Simulizi : Nilioa Jini Nikamsaliti
Sehemu Ya Pili (2)
Waliendelea kula kimyakimya hakukuwa na mazungumzo yoyote mpaka walipomaliza na kuondoka. Walipofika ofisini Thabit alionekana amechoka hakukaa alimuaga Subira kuwa anatoka kidogo.
Baada ya kutoka Subira alijiuliza maswali mengi juu ya hali ya bosi wake kugeuka vile wakati alikuwa amechangamka na kumpa matumaini hasa pale alipoonesha kumuulizia kuhusu uhusiano wake aliamini dawa za mzee Mukti zilikuwa zikifanya kazi.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Lakini hali iliyomtokea muda mfupi baada ya kufika Steers ilimshtua sana, alijiuliza hali ile ilitokana na nini. Alinyanyua simu yake na kumpigia mzee Mukti, baada ya kuita ilijibu kuwa inatumika. Alisubiri kwa muda kidogo na kupiga tena ambayo muda ule ilipokelewa.
“Haloo.”
“Haloo mzee wangu.”
“Ndiyo mama unasemaje?”
Subira alimweleza yote yaliyotokea muda mfupi, baada ya kumsikiliza mzee Mukti Buguju alishusha pumzi ndefu na kusema:
“Subiri kidogo,” mzee Mukti alisema na kukata simu ili aangalie kilichotokea kimetokana na nini.
Baada ya muda mfupi alipiga simu iliyopokelewa na Subira.
“Ndiyo mzee wangu.”
“Nimeona.”
“Umeona nini mzee wangu?”
“Hali iliyomtokea bosi wako ilitokana na kuhama kimawazo yalikuwa ni mawasiliano kati yake na mkewe jini Nargis. Lakini yalikuwa ya kumbukumbu baada ya kuingia, Jini Nargis alijitahidi kumvuta ili azungumze naye lakini hayakuweza kumpata vizuri. Mkewe ameisha jua nini kinatendeka duniani lakini kwa sasa hana nguvu tena baada ya kuiua nguvu ya pete ambayo ndiyo iliyokuwa kiunganishi kikubwa kati ya bosi wako na mkewe jini.
Walichoweza ni kumtia uchovu ili akalale awaze kuwasiliana naye, kwa vile pete haikuwa na nguvu, lazima Jini Nargis atawatuma vijakazi wake waichukue na kuirudisha chini ya bahari kwenda kuongezewa nguvu kisha atarudishwa kabla hajaamka na kuvisha kuanzia hapo mawasiliano yatarudi kama kawaida. Na tukichelewa tutakosa kila kitu na wewe kufukuzwa kazi”
“Mungu wangu! Sasa itakuwaje?” Subira aliuliza.
“Kuna kazi nataka nikupe muda huu ili kumuwahi.”
“Kazi gani?”
“Ile dawa ya unga ipo?”
“Ndiyo.”
“Unajua anapokaa bosi wako?”
“Ndiyo, lakini sijawahi kufika.”
“Chukua hiyo dawa, kanunue maji safi lita moja na nusu kisha chukua dawa kidogo changanya. Ondoka na hayo maji nenda moja kwa moja hadi anapokaa bosi wako ukifika getini mwaga kidogo kisha ingia ndani ya uzio mwaga kidogo. Nenda mpaka kwenye nyumba ya bosi wako mwaga kidogokidogo kuizunguka nyumba yote kisha ingia ndani na kumwaga kidogokidogo nyumba nzima.
“Kuna vitu utavisikia wakati ukiendelea na zoezi hilo usiogope fanya kazi niliyokuelekeza, hata viwe vinatisha vipi endelea na zoezi lako kwa vile havitakudhuru kwani utakuwa ukiua nguvu za kijini. Utashangaa kukuta jumba lote lile hakuna mtu, kama nilivyokueleza awali baada ya mkewe jini Nargis kuondoka alimuachia vijakazi ambao walimfanyia kazi zote za usafi na kumpikia. Lakini dawa utakayoimwaga ndiyo itakayo waondoa na kutimka kwa maumivu.
“CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Ukiisha maliza zoezi hilo ingia chumbani kwa bosi wako utamkuta amelala lakini kidoleni hana pete ambayo itakuwa imepelekwa ujinini kurudishiwa nguvu ya awali. Mpake maji kichwani na kumuacha, nenda bafuni weka maji kwenye beseni, weka dawa hiyo oga maji hayo na kubakisha mengine. Rudi ndani muamshe Thabit akiamka mshike mkono atakuwa kama zezeta kwa vile nguvu za kijini zitakuwa zimetoka.
“Mpeleke bafuni mwogeshe maji ya dawa, muda ule atarudi katika hali yake ya kibinadamu. Mtarudi chumbani mtalala kama wapenzi. Ukifanya zoezi zima kwa umakini huo ndiyo utakuwa mwanzo wako wa kuishi na Thabit.
“Najua vita itakuwa kubwa ya kutaka kukutoa mikononi mwake lakini kuna dawa nitakupa hakuna jini wala mchawi atakae kugusa. Kisha kuna kazi nyingine nzito ya kulinda mali ya Thabit ambayo ni ya majini ambao watataka kuirudisha mikononi mwao kama wakishindwa kumpata Thabit. Japokuwa najua ni ngumu lakini tutashinda na zawadi mtanipa.”
“Sawa mzee wangu nikikwama nitakupigia simu.”
“Hakuna tatizo lakini zoezi hilo lifanye sasa hivi.”
“Sawa mzee.”
“Nilitaka kusahau hakikisha baada ya kukutana naye kimwili unaondoka kuja kwangu, jitahidi kabla kivuko hakijasimama.”
“Sawa mzee wangu.”
Baada ya mazungumzo Subira alivuta droo ya meza yake na kutoa karatasi iliyokuwa na dawa ya unga, aliirudisha na kutoka kwenda dukani na kununua maji ya lita moja na nusu na kurudi nayo ofisini. Aliingia ofisini kwa bosi wake ambako aliamini ni sehemu salama na kuitia dawa kwenye maji na kuitikisa kisha aliiweka kwenye mfuko wa plastiki.
Alitoka na kukodi bodaboda hadi nyumbani kwa bosi wake, aliteremka na kumlipa dereva. Alisogea karibu ya mlango wa kuingilia, alitoa chupa yake kwenye mfuko na kuishikilia mkononi. Huku mapigo ya moyo yakimwenda kwa kasi alitembea kuelekea mlango mkuu.
Aliifungua chupa na kuanza kumwaga getini, maji yalipogusa chini alisikia mtikisiko, japokuwa mapigo ya moyo yaliongezeka lakini alijikaza na kuingia ndani. Kila alipomwaga maji mtikisiko mkubwa ulitokea. Akwenda hadi kwenye jumba la kifahari na kuendelea na zoezi la kumwaga maji kuizunguka nyumba ile.
Mtikisiko uliongezeka mara dufu aliona kama nyumba inataka kudondoka, kama asingepewa maelekezo angekimbia hali ilikuwa ikitisha sana. Baada ya kumaliza zoezi la kuzunguka nyumba aliingia ndani na kuendelea na zoezi lake. Alishangaa kukuta nyumba tupu lakini ikinukia manukato mazuri sana.
Alipoanza kunyunyiza maji ndani alisikia vishindo na sauti za vilio vya maumivu.
Woga ulimtawala alitaka kukimbia nyumba ilikuwa na mtikisiko mkubwa huku akisikia sauti za watu wakikimbia na vishindo kama watu wakiruka toka juu na kutua chini.
Alijipa moyo na kuendelea na zoezi lake, nyumba ilikuwa kama imekumbwa na tetemeko zito, hakuacha kunyunyuzia maji kila kona kama alivyoelekezwa mpaka alipoingia chumba cha Thabit alishangaa kukuta chumba kizuri sana chenye kitanda kizuri ambacho hakuwahi kukiona katika maisha yake.
Kilikuwa kimenakshiwa na fito za dhahabu na shuka zake za uzi wa hariri. Kitandani alikuwa Thabit amelala hajitambui, alimuangalia kidole cha mkono wa kulia hakuiona pete. Hakushangaa kwa vile aliisha elezwa kila kitu na mzee Mukti alijua imeenda wapi.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mara moja alimuosha maji ya dawa kichwani na kumuacha kitandani bila kumuamsha na kwenda bafuni. Bafu nalo lilikuwa zuri likinukia manukato mazuri sana. Hakupoteza muda alifungulia maji kwenye beseni kisha aliweka dawa kidogo na kuyachanganya.
Alioga maji ya dawa na kubakisha nusu, alirudi chumbani ambako alimuamsha Thabit ambaye aliamka kwa shida. Alionekana kama mtu asiyejielewa alimshika mkono hadi bafuni ambako alimuosha maji ya dawa. Baada ya maji kumpata mwili nzima Thabit alirudi katika hali yake ya kawaida.
Alishangaa kumuona Subira aliyekuwa kwenye vazi la khanga moja mbele yake.
“Vipi tumekuja saa ngapi?” Thabit aliuliza akiwa anamtazama.
“Tumekuja muda,” Subira alidanganya.
Alimshika mkono na breki ya kwanza ilikuwa kitandani, kwa vile Thabit alikuwa hajielewi alifanya mapenzi na Subira. Baada ya kustarehe kila mmoja alipitiwa usingizi. Subira alishtuka usingizini, alipoangalia saa ya ukutani ilimuonesha saa nne usiku. Kwa vile hakutakiwa kulala alimshtua Thabit aliyekuwa usingizini.
“Thabit.”
“Naam.”
“Mpenzi naomba niondoke.”
“Kwa nini usilale uondoke kesho?” Thabit alijibu huku akiangalia saa ya ukutani.
“Hapana mpenzi sikuaga nyumbani kuja huku ulinilazimisha kwa vile nakupenda nilikukubalia sikutaka kukuudhi mpenzi wangu,” Subira alizidi kutengeneza uongo ambao Thabit aliukubali.
Thabit alitaka kumsindikiza, lakini Subira alikataa kusindikizwa kwa vile alitakiwa usiku ule lazima arudi kwa mzee Mukti ili amalize mambo kabisa. Alitoka nje na kukodi gari mpaka Kigamboni na kukodi Bajaj mpaka Mji Mwema kwa mzee Mukti Buguju.
Alifika majira ya saa tano kasoro, hakuchelewa alipatiwa tiba ya mwisho na kupewa hirizi ndogo ambayo ataifunga kwenye mkono sehemu za begani. Pia alipewa dawa ya kuweka pembe nne za jumba lile kama kinga ili majini yasiingie.
“Mzee zingine ungenisaidia wewe.”
“Basi weka unga huu kwenye kona kila siku, wiki moja baada ya kuanza kukaa pale nitakuja kuzindika nyumba pia sehemu zote za biashara ili zisichukukiwe na nguvu za kijini.”
“Sawa kama hivyo.”
“Dawa ya kufukiza utafukiza kila ikifika saa sita usiku muda ambao majini huja duniani.”
“Sawa nitafanya hivyo, mzee wangu nina zawadi kubwa nimekuandalia.”
“Wewe tu.”
“Kuna kitu nilisahau, unatakiwa kuwahi nyumbani kwa mpenzi wako ili umuandalie kifungua kinywa. Nitakupa dawa ambayo utatumia kumpikia chakula ili kuondoa chakula alichokuwa akila toka ujinini. Kuanzia kesho utahamia kwake hapo hutotoka tena mpaka ndoa yenu.”
“Nitafurahije mzee wangu.”
“Kazi imekwisha sasa hivi Thabit ni mume wako.”
Baada ya zoezi zito lililoisha saa sita usiku. Subira hakulala alikodi gari mpaka kwake na kulala na kuamka alfajiri na kununua vitu vya kwenda kumuandalia kifungua kinywa Thabit. Alimkuta bado hajaamka aliingia ndani na kwenda jikoni kumuandalia kifungua kinywa kisha alimuamsha aoge afungue kinywa na kuondoka pamoja kwenda kazini.
***
Chini ya bahari jini Nargis mke wa Thabit alishtuka kitandani kwake na kuona kiza sehemu iliyokuwa ikimuonesha kila alipokuwa mume wake. Alijaribu kutumia nguvu za kijini kumvuta mpenzi wake lakini hakumuona. Alichanganyikiwa na kusimama na kuanza kutangatanga chumbani kama kuku anayetaka kutaga.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Alitoka chumbani bila ushungi kichwani hadi sebuleni alipokuwa amekaa mama yake malkia Zabeda na dada yake Hailat ambao walishtuka kumuona Nargis katika hali ya taharuki.
“Vipi mbona hivyo?” mama yake alimuuliza.
“Baba Zumza (Thabit) simuoni.”
“Humuoni kivipi?” dada yake alimuuliza.
“Nimeshtuka usingizini na kuona kiza kizito sehemu niliyotegesha kumuona kila wakati,” Nargis alisema machozi yakimtoka.
“Kwani pete yake si anayo?” dada yake Hailat aliuliza.
“Ndiyo lakini nashangaa simuoni.”
“Basi atakuwa ameivua.”
“Hebu rudi kwanza ndani ukaangalie vizuri,” mama yake alimshauri.
Nargis alirudi ndani kuangalia tena, lakini alikuta hali ni ileile kiza kizito kilitanda eneo lile.
Alitoka kwenda kuwaeleza nao walinyanyuka na kuingia naye chumbani kwake kuangalia. Walishtuka kuona kiza kizito sehemu iliyokuwa ikimuwezesha Nargis kumuona mumewe.
“Mmh! Itakuwa nini?” Dada yake Hailat alishtuka.
“Mmh! Lazima kuna mchezo umechezwa si bure,” mama yake alijibu.“Kibaya hata sioni dalili za pete,”Nargis alisema kwa kukata tamaa.
“Siyo tatizo, watume Watwana wakamtie uchovu akirudi nyumbani wamvue pete na kuileta huku na kuirudishia nguvu yake kisha tutamchukua na kumwekea kivuli kisha tunamrudisha duniani huku tukiwaondoa wafanyakazi wote wanadamu na kampuni yake itaendeshwa na majini, kila atakapokuwa wanadamu hawatamuona,” alisema mama yake.
“Hilo ndilo la kufanya japokuwa najua vita ya wanadamu ni nzito sana, basi tu mdogo wangu mbishi kwa nini usiachane na huyo mwanaume kwa vile tayari amekupatia watoto,” dada yake alimshauri.
“Dada hayo ni maneno gani? Kumbuka yule ni mume wangu wa ndoa halali, baba wa watoto wangu, siwezi kurudi nyuma nitapambana hadi tone la mwisho la damu yangu,” Nargis alisema kwa uchungu.
“Basi tu ingekuwa amri yangu ningemuulia mbali mwanaume anayekosa uaminifu,” dada yake alisema kwa hasira.
“Mmh! Sasa hebu waite watwana wafanye hiyo kazi muda huu,” Malkia Zabeda alitoa amri.
Nargis alijishika katika paji la uso, mara walitokea watwana na kupiga magoti mbele yake na kuuliza.
“Mwana wa mfalme una shida gani?”
Aliwapa maelekezo ya kumtia uchovu Thabit, akilala wachukue ile pete haraka na kuipeleka chini ya bahari. Baada ya kuelezwa vile walitoweka ghafla na kwenda moja kwa moja ndani ya ofisi alipokuwa Thabit amerudi muda mfupi toka hotelini walipokwenda kupata chakula cha mchana na Subira.
Waliingia na kumpuliza kisha walisimama pembeni, ghafla Thabit alianza kujinyoosha baada ya kusikia uchovu mkubwa mwilini mwake. Aliona hawezi kuendelea na kazi alitoka na kumuaga Subira aliyeshtuka na kurudi nyumbani kulala. Alipopanda kitandani usingizi mzito ulimchukua.
Watwana waliotumwa walimvua pete na kuondoka nayo kurudi nayo chini ya bahari, walipofika walimkabidhi Nargis. Aliipokea na kuishangaa ilivyokuwa imepoteza mvuto kwani ilikuwa imechakaa sana. Hakuamini kama ile ndiyo pete aliyomvalisha mumewe Thabit.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya kuichunguza sana aligundua ilikuwa yenyewe isipokuwa ilichezewa na kuondolewa nguvu za kijini. Baada ya kugundua hali ile roho ilimuuma sana mpaka machozi yakamtoka. Moyoni alijikuta akiwachukia wanadamu kwa kitendo cha kumchokonoa kila kukicha.
Aliishika ile pete na kumpelekea mama yake huku akilia.
“Mama hebu ona jinsi wanadamu wanavyonitafuta ubaya.”
“Mmh! Kazi ipo kama pete imekuwa hivi basi kweli wamefanya kazi kubwa.”
“Sasa tutafanyaje?”
“Irudishiwe nguvu, irudishwe kwa Thabit kisha aletwe hapa mara moja.”
Ilichukuliwa pete na kurudishiwa nguvu kubwa kuliko ya awali ambayo kila atakayeigusa kwa nia mbaya anaungua moto.
Pete ilikuwa ikiwaka mwanga mkali, kama una nia mbaya ukiutazama lazima ukupofue macho.
Pete ilikuwa nzito kubebeka hata Nargis ilimshinda kuinyanyua na kumuuliza mama yake.
“Mama mbona imekuwa nzito hivi?”
“Uzito wake ndiyo utakavyokuwa uzito wa mumeo, hataguswa na kitu chochote.”
“Sasa ataivaaje?’
“Hebu ibebe tena.”
Nargis alibeba na kushangaa kuona ikiwa nyepesi kama kawaida:
“Mbona imekuwa nyepesi?”
“Ilikuwa haijapoa sasa hivi ukimvisha mumeo hataguswa na kitu chochote.”
“Asante mama,” Nargis alimshukuru mama yake.
Baada ya zoezi lile waliitwa watwana na kutwa wairudishe pete kwa Thabit na kumchukua kurudi naye chini ya bahari kwa ajili ya kumtengeneza ili asiweze kuonekana kwa macho ya kibinaadamu. Safari ile aliyewaita watwana alikuwa Malkia Zabeda mama wa Nargis ambaye alitoa kauli nzito kuhakikisha hawafanyi mchezo siku zote atakacho watuma na kwenda kinyume ningegharimu maisha yao.
Walipofika kwake walilala kifudifudi ili kusikilia mke wa mfalme anataka kuwatuma nini. Lakini kabla hajawatuma walishtushwa na vilio vya wajakazi walioingia ghafla.
“Kuna nini?” Malkia Zabeda aliuliza kwa mshtuko.
“Hatari, “ walisema kwa pamoja huku wakijilaza kifudifudi mbele na malkia wa bahari.
“Ya nini?”
“Nyumba inawaka moto.”
“Nyumba inawaka moto! Nyumba gani?”
“Ya..ya..dada.”
“Nyumba ya mume wangu Thabit, baba Zumza?” Nargis aliuliza kwa mshtuko.
“Ndi...yo mwana wa mfalme.”
“Mungu wangu!” Nargis alisema huku akishika mikono kichwani.
“Hebu kwanza elezeni vizuri kuna nini?” Hailat dada yake Nargis aliuliza.
“
Tulikuwa ndani tumepumzika, baba Zumza alirudi mapema na siyo kawaida yake na kusema amechoka na kwenda chumbani kwake kupumzika. Ghafla walikuja kina Suunu ambao walisema umewatuma pete ya mumeo. Baada ya kuichukua waliondoka na kutuacha tukimuandalia kinywaji,” alisema mmoja wao.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Lakini ghafla tulianza kusikia mtikisiko mkubwa nje ya nyumba na baadaye nyumba ikaanza kutikisika ghafla tukaanza kuona moto kila kona kitu kilichotufanya tutoke mbio kuokoa maisha yetu.”
“Mmh! Wakati nyumba inaungua mume wangu alikuwa wapi?” Nargis aliuliza kwa hofu.
“Ndani amelala.”
“Mungu wangu mume wangu atakufa, mama watume wakamuokoe.”
Watwana waliokuwa bado wamelala kifudifudi walitumwa kwenda kumuokoa Thabit, baada ya amri ile walitoweka mara moja na kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Thabit.
Walipofika eneo la nyumba walishangaa kukuta bahari, hali ile iliwashtua sana na kujikuta
wakijiuliza labda wamekosea kila waliporudia ramani yao eneo lilikuwa lilelile.
Walijikuta wakiulizana wenyewe:
“Jamani tumekosea wapi?”
“Hatujakosea hapo kwenye bahari ndipo kwenye hiyo nyumba kwani nyumba tuliyofikia kabla ya kuingia ndani si hiyo hapo pembeni
ya bahari?” mmoja alisema.
“Sasa tutafanyaje kama hakuna nyumba tuliyotumwa na mume wa mwana wa mfalme tutamuona wapi?”
“Jamani ile si bahari basi tuingie ndani ya maji ili tujue ndani kuna nini.”
“Poa.”
Walikubaliana na kuteremka ndani ya ile bahari, walipoyagusa maji wote walitoka haraka kila mmoja akipiga kelele za maumivu ya kuungua na moto.
“Motooo!”
Bahari ilikuwa inaunguza walisimama huku kila mmoja akionesha majeraha ya moto.
“Jamani hii ngoma nzito turudishe taarifa.”
“Hatuna jinsi.”
Walikubaliana kurudi chini ya bahari kurudisha taarifa ya hali halisi waliyokutana nayo sehemu yenye nyumba ya Thabit.
Walirudi chini ya bahari kurudisha taarifa, walipofika walimkuta Nargis akiwasubiri kwa hamu kutaka kujua wamefikia wapi
badala ya kurudi bila mumewe.
“Vipi?”
“Hali ni mbaya.”
“Kuna nini?”
“Nyumba haionekani zaidi ya bahari.”
“Bahari imefanya nini?”
“Sehemu yenye nyumba kuna bahari kubwa sana.”
“Sasa kwa nini msiingie ndani?”
“Yaani hali inatisha tumeingia tumeungua vibaya, bahari ina maji ya moto ajabu,” walionesha majeraha.
“Mmh! Sasa nimeelewa,” malkia Zabeda alisema.
“Nini mama?” Nargis aliuliza huku machozi yakimtoka.
“Wametuwahi.”
“Kivipi mama?”
“Inaonesha jinsi gani aliyepanga mpango wa kumchukua mumeo amefanikiwa. Tulitakiwa tumchukue badala ya kuichukua pete tu lakini tumechelewa.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mama sikubali... sikubali nitakufa na mtu.”
“Lazima tujipange la sivyo safari hii tutapotea kabisa.”
“Sasa nitafanyaje?” Nargis aliuliza huku machozi yakimtoka.
“Labda dada yako akusaidie kwa vile wewe huwezi kwenda huko kwa sasa.”
“Mama mimi siendi kokote nilimueleza toka zamani akawa mbishi juu ya wanadamu, mimi nawafahamu vizuri kuliko yeye anayekurupukia mambo.
Wanadamu tunawapenda tu lakini ni viumbe wabaya kuliko hata nyoka mwenye sumu kali. Kama walishindwa kuishi katika bustani ya edeni waliyopendelewa na Mungu wataweza vipi kukaa na viumbe wengine.
“Ningekuwa mimi ningemuulia mbali tena mdogo wangu una bahati umepata watoto ulikuwa ukiwatafuta. Muulie mbali uachane na
maisha ya mashaka, wapo majini wazuri kuliko Thabit wanaokupenda Zahal au Mehoob wapo tayari kukuoa hata leo.”
“Dada bado hujanishawishi yule ni mume wangu hivyo siwezi kumuua kwa ajili ya yaliyotokea, vilevile hakuna mwanaume wa kijini atakayemshinda uzuri mume wangu Thabit.
Najua aliyefanya vile ni mwanamke, kwani siku zote wanawake tumekuwa ndiyo chanzo cha
matatizo.
Hao wanadamu wasingetoka katika bustani ya edeni bila sisi wanawake ambao ndiyo chanzo cha kufukuzwa kwao.
“Hata kama hamtanisaidia nitapigana peke yangu hata nikifa kwa ajili ya kupigania haki yangu siogopi kitu.”
“Ukifa nani atakulelea wanao?” dada yake alimuuliza.
“Mtavyowafanya mtajua nina imani nao wakikua watalipa kisasi kwa atakayeniua mama yao.”
“Nargis mwanangu, inavyonekana watu tutakaopambana nao wamejizatiti. Kama wameweza kuua nguvu ya pete na kuingia kwenye nyumba tuliyoitengeneza, basi kazi ipo tunatakiwa kuongeza nguvu.”
“Ninyi piganeni mimi simo, siwezi kuumia kwa kitu kisicho na faida, atajua mwenyewe atakavyofanya. Kwa nini kila siku tuwe tunapambana na wanadamu hamuoni nao wana akili pengine wameshatujulia, ndiyo maana wanafanya wanavyotaka,” dada yake Hailat alisema kwa uchungu.
“Mama naomba mnisikilize kwa makini, nina miaka minne ya kuwa huku, naomba mniachie kila kitu, sihitaji msaada wenu muda wangu ukifika nitapambana mwenyewe.
Tusije tukakosana bure kwa jambo linalonihusu mwenyewe,” Nargis alisema.
“Hilo ndilo neno hata mimi nakuunga mkono,” dada yake aliunga mkono kauli ya mdogo wake.
“Dawa iliyopo ni kuiharibu mali yake ili kumtia umaskini,” mama yao alitoa wazo.
“Mama hiyo siyo dawa, Thabit hana kosa lolote zaidi ya huyo aliyefanya mchezo ule,” Nargis alimtetea mumewe.
“Sawa lakini tukimtia umaskini, lazima yule mwanamke atamkimbia na wewe utapata nafasi ya kumpata mume wako.”
“Una uhakika gani kama huyo mwanamke atamkimbia, sitaki kuharibu chochote kwenye mali ya Thabit. Sitaki apate tatizo lolote ila nitahakikisha anarudi mikononi mwangu.”
“Sawa lakini tukimtia umaskini lazima yule mwanamke atamkimbia na wewe kupata nafasi ya kumpata mume wako.”
“Una uhakika gani kama huyo mwanamke atamkimbia, sitaki kuharibu chochote kwenye mali ya Thabit. Sitaki apate tatizo lolote ila nitahakikisha anarudi mikononi mwangu kwa jasho na damu.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Sawa, kwa vile umeamua mwenyewe hatutaingilia uamuzi wako,” mama naye aliunga mkono.
Walikubaliana kuliacha lile jambo mpaka muda wa Nargis kurudi duniani na kujua watafanya nini. Baada ya Nargis kwenda chumbani kwake mama na dada yake walikuwa na kikao cha faragha kuhusiana na jambo lile ambalo Malkia Zabeda lilimuumiza sana akili kutokana na kumpenda sana mtoto wake wa mwisho Nargis.
“Mwanangu sasa tutafanyaje suala la mdogo wako?”
“Mama mimi msimamo wangu ni uleule, kama upo tayari nikamuulie mbali baba Zumza ili tumalize kero zote.”
“Hapana tutafute njia nyingine kwa vile unamjua vizuri mdogo wako kifo chochote na mumewe tutazua ugomvi mkubwa hata kupoteza uhai wa mmoja wenu.”
“Ndiyo maana mimi nimejitoa kwenye jambo hili najua lina lawama baadaye.”
“Kwa nini usitekeleze mpango nilioupanga?”
“Mpango gani?”
“Wa kumtia umaskini Thabit ili mwanamke aliyenaye amkimbie kwa vile najua amempenda kwa ajili ya mali kisha mdogo wako ampate mumewe.”
“Mamaaa! Bado tatizo litakuwa palepale.”
“Kwa nini?”
“Hata tukimrudisha, kwa vile wataendelea kuishi duniani tatizo lazima litajirudia huenda hilo likawa kubwa kuliko yaliyotangulia.”
“Wee fanya kwanza nilivyokutuma kilichobaki niachie mimi.”
“Sawa basi kazi hiyo nitaifanya usiku wa kesho ili akiamka siku ya pili akute amerudi katika umaskini.”
“Tena itatusaidia kwa vile miaka minne atamkuta amechoka kama mpira wa makaratasi.”
“Sawa mimi nitatekeza ulichonituma.”
“Ukifanya hivyo utanifurahisha sana, kazi itakayobaki niachie mimi,” Malkia Zabeda alifurahi mwanaye mkubwa kukubali kumsaidia mdogo wake.
Baada ya kikao kile cha faragha waliendelea na mambo mengine huku mpango ukiwa wa siri ambao Nargis hakuujua.
***
Baada ya Subira mipango yake kwenda kama alivyotaka na kufanikiwa kumteka kimapenzi Thabit bila kujua, aliianza siku kwa Thabit.
Alimuandalia kifungua kinywa kitamu kilichochanganywa na dawa ili asione tofauti ya mapishi ya kijini na kibinaadamu.
Baada ya kufungua kinywa waliondoka pamoja hadi kazini kama mke na mume. Thabit aliingia katika ofisi yake na kumuacha Subira akifanya majukumu yake kama msaidizi. Akiwa anaendelea na kazi alikumbuka kumueleza mzee Mukti kuhusu mipango ilivyokwenda.
Baada ya kumueleza hatua waliyofikia mganga naye alimueleza kuwa ameota ndoto iliyomtisha sana kuwa mali zote za Thabit zinateketea na moto na Thabit kawa maskini anayetembea mjini akiomba.
“Mungu wangu! Hilo si tatizo?” Subira alishtuka.
“Ni kweli tatizo, lazima usiku wa manane tuzunguke sehemu zote kwenye mali za mpenzi wako kuzizindika kwa vile inaonesha hali ya hatari ipo mbele juu ya mali hizo.”
“Sawa mzee wangu.”
Walikubaliana usiku wafanye zindiko kwenye maduka yote ya Thabit kabla kitu kibaya hakijatokea. Subira alifanya kazi moyo wake ukiwa umejaa hofu, alifikiria kumweleza Thabit ndoto ya mganga lakini alihofia kuulizwa ilikuwaje akajuana na mganga. Alitamani usiku uingie upesi ili wakaifanye kazi ile kabla tatizo halijatokea.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Majira ya saa saba usiku mganga Mukti Buguju aliongozana na Subira katika maduka ya Thabit kuyafanyia zindiko kabla tatizo aliloota halijatokea. Alianza na maduka mawili ya Kariakoo yaliyokuwa karibukaribu. Mzee Mukti na wasaizidi wake wakiwa katika vazi la shuka nyekundu waliyojifunga chini mgongo wazi na vilemba vyekundu. Mkononi alishika usinga huku msaizidi wake akiwa ameshika beseni lenye dawa.
Mganga alichovya usinga kwenye maji ya dawa na kumwagia kuzunguka ofisi kisha aliingia ndani na kufanya dawa zake kila kona na kutoka. Baada ya kumaliza duka moja alikwenda la pili na kufanya aliyofanya duka la kwanza. Baada ya kumaliza zoezi lile walipanda gari kuelekea Posta kwenye duka lililobakia.
Mzee Mukti hakuvua nguo za kazi na vijana wake mpaka maeneo ya Posta, walipokaribia jengo lenye duka la Thabit walishtuka kuona moto ukiwaka.
“Ha! Jengo linaungua,” Subira alipiga kelele.
“Kwani tunakwenda jengo gani?” mganga aliuliza.
“Hilo linaloungua.”
“Mmh!” mganga aliguna na kufanya Subira kushtuka.
“Vipi mbona unaguna?”
“Tunachelewa,” alisema mganga kwa sauti ya kukata tamaa.
“Tumechelewa nini?” Subira aliuliza.
“Ule moto si wa kawaida, kwani duka lake lipo wapi?”
“Pale moto unapowaka.”
“Tungejua tungeanza zoezi letu mapema, inaonesha ile ndoto leo ndiyo siku yake ya kuteketeza mali za Thabit ili arudi katika hali ya umaskini,” alisema mzee Mukti.
“Mungu wangu!” Subira alishika mikono kichwani.
“Majini wana hasira baada ya kushindwa kumrudisha Thabit kwao wameamua kuharibu mali zake ili arudi katika umaskini.”
“Kwa hiyo na yale maduka nayo yatateketea?”
“Yale yatakuwa salama hawataweza kufanya chochote kwa vile tumewahi tungechelewa ingekuwa kilio cha kusaga meno.”
Wakati wakizungumza walishangaa moto kuzimika ghafla na kujikuta wote wakishangaa.
“Mmh! Mbona moto umezimika ghafla?” aliuliza subira na kumfanya mzee Mukti naye kushangaa.
“Hii ajabu!”
Waliteremka kwenye gari na kuelekea kwenye duka lililokuwa sehemu ya chini, kama kawaida alianza kufanya dawa zake kwa nje ya duka kisha aliingia ndani. Walipoingia ndani walishtuka kukuta vitu vyote vimeteketea kwa moto. Ajabu ilikuwa vilivyoungua ni vitu vyote vya dukani tu lakini ndani hakukuwa na dalili za moto kuwaka.
“Mungu wangu mbona maajabu haya,” Subira alisema huku akishika mikono kichwani.
“Ule moto ni wa kijini ambao huaribu kilichokusudiwa tu.”
“Jamaniiii!” Subira alisema kwa sauti ya kukata tamaa.
“Huku tumechelewa, hatuna jinsi turudini nyumbani.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana waliingia kwenye gari na kurudi nyumbani.
***
Subira ilibidi akae kimya kuhusiana na tukio zito la usiku ule huku akiwa haamini kama kweli moja ya duka la Thabit lilikuwa limeunguzwa na moto wa kichawi. Walilala mpaka asubuhi ili asikie nini kimetokea au ilikuwa ndoto na wala hakuna kilichotokea.
Asubuhi wakiwa bado wapo kitandani simu iliingia, Thabit aliichukua na kuweka sikioni na kupokea.
“Haloo Juma,” alikuwa msimamizi wa duka la Posta.
“Za asubuhi bosi.”
“Nzuri, kwema.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Si kwema bosi.”
“Kuna nini?”
“Duka limeungua lakini moto wake wa ajabu.”
“Mungu wangu! Jengo zima limeungua?” Thabit alitaharuki.
“Siyo jengo lote ni duka letu tu.”
“Hakuna hata kimoja kimepona.”
“Kumebakia majivu tu.”
“Na maduka ya mjini?”
“Huko sijui.”
”Subiri.”
Alikata simu na kupiga mjini, baada ya kuita kwa muda ilipokelewa.
“Haloo bosi.”
“Sadiki upo wapi?”
“Kazini.”
“Kwema?”
“Kwema, tena bosi lile kontena nasikia linatua kesho usiku, nina imani tutatumia mwezi mzima na kazi ya kupakua na kupanga vitu madukani.”
Kutokana na nguvu za kijini zilizowekwa na jini Nargis kwa mumewe kila kukicha utajiri wa Thabit ulikuwa ukikua kutokana na kuwa karibu kiutendaji na majini waliosimamia mali zake chini ya usimamizi wa mkewe.
Zaidi ya maduka yale matatu, alikuwa amepanga kufungua maduka makubwa ya vyakula kila wilaya pia duka kubwa sana maeneo ya kituo cha daladala cha Mwenge, lingine kubwa kuliko yote City Center. Alikuwa ameagiza kontena kumi za bidhaa mbalimbali. Kati ya maduka hayo matatu la City center matano, la Mwenge matatu na mengine mjini.
Ndoto ya Nargis kuhakikisha Thabit anakuwa tajiri mkubwa dunia hiyo alipanga atakaporudi duniani na kuishi na mumewe kama mwanadamu wa kawaida basi wawe na maisha mazuri. Kila kukicha alihakikisha utajiri wa Thabit unazidi kuongezeka na si kupungua.
“Hakuna tatizo lolote.”
“Hakuna tupo shwari.”
“Sawa.”
Alikata simu na kupiga duka lingine na kukuta nako hali shwari, alirudia kupiga tena Posta na kupokelewa.
“Naam bosi.”
“Kuna mabadiliko yoyote?”
“Hakuna.”
“Nakuja.”
“Sawa.”
Alikata simu na kuteremka kitandani kitu kilichofanya Subira aulize.
Mpenzi mbona umeamka haraka hivyo?” Subira alijifanya hajui kitu.
“Kuna tatizo.”
“Tatizo gani?”
“Sijajua ila nimeambiwa niende duka la Posta.”
“Twende wote,” Subira alisema huku akinyanyuka kitandani na kumfuata Thabit, walikwenda bafuni kuoga na kutoka pamoja hata kifungua kinywa hawakunywa siku hiyo.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Waliingia kwenye gari na kuelekea Posta, walikwenda hadi eneo la tukio na kukuta nje ya jengo kazi zikiendelea kama kawaida hakukuwa na mshtuko wowote kama kuna tukio kwani jengo lilikuwa katika hali ya kawaida hakukuwa na dalili zozote za moto kutokea. Aliwakuta wafanyakazi wake zaidi ya arobaini wakiwa ndani ya jengo wakiwa wameshika tama na wengine kutoka machozi.
Walishangaa kukuta ndani ya duka kumejaa jivu vitu vyote vya mamilioni ya fedha vikiwa vimeteketea. Ilikuwa ni hasara kubwa kwani ilikuwa ni wiki tu aliingiza dukani mali ya zaidi ya milioni mia sita na nusu. Alijisikia miguu kumwisha nguvu lakini alijikaza na kujiuliza kile ni kitu gani, kwani kuta na sakafu za duka zilikuwa hazioneshi dalili zozote za kuungua na moto ulioteketeza mali ya mamilioni.
Wote walikuwa wapo kwenye usiku wa giza kasoro Subira alikuwa akijua kila kitu na sababu ya kuwa vile. Alimshukuru kimoyomoyo mzee Mukti kwani kama angechelewa maduka yote yangeteketea na kuwa kilio cha kusaga meno. Kutokana na dawa alizolishwa Thabit na Subira alijikuta akisahau kabisa chanzo cha mali ile ni mkewe jini Nargis.
“Hii si bure lazima kuna mkono wa mtu,” alisema mmoja wa wafanyakazi.
“Wameona sisi ndiyo tunafanya vizuri hivyo lazima wametuendea mbali, moto gani usiounguza sehemu yoyote zaidi ya bidhaa za dukani wanataka tukale wapi?” msichana mmoja alisema huku akili.
“Nendeni nyumbani ili nitafakari kisha kesho nitawajulisha kinachoendelea, kuna kontena kumi za bidhaa zinaingia kesho usiku ambazo zilikuwa za maduka mengine nitapunguza baadhi ya makontena na kuleta hapa ili muendelee na kazi,” Thabit aliwaambia wafanyakazi wake waliokuwa wamechanganyikiwa.
“Tutashukuru bosi,” walijibu kwa pamoja.
Subira muda wote alikuwa akilia kitu kilichomfanya Thabit ambembeleze.
“Mpenzi nyamaza tutarudisha kila kilichopotea.”
“Lazima tuhangaike yasije tokea tena,” Subira alitoa wazo mbadala.
“Tutafanya hivyo.”
“Basi tumtafute mtaalamu wa kulinda mali zetu.”
“Tutamtafuta wapi?”
“Mi namjua.”
“Basi tutakwenda.”
“Tena leo hiihii.”
“Hakuna tatizo, twende tukaangalie sehemu nyingine, maana mpaka sasa moyo wangu hauna amani. Moto wa leo umenipotezea zaidi ya milioni mia nane.”
Kusikia vile Subira aliangua kilio na kumfanya Thabit aingie kazi ya kumbembeleza.
“Mpenzi nyamaza japo zimepotea hizo bado hatutatetereka.”
“Naomba jioni twende kwa mtaalamu ili alinde mali zetu.”
“Lazima tufanye hivyo ni wapi?”
“Kigamboni.”
“Itabidi tuwahi kwenda.”
“Tuondoke saa kumi na mbili.”
Walikubaliana saa kumi na mbili kwenda Kigamboni kwa mganga, kukubali kwenda kwa mganga kulimfanya Subira kufurahia kuweza kumpeleka Thabit bila kujua na yeye kumaliza mambo yake ya kumdhibiti ikiwemo ndoa ya haraka.
Baada ya kukubaliana Subira alimpigia simu mzee Mukti kumjulisha mpango wa kumpeleka kwake umefanikiwa.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Niambie binti,” alisema mzee Mukti baada ya kupokea simu.
“Babu kila kitu kimekwenda vizuri, jamaa kakubali kuja hivyo maliza kila kitu.”
“Hilo si la kuniambia bali ndiyo nilichokuwa nikikiomba usiku na mchana, mkitoka hapa utaniambia ndoa itavuma kwa kasi kama vumbi kwenye upepo mkali.”
“Yaani nitashukuru mzee wangu.”
“Kama amekubali mwenyewe jua amekwisha.”
“Basi jioni wageni wako.”
“Karibuni sana.”
Baada ya kukubaliana na mganga Subira alijipanga jioni kumpeleka Thabit ili akammalize kabisa.
CHINI YA BAHARI
hini ya bahari jini Hailat dada wa Nargis alirudi akiwa amechoka sana mwili ukiwa na mabaka ya moto. Mama yake alipomuona alishtuka na kutaka kujua mwanaye safari aliyokwenda amekutana na nini kilichomfanya aumie vile.
“He! Vipi tena mwanangu?”
“Mama hatari, wametuwahi!” alisema huku akijiangalia makovu ya moto.
“Kivipi?”
“Wamewahi kuzikinga mali zao japo tumefanikiwa kuharibu duka moja ambalo ndilo kubwa. Lakini mengine wameyakinga yanaonekana kama bahari nilipojaribu kuingia niliungua, bila uwezo wa kijini ningekufa kifo kibaya.
Mama sikubali nami naingia katika vita hii kuhakikisha namuondoa duniani Thabit na mganga wake sijali atakachokifanya Nargis, nipo tayari kwa lolote,” Hailat alisema huku akimwaga machozi ya hasira.
“Hebu tulia basi kazi hii nimekutuma mimi, nataka unisikilize mimi si mtu mwingine.
Kama umefanikiwa kuharibu mali moja tutajipanga kuharibu zote. Kuna kitu kimeingia kwenye akili yangu muda si mrefu. Kuna mali ya mabilioni ya Thabit ipo baharini inapita usiku huu utakwenda kuimaliza yote, hakikisha linabaki jivu.
Kwa pigo hilo tutakuwa tumemmaliza na mali zake zote zitakazopitia majini tutaziharibu, lazima atafilisika tu,” Malkia Zabeda alipanga kuyateketeza makontena yote kumi ya mali za Thabit na mali zote zitakazopita baharini.
“Sawa mama, kwa kazi hii sina haja ya kupumzika wala kusikilizia maumivu ya moto, tena nitaifanya mwenyewe bila kumshirikisha mtu,” Hailat alikubaliana na mama yake.
Hailat pamoja na maumivu ya moto lakini alifurahia kuziteketeza mali zote za Thabit zilizokuwa zikipita baharini usiku ule.
Alipanga kutopumzika na kuifanya usiku uleule ili asubuhi kila kitu kiwe kimekwisha. Alijipanga kuifuata meli yenye makontena ya bidhaa za watu na kuharibu za Thabit tu.
Hakutaka kuwashirikisha majini wengine kwa kuogopa taarifa kumfikia Nargis na kuharibu mpango mzima.
Aliamini hasara ya kuteketeza mali zile lazima zingemtia umaskini kwa kujua kwa mtindo ule lazima atayumba kifedha kwa vile wangeendelea kuharibu vitu vyote vitakavyopita njia ya bahari. Alihakikisha kila kona atakayoitumia kuingiza mali zake wanaziharibu.
***
Majira ya saa kumi na mbili jioni Thabit na Subira walivuka kivuko cha Feri mpaka Kigamboni. Baada ya kuvuka waliendelea na safari yao kuelekea Mji Mwema kwa mganga Mukti Buguju. Baada ya muda mfupi walifika nyumbani kwa mganga. Kwa vile Subira aliishamtaarifu kuwa wanakwenda walipokewa kwa heshima zote.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Hakukuwa na haja ya kukaa foleni, waliingizwa moja kwa moja chumba cha matibabu.
“Karibuni sana.”
“Asante,” waliitikia pamoja.
“Karibu mzee,” mzee Mukti alimkaribisha Thabit aliyeoneka kapendeza kwa fedha.
“Asante mzee wangu.”
“Jamani mna tatizo gani?” mzee Mukti alijifanya kama ndiyo siku ya kwanza kuonana na watu wale.
“Mzee wangu tuna tatizo, kuna vitu vimetutokea leo asubuhi ambavyo vinaonekana si vya kawaida,” Subira alianza kutoa maelezo.
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment