Search This Blog

THE NIGHTMARE - 5

 







    Simulizi : The Nightmare

    Sehemu Ya Tano (5)



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sharji alifikicha macho yake ili kuhakikisha kuwa ni kweli aliyesimama mbele yake ni kaka yake.

    Alimsogelea na kuanza kumpapasa kama anamkagua Fulani hivi.



    “vipi kwani, umeota ndoto mbaya nini?” aliuliza Katimu huku akionyesha wazi kumshangaa mdogo wake.



    “kaka, hivi Balqis yupo wapi?” aliuliza Sharji na kumfanya kaka yake acheke.



    “Balqis?.... Balqis ndio nani?... yaani watu uliowaota ndio unanitajia mimi, hebu amka basi twende.”

    Aliongea Karimu na kumfanya mdogo wake kutaharuki. Kila kilichomtokea usiku kucha kilifanana na ukweli. Alivuta taswira ya toka jana yake kuanzia aliposikia harufu kali ya perfume ya Baiqis mpaka alipopewa bahasha ya hela. Pia alivuta taswira ya safari ya mashaka ambayo mpaka muda huo alikua haamini yote hayo yalikua ni ndoto.



    “twende wapi?” alijikuta sharji akimuuliza kaka yake.



    “acha ubwege, we hujui kama leo ndio safari yetu ya kuelekea visiwa vya Comoro?” aliuliza kaka yake ambaye mpaka muda huo aliamini mdogo wake alikuwa na mawenge ya ndoto.



    “nyie nendeni tu, mimi siendi popote.” Aligoma Sharji.



    “acha utoto wewe, unajua hii safari nimeiandaa kwa ajili yako?” aliongea Karimu kwa hasira.



    “tatizo lako kaka hujui nilichokiota juu ya hii safari. Laiti kama ungelijua, basi ungeli ghairi hii safari.” Aliongea Sharji na kumuangalia kaka yake ambaye alikua amekasirika muda huo.

    “haya niambie umeota nini?” hatimaye Karimu alimuachia uhuru mdogo wake amuelezee.



    “tuache tu kaka, maana inatisha sana.” Aliongea Sharji na kuonyesha hali ya kuogopa kumuelezea kaka yake.



    “pole mdogo wangu kwa ndoto mbaya uliyoota juu ya safari yetu. Hayo ni mawenge tu yampatayo mtu yeyote ambaye hajawahi kusafiri majini. So we amka kajiandae tuondoke zetu.”aliongea Karimu kwa sauti ya upole.



    Baada ya kubembelezwa sana, Sharji akakubali kiroho upande na kwenda kujiandaa kwa kuoga na kuvaa nguo nyingine tofauti na ile aliyopanga kuvaa hapo awali ambapo aliiota ile nguo.



    Alipomaliza kunywa chai, alitoka nje na kuwakuta wasafiri wote wakiwa hai wanamsubiri yeye tu kwenye coaster iliyopaki nje kwao.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Katika watu wote waliokuwa pale, hakumuona Balqis. Ndipo alianza kuamini kuwa ile ilikuwa ni ndoto tu.



    Walipofika feri, walipewa nahodha mwingine tofauti na yule aliyemuota na boti ilikuwa ndogo tu ya kawaida tofauti na ile aliyoiota.



    Safari hiyo ilianza kwa furaha ya watu wengi kasoro Sharji ambaye bado ana wasi wasi japokuwa upande mwingine aliamini kuwa ile ilikuwa ni ndoto tu na haiwezi kuwa kweli.



    Mziki mkubwa ulirindima. Watu walicheza, walikula na kunywa huku wakiburudika kutokana na upepo mwanana uliokuwa unawapuliza.



    Walifika salama usalimini safari yao hiyo na kupokelewa na wenyeji wa hotel waliyopanga kufikia na kwenda kwenye vyumba vyao.



    Usiku wa siku hiyo hawakulala. Maana wasanii wawili mapacha kutoka Nigeria walikuwa na shoo huko visiwa vya Comoro.



    Baada ya kuwashuhudia P.square live walirudishwa hotelini na gari ya hotel na kwenda kupumzika.



    Mchana wa siku hiyo walienda kwenye zoo ya wanyama na kuangalia wanyama mbali mbali. Baada ya hapo jioni walirudi hotelini na kuangalia Live band ya huko iliyokuwa ikitumbiza kwenye hotel hiyo.



    Matukio yote hayo yalimfanya Sharji kurudi katika hali yake ya kawaida kwakua alikua na hofu kubwa iliyokaa akilini mwake muda mrefu. Sasa alikuwa huru na furaha yake ikajitokeza dhahiri baada ya kuwaona wanenguaji wa kicheza kwa style iliyomvutia.



    “ndoto zingine zinaweza kukufanya uwe kichaa.” Aliongea Sharji peke yake na kujicheka ujinga kwa kutaka kukataa kula raha zile ugenini.



    Baada ya live band kumaliza. Waliamua kwenda kupumzika kwenye vyumba vyao.



    Asubuhi ya siku ya tatu iliwadia na Ratiba ilikua ni kwenda kwenye jumba la makumbusho ya huko Visiwa vya Moroco.



    “ Fred anapenda sana kulala. Yaani mpaka muda huu hajaamka?” aliongea mmoja wa marafiki wa Karim.

    “si unajua jana alipombeka sana. Sasa tunafanyaje, tunamuamsha au tunamuacha?” aliongea Karim baada ya gari la ile hoteli kuwa lipo tayari kwa safari yao.



    “tumuamshe bwana, sio vizuri kumuacha.” Alishauri Sharji .

    “poa, kamgongee.” Aliongea Karimu na Sharji akaenda kugonga kwenye chumba alicholala Fred.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “ mbona mtu mwenyewe haamki?” aliongea sharji baada ya kugonga muda mrefu bila ya majibu.



    Wote kwa pamoja waliungana na kugonga mlango. Lakini waliambulia patupu.



    “itakuwa amepatwa na tatizo. Mtafute manager wa hotel atupe funguo nyingine tufungue.” Aliongea Karimu na zoezi la kumtafuta manager lilianza. Baada ya manager kufika pale, walifungua mlanguo na kupigwa na butwaa baada ya kumkuta Fred yupo kitandani huku akiwa na mapovu mdomoni,



    Manager alimsogelea na kuangalia mapigo ya moyo wake, hakusikia chochote.. alipomgusa mwili wake ulikuwa wa baridi.

    Manager alimfunika macho na kuwafanya watu waliokuwa pale kujiinamia.



    “ameshapoteza maisha huyu. Ngoja tutoe taarifa polisi.”



    Aliongea Manager wa hotel hiyo na kuwapigia simu polisi.

    Waliuchukua mwili wa Fred na kuupeleka kwenye maabara kwa uchunguzi.

    Karim na wenzake waliitwa polisi kwa mahojiano.



    Wakati wote wa tukio hilo, Sharji alianza kukosa amani tena kutokana na tukio hilo kufanana na ndoto yake. Maana kwenye ndoto alilala na Fred na yeye kumtoroka na kwenda kulala na Balqis hali iliyomfanya Fred kupoteza maisha wa kwanza katika ndoto yake.



    Walipofika polisi walianza kuhojiwa mmoja baada ya mwengine. Ilipofika zamu ya Sharji, alianza kutetemeka huku kijasho chembamba taratibu kikaanza kumtoka. Hata siku moja hajawahi kufika kituo cha polisi. Hali ya uoga ikichanganywa na hali ya wasi wasi juu ya safari hiyo ndio kulimfanya apatwe na kitete.



    Baada ya muda alimaliza mahojiano japokuwa alikuwa na wasi wasi mkubwa. Waliingia watu wote na Amina ndio alikuwa wa mwisho kufunga dimba.



    Muda ulizidi kwenda toka Amina aingie kwenye chumba cha mahojiano. Hatimaye masaa mawili yalipita bila Amina kutoka.



    “huyu askari anamuhoji kweli au anafanya mambo mengine?... maana masaa mawili sasa yameshapita” aliuliza Juma baada ya kuona muda unazidi kuyoyoma bila dalili zozote za Amina kutoka.



    Dakika tano baadae, walishangaa kumuona yule askari aliyekuwa anawahoji akiwa ndio anaingia na gari la polisi.



    “samahani afande, kwani nyie mpo mapacha?” aliuliza Karim ambaye alimsimamisha yule askari.

    “hapana, kwani vipi?.” Alikanusha yule askari.

    “sijakuona wakati unatoka ndio maana nashangaa?” aliongea Karim na kumfanya yule askari kumshangaa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “kwani tumesha onana mimi na wewe leo?” aliuliza yule afande na watu wote waliokuwa pale nje wakabaki wameduwaa.

    “jamani maajabu haya, wewe si ulikua unatuhoji ndani!!!?” aliuliza Karimu kwa mshangao mkuu.

    “mmenifananisha, mimi ndio kwanza naigia ofisini mida hii.” Aliongea yule afande na kuigia kituoni.



    “sasa aliyekuwa anatuhoji ni nani kama sio huyo?”



    Alijikuta anajiuliza mwenyewe swali lililompa utata mkubwa kichwani mwake.

    Wakati wakiwa hawajui hili wala lile, walishangaa kuona maaskari wakijazana pale na ambulance ikafika haraka. Wakiwa makini kufuatilia ni nini kilichotokea, walishangaa kuuona mwili wa Amina ukiwa umeraruriwa vibaya huku damu iliyoganda ikiwa imechafua nguo zote alizovaa..



    Hali hiyo iliwashangaza sana na kubaki wakiwa wamepigwa na bumbuwazi. Sharji ndio kabisa. Aliamua kuondoka na kukimbia bila kujua alikua anaelekea wapi.



    “Sharji,…..Sharji subiri.”

    Ilikua sauti ya kaka yake ikimuomba asimame.

    Ilikua kama kachanganyikiwa baada ya kuushudia mwili wa Amina. Kumbu kumbu zikamrudisha kwenye boti na kugundua kua ni Amina ndio mtu wa pili kufa. Hapo aliamini si ndoto tena. Hali waliyonayo ni halisi na hakuna atakayesalimika.



    Baada ya kukimbia mwendo mrefu, Sharji alichoka na kujibwaga chini. Alijua bila shaka atakua jini Baqlis aliyemuota kwenye ndoto.



    Dakika tatu baadae, Karimu na kundi lake walimfikia Sharji pale alipo huku na wao wakiwa wanahema kutokana na kukimbia umbali mrefu.



    “kuwa na moyo wa kijasiri mdogo wangu. Hapa inatakiwa leo hii hii turudi kwetu.” Aliongea Karimu baada ya kupumzika kwa muda wa dakika tatu.



    “kaka ile ndoto niliyoi….. angalieni kulee”

    Sharji hakumalizia kauli yake, kwa mbali alimuona ndege mkubwa mwenye umbo la binaadamu akishuka kwa spidi ya ajabu. Kabla hawajafanya lolote, yule ndege alitua na kumchukua mtu mmoja kati ya watu waliokuwa pale.



    Walinyanyuka na kuanza kukimbia kila mtu na njia yake. Baada ya mwendo mrefu. Sharji alianza kusikia sauti ya kaka yake ikimuita huku analia. Alipogeuka nyuma. Alimkuta yule ndege akimkata kata kaka yake kwa makucha yake. Sauti ya kaka yake ikakatika baada ya kushuhudia kwa macho yake kichwa cha kaka yake kikichomolewa na kudondoka chini.

    Baada yule ndege kumaliza mauaji hayo, yule ndege wa ajabu mweye umbo la binaadamu, alimuangalia kwa macho makali Sharji na kumrukia

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yule ndege alimchukua Sharji kwa spidi na kuruka naye juu kabisa ya anga. Kutokana na spidi kuwa kali,Sharji hakuweza kuona vizuri kutokana na upepo mkali. Alilia huku akimuomba yule ndege amshushe. Yule ndege alimpulizia hewa yake usoni na Sharji akazimia.



    Fahamu zilipomrudia. Alijikuta yupo sehemu nzuri yenye maua mengi yenye harufu nzuri. Akiwa anashangaa mandhari hiyo ambayo hajawahi kuyaona toka azaliwe, alisikia jina lake linatajwa.



    Alipogeuka nyuma, alishangaa kumuona msichana mzuri akija kwa madaha akiwa amevaa kofia iliyokuwa na nyavu mbele ambayo ilimzuia kuiona sura ya yule msichana.

    Yule msichana alimsogelea na kuivua ile kofia na kuiweka pembeni. Uzuri wa binti huyo ulimfanya Sharji ashtuke baada ya kumkumbuka. Huyo msichana alikuwa ni BALQIS aliyemuota kwenye ndoto yake. Alifikicha macho yake labda alikua ndotoni. Lakini aliamini kuwa haikuwa ndoto baada ya msichana huyo kumsogelea na kumuamuru akae. Bila ubishi, Sharji alikaa na kusikiliza kitu atakachoambiwa.

    “pole kwa kufiwa na kaka yako mpendwa.” Aliongea Balqis na kumuangalia Sharji aliyekuwa na wasi wasi mkubwa.

    “wewe ni mtu mbaya sana. Kama umeamua kumuangamiza kaka yangu. Unasubiri nini kuniangamiza na mimi?” aliongea Sharji huku akimuangalia Balqis kwa macho makali.



    “upo gizani Sharji. Hivi unajua kuwa safari ya Comoro ilikuwa inahusiana na kifo chako?” aliuliza kwa hasira Balqis.

    “unamaanisha nini?” aliuliza Sharji kwa mshangao mkuu.



    Balqis alinyanyuka bila kuongea kitu chochote. Alinyoosha kidole chake kwenye moja ya maporomoko ya maji yaliyokuwa eneo hilo na kutokea TV kubwa.

    “angalia mwenyewe ujionee.”aliongea Balqis baada ya kuiwasha ile tv ya ajabu.



    Alionekana Karimu akiwa ofisini kwa baba yake wakigombana kuhusu swala la hela. Karim aliondoka na kwenda kumuhadithia rafiki yake juu ya mzazi wake anavyombania hela za matumizi. Rafiki yake akamshauri kwenda kwa mganga. Walipofika, mganga aliwasikiliza shida yao na maamuzi yalikuwa kumtoa uhai baba yake.



    Tukio la uchawi wa mganga kumuingia Khalidi na kusababisha ajali aliuona Sharji kwa macho yake. Baada ya hapo mganga alienda hospitali kummalizia na ndio ukawa mwisho wa maisha ya baba yake na mama yake kufa kwa preasure baadae.



    Haikutosha, alimuonnyesha pia baada ya miezi sita kupita. Karim akishirikiana na rafiki yake wakirudi kwa mganga ambaye aliwaambie wafanye kafara ya mwisho ambayo ni kumtoa mdogo wake ampendaye Sharji. Karimu alikubali na kupewa masharti ya kuazisha safari ya mbali na wanapoishi na kumuua huko bila yeye mwenyewe kujua wala kuhisi tukio hilo. Wakishirikiana na marafiki wengine, walipata wazo la kuandaa picnic na kwenda visiwa vya Comoro ambapo watamuua huko.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “nadhani umeona yaliyotaka kukuta… we unafikiri ningefanyaje?... nilikuotesha ile ndoto ili ukatae hiyo safari. Lakini uliidharau hiyo ndoto na ndio maana nikatumia uwezo wangu kuwaangamiza wabaya wako ili mradi wewe uwe mzima.”

    Aliongea Balqis baada ya kuzima ile tv kimaajabu. Sharji aliipata picha nzima na hakuamini kuwa kaka yake alikuwa mnyama kiasi kile. Alipigwa na butwaa na kumuangalia Balqis na kujiuliza maswali ambayo yalikosa majibu ya haraka.



    “kwanini umeamua kunisaidia?” aliuliza Sharji baada ya kuona ni jinsi gani jini huyo alivyokuwa karibu na yeye muda wote huo.



    “mimi narudisha fadhila kwako kwa kunikomboa mimi.” Aliongea Balqis na kumfanya Sharji ashangae.

    “nimekukomboa?.. kivipi yaani. Maana hatujawahi kuonana wewe na mimi zaidi ya kwenye ndoto na leo ndio nakuana live.” Aliuliza Sharji kwa mshangao mkuu.



    Balqis alinyanyuka na kuileta ile Tv.



    Alijiona yeye akiwa na familia yake yote wakiwa Beach. Wakiwa wanaogelea maji ya bahari, alikiokota kichupa kilichofungwa na kukifungua. Alipoona hamna kitu, alikitupa na kuendelea kuogelea.



    Balqis alizima tv yake na kuanza kumuelekeza Sharji.

    “mimi ni jini mzuri na ninayependa kuwasaidia watu. Pia nina uwezo mkubwa tofauti na majini wengi. Kwa hiyo majini wengi walinichukia na kuniwinda kwa ajili ya kuniangamiza. Walifanikiwa kunikamata na kunifungia kwenye ile chupa miaka mia mbili iliyopita. Siku hiyo ulipoifungua ile chupa. Ulinifanya nitoke na kuwa huru tena. Toka siku hiyo nikaanza kuangalia maisha yako na kuyalinda. Na yeyote aliyekuwa na nia mbaya na wewe. Nilikuwa tayari kupoteza maisha yake. Akiwemo kaka yako na wenzake. Samahani na pole kwa kukupotezea kaka yako uliyempenda lakini ukweli yeye hakukupenda hata kidogo.”

    Aliongea Balqis na kumfanya Sharji amshukuru baada ya kugundua ukweli.



    “ukijihisi mpweke duniani, unaweza kuishi na sisi huku. Au una semaje?” aliongea Balqis na kuwaita majini wenzake anaoishi nao. Walikuwa wazuri na wenye sura za kuvutia. Walikuwa rika mbali mbali. Na wote walionekana wakitabasamu kama ishara ya utayari wa kumpokea Sharji kama mwenzao.



    “nashukuru. Sema naomba unirudishe duniani.” Aliongea Sharji baada ya kufikiria kwa muda.

    “sawa. Fumba macho yako. Na nikikuambia fumbua utakuwa umeshafika duniani.”



    Sharji alifumba macho yake. Haikupita hata dakika moja. Akasikia sauti ya Baiqis akimuambia fumbua.



    Alipofumbua macho yake alijikuta yupo nyumbani kwao. Alishangaa na kuanza kuikagua ile nyumba ambayo ilikuwa haina mtu mwingine zaidi yake.



    Alienda kudhuru makaburi ya wazazi wake na kumuombea msamaha kaka yake kwao kwakua alikua hajui alitendalo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Balqis alimtokea mara kwa mara Sharji na kumpa company alipokuwa mpweke. Alimuokoa na vitu vingi kama ajali na mambo mengi yaliyohatarisha uhai wake.



    MWISHO



0 comments:

Post a Comment

Blog