Search This Blog

BABA KIUMBE WA AJABU - 1

 







    IMEANDIKWA NA : ALLY MBETU



    *********************************************************************************





    Simulizi : Baba Kiumbe Wa Ajabu
    Sehemu Ya Kwanza (1)


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Katika dunia ya Mungu kuna mambo mengi ambayo ukihadithiwa unaweza kudhani ni simulizi za kutunga na za kusisimua. Lakini siku zote kila aisifiaye mvua basi ujue imemnyea. Dunia imezungukwa na siri nzito ndani ya majumba ya watu, kuna mambo mazito ambayo ni chukizo kwa Muumba.
    Si kila mwenye maisha mazuri au tajiri mali alizonazo kazipata kihalali. Wengi utajiri wao unatokana na nguvu za giza, utajiri anaoambatana na kutoa kafara ya kitu. Wapo wanaotoa kafara watoto, wake au waume zao, pia wapo wanaowageuza watoto, wake au waume zao kuwa mandondocha kama ‘chuma ulete’ wa kuwaongezea kipato.
    Nyumba nyingi huwa na vyumba vya siri ambavyo huwa havifunguliwi kutokana na masharti ya mganga na kufanya watu wabaki na maswali. Pia nyumba nyingine unakuta kuna mtoto ambaye akili zake si nzuri, akikaa yupoyupo tu, mate yanamtoka ovyo kumbe ni dawa ya utajiri. Ajabu huyo ndiye anakuwa kipenzi cha baba ambaye anajua siri yake.




    Wapo ambao huambiwa kama mtoto huyo atakufa basi na utajiri nao utayeyuka, ni mambo mengi yaliyoizunguka jamii na uchafu wa tamaa za watu kutaka utajiri kwa njia ya mkato na kujikuta wakifanya uchafu au ukatili mkubwa bila kuwa na huruma ilimradi wapate utajiri. 
    Nayasema haya nikiwa na uchungu mkubwa baada ya baba yangu kutugeuza chuma ulete sisi wanaye kwa ajili ya kumuingizia pesa bila kujua. Nayasema haya baada ya kuteseka zaidi ya miaka saba bila kujua kumbe mateso yangu ndiyo yalikuwa chachu ya utajiri wa familia yangu. 
    Tangu nilipoanza kupata matatizo yaliyosababisha mateso kila kukicha, hata siku moja sikuruhusiwa kwenda hospitali zaidi ya kutumia dawa za kienyeji zilizokuwa zinapunguza maumivu na si kuniponesha.
    Miaka saba nyuma, tatizo kama langu alikuwa nalo dada yangu ambaye nilimfuata mara ya nne ambaye sasa hivi ni marehemu. Mwanzo nilipomuona dada nilijua ni kidonda cha kawaida  japo kilinishangaza kuchukua muda mrefu tangu nikiwa na miaka sita mpaka nilipokuwa na utambuzi kujua kuwa dada yangu anateseka na kidonda kile ambacho kilikuwa hakiponi.
    Miaka mitatu baadaye nilisikia ugomvi mkubwa kati ya baba na dada, nilijificha na kumsikia dada akisema:
    “Nimechoka! Siwezi kuteseka wakati wenzangu wanafaidi kwa mateso yangu, siolewi sina maisha mazuri kama wenzangu niponipo tu. Haya maisha mpaka lini? Nasema sasa hivi naondoka na hili sasa mtafutie mwingine, nakwenda kuishi maisha yangu, kama pesa nimekuingizia sana naomba niondoke.”
    “Monika mwanangu, kuondoka kwako kutaharibu kila kitu.”
    “Baba acha viharibike, nimechoka.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Mwanangu unajua kabisa dawa hii haitaki uchafu, ukikutana na mwanaume tu umeharibu kila kitu.”
    “Ndiyo maana nimekwambia tafuta wengine, baba wewe ni kiumbe gani usiye na huruma. Miaka yote nateseka peke yangu wakati wengine wanafaidi, watu wana majumba wana magari ya kifahari lakini mimi bado naishi maisha duni, kuna faida gani kuendelea kuteseka.”
    “Basi nipe muda nivifanyie kazi.”
    ”Sina muda huo nimechoka.”
    Kwa kweli kutokana na uchanga wangu wa akili, sikujua baba na dada walikuwa wanabishana nini, pia nilijiuliza dada ana mateso gani ambayo anamlalamikia baba. Lakini baada na mimi kunikuta nilielewa dada alikuwa akimaanisha nini. Maisha tuliyokuwa tukiishi yalikuwa ya ajabu sana, kwa sisi tuliokuwa tukiishi nyumbani tuliishi maisha ya dhiki sana tofauti na utajiri mkubwa tuliokuwa nao.
    Tulikuwa na majumba kila kona ya Jiji la Mwanza, pia tulikuwa na mashine za kusaga na kukoboa ambazo ziliingiza pesa nyingi sana. Kaka zangu na dada zangu wote kila mmoja alikuwa na duka kubwa, gari na majumba makubwa. Lakini sisi tuliobakia maisha yetu hayakulingana na utajiri wa baba yetu.
    Kitu kingine wakati ule kilichonishangaza ni hali ya mama, pamoja na kuwa na utajiri mkubwa kama ule, kila siku mama alikuwa akiamka asubuhi na kwenda shamba ambako alilima mpaka jioni na kurudi nyumbani. Kila mama aliporudi nyumbani alikuwa akirudi na kuni ambazo alipikia katika jiko la mafiga. 
    Kwa vile mwanzo zilikuwa akili za kitoto sikuelewa nini kinaendelea wala wakati huo sikujua faida ya utajiri tuliokuwa nao. Kitu kingine ambacho sikukielewa muda ule kilikuwa ni nyumba tuliyokuwa tukiishi. Ilikuwa ni ya zamani ambayo baba aliinunua wakati anaanza maisha. 
    Lakini haikuwa na mabadiliko yoyote pamoja na mabadiliko ya kimaisha kwa baba kuwa na pesa kama mchanga. Dada baada ya kubishana na baba alikaa kwa wiki mbili.
     Siku moja niliporudi sikumkuta, alikuwa ameamua kuondoka, sikujua amehamia wapi. Lakini baada ya siku tatu nilipata taarifa kuwa dada amehamia Mkuyuni ambako alikuwa amepanga na kufungua duka lake. Kuondoka kwa dada kulifanya nyumba igeuke kama pametokea msiba, kitu ambacho kilinishangaza sana.
    Kuondoka kwa dada hakukuwa kitu cha ajabu kwa vile dada na kaka zangu wote walipotaka kuanza maisha yao waliondoka lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote. Baba alionekana kukosa raha, mama naye muda mwingi mkono ulikuwa shavuni. Kitu kile kwa kweli kilinishangaza sana.
                                                              ****
    Nakumbuka siku moja ndugu wote walikutana nyumbani kasoro dada Monika na kuwa na kikao kizito, cha ajabu mimi nilitolewa nje hivyo kilichoendelea sikujua kwa vile nilibaguliwa kutokana na kuonekana mdogo nisiye na mchango wowote. 
    Baada ya kikao kilichochukua zaidi ya saa nne, ndugu zangu waliondoka.
    Kuondoka kwao kidogo kulifanya baba achangamke bila kujua walikuwa wamezungumza nini na nini chanzo cha wazazi wangu kuwa katika hali ya majonzi.
     Nilijiuliza ilikuwa ni dada kuondoka au kulikuwa na jambo kubwa zaidi, katika akili yangu nilifikiria kuna umuhimu wa kumtafuta dada Monika ili nijue kwa nini ameondoka nyumbani na vilevile ni mateso gani aliyoyapata. Kuna kitu kimoja ambacho kilikuwa kikinishangaza tangu nilipopata akili. Kilikuwa ni donda la mguu la dada ambalo lilikuwepo kila siku na wala halikupata dawa ya kuliponesha.
    Nilijikuta nikipata hamu ya kutaka kujua kwa nini dada aliyasema yale maneno ambayo yalionesha machungu kwa kuonekana akizuiwa nyumbani asiondoke lakini wengine wote waliruhusiwa. Kingine kilichoacha maswali kichwani mwangu ambacho kilikuwa hakijakomaa akilini ni hali ya dada kuonekana kama hajaliwi na baba tofauti na ndugu zangu tokea kwenye elimu mpaka maisha ya kawaida.
    Wote walikuwa na maisha mazuri kasoro yeye, lakini sikutaka kujua zaidi kwa vile nilikuwa mtoto mdogo nisiye na uwezo wa kuhoji jambo. Nilipeleleza anapokaa dada, mama alinieleza anakaa pembeni ya Soko la Mkuyuni, duka lake linatazamana na soko. Siku moja baada ya kutoka shule nilipitia moja kwa moja hadi kwa dada.
    Kufika kwake sikupotea, nilifika bila tatizo kutokana na duka lake kuonekana, pia ndilo lililokuwa  kubwa. Nilipofika dukani, dada aliponiona alifurahi sana.
    “Karibu mdogo wangu.”
    “Asante.”
    “Umekuja na nani?”
    “Peke yangu.”
    “Umepajuaje hapa?” Dada alinishangaa.
    “Amenielekeza mama, sehemu yenyewe si ya kupotea.”
    “Ni sehemu nyeupe, karibu mdogo wangu.”
    “Asante”
    “Nyumbani hawajambo?”
    “Hawajambo, mama anakusalimia.”
    “Baba anajua umekuja huku?”
    “Walaaa”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Karibu soda upoze koo,” alisema dada huku akinifungulia soda.
    Nilipokea soda na kuanza kunywa, wakati huo dada alikuwa akihudumia wateja waliokuwa wakinunua bidhaa dukani kwake, baada ya kumaliza kuwauzia alinigeukia.
    “Mmh! Habari za shule?”
    “Nzuri tu dada.”
    “Umetumwa au?”
    “Dada siji kwako mpaka nitumwe?”
    “Siwajahi kukuona ndiyo maana nashangaa, ni muda gani toka niondoke nyumbani. Najua wote mlinichukia kwa kujua nataka kuwanyang’anya utajiri wenu.”
    “Dada mimi sijui chochote zaidi ya baba kukukatalia na kuondoka kwa nguvu, zaidi ya hapo sijui lolote. Na mimi nikukasirikie kwa sababu gani wakati kuondoka kwako kumekuwa mateso na simanzi kwangu kama kuna uwezekano nije nikae kwako.”
    “Najua mdogo wangu unanipenda, lakini baba yako hatakubali, ataona nataka kuuhamisha ukoo mzima.”
    “Kwani dada kuna nini, mbona mazungumzo yako yamejaa uchungu?”
    “Si wenzako wamekuja hapa bila aibu wala huruma na kuzungumza maneno ya kipuuzi,” dada alisema kwa sauti yenye kuonesha huzuni kidogo.
    “Tena kweli dada kuna siku kulikuwa na kikao wote walikuwepo kasoro wewe, kwa nini hukuja?”
    “Kikao hicho kilikuwa cha kunijadili mimi.”
    “Wewe! Umefanya nini?”
    “Unajua mdogo wangu wewe bado unakua, lakini kuna mambo ambayo sitaki yakutokee kama yaliyonitokea mimi.”
    “Mambo gani?”
    “Sasa hivi Masalu unazidi kukua na kupata ufahamu, kidato cha tatu ni upevuko wa akili.”
    “Ni kweli dada.”
    “Unajua kwa nini nimehama nyumbani?”
    “Mmh, sijui.”
    “Masalu sasa hivi una akili unajua zuri na baya.”
    “Ni kweli dada.”
    “Hivi maisha yangu ni sawa na ndugu wengine?”
    “Kivipi?”
    “Nina nyumba?”
    “Hapana”
    “Nina gari?”
    “Hapana”
    “Nina mtoto?”
    “Unajua ni kwa nini?”
    “Sijui.”
     “Hivi maisha tunayoishi ni sawasawa na utajiri wetu?”
    “Hapana


    “Hujiulizi kwa nini wengine wanafurahia maisha, wanakula chakula kizuri wanalala pazuri wanatembelea magari ya kifahari wewe na mimi tunateseka wakati baba na mama yetu ni mmoja.”
    ”Huwa najiuliza, nikienda kwa kina kaka au dada nakula chakula kizuri hata kulala sehemu nzuri tofauti na kwetu.”
    “Hivi uwezo wa baba bado mama anaweza kulima tena kwa mkono na kuokota kuni kuja kupikia?”
    “Dada hata mimi nachanganyikiwa.”
    “Na wewe bila mimi kukuongeza pesa ungenunua hata chungwa ukienda shule?”
    “Yaani dada toka uondoke napewa nauli ya daladala tu, tena pesa ya mwanafunzi shilingi mia.”
    “Unaona sasa, hebu subiri,” dada alisema huku akimsogelea mteja kumuuzia kitu.
    “Na donda lililokuwa mguuni kwangu uliliona kwa muda gani?”
    “Mmh, muda mrefu sana.”
    “Unaliona tena?” Dada alinionesha sehemu iliyokuwa na donda ambayo ilikuwa imepona na kuweka alama nyeusi.
    “Ha! Dada umepona?”
    “Nimepona mdogo wangu, lakini utajiri umeingia ufa”
    “Ufa! Una maana gani?”
    “Donda langu ndilo chanzo cha utajiri.”
    “Unasema!” Kauli ya dada ilinishtua.
    “Masalu utajiri wetu una siri nzito.”
    “Siri! Siri gani hiyo?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Masalu utajiri wetu una siri nzito ambayo mimi ndiye niliyeibeba na sasa hivi nimeitua.”
    “Una maana gani kusema hivyo?”
    “Masalu kuna mambo huwezi kuyajua kutokana na umri wako, lakini kutokana na ukaribu na kuelewana kwetu sina budi kukufunulia yaliyojificha ili ujue nini kimetuzunguka. Mwanzo nisingeweza kukuambia kwa vile nimeelezwa kuwa maisha yangu hayatakuwa marefu hivyo leo nimefurahi sana kuja hapa. Haya nitakayokueleza leo si ya kutunga na kila ulilokuwa na swali nalo leo nitakupa jibu lake.
    “Masalu mdogo wangu maisha yetu kabla hujazaliwa yalikuwa ya kawaida tu, baada ya baba kustaafu kazi pesa alizolipwa alinunua nyumba mnayoishi sasa hivi na pick up moja ambayo alifanyia kazi zake za kutuingizia kipato na kufungua duka ambalo lilikuwepo muda mrefu toka nikiwa darasa la nne.
    “Maisha yaliendelea kama kawaida huku tukionekana familia yenye uwezo kwa sisi wote kusoma elimu nzuri. Walionitangulia wote walisoma elimu ya sekondari, lakini mimi nilipomaliza darasa la saba sikuweza kuchaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza. 
    “Lakini niliamini ningeendelea kusoma shule ya kulipia kama ndugu zangu walionitangulia. Wakati tukifanya taratibu za kunichukulia fomu ya kuanza kidato cha kwanza, siku moja nikiwa natoka chooni usiku kuna kitu kilinigonga mguuni. Nilipiga kelele kuomba msaada.
    “Baba na mama walitoka na kuja nilipokuwa nimeshika mguu huku nikirukaruka, lakini ajabu hakukuonekana kitu chochote cha kuwashtua kutokana na nilivyokuwa. Nikiwa na wasiwasi labda nimegongwa na nyoka baba alinipa dawa ya maumivu na kunieleza patapoa tu.
    “Usiku nililala vizuri, lakini asubuhi nilipoamka nilikuta mguu umevimba hata kutembea sikuweza. Sehemu ya juu kidogo ya mguu wa kulia kwa ndani kuliweka alama nyeusi, sikupelekwa hospitali zaidi ya kukandwa na dawa ya majani. Basi mdogo wangu mguu huo umenisumbua kwa muda mrefu bila kupelekwa hospitali.
    “Hata muda wa kwenda shule ulipofika sikuweza kupelekwa shule kutokana na hali ya mguu wangu. Mpaka kipindi cha uandikishaji wanafunzi kinakwisha bado hali yangu ilikuwa tete hivyo sikuweza kujiunga na sekondari. Roho iliniuma rafiki zangu wengi walianza kidato cha kwanza. Nikawa mimi na ndani ndani na mimi, sehemu iliyokuwa na weusi ilikuwa ikiwasha na mwisho iliweka kidonda.
    “Ajabu baada ya kutoka kidonda, mguu ulirudi katika hali yake ya kawaida, hata mti niliokuwa natembelea niliutupa. Niliona kama muujiza mguu wangu kurudi katika hali yake, niliamini mguu wangu ulikuwa wa kukatwa tu baada ya wazazi wangu kutoonesha juhudi zozote za kunipeleka hospitali.
    “Hata nilipoweza kutembea sikuruhusiwa kutoka nje kama wenzangu, maisha yangu yalikuwa ya uani, kidonda changu kila siku kilikuwa kikivuja maji. Mdogo wangu wakati huo sikujua kama kidonda kile kilikuwa na sababu yake. Hali ya  maisha nayo ilibadilika, kulitokea mabadiliko makubwa sana.
    “Kwa muda mfupi tulinunua magari, kuongeza majumba kila kona ya Jiji la Mwanza na miradi mingi, ndugu zangu walifunguliwa maduka makubwa Mwanza mjini na mimi kukabidhiwa duka la pale nyumbani ambalo liliongezwa vitu vingi. Naimani mpaka unapata ufahamu ulinikuta dada yako nina kidonda mguuni.
    “Siku zote nilihoji kwa nini wazazi wangu hawataki kunipeleka hospitali au kuniwekea dawa. Baba alinieleza kuwa kama wataniwekea dawa ya aina yoyote kidonda mguu utaoza, akaniambia kitapona chenyewe, nami nilikubali mwanzo bila kujua mwisho wake utakuwa nini. 
    “Pia nilipewa masharti ya kutotembea na mwanaume, nikaambiwa nikifanya hivyo nitakufa. Kwa vile umri wangu ulikuwa mdogo usiotakiwa kujiingiza katika mapenzi halikunisumbua sana. Siku zilizidi kukatika huku maisha yakibadilika kila siku, nami nilivunja ungo wa kuwa na hamu ya wanaume. 
    “Katika wateja wangu kuna kijana mmoja ambaye kwa kweli tulipendana naye sana na kunitamkia kuwa anataka kunioa si kunichezea baada ya kumueleza simjui mwanaume. Nilimueleza mama ambaye alinikemea sana kuwa nisirudie tena kusema kitu kama kile nitaweza kukorofishana na baba.
    “Kutokana na kumuogopa baba niliamua kukaa kimya, siku zilikatika huku utajiri wa baba ukizidi kuwa wa kutisha na ndugu zangu wote wakinunua magari ya kifahari na kujenga maghorofa. Kila nilipotaka na mimi kuhama nyumbani na kuanzisha duka langu, kununua gari zuri na nyumba ya kifahari kama wenzangu nilizuiwa.
    “Ajabu nilikaripiwa sana tena eti nisirudie tena kusema hivyo, majibu ya mama yalinishtua sana na kujiuliza iweje wote wawe na maisha mazuri kasoro mimi? Nilijiuliza labda mimi si mtoto wa mzee Makumiyane, lakini mama alinihakikishia ni mtoto halali wa mzee Makumiyane.
    “Na hilo niliamua kuliacha kutokana na kumuogopa sana baba, muda ulivyokuwa ukienda ndugu zetu wote waliondoka na kuanzisha maisha yao na kubakia sisi wawili na wazazi wetu. Roho iliniuma sana siku ndugu zangu walipokuja kututembelea, kila mmoja alikuja na gari la kifahari. Hiyo ilikuwa tisa, kumi ilikuwa harusi za ndugu zangu ambazo ziliniumiza roho na baada ya muda walipata watoto.
    “Nilijikuta nikijitoa mhanga na kumfuata baba kumuomba haki yangu kama wenzangu, baba alinigombeza kama ilivyokuwa kawaida yake. Lakini nilimueleza kuwa kama hataki basi kuna siku nitatoroka na kwenda kuanzisha maisha yangu kutokana na yeye kutoonesha kunijali au kunipa haki sawa na wenzangu.
    “Alinitisha kama nitajaribu kutoka nyumbani nitamtambua, vitisho vyake havikunibabaisha baada ya kuona sina faida ya kuwepo pale eti kisingizio nina duka. Siku iliyofuata nilibeba kila kilicho changu na kuondoka, mama alinibembeleza nisiondoke lakini sikubadili uamuzi wangu. Ilibidi akimbiliwe baba alipokuja alishangaa uamuzi wangu. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
     “Nilimueleza nipo tayari kwa lolote atakalotaka kunifanyia, msimamo wangu ulimtisha sana baba na kuamua kuniweka chini na kunieleza siri iliyoniacha mdomo wazi.
    “Nikabakia mimi siolewi, sina maisha mazuri, sina mtoto. Sikuwa na jinsi zaidi ya kuvumilia. Nakumbuka siku moja kijana ambaye alitaka kunioa alikuja na kuniulizia ombi lake, siku ile baba na mama walikuwa wamekwenda kwenye sherehe ya mtoto wa dada aliyekuwa akipata ubatizo.
    “Siku ile mdogo wangu lazima niseme ukweli kwa vile sina jinsi, nilitoka na kwenda kwa yule kijana na nilifanya naye mapenzi. Kwa kweli penzi nililopata lilinichanganya nikawa sisikii wala sioni. Ilifikia wakati wa kutoroka usiku kwa kuruka ukuta na kwenda kwa yule bwana.
    “Mchezo ulinichanganya sana hata kutamani kuhama nyumbani.
    “Kumbe kufanya kwangu mapenzi kulikuwa kunasababisha matatizo katika familia, kwa wiki moja kulitokea mambo ya kutisha. Moja nyumba ya Malimi iliungua moto na hakuna kilichosalimika, kabla hatujatulia gari la kaka lilipata ajali mbaya iliyosababisha lisirudi tena barabarani.
    “Baba naye alivamiwa na majambazi akipeleka pesa benki za mauzo ya mwezi mzima. Hali ile ilimchanganya baba na kwenda kwa mganga wake kuulizia sababu ya majanga yale. Jibu aliambiwa mali imeingia uchafu kwa mimi kufanya mapenzi.
    “Baba alikuja juu na kunitishia, nami sikumuogopa nilimueleza ukweli kama mimi ndiye chanzo cha utajiri kwa nini niwe na maisha duni wakati watu wasiojua adha niipatayo kutokana na mali wanazochezea kuishi maisha mazuri. Nilimueleza baba kuwa kama hatanipa mali tena iwe zaidi ya ndugu zangu wote lazima nitaondoka na kwenda kuishi maisha yangu.
    “Baba alinitisha kwa kusema kama nitaondoka sitakaa muda mrefu lazima nitakufa, vitisho vile sikuviogopa na kumhakikishia kuwa nitaendelea na msimamo wangu na nipo tayari kufa lakini si kuwa kitega uchumi cha watu. Mama naye aliingia kwenye kazi ya kunibembeleza ili nibadili tabia zangu zilizoonekana chafu.
    “Nilikubali kubaki nyumbani kwa masharti na mimi natakiwa niwe na gari na duka kubwa ambalo nitalimiliki mwenyewe. Tulikubaliana na mimi kufuta wazo la kuondoka nyumbani. Nilisubiri kutekelezewa niliyoyataka kwa hamu kubwa, nami nilikuwa na hamu ya kuendesha gari, nilikuwa na hamu ya kumiliki mali yangu mwenyewe.
    “Siku zilikatika bila kuona dalili zozote za kununuliwa gari wala nyumba, wakati huo nilikuwa nimesimamisha mapenzi na shemeji yako. Mambo yalizidi kunyooka kwa  Malimi aliyeunguliwa nyumba yake kujenga ghorofa analoishi sasa.
    “Lakini mwenyewe sikuona kitu chochote, kila nilipouliza niliambiwa nisubiri mambo hayajakaa vizuri. Mambo hayajakaa vizuri wakati ndugu zangu kila kukicha  walibadilika kimaisha? Niliona kama wananichezea, nikaanza kuweka pesa zangu taratibu bila kumshirikisha mtu.
    “Shemeji yako nilimtuma anitafutie sehemu ya kufungulia duka akapata huku, nilimpa pesa za kulipia mwaka mzima na kumuagiza anunue vitu vyote muhimu kwa ajili ya duka naye alifanya kama nilivyomuagiza. Unajua Masalu katika maisha yangu huwezi kuamini toka nipatwe na tatizo la mguu lililozaa kidonda sikuruhusiwa kwenda kanisani.
    “Ndugu zangu wote ndiyo waliokuwa wakienda kanisani, lakini mimi nilizuiwa kwa kuambiwa kama nitakwenda kanisani nitasababisha maafa makubwa kuliko yale ya kutembea na mwanaume. Nilijiuliza mimi ndiye sitakiwi kwenda kanisani lakini wadogo na dada zangu wote mlikuwa mnakwenda, kwa nini?
    “Nilikatazwa hata kusoma Biblia, baba alisema mizimu haitaki kuchanganya mambo ya Mungu na mizimu. Basi nilibakia simjui Mungu wala kanisa. Baada ya kukamilisha vitu vyote muhimu vya dukani, shemeji yako alilisifia duka alivyolijaza. Nilijipanga kwa siri na siku moja nilitoroka usiku na nguo zangu bila wao kujua. Masalu siku mlipoamka na kunikosa ilikuwaje nyumbani?” Dada Monika aliniuliza huku akiwa ametuliza macho usoni kwangu.
    “Mmh, kwa kweli walichanganyikiwa sana, walihaha kila kona, familia yote iliitwa asubuhi ile na kukutana. Hata mimi nilizuiwa kwenda shule, kilikuwa kikao kizito kilichokujadili. Niliwasikia wakisema bila kukuona kila kitu kitaharibika, siku ile hakuna kazi iliyofanyika, maduka yote yalifungwa na kuanza kukutafuta.”
    “Basi mdogo wangu nilikuja huku kuanza maisha yangu ili kupata uhuru wa maisha wa kupanga mambo yangu bila kuingiliwa na mtu. Pesa niliyokusanya niliamini mpaka iishe nitakuwa nimepiga hatua kubwa katika biashara kwa vile nilikuwa naijua vizuri.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Walianza upelelezi wa chinichini na kumjua mpenzi wangu ambaye walimbana kwa kumpeleka polisi ili awajulishe nilipo. Mwanzo aligoma kutokana na masharti niliyompa kama wazazi wangu watamuona asikubali. Mpango wetu ulikuwa kuishi pamoja nami nilitaka yeye asirudi tena kule.
    “Lakini kwa vile familia yake ipo kule walifanikiwa kumpata na baada ya kumbana sana aliwaleta hapa. Kama utakumbuka siku waliyokusanyana kuja kwangu ilikuwa baada ya kumtuma mtu kwa siri bila kujua ninapofanyia kazi zangu na kuamua kukusanyana kuja hapa ili nikubali kurudi nyumbani.
    “Basi walipofika kila mmoja ooh, Monika umefanya vibaya kuondoka nyumbani wakati unafahamu kila kitu. Niliwaeleza siwezi kuumia mimi wakati wenyewe wanakula maisha, kama hivyo basi kidonda changu achukue mtu mwingine. Hakuna aliyekuwa tayari kuchukua ugonjwa wangu.
    “Nilijua mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu mchungu, mwisho wa yote walikubali niendelee na kazi zangu kwa makubaliano nisitembee na mwanaume au kukitibu kidonda. Niliwakubalia ili kuwaridhisha kuwa nitafanya kama wanavyotaka. Lakini sikuwa tayari kukubaliana na ujinga wao tena.
    “Nami nilikuwa na hamu ya kuwa na mwanaume ambaye muda ule alikuwa akija mara moja na wakati huo ndiyo alikubali kuhamia kwangu kabisa.
    “Baada ya kuondoka niliendelea na mpenzi wangu ambaye muda huo nilikuwa nakaa naye nyumba moja, kupika na kupakua, sasa hivi yupo kwenye mihangaiko yake muda wake wa kurudi ni saa moja usiku. Ila jumapili huwa haendi popote.
    “Tangu nihamie huku siku hizi nakwenda kanisani kama kawaida, ajabu ya Mungu kidonda kilianza kupona chenyewe bila kukiwekea dawa. Kumbe kidonda changu kilivyokuwa kikipona na mambo yalibadilika katika utajiri wa familia yetu. Matatizo yalitawala kwa maduka kuibiwa vitu vyote bila kujua tatizo ni nini.
    “Kama kawaida walirudi kwa mganga na kuelezwa kuwa nimeishapona pia ninaendeleza kufanya uchafu katika mali ya familia yangu. Walijikusanya kama ilivyo kawaida na kuja kuniomba niokoe mali ya familia, niliwaeleza katu sitakubali kufanya tena ujinga ule.
    “Baada ya juhudi zote kushindikana baba aliniapia mwaka huu siumalizi lazima nitakufa. Nilimhakikishia yeye si Mungu, kama kufa nitakufa kwa amri ya Mungu. Wote waliondoka vichwa chini wakiamini wanarudi katika maisha ya kawaida, tokea siku hiyo sijawaona tena na maisha yangu yanaendelea kama kawaida na muda si mrefu nawe utapata mjomba.”
    “Dada una mimba?”
    “Ndiyo mdogo wangu.”
    “Mmh, Mungu mkubwa.” 
    “Basi mdogo wangu siri uliyokuwa huijui ndiyo hiyo, nasikia sasa havi mambo yote hayaendi vizuri kabisa na wamechanganyikiwa.”
    “Ni kweli dada sasa hivi kila siku baba analalamika na kusema angekuwa na uwezo angekuulia mbali.”
    “Sasa aniue kwa sababu gani? Kwa watoto wa mzee Makumiyane ni mimi peke yangu? Niliwaeleza mmoja ajitoe akichukue kidonda change lakini kila mmoja alikaa nyuma kukikimbia kidonda. Basi mdogo wangu nikifa leo ujue nimekufa kwa kukikataa kidonda.


    “Siogopi kufa hata siku moja, kila kiumbe kitakufa! Kama nitakufa kwa kukataa kidonda nipo tayari, ila namuomba Mungu aniue baada ya kumzaa mwanangu ili niache jina langu,” dada alisema huku machozi yakimtoka,  moyo wangu uliingia baridi ya woga wa ajabu kwa yote niliyoelezwa na dada juu ya siri nzito ya utajiri wetu iliyokuwa ikibebwa na kidonda cha dada.
    Kingine kilichonitisha kilikuwa kusikia kuwa dada eti atakufa baada ya kukikataa kidonda. Machozi ya dada yaliniumiza sana moyo wangu na kumuonea huruma.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Dada kwa nini usikubali kuliko kukubali kufa?”
    “Masalu wewe hujui lolote katika maisha, lakini unakumbuka haya niyasemayo  hata kama nikifa leo utayakumbuka maneno yangu. Kwa vile wote wameshazaa na kufanya mapenzi hawawezi kupatwa na kidonda. Wasiwasi wangu kikitoka kwangu kinaweza kurudi kwako.”
    “Ha! Dada mbona unanitisha.”
    “Kutokana na siri ya kidonda niliyoelezewa na baba, nakumbuka nilimuuliza kwa mfano nikifa itakuwaje? Alinieleza itabidi atafutwe aliye safi ndani ya familia. Nilimuuliza tena ni kwa mwanamke tu? Alinijibu ni kwa mtu yoyote mwanamke au mwanaume aliye msafi, unafikiri nani atakayekichukua kidonda changu kama si wewe?”
    “Mimi sikubali.”
    “Masalu huna jeuri ya kumbishia baba.”
    “Nitahamia kwako.”
    “Uhamie wapi nami umesikia lazima nitakufa?”
    “Huwezi kufa dada, ni vitisho.”
    “Hata nisipokufa siwezi kukukubali tena hicho kidonda kisicho na faida zaidi ya mateso.”
                                                                         ****
    Kwa kweli sikuweza kumshawishi dada kutokana na msimamo wake mkali, jioni ilipofika niliagana na dada kwa kupanda daladala mpaka nyumbani. Nilipofika nyumbani nilikuwa na mawazo mengi juu ya maneno ya dada ambayo sikuamini kama yana ukweli wowote, nilipinga kuwa utajiri wetu si kupitia kidonda chake. Nilipoangalia hali ya maisha yetu ilikuwa ya kawaida tofauti na kauli ya dada ya kusema sasa hivi maisha ni magumu upande wa familia.
    Chakula tulikula kama kawaida ambacho kwa kweli hakikuwa na hadhi ya utajiri uliotuzunguka. Lakini kwa muda ule sikushtuka kutokana maisha yale ndiyo yaliyokuwa ya kawaida ya siku zote. Japo kwa mbali nilijawa na maswali iweje nyumbani maisha yetu ya kawaida.
    Kingine ambacho alikisema dada kiliniingia akilini kilikuwa kwa mama kuamka kila siku asubuhi na kwenda kulima wakati baba alikuwa na pesa nyingi. Kingine nilichokubaliana na dada ni mama kuokota kuni na kuja kupikia wakati dada zetu wanatumia majiko ya umeme na gesi.
    Lakini kitu ambacho sikukubaliana naye ni imani za kishirikina kwanza maisha yetu yanategemea ushirikina wa kidonda chake. Katika akili yangu niliamini kidonda cha dada hakikuwa kimepata tiba sahihi. Lakini baada ya kupata tiba sahihi kilipona.  Niliamini dada alitaka kunijengea uadui na wazazi ili niwaone ni watu wabaya wasiofaa.
    Sikutaka kumuamini dada zaidi ya kuona anataka kunipotosha, lakini siri ile nilibaki nayo moyoni sikutaka kumwambia mtu. Siku zilizidi kukatika nami niliendelea na masomo kama kawaida. Pamoja na kuyapuuza ya dada na kuyaona kama ya uchonganishi lakini kuna vitu vilikuwa vikitia wasiwasi. Kuna siku nilimsikia baba akimwambia mama kwa sauti iliyoonesha hawakuniona kutokana na kiza kilichokuwepo.
    “Mama Monika nimempa mpa muda mwanao wa kutosha, litakalotokea tusilaumiane.”
    “Sasa mimi nitafanyaje kama mwenyewe hajihurumii.”
    “Hali ni mbaya tukiendeleza huruma tutaadhirika.”
    “Baba Monika mimi mwenyewe nilikwenda kwa Monika, lakini kiburi kimemjaa tena amekosa hata heshima kujua anazungumza na mama yake.”
    “Mganga amenipa mwezi huu mwisho la sivyo kihame kwa mwingine.”
    “Unafikiri kitaenda kwa nani?”
    “Hilo suala tutalizungumza baada ya kushindikana kabisa.”
    “Yaani Monika kanichanganya sana.”
    “Basi uamuzi ni huo sina mwingine.”
    “Utakavyokuwa mimi tena simo kayataka mwenyewe.”
    Mazungumzo ya baba na mama kumhusu dada Monika yalinishtua sana na kujiuliza baba alikuwa anataka kufanya nini? Nilijiuliza au ndiyo niliyoelezwa na dada Monika juu ya kumlazimisha aendelee kuwa na kidonda na kama kikihama kitaenda kwa nani?” 
    Pia nilijiuliza mama alikuwa na maana gani kusema yakimkuta dada Monika hayumo ni mambo gani hayo. Nilijikuta nikiingiwa na wasiwasi wa maneno ya dada Monika kuwa baba alimtishia maisha kuwa kama akikataa kuendelea kuwa na kidonda hatadumu lazima atakufa.
    Nilijikuta nikikosa raha na kutamani kwenda kumuomba dada akubali kuliko kutokewa na balaa lile. Kwa mbali nilijikuta njia panda kuamini kuwa kidonda cha dada ndicho kilikuwa kikifanya tuwe matajiri. Nilitamani nizungumze na mama kuhusu kujua baba alikusudia kufanya nini kwa dada.
    Japo niliogopa kuulizwa nimejuaje, lakini nilipanga siku ya pili sitakwenda shule na kumfuata mama shambani kumuuliza kuna kitu gani dada Monika anataka kufanyiwa baada ya kukataa kuwa na kidonda kile. Usiku kwangu ulikuwa mzito sana niliota mambo mazito ambayo yalinitisha na kunifanya niamke saa nane za usiku na kukesha bila kulala.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Niliota familia yetu ikifanya sherehe kubwa huku dada Monika akiwa amekufa na mwili wake haukuwa na mguu mmoja uliokuwa ukivuja damu, ule mguu uliokuwa na kidonda. Damu ya dada Monika ndugu zetu walikuwa wakinywa kwa furaha. Niliamka na kukaa kitandani nikitweta. Nilijiuliza ndoto ile ina maana gani.
    Baada ya muda usingizi ulinipitia, muda haukupita niliota ndoto nyingine mbaya, niliota nimeoza mguu sehemu ya ndani na kuanza kutoka funza, ajabu ndugu zangu walifurahia kama ndoto ya mwanzo ya kufurahia kifo cha dada Monika kwa kumla na kunywa damu yake.
                                                                *****
    Nilishituka usingizini na kuogopa kulala tena mpaka asubuhi, asubuhi nilisingizia naumwa. Sikwenda shule, nilitoka ndani na kwenda kulala sebuleni ili kuogopa kuota ndoto za kutisha. Sebuleni nilipolala sikuota ndoto mpaka nilipoamka kujiandaa kwenda kwa mama shamba baada ya kufungua kinywa.
    Nilioga na kufungua kinywa kisha nilielekea shambani kwa mama ili nikamuulize kuna kitu gani dada Monika anataka kufanyiwa na baba, kama kumuua ningepinga kwa nguvu zangu zote.
    Nilikwenda hadi shambani na kumkuta mama akiwa katikati ya kilimo, sikumsemesha kitu, nilijiuliza iweje tuwe na pesa majumba na magari mama ateseke kiasi kile. Nilizidi kuingiwa na wasiwasi juu la mambo yaliyokuwa yakifanyika.
    Baada ya muda nilimwita mama, aliponiona alishtuka na kuniuliza.
    “Masalu kuna usalama?”
    “Upo mama.”
    “Si unaumwa, umekuja huku kufanya nini?”
    ”Kuna kitu nataka kuuliza mama.”
    “Kitu gani?”
    Mama alisema huku akiweka pembeni jembe na kunifuata nilipokuwa nimesimama.
    “Masalu una nini mwanangu?”
    “Mama jana nimeota ndoto mbaya sana.”
    “Ndoto gani mwanangu?”
    “Kuhusu dada Monika.”
    “Monika! Ndoto inahusu nini?”
    Nilimhadithia ndoto niliyoota, mama alishtuka na kutulia kwa muda kisha alisema kwa sauti ya chini.
    “Sasa wewe wasiwasi wako nini?”
    “Mama kuna maneno nilizungumza siku moja na dada Monika kuhusu baba kumtishia kifo na kunieleza kama akifa nijue baba ndiye aliyehusika.”
    “Masalu!” Mama alishtuka.
    “Naam mama.”
    “Mlifikia wapi mpaka mkazungumza hayo?”
    “Kuna siku nilikwenda kwa dada Monika na kumuuliza sababu ya yeye kuhama nyumbani. Mama dada alinieleza mambo mengi ya kutisha sana lakini sikuyaamini.”
    “Masalu alikueleza mambo gani Monika?”
    Nilimuhadithia baadhi ya mambo kisha nilimueleza ya yeye kulima wakati tuna pesa.
    “Eti mama hata kulima kwako amesema ni imani za kishirikina iweje tuwe na pesa wewe ulime wakati ungewalipa watu wakatulimia?”
    “Mmh, mbona makubwa!” Mama alizidi kushangaa.
    Mama alisema huku akitoka shambani na kunisogeza chini ya mwembe.
    “Masalu wewe hayo unayaamini?”
    “Siwezi kuyaamini japo kuna mengine yana ukweli.”
    “Nakuomba asikubaliane na maneno ya Monika ni ya uongo.”
    “Mama mbona baba alisema jana litakalomtokea asilaumiwe, nini kitamtokea dada Monika?”
    “Wee Masalu!” Mama alizidi kushtuka kuona ninajua vitu vingi. 
    Ilionesha mama aliamini siyajui mengi kuhusiana na mambo yaliyokuwa yakitendeka nyumbani. Nilimuona akifuta jasho kwenye paji la uso kisha alinipandisha na kunishusha na kusema.
    “Masalu wewe ni mtoto, hujui kitu hata nikikueleza hutanielewa, nakuomba uachane na hayo, swali hili ungemuuliza baba yako mngekosana.”
    “Mama hujanijibu, jibu si kukosana bali kupata ukweli nilioelezwa na dada Monika juu ya kukataa kwake kidonda na baba kumtishia kuyakatisha maisha yake.”
    “Hilo si kweli, ni ujinga wa dada yako kama kufa atakufa na yake.”
    “Mama, baba aliposema kuwa asilaumiwe na wewe kusema shauri yake alikuwa na maana gani?”
    “Masalu naomba usiniulize swali kama hilo tena,” mama alikuwa mkali.
    Niliona nibadili mada kwa kumuuliza swali lingine.
    “Halafu mama kwa nini tusitafute mtu atulimie na wewe kupumzika, tuna faida gani kuwa na pesa na wewe mama unaendelea kuteseka?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Masalu nakuomba uondoke, nakuona umekosa maneno ya kuzungumza,” mama alikuwa mkali.
    Kila neno nililolisema kwa mama lilimuudhi, sikutaka kuendelea kulumbana naye, niliamua kurudi zangu nyumbani nikiwa bado nipo njia panda. Wazo la haraka lilikuwa kwenda kwa dada Monika kumueleza akubaliane na matakwa ya wazazi ili asije kujutia maisha yake. Nilipofika nyumbani nilijawa na mawazo mengi sana kuhusiana na majibu ya mama.
                                                                *****                                                      
    Nilipanga siku ya pili nitaaga na kwenda shule lakini kituo changu cha kwanza kingekuwa kwa dada Monika kumueleza hali halisi kutokana maneno ya baba. Siku ile sikushinda na furaha kila nilipokumbuka ndoto nilizoota usiku na majibu ya mama.
    Japo niliamini mama hawezi kumueleza baba niliyomuuliza, bado nilikuwa na wasiwasi kama atamueleza basi lazima baba angenishikisha adabu kufuatilia mambo yasiyonihusu. Lakini siku ilikatika bila kuulizwa swali lolote na baba zaidi ya mama kuniita na kunionya nisirudie tena kuuliza mambo yale wala kumueleza mtu yoyote.
    Nilimuahidi mama sitarudia kumueleza mtu maneno yale, kwa furaha ya mama alinipa pesa za kula shule kitu ambacho hakuwahi kukifanya zaidi ya kila siku kunipa nauli tu. Niliamini ile itanisaidia kuongeza nauli ya kwenda kwa dada. Usiku nilipolala ndoto ya jana yake ilijirudia.
    Nilijikuta nikikesha kwa mara nyingine mpaka asubuhi kwa kuogopa kila nilipofumba macho njozi mbaya zilinifuata. Chumba nilikiogopa na kujiuliza njozi zile mbaya za dada Monika kuliwa nyama huku familia yote ikifurahia zilikuwa na maana gani? Kingine kilichonitisha mguu wangu kuoza na kutoa wadudu.
    Nilijikuta nikiogopa kufumba macho na kubaki macho mpaka kunakucha, alfajiri nilisikia habari zilizonishtua sana. Nilimsikia baba akimwambia mama:
    “Aliyoyataka mwanao yametimia.”
    “Unataka kuniambia Monika ame...”
    “Ishia hapohapo na sitaki utoe chozi unajua nini tuliambiwa.”
    Nilishtuka na kutoka nje na kuwakuta baba na mama sebuleni, mama aliponiona alishtuka tofauti na baba.
    “Mama dada Monika kafanya nini?”
    “Kwani umesikia nini?” Baba aliniuliza.
    “Sijui...ame..”
    “Amefanya nini?”
    “A..me..mee,” nilijikuta nikipata kigugumizi.
    “Hebu ondoka hapa asubuhi yote nini kimekuamsha,” baba alinifokea.
    Nilirudi chumbani kwangu nikiwa bado sielewi dada Monika kafanya nini japo bado wasiwasi wangu ulikuwa labda amefariki kutokana na maelezo ya dada Monika na kauli ya baba juu ya dada Monika. Kwa kauli ya baba ambayo aliifunga, niliamini kabisa dada Monika huenda kweli amefariki. Kwa vile muda wa kujiandaa kwenda shule ulikuwa umekaribia nilikwenda kuoga ili nijiandae na shule. 
    Baada ya kuoga nilirudi chumbani kwangu kujiandaa kwenda shule, nikiwa bado nipo katika maandalizi nilishtuka kusikia sauti za ndugu zangu, ujio wao wa asubuhi ile ulinishtua sana.Niijiuliza kuna kitu gani kimetokea au ndiyo niliyokuwa nayafikiria ya kifo cha dada Monika? Sikutaka kutoka haraka, nilimalizia kuvaa nguo za shule, baada ya kuvaa nilitoka ili nijiandae.                                                              
    Nilishtuka kuwaona dada na kaka zangu wamekaa sebuleni, waliponiona walishtuka na kuniuliza:
    “Masalu unakwenda wapi?”
    ”Shule.”
    “Unakwenda shule hujui hapa nyumbani kumetokea nini?”
    ”Sijui.”
    “Mmh, makubwa, Monika amefariki.”
    “Eti?
    “Monika amefariki.”
    “Dada Monika?” Bado sikuamini.
    “Eeeh, huyo huyo.”
    “Siamini …siamini.”
    Bila kujielewa nilijizoa mzimamzima na kujipiga chini na kupoteza fahamu, baada ya huduma ya kwanza nilipata fahamu na kuangua kilio tofauti na wenzangu ambao hakuna hata mtu mmoja aliyemwaga chozi. Juhudi za kunibembeleza zilishindikana. Bila kujielewa nilijikuta nikisema kwa sauti ya juu:
    “Yote uliyonieleza dada yangu nilifikiri utani kumbe kweli wamekuua.”
    “Alikueleza nini?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    ”Baba kwa nini umemuua dada Monika?”
    “Wee Msalu maneno gani hayo?”
    “Maskini dada yangu kumbe ulikuwa na siri nzito moyoni mwako ambayo imenifumbua leo, ungekufa dada yangu bila kujua lakini Mungu mkubwa.”
    “Masalu hebu ondoa uchuro hapa.”
    “Siwezi… siwezi, kwa nini lakini umemuua dada Monika?” Niliendelea kulia kwa uchungu huku nikijipigiza chini.
    “Nani kamuua Monika?”
    “Nyinyi wote kwa tamaa za mali.”
    “Masalu unatukosea adabu.”
    “Siwakosei adabu bali ukweli ni huo.”
    Kaka mkubwa alinichukua na kutoka na mimi uani huku nikiendelea kulia, roho iliniuma kumpoteza kipenzi dada yangu Monika mtu aliyenipenda kuliko yeyote. Kutokuonesha ndugu zangu kuguswa na kifo cha Monika niliamini ndoto niliyoota ilikuwa na maana kubwa. Kama dada Monika wamemla nyama nini maana ya kidonda mguuni kwangu chenye kutoa wadudu?
                                                            ****
    Tulipofika nje kaka alinibembeleza na kunieleza maneno ya busara kuhusiana na kifo cha Monika kuwa kilitokana na uzazi wala hakihusiani na masuala ya ushirikina. Na kutokuonesha kuguswa kila mmoja alikuwa  akililia moyoni kwa vile hakuna aliyetegemea. 
    Kwa vile nilikuwa namheshimu nilimkubalia ili kumridhisha lakini siri ilibakia moyoni mwangu. Wengi walishtuka maneno yangu na kunionya nisiyasikilize ya Monika kwa vile alikuwa ni muongo na mgombanishi, nao nilikubaliana nao ili yaishe.
    Ajabu ya mwaka ambayo baada ya akili ya ufahamu kukomaa niligundua kuna kitu kilitendeka mpaka leo hii sijui. Baada ya taarifa za msiba wa dada Monika ambao  hakuna aliyefunua mdomo wake kulia zaidi  yangu mwenyewe. 
    Taarifa za msiba ule hata majirani hawakujua nyumbani kulitokea msiba. Mwili wa dada ulifuatwa na kurudishwa nyumbani. Gari lililouleta mwili wa dada ilipita mpaka uani. Waliuteremsha na kuuingiza chumbani kisha ndugu wote walitawanyika kwenda kuendelea na kazi zao kama kawaida. Kitu kile kilinishtua iweje kuwepo na msiba hakuna mtu aliyeguswa wala taarifa kuwafikia majirani.
    Usiku nilipelekwa kwa kaka ambako nililala siku mbili na kurudishwa nyumbani, niliporudi hali ilikuwa ileile na kunifanya niwe na mawazo ni kweli dada alikufa au taarifa zile zilikuwa mgonjwa mahututi? Kwa hiyo yupo hospitali, sikutaka kuhoji haraka baada ya wiki sikuona mabadiliko wala taarifa zozote za dada Monika.
    Hata majirani waliotuzunguka hawakujua kitu zaidi ya ndugu wa mpenzi wa dada Monika kuulizia dada alizikwa wapi. Maswali yale kwa kweli yalinichanganya sana. Kila nilivyojitahidi kuchunguza sikupata taarifa zozote zaidi ya watu kufurahia maisha.
    Mwezi ulikatika nikiwa bado njia panda kuhusu maswali dada Monika wakiulizia mazishi yake yalifanyika lini na kwa nini baba hakuwataarifu kama kuna msiba, kama majirani wajumuike pamoja katika msiba ule. Siku moja nilikwenda hadi Mkuyuni kwenye nyumba aliyokuwa akikaa dada Monika. 
    Nilikuta mlango umefungwa, kuuliza nilishindwa kutokana na kuogopa maswali huenda amekufa na kunifahamu mimi ni nani. Niliamua kurudi bila kupata jibu kuhusiana na kupotea kwa dada Monika kwamba amekufa kweli au hali yake ni mbaya. Lakini nilikumbuka kaka mkubwa aliniambia kuwa Monika alikufa kutokana na uzazi.
    Nilijiuliza kama alikufa alizikwa wapi na kwa nini majirani hawajui lolote, na kama kweli alikuwa amekufa mazishi yake yalifanyika wapi. Kutokana na kuja mjini muda mrefu mazishi yote tuliyafanyia mjini. Ingekuwa kama wengine mazishi huyafanyia vijiji walikozaliwa lakini dhana ile baba aliikataa.
    Bado sikutaka kukubali, nilizunguka kwenye makaburi labda nitaliona kaburi jipya la dada Monika, lakini sikuona kitu chochote zaidi ya makaburi mapya yenye majina tofauti na la dada Monika.  Nilibakia njia panda siku zote kujiuliza ni kweli dada Monika alikufa au yupo kwa mganga.
    Siku moja nilikutana na shemeji aliyekuwa akikaa na dada Monika, nilimuulizia kitu ambacho kilionekana kituko mbele yake.
    “Shemu za siku?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Nzuri sijui zako?”
    “Eti shemu dada Monika yupo wapi?”
    “Masalu swali gani hilo? Ina maana mtu akifa huwa anakwenda wapi?”
    “Una maana ni kweli dada Monika amekufa?”


    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog