Search This Blog

NILIOLEWA NA MGANGA KWA TAMAA YA CHEO KAZINI - 4

 







    Simulizi : Niliolewa Na Mganga Kwa Tamaa Ya Cheo Kazini

    Sehemu Ya Nne (4)





    ILIPOISHIA:

    Baada ya kufika kwenye hoteli iliyokuwa na hadhi ya nyota tatu, tulitafuta meza ya pembezoni na kukaa kisha tuliagiza chakula. Baada ya chakula kuletwa tulianza kula huku nikiwa na shauku ya kuujua huo ubuyu. Lakini Safia alinieleza nipunguze pupa, tule kwanza baada ya chakula tulikuwa na muda wa kutosha wa mazungumzo.

    SASA ENDELEA...



    Sikumbishia, tulikula kwa muda wa nusu saa kama ujuavyo ulaji wa kike, tunashika chakula kama tunakiogopa. Baadaye tulipata muda wa kuzungumza huku nikiwa na hamu ya kujua nini kimejiri ndani ya mchakato wa kupata jina la mtu mmoja.



    “Eflazia,” Safia aliniita huku akifuta midomo yake kwa kitambaa baada ya kumaliza kunywa funda la juisi.

    “Abee,” niliitika huku nikikaa vizuri na kumtazama kama maneno yake yanaonekana kama sinema.

    “Si unajua kuna ushindani mkubwa katika uteuzi wa jina la kwenda kusoma?”

    “Najua.”



    “Unakumbuka nilikwambia nini kuhusiana na sifa za waombaji?”

    “Ulinieleza hakuna anayenifikia sifa kama zangu na nafasi ile ni yangu.”

    “Hiyo ilikuwa siku ya kwanza, baada ya hapo nilikueleza nini?”



    “Uliniambia kuna binti mmoja aliye mkoani kwenye moja ya matawi yetu ameleta CV yake, lakini bado hakuwa na elimu kama yangu japokuwa alikuwa na elimu kuwashinda wote waliotangulia.”

    “Sasa shoga kuna kitu nilikisia Jumatano, meneja wa kanda akizungumza na mkurugenzi yalinitia mashaka.”

    “Ulisikia nini?” nilijikuta nikishindwa kuvumilia.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Yaani hawa wakubwa wana mambo ya kijinga sana.”

    “Niambie shoga ulisikia nini?”

    “Nilimsikia mkurugenzi akimwambia meneja wa kanda kuwa mtu wake ajiandae kwa safari ambayo alitakiwa asafiri baada ya wiki tatu.”

    “Safari! Safari gani?” nilimsikia lakini nilishindwa kumwelewa.

    “Ya kwenda kusoma.”



    “Kwenda kusoma! Wapi?” bado sikuelewa.

    “Jamani kwani wewe ulikuwa unataka kwenda kusoma wapi?”

    “Ha! Sasa nani anaenda ikiwa uteuzi haujafanywa?”

    “Jambo likishikwa na wakubwa wadogo hawana nafasi.”



    “Ina maana wamekaa lini na wamechagua ikiwa kikao ni Ijumaa?”

    “Wakae wapi, nafasi ile wamepeana wenyewe kwa wenyewe.”

    “Unamaanisha kikao hakitakuwepo?”



    “Kitakuwepo kwa mujibu wa bodi lakini kila kitu kimekwisha, baada ya kunasa mazungumzo yale nilithibitisha siku iliyofuata baada ya kuiona tiketi na viza ya yule msichana.”

    “Mungu wangu,” nilihisi kama mapigo ya moyo yakienda kasi.

    “Eflazia mbona hivyo?” Safia alishtuka baada ya kuona mabadiliko yangu.

    “We acha tu, yaani nilivyoipania safari hiyo halafu kuna washenzi wachache wamenizunguka siamini,” nilisema kwa uchungu.



    “Eflazia kwani mzee wako vipi?”

    “Kwa kweli yupoyupo si kama zamani.”

    “Nina imani ungemshirikisha nafasi ungeweza kuipata.”

    “Yaani wee acha, pozi lote limeisha hata sijui itakuwaje?”

    “Kivipi?”



    “Sijui ofisi nitaionaje?”

    “Eflazia isikuumize sana kwa vile nafasi bado zipo.”

    “Sawa zipo lakini kwa upande wa kazi yangu hii ilikuwa ya juu, kinachoniuma zaidi kuchaguliwa kwenda msichana aliyenikuta kazini, nimemzidi kwa kila kitu.”



    “Juzi ndiyo nimeelezwa kumbe yule msichana alikuwa aolewe na meneja hivi karibuni lakini safari ya kwenda kusoma imesogeza mambo mpaka atakaporudi ndipo harusi ifungwe.”

    “Mmh! Sawa nashukuru kwa ubuyu wako uliogeuka shubiri.”

    “Basi shoga ni hayo yaani kila kitu kimeisha kilichobaki danganya toto tu.”

    “Sawa shoga nashukuru.”



    Kwa vile muda ulikuwa umekwenda tulirudi ofisini, nilipofika sikukaa sana niliamua kuondoka kwa hasira nilikuwa tayari kwa lolote. Nikiwa nyumbani nilijikuta nikikumbuka, nilitakiwa kupeleka majina ya watu wanaokuwepo kwenye bodi ya uteuzi



    Hata katika mazungumzo yetu hakugusia habari za mjini zaidi ya kusifia mapenzi anayopata toka kwa mzee Sionjwi, mtu aliyemuona ni kila kitu katika maisha yake. Pamoja na moyo wa mtu kupenda ni utashi wake, sikuamini kama mapenzi ya Rose kwa kizee kile yanatoka moyoni.



    Lakini wazo langu lilipingana kwa vile uhusiano wa Rose na mzee Sionjwi haukuwa wa ghafla bali ni watu walioanza muda mrefu toka wakati alipokuwa akinisindikiza. Siku zote nilibaki nikijiuliza maswali yasiyo na majibu kipi kimemvutia shoga yangu mpaka kukubali kuhama mjini na kuhamia shamba.



    Ingekuwa mzee Sionjwi ni tajiri ningesema labda kafuata mali ya kizee kile ambacho kisingekaa muda mrefu kingejifia na yeye kupata sehemu ya mali ile. Lakini hakuwa na mali yoyote ya maana zaidi ya mashamba na vimifugo vichache, ningesema labda sura yake imemvutia lakini mzee alikuwa kituko, kama una moyo mwepesi ukikutana naye lazima avunjike mbavu sura yake kama ngedere.



    Ila niliamini uwezo wa kimapenzi, mzee yule Mungu alimjalia kwa vile hata mimi nilionja ladha yake akimshika mwanamke lazima amuweke moyoni mwake. Lakini bado sikuona sababu ya kumtoa Rose mjini kwenye maisha mazuri kuhamia kijijini kwenye maisha kama yale.



    Lakini bado niliyaheshimu maamuzi yake kwa vile kila mtu ana sababu ya kumpenda mtu, hata wanawake wazuri huwakimbia wanaume wenye pesa na kuwafuata wasio na kitu kutokana na kukidhiwa haja zao za mwili.



    Mpaka kiza kinaimeza nuru ya mchana hakukuwa na dalili za kuonekana mzee Sionjwi, nilijua yaleyale ya kulala shamba. Sikuwa na matumaini ya kufanyiwa kazi yangu kwa vile ilikwenda tofauti na nilivyoagizwa zaidi ya kumueleza kilichotokea ili nijue atanisaidia vipi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pamoja na kumuamini katika kazi zake ya kutegua mabomu ya hatari kwa hatua iliyofikia ya yule msichana aliyechaguliwa kwa siri, hakukuwa na njia nyingine zaidi ya kuelezwa nisubiri safari nyingine kitu ambacho sikutaka kukisikia kuwa nijiandae na safari.



    Baada ya mazungumzo ya muda mrefu, Rose aliniomba akajilaze ndani, alikuwa hajisikii vizuri.

    “Shoga leo sijaamka vizuri na mzee mwenyewe alisema atarudi mapema mpaka sasa hivi sijamuona, naomba nikajipumzishe kidogo kitandani.”

    “Hakuna tatizo.”



    “Lakini usiondoke bila kuonana.”

    “Lazima nitakuamsha.”

    “Basi bakia na bibie akupe kampani.”

    “Hakuna tabu.”



    Nilibakia na mmoja wa mke wa mzee Sionjwi ambaye naye alikuwa mchangamfu kuliko wenzake. Pamoja na uchovu wa kutopumzika sikutaka kufumba jicho mpaka mzee Sionjwi atakaporudi ili nijue nitasuka au nitanyoa.

    Mpaka saa tatu usiku alikuwa hajarudi.



    Pamoja na kuzungumza na kucheka na mke wa mzee Sionjwi akili yangu ilikuwa mbali hasa baada ya usiku kuwa mkubwa na mwenyeji wangu haonekani. Nilijikuta nikiwaza jinsi mkurugenzi na meneja wa kanda kutuzunguka na kumpeleka mtu wanayemtaka.



    Kiherehere chote kiliniisha mtoto wa kike na kuziona ndoto zangu za mchana kuwa mtu mkubwa katika kampuni yetu upande wa fedha zikiyeyuka. Kila nilipofika hapo moyo uliniuma na kutamani kulia kwa kupiga kelele lakini nilijikaza na kutulia.



    Nilijiuliza nitakuwa nimekosea kitu gani kilichosababisha kuipoteza nafasi ile, niliamini kuna kitu nilikuwa nimekosea. Lakini nilikumbuka sikupewa sharti lolote zaidi ya kupeleka majina. Tukiwa katikati ya mazungumzo mzee Sionjwi aliingia. Alikuja moja kwa moja tulipokuwa tumekaa kwenye mkeka akiwa na kikapu na mfuko wa rambo.

    “Jamani kumbe kuna mgeni?”

    “Ndiyo babu, shikamoo.”



    “Marahaba mjukuu, umefika zamani?”

    “Toka saa kumi na moja.”

    “Ooh! Kumbe muda, karibu sana.”

    “Asante.”



    Wakati huo mkewe alikuwa amempokea mizigo aliyokuwa nayo na kupeleka ndani na kutuacha wawili. Kabla ya kusema kitu alipaza sauti kutaka maziwa, mmoja wa wakeze alikuja na kibuyu cha maziwa. Ilionesha jinsi gani mzee yule alivyokuwa akiwanyanyasa wakeze, kama hayupo basi hakuna kulala mpaka arudi.



    Baada ya kunywa maziwa alitulia kwa muda kisha alisema:



    “Nina imani kazi itafanyika usiku huu ili uondoke alfajiri uwahi kazini.”



    Kauli ile ilinishtua na kuamini mzee Sionjwi anajua mambo bado yako vilevile, ilibidi niingilie kati maneno yake.



    “Babu.”



    “Nina imani majina umeyapata hivyo nipe nikayafanyie kazi sasa hivi ili usiku nimalize kazi kwa kuwazika na kuipandisha nyota yako juu yao.”



    “Babu mambo yamekwenda tofauti.”



    “Kivipi?”



    Nilimweleza hali ilivyokuwa , baada ya kunisikiliza sikumuona kushtuka zaidi ya kusema:



    “Bado nafasi yako iko palepale.”



    “Mmh! Babu maneno yako yana ukweli?”



    “Binti hujawahi kunifundisha kazi hata siku moja, wewe unaitaka nafasi au unataka kujua utaipataje?”



    “Hapana babu, mazingira yamenikatisha tamaa.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa kama yamekukatisha tamaa kwa nini umekuja huku?” aliniuliza kwa sauti ya ukali kidogo.



    “Nisamehe babu, nimechanganyikiwa,” niliomba msamaha baada ya kuona nimeingilia kazi yake.



    “Wewe kazi yako kuleta tatizo litakalobaki niachie mwenyewe.”



    “Sawa babu nimekuelewa.”



    “Haya nipe hayo majina ya watu wako, kwa vile kuna kazi mpya imeingia nipe jina la huyo msichana aliyechaguliwa ambalo nitaanza nalo kisha nimalizie hao mabosi wako. Kazi zote zinafanyika usiku huu ili kesho uwahi kazini. Safari yako iko palepale na tarehe ikifika lazima uende wewe.”



    Mmh! Zilikuwa habari njema kwangu, lakini majina sikuwa nayo hata huyo msichana sikuwa na jina lake. Nilijikuta nikichanganyikiwa mtoto wa kike, lakini nilikumbuka mtu muhimu wa kunipatia majina alikuwa Safia. Nilimkubalia mzee Sionjwi kumpatia majina ya watu watakaokuwepo kwenye kikao na jina la msichana aliyechaguliwa kwenda kusoma.



    Mwaka wa mkosi ni wa mkosi kumbe simu yangu tangu jana haikuwa na chaji na nilitegemea kuichajia ofisini lakini kutokana na kuchanganywa sikuchaji simu iliyokuwa inaishia chaji.



    Pia sikutegemea kutumia simu nikiwa kijijini kwa vile sikuwa na kitu cha kuhitaji mjini kutokana na muda niliokuwa nao huko na kuwahi kurudi mjini.



    Kila nilipojaribu kuiwasha simu iliwaka nilipojaribu kupiga ilizimika, mwanzo ilikuwa inawaka lakini baadaye ilikataa  kabisa .



    Nilijikuta nikijilaumu kwa kuitanguliza hasira mbele na kuondoa akili ya kufikiri. Nakiri kuchanganyikiwa baada ya kujua nimeikosa nafasi niliyoiona kama bahati ya mtende.



    Kwa vile nilichanganyikiwa nilisahau hata kujua jina la msichana aliyechaguliwa, kuhusu majina ya watu wa bodi ukweli wa Mungu sikuwa na shida nayo baada ya kupata ukweli kuwa mtu wa kuondoka tayari kachaguliwa mpaka tiketi na viza vipo tayari kilichokuwa kikisubiriwa ni safari tu.



    Kitendo cha simu yangu kuzimika kilinikosesha raha kwa kuamini zoezi lile litashindikana na kujilaumu sana kwa kushindwa kutekeleza  niliyoagizwa na mzee Sionjwi na kujifanya najua kumbe naungua na jua.



    Sikuwa na jinsi ilibidi nimweleze ukweli mzee Sionjwi aliyekuwa amekwenda ndani mara moja.  Nilimtuma mmoja wa wakeze aniitie mzee ili nizungumze naye nijue atanisaidia vipi. Niliambiwa anaoga kisha apate chakula ndipo azungumze na mimi.



    Kwa hatua ile niliona hakukuwa na umuhimu wowote wa kulala pale kwa vile sikuwa na kitu cha kufanya. Nilitamani nikutane haraka na mzee Sionjwi ili niwahi kurudi mjini kuchukua majina ya watu watakaokaa kwenye bodi na jina ya mhusika.



    Hamu ya kukaa kijijini iliniisha na kupachukia kuendelea kuwa pale kwa muda ule. Mzee Sionjwi nilijua anajua nina majina hivyo kazi ingefanyika usiku ule kumbe mwenzake nilishafanya upuuzi.



    Baada ya saa moja kupita mzee Sionjwi alikuja na sufuria lililokuwa limefungwa shanga za rangi nyingi na kitambaa cha sanda. Wakati huo ilikuwa imefika saa nne na nusu za usiku, alipofika alisema:



    “Haya mjukuu nipe hayo majina nikuonesha muujiza anaofanya Mungu kuwachukia wachawi kwa vile huwa tunageuza anachokifanya. Hii kazi sawa na kumfufua mtu aliyekufa kitu ambacho kimewashinda waganga na wachawi wote duniani,” mzee Sionjwi alisema huku akiweka sufuria mbele yangu.



    “Babu,” nilimwita ili nijitetee.



    “Mjukuu huu si muda wa kuitana nipe kwanza majina hayo nikayazike, naomba katika hayo majina uandike na lako liweke kwa juu kisha nilichoree nyota ili kuonesha mwanga.”



    Mmh! Nilijiona mtu mwenye mkosi kufanya papara za kukimbilia kwa mganga  bila kupeleka nilivyotumwa. Mzee Sionjwi aliendelea kuzungumza bila kujua mwenzake nipo kwenye hali gani.



    “Bibi hebu fanya haraka kwa vile kazi kubwa itafanyika usiku wa manane unaoga na kuondoka. Siku ya pili ukifika ofisini utaniambia mimi ni nani. Hata ungetaka ukurugenzi wa kampuni ningeweza kukupatia hapa ni zaidi ya kufuru.”



    “Sawa babu nimekuelewa ila..”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nini tena mjukuu sema kinachokusibu wala usiwe na wasi siwezi kumrudisha aliyekufa tu lakini tatizo lako lolote hapa ndipo kiboko yake. Huu ni muda wa kunitumia nikifa usijejuta.”



    “Sawa babu ila…” nilijkuta nikishindwa kumalizia sentesi nilianza kulia kitu kilichomfanya mzee Sionjwi kunisogelea na kunishika begani, mmh! Makubwa ngozi yake kavu ya mkono ilipogusana na ya kwangu nilihisi msisimko wa ajabu.



    “Una nini mjukuu?” aliniuliza kwa sauti ya kubembeleza.



    “Sina majina uliyonituma.”



    “Ha! Mjukuu, kwa sababu gani umekosa majina?”



    Huku nikilia nilimweleza sababu ya kutopata majina, baada ya kunisikiliza alinibembeleza na kuniambia:



    “Mjukuu hakijaharibika kitu kwa vile muda bado unaweza kuondoka usiku huu ili uwahi kupumzika, ili kesho uamkie kazini na kupata majina yote kisha njoo nayo ili usiku wa kesho tufanye kazi. Huko Ulaya amini umeshaenda unasubiri kuambiwa.”



    “Asante sana babu.”



    “Basi mjukuu wahi ila kesho ukija usisahau ugonjwa wangu,” babu alikuwa akipenda sigara Embasy.



    “Nitakuletea wala usiwe na wasiwasi na kesho nitakuletea vitu vingi.”



    “Ndiyo maana nakupenda, nami nitaendelea kukufanyia maajabu ambayo toka niujue uganga sijamfanyia mtu. Siku zote mtu akikupa moja nawe usiwe mchoyo mpe tano.”



    “Basi naomba uniamshie shoga yangu nimuage.”



    “Mwache alale kwa vile kesho utarudi mtaonana.”



    “Namjua lazima atanilaumu, hasa mwanamke akiwa kwenye hali ile hukasirika bila sababu ya msingi.”



    “Basi twende ukamuage ndani maana yupo hoi.”



    Niliongozana na mzee Sionjwi hadi chumbani alipokuwa amelala Rose, alimuamsha na kumfanya alalame.



    “We mwanaume mbona huna huruma, mzigo wote huu ulionitwisha hunipi nafasi ya kupumzika.”



    “Siyo hivyo bibie.”



    “Siyo hivyo nini wakati mapenzi umegeuza chakula.”



    “Bibie utanilaumu bure, siyo miye ni shogayo anataka kukuaga.”



    “Mwambie aende.”



    “Rose…Rose unasema hivyo wakati wewe ndiye ulisema nisiondoke bila kukuaga.”



    “Ha! Kumbe shoga upo? Nilijua hiki kibabu kinanitania.”



    “Ningekuwa kibabu ningekulaza kitandani?” mzee Sionjwi alijibu.



    “We unatutafutia mada kesi, siku moja ufie kwenye kifua cha mtu,” Rose alijibu huku akikaa kitako  kufikicha macho na kupiga miayo.



    “Mmh! Ninyi waarabu wa Pemba siwawezi, sasa shoga nakuage Mungu akijalia tutaonana kesho jioni.”



    “Nashukuru shoga, basi ukija usisahau nilivyokuagiza.”



    “Ooh! Mwambie aende, haya ungemkumbusha saa ngapi?” mzee Sionjwi alimshushua Rose.



    “Nawe unavishwa shanga unapenda mambo ya kike,” Rose alimjibu mzee Sionjwi.



    Niliona malumbano ya waarabu wa Pemba yatanichelewesha , niliwaaga na kuwaacha wakirushiana vijembe. Kwa vile muda ulikuwa unaruhusu niliondoka mapema ili niwahi kupumzika ili kesho yake niwahi mjini.



    Nilifika mjini majira ya saa saba kasoro usiku, kwa vile chakula cha usiku nilikula kijijini, nilipofika nilioga na kuiacha simu kwenye chaji kisha  kupanda kitandani kuitafuta siku ya pili.



    ****



    Siku ya pili niliamka kama kawaida na kwenda zangu ofisini nikiwa na kazi moja  ya kuchukua majina ya watakaokaa kikao cha bodi pia jina la msichana atakayekwenda kusoma nje.  Nilipofika ofisini nilikwenda ofisini kwangu huku nikijipanga kukabiliana na bosi wangu kwa kuondoka jana yake bila kuaga.



    Kama kawaida nilitaka kumpigia simu Safia ili anipe ubuyu mpya  japokuwa niliamini huenda ukazidi kuniumiza moyo. Kabla sijampigia, simu ya mezani iliita. Nilijiuliza nani anayeweza kunipigia simu asubuhiasubuhi, nilibeba mkonga na kuweka sambamba ya sikio na mdomo na kupokea.



    “Haloo.”



    “Haloo mhasibu,” ilikuwa sauti ya mkurugenzi.



    “Abee bosi.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Vipi mama, mbona kimyaa?”



    “Nilipatwa na dharura, shikamoo.”



    “Marahaba, sasa mbona hukunijulisha?” aliniuliza kwa sauti ya upole.



    “Kwa kweli nilichanganyikiwa, nilipigiwa simu na mlinzi wangu wa nyumbani kuwa kuna watu wamevunja nyumbani kwangu,” nilitengeneza uongo.



    “Ooh! Pole sana basi ungetujulisha, nini kimeendelea?”



    “Watu wale wamekamatwa namshukuru Mungu lakini hawakuchukua kitu.”



    “Ooh! Afadhari, sasa ni hivi muone msaidizi wako kuna pesa unatakiwa kuidhinisha asubuhi hii kwa ajili ya kikao.”



    “Sawa mkuu.”



    Baada ya kukata simu, nilishusha pumzi ndefu baada ya uongo wangu kukubaliwa. Nilinyanyua simu na kumpigia msaidizi wangu ambaye alichelewa kidogo.



    “Haloo Pili, njoo mara moja na maagizo uliyopewa jana.”



    “Sawa dada Eflazia.”



    Baada ya muda Pili aliingia na karatasi na kuniweka juu ya meza kisha alitoka. Nilizipitia haraka na kunionesha kunatakiwa pesa za kikao cha bodi, nilijiuliza kikao kile cha nini na mbona sikukijua mapema. Sikutaka kukihoji sana kwa vile kilikuwa hakinihusu.



    Baada ya kuishinisha pesa nilimpa msaidizi wangu apeleke kwa mtoa pesa, nilipigia simu mkurugenzi amtume mtu akachukue pesa za kikao. Alimtuma Safia aje achukue, baada ya muda alifika kuchukua pesa za matumizi ya kikao.  Alipoingia ofisini kwangu nilimuona mtu mwenye jicho la kutaka kusema kitu.



    “Karibu shoga.”



    “Asante, naona jana umeondoka na kutuzimia simu.”



    “We acha tu nilichanganyikiwa sana.”



    “Sasa ndiyo ukazima simu?”



    “Niliona usumbufu hasa baada ya kuona simu ya bosi.”



    “Ndiyo maana alinieleza nikutafute, nimepiga simu mpaka nimekoma kumbe umezima.”



    “Shoga kikao cha ghafla kinahusu nini?”



    “Si kile cha kuteua jina.”



    “Jina! La nini?”



    “Kweli Eflazia umevurugwa, si la kwenda kusoma nje.”



    “Kikao si wiki ijayo?”



    “Ni kweli kilitakiwa kiwe wiki ijayo, taarifa zilizofika jana zimesema masomo yataanza mapema hivyo mtu anayetakiwa kwenda  aondoke Jumatano ya wiki ijayo.”



    “He! Makubwa, unamaanisha bado siku nne tu?”



    “Siyo nne, kikao hiki si kilitakiwa kukaliwa Ijumaa ya wiki kesho?”



    “Ndiyo.”



    “Basi  baada ya kikao hiki jina litatoka baada ya kikao kwenye ubao wa matangazo japokuwa kila kitu kama nilivyokueleza. Baada ya hapo msafiri atatumia wiki kesho kujiandaa na Jumapili au Jumatatu saa saba usiku anaondoka.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mmh! Sawa,” nilijibu kwa unyonge.



    “Sasa shoga kuna vitu vinatakiwa kikao kinaanza saa mbili na nusu asubuhi hii.”



    “Sawa basi.”



    “Kuna mengi tutazungumza baadaye.”



    Niliagana na Safia na kubakia ofisini nikiwa nimechanganyikiwa na kuona kama nataka kufanya mchezo kwa kupeleka majina ya watu watakaokuwepo kwenye kikao  kwa vile isingesaidia kitu kwa vile kikao kitakuwa  kimeisha na jina litakuwa limebandikwa na mwisho wa wiki itakayofuata mtu anaondoka.



    Lakini bado sikutakiwa kuhukumu kwa kukata tamaa kurudia kosa la awali la kufanya tofauti na nilivyoagizwa na mzee Sionjwi  na matokeo yake kwenda kinyume na mganga. Japo niliamini  ilikuwa kazi ngumu ya kubadili matokeo lakini sikutakiwa kwenda kinyume zaidi ya kumpelekea majina anayoyataka nione uongo wake.



    Japokuwa sikuwa na hamu ya kazi, nilijilazimisha kufanya kazi ili niimalize siku ile ambayo kwangu ilikuwa sawa na mwaka mzima. Nikiwa naendelea na kazi Safia alikuja na karatasi iliyokuwa na majina ya watu wa kikao cha bodi ambao walitakiwa kupewa posho baada ya kikao.



    Kwangu ilikuwa kama bahati ya mtende kupata majina niliyokuwa nikiyatafuta bila Safia kujua kitu. Nilipiga foto kopi na kubaki na majina yale kisha niliandaa pesa za posho za kikao.



     Baada ya kupiga mahesabu ya pesa wanayotakiwa kulipwa kwa ujumla nilimpigia mtunza fedha aliyekuja kuchukua karatasi ya malipo ili awalipe watakapomaliza kikao chao.



    Baada ya kupata majina ya watu waliokuwa kwenye kikao cha bodi nililipitia karatasi lingine lililokuwa nyuma ambako pia ilikuwa mshangao baada ya kukuta kuna majina yetu watu watano tulioingia katika kinyang’anyiro cha mwisho.



    Katika majina yale kulikuwa na wanaume watatu na wanawake wawili mmoja nikiwa mimi. Mwanamke aliyebaki niliamini ndiye aliyeteuliwa kwa  upendeleo na mkurugenzi na rafiki yake. Nilichukua jina lake alikuwa akiitwa Happy Kinono, sikuwa na haja ya kuliandika pembeni kwa vile karatasi zile zilikuwa  jibu la maswali yangu.



    Niliamini chochote kinachotokea hakuna mtu atakayenishuku hata Safia asingejua kitu, ila niliamini kama ningemuulizia majina ya wajumbe na la msichana aliyeteuliwa na kikatokea kitu basi angeweza kujua mimi ndiye niliyefanya.



    Nilijikuta nikipata furaha ya ajabu baada ya kupata kitu nilichokitafuta kwa muda mrefu na kukipata bila kumshirikisha mtu. Japokuwa kazi ya kubadili matokeo niliiona ngumu lakini kidogo moyo ulitulia na kufanya kazi yangu kwa utulivu.



    Nikiwa najiandaa kwa ajili ya chakula cha mchana simu yangu iliita, alikuwa Safia, ajabu baada ya kuona jina lile mapigo ya moyo yalianza kwenda kwa kasi. Nilijiuliza anataka kuniambia kitu gani kipya ikiwa kila kitu kilikuwa wazi. Lakini nilipokea simu kutaka kujua ana lipi la kusema:



    “Haloo Safi niambie.”

    “Poa, vipi leo huendi kula?”

    “Nakwenda tena nilikuwa nataka kukupigia, vipi kikao kimekwisha?”

    “Kimekwisha na jina la mwendaji limebandikwa kwenye ubao wa matangazo.”

    “Mmh! Haikuwa riziki yangu.”



    “Vipi nikufuate au nikusubiri nje.”

    “Nakuja nje.”



    Niliweka vitu vyangu vizuri na kutoka, ili kupata ukweli nilipita kwenye ubao wa matangazo kuangalia jina la mtu aliyechaguliwa. Kwa vile wengi waliamini mimi ndiye nitakayechaguliwa sikutaka watu wajue nimepita kuangalia jina.

    Nilitumia muda ule wa watu kwenda kula, wafanyakazi wengi walikuwa wamekwenda kula. Ubaoni hakukuwa na tofauti jina Happy Kinono lilikuwa limebandikwa. Baada ya kupata uhakika nilitoka kumfuata Safia aliyekuwa akinisubiri nje.

    Kama kawaida tulitumia gari langu, tulikwenda hoteli tuliyoenda mara ya mwisho na kuagiza chakula, tukiwa tunaendelea kula, Safia aliniambia kitu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Eflazia leo kidogo pachimbike.”

    “Kwa sababu gani?”

    “Kuna watu wamepinga yule msichana mgeni kupata nafasi ya juu wakati mpo wakongwe kama wewe na kaka Samwel.”

    “Sasa nini kiliendelea?”

    “Wakubwa walimkingia kifua na kuwapoza baadhi ya wajumbe na kukubaliana nao.”

    “Nimtakie kila la heri,” nilimpongeza kinafiki.



    “Huo ndiyo moyo wa kibinadamu, mwenzako akipata muombee kwa Mungu.”

    “Kweli kabisa, kila mtu ana nafasi yake huwezi kusafiria nyota ya mwenzako.”

    Baada ya chakula tulirudi kazini huku nikijitahidi kuonesha uchangamfu na kuficha maumivu makali ya moyoni mwangu. Nikiwa naendelea na kazi nilijiuliza maswali mengi juu ya kupeleka majina kwa mzee Sionjwi wakati tayari mtu katangazwa na hakuna kikao kingine.



    Lakini nilijua yote yangejulikana jioni kwa mzee Sionjwi, niliwahi kutoka ili niwahi kuondoka kwenda kijijini. Niliondoka hadi nyumbani kubadili nguo kisha niliingia madukani na sokoni kufanya manunuzi muhimu ya kijijini pamoja na vitu nilivyotumwa na mzee Sionjwi na Rose.



    Baada ya kukamilisha nilielekea kijijini kujua hatima yangu japokuwa moyo wangu uliisha kata tamaa. Kwa vile niliwahi kuondoka, nilifika kijijini mapema saa kumi na moja kasoro jioni. Kama kawaida nilipokewa na wake wa mzee Sionjwi na shoga yangu Rose aliyekuwa amechoshwa na mimba.



    Walipokea mizigo niliyowapelekea huku kila mmoja akionesha furaha. Kila nilipoonekana kijijni ilikuwa faraja kwao. Hata nguo niliwapelekea kwa ajili yao na watoto. Kwangu mimi sikuwa napoteza kitu kwa vile kazi aliyonifanyia mume wao ilikuwa kubwa sana.



    Siku ile bahati nzuri nilimkuta mzee Sionjwi, baada ya kupokewa nilikwenda kumsalimia chini ya mti alipokuwa amejilaza.

    “Babuu,” nilimwita.

    “Mjukuu.”

    “Hata karibu?”

    “Jamani mgeni lazima apate karibu ya heshima haya karibu mjukuu.”

    “Asante, za tangu jana?”



    “Mmh! Nzuri, sijui wewe mambo yamekwenda vizuri?”

    “Sana ushindwe mwenyewe.”

    “Sijawahi kushindwa na kitu cha kibinaadamu, siwezi kudra ya Mungu lakini si ya mwanadamu wala majini sijawahi kushindwa.”



    “Sasa babu leo ndiyo kikao kimekaa na jina tayari limepitishwa unafikiri hapo kuna uwezekano?”

    “Hii kazi ilikuwa iishe jana usiku lakini haikwenda tulivyotaka, japokuwa najua kazi iliyopo mbele yangu si ya kitoto sawa na kumrudisha duniani mtu aliyekufa kwa amri ya Mungu.”



    “Ni kweli babu ndiyo maana naona kuna ugumu .”

    “Ugumu gani?”

    “Kwa vile kikao tayari kimefanyika na jina limeisha teuliwa tutakuwa tumechelewa.”

    “Mjukuu, hata kama angekuwa ameishafika chuoni hilo lisingenishinda, nilikuahidi utakwenda kusoma na cheo kitapanda, ahadi yangu ipo palepale.”



    “Mmh,” kauli ya babu ilinifanya nigune.

    “Mjukuu hii si kazi ngumu, zipo kazi nilifanya, ambaye nilimfanyia haamini mpaka leo.”

    “Kazi gani?”

    “Ilikuwa kwenye uchaguzi mmoja, mteja wangu nilimfanyia dawa akashinda lakini aliwasahau wapiga kura wake mwaka mwingine alipogombea alikuwa hakubaliki na mpinzani wake, ndiye aliyekuwa akikubalika sana.”

    “Ehe kitu gani kiliendelea?”



    “Huwezi kuamini hata mikutano yake ya kampeni alikuwa hapati watu, alipokuja alionesha kukata tamaa. Lakini nilimuahidi lazima atashinda na siku ya mwisho alishinda.”

    “Mmh! Babu alishindaje?”



    “Ni kweli mpinzani wake alishinda tena kwa kura nyingi, lakini siku ya mwisho nilibadili majina kwa njia nijuazo na msoma matokeo aliposoma alimsoma ameshinda.”

    “Mmh! Hii kali, unataka kuniambia mpinzani wangu kama akifika chuoni nitawezaje kwenda kusoma au kuna nafasi nyingine itapatikana?”

    “Walaaa, hiyohiyo tu.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa nitaendaje?”

    “Wewe unataka kwenda kusoma au kujua utakwendaje?” swali la babu lilionesha kama kuchoshwa na maswali yangu ya kitoto.

    “Hapana, nataka kwenda kusoma.”

    “Basi kazi yote niachie mimi ili kesho ukitoka hapa ukajiandae kusafiri na safari hiyo utakwenda wewe badala ya huyo msichana.”



    “Sawa babu,” nilikubali mdomoni lakini moyoni niliona kama haiwezekani, kama ingekuwa bado hakijafanyika kikao ningeona inawezekana. Lakini nilitakiwa kukaa kimya ili nije unione uongo wa mganga.



    “Nina imani mambo yamekwenda vizuri!” babu aliniuliza.



    “Ndiyo babu leo kila kitu kimekwenda vizuri.”



    “Sasa yako umemaliza imebakia kwangu kukutengenezea maajabu ambayo hutokea ndotoni tu.”



    Mzee Sionjwi alinyanyuka kwenda kilingeni kwake na kurudi na chungu nilichokuwa kimezungushwa sanda na shanga za rangi mbalimbali na kukiweka mbele yangu na kusema:



    “Nipe kwanza majina ya viongozi waliokaa kikao.”



    Nilinyofoa karatasi lililokuwa na majina ya viongozi wa bodi na kumpatia mzee Sionjwi ambaye alichukua karatasi na kuiweka kwenye chungu kilichokuwa na maji yaliyochanganywa na dawa. Baada ya muda alichukua kipande cha sanda alichokiweka kwenye maji yale kisha aliitoa karatasi ya majina na kulifunga kwenye sanda na kuiweka pembeni.



    Aliniomba jina la yule msichana aliyechaguliwa kwenda kusoma, kwa vile karatasi ilikuwa na majina mengi, kila jina lilikuwa na picha mbele yake.



    “Sasa babu karatasi hii ina majina na picha nyingi tutafanyaje?”



    “Chana sehemu zenye majina mengine na kubakiza moja.”



    “Sawa.”



    Nilifanya vile kwa kuchana majina manne, kwa vile jina la mhusika lilikuwa la mwisho, niliyachana ya mwanzo na kuliacha jina moja linalotakiwa. Aliishika picha ya yule msichana na kuchukua kisu kisha aliipasua kichwani na kuweka dawa eneo la kichwa huku akisema maneno yake na kulitaja jina yule msichana.



     Baada ya kumaliza maneno yale alichukua kiberiti na kuichoma picha ile ambayo iliungua yote na kuchukua majivu yake kisha alitoa kitambaa cheusi na kuliweka jivu lile. Baada ya zoezi lile alibeba  vitambaa vyote viwili na kuniambia nimfuate.



    Nilimfuata hadi nyuma ya nyumba kulikokuwa na mashimo madogo mawili.



    Alichukua kitambaa kimoja chenye majina ya bodi ya uteuzi na kukiweka kwenye moja ya shomo na kumwagia dawa na kuyazika. Alichukua jina la msichana aliyeteuliwa alilokuwa amelifunga kwenye kitambaa cheusi nalo akalizika.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya zoezi lile alinieleza  nilifuate ndani ya kilinge, tuliingia ndani na kunieleza nikae chini na yeye alikaa kwenye kigoda mbele yangu na kuchukua karatasi nyeupe iliyokuwa na picha ya nyota na kalamu nyekundu na kunipa kisha aliniambia niandike jina langu  katikati ya picha ya nyota.



    Nilifanya vile, wakati huo alikuwa ameisimamisha mishumaa minne mbele yangu na kuuwasha mmoja, ilipokolea moto alinieleza niichome ile karatasi kisha moto wake niiwashe mishumaa iliyobaki, nilifanya vile kwa kuiwasha yote na wakati huo karatasi yenye jina langu ilikuwa imewaka yote na kubakia jivu ambalo nilielezwa niliweke kwenye sahani.



    Baada ya kumaliza zoezi lile alinieleza nikapumzike ili nijiandae na zoezi usiku kwa ajili ya kumalizia kazi iliyobaki na mimi kurudi mjini kujiandaa na safari ambayo kwangu bado niliona ni ndoto.



    Baada ya chakula cha usiku na kupumzika majira ya saa tano usiku mzee Sionjwi alinieleza twende kwenye mti wa mzimu ili tukafanye kazi ya kuondoa kiza na kupandisha nyota yangu.



    Alinieleza nichukue kanga ya kujifunga wakati wa kuoga dawa, nilichukua kanga kisha tuliongozana kuelekea kwenye mti mkubwa wa mzimu. Siku ile mwezi ulikuwa katikati hivyo njia yote ilikuwa nyeupe kama mchana na kupunguza hofu ya usiku.



    Tulitembea kwa muda wa nusu saa mpaka kwenye mti mkubwa wa mbuyu, tulipofika alinieleza nivue nguo zangu zote na kujifunga kanga ili anioshe kuondoa kiza cha mwili kisha anifunge shuka nyeupe na kunipandisha kwenye kichuguu kupandisha nyota zangu. Zoezi lile hufanyika mchana wa jua kali au usiku wa mbalamwezi kama ile.



    Nilifanya zoezi lile mara moja, pembeni ya mti ule mkubwa kulikuwa na maji yaliyotuama hivyo alichukua beseni na kwenda kuchota maji na kuja nayo. Aliweka dawa ya unga kisha alinielekeza nijimwagie maji ya dawa naye kunisugua kwa majani ya dawa mwili mzima kasoro sehemu za siri tu.

    “Sasa mjukuu tutafanya zoezi gumu kidogo.”

    “Zoezi gani babu? Mbona unanitisha.”



    “Walaa la kawaida, kwa vile maji haya yana dawa, wewe kazi yako itakuwa kujimwagia maji na mimi kukusugua kwa majani haya. Hapa tunafanya kazi mbili kwa wakati mmoja. Moja kukutoa nuksi na kiza kwa kukusugua na majani uchafu unaotoka mwilini unausafisha kwa maji utayojimwagia.”

    “Hakuna tatizo babu kwa vile mimi na wewe si wageni unanijua nakujua.”

    “Nashukuru kulijua hilo.”



    “Ili nami nguo zangu zisiloe nitajifunga kipande cha shuka nyeupe.”

    “Hakuna tatizo.”

    Baada ya kusema vile alisogea pembeni kubadili nguo na kurudi akiwa amejifunga kipande cha shuka. Aliniambia nisimame kwenye jiwe dogo kisha alinieleza nichote maji na kujimwagia miguuni. Nilifanya vile kwa kujimwagia.



    Kila alipomwagia maji, mzee Sionjwi alinisugua na majani kisha nilijimwagia tena kuondoa uchafu niliosuguliwa. Alianzia miguuni kwa kunisugua na mimi kujimwagia maji, alipanda hadi kwenye mapaja kwa mimi kukunja kanga ili kuziziba sehemu nyeti zisiwe wazi.



    Aliendelea na zoezi lake huku akiniweka kwenye wakati mgumu kwani nilijisikia hali tofauti lakini nilijikaza kwa vile pale nilikuwa kwenye kazi maalum. Ilipofika zoezi la sehemu za siri alinipa majani na kunieleza nijisugue mwenyewe sehemu zote na kujimwagia maji ya dawa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alisimama kando na kuniacha nifanye yangu, nilijisugua kwa majani sehemu zote kwa kuhakikisha nagusa kila kona.

    Nilipomaliza kujisugua nilimwita tuendelee na zoezi la kuendelea kunisugua. Baada ya zoezi lile tulihamishia juu kuanzia kichwani kuteremka mpaka kiunoni ili kukamilisha zoezi letu la awali kwa mimi kujimwagia maji kichwani na yeye kunisugua.



    Kila aliponisugua alinieleza nijimwagie maji nami nilifanya vile, alipomaliza kichwani alihamia mabegani na kunisugua na mimi kujimwagia maji. Kazi ilikuwa ngumu alipokuwa akinisugua kifuani hasa kwenye matiti, yule mzee alikuwa kama anafanya makusudi kwa kunisugua kama ananitomasa.

    Pamoja na kuwa kwenye tiba hali yangu ilikuwa mbaya na kutamani.



    Pamoja na kuwa kwenye tiba hali yangu ilikuwa mbaya na kutamani nimuombe mzee Sionjwi apunguze angalau kidogo hali yangu iliyokuwa mbaya sana. Asikuambie mtu sisi wanawake tuna wakati mgumu sana tunapokutana na waganga wa kiume hasa katika tiba inayohusu kuguswa sehemu zenye mihemko.



    Wakati huo nilihisi mwinuko chini ulionigusa niliamini kabisa hata babu hali yake haikuwa nzuri. Niliamini kwa mwanaume yoyote shababi hawezi kustahimili kuugusa mwili kama wangu na kubakia vilevile. Umbile langu hata likiwa kwenye nguo lilikuwa utata mtupu itakuwa nimevua nguo zote na kujifunga kanga ambayo nayo ilikuwa imeloa na kuganda mwilini.



    Ajabu nyingine babu alipokuwa akinisugua kifuani aliganda eneo moja la matiti kwa muda mrefu huku akitoa pumzi za kushikika. Wakati huo mwili wangu nao ulikuwa kwenye hali mbaya sana na kuhisi miguu kutetemeka kwa ashki. Hata sikuelewa kilichoendelea zaidi ya kujikuta katikati ya kilele cha burudani.



    Mtoto nilisahau kabisa kama nipo kwenye tiba kwani nilikuwa na muda mrefu sijakutana na shuruba pevu kama ile. Tiba ilibadilika na kuwa penzi zito lililokata kiu yangu mpaka tunaachiana mwili niliusikia mwepesiii. Moyoni nilipanga kama nitakwenda kusoma basi nitahakikisha hata nikiolewa lazima niwe nakutana naye hata mara moja kwa mwezi.



    Baada ya mtanange wa kukata na shoka kwenye majani na zoezi kubadilika babu alinieleza kuwa tiba imeharibika hivyo tulitakiwa kurudia zoezi lile siku ya pili muda kama ule.

    “Babu huoni muda unakwenda?”



    Japokuwa ilikuwa mwisho wa wiki niliona kama naweza kuchelewa kama mchezo ule utaendelea na kujikuta badala ya tiba ingegeuke kijiwe cha kufanyia mapenzi na kupoteza maana yote ya mimi kufunga safari kufuata tiba.

    “Hatuna jinsi tukilazimisha tutaharibu kila kitu.”



    “Sasa babu kama ulijua hivyo kwa nini umekubali kufanya mapenzi?”

    “Mjukuu, huwezi kuamini hata mimi sijui ilikuwaje zaidi ya kujikuta katikati ya safari.”

    “Kwani tukioga na kuanza upya kuna nini?”



    “Mzimu umekasirika badala kufanya kilichotupeleka tumechafua kazi. Kwa leo haiwezekani tena baada ya kuuita ulifika kwa ajili ya kusikiliza shida yetu lakini kitendo tulichokifanya umekasirika na kuondoka.”



    “Ha! Babu huoni tumeharibu kila kitu sasa tutafanyaje kama tumeuudhi mzimu?” nilishtuka kusikia tumeuudhi mzimu ambao ulifika kutusikiliza shida yetu lakini tukaudharau kwa kufanya mapenzi mbele yake tena kwenye sehemu yake inayoiheshimu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ni makosa ya kawaida katika kazi.”

    “Sasa itakuwaje?”

    “ Hiyo niachie mimi.”



    “Lakini babu taratibu za huku unazijua vizuri, mimi na wewe nani mganga?”

    “Mganga mimi, ndiyo maana nikakuambia kesho tunarudia zoezi.”

    “Mzimu utakubali?”



    “Nimekueleza kazi yote niachie mimi, hii si mara ya kwanza kutokea kitu kama hiki, najua namna ya kurekebisha. Kesho tutakuja na kuku mwekundu tutamchinja kabla ya kazi kila kitu kitakuwa sawa.”



    Kauli ya babu ilionesha kabisa ule ulikuwa mchezo wake alipowapeleka wanawake katika zoezi la kuwaosha. Hali ile ilinitisha sana kuonesha babu atakuwa ametembea na wanawake wengi kibaya bila kondomu. Lakini sikutaka kuuliza kitu kwa vile nilimjua lazima tungetibuana nilikaa kimya na maswali yangu moyoni.

    “Sasa vipi na kesho ikitokea kama leo itakuwaje?”



    “Kesho nitatumia njia nyingine ambayo haitatuingiza kwenye vishawishi vya ngono.”

    “Kwa nini hukuitumia leo?”

    “Hii niliyotumia ni njia fupi unafanya vitu viwili kwa wakati mmoja, lakini kilichotokea ni bahati mbaya kwa vile hata mimi mwanadamu pamoja ni mganga nina roho ya matamanio kama wengine.”

    “Mmh!” nilijilaumu kuacha kilichonipeleka na kuingia kwenye kitu kingine kilichofanya tuharibu zoezi lililonitoa mjini kwenda kugeuza matokeo ya mimi kwenda kusoma nje ya nchi.



    Lakini kwa upande wa pili mzee alinitendea haki kwa kunikata kiu ya muda mrefu kukutana na mwanaume mwenye nguvu kama faru. Umri wa babu na kazi aliyonifanyia vilikuwa vitu viwili tofauti.



    Baada ya zoezi kuharibika tuliahirisha tiba na kukubaliana kazi ile tuifanye kesho yake. Baada ya kuoga na kila mtu kuvaa nguo zake tulianza safari ya kurudi nyumbani. Njiani nilimuuliza babu kuhusiana na uwezo wake wa kuweza kumridhisha mwanamke tofauti na umri wake wakati kuna vijana wadogo hawana nguvu kama zake.

    “Babu kuna siri gani ya umri wako na nguvu ulizonazo?”



    “Mjukuu sisi watu wa zamani hatuli vitu vya kutengeneza tunakula chakula cha asilia pia hata dawa zetu zina nguvu hazichanganywi na kitu cha kuipunguza nguvu.”

    “Unawezaje kuwaridhisha wanawake wote tena vijana?”

    “Kwa vile nina uwezo, ukiona kapu linaendelea kuingia vitu ujue bado lina nafasi.”



    “Babu hapo umeniacha njia panda unamaanisha nini?”

    “Ukiona mimi mzee nachukua wasichana wadogo ujue uwezo wa kuwahudumia ninao. Naweza kugawa dozi kwa kila mmoja kila siku, lakini sasa hivi kila mmoja anapata siku mbili anamuachia mwenzake ila anayeshikika kwa dharura huwa anapata huduma ya kwanza.”

    “Mmh! Kweli wewe kiboko.”



    “Kwani we umeonaje?”

    “Mmh! Temea chini babu umekamilika.”

    “Basi mjukuu, kama babu hakufikishi kuna dawa nitakupa utamwekea kwenye chai, nakuhakikishia tabu zote zitaisha nawe utafaidi kama wenzako.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nitashukuru babu, lakini baada ya kurudi safari yangu, naogopa nikimwekea sasa hivi na mimi kuondoka nitakuwa nawatengenezea wengine huenda nikirudi asiwe wangu.”



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog