Search This Blog

MIMBA YA JINI - 3

 







    Simulizi : Mimba Ya Jini 

    Sehemu Ya Tatu (3)







    Weee! Mustafa unataka kusema nini, usithubutu tena kumwita mkeo mshenzi, tatizo nini?” sauti ya Shehna ilikuwa kali kidogo iliyomkata kauli.

    “Si..si..,” aliingiwa na kigugumizi.

    “Mustafa nakuamini kwa nini unataka kuharibu mambo, tatizo la mkeo umeishalijua ulitakiwa uzungumze naye kwa sauti ya upole kuliko kuzungumza kama mhuni.”
    “Samahani nilipandwa na jazba.”

    “Mpe simu mkeo.”


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mustafa alimpa simu mkewe aliyekuwa akitokwa na machozi huku akiamini ndoa yake imekalia kuti kavu baada ya siri zake kuwa nje kutokana na kiburi chake cha kutofuata masharti ya kupata mtoto wakati mumewe alikuwa amepoteza fedha nyingi. Alipokea simu katika sauti ya kilio, huku akiwa na donge moyoni baada ya kujua yule ndiye mbaya wake hata akiachika yule ndiye mchawi wake.
    “Haloo.”

    “Haloo, asalam aleiykhum.”

    “Waleiykhum msaalam.”

    “Vipi mbona unalia?”

    “Ha..ha..pana.”
    “Ni hivi yaliyopita yamepita, kama kweli unataka mtoto acha mambo ya kijinga, kuchanganya dawa za uzazi utakuwa mgumba. Wa kulia ningekuwa mimi kwa vile gharama ya dawa niliyowapa ni kubwa zaidi ya kununua gari la kifahari, lakini mwisho wa yote ukafanya kiburi chako ambacho kuna siku kutakuharibia maisha yako.

    “Sasa nasema hivi kuanzia leo nitakupa dawa ya kuoga na kujipaka kwa mwezi mzima bila kukutana na mumeo. Baada ya mwezi ruksa kukutana na mumeo, sasa upo tayari nikuletee hiyo dawa?”
    “Ndi..ndiyo.”

    “Usiseme kutufurahisha, litoke moyoni lisije la kutokea ukasema sijakuambia, najua moyoni mwako unaniona adui. Lakini napigania ndoa yako la sivyo siku zako zilikuwa zikihesabika… Unazungumza vizuri na familia ya mumeo kama zamani?”

    “Hapana.”

    “Unajua kwa nini?”

    “Sababu ya kuchelewa kupata mtoto.”
    “Sasa kwa nini unafanya mchezo wa kitoto.”

    “Hata sijui, labda nimerogwa.”

    “Hujarogwa na mtu bali kiburi chako, kama utaendelea nacho nyumba utaiacha bado unaipenda. Wa kukutoa ndani ni ndugu wa mumeo, nakuibia siri kuna msichana ametafutwa kuja kukutoa ndani, hivyo sasa kazi kwako kufuata masharti ili ubakie katika nyumba yako au vinginevyo.”
    “Sasa kwa mwezi huo hawatakuja kunitoa ndani?” Husna aliingiwa na uoga.

    “Hawawezi, we nisikilize mimi kila kitu kitakwenda vizuri.”

    “Ninakusikiliza dada yangu.”

    “Ukifanya hivyo utanifurahisha, nakuahidi kukupa zawadi kubwa sana maishani kwako.”


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nakuahidi dada yangu kukufurahisha, nitayafanya yote utakayoniambia.”
    “Utakuwa umefanya jambo zuri, haya mpe simu mumeo.”

    Husna alichukua siku na kumpa mumewe aliyekuwa bado amesimama koti na mkoba wake vikiwa mkononi. Mustafa aliipokea simu.

    “Haloo.”

    “Nina imani kila kitu tumemaliza, sasa sitaki ufikie alipotaka kufikia kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa.”

    “Nashukuru, kama amekuelewa mi sina tatizo.”
    “Haya baba wahi kazini.”

    “Nashukuru.”

    Mustafa alikata simu na kumgeukia mkewe na kumweleza.

    “Nina imani mmemalizana naye.”

    “Ndiyo mume wangu, nisamehe kwa yote.”

    “Yote yameisha tumefungua ukurasa upya.”
    “Asante mume wangu.”

    Walikumbatiana kisha Husna alimpokea mumewe alivyobeba na kumsindikiza mpaka kwenye gari.

    Kabla ya kuingia walikumbatiana na kubusiana kisha Mustafa aliingia ndani ya gari na kuondoka kuwahi kazini. Alikwenda moja kwa moja mpaka ofisini, alishangaa kuikuta ofisi haijafunguliwa, kwa vile tangu siku Sara alipochelewa ofisini ufunguo mmoja alikuwa akiondoka nao mwenyewe.

    Alifungua na kuingia ndani ambako alikuta ofisi imejaa vumbi na uchafu kutokana na kutofanyiwa usafi.




    Alijiuliza Sara amepatwa na nini mpaka muda ule hajafika ofisini, aliingia ofisini na kuweka vitu vyake kisha alitoa simu na kumpigia, simu iliyopokelewa na mwanamke upande wa pili.

    “Haloo.”

    “Haloo, nazungumza na nani?”

    “Maria.”

    “Sara yupo wapi?”

    “Alitoka jana kufuata chakula lakini ajabu mpaka kunakucha hatujamuona.”

    “Sasa kaenda wapi?”

    “Hata sisi tunashangaa kibaya hata simu hakuchukua.”

    “Mmh! Sawa.”


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mustafa alikata simu na kujikuta akichoka na kukaa kwenye kochi lake huku akijawa na mawazo ya kujiuliza Sara atakuwa amekwenda wapi. Akiwa katikati ya mawazo alisikia mlango wa ofisi ukigongwa alijua Sara ndiyo anafika.

    “Ingia,” alisema kwa sauti.

    Mlango ulifunguliwa na kutanguliwa na harufu nzuri ya manukato aliyoyazoea ya Shehna, mara aliingia shehna katika vazi la gauni refu la kitambaa cha kitenge na kiremba chake alionekana mwanamke mzuri kuliko siku zilizopita.

    Mustafa kuzungumza alishindwa alibaki kamtumbulia macho kama siku yake ya kwanza kumuona.

    “Mustafa kushangaa gani huko kama ndiyo leo siku yako ya kwanza kuniona?” alimuuliza huku akimsogelea alipokuwa amekaa.

    “Shehna lazima nimsifu Mungu kwa utundu aliofanya kukuumba, Shehna wewe ni mwanamke mzuri wa wazuri, uzuri wako kama nyoka anayejibadili mwili wake, kila siku uzuri wako unaongezeka, wa leo unashinda wa jana pia naamini wa kesho utauzidi wa leo.”

    “Mmh! Kawaida sema bado hutatuliza macho kwangu unaniangalia kwa wasiwasi, kama ungekuwa hunitazami kwa wasiwasi wala usingenishangaa. Nilichokibadili asubuhi hii ni nguo tu, mimi ni yuleyule wa jana wa leo na kesho vilevile.”

    “Wewe unaweza kusema hivyo, najuta kuchelewa kukujua mapema.”

    “Ulinifahamu mapema lakini hukunitilia maanani, nilikuja kwako kila wakati lakini labda uliniona mwanamke malaya.”

    “Ha..ha..pana, sijakufikiria hivyo!”

    “Sasa tatizo lako nini?”

    “Nina wasiwasi wenye fedha zaidi yangu wataninyang’anya.”

    “Kwani nipo wapi siku zote wasikunyang’anye wakunyanganye leo?” Shehna alimuuliza huku akimuangalia jicho tata lililozidi kumchanganya Mustafa na kutamani heri angekuwa mkewe wa ndoa. Lakini bado aliona maisha ya Shehna asingeyaweza kwani kila alipokutana naye alikuwa na nguo na vito vya thamani ambavyo aliamini hawezi kuvinunua.

    Shehna aligundua alichokuwa akikiwaza Mustafa baada ya kukaa kimya kwa muda. Alimshtua kwa kumwita jina lake.

    “Mustafa.”

    “Naam.”


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwa nini unajibebesha mawazo mazito ambayo sivyo unavyonifikiria?”

    “Umejuaje?’

    “Si kujuaje, bali nataka kukuthibitishia maisha yangu na wewe ni tofauti unavyonifikiria, kila kitu juu ya mustakabali wetu niachie mimi.”

    “Sawa nimekuelewa.”

    “Na..na mbona ofisi chafu?”

    “Nashangaa mpaka muda huu msaidizi wangu sijamuona, ha..halafu nasikia toka jana usiku hajarudi.”

    Kauli ile ilimfanya Shehna acheke kicheko cha umbea kilichomfanya Mustafa ashtuke na kuhoji.

    “Vipi mbona unacheka kama unajua kinachoendelea.”

    “Walaa, nimecheka tu.”

    “Yaani hapa nimechanganyikiwa ngoja nimwite mlinzi ufanye usafi.”

    “Walaa, kazi hiyo nitaifanya miye.”

    “Hapana Shehna, acha ataifanya mlinzi.”

    “Kwani mimi kufanya kuna nini?”

    “Utajichafua bure wakati watu wa kuifanya kazi hii wapo.”

    “Basi leo nitaifanya mimi, naomba unipishe mara moja.”

    “Sawa, basi nipo nje kwa mlinzi.”

    “Hakuna tatizo.”

    Mustafa alitoka nje na kumuacha Shehna ofisini, kabla ya kufanya kitu aliangua kicheko cha mfululizo kufurahia alichomfanyia Sara mwanamke aliyemuona asidi aliyetaka kushindana naye. Kisha alijishika kwenye paji la uso na kutulia kwa muda, mara vijakazi na watwana toka ujinini walipiga magoti mbele yake na kumuuliza.

    “Mwana wa Mfalme wa jini la bahari ya dhahabu una shida gani unayotaka tukufanyie?”

    “Nataka baada ya muda mfupi ofisi yote uwe safi kuliko siku zote.”

    “Hewala mwana wa mfalme.”

    Vijakazi na watwana waliingia katika kazi ya usafi iliyochukua dakika tano kila kitu kilikuwa safi ndani. Kilibadilishwa kila kitu na kuwekwa pazia nzuri la halili na kuifanya ofisi ipendeze mara dufu. Baada ya kufanya usafi walipiga magoti mbele ya Shehna na kusema....


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mtukufu mwana wa Mfalme wa jini la bahari ya dhahabu tumemaliza kazi, kama kuna kasoro tupo tayari kwa adhabu yoyote kutoka kwako."



    "Hapana nawamini."

    "Asante mwana wa mfalme."

    Shehna hakuwa na shida ya kukagua kwa kuamini majini walikuwa wakijua usafi kuliko mwanadamu.

    "Nimefurahi kwa yenu nzuri, mnaweza kuondoka."

    Kufumba na kufumbua vijakazi na watwana walitoweka na kumuacha Shehna alifurahia hali nzuri ya kupendeza ya ofisi. Alitoka nje na kumwita Mustafa aliyekuwa akizungumza na mlinzi. Alikwenda ndani na kuishangaa ofisi ilivyopendeza tofauti na siku zote.

    "Duh! Kazi hii imeifanya peke yako?"

    "Umemuona nani akinisaidia?"

    "Hongera sana."

    "Asante, ila kama Sara hatatokea na kesho funguo iache mlangoni, nitakuwa nawahi mapema kufanya usafi kabla hujafika mpaka atakaporudi kazini ."

    "Nitafanya hivyo."

    "Mustafa mimi si mkaaji ilikuja kukushukuru wa mapenzi yako matamu, hakika leo nimefaidi usichana wangu kwa kupata penzi lililokamilika. Nakuahidi baada ya kushika ujauzito nitakupatia zawadi kubwa sana."

    "Wala usihofu, lakini nina wasiwasi wa kuharibu masharti yako."

    "Wala usiwe na wasiwasi, asubuhi umenilaisishia kufanya mambo yetu bila mkeo kukusumbua. La muhimu kufanya yote kama niliyokuelekeza."

    "Nitafanya hivyo."

    "Basi nikuache uendelee na kazi."

    "Nashukuru."

    Walikumbatiana kisha Shehna aliondoka na kumuacha Mustafa alimsindiza kwa macho.

    ***


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wiki nzima ilikatika bila kuonekana kwa Sara huku Shehna akiendelea kufanya usafi kila siku na kuifanya ofisi izidi kupendeza. Kwa hali ile ilifikia hatua ya Mustafa kuomba Sara isirudi tena kutokana na usafi uliokuwa ukifanywa na Shehna uliifanya ofisi yake isifikiwe kwa kila aliyeingia na kutaka kupatiwa mtu mwenye uwezo wa kufanya usafi kama wa ofisini kwake.

    Wakati wote huo kila siku Shehna alikwenda nyumbani kwa Mustafa na kufanya naye mapenzi kitandani kwake huku mkewe akiwa amepitiwa usingizi. Siku zote alifuata masharti aliyopewa kuyafanya kabla ya kulala. Zoezi kubwa kwake lilikuwa kumpaka mafuta mkewe ambayo humfanya alale mpaka asubuhi bila kugeuka na kuacha wafanye mambo yao bila yeye kujua kinachoendelea.

    Mustafa alifanya vitu vyake siku zote kwa umakini mkubwa kwa vile mkewe hakuweza kukutana naye tena kimwili baada ya kuelezwa na Shehna ili aweze kupata mtoto huku akiendelea kutumia dawa alizopewa. Hata kulala sehemu ya ukutani hakulazimishwa kwa vile lilikuwa moja ya masharti ya dawa.

    Siku zote alifanya kama alivyoelekezwa, lakini siku moja alirudi nyumbani akiwa amechoka sana na kusahau kumpaka mafuta mkewe kwa kuamini aliisha mpaka. Usiku kama kawaida Shehna aliingia ndani na kunyanyua Mustafa na kwenda naye bafuni kuoga baada ya kuoga alirudi kitandani na kuanza kuandaana kisha waliingia kwenye tendo.

    Hatua ya awali iliisha kila mmoja alifurahia penzi la mwenzake kisha walipumzika kwa muda ili kujiandaa kwa hatua nyingine. Shehna kama kawaida alimpa Mustafa maji ya kunywa yaliyomrudishia nguvu na kurudi tena bafuni kuoga na kuingia hatua ya pili. Mapenzi yalipopamba moto Shehna aligugumia kimapenzi kwa kuusifia uwezo wa Mustafa kimapenzi.

    Kwa vile mke wa Mustafa hakupakwa mafuta ya kumlaza, sauti ya kulalamika kimapenzi ilimshtuka usingizini.









    Alipoangalia pembeni yake alimuona mumewe akifanya mapenzi na mwanamke mzuri wa Kiarabu, wote walikuwa katikati ya tendo. Alitulia kwa muda na kujiuliza alichokiona ni kweli au anaota.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alikaa kitako na kupekecha macho yake kama kweli amelala au yupo macho, akili yake ilimweleza hakulala bali yupo macho na anachokiona ni kitu cha kweli wala si cha ndotoni.

    Alijiuliza yule ni mwanamke gani asiye na woga aliyeingia ndani mwake bila hofu, alijiuliza tabia ile ya mumewe kuingia na mwanamke ndani na kufanya naye mapenzi kitanda wanacholala bila woga, imeanza lini?

    Wakati akiwaza vile, Shehna alishtuka baada ya akili yake kutambua mke wa Mustafa ameamka na kuangalia kilichokuwa kikiendelea pembeni yake.

    Alijibadili ghafla na kutoweka kitandani na kumuacha Mustafa akilalamika kwa kumwita jina lake.

    “Shehna mpenzi unaenda wapi?”

    Shehna hakujibu, alisogea pembeni ya mke wa Mustafa na kumpuliza usoni, usingizi mzito ulimchukua Husna na kurudi kitandani kulala.

    Baada ya kulala, Shehna alimuuliza Mustafa aliyekuwa hajui nini kilichokuwa kikiendelea.

    “Mustafa umefanya nini?”

    “Kuhusu nini mpenzi?”

    “Kwa nini hukumpaka mafuta mkeo?”

    “Nilimpaka.”

    “Muongo! Tutamwambia nini mkeo ikiwa ameona kila kitu?”

    “Kwani aliamka?”

    “Ameamka na ameona kila kitu.”

    “Mungu wangu!” Mustafa alishika mikono kichwani.

    “Basi mi naondoka na hutaniona tena katika maisha yako,” Shehna alisema kwa hasira huku akielekea alipoweka nguo zake.

    “Usifanye hivyo mpenzi, nakuhitaji kuliko kitu chochote, inawezekana uchovu ulisababisha nipitiwe. Naomba unisamehe sana.”

    “Mustafa nakupenda sana, lakini masharti yangu ya kuendelea kuwa na wewe yatakuwa magumu sana kuliko mwanzo na nina imani utayashindwa.”

    “Nakuahidi kuyatekeleza yote.”

    “Kweli?”

    “Kweli kabisa.”

    “Unajua nakupenda?”

    “Tena sana.”


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kesho mkeo lazima atakuuliza kuhusiana na alichokiona usiku huu kwa vile aliendelea na usingizi atataka ukweli kutoka kwako. Wewe kataa kwa vile hana uhakika kwa kile alichokiona kama ni kweli au ndoto.”

    “Sawa nitafanya hivyo.”

    “Kwa vile amelala tuendelee na dozi ya mwisho lakini kuanzia kesho tunabadili mfumo.”

    “Sawa mpenzi nipo radhi kwa lolote.”

    Walikwenda kuoga na kurudi kumalizia dozi ya mwisho kisha Shehna aliondoka na kumuacha Mustafa usingizini.

    ***

    Husna alikuwa wa kwanza kuamka mumewe alikuwa bado amelala, alimuangalia na kujikuta akivuta kumbukumbu ya usiku na kujiuliza alichokiona usiku kilikuwa kweli au ndoto kwa vile toka aolewe na Mustafa, hakuwahi kutokewa na tukio kama lile kwa sababu alimuamini sana mumewe kwa uaminifu wa ndoa yao kwa kipindi chote pamoja na matatizo yote, hakuwahi kumdharau wala kumsaliti.

    Kwa akili ya kawaida aliamini kabisa aliamka usiku na kukuta mumewe akifanya mapenzi na mwanamke wa kiarabu. Lakini kilichomshtua mbona ameamka asubuhi kutoka usingizini?

    Kila lililokuja mbele yake lilimchanganya, ili apate jibu la kitendawili chake aliamua kumuamsha mumewe. Baada ya kumtikisa kwa muda huku akimwita kwa jina lake, Mustafa alishtuka usingizini na kumgeukia mkewe.

    “Vipi?” alimuuliza huku akilazimisha macho kufumbuka.

    “Mume wangu hebu amka.”

    “Kuna nini?”

    “Si uamke,” Husna alisema kwa sauti kali kidogo.

    Mustafa aliamka na kukaa kitako ili amsikilize mkewe.

    “Mume wangu,” alianza kwa kumwita.

    “Naam.”

    “Kuna kitu kimetokea sijui ni kweli au ndoto.”

    “Kitu! Kitu gani?” Mustafa alijifanya kushtuka.

    “Kuna kitu nimekiona usiku, kimenichanganya sana.”

    “Kitu gani?” Mustafa alimuuliza huku akifikisha macho yake na kupiga miayo ya uchovu wa kulala.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Husna alimweleza mumewe kila kitu alichokiona ambacho yeye aliamini haikuwa ndoto. Kwa vile alielezwa na Shehna kilichotokea na nini ajibu, alimwambia mkewe.

    “Kwa akili ya kawaida kitu hicho kinaweza kufanyika?”

    “Hata mi nashangaa, lakini nakumbuka niliamka na kukaa kabisa.”




    "Baada ya kukaa nini kiliendelea?"

    "Sikumbuki zaidi ya kushtuka alfajiri na kujikuta nimelala."

    "Sasa wasiwasi wako nini?"

    "Ndipo hapo ninapo changanyikiwa kilikuwa nini."

    "Hebu achana na ndoto, hivi kweli nilete mwanamke ndani na kufanya naye mapenzi kitanda tunacholala, imeanza lini?" Mustafa alizidi kujifanya kumshangaa mkewe.

    "Hata mi namshangaa."

    "Hebu achana na ndoto za kijinga."

    "Basi samahani mume wangu kama nimekukwaza."

    "Walaa, una haki ya kuniuliza chochote."

    Wakiwa katikati ya mazungumzo simu ya Mustafa iliita, alipoangalia ilionesha inatokwa kwa Shehna. Aliipokea na kuzungumza naye.

    "Haloo."

    "Haloo, asalam aleykum."

    "Waleykum salam."

    "Vipi mmeamkaje?"

    "Mmh! Salama."

    "Kweli?" Shehna aliuliza.

    "Kweli."

    "Mbona kama mkeo ana tatizo?"

    "Sijui ameota nini."

    "Ameota nini?" Shehna alijifanya kushtuka.

    "Sijui ameniona eti mimi nina fa...fa.."

    "Hebu mpe mwenyewe azungumze, acha kung'ata maneno," Shehna alimkata kauli Mustafa.

    Mustafa alimpa simu mkewe aliyekuwa bado amesimama pembeni ya kitanda. Husna aliipokea na kuzungumza.

    "Asalam aleykum."


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Waleykum salam, eti mpenzi kuna nini?" Shehna alimuuliza kwa sauti ya upole.

    Husna alimweleza kama alivyomweleza mumewe kilichotokea usiku. Baada ya kumsikia alisema:

    "Mpenzi hizo ni ndoto ambazo huvunja ndoa nyingi kwa vile mtu huota ukiwa macho na kuweza kuamini ni jambo la kweli. Hizo ni ndoto tu, lakini mumeo akirudi kazini atakupatia dawa ya kujipaka wakati wa kulala haitakutokea tena."

    "Nitashukuru kwa kweli ilinishtua sana."

    "Pole mpenzi."

    "Asante dada yangu, jamani nina hamu ya kukuona tutaonana lini?"

    " Utaniona tu usiwe na wasiwasi hata mimi nina hamu na wewe, unasema uliyemuota akifanya mapenzi na mumeo uliiona sura yake?"

    "Ndiyo."

    "Kwa mfano akutokee mbele utamjua?"

    "Nitamjua nilimuona vizuri sana japo nilikuwa naota."

    "Basi mpenzi nikimaliza mizunguko yangu nitakuja utanichoka mwenyewe."

    "Walaa labda unichoke wewe."

    "Basi mpenzi usiendekeze ndoto."

    "Nimekuelewa."

    Shehna alimalizia kuzungumza na Husna na kumalizia kuzungumza na Mustafa kisha alikata simu. Mazungumzo yake yalirudisha imani moyoni kwa Husna na kuamini aliyosema Shehna yalikuwa na ukweli mkubwa. Baada ya moyo wake kuamini ile ilikuwa ndoto, alimtayarishia mumewe maji ya kuoga na kifungua kinywa huku moyo wake ukiwa mweupe.

    Mustafa baada ya kufungua kinywa alimuaga mkewe na kuelekea kazini, kama kawaida alikuta ofisi imesafishwa. Akiwa ofisini Shehna alimtokea kabla hajaanza kazi na kuzungumza naye sakata la usiku.

    "Mustafa nilitaka kukulaumu lakini umenilahisishia kazi, yale mafuta niliyokupa kumpaka mkeo mpe ajipake mwenyewe. Hakikisha unamkumbusha kujipaka kabla hajalala, itatusaidia kumteka bila kujijua."

    "Yaani nashukuru sana sijui bila wewe ingekuwaje?"

    "Ungekataa tu, lakini lazima angeuliza kwa watu na kutaka kuchimba na kuujua ukweli."

    "Unafikiri angeujua ingekuaje?"

    "Mmh! Tungejua tifanyeje japo ingetusumbua kidogo."

    "Nashukuru sana mpenzi umenisaidia."

    "Basi nikuache ufanye kazi."

    "Nashukuru."

    Shehna aliaga na kuondoka na kumuacha Mustafa akijiandaa kuanza kazi ya siku ile.





    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Msichana mmoja alionekana amelala chini ya mti mkubwa pembeni ya barabara kuu ya kutoka Dodoma kwenda Mpwapwa akiwa amejifunga kipande kichafu cha khanga kwa chini na juu matiti yalikuwa wazi.

    Miguu ilikuwa pekupeku, ilijaa tope lililokauka na kujaa vumbi. Wasamaria wema waliopita njia ile waliamini yule ni mwendawazimu, lakini ilikuwa ajabu kwa eneo lile hakuna hata mmoja aliyekuwa akimfahamu.

    Toka watu walipomuona amelala chini ya mti, ilipita zaidi ya saa sita bila kugeuka kitu kilichowatisha na kufikiria labda amefariki.

    Walimsogelea na kumtikisa, alifumbua macho kuwatazama lakini alikuwa amechoka kwa njaa na uchovu. Walimchukua na kumpeleka kwenye makazi ya watu na kumpatia chakula baada ya kushiba, walimpatia maji ya kuoga na nguo. Alionekana ni mtu mwenye akili zake timamu wala si kichaa kama walivyomfikiria.

    Baada ya kutulia, walimuuliza maswali kutaka kujua ametoka wapi na amefikaje pale.

    “Unaitwa nani?”

    “Sara.”

    “Umetokea wapi?”

    “Dar es salaam.”

    “Umefikaje huku?”

    “Kwani huku wapi?” aliuliza huku akipepesa macho kuishangaa sehemu ile ambayo ilikuwa ngeni kwake.

    “Hapa ni Kongwa njia ielekeayo Mpwapwa.”

    “Kongwa si Dodoma?” Sara alishtuka.

    “Ndiyo.”

    “Waongo!” Sara alibisha haku haamini kufika Dodoma kwa kutembea usiku mmoja tena kwa miguu.

    “Dada kwani sehemu hii unaijua?”

    “Mmh! Hapana.”

    “Duh! Uliondoka kwako lini?”

    “Jana usiku?”

    “Mmh! Upo sawa kiakili?” mmoja alimshangaa majibu ya Sara.

    “Na wala sijawahi kuugua ugonjwa wa akili.”

    “Basi hapa ni Kongwa.”

    “Mungu wangu, nimefikaje huku?” Sara alishtuka huku macho yakimtoka pima.

    “Kwani ilikuwaje?”

    Sara aliwaeleza jinsi alivyopotea baada ya kutoka kwake kuelekea kwenye banda la chipsi kununua chakula cha usiku na kujikuta akipotea njia na kushangaa kujiona yupo katikati ya pori na kutembea bila kufika mpaka alipofika chini ya mti ule alfajiri, akiwa amechoka sana na kuamua kupumzika kwa vile hakujua anapoelekea.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haiwezekani utoke Dar kwa miguu jana usiku ufike Dodoma alfajiri!” mtu mmoja alipingana na maelezo ya Sara.

    “Basi hapa ni Kongwa mkoa wa Dodoma ndiyo maana tuna wasiwasi na maelezo yako huenda akili yako haipo sawa.”

    “Akili yangu iko sawa, kwani leo ni siku gani?” aliuliza baada ya kumuona watu wakipita kuelekea kanisani.

    “Jumapili.”

    “Mungu wangu! Haiwezekani nitoke nyumbani Jumatatu mpaka leo Jumapili, haiwezekani nitembee kwa miguu wiki nzima, nimewakosea nini kunitesa hivi,” Sara alilalamika huku akitokwa machozi.

    “Kina nani?”

    “Hata najua, Mungu atanilipia.”

    Sara alianza kulia na kuwafanya wasamaria wema kumbembeleza, baada ya kunyamaza. Aliwaomba msaada wa kumrudisha Dar kwa vile muda ulikuwa umekwenda, walimpa hifadhi ya kulala pale ili siku ya pili alfajiri wampandishe basi mpaka njia panda kisha apande basi kurudi Dar.

    Usiku kucha hakulala kuwaza yaliyomtokea, kwake hakuamini, aliamini tukio lile ni la ndotoni halina ukweli wowote. Siku ya pili aliamshwa alfajiri na wenyeji wake na kupandishwa mabasi yanayokwenda njia panda ili apande yanayokwenda Dar es Salaam.

    Baada ya kupanda haisi iliyompeleka njia panda ambapo alipanda basi la Shabib na kutulia kwenye siti, basi likiwa linakwenda aliangalia mapori ya njiani ambayo yalimfahamisha yupo safarini lakini bado hakuamini njia nzima alikuwa akijiuliza nini kilichomfanya afike mkoani Dodoma kwa miguu bila kuchoka wala kudhurika na wanyama wakali.

    Pamoja na kuamini yumo ndani ya basi, bado hakuamini tukio lililomtokea ni la kweli. Kwake aliamini ile ni ndoto iliyomchanganya na akiamka asubuhi atajikuta yupo kitandani amelala. Basi lilingia Dar majira ya saa sita na nusu mchana, bado Sara hakuamini. Aliteremka kwenye basi baada ya abiria kuanza kuteremka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/




     Baada ya kuteremka aliangalia pesa yake ya nauli aliyokuwa amefunga kwenye khanga chakavu.

    Alifungua na kuikuta elfu moja iliyochafuka kwa udongo wa kijijini, chini alikuwa amevaa ndala rangi mbili moja nyekundu na nyingine bluu. Nywele zake zilikuwa timutimu.
    Sara alionekana kweli mwana kijiji kutokana na jinsi alivyokuwa, muda wote hakujiona kwani kama angejijua alivyo asingeweza hata kutembea kutokana na jinsi anavyojipenda. Hata alipotaka kupanda daladala konda alimuona wa kuja na kumsemesha maneno ya kejeri.Sara hakujali aliingia ndani ya daladala hadi Kinondoni Kanisani anapokaa. Baada ya daladala kusimama aliteremka na kuelekea kwake. Alipokaribia alishangaa kuona mlango wa chumba chake ukiwa wazi. Shoga yake Happy aliyekuwa amekaa nje alikuwa wa kwanza kumuona na kushtuka kufuatia rafiki yake huyo kuwa katika mavazi ya ajabu, gauni lililochanika mabegani khanga iliyopauka na kandambili rangi mbili."Sara!" Happy alimwita kwa sauti ya juu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sauti ile ilikuwa kama kitu kilichomzindua toka usingizini na kujikuta naye akijishangaa.

    "Shoga ulikuwa wapi? Jamani mbona umevaa nguo za ajabu?"

    Kauli ile ilimfanya ajichunguze na kujikuta akijishangaa mavazi aliyovaa na kujikuta akiangua kilio huku akisema.
    "Mungu wangu! Kumbe kweli nilidhani ndoto."

    "Kumbe kweli nini jamani?" Happy alitaka kujua.

    Sara hakusema kitu alikimbilia ndani na kujitupa kitandani na kuanza kulia kilio cha sauti na kuwafanya majirani wakusanyike nje ya chumba chake. Happy ndiye aliyeingia ndani kutaka kujua shoga yake alikumbana na nini, kitu kilichofanya atoweke nyumbani kwa wiki nzima na kurudi akiwa kama mwana kijiji.
    "Sara umepatwa na nini?" Happy alitaka kujua.

    "Mmh! Hata simamini nitembee usiku kucha mchana kutwa kwa siku sita bila kupumzika mpaka Dodoma?"

    "Dodoma?" Happy alishtuka.
    "Ndiyo dada hata siamini hizi nguo nimepewa na wasamaria wema wa Kongwa walioniokota nikiwa nimelala barabarani."

    "Wewee!" Sara alishtuka.

    "Yaani kama nisingepanda Hiace toka Kongwa kisha basi la Shabiby ningebisha na tiketi yake ni hii," Sara alimuonesha Happy tiketi ya basi ambayo ilionesha ilikuwa ya siku ile.
    Baada ya Sara kuisoma akili yake bado haikuamini shoga yake kwenda Dodoma kwa miguu aliona kama mchezo wa kuingiza.

    "Sara, siku ile si ulisema unakwenda kununua nyama ya nguruwe na ndizi?"

    "Ndiyo shoga yangu, nimetoka vizuri mpaka karibu kwa Macha Kitimoto. Ghafla nilijishangaa kujikuta katikati ya pori hata sijui ni pori gani."
    "Wewee!" Happy alizidi kushtuka.

    "Yaani niliogopa mpaka haja ndogo ikanitoka, kibaya zaidi nyuma yangu kulikuwa na milio ya ajabu ya kutisha na kunifanya nikimbie kwenda mbele japosikujua ni wapi nilipokuwa nakimbilia. Kila nilivyokuwa nikikimbia ndivyo sauti za kutisha zilivyokuwa zikinisogelea na kunifanya nizidi kukimbia.
    "Nakumbuka upande wa khanga wa juu ulinidondoka lakini sikuujali zaidi ya kuyaokoa maisha yangu ambayo niliyaona yapo hatarini. Kandambili nilizokuwa nimevaa zilinidondoka na kujikuta nakimbia pekupeku huku nikikatiza kwenye vichaka na kukanyaga miba."Kutokana na kutokewa na vitu vile vya kutisha ambavyo sikudhania kukutana navyo hata siku moja, nilijua ile ni ndoto tu wala si kweli. Baada ya kukimbia kwa muda mrefu bila kupumzika, nilianza kusikia vichomi kwenye mbavu na kunifanya nishindwe kutembea."Zile sauti za kutisha zilizidi kunisogelea nikaona kama nitazubaa basi nitakufa. Nilijilazimisha kukimbia huku nimeshika mkono kwenye mbavu. Nilikwenda hivyo kwa kuchechemea mpaka nilipotokea kwenye mti mkubwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/





    "Kwa vile nilikuwa nimechoka sana, nilijiegemeza kwenye mti mkubwa pembeni ya barabara, pamoja na alfajiri ile kuwa na baridi kali lakini usingizi ulinichukua.

    "Mpaka nilipoamshwa na wanakijiji, sikuamini waliponiambia pale ni Kongwa Dodoma na muda ule ni saa nane mchana, kingine kilichonishangaza kuelezwa siku ile ni Jumapili wakati niliondoka nyumbani Jumatatu.
    "Yani bado siamini kutembea kwa mguu kwa wiki nzima, kibaya zaidi nakumbuka nilitembea usiku mmoja lakini imeonekana nilitembea wiki nzima. Kama nilitembea wiki nzima, mbona sikuuona mchana zaidi ya usiku tu?" Sara alihoji huku machozi ya uchungu yakimtoka.

    "Dada hiki ni kituko yani lazima uende kanisani ukaombewe, lazima watakuwa ni wachawi tu walikuchukua."
    "Na..na..kwe...," Sara alisita kuzungumza baada ya kumuona nguruwe amekaa kwenye kiti alichokaa Happy, alipiga kelele za uoga.

    "Mamaa nakufa nguruwe."

    "Sara nguruwe yupo wapi?" Happy alimshangaa rafiki yake.

    "Si..si...," alituliza macho na kushangaa kumuona aliyekaa mbele yake ni Happy na si nguruwe kama alivyoona..
    "Sara upo sawa?" Happy aliamini rafiki yake hayupo sawa.

    "Ni..ni..hapana..hapana," Sara alituliza macho yake baada ya kumuona tena nguruwe kwenye kochi hakupiga kelele, alitulia na kufikicha macho ili kupata uhakika kama kweli kilichopo mbele yake ni nguruwe au anaona maruweruwe. Baada ya macho kutulia alimuona tena shoga yake Happy wala si nguruwe.

    "Happy naomba nipumzike, siko vizuri sijielewi kabisa."
    "Sawa dada lakini kwanza nenda ukaoge ili kuufanya mwili upumue."

    "Sawa," Sara alisema huku akivua nguo alizokuja nazo na kuchukua taulo ili aende bafuni.

    Alichukua sabuni na mswaki kisha alitoka nje na kumuacha shoga yake akimfanya usafi wa chumba. Sara alielekea nje alipofika mlangoni alisita kutoka baada ya kuona nguruwe wamejaa uani. Alizidi kushangaa na kumwita Happy kwa sauti.

    "Happy njoo."

    Happy aliacha kufanya usafi na kusogea mlangoni.

    ‘Vipi?"

    "Eti nje unaona nini?"

    "Kawaida, kwani umeona nini?"

    "Nguruwe."

    "Nguruwe?" Happy alishtuka.
    "Hebu ngoja," Sara alisema huku akipekecha macho na kuona wapo wapangaji wenzake na si nguruwe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mmh! Mbona mwaka huu wangu."

    "Shoga kuna umuhimu twende kanisani ukaombewe."

    "Ngoja nikaoge."

    Sara alikwenda hadi bafuni na kuoga kisha alirudi ndani bila hali ile kumtokea tena. Kwa vile alikuwa amechoka sana, alipanda kitandani na usingizi mzito ulimchukua.

    ****

    Siku ya pili Sara alidamka mapema na kuoga kisha alitoka kwenda kazini kwa kumuaga shoga yake Happy. Happy alimuuliza alivyolala.

    "Vipi umelala salama?"

    "Namshukuru Mungu nimelala salama, wacha niwahi kazini japo sijui bosi wangu kama atanielewa."

    "Atakuelewa tu kwani kilichotokea si cha kawaida."

    "Mmh! Ngoja niwahi."

    "Mi nilikuwa na wazo."

    "Wazo gani?"

    "Nilikuwa na wazo la kwenda kwanza kanisani ukaombewe pepo mchafu."

    "Wazo zuri lakini lazima nifike kwanza ofisini nijue hatima yangu ndipo twende huko kanisani."

    "Basi ukirudi jioni tutapanga."

    "Sawa."

    Sara aliagana na shoga yake na kuwahi kazini kama kawaida kwa kuwahi ili afanye usafi kabla bosi wake hajafika.






    Mlinzi alimpa ufunguo kama kawaida, alifungua ofisi na kushtuka kuikuta safi imeisha safishwa. Hali ile ilimshtua na kumfanya atoke nje mpaka kwa mlinzi na kumuuliza;



    "Eti nani kafanya usafi?"

    "Wapi?"

    "Ndani ya ofisi?"

    "Wewe ndo wa kwanza kuja sijamuona mtu yeyote."
    "Kwa...kwa niiii toka nilipoondoka nani alikuwa akifanya usafi?"

    "Kwani da Sara ulienda wapi?"

    "John si muhimu kujua, nijibu swali langu."
    "Toka uondoke sijawahi kumuona mtu akifanya usafi, nakumbuka siku ambayo wewe hukuja bila taarifa nilitaka kwenda kufanya usafi lakini bosi alinikataza, tokea siku hiyo sijamuona mtu akifanya usafi."

    "Ina maana toka niondoke hakuna mtu uliyemuona anafanya usafi?"


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sijawahi kumuona."
    "Mbona ofisi inaonesha imefanyiwa usafi muda si mrefu tena wa hali ya juu?"

    "Basi majini ndiyo yamefanya usafi," mlinzi alisema kwa utani.

    "John na wewe umeligundua hilo?"

    "Lipi?"
    "La kuwepo na jini ofisini?"

    "Mi nimesema tu, hilo jini lifanye usafi kwa ajili gani?"

    "Kama mimi nilikuwa sifanyi usafi, basi nani amefanya?"

    "Mmh! Labda bosi."
    "Nataka kukuambia hapa kuna mchezo, unamjua yule mwanamke?"

    "Mwanamke gani?"

    "Yule mrembo anayekujaga ofisini."

    "Ndiyo."
    "Yule nina wasiwasi siyo mtu wa kawaida."

    "Una maanisha nini?"

    "Mimi simwelewi huenda ni jini!"

    "Jini? We acha mambo ya ajabu angekuwa jini tungemuona?"

    "Nakwambia ipo siku utakubaliana na mimi."
    "Kwa hiyo bosi wateja wake wengine ni majini?"

    "Hebu kwanza nikuulize?"

    "Uliza."

    "Tangu niondoke yule mwanamke kaja mara ngapi?"

    "Kwa kweli sijamuona."
    "Muongo!"

    "Kweli."

    "Basi we subiri kama ni yeye nitakomeshana...na...na,"Sara alinyamaza baada ya kuliona gari la bosi wake likisimama getini.
    Hakutaka kuongeza neno alichepua mwendo kuwahi ofisini, alijisikia vibaya bosi wake kumkuta eneo lile badala ya ofisini. Lakini alipanga kujitetea alikuwa akimuuliza kitu mlinzi.

    Mustafa toka akiwa ndani ya gari alishtuka kumuona Sara, baada ya kupaki gari alielekea ofisini na kupokewa na Sara kama ilivyokuwa kawaida na kupeleka vitu ndani.
    Wakati wa kupokelewa alitaka kukataa lakini hakuona sababu ya kukataa, alimuacha apokee lakini alitaka maelezo ya kina atakapomuuliza ili aendelee na kazi lakini kinyume na hapo alipanga kumfukuza kazi kwani tangu aondoke hakukuwa na pengo lolote.Baada ya kutulia kwa muda Sara aliingia ofisini kwa bosi wake akiwa hajiamini na kufika kusimama mbele ya bosi wake. Mustafa aliacha kusoma gazeti la siku ile na kunyanyua uso wake kumtazama.

    "Shikamoo," Sara alimuamkia kwa kupiga magoti.
    Ilikuwa mara ya kwanza Sara kumuamkia kwa heshima vile jambo ambalo hakuwahi kulifanya siku za nyuma. Mustafa alijikuta akimshangaa Sara kwa kitendo kile, wakati huo Sara alishtuka 

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kuona aliyekaa mbele yake si bosi bali nguruwe. Alituliza macho ili kupata uhakika.Hakukuwa na mabadiliko zaidi ya kuona nguruwe amesimama kwenye kiti cha bosi wake akichezesha pua. Alikaza macho kuangalia kama alichokiona ni kweli au maruweruwe. Bado hali ilibakia ileile ya kumuona nguruwe mbele yake, alipekecha macho ili kuikataa hali ile kwa kuamini yale yalikuwa maruweruwe kama yaliyomtokea jana yake.



    Aliamini yule ni nguruwe kweli wala si bosi wake baada ya kutoka mlio wa nguruwe ambao ulimfanya apige kelele za woga.

    “Mamaa nakufa!”

    Alishangaa nguruwe yule kuzungumza kwa sauti ya kibinadamu:

    “Sasa unaogopa nini wakati ulifunga safari kunitafuta mpaka Dodoma, nimekuja unapiga kelele.”

    “Ha..hapana..hapana,” Sara alikataa huku akitikisa kichwa.

    “Mimi muongo hujatoka nyumbani kwako kunifuata unilete ofisini?”

    “Ha..ha..hapana,” Sara kwa woga haja ndogo ilimtoka bila kujijua.

    “Saraaaa!” Sauti kali ya Mustafa ilimshtua.

    Hakuitika alishika mikono masikioni kuzuia sauti ya nguruwe, alishangaa kumuona bosi wake akiwa amesimama mbele yake huku akimshangaa.

    “Sara nini?” alimuuliza kwa sauti kubwa baada ya kushindwa kumuelewa.

    “Nakufa bosi,” alisema huku pumzi zikimtoka kama alikuwa akikimbizwa na simba.

    “Sara kipi kinakuua?”

    “Mungu wangu nakufa..nakufa mimi,” Sara alisema huku akikaa chini baada ya nguvu kumuishia na kuhema kwa nguvu.

    Mustafa alizunguka meza na kumsogelea Sara aliyekuwa amekaa chini, alimshika kichwani na kumuuliza kwa sauti ya upole.

    “Sara una nini?”

    Sara pumzi zilikuwa zimemjaa na kushindwa kuzungumza, alijiuliza amekumbwa na nini kwa vile kitu kama kile kilikuwa hakijawahi kumtokea. Sara alikuwa akitetemeka na jasho kumtoka kitu kilichozidi kumtia kwenye wakati mgumu Mustafa kwa kuamini angesema angejua tatizo lake.

    Akiwa katika kizungumkuti asijue nini kimemtokea Sara ambaye aliendelea kuhema huku macho kayatoa pima. Mlango uligongwa na kumfanya ahamishe macho yake kuelekea mlangoni bila kuitikia. Mlango uligongwa tena hakutaka kumkaribisha mtu ndani kutokana na hali ya Sara ilivyokuwa aliamua kusogea mlangoni.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alikwenda hadi mlangoni na kufungua, alijikuta akikutana uso kwa uso na Shehna.

    “Ha! Karibu!”

    “Mbona umeshtuka?”

    “Sikutegemea kukuona.”

    “Kwa nini unasema hivyo au kuna muda uliopanga mimi kuja hapa.”

    “Walaa, karibu.”

    “Asante.”

    Sauti ya Shehna ilimshtua Sara ambaye mapigo ya moyo yaliyoanza kupoa, yalianza upya tena kwa kasi kubwa. Alijiuliza nini hatima yake kama kweli ni jini na kama ndiye aliyekuwa akimfanyia mchezo ule nini atamfanya. Alitamani kumuomba msamaha lakini alijiuliza ataanzia wapi ikiwa hana uhakika yale yalikuwa mawazo yake tu.

    Shehna aliingia ndani ya ofisi na kushtuka kumuona Sara amekaa chini.

    “Mustafa! Shoga yangu kafanya nini tena?”

    “Yaani nashangaa ameingia ofisini tu na kuanza kupiga kelele.”

    ”Kelele! Kipi kimemtisha?”

    Sara alijikuta njia panda kutokana na maneno ya Shehna yalimshangaza na kuona kama mawazo yake ni tofauti na alivyokuwa akifikiria.

    “Ha...halafu si ulisema alisafiri amerudi lini?”

    “Ulinisikia vibaya nilisema haonekani ofisini sikujua amekwenda wapi.”

    “Sasa nini kimemsibu?”

    “Hata najua? Namuuliza amegeuka bubu, yaani nachanganyikiwa.”

    “Sasa kipi kimemsibu jamani shoga yangu?” Shehna alisema huku akimsogelea na kumuinamia Sara.

    “Eti Sara umepatwa na nini?”

    Sara bado mdomo ulikuwa mzito kwa vile mapigo ya moyo bado yalikuwa juu.

    “Mustafa niletee maji ya baridi niwekee kwenye glasi.”









    Ofisini walibakia Mustafa na Sara aliyekuwa amesimama.

    "Kaa," Mustafa alimwambia Sara.

    Sara alikaa kwenye kiti, Mustafa aliendelea kusimama.

    "Sara," alimwita."

    "Abee."


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Una tatizo gani?"

    Sara ilibidi amueleze mkasa mzima kuanzia siku aliyotoka kwenda kununua nyama ya nguruwe. Lakini alificha kufuata nyama ya nguruwe na kusema alifuata chakula cha usiku na yaliyomtokea na vituko vilivyokuwa vikimtokea toka siku aliyofika nyumbani na ofisini.

    "Sara mbona unafanya utani."

    "Kweli bosi, siwezi kusema uongo."

    "Kwa hiyo hata hapa ilitokea?"

    "Kule ilikuwa tisa kumi hapa mpaka sauti katoa."

    "Mmh! Itakuwa nini? Hebu ngoja," Mustafa alisema huku akielekea mlangoni na kuufungua kisha aliita.

    "Shehna njoo."

    "Vipi mmemalizana?"

    "Hebu njoo mara moja."

    Shehna aliingia ofisini na kusimama pembeni ya Mustafa ili kusikiliza alichoitiwa.

    "Unasemaje?"

    Alimweleza yote yaliyomtokea Sara, baada ya kumsikiliza alisema.

    "Mmh! Pole, lakini maji aliyokunywa yatamsaidia haitamtokea hali ile tena."

    "Kwa hiyo aendelee na kazi au akapumzike?"

    "Mwache akapumzike ili kesho aanze kazi vizuri."

    Mustafa alimpa ruhusa Sara akapumzike ili kesho aende kazini, Sara alishukuru na kuondoka na kutaka kutoka lakini alikumbuka alichafua chini kwa haja ndogo baada kumtoka bila kujijua kutokana na hofu ya maruweruwe.

    Alikwenda msalani kuchukua Mop kwa ajili ya kufanya usafi, alipoingia Shehna alimuwahi na kumwambia.

    "Shoga kapumzike nitakusaidia mimi."

    "Acha tu dada."

    "Hapana kapumzike."

    Sara alikubaliana kumpa Mop Shehna na kuondoka kuelekea nyumbani, lakini Shehna alimwambia Mustafa.

    "Mustafa mpeleke Sara, ukirudi utakuta nimemaliza kufanya usafi."

    "Sawa."

    Mustafa alitoka kumpeleka Sara nyumbani na kumpa nafasi Shehna kufanya usafi. Baada ya kuondoka tu Shehna aliwaita vijakazi wake ambao walianza mara moja kazi ya usafi.

    Mustafa alimpeleka Sara mpaka nyumbani na kumuacha kisha alirudi nyumbani na kumkuta Shehna kaisha maliza kazi ya usafi. Baada ya kuachwa Sara aliingia chumbani kwake na kujikuta akianguka kilio kutokana na matukio yaliyokuwa yakimuandama kila kukicha.

    Katikati ya kilio aliisikia tena sauti aliyoisikia wakati alipomuona nguruwe ofisini kwa bosi wake.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kulia siyo dawa zaidi kuacha kuyafuata mambo yasiyo kuhusu la sivyo utageuka nguruwe kabisa."

    Sauti ile ilimfanya anyamaze na kujiuliza kitu gani ambacho amekuwa akikifuatilia zaidi ya kutaka kumjua Shehna ambaye kwa jinsi alivyomuona na upole wake aliamini si jini bali kiumbe cha kawaida tena mwenye upendo tofauti na alivyomfikiria. Hakuamini mwanamke mrembo kukubali kusafisha haja yake ndogo.

    Lakini alimuhakikishia hali ya kumtisha haitamrudia tena, haikuwa kama alivyomwambia na kusikia sauti ile. Akiwa hajapata jibu simu yake iliita, namba ilikuwa ngeni. Alipokea na kuzungumza.

    "Haloo."

    "Sara umefika salama?" sauti haikuwa ngeni lakini hakuwa na uhakika nayo ilibidi aulize.

    "Nani?"

    "Mi shogayo Shehna."

    "Aah! Dada nimefika salama."

    "Ile hali haijatokea?"

    "Ndi..ndiyo."

    "Mbona kama una wasiwasi?"


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ni kweli kuna sauti naisika kwa mara ya pili lakini siielewi."

    "Inasemaje?"




    ITAENDELEA  

0 comments:

Post a Comment

Blog