana wenyewe kwa wenyewe na kuulizana bila kupata jibu la uhakika, na mwisho walipanga kwenda kuwaogongea, ila

    walitaka kutumia njia ya kutaka kufanya usafi ndio iwe kigezo, wakanteua mwenzao mmoja akawagongee mlango.



    Mhudumu alipofika mlangoni akagonga,

    hakusikia jibu, akagonga tena kwa nguvu kidogo pia hakusikia jibu,

    akarudi nyuma kidogo alafu akachungulia korido, hakuona mtu,

    akaenda upande wa vyoo na bafu pia

    hakuna mtu, akakata shauri ya kurudi kufungua mlango ambao ndani alikuwepo Stellah na Tausi, akanyonga

    kitasa akazama ndani, akakuta hamna mtu,



    "khaa! wametutapeli!" Mhudumu akashangaa moyoni mwake huku akiwa amejishika kiuno, wakati akiendelea kuwaza na kuwazua, mbele akaona suruali ya

    kike iko chini pamoja na pochi, ndio akapata faraja kidogo,



    "Hodi wadada" Mhudumu aligonga hodi ilihali ameshaingia ndani, lengo lake alitaka kujua wakina Stellah wapo upande gani, alijaribu kuita tena na tena bila mafanikio,



    "Ebu Ngoja niwaokotee pochi yao" Mhudumu aliongea huku akiinama chini kuokota pochi, wakati anaokota ndio

    akaona mkono wa mtu chini ya

    kitanda, akashtuka, akasimama

    akalinyanyua godoro kidogo, alichokiona kilipekea kupiga kelele

    hadi akapoteza fahamu.



    Alipopata fahamu alijikuta yupo hospital huku pembeni yake yuko polisi,



    "habari

    yako dada, unajisikiaje?" Polisi alimsalimia yule

    mhudumu,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "nzuri" Mhudumu akajibu huku akishangaa mazingira yaliyomzunguka,



    "unajisikiaje sasa, una nguvu

    kidogo?" Polisi aliendelea kuuliza.



    "najiskia vizuri" Mhudumu alijibu,



    Polisi akatoa simu akapiga, baada ya

    dakika mbili, akaja daktari na askari

    mwingne, daktari akamuuliza

    maswali mawili matatu mhudumu

    kuhusu hali yake, kisha akampima

    pima, alafu akamruhusu.



    Akapelekwa kituoni kwa ajili ya mahojiano. Pale kituoni walimkuta askari mmoja kijana mdogo mdogo, mweupe ila alikuwa amevaa nguo za kiraia, kilichomtambulisa kuwa ni Askari ni saluti kadhaa alizokuwa anapewa na askari wengine. huyu polisi kijana jina lake ni Joel Minja, ila jina ambalo hutumiwa na wengi kumuita ni Sajenti Minja.



    "Mkuu, binti mwenyewe ni huyu hapa" Askari aliyeongozana na Mhudumu wa bar alimuongelesha Sajenti Minja,



    "Oooh vizuri, mpeleke kule katika chumba cha mahojiano, mimi nakuja" Sajenti Minja aliongea huku akimuangalia yule Mhudumu, kisha akaelekea nje ambapo alienda mpaka katika moja iliyokuwa imeegeshwa hapo nje na kuchukua simu, kisha akaelekea katika chumba cha mahojiano na kumkuta yule dada Mhudumu akiwa amekaa anamsubili.



    "unaitwa nani mrembo?" sajenti joel Minja alimuuliza mhudumu.



    "Sania" Mhudumu ndivyo alivyojibu,



    "huna baba au ubini?

    Jitambulishe majina yako yote matatu" Sajenti Minja akatia msisitizo,



    "Sania Juma Baruti" Mhudumu akajibu,



    "unakumbuka tukio lililosababisha

    ukapelekwa hospitali?" Sajent Minja

    akauliza tena.



    Mhudumu akaelezea

    mwanzo hadi mwisho.



    "je unawakumbuka vijana waliongia

    na hao mabinti?" Sajenti Minja akauliza,



    "nikiwaona nitawajua" Mhudumu

    akajibu kwa ufasaha kabisa. Baada ya mahojiano yule Mhudumu alipelekwa selo kwa ajili ya usalama wake.



    Kesho yake mishale ya saa kumi jioni, Sajenti Minja akiwa na Askari wengine, wakamchukua Mhudumu na kwenda nae hospitali ili

    akahakishe kama wale maiti ni wateja aliowapokea au sio wao



    * * * * * * *



    Baada ya wakina Kayoza kutoka kuaga

    maiti, Omari akaaga anaenda msalani

    kukojoa na kuwaacha kayoza na Denis wakitangulia kutoka na kwenda nje ya eneo la hospitali.



    Omari alipotoka msalani akawa anaelekea nje kuwafuata wenzake, ndipo mbele yake akawaona Askari wapatao watano wakiwa wanaelekea upande aliopo huku wameongozana na msichana ambae hakuweza kumtambua kutokana na umbali ulikuwa kati yao, ila kadri walivyozidi kusogeleana ndipo sura ya yule msichana ilivyozidi kumjia, zilipofika hatua mbili kabla hawajapishana ndipo Omary alipopata mshtuko baada ya kugundua kuwa yule msichana ni Mhudumu wa ile bar ambayo Kayoza alifanya mauaji.



    Omary aliuficha mshtuko wake ila sasa yule Mhudumu akawa anamuangalia sana Omary, Omary akatamani hata apotee ghafla kama upepo ila ilishindikana na akaamua aendelee tú kwenda mbele kiume.



    Wale Askari na mhudumu walipomfikia Omary wakampita na kufanya Omary ashukuru Mungu baada ya kupishana nao.



    Yule Mhudumu alipompita Omary, alihisi hiyo sura siyo ngeni kwake, alitembea hatua mbili kisha akasimama, ikabidi Askari wote nao wasimame, kisha Mhudumu akageuka na kumtupia jicho Omary ambaye nae aliwageukia na sura yake ikaonekana vizuri na Mhudumu na kumfanya Mhudumu atoe mguno wa mshtuko..



    Omari akaona akijifanya kukimbia atakuwa amejikamatisha, akajifanya hana habari nao na kuendelea kutembea kuelekea nje, tena ukizingatia wale polisi walivaa kiraia basi hata wasiwasi kwa Omary haukuwa mkubwa.



    Mhudumu akiwa na

    hakika asilimia 95 kwa kile anachokiamini, aliendelea kumuangalia Omary aliyekuwa anatembea na kuzidi kuwaacha,



    "Wewe dada vipi?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuangalia Mhudumu,



    "yule ni mmoja kati ya

    watu waliongia guest kwetu na wale wasichana waliokufa" Mhudumu alijibu huku akimuelekezea kidole Omary, Polisi bila

    kupoteza muda wakamuita Omary aliyekuwa tayari yuko mbali nao, ila sijui ni kutokana na uoga au kujiamini, Omary alijikuta akirudi mpaka Pale alipo yule Dada Mhudumu na Askari,



    "mambo vipi kaka", sajenti minja

    akamsalimia omari,



    "poa", omari

    akajibu huku wasiwasi ukianza kuchukua nafasi,



    "sisi ni askari, je unamjua huyu

    binti?" Sajenti Minja alijitambulisha na kisha akauliza swali huku akinyooshea kidole

    mhudumu.



    kiukweli Omary alishtuka

    ila hakutaka kuunyesha mshtuko wake, ila tayari askari walishaligundua hilo kitambo.



    "simjui, kwani vipi?" Omary akajibu kwa pupa,



    "Dada unamjua huyu?" Sajenti Minja alimuuliza Dada Mhudumu huku akimuangalia Omary,



    "Ndiyo namjua" Dada Mhudumu alijibu na kumfanya Omary ahisi tumbo likimvuruga,



    "Unamjua kama nani?" Sajenti Minja alimuuliza tena,



    "Huyu ni mmoja kati ya wale vijana waliokodi chumba na wale wasichana wa chuo waliouwawa" Dada Mhudumu alijibu,



    "Wewe dada utakuwa sio mzima wewe" Omary alijikuta anaongea huku amemtolea macho yule dada Mhudumu,



    "mkamateni mumfunge pingu, atajieleza zaidi

    kituoni" Sajenti Minja akatoa amri.



    Omari ujanja mfukoni, akachukuliwa

    mpaka kwenye land cruiser ya polisi iliyokuwa imeegeshwa nje.



    Ile gari ya polisi ikatoka

    eneo la hospital kwa spidi ya ajabu utasema imempakia jambazi sugu.



    * * * * * * * *



    Baada ya shughuli ya kuaga miili kuisha, uongozi wa chuo

    ukatoa risala fupi kuhusu marehemu

    na shukrani kwa wanafunzi waliofika

    kuaga wenzao, pia uongozi wa chuo

    ukachukua mda huo kuwatangazia

    wanafunzi likizo ya mwisho wa

    semister.



    Kayoza na Denis baada ya

    kutawanyika eneo lile, wakaenda moja kwa moja nje

    ya hospitali.



    "mchizi kaenda kukojoa

    kamba nini? Mkojo gani nusu saa?" Denis aliuliza huku akiangalia saa yake ya mkononi,



    "simu yangu hainaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kitu, kama una salio muendee

    hewani" kayoza alimueleza mwenzake.



    Denis akachukua simu yake akapiga namba ya Omary, lakini

    simu iliita muda mrefu bila kupokelewa, akarudia tena na tena lakini hali ilikua ile ile.



    "mpotezee, si unajua leo siku ya kufunga shule,

    labda yuko na demu" Kayoza akasema.



    "poa, nini kinafuata sasa?" Denis akauliza,



    "twende chuo tukachukue mabegi, leo tulale mjini" Kayoza akatoa

    maoni yake,



    "haina mbaya, ni wazo zuri" Denis

    alijibu kwa kumuunga mkono mwenzake na kisha wakaenda kutafuta usafiri uliowafikisha chuo.



    Walipofika chuo baada ya

    kuoga na kujitayarisha kuondoka, Denis akarudia tena kupiga simu ya

    Omari, safari hii alipiga mara moja tu na simu ikapokolewa



    "wewe dogo vipi

    napiga simu muda mrefu haupokei, uko

    wapi?" Denis akaongea kwa pupa,



    "samahani mwenye simu yuko Polisi, hapa ni kituo kikuu cha Polisi dodoma

    mjini" upande wa pili ukajibu,



    "Polisi?, amefanya nini tena?" Denis

    akauliza,



    "wewe ni nani yake kwani?" ule upande wa pili badala ya kujibu, wakaongeza swali.



    Denis kichwa kikafanya kazi haraka, akahisi akijibu hovyo hovyo bila kufikiria, anaweza akajiingiza matatizoni,



    "mimi ni kaka yake" Denis alijibu,



    "Sawa, mdogo wako anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kuua wasichana wawili akishirikiana na wenzake ambao nao bado

    wanatafutwa" upande wa pili ukatoa

    maelezo,



    "Sawa, nipe dakika kumi nitakuja hapo" Denis

    akamalizia kisha akakata simu na kuanza kupumua kwa nguvu,



    "kaka kumeshaharibika, beba mabegi tuondoke" Denis alimwambia kayoza,

    "Sikuelewi, ebu nyoosha maelezo" Kayoza aliongea huku akimuangalia kwa makini Denis,



    "Omary amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za mauaji ya pale guest" Denis alimjibu Kayoza,



    "Mimi si niliwaambia hapa sio pa kukaa tena?" Kayoza aliuliza huku hiyo habari ikionekana kumgusa,



    "Hakuna muda wa kubishana hapa" Denis aliongea kwa ukali kisha wakabeba mabegi yao haraka, safari ya

    kwenda mjini ikaanza.



    * * * * *



    Omari baada ya kuchukuliwa na

    polisi, alifkishwa kituoni kwa ajili ya mahojiano hawali.



    "unaitwa Omary Said

    Mkwiju, si ndio hivyo?" Sajenti Minja alikuwa anamuuliza Omary huku

    kashuka kitambulisho cha Omary,



    "ndio" Omary akajibu.



    "sisi hatuna ubaya na wewe, ila ukweli wako ndiyo

    utaokusaidia" Sajenti Minja alianza kwa mtindo huo, kisha akaendelea,



    "mlikua watatu,

    wenzako wako wapi mlioshirikiana

    nao katika mauaji?"



    "jaman mimi sijaua,

    huyu dada kanifananisha" Omary alijitetea huku macho yakiwa makavu,



    "mchukueni mmuweke

    ndani, naona hayuko tayari kutoa ushirikiano" Sajenti Minja alitoa amri.



    Omary akabebwa juu juu akapelekwa

    Selo ingawa aliendelea kulalamika anaonewa kwani yeye hajui chochote kuhusu vifo vya hao wasichana.



    "Kwanini asipelekwe magereza kabisa" Askari mmoja aliuliza,



    "Muacheni huku kwanza, nitamrudia usiku" Sajenti Minja alijibu huku akichukua koti lake la suti alilokuwa amelitundika ukutani, na kisha aliondoka.



    Usiku Sajenti Minja alirudi

    tena, akaongea na askari wa zamu, kisha Omary akatolewa nje, akavuliwa

    nguo zote, kisha akaanza kuhojiwa tena, ila bado alikua mbishi,

    wakaitwa watu wanne waliokuwa wameshiba

    haswa, ni mijibaba ya miraba minne,

    wakaamrishwa wamchape.



    walimchapa haswa. Hadi akalainika, akawataja wenzake. Mda huo huo wa usiku Sajenti Minja akamfundisha

    Omari jinsi ya kuongea na simu, kisha akawapgia wakina wakina

    kayoza.



    "oya mko wapi wana?" Omary alianza kuongea

    hivyo,



    "vipi, wewe si uko polisi?" Kayoza

    aliuliza huku akishangaa mwenyewe,



    "ni habari ndefu ila

    wameniachia, wamedai

    wamenifananisha, wamenipa hela

    kwa ajili usumbufu" Omary alijibu huku akishusha pumzi ndefu,



    "ehe siku hizi polisi wanatoa hela!?, aya

    upo wapi?" Kayoza aliuliza,



    "Mi niko guest moja hivi karibu na Railway,

    nimeona giza limeshaingia nikaona bora nipumzike tu kwa maana polisi wamenisumbua sana. Nyie mko

    wapi?" Omari aliuliza,



    "tupe ramani tukufuate hapo ulipo kwa maana hata mabegi yako ya nguo tumekubebea" Kayoza alimwambia Omary,



    "Chukuenu bajaji, mwambieni awapeleke kilimani lodge, mtanikuta hapo" Omary aliongea huku Sajenti Minja akiwa pembeni akimfundisha maneno ya kuongea na kisha akakata simu.



    Baada ya mtego wa Sajenti Minja kukamilika na kufanikiwa kwa

    asilimia nyingi, akachukua taxi, kwa maana aliogopa kwenda na gari ya polisi kwa kuwa endapo wakina kayoza wataiona kipindi wamawasili, basi wanaweza kukimbia.



    Sajenti Minja alichukua taxi na askari watatu wenye bunduki, wakafunga safari hadi eneo walilopanga kukutana na wakina Kayoza, akachukua chumba,

    kisha wakamuingza omari na askari wote watatu wakaingia chumbani kwa ajili ya kuwakamata wakina Kayoza pindi watakapofika, kisha Sajenti Minja yeye alirudi

    nje kakaa ndani ya ile taxi na Dereva, huku akifuatilia kila kinachoendelea nje.



    Wakina kayoza walipofika Kilimani lodge, wakampigia simu Omary,



    "Tumefika, tupo nje hapa" Denis aliongea baada ya Omary kupokea simu,



    "njoon chumba namba

    7" Omary akawaambia wenzake ambao walimlipa dereva wa bajaji pesa waliyokubaliana nae, kisha wakabeba mabegi yao na kuelekea ndani.



    Sajenti Minja hakuwa na wasiwasi na vijana wake,

    aliona jinsi wakina KayozaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wanavyopiga simu na aliwasikia pia wanachoongea na Omary,

    ila hakua na pupa, aliamini wakina Kayoza wanaenda kukamatwa na vijana wake aliowaweka chumbani pamoja na Omary, kwa hiyo akaacha vijana wake wafanye kazi.



    Denis na Kayoza

    walipofika mlango namba 7, wakagonga mlango, na Omary akafungua,



    "Karibuni ndani, ingieni" Omary aliongea huku akiwa amechangamka na wakina Kayoza wakaingia ndani bila kujua katika hicho chumba walichoingia,wapo Askari watatu wenye bunduki wakiwasubiri wao.....



    wakakaribishwa na mdomo wa

    bunduki,



    "mko chini ya ulinzi" Polisi

    mwenye bunduki aliwaambia. Ghafla

    bin vuu, kayoza alimrukia yule askari

    mwenye bunduki, akatua shingoni

    mwake, ila hakumnyonya damu, badala yake yule Askari alipokea kofi zito na kuanguka chini huku bunduki yake ikidondokea chini ya kitanda.



    Yaani hapo Kayoza alikuwa tayari kishabadilika,

    macho yamekua meupe, meno yamechomoza.



    Askari wa pili kuona

    vile, nae akaokota bunduki,

    akamfyatulia Kayoza risasi, Kayoza

    akamuacha Askari wa kwanza, akamrukia wa

    pili nae akamtandika kofi lilimfanya apoteze fahamu, yule

    askari wa tatu kuona vile akakimbilia

    mlangoni, Omari akachukua bunduki,

    akampiga risasi ya mgongoni na akadondoka

    pale pale.



    Kayoza akiwa katika hali ile ile, akaenda dirishani akavunja nondo za madirisha, alikuwa na nguvu kama mnyama na alikuwa akiunguruma kama Simba.



    Alipomaliza kuvunja zile nondo za madirisha, akawarudia wale Askari ambao wawili walikuwa hawana fahamu na mmoja alikuwa anaugulia maumivu baada ya kupigwa risasi ya mgongoni.



    Akasukumia wale majeruhi chini ya

    kitanda kisha akawaangalia wenzake ambao walikuwa wamekaa kwenye kona moja Pale chumbani huku wakiwa na hofu kutokana na muonekano wa Kayoza, kwa maana hawajawahi kumuona hivyo kabla.



    Kayoza akarudisha macho dirishani na kisha akatokea dirishani, wenzake wakabaki wanaangalia,



    "Bab umeiona hiyo?" Omary alimuuliza Denis,



    "Ebu tutoke kwanza hapa, hayo tutayajadili baadae" Denis alijibu kwa upole,



    "Poa twende basi" Omary aliongea huku akianza kuondoka kuelekea mlangoni,



    "Usipitie uko wewe" Denis alimwambia mwenzie,



    "Sasa na sisi tupitie dirishani?" Omary aliuliza,



    "Hiyo ndio njia sahihi kwetu, maana nahisi Polisi wengine watakuwa nje" Denis aliongea,



    "Sio unahisi, ni kweli kuna Polisi nje" Omary aliongea baada ya kukumbuka kuwa Sajenti Minja alibaki nje. Wakatoka nje wote kwa kupitia dirishani huku wakibeba mabegi yao na begi la Kayoza.



    *********



    Nje, Sajenti Minja baada ya kusubiri muda mrefu

    bila majibu, akapata wasiwasi, mara

    akasikia mlio wa bunduki,

    akakurupuka kwa kasi hadi mlango mkuu wa kuingilia ile guest, alipata

    shida kuingia, kutokana na wingi wa

    wapangaji ambao walikua wanatoka

    huku wanakimbia baada ya wao kusikia pia mlio wa bunduki. Mara mlio

    mwingne wa bunduki ukasikika.

    Sajenti Minja akafanya juhudi binafsi, mpaka

    akafanikiwa kuingia, alipofika mlangoni, akausukuma mlango lakini

    haukufunguka, kipindi iko

    wahudumu walikuwa wanamuangalia

    tu,



    "nipeni ufunguo wa hapa" Sajenti Minja akawaambia wale wahudumu waliokuwa wanamtolea macho,



    "mwenye funguo

    kakimbilia nje" wahudumu wakamjibu,



    "Sawa, mimi navunja sasa" Sajenti Minja aliongea huku akionekana ana hasira,



    "huwez kuvunja bila meneja wetu

    kuwepo" Wahudumu wakamjibu.



    Mara kwenye mlango mkubwa wa kuingilia ile Guest wakaingia askari wanne, wote

    wamebeba bunduki, nyuma yao

    anaonekana askari mwingine mrefu,

    mweupe ana mwili wa mazoezi, huyu

    anaitwa Afande Juma Ally Mbago.



    "Sajenti Minja, umefika saa ngapi huku" Afande Mbago alimuuliza

    Minja aliyemkuta eneo hilo na kisha Sajenti Minja akampa mkasa

    mzima hadi yeye kuwepo pale.



    "kama wamesema ufunguo hawana vunjeni

    mlango" Afande Mbago aliwaamuru vijana wake.



    Vijana wakavunja

    mlango, walipoingia tu, wakakuta

    dirishani hakuna nondo,



    "bwana Minja si umesema, vijana wako

    walikuwepo humu pia?" Afande Mbago aliuliza,



    "ndio," Sajenti Minja

    akajibu,



    "sasa mbona hamna mtu

    humu?" Afande Mbago akauliza tena,



    "hata mimi nashangaa" Minja akajibu huku akishangaa.



    Askari mmoja akapanda kitandani ili aende

    karibu ya dirisha, alipofika mwisho

    wa kitanda, akaangalia chini

    akashtuka, tena alishtuka haswa,



    "kuna mtu chini ya

    kitanda" Askari akalopoka huku macho yakiangalia chini ilipokuwepo miili ya wale Askari waliopoteza fahamu. Wakavuta

    kitanda, wakakuta miili ya askari

    watatu ambao alikuja nao Sajenti

    Minja,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Wazima kweli hawa?" Sajenti Minja aliuliza huku hali ya hofu ikimuingia kuhusu watu anawafuatilia,



    "Wote wazima" Afande Mbago alijibu baada ya kuwakagua kisha wakawachukua na wakawapakia kwenye gari la

    Polisi, safari ya kuwapeleka hospitali

    ikaanza.



    ********* *******



    kayoza akiwa katika hali yake ya kutisha,

    aliendelea kukimbia,

    mbele kidogo akadondoka chini, akawa

    anajigeuza geuza kama mtu anayekata roho, mara akatulia kama mtu aliyekufa.



    Wenzake ambao ni Denis na Omary walikuwa pia wanakimbia huku wakiwa hawana uhakika wa kumpata mwenzao, ila wakiwa katika marathon hizo, ndipo walipomkuta Kayoza akiwa amelala chini.



    "Kafa au?" Omary alimuuliza mwenzake huku kila mmoja akiwa na uoga wa kumsogelea Kayoza kutokana na hali waliyoiona Pale lodge,



    "Sijui" Denis alijibu. Baada ya muda wa mrefu wa sintofahamu kati yao, mwisho walijitoa mhanga na kuusogelea mwili wa Kayoza na kugundua kuwa amepoteza fahamu, ila baada ya muda kidogo fahamu zilimrudia na akarudi kwenye

    hali yake ya kawaida, ila mwili wake haukuwa na nguvu.



    Wenzake wakambeba, ila bahati nzuri wakaona taxi inakuja, wakaisimamisha, kisha wote wakaingia ndani ya ile taxi.



    "tupeleke hospitali yoyote

    Iliyo karibu na hapa" Omary akamwambia dereva

    taxi,



    "hospital kufanya nini?, we mjinga nini" Denis akaongea kwa ukali,



    "polisi wamenitandika sana mgongoni, kwa hiyo nina vidonda vikubwa sana mgongoni" Omari

    alimwambia Denis huku

    akimuonesha hivyo vidonda,



    "poa, suka twende hospital" Denis

    akakubali baada ya kuviona hivyo vidonda.



    Walipofika hospitali, gari

    ikawa inaelekea sehemu ya maegesho, ilipofika ikasimama pembeni ya gari la polisi, wakati wanataka kushuka, Mara ghafla Sajenti Minja

    akawa anatoka ndani ya hospitali na

    kuelekea sehemu ya maegesho ya magari.



    Akaenda mpaka ilipopaki gari ya polisi,

    akawa anaongea na mwenzake

    kuhusu ishu iliyopelekea wale askari

    wenzake kuwa vile, na kibaya zaidi ni kwamba alimwambia mwenzake kuwa wale Askari wote wameshakufa, tena aliongea kwa hasira mpaka machozi yakawa yanamtoka.



    Ndani ya ile taxi, Omary alimjua fika sajenti minja,

    akawashtua wenzake, wote uoga

    ukawaingia, wakatega masikio ili wasikie maongezi ya Sajenti Minja na

    wenzake,



    "ngoja nikapumzike, maana

    nimechoka mno" Sajenti Minja alimwambia mwenzake,



    "taxi hiyo imeingia sasa hivi, ongea na dereva

    akupeleke" mwenzake alimjibu huku

    akinyooshea kidole gari waliomo ndani

    wakina kayoza,



    "poa basi, tutakutana kesho ili tujue ofisi itasema nini kuhusu hili tukio" Sajenti Minja aliongea Kisha

    akapeana mikono na mwenzake ikiwa ni ishara ya kuagana.



    Alafu akawa anaelekea kwenye gari ambalo ndani wapo wakina Kayoza....





    Sajenti Minja aliendelea kuisogelea ile taxi waliyokuwamo wakina kayoza,



    "Au mkuu..." Dereva wa kwenye ile gari ya Polisi aliita na kumfanya Sajenti Minja asimame,



    "Unasemaje tena Timo?" Sajenti Minja aliuliza huku akisimama,



    "Njoo nikukimbize mara moja, maana nahisi waliopo ndani hawatatoka sasa hivi" Dereva wa gari la polisi aliongea,



    "Ni jambo la kheri, ila wakitoka alafu wakakukosa?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Wewe twende tu, hata usijali" Dereva wa Gari ya polisi alijibu na kumfanya Sajenti Minja aache kuifuata gari waliyokuwepo wakina Kayoza na kurudi kuipanda gari ya Polisi, kisha ikaondoka.



    Wakina Omary walikuwa katika taxi walishuhudia kila hatua iliyokuwa inafanywa na Sajenti Minja, na kila mmoja tumbo lilikuwa na joto,



    "Umeshakuwa mkosi huu, hamna ya kushuka, bora tuondoke tu" Omary aliongea huku akitetemeka,



    "Na hivyo vidonda vyako vitapona vipi bila kutibiwa?" Denis alimuuliza Omary,



    "Tutajua mbele ya safari" Omary alijibu,



    "Usije ukaoza mgongo" Denis alimtahadharisha Omary,



    "Dereva ebu tupeleke Lodge yoyote iliyo karibu na Stendi ya mabasi ya mikoani" Kayoza aliongea baada ya ukimya wa muda mrefu na kuwafanya wenzie wamuangalie,



    "Vipi, unajisikiaje bab?" Omary alimuuliza kayoza huku akimshangaa,



    "Tutaenda kuulizana mbele ya safari" Kayoza alijibu huku akijishangaa alivyochafuka kama alilala kwenye vumbi.



    Dereva wa taxi aliindoa gari eneo la hospitali na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye eneo ambalo aliamini zinapatikana nyumba za wageni na pia ni jirani na stand ya mkoa wa Dodoma, na kuwashusha hapo,



    "Shilingi ngapi unatudai?" Omary alimuuliza Dereva baada ya kushusha mabegi yao,



    "Kwa mizunguko tuliyofanya, uwa nafanya shilingi elfu kumi na tano, kwa kuwa nyinyi Mi washkaji, nitawafanyia elfu kumi" Dereva taxi aliongea huku akitabasamu,



    "Punguza bwana, sisi tuna elfu saba" Omary aliongea kwa kulalamika,



    "Suka shika pesa yako" Kayoza aliongea huku akimpa noti ya shilingi elfu Dereva taxi,



    "Ungesubiri kwanza nimsaundishe" Omary aliongea huku akimlaumu Kayoza,



    "Hakuna kusaundishana hapa, unapoteza muda tu" Denis aliongea huku akibeba begi lake na kuingia ndani, Kayoza akamfatia.



    "Niachie namba yako, kesho asubuhi tunaweza kukupigia utufuate ili utupeleke stand" Omary alimwambia Dereva taxi,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Stand si hapo nyuma tu, mnaweza kwenda hata kwa mguu" Dereva taxi alimjibu Omary,



    "Wewe nipe tu hizo namba, unakuwa kama sio mfanyabiashara bwana" Omary aliongea na kumfanya Dereva taxi ampe namba zake za simu na kisha wakaagana.



    Omary akachukua begi lake na kuingia nalo ndani, kwa bahati nzuri aliwakuta wenzake wakimsubiri mapokezi,



    "Jamaa unatuyeyusha sana" Denis alimwambia Omary huku wakielekea sehemu vyumba vilipo,



    "Nawayeyusha na nini sasa?" Omary alihoji huku akiwafuata wenzake,



    "Sasa muda wote ulikuwa unaongea nini na Dereva?" Kayoza alimuuliza Omary,



    "Nilikuwa nachukua namba ya simu ya Dereva" Omary alimjibu kayoza,



    "Sasa namba ya simu ya nini wakati stand ipo karibu?" Denis aliuliza,



    "Hamuwezi jua, kama sio kesho anaweza kuwa msaada siku nyingine" Omary alijibu wakati Denis akiufungua mlango wa chumba walichotakiwa kulala,



    "Alafu huo ujinga wako uachage. Kwanza jana ilikuwaje mpaka ukakamatwa?" Denis aliuliza wakati akikaa kitandani,



    "Dah, ilikuwa kama movie yaani" Omary aliongea huku akicheka utadhani anasimulia jambo zuri,



    "Hivi utakua lini wewe?" Kayoza aliuliza kwa hasira,



    "Kwani nimefanyaje boy?" Omary aliuliza huku akimshangaa Kayoza,



    "Wewe si umeulizwa ilikuwaje ukakamatwa jana? Badala ya kujibu unaleta utoto" Kayoza aliongea huku akivua suruali,



    "Sasa si ndio nilikuwa naanza kujibu?" Omary aliongea,



    "Jibu sasa, acheni kulumbana" Denis aliongea huku akimuangalia Omary.



    Omary akaelezea mwanzo mpaka mwisho wa kukamatwa kwake na mpaka Mipango ilivyosukwa na Sajenti Minja ili kuwaingiza mtegoni Kayoza na Denis.



    "Sajenti Minja ndiyo nani?" Denis aliuliza,



    "Yule polisi aliyetaka kuja kwenye taxi tuliyokuwepo" Omary alimjibu Denis wakati huo Kayoza alikuwa ameingia bafuni kuoga,



    "Alafu tumuulize Kayoza ni kwa nini alikuwa katika umbo la kutisha namna ile kule lodge?" Omary alimshauri Denis,



    "Kweli aisee, ila tutaanzaje sasa? maana anaogopesha" Denis aliuliza kwa mashaka,



    "Hawezi kutufanya kitu bwana, kama angekuwa na lengo la kutudhuru, angetudhuru toka zamani" Omary aliongea kwa kujiamini,



    "Kama ni hivyo ni sawa, ila utamuuliza wewe" Denis alimwambia Omary,



    "Sawa, mimi nitamuuliza" Omary alijibu kisha nae akavua suruali kwa lengo la kwenda kuoga Kayoza akitoka bafuni.



    ********



    Baada ya saa moja, wote watatu walikuwa tayari wameshaoga na kila mmoja alikuwa akiwaza jambo lake,



    "Jamani eeh, wote tumebeba mabegi lakini hatujahambiana kila mmoja wapi anaelekea" Denis aliuliza baada ya ukimya wa muda mrefu,



    "Sasa si tulikuwa na matatizo, unadhani huo muda wa kuambiana ungepatikana vipi?" Kayoza nae aliuliza,



    "Mimi naenda Tanga, hadi hapo tayari nimeshawajibu" Omary alijibu huku macho yakiwa kwenye simu yake,



    "Tanga kufanya nini? Wewe kwenu si ni kondoa wewe?" Denis alimuuliza Omary huku akicheka,



    "Kule kuna babu yangu, sijamuona siku nyingi na inabidi nikamuone kwanza kama wiki mbili hivi" Omary aliwaelezea wenzake,



    "Na wewe Kayoza unaenda wapi?" Denis alimuuliza kayoza,



    "Mimi nitaenda Bukoba" Kayoza alijibu,



    "Mimi kama kawaida, Dar hiyo" Denis aliongea kwa furaha,



    "Nadhani tutaondoka pamoja ingawa tutapanda mabasi tofauti" Omary aliwaambia wenzake,



    "Wazo zuri sana hilo" Denis aliongea kukubaliana na Omary,



    "Ila ndugu yetu, ebu tueleze nini tatizo?" Omary alimuuliza Kayoza,



    "Tatizo lipi?" Kayoza nae akamuuliza Omary na kufanya washangaane,



    "Hujui au?" Omary aliuliza kwa upole,



    "Sio sijui, ebu liweke swali lako vizuri ili nijue nianzie kujibu wapi" Kayoza nae alijibu kwa upole,



    "Sawa. Ilikuwaje ukawaua wakina Stellah kule Guest?" Omary aliuliza huku akiwa na wasiwasi kidogo,



    "Dah, sijui nianzaje kujibu, ila kifupi Stellah naweza kusema sijamuua ila Tausi nilimuua bila kutegemea" Kayoza alijibu huku machozi yakimtoka kuonesha kujutia kile alichokifanya,



    "Sasa kama hukumuua Stellah ni nani alimuua wakati mlikuwa peke yenu chumbani?" Denis aliuliza,



    "Mimi sijui ndugu zangu, niliamka asubuhi nikamkuta katika hali ile na sijui nini kilitokea" Kayoza alijitetea,



    "Na Kwanini ulimuua Tausi?" Omary aliendelea kuuliza,



    "Tausi nilimuua bahati mbaya baada ya kumziba mdomo asipige kelele alipouona mwili wa stelah, Kumbe wakati namziba mdomo nilimziba na pua akajikuta anashindwa kupumua" Kayoza aliwaeleza wenzake,



    "Hiyo hali ya kubadilika na kuwa kiumbe cha kutisha inatokana na nini?" Denis alimuuliza Kayoza,



    "Mimi?" Kayoza aliuliza huku akijioneshea kidole,



    "Sasa kwani naongea na nani?" Denis nae aliuliza huku amemtolea macho Kayoza,



    "Mnanishangaza mjue, mimi sijaiona hiyo hali initokee" Kayoza alitoa jibu lililofanya wenzake waangaliane,



    "Tulivyoingia kwenye chumba alichoruelekeza Omary tumfuate, ulifanya nini?" Denis alimkumbusha Kayoza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Si tuliwakuta polisi watatu, alafu sikumbuki kitu zaidi ya kujikuta nimelala barabarani" Kayoza alitoa jibu jingine lililowashangaza wenzake,



    "Makubwa basi, Ngoja nilale mie" Omary aliongea kisha akajifunika shuka na kuwaacha wenzake wakiendelea kuongea.



    Saa kumi na moja alfajili waliamka na kuanza kujitayarisha kwa ajili ya safari.



    Ilipotimia saa kumi na mbili kila mtu alikuwa tayari na wakatoka mpaka mapokezi, wakakabidhi chumba na kuondoka kuelekea stand ya mabasi, walitembea kwa miguu tu kwa maana haikuwa mbali na lodge waliyoichukua.



    Walipofika karibu na Stand walishangaa kuona Askari wakiwa wengi, wamejitawanya eneo lile la Stand ya mabasi,



    "Nadhani wako Pale kwa ajili yetu" Kayoza aliongea huku akisimama na wenzake pia wakasimama,



    "Dah, kweli imeshakuwa tabu" Denis aliongea kwa kukata tamaa,



    "Tunafanyaje sasa?" kayoza aliuliza,



    "Turudi tukajipange" Denis alijibu,



    "Hapa hakuna kurudi, ngojeni kwanza" Omary aliongea huku akiitoa simu yake na kumpigia Dereva taxi,



    "Kwa hiyo akishakuja ndio tunafanyaje?" Kayoza aliuliza,



    "Anatupeleka mpaka nje ya mji, alafu uko mbele tutashuka kuyasubiri mabasi" Omary aliwaambia wenzake,



    "Hapo umefanya vizuri" Denis alimpingeza mwenzake kisha wakasubiri dakika kadhaa na taxi ikaja kuwachukua,



    "Mpaka nzuguni utadai shilingi ngapi?" Omary alimuuliza dereva taxi,



    "Elfu kumi na tano tu bosi wangu" Dereva taxi alijibu kwa unyenyekevu,



    "Twendeni wanangu" Omary akawaambia wenzake ambao waliingia ndani ya gari.



    Safari ikaanza, ubaya ilikuwa ni lazima upite karibu na Stand, wakati wanapita eneo hilo kulikuwa na gari ya polisi imeegeshwa pembeni huku likiwa na Askari wamekaa pembeni yake.



    Gari waliyopanda wakina kayoza ikasimamishwa na wale Askari,



    "Usisimame wewe" Omary alimsisitizia Dereva taxi ambaye alikuwa anataka kusimama,



    "Kwanini nisisimame? Au nyie waarifu?" Dereva taxi alijibu huku akisimama,



    "Acha upumbavu wewe" Denis aliyekaa kiti cha mbele aliongea huku akimsukumia Dereva nje na yeye akakaa kwenye kiti cha Dereva na kuiondoa gari kwa kasi.



    Polisi kuona hivyo nao wakawasha gari yao na kuanza kuifukuza ile gari waliyokuwemo wakina Kayoza.



    "Umefanya jambo la maana sana. Kumbe nawe ni jasiri hivyo?" Omary aliongea kumpongeza Denis kutokana na tukio alilolifanya,



    "Ilikuwa haina namna" Denis aliongea huku macho yakiwa mbele,



    "Lakini umeona wako nyuma wanatufuata?" Kayoza aliongea huku macho yake yakiwa nyuma,



    "Nimeshawaona, hapa tuombe tu gari iwe na mafuta ya kutosha, vinginevyo hawatupati" Denis aliongea huku akizidisha mwendo wa gari,



    "Kuwa makini lakini, usije ukatumwaga" Omary aliongea huku akitetemeka.



    Gari zilifukuzana kwa mwendo wa dakika thelathini mpaka kwenye barabara moja nyembamba iliyo juu juu na chini kulikuwa na mabonde.



    Kufika eneo lile, Denis akapunguza mwendo kwa kuwa barabara ni mbaya.



    Gari ya polisi ikaongeza mwendo na kuwafikia kisha ikaigonga kwa nyuma gari waliyokuwemo wakina Denis na ile gari ikapoteza muelekeo na kupinduka kuelekea kwenye korongo huku ikibiringita zaidi ya mara kumi na kusimama ikiwa haitamaniki kwa jinsi ilivyopondeka baada ya ile ajali.



    Gari ya polisi baada ya kuigonga gari waliyokuwamo wakina kayoza, nayo ilipoteza muelekeo na kuanza kubiringita kuelekea kwenye korongo na mwisho ikaenda kuokita ile gari waliyopanda wakina Denis na baada ya hapo ni damu tu zilitawala eneo lile..



    kilikua ni kishindo kikubwa sana,

    na kwa kuwa eneo lile kulikuwa na

    vimilima vidogo vidogo, zile gari

    zikaanza kujibiringisha kuelekea

    chini, zilijibingirisha kwa muda wa

    dakika mbili, ya kwanza kusimama

    ilikuwa ya polisi, alafu ya wakina

    denis ikaja kujiegemeza kwa

    pembeni yake, askari nane walikuwa

    wamepoteza maisha na wengine

    watatu walikuwa hawana fahamu.



    Upande wa gari waliyopanda wakina Kayoza. Denis ambae ndo alikaimu nafasi

    ya udereva alikufa pale pale, usukani

    ulimbana sehemu za kifua na

    kupelekea Denis kutokwa na damu

    puani, masikioni na mdomoni, Omari

    na Kayoza nao pia walipoteza

    fahamu, tena kayoza alitupwa umbali

    mrefu sana kutoka yale magari

    yaliposimama, eneo lote kulikuwa na

    harufu ya damu.



    Baada ya robo saa, katika gari ya Polisi alionekana

    askari mmoja akifumbua macho, ila

    alikuwa hana nguvu za kutosha,

    akajaribu kuinuka, ila akashindwa,

    akasubiri mda kama dakika kumi, ndio

    akapata nguvu kidogo za kujikongoja.



    Akafungua mlango wa land cruiser ya polisi kisha akatoka nje.



    Baada ya kutoka nje akaiangalia gari yao jinsi

    ilivyo, kiukweli hakuamini kama amepona.



    Akazunguka upande wa nyuma ya gari na kwa bahati nzuri gari yao ilikuwa imesimama, kwa hiyo aliweza kuwaona wenzie wakiwa wamelala kwenye bodi ila hawakuwa na fahamu.



    Akaanza Kutoa msaada.

    akawa anamtoa mtu mmoja mmoja,

    paka wakakamilika kumi na yeye wa

    kumi na moja, akaenda katika mlango wa pili wa pili wa gari kumtoa Askari aliyekuwepo kakaa kiti cha mbele ambaye alikuwa Sajenti Minja kisha akakitoa kidumu cha lita 5 ambacho kilikuwa na maji, akawa

    anawamwagia kidogo kidogo, ila ni

    wawili tu ndo walikua wamezinduka,

    kati yao alikuwepo Sajenti Minja,

    ambae alikuwa hana majeraha mengi

    sana usoni.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sajenti Minja alipopata

    nguvu, akaenda moja kwa moja hadi

    kwenye gari ambalo walikuwemo wakina Kayoza,



    "shit" Sajent Minja alisema maneno hayo

    baada ya kuhisi watuhumiwa wote

    wamekufa,



    Akawatoa ndani ya gari,

    akawalaza nje, lakini aliwakuta wawili tu, Omary na Denis ambaye alikuwa ameshakufa muda mrefu na Omary ambaye alikuwa hana fahamu.



    "hivi hapa ni wapi?,

    maana hata sioni dalili ya kuwepo

    mtu eneo hili?" Sajent Minja alihoji wenzake,



    "duh! Hata mi sipajui" mwenzake

    alijibu huku akitupa macho yake kule na huku.



    Baada ya muda kidogo. Omary alianza kuijgeuza geuza ikiwa ni ishara ya kurejewa na fahamu,



    "ah, ebu mmwagieni maji huyo" Sajenti Minja

    akatoa amri huku akimnyooshea kidole Omary.



    Wakammwagia Omary maji na akakurupuka huku akijishangaa huku akiwa na maswali mengi kichwani mwake, ila

    alionekana ana maumivu sehemu ya

    mguu wa kushoto, hasa kwenye goti,



    "nyie mbwa mmetusumbua sana, na

    hamna haki ya kuendelea kuishi"

    Sajenti Minja aliongea maneno hayo

    huku akichomoa bastola yake kutoka

    katika maeneo ya kiuno, kisha

    akaikoki, alafu mdomo wa bastola

    akauelekeza kwa

    omari.



    *****************



    Baada ya muda mrefu wa kulala, Kayoza akakurupuka, akawa anahisi

    maumivu eneo lote la kichwa,

    akajaribu kuvuta kumbukumbu,

    akakumbuka yote yaliyosababisha

    kuwepo pale.



    Ila alishangaa mbona haoni magari aliyopata nayo ajali na pia lile eneo alijikuta yupo peke na swali jingine akajiuliza wenzake wako wapi?



    Akajiinua na kuanza kuranda randa lile eneo, na mwisho akawa anasikia sauti za watu wakibishana kwa mbali sana.



    Akaamua aanze kuifuatilia zile sauti.



    Alitembea mwendo wa dakika tano, akaanza kuhisi arufu ya damu puani ni kutokana na damu zilizomwagika eneo la ajali zilikuwa zinatoa harufu.



    Akaanza kuhisi kizungu zungu na mwisho akaanguka chini na kuanza kugalagala huku mwili wake ukianza kubadilika taratibu na kuwa katika umbo la kutisha. Ilimchukua dakika chache za mabadiliko na alipokamilika, alisimama na kuanza kukimbia kuifuata harufu ya damu aliyokuwa anaisikia.



    Baada ya dakika kadhaa aliweza kuyaona yale magari waliyopata nayo ajali yakiwa yameegemeana. Pia aliweza kumuona Omary yuko mbele ya watu

    watatu ambao ni Askari, huku akinyooshewa bastola.



    Pembeni ya Omary kulikuwa na maiti

    ambae alikuwa katapakaa damu

    mwili mzima, huyu ndiye aliyemvutia zaidi Kayoza.



    Sajenti Minja akiwa na wenzake huku bastola yake akiielekeza kwa Omary, walisikia kichaka kikipiga kelele kama kuna mtu au mnyama ndani yake,



    "Mh..nini hicho?" Askari mmoja aliwauliza wenzake,



    "Simba nini?" Askari mwingine aliuliza baada ya ule mtikisiko kuwa mkubwa,



    "Simba hawezi kuishi katika kakichaka kama haka" Sajenti Minja alijibu huku macho yake pia yakiwa yanaangalia sehemu zinapotokea hizo kelele,



    "Usidharau mkuu, Simba anaishi mahali popote penye chakula" Askari mwingine aliongea.



    Wakiwa bado wako katika sintofahamu, Kayoza alichomoza kama mshale na akawa anaelekea eneo

    walilopo, wakina Sajenti Minja. Nao

    walimuona pia, mmoja akakimbilia

    ndani ya gari, akatoka na bunduki,



    "usimpige" Sajenti Minja,

    akamwambia yule askari mwenye

    bunduki.



    "sasa mkuu huoni anakuja

    upande wetu" Askari akajaribu kujitetea huku akiwa bado na bunduki yake mikononi



    "ngoja kwanza, labda hawezi kuwa na madhara" Sajenti

    Minja akajibu huku wote Wakiwa hawajui kile ni kiumbe cha aina gani?.



    Kayoza aliendelea kuwasogelea na alipofika

    pale, akaenda karibu ya Omary, akamuangalia kwa dakika kadhaa,

    Omary alikuwa anatetemeka mpaka

    mkojo ukamtoka.



    Kisha Kayoza

    akaikota maiti ya pembeni ya Omary, ambayo ilikuwa ni maiti ya Denis.



    Akailamba damu iliyopo katika ile

    maiti kisha akaitupa ile maiti.



    Kipindi chote hicho Askari walikuwa wanaangalia kinachoendelea.



    Kayoza akawaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    anaelekea upande waliopo wale

    Polisi, wale askari kuona vile, yule

    mwenye bunduki akampiga risasi Kayoza,

    Kayoza akasimama, kisha akaangalia

    eneo ambalo risasi ilipita, akaingiza

    kucha akaitoa, kisha kwa kasi ya hatari alikimbia kumuelekea yule Askari aliyempiga risasi na akamrukia, akatua shingoni akaanza kumfyonza damu,

    wale wengine kuona vile wakaanza

    kukimbia, ila walichelewa, mmoja

    alishikwa akapigwa kucha ya tumbo,

    kayoza alipovuta kucha zake, zikatoka

    na utumbo wote, mwingne

    akanyonywa damu kama mwenzake.



    Sajenti Minja

    akaona njia sahihi ya kujiokoa ni

    kuingia chini ya uvungu wa gari, akaingia,

    Kayoza hakumuona.



    kayoza alipomaliza kumnyonya yule askari,

    akamuona Omari kashika bastola

    anachungulia chini ya gari, Kayoza

    kama mshale, akalisogelea lile gari,

    kisha akalibeba juu, akalitupa

    umbali mrefu. Alikuwa na nguvu kwelikweli, kama mashine au mnyama mkubwa.



    Baada ya kurirusha gari, akawa anamsogelea

    Sajenti Minja aliyekuwa amelala chini huku akiwa amekata tamaa.



    Kayoza alipomfikia,

    akamkamata Majenti Minja mabega na kumnyanyua juu, Sajenti Minja akawa kama ametundikwa.



    Kayoza akamvuta karibu na kumkumbatia kisha akawa anaupeleka mdomo wake

    shingoni kwa Sajenti Minja kwa huku meno yakiwa tayari kumng'ata Sajenti Minja.



    Sajenti Minja akafumba macho huku akiwa tayari amekubaliana na matokeo..





    Kayoza akaingiza meno kwenye

    shingo ya Sajenti Minja na kuanza kumnyonya damu, ghafla

    akamuachia huku akiwa anamuangalia kwa

    mshangao.



    Kayoza akamuangalia

    Sajenti Minja kwa dakika kadhaa. Akamfuata tena na kumshika kichwani Sajenti Minja huku akimgeuza geuza kichwa kumuangalia kama mtu anayemjua, kisha akamuachia na kugeuka nyuma huku akianza kuondoka jirani na Sajenti Minja.



    Alipopiga hatua mbili tú ghafla akaanguka chini akapoteza

    fahamu.



    Sajenti Minja aliendelea kuganda tu,

    huku yanayomtokea akihisi labda

    huenda ni ndoto. Baada ya kumuona Kayoza ameanguka, sasa akawa kama

    kagutuka, akatoka mbio kuelekea

    eneo ambalo litakua ni salama kwake, na njia aliyokua anaelekea ni ile iliyokuwa inaelekea barabarani.



    Alikimbia huku kila dakika akigeuza

    shingo kuangalia kama Kayoza anamfuata

    kwa nyuma, huku jeraha lake la

    shingoni kalifunika na kiganja cha

    mkono.



    Alipowapoteza kabisa

    machoni kwake, akagutuka, kisha

    akaingiza mkono mfukoni, akatoa

    simu, akatafuta namba anayoijua

    yeye, alafu akapiga, akaonekana

    kukunja sura



    "hili eneo gani, hata

    network hakuna?" Sajenti Minja aliongea peke yake kisha akairudisha simu

    mfukoni, akakimbia kama dakika saba hivi,

    ndio akaiona barabara kwa mbali.



    Akajitahidi kuongeza mwendo hadi akaifikia.



    Alipifika alikuwa anahema haraka haraka huku kila muda akiangalia njia aliyotokea.



    Magari mawili ya mwanzo alipoyasimamisha

    yalimpita, ni kutokana na hali

    aliyokuwa nayo, vidonda, damu

    ilimtapakaa karibia eneo lote la

    mwili wake na pia eneo alilokuwepo lilikuwa linatisha na kingine cha ziada ni kwamba hakuvaa sare za polisi,



    "mh....hapa nisipotumia

    akili naweza kulala huku huku" Sajenti Minja alijisemea peke yake.



    Gari la tatu

    lilikuwa Toyota prado, na

    ayelikuwa anaendesha ni mwanamama na

    siti ya pembeni yake alikaa

    msichana ambaye nadhani alikuwa ni mwanaye.



    Sajent Minja akaichomoa

    bastola yake kiunoni, kisha akawa

    ameilenga ile gari na akitoa amri

    isimame, yule mama akaisimamisha

    huku akionekana ana hofu,



    "mnaelekea wapi?" Sajenti Minja

    akawauliza.



    "singida mwanangu"

    yule mama akajibu huku akitetemeka.



    Sajenti Minja akawaonyesha kitambulisho chake,

    ndipo hofu ikawatoka, kishaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akawaomba msaada, wakamkubalia,

    akajipakia katika gari na kisha wakaishia



    *****************



    Baada ya Sajenti Minja kuondoka eneo la tukio,

    ilichukua mda kama wa dakika tano

    kayoza kupata fahamu.



    Alishtuka akamkuta Omary yuko pembeni yake,



    "mapolisi wameenda wapi?" Kayoza ndio

    lilikuwa swali lake la kwanza kumuuliza

    Omary,



    "umewaua" Omary akajibu na kumfanya Kayoza ashangae,



    "Mimi nimewaua?" Kayaza aliuliza kwa mshangao,



    "Ndio, si hapo wamelala" Omary alijibu huku akiwaonyeshea kidole Askari waliikuwa wamekufa,



    "na Denis nae kaenda wapi?" Kayoza akauliza

    tena.

    Hapo wote wakashtuka,

    wakaenda kuingalia gari waliyokuwa

    nayo lakini hawajamkuta, ndipo Omary akakumbuka kuwa aliporejewa na fahamu pembeni yake kulikuwa na mtu, ndipo alipohisi huyo mtu atakuwa Denis.



    Wakarudi mpaka eneo la mwanzo, masikini ya mungu, walimkuta

    Denis Paul Simiwe, akiwa amelala

    huku damu zikiwa zimeganda kwenye

    pua na midomo yake.

    wote wakajikuta machozi yanawatililika mashavuni.



    "Tuondoke, hili eneo sio salama" Omary alimtahadhalisha Kayoza,



    Wakachukua kitambulisho cha Denis

    kama kumbukumbu ya jamaa yao,

    kisha wakabeba mabegi yao, wakawa

    wanaelekea barabani.



    walipofika barabarani

    walikaa kama nusu saa, wakaiona

    gari ndogo inakuja na aliyekuwa anaendesha ni mzee mmoja wa makamo.

    Omary alisimama katikati ya barabara na kuipungia

    mkono ile gari, ikasimama,



    "shikamoo mzee"

    wakamsalimia kwa pamoja,



    "marhaba waheshimiwa" Mzee makamo aliwaitikia.

    "mzee tunaomba

    Lifti" Omary akasema katika sauti

    tulivu,



    "mnaelekea wapi?" Mzee wa makamo akawauliza,



    "tulikuwa tunaenda

    tanga, ila hata ukitufukisha eneo

    lenye usafiri tutakushukuru" Omary akajibu,



    "vizuri, hata mi naelekea

    Tanga, mbona mko katika hali hiyo?"

    yule Mzee wa makamo akauliza baada ya kuwaona wana damu katika baadhi ya sehemu mwilini,



    "tumepata

    ajali"Omary akajibu huku akijifuta damu shavuni,



    "poleni sana,

    ingieni twendeni" Mzee

    akaongea.



    Wakaingia, safari ikawa

    inaendelea, mwendo kama wa nusu

    saa hivi, yule mzee kupitia kioo cha

    juu mbele, alishuudia kitu,

    kinachoendelea kwenye siti ya

    nyuma, ambayo walikaa wakina

    kayoza, akapata mshtuko,

    akapunguza mwendo wa gari, kisha akageuka ili kuhakikisha kama ni kweli au kioo kinamdanganya?..





    "mbona unalia kijana?" yule mzee alimuuliza

    kayoza,



    "ni maumivu tu, mzee

    wangu" Kayoza akadanganya huku akijifuta machozi, ila

    kilichokuwa kinamliza, ni mambo ya ajabu ambayo yanayomtokea, na kikubwa

    haswa ni kumpoteza rafiki yake,

    denis. Mzee akairudisha gari barabarani baada ya kuridhika na majibu ya Kayoza.



    Gari ikaenda hadi morogoro

    mjini, yule mzee akaipaki gari nje ya

    hoteli moja maarufu pale Morogoro.



    "twendeni tukale waheshimiwa" Yule mzee

    aliwaambia wakina Kayoza huku

    akiuchomoa ufunguo wa gari kutoka

    mahali pake, wakina kayoza

    wakashuka, huku kila mmoja akiwa

    kabeba suruali na fulana ili wakazivae mariwatoni, kwa hali

    waliyokuwa nayo, watu wengi

    waliwashangaa kutokana na nguo zao kuchanika na kuchafuka kutokana na ajali waliyoipata.



    Wakaingia hadi ndani, kisha Omary akaomba

    kuelekezwa choo kilipo,

    alipoonyeshwa, wakaenda kishaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wakabadili nguo, alafu wakarudi

    kujumuika na yule mzee pale

    mezani.



    Baada ya kumaliza kula,

    wakajipakia kwenye gari, kisha safari

    ikaendelea.



    "mnaenda Tanga katika

    eneo gani?" Mzee yule aliwauliza wakati

    gari ikianza kushika kasi.



    "Chumbageni" Omary akajibu huku safari ikiendelea.



    Tanga mjini waliingia saa nne usiku. Yule mzee

    akawashusha, wakamshukuru sana,

    kisha yule mzee akaendelea na safari

    zake, hakuna aliyejua yule mzee alikuwa

    anaelekea wapi?, ila walichoshukuru

    ni kufika salama.



    "kwa muda huu

    hatuwezi kupata usafiri, itabidi tutafute guest ya kulala, kesho

    tutaamka na hiyo safari yachumbageni" Omary alimwambia

    Kayoza hayo maneno,



    "mi nakusikiliza wewe" Kayoza ndivyo

    alivyomjibu. Wakatafuta nyumba ya wageni, wakaipata.



    wakaweka mizigo yao,

    kisha wakaenda kutafuta chakula, waliporudi wakalala.



    Waliamka saa

    nne za hasubui, wakaoga, kisha

    wakaenda kupata chai, alafu

    wakarudi kuchukua mabegi yao,

    safari ya kwenda Chumbageni

    ikaanza, wakaulizia sehemu

    yanapopaki magari ya Chumbageni,

    wakaonyeshwa, wakatafuta gari

    iliyokuwa karibu kuondoka,

    wakajipakia.



    **************



    Sajenti Minja alifikia moja kwa moja kituo

    kikuu cha polisi, akatoa ile taharifa

    ya mauaji, ikatayarishwa gari,

    ikambeba yeye pamoja na askari

    wengine watatu, wakaondoka, huku

    nyuma wakifuatiliwa kwa karibu na

    gari la wahandishi wa habari,

    wakaenda hadi eneo la tukio,

    likapigwa picha pamoja na maiti

    zote, kisha miili ya marehemu

    ikawekwa ndani ya gari, safari ya

    kurudishwa Dodoma mjini ikaanza,

    walipofika, maiti zote zikaenda

    kuifadhiwa katika monchwari ya

    hospitali ya mkoa, kisha polisi

    wakafanya kikao na waandishi wa

    habari, kuhusu ule mlolongo wa

    matukio ya kutisha, ila kwa bahati

    nzuri, Sajenti Minja alikuwa na

    kitambulisho cha Omari Said Mkwiji,

    kwa hiyo akawapa nafasi waandishi

    wa habari waipige picha, huku

    Sajenti Minja akiwaambia ile picha ni

    ya mmoja kati ya wale watuhumiwa

    watatu wa mauaji na akaongeza

    kuwa mtuhumiwa mwingine (Denis)

    amekufa katika ajali iliyotokea wakati

    wanakimbizana na polisi.



    Kesho yake asubuhi, magazeti yote yalitoka na

    habari hizo za mauaji, na pembeni

    ya hizo habari kulikuwa na picha

    kubwa ya Omari, akitajwa kama

    mmoja wa wahusika wa mauaji ya unyonyaji damu.



    *******************



    Wakina kayoza walipoingia ndani ya basi, walikaa

    siti ya nyuma kabisa, siti ya mbele

    yao walikaa wakina mama wawili

    ambao walikuwa wanazungumzia juu

    ya mauaji ya kutisha yaliyotokea kati

    ya Dodoma na Morogoro.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "na tena hadi picha ya muuaji imetolewa"

    mama mmoja wapo. ambae alikuwa

    kabeba mtoto katika miguu yake

    alikuwa akimsimulia mwenzie,



    "imetolewa na gazeti gani?" yule

    mama mwingine wa makamo

    akamuuliza yule mama mwenye

    mtoto.



    "magazeti yote unayoyajua

    wewe wametoa hiyo habari" mama

    mwenye mtoto akajibu.



    "chumbageni

    si hapo tu tunakaribia, nitanunua

    gazeti ili na mimi nione" yule mama wa makamo

    akajibu.



    Kipindi chote wakati

    wanaingia, hadi safari ilipoanza,

    wakina Omary walikuwa

    wanawasikiliza tu, ila habari

    iliyowashtua ni kuchapishwa kwa

    picha ya Omary kwenye magazeti.



    "Bab hii ishu imeshakuwa kubwa kupita kiasi" Kayoza alimwambia mwenzake wakati wale wakina mamá wanaongea,



    "Maji tumeshayavulia nguo, kuyaoga haina budi" Omary aliongea kwa sauti ndogo,



    "Maisha ya kukimbia kimbia tutaishi mpaka lini sasa?" Kayoza aliuliza kwa masikitiko,



    "Kila lenye mwanzo halikosi mwisho" Omary alijibu kifupi.



    Walipofika karibu na

    chumbageni, ile gari ikasimama kwa

    dharura, kulikuwa na mushkeli katika

    upande wa injini, wale wakina mama

    wakanunua gazeti, wakawa wanasoma

    ile habari



    "mimi nikimuona, yaani

    haraka nawajulisha polisi" yule

    mama mwenye mtoto aliongea.



    "hata mimi, mwenzangu milioni kumi

    nyingi" yule mama wa makamo

    akajibu baada ya kusoma habari

    kuwa atayemkamata au atakayefanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa atapewa kiasi

    hicho cha pesa, kipindi chote hicho wakina Kayoza walikaa tu kwenye siti za nyuma ya gari, hawakuthubutu kushuka.



    Gari lilipotengemaa likaendelea na

    safari. Kipindi chote Omari alikuwa

    kaielekeza sura yake sanjari na

    dirisha ili kukwepa sura yake isionekane na abiria wengine kwa maana alishapatwa na wasiwasi.



    Gari ikafika mwisho wa safari,

    watu wakaanza kutelemka, wale

    wakina mama kwa ajili ya kuwa na

    mtoto, ikabidi wasubiri ili watu wote watoke na wao watoke wa

    mwisho, sasa wakati wakina kayoza

    wanawapita, Omary akamkanyaga yule

    mama mwenye mtoto kwa bahati

    mbaya,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "samahani mama" Omary

    akamtaka radhi yule mama huku akimwangalia

    usoni, yule mama akapata mshtuko,



    "ah!, si ndo

    huyu?" Yule mama alisema kwa kupayuka.



    "sio mimi" Omary aliongea bila kutarajia huku akijinasua kutoka kwenye mkono wa yule mwanamke, kisha wakatoka haraka ndani

    ya ile gari na kukimbilia nje.



    Yule mama akachukua

    gazeti kutoka kwa mwenzake, kisha

    akaiangalia ile picha ya Omary iliyokuwepo katika gazeti



    "mh!, haswaa

    ndiye yeye" Yule mama akajisemea moyoni, kisha

    akatoka kwa lengo la kuwatazama

    walipoelekea wakina Omari, ila

    alichelewa, akakuta peupe.

    akaangaza tena, hakuona mtu,

    akaishia kusonya.



    Baada ya wakina

    kayoza kufanikiwa kushuka kwenye

    gari, wakakimbilia nyuma ya ile gari,

    wakawa wanamchunguza yule mama,

    paka alivyotoka ndani ya gari na kuanza kuangaza

    walikuwa wanamuangalia, mpaka ule

    msonyo uliotolewa na yule mama pia waliusikia, wakasubiri mpaka yule mama alipoondoka, nao

    ndio wakaondoka ila kwa kujificha ficha sana nyuma ya magari mengine yaliyokuwepo pale.



    "Yaani tayari habari zimeshasambazwa katika vyombo vya habari?" Omary alimuuliza mwenzake wakiwa tayari wameshatoka katika kituo cha mabasi,



    "Tena wamechelewa kweli, ilitakiwa watoe taharifa jana" Kayoza alijibu huku akikagua mandhari ya mji wa Tanga,



    "Ebu twende pale tukasome some magazeti" Omary aliongea huku akielekea sehemu ambapo kulikuwa na magazeti yametandazwa juu ya meza,



    "Acha ujinga wewe" Kayoza aliongea huku akiwa anamzuia Omary,



    "Kwanini?" Omary aliuliza huku akimshangaa Kayoza,



    "Unajua kuwa sisi tunatafutwa na mbaya zaidi picha yako ndiyo imeonekana kwenye magazeti, kwa hiyo wewe huoni kwenda eneo kama lile ni rahisi sana kukamatwa?" Kayoza aliuliza baada ya maelezo marefu,



    "Ila kweli, basi nenda wewe kaangalie, alafu uje unijulishe" Omary alimwambia Kayoza,



    "Mimi naenda, ila sio kuangalia. Naenda kununua gazeti tutaenda kusoma mbele Safari" Kayoza aliongea huku akielekea pale walipotandaza magazeti mezani. Alifika na kununua magazeti mawili ya kisiasa na jamii na kisha akarudi mahali Omary alipo na kumpa gazeti moja, nae akabaki na moja,



    "Alafu ujue umenishangaza sana" Omary alimwambia Kayoza,



    "Kwanini?" Kayoza aliuliza,



    "Kwanini yule Askari mweupe haujamuua?" Kayoza aliuliza huku akimaanisha Sajenti Minja,



    "Mimi?" kayoza aliuliza tena,



    "Ndio, ni wewe" Omary alikazia swali lake,



    "Sasa mimi nitajuaje wakati unajua kabisa mimi nikiwa katika hali ile uwa sijitambui?" Kayoza nae alijibu kwa mtindo wa kuuliza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Hicho kitu kimenishangaza sana" Omary aliongea huku akiendelea kushangaa,



    "Wewe mwenyewe uwa sikudhuru na Kwanini hushangai?" Kayoza alimuuliza Omary,



    "Dah, tuachane na hayo, maana tukiulizana sana hatutapata majibu ila tutaongeza maswali" Omary aliamua kupotezea huo mjadala,



    "Na mbona hawajaandika habari za Denis katika haya magazeti?" Kayoza alimuuliza Omary,



    "Hata mimi sijaelewa, au labda kuna sababu waliyofanya wafiche kifo chake?" Omary aliongea ila wote walilijadili jambo hilo huku wakiwa na huzuni,



    "Muda bado upo, Ngoja tusubiri habari za kesho, labda wanaweza kuja na habari zake" Kayoza aliongea na baada ya hapo ukimya ukafuata.



    *******************



    Sajenti Minja hakuwa na raha kabisa siku hiyo, maana ndani ya siku chache alishuhudia vifo vya ajabu sana na pia na yeye aliponea chupuchupu kufa na akaachwa na alama ya meno kwenye shingo,



    "Kiongozi bora uende hospitali ukaangaliwe kama ayo meno yanaweza kukuletea madhara" Askari mmoja alimshauri Sajenti Minja,



    "Nina mpango huo, ila mkuu amesema anataka kuongea na mimi muda huu, so nasubiri nimalize nae maongezi ndio niende hospitali" Sajenti Minja alimjibu yule Askari na muda huo huo kuna Askari mwingine akaja kumwambia Sajenti Minja kuwa anahitajika na mkuu.



    Sajenti Minja akanyanyuka na kwenda moja kwa moja ofisini kwa mkuu wake.



    "Poleni kwanza kwa matukio mabaya" Mkuu wa polisi aliongea baada ya salamu,



    "Tumeshapoa" Sajenti Minja alijibu kwa unyonge,



    "Nini maoni yako kuhusu hii kesi?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja,



    "Naomba mnitoe kwenye hii kesi, naona kama nimeishindwa" Sajenti Minja aliongea kwa heshima mbele ya mkuu wake,



    "Kwanini?" Mkuu aliuliza,



    "Nafikiri hiyo ndio njia pekee ya kuweka maisha yangu salama, maana wale tunaowafuatilia sio watu wa kawaida" Sajenti Minja alimueleza mkuu wake,



    "Wewe unadhani kufanya hivyo ni sahihi?" Mkuu aliuliza,



    "Nadhani inaweza kuwa sahihi" Sajenti Minja alijibu,



    "Sawa, nakupa muda wa kwenda kujiuliza tena kuhusu hili, alafu kesho uje tena kuzungumza kuhusu jambo hili hili" Mkuu aliongea na kumruhusu Sajenti Minja aondoke.



    Sajenti Minja akatoka na akili yake yote akaielekeza hospitali kwa nia ya kwenda kuangalia kama jeraha aliloachiwa na Kayoza lina madhara gani.



    ********?******



    Kayoza na Omary baada ya mwendo mrefu kutoka kituo cha mabasi, Wakatafuta

    baiskeli za kuwafikisha kijijini, bahati

    nzuri wakaipata. Walitumia muda wa

    dakika ishirini kufika kijiji husika,

    wakawalipa madereva ujira wao,

    kisha wakaanza kutembea kwa

    miguu, walitembea hadi wakafika

    sehemu moja, ambayo kulikuwa na

    kajumba kadogo kamejitenga kidogo

    na nyumba nyingine,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "sijui ndio hapa, ebu ngoja tujaribu" Omari

    aliongea bila ya uhakika,

    wakiisogelea ile nyumba, kisha wakagonga mlango,



    "karibu" sauti

    ikajibu kutoka ndani, wakasubiri

    mwenyeji hatoke, lakini hakuna

    aliyetoka, wakarudia tena kugonga



    "shabashi, pita ndani" ile sauti ikajibu kwa ghadhabu kidogo, Omari

    akausukuma mlango kisha akaingia,

    akamkuta mzee mmoja mfupi mweupe, kavaa baraghashia,



    "shikamoo babu" 0mari akamsalimia

    kwa furaha.



    "marhaba, karibu" yule

    mzee aliitikia huku sura yake

    ikionesha anajaribu kuvuta

    kumbukumbu fulani.



    "asante" 0mari

    akajibu huku akitambua alichokuwa

    anakifikiria babu yake,



    "Karibuni mkae" Yule mzee aliongea huku akiendelea kuvuta kumbukumbu,



    "babu mimi

    mjukuu wako 0mari" Omari akasema huku akitabasamu,



    "omari, omari, Omary wa wapi? " Babu aliuliza akiwa bado

    anafikiria huku akijaribu kuvuta

    kumbukumbu.



    "omari mkwiji mtoto wa mwanao wa Dodoma" Omari akamsaidia babu yake kumuelewesha.



    "ooh, karibu babu, vipi

    mbona umekuja bila taharifa" Babu

    akauliza huku akimpa mkono Omary na Kayoza.



    "ni matatizo babu,

    nitakusimulia tu babu" 0mari akamwambia babu yake huku akifurahi babu yake kumtambua,



    "Naona umekuja na mwenzako?" Babu akamuuliza Omary,



    "ndio babu" 0mari akajibu,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "karibu kijana" Babu akamwambia Kayoza huku

    akimpa mkono, ila kitu cha ajabu,

    babu aliung'ang'ania mkono wa

    kayoza kwa dakika mbili nzima huku akiwa amemkazia macho,



    "kijana una mzigo mzito sana wa matatizo" Babu alimwambia Kayoza huku machozi yakimtoka....



    ******ITAENDELEA*****

0 comments:

Post a Comment

Blog