IMEANDIKWA NA : GLOBAL PUBLISHERS
*********************************************************************************
Simulizi : Nilioa Jini Nikamsaliti
Sehemu Ya Kwanza (1)
SAA nane usiku jini Nargis aliamka na kukaa kitako akiliangalia tumbo lake lililokuwa kubwa na kubakiza siku chache za kujifungua, alilipapasa taratibu kwa kuzungusha mkono pembeni.
Aliyahamisha macho yake toka kwenye tumbo lake na kumuangalia mumewe Thabit aliyekuwa katikati ya usingizi. Aliinama na kumbusu shavuni na kurudi kukaa kitako. Alijikuta akibubujikwa na machozi bila kizuizi.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Siku ile ilikuwa ngumu maishani kwake kutengana na mumewe waliyezoeana na kuishi kama mke na mume kwa muda mrefu. Pamoja na kuwa jini lakini alimpenda sana mwanaume yule kuliko kitu chochote chini ya jua na maji.
Alikumbuka mpaka kufika pale, alimpigania Thabit kwa hali na mali kwa muda mrefu kwa vita kali na nzito toka kwa wanadamu na majini wenzake waliyoyatamani maisha ya mpenzi wake.
Ili kuhakikisha anamlinda mpenzi wake iliyagharimu maisha ya wanadamu na majini kwa kuwaua.
Aliweza kuishi na mumewe maisha ya raha mustarehe baada ya kutokwa na jasho na machozi ya damu. Matunda ya kwanza yalikuwa kupata ujauzito alioutamani usiku na mchana kwa kuamini ile ndiyo sababu ya kuishi naye milele.
Baada ya kupata ujauzito wazazi wake walimweleza arudi haraka ujinini akailee mimba yake ili wanadamu wasiichezee. Lakini aliwaomba sana abakie duniani mpaka ikibakia wiki mbili kujifungua ndipo aende.
Wazazi wake walipinga, lakini aliwapa masharti yaliyokuwa magumu kwao kuwa aende na mumewe ambaye hakutakiwa kwa kipindi kile. Baada ya kushindwa masharti ya mtoto wao walikubaliana naye akae mpaka akibakiza wiki mbili kujifungua ndipo aende.
Sharti lingine lililomuumiza akilini Nargis ni kukaa miaka kumi chini ya bahari baada ya kujifungua ndipo atoke kurudi duniani na kuishi na familia yake japokuwa wazazi walitaka watoto waendelee kuishi ujinini mpaka watakapokuwa wakubwa.
Kwa mapenzi aliyokuwa akimpenda Thabit hakutaka kumuacha, alitaka aende naye akaishi naye kipindi chote cha kujifungua na kulea watoto wao. Lakini familia yake ilimruhusu kitu kimoja kuolewa na mwanadamu tu na si kumpeleka mwanadamu kuishi ujijini kipindi kirefu. Alijikuta akilia kwa zaidi ya saa nzima kutokana na maumivu ya moyo kwa kutengana na kipenzi chake.
Akiwa amezama kwenye lindi la mawazo, muda nao ulikuwa ukikaribia alikuwa na saa moja tu kuwepo duniani. Huko baharini majini waliokwenda kumpokea walikuwa wamejaa juu ya bahari huku wakiimba nyimbo tamu za kumkaribisha malaika wa majini Nargis. Alijizuia kulia na kumtikisa Thabit ili amuage kwa kumwita jina.
“Thabit…Thabit.”
“Mmh!” Thabit aliitika bila kufumbua macho na kujigeuza upande wa pili.
“Thabit mume wangu hebu amka basi,” alisema huku akimtikisa.
“Naam.”
“Hebu amka mwenzio nachelewa.”
“Ha! Kwani sasa ni saa ngapi?” Thabit alikurupuka usingizini.
“Nina nusu saa tu ya kuendelea kuwa hapa.”
“Mungu wangu! Mbona umechelewa kuniamsha?”
“Nisamehe mpenzi wangu.”
“Mbona macho yamevimba?”
“Acha tu, Thabit sikupenda kuwa mbali na wewe kwa kipindi kirefu, kitendo walichonifanyia wazazi wangu kimeniumiza sana. Kama walikubali uwe mume wangu kwa nini hawataki tukae wote kipindi cha kujifungua na kulea watoto wetu?” Nargis alianza kulia tena.
“Hatuna budi kukubaliana nao, hata mimi najua nitateseka sana, miaka kumi ni mingi sana Nargis, nitakuwa mpweke sana. Pamoja na kukupenda lakini ulikuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu, nilikuzoea sana, nitacheka na nani na nitacheza na nani?” Thabit alijikuta akizungumza sauti ya kilio kutokana na kutengana na mpenzi wake Nargis.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Hilo hata mimi linaniumiza, lakini naomba uniombee nijifungue salama.”
“Nitakuombea siku zote.”
“Thabit naondoka nikiwa nimekuachia utajiri mkubwa ambao hutaumaliza mpaka unakufa, unajua kiasi gani nilivyopigana na majini wenzangu na wanadamu kukulinda.
“Nina dhambi ya kuua majini na wanadamu kwa ajili yako. Nimewatia wanadamu na majini vilema ambavyo watakufa navyo kwa ajili yako.
“Thabit naondoka nakuacha peke yako, kwa utajiri ulio nao una mtihani mzito kwa wanadamu, kila mwanamke atakutaka, wapo watakaokuendea kwa waganga ili wakupate. Kipindi changu cha kujifungua sitaweza kutoka mpaka miaka kumi hivyo sitakuwa karibu na wewe tena.
“Mpenzi naomba usinisaliti nimechoka kubeba dhambi za wanadamu na majini kwa ajili yako.
Nakuomba baada ya kuondoka kaa mbali na wanadamu, mafuta niliyokuachia siku ukinikumbuka sana jipake usiku wakati wa kulala utaniota usingizini lakini hatutaonana mpaka miaka kumi ipite,” Nargis alisema kwa hisia kali.
“Nakuahidi kuwa muaminifu kwako, sitakusaliti nakupenda sana Nargis, nilitamani niwapokee wanangu wakati wa kuzaliwa lakini sina jinsi. “Nenda mpenzi wangu ukijua nakupenda kuliko kiumbe chochote kilichoumbwa na Mungu. Nakuahidi kukusubiri hata kwa miaka mia moja,” Thabit alimuahidi Nargis.
“Kweli Thabit?” Nargis alimuuliza Thabit huku akimkazia macho yake makubwa lakini yenye urembo wa aina yake.
“Kweli kabisa.”
“Hutanisaliti?” alimuuliza tena.
“Siwezi.”
“Na hii nyumba ya baharini kuanzia leo utaihama na kwenda kuishi kwenye nyumba tuliyojenga. Naogopa kukuacha hapo unaweza kufanya kosa nyumba ikayeyuka na wewe kufa maji. Sitaki kukupoteza mpenzi wangu nakupenda sana.”
“Nitajilinda kulilinda penzi letu.”
“Basi amka tukaoge ili niwahi, wenzangu wamefika zaidi ya saa nne kunisubiri.”
Walikwenda kuoga kisha alibadili nguo na kuvaa mavazi ya kijini na kumkumbatia Thabit wote waliruka hadi pembeni ya bahari ambako walikuta bahari ikimeremeta kwa mishumaa iliyokuwa imebebwa na majini.
Walitembea wameshikana mkono kama siku ya harusi yao mpaka walipokaribika kwenye kina kirefu, waliagana kila mmoja alilia kutengana na mwenzie.
Nargis kabla ya kuondoka alisema neno moja la mwisho.
“Thabit nakupenda sana usinisaliti, kwa heri.”
Ghafla juu ya bahari kiza kizito kilitokea, Thabit alijiona kama akizamishwa ndani ya bahari, alipotaka kupiga kelele maji tayari yalikuwa yamejaa mdomoni. Aliposhtuka alijikuta amelala kwenye nyumba yao mpya waliyojenga kama Nargis akiondoka kwenda kujifungua ili aishi maisha ya kawaida ya kibinadamu.
Nyumba ilikuwa na kila kitu, kama kawaida Nargis alimuachia mumewe vijakazi toka ujinini kwa ajili ya kumpikia na kumfanyia usafi. Yalikuwa maisha mapya ya Thabit kuishi bila ya mpenzi wake jini Nargis.
Thabirt aliyaanza maisha mapya wakati huo alikuwa amefunguliwa miradi mingi ambayo itamfanya awe bize ili watu washtuke kutaka kujua maisha yake ya kukaa tu akiwa na maisha mazuri. Thabit kila asubuhi alikwenda mjini kwenye moja ya duka lake kusaidiana na wafanyakazi wake kufanya biashara na jioni alirudi nyumbani.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Maduka mawili yalikuwa Posta na mengine mawili Kariakoo, yalikuwa maduka makubwa sana yaliyouza vitu mbalimbali. Moja liliuza vifaa vya elektoroniki ambavyo ni simu, redio, feni, friji na vifaa vyote vya umeme.
Lingine lilikuwa likiuza nguo za kike na kiume na viatu. Maduka ya Kariakoo moja liliuza vyombo vya ndani na lingine liliuza nguo za majumbani kama mashuka mapazia na vitu vyote vya ndani.
Pia alikuwa akimiliki magari ya kifahari, kila mtu alimfahamu mjini kwa utajiri wake. Wafanyakazi wake walifurahi malipo aliyowalipa na kufanya wamheshimu sana.
Kwa muda mfupi aliweza kufungua kampuni kubwa iliyokusanya miradi yake yote na yeye kuwa mkurugenzi wake. Jina la Thabit lilisambaa haraka kama moto kwenye nyasi kavu. Alikuwa ni mmoja wa watu wenye utajiri nchini huku kila mmoja akishamgaa uwezo wake wa kifedha kwa watu waliomfahamu toka enzi wakifanya kazi pamoja za vibarua kwenye makampuni ya Wahindi miaka ya nyuma kabla hajaonana na Jini Nargis.
Maisha yalimwendea vizuri japokuwa aliyakosa mapenzi ya mkewe Nargis, lakini kila usiku ulipoingia alijipaka mafuta. Usiku wote huwa na mpenzi wake Nargis ndotoni mpaka kunakucha ile kidogo ilimfariji na kujiona kama walikuwa pamoja.
Wasichana wengi kazini walimshangaa bosi mzima kama yule kutokuwa na mke, walipomuuliza aliwaeleza ana mke ambaye muda ule alikuwa amesafiri. Aliwaonesha mpaka pete ya ndoa kuonesha yeye ni mume wa mtu.
Lakini walishangaa toka awaeleze miaka zaidi ya mitatu ilikatika bila kumuona huyo mkewe kitu kilichoanza kuwafanya wawe na maswali labda bosi wao si rijali.
Subira sekretari wake siku zote alimpenda sana bosi wake lakini alishindwa kumwambia mateso ya moyo wake toka alipomweleza ana mke. Lakini muda ulizidi kukatika bila kumuona huyo mwanamke.
Alijiuliza kwa nini bosi wake hakuwa na mke! Siku zote aliumia sana lakini hakutaka kuendelea kuteseka, alimfuata shoga yake Sofia naye alikuwa mchemsha chai mpaka mpenzi wa bosi na kuwekwa kuwa sekretari wa kampuni tofauti.
Kwa vile walikuwa wameshibana na kuujua machepele wake wa kubadilisha wanaume alimweleza anavyompenda bosi wake.
“Si ana mke yule?”
“Ndiyo anavyosema lakini mwaka wa tatu unakatika hatujawahi kumuona mke wake.”
“Mmh! Basi atakuwa na tatizo!”
“Hapana naamini hana tatizo ila bado hatujamvutia kati yetu.”
“Sasa utafanyaje?”
“Ndiyo maana nimekuja unipe mawazo.”
“Labda tumwendee kwa babu.”
“Wewe unamjua nani mkali?”
“Mzee Mukti Buguju dawa za mapenzi mzee yule anatisha. Si unakumbuka yule shemeji yako Muhindi aliyekuwa bosi wa kampuni yetu? “
“Eeh! Mukesh, kweli siku hizi yupo wapi?”
“Shoga yaani majanga, nilipewa siku tatu nikamtia mikoni.
Aliniahidi vitu vingi wiki moja kabla ya kuvitekeleza si akaondoka kumbe mkataba wake ulikuwa umekwisha. Yaani kama angekuwepo mpaka sasa ningekuwa na nyumba na gari. Mzee Mukti Buguju namuamini sana.“
“Dawa zake hazima masharti magumu?”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Wala zipo za kwenye chai na zingine za kufusha usiku chumbani na kuoga basi.”
“Yaani hivyohivyo tu mwanaume anakuwa wako?” Subira kama hakuamini vile.
“Tena anakutamkia mwenyewe.”
“Mmh! Nikipata bosi wangu mbona nitakuwa tajiri, nashangaa mwanaume mwenye pesa kama nini hana hata mtoto!”
“Basi shoga ukiwa tayari twende kwa mzee Mukti Buguju.”
“Anakaa wapi?”
“Mji mwema.”
“Si kuvuka Kigamboni?”
“Ndiko hukohuko.”
“Mmh! Huko panafaa mwisho wa wiki siku ambayo siendi kazini.”
“Kwani chai anamtengea nani?”
“Mimi.”
“Basi amekwisha, jihesabu ni wako.”
“ Yaani shoga nakuahidi zawadi kubwa kama nikimpata hata gari nitakununulia.”
“ Mmh! Gari?” Sofia alishtuka.
“Jamaa ana hela kama nini, nikimpata utakubaliana na mimi.”
“Ukifika kwa mzee Mukti Buguju utakubaliana na mimi.”
****
Wakati Thabit akifarijika kuwa na mkewe jini Nargis ndotoni, Subira naye alikuwa mawindoni. Mwisho wa wiki walielekea Mji Mwema kwa mganga mzee Mukti Buguju. Kama walivyopanga walipitiana na kupanda daladala mpaka feri na kuvuka kisha walipanda daladala kuelekea Mji Mwema.
Walipofika waliteremka na kutembea kwa dakika kumi kuingia ndani kidogo hadi kwa mganga Mukti Buguju. Alikuta nje ya nyumba kuna magari manne ya kifahari, alipita ndani na kukaa kwenye mkeka. Watu hawakuwa wengi sana kutokana na siku yenyewe.
Mzee Mukti Buguju alikuwa na wasaidizi wengi ambao ndiyo waliopokea wateja. Baada ya kukaa alipewa namba ya kuonana na mzee na kutulia baada ya kuelezwa wataitwa kwa namba. Wakiwa wamekaa waliona watu wazito serikalini wakitoka ndani na kuingia kwenye magari yao na kuondoka.
Sofia alimnong’oneza Subira kwa kumwambia:
“Yaani huyu mzee kiboko hakuna anachoshindwa kwake mpaka nanii anakuja hapa!”
“Muongo, ulimuona?”
“Hapana alinieleza mzee Mukti, siku anayokuja huwa hakuna mteja.”
“Mmh! Basi atakuwa kiboko.”
“Wee utaniambia mwenyewe baada ya kumpata bosi wako.”
Baada ya muda namba yao iliitwa, waliingia ndani ya chumba kikubwa chenye mikeka ya kisasa kila kona kulikuwa na udi uliokuwa ukiwaka na kukifanya chumba kinukie.
“Karibuni,” mzee Mukti aliwakaribisha, alikuwa mzee wa makamo mwenye mwili ulioshiba. Alivalia kanzu nyeupe na kibalaghashia.
“Asante mzee, shikamoo.”
“Marahaba, mmh! Mna shida gani?”
“Ni mwenzangu hapa, mimi nimemleta tu,” Sofia alisema.
“Ndiyo nimeona hapa mwenye matatizo ni mmoja, haya bibi shida yako nini?”
Subira alielezea shida iliyompeleka pale, baada ya kumsikiliza alisema:
“Mwanangu shida huyo imekwisha, dawa nitakayokupa nitakupa siku tatu usipompata njoo uchome moto dawa zangu.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nitashukuru mzee wangu.”
Subira alipewa dawa ya kuweka kwenye chai na juisi, kufukiza chumbani kwake na ya kuoga, kazi yake haikuchukua muda mrefu.
“Mzee wangu ndiyo kiasi gani?”
“Hapana leo sitaki hela yoyote kwa vile huna hela ya kunipa, najua baada ya mwezi utaleta zawadi yangu.”
“Nashukuru mzee.”
“Haya kwaheri.”
Walitoka kwa mganga kuelekea barabarani huku Subira akiwa haamini kwa vile hawakutumia muda mrefu kupata huduma tofauti na watu waliowakuta. Walipanda daladala na kurudi nyumbani, wakiwa njiani Subira alikumbuka kuna kitu alisahau kuuliza.
“Sofi kuna kitu nimesahau kuuliza.”
“Kitu gani?”
“Kuhusu matumizi ya kwenye chai na juisi naweka kiasi gani?”
“Kumbe hilo, kiasi kidogo tu nusu kijiko cha chai.”
“Mara ngapi?”
“Subira mara moja, kwani mumeo useme utampa hata jioni.”
“Nilitaka kujua tu si unajua dawa hizi ukikosea masharti umeharibu kila kitu?”
“Ni kweli, lakini dawa za mzee huyu hazina masharti magumu kwa vile anaziamini.”
Baada ya kufika nyumba wakiagana kila mmoja alikwenda kwake, Subira pamoja na kuhakikishiwa kumpata Thabit kwake aliona kama ni uongo usiowezekana kwa mtu kumuwekea dawa kwenye chai na kumkubali kimapenzi.
Aliachana na mawazo yale aliangalia dawa alizofunga kwenye karatasi na kuzisoma, alichukua ya kuoga na kuweka kidogo kwenye maji na kwenda kuoga kisha alipata chakula.
Kabla ya kulala aliwasha moto wa mkaa na kuweka mikaa michache ya moto kwenye bakuli. Alichukua dawa ya kujifusha na kujifunika shuka kisha aliiweka kwenye moto huku akinuiza maneno ya kuhakikisha Thabit anaingia mikononi mwake. Baada ya kujifusha alipanda kitandani kulala.
***
Siku ya pili Subira aliwahi kazini na kufanya usafi kisha alimchemshia chai bosi wake na kuiweka kwenye chupa na kurudi sehemu yake kuendelea na kazi. Baada ya muda Thabit aliingia na kumsalimia kama ilivyo kawaida yake siku zote huwa mcheshi kitu kilichomchanganya Subira kushindwa kueleza badadiliko lolote kutokana na dawa alizofanya usiku.
Subira muda wote kazi ilimshinda macho yake hayakucheza mbali na saa yake ndogo ya mkononi kuangalia muda wa kumpelekea chai bosi wake. Kila alipoiangalia aliona kama mishale imesimama. Mapigo muda wote yalimwenda kasi kutokana na kuwa na wasiwasi na kitu alichotaka kukifanya kitakuwa na matokeo gani.
Wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kama bosi wake akigundua na kuamua kumfukuza kazi itakuwa kilio kwake. Aliona kama saa ya mkononi inamdanganya alibadili na kuangalia ya kwenye kompyuta. Nayo hakuiamini aliangalia kubwa ya ukutani ilimuonesha bado dakika tano muda wa kupeleka chai utimu.
Aliporudia kuangalia saa zingine zilionesha zilikuwa sawa ila wasiwasi wake ulifanya azione kama zimesimama. Alinyanyuka hadi jikoni na kuchukua kikombe cha bosi wake na kufungua kikaratasi alichoweka dawa ya unga na kuchukua kidogo na kuiweka kwenye kikombe huku akinuiza kumpata bosi wake na kuiweka chai ya maziwa na kukoroga huku akinuiza kuukoroga moyo wake kama ile chai na kumfanya amejaze moyoni kama utamu wa chai ile.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya kukoroga alijifuta vizuri na kuibeba chai na kwenda ofisini, alipofungua mlango alikutana na tabasamu pana la bosi wake.
“Karibu Subira.”
“Asante bosi.”
“Hongera umependeza,” kauli ile ilimpa matumaini, tangu aanze kazi pale hakuwahi kusifiwa na bosi wake.
Subira aliitenga chai juu ya meza ya bosi wake na kumkaribisha.
“Karibu bosi.”
“Asante.”
Alisema huku akishika mkono wa kikombe na kunyanyua ili apeleke mdomoni. Subira alikuwa amesimama pembeni kumuangalia bosi wake akipiga funda la chai ndipo aondoke kwenda kuendelea na kazi kusubiri kutoa vyombo na kuangalia matokea ya siku tatu aliyopewa kumtia mikononi Thabit.
Kikombe kilipokaribia mkononi alishtuka kukiona kikipasuka na kutoa mlio huku chai ikitawanyika na kumuunguza kifuani kitu kilichofanya Thabit apige kelele za maumivu huku Subira akipigwa bumbuwazi na kutoamini kikombe kupasuka kama kimefungwa bomu.
“Bosi nini?” Subira aliuliza kwa mshtuko.
“Hata najua nashangaa kikombe kupasuka kama kimefungwa bomu.”
“Pole sana bosi hukuungua?”
“Kiasi si sana.”
“Itabidi uende hospitali.”
“Lazima kwanza nirudi nyumbani nikabadili nguo.”
Thabit alivua shati lililochafuka kwa chai alivaa koti na kutoka kuelekea nyumbani kubadili nguo. Baada ya kuondoka bosi wake, Subira aliingia woga moyoni mwake na kujiuliza kile kilichotokea ni nini. Kwa nini hakikutokea siku zote kitokee alipoweka dawa?
Alijiuliza Thabit akigundua alitaka kumuwekea dawa atamchukulia hatua gani. Mawazo yale yalimchanganya sana na kujikuta akikosa raha na kuanza kujilaumu kujiingiza kwenye mambo ya kishirikina. Aliamua kumpigia simu shoga yake kumueleza yaliyotokea ofisini.
Baada ya simu kuita ilipokelewa upande wa pili.
“Haloo shoga vipi?”
“Mambo mabaya.”
“Kivipi?” Sofia alishtuka.
Alimweleza kilichotokea muda mfupi na kuichanganya akili yake.
“Wewee! Hakijamponyoka?”
“Hakijamponyoka kimepasuka.”
“Amekwambia au umekiona kwa macho yako?”
“Yaani nimeona mwenyewe kwa macho yangu.”
“Kimepasuka kabisa?”
“Tena kimelia kama bomu.”
“Mmh! Hukukosea kitu?”
“Sijakosea nimefuata kila hatua toka jana usiku.”
“Sasa itakuwa nini, mbona mara zote haikikutokea kitu kama hicho.”
“Nikuulize wewe!”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Basi turudi kwa mzee Mukti.”
“Kwa lililotokea, leoleo twende jioni.”
“Hakuna tatizo.”
***
Baada ya muda Thabit alirudi akiwa amebadili nguo, Subira alishtuka na kujiuliza ataambiwa nini.
“Vipi bosi?” aliuliza kwa unyenyekevu.
“Nipo sawa.”
“Vipi umeenda hospitali?”
“Sijaenda kwa vile sijaumia chochote.”
“Pole sana.”
“Asante, nipo ofisini.”
“Sawa.”
Subira aliendelea na kazi zake huku akihofia kumuwekea dawa kwenye juisi kwa kuhofia tukio lile kutokea tena. Muda wote alifanya kazi bila amani moyoni, akili yake iliwaza kwenda kuonana na mzee Mukti ili ajue tatizo nini.
Muda wa kutoka kazini Subira alikodi teksi na kumpitia shoga yake na kwenda Mji Mwema kwa mganga Mukti Buguju. Kutokana na foleni walifika saa kumi na mbili na nusu jioni. Walikuta kuna wateja wengi ilibidi wasubiri kuonana naye mpaka saa mbili na nusu usiku ndipo walipokutana.
Baada ya kuingia kwenye chumba cha uganga walikaa kwenye mkeka na kumsalimia mzee Mukti.
“Marahaba warembo, kama sikosei mlikuja jana?”
“Ndiyo mzee.”
“Vipi mbona ghafla?”
“Kuna tatizo mzee wangu,” Sofi alisema kwa niaba ya Subira aliyekuwa amenyamaza kimya.
“Tatizo gani?”
“Subira mueleze,” Sofi alimgeukia Subira na kumwambia.
“Ndiyo binti,” mzee Mukti alimsemesha Subira aliyekuwa ameinama.
“Kumetokea tatizo ofisini.”
“Tatizo gani?”
“Kuhusiana na ile dawa ya chai.”
“Imefanya nini?”
Subira alielezea yote yaliyotokea baada ya kufuata maelekezo ya kutumia dawa kuanzia usiku na asubuhi alipomtengenezea chai na maajabu yalitokea.
“Hicho kikombe kimemdondoka wakati anakunywa chai au vipi? Hebu nifafanulie.”
“Kimepasuka kabla hajainywa, kikombe kilipokaribia mdomoni kilipasuka kama bomu.”
“Eti?” mzee Mkuti alishtuka.
“Hakikumponyoka bali kimepasuka kama bomu kabla hakijagusa mdomo,” Subira alirudia.
“Chai haikumuunguza?”
“Kidogo lakini hakwenda hospitali.”
“Mmh! Kazi ipo,” mzee Mukti alisema huku akichukua unga kwenye kichupa kidogo kilichokuwa kwenye chupa nyingi za dawa na kumwaga kwa kuusambaza na kutulia kuutaza sehemu alizotupa kwa muda akiwa ameshika tama kisha aligeuka na kusema.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mmh! Kazi hii niliidharau kumbe ni nzito sana, bosi wako ni mume wa jini lililopo chini ya bahari na utajiri ule jini yule ndiye aliyempa. Kwa sasa yupo ujinini amekwenda kujifungua na atarudi baada ya miaka kumi. Kwa hiyo ametegesha mawasiliano yake na kuona kila kinachotendeka duniani ili kumlinda mumewe.
“Jini yule ni mpole sana ila ni mkorofi anapotaka kuingiliwa katika maisha yake hasa kumchukua kipenzi mume wake. Ile pete anayovaa bosi wako ndiyo mawasiliano makuu kati yake na mkewe jini Nargis. Kila kitu kinachofanyika lazima ajue na kutumia nguvu zake za kijini kupitia pete ile kuzuia Thabit asipatwe na tatizo lolote, ndiyo maana nikasema kazi ile sikuiangalia mapema kumbe nzito sana.”
“Kwa hiyo tutafanyaje maana kama ni hivyo rafiki yangu yupo hatarini?” Sofi aliuliza kwa niaba ya shoga yake.
“Kama mna nia ya dhati, itabidi muingie gharama za kuweza kuvunja mawasiliano kati ya Thabit na mkewe jini, kisha nikutengeneze wewe hata miaka kumi ikiisha akirudi asikufanye kitu kwa vile tutakuwa tumemdhibiti.”
“Kama kiasi gani?”
“Laki tatu.”
“Mzee wangu mbona nyingi sana?” Sofi aliuliza.
“Ni kweli ni nyingi lakini ni ndogo kulingana na kazi yenyewe, kumbuka nikikosea hata mimi naweza kufa kwa vile vita hiyo lazima itageukia kwangu. Pia baada ya zoezi letu utakuwa na maisha mazuri sana.”
“Sawa nitalipa,” Subira alikubali.
“Kazi hii inatakiwa ifanyike haraka sana kwa vile tayari tumeichokoza.”
“Sawa mzee wangu, lini?”
“Kwa vile mwezi bado haujamezwa na mawingu, kazi yako itafanyika kesho usiku saa sita baharini. Unatakiwa uje kulala huku na ukitoka hapa unafikia moja kwa moja kazini.”
“Sawa hakuna tatizo.”
“Nina imani lile ni tatizo ambalo halina madhara kwako, endelea kutumia dawa kujifusha kuoga ya chai na juisi achana nayo kwa muda.”
“Sawa mzee wangu, naweza kukutumia leo kutoka katika simu?” Subira aliuliza.
“Hakuna tatizo.”
Mganga alimtajia namba za simu, Subira alimtumia fedha yote kisha waliagana na kuondoka kuwahi nyumbani kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana.
***
Siku ya pili majira ya jioni Subira alielekea Mji Mwema kwa mzee Mukti Buguju peke yake kwa vile siku ile alitakiwa kulala kule. Alifika saa moja usiku na kwenda moja kwa moja kwa mzee Mukti alipomuona alimkaribisha na kumuomba atulie kwa vile kazi yake ilitakiwa kufanyika saa sita usiku mwezi ukiwa katikati.
Majira ya saa tano usiku alifuatwa na kijana wa mzee Mukti na kumwambia ajiandae kuna safari ya kwenda baharini. Alipewa shuka nyekundu na kilemba chekundu na kuambiwa avue nguo zote ajifunge zile kisha asuburi. Baadaye aliitwa nje, alipofika alikuta watu wanne na mzee Mukti na kuelezwa;
“Sasa mama kazi ndiyo inakwenda kuanza kwa vile hali ya hewa inaruhusu.”
“Sawa.”
Waliongozana kuelekea baharini wakiwa wamebeba kikapu chenye vitendea kazi na mbuzi mwekundu aliyekuwa amefungwa vitambaa vyekundu kwenye pembe. Subira kwa vile alikuwa mgeni alikaa katikati, msafara ulichukua dakika ishirini kufika baharini.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Walikuta maji yamejaa pomoni, alisimama pembeni ya maji, mzee Mukti alitoa vitendea kazi na kutengeneza mavazi yake mekundu. Baada ya mganga kupanga vitu vyake, Subira alielezwa ampande mgongoni na yule mbuzi alishikwa kwa mbele na kuingia naye ndani ya bahari.
Subira alikuwa akitetemeka kwa vile hali ya bahari ilikuwa tulivu lakini kulikuwa na milio ya kutisha. Hawakuijali waliendelea na kazi yao, alitembea na mbuzi yule mpaka maji ya kifuani wakiwa bado yupo chini. Wasiwasi wa Subira mbuzi yule kufa kwa kukosa hewa.
Baada ya kufika usawa ule mzee Mukti alishika usinga na kibuyu kidogo na kuingia nacho ndani ya maji. Baada ya kumsogelea Subira alizungumza kwa lugha anayoijua huku akimshika sikio la kulia kisha kumuwekea mkono katikati ya kichwa. Aliambiwa autazame mwezi na asipumue mpaka amalize kumshika kichwani. Baadaye alimuachia na kufanyika maombi mengine kazi iliendelea kwa zaidi ya saa mbili bila mbuzi aliyemkalia kutolewa ndani ya maji.
Baada ya zoezi kwenda vizuri alielezwa atoke, ajabu mbuzi aliyemkalia hakuwepo kwenye miguu yake. Alielezwa atoke ndani ya maji naye alifanya kama alivyoekekezwa. Alitoka mwenyewe bila mbuzi na kusikia wakisema:
“Kazi imekwenda vizuri tofauti na tulivyofikiria.”
Baadaye aliambiwa asogee pembeni ili aoge kisha warudi nyumbani, Subira alisogea pembeni na kuoga baada ya kuoga alipewa shuka nyeupe kujifunga kisha walirudi nyumbani. Walipofika mzee Mukti alimweleza:
“Kazi yako imekuwa rahisi tofauti na tulivyofikiria, mpeni chakula kisha apumzike ili asubuhi awahi kazini.”
“Sawa mzee,” waliitikia wasaidizi wake.
Baada ya kupata chakula na kuoga tena, alijifunga shuka nyeupe na kulala nayo hadi alfajiri alipoamshwa kuoga tena ili kujiandaa awahi kazini. Kabla ya kuondoka alipewa dawa nyingine.
“Hii utaiweka ndani ya maji kisha haya majani utatumia kunyunyiza kila kona ya ofisi kisha yatupe. Dawa hii inaua nguvu za kijini ambazo zipo pale ofisini.
Hii nyingine utainyunyizia kwenye meza ya bosi wako akigusana na pete mawasiliano yatakuwa yamekatika kati yake na mkewe jini, hivyo utatumia ile dawa ya chai na juisi kwa vile tayari tutakuwa tumekata mawasiliano.
Mtakapoanza uhusiano usikubali kukutana naye mpaka uje huku kuna dawa nitakupa kuhakikisha unakuwa salama katika penzi lako na kuifanya ndoa yako iwe ya haraka. Nina imani ikifanya kwa kuzingatia maelezo yangu utashangaa mwenyewe.”
“Nashukuru mzee wangu, nakuahidi zawadi kubwa.”
“Wewe tu kazi yangu nimemaliza.”
Baada ya kupewa dawa na maelekezo Subira aliondoka kuwahi kazini, alikodi Bajaj ambayo ilimpeleka moja kwa moja mpaka ofisini. Siku ile aliwahi kazini tofauti na siku zote mpaka mlinzi alishangaa.
Baada ya kuingia ofisi kwa bosi wake, alianza usafi mara moja kisha alichukua kikombe cha chai na kuweka maji kidogo na kuweka dawa ya unga na kuikoroga kisha alichukua majani aliyopewa na kuanza kunyunyiza ndani ya ofisi. Ghafla mle ndani ulitokea mtikisiko mkubwa , Subira alitoka mbio kuhofia uhai wake na kwenda kusimama pembeni ya ofisi huku akitweta.
Bahati nzuri alitoka na mkoba wake na kumpigia simu mzee Mukti ili kumweleza yaliyotokea huku yakizidi kumkatisha tamaa. Baada ya kuita kwa muda mfupi ilipokelewa upande wa pili.
“Haloo.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Haloo mzee.”
“Vipi mbona hivyo?”
“Huku kuna tatizo lingine limetokea.”
“Tatizo gani?”
Subira alimwelezea kilichotokea muda mfupi baada ya kuanza kunyunyiza dawa aliyompa.
“Kumbe ni hilo endelea tu.”
“Mzee yaani mtikisiko mpaka mwenyewe nikashtuka, hapa nilipo natetemeka mwili hauna nguvu kabisa halafu unaniambia niendelee?”
“Zile ndizo nguvu za kijini zilizomo ofisini, unaponyunyiza maji huo mtikisiko uliousikia ni kuvunjika kwa nguvu hizo. Kwa hiyo kaendelee wala usihofu, jitahidi umalize zoezi kabla bosi wako hajafika.”
“Sawa.”
Subira alirudi ofisini akiwa hajiamini, alichukua kikombe chenye maji na kuanza kunyunyiza ile dawa. Mtikisiko wa mwanzo ulijirudia tena lakini hakuacha aliendelea kufanya hivyo kila kona ya ofisi na hali ya mtikisiko ilitulia. Baada ya zoezi lile kwenda vizuri alichukua dawa nyingine na kuipaka kwenye meza na kurudi sehemu yake ya kazi.
Majira ya saa tatu na nusu asubuhi Mustafa aliingia ofisini, kama kawaida aliachia tabasamu lililokuwa likimtesa Subira. Baada ya kusalimiana aliingia ofisini kwake kuendelea na kazi. Haikuchukua muda kishindo kizito kilitokea ndani ya ofisi kilichomshtua Subira na kujiuliza kulikuwa na kitu gani ndani.
Alinyanyuka taratibu huku mapigo ya moyo yakiwa juu na kugonga ofisini kwa bosi wake taratibu. Hakukuwa na majibu yoyote, ile hali ilizidi kumtisha aligonga tena kwa nguvu kidogo huku akimwita kwa jina lake.
“Bosi…bosi.”
Vilevile hakukuwa na jibu, aliufungua mlango taratibu na kuchungulia ndani, alishtuka kumuona bosi wake akiwa amejilaza kwenye meza huku kidoleni pete yake ikionesha kama moto unawaka. Alijiuliza kile ni nini kwa vile hakuelezwa na mganga kutokea na kitu kile.
Alimsogelea huku akitetemeka alimtikisa akimwita, lakini hakukuwa na jibu, alipomuangalia vizuri aligundua amepoteza fahamu. Haraka alirudi ofisini kwake na kumpigia simu mzee Mukti ili kumpa kinachoendelea pale ofisini.
“Vipi binti?” aliuliza baada ya kupokea.
“Mzee wangu kila dakika kunatokea kitu cha ajabu.”
“Kitu gani?”
“Baada ya bosi kuingia, ilichukua muda mfupi kusikia kishindo kizito, nilipoingia ndani nimemkuta amelalia meza akiwa amepoteza fahamu. Kilichonishtua zaidi pete aliyovaa inawaka moto.”
“Hiyo kawaida wala usihofu zoezi limekwenda vizuri sana, umenifurahisha kufanya kama nilivyokuelekeza.”
“Mzee zoezi limeenda vizuri wakati hali ya bosi ni mbaya?” Subira alimshangaa mzee Mukti kusema vile.
“Kazi imeisha, sasa fanya hivi mvue pete hiyo iweke kwenye maji yaliyochanganywa na dawa iliyopakaza kwenye meza kwa dakika tano. Kisha utaitoa na kumvisha kidoleni na kumuacha bila kumfanya chochote.
Ukitoka hapo kamuandalie chai, akishtuka mpe chai kisha endelea na kazi. Mchana mpe juisi kitakachofuata utanijulisha. Nilitaka kusahau na lingekuwa kosa kubwa, kabla hujaishika pete jipake dawa hiyo mkononi.”
“Sawa mzee.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Subira alifanya kama alivyoelekezwa kwa kuweka maji kidogo kwenye kikombe na kuchanganya na dawa, alijipaka dawa mikononi kisha alimvua pete iliyokuwa ikiwaka moto huku akitetemeka na kuiweka kwenye kikombe.
Ilipogusa maji moto ilizimika kama kaa la moto huku ikitoa moshi na kutulia. Baada ya zoezi lile aliifuta pete kumvisha tena na kutoka ofisini kwa bosi wake kwenda kumtengeneza chai ili amalize zoezi la asubuhi.
Baada ya kuchemsha chai aliweka kwenye chupa na kurudi kuendelea na kazi, lakini kazi ilimshinda kwani hakujua hatima ya bosi wake.
Kompyuta aliiwasha na kutulia akiiangalia huku akisubiri kitakachoendelea. Baada ya dakika kumi alishtushwa na sauti ya Thabit.
“Subira.”
“E..eeeh! Abee bosi,” Subira alishtuka toka katika dimbwi la mawazo.
“
Chai tayari maana nashangaa nasikia mwili kuchoka ghafla,” Thabit alisema huku akijinyoosha.
“Tayari.”
“Ndiyo maana nakupenda.”
“Nioe basi,” Subira alijikuta akiropoka.
“Kila kitu mipango.”
Subira alijikuta alijishtukia kwenda mbali zaidi wakati zoezi aliloambiwa na mzee Mukti lilikuwa halijakamilika.
Alikwenda jikoni kuchukua chai kabla ya kuibeba aliweka dawa na kuikoroga vizuri kisha alibeba kikombe kumpelelea bosi wake. Aliitenga juu ya meza na kusema kwa unyenyekevu:
“Karibu chai bosi.”
“Asante,” Thabit alisema huku akichukua kikombe cha chai ili akipeleke mdomoni.
Subira alishindwa kuondoka alisimama akiangalia nini kitatokea wakati huo mapigo ya moyo yalikuwa juu. Wakati akikipeleka kikombe mdomoni hali ilikuwa mbaya kwake jasho la hofu lilimtoka na kubana pumzi.
Thabit alipiga funda mbili za haraka kutokana na moto wa chai na kumumunya midomo kisha alisema:
“Dah! Subira unajua kupika chai, umeolewa?”
“Sijaolewa.”
“Mmh! Sawa, chai tamu sana.”
“Kwani vipi?”
“Kaendelee na kazi.”
Subira hakuongeza neno alitoka na kwenda ofisini kwake huku akizidi kuyaona maajabu ya mzee Mukti pale bosi wake alipokunywa chai bila kikombe kupasuka. Alitaka kumpigia simu mzee Mukti Buguju kumweleza alipofikia lakini aliona mapema alisubiri aone kinachoendelea.
***
Thabit akiwa ofisini kwake alijiona mtu tofauti na alivyojizoea kwa kipindi kirefu, aliushangaa uzuri wa sekretari wake. Kwake alikuwa kama kiumbe kipya ambacho hakuwahi kukiona siku za nyuma. Alinyanyua simu na kumwita ofisini kwake ili amuulize kitu.
Baada ya muda Subira alisimama mbele yake huku akiachia tabasamu pana lililozidi kuuteketeza moyo wa bosi wake.
“Abee bosi.”
“Kaa.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Subira alikaa na kumtazama bosi wake aliyeonekana kumshangaa kitu kilichomfanya amuhoji.
“Bosi mbona unanishangaa?”
“Una muda gani hapa kazini?”
“Miaka mitano sasa.”
“Miaka hiyo mitano! Ulikuwa ukifanya sehemu gani?”
“Kama msaidizi wako.”
“Muongo, mbona nilikuwa sikuoni?”
“Kweli bosi, basi tu labda sina mvuto moyoni mwako.”
“Hapana, umeolewa?”
“Bado.”
“Una mchumba?”
“Sina.”
“Jiandae mchana tukapate chakula cha pamoja kwa mazungumzo zaidi.”
“Bosi wewe si unakula kwako?”
“Ndiyo.”
“Kwa hiyo nikale na wewe kwako?”
“ Ndiyo.” “Kwa hiyo nikale na wewe kwako?” “Hapana leo tutakwenda hotelini.” “Hakuna tatizo.” “Basi kaendelee na kazi yako.” Subira alitoka huku moyo wake ukicheka alitamani kupiga vigelele, hakukaa alimpigia simu mzee Mukti ili kumjulisha kilichoendelea.
“Basi binti kazi imekwisha, jioni njoo tumalize kazi kabisa.” “Sawa mzee wangu.” Subira alijiandaa kutoka na bosi wake kwenda kupata chakula cha mchana, alifanya kazi iliyobakia haraka ili asibakishe kiporo. Baada ya muda Thabit alimpigia simu ajiandae watoke wakapate chakula cha mchana.
Alikwenda maliwatoni kujitengeneza akiwa pamoja na kuupodoa uso wake ili azidi kuonekana mpya kwa bosi. Thabit alitoka na kumpitia Subira aliyekuwa tayari amejiandaa, walitoka hadi kwenye gari, Kabla ya kuondoka Thabit alimuuliza Subira: “Twende wapi?” “Sijui, utakapotaka wewe.”
“Nimekupa upendeleo chagua unapopaona panafaa wewe.” “Mmh! Basi Steers.” “Hakuna tatizo.” Thabit aliwasha gari kuelekea Steers kwa ajili ya chakula cha mchana na sekretari wake.
Walipofika waliagiza chakula na kuanza kula, muda wote moyo wa Thabit ulikuwa ukimsukasuka kutokana na kumpenda sana Subira. Alijikuta akishindwa kuzuia hisia zake japokuwa alikuwa akikumbuka masharti aliyopewa na jini Nargis.
“Subira unajua wewe ni mzuri?” Thabit alisema huku akipeleka kijiko cha chakula mdomoni. “Nitajuaje wewe ndiye unayeuona,” Subira alijibu kwa tabasamu la mtego. “Unajua Subira lazima niseme ukwe…” Thabit alinyamaza baada ya kusikia sauti ya mkewe aliyosema muda mfupi kabla ya kuondoka kurudi ujinini.
Alitulia akiwa kama anaangalia tivii baada ya kuona marudio ya siku ambayo mkewe Nargis alipomuamsha ili amuage na kumkuta akilia. “Mbona macho yamevimba?” “Acha tu, Thabit sikupenda kuwa mbali na wewe kwa kipindi kirefu, kitendo walichonifanyia wazazi wangu kimeniumiza sana.
Kama walikubali uwe mume wangu kwa nini hawataki tukae wote kipindi cha kujifungua na kulea watoto wetu?” Nargis alianza kulia tena. “ Hatuna budi kukubaliana nao, hata mimi najua nitateseka sana, miaka kumi ni mingi sana Nargis, nitakuwa mpweke sana.
Pamoja na kukupenda lakini ulikuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu, nilikuzoea sana nitacheka na nani nitacheza na nani?” Thabit alijikuta akizungumza sauti ya kilio kutokana na kutengana na mpenzi wake Nargis. “Hilo hata mimi linaniumiza, lakini naomba uniombee nijifungue salama.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nitakuombea siku zote.” “Thabit naondoka nikiwa nimekuachia utajiri mkubwa ambao hutaumaliza mpaka unakufa, unajua kiasi gani nilivyopigana na majini wenzangu na wanadamu kukulinda. “Nina dhambi ya kuua majini na wanadamu kwa ajili yako.
Nimewatia wanadamu na majini vilema ambavyo watakufa navyo kwa ajili yako. “Thabit naondoka nakuacha peke yako, kwa utajiri ulionao una mtihani mzito kwa wanadamu kila mwanamke atakutaka, wapo watakaokuendea kwa waganga ili wakupate.
Kipindi changu cha kujifungua sitaweza kutoka mpaka miaka kumi hivyo sitakuwa karibu na wewe tena. “Mpenzi naomba usinisaliti nimechoka kubeba dhambi za wanadamu na majini kwa ajili yako.
N akuomba baada ya kuondoka kaa mbali na wanadamu, mafuta niliyokuachia siku ukinikumbuka sana jipake usiku wakati wa kulala utaniota usingizini lakini hatutaonana mpaka miaka kumi ipite,” Nargis alisema kwa hisia kali.
“Nakuahidi kuwa muaminifu kwako, sitakusaliti nakupenda sana Nargis, nilitamani niwapokee wanangu wakati wa kuzaliwa lakini sina jinsi. Nenda mpenzi wangu ukijua nakupenda kuliko kiumbe chochote kilichoumbwa na Mungu. Nakuahidi kukusubiri hata kwa miaka mia moja,” Thabit alimuahidi Nargis.
“Kweli Thabit?” Nargis alimuuliza Thabit huku akimkazia macho yake makubwa lakini yenye urembo wa aina yake. “Kweli kabisa.” “Hutanisaliti?” ulimuuliza tena. “Siwezi.” Thabit alijikuta amehama kimawazo kitu kilichomshtua Subira.
“Vipi bosi?” “Ee...ee...eeh,” Thabit alishtuka na kujikuta akifuta uso kwa mikono kama anaondoa kitu na kutuliza macho kwa Subira huku mapigo ya moyo yakienda mbio. Alitikisa kichwa kujiweka sawa huku uzuri wa Subira ukijaa tena machoni mwake.
“Bosi mbona hivyo una nini?” Subira alimuuliza akiwa amemkazia macho huku akirudisha kijiko chenye chakula kwenye sahani. “Mmh! Achana nayo tuendelee na yetu, vipi mbona huli?” Thabit alisema huku akichota chakula na kupeleka mdomoni.
“Nakula,” Subira alijibu huku akichota chakula. W aliendelea kula kimyakimya hakukuwa na mazungumzo yoyote mpaka walipomaliza na kuondoka. Walipofika ofisini Thabit alionekana amechoka hakukaa alimuaga Subira kuwa anatoka kidogo.
Baada ya kutoka Subira alijiuliza maswali mengi juu ya hali ya bosi wake kugeuka vile wakati alikuwa amechangamka na kumpa matumaini hasa pale alipoonesha kumuulizia kuhusu uhusiano wake.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment