Search This Blog

NILIFANYA MAPENZI NA MAITI 20 ILI NITAJIRIKE - 4

 







    Simulizi : Nilifanya Mapenzi Na Maiti 20 Nitajirike

    Sehemu Ya Nne (4)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliendelea kuwa gumzo kila kona ndani ya kijiji hicho na hata vijiji vya jirani, wale wanaume waliokuwa wamenikataa, walishangaa, nilijua kwamba walijuta kwani waliamini kama wangekubali kunioa, inawezekana katika maisha hayo tungekuwa pamoja, kutanua pamoja na kufanya mambo mengine pamoja, hata huo utajiri ungekuwa wao pia.



    Sikutaka kujali, niliamua kusahau kila kilichotokea na katika kipindi hicho nilikuwa bize kufanya mambo yangu. Nilifika kijijini, familia yangu haikuwa hata na fedha za kutosha, hivyo haikuweza hata kuandaa chakula kwa ajili ya watu wengine lakini kwa sababu nilikuwa kijijini hapo, nilihakikisha hakuna kitu kinachoharibika.



    Nilikanunua magunia ya mchele na maharage, wanawake waliokuwa hapo, huku nikisaidiana nao tukaanza kupika chakula kwa ajili ya watu waliokuwa msibani hapo.



    Maisha yaliendelea, sikutaka kurudi, niliendelea kukaa kijijini hapo huku nikisubiri arobaini ya baba na ndipo nirudi nyumbani. Biashara zangu hazikusimama, kila siku fedha ziliingia kwani watu niliowaweka katika biashara hizo, hawakuweza kunizunguka au kunidhulumu kwani fedha zenyewe zilikuwa na ulinzi mkubwa.



    Niliendelea kuwa gumzo, ilikuwa vigumu sana watu kugundua mahali nilipoupata utajiri huo. Wengine waliulizana maswali, majibu yao yalikuwa ni hisia kwamba inawezekana nilijishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya mjini, wengine wakahisi kwamba inawezekana nilikuwa changudoa, kilichowashangaza ni kwamba japokuwa nilikuwa hapo kijijini, bado niliendelea kuingiza fedha kama kawaida.



    Sikutaka mama na ndugu zangu wengine waendelee kuishi kwenye nyumba hiyo, nilichokifanya ni kuirekebisha huku nikinunua nyumba nyingine na kuzikarabati, zikaonekana kisasa, kulikuwa na mabati, zilipakwa rangi na kuonekana kama nyumba za mjini.



    Wanaume waliniogopa, hawakujiamini, nilipata taarifa zao kwamba walikuwa wakinizungumzia sana, hasa uzuri wangu lakini hakukuwa na aliyekuwa tayari kunifuata, waliniogopa sana, sikutaka kujali kwani kijijini hakukuwa makazi yangu tena, nilikuwa nakaa kwa muda kabla ya kurudi Dar es Salaam.



    Baada ya wiki mbili kukaa kijijini hapo ndipo nilipoanza kuona mambo ya ajabu ambayo yalinishangaza sana. Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuota ndoto mbaya na za kutisha zilizonisisimua usiku mzima.



    Haikuwa kawaida, kipindi hicho hali ilikuwa mbaya kabisa. Kuna siku niliota nikiwa kwenye mlima mmoja mkubwa, nilisimama kileleni kabisa, mlimani kule kulikuwa na makaburi ishirini na moja, nilijiuliza yale makaburi yalikuwa ni ya nini, majibu niliyopata ni kwamba yale ishirini yalikuwa ni ya zile maiti nilizofanya nazo mapenzi na lile moja lilikuwa ni kaburi la baba yangu.



    Niliogopa sana, nilitamani kuondoka mahali hapo, kila niliponyanyua mguu, nilishindwa kukimbia. Wakati nawaza ni kitu gani nilitakiwa kufanya, ghafla nikaanza kusikia sauti za paka wengi, nilishangaa, iweje nisikie sauti za paka wengi na wakati nilipopiga macho huku na kule hakukuwa na paka? Nilijiuliza lakini hata kabla sijapata jibu, kwa mbele yangu nilimuona paka mkubwa, ukubwa wake ni mithili ya mbuzi.



    Nilibaki nikimshangaa paka yule, sikuwahi kumuona kabla, alikuwa mweusi tii na macho yake yalikuwa yaking’ara sana usiku ule, mwendo wake ulikuwa ni wa madoido, na kila alipokuwa akipiga hatua, alikuwa akilia.



    Paka yule alinisogelea, nilibaki nikitetemeka tu, nilitamani kukimbia ila nikashindwa, paka yule akanisogelea na kuanza kuniangalia machoni, kilichonishangaza, macho yake hayakuwa ya paka bali yalikuwa ni ya binadamu.



    “Kwa nini umefanya hivi Zakia?” aliniuliza paka yule.



    Hapo ndipo nikashangaa zaidi, paka kuongea, tena alitoa sauti iliyofanana kabisa na ya baba yangu. Paka yule akaanza kutokwa na machozi ya damu, niliogopa na kuhisi kwamba kulikuwa na kitu mahali hapo, huku nikiwa namshangaa, paka yule akabadilika na kuwa katika umbo la binadamu. Alikuwa baba yangu.



    “Baba…” nilianza kuita huku nikibubujikwa na machozi.



    “Kwa nini umeniua binti yangu?” aliniuliza, nilibaki nikitetemeka, sikumjibu, nilibaki kimya huku nikimwangalia.



    “Umeniua kwa sababu ya pesa! Pesa kitu gani Zakia, utakufa, utaziacha na hutoweza kuzikwa nazo, yaani umeniua kwa sababu ya tamaa ya pesa!” alisema baba huku akitia huruma sana, hata mimi mwenyewe nilibaki nikimshangaa.



    Wakati akizungumza maneno hayo, ghafla nikawaona paka wengine wakija kutoka katika upande aliokuwa baba, nilibaki nikijiuliza wale paka walikuwa wakina nani. Walikuwa ishirini kwani niliwahesabu kwa haraka sana, walipofika karibu yangu, wakabadilika na kuwa zile maiti ambazo nilifanya nazo mapenzi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Umefanya mapenzi na sisi kwa sababu ya utajiri!” alisema maiti moja huku wote wakiniangalia.



    Sikujibu kitu chochote kile, mwili mzima ulikuwa ukitoka jasho, nilitetemeka kana kwamba nilikuwa katika sehemu iliyokuwa na baridi kali. Hofu ilinijaa moyoni mwangu, nilipoziangalia maiti zile, zilitisha, zilikuwa na damu, hazikuoshwa, yaani kama zilikuwa zimetoka kupata ajali muda si mrefu.



    “Kwa nini uliniua?” aliniuliza baba kwa sauti kubwa iliyozitetemesha ngoma za masikio yangu. Hapohapo nikaanza kupiga kelele na kukurupuka kitandani pale huku nikihema kwa nguvu kama mtu aliyenusurika kufa.



    “Kuna nini Zakia?” aliniuliza mama baada ya kuniona nikiwa nimeshtuka kutoka usingizini huku nikitetemeka.



    “Mama! Baba! Nimemuona baba…” nilimwambia mama huku nikimsogelea, nilikuwa na hofu kubwa.



    “Ni ndoto Zakia, ni ndoto tu!” mama aliniambia huku akinivuta nisogee karibu yake.



    “Nimemuona baba!’



    Wakati nazungumza hayo, ghafla katika hali iliyonishtua, mbele yangu kukatokea kundi kubwa la watu, walivalia sanda, nilipowaangalia vizuri wale watu, zilikuwa zile maiti, mbele yao kabisa waliongozwa na baba ambaye alikuwa na damu mwili mzima. Kuona hivyo tu, nikaanza kupiga kelele, cha kushangaza, mama hakuziona maiti hizo.



    “Mama…mama…maiti…maiti mama…” nilipiga kelele huku nimwambia mama aziangalie zile maiti zilizokuwa zimesimama mbele yetu lakini mama hakuona kitu zaidi ya giza ambalo lilitawala chumbani mule.



    “Maiti?”

    “Ndiyo mama! Hizo hapo zimesimama, zimevaa sanda, mama, naogopa wataniua,” nilimwambia mama.



    Wakati nazungumza hayo, mwili wote ulikuwa umelowa jasho, mauzauza yaliyokuwa yakitokea yaliniogopesha mno, kuna kipindi niliona bora kufa kuliko kuendelea kuyaona yale niliyokuwa nikiyaona mbele yangu.



    Usiku wa siku hiyo sikulala tena, niliendelea kubaki macho, maiti zile hazikuzungumza kitu chochote kile, zilibaki zikiwa zimesimama mahali pale. Maiti ya baba ilikuwa mbele kabisa, ilivalia sanda nyeupe zaidi ya sanda zilizovalishwa kwa zile maiti nyingine.



    Mpaka inafika alfajiri, saa kumi, maiti zile ndipo zilipoanza kupotea chumbani mule. Bado nilikuwa nikiweweseka sana na niliona njia sahihi ya kuepukana na hayo yote ilikuwa ni kuondoka tu.

    Sikutaka kukaa tena kijijini kwa kuamini kwamba mauzauza kama yale hutokea vijijini tu kwani nilipokuwa Dar, hakukuwa na mauzauza hayo, hivyo nikapanga kuondoka hata kabla ya arobaini ya baba.



    “Mama! Nataka kuondoka,” nilimwambia mama, akaonekana kushtuka.



    “Unasemaje?”

    “Siwezi kukaa hapa, kuna uchawi sana, naogopa kufa, siwezi kukaa hapa,” nilimwambia mama huku nikimaanisha kile nilichokuwa nikikizungumza mbele yake.



    “Lakini arobaini ya baba yako bado.”

    “Najua mama, ila si kukaa kwa hofu namna hii, kila siku maiti, ninaweweseka mama, kuna watu wananiroga hapa,” nilimwambia mama.



    “Basi tutakwenda kwa mganga,” aliniambia.



    “Kwa mganga? Siwezi mama, siwezi kwenda kwa mganga,” nilimwambia.



    Nilijua kile ambacho kingetokea huko, najua kwamba mganga ambaye tungemwendea angeweza kusema kila kitu kilichotokea kwamba maiti hizo zilinitokea kwa kuwa ni lifanya nazo mapenzi.



    Sikutaka mama au mtu mwingine yeyote ajue kilichokuwa kimeendelea na ndiyo maana nikakataa kwenda kwa mganga. Hakukuwa na mtu aliyezungumza lolote lile, kwa kuwa nilikuwa na fedha, walifanya kila kitu nilichowaambia.



    Wanakijiji wengi walinishangaa, hawakuamini kama hayo ndiyo yalikuwa maamuzi yangu, kuondoka kijijini hata kabla ya robaini ya baba. Hakukutakiwa mtu yeyote aniambie kitu chochote kile ili nibadilishe msimamo wangu, niliendelea kuwaambia kwamba ni lazima niondoke kijijini na kurudi mjini.



    Siku hiyo, nikaanza safari ya kurudi Dar huku nikiwa nimewaachia kiasi kikubwa cha fedha na kuahidi kuendelea kuwatumia fedha zaidi. Ndani ya gari, nilikuwa na mawazo tele, sikuamini kama kweli kile kilichokuwa kikitokea, kilinitokea kipindi hicho.



    “Kwa nini mimi? Kwa nini hili linatokea?” nilijiuliza, wakati nikijiuliza hilo, hapohapo nikasikia sauti ya mganga ikinijibu.



    “Kwa sababu kuna mengi tumeandaa kwa ajili yako,” niliisikia vema.



    “Yapi?”

    “Tunataka kukufanya zaidi ya ulivyokuwa. Uwe mwanamke mwenye heshima kuanzia Tanzania mpaka Afrika kwa ujumla,” niliisikia sauti hiyo.



    “Mimi?”

    “Ndiyo!”



    Sikushangaa, niliamini kwamba hilo linawezekana kutokana na maisha niliyoamua kuishi kipindi hicho. Kama ni kumtumikia shetani, niliamua kufanya hivyo kwa asilimia zote, sikutaka kuacha kumtumikia kwani niliweza kuyaona mafanikio makubwa mbele yangu.



    Niliendesha gari kwa mwendo wa kasi mpaka nilipofika Ifakara, sikutaka kumtafuta Mudi, nilikuwa na mawazo yangu, nikachukua nyumba ya wageni na kulala humo.



    Wakati nikiwa kwenye usingizi mzito, ghafla nikaanza kuota ndoto moja hivi, ndoto iliyousisimua mwili wangu, sikuamini kile nilichokuwa nikikiona kwenye ndoto ile kingekuja kutokea siku moja katika maisha yangu, nilibaki nikiweweseka kitandani pale huku nikijiuliza swali moja la msingi, je ni kweli nilichokiona kingetokea? Sikuwa na jibu hata kidogo. Ndoto yenyewe ilikuwa hivi…



    Nilijiona nikiwa nimesimama mbele ya umati mkubwa, sikujua ilikuwa sehemu gani lakini kwa jinsi ilivyoonekana, ilikuwa ni moja ya sehemu iliyowakutanisha viongozi wengi wa nchi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilikuwa nazungumza juu ya jukwaa, kila mtu alikuwa akiniangalia, walikuwepo watu wa mataifa mbalimbali, Wazungu, Wahindi, Wachina na watu wengine. Nilishangaa, sikuwa nikifahamu lugha ya Kiingereza lakini cha ajabu, mahali hapo nilikuwa nazungumza lugha hiyo kwa ufasaha kabisa.



    Wote walikuwa kimya wakiniangalia, walikaa katika viti vyao kwa heshima kubwa, nilikuwa na furaha mno, yaani watu hao, ambao kwa kuwaangalia tu walikuwa wasomi watulie na kunisikiliza mimi, nilikuwa na lipi la maana?



    Wakati nikiendelea kuota ndoto hiyo, ghafla katika umati ule alisimama mtoto mmoja, alikuwa kama na miaka miwili, alikuwa akilia sana lakini hakukuwa na mtu aliyejali chochote kile na wala hakukuwa na mtu yeyote aliyemtaka anyamaze.



    Nilishtuka kutoka usingizini, nilikuwa katika hali isiyokuwa ya kawaida, niliangalia saa yangu na kugundua tayari ilifika saa moja asubuhi. Nikatoka kitandani na kuanza kujiandaa tayari kwa kuondoka hotelini hapo na kuendelea na safari.



    Nilichukua taulo na kwenda bafuni. Kitu cha ajabu kabisa, nilikuta bafu likiwa na ndoo mbili, moja ilikuwa ya bluu na nyingine ilikuwa nyekundu. Usiku wa jana nilipokuwa nimefika, nakumbuka kwamba kulikuwa na ndoo moja tu, ile ya bluu, sasa hii nyekundu ilitoka wapi? Nikahisi labda mhudumu aliingia, ila napo haikuniingia akilini kwa sababu tangu nimeingia, sikutoka na mlango nilifunga kwa ufunguo.



    “Unashangaa nini?” niliisikia sauti yangu moyoni mwangu, ilikuwa sauti ya yule mganga.



    “Hii ndoo imetoka wapi? Tena ina maji!” niliuliza.



    “Hii ndoo tumekuwekea sisi….”

    “Ya nini?”

    “Tunataka uoge maji hayo, tunakupa nguvu ya kukufanya kuwa mtu mwenye nguvu sana. Umekwishawahi kusikia kuhusu Illumiterant?” aliniuliza mganga yule.



    “Hapana! Ndiyo nini?”



    “Hiyo ni dini yetu, tuna dini ya tofauti kabisa, tupo hapa duniani kwa ajili ya kumuabudu Lusifa, hakuna kingine, yeye ndiye anatupigania na kutulinda, kwa sababu umehitaji utajiri na kupata, hatuna budi kukuingiza katika dini hii, imetapakaa dunia nzima na itakufanya kuwa na utajiri mkubwa, heshima kila kona,” aliniambia mganga huyo.



    Kwanza nikashtuka, sikuamini kama maisha yangu yote, mwisho wa siku ningeingizwa katika dini hiyo ya kumtumikia shetani. Nikawa kama nimepigwa butwaa fulani lakini nilitakiwa kukubaliana na mganga huyo pamoja na dini hiyo mpya ambayo niliingizwa kutokana na tamaa za kidunia.



    “Nipo tayari…ila unapozungumzia heshima, unanishangaza, nipata hiyo heshima kivipi?” nilimuuliza, mawasiliano yetu wote yalikuwa ya kimoyomoyo.



    “Utakuwa mwanamke mwenye cheo kikubwa sana hapa Tanzania, nitakwambia sehemu ambayo tunaabudia, utakwenda huko, utakuwa ukiabudu kila siku utakazotakiwa kufanya hivyo,” aliniambia na kukubaliana naye.



    Nilifanya kama alivyoniambia, nikachukua yale maji yaliyokuwa katika ndoo ile na kuanza kuyaoga, kadiri nilivyokuwa nikijimwagia, nilijisikia kuwa katika hali ya tofauti kabisa, mwili ulikuwa ukisisimka na wakati mwingine niliona kama ukitiwa nguvu.



    Nilipomaliza, nikatoka na kuvaa nguo zangu, kilichofuata ni kuondoka hotelini hapo. Njiani, sikuona kitu chochote cha ajabu, nilikuwa kimya muda wote, sikuhitaji kelele, hata redio sikuiwasha.



    Nilitumia saa kadhaa nikafika Dar es Salaam ambapo niliendelea na kazi zangu kama kawaida. Biashara zile nilizokuwa nimezifungua, ziliendelea kuniingizia kiasi kikubwa cha fedha mpaka kufikia hatua ya kuhama na kuhamia Mbezi Beach, katika jumba kubwa ambapo pia nilikuwa na harakati za kujenga jumba langu la kisasa maeneo ya Bunju.



    Baada ya siku mbili, nakumbuka nilitembelewa na wageni wawili, walikuwa wanaume nadhifu, sikuwahi kuwaona kabla, nilipowakaribisha wakaniambia kwamba walifika hapo kwa ajili ya kwenda nami kanisani. Kwanza nikashangaa, ilikuwaje wanifuate na kunitaka niende nao kanisani na wakati sikuwa nikiwafahamu? Mimi na kanisa wapi na wapi na wakati nilikuwa Muislamu na hata jina langu lilikuwa Zakia?

    Wakati najiuliza hayo, nikaisikia sauti ya mganga ikiniambia nifanye kile wanachoniambia watu wale, nikakubaliana nao, nikajiandaa na kuondoka nao mahali hapo.



    Ndani ya dakika kadhaa tulifika katika jumba fulani hivi, lilikuwa kubwa mno. Kuna kitu cha ajabu kilitokea, mimi ndiye nilikuwa dereva lakini kama ungeniuliza nilipita njia gani mpaka kufika katika jengo hilo, wala sifahamu chochote kile, yaani nilikuwa mtu niliyeendeshwa na mtu na wakati mimi ndiye nilikuwa dereva.



    Watu wale wakanitaka kuteremka, tukafanya hivyo na kuanza kulisogelea jumba lile kubwa lililoandikwa Illumiterant, yaani wenyewe wakiwa na maana ya KANISA LA SHETANI.



    Nilibaki nikishangaa, sikuamini kama mwisho wa siku nilitakiwa kuingia kanisani. Lilikuwa jengo kubwa, zuri, lililokuwa na urembo fulani wa dhahabu mlangoni, lilivutia kwa kuliangalia.



    Mlango ukafunguliwa, kabla ya kuingia ndani kabisa, tukatakiwa kwenda sehemu fulani, hapo, tukaambiwa tuvue nguo, wenzangu niliokwenda nao waliufahamu utaratibu huo hivyo wakavua na mimi kufuata.



    Ngoja nikwambie kitu kimoja ambacho watu huwa hawakifahamu. Kuna wengi niliwahi kuwasikia kwamba unapoingia katika makanisa kama hayo ambapo watu mnavua nguo na kusali miwa watupu, basi ni lazima mtatamaniana tu, haipo hivyo, ile hali ya kutamaniana kufanya ngono inaondoka kabisa.



    Tuliingia mpaka ndani, hatukuingia tukiangalia mbele, tuliambiwa tugeuke na tuingie kinyumenyume, tukafanya hivyo. Katika kipindi chote hicho nilikuwa nikishangaa, hilo lilikuwa kanisa la aina gani? Mbona lilikuwa tofauti na yale ambayo ninayafahamu mimi?



    Tuliingia ndani kabisa, kulikuwa na viti kadhaa, hakukuwa na idadi kubwa ya watu ila niliambiwa kwamba watu wangeongezeka kadiri muda unavyozidi kwenda mbele.



    Tulikaa katika viti vile tukiwa watupu kabisa ila baada ya dakika chache tukaletewa mavazi, yalikuwa mesui tu, ya moja kwa moja kama kanzu, mavazi hayo yalikuwa na alama ya msalaba kwa nyuma, msalaba ule ulikuwa tofauti kabisa, si kama ule aliosulubiwa Yesu, ulikuwa umegeuka, yaani kichwa chini miguu juu.



    Nilipolivaa vazi hilo, nilihisi mwili wangu ukipata nguvu za ajabu, hofu ambayo ilianza kuutawala moyo wangu ikapotea na kuhisi nikipata nguvu mpya.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ndani ya kanisa hilo watu walisimama mistari miwili, waliziba nyuso zao, tulikuwa kama watu ishirini hivi. Nakumbuka wote walikuwa wakiimba wimbo kwa sauti za chini, ilikuwa ni vigumu kufahamu ni wimbo upi waliokuwa wakiimba.



    Mbele kabisa ya kanisa lile alisimama mwanaume mmoja, naye alikuwa ndani ya vazi hilo, alisimama imara huku mkononi akiwa na fimbo moja ya chuma iliyonakshiwa na dhahabu, yeye ndiye alikuwa kiongozi na watu wote walitakiwa kumsikiliza yeye.



    “Kaeni chini,” alisema mwanaume huyo, wote wakakaa chini, na mimi nikafanya hivyo.



    Kila mmoja alibaki kimya, ilikuwa ni kama wanamsikilizia mtu fulani afike mahali hapo, hakukuwa na mtu aliyezungumza kitu chochote na hata yule kiongozi aliyekuwa amesimama pale mbele naye akaungana nasi na kutulia.



    Baada ya dakika kama tatu, mwanaume mmoja akatokea mahali hapo, yeye alivaa vazi kama yetu lakini lake lilikuwa na rangi nyekundu. Mwanaume huyo alituangalia kisha kutuamuru wote tuvue vazi lile sehemu ya usoni na kumwangalia yeye.



    Watu walipovua hapo ndipo niliposhangaa, sikuamini kile nilichokiona mbele yangu. Miongoni mwa watu waliokuwa mahali hapo, zaidi ya watu sita nilikuwa nikiwafahamu vilivyo.

    Wa kwanza alikuwa bwana Saidi Abdulaziz, huyu alikuwa Mpemba mwenye mabasi mengi yaliyokuwa yakifanya safari za kutoka Dar es Salaam na kwenda Mwanza, alikuwa na kiwanda cha kutengenezea karatasi na pia alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na fedha nyingi, yaani kwa kifupi alikuwa bilionea.



    Baada ya kushangaa kuhusu bwana Saidi, mtu wa pili alikuwa Simon Peter, huyu alikuwa kijana wa miaka ishrini na tatu, alikuwa miongoni mwa vijana waliokuwa na mafanikio makubwa. Alikuwa akimiliki vitu vingi vya thamani kama magari huku biashara zake zikiwa tata na wengine kuhisi kwamba alikuwa muuzaji mzuri wa madawa ya kulevya.



    Mtu wa tatu ambaye nilimfahamu alikuwa msichana Pamela Ndanshau. Huyu alikuwa msichana mrembo, aliwavutiwa watu wengi, alikuwa mwanamuziki mwenye jina, aliimba nyimbo zilizompa mafanikio makubwa mpaka wakati mwingine watu kuhisi kwamba alikuwa mmoja wa watu kutoka katika dini hiyo kitu ambacho alikipinga sana.



    Uwezo wake wa kuimba na umaarufu wake ulikuwa tofauti kabisa, alipendwa japokuwa watu wengi walisema kwamba hakuwa muimbaji mzuri. Hakuwa mtu wa kutulia, alitembea huku na kule bila kuchoka, kumbe katika yote hayo, alikuwa na nguvu kubwa ya shetani iliyokuwa ikimuongoza na ndiyo maana alipewa mashabiki wengi japokuwa uwezo wake ulikuwa mdogo.



    Mtu wa nne kumuona alikuwa Potifa Maliki. Huyu alikuwa mzee mwenye asili ya Kiarabu kutoka nchini Misri. Alipenda sana kuwafundisha watu kuhusu mafanikio, watu walimpenda kwa kuwa alikuwa kioo cha jamii, alisaidia watu wengi, kuna tetesi zilisema kwamba kutokana na utajiri wake, kuna baadhi ya serikali hapa Afrika ziliazimwa pesa na yeye mwenyewe, bila kujua, kumbe naye bwana Potifa alikuwa ndani ya dini hiyo.



    Mtu wa tano kumgundua alikuwa muigizaji Rashida Abdul, msichana mrembo ambaye naye alipendwa sana nchini Tanzaniia kutokana na filamu kali alizokuwa akiigiza. Msichana huyu alikuwa bilionea, kila filamu aliyoitoa, ilipendwa, alijikusanyia mashabiki wengi, jina lake lilijulikana Afrika nzima, aliitetemesha Afrika kipindi hicho, hakukuwa na aliyejua kwamba naye alikuwa na nguvu kutoka katika dini hiyo iliyokuwa ikikusanya watu.



    Mtu wa sita na wa mwisho kumgundua sikuweza kuamini kama alikuwa yeye, alikuwa mtu mwenye nguvu Tanzania, aliposema hili lifanyike, lilifanyika, alisikilizwa sana, alikuwa na cheo kikubwa mno. Mtu huyu alijulikana kwa jina la Mtazar.



    ****



    Kwa jina aliitwa Gabriel Mtazar, huyu alikuwa waziri wa mambo ya ndani na nje nchini Tanzania kipindi hicho. Alikuwa miongoni mwa watu waliopendwa sana, katika uchaguzi ambao ulifanyika nchini humo kipindi hicho cha nyuma, aliongoza kwa kura nyingi zaidi ya wabunge wote nchini Tanzania.



    Alikuwa kipenzi cha watu, alipendwa na alikuwa maarufu hata zaidi ya rais wa nchi hiyo. Kila siku katika maisha yake alikuwa mtu wa kuwasaidia watu wengiine, alikuwa bilionea mkubwa ambaye alijitangaza kabisa kwamba yeye alikuwa mtu wa watu, mali alizokuwa nazo hazikuwa zake bali alichangia na wananchi wote.



    Naomba niseme kwamba, watu waliokuwa katika chama hiki hawakuwa kama wale watu waliochukua utajiri kutoka kwa waganga wa kienyeji, hakukuwa na masharti ambayo yalionyesha dhahiri kwamba wewe ulichukua utajiri kutoka kwa shetani, yaani si kwamba uwe tajiri lakini usile nyama, uwe tajiri halafu usivae viatu, watu wa dini hii ya kishetani ilikuwa tofauti kabisa, unapopata utajiri, kitu cha kwanza ni kusaidia watu.



    Sikuamini kama ningemkuta mahali hapo, aliaminika sana, alipendwa, wakati nikiwa nikijiuliza maswali mengi, mara yule mkuu wetu akakohoa kidogo, macho yangu nikayarudisha kwake na kuanza kumwangalia.



    “Nimesikia kwamba tuna mwanachama mpya,” alisema kiongozi yule huku akituangalia.



    “Ndiyo mkuu!” aliitikia mwanaume mmoja.



    “Aje hapa mbele!” alisema.



    Nikabaki nikijiuliza kama nilikuwa mimi au alikuwa akizungumziwa mtu mwingine. Wakati nikijiuliza, ghafla nikajikuta nikisimama na kuanza kuelekea kule mbele.



    Naweza kusema haikuwa amri yangu kwani bado niliendelea kujiuliza ila kuna hiyo nguvu iliyonitoa pale na kuelekea mbele. Nilipofika hapo, nikasimama na kuanza kumwangalia mtu huyo ambaye wote humo ndani walimuita mkuu.



    “Unaitwa nani?”



    “Zakia…”



    “Ulishawahi kusikia kuhusu sisi?” aliniuliza.



    “Hapana! Si mtu wa kukaa sana na watu, ila nilijikuta nikiletwa huku,” nilimjibu huku nikimwangalia kwa macho yaliyokuwa na hofu tele.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwa nini upo hapa?” alinitupia swali.



    “Nimeletwa tu.”



    “Ulikuwa ukihitaji utajiri! Si ndiyo?” aliniuliza.



    “Ndiyo!”



    Mwanaume yule akabaki kimya, aliendelea kuniangalia kwa macho yaliyokuwa na shauku ya kutaka kufahamu mengi kutoka kwangu. Nilibaki nikimwangalia tu.



    Kwa kweli nilijiona kama kuwa na nguvu mpya, nilijikuta nikipewa nguvu ambayo sikujua ilikuwa wapi. Nikiwa hapo, nikaanza kupata maono ya ajabu kabisa kwamba nilikuwa tajiri mkubwa mno, kila mtu alikuwa akiniangalia kwa heshima, utajiri ambao nilikuwa nao ulimtetemesha kila mtu.



    Sikujua maana ya maono hayo, nikawaza kwamba labda ndivyo itakavyokuwa hapo baadaye, hivyo nikayapuuzia. Baada ya kuniangalia kwa sekunde chache, akachukua kitu fulani, kilikuwa kama chuma fulani, akaniwekea kifuati mwangu na kusema kwamba huo ulikuwa ni utambulisho kwangu kwamba nilikuwa mwanachama kamili wa hiyo dini.



    “Utataka tukufanyie nini kingine?” aliniuliza.



    “Niwe tajiri!”



    “Wewe ni tajiri tayari!”



    “Zaidi ya hivi nilivyo!”

    “Hakuna tatizo! Kuna kingine?” aliniuliza.



    “Ninataka heshima pia.”

    “Umepata. Kingine?”

    “Ninataka kulindwa, niwe na ulinzi mkubwa.”

    “Umepata!”



    Nilimwambia mahitaji yangu yote, baada ya kumaliza akaniambia kwamba nilitakiwa kujumuika na wenzangu, nikafanya hivyo na wote kunipongeza kwa uamuzi mzuri nilioufanya wa kujiunga nao.



    Tulikaa huko kwa saa moja na ndipo tukaondoka, moyo wangu ulikuwa na furaha tele, sikuamini kama ningepata yote yale niliyoyaomba ndani ya kanisa lile, usiku huo, sikulala, nilibaki nikiwa na furaha tele.



    Utajiri unachanganya, unapoushinda umasikini unajiona kuwa mshindi mkubwa, mshindi zaidi ya watu wote katika dunia hii. Nilibaki nikiyafikiria maisha yangu yaliyopita, niliendelea kuwa katika hali hiyo mpaka saa tisa alfajiri, manyunyu ya mvua yakaanza kusikika kutoka nje, nikachukua shuka na kujifunika.



    “Ngo ngo ngo…” nilisikia geti likigongwa.



    Kwanza nilishtuka, sikujua ni nani alikuwa akigonga, nikatoka kitandani na kuangalia nje kwa kutegemea kwamba mlinzi angesikia, cha ajabu, mlinzi hakusikia kabisa kwani alikuwa amelala.



    Nikatoka na kwenda nje, ghafla, hata kabla sijalifikia geti na kulifungua, watu waliokuwa wakigonga, nikashtukia wakiwa wameingia ndani, mikononi walishika mfuko mkubwa mweusi, walisimama wima huku wakiniangalia, mvua kubwa ikaanza kunyesha lakini hawakutoka hapo kwenye mvua, wakanitaka na mimi niwafuate. Kwa kweli, niliogopa mno.



    “Nyie ni wakina nani?” niliuliza huku nikiwa na hofu moyoni mwangu.



    Watu wale ambao walikuwa wawili hawakujibu swali hilo, walikuwa kimya huku wakiendelea kuniangalia, nilibaki kuwa na maswali mengi, wale walikuwa wakina nani na walitoka wapi.



    Walichokifanya ni kuanza kupiga hatua kunifuata, kwa kweli niliogopa mno hivyo kuanza kurudi nyuma na kuufunga mlango. Nilijua kwamba siku hiyo ndiyo ingekuwa mwisho wa maisha yangu, akili yangu iliniambia kwamba watu wale walikuwa majambazi ambao waliingia na kutaka kuniibia.



    Sikuuona msaada wowote wa mlinzi kwani wakati watu hao wakiingia, yeye alikuwa amelala kitu kilichonifanya kukosa amani, wakati mwingine nikahisi kwamba hiyo ndiyo ilikuwa siku yangu ya kufa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ngo…ngo…ngo..” nilisikia mlango ukigongwa.



    “Nyie ni wakina nani?” niliuliza huku nikitetemeka.



    “Ngo…ngo…ngo..” nilisikia tena ukigongwa.



    Wakati nikiwa najiuliza kama ilipaswa nifungue mlango au la, mara nikauona mlango huo ukifunguliwa taratibu. Nilishangaa sana, niliufunga mlango kwa ufunguo, sikusikia wakivunja kitasa, sasa kama kuufungua mlango huo waliwezeaje? Nikabaki nikitetemeka, wakaingia na kuanza kuniangalia usoni. Nilitamani ardhi ipasuke niingie ndani.



    “Sisi ni wageni wako leo,” aliniambia mwanaume mmoja.



    “Wageni wangu?”



    “Ndiyo!”



    “Usiku huu?”

    “Ndiyo!”

    “Ila siwajui, nyie ni wakina nani na mnahitaji nini? Naomba mniambie mnataka kiasi gani niwape ila mniache hai,” niliwaambia, kabla ya kujibu, wakaanza kucheka, walicheka sana kitu kilichonifanya niwashangae kwani nilihisi kwamba walikuwa majambazi waliokuwa wakiiba kwa kutumia uchawi.



    “Sisi si wezi wala majambazi.”

    “Kumbe ni wakina nani?”

    “Tumekuja kukuletea vitu!”

    “Vitu gani?”



    Mwanaume aliyeshika mfuko ule mweusi akaufungua na kutoa nguo mbili, yalikuwa ni kama madela ila yale yalikuwa na rangi mbili tofauti, yaani kulikuwa na vazi moja lililokuwa na rangi nyekundu na nyingine rangi nyeusi.

    Mwili wangu ulisisimka sana, sikufahamu mavazi yale yalikuwa ni ya nini, akaniambia nimsogelee na kuchukua, nikafanya hivyo. Niliyachukua na kuanza kuyaangalia, yalionekana kuwa mazito ambayo kwa kifuani kulikuwa na alama ya nyota kubwa ambayo ilizungukwa na miale ya moto.



    Kiukweli niliogopa sana, mbali na mavazi yale, watu wale walinipa fimbo ndogo. Kiukweli ukiniuliza mahali walipoitoa ile fimbo ndogo, sifahamu kwani kipindi walichokuwa wameingia ndani, hawakuwa na fimbo yoyote, ila kwenye kunipa, nikashangaa wakiwa na fimbo.



    “Hii ni ya nini?” niliwauliza huku nikiichukua fimbo ile.



    “Hii ni ya kutoa kafara!”

    “Kutoa kafara?”

    “Ndiyo! Utakapokuwa pamoja nasi, kuna kipindi utahitajika kutoa kafara. Sisi huwa hatuna masharti kwamba unapotaka uwe tajiri uwe unaishi maisha fulani ya kukubana, yaani usilalie kitanda chako au usivae viatu au kula nyama, unapokuwa pamoja nasi, upo tayari kufanya kitu chochote kile, kwenda popote pale, ila tunachokitaka ni wewe kutoa kafara kila tutakapohitaji damu, si kafara za ndugu zako pekee, hata watu wengine,” aliniambia mwanaume huyo.

    “Sawa. Nimeelewa.”

    Nilibaki nikizungumza na wale watu kwa dakika zaidi ya tano, baada ya hapo wakaniambia wanaondoka, wakatoka nje huku nikiwasindikiza kwa macho, walipotoka nje ya geti tu, nayo yale manyunyu ya mvua yakaisha muda huohuo, nikashangaa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mlinzi akashtuka kutoka usingizini, sikuwa na uhakika kama alikuwa amelala, nilijua kwamba kulikuwa na nguvu fulani iliyokuwa imemfanya kulala namna ile, yeye mwenyewe alishangaa sana, nilipomwambia kwamba alikuwa amelala, aliniomba msamaha.



    “Naomba unisamehe shangazi,” aliniambia mlinzi.



    “Wala usijali, nimekusamehe,” nilimwambia na kurudi ndani.



    Niliondoka na kuelekea chumbani, nilipofika nikayaangalia vizuri yale mavazi niliyopewa. Hayo yalikuwa sare kwa ajili ya wanafunzi ambao walijiunga na dini ile ya kishetani, niliyachukua na kuyavaa kwa zamu kwani nilitaka kuona yanafafanaje.



    Huo ndiyo ulikuwa muda wa kujiunga na hiyo dini, ndugu yangu, ninayaandika haya nikiwa na uchungu mkubwa, shetani ana nguvu mno, niliyachukulia kuwa kawaida lakini asikwambie mtu, kumtumikia shetani kuna hasara na hakuna faida yoyote ile.



    Asubuhi ilipofika nikaamka na kufanya mambo yangu, sikutaka kutoka kwenda sehemu yoyote ile, nilitulia nyumbani kwani nilijisikia furaha na mchoko wa ajabu.



    Ilipofika mchana, kama saa nane hivi nikapigiwa simu na wasimamizi wa biashara zangu kwamba siku hiyo kulikuwa na wateja wengi sana walikuwa kwenye maduka yangu, wao wenyewe walishangaa kwani haikuwa kawaida hata kidogo.

    Waliponiambia hivyo, akili yangu ikaanza kupata jibu juu ya kile kilichotokea, mafanikio makubwa yakaanza kuonekana mbele yangu, sikuamini, yaani kujiunga na dini ile, tena siku ya kwanza tu, basi biashara zangu zikaanza kupata wateja wengi.



    Kwa sababu nilikuwa kwenye dini yao ya kumtumikia shetani, wafanyabiashara wale wakubwa ambao niliwaona kule wakataka kuonana na mimi, walitaka kuniambia nini cha kufanya ili niwe bilionea mkubwa.



    Nikakutana nao na kuzungumza pamoja, walifurahi mno kuniona. Waliniambia nini cha kufanya ili nitajirike zaidi, nilifurahi, mbinu zao zilikuwa kabambe ila wakaniambia kwamba ni lazima nihakikishe najituma na kusaidia watu, ningetajirika zaidi ya nilivyokuwa. Walizungumza kama watu waliomwamini Mungu, kumbe nyuma ya pazia, walimwabudu shetani kwa nguvu zote.



    ****



    Miezi sita ilipita, nilikuwa kwenye mafanikio makubwa mno, Zakia yule hakuwa huyu tena, huyu alikuwa na pesa ndefu ya kufanya kila kitu alichotaka kukifanya. Niliona raha sana, kuna kipindi nilijiona mimi kuwa Mungu kwani niliweza kufanya kila kitu nilichotaka kukifanya.



    Kwa kawaida, huwa tunafanya ibada kila siku ya Ijumaa, ibada hiyo huanza saa sita usiku mpaka saa kumi huku kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi tukipewa kazi kubwa ya kutoa kafara.



    Hii haimaanishi kafara ya ndugu zako, huwa na maana ya kafara ya watoto, si lazima wawe watoto wako, watoto wowote wale na ndiyo maana mitaani huwa kuna kesi nyingi za kupotea kwa watoto.



    Baada ya kukutana katika Ijumaa ya mwisho wa mwezi, hapo ndipo niliambiwa kwamba ilikuwa zamu yangu kutoa kafara kwani ndiyo ilikuwa sheria ya kule tulipokuwa tukikutania.



    Kwanza nilishangaa, sikujua kama zamu yangu ingefika kwa haraka namna hiyo, sikutaka kufanya hivyo lakini ugumu ulikuja baada ya kuona kwamba nilitamani kuendelea kuwa tajiri, hivyo isingewezekana kukataa, na kama ningekataa basi ni lazima wangeniambia kwamba wanautaka utajiri wao.



    Sikuwa na jinsi lakini sikujua ni kwa namna gani natakiwa kutoa kafara kama walivyokuwa wakifanya. Walichoniambia ni kwamba haikuwa kazi ngumu hata kidogo, walinipa shilingi elfu tano na kuniambia kwamba hiyo ndiyo ingetumika katika kumchukua mtoto.



    Haikuniingia akilini kabisa lakini wao walisisitiza kwamba ile ndiyo njia nyepesi ya kufanya kile nilichotakiwa kukifanya. Nikakubaliana nao na hivyo baada ya ibada hiyo, nikaondoka zangu na kuahidi kwamba Ijumaa ya siku hiyo ningekwenda na mtoto hapo kanisani.



    Nilipofika nyumbani, usiku sikulala, nilibaki nikijifikiria ni kwa namna gani ningeweza kukamilisha kile nilichoambiwa. Muda ulizidi kwenda mbele, nakumbuka vizuri kabisa kwamba usiku wa siku hiyo sikulala, nilibaki nikifikiria namna ya kufanya.



    Mtaa niliokuwa nikiishi hakukuwa na watoto wengi, tena hao wachache waliokuwa wakiishi mtaa huo walikuwa ndani ya nyumba zao, ilikuwa ngumu sana kukamilisha kile nilichotaka kukifanya hivyo nilitakiwa kwenda katika mitaa ya uswahili, sehemu kulipokuwa na watoto wengi na kisha kufanya kile nilichotaka kukifanya.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikaondoka nyumbani na kuelekea huko. Kumbuka kwamba sikuwa mtu maarufu, yaani kama ningekuwa maarufu basi ningewatumia vijana kwenda kutafuta mtoto ila kwa kuwa sikujulikana, nikaona si tatizo kama nikienda mimi mwenyewe.



    Wazazi wenye watoto wenu wadogo, kuweni nao makini, uchawi upo na bado watoto wanaendelea kutolewa kafara kwa sababu tu wanaachwa peke yao mitaani hivyo kuwapa nafasi watu wabaya kuwaiba na kuondoka nao.



    Nakumbuka nilifika Tandale Kwa Tumbo, huko, mimi mwenyewe nilishangaa, kulikuwa na idadi kubwa ya watoto barabarani na hakukuwa na mtu yeyote aliyejali, walionekana kama watoto waliotelekezwa lakini ukweli ni kwamba walikuwa na wazazi wao na kila giza lilipokuwa likikaribia kuingia, waliondoka na kuelekea nyumbani.



    Nililipaki gari mbali kabisa na sehemu iliyokuwa ikionyesha video hapo Tandale, nakumbuka iliitwa Tandale kwa Tumbo. Nilijua kwamba ndani kulikuwa na watoto wengi, sikuteremka, nilikuwa nangalia huku na kule, tena nikiwasubiri hao ambao walikuwa ndani.



    Nakumbuka nilikaa kwa dakika kama thelathini, nikaona watu wakitoka ndani ya ukumbi ule huku kukiwa na watoto wengi tu. Nikaufungua mlango na kutoka nje, nikamfuata mtoto mmoja wa kiume aliyekuwa mchafumchafu, nikamuita.



    “Hujambo mtoto mzuri?” nilimsalimia.



    “Sijambo! Mambo anti!” alinisalimia.



    Kwanza nikashtuka, alikuwa mtoto kama wa miaka saba, sasa ilikuwaje asiniamkie na mwisho wa siku kunipa salamu ambayo kijana alipaswa kumpaka kijana mwenzake?



    Sikutaka kujiuliza sana kwani sikufika hapo ili niamkiwe bali nifanye kile nilichokuwa nimekifuata. Nikaingiza mkono mfukoni na kuitoa ile elfu tano.



    “Unaitwa nani?”



    “Naitwa Mudi.”

    “Unaishi wapi?”

    “Naishi hapo mbele…”



    Wakati amejibu maswali hayo, nikampa ile elfu tano, akaipokea, nikalifuata gari na kuanza kuondoka kwa mwendo mdogo kuelekea lilipokuwa soko la Tandale.



    Wakati naendesha, macho yangu yalikuwa yakiangalia nyuma kupitia kioo kidogo, nikamuona yule mtoto akianza kulifuata gari langu huku akikimbia, sikuendesha kwa mwendo wa kasi, mwisho wa siku nikaona nilisimamishe kumsubiria.



    “Anti…” aliniita, nikamfungulia mlango.



    “Unasemaje Mudi?”

    “Naomba twende wote!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wapi?”

    “Unapokwenda wewe!” alinijibu.



    “Sawa. Ingia.”



    Hakuwa na hofu hata kidogo, nilijua kwamba ile noti ilibadilisha kila kitu, basi hapohapo akaingia ndani ya gari, watu hawakuwa wakitujali sana, kila mtu alikuwa bize na mambo yake, nilichokifanya ni kumwambia afunge mlango, baada ya hapo, hao tukaondoka zetu huku nikiwa nimefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Ilibaki kumtoa kafara mtoto huyo.



    ****



    Niliondoka naye nikiwa na matumaini makubwa sana kwamba tayari nilimpata mtoto wa kumtoa kafara. Niliendesha gari mpaka nyumbani ambapo nililiingiza gari na kumteremsha na kumpeleka ndani.



    Ile noti ilimlevya na hakujua kitu chochote kilichokuwa kikiendelea, hakuwa na akili ya kurudi nyumbani wala kuondoka nyumbani hapo. Nilikuwa na uhakika wa kufanikisha kile ambacho niliambiwa, niliendelea na maisha yangu huku Mudi akiendelea kuwa ndani ya nyumba yangu.



    Hakuuliza swali lolote wala hakupaulizia nyumbani kwao. Mara kwa mara marafiki zangu wale mabilionea walinipigia simu na kuniuliza kama tayari nilimpata mtoto, nikawajibu tayari nilikuwa naye.



    “Kweli?”

    “Ndiyo!”

    “Wewe hatari sana, sisi huwa tunapata tabu sana mpaka kupata watoto, yaani wewe ndani ya siku mbili tu tayari! Heshima kwako,” aliniambia waziri mkuu.



    Ilipofika Ijumaa ya kutoa kafara, nikamchukua Mudi na kuondoka naye kuelekea kanisa. Kiukweli nilimuonea huruma kwani nilijua kwamba alikuwa akienda kuuawa lakini hakukuwa na jinsi, ili niendelee kuwa tajiri ilimpasa atolewe kafara kama ilivyokuwa kwa watoto wengine.



    Nilionekana shujaa mkubwa, tulipoingia kanisani tu, wanaume wawili wakatokea, hao hutumika kuwashika watoto na kuwapeleka katika chumba fulani, huko huwavua nguo na kuwaleta mbele yetu kisha kuwalaza kwenye meza iliyokuwa maalumu kwa ajili ya kutolea kafara.



    Kuna vitu vikitokea, kama binadamu wa kawaida ni lazima uwe na huruma, ndivyo ilivyotokea ndani ya kanisa lile. Wakati Mudi ameshikwa na watu wale, alilia sana, alitaka aachiwe lakini hakukuwa na mtu aliyemwachia, wakamchukua na kuondoka naye kwenda katika chumba kile ambapo akaandaliwa tayari kwa kutolewa kafara.



    Mimi na watu wengine tulikaa pale kanisani huku tukiwa na mavazi yetu, tuliendelea kumwabudu shetani pale tulipokuwa huku tukisubiria kila kitu kiendelee.



    Baada ya dakika kadhaa, wanaume wale wakaja mahali pale huku wakiwa na Mudi, sikujua walimfanya nini kwani hakubisha wala hakupiga kelele, walipomlaza katika meza ile, kilichofuata ni kuchukua kisu tayari kwa kumtoa kafara.



    Wote tuliambiwa tuviinamishe vichwa vyetu, tukafanya hivyo na nilichokisikia baada ya hapo ni kelele za maumivu za Mudi hivyo nikahisi kwamba muda huo ndiyo alikuwa akichinjwa na kutolewa kafara kama ilivyotakiwa kuwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliumia mno moyoni mwangu, sikuamini kama mwisho wa siku mimi ndiye nilisababisha kifo cha mtoto huyo. Nafsi yangu ikaanza kunihumu, nilijiona kuwa mtu anayestahili adhabu yoyote ile kwani kwa kile nilichomfanyia Mudi, hakika hakustahili mauaji hayo.



    “Yote ni kwa ajili yako Zakia! Hivi unafikiri ukifa utazikwa na fedha zako? Mbona unafanya mambo hayo! Au unafikiri ukiwa na pesa ndiyo utanunua kila kitu! Wangapi wamekufa kwa magonjwa hospitalini na wakati walikuwa matajiri, unadhani pesa zao ziliwasaidia?” niliisikia sauti, haikuwa kichwani mwangu au moyoni, niliisikia kama kuna mtu alisimama mbele yangu ndipo akaanza kuniambia maneno hayo.



    Nilishindwa kuvumilia kukiinamisha kichwa changu, nikakiinua kidogo kumwangalia mtu aliyekuwa akiniambia hivyo, sikumuona mtu yeyote yule.



    “Wewe ni nani?” niliuliza kwa sauti ndogo kabisa.



    “Huwezi kunijua, nipo dunianii kote, sionekani ila kazi zangu zinaonekana,” alinijibu kitu kilichonishtua sana.



    Akili yangu ikahisi kabisa kwamba huyo alikuwa shetani, nilijipa uhakika huo kwani wakati tulipoinamisha vichwa vyetu, tuliambiwa hiyo ni ishara ya kumwabudu shetani hivyo hata sauti ile niliyoisikia, niliamini kwamba ilikuwa yake.



    “Usitake kujiuliza mimi ni nani,” niliisikia tena ikiniambia.



    “Ni lazima uniambie, je ni shetani ninayemuabudu?” niliuliza, nilianza kutetemeka kwa hofu, nilijishangaa kuona jasho likinitoka.



    “Ninachukia kumuona binadamu niliyemuumba akimuabudu mwingine zaidi yangu. Sikukuumba kumwambudu shetani, nilikuumba uniabudu mimi,” alinijibu, sauti yake ilikuwa ni tofauti kabisa, haikuwa sauti ya ukali, ilikuwa ni ya kipole sana, sauti iliyoonyesha ni jinsi gani alinionea huruma.



    “Wewe ni Mungu?” niliuliza, wakati nilipolitaja jina hilo tu, hapohapo nikasikia mahali pale kukianza kutetemeka, watu wote tuliokuwa mahali hapo tukaanguka, mtetemo wake ulikuwa ni kama tetemeko la ardhi.



    “Ni nani amelitaja jina hilo?” nilimsikia yule mwanaume aliyekuwa mbele akiuliza huku akiwa anatetemeka kwa hasira.



    Hakukuwa na mtu aliyejibu swali lake, kila mmoja akabaki kimya. Nilibaki nikijiuliza juu ya ya mahali pale kutetemeka. Wakati sijapata jibu, nikaisikia sauti ile ikiniambia tena:



    “Jina langu ni kuu, jina langu lina utukufu. Kuna kipindi kitafika, nitakutoa katika shimo ulilokuwemo, wewe si mtu wa kuishi humo,” nilisikia sauti hiyo ikiniambia, ghafla nikasikia upepo mkali, hakukuwa na mtu mwingine aliyeusikia zaidi yangu, nikasikia ikiniambia maneno ya mwisho yasemayo:



    “Nitakurudia tena muda na wakati kama huu.”



    Ukimya ukatawala.



    Mara baada ya tukio hilo kutokea, hapo ndipo nilipoamini kwamba Mungu alikuwa na nguvu kubwa, kitendo cha mahali pale kutetemeka mara baada ya kulitaja jina lake, nikaona kabisa kule nilipokuwa hakukuwa sahihi hata kidogo, nilitakiwa kuondoka haraka iwezekanavyo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ila wakati nayafikiria hayo bado nilikumbuka kwamba nilikuwa na utajiri wa kishetani, sikutakiwa kuuacha kwa sababu bila kuwa tajiri kama nilivyokuwa maisha yangekuwa ya shida mno, moyo wangu ukagawanyika, upande mmoja ukatamani kumrudia Mungu lakini upande mwingine ukatamani sana kuendelea kuishi maisha niliyokuwa nikiishi kwani kupitia fedha, nilianza kuheshimika sana.

    Siku hiyo ikapita na kurudi nyumbani, nilikuwa na mawazo tele na muda mwingi nilikuwa namfikiria yule mtoto, moyo uliniuma sana lakini sikuwa na la kufanya, kuna wakati mwingine nilipokuwa nikikaa, taswira ya mtoto yule ilinijia kichwani, alikuwa akinililia sana kiasi kwamba nikabaki nikiogopa.



    “Kisa fedha umeniua…” niliiona taswira ya mtoto yule kichwani mwangu, ilisimama mbele yangu, alikuwa akilia mno.



    Nilibaki kimya, moyo wangu ulikuwa kwenye maumivu makali, hakika alistahili kuishi, hakutakiwa kuuawa kinyama kama nilivyokuwa nimemfanyia, nilipoiangalia mikono yangu, kitu cha ajabu ilionekana kujaa damu za yule mtoto.



    Siku ziliendelea kukatika huku nikiishi katika maisha ya hofu mno, nilikuwa tajiri lakini sikuwa na amani na muda mwingi nilionekana kuwa na mawazo tele.



    Baada ya kuendelea kuishi katika maisha hayo, siku kadhaa mbele tukaambiwa kwamba kulikuwa na mkutano mkubwa ambao ulitakiwa kufanyika nchini Marekani.



    Mkutano huo ulituhusu sisi watu tuliokuwa katika dini ya Illumiterant ambayo kazi yetu kubwa ilikuwa ni kumwabudu shetani. Sikuwahi kufika nchini Marekani, japokuwa nilikuwa na fedha nyingi lakini bado nilikuwa na imani kwamba mtu yeyote ambaye alikuwa na uwezo wa kufika katika nchi hiyo ilikuwa ni lazima uwe msomi.



    Sikuwa nimesoma, sikuwahi kupelekwa darasani kwa kuwa baba yangu hakuamini katika elimu, nilibaki nikijiuliza ingekuwaje katika siku yangu ya kwanza kufika nchini humo? Hakika niliona kama ndoto ambayo kipindi hicho ilitakiwa itimie.



    Hatukuhangaikia viza. Ngoja nikwambie kitu kimoja. Unapokuwa katika dini hii, kila kitu wanashughulikia wao, kuhusu viza, pasipoti na vitu vingine wao ndiyo wanafuatilia, tena si kwa kwenda ofisini huko bali wanaletewa mpaka hapo kanisani.



    Kumbuka hiyo ilikuwa dini kubwa, yenye watu wengi duniani, tena wale watu maarufu na hata viongozi mbalimbali wa nchi nyingi hapa duniani. Kuhusu mambo madogo kama ya hati za kusafiria pamoja na vibali vingine vyote vilikuwa chini yao.



    Baada ya siku kadhaa, nikapewa taarifa kwamba kila kitu kilikuwa tayari na kilichokuwa kikisubiriwa ni safari ya kwenda huko Marekani. Nilijiandaa vilivyo, ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kutoka nje ya Tanzania, kuna kipindi nilihisi kwamba nilikuwa kwenye ndoto ambapo baada ya muda mfupi ningeamka na kujikuta nikiwa kitandani kijijini lakini ukweli ni kwamba kila kitu kilichokuwa kikiendelea, kiliendelea katika maisha halisi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku ambayo ndiyo tulitakiwa kufanya safari, nikaelekea mpaka uwanja wa ndege ambapo nilichukua ndege ya Shirika la Ndege la KLM na kuanza safari ya kwenda nchini Marekani.



    Katika hili naomba nizungumze kitu kimoja. Huwa kwenye dini ile kuna aina mbili ya vikao, kuna kikao kinachoitwa Community, hicho ni kikao kinachowakutanisha wanachama wengi wa kanisa hili kwa watu wa Afrika, yaani kuna kipindi sisi tunaoishi Afrika tunakutana na kupanga mambo yetu, huko tutapanga ni jinsi gani ya kuendelea kuiteka dunia kutokana na mambo yetu mengi, mipango ambayo inapangwa kabla ya kukutana.



    Ukiachana na Community, kuna kikao kikachoitwa Together, hiki ni kikao ambacho kinawakutanisha wanachama wote duniani. Wote tuliokuwa katika nchi mbalimbali tunatakiwa kufika sehemu husika ambapo mara nyingi tunafanyia nchini Marekani na kikao hiki hutokea mara mbili kwa mwaka.



    Huwa kunakuwa na sadaka ya kafara na kila kipindi huwa na bara moja linalotoa kafara. Katika kipindi hiki tulichokwenda, Bara la Australia ndilo lililokuwa likihusika katika kuleta kafara, ilikuwa ni lazima wakusanye watu sita, kutokana na mgawanyiko wa mwaka na kisha kuwapeleka katika mkutano huo ambapo watatolewa kafara.



    Siku iliyofuata nikapanda ndege na kuanza safari ya kuelekea nchini Marekani, pale nilipokaa, nilikuwa peke yangu, hakukuwa na mtu mwingine kwani ndege haikuwa na abiria wengi.



    Ndege ilikata mawingu angani na baada ya saa kadhaa, tukafika katika Jiji la Nairobi nchini Kenya ambapo baadhi ya abiria wakaingia ndani ya ndege tayari kuelekea nchini Marekani pamoja nao.



    “Habari yako!” nilimsikia mwanaume akinisalimia. Nikageuka kumwangalia.



    Macho yangu yakakutana na sura ya mwanaume mzuri sana, alikuwa ana asili ya kiarabu, alikuwa akiniangalia huku akitabasamu, uzuri wake naweza kusema kwamba sikuwahi kuuona sehemu yoyote ile katika dunia hii, nilimwangalia kwa umakini hata kujibu salamu yake nikashindwa.



    Ndiyo kwanza tulikuwa Nairobi nchini Kenya na yeye alikuwa amepanda ndege mahali hapo. Nilikuwa kama mtu aliyekuwa na kigugumizi, kila nilipotaka kuitikia salamu yake, nilishindwa kwani uzuri wake wa sura ulinipagawisha mno.



    “Nimekusalimia, habari yako dada,” alinisalimia tena, tabasamu lake likaongezeka usoni mwake.



    “Salama tu, karibu,” niliitikia na kumkaribisha tena, macho yetu yalipogongana kwa mara ya pili, mapigo ya moyo yakazidi kuongezeka, kwa kifupi ni kwamba nilianza kumpenda na kumuhitaji maishani mwangu. Swali likawa, je alikuwa ameoa au alikuwa na mchumba? Na yeye alikuwa safarini, je kule nilipokuwa naelekea au la! Kila nilichojiuliza, nikakosa majibu.



    ****



    Kiukweli nilikuwa sijiwezi moyoni mwangu, nilimwangalia mwanaume yule mara mbilimbili na kujiuliza kama kweli alikuwa binadamu au jini. Mapigo yangu ya moyo yaliendelea kudunda kwa nguvu mpaka kuna wakati nilihisi kama yangeweza kuchomoka.



    Kama ni nyota, basi nyota yake ilikuwa kali mno na iliikimbiza nyota yangu kwa kiasi kikubwa sana. Nilimwangalia kwa umakini lakini yeye wala hakuwa na habari, aliendelea kufanya mambo yake, kiukweli nilitamani kumwambia tuzungumze kwani mwenzake kipindi hicho nilikuwa hoi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Unaelekea wapi?’ aliniuliza mwanaume huyo, Kiswahili chake kilikuwa kizuri na sidhani kama kweli alikuwa Mkenya.



    “Naelekea Marekani, wewe?” alinijibu na kuniuliza.



    “Hukohuko! Nakwenda New York kisha nitaruka Texas,” alinijibu, muda wote alikuwa akitoa tabasamu lililonifanya niwe hoi.



    “Ooh! Oke!’



    “Na wewe?”



    “Nakwenda Florida,” nilimjibu.



    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa mazoea yetu, tulikuwa tukizungumza sana kana kwamba tulikwishawahi kuonana miaka kumi iliyopita, hakuna aliyetaka kuonekana mnyonge katika mazungumzo, tulizungumza mpaka watu wengine wakaonekana kutushangaa.



    Moyoni mwangu niliridhika kabisa, kuna wakati nilijiona kuwa mtu mwenye bahati kuliko hata yule aliyeshinda mamilioni ya shilingi kutokana na jinsi nilivyokuwa nikizungumza pamoja na mwanaume huyu aliyejitambulisha kwa jina la Majeed.



    “Ninapenda kukupa kampani hata tukiwa huko Marekani, hivi itawezekana kweli?’ aliniuliza.



    “Hahah! Kwa nini isiwezekane!”



    “Mmh! Isije ikawa mke wa mtu halafu sumu yote nikawekewa mimi,” aliniambia.



    “Hakuna bwana! Sijaolewa wala nini, nipo singo,” nilimwambia.



    “Kwa maana hiyo hata mpenzi huna?”



    “Sina kabisaaaa…”

    “Acha uongo, inakuwaje uwe singo na wakati u mzuri namna hiyo?” aliniuliza huku akiniangalia kwa macho ya kunichunguza.



    “Ni maamuzi tu.”

    “Mh! Aya bwana!”



    Safari ilikuwa ikiendelea mpaka tulipofika nchini Uholanzi ambapo hapo tulitakiwa kubadilisha ndege, yaani kwa wenye lugha yao husema kupata connection nyingine ya ndege na kuendelea na safari.



    Mahali ambapo tulikaa, tuliagiza chakula na kuletewa, tulikula na kunywa kwa furaha, tulionekana kama mume na mtu na wakati ndiyo kwanza hiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza kuonana.



    Nakumbuka tulikaa Uholanzi kwa saa mbili ndipo tukaitwa katika ndege nyingine ya Shirika la KLM na safari kuendelea kama kawaida, hapo tukaanza kuitafuta Hearthrow, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Uingereza uliokuwa katika Jiji la London.



    Kutoka hapo Uholanzi mpaka Uingereza tulichukua saa mbili, tukafika na hivyo kuunganisha na ndege kuelekea nchini Marekani kwa kuivuka Bahari ya Atlantiki. Mpaka tunaanza kuitafuta Marekani tayari tulitumia saa ishirini na tatu lakini kitu cha ajabu sikuwa nimelala kabisa, muda wote tulikuwa tukizungumza pamoja na hakukuwa hata na mtu mmoja aliyejisikia kuchoka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Safari iliendelea mpaka tunaingia nchini Marekani, tayari tulitumia saa nyingine tano, tulipofika tu katika Uwanja wa Ndege wa JFK, sikutakiwa kubaki mahali hapo, nilitakiwa kupanda ndege nyingine na kuelekea Florida ambapo ndipo kulikuwa na kikao chetu.



    “Kwa hiyo mpenzi?” nilimuuliza mara baada ya kuteremka, hata hilo jina la ‘mpenzi’ lilinitoka tu mdomoni.



    “Basi sawa, naomba tuachane hapa, ila kesho, nitakuja kukuona,” aliniambia.



    “Hakuna tatizo.”



    Tukaagana kwa mabusu kemkem kisha kupanda ndege na kuelekea Florida. Njiani nilikuwa na mawazo tele, Majeed alinipagawisha sana, aliiteka akili yangu mpaka kuona sili silali kwa ajili yake.



    Kipindi hicho cha kwenda Florida nilijiona mpweke sana, sikuwa kama kipindi cha nyuma, hata kama ungeniangalia ungegundua kwamba sikuwa na furaha kabisa, nilikuwa mnyonge kupita kiasi.



    Tulitumia saa mbili mpaka kufika, harakaharaka nikateremka kutoka ndani ya ndege na kwenda nje ambapo huko nikamkuta mtu akinisubiri huku akiwa na bango lililoandikwa jina langu.



    “Are you Zakia?” (wewe ni Zakia?) aliniuliza, nikamjibu kwa kutingisha kichwa mimi ndiye.



    Tukaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea hotelini. Njiani nilikuwa kimya, macho yangu yalikuwa yakiangalia huku na kule, nilishangazwa na jinsi jiji hilo lilivyokuwa.



    Nilihisi kama nilikuwa peponi na ilikuwa ngumu kuamini kama pale nilipokuwa ilikuwa duniani, kila kitu nilichokuwa nikikiangalia, kilionekana kuwa kigeni machoni mwangu, nilibaki na mshangao mkubwa mno na wakati mwingine nikaanza kumkufuru mpaka Mungu.



    Tulipofika hotelini, nikateremka na kisha kuanza kuingia ndani huku nikitangulizana na yule mwanaume aliyekuja kunipokea. Yeye ndiye alikuwa mkalimani wangu ambaye alinisaidia kuuliza na hata kujibu maswali niliyokuwa nikiulizwa, baada ya hapo, nikaingia hotelini.



    Chumba kilikuwa kizuri mno, kilinishangaza na namna kilivyokuwa, nadiriki kusema kwamba tangu nizaliwe sikuwahi kuingia katika chumba kilichokuwa na uzuri kama hicho, nilifurahi sana lakini niliona kama kutokukamilika kwani kama ningekuwa na Majeed chumbani hapo basi ingekuwa furaha sana kwa usiku huo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya kukaa na kumfikiria sana Majeed, nikajilaza kitandani ambapo nikapitiwa na usingizi, nilipokuja kushtuka, tayari ilikuwa asubuhi. Nikatoka kitandani na kwenda kuoga bafuni, nilikaa katika sinki kubwa huku nikijimwagia maji taratibu, huku nikiwa huko, nikaanza kusikia simu ya mezani ikiita, harakaharaka nikaenda kuipokea, nilipoipokea, nikamsikia dada akiniuliza maswali, sikumuelewa alichoniambia ila hapohapo akalitaja jina la Majeed. Nikashtuka.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog