Search This Blog

KIJIJINI KWA BIBI - 3

 







    Simulizi : Kijijini Kwa Bibi

    Sehemu Ya Tatu (3)



    ILIPOISHIA...

    ______________

    Mara ghafla panya akatokea

    kichakani, alikuwa kama anakimbizwa na kitu.



    akawa anaelekea kwenye miguu ya Omary, katika

    jitihada za kumkwepa, Omary akajikuta anamkanyaga yule Panya,

    damu ikaenea katika viatu vya Omari, mganga aliliona lile tukio,

    akajikuta anasema kwa sauti iliyokata tamaa



    "tumekwisha...".



    Na wakati huo huo mzimu ukachomoka kutoka katika mwili wa maiti na



    huku ukifoka kwa hasira kiasi kwamba ndege na wadudu walioloala



    maeneo Yale ya makaburini waliamka na kukimbia hovyo..............



    ___________

    ENDELEA

    ___________



    "Hapa sijui kama tutapona" Mganga alitamka maneno hayo, huku akiwa

    kama anajitayarisha na pambano jingine.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mzimu ulipiga kelele zilizowatisha watu wore pale, kisha ulirudi



    kwa kasi ndani ya mwili wa Kayoza, kisha Kayoza

    akanyanyuka taratibu, alikuwa tayari

    keshabadilika, alikuwa anaogepesha ukimtazama msoni, macho yalikuwa



    meupe yasiyo na mboni na meno ya mbele pembeni yalikuwa marefu kama



    ya mnyama simba.



    Kayoza akawatazama wote, alafu akawa

    anamfuata Omari, Omari kuona hivyo, mkojo

    ukaanza kumtoka na hata kukimbia akawa anashindwa ila alibaki



    ametoa macho huku machozi yakimtoka ingalikuwa halii.



    Kayoza alipomfikia Omary

    akamuangalia kisha akaachane nae, sasa akawa

    anafuata mganga ambaye muda wote alikuwa bado anafanya mambo yake



    ya kiganga kwa ajili ya kujaribu kuutuliza mzimu wa Kayoza.



    Mganga baada ya kuona mzimu unamfuata, maamuzi aliyoyachukua ni



    kutoka tu

    mbio, akasababisha na watu walikuwepo katika

    hilo eneo nao watoke mbio

    mganga hakufika hata mbali, Kayoza akamkamata,



    "Wewe ni nani mpaka utake kunitoa katika nyumba yangu?" Mzimu



    ulimuuliza mganga huku ukiwa umemkaba katika shingo na kusababisha



    kucha zake ndefu zipenye kwenye shingo ya mganga,



    "Mi...mii..nimeagi..zwa tu na ndugu za...ko" Mganga aliongea kwa



    tabu huku damu zikimchuruzika shingoni.



    Ila pamoja na utetezi wake ule mzimu ulimbeba juu na kung'ata



    shingoni kisha aakaanza kumnyonya damu, alipomaliza akamtupa



    pembeni.



    Kisha mzimu ukatoka mbio na kuwakuta wasaidizi wa mganga wakiwa



    wanakimbia na wale

    wasaidizi wake pia wakanyonywa damu.



    Kisha Kayoza akamfuata sajenti Minja, ambae yeye alikimbia ila



    mwisho akaamua asimame tu maana aliona hata kama akikimbia ni



    lazima tu akamatwe.



    Mzimu akamkamata mkono Sajenti Minja alafu akawa anamvutia

    kichakani sehemu ambayo kulikuwa na miti mingi, alipofika katika



    eneo lenye miti,



    "Usipate kichwa kwa kuwa niliahidi kutoidhuru damu yenu, wewe ndiyo



    utasababisha nivunje ahadi yangu" Mzimu uliongea huku

    Ukikata fimbo, na kisha ukaanza kumtandika Sajenti Minja,



    alimtandika

    kisawa sawa, mpaka sajenti Minja akawa analia kama mtoto.



    Mzimu uliporidhika na bakora alizozipata Sajenti Minja ukamuachia



    na Sajenti Minja akatoka mbio kama mwendawazimu na kuishika ile



    njia waliyokuja nayo ambayo ilikuwa inaelekea nyumbani kwa Mganga.



    Mzimu ulipomuachia Kayoza, Kayoza akadondoka chini kama kifurushi



    na akapoteza fahamu.



    Omary yeye baada ya kuachwa na mzimu wala hakukimbia, alikuwa



    anaangalia tu unyama unaofanywa na mzimu na hata wakati Kayoza



    anaanguka na kupoteza fahamu Omary aliona na akaamini tayari mzimu



    umemuachia rafiki yake, Maamuzi aliyoyachukua Omary ni kwenda kumpa



    msaada Kayoza, alipofika, akambeba Kayoza kisha akawa kwenda



    walipoacha gari lao ambapo ni nyumbani kwa Mganga.



    Walifanikiwa kufika salama nyumbani kwa mganga na wakamkuta Sajenti



    Minja anaangaika kufungua mlango wa gari ili aingie,



    "Vipi huyo tayari au bado?" Sajenti Minja alimuuliza Omary baada ya



    kumuona anakuja na Kayoza,



    "Tayari amerudi katika hali yake" Omary alijibu huku akifungua



    mlango wa gari na kumuingiza Kayoza,



    "Aisee hii siwezi kuisahau" Sajenti Minja aliongea huku akiwasha



    gari na kuiondoa kwa kasi.



    "Hii ilikuwa hatari, ila wewe hajakudhuru" Omary aliongea huku



    akijua fika Sajenti Minja alipewa bakora zisizo kuwa na idadi,



    "Usiseme hivyo wewe, dah yaani nimefanywa mtoto Leo, tena mtoto wa



    shule" Sajenti Minja aliongea kwa huzuni,



    "Umefanywaje kwani mjomba?," Omary aliuliza huku akimcheka



    kimoyomoyo,



    "Hata kuhadithia siwezi, ni kitendo cha aibu sana" Sajenti Minja



    aliongea,



    "Si uniambie tu mjomba" Omary alikazania huku akiendelea kumcheka



    moyoni,



    "Nitakuambia tukifika bwana" Sajenti Minja alijibu huku akiongeza



    mwendo wa gari.



    *****************



    Katika hospitali ya mkoa kulikuwa na kasheshe

    kubwa sana, kuna watu waliambiwa ndugu yao

    amefariki, ila walipoenda monchwari hawakuikuta

    maiti ya ndugu yao, walipowafata madaktari

    wakawathibitishia kuhusu kifo cha ndugu yao, na

    hata babu wa monchwari alithibisha kupokea maiti

    ya huyo ndugu yao, sasa cha ajabu maiti ikawa

    haionekani

    Polisi walipofika pale hospitali, wakamchukua

    babu wa mochwari huku wakiwa na uhakika kuwa

    huyu mzee anahusika kwa namna moja au nyingine

    katika upotevu wa ile maiti.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Babu akachukuliwa hadi kituoni, walipomfikisha

    wakaanza kumuhoji,



    "Mzee kuwa mkweli, tuambie huo mwili umeupeleka wapi?" Askari



    alimuuliza Babu wa monchwari,



    "Yaani hata mimi sielewi, ule mwili kweli niliupokea ila hata



    ulivyopotea mimi sijui" Babu alijibu kwa kujiamini,



    "Kwani walinzi mpo wangapi pale monchwari" Askari aliuliza,



    "Tupo wawili" Babu alijibu,



    "Umesema wewe ndiye uliupokea mwili, he wakati mwili unapotea



    ilikuwa zamu ya nani kulinda?" Askari akaendelea kuuliza,



    "Yaani huo mwili niliupokea Jana saa mbili usiku, na imeonekana



    haupo Leo saa kumi na mbili alfajiri" Babu alijibu,



    "Ilikuwa zamu ya nani?" Askari aliuliza,



    "Zamu yangu" Babu alijibu,



    "Babu acha kutuchanganya, inaonesha wewe unajua kila kitu kuhusu



    kupotea kwa huo mwili" Askari aliongea huku akitabasamu ili



    asimtishe Babu,



    "Unadhani nakutania mjukuu wangu?, kweli mimi sijui kitu,



    inawezekana mile chumba cha monchwari kina wachawi, si unajua



    wachawi wanazipenda sana maiti" Babu alijitetea na kumfanya askari



    acheke,



    "Babu sema kweli usiogope, hata kama umeusika hatuwezi kukufunga,



    maana utakuwa kama shahidi, na si unajua shaidi hafungwi?" Askari



    alimlainisha Babu huku akiendelea kucheka,



    "Kweli hamuwezi kunifunga?" Babu aliuliza huku akimuangalia Askari,



    "Kama utamtaja muhusika hautofungwa mzee, ila ukishikiria msimamo



    wako wa kuficha ndio utakaokuingiza matatizoni" Askari alimwambia



    babu wa monchwari,



    "Kusema ukweli aliyeuchukua ule mwili namjua kwa sura ila jina



    simjui" Babu aliamua kusema ukweli,



    "Anakaa Wapi?" Askari aliuliza,



    "Sijui ila nikimuona tu sura yake namjua hata kama nikitoka kulala"



    Babu aliendelea kukazania maneno yake,



    "Kulikuwa na makubaliano yoyote kati yenu mpaka auchukue huo



    mwili?" Askari aliuliza,



    "Hapana aisee" Babu alikataa,



    "Sasa alichukuaje na wakati wewe mlinzi ulikuwepo?" Askari



    aliendelea kumbana kwa maswali,



    "Alikuja na bunduki akanitishia, kisha akaingia ndani na kubeba



    maiti" Babu wa monchwari aliamua kusema uongo,



    "Sasa kwa nini tokea mwanzo hukusema hivyo?" Askari aliuliza huku



    akimuangalia usoni,



    "Nilikuwa siamini kama mtaniamini" Babu alijibu,



    "Sawa babu, itabidi urudi ndani" Askari aliongea huku akisimama,



    "Ndani tens kufanya mini?" Babu aliuliza kwa kuamaki,



    "Utatoka tu babu, ila kwa sasa mtuhumiwa bado unahesabika ni wewe



    mpaka apatikane huyo mwingine unaedai alikuvamia na bunduki" Askari



    aliongea na kubonyeza kitufe kilichopo mlangoni na mlango



    ukafunguka wakaingia Askari wengine wawili,



    "Mpelekeni selo" Askari aliwaamrisha wenzake ambayo walimshika babu



    huku na huku na kutoka nae nje.



    wanamtoa katika chumba cha mahojiano, ili

    wampeleke rumande.



    ****************



    Mida ya saa tano asubuhi, ndio sajenti Minja

    alikurupuka, akaangalia simu yake, akukuta

    missed call 12 za mkubwa wake wa polisi,

    akawaamsha wakina Kayoza, kisha wakaenda

    kujiswafi, wakatengeneza chai wakanywa.

    Sajenti Minja akawarudisha wakina Kayoza kwa

    mama Kayoza, kisha yeye akawa anaelekea

    kituoni,

    alipofika, akapaki gari lake kisha akawa anaenda

    katika ofisi ya mkubwa wake, katika kolido ya

    ofisi akapishana na askari watatu waliokuwa

    wamemfunga pingu mzee mmoja ambae sura

    yake haikuwa ngeni kwake yeye Sajenti Minja, ikabidi

    ageuke amwangalie tena, na yule mzee nae

    akageuka kumuangalia sajenti Minja, ndipo

    sajenti Minja akamkumbuka, ni yule mzee mochwari na hapo pia ndipo



    yule mzee monchari akamkumbuka kuwa yule wanaepishana nae ndiye



    aliyemuuzia maiti na kumsababishia madhira Yale, Babu wa Monchwari



    akasimama huku akiwa bado amemgeuzia shingo Sajenti Minja ....



    ...yule babu wa mochwari akasimama, "vipi we mzee, songa mbele"



    askari mmoja akaongea kwa hasira.

    "taratibu wanangu, nimemuona mtu kama aliekuja kununua ile maiti"



    yule babu akaongea kwa matumaini huku shingo yake akiitoa kwa



    Sajenti Minja na kuwageukia wale maaskari,



    "yuko wapi?" askari mwenye hasira akauliza.

    Yule babu akageukia ile sehemu aliyokuwepo sajenti Minja ili



    awaoneshe maaskari,



    "kha!," yule babu akajikuta anashtuka kwa mshangao baada ya



    kutomuona tens Sajenti Minja,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "vipi babu?, tuoneshe haraka, unatuchelewesha" yule askari mwenye



    hasira akauliza huku amemtolea macho babu,

    "alikuwepo pale" yule babu akasema huku akionesha lile eneo



    alilokuwepo Sajenti Minja.

    "kwa hiyo hayupo?", yule askari mwenye hasira akahoji.

    "alikuwepo pale", Babu akajitetea.

    "hujanijibu bado, kwa hiyo hayupo" yule askari aliuliza tena huku



    akiwa na shauku ya kufanya kitu.

    "ndio mwanangu" Babu akajibu kwa upole.

    Bila kutegemea, babu alipigwa mtama mmoja mkali sana, akaangukia



    makalio.

    "unatuchelewesha majumbani kwetu, hatujalala na wake zetu tokea



    juzi usiku" askari mwenye hasira aliongea huku akimnyanyua babu



    babu baada ya kumpiga mtama.



    Sajenti Minja akacheka tu baada ya kushuhudia ule mtama aliopigwa



    babu kisha akaishia kujiuliza ni kwanini babu amekamatwa, akajiona



    mkosaji kwa kukimbia kwa maana yeye angeweza kuwa msaada wa babu,



    pia akaona alichokifanya kinaweza kubwa sahihi zaidi kwa kuwa



    huenda Babu atakuwa amekamatwa kutokana na kesi ile ya kuiba maiti,



    yaani inawezekana kabisa ndugu wa marehemu wamegundua kuwa



    wameibiwa, na mwisho akajisemea itabidi achunguze ni kitu



    kilichofanya mpaka yule babu awe katika mikono ya polisi.



    "Vipi mbona una mawazo hivyo?" Askari mmoja aliyekuwa anatoka



    msalani alimuuliza Sajenti Minja aliyekuwa amezama katika bahari ya



    tafakuri,



    "Ah, si unajua tena mawazo ni kawaida kwa binadamu" Sajenti Minja



    alijibu baada kushtuka kutoka katika lindi la mawazo,



    "Wewe ni mgeni kituoni hapa? Maana sura yako sijawahi kuiona" Yule



    askari alimuuliza Sajenti Minja,

    "Kabisa, inaelekea kila mtu anaefanya kazi hapa umemkariri?"



    Sajenti Minja aliuliza,

    "Yaani wote, sisi ndio wakongwe wa hapa" Yule askari alijibu huku



    akitabasamu,

    "Sawa bwana, mimi ndio nawasili muda huu kuja kuripoti kwa mara ya



    kwanza" Sajenti Minja aliongea huku nae akitabasamu,



    "Bila shaka wewe ndiye Joel Minja?" Yule Askari aliuliza,

    "Haswaa, umenijuaje?" Sajenti Minja aliuliza,

    "Tuliambiwa Leo kuna ugeni wa askari mpelelezi kutoka Dodoma" Yule



    askari aliongea,

    "Basi ndio huyo" Sajenti Minja aliongea,

    "Umeshafika ofisini kwa mkuu?" Yule Askari aliuliza,

    "Bado, yaani hapa ndo mahala pa kwanza kufika" sajenti Minja



    aliongea na wote wakacheka,

    "Sasa ofisi ya mkuu unaijua?" Yule askari alimuuliza,

    "Nitaijulia Wapi mimi?" Sajenti Minja alijibu,

    "Sasa ungefikaje" Yule askari aliuliza,

    "Ningefika tu, ila kwa kuwa nimekutana na wewe, mambo yatakuwa



    sawa" Sajenti Minja aliongea,

    "Twende nikupeleke" Yule askari akaongea huku akitangulia mbele



    Wakatoka katika eneo la chooni, akawa anaelekea katika ofisi ya



    mkubwa wake, walipofika yule askari aliyempeleka hakutaka kuingia,



    aliishia mlangoni na kuondoka zake na kumuacha Sajenti Minja



    mlangoni.



    Sajenti Minja akapiga hodi kisha akaingia, aliporudishia mlango,



    akampa heshima yake mkuu wa polisi,

    "kaa hapo sajenti" Mkuu wa polisi wa shinyanga alimuelekeza sajenti



    Minja sehemu ya kukaa.

    sajenti Minja akasogeza kiti, kisha akakaa.

    "habari yako Minja" Mkuu wa polisi akamsalimia.

    "nzuri tu, shikamoo mkuu" sajenti Minja akajibu.

    "Marhaba, Leo ndio siku ya kwanza kuwasili kituoni hapa" Mkuu wake



    alimuuliza huku akiwa jibu analo kabisa,

    "Naam mkuu" Sajenti Minja alijibu kikakamavu,

    "Vizuri sana, na kilichokuleta huku nadhani unakijua" Mkuu wake



    aliuliza tena,

    "Ndio mkuu" Sajenti Minja alijibu,

    "Tukupatie Askari wa huku ili msaidiane au wewe una pendekezo



    Gani?" Mkuu wake alimuuliza,

    "Naimani peke yangu nina uwezo wa kufanikisha" Sajenti Minja



    alijibu,

    "Kwanini hutaki msaada?" Mkuu wake aliendelea kumbana,

    "Kwa sababu hata niliyofikia katika upelelezi wa hii kesi ni hatua



    nzuri, sasa ukinipa mtu wa kusaidiana nae itakuwa kama tunaanza



    upya kwa kuwa atakuja na mipango, mbinu na mawazo tofauti kuhusu



    hii hii kesi" Sajenti Minja alijibu,,



    "Lakini kumbuka umoja ni nguvu" Mkuu wake aliongea huku



    akitabasamu,



    " hilo nalijua mkuu, nitapohitaji msaada nitakwambia" Sajenti Minja



    aliongea,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Kesi unayoifuatilia umeishia nayo wapi?" Mkuu wake aliuliza,



    "Kwa kweli hata niliyopiga ni ndogo sana, bado nahitaji mwanga



    zaidi ili hata nijue wa kumtia hatiani" Sajenti Minja aliongea,



    "Sawa, basi hapa nna habari ambazo zinaweza kukupa mwanga kidogo"



    Mkuu wake aliongea na kumfanya Sajenti Minja atege masikio vyema,



    "Habari zipi hizo mkuu?" Sajenti Minja aliuliza,



    "leo asubuhi wasamalia wema walitoa taharifa za kuwepo watu wanne



    ambayo walikuwa wana alama ya kung'atwa shingoni na kitu kama



    mnyama mwenye meno makali, tulipoenda tuliweza kukuta watatu



    waliokuwa wamenyonywa damu makaburini, ila habari nzuri mmoja wapo



    amekutwa yuko hai, lakini hali yake sio nzuri, ni wa leo au wakesho



    muda wowote anaweza kufa", Mkuu wa Polisi aliongea huku akiangalia



    baadhi ya makabrasha yaliyopo mezani kwake,

    Sajenti Minja alivyosikia habari ya watu kukutwa wakiwa wamekufa



    kwa kunyonywa damu eneo la makaburini, moja kwa moja akajua kuwa ni



    yule mganga na wasaidizi wake, ila habari ya mmoja kuwa hai ndio



    hakuipenda,

    "ndio, nakusikia mkuu" sajenti Minja akajibu baada ya ukimya wa



    muda mfupi,

    "Sasa kwa fikra zangu za haraka haraka haya mauaji nayafananisha na



    yanayofanywa na mtu unaemtafuta kwa maana hata wale watu waliokutwa



    wamekufa katika geti la mchungaji walikuwa hivyo hivyo na hizo



    alama shingoni" Mkuu wake alitoa maelezo,

    "Nadhani kwa kuwa huyu mmoja yupo hai basi anaweza kutusaidia



    tukapata mwanga kidogo" Sajenti Minja aliongea huku moyoni akiwaza



    hata huyo mtu afe,



    "Sasa hivi yupo sehemu ya wagonjwa mahututi amepumzishwa, jioni



    tutaenda kuongea nae" Mkuu wake aliongea,



    "Litakuwa jambo jema sana" Sajenti Minja aliongea,



    "sasa ni hivi tutatoka mimi na wewe hadi katika ofisi za akari



    wengine ili nikutambulishe, alafu jioni ndio tutaenda hadi



    hospitali ili tuchukuwe maelezo ya huyo aliebakia, maana anaweza



    kutupa pa kuelekea" mkuu wa polisi alimalizia kuongea huku



    akisimama,

    "sawa mkuu" sajenti Minja akajibu.



    Walitoka nje ya ofisi ya mkuu na kisha muda huo sajenti Minja



    akaanza kutembezwa katika ofisi za askari wa ngazi mbalimbali ili



    atambulishwe kwa wenzake hao, na kisha pia alizungushwa katika



    mazingira yote ya eneo like la Polish kwa ajili ya kupata kuyaona



    ili hata akitoka nje ajue duka linapatikana wapi? vyoo vinapatikana



    wapi na mambo mengine yanayolizunguka eneo lile.

    Baada ya Mkuu wake kuridhika aliamua na kumpeleka katika ofisi



    ambayo Sajenti Minja ataitumia muda wote ambao atakuwepo pale na



    kisha wakaagana huku wakikumbushiana kuwa jioni ni lazima waende



    hospitali kumuona huyo mtu aliyebakia ya wenzie kunyonywa damu,



    Sajenti Minja hakupenda kabisa hyo safari ila hakuwa na la kufanya,



    ilibidi atimize matakwa ya kazi yake.



    ************************



    Jioni ilifika haraka sana kwa upande wa Sajenti Minja, alitamani



    hata isifike kabisa.

    Mkubwa wake alimpitia na wakatoka eneo la kituoni.

    Baada ya kutoka kituo cha polisi, sajenti Minja na mkuu wake



    wakafunga safari hadi hospitali, njia nzima sajenti Minja alikuwa



    anatetemeka, alijua fika kuwa anaenda kuumbuka mbele ya mkuu wake,

    "vipi Minja, mbona unatetemeka sana?" mkuu wa polisi akauliza.

    "leo nimeamka na homa, kwa hiyo sijisikii vema kabisa" sajenti



    Minja alidanganya.

    "itakuwa malaria, tukifika itabidi upime kabisa" mkuu wa polisi



    alimshauri Sajenti Minja.



    Gari ilipofika, sajenti Minja na Mkuu wa polisi wakatelemka kisha



    wakawa wanaelekea sehemu ilipo wodi za wagonjwa mahututi, walitumia



    dakika mbili mpaka kufika katika chumba ambacho alilazwa yule



    msaidizi wa Mganga ambae alikuwa amenusurika na kifo, ila chumba



    kilikuwa kitupu,



    "Eh, mbona hayupo, ameshakufa nini?" Mkuu wa polisi aliuliza huku



    akitoa macho kuangaza bila mafanikio. Kwa upande wa Sajenti Minja



    hiyo habari ilikuwa nzuri, alijikuta anatabasamu waziwazi mbele ya



    Mkuu wake,



    "Mbona unacheka, unafurahia kumpoteza shahidi?" Mkuu wake



    alimuuliza kwa mshangao,

    "Hapana mkuu, nacheka unavyopeleka imani yako katika kifo wakati



    hata hujaenda kuuliza kwanza kwa madaktari" Sajenti Minja



    alijitetea kwa njia ya uongo,



    "Kweli bwana, ebu twende tukaulize" Mkuu wake aliongea huku



    akielekea upande zilizopo ofisi za madaktari na huku Sajenti Minja



    akiendelea kuomba wakifika waambiwe yule bwana amekufa.

    Baada ya sekunde kadhaa walitokea sehemu zilipo ofisi za madaktari,



    ila kwa bahati nzuri hata kabla hawajaingia ndani, walikutana na



    Daktari ambae ndiye anayesimamia matibabu ya msaidizi wa Mganga,



    "Ooohoo kamanda umeshawasili?" Daktari aliongea huku akimpa mkono

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mkuu wa polisi,



    "Vipi kuna wema kweli? mbona mgonjwa wetu hayupo kule katika wodi



    aliyokuwepo asubuhi?" Mkuu aliuliza huku akionesha wasiwasi,



    "Wema upo, tens mkubwa sana" Daktari alijibu huku akicheka,



    "Hapo kidogo umenipa nguvu, haya niambie huo wema" Mkuu aliongea



    huku akiwa bado yupo makini kumsikiliza Daktari,



    "Mgonjwa wako amepata nafuu na hata kuongea anaongea" Daktari



    alitoa habari zilizokuwa nzuri kwa Mkuu wa polisi ila hizo hizo



    habari zilikuwa mbaya sana kwa Sajenti Minja,



    "Mmempeleka wapi sasa?" Mkuu wa Polisi aliuliza,



    " yuko katika wodu ileee" Daktari aliongea huku akiwaelekeza kwa



    kidole katika wodi ambayo amehamishiwa msaidizi wa Mganga.



    Sajeni Minja na Mkuu wa Polisi baada ya kumshukuru Daktari wakawa



    wanaelekea kwenye wodi aliyokuwamo yule msaidizi wa mganga huku



    Sajenti Minja mapigo yake ya moyo yakiongezeka kasi.



    wakaingia ndani ya wodi, kisha wakawa wanaelekea kwenye kitanda cha



    yule msaidizi wa mganga, hapo Sajenti Minja moyo ulikuwa unamkimbia



    ajabu, akatamani hata sura yake ibadilike au akatamani hata yule



    msaidizi wa Mganga awe amepoteza kumbukumbu zake, lakini haikuwa



    hivyo.



    Walipofika katika kitanda cha yule msaidizi wa mganga, wakakuta



    kalala huku kawapa mgongo, yule mkuu wa polisi akamshika bega kwa



    lengo la kumuasha, yule msaidizi wa Mganga akageuza sura na macho



    yake yakagongana na macho ya Sajenti Minja........





    .. "umekuja kuniona mheshimiwa?," yule msaidizi aliongea kwa



    tabasamu huku akimuangalia sajenti Minja.

    "ndi...ndio, unaendeleaje?" sajenti Minja akamuuliza huku



    akitetemeka, kiasi kwamba mkuu wa polisi akaliona hilo.

    "nashukuru mungu, vipi wewe?" yule msaidizi wa mganga akamtupia



    swali jingine.

    "mi sijisikii vizuri kabisa" sajenti Minja akajibu.

    "Minja ebu twende ukapime malaria, ukimaliza utakuja kuongea nae



    zaidi" mkuu wa polisi akasema.

    Sajenti Minja akashusha pumzi ya kushukuru kwa maana aliona



    amepona.

    "nakuja ili tuongee zaidi" sajenti Minja akamwambia yule msaidizi



    wa mganga huku akiwa anatoka na mkuu wa polisi.

    "inaelekea mnafahamiana?" mkuu wa polisi akamtupia swali sajenti



    Minja wakiwa wanaelekea katika mabenchi ya kusubiria vipimo.

    "hapana, hatakuwa kanifananisha tu, au inawezekana kachanganyikiwa



    kutokana na kukoswa koswa kufa, yaani nimekuja Jana tu alafu



    nijuane na watu wa huku?" sajenti Minja akajibu kwa kumdanganya



    mkuu wa Polisi,

    "Ila nadhani endelea kujifanya hivyo hivyo kama unamjua ili umuweke



    karibu maana mkiwa marafiki anaweza akakueleza mambo mengi zaidi"



    Mkuu wa polisi alimshauri Sajenti Minja,



    "Hilo nadhani ni jambo zuri na inaweza kuwa mbinu safi" Sajenti



    Minja alijibu,

    "Au hii kesi nimpe mtu mwingine ili wewe uifuatilie tu iliyokuleta"



    Mkuu wa polisi alimuuliza Sajenti Minja,



    "Mi nadhani zinaufanano na kesi iliyonileta, kwa hiyo ni vyema tu



    niendelee nayo" Sajenti Minja alijibu,



    "ok, we chukua vipimo hapa, acha mi nirudi ofisini, ukishamuhoji



    tu, uje unipe taharifa" mkuu wa polisi akatoa maagizo.



    "Kwanini tusimpe muda kidogo wa mapumziko, tumuhoji hata kesho ili



    akili yake itulie kidogo" Sajenti Minja alitoa ushauri,

    "Sawa, ila inabidi haya mambo yaende haraka haraka na yafanikiwe



    ili ionekane tunafanya kazi kwa bidii" Mkuu wa polisi alimwambia



    Sajenti Minja,

    "Kuhusu hilo wala usijali, mambo yataenda sawa tu" Sajenti Minja



    alijibu,

    "Sawa basi, sasa wewe kachukue vipimo tu tutakutana kesho tena,



    maana giza linaanza kuingia" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti



    Minja,

    "sawa mkuu" sajenti Minja akajibu huku akijifanya anaelekea sehemu



    zilipo mahabara za hospitali.

    "Huu ushakuwa msala, sasa huyu msaidizi wa Mganga ataniletea balaa



    kubwa sana uko mbele" Sajenti Minja aliongea huku akiwa bado



    anatembea.



    ***********************



    Wakina Kayoza waliporudi kwa mama yao, walimsimulia yote



    yaliyotokea, mama kayoza alisikitika sana,

    "mchungaji kashindwa, kwa mganga ndio hivyo tena bahati mbaya, mi



    hata sijui nifanyaje?" Kayoza aliongea kwa kulalamika.



    "Mchungaji hajashindwa, vuta subira tu utapona" Mama Kayoza



    aliongea,



    "Mama sio kwa matukio haya, maana hii imeshakuwa kesi nyingine"



    Kayoza aliongea,



    "Mjomba yenu nae hajafanywa kitu na mzimu huko makaburini?" Mama



    Kayoza aliuliza na kufanya Omari aangushe kicheko baada ya



    kuzikumbuka zile bakora alizochapwa Sajenti Minja,

    "Sasa mbona mimi nauliza wewe unacheka?" Mama Kayoza aliuliza huku

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akiwa amekasirika,

    "Mimi sikuona ila Omari alinihadithia" Kayoza nae aliongea huku



    akicheka,

    "Mbona mnanicheka? omary amekuhadithia nini" Mama Kayoza aliuliza



    huku akiwa anawaangalia kwa zamu,

    "Mjomba nasikia amekula bakora za kutosha, mpaka kukaa anakaa kwa



    shida" Kayoza alimwambia mama yake huku akicheka,

    "Sasa ndio kinachowachekesha?" Mama Kayoza aliwauliza,

    "Sio tukio zuri, ila inachekesha mama, mtu mkubwa kama mjomba



    kutandikwa kama mtoto" Kayoza aliongea na kumfanya mama yake scheme



    chini chini,

    "Ebu acheni upumbavu" Mama Kayoza aliongea huku akicheka,



    Mara wakasikia mlango unagongwa, Mama Kayoza akaenda kuufungua

    "karibu mchungaji" mama kayoza akasema huku akiacha nafasi alie nje



    apite.

    "asante mpendwa" mchungaji alijibu huku akiingia ndani.

    "vipi mgonjwa, unaendeleaje?" mchungaji akaongea huku anamtazama



    kayoza.

    "namshukuru Mungu" kayoza akajibu.

    "lazima umshukuru Mungu, kwani ye ndo muweza ya yote" mchungaji



    aliongea huku akikaa kwenye kochi.

    "Za nyumbani?" Mama Kayoza alimuuliza Mchungaji Wingo,

    "Uko ni wazima, bwana yupo pamoja nasi. Sijui nyinyi hapa?"



    Mchungaji Wingo alijibu na kuuliza,

    "Sisi nasi ni wazima, karibu" Mama Kayoza aliongea,



    "kilichonileta hapa ni kitu kimoja tu, leo usiku kutakuwa na



    maombi, mnakaribishwa wote mje" Mchungaji Wingo akasema



    kilichompeleka.

    "haya mchungaji, tunashukuru kwa kutupa taharifa" mama Kayoza



    akajibu.

    "Ndio kazi yangu" Mchungaji Wingo alijibu,

    "Itakuwa usiku wa saa ngapi" Mama Kayoza aliuliza,

    "Kuanzia saa mbili" Mchungaji Wingo alijibu,

    Kisha mchungaji akaaga, ila alitaka asindikizwe na Kayoza.

    Kayoza akaongozana na mchungaji hadi nyumbani kwake,

    Pale kwa mchungaji kuna msichana ambae ni mtoto wa kwanza wa



    mchungaji, tokea siku ya kwanza alipomuona Kayoza, alijenga upendo



    juu yake,

    Mchungaji alipofika akaingia chumbani kuchukua biblia, akamuacha



    kayoza kakaa peke yake,

    mara yule binti wa mchungaji akaja, alipomuona kayoza akatabasamu,

    "amani ya bwana iwe nawe" kayoza akamsalimia yule binti.

    "sema mambo bwana, mi sio mlokole" yule binti akajibu kwa mbwembwe.

    Kayoza akatabasamu, "mambo" kayoza akasema.

    "safi, mzima?" yule binti nae akauliza uku akikaa jirani na kayoza.

    "mi mzima" kayoza akajibu,

    "Kayoza mimi na wewe tunajuana ingawa sio sana, si ndio" Binti



    mchungaji alimuuliza Kayoza,



    " ndio" Kayoza alijibu.



    "Basi kuna kitu kinaitwa hisia, sidhani kama zunazuilika" Binti



    Mchungaji aliongea na kumfanya Kayoza awe makini kidogo



    kumsikiliza,



    "Unataka kusema nin?i" Kayoza aliuliza,



    "Sitaki kupoteza muda, ninachotaka kusema ni kwamba Kayoza



    nakupenda" Binti akajivika ujasiri, kisha akamueleza Kayoza jinsi



    anavyojisikia juu yake,



    "Sawa, nashukuru" Kayoza aliongea huku akimuomba Mungu amuepushe na



    huo mtihani,



    "Ukisema unashukuru unamaanisha nini?" Binti Mchungaji aliuliza,

    "Nimekuelewa" Kayoza alijibu,

    "Naomba unijibu ili nijue hisia zako kwangu" Binti mchungaji



    aliongea,

    "Usijali, kesho tutaongea vizuri" Kayoza alijibu huku akitabasamu,



    "nibusu basi ili nishinde vizuri mwenzio" mtoto wa mchungaji



    akaongea kwa mahaba.

    "kesho rafiki yangu, hivi huogopi kusema hayo maneno katika nyumba



    takatifu kama hii?" kayoza akamjibu kwa busara,

    "si unibusu jamani wewe." yule binti akakomalia kwa sauti ya juu



    kidogo.

    "unamwambia nani akubusu?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akiwa



    anaingia Sebuleni.....



    .."hakuna kitu baba" binti mchungajibu akajibu.

    "kwa hiyo nimesikia vibaya?" Mchungaji Wingo akauliza huku



    anamuangalia binti yake.

    "nilikuwa namsimulia filamu moja hivi ilioneshwa jana ." binti wa



    Mchungaji akajibu huku akiangalia chini kwa aibu,



    "Umekalia kuangalia filamu tu, badala ukazane kusoma biblia ili



    uongeze imani unakalia kuongeza ujinga tu" Mchungaji Wingo



    alimwambia binti yake aliyekuwa amesimama mbele yake

    "Nisamehe baba, ila hiyo filamu ilikuwa na Mafundisho tu mazuri"



    Binti Mchungaji alijitetea,



    "Ebu tupishe bwana" Mchungaji Wingo akamwambia mwanae na binti



    akaondoka haraka,

    "Huyu mwanangu ni muongeaji sana, yupo tofauti na wenzake kabisa"



    Mchungaji Wingo aliongea huku akimgeukia Kayoza na usoni akikunjua



    tabasamu,



    "Ila ni mcheshi sana, yaani amenizoea muda mfupi sana" Kayoza nae



    alijibu,



    Kisha mchungaji na kayoza wakawa wanaongea, ila jambo kubwa ambalo



    mchungaji alimsisitiza Kayoza asikose katika maombi ya usiku.

    Kayoza akarejea kwao kujumuika na mama yake.

    "vipi mwenzetu, mchungaji alikuwa anakuambia nini?" mama kayoza



    alimuuliza mwanae.

    "tulikua tunaongea mambo ya kawaida tu" kayoza akajibu.

    Kisha mama kayoza akaenda jikoni kutayarisha chakula.

    "eh, mwana leo nimekutana na vituko" Kayoza alianza namna hiyo

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kumuelezea Omari.

    "wapi tena shee" Omari akauliza kwa shauku .

    "si kwa mchungaji mwanangu, kuna binti yake mkubwa amedata na flag



    yangu"Kayoza aliongea huku akitabasamu

    "kwa hiyo unataka kufanyaje?" Omari akauliza huku amekunja sura.

    "nitafanyaje ndugu yangu, na hili dubwana linanibana" Kayoza



    alijibu kwa upole

    "aah, ok, we mshiti au kama ana mahamu nitajaribu kumseti mimi"



    Omari aliongea, na kusababisha wote wakacheka.



    "Poa mi ntakupigia pande, we si mwanangu bwana" Kayoza aliongea



    huku akicheka...



    *****************



    Sajenti Minja hakwenda kupima, alimfuatilia mkubwa wake mpaka



    alipomuona anapanda gari na kuondoka, naye akarudi ndani moja kwa



    moja hadi katika kitanda cha msaidizi wa mganga..

    "vipi, unaweza kukaa" Sajenti Minja alimuuliza yule msaidizi wa



    mganga.

    "kwanini nisiweze?, naweza tu" Msaidizi wa mganga akajibu,

    "kuna maswali machache nataka nikuulize" Sajenti Minja akaongea kwa



    upole.

    "kwani wewe ni polisi" Msaidizi wa mganga aliuliza ili apate



    uhakika, kwa sababu alimuhisi.

    "ndio" sajenti Minja alijibu.

    "sasa unataka kuniuliza nini wakati tulikuwa wote kuanzia mwanzo



    hadi mwisho" Msaidizi wa mganga alijibu huku akionekana akimshangaa



    Sajenti Minja,

    "najua ndugu yangu, ila naomba unisaidie kitu kimoja" Sajenti Minja



    aliongea huku akisubiri sauti itakayomruhusu aendelee .

    "endelea" Msaidizi wa mganga alijibu.

    "naomba polisi yeyote atakaekuuliza kuhusu yale mambo yaliyötokea



    kule, mjibu hujui chochote, sawa?" Sajenti Minja aliwasilisha ombi



    lake huku akiwa hana uhakika wa kukubaliwa,

    "kwanini tufiche ukweli?" Msaidizi wa mganga aliuliza kwa mshangao,



    "Ukiongea ukweli utakuwa umeniharibia kila kitu katika maisha



    yangu, yaani hata kufungwa nitafungwa" Sajenti Minja aliongea kwa



    huruma ili kumshawishi Msaidizi wa Mganga akubaliane nae,



    "Kwa maana hiyo wewe umependa lile tukio lililotokea siku ile?"



    Msaidizi wa Mganga alimuuliza Sajenti Minja,



    "Tukio sasa, maana yalikuwa mengi" Sajenti Minja aliuliza,



    "La wenzangu kuuawa kinyama?" Msaidizi wa Mganga aliuliza,



    "Hapana, nitalifurahia vipi wakati lilikuja kuharibu tiba ya ndugu



    yangu na nikampoteza mtu ambaye ndiye nilikuwa nategemea yeye



    atamponya ndugu yangu?" Sajenti Minja aliongea kwa upole na machozi



    yakimtoka kwa mbali ili kumshawishi tu Msaidizi wa Mganga asiseme



    ukweli mbele ya Polisi wengine,



    "Sasa kwanini nifiche?" Msaidizi wa Mganga akauliza tena ila



    kipindi hiki aliuliza kwa upole,



    "Kuwa na utu ndugu yangu, maana unachotaka kukifanya ni kuniharibia



    maisha tu" Sajenti Minja aliendelea kumlalamikia Msaidizi wa



    Mganga,



    "Sio nakuharibia maisha, mbona mimi maisha yangu yameshaharibika?"



    Msaidizi wa Mganga aliongea huku anamkodolea macho Sajenti Minja,



    "Yameharibikaje sasa wakati upon hai na upon huru?" Sajenti Minja



    alimuuliza,



    "Hill sio tatizo, tatizo ni kwamba yule Mganga nilimchukulia kama



    mkombozi wangu kutokana na maisha yangu" Msaidizi wa Mganga



    aliongea,



    " kivipi yaani?" Sajenti Minja alimuuliza,



    "Yaani nilikuwa sina mbele wala nyuma, ila yule mzee aliniokota tu



    mjini na kunichukua kisha akawa ananifundisha uganga na akawa



    ananipa kipato kidogo angalau nikajiona mtu" Msaidizi wa Mganga



    aliongea,



    "Hilo sio tatizo, ngoja upone tutaongea zaidi, mimi nitakusaidia"



    Sajenti Minja aliongea kwa huruma huku akichomoa noti nyingi kutoka



    katika mfuko wake wa suruali na kumpa msaidizi wa Mganga,



    "Za nini hizi?" Msaidizi wa Mganga aliuliza huku akiwa anaziangalia



    zile hela akiwa hataki kuzipokea,



    "Zitakusaidia kununua vitu vidogo vidogo kipindi upo hapa



    Hospitali" Sajenti Minja aliongea huku akiwa bado amezishikilia



    zile pesa,



    "Wewe ni ndugu yangu bwana, tusaidiane" Sajenti Minja aliongea kwa



    upole,



    "Ngoja nitoke hospitali tutaongea vizuri ndugu yangu" Msaidizi wa



    Mganga aliongea huku akizitia pesa zile mfukoni,



    "Nikununulie chakula gani kabla sijaondoka" Sajenti Minja



    alimuuliza,



    "Chochote tu, mimi mswahili bwana sichaguagi chakula" msaidizi wa



    Mganga aliongea,



    "Wewe mgonjwa bwana, itabidi ule minyama nyama, ngoja nikakutafutie



    kuku bosi" Sajenti Minja aliongea kwa furaha huku akitoka nje na



    akiamini tayari ameshamteka hisia yule Msaidizi wa Mganga.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **"***********



    Babu wa monchwari alivyopigwa ule mtama ile asubuhi kumbe aliteguka



    mguu maeneo ya nyuma ya paja chini ya kiuno ila alivumilia na



    hakuwaambia kitu chochote wale polisi kwa sababu walikuwa na hasira



    muda ule, ila ilivyofika jioni maumivu yalimzidia na Babu wa



    monchwari akawaambia polisi ila walimpuuza tu, masikini Babu wa



    watu maumivu yalimzidia mpaka akawa Amalia kwa sauti kubwa kama



    mtoto, kilio kikamfikia mkuu wa polisi na kuja kuangalia kuna nini,



    " mbona huyo mzee analia?" Mkuu wa polisi aliwauliza askari



    aliowakuta hapo ambayo walibaki wakitazamana bila kutoa jibu,



    "Anamaumivu nadhani" Askari mmoja alijibu,

    "Babu una tatizo gani?" Mkuu wa Polisi aliamua amuulize mwenyewe,

    "Mguu nahisi umevunjika, nawaambia wanisaidie ila wananitukana"



    Babu alijibu huku akiendelea kulia,

    "Umevunjikaje, umeanguka?" Mkuu wa Polisi aliuliza,

    "Hao wenyewe walinipiga asubuhi" Babu alijibu,

    "Hata mambo ya kuwapiga watuhumuwa si tulishawakataza?, tena



    mnampiga mzee kabisa..ebu chukueni gari ya doria mumpeleke



    hospitali" Mkuu wa Polisi aliongea kwa ukali na vijana wake



    wakanyanyuka haraka,



    "Kwani yupo hapa kwa kosa gani" Mkuu wa polisi akauliza,



    "Huyu ndiye yule mlinzi wa monchwari" Askari mmoja akajibu,

    "Hata mumpeleke hospitali akapatiwe matibabu na mumrudishe hapa,"



    Mkuu wa polisi aliongea na kuondoka huku akiwaacha vijana wake



    wakimbeba Babu monchwari na kumpeleka kwenye gari na safari ya



    hospitali ikaanza.



    Iliwachukua dakika chache kufika hospitali, walimshusha Babu na



    kumpeleka kupata matibabu.



    Babu akapatiwa huduma kisha kwa Saa nzima na akaonekana ni mfupa tu



    ulikuwa umehama eneo lake, madaktari wakafanya jitihada na kumtibu



    bila tatizo na kuwaruhusu askari waondoke nae.

    Askari walipotoka nje walienda moja kwa moja mpaka kwenye gari yao,



    wakapanda gari ili warudi kituoni, kwa bahati mbaya gari yao



    ilipata itilafu ikawa haiwaki, ikabidi wapige simu kwa mkuu wao ili



    wapate msaada, mkuu wao akawapa namba ya sajenti Minja na kuwaambia



    yuko pale hospitali kwa hiyo wampigie awape msaada wa kuwarudisha



    kituoni kwa maana Sajenti ana gari.

    Sajenti Minja baada ya kupigiwa simu akawaelekeza mahali gari lake



    lilipo, wale askari na Babu wa mochwari wakafika mahali gari



    lilipo, kisha wakawa wanamsubiri sajenti Minja atoke ndani ili



    awarudishe kituoni, na Babu wa monchwari ndio kabisa alikuwa



    anaangalia katika mlango wa kutokea hospitali ambayo ndio njia



    anayokuja nayo Sajenti Minja..



    ...Sajenti Minja wakati anatoka ndani ya hospitali, akawaona wale



    polisi na yule babu wa mochwari kupitia dirishani, akasita, kisha



    akili yake ikafanya kazi haraka.

    akarudi kisha akawapigia simu wale askari na kuwaambia kuwa yeye



    bado ana shughuli anazifanya katika eneo like la hospitali, kwa



    hiyo askari mmoja amfuate ndani ili akampe ufunguo,

    mmoja kati ya wale polisi akaenda alipoelekezwa na sajenti Minja,



    akapewa ufunguo, kisha akaambiwa arudishe gari pale hospitalini



    baada ya kazi zao



    ***********************



    Sajenti Minja aliingia katika nyumba ya dada yake saa mbili usiku,



    baada ya salamu wakakumbushana mambo yaliyowakuta usiku uliopita,



    wakafurahi na kuhuzunika pia,

    Ila habari iliyowashtua wote ni kupatikana kwa wale maiti na mtu



    mmoja akiwa mzima, pia sajenti Minja akawaambia namna



    alivyofundisha yule msaidizi wa mganga kukana kujua lolote.

    Mama kayoza kidogo akashusha presha baada ya kusikia hivyo,

    "Kitu kingine kibaya ni kwamba hata yule babu wa monchwari



    aliyetusaidia kuiba ile maiti nae amekamatwa ila sijajua kwa kesi



    gani?" Sajenti Minja aliendelea kutoa habari mbaya,



    "Ni hiyo hiyo ya kupotea kwa maiti, asubuhi si nilikuwa hospitali



    nilienda kumuona mtu, ndio nikakutana na hizo habari, ila maiti



    yenyewe imeshapatikana uko makaburini ilikutwa pamoja na hiyo miili



    ya waganga wenu" Mama Kayoza aliwapa habari,



    "Kama maiti imepatikana itakuwa afadhali kwa Babu" Kayoza aliongea,



    "Hujui sheria mjomba, Babu hawezi kuachiwa mpaka ipatikane au



    ijulikane sababu za kuuza ile maiti" Sajenti Minja aliongea huku



    akimuangalia Kayoza,



    "Sababu iliyomfanye auze si ni pesa?" Kayoza alijibu kiutani na



    wenzake wacheke,



    "Haya mambo mazito msiyachukulie kiutani utani hivyo" Mama Kayoza



    aliongea huku akionekana kutofurahishwa na jibu la Kayoza,



    "Mama inabidi tujifurahishe tu, ukisema uegemee sana upande wa



    yanayotukuta, tutakuwa watu wa machozi kila siku" Kayoza alimwambia



    Mama yake,



    "Ujinga huo, badala uangalie namna ya kujisaidia unakalia kuongea



    vitu visivyo na kichwa wala miguu" Mama Kayoza aliendelea



    kumshambulia mwanaye,



    "Vitu vya maana kama vipi?, ngoja nijiandae niende kanisani" Kayoza



    aliongea kwa hasira huku akiondoka sebuleni,



    "Ana hasira kama babu yake, mzee John Minja" Sajenti Minja aliongea



    huku akicheka,



    "Mjinga tu, hasira ananiletea Mimi badala ya kumpelekea bibi yake



    uko kijijini" Mama Kayoza aliongea,



    "Kayoza anaenda kanisani?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Leo kuna maombi, tena na wewe itabidi uende ili bwana akakupe



    wepesi uenda kazi ya kumsaidia mjomba wako itatimia haraka" Mama



    Kayoza alimwambia Sajenti Minja,



    "Sawa itabidi tuongozane, kwani maombi yataisha saa ngapi?" Sajenti

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Minja akauliza,



    "Tunakesha" Mama Kayoza alijibu,



    "Mh..sasa si itabidi niende nyumbani nikabadili nguo" Sajenti Minja



    aliongea,



    "Kwani hizo ulizovaa zina ubaya Gani? Mama Kayoza aliuliza,



    "Mimi naona sio vizuri kwenda Nazi kwa sababu nimeshinda nazo kutwa



    nzima" Sajenti Minja alijibu,



    "Hiyo sio sababu, nenda kaoge uende kanisani" Mama Kayoza aliongea,

    "Sawa basi, nirudi baada ya muda gani?" Sajenti Minja aliuliza huku



    akiinuka,



    "Hakuna kuondoka, nilipokwambia ukaoge nilimaanisha uingie bafuni,



    sasa unavyotaka kuondoka unadhani bafu lipo kwako tu?" Mama Kayoza



    aliuliza,



    "Sawa bwana, basi ngoja nikajitayarishe" Sajenti Minja aliongea



    huku akielekea vilipo vyumba vya wakina Kayoza,



    Baada ya saa moja na nusu wote walikuwa wamejiandaa mpaka Omary



    wakaanza kwenda eneo la maombi.

    Walienda kwa miguu tu kwa maana ni eneo jirani na wanapoishi.

    Walifika na muda ulipofika waumini walikuwa wengi sana kanisani,



    walianza kwa kuimba nyimbo mbalimbali za kutukuza.



    Baada ya saa zima Mchungaji Wingo aliingia, akakaa katika kiti



    anachopaswa kuwepo. Nyimbo ziliimbwa kisha waimbaji wakamaliza,



    sala zilianza, walisali muda mrefu sana mpaka kayoza akachoka



    kutokana na kwamba yeye sio mtu aliyezoea sana kwenda kanisani,

    "oya kaka, tusepe" kayoza alimwambia Omari ambae alikuwa anasinzia



    tu muda wote.

    "wapi sasa" Omari akauliza kivivu huku akijinyoosha,

    "maskani dogo, we unasinzia tu bila ya mpango, usije ukaharibu hewa



    bure" Kayoza aliongea kwa utani.

    "aah wapi, mimi nina kontroo wewe" Omari akajibu kisha wote



    wakacheka.

    Wakatoka nje ya kanisa wakawa wanaelekea nyumbani, ilikuwa kama saa



    saba usiku hivi, kwa mbali wakaona msichana anawakimbilia, alikuwa



    yule binti wa mchungaji,

    "habari jamani" Binti akawasalimu.

    "nzuri" wakajibu kwa pamoja.

    "Kaka unaweza kutupisha kidogo?" Binti Mchungaji aliongea huku



    akimuangalia Omary,

    "Sawa" Omary alijibu huku akitangulia mbele na kuwaacha Kayoza na



    Binti Mchungaji wakiwa wamesimama,

    "vipi jibu langu Kayoza" Binti Mchungaji alimuuliza kayoza huku



    akiwa hana chembe ya aibu.

    "kesho nitakujibu" Kayoza akajibu kwa ufupi.

    "jamani mbona unanifanyia hivyo, au kwa kuwa nimekwambia



    nakupenda?" Binti Mchungaji alilalamika kwa huruma.

    "sikia binti, hapa unapoteza muda wako bure, kiukweli kabisa mi



    siwezi kukubalia ombi lako" Kayoza aliongea kwa ujasili kwa maana



    aliona bora amueleze ukweli tu kuliko kumpotezea muda, Binti



    Mchungaji alijishusha sana, alafu akajenga chuki kali sana kwa



    Kayoza.

    "Kwanini umeamua kufanya hivyo? au kwa kuwa nimeamua kukueleza



    hisia zangu?" Binti Mchungaji aliongea huku machozi yanamtoka,

    "Nimefanya hivi kwa sababu nakupenda na najipenda pia" Kayoza



    aliongea kwa sauti ya chini kisha akaondoka kumfuata Omary,



    "anajiona mzuri kumbe hana lolote, ni shetani tu ananyonya damu za



    watu, na kesho nitaitoa taharifa polisi ili nipate yale mapesa



    waliyotangaza" Binti Mchungaji aliongea kimoyo moyo huku akiwa



    anarudi kanisani na hasira kibao zikiwa zimemtawala.



    *******



    "kaka umeniangusha" Omari aliongea huku akitabasamu

    "achana nae, mtoto wa mchungaji alafu anaendekeza ukicheche" Kayoza



    alijibu.

    "Ila mpaka mwanamke akuambie maneno nayo, ujue anakupenda kweli"



    Omary alimwambia Kayoza,

    "Akampende baba yake na mama yake, mimi sina taimu nae" Kayoza



    alijibu kijeuri,



    "Sawa bwana, kufanya hivyo umemuepusha na kifo",Omary aliongea,



    "Sijamuepusha, sema nimemsogezea mbele kifo kwa maana kifo



    hakiepukiki" Kayoza aliongea wakati wanafika eneo la nyumbani kwao.



    **""""***************



    Ilipofika alfajili, Sajenti Minja aliondoka kanisani na kuelekea



    moja kwa moja nyumbani kwake kupumzika, kwa kuwa alichelewa sana



    kulala alijikuta anautandika usingizi mzito.

    Mida ya saa nne akakurupuka kitandani kwake, ni kawaida yake



    kujisachi anapoamka, hasa pale anapolala na nguo alizotoka kutembea



    nazo,

    alipojisachi, akakuta hana kitambulisho cha ofisini,

    "mh, kitakuwa wapi, ila ngoja nikakicheki kwa dada kule na nidoee



    chai kabisa" sajenti Minja alijiongelesha peke yake.



    Akaenda kuoga na kujisafisha kinywa kisha akajiandaa ili aende kwa



    Dada yake.

    Akatoka nje akawasha gari, akaondoka



    **********************



    Binti wa mchungaji aliamka ana hasira sana siku hiyo, aliamka saa



    tatu, ila mpaka saa nne alikuwa ameshawapiga makofi wadogo zake



    wawili kutokana na hasira alizonazo. Tena aliwapiga kwa makosa



    madogo madogo tu yasiyo na msingi.



    Binti Mchungaji alipomaliza kazi zake, akaenda kuoga, kisha akanywa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    chai, akavaa viwalo vyake vilivyompendeza, akamuaga mama yake kuwa



    anaenda kununua nguo.

    "leo ndio mwisho wake, anaringa kama hana dhambi!" Binti Mchungaji



    aliongea kimoyo moyo wakati akitoka ndani ya geti la nyumba yao na



    kuishika barabara iendayo sehemu kilipo kituo kikubwa cha polisi



    cha mkoa,

    "nikifika pale polisi namueleza askari yeyote, hata wasiponipa hela



    sawa, nataka tu nimkomeshe" Binti Mchungaji aliendelea



    kujiongelesha Mwenyewe, mara akasikia gari inapiga breki miguuni



    kwake, alishtuka na kuruka pembeni mpwa barabara, maana alikuwa na



    mawazo kiasi kwamba hakujua kama anatembea katikati ya barabara,



    "punguza mawazo dada, mbona we bado mdogo tu" yule dereva wa ile



    gari alimwambia binti wa mchungaji.

    "samahani kaka yangu" binti wa mchungaji alijitetea.

    Kisha yule dereva wa gari akashuka ili kuiangalia gari yake iko



    salama, maana breki aliyoipiga ilikuwa Kali sana.

    "aha! Kumbe polisi!" Binti Mchungaji alijikuta anahamaki baada ya



    kumuona yule dereva wa ile gari amevaa gwanda za polisi.

    "ee, kwani vipi?" yule polisi aliuliza huku akimuangalia Binti wa



    Mchungaji,

    "kuna habari njema nataka kukwambia" Binti Mchungaji alisema huku



    furaha yake ikionekana dhahiri machoni pake,

    "habari gani hiyo?" yule polisi akamuuliza huku akiwa na shauku ya



    kutaka kujua,

    Yule binti akageuka nyuma kuangalia kama kuna mtu anakuja,



    aliporidhka kuwa hakuna mtu, akasema,



    "yule kijana anayenyonya damu za watu anakaa palee" Binti Mchungaji



    akasema huku akiionyeshea nyumba ya Mama kayoza ambayo ilikuwa



    inaonekana kwa mbali kidogo.



    "Una uhakika binti?" Askari aliuliza huku akiwa ahamini



    anachoambiwa,

    "Twende unipeleke" askari aliongea huku akimfungulia Mlango binti



    Mchungaji ambayo aliingia kwenye gari kwa madaha kwa maana



    alishaimaliza kazi aliyokusudia kuifanya....





    Binti Mchungaji akaingia ndani ya gari na kukaa siti ya mbele,



    "Wewe umejuaje kuwa huyo kijana ndiye mnyonya damu?" Askari



    aliuliza huku akimuangalia Binti Mchungaji machoni,



    "We hutakiwi kuniuliza, unachotakiwa ni kwenda kumkamata" Binti



    Mchungaji aliongea,



    "Akikataa kuwa sio yeye unafikiri tutafanyaje, inatakiwa uniambie



    umejuaje kuwa ndiye yeye ili ninapoenda kumkamata niwe na ushahidi"



    Askari aliuliza,



    "Ameshawahi kuja kanisani kwetu ili tumuombee ili apone na ahachane



    na hayo mambo ya kuua kwa kunyonya damu" Binti Mchungaji alijibu,



    "Kumbe hata yeye hapendi we kunyonya damu na kuua?" Askari aliuliza



    huku akimtazama,



    "Itakuwa hapendi, na ndio maana alikuja kanisani kuombewa" Binti



    Mchungaji alijibu,



    "Sasa kama hata yeye hapendi kuua kuna haja gani ya kumkamata na



    wakati anaonekana ni mtu mwema?" Askari aliuliza,



    "Wewe kaka ni hakimu au askari? Maana unauliza tu badala ya kwenda



    kumkamata mtuhumiwa, au unaogopa kunyonywa damu?" Binti Mchungaji



    aliuliza kwa hasira,



    "Samahani, naomba nikuulize swali la mwisho kabla sijaenda



    kumkamata" Askari alitoa ombi,



    "Sitaki swali, kama hauendi niambie nishuke, mbona askari mpo wengi



    tu, nitaenda kuwaambia Askari wengine" Binti Mchungaji aliongea kwa



    jeuri huku akiangalia pembeni,



    "Naomba uniruhusu tu nikuulize hill swali, baada ya hapo



    sitokuuliza tena" Askari aliongea kwa upole,



    "Na liwe la mwisho kweli, haya uliza" Binti Mchungaji aliongea kwa



    mbwembwe,



    "Je huyo mnyonya damu angekua ndugu yako ungetoa taharifa polisi?"



    Askari aliuliza huku akiwasha gari,



    "Inategemea na undugu wenyewe, kama ni wa mbali namchomea tu" Binti



    Mchungaji aliongea huku akifurahi gari kuwashwa kwa maana alipata



    uhakika wa kutimiza malengo yake,



    "Angekuwa mtoto wa Dada yako au wa kaka yako je?" Askari aliuliza



    huku akiliondoa gari,



    "Huo ni undugu wa karibu kabisa, siwezi kwenda kumsemea polisi



    kamwe" Binti Mchungaji aliongea huku akijitengeneza nywele vizuri,



    akiwa bado anajiweka vzuri alishangaa yule askari akisimamisha gari



    na kumpiga Kofi zito la usoni,



    "Unanipigia nini sasa?" Binti Mchungaji aliuliza huku akiwa



    amejishika uso, ila yule Askari hakumjibu, akamuongeza jingine la



    uso tena pale pale alipopapiga mwanzo,



    "Unanipigia nini sasa?" Binti Mchungaji aliuliza huku akisikilizia



    maumivu,



    "Hiyo tabia yako ndio imekuponza" Askari aliongea huku akitabasamu,



    "Tabia gani jamani" Binti Mchungaji alilamika huku akiwa amejishika



    shavu,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Umbea, sio kila kitu kinatolewa taharifa" Askari aliongea huku



    akimuongezea kofi na kisha akafungua mlango wa gari ili yule



    msichana ashuke.



    Binti akatelemka haraka haraka na yule Askari akaiondoa gari kwa



    spidi ya juu.



    Gari la yule askari lilipopotea, yule binti mchungaji nae



    akahairisha safari yake,



    "akha mwenzangu, huyu mmoja tu nimekutana nae njiani kanipiga vibao



    namna hii, je nikienda huko polisi si wataniua kabisa?" yule binti



    wa mchungaji aliongea huku akiwa ameshika njia ya kwenda kwao.



    ***********************



    Sajenti Minja aliingia kwa Dada yake asubuhi na kuwakuta wakiwa



    wamekaa,



    "Hivi huyu Mchungaji wenu ana binti mkubwa?" Sajenti Minja aliuliza



    baada ya salamu,



    "Anae binti mkubwa kabisa, kwani vipi?" Mama Kayoza aliuliza,



    "Aisee yule sio mtu mzuri kwetu, so nimekutana nae hapo njiani



    akanisimamisha na kuanza kunipa habari za Kayoza" Sajenti Minja



    aliongea,



    "Eeeh, makubwa, amekwambiaje?" Mama Kayoza aliuliza,.



    "Ooh Mara mnyonya damu namjua, alikuja kanisa kwetu na kuombewa,



    ooh Mara sijui nini, yaani inaonekana anamjua vzuri Kayoza" Sajenti



    Minja aliongea,



    "Ikawaje sasa?" Mama Kayoza akauliza,



    "Aisee nimemuwasha mabanzi, sijui hata kama atarudia tena kusema"



    Sajenti Minja aliongea huku akicheka,



    "Usiseme hivyo, anaweza kwenda kituoni yule, maana ameshaonekana



    sio mtu mzuri" Mama Kayoza aliongea,



    " hata akienda atakuwa hana Maelezo ya kutosha" Sajenti Minja



    aliongea kwa dharau,



    "Tatizo lako wewe ni mpuuzi" Mama Kayoza aliongea kwa hasira baada



    ya kumuona Sajento Minja ana dharau



    "Sasa Dada mbona unanitukana tena?" Sajenti Minja aliuliza,.



    "Mpuuzi sio tusi, mtu anayepuuza jambo ndio huitwa mpuuzi" Mama



    Kayoza alimjibu ndugu yake,



    "Sijapuuza hill jambo, mimi bado namfuatilia huyo binti ila sidhani



    kama ataenda kutoa taharifa polisi" Sajenti Minja aliongea,



    "Haya bwana" Mama Kayoza aliongea kinyonge,



    "Jana niliangusha kitambulisho changu, alafu hata sijui



    nilipokiangushia" Sajenti Minja aliamua kubadilisha mada,



    "Kipo ndani, ulikiangushia hapa" Mama Kayoza alijibu,



    "Afadhali, maana nilishapatwa na wasiwasi wa kukipoteza" Sajenti



    Minja aliongea.



    Baada ya kukichukua kitambulisho chake aliaga na kwenda moja kwa



    moja hospitali kwa ajili ya kwenda kumuona Msaidizi wa Mganga.



    Alifika mapema na moja kwa moja akaenda kumjulia hali Msaidizi wa



    Mganga, baada ya kumjulia hali mgonjwa wake, Sajenti Minja



    alifarijika kumuona mgonjwa wake amepata nguvu na anatembea kama



    kawaida.



    Bila kupoteza muda, sajenti Minja akamtafuta daktari, kisha akapewa



    ruhusa ya kuondoka na mgonjwa wake, akamchukua hadi nyumbani kwake.



    Kisha akampa taharifa mkuu wa polisi kuwa yule msaidizi wa mganga



    ametoka hospitali na anakaa nae nyumbani kwake, mkuu akafurahi



    kusikia hivyo.



    ***********************



    Kayoza na Omari walijua sababu kubwa ya binti wa mchungaji kutaka



    kwenda polisi ni kutokana na kukataliwa na Kayoza kuwa mpenzi wake,



    Omari akaamua amchukue yeye, ikawa kila siku ni lazima aende kwa



    mchungaji, tena gia aliyokuwa anaenda nayo ni kununua maziwa,



    taratibu mazoea yakaanza hadi wakazoeana kabisa, mwisho kabisa



    Omari akamtongoza binti wa mchungaji, bila iyana alikubaliwa kwa



    roho safi, na sasa Omary na Binti Mchungaji wakawa Wapenzi rasmi.



    ***********************



    Siku moja mkuu wa polisi alikuwa anafungua mlango wa ofisini kwake,



    ndio akawaona askari watatu wakiwa wameongozana na babu aliyefungwa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    pingu. Alikuwa ni yule Babu wa monchwari, akawaita, kisha akaingia



    ofisini, wale askari na yule babu nao wakaingia,



    "hii kesi ya huyu mzee mbona mnaiendesha pole pole sana". Mkuu wa



    polisi aliwauliza wale askari.



    "ushaidi ndio unatuchelesha mkuu" Askari mmoja alijibu



    "niambieni katika uchunguzi wenu mmefikia wapi" Mkuu wa Polisi



    akawatupia swali jingine,



    "hakuna mwanga wowote tuliopata" yule askari akamjibu tena mkuu wa



    polisi.



    "nyie wazembe kweli, ile maiti iliyoibiwa si iliokotwa pamoja na



    zile maiti zilizonyonywa damu?" Mkuu wa polisi akauliza kwa jazba,



    "ndio mkuu" wale askari wakajibu kwa pamoja,



    "mlienda kumuhoji yule mtu aliekutwa hai?" Mkuu wa Polisi akawapa



    swali jingine.



    "hapana mkuu" akajibu yule Askari ambae siku zote uso wake



    utawaliwa na hasira.



    "kwanini" mkuu wa polisi akaendelea kuwabana na maswali.



    "yule anahusika na kesi ya sajenti Minja" yule askari akajitetea



    kipumbavu.,



    "ok, sasa hii kesi ya huyu babu nampa sajenti Minja kwa sababu



    mmesema zinaingiliana, basi atazishughulikia zote" Mkuu wa polisi



    alimaliza kisha akawaamuru watoke ofisini kwake, wamuache babu wa



    monchwari peke yake, wakamtii kisha wale askari wakaondoka.



    Kisha mkuu wa polisi akachukua simu yake ya mkononi alafu akapiga,

    "hallow Minja uko wapi?"mkuu wa polisi aliuliza. Baada ya kujibiwa



    akaendelea,



    "Nipo ofisini kwangu" Sajenti Minja alijibu huku akishangaa ile



    simu ya ghafla kutoka kwa mkubwa wake,



    "ok, njoo ofisini kwangu" Mkuu wa Polisi aliongea kisha akakata



    simu.



    "nakukabidhi kwa mtu anaejua kazi" Mkuu wa polis alimwambia babu wa



    mochwari,



    "Nashukuru sana kwa kunijali mwanangu" Babu wa monchwari aliongea



    huku akiangalia chini.



    "Sio nakujali, huo ndio utaratibu wa kazi" Mkuu wa Polisi aliongea.



    ************



    Sajenti Minja baada ya simu aliyopigiwa na mkuu wake kukatwa,

    akatoka ofisini kwake huku akiwa na maswali kibao juu ya kuitwa



    kwake na Mkuu wa Kituo.



    Akawa anaelekea ofisi ya mkuu wa polìsi, alipofika mlangoni



    akagonga hodi,



    "yes, come in" sauti ya mkuu wake kutoka ndani ilimjibu,



    Sajent Minja akashika kitasa cha mlango akanyonga kwa nia ya



    kufungua mlango.....





    ...sajenti Minja akanyonga kitasa, haikuonekana dalili ya mlango



    kufunguka, mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani, mara akasikia mlango



    unafunguliwa, akatoka mkuu wa polisi,



    "minja nisubiri ndani mara moja, naenda msalani dakika moja", mkuu



    wa polisi alipofungua mlango aliongea maneno hayo huku akiwa



    anatembea kumuacha sajenti Minja, mlango ulikuwa bado uko wazi,



    Sajenti Minja akanyanyua mguu wa kulia ili kuingia ndani,



    "jesus christ" alijikuta anasema kwa sauti ya chini baada ya



    kugundua kuwa aliekuwa ndani ni babu wa mochwari, ila bahati nzuri



    ni kwamba yule babu alikuwa ameinamia chini, kwa hiyo hakuweza



    kumgundua Sajenti Minja.



    Sajenti Minja alirudi nje kwa kasi, kisha akaurudishia mlango huku



    anahema kwa fujo kama katoka kukimbia mbio ndefu,



    "vipi Minja, mbona unaonekana hauko kawaida", sauti ya mkuu wa



    polisi ilimshtua Sajenti Minja,



    "nimepigiwa simu, nyumbani kuna matatizo" Sajenti Minja alitumia



    uongo,



    "ila kulikuwa na kazi nataka kukupa, tuingie ndani kuna kesi nataka



    kukupa, alafu utaendelea na ratiba zako", Mkuu wa Polisi alimwambia



    Sajenti Minja,



    "samahani mkuu, niko chini ya miguu yako, naomba hiyo kesi unipe



    baadae, uko nyumbani sio kwema kabisa", Sajenti Minja aliongea uku



    akiwa ameweka sura ya huzuni,



    "mmmh, ok, sawa, ukimaliza ya nyumbani, unijulishe, maana nataka



    nikupe kesi ya mzee mmoja hivi", Mkuu wa polisi alimkubalia,



    "Nikimaliza nitakujulisha na asante mkuu kwa kunikubalia niende



    nyumbani, nikirudi nitakufahamisha" , Sajenti Minja alijibu huku



    akiwa anaanza kuondoka,



    "Minja" Mkuu wa Polisi aliita tena wakati Sajenti Minja anaanza



    kuondoka,



    "naam mkuu" Sajenti Minja aliitikia baada ya kuitwa,



    "unaondoka tu, ila hujaniambia nyumbani kuna tatizo gani", Mkuu wa



    Polisi alihoji,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "kuna kajomba kangu, ambacho ni katoto ka dada yangu ambae



    nilikuambia anaishi hapa, nimeambiwa amegongwa na gari na hali yake



    sio nzuri", Sajenti Minja aliendelea kutunga uongo mbele ya bosi



    wake,



    "ooh, poleni sana, haya bwana wahi,"Mkuu wa Polisi alimruhusu



    sajenti Minja kwa mtindo huo.



    Sajenti Minja aliondoka kwa mwendo wa haraka haraka mpaka gari yake



    ilipokuwepo,



    "mhm, nimesevu so hadi raha, leo nilikua nahaibika mbele ya bosi",



    Sajenti Minja aliongea wakati anajipakia kwenye gari yake.



    ********************



    "duh, mama ujue mi nashindwa kuelewa, naona kama ndio mmeniacha



    niendelee kuwa katika hali hii", Kayoza alimwambia mama yake wakiwa



    wanapata chakula cha mchana,



    "ebu, acha uwendawazimu uko, mzazi gani anaependa mwanae awe katika



    matatizo?, we msubiri mjomba ako arudi labda atakuwa na mpya", Mama



    kayoza alimjibu mwanae huku akiwa anasafisha mikono yake kwa maji,



    "lakini mama", Kayoza kabla hajamaliza kuongea, ilisikika sauti ya



    mtu ikigonga mlango,



    "sukuma, mlango uko wazi", Mama Kayoza aliongea kwa sauti ya juu



    kidogo, ili mgongaji amsikie,



    "hodi mpaka ndani, eeh, nina mguu mzuri kweli, yaani nimefika



    wakati wa mahakuli", Sajenti Minja aliongea huku akiurudishia



    mlango



    ,"karibu anko, ingawa ndo kinaisha", Omari alimwambia sajenti



    Minja, kisha wote wakacheka,



    "ebu tuachane na hayo, leo kidogo nipate aibu ya mwaka mbele ya



    bosi wangu", Sajenti Minja alibadilisha stori,



    "ehe, nini tena?", Mama Kayoza aliuliza kwa shauku.Sajenti Minja



    aliwaeleza mwanzo mpaka mwisho,



    "kwa hiyo inavyoonekana anataka na kesi ya yule babu wa mochwari



    iwe chini yako?" Mama Kayoza aliuliza,



    "ndio hivyo" Sajenti Minja alijibu kinyonge,



    "sasa utafanyaje" Mama Kayoza aliuliza,



    "nitamkimbia kimbia hivyo hivyo mpaka achoke", Sajenti Minja



    alialiongea,



    "Mimi naona bora uichukue na hiyo kesi hili uweze kuwadhibiti



    vizuri wahusika" Omary alichangia



    "Hapana, mimi nitajitahidi niikwepe tu" Sajenti Minja aliongea,



    "Ichukue hiyo kesi kwa maana huwezi jua mipango ya Mungu" Mama



    Kayoza aliongea,



    "Tutajua uko mbele ya safari. jamani kuna kaugali kalichobaki?"



    Sajenti Minja aliuliza,



    "ugali upo, ila mboga ndo imeisha, ngoja wajomba zako wakakununulie



    maziwa kwa mchungaji", Mama kayoza alimjibu Sajenti Minja huku



    akimpa kayoza hela ya maziwa,



    "Kwani hatuwezi kununua mboga nyingine zaidi ya maziwa" Sajenti



    Minja aliuliza,



    "Mbona tunaweza kununua hata maharage au nyama, tatizo tukiinjika



    mpaka viive si utakuwa umeshakufa na njaa yako?" Mama Kayoza



    aliongea,



    "Kweli Dada, basi nyie wahini, maana njaa niliyonayo ni ya



    hatari...



    baada ya wakina kayoza kutoka, Sajenti Minja na dada yake



    waliendelea na maongezi yao.



    "afadhali umekuja mwenzangu, maana mjomba ako kanichachamalia



    hapa", Mama Kayoza alimwambia Sajenti Minja



    "kachachamaa na nini tena?"Sajenti Minja akauliza,



    "eti anadai tuko kimya katika kufuatilia matatizo yake", Mama



    Kayoza akajibu,



    "kuna askari niliongea nae jana, akaniambia kuna mtaalam wa jadi



    ana uwezo mkubwa wa kusaidia watu", Sajenti Minja alimwambia dada



    yake



    ,"kwa hiyo ulimwambia una ndugu yako ananyonya damu?", mama Kayoza



    aliuliza kwa mshtuko,



    "kwani mi sina hakili mpaka nimwambie hivyo?, nilimdanganya



    natokewa na mauzauza kila nikitaka kulala", Sajenti Minja akamjibu



    dada yake,



    "ataweza kweli kumtibia kayoza?", Mama kayoza akamtupia mdogo wake



    swali jingine,



    "dada nawe kwa maswali!, tutajua uko uko kama ataweza au lah",



    Sajenti Minja alimjibu dada yake,



    "lini mtaenda uko", mama Kayoza akauliza tena



    "nafikiri kesho, kama nitapata nafasi", Sajenti Minja alijibu



    "haya bwana, wacha nikakutayarishie chakula jikoni", mama kayoza



    aliongea huku akinyanyuka kwenye kochi,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "hayo ndo mambo sasa, kama kuna pilipili niwekee", Sajenti Minja



    alisema na kumfanya mama kayoza ahangue kicheko.



    "Sasa hiyo pilipili utaiweka katika maziwa?" Mama Kayoza aliuliza



    huku akicheka,



    "Nitaitafunia tu na ugali" Sajenti Minja alijibu,



    "Ngoja nikutafutie kama ntaipata" Mama Kayoza aliongea huku



    akiingia jikoni.



    "Sema siku hizi umekuwa mswahili kweli Dada yangu" Sajenti Minja



    aliongea huku akitabasamu,



    "Kwanini unasema hivyo?" Mama Kayoza aliuliza huku akisimama,



    "Naona nawe unakubali tu tumpeleke mwanao kwa waganga sio kama



    zamani ulivyoshikilia msimamo wako wa kanisani" Sajenti Minja



    alimwambia Dada yake,



    "Ujue Mungu hana njia moja ya kukupa mafanikio, unatakiwa upitie



    njia nyingi lakini ukimuamini yeye tu na sio vitu vingine" Mama



    Kayoza alimwambia Sajenti Minja,



    "Sawa mama mchungaji, inabidi na wewe ujenge kanisa lako sasa"



    Sajenti Minja alimwambia Mama Kayoza,



    "Ebu kwenda zako uko, kwanza ulivyosema mchungaji umenikumbusha awa



    wendawazimu waliofuata maziwa, mbona wamechelewa hivyo?" Mama



    Kayoza aliuliza,



    "Wana mambo mengi wale vijana, usikute wanamnyatia yule binti wa



    mchungaji" Sajenti Minja aliongea kwa utani huku akicheka,



    "Acha uwendawazimu wako, watoto wa mchungaji wana maadili wewe"



    Mama Kayoza aliongea,



    "Sio wote, kama yule binti mcharuko niliekutana nae juzi ni bure



    kabisa, bora angeishi uswahilini tu" Sajenti Minja aliongea huku



    akicheka,



    "Kwani ana kosa gani? Si alikuwa anaenda polisi kusema habari za



    ukweli" Mama Kayoza aliongea huku akitabasamu,



    "We si ni mlokole? Nenda na wewe polisi kaseme hizo hizo habari



    kuwa mwanao muuaji" Sajenti Minja alimwambia Mama Kayoza,



    "Mtoto anauma bwana, mtoto mwenyewe ndio huyo huyo mmoja kama roho"



    Mama Kayoza aliongea huku akicheka,



    "Nenda jikoni bwana, maana story zimezidi mpaka unasahau kuwa mimi



    njaa inaniuma" Sajenti Minja alimwambia Dada yake,



    "Hata baba, usije ukanifia bure kwa njaa" Mama Kayoza aliongea huku



    akielekea jikoni.



    *********************



    Baada ya mkuu wa polisi kurudi ndani, alimpgia simu askari mwingine



    na kumwambia amrudishe rumande Babu wa mochwari,



    "jamani nitakaa huku mpaka lini, nina mke na watoto mimi",Babu wa



    mochwari aliongea huku machozi yakimtoka,



    "usijali mzee wangu, upepelezi utakamilika hivi karibuni", Mkuu wa



    polisi alimjibu Babu wa mochwari kwa huruma.



    "Mwanzo askari wako waliniambia nikiri kosa ili niachiwe, nikakiri



    kosa kuwa ni kweli mwili umeibwa, lakini hawajaniachia, naambulia



    kipigo tu mpaka viungo vinateguka" Babu wa monchwari alilalamika,



    "Mzee ujue upelelezi sio kitu cha kukurupuka tu, inahitajika muda



    mrefu wa kuchunguza na kujiridhisha na jibu la kile



    kilichopelelezwa, na hapo sasa ndipo sisi tutaachana na wewe na



    kesi yako itakuwa mahakamani" Mkuu wa polisi alimuelewesha Babu wa



    monchwari,



    "Mahakamani tena?, si nitafungwa jamani mie?" Babu wa monchwari



    aliuliza huku akilalamika,



    "Sasa sisi hatutaki ufungwe, na ndio maana tunaendelea kukuhifadhi



    ili utusaidie kumpata huyo aliyeichukua hiyo maiti" Polisi



    alimwambia Babu wa monchwari,



    "Sasa mbona sioni juhudi zozote ukizifanya kumtafuta huyo mtu na



    nilishawahi kumuona eneo hili huyo mtu mwenyewe" Babu wa monchwari



    aliongea na kumfanya Mkuu wa polisi ashtuke kidogo,



    "Alikuwa anafanya nini na kwa nini hukuwaambia Askari?" Mkuu wa



    polisi aliuliza huku akimshangaa,



    "Kitu ninachokishangaa ni kwamba alipotea ghafla, inawezekana



    kabisa yule bwana si mtu wa kawaida, atakuwa mshirikina tu" Babu wa



    monchwari aliongea,



    "Kumbe ukimuona kwa sura unamjua vizuri tu?" Mkuu wa polisi



    aliuliza,



    "Vizuri sana tu, hata akiwa mbali namtambua" Babu wa monchwari



    aliuliza,



    "Ulivyomuona alivaaje, au alivaa kiaskari?" Mkuu wa polisi



    alimdadisi Babu wa monchwari,



    "Hajavaa kiaskari, na kwanza hawezi kuwa askari yule, ana ndevu



    kabisa" Babu wa monchwari alijibu,



    "Basis usijali babu, tunaendelea kufuatilia" Mkuu wa Polisi



    aliongea,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kisha yule askari aliepigiwa simu aliingia na kisha akamchukua Babu



    wa mochwari na kumrudisha rumande.



    ***********************



    Wakina kayoza walipofika kwa Mchungaji Wingo, walimkuta Binti wa



    mchungaji anafagia fagia



    "karibuni", Binti wa mchungaji aliwakaribisha alipowaona,



    "asante, za hapa?", Omari alijibu alafu akamjulia hali,



    "poa my husband, Kayoza mambo?", baada ya kujibu salamu ya Omari,



    binti wa mchungaji akamgeukia Kayoza,



    "poa, kuna maziwa ya mtindi?" Kayoza akamjibu kwa mkato, kisha



    akasema kilichompeleka,



    "yapo, mnataka kiasi gani?" Binti Mchungaji akauliza,



    "nusu lita" Kayoza alijibu huku akimpatia pesa, Binti wa mchungaji



    akachua hela kisha akaingia ndani kuwapimia maziwa.



    "kaka uko siriazi, hutaki hata kucheka nae", Omari alimwambia



    kayoza huku akijichekesha



    "boya sana huyu demu", Kayoza aliongea akiwa na chuki za wazi kwa



    binti wa mchungaji.



    Baada ya dakika tano binti wa mchungaji alitoka, akawapa maziwa



    ,"Omari baki, kuna kitu kizuri nataka kukwambia", Binti wa



    mchungaji alisema,



    "nibaki?, kwani ndani uko na nani?", Omari alimuhoji Binti wa



    mchungaji,



    "niko peke yangu, wote wameenda mjini, ila baba kaenda kanisani",



    ndivyo alivyojibu,



    "Boy we tangulia, mimi ninakuja" Omary alimwambia Kayoza,



    "Sasa nikifika peke yangu mama si ataniuliza?" Kayoza alihoji,



    "Utajua namna ya kumdanganya, ila hata sitochelewa" Omary aliongea,



    "Poa, jitahidi kuwahi bwana" Kayoza aliongea huku akianza kuondoka.



    "Twende ndani basi" Binti Mchungaji alimwambia Omary huku akimvuta



    mkono,



    "Huogopi?" Omary aliuliza huku akijatahidi kutosogea zaidi ya pale



    alipo,



    "Twende ommy, utaniudhi ujue" Binti Mchungaji aliongea sauti ya



    kudeka na kumfanya Omary alegeze msimamo,



    "Una hatari sana" Omary aliongea huku akipiga hatua kumfuata binti



    mchungaji



    "Twende usiogope, awa hawarudi sasa hivi" Binti Mchungaji aliongea



    huku akifungua mlango wa chumbani kwake,



    "Bora ungenipeleka sebuleni, huku ndio pabaya kabisa" Omary



    aliongea huku akiingia katika chumba cha Mchungaji,



    "Kelele bwana, kaa hapo mimi nakuja sasa hivi" Binti Mchungaji



    aliongea huku akimkalisha Omary kitandani,



    "Uwahi basi" Omary aliongea wakati Binti Mchungaji akitoka,



    "Nakukuja sasa hivi, kuna kazi naenda kuimalizia chap chap" Binti



    Mchungaji aliongea na kisha akatoka nje baada ya kuurudishia



    mlango, Omary akabaki chumbani peke yake huku macho yake yakitalii



    katika kila kona ya chumba kile cha Binti Mchungaji.



    Baada ya Binti mchungaji kumaliza kazi, akaenda kujisafi mwili,



    kisha akarudi chumbani kwake na kufunga mlango kwa ndani,



    "we mtoto huogopi?, Omari alimuuliza huku akiwa na sura ya



    wasiwasi, Binti wa mchungaji badala ya kujibu, yeye akaitoa ile



    khanga aliyotokanayo kuoga na kubaki mtupu kama alivyozaliwa, Omari



    akili ilimruka na uoga wote ukamtoka, bila kutarajia akamvuta binti



    wa mchungaji kitandani, na kuamia katika ulimwengu mwingie.



    Mchungaji Wingo aliporudi nyumbani kwake, akakuta mlango wa mbele



    uko wazi, video sebuleni inawaka, akamuita binti yake, lakini



    hakupata jibu, akaamua aende akamuangalie chumbani kwake,



    alipokaribia mlango wa chumba cha binti yake, alisikia mlio wa



    kitanda cha binti yake kikilalamika kwa fujo,



    "mh..", mchungaji Wingo aliguna...



    ...mh", mchungaji aliguna, kisha akagonga mlango, mlio wa kitanda



    ukakoma, kisha ukimya ukatawala,



    we happy", Mchungaji Wingo akamuita binti yake,



    "abee baba", happy akaitika,"una shughuli gani umo ndani?",



    Mchungaji Wingo akamuuliza, kimya kikatawala tena, ila cha sasa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hivi kilikuwa kirefu kidogo,



    "mbona hujibu?", Mchungaji Wingo akauliza baada ya ukimya,



    "nilikuwa naa...naa...naa.., sijakusikia ulichosema baba", Happy



    akashindwa kujibu akawa anajiuma uma tu,



    "nimekuuliza una shughuli gani umo ndani, mbona kitanda kinapiga



    kelele hivyo?", Mchungaji Wingo akarudia swali katika sauti ya



    ukali,



    "nafunga neti baba", happy akajibu huku sauti ikiwa na



    wasiwasi,"neti tu, ndo kitanda kipige kelele namna hiyo?",



    Mchungaji Wingo aliongea huku akiwa anarudi sebuleni, pia



    alionekana hakuridhishwa na jibu la binti yake



    .***************



    Ndani baada ya kusikia mtu anagonga hodi, wote walishtuka, ila



    hawakukurupuka, wakatulia tuli, baada ya kugundua kuwa anaegonga ni



    mchungaji, happy aliteremka chini taratibu kisha akavaa kanga yake,



    akawa anamjibu baba yake, kipindi hicho chote, Omari alikuwa



    anajing'ang'aniza kupita dirishani bila mafanikio, baada ya



    majibizano ya muda mfupi, kati ya happy na baba yake, Mchungaji



    aliondoka mlangoni kwa happy, hapo ndipo Omari akapata sauti,



    "Sasa nitatokaje nje?", Omari alimuuliza happy kwa sauti ya chini



    sana,



    "subiri kidogo, sasa hivi anaenda kuoga", Happy alimtoa Omari hofu.



    "Happy umeniponza mwenzio" Omary aliongea huku akitaka kulia,



    "Acha ujinga wewe, kwani baba amejua kinachoendelea?" Happy



    aliuliza kwa ukali,



    "Hata kama hajui, wewe unadhani nitatokaje nje?" Omary aliuliza



    huku akiwa anafunga vifungo vya shati yake,



    "Si nimekwambia ataenda kuoga muda si mrefu" Happy aliongea,



    "Sasa mimi nitaaminije?" Omary alijikuta anauliza swali la kipuuzi,



    "Mimi hapa ni kwetu, najua ratiba za watu wote hapa, ebu niamini



    acha ujinga" Happy alimuelewesha Omary.



    "Dah, tamaa nyingine mbaya sana" Omary aliongea peke yake huku



    akijifuta jasho ingawa ndani hakukuwa na hali ya joto,



    "Unasemaje" Happy alimuuliza Omary baada ya kumuona akiongea ingawa



    hakumuelewa,



    "Sijasema kitu bwana" Omary alijibu huku akionekana ana hasira I



    logic hang any in an a na hofu.



    "Mwenzangu ushaanza kuwa chizi" Happy aliongea huku akimcheka Omary



    chinichini.



    *********************



    Mchungaji Wingo alipotoka mlangoni kwa binti yake, alienda



    sebuleni, kisha akazima luninga, alafu akamuita happy,



    "Umeshamaliza kufunga chandarua?" Mchungaji Wingo alimuuliza binti



    yake,



    "Tayari, alafu sijisikii vzuri" Happy alimwambia baba yake,



    "Kwa hiyo umehisi itakuwa malaria na ndio maana ukafunga



    chandarua?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akitabasamu,



    "Ndio hivyo, mimi nadhani itakuwa ni malaria tu" Happy alijibu huku



    nae akitabasamu,



    "Kuna maji ya moto?" Mchungaji Wingo aliamua kubadili mada,



    "Ndio, yapo...yatakosaje wakati najua watumiaji mpo?" Happy



    aliuliza,



    "Ebu niandalie nikaoge mie" Mchungaji Wingo aliongea huku



    akinyanyuka,



    "Sawa mzee" Happy alijibu,



    "Mama bado hajarudi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akisimama,



    "Wakiendaga mjini wanawahigi kurudi kwani?, hiyo ni mpaka saa kumi



    na mbili jioni" Happy alijibu baba yake,



    "Huyu nae bwana, si ahache kwenda uwage unaenda wewe?, yeye



    ameshaanza kuzeeka" Mchungaji Wingo aliongea kwa kulalamika,



    "Wivu tu huo, muache aendage yeye, maana ndio anajua mahitaji ya



    watoto" Happy aliongea wakati baba yake anaelekea chumbani.



    Happy akaenda bafuni akachukua ndoo na kwenda nayo jikoni ambapo



    aliiwekea maji ya moto na kuirudisha tena bafuni.



    "Maji yapo tayari baba" Happy alipaza sauti kumwambia baba yake



    aliyekuwepo chumbani,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Oooh nakuja, umeshayachanganya na maji ya baridi?" Mchungaji Wingo



    aliuliza huku bado akiwa ndani,



    "Utachanganya mwenyewe, maana Jana nilivyokuchanganyia ulilalama



    nimezidisha ubaridi" Happy alimwambia baba yake,



    "Bora hujachanganya, maana Sikh hizi nahitaji maji ya uvugu vugu



    mkali kidogo" Mchungaji Wingo aliongea huku bado akiwa chumbani,



    "Umeshaanza kuzeeka ndio maana unataka maji yenye joto Kali" Happy



    alimwambia Baba yake huku akiwa bado amesimama mlangoni,



    "Kweli aisee, naona umri unanitupa mkono" Mchungaji Wingo aliongea



    huku akitoka ndani akiwa amejifunga taulo lake kiunoni na moja kwa



    moja akanyoosha mpaka bafuni.



    Alipoingia, akatoa taulo lake mwilini,



    "mh..kumbe sabuni imeisha?", mchungaji aliongea peke yake, baada ya



    kuangalia sehemu ya kuwekea sabuni ikiwa tupu mule bafuni,



    Mchungaji Wingo akakata shauri la kurudi kutoka bafuni na kurudi



    chumbani ambapo ndipo huifadhi sabuni nyingine.



    ********************



    Happy Binti Mchungaji alipoona kuwa baba yake kaingia bafuni,



    akaingia chumbani haraka,



    "Tayari baba ameingia bafuni, twende nikutoe nje" Happy aliongea



    kwa sauti ya chini ambayo ilisikika vyema masikioni mpwa Omary,



    ''Sasa njia tunayotokea si ndipo lilipo bafu, akisikia hatua za



    watu wawili zinatembea si atagutuka?" Omary alimuuliza happy Binti



    Mchungaji,



    "Hawezi kugundua bwana, twende acha uoga" Happy aliendelea



    kumwambia Omary,



    "Sasa si bora nisubiri Stoke bafuni aende chumbani?" Omary



    aliuliza,



    "Acha ujinga, mama anarudi sasa hivi na wadogo zangu, wakikukuta



    humu, je itakuwaje?" Happy nae aliuliza,



    "He!!!! Leo kweli siku yangu, haya twende" Omary aliongea kinyonge



    huku akisikitika.



    Happy akamshika mkono Omary, kisha akaanza kutoka nae nje kwa



    mwendo wa kunyata, yaani mwendo wa taratibu usiokuwa na vishindo.



    Walipofika usawa wa mlango wa baf na ndio muda huo Mchungaji Wingo



    alikuwa anafungua mlango ili akachukue sabuni chumbani.



    Ghafla tu Omary na Happy binti Mchungaji wakashuhudia mlango wa



    bafu ukifunguliwa na wote macho yakawatoka pima mithili ya mtu



    aliekwamwa na kitu kooni...





    Happy akauwai mlango wa bafuni, akaushikilia, tena kwa kuwa mlango



    wenyewe ulikuwa unafunguka kwa nje akaamua aulalie kabisa, Omari



    kuona hivyo akahisi kitakachomsaidia ni nduki tu. Akatoka mbio



    kuelekea nje,



    "we happy vipi, una nini leo?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti



    yake kwa sauti yenye mshangao huku akiusukuma mlango kwa utaratibu



    mzuri ili asimdhuru binti yake aliyekuwa amelala,



    "baba sijisikii vizuri, naona kizunguzungu", Happy aliongea huku



    akiwa bado amelala chini.

    Baba yake akamnyanyua, kisha akamrudisha chumbani kwake,



    "nikupelekee hospital mwanangu?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti



    yake kwa sauti ya huruma,



    "hapana baba, nafikiri ni tatizo la muda", Happy alijibu huku



    akijifunika shuka,



    "Hapana, lazima uende hospitali, ngoja nimalize kuoga nikupeleke"



    Mchungaji Wingo alimwambia mwanae,



    "Baba hii hali ya kawaida tu, itaisha" Happy alijibu baba yake,



    "Usichukulie vitu kirahisi rahisi, we jiandae tu nikupeleke"



    Mchungaji Wingo aliongea huku akitoka nje.



    "hii ya leo balaa, sijui baba angenichukuliaje?", Happy alijiuliza



    mwenyewe huku akiwa na tabasamu la mshangao na pia akimshukuru



    Mungu kwa kumuepusha na dhahama hii.



    *******************



    Omari alipotoka kwa mchungaji mbio mbio mpaka alipofika nyumbani,



    akasukuma mlango akaingia kwa fujo hadi ndani,



    "ehe, vipi mwenzetu?", Omari alipokewa na sauti ya Sajenti Minja



    aliyekuwa anamshangaa,



    "nilikuwa nakimbia kimbia, kuweka mwili fiti", Omari alijibu akiwa



    katika tabasamu la uongo huku akipumua bila mpangilio,



    "haya bwana, mi nilifikiri umefumaniwa na mke wa mtu uko, maana



    mbio ulizokuja nazo si mchezo", Sajenti Minja aliongea na kufanya



    vicheko vilipuke sebule yote.



    "Hanna mjomba, huku ugenini siwezi kufanya hivyo" Omary alijibu



    huku akijilazimisha kutabasamu,



    "Sisi tutajuaje bwana, nyie vijana mna mambo mengi" Mama Kayoza



    aliongea,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Hakuna mama" Omari aliongea huku akiingia ndani, akamwita Kayoza,



    wakaingia ndani,



    "duh, jomba uko noma", Omari alianza kwa mtindo huo,



    "vipi tena baab?", Kayoza akauliza kwa mshtuko,



    "mchungaji kanikuta juu ya mwili wa mwanae kaka", Omari akapasua



    lililomkuta,



    "naisi kama sijakusikia vizuri vile, ebu rudia", Kayoza akauliza



    kwa stahajabu,



    "nimesema kuwa, mchungaji kanikuta ndani kwake", Omari akaongea



    tena alichomaanisha,



    "ikawaje kaka?", Kayoza akauliza huku akiwa bado haamini



    anachoambiwa.



    Omari akamsimulia yote, mpaka alipofanikiwa kukimbia.



    "duh, pole mwanangu", Kayoza akampa pole Omari,



    "Cha kushukuru ni kuwa nimetoka salama" Omary aliongea huku akivua



    fulana yake,



    "Sasa huyo Happy kwa hali uliyomuacha nayo si itakuwa baba yake



    amejua?" Kayoza aliuliza,



    "Sijui bwana, kama baba yake atahisi labda inaweza kuwa tatizo, ila



    kuniona hajaniona" Omary alimjibu mwenzake,



    "Ila usirudie kufanya ujinga kama huo tena, yule mwanamke ni



    shetani angalia usiwe unamsikiliza kila anachokushawishi" Kayoza



    alimshauri Omary,



    "haina noma, kuna mpya gani hapa?", Omari akauliza,



    "kesho saa nne tutaenda kwa mganga", Kayoza akamtaharifu Omari.



    "maeneo gani",Omari akauliza,



    "mi mwenyewe sijajua bado", kayoza akajibu,



    "Dah, Mimi nina wasiwasi yasije yakatokea kama ya kwa yule mganga"



    Omary aliongea,



    "Sasa usiseme hivyo, cha muhimu ni kumuomba Mungu tu atusaidie"



    Kayoza alimwambia Omary,



    "Mungu tunamuomba ila pia tahadhari lazima" Omary alimwambia



    Kayoza,



    "Basis usiende, nitaenda Mimi na mjomba" Kayoza aliongea huku



    akionekana hajafurahishwa na maneno ya Omary,



    "Nitaenda tu" Omary aliongea kwa upole baada ya kugundua Kayoza



    amepaniki,



    "Sasa kama utaenda kwanini unaleta maneno ya kutishana?" Kayoza



    aliuliza,



    "Basi yaishe kaka, nisamehe kwa maana sikudhani kama utamaindi"



    Omary aliamua kujishusha ili mambo yaishe,



    "Hatugombani hapa, tunaeleweshana tu" Kayoza alimwambia Omary,



    "Sawa nimekuelewa ndugu yangu" Omary alijibu,



    "Kama umenielewa sawa, Mimi nipo sebuleni" Kayoza aliongea huku



    akielekea nje na kumuacha Omary akiwa amejimwaga kitandani.



    .*******************



    Kesho yake asubuhi Sajenti Minja aliwapitia wakina Kayoza, na



    safari ya kwenda kwa mganga ikaanza.



    Njia nzima hakuna alieongea, ndani ya gari kulikuwa na mziki laini



    wa unbreak my heart ulioimbwa na mwanamama wa kimarekani



    anayejulikana kama Tony braxton.

    Sajenti Minja alikuwa akiufatilia ule wimbo kwa sauti ya chini,



    Omari yeye alikuwa na mawazo yake, Kayoza pia alikuwa anafikiria



    anachokijua.



    "Huo wimbo vipi?" Kayoza aliuliza baada ya Sajenti Minja kurudia



    zaidi ya mara tatu kuupiga ule wimbo,



    "Si naupenda tu" Sajenti Minja alijibu kwa kifupi,



    "Mimi najua mtu akiupenda wimbo lazima kuna tukio linahusihana na



    huo wimbo" Omary alichangia,



    "Ebu acheni ujuaji, sasa mnataka niweke nyimbo gani? au niweke hayo



    manyimbo yenu yenye yo yo nyingi?" Sajenti Minja aliuliza,



    "Wewe tuambie tu kuhusu huo wimbo, acha kujikanyaga" Kayoza



    alimwambia mjomba ake huku akicheka,



    "Au shangazi hasomeki?" Omary akaongeza na swali,



    "Ebu niacheni bwana" Sajenti Minja aliongea huku akizima redio ya



    gari.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa mganga waliingia mishale ya saa sita kasoro robo, wakapokelewa



    na msaidizi wa mganga, ila kwa bahati nzuri hawakukuta foleni



    ndefu, watu walikuwa wachache tu.



    Baada ya nusu saa, zamu yao ikafika wakaingia ndani, kile kitendo



    cha kayoza kuingiza mguu katika mlango wa nyumba ya mganga, pale



    pale akabadilika na akawa katika taswira ya kutisha sana, ila



    alikuwa hawezi kutembea, aliganda pale pale, Sajenti Minja alipata



    uoga huku akidhani kuwa zile bakora za kipindi kile zinarudi tena



    kwa hiyo akakaa mbali kabisa na Kayoza hata alipogundua kuwa Kayoza



    ameganda pale, bado alikuwa anaogopa kumsogelea. Unacheza na viboko



    nini.



    Mganga akapelekewa taharifa kuhusu lile tukio, Mganga ikambidi



    atoke katika chumba chake cha kazi na kwenda mahali alipo Kayoza,



    alipofika akamuangalia zaidi ya dakika kumi, kisha mganga akafunga



    macho yake, alafu akatoa pumzi kumuelekea kayoza kwa njia ya mdomo,



    pale pale Kayoza akadondoka chini huku akiwa katika ile ile taswira



    ya kutisha.



    "Mtoeni nje" Mganga akawaamuru wamtoe nje, wakambeba wakampeleka



    nje, wateja waliokuwa nje wanasubiria tiba wote walikimbia



    walipomuona Kayoza katika hali ile ya kutisha.



    "Aliyekuja na huyu kijana yupo Wapi?" Mganga aliuliza huku



    akimuangalia msaidizi wake,



    "Yule kule" Msaidizi wake aliongea huku akinyoosha kidole kuelekea



    alipo Sajenti Minja,



    "Mbona amekaa mbali sana?" Mganga aliuliza huku akishangaa,



    "Hata sisi hatujui, labda anamuogopa" Msaidizi wake alijibu,



    "Kamuite" Mganga alimtuma msaidizi wake na yule bwana akaenda



    kumuita.



    Sajenti Minja alipofika alimsalimia mganga kisha mganga akawaambia



    aliefuatana na Kayoza amfuate ndani, Sajenti Minja na Omari



    wakamfuata mganga.



    Mganga alikuwa ni mwanamke wa makamo, alikuwa na macho mekundu



    sana, akamkazia macho Sajenti Minja, kisha mganga akasema,



    "Minja mna tatizo kubwa sana" Mganga aliongea na Sajenti Minja



    alishtuka kusikia mganga kamtaja jina lake, ila akapata matumaini



    ya kumaliza tatizo,



    "ila kwako naamini litaisha", Sajenti Minja alijitutumua na kumjibu



    mganga,



    "bibi yake mzaa baba yupo hai", Mganga akamtupia swali Sajenti



    Minja,



    "ndio mama", Sajenti Minja akajibu,



    "anaishi wapi?", Mganga akauliza tena huku akiwa amemkazia macho



    Sajenti Minja,



    "anaishi Bukoba vijijini", Sajenti Minja akajibu,



    "Sasa itabidi huyo kijana apelekwe uko", Mganga akawaambia Sajenti



    Minja,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "tumpeleke wapi?", Sajenti Minja akauliza ili apate ufafanuzi



    zaidi,



    "mpelekeni kijijini, kijijini kwa bibi yake" Mganga aliongea akiwa



    amefunga macho.........



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog