Simulizi : Nilioa Jini Nikamsaliti
Sehemu Ya Tatu (3)
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Karibuni sana.”
“Asante,” waliitikia pamoja.
“Karibu mzee,” mzee Mukti alimkaribisha Thabit aliyeonekana kapendeza kwa fedha.
“Asante mzee wangu.”
“Jamani mna tatizo gani?” mzee Mukti alijifanya kama ndiyo siku ya kwanza kuonana na watu wale.
“Mzee wangu tuna tatizo, kuna vitu vimetutokea leo asubuhi ambavyo vinaonekana si vya kawaida,” Subira alianza kutoa maelezo.
“Eti mzee kuna nini?” mzee Mukti alimgeukia Thabit hakutaka Subira azungumze.
“Mzee wangu leo nimetokewa na jambo la ajabu baada ya moto wa ajabu kuteketeza duka langu lenye thamani ya mamilio ya fedha. Kwa kweli mpaka sasa nimechanganyikiwa sana sijui tatizo lile linatokana na nini.”
Mzee Mukti alijifanya akipiga ramli ya uongo kwa vile kila kitu alijua kisha alisema:
“Hapa panaonesha kuna kijicho kwa watu wasiopenda maendeleo yako ambao ndiyo wamefanya mchezo huu.”
Ilibidi atengeneze uongo kuogopa kumwambia ukweli kuwa aliyefanya vile ni jini anayetaka kumtia umaskini baada ya kuchukuliwa mumewe. Aliamini angemwambia vile lazima angekumbuka ahadi aliyomuahidi mkewe jini Nargis kwamba hatamsaliti akiwa mbali naye.
“Nani aliyefanya hivyo?” Thabit alitaka kujua.
“Kwa kweli hapa kuna giza hawaonekani vizuri, lakini najitahidi kuliondoa giza ili tuwajue.
“Kwa hiyo shida yao nini?”
“Kutaka kukurudisha katika umaskini.”
“Kwa hiyo mzee utatusaidiaje?”
“Kwa vile tatizo nimeshaliona nitazindika mali zako zote pamoja na nyumba yako kuhakikisha hupotezi tena mali zako. Na zoezi lifanyike usiku wa leo pia nitakupeni dawa za kuwalinda wote na watu hao wabaya.”
“Na mali zilizopotea zitapatikana?”
“Ile haitapatikana ila iliyopo haitapotea tena.”
“Mmh! Nitashukuru.”
“Kwa hiyo kuna dawa nitawapa mnywe na kuoga pamoja, kisha nitawapa zindiko.”
“Hakuna tatizo.”
Baada ya kusema vile mganga aliandaa tiba ili baadaye waende kwenye kazi ya kuzindika maduka kwa kulashia kwa vile kazi alikwisha imaliza toka jana yake usiku.
Mzee Mukti aliwaandalia dawa ambayo ilikuwa ya aina mbili moja ya kumlinda Thabit na majini na nyingine kumsukumia kwa Subira ili ndoa iwahi mapema.
Baada ya zoezi lile waliondoka mpaka kwenye maduka na mzee Mukti alijifanya yupo bize kumbe uongo alikuwa akipaka maji tu. Baada ya zoezi ambalo halikuchukua muda mrefu walirudi nyumbani. Mzee Mukti siku hiyo alilala nyumbani kwa Thabit na kuongeza nguvu kwenye zindiko lake la awali usiku uleule.
Baada ya zoezi lake alipewa chumba kizuri akalala, katikati ya usingizi alishtuliwa na ndoto iliyomtisha, aliota bahari yote ikiwaka moto. Alijiuliza ndoto ile ina maana gani, kwani kila alipoangalia kwenye rada zake hakuona kitu kingine zaidi ya moto mkubwa umetanda baharini.
Baada ya kushindwa kutambua ndoto ile aliachana nayo na kuendelea kulala akisiburi taarifa yoyote kutokana na njozi yake.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Usiku mkubwa jini Hailat dada wa Nargis pamoja na uchovu alitoka chini ya bahari na kwenda kwenye meli iliyokuwa imebeba Makontena ya bidhaa mbalimbali yakiwemo ya Thabit. Alipofika aliyachagua ya Thabit na kuyawasha moto wa kijini na kurudi chini ya bahati kumpelekea taarifa mama yake. Alipofika alimueleza mama yake kazi aliyomtuma aliifanya.
“Vipi hukukutana na vikwazo?” mama yao Malkia Zabeda aliuliza.
“Walaa, kazi ilikuwa nyepesi kuliko ya madukani.”
“Basi kapumzike mwanangu na jambo hili libakie siri yetu.”
“Hakuna tatizo.”
“Ila bado kuna kazi nyingine nitakupa.”
“Juu ya Thabit?”
“Ndiyo, nina imani hiyo ukiifanya japo utakutana na upinzani mkubwa lakini utaifanikisha. Mdogo wako Nargis kwa sasa hawezi kutuelewa lakini baadaye atatushukuru.”
“Na kuhusu yule mganga?”
“Achana naye, huyo atuhusu alichofanya ni kazi.”
“Nilitaka kula naye sahani moja hawezi kunitia makovu ya ukubwani.”
“Achana naye inaweza kumbumbulua Nargis.”
“Sawa mama nimekuelewa.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana waliagana kila mmoja aliingia chumbani kwake kulala.
Kama kawaida meli ilitia nanga katika bandari ya Dar es Salaam, baada ya taratibu zote mizigo ilianza kupakuliwa na kuwekwa sehemu kwa ajili ya kuchukuliwa na wenyewe. Vijana wa Thabit nao walikuwepo na magari makubwa ya kubebea mizigo ili kuisambaza.
Magari yalibeba mizigo kama kawaida na kuisambaza kwenye maduka yote ikiwemo kutenga makontena mawili kwa ajili ya duka la Posta lililounguzwa vitu vyake na moto wa ajabu. Baada ya kufikishwa zoezi la kufungua makontena lilianza mara moja. Msimamizi alishtuka kuona majivu ndani ya kontena bila bidhaa zilizoagizwa.
Hakuamini macho yake, alifungua lingine hali ilikuwa ileile, ilibidi apigiwe simu Thabit kuelezwa kilichoonekana kwenye kontena badala ya bidhaa walikutana na majivu kama yale yaliyokutwa dukani kwake.
Taarifa ile ilimfanya Thabit kwenda haraka kujionea, alipofika alioneshwa mali iliyoteketea kwa moto wa ajabu. Lilikuwa pigo jingine, hakuamini alikwenda kwenye makontena yote hali ilikuwa ileile. Ilikuwa mali ya fedha nyingi sana aliamini kabisa wamemmaliza.
Kutokana na mshtuko alianguka chini na kupoteza fahamu, ilibidi akimbizwe hospitali. Alipimwa vipimo vyote lakini ugonjwa haukuonekana. Upande mmoja wa mwili wake ulipooza ghafla. Lilikuwa pigo mujarabu lililomchanganya sana, Subira naye alichanganyikiwa na kumpigia simu mzee Mukti na kumueleza kilichotokea.
“Mzee wangu mbona kila siku matatizo yanazidi?”
“Kilichotokea kilikuwa nje ya uwezo wangu, ndoto ya kuungua vitu ndani ya maji niliiona lakini sikujua ilikuwa ina maana gani.”
“Kwa nini hukuzuia?”
“Ilikuwa vigumu kama ningeingia kwenye ufalme wao wa maji kwa ajili ya vita nisingerudi salama, wangenipoteza kwa njia yoyote.”
“Sasa tutafanyeje maana hali na mpenzi wangu ni mbaya sana?”
“Atapona ni mshtuko tu.”
“Nini hatima yetu?”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Ulichelewa kunijulisha tungeweza kuanza mchakato mapema ili kuokoa mali zenu.”
“Mmh! Nitaolewa kweli?”
“Utaolewa, kuna dawa utaletewa na kuitumia kumpa itamsaidia.”
“Sawa, na mali iliyobakia itasalimika kweli?”
“Ile ipo salama wala usihofu.”
“Sawa basi nasubiri.”
Mzee Mukti ilibidi aangalie ugonjwa wa Thabit tatizo nini, jibu lilimtisha kuonesha bila kazi ya ziada Thabit atakuwa mlemavu milele. Aliamini dawa zake zote zisingeweza kumtibu ilikuwa lazima asafiri kwa siku mbili ili afuate dawa ambayo nayo ilikuwa bahati nasibu japo ilionesha kila dalili za kulemaa kwa Thabit.
Ugonjwa wa Thabit ulifanya iwe furaha kwa Hailat na mama yake.
“Mama Thabit kwisha.”
“Kwa nini?”
“Kazi uliyonituma imeleta matokeo mazuri.”
“Imekuwaje?”
“Amepooza upande mmoja si wa kupona leo kesho.”
“Sasa tuone kama yule mwanamke ataendelea kuwa naye.”
“Halafu yule mganga anajitia kiherehere kumtibu, tumshughulikie nini?”
“Mwache amtibu, lakini atachukua muda kupona na muda wote huo lazima yule mwanamke atamkimbia.”
“Kama hivyo sawa.”
Nargis akashangaa kuona mama na dada yake wakinyamaza ghafla baada ya kumuona. Ilimshtua sana na kuamini kuna kitu juu yake walikuwa wakimteta. Aliwapita bila kuwasemesha lakini moyoni alijawa na wasiwasi juu ya kikao kile cha faragha cha mama yake na dada yake. Alizunguka na kujificha nyuma ya mlango.
Alichokisikia roho ilimuuma sana na kuona jinsi gani familia yake imeamua kwenda kinyume na makubaliano juu ya mumewe Thabit kumuacha kama alivyo. Hakutaka kusema chochote alijipanga kurudisha kila kitu kilichopotea kwa mpenzi wake bila kujua kama akirudi duniani atakubaliwa na mumewe au atatoswa.
Alijipanga kuondoka usiku kwenda kurudisha kila kitu cha mumewe kilichopotea kuanzia dukani mpaka kwenye makontena. Naye aliamua kufanya kwa siri ili familia yake wasijue kinachoendelea. Usiku baada ya kuwaweka vizuri wanawe alitoka chini ya bahari na kwenda moja kwa moja nyumbani kwake.
Alipokaribia kwenye nyumba ya Thabit aliona bahari, japo moyo ulimuuma nyumbani kwake kuwa kwenye hali ile.
Alijaribu kuingia katika umbile la kijini joto la maji ya moto lilimzuia, akalazimika kurudi katika umbile la kibinadamu na kuteremka kwa mbali kidogo. Aliweza kuiona nyumba yake.
Alitembea taratibu kuelekea kwenye nyumba ile, alipokaribia moto mkubwa ulionekana ukiizunguka nyumba yake. Alijua nyumba imezindikwa ili yeye na majini wote wasiingie katika nyumba ile. Kwa vile shida yake ilikuwa kurudisha mali iliyopotea aliondoka hadi dukani.
Kama kawaida alijirudisha katika umbile la kijini na kuruka kwenda sehemu ya maduka. Alipokaribia alijirudisha katika umbile la kibinadamu na kuweza kusogea kwenye duka. Aliusogelea ukuta wa duka na kuushika, akafumba macho na kuvivuta vitu vilivyopotea.
Baada ya muda aliviona vitu vyote vilivyokuwemo kabla, alivivuta taratibu mpaka kila kitu kilirudi kama zamani. Alitabasamu kuona mali ya mpenzi wake imerudi na duka lilijaa kama mwanzo.
Baada ya kumaliza zoezi lile alijirudisha katika umbile la kijini na kuruka hadi kwenye makontena yote na kuyashika kila moja na kurudisha kila kitu. Baada ya hapo alikwenda hospitali alipokuwa amelazwa mumewe.
Kwa vile hakukuwa na zindiko aliingia katika umbile la kijini na kuwapita watu bila kumuona.
Baada ya kuingia kwenye wodi aliyokuwa amelezwa mumewe, wakati huo hakukuwa na mtu mwingine chumbani.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Alimuangalia kwa huzuni na kuona ubaya wa viumbe kutaka kumuua mumewe bila sababu.
Akiwa amelala kitandani alipotaka kumshika alipigwa na shoti kama umeme na kumrusha upande wa pili. Alijua tayari na mumewe amezindikwa ili asiwe naye karibu. Hakuondoka alisimama pembeni ya Thabit aliyekuwa amelala hajitambui.
Kutokana na uchungu moyoni alijikuta akilia na machozi kumtoka, kwa vile alikuwa ameinama machozi yake yalitua kwenye paji la uso wa mumewe. Alishangaa kumwona akibadilika rangi mchanganyiko huku mwili ukitikisika kisha alirudi katika hali ya kawaida na mwili ulitulia.
Itaendelea wiki ijayo.
Alimuona Thabit akifumbua macho na kupepesa kasha alijinyoosha kuonesha yupo sawa. Nargis alitaka kumsemesha lakini hakutakiwa kufanya vile kwa vile sicho kilichompeleka na muda ule.
Aliamini kila alichokipanga kimekwenda kama alivyotaka aligeuka na kuondoka na kumuacha mumewe akiwa hajambo na kuamini taarifa atakayoisikia juu ya mali zake kurudi atamuongezea furaha.
Kwa vile alikuwa ametoka usiku sana aliwahi kurudi chini ya bahari kabla familia yake haijagundua kitu.
Kutokana na uchungu moyoni alijikuta akilia na machozi kumtoka, kwa vile alikuwa ameinama machozi yake yalitua kwenye paji la uso wa mumewe. Alishangaa kumwona akibadilika rangi mchanganyiko huku mwili ukitikisika kisha ilirudi yake ya kawaida na mwili ulitulia.
Alimuona Thabit akifumbua macho na kupepesa kisha alijinyoosha kuonesha yupo sawa. Nargis alitaka kumsemesha lakini hakutakiwa kufanya vile kwa vile sicho kilichompeleka muda ule.
Aliamini kila alichokipanga kilikwenda kama alivyotaka aligeuka na kuondoka na kumuacha mumewe akiwa hajambo na kuamini taarifa atakayoisikia juu ya mali zake kurudi atamuongezea furaha. Kwa vile alikuwa ametoka usiku sana aliwahi kurudi chini ya bahari kabla familia yake haijagundua kutoka kwake.
Thabit baada ya kujiona yupo vizuri alinyanyuka kitandani na kutoka nje ya wodi, muuguzi alishtuka sana kumuona mtu aliyekuwa yupo hoi hajiwezi ameweza kunyanyuka kitandani na kutembea kama kawaida.
“Kaka vipi?”
“Safi.”
‘Si...si ni wewe uliyekuwa u...u..kiumwa?” muuguzi alishtuka.
“Ndiyo.”
“Mmh! Haya ni maajabu, muda mfupi ulikuwa hoi na mimi nimetoka kukuhudumia. Nashangaa kukuona ukiwa mzima…halafu kuna dada alikuja kukuona yupo wapi?”
Wakati Nargis akija katika umbile la kibinadamu alikutananaye akitoka kumpa dawa mgonjwa akiwa hajiwezi. Lakini dakika chache alishtuka kumuona akitoka akiwa mzima wa afya njema kama hakuwahi kuugua ugonjwa wowote, lakini yule dada mrembo hakumuona.
“Dada gani?” Thabit alishtuka.
“Kuna dada mmoja mrembo sana, aliniomba akuone, nilipomkatalia alianza kulia kwa kusema wewe ni mtu wake muhimu sana na asipokuona leo itachukua muda wa miaka minne kuonana. Nilimruhusu lakini ajabu alivyotoka sikumuona na wewe kukuona hujambo.”
“Kwa kweli sijamuona mtu, ila namshukuru Mungu sasa sijambo.”
Thabit akiwa bado anazungumza na muuguzi aliyemshangaa simu yake iliita.
“Haloo.”
“Asalam aleykum mpenzi?”
“Waleykum salam, mpenzi wangu nani?”
“Huwezi kunitambua kwa kujieleza mpaka unione, nilitaka kukujulisha nimefurahi kukuona umepona pia mali zako zote zipo kama kawaida.”
“Mali zangu zipi?”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kwani kipi kilichokufanya uugue ghafla?”
“Mmh! Za dukani.”
“Basi kila kitu kipo vizuri, ila kumbuka ahadi.”
“Ahadi gani?”
“Utaijua baada ya miaka minne.”
“Sawa.”
“Kwaheri ya kuonana,” baada ya ujumbe wa utata Nargis alikata simu na kurudi zake chini ya bahari.
Baada simu ya Nargis kukatika bila kumshtua Thabit juu ya ahadi aliyowekeana na mkewe siku aliporudi chini ya bahari kujifungua baada ya kuvurugwa akili na Subira na kumfanya asimkumbuke tena mkewe Nargis.
“Kaka naomba niwasiliane na mganga mkuu ili nimueleze maajabu haya ili nijue atafanya nini,” muuguzi alishindwa kumruhusu.
“Hakuna tatizo niache niondoke .”
“Subiri.”
Muuguzi alimjulisha mganga mkuu aliyefika pale na kumshangaa Thabit ambaye walikuwa wakipanga kumpeleka nje ya nchi kimatibabu.
“Haya ni maajabu, mtu uliyekuwa hujiwezi lakini ghafla umepona!”
“Kwani nilikuwa naumwa sana?”
“Kila aliyekuona alikuwa akilia, mpaka sasa hivi naona kama ndoto.”
“Yote ni maajabu ya Mungu.”
“Basi tunaomba tukufanyie vipimo kabla ya kukuruhusu kwa vile bado akili yangu haiamini.”
“Hakuna tatizo.”
Walikwenda chumba cha uchunguzi ili kumfanyia uchunguzi wa kina Thabit, muda wote muuguzi na mganga mkuu walikuwa wakijiona kama wapo ndotoni. Wakiwa chumba cha uchunguzi simu ya Thabit iliita, alipoangalia ilikuwa ikitoka kwa msaidizi wake.
“Haloo.”
“Bosi?”
“Ndiyo.”
“Haya ni maajabu ya karne.”
“Kwa nini?”
“Kuna simu nimepigiwa na mwanamke mmoja yenye lafudhi ya mwambao na kunieleza kuwa vitu vyote vya bosi wako vimerudi kama zamani, vyote tulivyoviona ilikuwa kiini macho. Niliondoka hadi kwenye makontena na kukuta kweli vitu vyote tulivyoagiza vipo.
“Kingine alichoniambie eti hata ugonjwa wako ni kiini macho na kama siamini baaada ya kuona vitu vyote nikupigie simu. Baada ya kukuta vitu vyote vipo nimekupigia simu na wewe kupokea na kukuta hujambo haya ni maajabu ya karne.”
“Hata mimi mtu huyo kanipigia simu na kunieleza kuwa vitu vyangu vimerudi.”
“Ni nani?”
“Hata simjui amesema nitamjua baada ya miaka minne.”
“Sasa atakuwa nani?”
“Akija tutamuona.”
“Basi bosi lazima tufanye sherehe kubwa.”
“Lazima tufanye.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya kuzungumza na msaidizi wake, alifanyiwa vipimo vilivyoonesha hakuwa na tatizo lolote mwilini. Kabla ya kuondoka alimpigia simu Subira aliyekuwa amefuata dawa Kigamboni kwa mzee Mukti. Baada ya kupokea alishtuka na kusikia anayezungumza ni mpenzi wake Thabit alikataa.
“Wewe unayezungumza ni nani?” Subira hakuamini kusikia sauti ya mpenzi wake.
“Nini mpenzi wako.”
“Hebu acha utani, niambie wewe ni nani?”
“Subira mpenzi wangu ni mimi Thabit mpenzi wako.”
“Siwezi kuamini wewe si Thabit,” Subira alikataa katakata.
“Nifanye nini ili ujue mimi ni mpenzi wako?”
“Hata ufanyeje siwezi kukukubalia,” Subira alibisha kutokana na hali aliyomuachanayo jioni ile.
Mpaka kukimbilia kwa mzee Mukti ambaye aliangalia na kumweleza mpenzi wake atapona lakini ugonjwa lazima ungemsumbua na kuchukua muda mrefu.
“Fanya hivi nifuate hospitali, kwani upo wapi?”
“Nipo Kigamboni.”
“Basi fanya haraka nimeruhusiwa muda si mrefu.”
“Nakuja, lakini wewe si Thabit,” bado alikataa.
Subira pamoja na kuelekea hospitali alipokuwa amelazwa Thabit akiwa na dawa za kumchua na kunywa alizopewa na mzee Mukti.
Aliendesha gari hadi hospitali na kulipaki pembeni na kukimbilia ndani ya wodi. Kutokana na papala alimpita mpenzi wake aliyekuwa amekaa mapokezi.
Aliingia mpaka wodini na kushtuka kukuta kitanda kitupu mawazo yake yalimpelekea labda Thabit amefariki. Alijikuta akiangua kilio cha sauti na kufanya muuguzi kumfuata na kumuuliza analia nini.
“Yupo wapi mpenzi wangu?”
“Umemuacha mapokezi.”
Bila kusema neno aligeuka hadi mapokezi na kumkuta Thabit amejaa tele akiwa mzima wa afya kwa mshtuko alianguka chini na kupoteza fahamu asiamini alichokiona na kuona kama yupo ndotoni.
Alipewa huduma ya haraka iliyomrudisha katika hali yake ya kawaida.
Baada ya kupata nafuu alimuangalia mpenzi wake asiamini kilichotokea bado alijiona kama yupo ndotoni.
“Ni wewe mpenzi wangu?”
“Ni mimi.”
“Hapana,” Subira alisema huku akimpapasa mpenzi wake ili kuhakikisha kama ni yeye kweli au anaota mtu aliyemuacha muda mfupi akiwa hajitambui viungo vyote havifanyi.
“Ni mimi.”
Subira alimkumbatia Thabit kwa furaha baada ya kuamini kweli aliyembele yake ni mpenzi wake akiwa mzima wa afya njema.
“Yaani siamini.”
“Basi amini, hata vile mali zilizopotea zimerudi.”
“Unasema!”
“Mali zilizoungua dukani na kwenye makontena zimerudi kama kawaida.”
“Jamani huu si utani au unanitania mpenzi wangu?”
“Sikutanii kama umenikuta mzima kabisa basi na kila kitu changu kipo salama.”
“Haya ni maajabu ya dunia.”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Walaa si maajabu lile ni jasho langu la halali haliwezi kutoweka kiajabu.”
Kabla ya kuondoka Subira alimpigia simu mzee Mukti kumjulisha juu ya tukio lile la ajabu ya karne. Taarifa ile ilimshtua sana na kuuliza:
“Ha! Unasema kweli?”
“Kweli kabisa ninavyokuambia nipo naye sasa hivi mzima wa afya kabisa.”
“Subira unanigeuza mtani wako wa kunitania?”
“Walaa kweli kabisa.”
“Mmh! Unajua siamini.”
“Kama huamini ngoja nikupe uzungumze naye.”
“Hebu nipe.”
Subira alimpa simu Thabit aliyezungumza:
“Haloo mzee.”
“Wewe ni Thabit?”
“Ndiyo.”
“Mpenzi wa Subira?”
“Ndiyo.”
“Mmh! Kimetokea nini?”
“Kwa kweli mpaka sasa sijui, namshukuru Mungu kama nilikuwa mgonjwa lakini sasa mzima wa afya.”
“Sawa, umeishafika nyumbani?”
“Ndiyo nataka kutoka hospitali.”
“Basi kapumzike.”
“Sawa mzee naomba basi utengeneze mambo naona wabaya wangu bado wananiandama.”
“Hakuna tatizo.”
Kabla ya kukata simu Subira alichukua simu na kumwambia kitu mzee Mukti kilichozidi kumshangaza.
“Babu yaani haya ni maajabu ya mwaka hata vitu vyote vilivyoungua dukani na kwenye makontena vimerudi.”
“Wewee!” mzee Mukti aliona sasa ule ni utani.
“Hata mimi nilikuwa kama wewe, kwangu bado naona kama ndoto lakini huo ndiyo ukweli wenyewe.”
“Hebu subiri niangalie kipi kimetokea.”
“Sawa, sisi tunakwenda nyumbani, vipi zile dawa nimpe?”
“Usimpe mpaka nitakapokupa maelekezo.”
“Sawa.”
Baada ya Subira kukata simu na kumshika mkono mpenzi wake ili waondoke, mzee Mukti alichanganyikiwa na kuingia kwenye rada zake kuangalia nini kimetokea tofauti na kitu alichokiona juu ya matukio yale. Kwanza kwenye rada yake kuonesha moto mkubwa.
Hakukubali alitumia uwezo wake wote kutaka kujua nini kimetokea tofauti na kitu alichokiona. Baada ya moto kutulia aliona jinsi jini Nargis alivyo mponya Thabit na kurudisha mali zote zilizoteketezwa kijini. Matukio yale yalimshangaza na kujiuliza kufanya vile alikuwa na maana gani.
Lakini aliamini mali yote iliyorudi haitateketea tena kwa vile sehemu ile alikuwa imeizindika. Ila kwenye makontena kulionesha pepesi hivyo palitakiwa kudhibitiwa usiku ule kabla upande wa pili haujarudi tena.
Aliwapigia simu na kuwajulisha baada ya mali kurudi walitakiwa kuzizindika ili zisiharibike tena. Walikubaliana na mzee Mukti alikwenda kuzizindika na kazi ilifanyika usiku wa manane.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Siku ya pili ilikuwa sherehe kwa wafanyakazi wote waliokata tamaa baada ya kuchanganyikiwa kutokana na mali kuteketea kila kukicha. Hali ilirudi kama kawaida na biashara iliendelea kwa Thabit kufungua maduka mengine makubwa kila kona ya jiji na kuanza kujipanga kufungua matawi mikoani.
Subira naye alitumia nafasi hiyo kuomba ndoa, Thabit hakuwa na pingamizi aliwatuma washenga walikwenda nyumbani kwao na Subira ndoa ilipangwa mara moja na siku ilipofika Subira aliolewa na Thabit kuwa mke wake halali wa ndoa.
Ilikuwa furaha isiyo na kifani baada ya Subira kutimiza ndoto yake ya kuwa mke wa Thabit.
Kutokana na kutoa ahadi kwa mzee Mukti Buguju kama akiolewa atampa zawadi kubwa, alimnunulia gari la kifahari la kutembelea na kumjengea nyumba kubwa pamoja na fedha taslimu milioni kumi. Alimuahidi kuendelea kumpa vitu vingi kwa vile alimfikisha alipopaota na kuona muujiza kufika pale.
Siku nazo zilikatika huku muda wa Nargis kurudi kwa mumewe ukikaribia, ilikuwa miaka ikawa mwaka ukawa mwezi na hatimaye siku. Nargis akiwa na wanawe wenye umri wa miaka kumi kila mmoja. Alikwenda kwa wazazi wake na kuwaeleza wiki ile alikuwa anarudi kwa mume wake Thabit baba wawili Zumza (Kurwa) na Zamzu (Doto).
“We Nargis una kichaa, utawezaje kurudi kwa mumeo ikiwa umeambiwa wanadamu wamekuwahi?”
“Mama mwanadamu na jini nani zaidi?”
“Jini, lakini mwanadamu yupo kama kinyonga hivyo anaweza kukuharibia maisha yako.”
“Mama kwa vile sasa nina uhuru wa kwenda popote, niacheni mwenyewe nakuhakikishia kama haitarudi maiti yangu hapa basi nitarudi na mume wangu.”
“Mmh! Mtoto wewe mbishi sana, we nenda yatakayokukuta usitushirikishe.”
“Hilo nalijua ila nilitaka kuwajulisha kuwa natoka kama nikifa nitunzieni wanangu.”
“Sawa.”
Nargis alirudi chumbani kwake kuwaaga wanawe, aliwakusanya kisha aliwaeleza:
“Wanangu, leo ninawaacha nakwenda kumtafuta baba yenu.”
“Mama unakwenda kumtafuta wapi wakati ulitueleza tutaondoka wote kwenda kwa baba?”
“Walimwengu wamenizidi akili lazima nitatumia uwezo wangu wote kumrudisha baba yenu mikononi mwangu la sivyo mtakuwa watoto wasio na baba.”
“Kwa nini tusiende wote?” Zamzu alimwambia mama yake.
“Hapana wanangu ninyi pumzikeni kazi hii nitaifanya bila tatizo.
“Mama mimi nina hamu ya baba naomba nikamuone tu kisha nirudi,” Zumza (Kurwa) naye alimwambia mama yake.
“Hapana wanangu nitamleta huku.”
“Mama mbona hatukuelewi mara unaenda kumtafuta umlete huku wakati ulituambia muda umebakia mdogo twende kwetu huku siyo kwetu sasa unakwenda kumleta baba aje afanye nini?”
“Zumza na Zamzu wanangu majibu yenu yote nitawajibu nikirudi.”
“Haya mama safari njema msalimie baba.”
Nargis baada ya kuagana na watoto wake alitoka rasmi kwenda duniani kumfuatilia mumewe.
Akiwa katika umbile la kibinadamu, jini Nargis alitokea duniani baada ya muda wake wa kukaa chini ya bahari kwisha.
Kabla ya kuondoka eneo la Salenda alitembeza macho kuiangalia dunia aliyoikosa kwa muda mrefu. Moyoni alijiapia hatarudi chini ya bahari mpaka amempata mumewe au arudi yeye akiwa maiti.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya kiapo chake aliachana na bahari na kutembea taratibu hadi karibu ya barabara na kujishika katika paji la uso baada ya muda mfupi alikuwa mbele ya ofisi ya Thabit ambayo ilikuwa imepanuka na kuwa ya kisasa zaidi.
Akiwa katika umbile la kibinadamu alitembea hadi akaingia ndani. Alifika mapokezi ambako ndipo alipokuwa mbaya wake Subira aliyemchukulia mumewe. Japokuwa moyo ulimuuma lakini alijikaza na kuficha hasira zake kwa vile hakurudi duniani kwa shari bali kuitafuta suluhu ya kumpata mumewe bila kumwaga damu.
“Asalaam aleykumu?” Nargis alimsalimia Subira aliyekuwa bize na kazi.
“Waleykum salaam,” Subira aliitikia huku akinyanyua uso kumwangalia aliyemsalimia mwenye sauti nzuri huku pua zake zikilakiwa na harufu nzuri ya manukato. Alishtuka kumuona mwanamke mzuri amesimama mbele yake.
“Karibu dada,” alimkaribisha bila kumjua ni nani.
“Asante.”
“Nikusaidie nini dada yangu?”
“Bwana Thabit yupo?”
“Mmh! Yupo, unaweza kukaa hapo ana wageni.”
“Inshaallah.”
Nargis alikaa kwenye kochi na kutulia kusubiri kuingia ofisi ya mumewe ambaye wakati huo alikuwa amemuoa Subira. Subira pamoja na kuendelea na kazi alimtazama kwa wizi mwanamke huyo mrembo aliyekuwa amekaa kwenye sofa akitembeza macho kuiangalia jinsi ofisi ilivyopendeza.
Baada ya nusu saa alitoka mtu aliyekuwa akizungumza na Thabit, kabla Subira hajanyanyua simu amweleze kuna mgeni, Thabit alitoka.
“Vipi kuna mgeni?”
Aliuliza baada ya kumuona Nargis aliyekuwa ametulia kwenye kochi.
“Ndiyo sweet.”
“Karibu,” Thabit alimgeukia Nargis na kumkaribisha.
“Asante,” Nargis alijibu huku akinyanyuka.
Thabit alitangulia mbele kuingia ofisini huku akifuatwa nyuma na Nargis, Subira alijikuta akivutiwa na mshono wa gauni alilovaa mgeni huyo. Thabit baada ya kukaa kwenye kiti alimkaribisha tena mgeni wake.
“Karibu bibie ukae.”
“Asante,” Nargis alijibu huku akikaa.
Thabit alijikuta akivutiwa na mgeni kwa uzuri wake na jinsi alivyovaa kiheshima na manukato, aliamini kabisa ni mmoja wa wateja wake lakini mwenye uwezo wa juu.
“Karibu bibie.”
Kwa vile Nargis alikuwa amejitanda ushungi aliutoa na kumtazama Thabit ili amtambue aliyekaa mbele yake ni nani. Ilikuwa tofauti na mawazo yake macho ya Thabit yalishawekwa upofu na kumfanya amuone mwanamke mrembo lakini asiyemfahamu.
Pia hakupenda hali ile kwa vile mkewe angeingia angeweza kumfikiria vibaya kuwa ana uhusiano na yule mwanamke wakati hamjui na siku ile ndiyo ya kwanza kumuona.
“Samahani bibie hapa ni ofisini halafu aliye mapokezi ni mke wangu, akiingia ndani na kukuta kwenye hali hii unafikiri atanifikiriaje?”
“Thabit,” Nargis alimwita kwa sauti ya upole bila ya kuurudisha mtandio.
“Naam.”
“Mimi ni nani?”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kwa kweli nimekusahau, unajua kampuni yangu inatembelewa na wateja wengi.”
“Najua, lakini mimi si mteja kama unavyonifikiria.”
“Kama si mteja wewe nani?”
“Hebu niangalie vizuri.”
Thabit alimuangalia Nargis kama atamkumbuka lakini kumbukumbu hazikumpa kabisa kama yule ni nani. Baada ya kushindwa kumkumbuka alimjibu:
“Mmh! Kwa kweli sikukumbuki kabisa.”
“Hebu rudisha kumbukumbu ya miaka kumi nyuma na siku moja.”
“Huo muda sina hebu nieleze wewe ni nani?”
“Naitwa Nargis.”
“Jina zuri lakini bado sikukumbuki.”
“Thabit unasema kweli au unatania?”
“Mimi na wewe tumeanza kutaniana lini?”
“Thabit mimi ndiye mkeo niliyeondoka miaka kumi iliyopita kwenda kujifungua na kufanikiwa kupata watoto mapacha. Nimerudi leo kwa mume wangu.”
“Mume wako nani?”
“Wewe Thabit.”
“Utakuwa umekosea huenda Thabit mwingine siyo mimi,” Thabit alimruka mkewe kwa vile dawa za mzee Mukti zilikuwa zikifanya kazi.
“Thabit ni wewe mume wangu najua walimwengu tayari wamesha kuroga, ahadi yetu ipo wapi, kwa nini umenisaliti mume wangu?” Nargis alisema huku akilia.
“Dada eeh, naomba uondoke usije nivunjia ndoa yangu bure.”
“Thabit…Thabit…nimechoka kuua kwa ajili yako, hebu nihurumie nimejitoa kwa ajili yako kumbuka matatizo yaliyokutokea lakini nilisimama kuokoa maisha yako na mali zetu.”
“Samahani dada naona umechanganyikiwa, naomba utoke ofisini kwangu,” Thabit hakumuelewa aliona akimchanganya.
“Sitoki mpaka nipate haki yangu nataka kurudi kwa mume wangu na nyumbani kwangu ili tulee wanetu niliokwenda kujifungua nyumbani.”
Thabit aliona kama anapotezewa muda alinyanyua simu ili kumwita mlinzi amtoe nje.
“Wala usisumbuke sipo kwa shari, nitatoka kwa hiyari yangu, ila kesho nitarudi tena, ukitoka hapa kajifikirie.”
“Wala usisumbuke kurudi, mtafute mtu wako siyo mimi.”
Nargis alinyanyuka na kuzunguka meza kisha alimpiga busu Thabit shavuni na kutoka nje bila kuongeza neno. Alitoka hadi mapokezi na kumuaga Subira huku roho ikimuuma na kutamani kummaliza lakini bado alizuia moyo wake kuendelea kuua kwa ajili ya mume wake.
“Mpenzi nakwenda.”
“Ooh! Mara, karibu jamani.”
“Asante, kesho nitakuja.”
“Karibu dada yangu.”
Subira alimsindikiza kwa macho na kutamani kumuuliza gauni lile zuri alilovaa kalishona au kalinunua wapi ili na yeye akanunue, aliamini kwa utajiri wa mume wake angeweza kununua kitu chochote. Lakini kwa vile alisema atarudi kesho yake alipanga kumuuliza au hata kumtuma.
Baada ya Nargis kutoka Thabit alinyanyuka na kutoka mpaka kwa mkewe Subira aliyemkuta bado yupo kwenye mawazo ya kumuwaza mgeni.
“Mpenzi,” alimwita kwa sauti ya chini.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Abee mume wangu.”
“Kuanzia leo sitaki mgeni mwanamke,” alisema kwa hasira.
“Kwa nini mume wangu?”
“Sipo hapa kutafuta wanawake bali kufanya kazi?”
“Mbona sijakuelewa una maanisha nini?” Subira alishindwa kumuelewa mumewe aliyeonekana uso umejaa hasira.
“Yule mwanamke aliyekuja amekuja kutangaza mapenzi eti ananipenda wakati anajua kabisa mimi ni mume wa mtu.”
“Mmh! Kwa hiyo umemuambia nini?”
“Ameondoka baada ya kumtisha kumuitia polisi.”
“Mmh! Sawa nimekuelewa mume wangu, nashukuru kwa uaminifu wako angekuwa mwanaume mwingine kwa uzuri wa yule mwanamke angemkubali tu na kunisaliti.”
“Mpaka nakuoa niliamua kuachana na mambo yote mabaya.”
“Asante mume wangu.”
Lakini wakati Thabit anageuka ili aingie ofisini Subira alishtuka kuona love bite (alama ya midomo iliyobaki baada ya mtu kumbusu mtu akiwa na rangi ya mdomo) zilikuwa nyingi kwenye shati jeupe la mpenzi wake. Alijikuta akishtuka na mapigo ya moyo kwenda mbio na kuamini mumewe alikwenda kujihami lakini yule ni mpenzi wake.
“Thabit,” alimwita kwa sauti kama ya mtu mwenye pumu.
“Naam mke wangu,” Thabit aliyekuwa ameshika mlango wa ofisi ili afungue aligeuka kumsikiliza mke wake.
Itaendelea wiki ijayo.
Alipogeuka hali ilikuwa ile ile ‘love bite’ zilikuwa kifuani na kwenye mashavu na mdomoni. Subira alizidi kuchanganyikiwa na hali ile na kuona jinsi Thabit asivyo muaminifu na alitoka ili kumhadaa lakini ndani kulikuwa na matendo ya mapenzi.
“Mume wangu!”
“Naam.”
“Unanifanyia nini?”
“Kivipi?”
“Yaani unanigeuza mtoto mdogo kwa nini?” Subira aliuliza huku akilia kitu kilichomshangaza Thabit na kutaka kujua kulikoni.
“Mke wangu umekuwaje leo?”
“Siyo nimekuwaje, ila unaonesha jinsi gani ulivyo muongo tena si muaminifu.”
“Mbona sikuelewi una nini mke wangu?” Thabit alizidi kumshangaa mkewe na lawama zake.
“Unanidanganya eti umemfukuza kama mbwa kumbe ndani mlikuwa na matendo ya kimahaba.”
“Mimi Thabit?”
“Ndiyo, hata kama kusoma sijui basi picha nimeiona.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Hebu angalia kifuani mwako.”
Thabit alijitazama na kukuta kuna love bite na kushtuka.
‘Ha!”
“Unashtuka nini? Eti nilimfukuza kumbe mpenzi wako Mungu kakueleleza,” Subira alisema kwa hasira huku amemshikia pua.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Hii ni ajabu vitu hivi vimetoka wapi, nakuapia mke wangu hakunibusu kwenye nguo alinibusu shavu kwa nguvu na kutoka baada ya kumkatalia mambo aliyokuja nayo ya kimahaba,” Thabit alijitetea.
“Siwezi kukuamini naona unipendi na kumwita yule mwanamke mzuri ili kunionesha.”
“Sijamwita hata hizi love bite nashangaa kuziona.”
“Si mbele tu angaliana na nyuma.”
Kauli ile limfanya Thabiti kuvua shati ili aangalia, hali ilikuwa vilevile alama ya midomo ilikuwa kingi kwenye shati jeupe na kumfanya Thabit abakiwa akiduwaa na kujishangaa alama zile zimetoka wapi.
Alijikuta akishtuka na mapigo ya moyo kwenda mbio na kuamini mumewe alikwenda kujihami lakini yule ni mpenzi wake.
“Thabit,” alimwita kwa sauti kama ya mtu mwenye pumu.
“Naam mke wangu,” Thabit aliyekuwa ameshika mlango wa ofisi ili afungue aligeuka kumsikiliza mke wake.
Alipogeuka hali ilikuwa ileile ‘love bite’ zilikuwa kifuani na kwenye mashavu na mdomoni. Subira alizidi kuchanganyikiwa na hali ile na kuona jinsi Thabit asivyo muaminifu na alitoka ili kumhadaa lakini ndani kulikuwa na matendo ya mapenzi.
“Mume wangu!”
“Naam.”
“Unanifanyia nini?” Subira alimuuliza huku akiangua kilio.
“Kivipi?” Thabit alishtuka.
“Yaani unanigeuza mtoto mdogo kwa nini?” Subira aliuliza huku akilia kitu kilichozidi kumshangaza Thabit na kutaka kujua kulikoni.
“Mke wangu umekuwaje leo?”
“Siyo nimekuwaje, ila unaonesha jinsi gani ulivyo muongo tena si muaminifu.”
“Mbona sikuelewi una nini mke wangu?” Thabit alizidi kumshangaa mkewe na lawama zake.
“Unanidanganya eti umemfukuza yule mwanamke kama mbwa kumbe ndani mlikuwa na matendo ya kimahaba.”
“Mimi Thabit?” Thabit aliuliza huku akijishika kifuani kwake.
“Ndiyo, hata kama kusoma sijui basi picha nimeiona.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Hebu angalia kifuani mwako.”
Thabit alijitazama na kukuta kuna love bite na kushtuka.
‘Ha!”
“Unashtuka nini? Eti nilimfukuza kumbe mpenzi wako Mungu kakuumbua,” Subira alisema kwa hasira huku amemshikia pua.
“Hii ni ajabu vitu hivi vimetoka wapi, nakuapia mke wangu hakunibusu kwenye nguo alinibusu shavuni kwa nguvu na kutoka baada ya kumkatalia mambo aliyokuja nayo ya kimahaba,” Thabit alijitetea.
“Siwezi kukuamini naona hunipendi na kumwita yule mwanamke mzuri ili kunionesha.”
“Sijamwita hata hizi love bite nashangaa kuziona.”
“Si mbele tu angalia na nyuma.”
Kauli ile limfanya Thabiti kuvua shati ili aangalia, hali ilikuwa vilevile alama ya midomo ilikuwa kwenye shati jeupe na kumfanya Thabit abaki akiwa ameduwaa na kujishangaa alama zile zilitoka wapi.
Wakati huo Subira alikuwa akiendelea kulia kwa kuamini kwa uzuri wa yule mwanamke hana chake. Moyoni aliapa kama aliweza kumdhibiti jini basi hatashindwa kumdhibiti mwanadamu mwenzake hata angekuwa mzuri kama malaika.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mke wangu nakuapia yule mwanamke hakunibusu kote huku bali shavuni kwa nguvu na kutoka nje.”
“Si kweli Thabit una uhusiano naye hawezi kukubusu tu bila kuwa na uhusiano naye, kama umenichoka nipe talaka yangu,” Subira alitikisa kiberiti.
“Hapana mke wangu siwezi kufanya hivyo nakuhakikishia nakupenda wewe peke yako,” Thabit alisema huku akipiga magoti mbele ya mkewe kuomba afute kauli ya kuomba talaka.
“Mume wangu hunipendi,” Subira alijilaza kiuongo kuonesha ameumizwa.
“Haki ya Mungu sina uhusiano wowote na huyo mwanamke ndiyo maana nimekuambia asimruhusu kesho akija.”
“Nimekuelewa mume wangu,” Subira alisema huku akimnyanyua mumewe alipopiga magoti.
Thabit alirudi ofisini na kumuacha Subira akiwa na mawazo juu ya kauli ya mumewe kuhusu alama za midomo ya busu kwenye shati na usoni. Alijiuliza kama mumewe hakubusiwa sehemu zote zile basi aliamini yule mwanamke huenda si kiumbe wa kawaida.
Japokuwa alikuwa hajawahi kumuona jini lakini alisikia sifa zao kuwa majini wa kike huwa wazuri sana. Alijikuta akiingiwa na wasiwasi labda yule mwanamke ni jini, lakini alipingana na mawazo yake kutokana na kuelezwa na mzee Mukti Buguju kuwa jini hata wasogelea.
Lakini alitaka kujiridhisha alimpigia simu mzee Mukti ili kuupata ukweli wa tukio la yule mwanamke mrembo aliyemtia wasiwasi hasa kutokana na kauli za mpenzi wake. Baada ya simu kuita kwa muda bila kupokelewa alirudia tena mara mbili lakini haikupokelewa pia.
Alishtuka simu ya mzee Mukti kushindwa kupokelewa, alijiuliza kuna nini. Wakati akiwa katika lindi la mawazo simu yake iliita. Alipoangalia ilikuwa inatoka kwa mzee Mukti, aliipokea haraka.
“Haloo babu,” alipokea huku akihema.
“Eeh! Vipi mjukuu mbona presha juu kuna nini tena?” mzee Mukti alishtuka.
“Kuna kitu kimenichanganya mzee wangu!”
“Kitu gani?”
Subira alimueleza kilichotokea muda mfupi ofisini kwake, habari ile ilimshtua sana mzee Mukti akamuuliza:
“Unasema huyo mwanamke aliingia ofisini?”
“Ndiyo.”
“Yukoje?”
“Mmh! Mzee wangu uzuri wa yule mwanamke ndiyo kwanza leo nimeuona, tena hata manukato yake ni mageni puani kwangu, sijawahi kuyasikia.”
“Mmh! Subiri.”
Mzee Mukti alikata simu na kuangalia kwenye rada zake alijikuta mwili ukimtetemeka baada ya kuona ni jini Nargis mke wa Thabit waliyemdhibiti asiingie popote alipo Thabit na mkewe. Alijiuliza amekosea wapi mpaka kuingia alipopafunga, baada ya kuangalia zaidi aligundua ujaji wake ndiyo uliomaliza nguvu za kumzuia pale alipokwenda kibinadamu tofauti na mwanzo alipokwenda kijini.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment