Search This Blog

KIJIJINI KWA BIBI - 4

 







    Simulizi : Kijijini Kwa Bibi

    Sehemu Ya Nne (4)



    ILIPOISHIA....

    -----------------------------

    "Ebu mtaje, ni upuuzi huu" Mkuu wa Polisi aliongea na kumfanya Babu wa monchwari atulie kidogo kwa maana alikuwa amelisahau jina la Sajenti Minja,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mbona humtaji?" Mkuu wa Polisi aliuliza kwa hasira na kumgutusha Babu wa monchwari aliyekuwa bado analitafuta jina la Sajenti Minja,



    Baada ya muda akalikumbuka jina, na akaona haina haja ya kuuficha uovu, akaamua kulitaja jina sasa. Kabla hajalitaja kwanza akaamua atabasamu, akatoa tabasamu la ushindi kwa maana alijua akimtaja Sajenti Minja ndio utakuwa mwisho wa mchezo na yeye ndio utakuwa mwanzo wa utajiri wake,



    Babu wa monchwari akaendelea kutabasamu....



    *********ENDELEA*********



    ...Babu wa mochwari akaendelea kutabasamu,



    "Mzee acha mzaa, nimekwambia umtaje huyo askari" Mkuu wa polisi aliuliza kwa ukali na kumfanya Babu wa monchwari ashtuke,



    "askari mwenyewe si yule mwenye nanii, nini ile, ha, nimemsahau, ila nikimuona nitamjua", Babu wa mochwari aliendelea kuongea kwa kujiamini, ila hakutaka kumtaja moja kwa moja Sajenti Minja kwa kuwa alitaka kumfanyia jambo la kushtukiza Mkuu wa Polisi,



    "mzee usinichanganye, maana sikuelewi", Mkuu wa polisi aliongea kwa ukali,



    "niamini mwanangu, huyo muuaji napajua hadi anapokaa", Babu wa monchwar aliendelea kumwaga sera zake za kumshawishi Mkuu wa Polisi amuamini,



    "Anakaa maeneo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza,



    "Anakaa maeneo ya kota, karibu na kanisani" Babu wa monchwari alijibu huku akitabasamu,



    "Mzee unachoongea ni kweli au leo umeamua kunichezea akili tu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimuangalia kwa jicho kali Babu wa monchwari,



    "Kama itabainika nakudanganya, niweke ndani hata miaka mitatu" Babu wa monchwari alijibu kwa kujiamini,



    "Na wewe ulimjuaje huyo mtuhumiwa, au mna mahusiano naye ya kindugu, ujirani au urafiki?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Babu wa monchwari,



    "Mi naona kama maswali yako yanapoteza muda vile, cha msingi ulichotakiwa kufanya ni kutuma vijana wako wakamkakate alafu ndio mahojiano yaanze" Babu wa monchwari alimshauri Mkuu wa polisi,



    "Usinifundishe kazi mzee, ninachokifanya hapa ninakijua" Mkuu wa Polisi aliongea kwa hasira,



    "Sawa mkuu, aya endelea na maswali" Babu wa Monchwari alijikuta ananywea na kuwa mtumwa kwa muda ule mfupi,



    "Je kwa ujuzi wako, mtuhumiwa anaweza kuwa na silaha ya moto kama bastola au bunduki?" Mkuu wa polisi aliendelea kuhoji,



    "Mimi ninapajua anapokaa tu, hayo mengine siyajui" Babu wa monchwari alijibu lakini sura yake ilionesha hakuyapenda kabisa hayo maswali, kwa maana aliona kama yanamchelewesha tu,



    "Nimekuuliza hivyo ili nijue tumuingiliaje tutakapoenda kumkamate" Mkuu wa polisi alimuelesha Babu wa monchwari baada ya kugundua hapendi kuulizwa,



    "Ana mwili wa kawaida tu, ni kakijana tu kachekibobu ambacho hakawezi kushika hata jembe" Babu wa monchwari alijibu,



    Mkuu wa polisi akalainika, akatoka nje, kisha akawatafuta askari watatu aliowaamini, akawapa bunduki, kila mmoja risasi thelathini, kisha akawapa yule Babu kama dira ya safari yao,



    "Mwanangu unanipa askari watatu!? hivi unamchukuliaje yule kijana?" Babu wa monchwari aliongea huku anasikitika,



    "Wana bunduki hao, kwa hiyo usiwe na shaka, watafanikisha tu hiyo misheni" Mkuu wa polisi aliongea huku akimtazama Babu wa monchwari,



    "Ujue awa wanaenda kupambana na dubwana, sio mtu wa kawaida, sasa unapowapeleka watatu tu itakuwa unafeli" Babu wa monchwari aliongea kwa sauti tulivu,



    "Lakini si uliniambia ni kijana tu wa kawaida?" Mkuu wa polisi alimuuliza Babu wa monchwari,



    "Ni kijana wa kawaida, ila anabadilika na kuwa likitu moja la ajabu sana, linatisha hakuna mfano" Babu wa monchwari alijibu,



    "Nitakuongezea askari wawili wengine wawili" Mkuu wa polisi aliongea na kuagiza askari wengine wawili wenye silaha na walipofika, Mkuu wa polisi aliwapa maelekezo.



    Baada ya hapo, mkuu wa polisi aliwaruhusu kuondoka, kisha akarudi ofisini kwake, akachukua simu yake ya kiganjani, akabonyeza namba anazojua yeye, inaonekana hakupata majibu anayoyataka, akarudia tena na tena kuipiga ile simu lakini ilionekana inaita muda mrefu mpaka inakatika bila kupokelewa,



    "minja nae ana matatizo sana, anajijua yeye ni mtu muhimu, alafu hapokei simu", Mkuu wa polisi alijiongelesha na nafsi yake huku akiiweka simu yake mezani.



    *******************CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Hiyo siku sajenti Minja aliamka mapema, na katika ratiba zake, zilionesha ofisini kwao anaitajika mchana wa saa sita, wazo alilolipata ni kwenda nyumbani kwa Babu wa mochwari, maana tokea wameachana pale kwa sheikh hajajua Babu ana hali gani.



    Ilipofika saa nne, Sajenti Minja alijipakia kwenye gari na kwenda nyumbani kwa Babu wa monchwari.

    Hakupata tabu sana kufika kwa maana alishawahi kufika hapo Siku za nyuma.



    "leo sijisikii hata hamu ya kupika, ila nitaenda kula kwa dada, ningewajulisha ila simu nimeiacha kwenye chaji", Sajenti Minja alijisemea peke yake, wakati gari yake inapaki mbele ya kajumba kamoja kaudongo, akatelemka kutoka katika gari, na kwenda kugonga katika mlango wa kale kajumba, akatoka mtoto mdogo wa kike, mwenye umri kati ya miaka kati ya miaka kumi na mbili na kumi na nne,



    "karibu, shikamoo", yule mtoto akamsalimia Sajenti Minja,



    "marahabaa, Babu yako nimemkuta?",Sajenti Minja alimuuliza yule mtoto,



    "yupi, yule anaefanya kazi hospitali?", kale kabinti nako kalimuhoji Sajenti Minja,



    "ndio huyo huyo", Sajenti Minja akajibu kwa kifupi,



    "yule ni baba yangu na sio babu yangu kama unavyodhani", kale kabinti kalimtaharifu sajenti Minja,



    "alah, we ni mtoto wake wa ngapi?", Sajenti Minja alimuuliza yule binti,



    "wa tisa", yule binti akajibu,



    "kwani nyie mmezaliwa wangapi?", akakatupia swali jingine, inavyoonekana kalimvutia katika kupangua maswali,



    "kumi na nne, ila watatu wamefariki", kale kabinti kalijibu,



    "oooh, haya, baba yuko wapi?",Minja akarudi katika topic iliompeleka pale,



    "ameenda polisi", yule binti akajibu jibu lilomshtua kidogo Sajenti Minja,



    "polisi?!",Sajenti Minja akauliza kwa mshangao,



    "ndio, nilimsikia anamwambia mama kuwa, eti anaenda kutoa taharifa za mnyonya damu",yule binti aliendelea kupasua moyo wa Sajenti Minja bila kufahamu,



    "ha!, sasa si kuharibiana uko!", Sajenti Minja aliongea bila matarajio yake,



    "kwani nini kaka?", yule binti akamuuliza Sajenti Minja huku akiwa na wasiwasi,



    "hakuna, shika hii kanunue soda", Sajenti Minja aliongea katika hali ya kuchanganyikiwa huku akimpa yule binti noti ya shilingi elfu mbili (2000).



    Sajenti Minja akapanda gari, kisha akaliondoa gari kwa mwendo wa kasi sana,



    "ngoja nikawape taharifa kule kwa dada, kisha tujue cha kufanya", Sajenti Minja aliongea kwa sauti ya chini ambayo ilijawa na kitetemeshi kutokana na habari mbaya alizozipokea muda mfupi uliopita.



    Alitumia dakika kumi na tano mpaka kufika jirani na mtaa wa wakina kayoza, kulikuwa kuna kona kama tatu, ndio afike katika nyumba ya dada yake.



    Kona ya kwanza aliikata vizuri huku akiwa katika mwendo ule ule wa kasi, kwenye kona ya pili ndo kulikuwa na shughuli, gari ya polisi ambayo alikuwemo Babu wa monchwari na askari nayo ilikua katika spidi ya juu, ndio ya mwisho, nao walibakia mita chache waifikie nyumba ya mama kayoza, ile kukata kona tu, ili gari lishike barabara ya nyumba ya wakina kayoza, na Sajenti Minja nae ndio alikuwa anaingia katika hiyo hiyo barabara inayoelekea kwa dada yake, basi kikasikika kishindo kikubwa sana ambacho hakikuwai kutokea pale mtaani, ni gari ya polisi iliivaa gari ya Sajenti Minja kwa ubavuni, ilikuwa ni ajali ya kutisha sana.



    Ni damu pekee ndizo zilionekana vizuri katika eneo lile na gari ya Sajenti Minja ilibondeka vibaya sana, haswa upande wa dereva. Hakuna mtu aliyeweza kuiangalia Mara mbili gari ya Sajenti Minja na hakuna mtu aliyekuwa na akili timamu aliyedhani katika ile ajali kuna mtu yupo hai....



    ..eneo lote liligubikwa na harufu ya damu, watu wakaanza kujisogeza mmoja mmoja, dakika mbili tu zilitosha kujaza watu eneo la tukio.



    Wasamalia wema wakatoa taharifa polisi baada ya kugundua kuwa gari moja lilikuwa na polisi.



    Kwa jinsi hali ilivyoonekana, ilikuwa vigumu kujua kama watu waliohusika katika ajali ni wazima, ilionesha wote wamekufa. Kwenye gari ndogo ambayo ndani alikuwepo Sajenti Minja peke yake, yeye aliganda pale pale huku damu zikimtoka puani na mdomoni, wakati katika gari ya polisi, dereva, babu wa mochwari na askari mmoja aliekuwepo mbele, wote walitokea kupitia kioo cha mbele na kuangukia juu ya gari la Sajenti Minja, wote watatu walikuwa wamepoteza maisha, na nyuma ya gari, hakukuwa na dalili yoyote iliyoonesha bado kuna mtu ana hati miliki ya pumzi yake, wote walikuwa wamepoteza uhai.



    Baada ya dakika kadhaa, gari ya polisi ilifika huku ikiongozana na ambulance ya hospitali ya mkoa wa Shinyanga.



    Mkuu wa polisi alishtuka sana baada ya kugundua kuwa lile gari dogo ni la Sajenti Minja, aliakikisha kila jambo linafanyika haraka.



    Madaktari waliofika pale waligundua kuwa yule aliyekuwepo katika gari dogo ni mzima, baada ya kumpima na kugundua kuwa mapigo yake ya moyo yanapiga kwa mbali sana.



    Wakamwekea mashine ya kusukuma hewa safi (oxygen) puani kwake, pamoja na dripu, kisha gari ya hospitali ikaondoka kwa kasi sana, huku ikipiga king'ora kumuwahisha hospitali majeruhi.



    Kisha gari ya polisi nayo iliubeba mwili wa Babu wa monchwari na wale askari waliopoteza maisha na kuwapeleka monchwari kuwahifadhi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Masikini Babu wa monchwari, toka kulinda maiti mpaka kulindwa kama maiti.

    Ndivyo dunia ilivyo, kifo chake kilifanya aukose utajiri aliokuwa anaenda kuupata Siku chache zijazo. Kifo chake kimeacha majonzi kwa ndugu, marafiki na familia yake. Na zaidi kifo chake kimeacha tabu sana kwa watu waliokuwa wanamtegemea.



    Alazwe pema peponi babu wa monchwari.



    *****************



    Mama kayoza na wanae walikuwa wanaongea maongezi yao ya kawaida pale nyumbani, ghafla wakasikia kishindo kikubwa sana,



    "mh!, na huku kuna kambi ya jeshi karibu nini?", Kayoza alimuuliza mama yake,



    "hakuna, ila iko kishindo inaweza kuwa tairi la gari limepasuka", mama Kayoza alijibu,



    "Sio tairi ya gari hilo mama, mlio wa tairi naujua" Omary alimbishia Mama Kayoza na kisha Omari peke yake ndio aliamua kwenda nje kuangalia kilichotea.



    Baada ya kusikia kelele za watu, nae alitoka tu mlangoni akamuuliza mtu mmoja aliekuwa anapita pale nje, akamjibu kuwa kuna ajali, baada ya kuridhika na jibu, Omari akarudi ndani.



    "vipi, umeshaangalia?",Kayoza akamuuliza Omari,



    "yah, ni ajali imetokea pale kwenye kona", Omari akamjibu,



    "mtu kagongwa nini?", Kayoza akaendelea kudadisi,



    "mimi sijafika, ila kwa kile kishindo, itakuwa gari imeikuta gari pale", Omari alijibu,



    "madereva wa siku hizi hovyo kabisa, enzi zetu hizi ajali zilikuwa ni nadra sana", mama Kayoza aliongea kwa manung'uniko,



    "mama ile kona mbaya sana", Kayoza aliongea kuwatetea madereva wa siku hizi,



    "hata kama", mama Kayoza alishikilia msimamo wake,



    "Wewe mama hushangai Sikh hizi magari yapo chungu mzima lakini ajali ni chache sana?" Kayoza aliendelea kuwatetea madereva wa kisasa,



    "Zamani magari yalikuwa machache ndio, ila miundombinu ilikuwa mibovu na ajali zilikuwa chache pia" Mama Kayoza aliongea,



    "Mimi nafikiri madereva wa Siku hizi ndio chanzo cha ajali nyingi, kwanza hata leseni zenyewe hawasomei, ila wanazipata kiujanja ujanja tu kwa kununua kwa rushwa" Omary aliongea kwa kumuunga mkono Mama Kayoza,



    "Bora wewe mwanangu umeongea, hili likayoza bishi sana, kama marehemu Baba yake vile" Mama Kayoza aliongea,



    "Basi yaishe, maana mmeamua kunichangia sasa" Kayoza aliamua kumaliza mada,



    "Sio yaishe tu, kwanza kubali madereva wa sasa si madereva ila washika usukani tu" Mama Kayoza aliongea kwa utani,



    "Sawa, kwa hiyo hata Mjomba Minja ni mshika usukani tu?" Kayoza aliuliza huku akicheka,



    "Sasa yule udereva ni Nazi yake?, yule ni polisi bwana" Mama Kayoza alimjibu mwanaye,



    "Tunapozungumzia madereva tunajumuisha wote, wanaobeba abiria na wanaoendesha magari yako binafsi" Kayoza aliamua kuipa nguvu point yake,



    "Haya sawa umeshinda, maana unachotaka ni kubishana tu na mimi sitaki" Mama Kayoza aliongea,



    Na katika kipindi hicho hicho kuna mtu alikuwa akigonga hodi mlangoni, kwa hiyo hodi iliyokuwa inapigwa ndio iliwakatisha maongezi yao,



    "pita, mlango uko wazi", Mama Kayoza aliongea kwa sauti ili mgonga hodi amsikie,



    "hodi tena, jamani salama hapa?", Kijana mmoja ambae anakaa nyumba ya pili kutoka pale, aliwasalimia huku akionekana mwenye wasiwasi,



    "kumbe ni wewe Tino, sisi wazima, we hujambo?", mama Kayoza akamuuliza yule kijana,



    "jambo ninalo mama yangu", yule kijana alijibu,



    "haya tuambie hilo jambo sasa", mama Kayoza aliongea kwa sauti ya ucheshi,



    "yule bro polisi, white white hivi, anaekujaga hapa amepata ajali pale kona", Yule kijana alitoa taharifa iliyowapa mshtuko wote waliopo pale,



    "ah!, kagonga mtu", Omari aliuliza huku akisahau kuwa yeye ndiye aliyesema kile kishindo sio cha kugongwa mtu, ila ni magari yamegongana,



    "gari yake imegongana uso kwa uso na gari ya polisi", Yule kijana aliendelea kuelezea alichokiona,



    "ile gari ya polisi wote wamekufa, ila yule bro kabebwa hajielewi, sijui hata kama atafika hospitali", Yule kijana alipigilia msumari wa mwisho katika maumivu ya mama kayoza na wanae, kisha akawaaga, ila hakujibiwa kutokana na hali iliyokuwepo.



    "Mama sasa tunafanyaje?" Kayoza aliuliza kwa sauti tulivu,



    "Twendeni tu hospitali, hatuna muda wa kupoteza" Omary alijibu na kipindi chote mama Kayoza alikuwa amefumba macho anasali, hali aliyokuwa nayo ni dhahiri alikuwa amechanganyikiwa.



    "Haya twendeni" Mama Kayoza aliongea huku akisimama,



    "Sasa mama tunaenda hospitali gani?, au unajua hospitali aliyopelekwa?" Kayoza alimuuliza mama yake huku akimshangaa,



    "Acha kuuliza maswali ya kijinga, wewe unadhani atapelekwa hospitali gani zaidi ya hospitali juu ya mkoa?" Mama Kayoza aliuliza huku akijitanda khanga,



    "Mama tunapoteza muda bure, twendeni tuwahi" Omary aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,



    "Si huyu mpumbavu anauliza uliza vitu visivyokuwa na maana" Mama Kayoza aliongea kwa hasira huku akiuelekea mlango wa kutokea.



    ***********************



    Majira ya saa sita mchana, mama Kayoza na wanae walikuwa wameshafika hospitali, moja kwa moja wakaenda kujitambulisha kwa madaktari, kisha wakaambiwa mgonjwa wao alipowekwa,



    wakatoka tena hadi katika chumba cha wagonjawa mahututi(I.C.U), walizuiliwa mlangoni na manesi, wakaambiwa bado madaktari wako ndani wanapigania uhai wa mgonjwa.



    Wakarudi kukaa katika benchi lililo jirani na kile chumba na wote wakakaa kimya huku kila mtu akiwaza jambo lake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mama Kayoza ndiye aliyeonekana amechanganyikiwa zaidi kuhusu hali aliyokuwa nayo Sajenti Minja.



    Baada ya nusu saa, Daktari alitoka kutoka katika kile chumba alichokuwa amelazwa Sajenti Minja.

    Mama kayoza na wanae wakamkimbilia, kisha wakajitambulisha, yule Daktari akawaangalia sekunde kadhaa, kisha akatingisha kichwa,



    "Aya baba tuambie hali ya mgonjwa wetu ikoje?" Mama Kayoza aliuliza huku machozi yakianza kumtoka,



    "Sasa mama unalilia nini, usilie bwana unakuwa unaleta uchuro" Kayoza alimwambia mama yake,



    "Ebu ngojeni kwanza, wewe mama ni nani yake?" Daktari alimuuliza Mama Kayoza,



    "Mimi ni dada yake, tumezaliwa baba mmoja na mama mmoja, baada ya kuzaliwa mimi ndio akafuata yeye" Mama Kayoza alijibu na kumfanya Daktari akili kuwa Mama Kayoza hayupo katika akili zake za kawaida,



    "Na nyie vijana ni zake?" Daktari aliuliza huku akiwageukia Kayoza na Omary,



    "Awa ni wanangu kabisa, yule ni mjomba wao" Mama Kayoza aliamua kuwajibia, maana aliona kama watachelewa vile kutoa jibu,



    "Basi kama ni hivyo, mama nakuomba utusubiri nje, acha niongee na awa watoto wa kiume" Daktari aliongea huku akimtazama Mama Kayoza,



    "Sasa utawaeleza nini awa watoto? Nieleze mimi mama yao, awa watoto wenyewe wananitegemea mimi" Mama Kayoza aliongea kwa hasira huku akianza kulia,



    "Mama msikilize daktari, unapopayuka unakuwa unakosea mama" Kayoza alimwambia Mama Yake,



    "Kaa kimya, tena funga mdomo wako, hujui uchungu ninaousikia hapa" Mama Kayoza alimkaripia mwanae huku akilia,



    "Basi usilie, unalilia nini sasa?" Omary aliuliza baada ya kuona hakuna maelewano kutokana na kilio cha Mama kayoza,



    "Muache alie, anastahili kulia kwa maana hata nyinyi mtalia muda mchache ujao" Daktari alimjibu Omary na kisha akawaambia habari mbaya ambayo ilipelekea mama Kayoza kupiga mueleka wa nguvu na kupoteza fahamu palepale...







    ...wakina Kayoza pamoja na manesi, wakambeba juu juu Mama Kayoza na kumkimbiza wodini haraka. Kayoza na Omari wakaambiwa watoke nje, mgonjwa anatakiwa kupewa huduma ya haraka.



    Wakina kayoza ikawabidi waende nje wakasubiri.



    "Aisee, mbona mitihani inaongezeka hivyo?" Kayoza alimuuliza Omary huku wakiwa wamesimama nje ya jengo la wodi aliyolazwa mama yake,



    "Ila hatupaswi kukata tamaa, mjomba ataamka tu, Mimi nina imani hiyo" Omary aliongea kwa ujasiri,



    "Ni ngumu sana, si umesikia daktari alivyosema?" Kayoza alimuuliza Omary,



    "Kuna daktari, lakini kumbuka kuna Mungu pia" Omary alijibu,



    "Sawa, ngoja tuone" Kayoza alijibu na kisha ukimya ukatawala huku wakiendelea kusubiri nje, ingawa hawakuwa wanachosubiri. Kila mmoja alikuwa kimya.



    Baada ya robo saa wakarudi ndani ya eneo la hospitali, wakaruhusiwa kwenda kumuona mama yao, wakamkuta amekaa kitandani huku dripu ikiwa inahesabu matone yake,



    "pole mama", Kayoza na Omari waliongea kwa pamoja,



    "mh, mmeongea tena na daktari", Mama Kayoza badala ya kuitikia, akawauliza swali,



    "hapana, nafikiri kama kuna mabadiliko yoyote yametokea atatuambia",Kayoza alimjibu mama yake,



    "Atawaambiaje wakati hamjamtafuta?" Mama Kayoza aliuliza,



    "Si angekuja hata hapa wodini ulipolazwa" Kayoza aliongea,



    "Bado akili zako hazijakomaa, sasa hata kama angekuja unadhani angeongea nini na Mimi wakati Mimi ni mgonjwa?" Mama Kayoza aliuliza,



    "Sasa hivi unajisikiaje mama?" Omary alimuuliza Mama Kayoza,



    "mh, naisi mwili hauna nguvu kabisa",Mama Kayoza alimjibu Omary,



    "mama nawe una presha ya ajabu, je ungeambiwa amekufa, si na wewe ungekufa!", Kayoza alimwambia mama yake,



    "we Kayoza acha ujinga, sasa tumeambiwa uhakika wa kuishi ni asilimi 30, wa kufa asilimia 70, huoni ni jambo la kuogopa sana?",Mama Kayoza aliongea kwa ukali kidogo,



    "mama wewe ni mlokole, ulichotakiwa kufanya ni kumuomba Mungu na si kukata tamaa", Kayoza alimwambia mama yake,



    "Kwani mlokole sio binadamu? kuna hisia za kibinadam uwa zipo kwa kila mtu" Mama Kayoza aliongea,



    "Hata kama, mbona sisi hatujapoteza fahamu baada ya kusikia hiyo habari?" Kayoza alimkazania mama yake kwa maswali,



    "Kwanza nyie ni watoto wa kiume, alafu pia inawezekana upendo wenu kwa Minja sio mkubwa kama niliokuwa nao Mimi" Mama Kayoza alieleza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kwa hiyo sisi hatumpendi mjomba?" Kayoza aliuliza,



    "Sijui wenyewe, kwanza tuachane na hayo, kamtafute daktari aje kunipa ruhusa mimi", Mama Kayoza akamwambia mwanae.



    Kayoza akaenda kumtafuta Daktari, baada ya muda kidogo, akarudi na daktari, daktari akampima pima mama Kayoza, kisha akamuuliza maswali mawili matatu, akamuandikia maelezo katika kikaratasi, alafu akamruhusu.

    Walichofanya wakina Kayoza ni kumrudisha mama yao nyumbani, kisha wao wakarudi hospitali.Hata wenyewe hawakuelewa pale hospital wanasubiri nini, ilimradi walikuwa wanakaa tu ili kumridhisha mama yao ambae aliwataka wasiondoke eneo la hospitali.



    *****************



    Mkuu wa polisi kazi kubwa aliyokuwa anafanya ni kuwajulisha ndugu na jamaa wa marehemu juu ya ajali iliyotokea, na kuwapa taharifa za kifo, ila hakutaka kabisa kuwaambia askari wengine kuwa, yeye ndio aliwaagiza, maana angewaambia ni lazima angewajulisha kuwa aliwatuma kumkamata mtuhumiwa wa mauaji ya kunyonya damu na yeye hakutaka ijulikane, kwa sababu angetangazia uma, basi huyo muuaji angeshtuka na kuhama mkoa, ila alichoamua ni kufanya upepelezi wake wa kimya kimya. Alipekua makabrasha yake na kutoa gazeti ambalo lilionekana la siku nyingi, kisha akalikunjua, mbele kulikuwa na picha ya Omari, akaiangalia ile picha kwa muda mrefu sana, akajikuta anatabasamu mwenyewe,



    "Yule mzee wa monchwari alimuona kweli muuaji, na kama alimuona alimjuaje, au lao lilikuwa moja?" Mkuu wa polisi alijiuliza huku akiwa bado anaitazama picha ya Omary iliyopo katika kipande cha gazeti.



    "kama yupo hapa shinyanga, nitamkamata tu, huu mkoa ni mdogo sana", Mkuu wa polisi aliongea huku akiwa bado anaendelea kuitazama ile picha ya Omari.



    Kisha akaikunja vizuri kama mwanzo, na kuirudishia katika droo ya meza yake ya pale ofisini, kisha akainuka na kwenda kabatini kisha akaitoa kofia yake na kuibandika kichwani.



    Baada ya hapo, akamwita dereva wake na kumuamuru ampeleke hospitali.



    Walipofika hospitali, Mkuu wa polisi alitelemka, kisha akaenda katika wodi alipokuwepo Sajenti Minja, ila alizuiliwa mlangoni na daktari,



    "mimi nataka nimuone tu ili nijue hali yake", Mkuu wa polisi alimwambia daktari,



    "hali yake sio nzuri kamanda", yule Daktari alimjibu mkuu wa polisi, alionekana kumfahamu haswa,



    "kuna mtu yeyote aliyekuja kumuona?", Mkuu wa polisi alimuuliza daktari,



    "ndio, kuna mwanamama mmoja, alikuja na vijana wawili, walijitambulisha ni ndugu zake", yule Daktari alimjibu Mkuu wa polisi,



    "walikwambia wanapokaa?", Mkuu wa polisi alimuhoji Daktari,



    "hapana, ila wameondoka mida hii hii, kwa sababu yule mwanamama alipoteza fahamu baada ya kumwambia hali ya mgonjwa",yule Daktari alijibu,



    "kama mpaka alipoteza fahamu, basi anamuhusu",Mkuu wa polisi aliongea hivyo.



    "Ila kiukweli inahitajika sala kweli ili huyu jamaa apone" Daktari alimwambia Mkuu wa polisi,



    "Kwa maana hiyo nyie uwezo umefika mwisho?" Mkuu wa polisi alimtupia swali Daktari,



    "Nikisema hapana, nitakuwa nadanganya, kwa hata ile tuliyofikia hakuna hata nyingine ambayo tunaweza kuipiga, sasa hapo ni uwezo wa Mungu tu ndio utamuweka hai" Daktari aliendelea kuongea anachokijua,



    "Sasa kama ni hivyo si ni bora mmuandikie barua ya kumuhamishia hospitali nyingine zenye uwezo" Mkuu wa polisi alitoa maoni yake,



    "Hata tuna uwezo, tungekuwa hatuna uwezo tungeshamuandikia barua hata ya kumpeleka india" Daktari alimjibu Mkuu wa polisi,



    "Kwani tatizo ni hasa?" Mkuu wa polisi aliuliza,



    "Uti wa mgongo umepata itilafu kidogo, kwa hiyo mawasiliano ya mwili hayapo na pia kichwa chake inaonesha kilipigizwa sana" Daktari alimjibu Mkuu wa Polisi,



    "Tuweke imani tu atapona, tusiwe tunavunjika moyo kwa kitu ambacho kipo nje ya uwezo wetu" Mkuu wa polisi aliongea,



    "Na hata akipona kuna mawili, anaweza kupata ulemavu wa maisha kutokana na tatizo la uti wa mgongo, au anaweza akapoteza kumbukumbu kwa muda mrefu au pia vyote vinaweza kumtokea" Daktari aliendelea kutoa Maelezo,



    "Cha muhimu uzima, hayo mengine ni kuendelea kumuomba Mungu" Mkuu wa Polisi aliongea,



    Wakiwa bado katika maongezi yao, mbele yao walikuja Kayoza na Omari,



    "vipi Dokta?" Kayoza alimuuliza Daktari,



    "vijana wenyewe ambao ni ndugu wa mgonjwa ni awa hapa",Daktari hakumjibu Kayoza, ila alimtaharifu mkuu wa polisi kuhusu wakina Kayoza, lakini Mkuu wa polisi hakuonekana kumsikiliza Daktari kabisaaa, badala yake, alimtumbulia macho Omary huku ile picha iliyopo katika kipande cha gazeti ikimjia....





    aliendelea kumuangalia Omari kwa dakika nzima mpaka Omari akapata wasiwasi na lile jicho kali la Mkuu wa Polisi,



    "we kijana unaitwa nani?",Mkuu wa polisi alimuuliza Omari, tena aliuliza kwa sauti ya ukali,



    "remmy, naitwa Remmy", Omari akataja jina la uongo, alikuwa na wasiwasi ila alijitahidi kuficha hofu yake mbele ya Mkuu wa Polisi,



    "Minja ni nani kwako?", Mkuu wa polisi akamuuliza tena Omari,



    "ni mjomba wangu", Omari akajibu huku akikwepesha macho yake yasigongane na macho ya Mkuu wa polisi,



    "Mjomba ako kivipi?" Mkuu wa polisi akamtupia swali lingine Omary,



    "Mimi ni mtoto wa Dada ake" Omary akajibu,



    "unamfahamu Omari Mkwiji?",Mkuu wa polisi akamtupia swali lingine tena, ila hili swali la kipindi hiki ndilo lililokuwa gumu kuzidi yote aliyoulizwa kabla, na hata jasho lilianza kumtoka,



    "hapana", Omari akajibu, wakati huo wote, Kayoza moyo ulikuwa unamuenda mbio sana, mpaka jasho likawa linamtililika mgongoni kuelekea sehemu za makalio,



    "mh!, kweli duniani wawili wawili", Mkuu wa polisi aliongea huku akimgeukia Daktari,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "vipi kamanda, umemfananisha na ndugu yako nini?",Daktari alimuhoji mkuu wa polisi,



    "hapana, kafanana na mtu mmoja hatari sana"Mkuu wa polisi aliongea kitu ambacho kilimpelekea Omari atoe ushuzi kwa mbali kwa ajili ya uoga,



    "kama ni mtu hatari, basi asingekuwepo eneo hili",Daktari aliongea kauli iliyompoteza kabisa mkuu wa polisi.



    "Kweli kabisa, kama angekuwa mtu mbaya basi asingesogea eneo hili" Mkuu wa polisi aliamua kumuunga mkono Daktari.



    "Na wewe ni nani yake Minja?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimuangalia Kayoza,



    "Na mimi ni mjomba wake pia, mtoto wa Dada yake" Kayoza alijibu huku akijitahidi kujiamini,



    "Kwa hiyo nyinyi ni ndugu?" Mkuu wa polisi aliwauliza huku akiwaangalia kwa zamu,



    "Ndio" Omary alijibu,



    "Mnakaa na mama yenu?" Mkuu wa polisi aliwauliza,



    "Ndio tunakaa nae" Kayoza alijibu,



    "Basi baadae nitarudu hapa, naomba niwakute ili mnipeleke nyumbani kwenu nikapajue na pia nimjue mama yenu" Mkuu wa polisi aliongea,



    "Sawa haina shida, tena itakuwa vizuri sana" Omary alijibu huku akijitahidi kutabasamu,



    "Alafu inaonesha wewe ni muongeaji sana kuliko mwenzako" Mkuu wa polisi alimwambia Omary huku nae akitabasamu,



    Baada ya maongezi ya hapa na pale pamoja na kutambulishana, Mkuu wa polisi aliagana na wakina Kayoza kwa ahadi ya kuwafuata baadae pale hospitali na wampeleke akapajue wanapoishi.



    "pppfffuuuu", wakajikuta wanashusha pumzi nzito baada ya Mkuu wa polisi kuondoka,



    "duh!, mwana mi makalio yameloana hapa", Kayoza ndiye alieanza kuongea,



    "dah!,we acha tu, ebu twende tukatafute maji ya baridi nje, maana naisi moyo uko kasi sana",Omari aliongea huku akitanguliza mguu wa kulia mbele, hali iliohashiria waondoke.



    *************



    Wakina Kayoza walirudi kwao muda huo huo, ila hawakutaka kumwambia mama yao kama wamekutana na mkuu wa polisi na kukubaliana nae kuwa jioni atakuja hapo nyumbani, walitaka kumfanyia kama kitu cha kushtukiza.



    Kibaya ambacho hawakukijua ni kuwa kwa kufanya ujinga wao huo wa kutaka kumshtukiza mama yako, ni kitu ambacho kinaweza kuja kuwagharimu wao wenyewe.



    "Haya nipeni habari za hospitali" Mama Kayoza aliongea huku akijibwaga katika kochi lilokuwepo hapo sebuleni,



    "Hakuna mabadiliko yoyote mama, bado hali ya mjomba ipo vile vile" Kayoza alijibu kwa masikitiko,



    "Jamani mfunge na kusali, mmuombee mjomba wenu, kwa ile hali aliyokuwa nayo ni hatari sana" Mama Kayoza aliongea kwa huzuni,



    "Mke wake umempa taharifa?" Kayoza alimuuliza Mama yake,



    "Hapana, ila nimeongea na baba na yeye amesema tusimwambie mke wa Minja kwanza, tuvute subira huku tukiangalia ni namna gani tumueleze" Mama Kayoza alijibu mwanae,



    "Mimi naona hakuna haja ya kumficha, mwambieni tu ukweli ili kama likitokea la kutokea, asimlaumu mtu" Kayoza alimshauri mama yake,



    "Hakuna anayemficha, ila tunatafuta wakati sahihi wa kumwambia hilo tatizo" Mama Kayoza alijibu,



    "Na kama make wake anampigia simu na hampati hewani? Huoni na hiyo itampa wakati mgumu?" Kayoza aliendelea kuuliza,



    "Kwanza unachotakiwa kujua ni kwamba Minja anapoondoka nyumbani kwake kikazi uwa habebi simu, hii simu anayotumia aliinunua kwa ajili ya hii kazi tu, alipanga akimaliza hii kazi na ile simu na laini yake anachoma moto" Mama Kayoza aliwaambia kitu wasichokijua,



    "Sasa inawezekanaje muda wote huo asiwasiliane na mke wake?" Omary aliuliza huku akionekana kutokubaliana na Maelezo ya mama Kayoza,



    "Kwani imewezekanaje wewe kutowasiliana na wazazi wako kipindi chote hiki?" Mama Kayoza alimtupia swali Omary,



    "Sasa mama mimi si Nina matatizo, ni hatari sana nikiwasiliana na ndugu zangu, naweza kuwaingiza matatizoni pia" Omary alijibu, ila alijibu kinyonge,



    "Ebu tuachane na hayo, pumzikeni ili jioni mrudi hospitali" Mama Kayoza aliongea huku akielekea chumbani kwake.



    ***********************



    Jioni, Mkuu wa polisi aliwafuata wakina Kayoza pale hospitali, Kisha akawachukua, ili wampeleke wanapoishi.

    Njia nzima walikuwa wanapiga stori za hapa na pale, walipofika katika eneo ambalo ajali ilitokea, Mkuu wa polisi akashtuka,

    "mhm, wanakaa huku, yule Babu nae si alikuwa anakuja huku, mh, bado nina wasiwasi na huyu Remmy, ntaendelea kumchunguza taratibu", mkuu wa polisi aliongea kimoyo moyo.

    Wakafika kwa wakina Kayoza.

    "karibu nyumbani", Kayoza alimkaribisha mkuu wa polisi,

    "asante mheshimiwa, kumbe mlikuwa karibu sana na eneo la ajali?", Mkuu wa polisi aliuliza kinafki,

    "hata kile kishindo tulikisikia",Kayoza akamjibu.

    Wakamkaribisha ndani, kisha wakamtambulisha kwa mama yao, mama Kayoza akafurahi sana kutembelewa na mtu mkubwa pale nyumbani kwake. Mama yao alipata faraja kutembelewa na mkuu wa polisi,



    "Sasa mbona hamkunitaharifu kama ugeni?" Mama Kayoza aliwauliza wanae,



    "Tulitaka kukufanyia shambulizi la kushtukiza" Kayoza alijibu huku aki tabasamu,



    "Siku nyingine muwe mnasema bwana, ili tumuandalie mgeni chakula" Mama Kayoza alimwambia mwanae,



    "Kweli lakini, mlitakiwa mseme bwana, sasa si mnaona mmenikosesha chakula?" Mkuu wa polisi aliongea kwa utani huku akicheka,



    "Ila hakuna ubaya kaka yangu, ngoja nikuandalie" Mama Kayoza aliongea,



    "Hapana usiangaike, nitakula siku nyingine" Mkuu wa polisi aliongea kwa ucheshi,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mama sisi yupo ndani" Kayoza aliongea huku akiinuka pamoja na Omary,



    "Mlitakiwa mkae tuongee na mgeni" Mama Kayoza aliwaambia wanae,



    "Nyie ongeeni tu, sisi tunarudi muda si mrefu" Kayoza alijibu huku wakielekea ndani na Omary na kuwaacha Mkuu wa Polisi na Mama yao wakiongea.



    Wakaongea sana kuhusu Sajenti Minja, undugu wa Mama kayoza na Sajenti Minja.



    Mwishowe, Mkuu wa Polisi aliamua kuaga, ila Omari na Kayoza walikuwepo wako ndani, ikabidi Mama Kayoza hawaite, ila alikuja Kayoza peke yake,



    "Naam mama, nimeitikia wito" Kayoza aliongea alipotoka ndani,



    "mgeni anataka kuwaaga", Mama Kayoza alimwambia mwanae,



    "sawa, karibu tena", Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi,



    "Sio karibu tena, unatakiwa umsindikize" Mama Kayoza alimwambia mwanae,



    "Amekuja na gari" Kayoza alijibu mama yake,



    "Hata kama amekuja na gari, unatakiwa umtoe nje, ndio uungwana upo hivyo" Mama Kayoza alimwambia mwanae,



    "Yule mwenzio yupo wapi, yeye hataki kuniaga?" Mkuu wa polisi alimuulizia Omary,



    "Alafu kweli, ebu kamuite na Ommy, aje amuage", mama Kayoza aliongea huku akimuangalia Kayoza,



    "OMMY?", Mkuu wa polisi aliuliza kwa mshangao....





    .."we Remmy njoo mgeni akuage",Kayoza aliita kwa sauti ya juu ili kumvuruga mkuu wa polisi.



    Mkuu wa polisi ikambidi anyamaze, maana hakuna aliejibu swali lake, na isitoshe hata mama Kayoza alihisi kuna kitu, haiwezekani Omary aitwe Remmy ghafla kiasi mile.



    Baada ya sekunde chache, Omary alitoka ndani na kujongea sebuleni kujumuika na wengine waliokuwako eneo hilo.



    "bwana mdogo mi naenda, nawakimbia bwana",Mkuu wa polisi alimwambia Omari huku akiwa amemkazia macho na pia alikuwa anatabasamu tabasamu moja la kinafki sana, ila hakuna aliegundua jambo hilo,



    "haya, karibu tena",Omari akamuitikia huku nae akilazimisha tabasamu lake halisi,



    "Mama ukiwa na shida ndogo ndogo kipindi hiki Minja mgonjwa, usisite kuniambia" Mkuu wa polisi alimwambia Mama Kayoza,



    "Hata usiwe na shaka baba angu, tushakuwa kama ndugu sasa" Mama Kayoza alijibu Mkuu wa Polisi



    Baada ya maongezi hayo machache, wakamtoa mpaka nje, kisha Mkuu wa polisi akajipakia kwenye gari, gari ikaondoka.



    Mama Kayoza na wanae wakarudi ndani.



    "ehe mwenzetu, hilo jina umeliokota wapi?",Mama Kayoza alimuuliza Omari kwa utani,



    "jina gani hilo",Omari nae aliuliza kanakwamba hajui,



    "si hilo la Remmy Ongala!",Mama kayoza akajibu.



    "Kwanza mama bado kidogo tu uharibu" Kayoza aliongea huku akijitupia katika kochi,



    "Niharibu nini tena,!!?" Mama Kayoza aliuliza kwa mshangao,



    "Ujue huyu mkuu wa polisi alivyomuona omary Kyle hospitali alimtilia shaka, na alipomuuliza jina lake, omary ndipo alipodanganya anaitwa Remmy. Sasa wewe tena ukamuita ommy" Kayoza alimlalamikia mama yake,



    "Sasa huo ni ujinga wa nani?, huo ni ujinga wenu, kama mlitambua huyu mkuu wa polisi atakuja hapa, kwanini hakunitaharifu?" Mama Kayoza aliuliza kwa ukali,



    "Sasa sisi tungejuaje kama yangetokea haya?" Kayoza nae aliuliza,



    "Sasa ndio yameshatokea, ujinga wenu utawaponza, sijui mkuu wa polisi ameyaacha hapa hapa au ameenda nayo?" Mama Kayoza aliongea kwa hasira,



    "atakuwa ameyaacha" Kayoza alijibu,



    "Atakuwa ameyaacha" Mama Kayoza alirudia maneno ya mwanae, ila yeye alirudia kwa kebehi huku akiwa amebana pua.



    Baada ya hapo Mama Kayoza akaenda sake ndani kwa hasira huku akiwaacha wakina Kayoza wakiwa wamekaa wanatazamana kwa jicho la kulaumiana,



    "Hakuna haja ya kumtafuta mchawi, sisi sote tumehusika" Omary aliongea huku macho yake yakielekea kwenye runinga,



    "Kweli, tulikosea kumficha mama, ila hakuna kilichoharibika" Kayoza aliongea huku akijilaza katika kochi.



    ********************



    Mkuu wa polisi hakuridhika kabisa na hali aliyokutana nayo, tayari akili yake ilimwambia kuwa kuna kitu kinafichwa katika familia ya wakina kayoza.



    "yule Babu alisema kuwa kuna mwenzetu anatuzunguka, alikua anamaanisha Sajenti Minja au?",Mkuu wa polisi alijiuliza mwenyewe, kisha akaendelea,"na huyu Remmy nae....simuelewi kabisa, nilisikia kwa masikio yangu mwenyewe yule mama kasema OMMY, mara yule kijana akabadilisha akaita Remmy, mh.., kuna kitu kinaendelea hapa, ngoja nichunguze mwenyewe", Mkuu wa Polisi alikata shauri na kuamua kuifatilia mwenyewe ile kesi.



    "Ila kama yule babu alisema amemsahau jina huyo askari anaetuzunguka, inawezenaje amsahau Minja?, ila hapana, hii kesi ngoja niichukue Mimi mwenyewe kimya kimya, nitaujua tu ukweli.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hata yule kijana atakuwa ndio Omary Mkwiji, sasa sitokurupuka kumkamata, nitaangalia kwanza namna ya kupata ushahidi, hii kesi imeshakuwa nyepesi tayari. Hapa ni kuendelea kujifanya sijui kitu, alafu nakuwa nawachunguza pole pole" Mkuu wa polisi aliendelea kuongea peke yake ndani ya gari.



    *******************



    Jumapili tulivu, Omari na Kayoza, huku wakiongozana na happy binti mchungaji, walikuwepo katika maeneo ya hospitali pembeni ya kitanda cha Sajenti Minja,



    Hapo Happy hakuvaa kistara kama anavyovaaga na badala yake alivaa suruali ya jeans iliyombana na juu alivaa fulana nyeupe iliyomkaa vema, ukiwa nae mbali huwezi kumjua ni kama yeye, labda ungepata bahati ya kumsogelea ndio ungemjua.



    Pembeni ya kitanda alichokuwa amelazwa Sajenti Minja, hakuna aliyeruhusiwa kuongea neno lolote kutokana na hali ya Sajenti Minja.



    Walimuangalia kwa dakika tano na kisha wakaenda kwenye eneo la kupumzikia watu walioenda kuwaangalia wagonjwa wao. Lilikuwa eneo safi lenye bustani na miti kadhaa kwa ajili ya kivuli, ila wao walijitenga sana na watu kwa ajili ya kuwa na Happy binti mchungaji.



    "Kumbe mjomba wenu ndio yule?" Happy alimuuliza Omary wakati wakikaa na kipindi hicho Kayoza yeye aliwaacha umbali kidogo, alikuwa bize na simu yake,



    "Ndiyo yule, vipi unamjua?" Omary akamtupia swali Happy binti mchungaji,



    "Yule ameshawahi kuzaba vibao yule, namkumbuka vizuri" Happy alijibu huku akicheka kutokana na tukio alilolikumbuka la kupigwa makofi na Sajenti Minja,



    "Alikupigia nini sasa?" Omary aliuliza kanakwamba hajui, kumbe anajua kila kitu,



    "Tuachane na hayo bwana, nunua ice cream tule" Happy aliamua kuipotezea hiyo mada,



    "Hapa hospitali hawawezi kuuza Ice cream, labda tutoke nje ya hili eneo" Omary alijibu,



    "Ngoja tupumzike kwanza, tutaenda baadae" Happy aliongea,



    "Kayoza njoo utupige picha mshkaji wangu" Omary alipaza sauti kumuita Kayoza aliyekuwa amejitenga na wao.



    *******************



    Wakati wakina Kayoza wakiwa nje ya hospitali, ndicho kipindi ambacho mama Kayoza na Mchungaji Wingo walikuwa wanaenda kumuangalia Sajenti Minja pia,



    walipofika, wakamtafuta Daktari, kisha wakaongea nae maneno machache kabla ya kuruhusiwa kwenda kumuangalia Sajenti Minja,



    "ila nimeamua kuvunja kanuni tu, kwa ajili ya heshima yako na mchungaji, kwa sababu muda wa kuangalia wagonjwa umeshakwisha",Daktari aliwaambia huku akielekea sehemu ilipo wodi aliyolazwa Sajenti Minja,



    "asante baba, maana nisingekuja leo, hakuna ambae angejua hali ya mgonjwa pale nyumbani",Mama Kayoza alimshukuru Daktari,



    "kwani wale vijana ambao unakujaga nao hapa ukai nao?",Daktari akamtupia swali Mama Kayoza,



    "kwanini baba?, wale ni wanangu, ninachokula ndicho wanachokula", Mama Kayoza alijibu baada ya kuuliza swali,



    "Basi hao wanao wametoka hapa muda si mrefu", Daktari alijibu,



    "alah!, basi mimi hawakuniaga",Mama kayoza alimaliza namna hiyo.



    "Sasa hivi wameshaujua mji, kila kona wanaijua" Mchungaji Wingo aliongea,



    "Tena wanazurura hao, alafu kibaya zaidi uwa hawaagi" Mama Kayoza aliongea,



    "Sasa Mimi naona mtoke, muda umeisha wakubwa zangu" Daktari aliongea huku akiwaimiza watoke,



    "Jamani baba angu ebu niongezee hata dakika mbili tu" Mama Kayoza alimuomba Daktari,



    "Mama uje baadae, wakubwa zangu wakikuta nimewaruhusu kuingia muda huu, kibarua change kitakuwa mashakani" Daktari aliongea huku akiendelea kuwahimiza watoke,



    "Mama tutoke tu, tuje baadae" Mchungaji Wingo aliongea huku akitangulia kutoka na Mama Kayoza akamfuata kwa nyuma.



    Wakamuona mgonjwa wao, kisha wakatoka kuelekea sehemu ya kupumzikia, kwa mbali wakawaona wakina Kayoza wako na Binti ambae hawakumtambua, tena huyo binti alikua wanabusiana(kiss) mdomoni na Omari, kila baada ya dakika.



    Mama kayoza na Mchungaji Wingo wakawa wameshika njia ya kwenda walipo wakina kayoza,



    "Mungu wangu, awa watoto wapumbavu sana" Mama Kayoza alilalama baada ya kuona wanamdhalilisha mbele ya Mchungaji,



    "Alafu hata yule binti waliekuwa nae ni mjinga, eneo la hospitali unavaaje vile kama huna wazazi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku wakiwa bado wanaelekea sehemu walipo wakina Kayoza.





    Wakiwa wanazidi kuwasogelea na wamebakiza hata zisizo nyingi sana, Mara pasipo kutegemea, Mchungaji Wingo akatoa sauti ya mguno,



    "mh!"



    "vipi mchungaji?",Mama Kayoza akauliza..



    .."kuna fikra zimenijia",Mchungaji Wingo akajibu katika sauti iliyotulia,



    "nishirikishe tu mchungaji",Mama kayoza, nae akaomba ubia,



    "ujue katika mazingira kama yale waliopo vijana wako, sio vizuri sisi kufika pale, maana tunaweza kufanya wakose raha kabisa, hasa yule aliyekuwa na binti"

    ,Mchungaji Wingo alitoa busara zake,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "kwanini tusiende tu, wakituona ndio watapata funzo, hawatarudia tena kufanya uovu katika eneo la wazi kama hili",Mama Kayoza aliongea katika sura iliyojaa jazba,



    "hapana mama, wewe waache tu, ila ukifika nyumbani uwaambie vyote ulivyoviona",Mchungaji alimwambia Mama Kayoza



    "sawa mchungaji, ila hawa watoto wamenihaibisha jamani, loh!",Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko.



    "ni ujana tu mama, ila itafika kipindi watajua kuwa wanachofanya ni ujinga",Mchungaji aliongea kwa upole.



    "Yaani wanafanya ujinga uliokithiri, badala wakae hata wafunge wamuombee mjomba wao, wao wanazidi kujiongezea dhambi" Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko,



    "Bado hawajawa na akili hizo, ila kama nilivyosema kuwa itafika muda watajitambua" Mchungaji Wingo alijibu,



    "Alafu na yule binti sijui wa wapi?, ebu mchungaji niruhusu tu nikawaone nimtambue na yule binti" Mama Kayoza aliongea,



    "Kwa jinsi alivyovaa vile, ukienda pale itakuwa kama anakudhalilisha tu mwanamke mwenzake. Sio uvaaji ule, mi mwanangu akivaa vile namchinjilia mbali" Mchungaji Wingo aliongea kwa hasira,



    "Haya baba, tuondoke tu, nitaenda kupambana nao nyumbani" Mama Kayoza aliongea.



    Wakabadili njia na kushika njia iendayo nje ya hospitali. Hakuna aliyekuwa anaongea tena, kila mtu alikuwa na wazo lake, ila Mama Kayoza alionekana ana hasira nyingi zilizochanganyikana na fedhea iliyotokana na kitendo kilichofanywa na watoto wake.



    Hasira aliyokuwa nayo ilisababisha mpaka machozi yaanze kuchomozà katika ncha za macho yake,



    "Mbona kama unalia mama?" Mchungaji Wingo alimuuliza mama Kayoza,



    "Hapana, ni hasira tu. Yaani away watoto" Mama Kayoza alijibu Mchungaji Wingo,



    "Hutakiwi kuwaza sana, utavuka mipaka na mwisho itakuwa dhambi, kuwa na moyo wa hekima mama" Mchungaji Wingo alimwambia Mama Kayoza,



    "Sawa nimekusikia mchungaji" Mama Kayoza aliongea huku akijifuta machozi,



    "mama unaelekea wapi sasa hivi?",Mchungaji alimuuliza mama Kayoza wakiwa nje ya geti la hospitali,



    "nataka nipitie hapo sokoni nikachukue mahitaji ya nyumbani kidogo",Mama Kayoza alimjibu Mchungaji Wingo.



    "ok, ni vizuri, maana hata mimi naelekea uko uko",Mchungaji Wingo aliongea huku akionekana kuvutiwa na jibu la mama Kayoza.



    Kisha akawasha gari yake, na kuelekea maeneo ya sokoni.



    *******************



    Mkuu wa Polisi aliamua kuifatilia ile kesi kwa elimu yake yote aliyonayo, kwa mbinu zake zote alizokuwa nazo na kwa uzoefu wake wote aliokuwanao, ila hakutaka kumshirikisha askari yoyote, kwa maana alishakosa imani na askari wake.



    Na kwa kuanza, aliamua kumfuatilia Omari kwanza. Aliamini kwa kiasi kikubwa, kuwa ile picha iliyotolewa katika magazeti, ni taswira ya Omari kabisa, ila alichokuwa anafuatilia ni ushaidi tu.



    "Ukila na kipofu hutakiwi kumshika mkono" Mkuu wa polisi aliongea na kutabasamu mwenyewe.



    "na nikipata ushaidi wa kutosha tu, nahakikisha Sajenti Minja nae anafunguliwa mashtaka, lakini kama atapona, kama akifa na yenyewe itakuwa sawa, kwa maana yeye ni msaliti. Anakaa na mtuhumiwa na hasemi, hata kama ni ndugu yake inatakiwa afuate sheria", Mkuu wa Polisi aliongea na nafsi yake, kisha akaendelea,.



    "kesho nitamtafuta kijana mmoja wa mtaani, anisaidie kuchunguza taratibu hii kesi, siwezi kumpa askari hii kesi, bora nimtafute kijana achunguze taratibu nitamlipa pesa, tena itakuwa vzuri zaidi kama huyo kijana atakuwa anaishi mtaa ule ule wanaoishi wao".



    Hayo ndiyo maamuzi aliyofikia mkuu wa polisi. Na uzuri wa huyu bwana ni kusimamia maneno yake, ni mtu aliyekuwa anasifika kutokana na utendaji kazi wake na pia kulikuwa na tetesi kuwa huyu ndiye atakuwa mkuu wa polisi wa nchi nzima mwaka unafuata.



    ******************

    Wakina Omary walikuwa bado wanaendelea kula starehe zao na walikuwa hawana habari kama tayari mama yao alikuwa amewaona.



    Hiyo siku Omary aliamua kujikumbushia maisha yake ya chuo, kukaa katika garden na mtoto wa kike kama vile huku wakila ice cream ndio ilikuwa maisha yake.



    Kipindi chote hicho Kayoza alikuwa amekaa kimya ingawa alikuwa anataka kuondoka ila hakutaka kumwambia Omary kwa maana alihisi kama atamuharibia au atamkatishia starehe mwenzake, na alipofikiria kumtoroka pia aliwaza akifika nyumbani akiulizwa mwenzake yupo wapi? atajibu nini na walitoka pamoja?

    Ikabidi akae kinyonge tu huku akicheza game katika simu yake alipochoka alikichukua kitabu chake cha riwaya kilichoitwa FAZA WA KANISA kilichoandikwa na mwandishi ALEX KILEO, akawa anakisoma.



    "jamani eee, mi naona tuondoke sasa",Kayoza aliwaambia wenzake baada ya kusoma kurasa kadhaa za kile kitabu cha riwaya,



    "dah!, kweli mzazi, maana tumeuza kichizi", Omari alijibu kwa lugha ya vijana, akiwa na maana ya kwamba, wamekaa sana,



    "tunaenda kwa miguu au?",Kayoza akauliza,



    "leo kwa kuwa niko na malkia wangu hapa, nitakodi taxi", Omari aliongea huku akimshika mkono Happy binti wa Mchungaji.



    "Tutembeeni tu, kwani tunawahi wapi?" Happy binti Mchungaji aliuliza huku akitabasamu,



    "Hatutaki uchafuke, mrembo kama wewe ukichafuka kisa umetembea kwa miguu itakuwa aibu kwetu" Kayoza aliongea kwa utani na kufanya wenzie wacheke,



    "Mbona mi nimeshazoea jamani" Happy binti mchungaji aliongea huku akideka kwa Omary,



    "Umezoea kwenu ila sio kwangu. K ita gari mwanangu tusepe" Omary alimuagiza Kayoza kwa nyodo na kumfanya Kayoza aondoke huku akitabasamu kutokana na mbwembwe za jamaa yake huyo.



    Wakatafuta taxi, wakakubaliana bei na dereva taxi, kisha safari ya kurudi nyumbani ikaanza.



    Kayoza alikaa kiti cha mbele na Omary na Happy binti mchungaji walikaa siti za nyuma kwa ajili ya kuwa huru kufanya mambo yao kama wapenzi.



    Walipokaribia katika maeneo ambapo Sajenti Minja alipata ajali, wakamshauri dereva taxi apunguze mwendo kwa maana kulikuwa na kona mbaya na pia bado walikuwa na kumbukumbu ya tukio baya lililomkuta Sajenti Minja katika eneo hilo.



    Wakakata kona ya kwanza vzuri tu, ile wanakata kona ya pili tu, dereva taxi akafunga breki kali sana, ila alichelewa, maana tayari alishaikwangua kwa nyuma gari iliyopo mbele yake, ilikuwa ni gari ya Mchungaji Wingo ambayo ndani pia alikuwepo mama Kayoza.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Katika gari waliyokuwamo wakina kayoza, Happy binti Mchungaji alikuwa kachanganyikiwa kabisa baada ya kugundua gari iliyopo mbele ni ya baba yake, na omary pia alikuwa katika hali hiyo ya kutokujielewa, maana aliamini kabisa leo ndio arobaini yake.



    Mchungaji Wingo na Mama Kayoza wakatelemka katika gari ya Mchungaji, na Mchungaji akionekana mwenye hasira ya kukwanguliwa gari yake, akawa anaifuata taxi waliyokuwamo wakina Kayoza, Omari na Happy binti wa mchungaji, hapo ndipo hali za vijana hao zikawa mbaya zaidi kwa hofu.



    .Dereva taxi baada ya kuona yule dereva wa gari aliyoigonga anakuja, kwa haraka sana happy alimwambia taxi atelemke kwa maana yule anaekuja ni baba yake na yeye hataki ajue kama yupo ndani, Dereva taxi nae akaamua kutelemka, ili akabiliane na Mchungaji Wingo,



    "kijana leseni yako umekatiwa na serikali au umeipata mitaani?", ndio swali la kwanza kuuliza Mchungaji baada ya Dereva taxi kushuka, Mchungaji Wingo alikuwa na hasira sana na hilo lilionekana wakati anaongea maana sauti yake ilikuwa inatoka na mitetemo ya hasira,



    "nisamehe mzee wangu",Dereva taxi alikimbilia kujitetea badala ya kujibu swali, pia dereva taxi alishapata yoga kutokana na hasira alizokuwa nazo,



    "inaonesha hata shule hukuenda, maana nimekuuliza swali jingine, we unaniambia vitu vingine",Mchungaji aliendelea kumshambulia Dereva taxi ambae aliamua akae kimya.



    "Leseni nimepata veta, nilisomea pale" Dereva taxi alijibu huku akitetemeka,



    "Angalia sasa ulivyo mjinga, jibu la swali la kwanza unaweka katika swali la pili" Mchungaji Wingo aliongea huku akitoa tabasamu lisilo la furaha, lilikuwa tabasamu la karaha.



    Wakiwa bado wanaangaliana, Dereva taxi akiwa hana la kuongea kutokana na maneno ya Mchungaji Wingo, na Mchungaji Wingo akiwa anasubiri Dereva taxi aongee ili aendelee kumshambulia.



    Mlango wa mbele wa taxi ukafunguliwa, akatetelemka Kayoza,



    "shikamoo Mchungaji",Kayoza akasalimia kwa mashaka huku akimtazama mama yake aliyekuwa anamuangalia kwa jicho Kali mpaka Kayoza akawa anajiuliza ni kosa gani amefanya mpaka mama yake amuangalie kwa jicho Kali vile,



    "marhaba, kumbe wewe ndio umemkodi huyu?",Mchungaji alimuuliza kayoza huku kidole chake cha shahada kikimuelekea Dereva taxi,



    "ndio mchungaji",Kayoza akajibu kwa unyenyekevu,



    "alichokifanya hapa unakubaliana nacho?",Mchungaji alimtumpia swali jingine Kayoza,



    "hapana, ni bahati mbaya",Kayoza alimtetea Dereva taxi,



    "angaliaga vitu vya kutetea kijana, uwaga nakuona una busara sana",Mchungaji alimwambia Kayoza,



    Kayoza akaamua kukaa kimya,



    "ee, nijibu kijana, kwa hiyo angetugonga tukafa bado ungeng'ang'ania bahati mbaya?",Mchungaji aliendelea kung'aka kwa sauti ya upole iliyojaa hasira,



    "naomba unisamehe mzee wangu, nitakulipa pesa ya kupaka rangi katika eneo nililolichubua",Dereva taxi alidakia pasipo kuhusishwa, maana aliona ili kujiepusha na ile habari pale basi ni lazima akubali kulipa gharama za uharibifu wa gari ya Mchungaji,



    "acha uhuni bwana mdogo, nani kakwambia anahitaji pesa yako?"Mchungaji aliongea kwa ukali,



    "nakubali nimefanya kosa mzee, naomba unisamehe",Dereva taxi aliongea kwa huruma kiasi kwamba machozi yalikuwa yanataka kumtoka,



    "Imeandikwa Samehe saba Mara sabini" Kayoza aliongea huku akitupa jicho lake pembeni lisikutane na jicho la mchungaji na kufanya mchungaji atoe tabasamu huku akimuangalia Kayoza,



    "Imeandikwa na nani, sura ya ngapi na mstari wa ngapi?" Mchungaji alimuuliza Kayoza ambaye alikuwa hana jibu akabaki tu kuangalia chini,



    "Ni neno la Mungu liko kwenye biblia" Kayoza alijibu na kumfanya Mchungaji acheke kabisa, kwa maana maneno anayoongea Kayoza yalikuwa yanamtoka tu bila kutarajia,



    "Dereva we nenda bwana, mimi sina neno na wewe ila nilitaka nikufundishe ili usirudie kwa watu wengine",Mchungaji alimwambia Dereva taxi,



    "asante sana mzee wangu",Dereva taxi alishukuru



    "Usinishukuru Mimi, mshukuru huyu Mteja wako alietoa neno la Mungu" Mchungaji Wingo aliongea huku akiondoka eneo alilokuwepo Kayoza na Dereva taxi,



    "Man turudi katika gari tuendelee na safari" Dereva taxi alimwambia Kayoza,



    "Wapeleke hao, Mimi itabidi niondoke na hao wazee" Kayoza alijibu na kumfanya Dereva taxi ageuke na kwenda kupanda katika gari yake na kuliondoa kwa mwendo wa kistaharabu.



    "we Kayoza mwenzako yuko wapi?",Mama Kayoza alimuuliza mwanae wakati anaingia katika gari ya Mchungaji Wingo,



    "khe!, bi mkubwa hata sijakaa vizuri umeanza na maswali, ngoja nitulie kwanza",Kayoza alishangaa mama yake kuanza kumshambulia ndani ya gari,



    "nijibu bwana",Mama alisisitiza tena kwa hasira,



    "Alafu mbona unaonekana una hasira sana na Mimi, nimekukosea nini leo?" Kayoza aliuliza huku akimuangalia mama yake,



    "Wewe usiniletee ujinga ujue, si nimekuuliza hapa? Badala unijibu na wewe unauliza, ndio ulivyofunzwa hivyo na shangazi zako" Mama Kayoza aliuliza huku macho yake yakiwa mekundu kwa ajili ya hasira aliyokuwa nayo,



    "Umeuliza nini kwani?" Kayoza aliuliza tena na kumfanya Mama yake azidishe hasira,



    "Mpumbavu mwenzako yupo wapi?" Mama Kayoza aliuliza kwa sauti ya juu mpaka Mchungaji akatabasamu kwa namna Mama Kayoza alivyopaniki,



    "Atakuwa yuko nyumbani",Kayoza alijibu bila ya uhakika kwa maana hakujua kama Omary ataenda nyumbani au atakuwa bado anatanua na Happy binti Mchungaji,



    "nyie hospitali si mlikuwa pamoja, sasa imekuaje mnarudi kwa mafungu?",Mama kayoza akaongeza swali lingine lililomshtua Kayoza, ila akajifanya yupo sawa tu,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "we umejuaje tulikuwa hospitali wakati hatukukuaga?",Kayoza nae akamtupia swali mama yake,



    "sisi ndo tumetoka huko na tuliwaona",Mama Kayoza akamjibu mwanae



    "mlikuwa upande gani, mbona hukuja eneo tulilokuwepo?",Kayoza akaendelea kuhoji,



    "ningekuja vipi wakati mlikuwa na mkwe pale, si ndio kilichowaleta huku shinyanga, kutafuta wanawake tu wanaovaa hivyo hovyo",Mama kayoza alimjibu mwanae wakati anatelemka katika gari kuashiria wamefika, hill jibu lilimshtua Kayoza kwa maana aliamini kabisa Mchungaji atakuwa amewaona wakati Wapi na Happy.



    Mama Kayoza na Mwanae baada ya kutelemka katika gari ya Mchungaji Wingo, wakamuaga mchungaji,



    "Kijana kuweni makini sana na mabinti wa watu, huku shinyanga ni kubaya sana" Mchungaji Wingo alimwambia Kayoza kisha hakutaka kusubiri neno lolote kutoka kwa Kayoza, Mchungaji akaondoa gari yake kwa mwendo wa taratibu na kumuacha Kayoza akiwa anaitafakari ile kauli ya mchungaji Wingo ya kuwa makini na mabinti za watu,



    "We Kayoza twende ndani, mbona umeganda kama kichuguu?" Mama Kayoza alimgutusha mwanae kutoka katika tafakari na kumfanya Kayoza atabasamu ili mama yake amuone yuko sawa.



    Wkuingia ndani, ambapo walimkuta Omari anaangalia Runinga, Omari akamsalimia mama Kayoza.



    "mkwe umemuacha wapi?",Mama Kayoza akamuuliza Omari huku akiwa bado na hasira zake,



    "yupi tena huyo mama?",Omari akauliza huku anacheka kinafki, lakini nae tayari kengele ya hatari ilikuwa imeshagonga kichwani mwake, alidhani tayari picha yake na Happy Binti Mchungaji ilikuwa imeungua kumbe masikini ya Mungu hakuna kati ya Mama Kayoza wala Mchungaji Wingo aliyegundua kuwa yule binti waliyekuwa nae ni Happy binti Mchungaji.



    "jifanye tu humjui, kumbukeni mna matatizo, msitake kujiongezea mengine",Mama Kayoza alimaliza huku akielekea chumbani kwake na kuwaacha vijana wake wakitazamana.



    "vipi, kashtukia nini?",Omari alimuuliza Kayoza,



    "anadai alituona hospital, ila sijajua kama wamegundua yule demu tuliekuwa nae ni happy, maana kauli zao sizielewi elewi zimekaa kimafumbo mafumbo ",Kayoza alimjibu Omari,



    "He hii hatari, na mchungaji nae anasemaje?" Omary alimuuliza Kayoza huku wasiwasi ukianza kuchukua nafasi yake,



    "Huyo hakuongea kitu kabisa, ila wakati ametushusha hapo nje, ameniacha na kauli tata sana, amesema tuwe makini na mabinti za watu" Kayoza alimwambia Omary,



    "Itakuwa wamegundua nini?" Omary aliuliza kwa wasiwasi,



    "Ila kama wangemgundua yule binti ni Happy wangetuambia tu, hakuna mzazi anaeweza kuvumilia mwanae kujiingiza katika mapenzi kabla ya ndoa, tena ukizingatia Baba mwenyewe ni mchungaji" Kayoza aliongea kwa kujipa moyo,



    "Ila kweli man" Omary alimsapoti mwenzake,



    "Nilivyoshuka katika taxi, mbona sikuwaona tena ndani ya

    taxi? Maana kila nikijitahidi kuangalia sioni mtu", Kayoza aliuliza huku akicheka,



    "tuliinama nyuma ya siti mwanangu", Omari alijibu kwa hali ya ushindi,



    "mimi nilijua ndio tumekwisha",Kayoza nae akachomekea,



    "we acha tu mwanangu, nilivyoona dereva kaingia ndani, nilimwambia awai, alivyonishusha tu, nikampatia mpunga wake kisha nikamwambia amuwaishe wife",Omari aliongea kwa kujiamini,



    "ila mjomba, una zali",Kayoza alimfagilia Omari,



    "mi bad number kaka, na nilipofika, nikamnyonya mate Happy hapo nje",Omari aliendelea kujinadi, lakini Kayoza hakuonekana kumsapoti tena na badala yake alikodolea macho nyuma ya Omari, ikambidi Omari ageuka aangalie anachoangalia Kayoza, hapo sasa ndio akakutanisha Macho yake na Macho ya Mama Kayoza ambaye alikua kasimama nyuma ya kiti alichokaa Omary huku akiwaangalia kwa jicho la hasira, hasira zaidi ya hasira alizokuwa nazo mwanzo......



    ..."nyie watoto mjue ni wapumbavu sana?",mama Kayoza aliongea kwa jazba, wakina Kayoza walitulia kimya, kisha akaendelea,



    "mi nilifikiri kwa elimu ya chuo kikuu mliokuwa nayo mnaweza mkawa mnafikiri vitu vya maana, kumbe muda wote mnafikiria upumbavu tu, naishi na wajinga tu humu ndani tena mtanipa ugonjwa wa moyo bure, mi namfikiria kaka yangu, nyie mnafikiria mapenzi, hivi mnataka mimi nifanyaje?",Mama Kayoza aliuliza akitegemea kujibiwa, ila hakuna hata aliemjibu,

    "eti Kayoza, si nawauliza nyie, ee?",Mama Kayoza aliongea huku akimuangalia mwanae,

    "sasa mama unataka nikujibu nini",Kayoza aliongea katika sauti ya kupaniki",

    "unamjibu nani hivyo?",Mama Kayoza alipamba moto, tena wa gesi, Kayoza akanyanyuka alipokaa na kuelekea chumbani kwao,

    "endelea tu na kiburi chako, ila kina mwisho wake, na nina uhakika Kayoza utakuja kuniua na ugonjwa wa moyo", Mama Kayoza alimwambia mwanae wakati anaondoka, kisha akamgeukia Omari,

    "Omari mimi sikujui ila nakulea kama mwanangu, hata siku moja sikuwai kufikiria kama utafanya kitendo kama nilichokiona leo, tena hadharani, alafu unakuja hapa unaanza kujisifu kwa ujinga uliokuwa unaufanya!?, wewe unafikiri heshima ninayokupa itakuwa katika kiwango gani?, ee!, nijibu Omari" ,Mama Kayoza alikuwa kama mbogo aliyejeruhiwa na risasi,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mama naomba sana msamaha, ila haya ni mapito ya ujana mama yangu",Omari aliongea kwa hekima,



    "mbadilike, nyie ni wasomi bwana, nawashangaa mnavyofanya ujinga",Mama Kayoza alimwaga sera zake,



    "nakuahidi mama, haitokaa itokee tena, naomba uniamini mama yangu",Omari aliongea katika sura ya majuto na upole sana,



    "shauri yenu bwana, kamuite mwenzio, muende mkaninunulie maziwa mie",Mama Kayoza aliongea huku anaelekea jikoni.



    Omary akatoka sebuleni na kuelekea chumbani ambapo ndipo Kayoza alikuwepo,



    "Twende tukanunue maziwa, mama ametutuma" Omary alimwambia Kayoza,



    "Bado anawaka au amepoa kidogo?" Kayoza alimuuliza mwenzake,



    "Amepoa, ila dah..inawezekana ni kweli tumefanya kitendo cha kipuuzi" omary aliongea kwa majuto kuonesha kuwa amekosa,



    "Uwa inatokeaga, ila kumbuka kuwa hata katika kipindi cha huzuni uwa kuna muda mchache wa furaha" Kayoza aliongea huku akivaa fulana yake,



    "Kweli ila sio kwa kiwango kile tulichofikia, tulipitiliza" Omary aliongea huku akitoka nje kumfuata mwenzake.



    "Kawaida tu bwana, haina haja ya kujuta wala kusikitika" Kayoza aliongea huku nae akitoka,



    ******************



    BAADA YA MIEZI MIWILI



    wakina Kayoza na Mkuu wa polisi wakiwa katika eneo la hospitali, Mkuu wa polisi alitaka kuwatega tena, safari hii alitaka kujua kama awa vijana wameshawahi kuishi mkoani Dodoma.



    "Nyie mmezaliwa mkoa huu huu?" Mkuu wa polisi aliwauliza,



    "Mimi nimezaliwa bukoba" Kayoza alijibu kwa ufasaha huku akitabasama,



    "Na remmy wewe ulizaliwa wapi rafiki yangu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimfunga Omary kifungo cha juu cha shati,



    "Mimi kwetu Tanga na ndipo nilipozaliwa?" Omary alijibu huku nae akitabasamu,



    "Elimu zenu zopoje, yaani mmesoma mpaka kidato cha ngapi?, maana nyie ni ndugu zangu sasa, nataka nijue elimu yenu ili niwaangalizie hajira" Mkuu wa polisi aliuliza swali kwa kutumia akili nyingi ili aweze kuwataka hisia wakina Kayoza na atimize upelelezi wake,



    "Sisi tuna elimu ya chuo, chuo kikuu" Kayoza alijibu huku akidhani ni sifa kubwa kusema ana elimu ya chuo, hajui kuwa kama anapelelezwa,



    "Chuo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akitabasamu,



    "Chuo kikuu cha Dodoma, UDOM" omary alitoa jibu lililoanza kumpa mwanga mkuu wa polisi,



    "Mlisomea nini pale?" Mkuu wa polisi aliuliza,



    "Public relation, yaan mahusiano ya kijamii" Kayoza alijibu kwa kujiamini,



    "Mmemaliza mwaka gani" Mkuu wa polisi aliendelea kuuliza,



    "Mwaka jana, mwezi wa sita" Omary alitoa jibu lililomfanya Mkuu wa polisi aridhike kuwa ni kweli uenda awa vijana ndio wahusika wa mauaji, maana hata taarifa aliyokuwa nayo ulikuwa inasema ni wahitimu wa chuo, ila hawajarudi tena kuchukua vyeti vyao kutokana na kutafutwa na polisi baada ya kugundulika kuwa waliwaua wanafunzi wenzao wawili wa kike,



    "Mna vyeti vyenu ili mniletee copy kesho na barua ya kuomba kazi, maana kuna kampuni ya jamaa yangu ya uchimbaji madini hapo kahama" Mkuu wa Polisi aliuliza sasa kupata uhakika wa vyeti,



    "Vyeti hatuna, hatukwenda kuvifuata" Kayoza alijibu huku akijiuliza itakuwaje kama mkuu wa polisi atauliza sababu ya wao kutokwenda kuvifuata vyeti vyao, na kipindi hicho mkuu wa polisi alishaamini tayari hisia sake kuhusu Hawa vijana kuwa ndio wauaji wenyewe,



    "Kwanini hamjavichukua sasa?" Mkuu wa polisi aliuliza,



    "Matatizo ya ada, hali ya kiuchumi nyumbani ilikuwa ngumu kweli" Omary alijibu baada ya kumuona Kayoza akibabaika,



    "Hata mjomba wenu hakuwasaidia?" Mkuu wa polisi aliwatupia swali jingine, ila kabla hawajajibu walimuona Daktari akiwafuata mbio mbio huku akihema juu juu, naona kwa ajili ya kukimbia sana na hata uso wake ulikuwa na furaha sana Siku hiyo tofauti na furaha anayokuwaga nayo siku nyingine,



    "vipi Dokta, mbona hivyo?",Mkuu wa polisi alimuhoji Daktari,



    "Taratibu mkuu, usiwe na papara na maswali yako ya kipolisi" Daktari aliongea kwa pupa huku furaha yake ikiwa bado ipo nae,



    "Na wewe nawe uwa huishiwagi vituko? Sasa unavyokuja unakimbia hivyo alafu unapigia breki kwetu, ntaacha vipi kukuuliza?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akionekana hajapendezwa na kile kitendo cha daktari,



    "OK, nisamehe mkuu, ila sikukusudia kukukera, nipo hapa mbele yako kwa sababu maalum" Daktari aliongea huku ile hali ya mzaha aliyokuwa nayo mwanzo ikiwa haipo tena,



    "Sasa si ndio utuambie hiyo habari, wewe bwana vipi bwana" Mkuu wa polisi aliongea kwa sauti ya ukali kidogo,



    "mgonjwa wenu kafumbua macho",Daktari aliwaletea habari ile ambayo ilikua kama uokovu kwao maana hata hasira zao zilikuwa zimeyeyuka ghafla kutokana na hizo habari,



    "vipi, anaongea?",Mkuu wa Polisi aliuliza swali huku akiwa amemtolea macho daktari,



    "sijajua bado, maana nilipomkuta katika hali hiyo nilimuacha na Daktari wa zamu na kuamua kuwafuata nyie",yule Daktari alijibu,



    "Si tunaweza kwenda kumuona?" Kayoza alimuuliza daktari baada ya muda mrefu wa ukimya,



    "Twendeni" Daktari alijibu huku akiondoka na kufanya wote waanze safari ya kuitafuta wodi ambayo kalazwa Sajenti Joel Minja.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walipoenda wodi ya wagonjwa mahututi ambayo alilazwa Sajenti Minja hapo hawali, walikuta kitanda alicholala Sajenti Minja kitupu, ikambidi Daktari aliefuatana na wakina Kayoza amtafute Daktari wa zamu ili kujua mgonjwa amehamishiwa wapi. Alichukua simu yake na kumpigia mwenzake ili amuulize ni Wapi Sajenti Minja amehamishiwa,



    "twendeni grade C",Daktari aliwaambia baada ya kukata simu, walipofika huko grade C, walimkuta Daktari wa zamu anamalizia kumpima Sajenti Minja, wakasubiri kwa muda kidogo, kisha wakaruhusiwa kuingia, walipofika katika kitanda alicholala Sajenti Minja, wote watatu wakajenga tabasamu katika nyuso zao, lakini Sajenti Minja alikuwa tofauti kidogo, hakuonesha kuwakumbuka kabisa,



    "bado kumbukumbu hazijamrudia vizuri",Daktari wa zamu alimuambia Mkuu wa Polisi,



    "itachukua muda gani kurejea katika hali yake?",Mkuu wa Polisi aliuliza,



    "itategemea na nyinyi wenyewe, maana anapomuona mtu mara kwa mara ndio anapata kumbukumbu",Daktari alimjibu Mkuu wa Polisi, kisha wote wakawa wanamuangalia Sajenti Minja ambae alikuwa amelala uku macho yake yakiwa wazi yakipepesa pepesa,



    "Amekonda aisee" Mkuu wa Polisi aliongea huku akiwa bado anamuangalia Sajenti Minja,



    "Kukonda lazima, maana alikuwa anakula kwa mipira na dripu pekee" Daktari wa zamu alijibu huku akiuweka vizuri mkono wa Sajenti Minja,



    "Sasa mpaka atengemae kabisa itachukua muda gani?" Mkuu wa polisi alimuuliza Daktari wa zamu,



    "Hatuwezi kujua, ila kama atakuwa anakula vizuri na kunywa maji ya kutosha, anaweza kurudi kama hawali" Daktari alijibu,



    "Ila hata hii hatua aliyofikia, ni hatua ya kumshukuru sana Mungu" Kayoza aliongea huku machozi ya furaha yakimtoka, alishindwa kuzuia hisia zake, aliamini mpigania ubinadamu wake amepona kwa hiyo ana uhakika wa kupona kwa maana Sajenti Minja ndiye mtu pekee aliyekuwa anaangaika nae kwa vitendo na maneno.



    Wakati wakiwa bado wanaongea pembeni ya kitanda ambacho amelala Sajenti Minja, ndipo Sajenti Minja akamtolea macho mkuu wake wa Polisi huku akiwa kama anajitahidi kuvuta kumbukumbu juu ya mtu huyo,



    "vipi Minja mbona unaniangalia sana, unanikumbuka?",Mkuu wa polisi akamuuliza swali Sajenti Joel Minja,



    "ndio nimekukumbuka vizuri sana, ni mkuu wangu wa kazi",Sajenti alijibu kwa ufasaha kwa sauti iliyochoka sana kutokana na kulala kwa wiki nyingi sana.



    lakini jibu la Sajenti Minja likampa njia Mkuu wa Polisi, akaona huo ndio wa wakati halisi wa kumjua na kumuumbua mtu anayejiita Remmy, na muda huo ndio alitaka ahakikishe kuwa yule kijana ambae anamtilia mashaka ni yeye haswa,



    "huyu nae unamkumbuka?",Mkuu wa Polisi aliongea huku akimshika bega Kayoza, alikuwa na maana yake kuanza na Kayoza,



    "huyo ni mtoto wa dada, anaitwa Kayoza",Sajenti Minja alijibu tena kuashiria kumbukumbu zimemrejea.



    Omari na Kayoza waligundua mchezo anaocheza Mkuu wa Polisi, na wote walinyong'onyea kwa kujua kwamba wameumbuka, kwa maana anaefuata kutambulishwa ni Omari.



    "huyu nae anaitwa nani?, taja majina yake yote matatu, ili nijue kumbukumbu yako imerudi",Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja huku akimsogeza Omary mbele ya macho ya Sajenti Minja....





    ..."jamani waungwana muda wa kuangalia wagonjwa umekwisha",Daktari mmoja mwenye umri ulioenda kidogo aliingia ndani ya wodi na kutamka maneno hayo,



    "ebu tufanyie subra kidogo, kama dakika tano za nyongeza",Mkuu wa polisi alimwambia Daktari zamu ambaye alikuwa nae muda mrefu ,



    "haiwezekani kamanda, ni makosa makubwa sana kuongeza muda wa ziada wa kumuangalia mgonjwa",yule Daktari mwenye umri mkubwa kidogo aliongea huku akiwafungulia mlango ikiwa ni ishara ya kuwaruhusu watoke,





    "Minja mimi nitakuja baadae",Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja, ambae muda wote alikuwa kimya huku akijaribu kuvuta kumbukumbu zake kuhusu Omary,



    "sawa mkuu",Sajenti Minja alijibu kwa sauti ya uchovu,





    "baadae tukuletee chakula gani anko?",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,



    "mleteeni juisi au uji, msisahau maji, haya nendeni nje waheshimiwa",Daktari wa zamu alidakia, kisha akawaondoa wodini wakina kayoza.



    Sajenti Minja akageukia ukutani na kutabasamu,



    "Anaitwa Omary mkwiji, hilo ndilo jina lake mkuu" Sajenti Minja aliongea peke na kuendelea kutabasamu.



    Kayoza, Omary na Mkuu wa Polisi Waliondoka wakiwa na furaha sana,

    Kayoza alipata tumaini jipya la kupöna, kwa sababu mtu aliekuwa anamsaidia amepona.



    Huku Mkuu wa polisi akipata zaidi imani ya kumchunguza Sajenti Minja, nae alijikuta anatabasamu,



    "Naona leo umefurahi mjomba kupona" Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi baada ya kumuona akitasamu, na kumfanya Mkuu wa polisi ashtuke maana alikuwa anatabasamu bila kujijua,



    "Eeh, ndio...kwani nyie hamjafurahia?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akijifanya ni kweli anafurahia Sajenti Minja kupona,



    "Kwanini tusifurahi, lazima tufurahi" Omary alijibu huku akicheka,



    "Jambo la heri sana, bora ameamka maana akishatengemaa kabisa kila kitu kitakuwa sana" Mkuu wa polisi aliongea,



    "Kweli kabisa" Kayoza alijibu,



    "Mnaelekea wapi sasa?" Mkuu wa polisi aliwauliza wakina Kayoza,



    "Ni nyumbani tu, tukampe taharifa mama" Kayoza alijibu,



    "Atafurahi sana akisikia mdogo wake amefungua macho" Mkuu wa Polisi aliongea huku akitabasamu,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Tena sana, anaweza hata kuchanganyikiwa" Omary alimsapoti mkuu wa polisi,



    "Sasa Mimi leo siwapeleki, kuna sehemu kuna kikao natakiwa ndani ya dakika kumi hizi, chukueni hii hela mkapande bajaji" Mkuu wa polisi aliongea huku akitoa noti shilingi elfu kumi na kuwakabidhi,



    "Asante, ila baadae naimani baadae tutakutana hapa hapa" Kayoza aliongea huku akiiweka pesa mfukoni,



    "Lazima nine baadae, kikao kikiisha tu nitakuja kushinda hapa hapa" Mkuu wa polisi aliongea,



    "Haya, sasa sisi acha twende tukatafute hiyo bajaji ya kutupeleka nyumbani" Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi,



    "Sawa wajomba, baadae" Mkuu wa polisi aliongea huku akiingia katika gari yake na kuwaacha wakina Kayoza wakienda upande wa pili wa barabara ambapo ndipo bajaji zilikuwepo.



    *******************







    BAADA YA WIKI MOJA



    Sajenti Minja aliruhusiwa kutoka hospitali, ila Mkuu wa polisi alimuomba akae nae nyumbani kwake, mpaka pale Sajenti Minja atakapotengemaa kabisa ndipo arudi kwake. Ilo halikupingwa, Sajenti Minja aliamua akae kwa muda kwa Mkuu wa polisi kwa maana ndani ya nyumba ya Mkuu wa polisi alikuwa anaweza kupata kila kitu alichokitaka kutokana maisha mazuri aliyokuwa nayo Mkuu wa polisi ambayo yalikuwa tofauti na maisha ya kwa dada yake.



    Maisha katika nyumba ya Mkuu wa polisi yalikuwa ni mazuri sana, wakina Kayoza walikuwa wanaenda kila siku kumtembelea Sajenti Minja katika nyumba ya Mkuu wa polisi, na watu wote pale katika nyumba ya Mkuu wa polisi waliwazoea, kuanzia wafanyakazi, mke wa Mkuu wa polisi na mtoto wa kike na wa pekee wa Mkuu wa polisi.



    Sasa tatizo lilikuwa kwa mtoto wa pekee wa mkuu wa polisi, ambae alikuwa anaitwa Martha, huyu Martha toka aanze kuzoeana na Kayoza amekuwa akimuonesha dalili zote za kumpenda, ila Kayoza hakuelekea kabisa, sio kwamba hakuwa na hisia na huyo binti, la asha, aliohofia mzimu ambayo ungeweza kumletea matatatizo anapokuwa katika mahusiano ya kimapenzi. Kwa hiyo alimuwekea ngumu kabisa.



    ********************





    Mkuu wa polisi alifanikiwa kumpata kijana mmoja pale mtaani kwa wakina Kayoza, yule kijana aliitwa Ismail, ila wengi walizoea kumuita Suma, huyo kijana aliambiwa mkanda mzima jinsi ulivyo, kwa hiyo kazi yake ilikuwa kumchunguza Omari.



    Suma alikua ni kijana mchangamfu sana, na kwa kuanzia tu, alianza kwenda katika kijiwe cha mchezo wa drafti ambacho Omari alipenda sana kwenda, hatua ya kwanza alifanikiwa kujua kuwa Remmy sio jina halisi la Omari, ila hata hivyo hakujua jina halisi la Omari, maana pale walikuwa wanamuita mzee wa supa, ni kutokana na mtindo wa magoli anayowafunga wenzake. Ila suma hakukata tamaa, akajipa moyo kuwa lazima aifanikishe kazi aliyopewa, maana hata posho aliyoahidiwa kupewa na Mkuu wa polisi, ilikuwa ni posho nzito, ilimtosha kununua kila kitu cha ndani.



    Na sifa nyingine ya ziada, Suma aliweza kujenga mazoea ya haraka sana, tena na kila mtu.







    **************





    Jioni moja tulivu, Kayoza na Omari wakiwa nyumbani kwao,



    "Twenzetu basi, maana sioni kama una dalili za kutoka" Kayoza alimwambia Omary,



    "Si nilishakwambia najisikia hovyo, sijui ni malaria?" Omary aliongea kinyonge huku akiwa kitandani,



    "Sasa unaumwa alafu unakaa ndani?, si uende hospitali man" Kayoza alimwambia Omary,



    "Hela hamna kaka" Omary alijibu kinyonge,



    "Acha mambo yako bwana, si umuombe mama, usimuogope bwana, yule ni mama yako" Kayoza alimwambia Omary,



    "Sijamzoea kama wewe, basi kaniombee" Omary alimwambia Kayoza,



    "Ngoja nikamwambie, ila usirudie tena, utakuja kufa umelala" Kayoza alimwambia Omary,



    "Kamwambie mama bwana, acha blah blah blah nyingi" Omary alimwambia Kayoza,



    "Mi ndo natoka hivyo, sirudi tena huku chumbani, naenda kumcheki mjomba" Kayoza aliongea huku akitoka nje,



    "Poa, mwambie naumwa na ndio maana sijafika" Omary aliongea,



    "Poa" Kayoza aliongea huku akitoka.



    Alipofika sebuleni alimwambia mama yake hali ya Omary, kisha akaaga kuwa anaenda kwa Mkuu wa polisi kumuangalia mjomba ake.



    ++++++++



    Kayoza alifika nyumbani kwa mkuu wa polisi na kumkuta Martha yupo peke yake, na Martha alimwambia Kayoza kuwa Sajenti Minja na Baba yake ambae ni Mkuu wa Polisi wametoka, wameenda kunyoosha miguu kidogo.



    Sasa Martha akaona kuwa huo ndio muda mzuri wa kufanya, anachotaka kwa kayoza, Martha akaaga anaenda ndani Mara moja kufanya usafi na kumuacha Kayoza akiwa sebuleni anaangalia runinga.



    Baada ya dakika chache.......

    "mama weee, jamani panya panya",Martha alipiga kelele ndani ya chumba chake, kisha akatoka nje huku anakimbia, akaenda alipokaa Kayoza,



    "Yaani wewe mkubwa hivyo unaogopa panya?" Kayoza alimtania Martha huku akimcheka,



    "Usiseme huvyo Kayoza, kwanza naomba ukanisaidie kuua panya",Martha alimwambia Kayoza,



    "Sasa huyo panya atakuwa amekaa tu anakusubiri?" Kayoza alimuuliza Martha huku akiendelea kumcheka,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Yupo kwenye kabati, alafu limefungwa, yupo kwa ndani. Twende bwana ukamuue, uwa ananisumbua sana" Martha alimwambia Kayoza, Kayoza bila kubisha akanyanyuka alipokaa na kwenda chumbani kwa Martha, huku Martha akimfuata kwa nyuma.



    Kayoza alipoingia ndani, Martha akaubana mlango na funguo kisha funguo akaidumbukiza ndani ya kifua chake, kisha akamgeukia Kayoza,



    "Kayoza hakuna panya, ila ninachotaka toka kwako unakijua, Kayoza unaumiza moyo wangu sana, nifanyaje ili ujue nakupenda, eee?",Martha aliongea huku machozi yakimtoka,



    "Dah, Martha si nilishakuambia haiwezekani lakini?" Kayoza aliuliza baada ya kukaa muda mrefu akimuangalia Martha kwa hasira,



    "Naomba tu iwezekane, mpaka Mimi kufikia hata hii ya kukutamkia maneno haya, ujue hisia zangu zimenishinda" Martha aliongea huku akipiga magoti,



    "Sawa nimekuelewa, naomba unifungulie mlango nitoke nje" Kayoza aliamua kumkubalia ili amridhishe Martha,



    "Hapana sitaki utoke" Martha aliongea kwa hisia huku akimtazama Kayoza...



    mara sauti ya Mkuu wa Polisi ambaye ndiye Baba yake Martha ikasikika mlangoni,





    "we Martha unaongea na nani uko chumbani? Ebu nifungulie mlango"



    ..."hakuna kitu daddy",Martha alimjibu Mkuu wa polisi,



    "kwa hiyo unaongea peke yako uko"Mkuu wa polisi akamtupia mwanae swali jingine,



    "si naongea na simu",Martha akajibu.



    "Fungua basi mlango niingie" Mkuu wa polisi akamwambia mwanae,



    "Daddy navaa bwana, kwani unataka nini huku?" Martha alimjibu baba yake huku akideka.



    Hivyo ndivyo alivyolelewa na wazazi wake, amelelewa malezi ya kujibishana na wazazi wake kama rafiki zake,



    "Si nilitaka nikuone mwanangu, au vibaya mama?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akiwa mlangoni,



    "Nakuja sebulebi daddy, mammy umemuacha wapi?" Martha aliuliza,



    "Nimerudi nae, ameenda kuoga" Mkuu wa polisi alijibu huku akiamua aondoke zake, na kurudi sebuleni kuongea na Sajenti Minja,





    "naweza kupata juice",Sajent Minja alimuuliza Mkuu wa polisi alipokua anakaa,



    "mhmm..sidhani kama ipo, ebu ngoja, we Martha, marthaa",Mkuu wa polisi alijibu kisha akamuita mwanae,



    "nakuja daddy" Sauti ya Martha ilisikika kutoka chumbani kwake.



    Baada ya sekunde chache Martha akawa mbele ya Sajenti Minja na baba yake,



    "shikamoo anko",Martha alimsalimia Sajenti Minja,



    "marhabaaa anko, kuna juisi?",Sajenti Minja aliitikia, kisha nae akauliza swali,





    "ipo anko,",Martha alijibu,



    "naomba unipe ya pera",Sajenti Minja aliwasilisha ombi lake, mmmh, ya pera hamna, ipo ya orange, strawberry,mango na passion",Martha alijibu,



    "nipe ya chungwa na maji ya baridi",Sajenti Minja aliagiza na martha akamletea,



    "Vijana wangu hawajaja leo?" Sajenti Minja alimuuliza Martha, alikuwa akiwaulizia wakina Kayoza,



    "Hawajafika anko" Martha alijibu huku nafsi yake ikimsuta kwa maana aliongea uongo,



    "Leo naona watakuwa wamechoka" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja,



    "Wamechoka wapi, itakuwa wameona nimeshapona kwa hiyo hawaoni umuhimu wa kuja kunijulia hali" Sajenti Minja aliongea,



    "Acha wapumzike, maana wale watoto walikuwa wanashinda hospitali mpaka nikawa nawahurumia" Mkuu wa polisi aliwatetea wakina Kayoza,.



    "Hakuna haja ya kuwahurumia, hilo ndilo lilikuwa jukumu lao, mama yao umri wake umeshakwenda, anatakiwa apumzike" Sajenti Minja aliongea,



    "Wameshawahi kuishi Dodoma ee?" Mkuu wa polisi aliuliza swali lililomshtua Sajenti Minja,.



    "Nani alikwambia?" Sajenti Minja aliuliza huku akijifanya anacheka ili kuuficha mshtuko wake, ila tayari Mkuu wa polisi alikuwa ameshamsoma,



    "Waliniambia wenyewe, wakadai wamemaliza pale UDOM ila hawajachukua vyeti vyao" Mkuu wa polisi alizidi kutiririka na kuendelea kumshtua Sajenti Minja,.



    "Yah ni kweli walimaliza pale" Sajenti Minja alijibu kifupi,



    "Sasa ni kwanini hawajachukua vyeti?" Mkuu wa polisi aliuliza swali la kumtega Sajenti Minja ili zone kama jibu lake litafanana na la wakina Kayoza,



    "Hawajachukua vyeti?, mbona Mimi hawajaniambia kama hawajachukua vyeti vyao?" Sajenti Minja alijifanya kushangaa huku akiuliza,



    "Alah!!! Kumbe hujui?" Mkuu wa polisi aliuliza,



    "Aisee hawakuniambia, labda wamefanya makosa wanaogopa kuniambia, au wamekula ada?" Sajenti Minja aliamua kumuigizia sasa Mkuu wa polisi, alivyokuwa anaongea utasema kweli yaani,



    "Wameniambia wameshindwa kulipa ada ndio maana hawajachukua" Mkuu wa polisi aliamua kumwambia ukweli,



    "Wanekudanganya, niliwapa pesa yote, itakuwa wamefeli au wamekula ada...yaani awa watoto awa, utakuta hata mama yako hajui kama hawana vyeti" Sajenti Minja alijifanya kusikitika,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kwani walikuwa wanasomea nini?" Mkuu wa polisi aliuliza swali jingine lilimuweka mtegoni Sajenti Minja,



    "Hawajakwambia?" Sajenti Minja alimuuliza mkuu wa polisi huku akijitahidi kuvuta kumbukumbu ya masomo waliyokuwa wanasoma wakina Kayoza,



    "Hawakuniambia" Mkuu wa polisi alijibu huku akibonyeza controller ya runinga,



    "Mi hata nilikuwa sifuatilii wanachukua kozi gani, ili mradi nilikuwa nawalipia ada wamalize tu chuo" Sajenti Minja alilipangua swali la Mkuu wa polisi,



    "Ulikuwa unatakiwa uwafuatilie bwana" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja,



    "Shauri yao bwana kama walichezea masomo, ngoja nikajimwagie maji" Sajenti Minja alijibu huku akinyanyuka na kuondoka ili kuyakwepa maswali ya Mkuu wa polisi, maana yalimpa mashaka na akahisi inawezekana babu wa monchwari alimchoma.



    Kuanzia hapo akaanza kuishi kwa wasiwasi akihisi kuwa inawezekana kabisa Mkuu wa polisi anawapeleleza wakina Kayoza pasipo wao kujua.



    *******************



    Baada ya Martha kumuhudumia Sajenti Minja, Martha alirudi chumbani kwake, usiku ulikuwa umeshaingia,





    "sasa mimi nitatokaje humu?",Martha alipokelewa na swali la Kayoza ambae alikuwa yuko ndani ya kabati,



    "subiri bwana, sasa hivi wanaenda kulala, sebule itakuwa haina mtu",Martha alimjibu Kayoza kwa kujiamini,



    "Alafu mbona unajiamini sana, we huogopi kuniingiza mwanaume chumbani kwako?" Kayoza aliuliza huku akiwa ana hasira,



    "Lazima nijiamini, sasa nimuogope nani wakati nipo kwetu?" Martha alijibu kwa nyodo huku akitandika vizuri kitanda chake,



    "Usiwe unajiamini kwa kila kitu, vingine vitakutokea puani, shauri yako" Kayoza aliongea kwa hasira huku akichungulia dirishani,



    "Nikuletee chakula?" Martha alimuuliza Kayoza,



    "Hapana, sihitaji" Kayoza alijibu huku akionekana amesusa,



    "Ukisusa sisi twala" Martha aliongea kwa madaha huku akielekea sebuleni.



    Martha alibeba chakula kingi na kwenda kulia chumbani kwake kwa lengo la kula pamoja na Kayoza.



    "Njoo rule bwana K, usiwe unasusa Susa kama mtoto wa kike" Martha alimwambia Kayoza huku akimpa kijiko, lakini Kayoza hakutaka hata kujisumbua kupokea, badala yake alikaa tu kitandani huku mkono ukiwa shavuni.



    Baada ya masaa mawili, kila mtu aliyekuwa sebuleni alienda kulala, sebule ikabaki tupu.



    Ilikuwa ni mishale ya saa nne usiku, katika chumba cha Martha kulikuwa na sauti za mabishano ambazo zilikuwa zinasikika kwa chini chini sana,



    "Martha niachie niende, mama atakua na wasiwasi nyumbani",Kayoza alimlalamikia Martha,



    "ni vigumu kutoka Kayoza, lazima mlinzi kesho atamwambia baba alafu iwe msala kwako",Martha alijibu akiwa na lengo la kumzuia Kayoza asiondoke ili atimize azma yake ya kufanya nae mapenzi,



    "kulala na wewe ni kitu ambacho akiwezekani Martha, kwanza tulikubaliana kuwa watu wakienda kulala ndio unanitoa, ona sasa unaleta sababu nyingine",Kayoza aliongea kwa kulalamika,



    "isiwe tabu mwenzangu, wewe lala kitandani mimi nitalala chini",Martha aliongea huku akikunjua godoro jingine alilolitoa juu ya kabati.



    "Nani kakwambia anataka kulala hapa?" Kayoza aliuliza kwa jazba,



    "Alafu usiongee kwa sauti kubwa, Baba akisikia itakuwa tabu kwako, shauri yako" Martha alimtisha Kayoza,



    "Basi nitoe nje niende kwetu" Kayoza aliongea kwa sauti ndogo,



    "We lala, ikifika saa saba au saa sita nitakutoa, mlinzi atakuwa amesinzia" Martha alimlaghai Kayoza, ikambidi alale, ila kwa sharti moja, wasilale pamoja, ambapo Martha alikubali na kutandika godoro chini na kitandani alilala Kayoza.





    Ilimchukua saa moja tu Kayoza kupata usingizi, akalala fofofo huku akikoroma, saa sita ikafika, ikapita na saa saba ikafika na kupita na sasa ilikuwa saa Tisa usiku,



    Martha akakurupuka kutoka katika godoro la chini, taratibu akavua nguo zake zote, kisha akapanda kitandani kwa hadhari ya kutomshtua Kayoza, akaingia ndani ya blanketi, kisha akaanza kufungua zipu ya suruali ya Kayoza,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mmmh, mbona yuko hivi?",Martha aliguna baada ya kumuona Kayoza kalegea kama mtu aliepoteza fahamu, ila hiyo haikumzuia kuendelea na anachokifanya, akafanikiwa kuishusha suruali ya Kayoza hadi miguuni, sasa akawa anajiweka sawa ili atimize lengo lake, Kayoza aliinuka kama mshale, kwa kasi ya mwanga na meno yake yakapenya sawia katika shingo ya Martha,



    "mamaaaaaaaa nakufaaaaaaaaa",sauti ya Martha ilisikika kwa nguvu na kuwaamsha watu wote waliolala mpaka majirani..............



    ****"*****ITAENDELEA************



0 comments:

Post a Comment

Blog