Search This Blog

PENZI LANGU - 4

 





    Simulizi : Penzi Langu

    Sehemu Ya Nne (4)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    niliishia pale Happy akiwa na ndugu yake Joyce walipokwenda Tabata kwa mpenzi wake Wakiwa huko, Joyce aliyegundua kijana huyo alitaka kuwa faragha na laazizi wake aliwaaga kwamba anakwenda Segerea kwa baby wake . Je , baada ya Joyce kuondoka kilifuatia nini kwa wapenzi hao? Songa nayo . .. Kwa kuwa kutoka nyumba aliyopanga mpenzi wangu na kituo cha daladala hapakuwa mbali, Joyce aliondoka mwenyewe ndipo huku nyuma mpenzi wangu alinikumbatia na kuanza kunibusu kila sehemu aliyopenda. Sikubaki nyuma, nilijibu mashambulizi kisha tulihamia chumbani kwake ambako tuliendelea kuleteana fujo zote ambazo wapenzi walioshibana hufanyiana wanapokutana katika eneo lako la kujidai. Sijui nikuambiaje kuhusu umahiri wa mapenzi aliokuwanao mtu wangu , kwa ujumla alinipagawisha sana na alipoona nimeishiwa nguvu na kubaki nimemtumbulia macho, alinipa haki yangu kisawasawa . Siku hiyo pia sitaisahau katika maisha yangu , kwani nilifurahi kuwa na mpenzi wangu aliyejua nini maana ya mahabati, nikajisemea moyoni kwamba; ‘ hakika mume nimempata. ’ Tukiwa tunazungumza chumbani nilimwambia kuhusu kukosa nafasi ya kujiunga na chuo kikuu cha mlimani akaniambia nisijali kwani jijini Dar palikuwa na matawi ya vyuo vikuu vingi . Aliniambia kuwa palikuwa na tawi la chuo kikuu cha SAUT, KIU cha Uganda na Tumaini . Alinifahamisha kuwa miongoni mwa vyuo hivyo nisingekosa nafasi , nilifurahi sana aliponieleza hivyo nikamwambia nitawasiliana na baba kuhusu jambo hilo. Wakati tukipiga stori hizo tulikuwa tumejilaza kwenye kitanda chake cha futi sita kwa sita , si baadaye tena tukajikuta tumepatwa na mushawasha kama siyo sisi tuliotoka kula tende! Mpenzi wangu akakivamia tena kifua changu alichokisifia kwamba kilikuwa kizuri eti kilipambwa na viembe bolibo , akaanza kuzichezea hadi nikaishiwa nguvu . Kufuatia hali niliyokuwanayo, hakuona sababu za kuniacha niteseke, tulijikuta tumevamiana na kuanza kula nanasi kwa nafasi. Siku hiyo sitaisahau kwani mpenzi wangu alijua kunipa raha haswa mpaka mtoto wa kike nikadata kama siyo kuchanganyikiwa , hakika alinifurahisha mno . Tulipomaliza mambo yetu tukaoga pamoja kisha alikwenda kununua chipsi , ile tunaanza kula nikakumbuka Joyce aliniambia nikiwa tayari nimpigie simu. Nilichukua simu nikatafuta jina lake kisha nikampigia , simu iliita muda mrefu bila kupokelewa wakati

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    haikuwa kawaida yake, nikapata wasiwasi. Hata hivyo , sikukata tamaa nilimpigia mara kadhaa ambapo iliita tu bila kupokelewa nikabaki kujiuliza kwa nini hakupokea ! Nilipomwambia mpenzi wangu kwamba Joyce hakupokea simu akacheka , nikaishia kumshangaa kisha nilimuuliza kwa nini alicheka . Mpenzi wangu aliniambia si aliniaga kwamba anakwenda Segerea kwa baby wake, kwa vyovyote walikuwa wakizitafuna tende ndiyo maana hakupokea simu. Kauli ya mpenzi wangu ilinifungua nikajua kweli Joyce alikuwa akipewa haki yake kwani usiku wa kuamkia siku hiyo aliniambia alimmisi sana mtu wake . Wakati nikiwa nimepata jibu, meseji iliingia kwenye simu yangu , nilipoifungua ilitoka kwa Joyce, aliandika ; “ Mwaya nipo kama ulivyo wewe hapo kwenye kiwanja cha fundi seremala na shem wangu , nami baby wangu ananipa vitu adimu , tukimaliza nitakushtua ila siyo mchezo , hapa ni raha tupu !” Baada ya kusoma ujumbe huo nilimuonesha mpenzi wangu , alipousoma akacheka na kuniambia alijua tu naye alikuwa akilamba asali yake, tukacheka. Kwa kuwa sikuwa na wasiwasi kuhusu Joyce, tuliendelea kula chipsi kwa kulishana hadi tulipotosheka tukaingia chumbani kujipumzisha kusubiri Joyce anipigie simu . Tukiwa tumejilaza huku nikiwa nimevaa nguo ya mwisho kabisa na kifua wazi , mpenzi wangu alinisifia sana kuwa na kifua kizuri kilichokuwa na viembe vidogo alivyovibatiza jina la ‘ viembe mfumbato. ’ Nilipomuuliza maana ya viembe mfumbato, alicheka na kuniambia kwa vile vilikuwa vidogo ambavyo aliweza kuvibugia kama pipi, nikacheka na kumwambia apunguze utundu ! Nilipomwambia hivyo si akavimba kichwa , akalishika embe la kushoto na kulibugia mdomoni na kuanza kulimung’ unya , kutokana na alivyokuwa akinifanyia nilipigwa na shoti ya umeme. Hali niliyokuwa nayo ilinifanya niweweseke, kutumbua macho na kuhema kwa kasi kama siyo mimi niliyetoka kula tende muda mfupi uliopita. Mpenzi wangu aliyeonekana siku hiyo aliamua kukata kiu yangu aliendelea kunifanyia utundu wake, naye alipoona kama angechelewa angeharibikiwa , alinichapa bakora moja ya uhakika mtoto wa kike nikawa hoi bin taabani . Mpenzi wangu ambaye naye alikuwa kachoka alijilaza sambamba nami tukapitiwa na usingizi hadi tuliposhtushwa na mlio wa simu ya Joyce, nilipopokea aliniambia baada ya dakika 35 angewasili



    Njia nzima muongeaje mkubwa alikuwa Jonas , alikuwa akiongea mambo ya shuleni kwao , mara mambo ya disco na kusema ipo siku atakuja kutupitia ili twende kujirusha. Kijana huyo hakuishia hapo, aliniambia alifurahi kuniona na wala hakufikiria kama Joyce alikuwa na ndugu yake huko Musoma na mambo mengine kibao . Kwa kuwa nilikuwa mzoefu na wavulana . Nilijua alikuwa amenizimikia na lengo lake lilikuwa ni kutaka kunitokea , moyoni nilisema alikuwa akijisumbua kwani sikuwa na haja na mwanaume mwingine yeyote zaidi ya mpenzi wangu. Tulipofika nyumbani, mama alimkaribisha kwa bashasha Jonas ambaye tangu alipotoka shuleni hawakuwahi kuonana ambapo alimlaumu kutofika pale nyumbani kumsalimia . Kijana huyo alijitetea kwamba tangu alipowasili, alikuwa bize sana kisha alimuomba msamaha na kumweleza kwamba kuanzia siku ile angekuwa anakuja mara kwa mara. Baada ya maongezi , Jonas aliaga lakini kabla hajatoka alituomba tumsindikize , mimi nilikausha Joyce ndiye alimtoa nje ambapo hakufika mbali akarejea. Aliporejea alinikuta nipo chumbani , nikamuuliza kuhusu mashauzi ya Jonas . Joyce alicheka na kuniambia alikuwa anamfahamu vizuri kijana huyo kwa kupenda mademu wakali. “ Yule kujifagilia kote kule kwa sababu kakuona wewe, mimi huwa haniambii upuuzi wake kwani niliwahi kumchana tukawa hatuongei kabisa,” Happy alimkariri Joyce. Joyce aliendelea kunifahamisha kwamba, kutokana na tabia yake ya kupenda wasichana tayari alikuwa kawabebesha mimba mabinti wawili , mmoja alikuwa msichana wao wa kazi na mwingine binamu yake. Aliponiambia hivyo nilicheka sana na kuhoji kujifanya kote kule sharobaro alikuwa akitembea na msichana wa kazi na binamu yake? Nikamwambia hakuwa na maana kabisa! Nilimwambia siku akithubutu kunitokea ningempa maneno ya shombo hadi akome kuwashobokea wanawake wenye wapenzi wao , Joyce akacheka . Baada ya kumjadili Jonas tuliendelea na maongezi yetu , tulipokula tulirudi chumbani kwetu lakini kabla ya kulala nilimpigia simu baba na kumfahamisha kuhusu chuo nilichoshauriwa kujiunga . Baba alikubali kisha alimpatia simu mama ambaye tulizungumza naye lakini kubwa alilonisisitiza ni kutojihusisha na masuala ya mapenzi kujiepusha na balaa kama lililowahi kunikuta . Licha ya kwamba tayari nilikuwa na mpenzi, nilimwambia sikutarajia kufanya hivyo kwani nia yangu ilikuwa ni kusoma , mama alifurahi bila kujua Dar alikuwa na mkwewe msomi wa chuo kikuu . Nilipozungumza na mama , Joyce aliyekuwa akitusikia kufuatia chumba kuwa na utulivu alicheka na kuniambia alinisikia nilivyomdanganya

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mama kwamba sikuwa na mpenzi. Kufuatia kuniambia hivyo , nilimsimulia kisa cha mpenzi wangu aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa mahaba niliyetokea kumpenda hadi aliponisaliti na rafiki yangu . Nilimweleza jinsi nilivyochanganyikiwa na kupata ugonjwa wa kuumwa kichwa, moyo kiasi cha kuwaweka wazazi wangu katika wakati mgumu. Joyce alinipa pole na kunieleza yeye hakuwahi kupatwa na balaa kama hilo na aliomba lisimkumbe kwani alikuwa akisikia mapenzi yanaumiza sana . Nilimwambia asiombee hilo, akaniuliza kama ingetokea msomi wangu angenisaliti tena ningefanyaje ? Nilimwambia kwa jinsi nilivyokuwa namuamini asingeweza kufanya hivyo , Joy akacheka na kuniambia nitemee mate chini . Kwa jinsi tulivyokuwa tukipendana na mpenzi wangu huyo tuliyefahamiana kupitia facebook , nilimweleza haondoe kabisa mawazo ya kuja kusalitiwa na kusisitiza kwamba mtu huumizwa mara moja tu na siyo mbili , Joyce akacheka. Wakati namsisitizia Joyce kwamba mpenzi wangu msomi asingekuja kunisaliti, sikufikiria kabisa huko mbele jini angetutenganisha ndani ya saa 24. Baada ya kupiga stori tukajikuta tumepitiwa na usingizi, kulipokucha jambo la kwanza nilikwenda kujiangalia love bite zangu zilizokuwa shingoni na kwenye maziwa . Nilipoona zinaonekana kwa mbali nilitabasamu , si nikakumbuka mashamsham tuliyofanyiana na mpenzi wangu , mwili ukanisisimka ! Yaani alfajiri ile nilitamani kama angekuwa karibu anikumbatie , anibusu na kufanya kila kilichowezekana ili joto linipungue lakini haikuwezekana kwa sababu alikuwa mbali.





    Kwa kuwa simu yangu ilikuwa na fedha , niliamua kumpigia na kumweleza nilivyokuwa katika wakati mgumu, alinipa pole na kuniuliza kama ningeweza kwenda kwake mapema. Licha ya kwamba tulikubaliana kukutana mchana , nilimwambia asubiri ningempa jibu muda mfupi ndipo niliamka na kumfuata Joyce aliyekuwa akifanya usafi jikoni nikamweleza kwamba mpenzi wangu alibadili ratiba na kuniomba tukutane kabla ya saa tatu ili twende kwenye kile chuo . Joyce aliniuliza kama ningeweza kufika Tabata peke yangu , nikamwambia asiwe na shaka ningefika kwa sababu nilianza kulijua Jiji la Dar. Joyce aliniambia hakukuwa na tatizo kwa sababu hata mama alikuwa akifahamu ishu yangu ya chuo, akaniambia nikajiandae yeye angemfahamisha mama kuhusu safari hiyo . Wakati najiandaa, Joyce alikwenda kumwambia mama kuhusu mimi kwenda chuo peke yangu akapinga na kumwambia alipaswa kunisindikiza . Joyce alinifuata chumbani nilikokuwa najipodoa na kuniambia kwamba mama alisema alipaswa kunisindikiza , nilifurahi sana kuongozana naye . Tukiwa mle chumbani kila mmoja alimsifia mwenzake kwa kuwa na shepu nzuri ndipo Joyce alisema maeneo mengine walikuwa tofauti isipokuwa wote walikuwa na maziwa madogo ambayo watoto wa mjini wanayaita saa sita kamili mchana , tukacheka. Alichokuwa amesema kilikuwa kweli tupu kwani ndivyo tulivyokuwa na mpenzi wangu alikuwa akiyasifia kwa kuwa hivyo , tulipomaliza kujipodoa tulikunywa maziwa freshi na silesi za mikate tukamuaga mama ambaye alitusifia kwa kupendeza. “ Ila wanangu kwa sasa someni hatuhitaji wakwe . . . mkimaliza masomo yenu hapo ruksa!” mama alituasa. Joyce alimwambia mama haondoe shaka kwani tulikuwa tukijitambua, akasema tukifuata ushauri wake litakuwa jambo jema . Tulimuaga mama ambaye hakujua kama safari yetu itaanzia Tabata kwa mpenzi wangu, akasema tuwe na safari njema ila alisisitiza tusichelewe kurudi . Tukiwa kituo cha daladala, nilimpigia simu mpenzi wangu na kumwambia nilikuwa njiani kwenda Tabata , alifurahi sana kusikia hivyo akaniambia alikuwa akinisubiri kwa shauku . Halikadhalika, Joyce naye alimpigia simu mpenzi wake wa Segerea ambaye wakati huo alikuwa likizo, akamwambia hakuamini alichomweleza, Joyce akamweleza hakumtania muda mfupi angefika kwake. Joyce alinifahamisha kwamba tangu alipoanza kutoka na mpenzi wake huyo miezi saba iliyopita hakuwahi kulala kwake wala kukutana naye asubuhi na mapema kutokana na geti kali la nyumbani ndiyo maana hakuamini kama asubuhi ile alikuwa akimpelekea tende tamu. Joyce aliniambia kitendo cha mimi kufika Dar kilimpa mwanya wa kutoka nyumbani mara kwa mara , tukacheka kisha tukaingia kwenye daladala la Ubungo ambako tungepanda la Tabata Segerea . Tulipofika Ubungo tulipanda basi la Tabata Segerea, tukiwa njiani nilimpigia tena simu mpenzi wangu nikamuomba anisubiri kituo cha daladala, akasema sawa . Tukiwa njiani kila mmoja alikuwa bize kuchati na mpenzi wake , hatukutumia muda mrefu tulifika kituo cha Bima Tabata ambapo nilimkuta mpenzi wangu akinisubiri , tulikumbatiana na kupigana mabusu . Kwa hatua penzi letu lilipofikia , hakuna aliyeona aibu kumkumbatia mwenzake mbele ya

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    watu, baada ya salamu mpenzi wangu alinipokea mkoba nilioubeba tukashika njia kuelekea kwake. Kwa kuwa kila mmoja wetu alikuwa na hamu na mwenzake , tulipoingia ndani tulikumbatiana tena na kuanza kuleteana fujo ambapo d wangu alinishika sehemu alizojua akizishika nakuwa katika dunia ya peke yangu . Nami sikuwa nyuma, kwa kuwa nilikuwa nazijua sehemu ambazo naye alipagwa nikizishika, nikazivamia , acha apagawe si tukajikuta tupo uwanjani tukilicheza Segere ! Kufuatia kila mmoja wetu kuwa na shauku na mwenzake utafikiri ndiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza kukutana , tulikamiana haswa nikawa wa kwanza kupasua dafu kisha akafuatia . . . hakika ilikuwa raha! “ Happy !” mpenzi wangu aliniita kwa sauti nzito iliyolemewa na mahabati. Nilipoitikia aliniambia nilijua kumpa raha na hakufikiria kama kuna siku ataniacha na kuahidi kunioa , kauli yake ilinifurahisha sana nikamwambia nami sikufikiri kama angetokea mwanaume nitakayempenda kama yeye. Mpenzi wangu aliyekuwa kanilalia kifuani alifurahi mno , akanibusu na kunipiga kibao flani hivi chepesi mashavuni



    Alinisifia kwamba nilikuwa mzuri , kama unavyojua kila binadamu hupenda kusifiwa, kufuatia kunifagilia nilitabasamu tena na kumshukuru . Wakati tukiwa tunapiga stori za hapa na pale, meseji iliingia katika simu yangu , nilipoifungua ilikuwa imetoka kwa Joyce ambaye alinifahamisha kwamba tayari alikwishapewa haki yake kwa awamu ya kwanza. Ujumbe wake ulinifanya nicheke peke yangu kwani alichonifahamisha ndicho nilitoka kukifanya punde na muda huo nilikuwa nipo mweupe pee yaani sikuwa na vazi lolote mwilini. Mpenzi wangu aliniuliza kilichonichekesha, nilimpatia simu ili asome mwenyewe ile meseji, aliposoma alicheka na kuniambia Joyce alikuwa mtundu sana! Aliponieleza hivyo , nilimkubalia kwamba Joyce alikuwa mtundu na kwamba tukiwa nyumbani alikuwa akinichekesha kwa vituko vyake . Kwa vile tabia ya mpenzi wangu nilihisi ilifanana na ya mpenzi wa Joyce, nilimwambia tulitakiwa kwenda kumtembelea kwa lengo la kufahamiana. Aliponiuliza kwa nini nilimwambia tabia zao zilifanana , nilimweleza si mambo yake kwani tulipoingia tu chumbani hakunichelewesha kama ambayo Joyce naye hakucheleweshwa , tukacheka. Kwa kuwa nilikuwa sijamjibu Joyce , nilimwandikia ujumbe na kumweleza hata mimi muda ule nilikuwa kama nilivyokuja duniani na tayari nililishwa tende ya kwanza. Baada ya kumtumia ujumbe huo , Joyce alinipigia tukaanza kuzungumza. Kwa jinsi alivyokuwa huru nilimwuliza mpenzi wake alikuwa wapi, akasema alikwenda kununua chipsi. Baada ya kuongea kwa dakika kadhaa , tulikubaliana tusichelewe kurudi nyumbani ndipo akakata simu, mpenzi wangu ambaye alikuwa amejilaza pembeni yangu alinipokea tukakutanisha vinywa vyetu , tukaanza kufanya yetu . Kitendo hicho pamoja na alivyokuwa akinishika hapa na pale , nilisisimka sana nikajikuta nimemkumbatia kama ruba . . . kwa hali tuliyokuwanayo , akanichinjia tena baharini. Siyo siri , muziki wa pili haukuwa wa kitoto maana alinifanyia vitu vipya ambayvyo tangu tuanze kukutana naye hakuwahi kunifanyia, ni kama alikuwa amezificha silaha zake za maangamizi . Kwa kweli niliinjoi kuwa naye kwani kiu niliyokuwanayo aliimaliza kisha tulikwenda kuoga pamoja nikarejea kitandani yeye akaenda kununua chipsi. Tukiwa tunakula chipsi kwa mtindo wa kulishana, Joyce alinipigia simu na kunifahamisha alikuwa kituo cha daladala akisubiri gari hivyo atukute kituo cha Bima ili twenda chuoni . Alipotuambia hivyo , tulijiandaa chapuchapu na kwenda kumsubiri , gari alilopanda lilipowasili alituita tukaingia na kuelekea chuoni tukiwa pamoja na mpenzi wangu . Njiani tulipiga stori kibao hadi tulipofika katika chuo hicho, tulichukuwa fomu na kuzijaza kisha tuliondoka kurudi nyumbani ambapo tulimkuta mama kajipumzisha sebuleni . Tulimuamkia kisha alituuliza kama tulifanikiwa kupata fomu , Joyce akamweleza siyo kuipata tu tayari tulijaza. Baada ya kuzungumza mawili matatu na mama, tulikwenda chumbani ambako tulibadili nguo, kufuatia joto la Dar nilikwenda kuoga , akafuatia Joyce tukajongea mezani kwa ajili ya chakula. Tulipomaliza kula nilikwenda chumbani nikampigia simu baba na kumweleza kuhusu kupata chuo, alifurahi sana na kuahidi kunitumia fedha za maandalizi mbalimbali. Baada ya kukamilisha kila kitu, nilianza masomo katika chuo hicho lakini kufuatia kukaa mbali na chuo baba alinishauri nitafute hosteli karibu na maeneo ya shule . Kwa kuwa kila kitu nilichokuwa nakifanya ilikuwa lazima nimfahamishe mpenzi wangu, nilipomweleza kuhusu ushauri alionipa baba wa kukaa hosteli alifurahi sana . Mpenzi wangu aliniambia nitakapohamia hosteli tungepata muda mzuri wa kuwa pamoja yaani ningekuwa nakwenda kulala kwake siku za wikiendi naye angekuwa anakuja kunitembelea hosteli . Kwa ujumla nilifurahia sana kuhama pale nyumbani, Joyce pia alifurahi na kunieleza naye angepata sababu ya kuja kulala kwangu na kwa mpenzi wake . Tangu nilipoanza kusoma , nilikaa Kimara kwa baba mdogo wiki moja ndipo nilihamia hosteli na kuanza maisha ya kuwa huru kwa mara ya kwanza. Nasema huru kwa sababu nilikuwa najipangia kila kitu mfano kula, kwenda kutembea au kulala popote nilipoamua kwa sababu hakuna aliyenizuia japo wazazi wangu walinionya kutoutumia vibaya uhuru nilioupata .

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Nakumbuka kabla sijahamia hosteli mama alinieleza kuhusu wasichana wanaoharibika kwa kuiga mambo ya kihuni wawapo vyuoni hususan wanaoishi hosteli.Alinipa mfano wa wasichana wawili watoto wa majirani zetu Musoma ambao walibadilikatabia walipokuwa wakisoma chuo kimoja cha jijini Dar, ambapo walikuwa wahuni wa kupitiliza.Mama alinionya na kuniambia hakupenda nijihusishe na mambo yasiyofaa, nilimuahidi kuwa makini lakini moyoni nilijisuta kwa sababu tayari nilikuwa nina mpenzi niliyefahamiana naye kupitia facebook.Wiki ya kwanza siku ya Jumamosi tangu nilipohamia hosteli ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kwenda kulala kwa mpenzi wangu, siku hiyo sitaisahau maishani mwangu.Siku hiyo baada ya kumaliza kipindi cha jioni, niliwaaga rafiki zangu Melisiana na Salma ambao walitangulia kuhamia pale hosteli kwamba nakwenda kulala nyumbani.Melisiana alicheka na kuniambia alikuwa akifahamu siendi nyumbani bali nakwenda kwa mpenzi wangu ambaye nilikwisha watambulisha, nikamuuliza sababu za kuniambia hivyo.Melisiana alicheka tena na kuniambia kwa muda niliohamia pale sikuwa na sababu ya kwenda nyumbani na kunitania kwamba niende tu nikampe tende mpenzi wangu.Kufuatia kauli hiyo, niliwaeleza ni kweli nilikuwa nakwenda kwa mpenzi wangu akasema sawa na kunisisitiza niwe makini nisijepata ujauzito.Kutokana na ushauri alionipa, nilimshukuru na kumweleza nilikuwa nalijua hilo na kwamba nilikuwa makini sana wa kutumia kalenda.Baada ya kutaniana kwa muda, niliwaaga na kwenda Tabata kwa mpenzi wangu ambaye alinipigia simu na kunieleza alikuwa akinisubiri kwa hamu bila kujua ambacho kingetokea usiku.Nilipofika nilimkuta akiwa ananisubiri, alinikumbatia na kunibusu na  kuniambia kwamba jioni ile alitaka kunitoa out, nilifurahi sana ndipo tulitoka na kuelekea kwenye baa moja iliyopo Segerea.Tukiwa hapo, aliniuliza nilipenda kula nini nikamwambia atakachokula yeye ndicho nitakula, akanitania kwa kuniuliza hata akila panya.Nilimjibu kwamba nitakula kwa sababu sisi tulikuwa mwili mmoja, mpenzi wangu akacheka na kunipiga kibao cha huba shavuni, alikuwa akipenda sana kufanya hivyo, tukacheka.Wakati huo, tulikuwa  tunakunywa juisi ya boksi ndipo alimwita mhudumu wa jikoni na kumwambia anisikilize tulitaka kula chakula gani.Kufuatia kupewa nafasi hiyo, nilimwambia atuletee chipsi na nusu kuku sahani mbili, niliagiza chakula hicho kwa sababu ndicho alichokuwa akipenda kula mpenzi wangu.Mhudumu alipoondoka, mpenzi wangu aliniambia alijua tu ningeagiza mlo huo, tukacheka kisha nilimwambia mwanamke asiyejua chakula anachokipenda mumewe imekula kwake.Nilipotoa kauli hiyo, mpenzi wangu alicheka na kuzungumsha mkono wake wa kushoto maungoni mwangu na kunivutia kwake, akanibusu shavuni nami nikambusu mdomoni, ilikuwa raha sana!Tulikaa pale mpaka saa tatu ndipo tuliingia kwenye teksi tukarudi nyumbani, kama unavyofahamu wapenzi walioshibana wanavyoweuka wanapokutana, tulikumbatiana tukiwa tumesimama na kupigana mabusu ya nguvu.Hatukuishia hapo, tulikula mua a.k.a denda mpaka tukaiva mithili ya ndizi mbivu iliyokuwa tayari kuliwa, si mpenzi wangu akaanza kupembua blauzi niliyovaa akafuatia vingine mwisho nilibaki mweupe.Nami nilimpembua zake wote tukawa weupe pee, kwa hali tuliyokuwanayo zoezi lililokuwa mbele yetu sina haja kukueleza kwa sababu linajieleza, ila elewa d wangu alikula tende zangu kwa raha zake.Ingawa kila tulipokuwa tukikukutana alikuwa akinifanyia vimbwanga tofauti vya mahabati, usiku ule alivizidisha maana kila alipopagusa nilipata shoti ya umeme.Kutokana na vurugu hizo, nakumbuka nilipasua madafu mawili ya nguvu nikawa hoi. Nilipomuuliza ‘shujaa wangu’ alipasua mangapi, akacheka na kusema mawili yaliyokwenda shule.Siyo siri muda mfupi niliokuwa na d wangu nilifurahi mno kuwa naye ambapo nilimshukuru kwa yote aliyonifanyia, akasemanisijali  na kuongeza kuwa usiku ule ulikuwa maalum kwa ajili yetu.Kufuatia kuchoshwa na segere la nguvu, ilipofika saa sita na robo tulipitiwa na usingizihadi niliposhituka saa nane baada ya kumsikia mpenzi wangu aliyekuwa ameketi kitandani akiweweseka.Nilipomuuliza alipatwa na nini, hakunijibu badala yake aliniangalia tu akaanza kuishiwa nguvu na kujilaza kitandani. Tukio hilo liliniogopesha sana nikataka kwenda kuwaamsha wapangaji wenzetu lakini akanizuia.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akizungumza kwa sauti ya kinyonge aliniambia nisiwe na wasiwasi kwani hali hiyo ilikuwa ikimtokea mara kwa mara , akalala kitandani na kuomba nimfunike kwa shuka nyeupe iliyokuwa juu ya sanduku . Nikiwa nimekosa raha na kupoteza uchangamfu niliokuwanao , nilimfunika kama alivyoniambia nikatulia nikimuangalia huku nikitafakari kuhusu tukio hilo. Alitumia kama dakika 20, alijifunua lakini alikuwa akitokwa na jasho , akanipa pole kwa kuwa katika wakati mgumu , nikasema asante na kumuuliza alipatwa na nini badala ya kunijibu , akatabasamu. Baadaye mpenzi wangu aliniambia siku nyingine akitokewa na hali kama ile nisiogope kwani alianza kusumbuliwa na tatizo lile muda mrefu . Kutokana na hofu niliyokuwanayo nilimwambia jinsi nilivyoogopa , akaniambia nisihofu lilikuwa jambo la kawaida. Kuniweka katika hali ya kawaida alinivutia maungoni mwake akanibusu na kushika nido yangu ya kushoto sijui alifanyaje, nikahisi hali flani tamu. Kufuatia hali hiyo tukajikuta tumeanza kuleteana fujo upya , aliponishika hapa mi nikamshika pale , alipoteremka chini kabisa nami nikaingia ndani kabisa mpaka tukajikuta tumepata mhemko. Kwa kuwa wakati tunaleteana fujo taa ilikuwa inawaka, kila mmoja aliweza kuuona vyema mwili wa mwenzake , mpenzi wangu akanitania kwa kusema ; “ D , naona tu ulivyoiva maana macho yamekulegea na kuwa mekundu kimtindo . ” Baada ya kuniambia hivyo , nilicheka na kumweleza mbona na yeye alikuwa akihema utafikiri alitaka kukata roho, mpenzi wangu alicheka na kunivutia maungoni mwake . Kama vile ndiyo tulikuwa tunalianza segere upya , sijui alifanyaje bwana si nikajikuta mtoto wa kike naelea hewani kwenye sayari ya mapenzi huku naangua kilio cha raha. Mpenzi wangu ambaye imebakia historia baada ya kutenganishwa na jini , siku hiyo alinifanyia vitu adimu maana aliifikia kila sehemu aliyoona ilikuwa tamu. Baada ya kumaliza nngwe hiyo , wote tulikuta tunapitiwa na usingizi hadi kulipokucha . Kilichonishangaza ni pale mpenzi wangu alipochukua manukato yenye harufu nzuri na kupulizia kwenye lile shuka jeupe aliloniambia nimfunike , akalikunja na kuliweka juu ya sanduku . Nilipomuuliza sababu za kufanya vile aliniambia kwamba alikuwa akipendezwa sana na harufu ya yale manukato anapojifunika lile shuka. Kilichonishangaza ni kwamba lile shuka lilikuwa jeupe halafu halikuwa pana sana yaani kama lilikuwa la kazi maalum, hata hivyo nikaamua kupotezea. Kutokana na makasheshe tuliyofanyiana usiku , alfajiri hakuna aliyemhitaji mwenzake ambapo tuliamka tukaenda kuoga kisha mpenzi wangu alikwenda kununua maziwa na vitafunwa ili tupike chai . Hakutumia muda mrefu alirejea akiwa na maziwa freshi ya pakti , mayai na mkate pamoja na blue band, nilipika chai tukanywa , nikaosha vyombo kisha tukajibwaga sebuleni tukawa tunaangalia sinema za Kibongo. Ilipofika saa nne, tuliingia chumbani tukalala kwa staili ya kukumbatiana si tukapatwa na mushawasha wa yale mambo yetu , D wangu akanipa tena haki yangu . Kwa ujumla ilikuwa zaidi ya fungate maana tulifanyiana kila jambo ambalo wapenzi walioshibana walifanyiana bila kujua kama siku moja penzi letu lingekatishwa ghafla . Siku ya Jumatatu asubuhi , mpenzi wangu alinisindikiza mpaka chuoni akaniachia fedha za matumizi tukaagana kisha yeye alirudi nyumbani kwa kujiandaa kwenda darasani alasiri. Tulipokutana na dada Melisiana alinitania kwa kuniambia nilikuwa mwepesi baada ya kupewa haki yangu , niliishia kucheka na kumwambia aache tu kwani nilijipeleka mwenyewe. Baada ya kutaniana na dada huyo niliingia darasani lakini mawazo yalikuwa kwenye lile tukio la mpenzi wangu kuweweseka na kuishiwa nguvu kisha kuniomba nimfunike kwa shuka nyeupe . “ Usiwe na wasiwasi mpenzi wangu, chukua shuka nyeupe hiyo hapo juu ya sanduku nifunike, ” kauli ya mpenzi wake ilijirudia kichwani mwangu . Pia ilijirudia ile kauli iliyosema: “ Siku nyingine nikipatwa na hali kama hii usiogope kwani ni tatizo lililonianza muda mrefu . ” Nilijiuliza ni tatizo gani lililokuwa likimkabili mpenzi wangu , lakini nikaamua kuachana na maswali hayo na kuamini kauli yake kwamba lilikuwa ni tatizo la kawaida bila kujua undani wake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Kwa kuwa nilipika chakula kitamu ambacho mpenzi wangu alipenda kula , alifurahi na kuniambia kwamba hakutegemea kama nilikuwa najua kupika namna ile . Baada ya kunisifia nilijisikia raha na kumwambia kila wikiendi ningekuwa nakwenda Tabata kwa ajili ya kumuandalia chakula badala ya kula chipsi mara kwa mara . D wangu alifurahi kusikia hivyo na kuniambia akinogewa na chakula changu hatasubiri ndoa bali ataamua kunifungia ndani moja kwa moja. Nilicheka na kumweleza wazazi wangu wasingekubalina na suala hilo, akasema alikuwa akinitania na kwamba muda ukifika angeleta barua ya posa . Tulipomaliza kula tuliingia chumbani, kama unavyoelewa wanavyofanya wapenzi ambao penzi lao ndiyo changa , d wangu alinikumbatia na kunibusu midomoni na shavuni . Nilijisikia raha sana , nami nikambusu si tukaendelea na zoezi la kuleteana zile fujo za kiutu uzima , alipozichezea nywele zangu , mimi nikamchezea kidevu chake . Aliposhika mapaja yangu , nami nikawa namshika maeneo ya chini ya tumbo, aliponibusu shavuni , mimi nilimbusu midomoni, kwa ujumla ilikuwa ni zaidi ya raha! Baada ya kuleteana fujo hizo na kila mmoja wetu kuwa ‘ mbendembende ,’ ukizingatia tulikuwa tumeshiba tulijitupa uwanjani kwa lengo la kuendelea na zoezi letu. Tukiwa eneo hilo la kujidai, d wangu hakupata shida ya kuniacha kama nilivyokuja duniani, aliufungua upande wa kanga niliyojifunga kukatisha chini ya kifua changu na kuitupa chini kama haikuwa na kazi tena . Wakati huo tayari alikuwa amebaki na boksa macho yakiwa yamemlegea kuonesha hali ilikuwa mbaya na alichohitaji muda ule ni kucheza kidali poo na wala siyo kwaito. Nilipoangalia kimbeya mbele ya boksa yake niliishia kucheka, nafikiri mdau wangu utakuwa umegundua kilichonichekesha, hatua iliyofuata alikivamia kifua changu kilichopambwa na embe bolibo za mviringo . Kwa kuwa alikuwa akizipenda sana embe zangu , alianza kuzifanyia vimbwanga vilivyonipagawisha na alinimaliza kabisa pale alipoibugia moja na kuifyoza kutoa utamu uliojificha ndani. Siyo siri , siku hiyo nilipatwa na mashamsham ambayo nashindwa namna ya kusimulia ila elewa tu kwamba katika sayari tunayoishi wapo wanaume wanayajua mapenzi kama alivyokuwa mpenzi wangu . Alipoona nilifikia hatua ya mwisho ya kuweweseka na kuhitaji kitu kimoja tu kinachoitwa ‘ mkomboti’ , alimalizia kukitoa kiwalo changu cha mwisho a . k . a kitasa na kulivamia eneo hilo. Kama nilivyokuambia umahiri aliokuwanao d wangu katika sayari ya mapenzi , alinimaliza nguvu kabisa kwa staili yake ya kucheza na eneo hilo, nikahemka huku nikimwita kwa kulikata jina lake. Kilichofuatia hapo, acha iwe siri yangu ila napenda uelewe kwamba mambo yalikuwa matamu kupita maelezo, wote tulifika mwisho wa safari kwa wakati mmoja , ilikuwa safi sana ! Tukiwa tumejilaza kwa kauchovu kalikotokana na fujo tulizoleteana, nilimshukuru kwa alichonifanyia akasema asante naye akanifagilia kwamba mambo niliyaweza . Wakati tukiendelea kusifiana kwa penzi tulilopeana , nilitupa macho juu ya sanduku kubwa la mpenzi wangu nikaliona lile shuka jeupe alilokuwa akiniambia nimfunike alipopatwa na hali ya kuweweseka na kuishiwa nguvu. Sauti moja iliniambia nimuulize ili aniambie kwa kina kuhusu tatizo lake na alikuwa akizungumza na nani nilipomfunika , sauti nyingine ilinionya nisimuulize kwa sababu ningemkwaza kwani tayari aliniambia kuhusu tatizo hilo. “ Happy mpenzi wangu mbona umetulia unawaza nini?” Happy anasema alishtushwa na swali aliloulizwa na mpenzi wake . Kujibalaguza asijue kama nilikuwa natafakari kuhusu ishu yake ya kuweweseka na kuishiwa nguvu, nilimwambia nilikuwa nalitathmini penzi lake tamu. Nilipomwambia hivyo , alitabasamu na kunipiga kibao chepesi cha kwenye shavu na kuniambia kwamba alikuwa akinipenda sana , nikamwambia hakunifikia . “ Happy mke wangu mtarajiwa , najisikia raha sana ukiniambia unanipenda , ” Happy anasema mpenzi wake alimwambia hivyo na kumbusu midomoni. Usiku ule tulitumia muda mwingi kufanyiana fujo za malovee ambapo kila mmoja wetu aliridhika , kutokana na uchovu tulikumbatiana na kupitiwa na usingizi. Nikiwa nimelala niliota ndoto nipo ufukweni mwa bahari nimevaa taiti nyeupe , singilendi nyeupe ya nyavu iliyoonesha mwili wangu na kufanya maziwa kutokeza nje . Eneo nililokuwepo hapakuwa na watu isipokuwa kama mita hamsini ndipo palikuwa na watu waliokuwa wakiogolea . Wakati najimwagia maji , nilihisi nyuma yangu kasimama mtu , nilipogeuka nilimuona mwanaume mrefu sana , moyo ukapiga pa !

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa hofu niliyokuwanayo nilitaka kukimbia lakini yule mwanaume alinizuia, nikaanza kulia kwa sauti na kuwaita watu waliokuwa pale ufukweni . Cha kushangaza ni kwamba licha ya kuwaita na kulia kwa sauti kubwa, hawakunisikia wakawa wanaendelea kuogelea na kucheza michezo mingine ya ufukweni . Yule mwanaume aliniambia ninyamaze kwani nilikuwa nampigia kelele jambo ambalo hakulipenda, kufuatia sauti yake nzito niliogopa nikataka kukimbia akanizuia . Nilishangaa zaidi mwanaume huyo mweupe aliponiita kwa jina langu na kuniambia miongoni mwa watu aliokuwa akiwachukia na mimi nilikuwa mmoja wao . Nilimuuliza alinichukiaje wakati hakunifahamu na sikumtukana wala kumfanyia jambo baya , akaniambia alikuwa ananifahamu vizuri na kusisitiza alikuwa hanipendi . Kauli ya mwanaume huyo kwamba alikuwa hanipendi ilinishangaza , japo nilikuwa simfahamu niliamua kumuomba msamaha kama nilimkosea kwa lengo la kumfurahisha ili aondoke . Nakumbuka nilimwambia hivi : “ Baba yangu sisi ni binadamu siwezi kuendelea kukataa kwamba sikufahamu huenda nilikukosea , naomba unisamehe . ” Kufuatia kumweleza hivyo , aliingia kwenye maji akawa anatembea kwenda kwenye kina kirefu na akiwa umbali wa mita kama tano aliniambia pamoja na kumuomba msamaha alikuwa hanipendi na kwamba atanikomesha. Kutokana na kunieleza hivyo , niliogopa sana nikaanza kulia na kumwomba anisamehe hapo hakuzungumza tena nami akawa anarudi kinyumenyume na kupotelea baharini , nikashtuka usingizini na kuanza kuhema . Wakati nikihema kijasho chembamba kilikuwa kikinitiririka , kwa hofu niliyokuwanayo nilimuamsha mpenzi wangu aliyekuwa kapitiwa na usingizi . Alipoamka aliwasha taa , alipigwa butwaa kuona natiririkwa na jasho na jinsi nilivyokuwa nahema akaniuliza kulikoni , nikamwambia niliota ndoto mbaya ya jini . “ Jini ? akaniuliza kwa kuamaki. Nilimjibu kwamba ndiyo na kumweleza jini alinitokea ndotoni na kuniambia kwamba alikuwa hanipendi na kuahidi kunikomesha, mpenzi wangu akatulia kimya kwa sekunde kadhaa kisha akaniuliza : “ Kwa nini unasema jini , umewahi kumuona jini au unasikia tu habari zao kupitia stori za mitaani?” akaniuliza . Nilimsimulia ndoto niliyoota na jinsi yule mwanaume mrefu alivyopotelea baharini, mpenzi wangu akaniambia nisihofu kwani ilikuwa ndoto tu . Aliponiambia hivyo , nilimfahamisha kuwa zipo ndoto zinakuwa za kweli na kumsisitizia kwamba miongoni mwa ndoto hizo ilikuwa niliyoota . “ Nini kinakufanya uamini ndoto yako ina ukweli ?” mpenzi wangu aliniuliza . Nilimwambia yeye aamini tu ndoto yangu iliashiria jambo flani kutokea kwa vile tangu nilipozaliwa sikuwahi kuota ndoto iliyohusu majini wala kuwepo eneo la ufukweni . Kwa kuwa katika ukoo wetu tuna bahati ya baadhi ya mambo tunayoota kutokea , nilimwambia hilo lakini d wangu akabisha na kunieleza ndoto ni mrejeo wa mambo tunayowaza na kuyafanya mchana . Sikutaka kubishana naye , nilimwambia ipo siku ataamini kwamba ndoto niliyoota ilikuwa ya kweli , akacheka na kunieleza nisiwe na wasiwasi, si akalibinya embe langu la kushoto nikapata raha! Hakuishia hapo , akanibusu midomoni tukakumbatiana na kuanza kula mua a . k . a denda , tukaendelea kuleteana fujo zote ambazo wapenzi wakikutana kwenye eneo lao la kujidai hufanyiana. Kama ambavyo nilielezea huko nyuma juu ya umahiri aliokuwanao d wangu katika tasnia ya mapenzi , alinigusa kila eneo la hatari na kufyonza palipofaa kufyozwa , mtoto wa kike nikaishia kuhemka na kusahau kabisa ndoto mbaya ya yule jini . Nami sikumuacha anitese , niliyavamia maeneo ambayo nilikuwa nina uzoefu nayo kwa mpenzi wangu nikiyagusa au kuyafyoza alipagawa, nikayafanyia kazi sawasawa naye akahemka. Kila mmoja wetu akiwa amefikia joto la mwisho kabisa, unafikiri tuliendelea kuremba, sijui tulishikanaje bwana! Tulijikuta tumezama kwenye ile sayari ya wapendanao . Usiku ule ulikuwa wa aina yake mdau wangu, yaani acha tu ndugu yangu , aliyebuni sanaa ya mapenzi yupo matawi ya juu kabisa ndiyo maana alisema kila mwanaume au mwanamke aliyetimilifu awe na mtu wa kubembea naye . Baada ya kumaliza zoezi la kiutu uzima , nikiwa nimejilaza kifuani kwa d wangu nikajiwa na mawazo ya ile ndoto lakini licha ya awali kusema ilikuwa ya kweli nikayapuuza na kumwamini mpenzi wangu . Baada ya kumaliza zoezi la kiutu uzima , nikiwa nimejilaza kifuani kwa d wangu nikajiwa na mawazo ya ile ndoto lakini licha ya awali kusema ilikuwa ya kweli nikayapuuza na kumwamini mpenzi wangu . Kulipokucha, jambo la kwanza tuliingia bafuni tukapiga mswaki na kuoga pamoja kisha niliandaa kifungua kinywa tukanywa chai nzito, kwa kuwa nilikaa muda mrefu bila kwenda kanisani nilimuomba mpenzi wangu twende tukasali. Mpenzi wangu huyo ambaye kumbe hakuwa Mkristo isipokuwa kwenye facebook alitumia jina la Kikristo , aliniambia siku hiyo alitakiwa kwenda chuo kujisomea. Kwa kuwa nilifahamu mitihani ya majaribio ilikaribia, sikuwa na neno tulijiandaa tukatoka pamoja hadi kituo cha daladala, tukaagana kwamba tungekutana baadaye, yeye akaenda chuo nami nikaelekea kanisani. Baada ya ibada nilipitia sokoni ambako nilinunua mboga , viungo na vitu vingine nikarejea kwa mpenzi wangu , kwa mtu aliyeniona angeweza kufikiri tayari niliolewa . Nilipofika nilipika msosi wa nguvu, kutokana na mapenzi ya dhati niliyokuwanayo kwa mpenzi, ilikuwa siyo rahisi kula bila kumsubiri . Kufuatia hali hiyo ,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilikunywa juisi tu nikawasha runinga nikawa naangalia muvi ya Kibongo na kuchati na mpenzi wangu ambaye tangu tulipoachana asubuhi hatukuwasiliana. Moja ya ujumbe niliomtumia nilimwambia nilikuwa nimemmisi hasa nilipokumbuka utundu alionifanyia tulipokuwa kwenye eneo la kujidai. “ Mimi zaidi d wangu, vipi umeshatoka kazini?” mpenzi wangu alinitumia ujumbe huo. Nilimwambia nilirudi kitambo na tayari nilimpikia chakula anachokipenda lakini sikumweleza ni chakula gani , akaomba nimtajie nikamwambia akija atakiona. Alinibembeleza nimwambie , nilikataa na kusisitiza namsubiri arudi ili tule pamoja, akasema sawa ndipo nilimwuliza alitarajia kurudi saa ngapi. Mpenzi wangu aliniambia alikuwa anamalizia kujisomea hivyo muda si mrefu angefika, nikamweleza nilikuwa namsubiri kwa hamu , ukweli ni kwamba nilihitaji arudi ili tule pamoja kisha tujipumzishe chumbani. Wakati naendelea kuangalia filamu ndipo nilisikia mlio wa ujumbe katika simu yangu , nilipoufungua, mtumaji alikuwa dada Melisiana ambaye alinitania kwamba alijua muda ule nilikuwa nipo chumbani na mzee nimejifunga upande wa kanga nyepesi. Meseji hiyo ilinifanya nitabasamu kwani licha ya kutokuwa chumbani , nilikuwa nimevaa kanga tena nyepesi na viembe vyangu vya kuchoma vilichomoza . “ Hahahaha, huo uchokozi sasa. . . ” niliandika ujumbe huo na kumtumia . Dada Melisiana ambaye sikumficha mambo yangu alipousoma ujumbe huo aliniuliza kama mpenzi wangu alikuwepo nikamwambia hakuwepo, akanipigia. Nilipopokea alinitania kwamba alikuwa anatamani sana kuyaona macho yangu yanavyokuwa nikikolea maana kabla ya kukolea yalikuwa ya kurembua , niliishia kucheka na kumwambia aache utani wake . Wakati tunataniana na Melisiana , nilishtuka kumuona mpenzi wangu ameingia ndani bila kubisha hodi, bila kujali nilikuwa nazungumza na mtu alinisogelea na kunibusu juu ya shavu la kulia . Kwa kuwa alinibusu kwa sauti , dada Melisiana alisikia akaniuliza kulikoni ? Nikawa nacheka kisha nilimuaga nikakata simu. Baada ya kukata simu d wangu aliniuliza nilikuwa nazungumza na nani nikamwambia na Melisiana . “ Si yule anayependa utani?” mpenzi wangu aliyekuwa akimfahamu dada huyo aliniuliza . Nilimwambia ni yeye, tukacheka , alinifuata na kunikumbatia na kunibusu nami nikambusu na kumuuliza alipenda kula kwanza au akaoge , akasema nichague mimi aanze kufanya nini! Licha ya kwamba tangu tulipooga pamoja asubuhi sikufanya kazi ya kutokwa jasho , nilimwambia akaoge nitaungana naye katika zoezi hilo, alifurahi na kusema ndiyo maana alikuwa ananipenda. Nilichokifanya nilimvua nguo kisha tukaingia bafuni ambako tulioga tukarejea mezani tukapata mlo na kwenda chumbani ambapo tulijitupa kitandani tukaanza kupiga stori zilizohusu penzi letu tamu . Wakati tunazungumza alikuwa akizichezea embe zangu , kwa hisia nilizopata nilijikuta naishiwa nguvu na macho yakanilegea, d wangu aliongeza manjonjo yake nami nikajibu mashambulizi tukajikuta tumezama katika bahari ya wapendanao . Baada ya zoezi hilo tulipitiwa na usingizi hadi saa kumi jioni , d wangu aliamua kunitoa out . Baada ya kuoga na kubadili nguo tulielekea kwenye baa moja maarufu iliyopo jirani na eneo aliloishi. Kwa kuwa wote tulikuwa hatutumii kilevi , niliagiza soda yeye akaagiza maji tukawa tunakunywa huku stori zikiendelea baadaye aliagiza chipsi kuku . Tulipomaliza kula tulirudi nyumbani nikachukuwa begi akanisindikiza mpaka chuoni, kabla ya kuniaga tulikumbatiana tukapigana mabusu kisha alianza safari ya kurudi Tabata .

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog