Search This Blog

NYOKA WA KUTUMWA - 4

 





    Simulizi : Nyoka Wa Kutumwa

    Sehemu Ya Nne (4)



    Bibi sube alishangaa sana kuona Duba akifa kijinga kiasi kile utadhani mtoto mdog asie na nguvu ya kujitetea, wakaondoka mahara pale na kurudi nyumbani kwao na kumuacha Duba akiwa amelala chini huku damu nyingi zikiendelea kumvuja. Walipofika kwao na kubadilisha zile nguo zao, Bibi Sube akaanza kumuuliza mume wake hukusu kilichotokea.

    BIIBI SUME: Mume wangu umewezaje kumuua yule mtu kiurahisi vile, maana nilijinga ipasavyo kwa mapambano nilihisi kungekuwa na kurupushani kubwa.

    SUBE: Nilikuambia Duba kwangu mimi ni kama mtoto atambaae, anitishi hata kidogo, sisi wakubwa wewe.

    Bibi sube alitabasamu kisha wakalala zao na hatimae ile siku ikapita na kuja siku nyingine. Kwa upande wa yule kijana mgeni wa Duba akaamuka mapema sana na kwenda sehemu aliyokuwa amelala Duba, alipoona hayupo moja kwa moja akajua itawa ayari ameamka mapema zaidi yake, akatoka nje akitegemea kukutana na Duba. Hakuamini macho yake baada ya kuoona mganga aliekuja kumchukua akiwa amelala chini huku damu zikiwa zimemtapakaa. Akamsogelea huku akiwa na hofu kubwa nafsi mwake, akamtazama ndipo akagundua ameshakata roho, alishtuka sana na kuanza kupiga mayowe ya kuomba msahada kwa majirani wa yule mzee, na mda mfupi mbele watu wakaja nyumbani kwa Duba huku huzuni kubwa ikitawa kutokana na kuondokewa na mganga wao aliekuwa akiwasaidia. Wakaubeba mwili wa Duba na kuupeleka ndani kisha wakamtuma tena yule kijana apelike ile taarifa kwa mfalme. Kijana akatoka na kuinza safari yake huku akiwa anakimbia na baada ya masaa kadhaa akafanikiwa kufika kwa mfalme na kukuta akiwa na baadhi ya wazee wakiongelea mambo mengi kuhusu kijiji chao. Kabla hata ya salamu yule kijana akaanza kutoa ile taari huku akihema kwa haraka.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    KIJANA: mtukufu Mfalme mganga amefariki.

    Mfalme pamoja na wale wazee walishtuka maana ile taarifa ilikuwa mbaya kwa upande wao kutokana na umuhimu ambao alikuwa nao Duba kwa kipindi kile.

    MFALME: Eeeeeee !!? Amefariki ?

    KIJANA: Ndio mtukufu mfalme amefariki.

    MFALME: Kwahiyo wewe ulimemkuta ameshafariki au.

    Kijana wakati anataka kusimulia mara mzee sube akawasili sehemu ile, ndiupo mfalme akamkatisha yule kijana na kumkaribisha mzee sube na kumpa taarifa ya msiba wa Duba na wakati yeye ndie aliesababisha kifo chake.

    MFLME: Karibu sana mzee Wangu .

    MZEE SUBE: Ahsante sana mtukufu mfalme.

    MFALME: Mzee tumepatwa na tatizo yule mganga ambae tulitegemea atusaidie juu ya lile jambo letu amefarikii.

    alipoambiwa hivyo kwa unafiki akajifanya kushtuka na kushanga kama sio yeye aliefanya hilo tukio .

    MZEE SUBE: Eeeeee !! Duba amefariki, Tumeangamia.

    MFALME: Ndio hivyo mzee sube.

    MZEE SUBE: Mh! kwani alikuwa anasumbuliwa na nini mpaka amefariki maana imekuwa ghafla.

    MFALME: Hata mim sijui hivi hapa ndio nlikuwa nanimuulza huyu kijina ambae nilimtuma jana akamuite huyo mganga, yeye ndio ameleta hii taarfa za msiba. Haya kijina nambie ilikuwaje.

    Akaanza kusimulia huku watu wote wakimsikiliza kwa makini, mda wote mzee sube alikuwa akijifanya kusikitika kuhuzunisha na msiba ule.

    KIJNA: Mtukufu mfalme nilipofika nilimkuta yule mzee mzima wa afya tena akitengeneza dawa, nilipomueleza wapi natoka alifurahi sana nikampa ujumbe ulioniagiza, ila yeye akaomba jana nipumzike alafu leo asubuhi tuanze safari ya kuja huku, lakini cha ajabu leo nimeamka nimemkuta nje amekata roho huku damu nyingi ikiwa usoni mwake ususani maeneo ya poani, mdomoni na masikioni.

    Aliponyamaza Sube akadakia na kuanza kuongea kabla mfalme ajasema kitu chochote.

    MZEE SUBE:Mtukufu mfalme hapo kuna mkono wa mtu ambao unafanya hayo yote tena ni kati yetu sisi wazee maana haiwezekani kila tunachopanga kinaharibika, lazima kuna msaliti kati yetu..

    alisema vile ikiwa kama kujisafisha kwa upande wake, wote walikuwapo mahali pale walikubari kile alichokisema mzee Sube na kuamini kabisa kati yao kuna msaliti, Wakiwa kwenye hali ya kuulizana nani msaliti malme akasimama na kuanza kuongea.

    MFALME: kweli kabisa ulichokisema mzee sube haiwezekani kila siku mipango yetu ihalibike, sasa ninasema hivi endapo nitamgundua huyo msaliti hukumu ya kifo itakuwa juu yake.

    Waliendelea kuongea kwa mda kuhusu lile swala, walipomaliza wale wazee wakaruhusiwa warudi majumbani kwao lakini mzee Sube aliombwa abaki maana mfalme alikuwa anataka kuongea nae. Wazee wote wakaondoka huku wakiulizana nani msaliti, wakati huo maongezi ya mfalme na mzee sube yakaanza.

    MFALME:Nimekuambia ubaki kwa sababu katika wazee wote hapa kijijini wewe ndio ninakuamini na kukutegemea, ila kutokana na kile ulichokisema kuna kitu nimekihisi kutoka kwa wale wazee wenzako.

    MZEE SUBE: Kitu gani hiko mtukufu mfalme.

    MFALME: Katika hawa viongoz wangu kuna mzee mmoja namuhisi kuwa ndie anaetugeuka tunapokuwa tunapanga mambo yetu.

    MZEE SUBE: Nani huyo.

    Mfalme akamtazama Sube kwa jicho Fulani lililopelekea sube kuogopa na kuhisi labda amejirikana maana hata siku moja mfalme hakuwai kumwangalia kwa jicho kama lile, kisha akaanza kuongea.

    MFALME:Nahisi mzee Bugu ndie msaliti.

    Sube akashusha pumzi zake taratibu na kuanza kuongea.

    MZEE SUBE:Kweli kabisa mtukufu mfalme maana hata mimi nilikuwa ninamuhisi huyo huyo Bugu lakini nilikuwa nashindwa kukuambia niliogopa kuonekana mchonganishi.

    MFALME: Kumbe hadi wewe umegundua hilo, sasa tufanyaje.

    MZEE SUBE: Kwa kuwa hatuna uhakika bora umtoe uongozi na umpe mtu mwingine unae muamini ili tutakapokuwa tunapanga mambo yeye asiwepo.

    Sube alisema hivyo kwa sababu mara kwa mara Bugu alikuwa akipinga maneno yake na kwenda kinyume kabisa na yeye, aliona atamwaribia mambo yake. Mfalme bila kujiuliza wala kutafakari akakubaliana na mzee sube wafanye hivyo.

    MFALME: Sawa mzee wangu nimekuelewa na nitafanya hivyo.

    Mzee sube akaruhusiwa kuondoka maana walikuwa wamemaliza maongezi, akaenda nyumbani kwake na kumsimulia mke wake kila kitu kilichotea kwa mfale, Bibi sube alifurahi sana na kumpongeza mume wake kwa kazi mzuri aliyoifanya.Badaa ya hapo masaa yalienda na hatimae ile siku ikawa imepita, siku iliyofuata mfalme akaita wale viongozi wote na kufanya nao mkutano wa dharula ambao haukutegemewa na mtu yoyote yule.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MFALME: Nimewaita hapa kuna kitu nataka niwaambie na hiko kitu kinahusu kubadilisha uongozi maana kuna baadhi yenu kwa sasa mme zeeka sana kwahiyo inabidi muwapishe na wenzenu ili nyie mupumzike. Kwahyo leo nimeamua kumtoa uongozi mzee bugu na kumpatia mzee sube.

    Mzee sube alishangaa sana kusikia vile maana hakutegemea kama mfalme angempa kile cheo, ndipo akaanza kupiga makofi huku akimshukuru mfalme kwa hatua aliyoichua. wale viongozi wengine baada ya kuona sube akipiga makofi na wao wakajaribisha huku hali ya mshangao ikitawala usoni mwao, maana lile jambo lilikuwa la ghafla na kwa pale kijijinni kwao hakukua na sheria ya mfalme kumtoa mtu uongozi bila kuomba ushauri kutoka kwa wale wazee, lakin kwa upande wa sube furaha ilitawa. Mfalme akaendelea kuongea.

    MFALME: kwahiyo kuanzia leo mzee sube atakuwa kiongozi kama nyie wengine.

    Kikao kiliendelea kilipoisha na hatimae kikafika tamati ndipo wale wazee wakaondoka na kumuacha sube pamoja na mfalme, wakiwa njiani wakaanza kuwaongelea wawili wale.

    KIONGOZI 1: Jamani mwenzenu hata sielewi nini kinaendelea kati ya mzee sube pamoja na mfalme.

    KIONGOZ 2: He! Kwahiyo ww ndio umejua leo ?. Sisi wenzako tumeliona hilo tangu zamani sana.

    MZEE BUGU: mimi nashangaa kitu kimoja tu. leo mimi na mzee sube naonekana mimi ndio mzee kweli na wakati nimezaliwa nimemkuta mzee sube ndio anajifunza kuongea.

    KIONGOZ 1: Bugu pale lazima mzee sube kuna alichokifanya sio bure .

    KIONGOZ 2: Hata mimi naona hivyo hivyo, ila hebu tuachane na hizi mada maana sio mzuri.

    waliachana na ile mada na kuongea mambo yao mengine na hatimae wakafika makwao. Kwa upande wa vijana wa kile kijiji siku hiyo na wao walifanya kimkutano kidogo wakiongelea kuhusu yule nyoka jinsi gani wafanye ili wafanikiwe kumnasa.

    KIJANA 1: Hivi munajua huyu nyoka tusipomfanyia kazi atatumaliza wote.

    KIJANA 2: Kweli unachokiongea maana sisi ndio tunaotegemewa hapa kijijini tukiwa kama vijana na sifa ya hiki kijiji chetu kuwa na vijana mashupavu, mashujaa sasa itakuaje tushindwe kummaliza haka kadudu kadogo kabisa.

    KIJANA 3: Jamani kuna kitu nilisahau kuwaambia, Juzi nikiwa natoka msituni kuwinda nikapita nyumban kwa mzee sube maana njia ile ndio urahis mimi kufika nyumbani. Sasa wakati napita mbele ya nyumba ya mzee ghafla alinipta nyoka mmoja nakumbuka alikuwa na rangi ya njano kichwani pamoja na mkiani ila sehemu zingine zote alikuwa na rangi ya blue, baada ya nyoka kunipita akaingia kwenye kile kichaka ambacho kipo karibu sana na nyumba ya mzee sube. nikasogea mpaka pale kwenye kichaka ili nimuue yule nyoka ila cha ajabu wala sikumuona bali nilikuta kijisehemu fulani pakiwa pamemwagiwa unga mweupe na mwekundu pamoja na ukili ukiwa katika ule unga wenye rangi. Nikiwa nashangaa ghafla alikuja mzee sube na kunifukuza eneo lile na kuniambia kuwa nisipite tena njia ile .



    KIJANA 4: huyu mzee sube atakuwa anajua ukweli kuhusiana na huyu nyoka.

    KIJANA 1:Itakuwa kweli ulichokisema maana nilishangaa sana kuona tabibu wa kijiji anakosa dawa ya kutibu sumu ya nyoka alafu mzee sube awe nayo, wakati yule mzee Chala ameudumia sehemu hii kwa mda mrefu na hakuna ugonjwa ambao alikuwa anashindwa kutibu, na ndio maana yule mfalme wa jirani alikuwa anamuhitaji sana kutokana na umahiri wake wakazi.

    KIJANA 5: kama ndio hivyo inabidi tuanze kumchunguza huyu mzee maana asijifanye tabibu kumbe anatuchezea akili zetu.

    KIJANA 6: Itakuwa vizuri tukifanya hivyo, kwahiyo tutafanyaje ili tumchunguze.

    KIJANA 2: Inabidi tuwe tunazunguka zunguka sana pale nyumbani kwake mpaka tufanikiwe kumuona huyo nyoka, kama tukishindwa kumuona mchana tutaenda kumchunguza tena usiku mpaka tupate ukweli wa jambo hili.

    Baada ya kukubaliana vile kila mmoja akarudi nyumbani kwao kwa ajili ya kujiandaa na kazi, ilipoika majira ya saa kumi jioni wakakutana na kuanza kupanga njia watakazo zitumia pindi wakifika nyumbani kwa Sube.

    KIJNA 1: Jamani huku tuendako tunatakiwa tuwe makini ili tuifanikishe kazi yetu na itapendeza sana kama Mzee sube hatatuona, maana anaweza kutufukuza. Cha msingi kila mtu ajitoe kwa ajili ya kusaidi mbaka.



    Walipomaliza wakaianza safari yao na kuishia kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa karibu sana na nyumba ya Sube, ndipo akatumwa kijana mmoja aende kwenye kile kichaka kuangalia kama ataona kitu chochote, ila kabla ajaondoka aliambiwa endapo ataonekana na mzee Sube asirudi tena mule ndani bali atoe ishara, kama amefanikiwa kumuona huyo nyoka au laa kisha aende zake. Kijana akafanya kama alivyo akizwa alitoka mle ndani na kusogea mpaka kwenye kile kichaka na kujifanya anashangaa kitu Fulani, lakini kabla hajaona kitu chochote ghafla mzee Sube akatoka ndani kwake na kumkuta yeye akichakua chakua majiani. Kwa hasira sube aliongea.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MZEE SUBE: Wewe kijana unafanya nini hapo au wewe mwizi eee, ebu toka na ukawaambie wenzako sitaki nimuone mtu akipita shemu hii kwa sababu sio njia.

    Kijana baada ya kufukuzwa akatoka bila hata ya kutoa ishara maana Sube alikuwa anaendelea kumuangalia, kwahiyo akaogopa kufanya hivyo asije akagundua kuwa wanamchuguza, wale vijana wengine walishangaa kuona vile lakini hawakuwa na jinsi waliendelea kusubilia labda watoona kitu chochot . Baada ya mda Fulani kupita, nyumbani kwa mzee sube akafika kijana ambae alikuwa ameagizwa kutoka kwa mfalme.

    KIJNA: Mzee sube mtukufu mfalme ameniagiza nije nikuite na amesema tufanye haraka maana mke wake wa pili aitwae Mana ameng’atwa na yule nyoka.

    MZEE SUBE: Sawa tangulia mwambie ninakuja mda sio mrefu.

    KIJANA: Sawa ila amesema usichelewe maana hali yake mbaya sana.

    MZEE SUBE: Sawa kijana nimekuelewa ila wewe tangulia.



    Kijana akaondoka na kumuacha Sube akijianda, huku akimueleza mke wake kuhusu yule kijana

    MZEE SUBE: Mke wangu nahis vijana wa hapa kijijini kama wanachuguza mambo yetu.

    BIBI SUBE: He! Kwanini unasema hivyo mume wangu.

    MZEE SUBE: Nilipotoka nje nimemkuta kijina mmoja kwenye kile kichaka akichambua chambua kama anatafuta klitu Fulani, aliponiona akashtuka, mimi nikamfukuza, ila leo ni mara ya pili naona kijana akisogea maeneo yale ilaw wala usiwe na hofu mke wangu maana hakuna kitakacho alibika.

    BIBI SUBE: Mh! Iwe kweli tu maana mda mwingine huwa naogopa sana nikikumbuka hiki tunacho kifanya.

    MZEE SUBE: Usiogope mke wangu haiwezekani kutokea jambo baya lolote lile. Sasa sikiliza mfalme kamtuma kijana aje kuniita, mke wake kang'atwa na Yoka kwahiyo anataka nikamtibu tena amesema nifanye haraka maana hali yake ni mbaya sana. Kwaihiyo nakuomba ukae pale nje ili endapo atakuja kijana yoyote umkataze kusogea wala kupita karibu na kile kichaka.

    BIBI SUBE: Sawa mume wangu nmekuelewa.

    Sube akaondoka na kumuacha mke wake akijianda kwenda kulinda kile kichaka. Kwa upande wa wale vijanawalipoona Sube ametoka walifurahi sana na kuona kazi yao itakamilika mda mfupi maana aliekuwa akizuia wao kuchunguza kwenye kile kichaka ameondoka, lakini dakika kadhaa mbele walimuona bibi sube akitoka ndani ya nyumba huku akiwa amebeba kitanda cha ukambaa na kwenda kukiweka karibu na kile kicha, huku akifuma mkeka. Kitendo kile kiliwafanya wale vijana wazidi kuamini kuwa wawili wale wana siri kubwa na kwenye kile kichaka kuna kitu wanakificha ndipo wakaanza kuongelea swala lile.



    KIJANA 1: Jamani sasa hivi mimi naamini wazee wale kuna kitu wanakifanya haiwezekani wazuie watu kwenda au kupita kwenye kile kichaka, lazima kutakuwa na kitu sio bure.

    Maneno ya yule kijana yalikubaliwa na kila mtu pale ndani ndipo wakaanza kutafuta mbinu zaidi za kuwakamata wale watu.

    KIJANA 2: Mimi ninaaona bora tukamwambie mtukufu mfalme juu ya jambo hili. Ili tutakapofanya jambo lolote tuwe huru.

    .

    Wakiwa wanaendelea kuongea mara mwenzao moja akamuona mzee Sube anarudi ndipo akawashtua wenzake na kuanza kumchungulia kupita kidirisha kidogo kilichopo kwenye nyumba hiyo, Sube alipofika akaa alipokuwa mke wake na kuanza kuongea mambo ambayo wale vijana hawakuweza kuyasikia kutoka na wawili wale kuongea kwa sauti ya chini. Giza lilizidi kuingia wale vijana wakaamua kupumzika huku wakisubiria kwa hamu ifike siku nyingine wakampe taarifa mfale wao. Asubuhi ilipofika wakaondoka kwenye ile nyumba na kwenda nyumbani kwa mfalme, walipofika huko walipokelewa na kueleza shida yao.

    KIJANA: Mtukufu mfalme tumekuja hapa kuna kitu tunataka tukuambie ukiwa kama kiongozi mkuu hapa kijijini kwetu,kama unavyojua hapa kijijini kwetu tumekubwa na janga la huyu nyoka na mara kwa mara tumekuwa tukitafuta suruisho lakini ilikuwa inashindikana.

    MFALME: ni kwel kwahiyo nyie mnahitaji nini.

    KIJANA: Kwanza kilichotuleta hapa tumekuja kukuambia kuwa tumemjua mtu ambae anasababsha haya matatizo na ndio maana kila tukivyopanga mambo yetu tulikuwa atufanikiwi kwa sababu huyo mtu amekua akienda kinyume na sisi yani ni msaliti.

    Yule kijana baada ya kusema vile moja kwa moja mfalme kichwani mwake akajua wale vijana wanamzungumzia mzee bugu kwa sababu hata yeye amekuwa akimuhisi hivyo. Japokuwa alihisi wanamuongelea mzee bugu ila akaona bora awaulize wale vijana kuwa nani wanamuhisi ili endapo watamtaja mzee bugu atakuwa kapata uwakika kuhusu mzee bugu kuwa kweli ni msaliti.

    MFALME: Ehe vijana nani huyo munamuhisi kuwa ni msaliti wa hiki kijiji na ndie chanzo cha haya matatizo.

    KIJANA: Ni mzee SUBE mtukufu mfalme.

    MFALME: Eeeee !!! Munasemaje nyie vijana ?.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alishangaa sana kusikia vile maana hakutegemea kama wangemtaja mtu anae mwamini kupitakiasi.



    KIJANA: Ndio hivyo mtukufu mfalme, mzee Sube ndio chanza cha haya matatizo.

    MFALME: Hahaha nyie vijana munanchekesha sana. Mzee sube mimi ninamjua vizuri tena sana, katika wazee ambao nina waamini hapa kijiji mzee sube ndie namba moja alafu leo ndio mje mniambie kuwa yeye ndio msaleti.



    Mfalme alicheka sana na kuhisi wale vijana wametumwa na baadhi ya watu pale kijijni kutokana mzee sube kuwa karibu nae.



    KIJANA: Tunajua sio rahisi kutuamini kwa sababu mzee sube kwa sasa upo karibu nae kwahiyo uwezi kuona ubaya wake ambae amekuwa akiufanya.



    MFALME: Najua mnasema hivyo kwa sababu mzee sube yupo karibu na mimi na nimempa cheo kwahiyo mkaona bora mje kumuaribia ili nisielewane nae au itakuwa mumetumwa nyie ?. Sasa nasema huo mpango wenu mmeshindwa kufanikiwa.

    Vijana wliumia sana na kuona mfalme hana nia ya kusaidia kijiji bali yupo kwa ajili ya kumlinda mtu mmoja, lakini hawakukata tama wakaendelea kuongea nae.



    KIJANA: Mtukufu mfalme sisi atujatumwa na mtu yoyote kama wewe unavyofikilia bali hiki tunachokuambia ni kweli na ipo siku utakuja kuamini tunachokuambia.

    MFALME: Mh ! Leo nimeamini kuwa sio kila mtu anapenda mafanikio ya mwenzake bali kuna watu wanapenda kumuona wenzao wakiwa wanaiishi kwenye maisha ya shida. Sasa nyinyi mumekuja kuniambia hivyo ili mimi nifanye nini.

    KIJANA: Kwanza tumekuja kukupa taarifa ya kumgundua mbaya wa kijiji pili tumekuja kuomba ruhusa ya kumchunguza yule mzee.



    Mfalme akajibu kwa jeuri..

    MFALME: Mkitoka kumchunguza yeye mje kunichunguza na mimi, endapo itaonekana mnamsingizia hukumu ya kifo itakuwa juu yenu .

    KIJANA: Sawa mtukufu mfalme ila leo usiku tunaomba uje kwenye ile nyumba ambayo ipo karibu na nyumba ya yule mzee ili uone mwenyewe tabia zake, ila utamapokuja angalia asikuone na mtu yeyote sana sana mzee sube pamoja na mke wake.

    MFALME: Sawa nitakuja ila narudia tena ikionekana mnamsingzia hukumu ya kifo itakuwa juu yenu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walipomaliza maongezi wakaondoka na kumuacha mfalme akitafakari maneno yao huku akipanga na adhabu ambazo watapata pindi ikijulikana wanamsingizia mzee sube. Kuanzia hapo masaa yalienda na hatiamaemda wa kwenda kwenye kazi ukawadia, wale vijana wakajikusanya sehemu moja na kwenda kwenye ile nyumba waliyokuwa wamekaa siku ya kwanza



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog