Search This Blog

KIJIJINI KWA BIBI - 2

 







    Simulizi : Kijijini Kwa Bibi

    Sehemu Ya Pili (2)



    ILIPOISHIA..

    ______________



    "ooh, karibu babu, vipi

    mbona umekuja bila taharifa" Babu

    akauliza huku akimpa mkono Omary

    na Kayoza.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ni matatizo babu,

    nitakusimulia tu babu" 0mari akamwambia babu yake huku

    akifurahi babu yake kumtambua,



    "Naona umekuja na mwenzako?"

    Babu akamuuliza Omary,



    "ndio babu" 0mari akajibu,



    "karibu kijana" Babu akamwambia

    Kayoza huku

    akimpa mkono, ila kitu cha ajabu,

    babu aliung'ang'ania mkono wa

    kayoza kwa dakika mbili nzima huku

    akiwa amemkazia macho,



    "kijana una mzigo mzito sana wa matatizo" Babu alimwambia Kayoza

    huku machozi yakimtoka..



    _____________

    ENDELEA....

    _____________



    kayoza akashtuka,



    "hapana babu, mimi

    niko sawa tu" Kayoza akamjibu babu

    huku akijilazimisha kutabasamu,



    "kijana jaribu kuwa mkweli,

    vinginevyo utapata matatizo zaidi ya hayo

    yaliyokukuta" Babu akamsisitiza

    Kayoza,



    "babu tutakusimulia baadae" Omary akaingilia kati baada ya kuona Kayoza hawezi kukubali.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Babu yake na Omary

    anaitwa Mzee Salum Said Omari

    Shekindile Mkwiji, ila jina maarufu

    lililozoeleka kwa watu wa pale

    kijijini, wanamuita Mzee Mkwiji,

    huyu mzee katika maisha yake ya

    ujana alioa wanawake saba na

    kuwazalisha watoto zaidi ya hamsini,

    na ana wajukuu wasio na idadi, ila

    kitu ambacho kilichokuwa

    kinawachanganya watoto wake, ni

    kuwa huyu mzee hakuitaji kabisa

    msaada wao, wakimpelekea pesa,

    anawarudishia.



    Kuna kipindi watoto wake walijipanga

    wamjengee nyumba nzuri, akakataa,

    ila watoto wake hawakujua sababu

    ya yote hayo, ila sababu aliijua

    mwenyewe mzee Mkwiji, na sababu

    yenyewe ni kuwa na mizimu ya

    kiganga aliyorithishwa na baba yake,

    ambayo yenyewe inataka anayeimiliki

    awe anatoa tu misaada, na asiwe

    anapokea, anaishi peke yake, wake

    zake watano walishafariki, na wawili

    aliwapa talaka.



    Ni mganga

    anayependwa sana katika eneo

    analoishi.



    Baada ya kupata chai na

    mihogo, Omary na Kayoza walimsaidia

    kazi ndogo ndogo babu yao, baada

    ya shughuli za hapa na pale kuisha,

    wakatindika mkeka nyuma ya

    nyumba, wakaanza kumsimulia Mzee

    Mkwiji, kuanzia mwanzo hadi

    mwisho, Mzee Mkwiji aliwasikiliza

    kwa makini, kisha akaingia ndani

    kwake akatoka na kibuyu kidogo,

    alafu akamwambia Kayoza ateme

    mate chini, Kayoza akatema, Mzee

    Mkwiji akamimina dawa kidogo

    kutoka kwenye kibuyu alafu

    akaichanganya na mate ya kayoza,

    ukatokea moshi mweusi, ukawa

    unapanda juu kuelekea mashariki,



    "mh, kazi ipo" Mzee Mkwiji

    akajisemea huku akitingisha kichwa kwa masikitiko, kisha akarudia tena

    kufanya kama mwanzo, sasa hivi ule

    moshi ulipotoka, ukaingia puani kwa

    mzee Mkwiji, kisha akapiga chafya,

    akawa kama kasinzia, alikuwa katika

    hali hiyo kwa muda ya dakika tatu, kisha

    akafungua macho na kusema,



    "pole

    sana kijana, ningekusaidia ila

    mizimu yangu imeingiwa na uoga

    kupambana na mzimu ulionao" Mzee Mkwiji aliongea huku akimuangalia Kayoza kwa jicho la huruma,

    Kayoza akapoteza matumaini, ila

    babu akaendelea kumwambia,



    "mama yako ndio anaweza kuwa

    msaada mkubwa kwako" Mzee Mkwiji alitoa kauli ilijenga swali kwa Kayoza,



    "Samahani babu, umesema nina mzimu?" Kayoza aliuliza kanakwamba hakumsikia Mzee Mkwiji,



    "Tena wa hatari sana" Mzee Mkwiji alijibu,



    "Sasa unaposema mama yangu ndio anaeweza kuwa msaada kwangu hapo unanivuruga kidogo, kwa maana mama yangu sio mganga, kwa hiyo ni vipi atakuwa msaada kwangu?" Kayoza alimuuliza Mzee Mkwiji,



    "Kwa kweli hilo swali nitashindwa kukujibu, ila mizimu yangu ndio imeniambia hivyo" Mzee Mkwiji alijibu huku akimwaga yale maji yake aliyofanyia uganga,



    "Ila naweza kupona, si ndio?" Kayoza alimuuliza tena Mzee Mkwiji,



    "Kama mizimu imesema msaada upo, basi unaweza kupona" Mzee Mkwiji alitoa jibu lililompa matumaini Kayoza,



    "Sasa inabidi kesho tu nisafiri, niende kwa mama" Kayoza aliongea huku akimuangalia Omary,



    "Ungepumzika kwanza mjukuu wangu, yaani jana umekuja alafu uondoke kesho? Shinyanga ni mbali kutoka hapa" Mzee Mkwiji aliongea na kumfanya Kayoza ashtuke,



    "Umejuaje Nataka niende shinyanga?" Kayoza aliuliza huku akishangaa,



    "Si ndio mama yako yupo uko?" Mzee Mkwiji nae aliuliza badala ya kujibu,



    "Ndio, sasa umejuaje yupo uko?" Kayoza aliuliza tena huku akistahajabu maono ya Mzee Mkwiji,



    "Sina uganga wa kubahatisha, mizimu yangu uwa inaniambia ukweli" Mzee Mkwiji alijibu huku akitabasamu,



    "Aisee wewe mzee ni kiboko" Omary aliongea huku akicheka,



    "Kama nilivyosema hawali, kesho naondoka" Kayoza alirudia Kutoa taharifa,



    "Itabidi twende wote" Omary aliongea,



    "Wewe baki tu ndugu yangu, msaada ulionipa ni mkubwa sana. Nakushukuru sana" Kayoza alimwambia Omary,



    "Hapana siwezi kubaki, kama kutafutwa ni mimi ninayetafutwa kwa maana picha yangu ndio ipo katika vyombo vya habari, kwa hiyo ni bora niwe na wewe popote niendapo kwa maana wewe pekee ndiye unaweza kuniokoa mikononi kwa polisi" Omary aliongea kwa huzuni,



    "Omary unafuata kifo uko" Mzee Mkwiji alimwambia mjukuu wake,



    "Kivipi babu?" Omary aliuliza,



    "Mnapoenda mtapata utatuzi wa tatizo lenu, ila kurudi salama ni kazi sana" Mzee Mkwiji aliwaambia na kufanya vijana waogope,



    "Kwa hiyo tukienda uko shinyanga tunakufa?" Omary aliuliza kwa taharuki,



    "Shinyanga hamtokufa, ila kazi isipofanikiwa shinyanga, basi mtakuwa na safari nyingine itakayoambatana na kifo" Mzee Mkwiji alizidi Kutoa taharifa mbaya kwa vijana,



    "Kwa hiyo tusiende au?" Kayoza aliuliza,



    "Usipoenda itakuwa umeridhika na Maisha ya kuua, cha muhimu ni uende, ila kuweni makini na maamuzi yenu uko muendako" Mzee Mkwiji aliongea huku akijinyanyua mkekani,



    "Mbona umakini tunao tu babu" Kayoza alijibu wakati babu akiingia ndani,



    "Pamoja na umakini wako, kifo chako kitakuwa cha kujiua mwenyewe" Babu aliongea kwa utani huku akipotelea ndani,



    "Babu mzinguaji kweli, kaongea vya maana wee, ameona amalizie na utani" Kayoza aliongea huku akicheka,



    "Ndivyo alivyo huyo, akiona maswali yanakuwa mengi uwa anayapotezea kwa utani" Omary aliongea huku wakikunja mkeka kwa lengo la kuingia ndani.



    **********



    Sajenti Minja alienda hospitali na kufanyiwa vipimo katika jeraha lake na hakukutwa na tatizo lolote,



    "Daktari rudia kunipima, haiwezekani nikutwe sina kitu" Sajenti Minja aliongea na pia akishangaa majibu ya vipimo,



    "Ridhika na majibu, au kama hutuamini nenda kajaribu kucheki kwenye hospitali nyingine, labda jibu linaweza kuwa tofauti" Daktari alimjibu kistaharabu Sajenti Minja,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sio kama nadharau huduma zenu, kinachotisha ni kiumbe kilichoniachia hizo alama, kiko kama zombi, nahisi na mimi naweza kubadilika na kuwa kama hicho kiumbe" Sajenti Minja aliongea kwa upole huku akishika eneo la jeraha lililokuwa na bandeji,



    "Acha kuamini movie au masimulizi ya kizombi, zile uwa ni habari tu za kusadikika zisizo na ukweli wowote" Daktari alijibu huku akicheka,



    "Hayajakukuta wewe na ndio maana unasema hivyo" Sajenti Minja aliongea huku akinyanyuka katika kiti,



    "Usiondoke, bado hatujamaliza" Daktari alitoa kauli iliyomrudisha Minja kwenye kiti,



    "Bado nini?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Kuna dawa unatakiwa ukanunue kwa ajili ya kukausha jeraha lako" Daktari aliongea huku akimpatia Sajenti Minja kikaratasi chenye maandishi yaliyoandikwa kwa mkono, Sajenti Minja akapokea na kuondoka.



    ***************



    Baada ya Kayoza na Omary kumaliza mambo yao madogo madogo, ilipofika jioni Kayoza akachukua

    simu ya Omari akampigia mama yake,

    baada ya salamu,



    "mama keshokutwa

    nitakuja huko" Kayoza akamwambia

    mama yake.



    "chuo mmeshafunga?"

    mama yake akauliza.



    "Sio mda mrefu

    sana toka tufunge, mama" kayoza akamjibu,



    "uko wapi, au kwa shangazi yako?" mama yake akamuuliza.



    "nipo Tanga kwa rafiki yangu" Kayoza

    akajibu.



    "Kuna nini uko Tanga, au matembezi tu?" Mama Kayoza aliuliza,



    "Ni safari tu ya bahati mbaya mama" Kayoza alijibu,



    "Kwanini iwe ya bahati mbaya?" Mama Kayoza akauliza kwa shahuku,



    "Ngoja nije, tutaongea vizuri mama" Kayoza alimwambia mama yake,



    "Lakini wema upo au?" Mama Kayoza alimuuliza mwanaye,



    "Nikija tutaongea mama" Kayoza alijibu,



    "Sasa si inabidi kwanza nijue kama kuna wema au lah?" Mama Kayoza alitilia mkazo msimamo wake,



    "Wema upo" Kayoza alijibu ili kumridhisha mama yake, kwa maana anamjua jinsi alivyo na maswali mengi,



    "haya, karibu mwanangu"

    Mama yake akamwambia, kayoza akaitikia kisha akakata simu.



    ********



    Hiyo siku ya Safari ilipofika ikabidi waondoke

    pamoja na Omari kama walivyokubaliana. Mzee Mkwiji akawafanyia tambiko dogo kwa ajili ya usalama wao, kisha

    wakaagana nae kwa ahadi ya kurudi

    tena baada ya kutoka uko waendako.



    Wakaenda mpaka mjini, wakaingia

    kwenye mashine ya kutolea pesa (ATM), wakachukua

    pesa ya kuwatosha wao, wakatafuta

    mabasi ya Shinyanga wakapanda, safari ya kuelekea shinyanga ikaanza..

    ...Muda wote safarini Omari

    aliutumia kujificha na gazeti ambalo

    alikuwa analisoma, na hata

    aliposinzia, alilitumia gazeti hilo

    kujifunika nalo usoni.



    Shinyanga

    mjini waliingia saa tano usiku,

    walipokelewa na mama yake Kayoza,

    ila aliwashangaa kwa jinsi

    walivyokuwa na majeraha,

    "vipi jamani, mbona mna mavidonda hivyo

    usoni" mama yake Kayoza akauliza.



    "tulipata ajali mama" Kayoza akajibu

    kwa kudeka.



    "na hii gari, au?" mama

    Kayoza akaongeza swali lingine huku kidole chake akikielekeza katika basi walilokuja nalo wakina Kayoza.



    "sio hili mama, wakati tunaenda Tanga

    ndio tulipata ajali" Kayoza akajibu.



    "aah, haya twendeni wanangu"

    mama kayoza akaridhika na majibu

    ya mwanae.



    Wakabeba mizigo yao,

    wakaenda kwa dada yake mama

    Kayoza kwa kuwa nyumbani kwa mama Kayoza kulikuwa nje ya mji, iliwabidi walale hapo mpaka siku inayofuata ndio waende kwa Mama Kayoza.



    **********



    Sajenti Minja alishaanza kuiogopa ile kesi, maana tayari alishaona ile kesi ina mambo kama ya kishirikina na ukingatia si polisi wala serikali inayoamini kitu hicho, na swali alilojiuliza ni kwamba, akisema ahache kaifuatilia hiyo kesi, je kwenye ripoti yake ataandika sababu gani iloyopelekea kuacha hiyo kesi?



    Kipindi anawaza hayo yote, alikuwa ndani ya gari akirejea ofisini kwao ili akamshawishi tena mkuu wake ili aone kama atamuelewa katika jambo hilo la kuacha kwake kazi.



    Alifika na kumkuta mkuu wake akitoka,



    "Nina maongezi na wewe mkuu" Sajenti Minja aliongea kikakamavu huku amepiga saluti,



    "Ingia kwenye gari twende" Mkuu wake alijibu na Sajenti Minja hakutaka kuuliza wanaenda wapi, cha muhimu alichokiona ni kuongea na mkuu wake tu.



    "Nini tatizo?" Mkuu wake alimuuliza wakati akiiondoa gari,



    "Kama nilivyokwambia hawali, naomba hii kesi muiamishie kwa mtu mwingine" Sajenti Minja aliongea,



    "Sababu ni ipi?" Mkuu wake aliuliza,



    "Sababu ni ile ile, nahisi yule sio kiumbe wa kawaida" Sajenti Minja alijibu,



    "Je nikikuambia uniletee barua ya kutaka kuacha hii kesi utaandika sababu ni ipi?" Mkuu wake alimuuliza,



    "Hicho ndicho kinachonitatiza" Sajenti Minja alijibu,



    "Basi nenda katafute jibu, na ukilipata uje na barua yenye maombi yako" Mkuu wake alimwambia wakati akiliegesha gari nje ya mgahawa,



    "Dah, mbona ni mtihani" Sajenti Minja aliongea,



    "Huo sio mtihani, mtihani ni kushindwa kujielewa wewe kama askari una jukumu gani katika taifa?" Mkuu aliongea huku akiwa ndani ya gari,



    "Unamaanisha nini?" Sajenti Minja aliuliza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kama unashindwa kuelewa hata nilichomaanisha, basi napata wasiwasi kuhusu hata uwanajeshi wako" Mkuu aliongea huku akitelemka katika gari, Sajenti Minja nae akafuata huku akihisi kudharauliwa kwa ile kauli ya mkuu wa Polisi,



    "Lakini mkuu hiyo kauli inahusiana vipi na maongezi yetu?" Sajenti Minja aliuliza kwa upole,



    "Nadhani haihusiani, kwa maana uwanajeshi na akili ni vitu tofauti" Mkuu alijibu kwa kejeli huku akikaa juu ya kiti, na Sajenti Minja nae akakaa,



    "Tuachane na hayo mkuu, naomba tu unisaidie kunivua ile kesi" Sajenti Minja aliamua kupuuza kauli za mkuu,



    "Numeshakwambia nenda kaandike barua na ulete ofisini kwangu, ila iwe na sababu tofauti na hiyo" Mkuu aliongea kisha akaagiza chakula,



    "Na wewe kaka nikuletee chakula gani?" Mhudumu wa mgahawa alimuuliza Sajenti Minja aliyekuwa na mawazo,



    "Naomba wali, wali nyama. Atalipa bosi hapa" Sajenti Minja aliongea huku akimaanisha kuwa atakayemlipia chakula ni mkuu wa polisi,



    "Mimi na wewe biashara imekwisha, nyanyuka uondoke" Mkuu aliongea kwa amri na kwa kuwa uaskari ni utiifu, Sajenti Minja aliinuka kwa unyonge na kutoka zake nje ya mgahawa.



    *************



    kesho yake hasubui

    wakapanda gari ambayo iliwapeleka

    katika kijiji anachokaa Mama yake

    kayoza, iliwachukua mwendo wa nusu saa na daladala kufika mpaka eneo ambalo alikuwa anaishi Mama Kayoza, wakatelemka na kisha wakatembea mwendo wa dakika kumi mpaka kuifikia nyumba ya mama Kayoza.



    "karibuni, hapa ndio

    nyumbani" Mama Kayoza aliongea huku akifungua mlango,



    "asante mama" wakajibu

    kwa pamoja.



    Wakavua viatu, kisha

    wakapita ndani,



    "ehe, za chuo

    mwanangu" Mama Kayoza alimuuliza mwanae baada ya kukaa,



    "Za uko ni nzuri, sijui za hapa" Kayoza akajibu,



    " na huyu ni nani?",

    Mama kayoza akamuuliza mwanae

    huku akimwangalia Omari.



    "huyu ni ndugu yangu mama" Kayoza akajibu

    kwa kifupi.



    "ndugu yako?, mtoto wa

    shangazi zako au?" Mama kayoza

    akauliza tena.



    "ni rafiki yangu, ila

    kwa matatizo yalinitokea, alisimama kama ndugu yangu" Kayoza akamjibu

    mama yake.



    "Matatizo? matatizo gani

    yaliyokukuta uko dodoma?" Mama

    kayoza akamtupia swali jingine

    mwanae.



    "ni makubwa mama, na

    huyu mwenzangu hadi polisi aliwekwa kwa ajili yangu" Kayoza

    akamrejeshea jibu mama yake, huku

    akijilaza juu ya kochi la sofa ambalo

    awali alikuwa kalikalia.



    "sasa si ungenitahafifu nimwambie mjomba

    ako yuko pale ni polisi pia" Mama

    kayoza akaongea huku sura yake

    ikiwa na huzuni.



    "mama bwana, sasa

    we si ungenitaharifu kwanza kwamba

    una ndugu dodoma" Kayoza alisema

    maneno hayo kwa kudeka mbele ya mama yake.



    "mimi nina mambo

    mengi mwanangu" Mama kayoza akajitetea.



    "ulisema ni polisi eeh?,

    anaitwa nani?" kayoza akamuuliza

    mama yake.



    "ndio ni polisi, tena ana

    cheo cheo, anaitwa Joel Minja, ila wenzake wamezoea kumuita sajenti Minja" Mama kayoza akajibu.



    "mh, Sajenti Minja!!!!?" Omari akajikuta

    anauliza bila kutarajia...





    "ndio mwanangu, kwani

    unamjua?", Mama Kayoza akamuuliza

    Omary.



    "ndio mama, namfahamu"

    Omary akajibu.



    "si unaona mwenzio

    anamjua, ni mtu maarufu pale Dodoma" Mama Kayoza akasema

    huku akimuangalia Kayoza.



    "kaka umemjuaje hadi mimi nisimjue?"

    Kayoza akamuuliza Omary.



    "huyo jamaa ndio anaeshikilia kesi yetu"

    Omary akajibu.



    "ni yule jamaa white

    tuliyekutana nae siku zile

    hospitali?", kayoza akamuuliza

    Omary.



    "eeeh, ndio yule yule, na

    tena siku ile ya ajali ulitaka kumnyonya damu, ila ulimuacha",

    Omary akajibu.



    "eh, ulitaka kumnyonya damu?", Mama kayoza

    akaingilia kwa swali.



    "ndio mama, hayo ndio

    matatizo ambayo yananiandama

    mama, na sasa tunavyoongea,

    tunatafutwa nchi nzima na polisi kwa

    kosa la kunyonya watu damu na

    mauaji ya polisi" Kayoza akamjibu

    mama yake huku akiwa katika sura ya

    huzuni.



    "ina maana bado hayajaisha

    tu?" Mama kayoza akauliza huku

    akionekana ana mawazo.



    "hayajaisha?, kumbe mama unajua

    matatizo yangu?" Kayoza akamuuliza

    mama yake huku akimshangaa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ni hadithi ndefu

    mwanangu", mama kayoza akajibu.



    "nisimulie hata kwa kifupi" kayoza

    akamchachamalia mama yake amsimulie.



    "nitawahadithia baadae,

    ngojeni kwanza nikapike chakula cha

    mchana, maana nikisema tuongee tu,

    tutashinda na njaa

    hapa" Mama Kayoza alijibu kisha akanyanyuka na kuelekea jikoni huku akionekana ni mtu mwenye mawazo mengi sana.



    **************



    Sajenti Minja alikuwa na dhamira ya kuacha kazi, tena alipania haswa kuacha kazi. Aliona bora mjinga alie hai, kuliko kujifanya shujaa alafu mwishowe ufe.



    Alipotoka katika mgahawa ambao alikuwa na mkuu wa Polisi, alielekea moja kwa moja kwa secretary wa ofisi ya polisi kwa nia ya kwenda kuchukua ujuzi wa namna ya kuandika barua ya kuacha kazi kabisa. Aliona bora ahache kwa maana akisema aombe aondolewe katika ile kesi ni lazima angekataliwa kwa kuwa hakuwa na sababu za kutosha.



    Aliingia pale kwa secretary huku akiwa na mawazo mengi sana,



    "Naweza kupata nakala moja ya barua iliyoandikwa mtu aliyeomba kuacha kazi?" Sajenti Minja aliuliza baada ya salamu,



    "Zipo nyingi tu, hata ukitaka kumi utapata" Dada aliyepo alimjibu kwa utani lakini Sajenti Minja hakuonekana kuwa katika sura ya utani, badala yake alikuwa mnyonge sana kiasi kwamba yule dada akamshangaa kwa maana Sajenti Minja anajulikana sana pale ofisini kwa kupenda utani,



    "Naomba moja tu, tena iliyoandikwa na mfanyakazi aliyeacha kazi muda mfupi baada ya kuanza" Sajenti Minja aliongea huku akiangalia chini,



    "Mh...wewe unaitaka ya nini?" Dada alimuuliza huku akitilia shaka hali aliyokuwa nayo Sajenti Minja,



    "Kuliko kuendelea na hii kesi, nimeona bora niache kazi" Sajenti Minja alitoa kauli iliyomshangaza yule Dada,



    "Kwanini usingeandika barua ya kuomba hiyo kesi apewe mtu mwingine?" Dada aliuliza,



    "Nikiulizwa sababu nitajibu nini?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Dah, kweli mtihani" Dada alijibu baada ya kufikiria kwa muda mfupi,



    "Sasa kama wewe uliye mzoefu na kazi hii unaona huo ni mtihani, je mimi ambaye sina uzoefu wa kutosha?" Sajenti Minja aliuliza huku akiamini hawezi kujibiwa,



    "Ila hiyo sio sababu ya kuacha kazi, wewe si umeanza kazi juzi tu? Ungeizungusha hii kesi muda mrefu bila mafanikio yoyote ni lazima angepewa mtu mwingine" Dada alijaribu kumshawishi Sajenti Minja,



    "Mafunzo niliyopitia mimi sio uliyopitia wewe, mafunzo niliyopitia mimi yananifundisha kusimamia Ukweli" Sajenti Minja aliongea,



    "Hakuna mafunzo ya uaskari yanayofundisha kusema uongo, ila mimi nimeona bora utumie hiyo njia kuliko kuacha kazi" Dada aliongea kwa huruma ili kumshawishi Sajenti Minja akubaliane nae,



    "Naomba nipatie hiyo nakala ya barua, nitaenda kufikiria mbele ya safari" Sajenti Minja aliongea kuonesha amedhamiria kutekeleza hadhma yake,



    "Sawa bwana" Dada aliongea kisha akamtafutia hiyo nakala na kumpatia, Sajenti Minja akapokea na kuondoka.



    ***************



    Mama kayoza

    ni jina lake la ukubwani tu, jina

    alilozaliwa nalo ni Aika John Minja,

    ni mtoto wa tatu kutoka familia ya

    watoto wanne, na ni mtoto wa kike

    pekee katika familia yao, kaka zake

    wawili ni wafanya biashara wakubwa

    kiasi katika jiji la Arusha, na mdogo

    wake ni afisa wa polisi, anaitwa Joel

    John Minja.



    Mama Kayoza alipokuwa na umri wa

    miaka kumi na saba, alijiingiza katika masuala ya mahusiano ya

    mapenzi, ila aliambulia kupata ujauzito na kukataliwa na mwanaume

    aliempa huo ujauzito na mbaya zaidi hata nyumbani kwao alifukuzwa.



    Baada ya kuangaika na mimba yake mtaani na Maisha kumuendea vibaya, aliamua arudi nyumbani na kuwaomba msamaha wazazi, wazazi wake wakamkubalia kwa hali aliyonayo ila

    kwa kuwa alikuwa bado mwanafunzi,

    wazazi wake wakamshauri akaitoe ile

    mimba, nae akakubali.



    Ila katika

    utoaji wa hiyo mimba ilipelekea au kile kitendo cha Kutoa mimba kilitaka

    kumgharimu maisha yake, kwani alivuja damu nyingi kiasi kwamba

    ilimbidi alazwe hospitali takribani mwezi

    mmoja na nusu kutokana na damu kumpungukia mwilini.



    Alipotoka hospitali

    akahapa kutopenda tena

    mwanaume na akaahidi kutilia mkazo katika masomo yake.



    Baada ya kupona kabisa,

    aliendelea na shule na Mungu akamjaalia kumaliza

    kidato cha nne salama, ila alama aliyopata haikua salama kwani haikumruhusu kujiunga au kuendelea na madarasa yanayofuata.



    Baada ya miaka miwili ya kukaa nyumbani, kwa bahati nzuri akatokea mwanaume, mwenyeji

    wa Bukoba, alieitwa Ezekiel Kayoza

    Lutashobi na kutoa posa kwa wazazi

    wa Aika, wakamkubalia bila kipingamizi kwa sababu ya fedha

    alizokuwa nazo na pia waliona binti yao tayari amefikia umri wa kuishi na mume.



    Baada ya miezi kadhaa ya kufuata utaratibu wa dini na mila, bwana Ezekiel na bi Aika wakaoana kwa ndoa ya kikristo iliyokuwa na kila aina ya furaha kutoka kwa ndugu wa pande zote mbili, yaani upande wa mwanaune na upande wa mwanamke.



    Walikaa miaka miwili bila kupata mtoto, hapo ndipo chokochoko zikaanza kutoka kwa upande wa mwanaume wakidai wifi yao ni mgumba.



    Baada ya uvumilivu wa maneno na kashfa nyingi kutoka kwa mawifi, Aika alifanikiwa kupata ujauzito na kujifungua mtoto mmoja wa kiume aliyefuatiwa na wengine wawili wote wakiwa wa kiume na jumla ni kwamba alibahatika kupata watoto watatu.



    Wa kwanza aliitwa

    Zakaria, wa pili, Buguzo na wa tatu ndiyo huyu bwana mdogo alisebabisha niandike huu mkasa, anaitwa Kayoza.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    **********



    Mama Kayoza akatayarisha

    chakula, akawatengea wanae mezani,

    kisha akajumuika nao kula. Wakati wakiwa wanakula hakuna aliyemkumbusha mama Kayoza kuwa awasimulie ule mkasa, wote walikuwa kimya.



    Baada ya kula na kuoga, wote walikaa sebuleni

    wakawa wanaangalia filamu za

    Tanzania, kayoza akavunja ukimya,



    "mama, baadae yenyewe si ndio sasa

    hivi?, tuadithie basi" Kayoza alimkumbusha mama yake,



    "khaa!, nawe

    nae usahau?" Mama kayoza

    akamwambia mwanae kwa utani

    huku anacheka.



    "matatizo

    yanasahaulika nini?", kayoza akamjibu mama yake.



    "haya basi,

    nianzie wapi?" Mama kayoza akauliza huku akimuangalia mwanae.



    "anzia mwanzo" kayoza

    akajibu huku akitega masikio ili kusikiliza kisa kilichopelekea yeye kuwa mtu wa kubadilika na kuwa kama mnyama.



    Mama kayoza akaanza

    kuwaelezea...





    Alianza namna hii, "mimi

    nilipoolewa na baba yako, nilimkuta

    ana fedha zake za kutosha, alikuwa

    ana magari makubwa ya kubebea

    mizigo, alikuwa na daladala pale

    Bukoba mjini, alikuwa na gari ndogo

    tatu za kutembelea, na nyumba tatu

    pia.



    Kwa hiyo yeye alitoka Bukoba

    mpaka Kilimanjaro kuja kunioa mimi,

    kwa madai ya kuwa alinipenda toka

    zamani na alikuwa ananifuatilia chini

    chini.



    Baada ya ndoa nilitoka nyumbani na kuhamia kwenye nyumba ya baba yako ambayo aliijengea Bukoba.



    Ila baada ya kuhamia Bukoba,

    nilikaa pale nyumbani kwangu wiki

    mbili ndani, hakuna hata jirani

    mmoja aliyekuja kuniona, mule

    ndani nilikaa na wafanyakazi tu, na

    baadhi ya ndugu wa baba yako

    ambao walikuwa ndio

    wananichangamsha changasha, ila

    kingine kilichokuwa kinanishangaza ni

    kwamba kila ilipofika mwisho wa

    mwezi, baba yako alinunua, mbuzi

    wawili weusi na kondoo mmoja, alafu

    wanaukoo wote walikuja pale

    nyumbani, walikuwa wanaingia katika

    chumba kimoja kilichopo uwani na kujifungia uko, mimi sikuruhusiwa kuingia.



    Na nilipomuuliza, yeye

    aliniambia kile chumba ni kitakatifu,

    mimi sikuwa mtu wa kuhoji hoji sana,

    kwa hiyo sikutaka kudadisi zaidi kwa maana nilipojaribu kufanya hivyo uso wake ulionesha kutofurahishwa na maswali yangu.



    Ila niliendelea kujiuliza mwenyewe ni nini utakatifu

    wa hicho chumba?.



    Wanandugu wa baba yako na baba yako mwenyewe waliendelea kuingiaingia katika

    chumba iko ambacho ni kikubwa,

    kilikuwa na uwezo wa kubeba watu

    mia na zaidi.



    Kingine cha kushangaza ni kwamba, wote walikuwa wanavaa

    mavazi meusi, iwe shuka au nguo ya

    kawaida, ili mradi mwanamke avae

    nguo ndefu hadi katika vidole vya

    miguu yake.



    Na kila siku wanayoingia katika hicho chumba ikifika usiku mkubwa,

    walichukua magari makubwa ya

    mizigo na kuenda wanapopajua

    wenyewe, pamoja na wale mbuzi na

    kondoo.



    Ila baadae baba yako alikuja

    kuniambia kuwa uwa wanaenda

    kutoa sadaka katika mzimu wa mababu

    zao walikufa miaka iliyopita, na kwa sasa yeye ndio

    kaachiwa mamlaka ili autunze mzimu mmoja ambao ni mkuu kuliko mizimu yote wanayoiabudu.



    Sikufurahishwa

    na hali hiyo, ila sikutaka kumuudhi

    mume wangu, baada ya miaka miwili

    ya ndoa, nikajifungua mtoto wangu

    wa kwanza ambae ni kaka yako", Mama Kayoza aliongea kisha akamimina maji katika kikombe na kunywa,



    "mama mbona

    huyo kaka yangu simfahamu, au yupo mbali na nchi hii?" kayoza

    akahoji.



    "Subiri sasa mbona una

    haraka hivyo?" mama Kayoza

    akauliza huku akimshangaa mwanae,



    "Maswali ni lazima, sasa nisipouliza utajuaje kama nimekuelewa?" Kayoza alihoji



    "Sikiliza kwanza, maswali utauliza nikimaliza kusimulia" Mama kayoza alijibu kisha akaendelea,



    "baada ya kumzaa

    kaka yako wa kwanza, furaha

    iliongezeka katika familia yetu, ila kitu ambacho

    kilikuwa kinanitatiza ni kuwa,

    majirani hawakutaka kabisa

    kunizoea na wala hawakutaka hata kuja kutujulia hali kipindi nimejifungua, sikujua sababu, ila siku

    moja kuna jirani mmoja ndio

    akanipasulia sababu, eti kuwa mume

    wangu na ukoo wake ni wachawi wa

    kutupwa, na kila mke aliyemuoa

    hakukaa hata mwaka, alikufa,

    wananishangaa mimi nimemaliza

    miaka mitatu, na ninae mtoto

    mkubwa tu wa mwaka mmoja.



    Kiukweli ile habari ya wanawake kufa

    iliniogopesha, ikabidi jioni ilipofika

    nimuulize mume wangu, kwa kuwa

    alinipenda alinieleza ukweli...



    _____________________________

    SEHEMU YA KUMI NA SABA.

    _____________________________



    Aliniambia kuwa, kila mwanamke

    ambaye alimuoa, alimshauri aachane

    na mambo ya mizimu, ilo suala

    lilimuudhi na kuwaua kwa njia ya

    kuwadhoofisha kiafya, ila mwisho wa

    siku, mzimu wenyewe ukamshauri

    asioe mwanamke ambae anatokea

    Bukoba, ndo akaja kunioa mimi.



    Akaendelea kuniambia

    "tangu nimekuoa, sijaona hata siku

    moja ukifatilia mambo yangu, na leo

    ndio umeniuliza kwa mara ya kwanza

    kuhusu mambo yangu yaliyopitaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kipindi cha nyuma".



    Baada ya baba

    yenu kuniambia maneno haya,

    niliridhika nayo kabisa na wala sikutaka kuuliza tena ingawa nilianza kuishi kwa hofu.



    Baada ya miaka miwili nilifanikiwa

    kuzaa mtoto wa pili, na hapo tukapanga

    tusizae tena, na baba yako kwa mara

    ya kwanza akaniambia kuwa

    anaachana na mambo ya mizimu, mimi

    nilipingana nae, ila hakunielewa.



    Mimi niliendelea kupingana nae kwa sababu

    nilihisi kuwa ndugu zake wanaweza

    kuona mimi nilimshawishi baba yenu kuachana na mambo ya mizimu.



    Baada ya

    miezi sita tangu aitoe kauli ya

    kuachana na mizimu, ni kweli aliacha kununua kondoo wa kuchinjwa kila mwisho wa mwezi, na pia aliwaambia ndugu zake warafute sehemu ya kufanyia ibada zao kwa kuwa yeye hakuwa tayari kuendelea na hizo ibada.



    Mwanzo walikuwa wagumu kumuelewa, ila baadae walikubaliana nae ila kwa shingo upande.



    Baada ya mwaka mmoja, tulianza kufilisika, gari zilipata ajali

    kiutatanishi zikafa, nyingine

    alidhulumiwa na ndugu zake ambao

    walikuwa wanazisimamia, na hatua

    ya mwisho kabisa na ambayo sikuwa

    naifikiria kabisa, ni kwamba baba

    yako aliamua kuuza nyumba zake

    zote, hadi ile tuliyokuwa tunakaa,

    kisha akatuchukua mimi na kaka

    zako akatupeleka kijijini kwa mama

    yake, ambaye ni bibi yako.



    Huko sasa ndipo mauza uza yakaanza, Siku moja

    wakati natoka kisimani kuchota maji,

    nikamkuta kaka yako mkubwa,

    amekufa kifo cha ajabu sana,

    shingoni alikuwa na alama za meno,

    kile kifo hata baba yako

    kilimshangaza, tuliomboleza tukalia tukazika, mwishowe tukasahau.



    Siku ya harobaini baada ya kile kifo, usiku wakati tumelala

    na baba yako, tulishtushwa na

    upepo mkali ulioezua paa la nyumba

    tuliyokuwa tunakaa, wote tukakurupuka kitandani na kuanza kushangaa hiyo hali, wakati

    tunautafakari ule upepo, kilitokea

    kiumbe cha ajabu sana, wote tukabaki na mshangao ulioambatana na uoga.



    Kile kiumbe hakikuonekana kujali hali tuliyonayo, kilimwambia

    baba yako kuwa kinaitwa

    NDIFU, ni mzimu wa ukoo, na kimekuja kutaka hifadhi, baba yako

    akapata ujasiri na kumuuliza alikuwa

    anataka hifadhi ya nini?, kile kiumbe

    kikasema kinataka kuishi ndani ya mwili

    wa mtu alie hai, baba yako

    akamwambia sawa aende tu

    akaishi, kile kiumbe kikakataa na

    kusema anataka kuishi kwenye mwili

    wa baba yako au kaka yako ambae

    ndio huyo tu, tuliebaki nae, baba

    yako akakataa.



    Kile kiumbe kikasema,

    kitu kitakachotokea asubuhi

    tutakapoamka tusishangae, Kisha

    upepo mkali ukakibeba na paa la

    nyumba yetu likarudi kama

    mwanzo, tukabaki tunashangaa huku kila mmoja akiwaza lake, ila mwisho tukajadiliana na kukubaliana tusubiri mpaka kesho ili tuone hicho kitakachotokea, tukalala.



    Kesho tulipoamka ndipo

    tukapata kitu kilichotupa mshtuko,

    kiasi kwamba nikapoteza fahamu..



    tulimkuta mtoto wetu wa pekee

    amekufa kwa mtindo ule ule aliokufa

    nao mtoto wetu wa kwanza.



    Ndugu wa mume wangu walikuwa wanajua

    chanzo cha vifo vyote vya

    wanangu,baada ya mazishi kuisha na

    watu kutawanyika, ndugu wa baba

    yako wakamuita pembeni na

    kumshawishi aurudie ule mzimu na

    kuuomba radhi ili mambo yake

    yarudi kama awali, ila baba yako

    akakataa.



    Baada msiba kuisha, ule

    mzimu uliendelea kumuandama

    baba yako, mi kuona umezidi ikabidi

    nimwambie baba yako aukubali ili

    aulee kama mwanzo.



    Baada ya kauli ile, usiku mzimu ulitutokea tena tukiwa tumelala kitandani na kuongea maneno makali na ya kutisha juu ya msimamo wa baba yako, na kisha mzimu ukaongea maneno mazuri na kunisifia sana juu ya ushahuri niliompa baba yako, kwa ushauri ule niliompa baba yako, kuanzia hapo

    ule mzimu ulinipenda mimi na

    kuahidi kuwa kamwe hautanidhuru

    mimi na mtu yeyote yule ambae ana

    damu au nasaba moja na mimi, yaani mwanangu

    na ndugu zangu wote tuliochangia wazazi wote, au baba tu, au pia mama tu.



    "ndio maana Sajenti Minja haukumdhuru eee!?" Omary akauliza huku akimuangalia Kayoza,



    "inawezekana

    mwanangu, labda Minja hakudhurika kutokana na ahadi aliyonipa mzimu" Mama kayoza akajibu,



    "Duh, hii habari inazidi kunisisimua, inawezekanaje mimi nikawa mzimu?" Kayoza aliuliza huku akijishangaa,



    "Je unaamini kuwa nabii Musa aliweza kuipasua bahari ya shamu na akapita na wanaisraeli?" Mama Kayoza alimuuliza mwanae,



    "Hiyo naamini" Kayoza alijibu huku akimuangalia mama yake,



    "Sasa kwa nini huamini kuwa hata wewe unaweza kuwa mzimu?" Mama kayoza alimuuliza mwanae,



    "Sasa utafananishaje mambo ya Mungu na uchawi?" Kayoza alimjibu Mama yake huku akionekana kutofurahia hilo swali,



    "Huo uchawi uliumbwa na Mungu na manabii waliutumia ila waliuita muujiza na si uchawi" Mama Kayoza alimfafanulia mwanae,



    "Endelea na simulizi yetu mama bwana" Kayoza akamuambia mama yake,



    "Ngojeni kidogo" Mama kayoza aliongea kisha akainuka na kuelekea msalani.



    ****************



    Sajenti Minja alienda mpaka nyumbani kwake, akaingia mariwatoni na kuanza kusafi mwili.



    Alipomaliza alienda mpaka katika meza na kuanza kuandika barua ya kuacha kazi. Aliindika kwa ufanisi mkubwa kwa kutumia ile nakala ya barua aliyopewa na yule Dada polisi.



    Alipomaliza kuandika aliirudia tena na tena kuisoma na kuona haina makosa.



    Akaiweka vizuri katika bahasha na hakuona haja ya kuchelewa kuiwasilisha ofisini kwa mkubwa wake ingawa muda ulikuwa umeenda sana.



    Akatoka nje na kuchukua gari iliyomfikisha katika kituo cha kazi, na kwenda moja kwa moja mpaka kwa yule dada aliyempa maelekezo hawali, kwa bahati nzuri alimkuta,



    "Umerudi tena? umemaliza nini kuandika?" Yule dada aliuliza huku akiwa anaamini Sajenti Minja kuna kitu kingine kafuata na wala sio kuwasilisha barua ya kuacha kazi,



    "Ndio nimeileta barua hivyo" Sajenti Minja alijibu huku akimpatia ile bahasha yenye barua ndani,



    "Kha! Wewe mtoto mbona umeandika haraka hivyo, hujajipa hata muda wa kufikiri?" Yule dada alimuuliza huku akimshangaa Sajenti Minja,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mpaka nimefikia hatua hii, ujue nimefikiria sana" Sajenti Minja alijibu huku akionekana kutofurahishwa na maswali ya yule dada,



    "Wenzako wanatafuta kazi, wewe unaacha" yule dada alimuuliza Sajenti Minja huku akipokea ile bahasha,



    "Ni bora nikae bila kazi kuliko kupambana na kiumbe cha ajabu" Sajenti alijibu kijeuri,



    "Na kwenye barua umeandika sababu ya kuacha kazi ni kiumbe cha ajabu?" Yule dada aliendelea kuuliza huku akijua anamkera Sajenti Minja,



    "Ifungue uisome, ukimaliza utairudishia kwenye bahasha nyingine" Sajenti Minja alijibu,



    "Unaona huo ndio utakuwa ustaharabu?" Yule dada nae alimuuliza,



    "Nadhani ndio itakuwa nzuri zaidi kuliko kuniuliza maswali ilihali majibu nimekupa ndani ya hiyo bahasha" Sajenti Minja alijibu,



    "Okey, unaweza kwenda" Yule dada aliongea huku akiwa amekasirishwa na majibu ya Sajenti Minja,



    "Kuna hivi vitu pia" Sajenti Minja alimpa bahasha nyingine ila ilikuwa kubwa zaidi ya ile ya mwanzo na pia haikufungwa,



    "Na humu kuna nini?" Yule dada aliuliza huku akiipokea ile bahasha,



    "Ipo wazi hiyo bahasha, unaweza tu kuangalia vilivyomo ndani" Sajenti Minja alijibu kisha yule dada akaingiza mkono na Kutoa kitu kimoja moja, ilikuwepo bastola, namba ya uaskari na kitambulisho cha Sajenti Minja mwenyewe.



    "Sasa hivi unaniletea vya nini?" Yule dada aliuliza huku akimshangaa Sajenti Minja,



    "Unapoacha kazi si unatakiwa kurudisha hivi vyote?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Hivyo utamkabidhi mkubwa wako, tena atakapokubaliana na maombi yako" Yule dada alijibu huku akivirudisha vile vitu katika mfuko ambao vilikuwepo hawali,



    "Sasa kama nimeshawasilisha barua, hivi nikae navyo vya nini" Sajenti Minja aliuliza,



    "Zingatia nilichokwambia, tusibishane hapa. Tena ulete mkanda, kofia na buti" Yule dada alimalizia,



    "Sikupewa magwanda mimi, narudisha nilichopewa" Sajenti Minja alijibu huku akivipokea vile vitu vikiwa ndani ya ile bahasha,



    "Sawa, kesho mchana nenda kwa mkuu, nadhani atakuwa ameshaipitia barua yako" Yule dada alimpa maelekezo Sajenti Minja.



    Baada ya hapo Sajenti Minja akaondoka.



    *****************



    Mamá kayoza alipotoka msalani, akanywa maji kisha akaendelea,



    "kuanzia siku ambayo mzimu aliniahidi hatonidhuru mimi na kizazi changu, nikawa najihisi niko tofauti na

    mwanzo, kila nilichofanya

    nilifanikiwa, nadhani mzimu aliamua kunionesha namna anavyonijali.



    Baada ya miezi mitatu toka kaka yako wa pili amefariki, kwa bahati nikashika

    mimba.



    Siku ambayo niligundua nina mimba, mzimu alitutokea tena usiku na kuniomba sana niendelee na msimamo wangu wa kumshahuri baba yako juu ya kuujali huo mzimu, nami nikaitikia kwa kukubaliana nao.



    Mimba ilipofikisha miezi tisa ndipo nilikuzaa wewe,

    tena hapo ni baada ya kukaa mwaka mmoja tangu nilipompoteza

    mwanangu wa pili.



    Baada ya wewe kuzaliwa, sasa hapo yule

    mzimu alichachamaa, alitutokea usiku na kusema kuwa anataka

    kuingia kwenye mwili wa baba yako, Baba yako hakukubali hilo jambo,

    hata baba yako alipokataa yule

    mzimu hakuwa na cha kufanya kwa

    sababu nilimuomba ampe baba yako muda wa kufikiri kwanza, na kwa kuwa mzimu aliniahidi kutonidhuru mimi

    na ndugu zangu na damu yangu kwa

    hiyo kazi yake ilikuwa kunilinda mimi

    na nasaba zangu, mzimu akaondoka.



    Miaka ikasogea na

    mzimu haukuchoka kumsumbua

    baba yako, ulitutokea kila siku na kuongea maneno ya vitisho juu ya Maisha ya baba yako, ila Baba yako aliendelea kushikiria msimamo wake.



    Ikafika kipindi baba yako

    akaanza kuumwa, aliumwa wiki

    nzima na tulipoenda hospitali ugonjwa ukawa hauonekani, ghafla hali yake ikawa mbaya

    zaidi, mwili ukadhohofika na hakuweza hata kuamka

    kitandani.



    Ule mzimu kuona Baba yako yupo katika hali ile, ukabadilisha

    maamuzi ya kumuingia baba yako,

    ukawa unataka kuingia ndani ya

    mwili wako, ila baba yako

    akapinga tena jambo hilo, tena alilipinga kwa nguvu zote ingawa alikuwa mgonjwa.



    Kwa mila za kijijini kwa

    baba yako mtu anapokuwa anaumwa

    sana anatenganishwa na mke au

    mme wake. Huduma zote muhimu anakuwa anahudumiwa na

    mama yake au ndugu zake, kwa hiyo

    baba yako alikuwa anahudumiwa na

    mama yake ambaye ni bibi yako.



    Sasa siku moja wakati niko nje

    nakunyonyesha huku natayarisha

    chakula, ghafla upepo ulivuma kwa

    nguvu sana, kisha ukaingia katika

    chumba alichokuwepo baba yako ambaye pia ndani alikuwa bibi yako.



    Baada ya dakika tano za ukimya katika chumba kile, nikasikia mabishano yamezuka kati

    ya bibi yako na baba yako, mara ghafla bibi yako akaja kukuchukua

    mapajani kwangu, kwa ahadi ya kwamba kuna kazi anaenda kuifanya na

    anakurudisha mda si mrefu.



    Akaingia na wewe kwenye chumba alichokuwepo

    baba yako, kisha yale mabishano

    yakaendelea, baada ya muda kidogo

    nikaskia baba yako analia kwa sauti

    ya juu sana, ndipo nikatoka mbio hadi

    katika chumba alichokuwepo Baba yako na

    mama yake ambaye ni bibi yako, nikakukuta wewe Kayoza

    unamnyonya damu baba yako" Mama kayoza aliongea

    maneno haya huku machozi yakianza kumtoka....





    mama kayoza akaendelea,



    "baba

    yako aliponiona aliniangalia kisha

    akawa kama anataka kusema kitu, ila

    nguvu hakuwa nazo, akaishia

    kukunyooshea kidole, kisha akakata

    roho, Alafu wewe ukapoteza fahamu,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilijisikia uchungu sana, nilianza

    kulia kwa kwikwi pale mlangoni, nililia sana kiasi kwamba nikapoteza fahamu, nilizinduka nikaendelea kulia ila

    cha kushangaza bibi yako

    akuonyesha wasiwasi kabisa na wala hakutoa chozi la uchungu kuonesha kuwa amempoteza mwanae, badala

    yake aliniambia kuwa yule mzimu wa

    ukoo ameingia mwilini kwako wewe Kayoza

    kwa ruhusa yake, yaani ruhusa ya bibi yako.



    akaniambia kuwa kuanzia

    hapo hakutakuwa tena na shida, na

    kama shida itatokea ni kwa ajili ya

    kukulinda wewe (Kayoza), na sharti

    kubwa ambalo mzimu alitaka

    uzingatie ni kwamba, usifanye

    mapenzi mpaka uoe na pia ukae mbali na harufu ya damu ya aina yoyote na uepuke kuwa mtu wa hasira hasira. Shangazi yako hajawahi kumwambia hivyo?" Mama Kayoza akamuuliza mwanae,



    "Uwa ananisisitizia sana hayo mambo na kiukweli niliyamudu sana, hakuwahi kuniambia sababu ya mimi kutofanya hivyo" Kayoza alimjibu mama yake,



    "Kwanini hajakwambia?" Mama kayoza akamuuliza mwanae,



    "Mimi sijui" Kayoza akajibu,



    "Labda alikuwa na sababu zake" Mamá Kayoza aliongea huku akiinuka kitini,



    "Sasa mbona tena unaondoka?" Kayoza alimuuliza mamá yake,



    "Naenda jikoni kuangalia maharage, yasije yakaungua bure" Mamá kayoza aliongea huku akifuata uelekeo wa jikoni.



    ******************



    Sajenti Minja alirudi mpaka nyumbani kwake na kupanga nguo zake katika mabegi kwa ajili ya kujiandaa na safari, kwa maana alishajua kuwa kesho kukikucha ni lazima aitwe ofisini ili akakabidhi vitu muhimu vya kiaskari.



    Alipomaliza kupanga vizuri nguo zake, aliingia bafuni kuoga na kisha alipotoka tu alipotoka tu bafuni, akaona njia nzuri ya kupumzisha kichwa ni kulala. Akaingia chumbani kwake na kulala.



    _____________________

    SIKU ILIYOFUATA..

    _____________________



    Kama alivyotegemea kuwa ni lazima siku hii aitwe ofisini na ndivyo ilivyokuwa.

    Sajenti Minja baada ya kuamka na kupata kifungua kinywa, alipokea simu kuhitajika kufika ofisini kutoka kwa mkuu wa kituo chake cha polisi.



    Alijitayarisha haraka haraka na kuondoka mpaka kituoni na moja kwa moja akaenda kwenye ofisi ya mkuu wake,



    "Kaa hapo" Mkuu wake alimwambia huku akimuoneshea kiti kilichopo pembeni. Sajenti Minja akakaa.



    "Barua yako nimeipata na kuipokea asubuhi hii, nimeipitia na kwa upande wangu sina tatizo" Mkuu wake alimwambia huku akiwa anaandika andika vitu katika karatasi,



    "Asante sana mkuu kwa kunielewa" Sajenti Minja aliongea huku akimshukuru Mungu kwa kuitikia maombi yake,



    "Sasa cha muhimu ni kunikabidhi bastola uliyopewa na ofisi na namba zako za kazi na kitambulisho pia" Mkuu wake aliongea na kisha Sajenti Minja akavitoa vitu vyote alivyotakiwa akabidhi,



    "Hivi hapa mkuu" Sajenti Minja aliongea huku akiviweka vile vitu juu ya meza,



    "Mpaka hapa mimi na wewe tumemalizana" Mkuu aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja,



    "Nashukuru mkuu, kwa hiyo naweza kuondoka?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Kumbuka kuwa hapa ulikuja kufanya kazi tu, ila muajiri wako ni jeshi la wananchi, kwa hiyo ni lazima uende uko ndio watakupa majibu yao kama wamekubaliana na wewe au lah" Mkuu alimpa maelezo Sajenti Minja,



    "Hakuna shida, nitaenda pia uko" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu,



    "Wapo nje wanakusubiri" Mkuu aliongea na kumfanya Sajenti Minja ashtuke,



    "Wananisubiri?" Sajenti Minja akauliza,



    "Ndio" Mkuu aliongea huku akinyanyua mkonga wa simu na kubonyeza namba fulani, akawa anasubiri upande wa pili upokee simu,



    "Mimi nimeshamalizana nae, nawasubiri nyinyi mkuu" Mkuu wa polisi aliongea kwenye simu na kisha akairudisha simu mezani,



    "Sasa Kwanini wamenifuata?" Sajenti Minja aliuliza baada ya mkuu wake kukata simu,



    "Mimi sijui, labda Ndio utaratibu wenu wanajeshi" Mkuu alijibu kabla hawajasikia mtu akigonga hodi,



    "Pita ndani" Mkuu alijibu kisha wakaingia ndani wanajeshi wawili waliovaa gwanda zilizoandikwa MP begani, wakampigia saluti mkuu wa polisi,



    "Nyoosha mikono mbele" MP mmoja aliongea huku akiitoa pingu na kuishika mkononi,



    "Mambo gani tena ya kufungana pingu" Sajenti Minja aliongea huku akipingana na wale MP, alishangaa anapigwa makofi mengi sana yasiyokuwa na idadi,



    "Minja acha ukorofi, sikiliza unachoambiwa na kumbuka ndani ya jeshi hakuna maombi, kuna amri tu" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja ambaye alionekana kukubaliana nae na akakubali kufungwa pingu na kisha wale MP wakatoka nae nje na kumuingiza ndani ya gari nyeusi iliyokuwa na namba ya jeshi.

    Kisha ile gari iliondoka.



    ****************



    Baada ya kutoka jikoni, mama Kayoza alirudi sebuleni na kwenda kwenye jokofu na kuchukua maziwa fresh na kujimiminia kwenye glass,



    "Na sisi tunataka" Kayoza akamwambia mama yake,



    "Mimi Ndio nimeongea sana, kwa hiyo ni muhimu kulainisha koo" Mama Kayoza aliongea huku akitabasamu,



    "Sawa, endelea na story" Kayoza akamwambia mama yake,



    Ngoja niendelee, Baada ya miaka

    miwili tangu baba yako afariki,

    nilitaka kuondoka ili niende sehemu

    nyingine nikaanze kuishi maisha ya

    kujitegemea, kipindi hicho ulikuwa

    una umri wa miaka mitatu, Ilo wazo langu

    lilipingwa na shangazi zako na baba

    zako, mimi kuona hivyo nikawa naenda

    sana kanisani kufanyiwa maombi,

    kumbe yale maombezi yalikuwa

    yanaleta madhara katika mzimu wao,

    ila kwa kuwa mzimu ulishanipa

    ahadi ya kutonidhuru ukawa

    unavumilia tu, Siku moja wakati

    nimelala na wewe usiku, nakumbuka

    nilikuwa nasoma biblia, bila kutarajia nilikuona ukiinuka na

    ukakaa kitandani, mimi nikajua labda

    unataka kukojoa, nikakuvua nguo

    kisha nikakushusha chini ukojoe

    kwenye kopo, ila cha ajabu macho

    yako yakawa meupe ya kung'aa na

    meno yakakutoka yakawa marefu, mimi kuona hivyo nikahisi hatari nikataka kukimbia, ila ulinishika mkono na kunivuta na nikaangukia kitandani, hili nalo lilinishangaza, yaani mtoto wa miaka mitatu uwe na nguvu ya kunivuta na nikaanguka?



    Baada ya mimi kuanguka, ukaniangalia kwa sekunde kadhaa

    kisha ukasema kuwa umenivumilia

    kwa muda mrefu sana, hapo ndio

    nikagundua kuwa aliekua anaongea

    ni mzimu na wala sio wewe, kwa sababu

    ya muonekano wako, na maneno

    ulivyokuwa unayatamka kwa ufasaha,

    wakati katika hali yako ya kawaida

    ulikuwa huwezi kutamka maneno

    vizuri.



    Nakumbuka uliniambia ikifikaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kesho niondoke, maana nimeshindwa

    kulipa fadhira, ulidai ulinipenda sana ila maombi ninayofanyiwa uko kanisani ninapoendaga uwa yanamfanya anakosa raha, kwa hiyo basi, hana sababu ya kuniadhibu kwa kuwa aliniahidi kuwa kamwe hawezi kuniadhibu, ila cha kufanya ni mimi kuondoka hiyo kesho asubuhi.



    Kesho yake ilipofika,

    nikamwambia bibi yako kilichotokea,

    ikabidi awaite wanaukoo wote ambao walikuwa jirani na pale tunapoishi na kuwaelezea yote niliyoambiwa na mzimu.



    wakakubaliana niondoke,

    ila wewe nikuache, na kuhusu malezi

    yako, atakaehusika nayo ni shangazi yako

    mkubwa, ambae alikuwa anakaa

    kigoma, nikakubali kwa roho safi, kwa

    makubaliano ya kila baada ya miezi

    miwili ningeenda kwa shangazi yako kukuangalia......





    ....uko kwa shangazi yako walikuwa

    wanafuata masharti ya mzimu kama

    kawaida.



    kila mwisho mwezi

    walikuchinjia mbuzi na kondoo,

    damu walikupa ukainywa na sijawahi kusikia tena huo mzimu ukisumbua.



    Sasa hayo matatizo yanayokukuta uko chuo labda ni kutokana na masharti kutotekelezwa

    kwa sababu ya umbali uliopo" Mama

    kayoza akawa amemaliza masimulizi

    yake rasmi,



    "mh, mbona ni shughuli

    nzito?, sasa mama utanisaidiaje?"

    kayoza alimuuliza mama yake,



    "mwanangu sina msaada kwako"

    mama kayoza akajibu.



    "mama hamna

    mganga yeyote wa jadi

    unaemfahamu, ili anisaidie" kayoza

    aliendelea kumtupia maswali mama

    yake.



    "kusema kweli upande wa

    ushirikina huko mi sipaamini, ila..."

    mama kayoza akawa kama anafikiria

    kitu,



    "Ila nini?" Kayoza akamuuliza mama yake,



    "ila kuna mchungaji pale kanisani kwetu,

    nitajaribu kumuomba msaada" Mama

    kayoza akamalizia namna hiyo.



    "hata hivyo ni sawa pia, sasa utaenda

    kumwambia saa ngapi?" Kayoza kamuuliza mama yake.



    "nitaenda

    kumwambia jioni baada ya kula

    chakula" mama Kayoza

    akajibu.



    "mambo si hayo bwana"

    Kayoza akaongea huku akiwa na matumaini kibao ya kufanikiwa katika

    zoezi hilo.



    Baada ya kumaliza kula

    chakula cha jioni, mama Kayoza

    alijitanda vitenge vyake na kuelekea

    katika makazi ya mchungaji.



    Alipofika alikaribishwa na mtoto wa kike wa

    mchungaji, ambaye alimpa taharifa Mama kayoza kuwa mchungaji

    anaoga, ikambidi Mama Kayoza amsubiri mchungaji hadi

    alipomaliza kuoga.



    Mchungaji alipomaliza kuoga, akapelekewa

    ujumbe kuwa kuna mgeni wake anamsubiri varandani.



    Mchungaji akaenda mpaka

    Varandani na kumkuta Mama Kayoza akimsubiri,



    "karibu mpendwa"

    Mchungaji akamkaribisha mama

    Kayoza huku akimpa mkono,



    "asante mchungaji" mama

    kayoza akajibu.



    Baada ya salamu na

    kujuliana hali zao, mama kayoza

    akamuelezea mchungaji mwanzo

    mpaka mwisho wa matatizo aliyonayo

    Kayoza.

    Wakakubaliana hiyo kazi

    angeifanya kesho yake

    usiku.



    ***************



    Sajenti Minja alipakiwa katika gari kwa makofi kama mharifu aliyekuwa anabishana na Askari.



    Gari iliondolewa kwa mwendo wa kawaida lakini kipindi chote wakati gari ikitembea hakuna MP aliyemgusa Sajenti Minja.



    Baada ya mwendo wa dakika kumi, Sajenti Minja alishatambua uelekeo wa anapopelekwa na alishaanza kupata wasiwasi mkubwa kuliko ule wa hawali.



    "Jamani kwani nimefanya kipi kibaya?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwatizama wale MP kwa zamu,



    "Hauruhusiwi kuuliza wala kuongea kitu chochote" MP mmoja alijibu na Sajenti Minja akakaa kimya kwa kuwa alijua jeshini amri ndio kiongozi.



    Gari iliyombeba Sajenti Minja iliingia katika geti moja kubwa ambalo lilifunguliwa na wanajeshi.

    Gari ikapita ndani ya geti na ikatembea tena mwendo wa dakika tano mpaka ilipoenda kusimama mbele ya jengo moja lililokuwa limekaa peke yake.



    Sajenti Minja akashuka na kuangaza lile eneo ambalo lilipambwa na wanajeshi wakiwa katika majukumu mbalimbali pale kambini.



    Sajenti akaongozwa mpaka ndani ya lile jengo na kuingizwa katika ofisi moja nadhifu ambapo ndani ya hiyo ofisi walimkuta bwana mmoja mwenye umri wa miaka 40 - 45 akiwa amekaa katika kiti.



    Sajenti Minja na wenzake wote wakampigia saluti kwa ukakamavu yule bwana.



    "Asanteni vijana wangu, mnaweza kwenda nje na mniache na huyu bwana" Yule bwana aliongea kisha wale MP wakaelekea nje na kumuacha Sajenti Minja ndani tena akiwa amesimama,



    "Polisi wamekubali uache kazi?" Yule bwana alimuuliza Sajenti Minja,



    "Ndio mkuu" Sajenti Minja alijibu kikakamavu,



    "Ni nani aliyetaka wewe uende ukafanye kazi polisi?" Yule bwana alimuuliza,



    "Ni mimi mkuu" Sajenti Minja alijibu huku akiwa bado kasimama,



    "Ulisema kwanini ulitaka kifanya kazi ya polisi?" Yule bwana alimuuliza,



    "Ni kwa sababu nilitoka mafunzoni nje ya nchi, kwa hiyo niliitaji kupata sifa zaidi upande wa upelelezi wa ndani ili nipate nafasi ya kwenda kuongeza mafunzo ya nje ya nchi tena" Sajenti Minja alijibu,



    "Je kazi ya upelelezi ulipewa uko polisi?" Yule bwana alimuuliza,



    "Ndio nilipewa" Sajenti Minja alijibu,



    "Nadhani umeikamilisha?" Yule bwana aliuliza,



    "Hapana" Sajenti Minja alijbu,



    "Kwanini?" Yule bwana aliuliza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nimepata tatizo la afya, nikaona ni bora nipumzike" Sajenti alijibu,



    "Lete cheti cha daktari kinachothibitisha wewe no mgonjwa" Yule bwana alimwambia Sajenti Minja,



    "Nimekiacha nyumbani" Sajenti Minja alijibu ila alitoa jibu la uongo kwa maana hakuna cheti wala kitu chochote kinachoweza kuthibitisha yeye ni mgonjwa,



    "Ni tatizo gani la kiafya ulilonalo?" Yule bwana aliuliza,



    "Pumzi inanibana sana kiasi kwamba nashindwa kupumua" Sajenti Minja alijibu,



    "Ooh pole, basi nenda kapumzike, tutaendelea baadae na maswali" Yule bwana aliongea,



    "Sawa mkuu" Sajenti Minja alijibu na kuanza kuondoka,



    "Unaenda wapi?" Yule bwana alimuuliza kwa mshangao,



    "Umeniambia nikapumzike mkuu, naenda nyumbani" Sajenti Minja alijibu huku akisimama,



    "Utapumzikia hapa hapa kambini ili nitapohitaji kuongea na wewe, nikuite" Yule bwana aliongea kisha akapiga simu katika namba anayoijua yeye na kumtaka yule anaongea nae aende ofisini, kisha akakata simu.



    Baada ya sekunde kadhaa aliingia mwanajeshi na kusimama kikakamavu,



    "Mpeleke huyu akapumzike" Yule bwana alimwambia mwanajeshi aliyeingia,



    "Upande gani" Yule mwanajeshi aliyeingia akauliza,



    "Kwa wenye Matatizo ya kupumua au kwa wagonjwa wa mapafu na kifua" Yule bwana alijibu na kisha akamshuhudia yule mwanajeshi akimuongoza Sajenti Minja kwenda nje ya ofisi.



    Yule bwana akatoa tabasamu huku akitingisha kichwa kwa masikitiko.



    ************



    Huyu mchungaji ambaye Kayoza atamtembelea anaitwa Batoromeo

    mathayo wingo, jina maarufu

    lililozoeleka na wahumini wake ni

    Mchungaji Wingo, tokea ahamie pale

    kanisani ana muda wa mwaka mmoja

    na nusu, na watu wanaodaiwa kuwa

    wachawi, wameshadondoka kwenye

    eneo la makazi yake zaidi ya mara

    nne, hii ilimjengea imani sana kwa wahumini wake na pia alijikuta waumini wengine kutoka makanisa mengine wakifurika katika kanisa lake kila siku ambayo alifanya maombi kwa ajili ya wagonjwa na walemavu.



    Ndani ya muda mfupi Mchungaji Wingo aliweza kupata jina na heshima kubwa mkoani shinyanga.



    ***************



    Kesho yake ilipofika, mama Kayoza na Kayoza

    pamoja na Omari wakaongozana

    usiku ule mpaka kwa mchungaji

    Wingo, Walipofika, mchungaji na

    familia yake, wakawakaribisha ndani,

    na baada ya maongezi ya muda mrefu, mchungaji aliwaambia kuwa,

    mama kayoza na Omari warudi

    nyumbani, ila Kayoza abakie, kwa

    sababu anataka akeshe nae huku wakimfanyia maombi na familia

    yake, mama kayoza na Omari wakajiondokea zao, wakamuacha

    kayoza kwa mchungaji...



    KAMA MCHUNGAJI ANGEJUA KITAKACHOMTOKEA, ASINGEKUBALI

    KUBAKIA NA KAYOZA...





    Baada ya mama kayoza kuondoka, Mchungaji alielekea katika chumba kimojawapo ndani ya nyumba yake na kukaa kwa muda wa dakika chache kisha akarejea tena mahali alipomuacha Kayoza,



    "we ni mkristo wa dhehebu gani?" Mchungaji wingo alimuuliza Kayoza baada ya kukaa.



    "ni mromani, romani catholic" Kayoza

    alijibu huku akijaribu kutabasamu.



    "ok, je unaamini katika

    ulokole?" Mchungaji Wingo akarusha swali

    jingine.



    "mi naamini katika dini

    yeyote na dhehebu lolote ambalo linafuata matakwa na njia za

    Mungu" Kayoza akajibu,



    "Umeshawahi kukaa peke yako hata siku moja na kufanya maombi?" Mchungaji Wingo alimuuliza Kayoza huku akimuangalia kwa umakini,



    "Hapana" Kayoza alijibu,



    "Na kanisani uwa unaenda?" Mchungaji Wingo aliendelea kumuuliza Kayoza,



    "Hapana" Kayoza akajibu,



    "Sasa unaamini vipi katika dini zinafuata matakwa ya Mungu aliye hai ungali wewe hufuati njia za Mungu?" Mchungaji alimuuliza Kayoza,



    "Kuna kipindi uwa Nataka sana kwenda kanisani, ila uwa najikuta napata uvivu mkubwa sana" Kayoza alitoa jibu lililomfanya Mchungaji Wingo atabasamu,



    "Wewe unafikiri ni kitu kinapelekea upate uvivu siku ya kwenda kanisani?" Mchungaji Wingo aliuliza tena,



    "Mwanzo nilikuwa sijui, ila kwa hizi habari alizonieleza mama, nafikiri ni mzimu ndio ulikuwa unaniletea hali hiyo" Kayoza alijibu na kufanya mchungaji atabasamu tena,



    "Mbona mama yako alikuwa anaenda kanisani akiwa chini ya huo mzimu?" Mchungaji Wingo aliuliza,



    "Hivi mchungaji unadhani nyumba ya jirani yako unaweza kuitawala kama unavyoitawala nyumba yako?" Kayoza alitoa swali lililomfanya Mchungaji Wingo ashtuke kidogo,



    "Unamaanisha nini kusema hivyo?" Mchungaji Wingo aliuliza,



    "Mzimu kanifanya mimi kuwa nyumba yake, sasa anaweza kunikontroo atakavyo yeye, kwa hiyo mamlaka anayoweka juu yangu ni lazima yawe yana nguvu kuliko anayoweka juu ya mama yangu" Kayoza alimjibu Mchungaji Wingo,



    "Jibu lako zuri sana, ila lina kasoro, hakuna kiumbe kitakachoweza kukutawala hapa duniani kama utamuamini Mungu" Mchungaji Wingo aliongea huku anaangalia mazingira ya sebuleni kwake,



    "Kwa maana hiyo mimi simuamini Mungu?" Kayoza aliuliza,



    "Hiyo ni Imani iliyopo moyoni kwako, kwa hiyo hilo swali jiulize wewe" Mchungaji Wingo aliongea huku akitabasamu,



    "Kwani Mchungaji imani ipo kwenye nyumba za ibada tu?" Kayoza aliuliza,



    "Hilo swali nitakujibu siku nyingine. Nikuletee maji ya baridi au ya moto?" Mchungaji Wingo alimuuliza Kayoza huku akitabasamu,



    "ila mchungaji mimi sijaomba maji na wala sina kiu" Kayoza alijibu huku akionekana kumshangaa Mchungaji Wingo,



    "Sijamaanisha una kiu, na sio kila unachopewa, kuna vitu unapewa bila hata kuomba" Mchungaji Wingo aliongea huku akiondoka na kumuacha Kayoza akimuangalia huku akitabasamu kutokana na maneno ya Mchungaji Wingo.



    *******************



    Sajenti Minja alitolewa moja kwa moja kutoka katika ofisi za mkuu wake wa jeshi na kuanza kupelekwa katika nyumba moja nzuri ambayo ilionesha haikuwa inakaliwa na mtu au anaekaa pale atakuwa hayupo au ni watu ambao hawapendi kelele, uzuri mwingine ni kwamba ile kambi ni ngeni machoni kwa Sajenti Minja ila si ngeni masikioni mwake kwa maana alishapata habari za kambi hii kutoka kwa wenzake wachache aliokutana nao mafunzoni.



    Waliendelea kuisogelea ile nyumba huku kila mmoja akiwa kimya na uzuri wa ile nyumba kwa nje, tayari Sajenti Minja kichwani kwake alishatengeneza fikra za kule ndani ya nyumba kutakuwaje. Aliwaza kutakuwa na kitanda kikubwa, jakuzi, upepo mzuri wa Air condition na kila aina ya chumba kizuri ambacho mwanajeshi kama yeye anastahili kupumzika.



    "Mheshimiwa vua viatu" Mwanajeshi aliyeongozana na Sajenti Minja aliongea na kumfanya Sajenti Minja atoke kwenye dimbwi la mawazo,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Alaah! Kumbe tumefika?" Sajenti Minja aliuliza huku akitabasamu lakini yule Mwanajeshi hakushughulika kumjibu na badala yake alibonyeza namba zilizopo kwenye mlango na mlango ukafunguka, hapo ndipo alipokuta wanajeshi wengine wawili wakiwa mlangoni wakiwasubiri,



    "Huyu wa wapi?" Mwanajeshi mmoja kati ya wale wawili aliuliza,



    "Mgonjwa wa kifua" Mwanajeshi aliyeongozana na Sajenti Minja alijibu na kufanya Sajenti Minja ajikohoreshe kidogo,



    "Kumbe kweli unaumwa? Twende ukapate matibabu upumzike" Mwanajeshi yule mwenye herufi zilizoandikwa MP aliongea na kumfanya mwenzake atabasamu na wakati huo huo yule Mwanajeshi aliyemleta Sajenti Minja aliishia mlangoni na kurudi alipotoka.



    Wale wanajeshi wakiwa na Sajenti Minja walivipita vyumba kadhaa na mwisho waliingia katika chumba kimoja kilichoandikwa "BREATH",



    "Ebu ruka ruka kichura chura kidogo ili mwili upate joto" MP mmoja alimwambia Sajenti Minja,



    "Ni moja ya matibabu au?" Sajenti Minja aliuliza kwa mshangao,



    "Ruka bwana, dawa unazotakiwa kunywa zinahitaji joto kubwa la mwili" Yule MP aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja.



    Sajenti Minja akaanza kuruka kichura chura kwa kasi huku akicheka na kubadilisha mitindo mbalimbali ya kuruka kichura chura.



    Baada ya dakika mbili jasho lilianza kumtoka, akaamua asimame,



    "Nadhani hapa nipo poa, mwili umeshachemka huu" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu, lakini alikuwa amekosea sana, alishtukia akipigwa kofi zito sana la shingo,



    "Endelea kuruka, nani kakupa ruhusu ya kusimama?" MP mmoja aliongea kwa ukali huku akiwa amemkunjia uso Sajenti Minja,



    "Kwani ni adhabu hii?, sio lazima niruke" Sajenti Minja nae aliongea kwa ukali huku akiwa amepaniki,



    "Tutajua kama ni adhabu au sio adhabu" MP mwingine aliongea na kumpiga ngumi Sajenti Minja iliyompata vizuri usoni. Sajenti Minja alivyoona hivyo akaona imeshakuwa hatari, akaanza kupambana na wale MP, alipambana nao vizuri na akawadhibiti, maana alitoa kichapo cha hatari mpaka wale MP wakawa wanaogopa kumsogelea.



    Sajenti Minja akiwa bado anajiamini kwa kichapo alichotoa, alianza kuondoka kibabe, ila hata kabla hajapiga hatua mbili alitokea mwanajeshi mwingine akiwa na bastola,



    "Ukileta fujo nakufumua miguu, lala chini na uweke mikono juu" Mwanajeshi aliongea huku akiwa hatanii,



    "Kwani kuna tatizo gani, mbona siwaelewi?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Lala chini ndio uhoji" Mwanajeshi aliongea kwa sauti kubwa na kumfanya Sajenti Minja akubaliane nae, akalala chini na wale MP waliokula kichapo wakamwendea na kumfunga pingu kwa nyuma, kisha wakambeba juu juu mpaka katika chumba kingine na kumuweka juu ya kiti cha chuma na kumfunga na kamba, kisha wakaanza kumpiga kwa hasira walimchakaza haswa.



    Baada ya kuridhika na kipigo walichokitoa, ndipo alipoingia yule bwana mkuu wa jeshi aloyekuwa anamuhoji mwanzo kule ofisini, MP wakampigia saluti na kumsogezea kiti kwa kukiweka mbele ya kiti alichokalia Sajenti Minja,



    "Umelijua kosa lako?" Yule bwana alimuuliza Sajenti Minja huku akimuangalia kwa huruma, lakini Sajenti Minja hakuweza kujibu kitu,



    "Ulichofanya wewe ni kudhalilisha jeshi. Huwezi kuacha kazi kwa kuogopa kitu kwa sura wala muonekano. Ni bora ungeomba muda wa kujipanga tungekuelewa. Alafu ulipoamua kuacha kazi ukaamua utumie na kigezo cha kuumwa, hilo ni kosa pia, unadanganya wakati uliahidi kusimamia ukweli" Yule bwana mkuu wa jeshi aliongea kwa sauti ya upole ila iliyosikika vyema masikioni kwa Sajenti Minja.



    Kisha yule bwana akasimama huku akimuangalia Sajenti Minja,



    "Mpelekeni sehemu tulivu apoze maumivu" Yule bwana aliongea na kuanza kuondoka huku akiwa haonekani kama ni mtu mwenye kupenda kucheka.



    Yule bwana alitembea mpaka alipofika mlango wa kutokea nje ya lile jengo, ndipo aliposikia sauti kubwa ya Sajenti Minja ikipiga kelele kutokana na maumivu aliyokuwa anayapata muda huo,



    "Siku zote mwanajeshi mpumbavu utulivu anaostahili ni huo unaoambatana na maumivu" Yule bwana mkubwa aliongea huku akitabasamu na wakati huo huo alikuwa anatoka nje ya lile jengo lililokuwa tulivu kwa nje, ila kwa ndani si sehemu salama kwa wanajeshi wenye makosa.



    ***************



    Baada ya muda kidogo Mchungaji Wingo alirudi huku akiwa na jagi lililojaa maji,



    "Muda wa maombi unakaribia, umejiandaaje?" Mchungaji Wingo alimwambia Kayoza,



    "Kawaida tu, ila naimani tutafanikiwa" Kayoza alijibu,



    "Ni bora umetanguliza Imani mbele, ni jambo jema" Mchungaji aliongea kwa imani,



    "Nimekuletea maji hayo unywe, ingawa hujaniagiza ila itabidi unywe" Mchungaji Wingo alimwambia Kayoza,



    "Haina shida, nitakunywa tu" Kayoza alijibu huku akiyamimina yale maji katika glass.



    Muda wote ambao mchungaji alikuwa anaongea na Kayoza, watoto wake walikuwa wanatayarisha chumba cha kufanyia maombi.



    Baada ya maandalizi,

    mchungaji Wingo alimkaribisha Kayoza

    katika chumba cha maombi, kisha

    watoto na mke wa mchungaji Wingo

    wakaingia katika chumba cha maombi,

    huku kila mmoja akiwa amebeba biblia yake mkononi, hapo ilikuwa yapata saa tano za usiku

    usiku.



    Baada ya wote kujumuika ndani ya kile chumba, maombi yakaanza rasmi,

    Mchungaji Wingo na familia yake

    walikemea kwa juhudi zote, mpaka saa

    saba usiku, Kayoza alikuwa kama

    mwanzo, hakuwa na mabadiliko yoyote, Ila Mchungaji hakukata

    tamaa, pia alikuwa anahisi

    akishindwa kumtibu Kayoza, heshima

    yake inaweza kushuka katika kanisa, kwa hiyo alizidisha maombi .



    Ilipofika saa nane za usiku mabadiliko yakaanza kwa Kayoza, alihisi kizunguzungu, hakuna aliyeyaona hayo kabadiliko isipokuwa yeye mwenyewe.



    Wakati maombi yanaendelea Mchungaji

    akahisi, kuna nguvu nyingine iko kwa

    nje, inashindana nae, kwa maana yeye alikuwa na uwezo wa kuona mpaka visivyoonekana. Ile nguvu iliyokuwa inatoka nje ilikuwa haimdhuru ila hakuwa akiitaka iendelee kumuingilia katika maombi yake. Akaamua atoke nje mara moja na akaiacha familia yake inamuombea Kayoza. Ile

    kutoka nje, akakutana na watu zaidi ya kumi, wote wako uchi, wamejipaka

    majivu usoni.



    Mchungaji Wingo

    hakupata tabu kuwatambua kuwa

    wale ni wachawi. Katika kipindi cha

    maisha yake ya uchungaji ameshakutana na hayo mambo mara nyingi tu.



    Akaona dawa yao ni ndogo tu, akaanza kukemea, Baada ya kupambana nao kwa

    muda wa saa moja, wale wachawi

    wakawa wanaelekea kushindwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ila ghafla mambo yakabadilika, Mchungaji Wingo akaanguka chini kisha akapoteza

    fahamu. Sasa wale wachawi

    wakasogea pale alipolala mchungaji huku wakiruka ruka kwa furaha na kuongea lugha isiyoeleweka. Walimsogelea kwa ajili ya kummaliza kabisa Mchungaji Wingo, ila kila

    walipojaribu kurusha makombora

    yao, hayakumdhuru

    mchungaji.Wakajua sababu ya hayo

    mambo ni kutokana na nguvu ya maombi ya familia ya mchungaji

    waliyokuwa wanaendelea nayo chumbani.



    Wachawi wote wakavamia

    katika kile chumba kwa ajili ya kupambana na maombi ya familia ya Mchungaji, ni kitendo cha

    dakika kumi tu, familia yote ya

    mchungaji ilikuwa imepoteza fahamu ni kutokana na kwamba hawakuwa na imani ya kutosha.



    Wachawi wakawabeba kisha wakawalaza nje ya geti pamoja na

    mchungaji mwenyewe, kitu kilichowashangaza wachawi ni kuwa

    kulikuwa na kijana ambae ni kayoza, toka wale wachawi waanze kuloga,

    yeye hakudhurika, ndipo wachawi

    wakafanya kosa la mwaka,

    wakamweka kayoza katikati yao,

    kisha, wakaanza kumloga, bila kutegemea, kayoza akabadilika na

    kubeba taswira ya kutisha, wale wachawi mawazo yao yakaona zoezi

    lao limefanikiwa, mmoja kati ya wale

    wachawi, akamsogelea kayoza ili

    ammalize kabisa, ni kitendo bila

    kuchelewa, kayoza ndani ya sekunde

    kumi alishanyonya damu wachawi

    watatu, ndani ya dakika moja

    alishamaliza wachawi wote, nao

    akawatoa nje, kisha akawalaza

    pamoja na familia ya mchungaji,

    kisha akarudi katika chumba cha maombi na akapoteza fahamu.



    Asubuhi kulipokucha, watu wengi sana walijaa nje ya nyumba ya

    Mchungaji Wingo, na wote walikuja kuangalia watu ambao walilala nje ya nyumba ya Mchungaji huku wakiwa na alama za meno shingoni.



    Kati ya watu waliolala getini alikuwepo pia Mchungaji mwenyewe na familia yake... ila wao walikuwa na mavazi yao.............



    _____________

    ENDELEA

    _____________



    ...waumini wa mchungaji Wingo nao walikuwa

    wengi sana, polisi walifika mapema sana katika

    sehemu ya tukio, katika uchunguzi wao wa haraka haraka katika eneo lile,

    waligundua watu kumi waliokuwa uchi wa

    mnyama, wote walikufa na watu wengine sita

    walikuwa wamepoteza fahamu.



    Askari wakajadiliana wenyewe kwa wenyewe na mwisho wakaamua kuwabeba wale watu waliokufa huku wakiwa tayari wamepiga simu hospitali kwa ajili ya kuhitaji gari la wagonjwa, Ila baada ya muda kidogo, au tuseme kabla gari la wagonjwa halijafika mchungaji alizinduka na kujikuta yupo nje ya nyumba yake huku baadhi ya watu wakimuangalia na pia wakionekana wana maswali mengi vichwani mwao na mwenye majibu ni yeye mwenyewe Mchungaji Wingo



    "Vipi, unajisikiaje?" Polisi mmoja alimuuliza Mchungaji Wingo baada ya kuzinduka,



    "Namshukuru Mungu, maana ni mkubwa kuliko kila kitu hapa duniani" Mchungaji Wingo aliongea huku akiwatizama watoto wake na mkewe ambao nao walianza kuamka mmoja mmoja,



    "Hapa ni kwako?" Polisi akamtupia swali jingine,



    "Ndio, ni kwangu" Mchungaji Wingo alijibu,



    " unaweza kutueleza ni nini kimetokea?" Polisi aliendelea kuhoji,



    "Hapa tunajaza watu tu, ni bora tukafanyie mahojiano kituoni" Polisi mwingine alimshauri yule polisi aliyekuwa anamuhoji Mchungaji Wingo,



    "Sasa si inabidi tuwabebe wote ambao ni wazima" Polisi aliyekuwa anahoji alimuuliza mwenzie,



    "Hiyo ni familia yangu, mngewaacha tu, twendeni mkanihoji mimi mwenyewe, nadhani natosha" Mchungaji Wingo aliongea huku akilazimisha tabasamu,



    "Hapana, ni lazima tuchukue Maelezo ya watu wrote" Polisi aliongea huku akimhimiza Mchungaji Wingo aelekee mahali gari la polisi lilipoegeshwa. Polisi wakambeba yeye na familia yake kwa ajili

    ya mahojiano zaidi.



    ******************



    Hii habari za hili tukio lililotokea nyumbani kwa mchungaji ilitangazwa na vyombo vya habari vya nchi nzima, habari zikawafikia wakubwa zake Sajenti Minja, Wakubwa zake, ikabidi washauriane,



    " sasa tunafanyaje, au tumchague kijana mwingine aifuatilie hiyo kesi, kwa maana wapo wengi tu na si lazima awe Minja tu" Mkuu was polisi alimwambie mkuu wa jeshi,



    "Hilo ni jambo zuri, hila kufanya hivyo ni kuitia aibu hii taasisi ya jeshi na serikali kwa ujumla. Huyu Minja hapo alipo hana hata miezi sita toka atoke mafunzoni Korea ya kaskazini, sasa huoni kumuachia asiendelee na hii kesi hayo mafunzo yake yatakuwa hayana manufaa yoyote kwa taifa?" Mkuu wa Jeshi alimuuliza Mkuu wa Polisi,



    "Sasa kama kesi imemshinda tutafanyaje?" Mkuu wa Polisi aliuliza,



    "Watuhumiwa unapowahoji na wakaonekana hawataki kusema ukweli uwa unawafanyaje" Mkuu was jeshi aliuliza huku akiiwasha sigara yake,



    "Uwa nawashurutisha kwa kuwapa adhabu" Mkuu wa Polisi alijibu,



    "Unawasulubu, si ndio?" Mkuu wa Jeshi aliuliza huku anamuangalia Mkuu wa Polisi,



    "Ndio maana yake" Mkuu wa Polisi alijibu,



    "Hill ndio jibu" Mkuu was jeshi aliongea huku akinyanyuka katika kiti,



    "Kwa hiyo Minja nae utamsulubu?" Mkuu wa Polisi aliuliza,



    "Sio nitamsulubu, tayari kishaanza kusulubiwa muda mrefu tu" Mkuu wa Jeshi alijibu huku akivaa miwani yake,



    "Unamsulubia wapi?" Mkuu wa Polisi akauliza kwa mshangao,



    "Nifuate" Mkuu wa jeshi aliongea huku akianza kupiga hatua kuelekea nje ya ofisi yake, wakatembea mpaka katika like jengo ambalo ndani ndipo yupo Sajenti Minja anasulubika. Walipofika walibonyeza kitufe cha kengele na baada ya muda kidogo mlango ulifunguliwa na akatoka mwanajeshi mmoja aliyewapigia saluti na kuwaachia mlango wazi ili wapite. Walipoingia ndani walinyoosha moja kwa moja mpaka sehemu alipokuwepo Sajenti Minja na kumkuta akiwa amewekwa ndani ya bwawa la kuogelea huku mikono yake ikiwa imefungwa kamba kwa nyuma na pia alifungwa jiwe kubwa ili asielee juu ya maji,



    " mmemzamisha kwa muda Gani?" Mkuu wa jeshi aliwauliza vijana wake,



    "Hii dakika ya ishirini" Mwanajeshi mmoja alijibu huku akiitazama saa yake mkononi,



    "Dakika ishirini?, si atakuwa ameshakufa?" Mkuu wa Polisi aliuliza huku akishangaa,



    "Hawezi kufa kirahisi hivyo, huyo anaweza kuzama hata siku nzima?" Mkuu wa Jeshi alijibu,



    "Duh, aisee ni hatari sana" Mkuu Wa Polisi aliongea huku akisikitika,



    "Mtoeni nje" Mkuu wa Polisi aliwaamuru vijana wake ambao walitekeleza agizo bila shurti yoyote. Wakamtoa Sajenti Minja nje ya maji na kumuweka pembeni. Sajenti Minja alikuwa amechoka na mwenye majeraha mengi sana usoni kutokana na mateso aliyokumbana nayo,



    "Mfungueni hilo jiwe na mleteeni kiti" Mkuu wa Jeshi aliwaagiza vijana ambao walitii na kuleta kiti haraka,



    "Kaa hapo mheshimiwa" Mkuu wa Jeshi alimwambia Sajenti Minja aliyekuwa anaugulia maumivu. Sajenti Minja akajinyanyua na kujiweka juu ya kiti,



    "Mmempiga kama mharifu" Mkuu wa Polisi aliendelea kushangaa,



    "Pole sana, sasa kilichotuleta hapa ni kitu kimoja" Mkuu wa Jeshi aliongea huku akimtupia gazeti lenye habari zilizotokea huko shinyanga kwa mchungaji. Sajenti Minja akaisoma ile habari kwa umakini mkubwa na kisha akamrudishia mkubwa wake gazeti lake,



    "Umeielewa hiyo habari?" Mkuu wa Jeshi alimuuliza Sajenti Minja,



    "Hapana Mkuu" Sajenti Minja alijibu,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Hivo vifo waliokufa hao watu, havina tofauti na vifo vilivyokuwa vinafanywa na wale vijana unaowatafuta, kwa maana hiyo basi, sina budi kusema kuwa muuaji yupo shinyanga" Mkuu wa Jeshi aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja ambaye naye alikuwa anamuangalia mkubwa wake,



    "Sasa nambie unaendelea na hii kesi au bado umeshikilia msimamo wako?" Mkuu wa Jeshi aliuliza huku akiiangalia saa yake.



    Sajenti Minja aakabaki kimya asijue la kujibu,



    "Umesikia nilichouliza?" Mkuu wa Jeshi aliuliza huku akirudisha macho yake kwa Sajenti Minja,



    "Ndio nimesikia mkuu" Sajenti Minja aliitikia kwa unyonge,



    "Nipe jibu, maana kuna mambo mengine ya kufanya muda huu" Mkuu wa Jeshi aliongea kwa mamlaka,



    "Naweza nikapata muda kidogo wa kufikiria?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Unahitaji muda wa dakika ngapi?" Mkuu wa Jeshi aliuliza,



    "Nikipata angalau hata wa masaa kumi na mbili utanitosha" Sajenti Minja aliongea,



    "Saa hivi ni saa kumi na mbili jioni, kwa maana hiyo mpaka kesho saa kumi alfajiri utakuwa una jibu, so ndio?" Mkuu wa Jeshi aliuliza,



    "Ndio mkuu" Sajenti Minja alijibu,



    "Mpelekeni akapumzike, mpeni kila atachohitaji" Mkuu wa Jeshi aliwaambia wale wanajeshi waliokuwa wamesimamia mateso ya Sajenti Minja,



    "Sawa mkuu" Wanajeshi walijibu na kumuinua Sajenti Minja na kumpeleka wanapojua wao, Mkuu wa Jeshi akatoa tabasamu moja la karaha sana,



    "Kesho akija na jibu tofauti na ninalolitaka mimi, Kambi itapata habari mbaya za mwenzao" Mkuu wa Jeshi aliongea huku akianza kuondoka,



    "Utamuua au?" Mkuu wa Polisi aliuliza huku akimfuata,



    "Hata wewe pia utajua kesho hiyo hiyo" Mkuu wa Jeshi alijibu na kumfanya mkuu wa Polisi anyamaze kimya.



    ***************************



    Katika kituo cha polisi mahojiano kati ya

    mchungaji na polisi yaliendelea vema, ila

    mchungaji hakutaka kuwaambia kuwa mhusika

    wa mauaji alikuwa nae, ila alichowaambia polisi

    ni kwamba, hata yeye haelewi na hakumbuki kitu

    chochote kilichotokea, zaidi ya kujikuta yuko nje

    ya nyumba yake wamelala na familia yake na watu hasiowajua,



    "Hiyo inawezekanaje?" Askari mmoja alimtupia swali Mchungaji huku akiwa ahamini maelezo yake,



    "Hata mimi sijui imewezekanaje, ni kama maajabu Fulani hivi ya kiimani" Mchungaji Wingo alijibu huku akionekana dhahiri kushangaa,



    "Kwa hiyo unadhani wale watu kumi ambao wamekufa kwa kunyonywa damu ni nani tutamuhusisha na vifo vile?" Askari akamtupia swali jingine,



    "Sasa unaponiuliza mimi unataka nikujibuje, au unadhani nitasema unihusishe mimi na hivyo vifo?" Mchungaji Wingo aliuliza kwa sauti ya upole,



    "Kisheria ni kwamba wewe na familia yako mpo hatiani kwa vifo hivyo" Askari aliongea huku akiandika andika katika kikaratasi kidogo juu ya meza,



    "Sawa, ila hakuna mtu katika familia yangu ambaye ana uthubutu wa kuua hata mbu, sembuse mtu" Mchungaji Wingo aliongea kwa kujiamini,



    "He nikikuweka ndani nitakuwa nimekosea ingawa unajitetea hivyo" Askari aliuliza,



    "Siwezi kukupangia, fanya vile kazi yako inavyotaka" Mchungaji Wingo alijibu na kumfanya yule askari anyanyuke huku pingu zikiwa mkononi,



    "Afande kati ya wale watu waliokutwa wamekufa kwa mchungaji, mmoja kumbe mzima" Askari mwingine aliongea wakati anaingia ndani ya chumba cha mahojiano,



    "Kwa hiyo waliokufa ni tisa tu?" Askari aliyekuwa anamuhoji mchungaji aliuliza huku akianza kumfunga pingu mchungaji Wingo,



    "Sasa huyo Mzee usimfunge pingu kwa maana yule mtu ambaye amezinduka amesema kuwa wamepata ajali na wala mtu yoyote asiusishwe na vifo vya wenzake" Askari aliyeingia aliongea na kumfanya mwenzake amkodolee macho,



    "Una maana gani kusema hivyo?" Askari alimuuliza mwenzake,



    "Kwa Maelezo ya yule mtu kule hhospitali, basis huyu mzee hana hatia" Askari mwenzake alijibu,



    "Cha kuwashauri ni kwamba, kwa kuwa Huyo mmoja ameamka, ni vyema mngenipeleka na familia yangu mbele yake na aseme kama sisi tumewaua wenzake" Mchungaji Wingo aliongea kwa upole,



    polisi walionekana kuridhika na maneno ya

    mchungaji na familia yake, tena walimuamini

    zaidi kwa sababu alikuwa mtumishi wa Mungu.

    Baada ya mahojiano, polisi walimuachia

    mchungaji arudi nyumbani kwake, ila wakamwambia wakimuhitaji watamfuata.



    Mchungaji alipofika nyumbani kwake, moja kwa

    moja akaenda kwenye chumba chake cha ibada,

    akamkuta kayoza amekaa kimya anasoma biblia,

    akamsalimia, kisha akamsimulia kilichotokea,

    alafu akamrudisha kwa mama yake.



    BAADA YA SIKU TATU..

    __________________________



    Jioni wakati wanaongea kuhusu mambo yaliyotokea siku tatu nyuma.



    Sebuleni alikuwepo mama kayoza, Kayoza na Omari,



    "Hili tatizo hata mimi linaanza kunitisha, ina maana hata mchungaji ameshindwa?" Kayoza aliuliza huku anamtazama mama yake,



    "Hakuna kinachoshindikana kwa Mungu, sema tu hayo mambo yaliyotokea usiku yalimvuruga" Mama kayoza alimjibu mwanaye,



    "Kwa hiyo lini tena naenda Kuombewa?" Kayoza aliuliza,



    "Mchungaji amesema utakuwa unaombewa kila Siku kwa ajili ya kukujenga imani" Mama Kayoza alijibu,



    "Kwani mimi sina imani?" Kayoza aliuliza,



    "Yaani hauna kabisa, kwa ninavyofahamu mimi, hata ungekuwa na imani kidogo tu ungepona" Mama Kayoza alijibu,



    "Alafu kitu Kingine, hii habari ya tukio lililotokea juzi kwa Mchungaji lilivyotangazwa nchi nzima, hivi huoni hatari iliyopo mbele yangu?" Kayoza aliuliza,



    " mimi sioni tatizo, mbona hhakuna hata chombo cha habari kilichokuhusisha na hizo habari" Mama Kayoza alijibu,



    "sawa, ila ukae ukijua kuwa Polisi wana akili sana kuliko sisi raia wa kawaida" Kayoza alimwambia mama yake,



    "Wana akili kama sisi tu, mwenye akili kuliko sisi ni Mungu peke yake" Mama Kayoza aliongea kwa ukali kidogo,



    "Sasa mimi sijamaanisha hivyo mama" Kayoza alijitetea,



    "Mungu ni mkubwa kwa maana yoyote ile uliyoimaanisha" Mama kayoza alitilia mkazo maneno yake,

    "Alafu nasikia kama mlango unagongwa vile"Omary aliongea baada ya ukimya wa muda,



    "Hata mimi Nimesikia hivyo hivyo" Kayoza nae akamuunga mkono Omary



    "Sasa si mkafungue, mbona mmelegea hivyo nyie?" Mama Kayoza aliongea kwa ukali.



    Omary akasimama na kuelekea mlango ulipo, akaminya kitasa chini na kuvuta mlango, ile kufungua tu akakutana uso kwa uso na Sajenti Minja, Omary akarudishia mlango haraka na kukimbilia ndani............

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Omary alivyofungua na kufunga mlango, kisha akarudisha

    kichwa ndani, Sajenti Minja aliiona sura ya Omary na kupata mshtuko mkubwa sana, maana sura aliyoiona ndiyo ile ile inayotafutwa na serikali.



    Sajenti minja bado alikuwa na uoga kutokana na lile tukio la kutaka kunyonywa damu,

    kwa hiyo akabaki nje kaduwaa, huku anajiuliza

    pale ndio kwa dada yake, au kakosea nyumba

    kabla hajaamua chochote, akasikia mlango

    unafunguliwa tena, kwa haraka sana Sajenti

    Minja akatoa bastola yake, na kuilekezea mlangoni.



    "vipi tena kaka, unataka kuniua mwenzio" ilikua sauti ya Mama Kayoza baada ya kufungua

    mlango.



    "nimemuona kijana ndani ambae anatafutwa nchi

    nzima" Sajenti Minja akaongea kwa pupa huku bado akiwa anashangaa hali anayokutana nayo,



    "ndio, karibu basi kwanza ndani, alafu ndio ujue

    kwanini yupo hapa" mama kayoza aliongea kwa

    busara,



    "Haiwezekani kuingia humo, ngoja niwasiliane na Polisi makao makuu Shinyanga wake wanipe msaada" Sajenti Minja aliongea huku akiitoa simu yake mfukoni,



    "We Joel acha ujinga, unatapopiga simu na kuwaita polisi utakuwa umeniweka hatiani mimi na sio huyo kijana uliyemuona" Mama Kayoza aliongea na kumfanya Sajenti Minja asitishe zoezi lake,



    "Mbona sikuelewi Dada, unamaanisha nini kusema hivyo?" Sajenti Minja alimuuliza dada yake huku akimshangaa,



    "Twende ndani utanielewa tu" Mama Kayoza alimwambia Sajenti Minja,



    "Lakini dada ujue una hatari sana kuishi na Huyo kijana" Sajenti Minja aliongea kwa unyonge,



    "Twende ndani bwana" Mama Kayoza aliongea huku akiingia ndani na Sajenti Minja akaingia ndani huku akiongozwa na

    mama Kayoza, ila bastola yake, hakutaka kuificha tena, alivyoonekana, alikuwa amejiandaa

    kwa lolote litakalotokea

    Alipoingia sebuleni hakukuta mtu,



    "kaenda wapi?" Sajenti Minja akauliza kwa mshangao na wasiwasi,



    "baba vipi?!, mbona una haraka hivyo" mama

    kayoza aliongea huku akiwa anaelekea sehemu kulipokuwa na vyumba ambavyo wakina Kayoza walikimbilia kujificha. Alipofika katika mlango wa chumba cha wakina Kayoza, aligonga na mlango ukafunguliwa,



    "Haya twendeni mkamsalimie mjomba wenu" Mama Kayoza aliwaambia,



    "Mama mbona unataka kutupeleka matatizoni?" Kayoza aliongea huku akiwa ana hofu kuu,



    "Ebu twendeni uko, yule hana tatizo" Mama Kayoza aliongea na kuanza kutoka nje, nyuma yake alikuwepo Kayoza na Omary.



    Walipotokea sebuleni Sajenti Minja akawaelekezea bastola na kuwafanya wakina Kayoza kutaka kukimbia ila mama yao aliwahi kuwashika,



    "Mnakimbia nini nyie? Na wewe jiheshimu basi, kwangu ni mahali pa amani, hayo mabastola yako use unayatolea huko huko na sio hapa" Mama Kayoza aliongea kwa ukali huku anamuangalia Sajenti Minja,



    "ehe!, dada unaishi vipi na wauaji?" Sajenti Minja akamuuliza mama kayoza huku bado bastola yake ikiwa mkononi,



    "Ebu lifiche hilo libunduki lako ndio uhoji hayo maswali yako" Mama Kayoza alimwambia Sajenti Minja na Sajenti Minja akatii kwa kuirudisha bastola sehemu yake,



    "Dada mbona unawatetea sana, ni nani zako Hawa?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwaangalia kwa chuki wakina Kayoza,



    "hao ni wajomba zako, huyo hapo ndio kayoza, na

    huyo mwingine ni rafiki yake" Kama kayoza

    alimwambia sajenti Minja huku akiwaonyeshea

    kidole wakina Kayoza.



    "Kayoza? Kayoza mwanao au?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa ahamini kilichozungumzwa na dada yake,



    "Haswaa, Kayoza mwanangu ndio huyo" Mama Kayoza alijibu kwa furaha,



    "alah!, kayoza ndio kawa mkubwa hivi?" sajenti

    Minja alijishtukia kauliza bila matarajio.



    "kawa mbaba haswa" mama kayoza akajibu.



    Sajenti Minja akairudisha bastola yake kiunoni,

    kisha akamgeukia kayoza,



    "hujambo mjomba?" Sajenti Minja akamsalimia kayoza.



    "sijambo shikamoo" kayoza nae akamsalimia

    mjomba yake huku nae akiwa ahamini kinachotokea ingawa ni kweli aliambiwa Sajenti Minja ni ndugu yake,



    "marhaba, za siku?" Sajenti Minja akaendelea kumjulia hali Kayoza tena kwa uchangamfu kama hawakuwa maadui muda mfupi uliopita,



    "nzuri tu" kayoza akajibu.



    "unanikumbuka mimi?" Sajenti Minja akamuuliza kayoza,



    "sikukumbuki" kayoza alimjibu huku akitingisha kichwa kwa kukipeleka kushoto na kulia,



    "kalikuwa kadogo sana" Sajenti Minja alisema huku akimgeukia dada yake.



    "tena sana, kalikuwa na miaka sita, kipindi tulipoenda kumuona mimi na wewe kule kigoma" Mama kayoza akamjibu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ehe, kakuelezea sababu ya kufanya mauaji ya kutisha namna ile" Sajenti Minja akamuuliza dada

    yake,



    "yeye mwenyewe alikuwa hajui, hadi mimi nimemwambia ndio akajua" Mama Kayoza ndivyo

    alivyomjibu sajenti Minja. Sajenti akaonekana kushtuka kutokana na lile jibu kutoka kwa dada yake,



    "kwa hiyo wewe unajua

    sababu?" Sajenti Minja akamuuliza Mama Kayoza.



    mama kayoza akamuelezea mwanzo mpaka

    mwisho wa tatizo analokumbana nalo Kayoza.



    "Sasa utachugua mwenyewe umpeleke kwenye vyombo vya sheria au umlinde" Mama Kayoza alimaliza kwa maneno hayo na kumfanya Sajenti Minja ainamishe kichwa chini akitafakari,



    "Kwa hivyo unataka kuniambia kwamba huyu Kayoza hawezi kuwa mtu bila sababu mpaka huyo mtu mwenyewe stake kumdhuru?" Sajenti Minja aliuliza baada ya muda kidogo wa kutafakari,



    "Ndio hivyo na pia kama huyo mtu atataka avunje masharti ya mzimu" Mama Kayoza alijibu,



    "Kumbe nilikuwa nataka kumdhuru mtu asie na hatia, tens ndugu yangu" Sajenti Minja aliongea kwa masikitiko,



    "Na hayo majeraha usoni kwako ni ya nini?" Mama Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,



    "Hii ni adhabu ndugu yangu" Sajenti Minja alijibu,



    "Adhabu?, adhabu gani kama umepata ajali?" Mama Kayoza aliuliza,



    "Ndio adhabu zetu za kijeshi" Sajenti Minja alijibu,



    "Na ulifanya kosa gani mpaka upewe hivyo adhabu?" Mama Kayoza aliuliza kisha Sajenti Minja akaeleza mwanzo mpaka mwisho.



    "Kwa hivyo hii kesi ndio imekutesa hivyo" Mama Kayoza aliuliza,



    "Yaani nnilikubali kuirudia kwa sababu nilitaka nipate mwanya wa kukimbia nje ya nchi kabisa" Sajenti Minja aliongea,



    "Haya sasa, wewe kama mjomba kama baba, una maoni juu ya hili tatizo" Mama Kayoza alimuuliza Sajenti minja,



    "Hapa hakuna njia zaidi ya mganga, kwa maana hili tatizo limekaa kihasili hasili sana" Sajenti Minja akashauri kuwa ni lazima Kayoza

    apelekwe kwa wataalamu wa tiba za jadi,



    "Haiwezekani, atapelekwa kuombewa atapona tu" Mama

    Kayoza alipinga,



    "Ujue mama kwenda kwa mganga sio kupinga nguvu ya Mungu, inawezekana huko ndipo Mungu atatusaidia" Kayoza alimshauri mama yake,



    "Na pia tukienda kwa mganga sio mwisho wa kwenda kanisani, ikifika siku ya kwenda kanisani aende na ikifika siku ya kwenda kwenye tiba asili aende" Sajenti Minja aliongezea,



    "Sawa, maana cha muhimu ni mtoto kupona" Mama Kayoza alikubaliana na kaka

    yake na maongezi mengine yakaendelea huku Mama Kayoza akiandaa mezani chakula cha jioni.



    Baada ya chakula cha pamoja, Sajenti Minja alimwambia kayoza kuwa kesho atakuja

    kumchukua asubuhi, ampeleke kwa mzee mmoja

    ambae ni mganga anaefahamika pale Shinyanga.



    "Wewe si umekuja Leo tu, huyo mganga umemjulia wapi?" Mama Kayoza aliuliza kwa mshangao,



    "Shinyanga nimekaa sana na naijua vizuri sana kuliko unavyodhani" Sajenti Minja alijibu huku akicheka na kumfanya Mama Kayoza aishie kuguna tu,



    "Kwa hivyo umefikia wapi, au lodge?" Mama Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,



    "Kuna nyumba nimepewa na viongozi ambayo nitaishi kwa muda" Sajenti Minja alijibu,



    "Mi nikajua utaishi hapa bwana na ndio maana Jana ulivyonipigia simu na kuniambia unakuja sikutaka kuwaambia hata wanangu kuwa unakuja" Mama Kayoza aliongea,



    "Mimi naona niwaache, ila Kayoza jiandae kesho mapema nakuja kukuchukua ili nikupeleke kwa babu" Sajenti Minja aliongea huku akisimama,



    "Mbona unaondoka mapema, hata hukai tuongee ongee" Mama Kayoza alimwambia Sajenti Minja,



    "Ngoja niwahi kupumzika maana nnimechoka sana" Sajenti Minja aliongea na kisha akasindikizwa na Dada yake mpaka nje na kuondoka zake.



    ****************



    Kesho yake, sajenti Minja aliwai kufika pale kwa

    dada yake na kunywa chai kabisa, kisha Kayoza

    na Omari wakajitayarisha, saa nne iliwakuta wapo

    katika foleni ya kuingia kwa mganga,

    foleni ilikuwa ndefu.



    Baada ya kusubiri sana, muda wao ulifika na waliingia kuonana na

    mganga saa sita kasoro, mganga akawaambia

    kuwa tatizo lao ni kubwa, na wakitaka liishe, ni

    lazima wapeleke maiti ambae katoka mochwari.

    Ilikuwa ngumu, ila kwa ajili ya shida, wakasema wataipeleka usiku, mganga akasema itakuwa

    vizuri sana hiyo maiti ikifika usiku, ili kazi ianze usiku huo huo.

    Walipotoka kwa mganga wakaelekea moja kwa

    moja hospitalini, walipofika, Sajenti Minja

    akashuka ndani ya gari, kisha akaenda moja kwa

    moja hadi mochwari, akaongea na mzee mmoja hivi ambae ndiye alikuwa mlinzi wa kile chumba cha kutunza maiti na alimueleza

    kuhusu shida yake ni kutaka kupatiwa maiti moja, mara ya kwanza, babu

    anaetunza maiti alikuwa mgumu kukubali, ila

    alipoambiwa anapewa laki laki tatu, akakubali

    haraka, na akampa mbinu ambayo sajenti Minja

    atatumia kuchukulia maiti maiti usiku.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakampa babu pesa kiasi cha laki moja na wakakubaliana kuwa kiasi kilichobaki watammalizia usiku pindi watakapokabidhiwa maiti.



    Kisha wakaenda zao nyumbani kusubiri muda ufike.



    *****************



    Usiku ulipofika, Sajenti Minja na wakina Kayoza

    wakaenda nyuma ya chumba cha kuifadhia maiti,

    ilikuwa saa tano usiku, hata watu waliokuwa

    wanapita katika sehemu ya mochwari walikuwa

    wanahesabika,

    Yule babu mtunza maiti, akaingia ndani, akatoka

    na maiti amembeba mabegani, kisha akafungua

    geti la nyuma, akawakabidhi wakina Sajenti

    Minja, kisha akapewa pesa yake iliyobakia na kuwaachia maiti yao.



    Ile maiti waliiweka katika buti ya gari, kisha

    wakaanza safari ya kwenda kwa mganga. Ulikuwa usiku tulivu na ukizingatia kulikuwa nje ya nje, basi kulikuwa na hali ya kutisha kidogo kutokana na mapori machache maeneo Yale.



    Walipofika katika sehemu ambapo kulikuwa

    kumetulia na kulikuwa na kapori kidogo, ni umbali

    mdogo kutoka nyumbani kwav mganga aliyewaagiza maiti, walisimamishwa na gari

    ya polisi wa doria waliokuwa wanaimarisha ulinzi kile kipindi cha usiku.



    "mnaenda wapi?" askari mmoja akawauliza,



    "nyumbani" Sajenti Minja akajibu huku wasiwasi mwingi ukiwa umemtawala,



    "huku juzi tulipishana na watu nao tulipowauliza

    wakasema hivyo hivyo, kesho yake tukasikia

    majambazi yamepavamia na kuiba mali za watu, na nyie msije mkawa ni miongoni mwa hao waarifu" Askari yule akamwambia sajent Minja huku akiwa anawatilia mashaka,



    "sisi hatuwezi kuwa majambazi, afande" Sajenti

    Minja akajitetea,



    "hatuwezi kuwaamini, hadi tuwakague" yule askari aliongea huku akimulika upande wa ndani wa gari kwa kutumia tochi,



    "Sisi ni watu safi" Sajenti Minja aliongea huku ndani ya nafsi yake akiomba Askari wasikague buti ya gari,



    "Na huku kuna mini?" Askari mwingine aliongea huku akifungua buti ya gari na kuwafanya wakina Sajenti Minja waishiwe nguvu....



    ..."ebu toa lock ya buti" Askari yule akamuamrisha Sajenti Minja baada ya kufungua buti bila mafanikio.



    Sajenti Minja akaona akifanya uzembe kidogo,

    anaweza kuvuliwa nguo bila kutegemea, kwa

    maana kwa Sajenti kama yeye kukutwa na maiti

    ndani ya gari ni aibu kubwa.



    "unajua unaongea nani?" sajenti Minja akamuuliza yule askari wa doria kistaharabu,



    "haijalishi, kukujua wewe nani nadhani hakutasitisha kukukagua. fungua buti bwana" yule askari akaongea kwa ukali.



    "Ngoja nikuoneshe kitambulisho changu" Sajenti Minja akatoa kitambulisho chake, akamtupia yule

    askari,



    "alafu inaonekana una jeuri sana kijana?, unamtupia nani likitambulisho lako?" yule afande

    akawa anaongea huku akiwa anamfuata Sajenti Minja akiwa na gadhabu, alipomfikia, yule askari

    akamtandika sajenti Minja kibao cha nguvu.



    "haya okota likitambulisho lako na unipe mikononi, sio unirushie, umeona mi limbwa

    eeh!?", yule askari wa doria akahoji kwa ukali mpaka mate yakamtoka,



    Sajenti Minja akaona asilete mabishano wakati wanachelewesha kazi kwa mganga, akakubali kuwa mjinga, akakiendea

    kile kitambulisho, akakiokota kisha akampatia yule askari wa doria.



    Yule askari akakipokea,

    akashtuka baada ya kukiangalia kwa nje, maana kilikuwa cha kipolisi, alipokifungua kwa ndani, akakisoma ndani, kisha

    akammulika Sajenti Minja na tochi usoni, ghafla

    akampigia saluti, wale askari aliokuwa ameongozana

    nao, kuona hivyo, nao wakampigia saluti Sajenti Minja.



    "samahani sana mkuu, mi sikujua kabisa" yule

    askari wa doria aliongea huku sura yake

    ikionesha kama anataka kulia kutokana na hofu aliyokuwa nayo,



    "usijali, ndio kazi inatakiwa kufanywa hivyo" Sajenti Minja ndivyo alivyomjibu, kisha

    akamuuliza, "bado unataka nifungue buti?"



    "ha...hapa...hapana mkuu" yule askari wa doria akajibu kwa sauti iliyojaa kitetemeshi.



    "Kwa hivyo mnaweza kuturuhusu twende?" Sajenti Minja aliwauliza,



    "Nenda tu mkuu, samahani sana kwa usumbufu" Askari alijibu huku akimrudishia Sajenti Minja kitambulisho chake.



    Sajenti Minja akakipokea kitambulisho chake na wakaingia ndani ya gari, kisha wakaendelea na safari yao.



    "wajomba pale bila kutumia akili tulikuwa tunaumbuka" Sajenti Minja alianzisha maongezi baada ya kuondoka eneo walilosimamishwa,



    "Mimi ndio nilikuwa nimekata tamaa kabisa" Omari nae akachangia,



    "Mimi akili niliyokuwa nayo ilikuwa ni kutoka nduki tu" Kayoza aliongea na kufanya wenzake wacheke,



    "bila ya kitambulisho, sasa hivi sijui tungekuwa

    wapi?" Sajenti Minja akasema huku akiwa anaipaki gari nje ya nyumba ya mganga.



    Wakashuka, kisha wakaenda hadi mlangoni kwa

    mganga, wakabisha hodi, wakafunguliwa na

    msaidizi wa mganga,



    "sisi tulijua hamuwezi kuja tena, maana giza limekuwa kubwa sana" Msaidizi wa Mganga

    aliwaambia baada ya kuwagundua,



    "tulipata matatizo kidogo njiani, ila yameisha" Sajenti Minja aliongea huku akiwa anaingia ndani na nyuma yake wakina Kayoza wakimfuata.



    "Sasa itabidi ifanyike ingawa tumechelewa kidogo" Mganga aliongea baada ya kuwaona,



    "Itakuwa vyema sana" Sajenti Minja aliongea,



    "Sasa huyo kijana mwenye tatizo inabidi asogee hapa tumfanyie mambo kidogo" Mganga aliongea huku akitandika kitambaa cheusi chini. Kayoza akasogea na kuambiwa Amalie kile kitambaa cheusi na mganga akaanza kufanya matambiko.



    Baada mganga kumaliza matambiko madogo pale

    nyumbani, wale wasaidizi wa mganga, walikuwa

    wanne, wawili wakambeba yule maiti na wawili

    wengine wakabeba vifaa vya uganga, hapo

    ilikuwa saa sita na dakika zake za kutosha,

    mganga akawa anaongoza msafara.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Hizi sehemu zinatisha ila mnabidi mzizoee" Mganga aliwaambia wakina Sajenti Minja wakati wakiwa njiani,



    "Hizi sehemu za kutisha nimeshazizoea sana, labda vijana wangu hapa ndio wageni" Sajenti Minja alijibu,



    "Kwa hivyo mambo haya ya kutembea kwa waganga ushayazoea sana?" Mganga alimuuliza Sajenti Minja,



    "Hapana, kwa masuala ya kiganga mi ndio mara yangu ya kwanza" Sajenti Minja alijibu,



    "Sasa hata mazingira ya kutisha umeyazoeaje?" Mganga aliuliza,



    "Kutokana na kazi zetu mzee wangu" Sajenti Minja alijibu,



    "Kwani nyie mnafanya kazi gani?" Mganga aliwauliza,



    "Hao vijana wangu wanasoma chuo, mimi ni muangaikaji tu wa sehemu mbalimbali katika kutafuta ridhiki" Sajenti Minja alijibu,



    "Sasa kama huyu kijana mwenye matatizo yupo Chuo huko chuo anaishi vipi na chuo mzimu" Mganga alihoji,



    "Matatizo matatizo tu na ndio maana tumemleta hapa" Sajenti Minja alijibu na ukimya ukatawala tena njiani.



    Walitembea mda wa saa nzima hadi sehemu za makaburini.



    " inabidi tuchague kaburi moja ambalo limetengenezwa vizuri na liwe la mwanamke" Mganga alitoa maelekezo na wale wasaidizi wake wakatawanyika kila mmoja na upande wake wakitafuta hilo kaburi zuri alilozikwa mwanamke.



    "Naona hili hapa linafaa" Msaidizi mmoja wa mganga alipaza sauti na watu wote wakaelekea eneo alilopo.



    Walipofika katika kaburi moja lililosakafikiwa

    vizuri, Mganga alilidhika nalo baada ya kuona kila anachokihitaji kipo.



    Mganga akawaamuru wasimame, kisha

    akachukua kikapu cha uganga akatoa vifaa vyake

    akavipanga kulizunguka lile kaburi,



    "Were kijana njoo ulale hapa juu ya hili kaburi" Mganga alimwambia kayoza,



    "Mi naogopa mzee" Kayoza aliongea huku akiwa na wasiwasi,



    "We mpumbavu mini, ebu lala hapo kabla sijakuchapa makofi, we unafikiri utaponaje kama ukikahidi maneno ya mganga" Sajenti Minja aliongea kwa ukali, Kayoza akakubali kulala hivyo hivyo huku aakitetemeka.



    Baada ya Kayoza kulala juu ya kaburi, mganga akammwagia madawa yake Kayoza kichwani, haikuchukua

    hata dakika moja, Kayoza akapoteza fahamu na kulala kama maiti,



    "Haya mchukueni huyo maiti na mumlaze pembeni ya huyo kijana" Mganga akawaamuru wasaidizi wake

    wamchukue yule maiti na kumlaza pamoja na

    kayoza, wasaidizi wakatekeleza agizo.



    "Kazi ndiyo inaanza, sharti kubwa na la kuzingatia ni kwamba kazi itakapoanza haitatakiwa ionekane damu ya kitu chochote kile" Mganga aliongea,



    "Hata ya mbu?" Sajenti Minja aliuliza kutokana na eneo like kuwa na mbu wengi,



    "ndio, kama mbu atakung'ata hata usimuue, maana ukimuua ile damu yake inaweza kuwa tatizo kwetu" Mganga aliongea kwa msisitizo,



    "Na ikionekana ni kipi kitachotokea?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Huu mzimu tunaoutoa hapa, nguvu zake zipo kwenye damu ya kila kiumbe, kwa hiyo damu itakapoonekana, mzimu atapata nguvu na kati yetu hapa hakuna atakayepona" Mganga alitoa Maelezo,



    "Hilo litawezekana" Sajenti Minja alijibu,



    "Na pia kama mtu ana kidonda ajitahidi akizibe kisionekane" Mganga alitilia mkazo,



    "Basi kazi ifanyike tu, naona Maelezo yako yamejitosheleza" Sajenti Minja aliongea,



    "Kwa hiyo hapa kazi inayofanyika ni kuutoa huu mzimu kutoka kwa kijana wenu na kuuingiza katika maiti alafu kazi itayofuata ni kuizika hivyo maiti pamoja na mzimu" Mganga alimaliza.



    Mganga akaanza kazi yake, alimwaga madawa

    eneo lote, kisha akaanza kuongea lugha

    anayoijua yeye, alifanya kwa nusu saa, kisha

    likatokea dubwana la ajabu kwenye mwili wa

    Kayoza, kila mtu alipata uoga isipokuwa mganga tu.



    Sasa like dubwana likawa kama linavutwa kutoka kutoka kwenye mwili wa Kayoza, ila likawa

    halitaki,

    hiyo hali ilienda kama saa nzima, mganga

    akaanza kuona mafanikio, lile dubwana lilishatoa

    mwili mzima ikawa bado miguu, na mwisho hadi miguu ilitoka na likaanza kudumbukia katika ile maiti.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mara ghafla panya akatokea

    kichakani, alikuwa kama anakimbizwa na kitu,

    akawa anaelekea kwenye miguu ya Omary, katika

    jitihada za kumkwepa, Omary akajikuta anamkanyaga yule Panya,

    damu ikaenea katika viatu vya Omari, mganga

    aliliona lile tukio,

    akajikuta anasema kwa sauti iliyokata tamaa



    "tumekwisha...".



    Na wakati huo huo mzimu ukachomoka kutoka katika mwili wa maiti na huku ukifoka kwa hasira kiasi kwamba ndege na wadudu walioloala maeneo Yale ya makaburini waliamka na kukimbia hovyo..............



    *Je mganga atafanikiwa kuutuliza mzimu uliokuwa na hasira ya kudhuriwa au mzimu ndio utawamaliza wote waliotaka kumdhuru?



    ******ITAENDELEA*******

0 comments:

Post a Comment

Blog